STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

Mwanamke atafunwa na Simba akifanya mapenzi vichakani


MWANAMKE mmoja ametafunwa na simba hadi kufa wakati alipokuwa akifanya mapenzi na rafiki yake wa kiume nje nchini Zimbabwe, iliripotiwa jana.

Sharai Mawera alifariki juzi baada ya simba huyo alipomshambulia ghafla wakati akifurahia kitendo hicho cha kufanya mapenzi na mpenzi wake ambaye hakutajwa kwenye kichaka.

Tovuti moja nchini humo iliripoti kwamba mnyama huyo aliwashambulia wapenzi hao kwenye eneo lililojitenga katika kichaka hicho kilicho karibu na kaskazini mwa mji wa Kariba.

Rafiki wa kiume wa Sharai, ambaye hakutajwa, inaaminika aliruka na kutimua mbio akiwa uchi wakati simba huyo alipowashambulia ghafla.

Chanzo cha habari kimoja kimeieleza tovuti hiyo kwamba mwanamke huyo alifariki dunia katika eneo la tukio.

Alisema: "Kwa bahati mbaya mwanamke aliraruriwa hadi kufa na simba huyo, lakini rafiki yake wa kiume alifanikiwa kujiokoa akiwa uchi."

Rafiki wa wapenzi hao alieleza Sharai alikuwa akifanya shughuli zake kwenye soko moja mjini humo na kwamba mpenzi wake alikuwa mvuvi.

Rafiki huyo alisema: "Ni mvuvi na kila mara alikuwa akikutana mahali hapo na rafiki yake wa kike, ambaye kwa sasa ni marehemu.

"Wawili hao walikuwa wakirukaruka wakati tukio hilo lilipotokea.

Simba huyo alitokea kwa nyuma yao na kuwarukia.

"Mwanaume huyo alifanikiwa kutoroka kabla ya kusimama mbali ambako aliweza kushuhudia mwenzi wake alivyokuwa akishambuliwa.

"Baadaye ndipo akatimua mbio kuelekea barabarani kuomba msaada."

Tovuti hiyo iliripoti kwamba mtu huyo aliyekuwa amejawa hofu alifanikiwa kutoa taarifa.

Polisi wa mji huo na askari wenye silaha kutoka Mamlaka ya Hifadhi na Udhibiti Wanyamapori ya Zimbabwe walikimbia kuelekea eneo la tukio.

Chanzo hicho kilisema: "Askari na maofisa walifikia eneo la tukio na kufyatua risasi moja kabla ya kufika eneo husika.

"Mwanamke huyo alikuwa tayari ameshauawa. Alikuwa na mikwaruzo ya damu mwili mzima. Shingo yake na tumbo vilikuwa vimetafunwa."

Walenga shabaha walianzisha msako wa simba huyo kufuatia janga hilo, huku kukiwa na taarifa kwamba mnyama huyo anawezekana kuwa ameua mkazi wa eneo hilo ambaye alitoweka mwishoni mwa wiki.

Mabaki ya mwili wa marehemu yalipatikana juzi katika mpaka wa mji huo, ambao uko karibu na Mto Zambezi.

Polisi wanaamini mtu huyo, ambaye hakutajwa jina, aliliwa na simba wakati akielekea nyumbani kutoka klabu moja ya usiku.

Gazeti la serikali la The Helard liliripoti kwamba maofisa wanaamini taarifa kwamba mwanamke huyo aliyeuawa juzi alikuwa ameng'atwa kuliko kuliwa wakieleza kwamba simba huyo huyo anawezekana kuwa alihusika na mashambulio yote mawili.

Gazeti hilo liliongeza: "Wakazi wa mji huo kwa sasa wanaishi kwa hofu huku simba wakirandaranda kwa kujiamini kufuatia ukweli kwamba bado hawajakamatwa."
EDDY

No comments:

Post a Comment