KIUNGO mshambuliaji mpya wa Polisi Moro, Kassim Suleiman 'Selembe' amesema anajisikia faraja kubwa kufanya kazi chini ya nyota wa zamani wa kimataifa wa Tanzania Mohammed Rishard 'Adolph'.
Aidha mchezaji huyo aliyekuwa akiichezea Coastal Union, alisema kusuasusa kwa Polisi kwa sasa kunatokana na 'ugeni' wao wa Ligi Kuu, ila kadri watakavyokuwa wakiizoea watawashangaza watu.
Akizungumza na MICHARAZO, Selembe, alisema anajisikia furaha kufanya kazi na kocha Adolph, nyota wa zamani wa Yanga, Pan Africans na Taifa Stars ikizingatiwa ni moja wa nyota wa Tanzania waliojijengea jina kubwa Afrika.
"Kwa mchezaji yeyote anayejitambua kufanya kazi na mtu kama Adolph ni fahari kwa sababu alijijengea jina kubwa ndani na nje ya Tanzania enzi za uchezaji wake, wachezaji tunamfurahia," alisema.
Kiungo wa zamani wa Azam alisema kocha Adolph ni bonge la kocha na anawafanya wachezaji wa Polisi kujiamini na kurejea Ligi Kuu kabla ya yeye kuungana nao akitokea Coastal Union.
Juu ya mwenendo wa kikosi chao, Selembe alisema wanazidi kuimarika kadri wanavyoizoea ligi na kwamba hawana hofu ya kurejea walikotoka akidai ni mapema mno kujadili jambo hilo.
Timu hiyo ilipanda daraja sambamba na Ndanda na Stand United na ilianza kwa kufungwa mechi moja na kuambulia sare mbili katika mechi zao tatu za awali ya ligi hiyo inayoenda mapumziko.
Ligi hiyo itakuwa likizoni kwa wiki moja kupisha mchezo ya kimataifa ya kirafiki unaotambuliwa FIFA Taifa Stars itakapovaana na Benin na itaendelea tena kuanzia Oktoba 18.
STRIKA

USILIKOSE

Monday, October 6, 2014
Jahazi la QPR lazidi kutota, wapigwa 2-0 na West Ham
![]() |
Rio Ferdinand akiwajibika na QPR akifikisha mechi ya 500 katika miaka ya 18 ya kucheza kwake |
![]() |
Ooh kitu! Wachezaji wa QPR hawaamini wakitunguliwa bao na West Ham |
![]() |
Yebaaa! Wachezaji wa West Ham wakipongeza kwa kupata ushindi wa mabao 2-0 kwa vibonde QPR |
QPR wenye pointi na kuburuza mkia walianza vibaya mchezao huo baada ya beki wake kutoka Nigeria Chinedum Onuoha, aliyewahi kuichezea Mancjester City kujifunga bao dakika ya tano tu ya mchezo huo uliochezwa Uptown Park.
Kipindi chja pili kilikuwa majanga zaidi kwa wageni baada ya Diafra Sakho kuongeza bao la pili kwa West Ham kwa kuunganisha mpira wa kichwa katika dakika ya 55 na kuifanya West Ham kuchupa toka nafasi ya tisa katika msimamo wa ligi hiyo hadi ya saba, wakati QPR wakiendelea kung'ang'ania mkiani.
QPR haijawahi kushinda mechi yoyote ya uwanja wa ugenini tangu Machi 2, 2013.
Allan Kamote, Thomas Mashali mabingwa wapya wa UBO
Allan Kamote (kulia) akionyeshana umwamba na Osgood Kayuni wa Malawi katika pambano lao la kuwania Mkanda wa Dunia wa UBO na Kamote kushinda kwa pointi. |
Thomas Mashali akimrushia konde Ramadhani Ali 'Alibaba' katika pambano lao lililochezwa jana kwenye uwanja wa Mkwakwani na Mashali kushindwa kwa TKO ya raundi ya tatu na kutwaa ubingwa wa UBO Afrika |
Kamote alifanikiwa kutwaa ubingwa wa Dunia wa UBO baada ya kumshinda kwa pointi bondia Osgood Kayuni kutoka Malawi katika pambano la raundi 12 la uzani wa Light.
