STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 13, 2013

Mashali amtwanga Mkenya na kutetea taji la EAC

Mashali (kulia) akimshambulia Mackoliech katika pambano lao la usiku wa jana
Mwamuzi Mark Hatia akizungumza na Mashali baada ya kumtwanga kwa konde lililomuangusha Mkenya sakafuni
 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela akimvisha taji la ubingwa bondia Thomas Mashali baada ya kumtwanga kwa KO, Mkenya Benard Mackoliech.
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali, jana usiku aliendeleza rekodi yake ya 'kutopigika' baada ya kumnyuka kwa KO, Mkenya Benard Mackoliech na kutetea taji lake la Afrika Mashariki na Kati.
Mashali anayefahamika kama 'Simba Asiyefugika' alipata ushindi huo katika raunsi ya sita katika pambano hilo la uzito wa kati lililokuwa la raundi 10 lililofanyika kwenye ukumbi wa Friends Corner, Manzese jijini Dar es Salaam.
Mtanzania huyo tangu raundi za awali alionyesha dhamira yake ya kushinda pambano hilo kwa namna alivyokuwa akimpeleka puta mpinzani wake, japo Mackoliech alionyesha ubishi kabla ya kusalimu raundi ya sita.
Mwamuzi wa pambano hilo Mark Hatia, alilazimika kulimaliza pambano hilo katika raundi hilo baada ya kumhesabia Mkenya huyo baada ya kupigwa konde zito lililompeleka sakafuni na kushindwa kuinuka na kumpa ushindi Mashali.
Mara baada ya pambano hilo lililokuwa limeandaliwa na Promota Aisha Mbegu na kusimamiwa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBO, Mashali alivishwa mkanda wake na aliyekuwa mgeni rasmi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela.
Kenyela alimwagia sifa Mashali kwa kuipeperusha vema bendera ya Tanzania pamoja na kuwasifia waratibu wa pambano hilo lililosindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi iliyowasisimua mashabiki waliofurika ukumbini hapo.
Ushindi huo wa Mashali umemfanya afanikiwe kuendelea kulishikilia taji hilo la Afrika Mashariki na Kati alilotwaa Oktoba 14 mwaka jana kwa kumshinda kwa pointi bondia toka Uganda, Med Sebyala.
Pia imemfanya aendeleze rekodi yake ya kutipoteza mchezo wowote mpaka sasa tangu alipotumbukia katika mchezo huo wa ngumi za kulipwa mwaka 1999.

Mgosi atuliza 'mzuka' JKT Ruvu, aanza kujifua nao

Mussa Hassani Mgosi

KIUNGO mshambuliaji nyota wa zamani wa Simba, Mussa Hassani Mgosi amewatuliza mashabiki wa timu anayoichezea kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, JKT Ruvu baada ya kutua na kuanza rasmi mazoezi.
Mgosi, alianza kuwapa hofu mashabiki na benchi la ufundi la JKT baada ya kutoweka nchini kwenda China kushiriki michuano maalum, huku kukiwa hakuna taarifa zake za kurejea wakati kikosi cha timu yake kikiwa kimeshaanza mazoezi.
Mfungaji Bora huyo wa zamani wa Ligi Kuu, alijiunga na wenzake kufanya mazoezi jana kwenye uwanja wa Mlalakuwa inapojifua timu yake hali iliyomfanya kocha wake, Charles Kilinda kutabasamu.
Kocha huyo alisema kurejea kwa Mgosi kumempa faraja kwani amepanga kumtumia katika mechi za mzunguko wa pili wa ligi hiyo inayotarajiwa kuanza rasmi Januari 26.
Kilinda alisema uwepo wa Mgosi pamoja na ushirikiano wa wachezaji wengine inamfanya aamini JKT Ruvu itafanya vema kwenye duru lijalo na kutimiza ndoto zao za kuwa miongoni mwa timu zitakazokuwa kwenye 'Nne Bora'.
Mgosi alishindwa kuitumikia kikamilifu timu yake hiyo katika duru la kwanza kutokana na kuchezwa kuletwa kwa ITC yake kutoka timu ya DC Motema Pembe ya DR Congo aliyokuwa akiichezea baada ya kuondoka Simba.
Mara baada ya duru la kwanza kumalizika, Mgosi alitimka China kushiriki michuano maalum iliyohusisha wachezaji kutoka nchi za Afrika, ambapo mkali huyo aliongoza kwa ufungaji mabao katika michuano hiyo.

Mwisho

Saturday, January 12, 2013

Mbio za uchaguzi mkuu wa TFF kuanza rasmi J'3

Deo Lyatto katika majukumu yake ya Uenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF

KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la soka nchini TFF, jana ilitangaza kuzindua rasmi mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa Shirikisho hilo na kutoa fulsa kwa wadau wa soka kuchukua fomu za kuomba kugombea uongozi ndani ya shirikisho hilo.
Uchaguzi mkuu wa TFF umepangwa kufanyika Februari 24 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa kamati hiyo Deogratias Lyatto, alisema kuwa fomu kwa ajili ya kuomba kuwania uongozi wa TFF zitaanza kutolewa Jumatatu, Januari 14 ambapo zitatakiwa kurudishwa kabla ya Januarui 18.
Lyatto alisema kuwa mbali na kuanza rasmi mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa TFF, pia kamati yake imezindua rasmi mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa bodi itakayoendesha ligi kuu Tanzania bara (TPL- Board).
Lyatto alisema kuwa katika uchaguzi wa TFF, nafasi zitakazogombewa ni pamoja na Rais wa TFF, Makamu wa Rais pamoja na nafasi 13 za wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo ambazo zimepangwa katika kanda.
Pia alisema kuwa kwa upande wa Bodi ya TPL, nafasi zitakzogombewa ni Mwenyekiti wa Bodi, Makamu Mwenyekiti pamoja na wajumbe wawili wa bodi hiyo kutoka katika klabu za ligi daraja la kwanza.
Lyatto alisema kuwa kwa nafasi ya Mwenyekiti na makamu wake wa bodi ya ligi kuu ni lazima wawe wenye viti wa klabu za ligi kuu zilizoshika nafasi ya kwanza mpaka ya sita msimu uliopita.
"Kwa wajumbe wa bodi ni lazima wawe wenyeviti wa klabu za ligi daraja la kwanza ambao wote hao pamoja na mwenyekiti na makamu wake wa bodi lazima wapigiwe kura na vilabu," alisema Lyatto.
Alisema kuwa moja ya sifa za kugombea uongozi TFF na katika kamati ya ligi ni lazima mgombea awe na elimu isiyopungua kidato cha nne isipokuwa kwa nafasi ya Rais na Makamu wa Rais wa TFF ambapo atatakiwa kuwa na kiwango cha elimu kisichopungua Shahada ya Chuo Kikuu na awe na uwezo na haiba ya kuiwakilisha TFF ndani na nje ya nchi.
Pia sifa nyingine ni lazima mgombea awe na uzoefu wa uendeshaji wa mpira wa miguu uliothibitishwa kwa angalau miaka mitano na pia asiwe na hatia yoyote ya kosa la jinai na awe amewahi kua ama mchezaji wa mpira wa miguu, Kocha, mwamuzi au kushiriki katika uendeshaji wa mpira wa miguu katika ngazi ya mkoa.
Lyatto alisema kuwa ada ya uchukuaji fomu kwa upande wa Rais wa TFF ni Sh. 500,000, Makamu Rais ni Sh. 300,000 wakati wajumbe wa kamati ya utendaji ya TFF ni Sh. 200,000.
Kwa upande wa bodi ya ligi kuu Mwenyekiti na Makamu wake watachukua fomu kwa Sh. 200,000 wakati wajumbe wa bodi hiyo watachukua fomu kwa Sh. 100,000.
Lyatto alisema kuwa wadau wa soka wenye sifa wabnaruhusiwa kujitokeza kuchukua fomu kuwania uongozi katika chaguzi hizo.
Aidha, alisisitiza wadau wa soka kuwa makini katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi wa TFF.

Kitale azidi kumlilia Sharo Milionea

Kitale katika pozi zake matata

Kitale akiwa na Sharo Milionea katika moja ya kazi walizowahi kuzifanya pamoja
MSANII wa fani ya maigizo na muziki, Mussa Yusuf 'Kitale' amesema itamchukua muda mrefu kumsahau swahiba wake, Hussein Mkiety 'Sharo Milionea' kwa namna walivyokuwa wamezoeana na kufanya kazi pamoja.
Alisema namna rafikiye alivyofariki ghafla huku wakiwa wamejipanga kufanya mambo kadhaa ya kimaisha na kisanii ndiyo yanayomfanya kila mara kukumbwa na jinamizi la kumlilia Sharo, aliyefariki kwa ajali ya gari akielekea Tanga.
Alisema yeye na Sharo walikuwa zaidi ya marafiki, ndiyo maana analizwa na kifo cha msanii huyo aliyekuwa akizidi kupaa kwa umaarufu kwa 'swaga' zake za 'Ooh Mamaaaa', 'Kamata Mwizi Meen', 'Umebugi Meen' na nyingine.
"Ni vigumu kumsahau Sharo Milionea, alikuwa zaidi ya rafiki...kibaya zaidi tulikuwa na mambo mengi tumeyapanga kuyafanya ambayo baadhi tulishayaanza na mengine ndiyo hivyo yameishia njiani," alisema Kitale.
Kitale alisema kwa sasa anafanya mipango ya kuachia kazi mbili alizozifanya na Sharo filamu iitwayo 'Impossible' na wimbo uitwao 'Hili Toto'.

Rooney kuwakosa Liverpool kesho Uingereza

Mshambuliaji nyota wa Manchester United, Wayne Rooney



LONDON, England
MFUMANIA nyavu mahiri wa Manchester United,  Wayne Rooney kesho ataukosa mchezo Ligi Kuu ya England dhidi ya Liverpool baada ya kushindwa kupona jeraha lake la kifundo cha mguu amesema kocha wa timu hiyo Alex Ferguson.
Rooney aliumia kwenye mazoezi na kukosa michezop yote ya kipindi cha sikukuu dhidi ya Newcastle United, West Bromwich Albion na Wigan Athletic pamoja na mchezo waliotoka sare wa kombe la FA dhidi ya West Ham United.
"Wayne Rooney bado ataendelea kuwa nje ya uwanja ," Ferguson aliwaambia waandishi wa habari. "Natumaini leo ataanza mazoezi mepesi kwa maana hiyo hatachukua muda mrefu kuanzia sasa kurejea uwanjani. Sidhani kama hilo ni tatizo lakini tutakiwa kimlinda.
"Nategemea atakuwa tayari kurejea uwanjani kwenye mchezo wetu wa Jumatano wa marudiano (Dhidi ya West Ham).
Winga Nani na kiungo  Anderson wote wanarejea kikosini kuwakabili Liverpool kwenye uwanja wa Old Trafford.
"Nani ameanza mazoezi na atajumuishwa kwenye kikosi kwa ajili ya mchezo wa Jimapili (kesho).
"Anderson amerejea mazoezini kwa siku kumi sasa hivyo atakuwepo kikosini kwa ajili ya mchezo wa Jumapili. Lakini yote kwa yote tupo katika hali nzuri na ni vizuri kuwa nao kikosini wote.
United wanaongoza ligi kwa tofauti ya pointi saba nyuma ya majirani zao Manchester City baada ya kucheza michezo 21 na wapo mbele kwa pointi 14 dhidi ya Liverpool wanaoshika nafasi ya nane.
Furgeson alisema kuwa upinzani na Liverpool aubadiliki na siku zote mchezo dhidi yao (Liverpool) ni muhimu kwa kuwa unavuta hisia za mashabiki.

