STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 14, 2013

Man United yaing'ang'ania Real Madrid, Dotmund yakomaa ugenini

Danny Welbeck (kulia) akiruka juu kuifungia Manchester United bao la kuongoza katika mechi ya usiku wa jana.
VINARA wa Ligi Kuu ya England, Manchester United usiku wa kuamkia leo imelazimisha sare ya bao 1-1 ugenini dhidi ya wenyeji wao Real Madrid katika pambano la awali la mechi za mtoano za Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu, mjini Madrid, Hispania Manchester ilianza kutangulia kupata bao lililofungwa nyota wake, Danny Welbeck katika dakika ya 20.
Wenyeji walicharuka baada ya kufungwa bao hilo na kufanikiwa kusawazisha dakika kumi baadae kupitia mshambuliaji wake nyota, Cristiano Ronaldo.
Katika pambano jingine lililochezwa pia jana ilishuhudiwa wenyeji Shakhtar Donetsk ilishindwa kutamba kwa kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na wageni wao Borrusia Dotmund ya Ujerumani.
Wenyeji ndiyo waliotangulia kupata bao kupitia Darijo Srna dakika ya 31 kabla ya wageni kusawazisha kwa goli la Robert Lewandowski dakika ya 41 na kufanya hadi mapumziko matokeo kuwa 1-1.
Kipindi cha pili wenyeji waliendelea kutakata kwa kujipatia bao la pili lililofungwa na Douglas Coast dakika ya 68 kabla ya Wajerumani hao kuchomoa kipigo dakika mbioli kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kwa bao la Mats Hummels.
Timu hizo zinatarajiwa kurudiana Machi 5 mechi itakayoamua timu ipo itinge riobo fainali za michuano hiyo ya Ligi ya Ulaya.

Wednesday, February 13, 2013

MALINZI AFUNGIWA 'VIOO' TFF BARUA YAKE YADUNDA


Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Tarehe 13 Februari 2013



Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kuwajulisha wapenzi wa mchezo huu kuwa limepokea barua kutoka kwa Ndg. Jamal Malinzi ambayo inaomba kuangaliwa upya kwa maamuzi ya Kamati ya Rufaa za Uchaguzi ya TFF ya kuliondoa jina lake kwenye orodha ya wagombea urais wa Shirikisho.



Barua hiyo ya tarehe 13 Februari 2013 ilielekezwa kwa mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF. Baada ya kuipata barua hiyo, Sekretarieti iliwasiliana na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ambaye alielekeza kuwa Ndg. Malinzi alielekeza barua yake kwenye chombo ambacho hakikufanya uamuzi wa kuliengua jina lake na hivyo hakina mamlaka ya kuangalia upya suala hilo.



Mwenyekiti alishauri kuwa TFF imwandikie Ndg. Malinzi barua ya kumshauri kuwa aelekeze maombi yake kwenye chombo kilichofanya maamuzi kwa kuwa ndicho kinachoweza kuangalia upya maamuzi yake.



Sekretarieti pia imepokea maamuzi rasmi ya Kamati ya Rufaa za Uchaguzi ya TFF na imeshayawasilisha kwenye Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa ajili ya kuendelea na mchakato wa uchaguzi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Uchaguzi za TFF.



Angetile Osiah

Katibu Mkuu,

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Coastal yaangukia pua Kagera, Mgambo yatakata Tanga

Hamis Shengo (kulia) wa Coastal akijaribu kumtoka Felix Themi ya Kagera Sugar katika pambano la leo. (Picha kwa hisani ya Blog ya Coastal Union)
TIMU ya Coastal Union ya Tanga jioni hii imeangukia pua baada ya kunyukwa bao 1-0 mjini Bukoba na wenyeji wa Kagera Sugar, wakati majirani zao JKT Mgambo ikinawiri nyumbani mjini Tanga kwa kuilaza JKT Oljoro kwa mabao 2-0.
Bao pekee lililowazamisha wagosi wa kaya lilitupiwa kimiani kwa kichwa na Felix Themi akitokea benchi kwenye dakika ya 58 baada ya mabeki wa Coastal kuzembea.
Kipigo hicho kinaifanya Coastal kufuata mkondo wa Mgambo ambao nao walichezea kipigo kama hicho katika mechi yao iliyopita mjini humo.
Hata hivyo Mgambo leo ilizinduka na kuzima wimbi la ushindi la JKT Oljoro kwa kuwanyuka mabao 2-0 katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Mechi nyingine katika Ligi Kuu leo imeshuhudiwa Mtibwa ikilazimishwa sare ya 0-0 mbele ya Ruvu Shooting, huku Toto Africans wakiwa nyumbani CCM Kirumba Mwanza walilazimishwa sare ya mabao  2-2 na timu iliyozinduka tangu iwe chini ya nyota wa zamani wa Yanga, Pan na Taifa Stars, Mohammed Rishard 'Adolph' kama kocha wao, Polisi Morogoro.

