STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 13, 2014

Arsenal yaivua ubingwa Wigan, yatinga Fainali za FA









KLABU ya Arsenal imetinga Fainali ya Kombe la FA baada ya kuwavua taji waliokuwa mabingwa watetezi Wigan Athletic kwa kuitupa kwenye hatua ya Nusu Fainali kwa mikwaju ya penati 4-2 kufuatia sare ya bao 1-1 ndani ya dakika 120 katika pambano kali lililochezwa uwaja wa Wembley.
Arsenal sasa itasubiri kujua inacheza na nani kati ya timu ya Hull City na Sheffield United katika mechi ya Fainali itakayochezwa Mei 17 kwenye uwanja huo huo maarufu uliopo London.
Kutinga huko kwa Arsenal kumewapa faraja wa kukata kiu ya muda mrefu bila klabu hiyo kunyakua taji lolote tangu walipotwaa taji la FA mwaka 2005.
Timu ya Wigan iliyotwaa taji hilo mwaka jana kwa kuilaza Manchester City, ilikuwa wa kwanza kuandika bao katika dakika ya 63 kupitia Jordi Gomez aliyefunga kwa penati kufuatia Per Mertesacker kumuangusha Callum McManaman.
Mjerumani huyo hata hivyo alisahihisha makosa yake kwa kuisawazishia Arsenal bao zikiwa zimesalia dakika nane kabla ya mchezo huo kumalizika na timu hizo kuongezewa dakika 30 zilizoisha patupu na kufuatiwa na hatua ya kupigiana mikwaju ya penati.
Kipa Lukasz Fabianski alikuwa shujaa kwa kuokoa penati mbili za awali za Wigan zilizopigwa na Caldwell na Collison huku  Mikel Arteta, Källström, Olivier Giroud na Santi Cazorla kuzamisha zao wavuni dhidi ya mbili za Wigan zilizofungwa na Beausejour na McArthur.

No comments:

Post a Comment