Golden Bush Veterani, Wahenga hapatoshi leo TP Sinza


Kikosi cha Golden Bush Veterani

TIMU ya soka ya Golden Bush Veterani, leo inatarajiwa kushuka dimbani kupepetana na wapinzani wao, Wahenga Fc ikitaka kulipiza kisasi cha kipigo ilichopewa na wapinzani wao hao katika mechi ya kuuaga mwaka 2012.
Golden Bush, ilikumbana na kipigo cha aibu kwa kunyukwa mabao 4-3, licha ya kuchezesha nyota kadhaa wa zamani wa timu za Simba, Yanga na Mtibwa Sugar na waliomba mechi hiyo ya marudiano ichezwe leo kama mechi ya kuukaribisha mwaka mpya wa 2013 na kusherehekea miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Pambano hilo linalosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka wa maeneo ya Sinza na vitongoji vyake kutokana na vijembe vilivyokuwa vimetawala tangu baada ya mechi ya awali iliyochezwa wiki mbili zilizopita na Wahenga kuwazidi maarifa wenzao na kulipa kisasi cha kipigo walichowahi kupewa na wapinzani wao hao.
Wahenga walinyukwa mabao 4-2 katika pambano lililochezwa katikati ya Oktoba, wiki moja baada ya kutoka sare ya baoa 1-1 katika mechi zote zilizochezwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa TP Sinza.
Pande mbili za timu hizo wamekuwa wakitambiana kwamba leo ndio mwisho wa mzizi wa fitina, Golden Bush wakiapa lazima warejeshe kipigo hicho walichopewa na Wahenga walichokilalamikia kilichangiwa na maamuzi ya 'kimamluki' yaaliyokuwa yakifanywa na mwamuzi, Ally Mayay Tembele.
Mlezi wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema kuwa kikosi chao kimejiandaa vya kutosha kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa majira ya jioni kwenye uwanja wa TP, huku akiwahimiza mashabiki wajitokeze kwa wingi kushuhudia watakavyoishindilia mabao Wahenga.
"Tutakachofanya leo ni kujumlisha idadi ya mabao tuliyofungana mechi iliyopita, yaani 4+3 na idadi yake ndiyo ambayo Wahenga watakavyobeba kipigo hicho, tupo fiti na mie mwenyewe natarajia kusaidia safu ya mashambulizi kwa sababu jamaa wamechonga sana baada ya kutuotea Desemba 31," alisema Ticotico.

Hatari katika lango la Wahenga, Golden Bush siku walipotoka sare ya bao 1-1. Je leo nani atakayecheka au kulia?

Azam bila Kipre Tchetche kuivaa Tusker leo Zanzibar

Kikosi cha mabingwa watetezi wa Kombe la Mapinduzi, Azam Fc
Kikosi cha mabingwa wa Kenya, Tusker

TIMU ya soka ya Azam inatarajiwa kuvaana na Tusker ya Kenya katika pambano la fainali za michuano ya Kombe la Mapinduzi bila ya mshambuliaji wake nyota, Kipre Tcheche, ingawa inafurahia kurejea kwa kiungo wao, Abdulhalim Humud 'Gaucho'.
Azam ambao ni mabingwa watetezi wa michuano hiyo, itaumana na Tusker katika pambano litakalofanyika kwenye uwanja wa Amaan, Zanzibar, huku uongozi wa klabu hiyo ukitamba umejipanga kutetea taji hilo licha ya kukiri itakuwa mechi itakuwa ngumu.
Mabingwa hao watetezi walipata nafasi hiyo kwa kuing'oa Simba katika mechi ya fainali kwa mikwaju ya penati 5-4 baada ya kutoka sare ya 2-2 katika muda wa dakika 120 wakati Tusker walifuzu juzi kwa kuilaza Miembeni kwa mabao 2-0.
Azam itashuka dimbani bila ya nyota wake Kipre Tchetche aliyeumia katika pambano dhidi yao ya Coastal Union, japo karibu kikosi chake chote kipo imara hasa baada ya kurejea kwa kiungo nyota, Abdulhalim Humud 'Gaucho'.
Afisa Habari wa Azam, Jafar Idd 'Mbunifu' alisema kurejea kwa Humud kumewapa faraja na matumaini makubwa ya kutetea ubingwa huo walioutwaa mwaka jana kwa kuilaza Jamhuri ya Pemba mabao 3-0.
Idd alisema licha ya kutarajia kupata upinzani mkubwa kutoka kwa Tusker aliokiri ni moja ya timu ngumu isiyotabirika, lakini wamejipanga kutetea ubingwa wao kwa mara ya pili mfululizo.
"Kwa kweli tumejipanga vema, japo hatutakuwa na Kipre Tchetche aliye majeruhi, lakini kocha John Stewart Hall amemuita Humud aliyepona ambaye ameshatua mjini hapa tayari kwa pambano hilo la kesho (leo) dhidi ya Tusker," alisema Idd.
Kwa mujibu wa rekodi za michuano hiyo ni Yanga pekee iliyowahi kutetea taji kwa kulitwaa mara mbili mfululizo, ilivyofanya hivyo mwaka 2004 na 2005, wakati miaka mingine yote kila anayetwaa taji hilo hushindwa kulitetea.
Mabingwa waliopita wa michuano hiyo ni;
2003-Mtibwa Sugar
2004-Yanga SC
2005-Yanga SC
2006-Simba SC
2007-Yanga SC
2008-Simba SC
2009-Miembeni FC
2010-Mtibwa Sugar
2011-Simba FC
2012-Azam FC
2013   ???

