STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 22, 2013

Wanajeshi wanne wafa Nachingwea wakienda Mtwara kutuliza ghasia


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgRZcHVZ3CvZsU4ZT-KF1Whe3ITc-0bHzMl3d37SUPMrVc13MZKx6Iyfu8r9S5f6pDFDQCE_88ubI9JuNojGoqUyfGvP_uPOAUTi0P2GDoMRS7hqdPbZejXJaJ4EuGl0SWFwOV1gPFuELQ/s400/3.JPG
Wanajeshi wakipokea mwili ya askari mwenzao. Picha hii haihusiani na habari hapo chini

WANAJESHI wanne wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) waliokuwa wakielekea Mtwara kusaidia kutuliza ghasia zinazoendelea mjini humo wamefariki dunia, huku wengine 20 wakijeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali wilayani Nachingwea mkoani Lindi.
Habari zilizopatikana hivi punde na kuthibitishwa na baadhi ya mashuhuda zinasema kuwa ajali hiyo ilihusisha lori la wanajeshi hao na gari nyingine imetokea eneo la Kilimani Hewa, kilomita mbili toka kambi ya Jeshi hilo ya 41KJ wilayani humo.
Taarifa hizo zinasema kuwa jumla ya wanajeshi 31 walikuwa kwenye msafara huo na kwamba 20 wamejeruhiwa na kukimbizwa hospitali ya wilaya hiyo, huku wengine saba wakitoka salama bila ya kuwa na majeruhi yoyote.
Inaelezwa kuwa mwendo kasi na kona kali iliyopo eneo la tukio ndiyo chanzo cha ajali hiyo, ingawa Polisi bado haijathibitisha taarifa hizo kuhusiana na vifo vya wanajeshi hao wanne walioelezwa wamefariki katika ajali hiyo.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Viginia Ole Swai, amenukuliwa na kituo cha Radio One Stereo akisema huenda vumbi nalo lilichangia kutokea kwa ajali hiyo baada ya gari hizo kugongana katika ajali hiyo ambayo imepoteza uhai wa wapiganaji hao wa JWTZ wanne na wengine kujeruhiwa ambapo wapo hospitali wakitibiwa.

Azam Marine kuleta meli nyingine kali zaidi


 Muonekano wa Kilimanjaro 4
KAMPUNI ya Azam Marine, inaleta boti mpya ya Kilimanjaro 4, ambayo inatarajiwa kuwasili nchini, kuanzia mwishoni wa mwezi huu, ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 700 na kutumia muda wa dakika 70 kwa safari moja ya kati ya Zanzibar na Dar es Salaam. Hii ni boti mpya kabisa katika muendelezo wa boti za Kilimanjaro, ambayo itakidhi mahitaji ya wasafiri wa eneo hili kwa kuwa inabeba sifa zote, ambazo ni Usalama, Kasi zaidi na Unadhifu. Kaa tayari kwa mzigo mpya kutoka Azam Marine.

Pellegrini athibitika kuondoka Malaga, milango i wazi kutua Man City

http://images.gazzetta.it/Media/Foto/2009/10/30/pelle_01.JPG
Kocha Manuel Pellegrini

MENEJA wa timu ya soka ya Malaga ya Hispania, Manuel Pellegrini amethibitisha kuwa ataondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu wa Ligi Kuu ya nchi hiyo.
Duru za michezo zinasema kuwa, Pellegrini atajiunga na Manchester City kuchukua nafasi ya kocha aliyetimuliwa katika timu hiyo, Muitaliano Roberto Mancini.
Kocha huyo alithibitisha mapema leo kwamba ataondoka katika benchi la ufundi la timu hiyo aliyokuwa akiinoa tangu mwaka 2010.
Akinukuliwa na mtandao wa Marca.com wa gazeti moja la nchini humo , kocha huyo alisema yeye na klabu hiyo wanaelekea kuachana, lakini umoja wao utaendelea kuwepo hata kama watatenganishwa na miji watakayokuwepo.
"Naondoka," alinukuliwa kocha huyo aliyoifikisha Malaga kwenye Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kabla ya kutolewa na  Borussia Dortmund ambayo inatarajiwa kuvaana na wapinzani wao wa Ujerumani, Bayern Munich siku ya Jumamosi katika pambano la Fainali za mwaka huu.

Mkutano wa Tenga na wanahabari haupo tena kesho

 
Rais Tenga akiwa na Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah
ULE mkutano kati ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga na Waandishi wa Habari uliokuwa ufanyike kesho (Mei 23 mwaka huu) umeahirishwa mpaka hapo mtakapoarifiwa tena.
Taarifa iliyotumwa na Msemaji wa TFF, Boniface Wambura imesomeka kwamba mkutano huo wa kesho haupo kama ulivyokuwa umepangwa bila kufafanuliwa kilichosababisha kufutwa ghafla.
 

Mary Naali ashinda mbio za kimataifa za Marathon Romania

http://runners.ru/images/stories/atced.jpg
Mary Naali
MWANARIADHA wa Tanzania, Mary Naali, kutoka Klabu ya African Ambassadors Athletics (AAAC), ya Arusha ameibuka mshindi katika mbio za kimataifa za Bucharest. ‘Bucharest International Half Marathon’ nchini Romania, mwishoni mwa wiki.