Naye bondia Thomas Mashali alimchapa kwa TKO ya raundi ya tatu Mtanzania mwenzake Ramadhani Ali 'Alibaba' na kutwaa mkanda wa UBO Afrika katika pambano lao la raundi 10 na uzito wa kati. Michezo hiyo iliratibiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST) na ilishuhudiwa pia Francis Miyeyusho akimshinda kwa pointi bondia wa Tanzania anayeishi Kenya Emilio Norfat.
Bondia Kamote licha ya kufanikiwa kutwaa mkanda huo wa Dunia wa UBO, lakini pia amefanikiwa kulipa kisasi kwa mpinzani wake kutoka Malawi aliyewahi kupigana naye mara mbili na kupigwa.
Katika pambano hilo mabondia wote walikuwa wakiviziana na kutupiana makonde kwa ufundi, hali ambayo iliwafanya mashabiki kuwa roho juu kwa kutojua nani atakayeibuka na ushindi hadi jaji alipotangaza matokeo yaliyompa ushindi Kamote.
Katika mechi nyingine za utangulizi, bondia Francis Miyeyusho alimshinda kwa pointi Emilio Norfat, huku Jacob Maganga na Said Mundi wakishindwa kutambiana kwa kutoka sare.
Ronaldo azidi kutesa La Liga, Messi abakisha 2 tu!
![]() |
Ronaldo akishangilia moja ya mabao yake matatu usiku wa jana |
![]() |
Messi akifunga bao lake la 349 katika La liga dhidi ya Rayo Valecano |
Ronaldo alifunga mabao hayo katika dakika za 2, 55 na 88 akisaidiwa na Gareth Bale na Pepe, huku mabao mengine yakiwekwa kimiani na Karim Benzema katika dakika za 41 na 69 na kuifanya Madrid kufikisha jumla ya pointi 15, nne nyuma ya vinara Barcelona ambao wameendelea kushinda mfululizo katika ligi hiyo.
Mabao hayo yamemfanya Ronaldo kufikia rekodi ya ha trick nyingi za gwiji wa Madrid Alfredo de Stephano na Telmo Zarra waliowahi kufunga pia hat trick 22 akimtangulia Messi mwenye ha trick 19 akikamata nafasi ya tano.
Hata hivyo Messi aliisaidia Barcelona kushinda mechi yao ya sita na kuweka rekodi ya kutoruhusu kufungwa bao lolote katika mechi saba mfululizo wakati wakiizamisha Rayo Valecano kwao kwa mabao 2-0.
Messi alifunga bao lililomfanya afikishe jumla ya mabao 349 katika La Liga na kushika nafasi ya pili nyuma ya gwiji wa zamani wa Athletic Bilbao, Telmo Zarra aliyetamba miaka ya 1940-50 aliyefunga mabao 351, ikiwa na maana akifunga mabao mawili tu atamfikia na kuifukizia rekodi mpya katika ligi hiyo maarufu.
Bao jingine la wababe hao wa Nou Camp liliwekwa kimiani na Neymar na kuwafanya wachezaji hao wawili wanaotoka mataifa hasimu katika soka Amerika ya Kusini, Argentina na Brazil kufikisha jumla ya mabao 13 wakicheza pamoja..
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Atletico Madrid iokiwa ugenini ilikumbana na kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Valencia, huku Cordoba na Getafe walitoka sare ya 1-1 na Eibar kulazimishwa sare ya mabao 3-3 na Levante.
Almeria na Elche zilitoshana nguvu kwa sare ya 2-2 na Malaga ikaifumua 2-1 Grenada waliwafuata nyumbani kwao, huku Sevilla ikipata ushindi mnono nyumbani dhidi ya Deportivo la Coruna waliowafumua mabao 4-1 na Celta Viro ililala nyumbani 3-1 kwa Villarreal na Espaniol ilitaka nyumbani kwa kuilaza Real Sociedad kwa mabao 2-0.
