STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

Demba Ba aibeba tena Chelsea, yashinda ugenini

Demba Ba of Chelsea celebrates after scoring against Swansea.
Demba Ba akimshukuru Mungu baada ya kuifungia Chelsea bao dhidi ya Swansea muda mfupi uliopita

Chelsea's Eden Hazard and Swansea's Jose Canas
BAO pekee lililofungwa na Demba Ba limeiwezesha Chelsea kuzidi kuisogelea Liverpool katika mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya England baada ya kuifunga Swansea City ikiwa kwao bao 1-0.
Msenegal huyo aliyeivusha Chelsea kwenye Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya PSG aliyeanzishwa katika pambano hilo alitumbukiza wavuni bao hilo dhidi ya Swansea katika dakika ya 68 akimalizia kazi nzuri ya Nemanja Matic na kuwachambua mabeki wa Swansea kabla ya kufumua shuti kali lililoenda kimiani.
Wenyeji wa mchezo huowalijikuta wakicheza pungufu kwa muda mrefu baada ya beki wao Chico kutolewa mapema kwa kuonyeshwa kati ya pili ya njano dakika ya 16 ikiwa ni dakika mbili tangu aonyeshwe ya kwanza na kuifanya timu yake ipate pengo lililotumiwa vyema na vijana wa Jose Mourinho kuibuka na ushindi.
Ushindi huo wa Chelsea umeifanya ifikishe pointi 75, mbili pungufu na ilizonazo vinara wa ligi hiyo, Liverpool iliyoitia adabu Manchester City mapema leo katika pambano lililochezwa katika uwanja wa Anfield.

No comments:

Post a Comment