Kwa mujibu wa mtandao wa Bucharest International Half Marathon, Naali alishinda akitumia saa 1:16.32 na kufuatiwa na Salome Albere wa Ethiopia 1:18.20, Mromania Nicoleta Petrescu alishika nafasi ya tatu kwa 1:20.24 huku wa nne akiwa ni Rodean Veronica kutoka Ujerumani 1:24.51 na tano bora ikafungwa na Gradinariu Alexandra wa Sweden 1:30.26.

Simba, Yanga zitaanza hivi Kagame Cup 2013

http://www.gushit.com/files/bookmark_photos/542db1350bL.jpg
Hamis Kiiza 'Diego' akiwa na taji la Kagame, Yanga ilipotwaa kwa mara ya pili mwaka jana jijini Dar


MABINGWA watetezi wa mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), Yanga wataanza kutetea taji lao dhidi ya Express ya Uganda katika mechi ya kundi C Juni 20 kwenye Uwanja wa Elfasher saa nane mchana wakati Simba iliyopangwa kundi A la 'kifo' itashuka dimbani siku inayofuata kuivaa El Mereikh.

Kwa mujibu wa ratiba ya mashindano hayo yatakayoanza Juni 18 hadi Julai 2 mwaka huu iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), timu nyingine zinazounda kundi C pamoja na Yanga ni Vital'O ya Burundi na Ports ya Djibouti wakati kundia la kundi A la Simba linahusisha pia timu za APR ya Rwanda na Elman ya Somalia.

Ratiba hiyo inaonyesha kuwa kundi B limezoa timu wenyeji zote tatu za Al Hilal, Al Nasri na Al Ahly Shandy pamoja na Tusker ya Kenya na Super Falcon kutoka Zanzibar.

Yanga ambao ni mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara watashuka tena dimbani Juni 22 mwaka huu kuikabili Ports na watakamilisha mechi za hatua ya makundi Juni 25 kwa kuvaana na Vital'O.

Wawakilishi wengine wa Bara, Simba watatupa karata yao ya pili Juni 23 kwa kuwavaa APR na watamaliza na Elman Juni 26.

Mechi ya ufunguzi wa mashindano hayo itakayofanyika Juni 18 saa nane mchana itakuwa ni kati ya Tusker dhidi ya Super Falcon na saa 10:00 jioni Al Hilal itachuana na Al Nasri.

Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye, alisema jana kuwa timu nane zitakazosonga mbele kucheza hatua ya robo fainali ambapo mbili kutoka makundi ya A na C, tatu kutoka kundi B na moja (best looser) itakayofanya vizuri kutoa kundi lolote.

Musonye alisema kuwa maandalizi ya mashindano hayo yamekamilika na zawadi za mashindano hayo mwaka huu zitaongezeka kufuatia wadau kujitokeza kusaidia michuano hiyo.

Alisema kwamba sasa CECAFA ina jumla ya Dola za Marekani 100,000 za zawadi lakini kiwango cha fedha watakachopata mabingwa, washindi wa pili na watatu kitajulikana baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji ya shirikisho hilo itakayokutana kabla ya kuanza kwa mashindano hayo ya kila mwaka.

Mbunge Lema 'akanasa', Vodacom yamsafisha RC Arusha sms za vitisho dhidi yake


Mbunge wa Arusha, Godbless Lema

KAMANDA wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, amedai kuwa uchunguzi wa awali kuhusu ujumbe unaodaiwa kutumwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, umetumwa na mtandao wa simu wa nje ya nchi.

Kamanda alisema katika ujumbe huo ambao Lema anadai uliandikwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo na kutumwa kwenye simu yake Aprili mwaka huu, uchunguzi wa polisi umeonyesha kwamba haukutumwa kupitia kampuni moja wapo ya simu za mikononi ya hapa nchini.

“Katika kipindi cha mwishoni mwa Aprili mwaka huu, vyombo vingi vya habari vikiwemo radio, magazeti na mitandao ya kijamii viliandika na kutangaza habari iliyoelezea shutuma zilizotolewa na Mbunge Lema kuwa aliandikiwa ujumbe wa vitisho kwa njia ya simu na Mkuu wa Mkoa Mulongo na ulisomeka:

“Umeruka kihunzi cha kwanza nitakuonyesha mimi ni serikali, ulikojificha nitakupata na nitakupa kesi inayoitaka mimi.”

Kamanda Sabas alisema ujumbe huo ulidaiwa kutumwa kutoka namba 0752960276 inayotumiwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo kwenda kwenye namba 0764150747 inayotumiwa na Lema. Alisema kufuatia tuhuma hizo, polisi walianza uchunguzi kwa kuzingatia kuwa Mulongo alikanusha kutuma ujumbe wa aina yo yote kwa Mh Lema.

Alisema uchunguzi huo ulihusisha kampuni ya simu ambayo mtandao wake ulitumika katika utumaji wa ujumbe husika. Alisema uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa chanzo cha ujumbe huo mfupi hakikuwa kampuni ya simu husika (hakuitaja) kwa vile ‘Centre Number’ iliyotumika kutuma ujumbe huo mfupi wa maneno ni 44780200332, ambayo siyo ya mtandao wa kampuni husika bali ni ya mtandao ulio nje ya nchi.