ANGALIA WAKALI WA HAT TRICK LA LIGA
Cristiano Ronaldo | 22 |
Alfredo Di Stefano | 22 |
Telmo Zarra | 22 |
Edmundo Suarez | 19 |
Lionel Messi | 19 |
![]() |
Neymar na Messi wakishangilia mabao yao wakati wakishinda ugenini na timu iliyopoteza wachezaji wao wawili uwanjani kw akandi nyekundu Rayo Valecano. |
Sunday, October 5, 2014
Juventus yaizamisha As Roma, Tevez moto chini!

Tevez ambaye amekuwa akichuniwa kuitwa katika timu ya taifa ya Argentina, alifunga mabao yake yote kwa mikwaju ya penati katika dakika ya 27 na 45 wakati bao jingine likiwekwa kimiani na Bonucci dakika nne kabla ya pambano hilo kumalizika.
Mabao ya wageni yalifungwa na Francisco Totti pia kwa mkwaju wa penati dakika ya 32 na Iturbe dakika ya 44.
Kwa ushindi huo Juventus wamezidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo wakiwa na pointi 18 tatu zaidi ya wapinzani wao hao waliokuwa wametofautiana mabao ya kufunga na kufungwa kwenue msimamo huo.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo mapema leo mchana Empoli ikiwa nyumbani ilipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Palermo, huku Lazio ikiizamisha Sassuolo kwa mabao 3-2 waliowafuata nyumbani kwao, Parma walikubali kipigo cha magoli 2-1 dhidi ya wageni wao Genoa na Atalanta ikafa ugenini kwa bao 1-0 dhidi ya Sampdoria.
Timu za Udinese na Cesena zilitoshana nguvu kwa kufunga bao 1-1 na hivi sasa kuna mechi mbili zinachezwa ambazo hata hivyo haziwezi kubadilisha msimamo wa nafasi za juu za ligi hiyo.
Mtibwa Sugar ushindi 100%, Shomar ampumulia Kavumbagu
WAKATI Mtibwa Sugar ikikwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kuiengua Azam, Ally Shomari, mshambuliaji huyo wa Mtibwa amemuashia taa ya kijani Didier Kavumbagu kwa kufikisha bao la tatu kwenye orodha ya wafungaji bora wa ligi hiyo.
Shomari ndiye aliyeifungia Mtibwa Suigar bao pekee lililoizamisha Mgmabo JKT katika mfululizo wa mechi za ligi kuu katika pambano lililochezwa kwenue uwanja wa Manungu, Turiani Morogoro.
Mtibwa imeweka rekodi ya kushinda mechi zake zote tatu na kufikisha pointi 9 na kukwea kileleni mwa msimamo wakiizidi mabingwa watetezi Azam kwa zaidi ya pointi mbili baada ya timu hiyo jana kulazimishwa suluhu na Prisons-Mbeya.
Shomari alifunga bao hilo dakika ya 10 ya pambano hilo na kufanya afikishe idadi ya mabao matatu akiwa nyuma ya Kavumbagu kwa bao moja.
Didier anaongoza msimamo akiwa na mabao manne, kisha Shomar na kufuatiwa na wachezaji wanne wenye mabao mawili kila mmoja ambao ni Ami Ali wa Mtibwa Sugar, Shaaban Kisiga wa Simba, Rashid Mandawa wa Kagera Sugar na Nassor Kapama wa Polisi Morogoro.
Shomari ndiye aliyeifungia Mtibwa Suigar bao pekee lililoizamisha Mgmabo JKT katika mfululizo wa mechi za ligi kuu katika pambano lililochezwa kwenue uwanja wa Manungu, Turiani Morogoro.
Mtibwa imeweka rekodi ya kushinda mechi zake zote tatu na kufikisha pointi 9 na kukwea kileleni mwa msimamo wakiizidi mabingwa watetezi Azam kwa zaidi ya pointi mbili baada ya timu hiyo jana kulazimishwa suluhu na Prisons-Mbeya.
Shomari alifunga bao hilo dakika ya 10 ya pambano hilo na kufanya afikishe idadi ya mabao matatu akiwa nyuma ya Kavumbagu kwa bao moja.