TAIFA STARS HOI ETHIOPIA YAPIGWA 2-1 NA WAHABESHI


Na Boniface Wambura, Addis Ababa
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imepoteza mchezo wa kirafiki dhidi ya Ethiopia uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Addis Ababa hapa mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Mechi hiyo iliyochezeshwa na Bamlak Tesema wa Ethiopia ilikuwa ya kusisimua, hasa kutokana na timu zote kucheza kwa kasi kwa muda wote. Wenyeji Ethiopia ndiyo walioanza kupata bao dakika ya 13 lililofungwa na Fuad Ibrahim akiwa wastani wa hatua sita kutoka kwa mlinda mlango Juma Kaseja wa Taifa Stars.
Bao hilo liliweza kumudu hadi timu hizo zilipoenda mapumziko licha ya kuwepo kwa kosa kosa za hapa na pale.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kama kilivyokuwa cha kwanza, huku Ethiopia wakiwa wamefanya mabadiliko kwa wachezaji watano. Tanzania ilifanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 50 likifungwa na Mbwana Samata baada ya kumzidi maarifa beki mmoja wa Ethiopia.
Bao la ushindi kwa Ethiopia lilifungwa kwa kichwa dakika ya 69 na mshambuliaji Shemelis Bekele aliyeingia kipindi cha pili akiunganisha mpira wa krosi uliopigwa na winga Yossuf Sallah kutoka upande wa kushoto.
Taifa Stars inarejea nyumbani leo (Januari 12) ambapo itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 7 kamili mchana kwa ndege ya Ethiopian Airlines.
Katika pambano hilo Stars iliwakilishwa na kikosi kifuatacho;
Taifa Stars: Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Issa Rashid, Shomari Kapombe, Aggrey Morris, Amri Kiemba, Mrisho Ngasa, Salum Abubakar, Thomas Ulimwengu/Khamis Mcha, mwinyi Kazimoto na Mbwana Samata.

OMBAOMBA FEKI ATIMKA BAADA YA KUGUNDULIKA SIO MLEMAVU


Baada ya kugundua wananchi wamemshtukia baada ya kumhoji maswali na kushindwa kujibu aliamua kutimua mbio kukwepa kamera ya Francis Godwin isimpate picha yake, kama unavyomuona hapo mdau mguu gafla umetokea kimiujiza pamoja na mkono, yote hiyo alikuwa ameificha kwa kutumia koti lake na Suruali alizovaa. 
Baada ya hali kuwa tete alijikuta anazisaha umpaka kandambili zake, kama unavyoziona. 
Huyu ni omba omba anayeigiza kutokuwa na mkono mmoja na mguu Mmoja akiwa amekaa eneo la M.R Iringa mjini akisubiri kuomba chochote kutoka kwa wapita njia leo.

ULE usemi wa wahenga kuwa ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Firauni, ulitimia katika eneo la M.R,  mjini Iringa baada ya wananchi waliokuwepo eneo hilo kupigwa na butwaa baada ya ombaomba marufu anayefahamika kama Mzee Janja anayeshinda katika eneo hilo akijifanya mlemavu aliyekuwa na mkono na mguu mmoja mmoja, kutimua mbio kukwepa kamera ya mapaparazi mjini humo.
Tukio hilo limetokea majira ya saa 8 mchana baada ya kamera ya mtandao wa Francis Godwin kufika eneo hilo la kushuhudia umati wa wananchi wakiendelea kumpa fedha Mzee Janja, ambaye walikuwa wakidhani ni mlemavu wa viungo, na anayeongea kwa tabu..
Hata hivyo baada ya mmoja kati ya wananchi kufika eneo hilo alionyesha kufichua mbinu hiyo chafu ya mzee huyo kujifanya ni mlemavu wakati asubuhi alikutana nae maeneo ya mjini akiwa mzima wa afya njema na katika kumhoji zaidi ndipo kamera ya mtandao huo ilipoamua kufanya kazi yake ya kunasa kituko hicho na ndipo mzee huyo alipoanza kuongea kwa sauti vizuri tofauti na alivyokuwa akijifanya kuwa hawezi kuongea kabisa (bubu)

Wakati mabishano yakiendelea eneo hilo ghafla mzee huyo alisimama kwa miguu yake yote miwili pamoja tofauti na  awali alivyokuwa akijifanya ni mlemavu asiye na mguu mmoja ila baada ya watu kutaka apigwe picha ndipo mzee huyo alipoanza kutimua mbio huku ulemavu aliokuwa nao akiusahau hapo pamoja na kandambili zake na hakuna mtu aliyeweza kumfukuza na kufanikiwa kumkuta.

Baadhi ya wananchi wameuomba uongozi wa Manispaa ya Iringa kuwabana omba omba hao ambao wamekuwa wakidanganya watu kuwa wao ni walemavu kumbe ni wazima na kutaka kuwepo kw

THOMAS MASHALI, MKENYA KUMALIZA UBISHI LEO JIJINI DAR


Bondia  Benard Mackoliech wa Kenya akipimwa afya na Dk Madorina
Mabondia Thomas Mashali na Bernad Mackoliech wa Kenya wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito jana Dar es Salaam.


MABONDIA Thomas Mashali wa Tanzania na Mkenya Benard Mackoliech, leo wanatarajiwa kumaliza ubishi baina yao watakapopanda kwenye ulingoni kupigana kuwania ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati.
Mgeni rasmi katika pambano hilo la uzani wa kati litakalokuwa la raundi 10 anatarajiwa kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela pamoja na kuhudhuriwa pia na wabunge Idd Azan na John Mnyika.
Pambano hilo litafanyika kwenye ukumbi wa Friends Corner, Manzese Dar es Salaam na litasindikizwa na michezo minne ya utangulizi itakayowahusisha mabondia nane watakaoumana katika mapambano ya raundi nane nane.
Mratibu wa pambano hilo, Aisha Mbegu na Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa nchini, TPBO, Yasin 'Ustaadh' Abdallah, walisema kuwa maandalizi ya mapambano hayo yamekamilika na kuwahimiza mashabiki wa mchezo huo kujitokeza kwa wingi kuungana na wazanzibar kuadhimisha miaka 49 ya Mapinduzi.
Mabondia hao wanakutana kwa mara ya kwanza na Mashali atakuwa akitetea taji lake alilolitwaa Oktoba 14 mwaka jana kwa kumshinda kwa pointi Mganda Med Sebyala.