Alisema uchunguzi zaidi unaendelea kubaini chanzo cha ujumbe huo mfupi wa simu na mtu aliyehusika kutuma hatua za kisheria zitaweza kuchukua mkondo wake.


BARUA  TOKA  VODACOM
 

Tenga kutetea na wanahabari kesho

 
Rais wa TFF Leodger Tenga

Na Boniface Wambura
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga anatarajiwa kuteta na waandishi wa habari katika mkutano utakaofanyika kesho asubuhi.
Mkutano huo wa kesho (Mei 23 mwaka huu) uanatarajiwa kufanyika kuanzia saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF, Ilala jijini Dar es Salaam.



Mtwara hali tete, mabomu risasi zatawala

Baadhi ya matukio yanayoendelea Mtwara
HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema hali ni tete mjini Mtwara, hakuna amani, mabomu ya machozi yanarindima muda huu na huduma zote za kijamii zimefungwa hakuna usafiri, masoko, maduka na bar zote zimefungwa, daladala, Taxi na Bodaboda hazifanyi kazi.  
 
Kwa ujumla kinachoendelea ni mapambano makali kati ya Jeshi la polisi na wananchi wenye hasira wanaopinga vikali kuendelea kwa mchakato wa gesi ilihali nchi ikiwa haina sera inayosimamia nishati hiyo.
 
Kufuatia Kambi ya Upinzani kuukataa mpango wa serikali wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara Mpaka Dar es salaam ilihali Waziri wa Nishati akisoma hotuba yake kwa hisia kali na mbwembwe na kusema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara kwenda Dar es salaam Wananchi wa Mtwara walicharuka!
 
 Daraja la Mikindani limevunjwa hakuna mawasiliano Mtwara na Dar es salaam.
 
Baadhi ya Wananchi wamepora Silaha na wanazitumia kujibu mashambulizi ya Jeshi la Polisi (habari haijathibitishwa rasmi)
 
 Jengo la Ofisi ya CCM saba saba limechomwa moto. 
Lodge/Hotel (Shengena) inayoaminika kwamba ndiyo waliyofikia Askari wa Jeshi la Polisi (FFU) kutoka mikoa ya jirani kwaajili ya operation inayoendelea imechomwa moto.
 
Milio ya risasi na mabomu ndicho kinachosikika. 
Nyumba kadhaa  za watumishi  wa Serikali  zimechomwa  maeneo ya Shangani.

Ni magari ya FFU ndio yaliyopo barabarani nayo yanapata wakati mgumu kupita kwasababu ya mawe na magogo makubwa yaliyowekwa na Wananchi. 
Askari kadhaa wamekufa (habari hii haijathibitishwa rasmi)
Baadhi ya watu kadhaa wamechukuliwa na askari kwakuwa wamepita jirani na gari yao.
 Yadaiwa askari wengi waliokuja si wa Mtwara, wengi wametoka Masasi na Lindi. 
 Ving'ora vinalia hovyo. Watoto wamefungiwa mashuleni walimu wamekimbia. 
 Vituo vya Redio vya Mtwara havizungumzii hali hii ya hatari bali vinapiga Muziki pengine vinakusanya matukio na habari ya majanga haya ili Wananchi wayapate.
 Mabomu yanapigwa mfululizo maeneo ya Magomeni-Mtwara, mpaka sasa takriban mabomu 20 na ushee yameshapigwa.

Msouth kuzihukumu Stars na Morocco, TFF yaanika ratiba ya mazoezi ya Stars


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj5ta_2ly1qlzIPEMvk9-7RZw-jUtAQOF_M1x8hzY9FkGokWUR35u8p492S6fv93ojEEaSwnv5Isx0Oqz1sXA0ns71kzAKekOc-WhQCB9ETEs3ExFRGtjo1Zz6_8tQNl1uqOcAqy2IGfwjF/s1600/Daniel_Bennett.jpg
Refa Frasser Daniel Bennett atakayezichezesha Tanzania na Morocco

Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na wenyeji Morocco (Lions of the Atlas).

Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett.

Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.

Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda.

Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia.



Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo;
Mei 22                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume

Mei 23                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni   Uwanja wa Karume

Mei 23                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume

Mei 25                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni     Uwanja wa Karume

Mei 26                 Saa 3 asubuhi                            Uwanja wa Karume


Tuesday, May 21, 2013

Makundi ya Kagame Cup 2013 yapangwa

Wachezaji wa Yanga wakishangilia katika baadhi ya mechi zao za mwaka jana za Kagame ilipocheza Dar

 MABINGWA watetezi wa Kombe la Kagame, Yanga ya Tanzania imepangwa kundi l;a C pamoja na timu za Express ya Uganda, Vital'O ya Burundi na As Port ya Djibout, huku watani zao Simba wakiwekwa kundi A na El Merreikh ya Sudan na APR ya Rwanda.

