STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

Liverpool, Manchester City hapatoshi leo England

Liverpool v Manchester  City kivumbi kitakuwaje leo?
Chelsea wenyewe wataanza mapema kibarua chao ugenini na Swansea City
LONDON, England
LIGI Kuu ya England (EPL) inatarajiwa kuendelea leo kwa timu zilizopo Tatu Bora zinazowania ubingwa ambao kwa sasa unashikiliwa na Mashetani Wekundu zitashuka dimbani kusaka pointi tatu za kuelekea kwenye ndoto zao kabla ligi haijafikia ukingoni mwezi ujao.
Vinara Liverpool chini ya Brendan Rodgers watakuwa dimba la nyumbani la Anfield kuialika Manchester City wanaokamata nafasi ya tatu, huku Chelsea iliyofanya maajabu kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kufuzu Nusu Fainali, itakuwa wageni kwa Swansea City.
Liverpool wanaoongoza msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 74, pointi mbili zaidi ya Chelsea na nne zaidi ya wapinzani wao watakaovaana nao Anfield na ushindi wowote kwao moja ya timu hizo ina maana msimamo mzima kwa nafasi tatu za juu utabadilika.
Pambano hilo la Anfield litawakutanisha ndugu Yaya Toure anayekipiga Manchester City dhidi ya kaka yake Koro Toure wa Liverpool, huku Luis Suarez akiangaliwa kwa jicho la ziada kuona kama atafunga bao na kuweka rekodi ya kufumania mabao mengi katika msimu mmoja.
Nyota huyo wa Uruguay amefunga mpaka sasa mabao 29, akifuatiwa kwa mbali na mchezaji mwenzake wa Liverpool, Danile Sturridge mwenye mabao 20 kisha Yaya Toure akifuatia akiwa mabao 18 matatu zaidi ya Muargentina, Sergio 'kun' Aguero.
Upande wa pili pambano la Swansea wanaokamata nafasi ya 15 katika msimamo wakiwa na pointi 33 itakuwa na kazi ngumu kuwazuia Chalsea ambao wana furaha ya kuwanyoa PSG ya Ufaransa kwa mabao 2-0 na kufuzu Nusu Fainali akiungana na timu za Bayern Munich ya Ujerumani, Real Madrid na Atletico Madrid za Hispania kuwania kucheza Fainali.
Licha ya kocha Jose Mourinho kuiponda mara kwa mara safu ya timu yake, lakini timu hiyo wiki iliyopita kwenye ligi hiyo ilipata ushindi wa kishindo wa mabao 3-0 dhidi ya Stoke City mabao yakifungwa na viungo wake, Mohammed Sallah, Willian na Frank Lampard.
Hiyo ni kuonyesha kuwa hata kama mabeki wa Swansea watawakaba vilivyo, akina Samuel Et'oo, Fernando Torres na hata Demba Ba anayetokea benchi, bado Chelsea ni nouma kwa viungo wake kufuimania nyavu, hali inayofanya mechi hiyo kusubiriwa kwa hamu.

No comments:

Post a Comment