Wednesday, January 9, 2013

Chipolopolo aanza kusuka kundi lake

Chipolopolo katika pozi

MUIMBAJI wa zamani wa kundi la King's Modern Taarab, Mwanahawa Ally 'Mwanahawa Chipolopolo', ameanza kulisuka kundi lake la miondoko hiyo aliloliunda hivi karibuni baada ya kupata mfadhili aliyempa vyombo vya muziki.
Pia msanii huyo amekanusha kumnyakua wasanii waliodaiwa kujiengua katika kundi lake la zamani wa King's Modern, kwa kile alichodai hataki ugomvi na 'bosi' wake wa zamani wala kutaka wasanii wenye majina makubwa.
Akizungumza na MICHARAZO jana, alisema kundi lake linaloendelea kujifua kabla ya kutoa burudani, linaundwa na wasanii kadhaa wasio na majina makubwa lakini wenye vipaji vya hali ya juu katika muziki.
Msanii huyo aliwataja baadhi ya wasanii wanaounda kundi lake hilo lenye maskani yake Keko kuwa ni Haruna Hassani 'Bonge la Bwana', Kuruthumu Akida, Mwajuma Abdalla na Rehema 'Mtu Mzima Dawa ambao ni waimbaji.
Msanii huyo aliongeza hata taarifa kwamba wamewanyakua baadhi ya wasanii wenzake wa zamani wa Kings Modern waliodaiwa kulihama kundi hilo, sio za kweli kwa sababu hana mpango wa kunyakua msanii yeyote mwenye jina kubwa.
"Hakuna msanii hata mmoja mwenye jina aliyetua kwangu, wala sijamnyakua msanii aliyetoka Kings Modern au kokote kule kunakotajwa kuna wasanii wakali," alisema.






Dogo Muu ‘Siwezi Kushukuru’

Dogo Muu (kulia) akiwa na Dogo Aslay


MSANII chipukizi kutoka kituo cha Mkubwa na Wanae, Muharami Kajonjo 'Dogo Muu' anatarajiwa kuachia kazi mbili tofauti, moja ikiwa 'audio' ya wimbo wake mpya wa 'Nashukuru' na video ya kibao chake kiitwacho 'Siwezi'.
Meneja wa msanii huyo, Said Fella, aliiambia MICHARAZO kuwa wameamua kutoa 'audio' na video kwa lengo la kuwapa burudani mashabiki wa msanii huyo ambaye wanajiopanga ili kumtambulisha rasmi katika ulimwengu wa muziki.
Fella, alisema katika wimbo wa 'Nashukuru'. Dogo Muu ameimba pamoja na msanii nyota aliyetoka kuwania tuzo za Kora Africa, Dogo Aslay.
"Tupo katika maandalizi ya kutoa kazi za msanii wetu mpya, Dogo Muu, tutatoa nyimbo zake mbili katika mfumo wa 'audio' na video, lakini zikiwa tofauti," alisema Fella.
Aliongeza wakati Dogo Muu akijiandaa kujitambulisha kwa mashabiki wa muziki na kazi hizo, kundi la TMK Wanaume Family, nalo limefyatua vibao viwili vipya kimoja kiifahamika kwa jina la 'Tutaonekanaje?
Katika hatua nyingine, alisema pamoja na Dogo Aslay kushindwa katika tuzo za muziki za Kora, lakini fursa ya kuteuliwa kuwania tuzo hiyo kama Msanii Bora Chipukizi, imeonyesha ni namna gani kijana huyo alivyo na kipaji.
"Tunajivunia uteuzi wake, hata kama hatafanikiwa kushinda ikizangatiwa ndio kwanza ameingia kwenye sanaa hii baada ya kukitambua kipaji chake," alisema Fella.