Mbali na APR na Merreikh, kundi hilo A lina timu ya Elman ya Somalia, wakati kundi B l;ina timu za El Hilal ya Sudan, Ahli Shandi ya Sudan, Al Nasir Juba ya Sudan Kusini, Tusker Kenya na Super Falcon ya Zanzibar.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi mwezi ujao na kumalizika mwanzoni mwa Julai, ambapo jumla ya timu 13 zitachuana katika kinyang'anyiro hicho.
Makundi hayo ni kama ifuatavyo:
Kundi A: El Merreikh (Sudan), Simba (Tanzania), Elman (Somalia) na APR (Rwanda).
Kundi B: El Hilal (Sudan), Ahli Shandi (Sudan), Al Nasri Juba (S.Sudan), Tusker (Kenya) na Super Falcon (Zanzibar)
Kunci C: Yanga (Tanzania), Express FC (Uganda), Vitalo (Burundi) na AS Port (Djibouti).

MKALI WA RHYMES  PROF. JAY AAMUA KUMFUATA SUGU CHADEMA

 Wanachama wapya wa Chadema, Joseph Haule maarufu Professa Jay (katikati)  na mwenzake Levison Kasulwa maarufu Kwa Mapacha, wakifurahia mara baada ya kupokea kadi zao za wanachama ikiwa ni kujiunga na Chama hicho mjini Dodoma huku wakionyesha alama yan chama hicho . Hafla hiyo iliyofanyika mjini Dodoma jana ilihudhuriwa na wabunge kadha wa CHADEMA.Kushoto ni Mbunge wa Mbeya  Mjini JosephMbiliny leo

Prof Jay akiionyesha kadi aliyokabidhiwa kwa kujiunga na CHADEMA akiwa na Wabunge wa chama hicho, Josepj Mbilinyi 'Sugu' na John Mnyika.

KICHANGA CHA MIAKA MIWILI CHAFANYIWA UKATILI WA KUTISHA

Mtoto Joshua akiwa amekaa uwani kwenye nyumba  yao huku wazazi wake wakiwa wamemwacha peke yake toka asubuhi bila ya kumpatia chakula mtoto huyo tumemkuta katika hali mbaya sana kwani tunemkuta amejisaidia haja ndogo na hana hata nguo za kubadilisha


Kwa ujumla mtoto Joshua hata kutembea hawezi kwani simama yake ni ya kutetemeka migu tu 

Hizi ni nguo za joshua na kaka yake nguo hizi hazifuliwi bali zikirowa na mkojo huwanikwa tu juani na kisha kuvaliwa tena

Mtoto Joshua akiwa ana tushangaa maana anaona amevamiwa kwakweli inasikitisha sana

Hapa ndiyo mtoto joshua huwa anacheza wakati wa mchana

Mlango ulio wazi ndimo mtoto Joshua hufungiwa humo

Hiki ndicho chumba mtoto Joshua hufungiwa kama picha unavyoiona kona hiyo ndiyo mtoto huyo hujibanza


Kushoto ni kaka wa Joshua yeye amesema huwa anashinda nyumba za jirani kucheza wakati mdogo wake amefungiwa ndani

Mama wa mlezi wa Joshua akiingia numbani kwake na kutushangaa tumekuja fuatanini kwake

Angalia picha hii kwa makini jinsi mtoto Joshua anavyomwangalia mama yake mlezi yaani mama wa kambo

Sekera Watsoni (40) amembeba mtoto Joshua kuonyesha anampenda na kuwa anamhudumia vizuri mtoto huyo

Huyu mama pamoja na mumewe ndiyo wanaomtesa mtoto Joshua

Hawa kaka zake Joshua wakituonyesha sehemu wanayolala pamoja na joshua wakati mama huyo yeye amesema  yeye huwa analala na joshua chumbani kwake 

Baadhi ya majirani wakisimulia mkasa huo

Amini usiamini mtoto Joshua baada ya kuona mkeka mzuri alijilaza kwa furaha kwani amezoea kulala sakafuni



Mama mlezi wa Joshua akijiandaa kumpeleka joshua kituo cha afya akapate matibabu baada ya kuamriwa kufanya hivyo




Habiba Ibrahimu amesema kuwa tukio la kufungiwa ndani mtoto ni la aibu kubwa hivyo halipaswi kufumbiwa macho na jamii husika hivyo ametaka hatua za haraka zichukuliwe ili kuokoa maisha ya mtoto huyo



