STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

Liverpool yaikwanyua Man City 3-2

Philippe Coutinho scores Liverppol's winner against Manchester City
Coutinho akiifungia Liverpool bao la ushindi dhidi ya Manchester City
UZEMBE uliofanywa na Nahodha Vincent Kompany umeiwezesha Liverpool kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 na kuzidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England.
Nahodha huyo alishindwa kuondosha vyema mpira uliokuwa umeelekezwa lango mwake katika dakika ya 78 wakati matokeo yakiwa 2-2 na Philippe Coutinho kuukwamisha kimiani.
Liverpool waliwaendesha puta wageni wao kwa kutangulia kufunga mabao mawili ya haraka moja likifungwa na Raheem Sterling dakika ya sita akimalizia pasi ya Luis Suárez kabla ya Martin Skrtel kuongeza la pili akimalizia kazi ya Steven Gerrard dakika ya 26.
Mabao hayo yalidumu hadi wakati wa mapumziko kabla ya kipindi cha pili mabadiliko yaliyofanywa na kocha Manuel Pellegrini kumuingiza James Milner ilibadilika na kurejesha mabao hayo.
David Silva alifunga bao la kwanza dakika ya 57 akimalizia krosi pasi ya Milner kabla ya mchezaji huyo kufumua shuti kali dakika ya 63 na kumgonga Glen Johnson na kumpoteza maboya kipa wake na kufanya matokeo kuwa 2-2 bla ya Coutinho kuwapa uongozi Liver na kuwafanya wafikishe pointi 77 baada ya mechi 34.
Manchester City waliokuwa wakihitaji angalau sare kuweza kuweka hai matumaini ya kunyakua taji hilo, wakisaliwa na pointi 70 baada ya kucheza mechi 32.
Muda mfupi ujao Chelsea watakuwa ugenini kuumana na Swansea City katika mechi nyingine ya ligi hiyo ya England.
Katika mchezo huo Liverpool ilimpoteza Jordan Henderson alionyeshwa kadi nyekundu dakika chache kabla ya pambano hilo kumalizika.

No comments:

Post a Comment