STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

Sevilla yazidi kujisongesha La Liga

http://www.number1sport.es/wp-content/uploads/2012/01/Imagen-231.pngKLABU ya Sevilla imezidi kujiweka katia nafasi nzuri ya kufuzu Ligi ya Mabingwa barani Ulaya baada ya hivi punde kupata ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya wenyeji wao Real Betis katika mfululizo wa Ligi ya Hispania.
Mabao mawili yaliyofungwa na Kelvin Gameiro moja likiwa na mkwaju wa penati yaliiwezesha Sevilla wanaojiandaa kuvaana na Valencia kwenye mechi ya Nusu Fainali ya Ligi Ndogo ya Ulaya kufikisha jumla ya pointi 56 ikisalia katika nafasi ya tano nyuma ya Athletic Bilbao.
Gamerio alifunga bao la kwanza kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 33 na kuongeza la pili kipindi cha pili kwenye dakika ya 82 kumalizia kazi ya Diogo Figueiras.
Kivumbi cha ligi hiyo kitaendelea jioni hii kwa michezo mitatu ambapo Valencia itakuwa nyumbani kuikaribisha Elche, huku Getafe itavaana na vinara wa Ligi hiyo Atletico Madrid itakayowavuata kwao na Espaniol itaikaribisha Rayo Vallecano.

No comments:

Post a Comment