Didier anaongoza msimamo akiwa na mabao manne, kisha Shomar na kufuatiwa na wachezaji wanne wenye mabao mawili kila mmoja ambao ni Ami Ali wa Mtibwa Sugar, Shaaban Kisiga wa Simba, Rashid Mandawa wa Kagera Sugar na Nassor Kapama wa Polisi Morogoro.
Chelsea waizima Arsenal, Diego Costa hakamatiki
![]() |
Diego Costa akishangilia bao lake dhidi ya Arsenal |
Chelsea ikiwa chini ya Mourinho imekuwa ikiiadhibu Arsenal itakavyo, kitu ambacho kiliendelea leo kwenye uwanja wa Stanford Bridge wakati Chelsea walipopata ushindi huo kupitia mabao ya Eden Hazard aliyefungwa kwa mkwaju wa penati dakika ya 27 kabla ya kinara wa mabao katika ligi Diego Costa kufunga bao la pili katika dakika ya 78 akimalizia kazi nzuri ya Cesc Fabregas na kumfanya kufikisha jumla ya mabao tisa katika ligi hiyo.
Mechi inayoendelea kwa sasa ni kati ya West Ham ambayo ipo nyumbani kuikaribisha QPR na mpaka sasa ikiwa ni dakika chache tangu kuanza wenyeji waoangoza kwa bao 1-0.
Yanga yaendeleza ubabe kwa JKT, yailaza 2-1
Yanga ilipata ushindi huo kwenye uwanja wa Taifa na kuifanya timu hiyo kuchupa hadi nafasi ya tatu ya msimamo ikizipumulia timu za Mtibwa na Azam waliopo mbele yao.
Beki Kelvin Yondani aliianza kuiandika Yanga bao dakika ya 37 kwa mkwaju mkali ulioifanya timu yake kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao hilo.
Kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Niyonzima aliiongezea Yanga bao kipindi cha pili kabla ya Jabir Aziz kuifungia JKT Ruvu bao la kufutria machozi dakika chache kabla ya mapumziko.
Kwa ushindi huo Yanga imefikisha pointi sita wakati JKT wamendelea kusalia kwenye nafasi ya pili toka mkiani kutokana na kuwa na pointi mopja sawa na ndugu zao wa Ruvu Shooting Stars.
Mechi ijayo kwa Yanga itakuwa ni kati yao na watani zao Simba ambao wapo katika hali mbaya kwa kutoka sare katika mechi tatu mfululizo kiasi cha kubatizwa jina la wazee wa sare na watani zao.
Manchester Utd, Spurs zaua England, Di Maria achaa bwana!
![]() |
Falcao akishangilia bao lake lililokuwa la pili kwa Mashetani Wekundu mapema leo |
![]() |
Di Maria akishangilia bao la kwanza la Man Utd ambalo ni la tatu kwake tangu ajiunge na timu hiyo |
![]() |
Erikson akiifungia Spurs bao dhidi ya Southampton |
![]() |
Radamel Falcao akishangilia bao lake la kwanza tangu ajiunge Old Trafford |

Angel
Di Maria akishangilia baada ya kufunga goli la uongozi la Manchester
United dhidi ya Everton kunako dakika ya 27 hili likiwa ni goli lake la
tatu tangu kujiunga United

Wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafford, Mashetani Wekundu walionyesha dhamira ya ushindi kwa kuandika bao la kwanza lililofungwa na Di Maria dakika ya 27 akimalizia pasi ya Juan Mata.
Bao hilo lililodumu hadi mapumziko kabla ya wageni kuchomoa kupitia kwa Naismith katika dakika ya 55 kama ya nyota wa zamani wa Atletico Madrid na Monaco Falcao kufunga bao la ushindi dakika ya 62 kwa kazi nzuri iliyofanywa na di Maria na kuwapa ushindi muhimu vijana wa Luis Van Gaal.
Katika pambano jingine la ligi hiyo Tottenham Hotspur ikiwa uwanja wa nyumbani wa White Hartlane walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Southampton.
Bao pekee la pambano hilo lilifungwa na Christian Eriksen dakika ya 40 na kuwafanya Spurs kupata ushindi muhimu na pointi tatu zilizowafanya kufikisha jumla ya pointi 11 na kuchupa hadi nafasi ya sita.