Simba, Azam hapatoshi Mapinduzi Cup Z’bar leo

Simba na Azam katika mechi yao ya Ligi Kuu duru lililopita

Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar
MABINGWA  watetezi wa Kombe la Mapinduzi, klabu ya Azam wanashuka dimbani kucheza dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Simba katika mechi yao ya nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi 2012 kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo.
Mechi hiyo itaanza saa 2:00 usiku, ikitanguliwa na nusu fainali nyingine itakayochezwa jioni kati ya mabingwa wa Ligi Kuu ya Kenya, Tusker na Miembeni ya mjini visiwani hapa.
Tusker wamefanikiwa kuingia fainali wakiwa na pointi 7 na kuongoza katika kundi lao la A baada ya kushinda pia katika mechi yao ya mwisho kwa bao 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Pemba.
 Simba ambao wamekuwa wakionyesha kiwango kizuri kadri mashindano hayo yanavyosonga mbele, walitinga nusu fainali wakiwa pointi tano baada ya kutoka sare ya 1-1 katika mechi yao ya mwisho ya hatua ya makundi dhidi ya Bandari.
Azam pia waliingia hatua ya leo wakiwa na pointi tano baada ya juzi kutoka sare na Mtibwa Sugar na hivyo kuongoza katika kundi lao la B, huku Miembeni wakiingia nusu fainali wakiwa na pointi nne baada ya kutoka sare ya 0-0 na Coastal Union ya Tanga.
Kocha wa Simba, Jamhuri Kihwelu alisema kwamba lengo la timu yake ni kutwaa ubingwa baada ya wachezaji wake kuonyesha kiwango kizuri tangu kuanza kwa mashindano hayo.
“Nia tunayo na uwezo wa kutwaa Kombe la Mapinduzi mwaka huu tunao…  wachezaji wetu wameonyesha kiwango kizuri na hivyo naamini kesho (leo) tutashinda tu,” alisema Kihwelu.
Kocha wa Tusker, Robert Matano, alisema kwamba pamoja na timu yake kushiriki kwa mara ya kwanza mashindano hayo, wachezaji wake wameonyesha kiwango kizuri na kufanikiwa kuongoza katika kundi A, hivyo ni imani yake kwamba watashinda pia leo na kutinga fainali.
Hata hivyo, alisema kwamba timu zote zilizofanikiwa kuingia nusu fainali ni nzuri na mafanikio yao yatatokana na juhudi na maarifa ya wachezaji watakocheza leo.
Katibu wa Kamati ya Kombe la Mapinduzi, Abdallah Said, alisema bingwa wa mashindano ya mwaka huu atazawadiwa Sh. milioni 10, mshindi wa pili Sh. milioni tano na mfungaji bora atazawadiwa Sh. 300,000.
Aliongeza kuwa mwamuzi bora wa mashindano hayo na mwanahabari bora pia watapata zawadi ya Sh. 200,000 kila mmoja.
Fainali ya mashindano hayo zitafanyika Jumamosi ambayo ni siku ya kilele cha maadhimisho ya Mapinduzi ya Zanzibar na utachezwa pia kwenye Uwanja wa Amaan na kuhudhuriwa na mgeni rasmi,  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.


CHANZO:NIPASHE

SUGU AFUNGUA INTERNET CAFE YA IZZO B MJINI MBEYA


Mbunge wa Mbeya mjini Mh Joseph Mbilinyi (Sugu) ndiye aliye fanya ufunguzi wa biashara mpya ya msanii Izzo B "INTERNETE CAFE" iliyoko katika chuo cha Teku jijini Mbeya.
Huu utakua ni uwekezaji wa pili wa msanii Izzo B baada ya kufungua duka la nguo hapo mjini mbeya ambapo ndipo anapotoka.

NJEMBA APEWA KIPONDO BAADA YA KUIBA 'KITIMOTO' NA BIA



 Kijana mmojaambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja akilia kwa uchungu mara baada ya kupokea kichapo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali mara baada ya kudaiwa ameiba nyama ya Nguruwe (Kitimoto) pamoja na Bia katika glosali jijini Dar es Salaam.
Mmoja ya wasamalia wema akimtetea kijana huyo ambaye alipokea kichapo.
Akijitetea.
Akisaidiwa na wasamalia wema.

Mrisho Ngassa, John Bocco wainogesha Stars

Ngassa na Bocco wakipongezana


 
WASHAMBULIAJI Mrisho Ngassa wa Simba na John Bocco ‘Adebayor’ wa Azam ni miongoni mwa nyota zaidi walioripoti katika kambi ya timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itakayosafiri leo jioni  kwenda jijini Addis Ababa, Ethiopia kucheza mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya wenyeji keshokutwa Ijumaa.
Awali, Bocco, Ngassa, kipa Juma Kaseja na wachezaji wengine kadhaa walioitwa Stars kutoka katika klabu za Simba na Azam walishindwa kuripoti katika kambi ya timu hiyo kwavile walikuwa na klabu zao kwenye michuano inayoendelea visiwani Zanzibar ya Kombe la Mapinduzi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, alisema kuwa nyota kutoka Simba, Azam na Mtibwa wameungana na wenzao na kwamba sasa Stars itasafiri leo ikiwa na kikosi chenye wachezaji wengi zaidi miongoni mwa wale walioutwa na kocha wao Mdenmark, Kim Poulsen.
Mbali na Bocco, Ngassa na Kaseja, wachezaji wengine walioitwa Stars kutoka Simba, Azam na Mtibwa ni Shomari Kapombe, Amri Kiemba, Amir Maftaha, Mwinyi Kazimoto, Salum Aboubakar 'Sure Boy', Mwadini Ali, Mcha Khamis, Aggrey Morris,  Erasto Nyoni, Aishi Manula na nyota Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ na Shabani Nditi kutoka Mtibwa Sugar,
"Stars inaondoka leo huku ikiwa kamili baada ya nyota wengi kuripoti kambini," alisema Wambura.
Alisema timu hiyo itarejea jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa mechi dhidi ya Ethiopia na kuendelea na kambi yao kujiandaa kwa mechi nyingine mbili za kirafiki, zote zikiwa ni sehemu ya maandalizi kabla ya mechi ya kuwania kufuzu kwa fainali zijazo za Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Machi.

MTANGAZAJI ALIYEPOTEA AKUTWA PORINI AMEKUFA HANA SEHEMU NYETI

Bw. Issa Ngumba.

Mwandishi wa habari wa Radio Kwizera anayefanyia kazi wilayani Kakonko mkoani Kigoma,Bw. Issa Ngumba aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha amekutwa amekufa huku akiwa kanyofolewa  sehemu zake za  siri.
 

