STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

Parma chupuchupu kwa Bologna

http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Manolo+Gabbiadini+Bologna+FC+v+Parma+FC+Serie+lHGeErY1Sgpl.jpg
LIGI Kuu ya Italia Seria A imezidi kushika kasi wakati Parma ikiwa ugenini ikilazimika kupigana na kusawazisha bao dhidi ya vibonde, Bologna na kuambulia pointi moja kwa kutoka sare ya bao 1-1.
Bao la dakika ya 79 lililofungwa na Raffaele Palladino liliisaidia kuikoa Parma kuaibika kwa Bologna walioonekena kuelekea kushinda katika mechi hiyo.
Wenyeji walitangulia kupata bao dakika ya 44 kupitia kwa Nicolo  Cherubin akimalizia kati pande la Mgiriki Lazaros Christodoulopoulos.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo zilizochezwa jana Sassuolo na Cagliari zilitoshana nguvu ya kutoka sare ya 1-1, huku Roma ikitamba nyumbani dhidi ya Atalanta kwa kuikandika mabao 3-1.
Ligi hiyo itaendelea tena leo nchini huyo kwa michezo kadhaa; ambapo  Livorno itaumana na Chievo, Hellas Verona itaikaribisha Fiorentina, huku Torino wakiialika Genoa wakati Sampdoria itaumana na Inter Milan, huku Napili na Lazio zenyewe zitapimana ubavu na AC Milan itaikaribisha Catania.

No comments:

Post a Comment