HILI NDILO BANGO LA TFF SIKU YA LEO
![]() |
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inaingia kambini kwenye hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam ikiwa na kikosi cha wachezaji 26 walioitwa na Kocha Mart Nooij kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 11 jioni.
Kwa mujibu wa Kocha Nooij, timu hiyo itakuwa na vipindi (sessions) 11 vya mazoezi kabla ya kucheza na Benin (Squirrels). Stars itafanya mazoezi asubuhi na jioni kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa ambapo baadhi yatafanyika Uwanja wa Taifa, na mengine kwenye uwanja mwingine.
Wachezaji Thomas Ulimwengu na Mbwana Samata wanaochezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) pamoja na Mwinyi Kazimoto anayechezea timu ya Al Markhiya ya Qatar wanawasili nchini kesho (Oktoba 6 mwaka huu).
Naye mshambuliaji Juma Liuzio anayechezea timu ya Zesco ya Zambia atawasili nchini keshokutwa (Oktoba 7 mwaka huu) kwa ndege ya Kenya Airways akitokea Ndola.
MAFUNZO YA USAJILI LIGI DARAJA LA PILIShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaendesha mafunzo ya usajili kwa klabu za Ligi Daraja la Pili (SDL) yatakayofanyika kesho na keshokutwa (Oktoba 6 na 7 mwaka huu) kwenye hosteli ya TFF iliyopo Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kuanzia saa 3 asubuhi.
Mafunzo hayo yatahusu usajili wa mtandao ambao ndiyo klabu hizo zitautumia kwa ajili ya Ligi hiyo itakayoanza baadaye mwezi ujao katika makundi manne ya timu sita sita kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
Kesho mafunzo hayo yatakuwa kwa ajili ya maofisa wa usajili wa klabu za Abajalo, Arusha FC, Kiluvya United, Magereza Iringa, Milambo SC, Mji Mkuu (CDA), Mkamba Rangers, Mshikamano, Mvuvumwa FC, Navy, Njombe Mji, Singida United, Transit Camp, Volcano FC na Wenda FC.
Oktoba 7 mwaka huu mafunzo hayo yatahusisha maofisa usajili wa klabu za Bulyanhulu FC, Eleven Stars, JKT Rwamkoma, Kariakoo Lindi, Mbao FC, Mpanda United, Pamba, Town Small Boys na Ujenzi Rukwa.
MABADILIKO YA MECHI ZA FDL KUNDI BShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefanya mabadiliko kwa baadhi ya mechi za kundi B Ligi Daraja la Kwanza (FDL) baada ya kupokea barua kutoka Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) ikieleza kuwa Uwanja wa CCM Kirumba utatumika kwa shughuli za kidini kuanzia Oktoba 16 hadi 19 mwaka huu.
Kutokana na hali hiyo, mechi namba 17 kati ya Toto Africans na Green Warriors iliyokuwa ichezwe kwenye uwanja huo Oktoba 18 mwaka huu sasa itafanyika Oktoba 20 mwaka huu.
Mabadiliko hayo pia yameathiri mechi namba 19 kati ya Green Warriors na Oljoro JKT ambayo sasa itachezwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, Oktoba 23 mwaka huu badala ya Oktoba 21 mwaka huu.
Vilevile mechi namba 25 kati ya Burkina Faso na Oljoro JKT imesogezwa mbele kwa siku moja kutoka Oktoba 25 mwaka huu hadi Oktoba 26 mwaka huu. Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
BONIFACE WAMBURA
MKURUGENZI WA MASHINDANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA
AC Milan yazinduka Italia, Muntari aibeba Juve, Roma leo
![]() |
Sulley Muntari |
AC Milan inayonolewa na mshambuliaji nyota wa zamani wa timu hiyo na Azzurri timu ya taifa ya Italia, Philip Inzaghi 'Pipo' ilipata ushindiwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Giuseppe Meazza, mjini Milano kupitia mabao ya Sulley Muntari aliyefunga dakika ya 55 na Keisuke Honda aliyeongeza la pili kwa mkwaju wa adhabu ndogo dakika ya 78 na kuifanya Milan kufikisha jumla ya pointi 11 na kuchupa hadi nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo unaoongozwa na Juventus.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana katika mfululizo wa ligi hiyo timu Hellas Verona ilipata ushindi mwembamba nyumbani wa bao 1-0 dhidi ya Cagliari.