Katika hali isiyokuwa ya kawaida mtoto mwenye umri wa zaidi ya miaka miwili amefungiwa ndani na wazazi wake kwa kipindi cha miaka miwili sasa bila kutoka nje pamoja na kukosa matunzo muhimu hali ambayo imepelekea mtoto huyo kudhoofu kiafya.
Tukio hilo limetokea leo jijini mbeya katika  mtaa wa Ikuti kata ya Iyunga ambapo majirani wa karibu na mtoto huyo pamoja na baadhi ya viongozi wa mtaa huo kufika nyumbani anapoishi mtoto huyo kwa lengo la kufahamu maendeleo yake .
Mtoto huyo amefahamika kwa jina la Joshua Joseph umri unao kadiriwa  kuwa ni kati ya miaka miwili au mitatu  ambaye alikutwa nyumbani hapo akiwa pekee yake huku wazazi wake wakiwa wameondoka kuelekea kwenye shughuli zao .
Akizungumzia tukio hilo Kaimu barozi wa mtaa huo wa Ikuti Ndugu Aloni Mboya amesema kuwa hali hiyo imenza kujitokeza kwa kipindi cha miaka mitatu sasa hali ambayo imepelekea mtoto huyo kukumbwa na maradhi ya utapiamlo.
Amesema katika kipindi cha mwaka 2011 mwezi wa tatu alipokea  taarifa kuhusiana na   suala hilo  ambapo baba wa mtoto huyo ndugu Joseph Simoni aliitwa katika ofisi za mtaa kwa lengo la kumhoji juu ya malezi ya mtoto huyo.
 Aidha baada ya kuhojiwa alikiri kosa ambapo alipewa onyo na viongozi wa mtaa ambao walimtaka kuhakikisha anamtunza vema mtoto huyo kwa kumpatia chakula bora  pamoja na huduma nyingine.
.
Mara baada ya mtu huyo kupewa kalipio na viongozi wa mtaa hali hiyo iliendelea tena ambapo wao kama viongozi wa shina pamoja na wananchi walimuita yeye pamoja na mke wake aitwaye  Sekera Watsoni (40) kuhama mtaani hapo kwa kwa kipindi cha miezi sita ambapo walikaidi agizo hilo.
 Amesema mara baada ya watu hao kugoma waliamua kuwaacha na kuwaondoa katika umoja wa ubarozi wao na kuto watambua tena kama wananchi wa eneo hilo kutokana na vitendo vyao vya kikatili dhidi ya mtoto huyo.
Kwa upande wao Maafisa maaendeleo ya jamii kata ya Igawilo na Iyunga ambao ndio waliofika katika eneo hilo wamesema kuwa matukio kama hayo yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara ndani ya jamii hasa kwa vitendo vya kunyanyaswa kwa watoto wanawake.
Mmoja wa Maafisa hao Ndugu Habiba Ibrahimu amesema kuwa tukio la kufungiwa ndani mtoto ni la aibu kubwa hivyo halipaswi kufumbiwa macho na jamii husika hivyo ametaka hatua za haraka zichukuliwe ili kuokoa maisha ya mtoto huyo
  
Amesema hali ya kiafya ya mtoto si ya kulizisha kutokana na kusumbuliwanna maradhi mbalimbali yanayotokana na kukosekana kwa lishe bora pamoja na huduma nyingine.
Amesema anawashukuru majirani pamoja na viongozi wengine wa serikali ya mtaa ambao wamekuwa karibu na mtoto huyo kwa kipindi chote cha miaka miwili licha ya kutokuwepo kwa ushirikiano toka kwa  wazazi wa mtoto ambaye kwa sasa amefikishwa katika kituo cha afya  Inyala Kata ya Iyunga  jijini hapa.
Awali inaelezwa kuwa baba na mama wa mtoto huyo  wamekwisha tengana kwa kipindi kirefu sasa kutokana na kutokuwepo kwa maelewano ndani ya nyumba hiyo hali ambayo ilimfanya baba huyo kuoa mwanamke mwingine ambaye ndiye anaye ishi na mtoto kwa sasa kama mama wa kambo.
Amesema kutoka na kuwepo kwa mgawanyiko huo ndani ya familia baba pamoja na mama huyo ambaye ni mke wa pili walichukua jukumu la kuishi na watoto wote walio achwa na mwanamke wa kwanza ambapo kwa asilimia kubwa ndiko kuliko sabababisha kuwepo kwa hali hiyo ya manyanyaso ya mtoto.
Hata wakati wa tukio hilo la kumtoa mtoto huyo ndani baba mzazi wa mtoto hakuwepo katika maeneo hayo ya nyumbani ambapo maafisa ustawi wa jamii pamoja na majirani waliamua kuchukua jukumu la kumpeleka mtoto huyo katika kituo cha afya Inyala kilichopo Kata ya Iyunga kwa lengo la kumfanyia uchunguzi na kutambua nini kinacho msumbua mtoto huyo