Taarifa  kutoka Kigoma ambazo mtandao huu  MICHARAZO umezipata jana kuwa, mwili wa mwanahabari  huyo umekutwa nje  kidogo na mkoa  wa Kigoma.
Kamanda  wa  polisi  wa mkoa wa Kigoma Frasser Kishai, amethibitisha  juu ya kutokea kwa  tukio  hilo na kwamba  bado jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi.
Mbunge wa  jimbo la Kigoma Zitto Kabwe amenukuliwa kusikitishwa na kifo cha mwandishi huyo na kulitaka jeshi hilo kufanya uchunguzi wa kina juu ya kifo chake.
Kabwe  ameeleza  jinsi  mwanahabari  huyo  alivyokuwa akiifanya kazi yake kwa jamii ya Kigoma kwa ufanisi zaidi na kuwa wakati mwingine yeye kama mbunge alikuwa akizunguka na mwanahabari huyo katika jimbo lake.
" Kweli  nimeguswa   sana na kifo  cha kusikitisha cha mwanahabari huyo nilimfahamu  vema kwa  utendaji kazi wake  ila nawapa  pole sana  waandishi  wote nchini kwa  msiba huu mkubwa .....na zaidi nitapata  kueleza mengi mara baada ya  uchunguzi"
Taarifa za awali  zilizotolewa na  Jeshi la Polisi wilayani Kakonko baada ya  kupotea kwa mwanahabari huyo zilisema kuwa Bw Ngumba alipotea  tangu January 05 mwaka huu majira ya saa 11 jioni ambapo alimuaga mke wake Bi. Rukia Yunus kuwa anakwenda Muhange senta wilayani Kakonko na kwamba hajarudi nyumbani hadi sasa.
Kufuatia tukio hilo jeshi la polisi kwa kushirikiana na wananchi wa Kijiji cha Muhange wanaendelea kumtafuta katika mapori ya kijiji hicho baada ya rafiki zake kueleza kuwa aliwaanga kuwa anakwenda kutafuta dawa msituni.
Bw. Issa Ngumba.
Aidha jeshi la polisi Wilayani Kibondo liliomba kampuni za mitandao ya simu anayotumia Bw Ngumba kusaidia kutambua simu zake zilipotumika kwa mara ya mwisho ili kurahisisha upatikanaji wake.
Akizungumza kwa njia ya simu, Mke wa Bw Issa Ngumba, Bi Rukia Yunus amesema kuwa wananchi walio wengi ambao walikuwa wakimtafuta maporini wamerudi kijiji hapo baada ya kumkosa.

CHANZO:FRANCIS Godwin

OMARI OMARI KUZIKWA LEO TEMEKE


MSANII nyota wa miondoko ya Mchiriku, Omari Omari, aliyefariki jana alfajiri anatarajiwa kuzikwa leo saa 7 mchana kwenye makaburi yaliyopo eneo la Temeke Mikoroshini, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa rafiki ya karibu wa marehemu huyo aliyekuwa akitajwa kama mfalme wa Mnanda King Sapeto, alisema mipango ya mazishi yanaendelea vema na kwamba Omar Omar atazikwa leo mchana.
Sapeto, alisema ndugu na jamaa wa marehemu wanategemea kupata ujumbe mzito kutoka kwa viongozi wa Serikali watakaopishana kwenda kutoa mkono wa faraja kwenye nyumba ya msiba.
Kwa siku za hivi karibuni viongozi wa serikali na vyama mbali mbali vya siasa wamekuwa mstari wa mbele kwa kushiriki bega kwa bega kwenye misiba ya wasanii, hivyo watu wa karibu na Omari Omari wanategemea hali hiyo pia itatokea kwa ndugu yao kipenzi. 
"Hatutegemi ubaguzi wa misiba" anaeleza mmoja wa ndugu wa marehemu.
Omari Omari aliyetamba na wimbo “Kupata Majaaliwa”, alifariki katika hospitali kuu ya Temeke baada ya kuugua ugonjwa wa kifua kikuu.
Msiba wake umekuja siku chache baada ya watanzania kumzika nyota wa filamu, Juma Kilowoko 'Sajuki' aliyefarikia Januari 2, katika hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa matatizo ya kiafya.
 
Mwisho

Tuesday, January 8, 2013

Omar Omar mkali wa Mchiriku afariki dunia Dar

MSANII  nyota wa miondoko ya Mnanda a.k.a Mchiriku, Omari Omar amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Habari zilizoifikia MICHARAZO, asubuhii zinasema kuwa, Omar Omar aliyetamba na nyimbo mbalimbali ukiwemo ule maarufu wa 'Kupata ni Majaliwa' alifariki nyumbani kwao Temeke, saa chache baada ya kurejeshwa toka hospitali ya temeke alipokuwa amelazwa kwa siku kadhaa.
Taarifa hizo zinasema kuwa mara baada ya kurejea nyumbani, msanii huyo alizidiwa na hatimaye kufariki na kwamba msiba wake upo nyumbani kwao Temeke Mikoroshini kwa ajili ya mipango ya mazishi.
Msiba wa msanii huo umekuja siku chache baada ya tasnia ya sanaa na burudani kumpoteza Juma Kilowoko 'Sajuki' msanii nyota wa filamu aliyefariki pia kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya muda mrefu.
MICHARAZO inawamuombea kila la heri Omar Omar na wengine waliotangulia mbele ya haki mapumziko mema katika safari yao ya Ahera. Innallillah Waina Illah Rajiun.
Taarifa zaidi tutakuwa tunawaletea kujua mkali huyo wa mduara aliyewafanya wasanii wengine kufuata mkondo wake akiwemo Dogo Mfaume, Ferouz, Easy Man na wengine.