Kipute cha ligi hiyo kitaendelea leo kwa michezo nan, Empoli itaumana na Palermo, Lazio dhidi ya Sassuolo, Parma itaikaribisha Genoa, Sampodoria itaialika Atalanta, wakati Udinese itaumana na Cesena.
Mechi nyingine ni kati ya vinara wa ligi hiyo Juventus na As Roma zenye pointi 15 kila mmoja zitakapochuana mjini Turin nyumbani kwa Juve, wakati Fiorentina itaumana na Inter Milan na Napoli itaikaribisha Torino.
Mtibwa kuongoza ligi leo, Yanga, JKT ni vita Taifa
Mtibwa Sugar wana nafasi kubwa ya kukalia kiti cha uongozi wa Ligi Kuu msimu huu leo |
![]() |
Mgambo JKT watakubali kufanywa ngazi kwa Mtibwa Sugar leo Manungu? |
Kikosi cha JKT Ruvu kinachotarajiwa kuvaana na Yanga leo Taifa, watakuwa mdebwedo tena kama msimu uliopita? |
Yanga watakaokuwa wakijaribu bahati yao kwa JKT Ruvu leo Taifa, watacheka au kununa kama watani zao Simba? |
Mtibwa inaikaribisha Mgambo kwenye uwanja wake wa Manungu, Turiani kati ya mechi mbili zinazopigwa leo kukamilisha raundi ya tatu ya ligi hiyo, pambano jingine likiwa ni kati ya Yanga dhidi ya JKT Ruvu.
Mchezo wa Yanga na JKT Ruvu utapigwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo kila timu itahitaji kupata ushindi ili kujiweka nafasi nzuri katika msimamo kabla ya mechi zao zijazo Oktoba 18 na 19 mwaka huu.
Yanga iliyoifumua Prisons-Mbeya kwa mabao 2-1 katika mechi ya mwisho ipo katika nafasi ya 10 kwa sasa ikiporomoshwa na watani zao Simba ambao jana walilazimishwa sare nyingine ya tatu japo wanalingana pointi tatu kila mmoja, ila uwiano wa mabao unawatenganisha Simba wakiwa juu.
Mtibwa ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi sita baada ya kushinda mechi zake mbili na kuwa timu pekee mpaka sasa iliyoshinda mfululizo baada ya Azam jana kulazimishwa sare na Prisons.
Kama itashinda Mtibwa itaweka rekodi ya kushinda kwa asilimia 100 mechi zake na kukwea kileleni kwa kukusanya pointi 9, japo huenda wakata miwa hao wasipate mteremko kwa Mgambo JKt ambayo inauguza kipigo cha bao 1-0 ilichopewa na Stand United mjini Tanga katika mechi yao iliyopita.
Mtibwa inayonolewa na kocha mzawa na nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Mexime inajivunia kuwa na wachezaji vijana wenye vipaji vya soka pamoja na kuongezewa nguvu wa makongwe kama Shaaban Nditi, Mussa Mgosi na Vincent Barnabas.
Kwa Yanga itakayokuwa jijini Dar itakuwa na kazi kubwa mbele ya maafande wa JKT Ruvu wanaonolewa na beki wao wa zamani, Fred Felix Minziro kuweza kuendeleza wimbi lao la ushindi.
Baada ya kunyukwa na Mtibwa katika mechi ya kwanza mjini Morogoro, Yanga ilizinduka kwa kuilaza Prisons na leo ingependa kushinda ili kuchupa hadi kwenye Tatu Bora kwani itafikisha pointi sita na kuivuka hata Mbeya City waliopo nafasi ya tatu kwa sasa na pointi zao tano.