Picha na Mbeya yetu 

Aggrey Morris azikatisha tamaa zinazomwania adai ang'oki Azam


Aggrey Morris
BEKI mahiri wa Azam anayeichezea pia timu ya taifa (Taifa Stars), Aggrey Morris, amezikata maini klabu zinazodaiwa kumnyemelea ili zimsajili kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kusema wazi kuwa, haendi kokote zaidi ya kubaki Azam.
Aidha beki huyo kutoka Zanzibar, alikiri kwamba ligi iliyomalizika wikiendi ilikuwa ngumu na kudai kufurahishwa na namna Azam ilivyozipeleka puta Simba na Yanga kiasi cha kuonekana kama ingetwaa ubingwa msimu huu kabla ya kuteleza.
Akizungumza na MICHARAZO Morris alisema pamoja na kutajwa kuwindwa na klabu kadhaa nchini ili kumsajili, ukweli ni kwamba klabu hizo zinajisumbua bure kwa sababu hana mpango wa kuihama Azam kwa sasa.
Beki huyo wa kati alisema bado ana mkataba na Azam na anauheshimu vilivyo, kadhalika analo deni kubwa kwa klabu hiyo hasa kwa soka la kimataifa hivyo hafikirii kuondoka kirahisi kama inavyotangazwa na baadhi ya vyombo vya habari.
"Ukweli mimi siendi kokote, mimi ni mchezaji wa Azam nitaendelea kuwa mchezaji wa Azam mpaka mwisho wa mkataba wangu, ni klabu ninayoipenda na ninayoona nina deni kubwa ambalo napaswa kulipwa hasa kwa michuano ya kimataifa," alisema.
Morris ni miongoni mwa wachezaji wanne wa Azam walioshindwa kuitumikia klabu hiyo katika Kombe la Shirikisho Afrika ambapo klabu hiyo iliishia kwenye 16 Bora, kutokana na kusimamishwa na uongozi wao kwa tuhuma za Rushwa.
Hata hivyo Morris na wachezaji wenzake, Said Murad, Erasto Nyoni na kipa Deo Munishi 'Dida' walisafishwa na Taasisi wa Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na kurejeshwa klabu mwishoni mwa msimu.
Juu ya msimu ulioisha, Morris alisema ulikuwa mgumu na wenye ushindani, huku akidai kufurahishwa na jinsi Azam ilivyozikimbiza Simba na Yanga kiasi cha kukaribia kutwaa ubingwa kabla ya kuteleza na kuiachia Yanga inyakue taji la 24 kilaini.
"Ligi ilikuwa ngumu na huenda msimu ujao ikawa ngumu zaidi kutokana na timu kuonyesha kuimarika kila uchao na hasa kupewa nafasi kwa wachezaji vijana," alisema.

Matokeo Kidato cha Sita:Sifuri kibao zafutwa kimyakimya

http://laivu.com/habari/files/2013/02/kawambwa1.jpg
Waziri wa Elimu na Ufundi Stadi Dk Shukuru Kawambwa


MPANGILIO wa alama mpya za kufaulu kwa wahitimu wa kidato cha sita waliohitimu mwaka jana, ambao matokeo ya mitihani yao yanaweza kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa, unadaiwa kuzua aibu na kama si uamuzi uliotajwa bungeni wa matumizi ya alama za ufaulu za zamani, matokeo hayo yangeibua aibu kama ilivyojitokeza kwa kidato cha nne, 2012.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari kutoka Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) ambalo linaendelea kupanga matokeo hayo ya kidato cha sita kwa kuzingatia alama za zamani kama ambavyo taarifa ya awali ya Tume iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ilivyosomwa bungeni hivi karibuni, hali ingekuwa mbaya zaidi katika ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha sita kiasi cha kuweza kutishia uhai wa vyuo vikuu nchini kukosa wanafunzi wa kutosha.


“Hali ilikuwa mbaya sana kama alama za kufaulu zingeachwa zitumike zile mpya na si za zamani. Vyuo vikuu nchini visingeweza kupata wanafunzi wa kutosha.


 "Tatizo hapa si uwezo wa wanafunzi moja kwa moja katika kumudu mitihani bali ni kufanywa kwa mabadiliko ya alama bila kuwaandaa.

" Alama hizi zilipaswa kuanza kutumika na wanafunzi wapya, yaani kama wanaanza kidato cha kwanza wawe wanapewa mitihani ya kupimwa kwa kuzingatia alama mpya na waendelee nazo hadi mitihano yao ya mwisho.

“Na hivyo hivyo kwa wanafunzi wa kidato cha sita. Alama hizi mpya zinapaswa kutumika kwako kuanzia wakiwa kidato cha tano mara wanapoanza shule, kila mitihani wanayopewa isahihishwe na kupangiwa alama kwa kutumia hizi alama mpya,” kinaeleza chanzo chetu cha habari kutoka NECTA.


Kwa mujibu wa mabadiliko hayo ya alama, alama mpya zilizokuwa zimetumika awali ni daraja F kuanzia 34 hadi sifuri; badala ya alama hiyo F kuanzia 20 hadi 0; daraja D kwa kuzingatia alama mpya linapaswa kuanzia 35 tofauti na awali, yaani alama 21.


Taarifa zaidi zinabainisha ya kuwa, kati ya sababu za kuchelewa kutangazwa kwa matokeo ya kidato cha sita tofauti na muda uliotarajiwa yaani mwanzoni mwa Mei, ni pamoja na upangaji upya matokeo hayo, ikiwa ni tofauti na ilivyokuwa kwa kidato cha nne ambapo matokeo yalitangazwa na kisha kufutwa ili kuyapanga upya kwa kutumia alama za zamani.


Lakini alipoulizwa kuhusu masuala hayo ndani ya NECTA, Ofisa Habari wa Taasisi hiyo nyeti nchini, John Nchimbi alisema; “Kwa sasa niseme tu kwamba mchakato wa kuandaa matokeo ya kidato cha sita unaendelea, siwezi kusema lini hasa utakamilika lakini nina uhakika ni katika muda muafaka.”


Kuhusu matokeo ya kidato cha sita kucheleweshwa kutokana kupangwa upya ili kupunguza idadi ya waliofeli kutokana na matumizi ya alama mpya za kufaulu, Nchimbi anasema; “Unajua haya maagizo haya ya bungeni (kupanga matokeo kwa kuzingatia alama za zamani) yamekuja wakati mchakato wa kuandaa matokeo ulikwishaanza. Kwa hiyo baada ya maagizo ilibidi kufanya kazi hiyo tena kwa kufuata maagizo hayo.”


