STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

Real Madrid yaua, Barca ikipigwa na vibonde La Liga

Gareth Bale aliifungia Real Madrid bao la pili dhidi ya Almeria

REAL Madrid usiku wa jana ilikwea hadi nafasi ya pili wakiwashusha wapinzani wa Barcelona baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Almeria, huku Barca wenyewe wakifa kwa bao 1-0 dhidi ya timu chovu ya Granada katika Ligi ya Hispania.
Angel di MarĂ­a alianza kuandika karamu ya mabao ya wenyeji ambao wametoka kutinga Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya wakitarajiwa kuvaana na watetezi Bayern Munich kwa kufunga bao la kwanza katika dakika ya 28 na kudumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili Gareth Bale aliiandikia Real Madrid bao la pili dakika ya 53 akimalizia kazi nzuri ya Mfaransa Karim Benzema kabla ya Benzema kumpa pande Isco dakika tatu baadaye na kuandika bao la tatu na dakika tano kabla ya pambano hilo kuisha Alvaro Morata alihitimisha karamu kwa kufunga bao la nne kwa kazi ya Illarramendi na kuwafanya Madrid kufikisha pointi 79 na kulingana na vinara Atletico Madrid ambao watashuka dimbani leo kuumana na Getafe kwa kutofautiana uwiano wa mabao na kufunga na kufungwa.'
Barcelona waliokuwa wakishikilia nafasi ya pili wameshuka hadi ya tatu wakiwa na pointi 78 kutokana na kulazwa bao 1-0 na Granada uwanja wa ugenini kwa bao la mapema la Yacine Brahim.
Nazo timu za Osasuna na Real Vallodolid zilishindwa kutambia juzi kwa kutofungana, huku Celta Vigo ikiwa nyumbani kwao walilazimishwa sare ya mabao 2-2 na Real Sociedad na Levante ikafa ugenini kwa bao 1-0 dhidi ya Villarreal.

No comments:

Post a Comment