Mayweather Jr, kuvaana na Guerrero Mei 4

BONDIA Floyd Mayweather Jr anatarajia kupanda jukwaani katika ukumbi wa MGM Grand, Las Vegas, Nevada, USA kuwania taji la WBC welterweight title May 4 ,2013 kuzipiga na Robert Guerrero bondia huyo ambaye ajawai kupigwa tangia angie katika uwanja wa masumbwi ya kulipwa tarehe 11-10-1996 bondia huyo alichezo mpambano wake wa mwisho May 5 mwaka jana na kutumikia kifungo cha Miezi mitatu kwa kosa la kumshambulia aliyekuwa mpenzi wake mama watoto wake kwa sasa yupo katika maandalizi ya mpambano huo wa tarehe hiyo katika mchezo wake wa mwisho aliocheza na Miguel Cotto alipata ushindi mwembamba kwa kuibuka kumtwanga kwa point
www.superdboxingcoach.blogspot.com    BONDIA Floyd Mayweather Jr  anatarajia kupanda jukwaani katika ukumbi wa MGM Grand, Las Vegas, Nevada, USA kuwania taji la    WBC welterweight title May 4 ,2013 kuzipiga na Robert     Guerrero bondia huyo ambaye ajawai kupigwa tangia angie katika uwanja wa masumbwi ya kulipwa  tarehe 11-10-1996 bondia huyo alichezo mpambano wake wa mwisho May 5 mwaka jana na kutumikia kifungo cha Miezi mitatu kwa kosa la kumshambulia aliyekuwa mpenzi wake mama watoto wake kwa sasa yupo katika maandalizi ya mpambano huo wa tarehe hiyo katika mchezo wake wa mwisho aliocheza na Miguel Cotto alipata ushindi mwembamba kwa kuibuka kumtwanga kwa point

LIONEL MESSI TENA MWANASOKA BORA WA DUNIA

Lionel Messi akifurahi baada ya kupokea tuzo yake ya nne mfululizo ya Ballon d'Or ya kwenye Ukumbi wa Convention Centre mjini Zurich Uswisi jana.
Lionel Messi akiwa kwenye tuzo za FIFA jana
Ronaldo, Iniesta na Messi wakiwa kwenye tuzo.
Kikosi XI cha FIFA kilichotangazwa jana. Kutoka kushoto mstari wa nyuma Cristiano Ronaldo, Marcelo, Sergio Ramos, Gerard Pique, Dani Alves, Iker Casillas. Mstari wa mbele kutoka kushoto: Radamel Falcao, Lionel Messi, Andres Iniesta, Xavi Hernandez na Xabi Alonso
Winga wa Fenerbahce, raia wa Slovakia, Miroslav Stoch akishukuru kwa tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka wakati wa sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.
Vicente del Bosque akishukuru baada ya kupokea tuzo ya Kocha Bora wa Dunia wa Mwaka 2012
Mwanasoka Bora wa Dunia wa zamani, Fabio Cannavaro wa Italia akionyesha jina la mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia wa Mwaka 2012, Lione Messi
Straika wa timu ya taifa ya Marekani, Abby Wambach akishukuru baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike wa Dunia

Mwanasoka wa zamani wa Colombia, Carlos Valderrama (kushoto) na mchezaji wa zamani wa Uholanzi, Ruud Gullit wakati wa kukabidhi tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka.

Mwanasoka wa zamani wa Colombia, Carlos Valderrama akisoma jina la mshindi wa tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka.

Fuleco, kikatuni cha fainali za Kombe la Dunia 2014 za nchini Brazil kikimkumbatia mwanasoka bora wa zamani Ronaldo stejini wakati wa sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.

Kocha wa timu ya taifa ya Brazi, Luiz Felipe Scolari na mwanasoka wa zamani wa Colombia, Carlos Valderrama wakipozi kwa picha

Straika wa Real Madrid, Mreno Cristiano Ronaldo na rafikiye wa kike Irina Shayk wakiingia kwenye sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.

Rais wa FIFA, Joseph Blatter akiambatana na muigizaji wa Kirafansa, Gerard Depardieu wakati akiwasili kabla ya kuanza kwa kwenye sherehe za tuzo za FIFA Ballon d'Or.
Waongozaji wa sherehe ya tuzo za FIFA Ballon d'Or, Ruud Gullit (kushoto) na Kay Murray wakiwa mzigoni

NYOTA wa Barcelona, Lionel Messi (25) jana aliweka rekodi ya kipekee ya kuwa mwanasoka wa kwanza duniani kutwaa tuzo ya Ballon d'Or ya Mwanasoka Bora wa Dunia kwa miaka minne mfululizo baada ya kuwashinda wapinzani wake Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Andres Iniesta wa Barcelona.
Muargentina huyo amekuwa mtu wa kwanza katika historia ya miaka 61 ya tuzo hiyo kuibeba mara nne mfululizo.
Johan Cruyff (1971, 1973, 1974) na Marco Van Basten (1988, 1989, 1992) wa Uholanzi, na Michel Platini wa Ufaransa walishinda tuzo ya Ballon d'Or mara tatu.
Mwanadada Abby Wambach wa Marekani alishinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike, wakati tuzo ya kocha bora wa kiume ilienda kwa Vicente Del Bosque wa timu ya taifa ya Hispania baada ya kuwashinda, Jose Mourinho wa Real Madrid ambaye alishasema mapema kwamba hatahudhuria sherehe hizo nchini Uswisi na Pep Guardiola.
Tuzo ya Puskas ya Goli Bora la Mwaka
ilienda kwa winga wa Fenerbahce, raia wa Slovakia, Miroslav Stoch ambaye alifunga goli lake kwa kuunganisha moja kwa moja bila ya kutua chini mpira wa kona uliomfikia akiwa nje ya boksi. Stoch aliwaangusha Radamel Falcao aliyefunga goli la 'tik-taka' na Neymar aliyefunga goli katika mazingira magumu.
Kikosi cha wachezaji bora "First Eleven" wa dunia chote kimeundwa na nyota wanaocheza katika Ligi Kuu ya Hispania, huku Radamel Falcao pekee akitokea nje ya Barcelona na Real Madrid.
Real Madrid na Barcelona zimetoa wachezaji watano kila moja.

Kikosi Bora cha Dunia XI cha FIFA kilichotangazwa jana ni:

Kipa

Iker Casillas
Mabeki
Dani Alves, Marcelo, Sergio Ramos na Gerard Pique
Viungo
Xabi Alonso, Xavi Hernandez na Andres Iniesta
Washambuliaji
Cristiano Ronaldo, Radamel Falcao na Lionel Messi