Hata hivyo, hakuweka bayana kama matokeo ya awali kabla ya maagizo ya Serikali yaliyotolewa bungeni kutumia alama za zamani yamewafanya wanafunzi wengi kufeli na badala yake akasema; “Hilo siwezi kulizungumzia kwa sababu mchakato wa matokeo hayo haukuwa umefika mwisho. Takwimu rasmi hazikuwa zimekamilishwa. Kwa hiyo si sahihi kusema rasmi walifeli.”


Lakini wakati hali ikiwa hivyo kwa upande wa matokeo yanayotarajiwa ya kidato cha sita, taarifa zaidi zinabainisha ya kuwa, baada agizo la serikali la kufuta na kurejewa upya kwa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012, takriban wanafunzi 50,000 wamepata unafuu katika matokeo yao tofauti na awali.


Awali, kwa kuzingatia matokeo ya kidato cha nne mwaka jana yaliyotangazwa Februari, mwaka huu jijini Dar es Salaam, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa, jumla ya watahiniwa 126,847 tu kati ya watahiniwa 397,136 waliofanya mtihani huo walifaulu.


Katika matokeo hayo idadi ya wasichana waliofaulu ilitajwa kuwa ni 46,181 wakati wavulana waliofaulu ikiwa wanafunzi 80,686 na idadi ya watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu ni 16,112 kati yao watahiniwa 61,001 waliofanya mtihani wasichana ni 6,7751 na wavulana 9,361.


Katika matokeo hayo watahiniwa waliopata daraja la kwanza ni 1,641, daraja la pili 6,453 na daraja la tatu ni 15,426, wakati waliopata sifuri ni 240,903 lakini kwa kuzingatia taarifa za vyanzo vyetu ndani ya Baraza, idadi hiyo itabadilika kwa sababu ya alama kuongezwa kwa watahiniwa hao wa mwaka 2012.


Lakini matokeo hayo yalitangazwa pamoja na vituko walivyofanya baadhi ya wanafunzi, vikiwamo vituko vya kuandika matusi kwenye karatasi za majibu ya mitihani na kutokana na makosa hayo, watahiniwa 789 walifutiwa mitihiani yao.


Source: Raia Mwema.

FAINALI ZA VODACOM MIC KING KUFANYIKA  J'MOSI

Meneja Matukio wa Dar Live, Abdallah Mrisho (wa pili kushoto) akiongea na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho huo. Wengine pichani kutoka kushoto ni DJ John Dilinga (JD), Prodyuza Ally Baucha na Prodyuza Tudd Thomas.
Kutoka kushoto waliokaa ni msanii Stamina, DJ John Dilinga, Abdallah Mrisho, Ally Baucha na Tudd Thomas katika picha ya pamoja na washiriki wa The Vodacom Mic King waliosimama nyuma.
Wakali wa MIC wanaowania gari wakiwa katika pozi na gari hilo.
Wanahabari wakichukua baadhi ya matukio.
…Wakimsikiliza Abdallah Mrisho.
Hawa ndiyo wakali tisa wanaowania gari aina ya Toyota Funcargo (New Model).
Uongozi wa Dar Live Co. Ltd leo umetambulisha tamasha kubwa la kila mwaka la Usiku wa Hip Hop na fainali za kumtafuta Mkali wa Mic zijulikano kama ‘The Vodacom Mic King’ kwa wanahabari. Tamasha hili litafanyika Jumamosi hii, Mei 25, 2013 katika Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar. Jumla ya vijana tisa wenye vipaji watapanda stejini kuchuana na mshindi ataondoka na gari aina ya Toyota Funcargo (New Model) yenye thamani ya shilingi milioni 15. Mbali na zawadi ya gari, mshindi wa kwanza, pili na watatu, watapata fursa ya kurekodi wimbo mmoja chini ya Prodyuza mahiri nchini, Tudd Thomas, aliyerekodi wimbo maarufu wa Leka Dutigite wa Kigoma All Stars na nyingine nyingi. Majaji katika shindano hili ni mwandishi mkongwe wa habari za muziki na wasanii, Abdallah Mrisho, DJ John Dilinga (JD) na Prodyuza Ally Baucha.
Tamasha hilo litapambwa na burudani kutoka kwa wakali wa Hip Hop nchini ambao ni Fid Q, Joh Makini, Stamina, Kala Jeremiah, Nay wa Mitego pamoja na shoo kali kutoka kundi la Wakali Dancers. Katika usiku huo, zitatolewa tuzo kwa wasanii wa Hip Hop na kwa wimbo bora wa Hip Hop uliofanya vizuri mwaka 2012/13. Kutakuwa na Tuzo kwa Msanii Mkongwe Bora wa Hip Hop na Msanii Chipukizi Bora wa Hip Hop pamoja na Wimbo Bora wa Hip Hop.
(PICHA NA MUSA MATEJA / GPL)

Friends Rangers na wenzao kuchujana RCL Wikiendi


Na Boniface Wambura
LIGI ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kuwania nafasi tatu za kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao inaingia raundi ya pili wikiendi hii kwa kukutanisha timu 14 zilizofanikiwa kusonga mbele.