Cha kufurahisha Genlson Santana 'Jaja' na Coutinho, pamoja na wakali wote wa Jangwani wapo fiti na kumpa afueni kocha Marcio Maximo kupanga kikosi anachokitaka kusaka ushindi wao wa pili msimu huu.
Hata hivyo vijana wa Minziro ambao wametoka kupokea kipigo toka kwa Kagera Sugar katika mechi iliyopita hawatataka kufanywa ngazi ya kuipandisha Yanga kwenye Tatu Bora kwani wapo nafasi ya pili toka mkiani wakiwa na pointi moja tu.
Kadhalika bado wanakumbuka katika mechi za msimu uliopita walibugizwa jumla ya mabao 9-2 baada ya mechi ya kwanza kufungwa 4-1 na alipokuja kuipokea timu, Minziro alishindiliwa mabao 5-1.
Ngoja tuone mechi hizo mbili za leo zitatoa matokeo gani ambayo yanaweza kupangua msimamo wa sasa ulivyo kama unavyoonekana hapo chini;
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
P W D L F A GD Pts
01. Azam 03 02 01 00 05 01 +4 07
02. Mtibwa Sugar 02 02 00 00 05 01 +4 06
03. Mbeya City 03 01 02 00 01 00 +1 05
04. Prisons 03 01 01 01 03 02 +1 04
05.Kagera Sugar 03 01 01 01 03 02 +1 04
06.Coastal Union 03 01 01 01 04 04 00 04
07.Stand Utd 03 01 01 01 03 05 -2 04
08. Ndanda Fc 03 01 00 02 06 06 00 03
09.Simba 03 00 03 00 04 04 00 03
10.Yanga 02 01 00 01 02 02 00 03
11. Mgambo JKT 02 01 00 01 01 01 00 03
12. Polisi Moro 03 00 02 01 03 05 -2 02
13.JKT Ruvu 02 00 01 01 00 02 -2 01
14. Ruvu Shooting 03 00 01 02 00 04 -4 01
Manchester City yaifumua Aston Villa kwao
Yaya Toure akiwajibika uwanjani kabla ya kuifungia timu yake bao la kuongoza |
![]() |
Kosakosa langoni mwa Aston Villa |
![]() |
Ayaaa! Nimewekosaje |
![]() |
Kitu nyavuni bao la Toure likiwaliza Villa |
Kocha wa Villa haamini macho yake kama wanazamishwa nyumbani |
![]() |
City wakikoswakoswa na wenyeji wao |
Aguero akitafuta bao |

![]() |
Mashine isiyochoka ikielekezwa cha kufanya uwanjani kuisaidia City |
Sub ikifanyika kwa Villa |
Lampard akianza mambo yake uwanjani |


![]() |
Kun Aguero akishangilia bao la pili la Manchester City |
Magoli ya dakika 10 za mwisho za kipindi cha pili yalitosha kuwafanya watetezi hao kufikisha jumla ya pointi 14 na kukwea hadi nafasi ya pili wakiishusha Villa waliokuwa wakishika nafasi hiyo kabla ya kipigo hicho cha Manchester City.
Mabao ya washindi katika mchezo huo yaliwekwa kimiani na kiungo na Mwanasoka Bora wa Afrika, Yaya Toure dakika ya 82 kabla ya Sergio 'kun' Aguero kuongeza la pili dakika mbili kabla ya pambano hilo kumalizika.
