STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

Vita ya kushuka daraja nouma


Mgambo JKT
Ashanti United
BAADA ya Azam kupata ushindi wa mabao 2-1 na kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara bila kupoteza mchezo wowote, huku Yanga ikishinda mjini Arusha kwa idadi kama hiyo, vita kwa sasa ipo kwa timu zilizopo mkiani, baada ya Mgambo JKT leo kulazimishwa suluhu kwenye uwanja wa Mkwakwani na Kagera Sugar na kuwafanya wasipumue vyema.
Sare hiyo imeifanya timu hiyo kufikisha pointi 26 moja zaidi ya timu za Ashanti United iliyoinyoa Simba jijini Dar es Salaam na Prisons iliyoishusha daraja Rhino Rangers mjini Mbeya jana kwa kuilaza mabao 4-3 ambazo kila moja ina pointi 25 baada ya mechi 25 kwa kila timu.
Timu mojawapo kati ya hizo zitaungana na Rhino Rangers na Oljoro JKT iliteremsha leo kurudi Ligi Daraja la Kwanza na Mabingwa watetezi Yanga kwa kufungwa 2-1 kuzipisha timu za Polisi Moro, Ndanda Fc ya Mtwara na Stand United ya Shinyanga zilizopanda Ligi Kuu kwa msimu ujao.
Mechi za Jumamosi hasa inayozikutanisha AShanti United na Prisons mjini Morogoro ndiyo inayosubiriwa kwa hamu kuona inakuwaje kwa timu hizo zilizorejea ligi kuu kwa misimu miwili tofauti.
Pia kama Simba itaendelea kutoa takrima kwa wapinzani wake kuna uwezekano ikajikuta ikitolewa kwenye nafasi ya nne iliyoikalia kwa muda mrefu kutokana na Kagera Sugar na Ruvu Shooting kuonekana kuinyemelea nafasi hiyo nyuma yao.
Hapa chini ni msimamo kamili baada ya mechi za leo za ligi hiyo;

                            P     W      D     L     F      A         D      Pts
1.Azam              25     17     8     0     50     15     +35     59    
2.Yanga              25     16     7     2     60     18     +42     55    
3.Mbeya City    25     12     10   3     32     20     +12     46    
4.Simba             25      9      10    6     40     26     +16     37    
5.Kagera Sugar 25      8      11    6     22     20     +2       35    
6.Ruvu Shooting25     9      8      8     26     32      -6       35    
7.Ruvu Stars     25     10     1     14     23     39     -16     31
8.Mtibwa Sugar25      7      9       9      29     30     -1      30
9.Coastal Union25     6      11     8      16     19     -3      29
10.JKT Mgambo25    6       8     11     18     34     -16    26    
11.Prisons          25     5     10    10     25     33     -8      25    
12.Ashanti Utd   25     6     7      12     20     38     -18    25    
13.JKT Oljoro    25     3     9     13     18     36     -18     18    
14.Rhino Rangers25    3     7     15     18     37     -19     16    

No comments:

Post a Comment