Timu zitakazocheza raundi hiyo kwa mtindo wa nyumbani na ugenini ni Abajalo ya Dar es Salaam itakayokuwa mwenyeji Kariakoo ya Lindi katika mechi itakayochezwa Jumamosi (Mei 25 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

Siku hiyo hiyo Uwanja wa Azam ulioko Chamazi utatumika kwa mechi kati ya Friends Rangers ya Dar es Salaam na African Sports ya Tanga wakati Jumapili (Mei 26 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Machava FC ya Kilimanjaro na Mpwapwa Stars ya Dodoma itakayochezwa Uwanja wa Ushirika mjini Moshi.

Stand United ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida katika mechi itakayochezwa Jumapili (Mei 26 mwaka huu) Uwanja wa Namfua mjini Singida wakati Polisi Jamii ya Mara na Biharamulo FC ya Kagera zitaumana siku hiyo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

Mjini Kigoma kutakuwa na mechi kati ya wenyeji Saigon FC na Katavi Warriors ya Katavi. Nayo Kimondo SC ya Mbeya itakuwa mgeni wa Njombe Mji ya Njombe katika mechi itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Sabasaba.

Mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu wakati timu zitakazofuzu kucheza raundi ya tatu zitacheza mechi za kwanza kati ya Juni 8 na 9 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakuwa kati ya Juni 15 na 16 mwaka huu.

Wabunge nusura wachapane makofi

Wabunge Anna Kilango (kulia) na Tundu Lissu aliyeshikiliwa wakitupiana maneno

BAADA ya Bunge kuahirishwa jana, nje ya ukumbi hali haikuwa nzuri baina ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela.

Mtafaruku huo uliibuka baada ya Kilango kusikika akimtuhumu Lissu kwa uchochezi, akisema kwamba amekuwa mbunge pekee anayeongoza kwa vurugu.

 
Maneno hayo hayakumfurahisha Lissu ambaye alishindwa kuvumilia na kumgeukia Kilango kwa nguvu huku baadhi ya wabunge wakishuhudia na wengine wakimzuia Lissu.
 
Hata hivyo wawili hao walimalizana kiutu uzima, japo awali ilidaiwa ilikuwa mshikemshike kama sio kuamuliwa wangeweza kuchapana makofi hadharani.

Liunda kuwatathimini waamuzi mechi ya FIFA


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUOM9IRMZijo63-gOG0Myp2_FetrrPAa1FMIGgam1cJJeCV3Zw9RJxhccBlTqfqv1BugkRqtKZpQeEqBNDPehsoBY_0JHLwIcpdrPLMoLPcJYFT2o3h3y1-9g6SWu_adMOBBokNV6MFCU/s1600/liunda.JPG
Leslei Liunda

Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua Leslie Liunda wa Tanzania kuwa mtathmini wa waamuzi (referee assessor) katika mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia.

Mechi hiyo ya Kundi B, Kanda ya Afrika kati ya Cape Verde na Equatorial Guinea itafanyika Juni 8 mwaka huu saa 10.30 jioni kwenye Uwanja wa Verzea mjini Praia.

Waamuzi wa mechi hiyo ambao watatoka Angola ni Martins De Carvalho Helder, Dos Santos Jerson Emiliano, Da Silva Lemos Julio na Muachihuissa Caxala Antonio. Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Diarra Massa Momoye wa Mauritania.

Real Madrid yathibitisha kuacha na Mourinho

 
Kocha Jose Mourinho

KLABU ya Real Madrid imethibitisha kuwa kocha wake, Jose Mourinho ataondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu na kuwa nafasi kubwa ya kurejea Stanford Bridge kuinoa Chelsea.

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo iliyomnukuu Rais wao, Florentino Perez wakati akizungumza na waandishi wa habari jana jioni, kuwa Mourinho hatafukuzwa klabuni hapo.

Perez akasema kuwa, wamekubaliana na Mreno huyo kumaliza mkataba wao na hivuyo kuondoka Real Madrid mwishoni wa msimu huu.

Pia Rais huyo aliweka bayana kwamba hawajaanza kufanya mazungumzo na kocha yeyote kwa ajili ya kuziba nafasi ya Mreno huyo ambaye amekuwa akitajwa kuwa mbioni kurejea Chelsea.

Kwa taarifa hiyo ya klabu yake ya sasa ya kuachana naye ni wazi njia ya kurejea Uingereza imekuwa nyepesi tofauti na ilivyotarajiwa na kwamba mwenyewe amekuwa akisisitiza anatamani kurudi nchini humo kutokana na mazingira aliyokuwa nayo Madrid.

Kocha huyo amekuwa na msimu mbaya kwa mwaka huu baada ya timu yake kutoambulia taji lolote ikishindwa kufuzu fainali za Ligi ya Ulaya inayochezwa Jumamosi kwa kung'olewa na Borrusia Dortmund kwenye Nusu fainali, kufungwa Fainali ya Kombe la Mfalme na kushindwa kutetea taji kwa mahasimu wao Barcelona.