Vikosi vilikuwa hivi:
Aston Villa: Guzan 8, Hutton 5, Senderos 6.5, Baker 7, Cissokho 6.5, Cleverley 5.5, Westwood 5, Delph 7, Richardson 7 (Grealish 71), Weimann 6 (Benteke 61, 6.5), N'Zogbia 6.5 (Bacuna 71)
Man City: Hart 6, Zabaleta 6.5, Kompany 6.5, Mangala 7, Kolarov 7, Milner 6.5, Fernandinho 5.5 (Lampard 56, 6.5), Toure 7, Silva 7 (Navas 84), Dzeko 6 (Fernando 64, 6), Aguero 7.5
Simba bado gonjwa, Azam yabanwa, Ndanda yafa Tanga
Mshambuliaji wa Simba, Amissi Tambwe akitafuta mbinu za kumtyoka mchezaji wa Stand Utd |
Yalaaa! Ndivyo Emmanuel Okwi akilalama baada ya kuchezewa vibaya na mchezaji wa Stand |
Shaaban Kisiga akifumua shuti mbele ya mchezaji wa Stand |
Elias Maguli akiwa chini sambamba na beki wa Stand United katika mechi yao iliyoisha kwa sare ya 1-1 |
Mashabiki wa Coastal wakiangalia mpira
Manahodha wa Ndanda Fc na Coastal wakisalimiana |
Kocha wa timu ya Coastal Union, Yusuf Chippo akihojiwa na wanahabari
Mashabiki wa timu ya Ndanda wakishindwa kuhamini macho yao ya
kinachotokea baada ya kubugizwa bao 2.1 na Coastal katika uwanja wa
Mkwakwani
Shabiki wa Ndanda aliyejitambulisha kwa jina la Kadio Rashidi akiwa amejichora mgongoni kuisapoti timu yao ambayo hata hivyo ililala Mkwakwani kwa mabao 2-1.
Raia wa kigeni kutoka mataifa
mbalimbali wakifatilia mpambano wa Ndanda na Coastal uliokuwa ukipigwa
katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Raia wa kigeni kutoka mataifa mbalimbali wakifatilia mpambano wa Ndanda na Coastal uliokuwa ukipigwa katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.
****
WAKATI mabingwa watetezi wakibanwa mjini Mbeya baada ya kulazimishwa suluhu na maafande wa Prisons, huku Ndanda Fc ikizamishwa uwanja wa Mkwakwani na Coastal Union kwa kufungwa mabao 2-1, hali bado si shwari kwa Simba baada ya kulazimishwa sare ya tatu mfululizo katika Ligi Kuu Tanzania Bara.
Simba ilishindwa kufurukuta mbele ya wageni wa ligi hiyo, Stand United ya Shinyanga na kutoka nao sare ya bao 1-1 ikiwa ni sare ya tatu tangu ligi ya msimu huu ianze na kuleta hali ya taharuki kwa mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kongwe.
Simba ndiyo waliyokuwa wa kwanza kupata bao kama ilivyo katika mechi zao mbili za awali dhidi ya Coastal Union na Polisi Moro baada ya kiungo Shaaban Kisiga kudhihirisha kuwa 'utu uzima' dawa kwa 'kukusanya kijiji' kabla ya kufunga bao tamu lililoifanya Simba iwe mbele.
Hata hivyo dakika za mwishoni kuelekea mapumziko wageni Stand walichomoa bao hilo na kufanya timu ziende kupumzika zikiwa nguvu sawa, hali iliyoendelea hata katika kipindi cha pili na hadi mwisho wa pambano hilo na kuiacha Simba ikikusanya pointi tatu katika mechi tatu.
Katika mechi nyingine mjini Mlandizi, Ruvu Shooting ikiwa nyumbani iliambulia pointi yake ya kwanza baada ya kulazimishwa suluhu na Mbeya City katika pambano lililochezwa uwanja wa Mabatini, Mlandizi, huku Azam wakilazimishwa sare kama hiyo mjini Mbeya na maafande wa Prisons katika uwanja wa Sokoine.
Kwenye uwanja wa Mkwakwani, Coastal Union ilizinduka katika ligi hiyo kutoka kwenye kipigo kwa kuizamisha Ndanda Fc ya Mtwara kwa mabao 2-1. Mabao ya washindi katika mechi hiyo yalifungwa na Joseph Mahundi sekunde chache baada ya pambano kuanza na jingine kupitia Hussein Sued dakika ya 26 kabla ya Ndanda kuchomoa bao moja katika kipindi cha pili kupitia Nassor Kapama.
Maafande wa Polisi Moro wakiwa uwanja wao wa nyumbani wa Jamhuri Morogoro waliambulia pointi moja baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya wageni wao Kagera Sugar. Wenyeji walianza kufunga bao kupitia Nicolaus Kabipe kabla ya Kagera Sugar kuchomoa 'jioni' kupitia Rashidi Mandawa.
Subscribe to:
Posts (Atom)