Tegete azidi kung'ara Yanga ikiizamisha Lyon 4-0



Beki wa Yanga, David Luhende, (Kulia), akijaribu kumzuia mchezaji wa timu ya African Lyon Yusuph Mpili, wakati wa mchezo wa ligi kuu uliofanyika leo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaa Yanga imepata ushindi wa mabao 4 -0 ikiwa imebaki kileleni



MABAO mawili ya mshambuliaji aliyerejea kwa kasi nchini, Jerry Tegete ya kipindi cha kwanza na mawili mengine ya watokea benchi Didier Kavumbagu na Nizar Khalfan katika kipindi yameipa Yanga ushindi wa mabao 4-0 mbele ya vibonde African Lyon.
Tegete aliyekuwa mwiba mkali kwa mabeki wa Lyon, alifunga mabao hayo katika pambano lililokosa msisimko kama ilivyotarajiwa lililochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Ushindi huo umeifanya Yanga kuiacha Azam kwa pointi tatu katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku Tegete akijiongezea hazina ya mabao akiwafukuzia akina Kipre Tchetche wa Azam na Didier Kavumbangu aliyefikisha bao la tisa baada ya leo kutupia moja la penati.
Yanga imefikisha jumla ya pointi 36 kutokana na michezo 16 sawa na timu nyingine 13 zinazoshiriki ligi hiyo, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 33.
Katika pambano hilo beki wa Lyon, Mpilipili alilimwa kadi nyekudnu kwa kumchezea vibaya kiungo wa Yanga Haruna Niyonzima dakika za lala salama, huku Yanga ikikosa penati kupitia Hamis Kiiza.
Ushindi huo wa Yanga umekuja baada ya kupunguzwa kasi katika mechi iliyopita kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Mtibwa Sugar na kufikisha idadi ya mechi 18 tangu timu hiyo iwe chini ya kocha Ernest Brandts

MALINZI SASA AMTEGEMEA TENGA TFF





Mgombea Urais wa TFF aliyeenguliwa, Jamal Malinzi akizungumza na vyombo vya habari kuhusu sakata zima kwenye ukumbi wa Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo. Picha: Bongostaz.blogspot.com



YAH: KUENGULIWA KWANGU KUGOMBEA URAIS WA TFF 2013

Ndugu zangu,kupitia vyombo vyenu vya habari ninaomba niueleze umma wa watanzania,hususani wadau wa mpira wa miguu,yafuatayo kuhusu kuenguliwa kwangu.

Awali ya yote nieleze kusikitishwa kwangu na maamuzi yaliyotolewa na kamati ya rufaa ya TFF ya kuniengua kugombea urais wa TFF.Sikubaliani na maamuzi haya .

Katika kuniengua kamati ya rufaa ya uchaguzi ya TFF imetoa sababu mbili (nanukuu magazeti ya jana tarehe 12/02/2013 maana hadi leo sijakabidhiwa barua ya kuenguliwa).

1. Kukosa uadilifu kwa kupinga waraka uliotolewa na TFF wa kubadili Katiba ya TFF mwezi Desemba 2012.

2. Kukosa uzoefu wa miaka mitano ya uongozi.

Ndugu zangu,kiini cha maamuzi ya Kamati ya rufaa dhidi yangu ni pingamizi lililowekwa na mtu mmoja anayeitwa AGAPE FUE.Bwana Agape Fue aliniwekea pingamizi katika kamati ya uchaguzi akidai mimi nilipinga waraka wa kubadili katiba ya TFF na pia sina uzoefu wa miaka mitano ya uongozi wa mpira.Kinyume na matakwa ya kamati ya uchaguzi kama yalivyotangazwa kuwa mtoa pingamizi aje mwenyewe kutetea pingamizi lake ,Bwana Agape Fue hakutokea mbele ya Kamati ya Bwana Lyatto.Matokeo yake tarehe 31/01/2012 kamati ya uchaguzi ya TFF ilitoa maamuzi ya ya kutupilia mbali pingamizi hili.

Bwana Agape Fue hakuishia hapo kwa mara nyingine tarehe 06/02/2013 alikata rufaa kwenye kamati ya rufaa ya uchaguzi akidai kamati ya uchaguzi haikumtendea haki. Rufaa hii haikuwa na anwani wala namba ya simu ya Bw.Agape Fue.Rufaa ilisikilizwa tarehe 10/02/2013 na maamuzi ya kukata jina langu yakatangazwa jioni ya tarehe 11/02/2013.

Mpaka leo najiuliza hivi huyu Bw. Agape Fue ni mwanaume au ni mwanamke?(hakueleza kama ni Bwana au Bibi Agape Fue). Agape Fue ni nani hasa? Anaishi wapi?Je ni Mtanzania au sio Mtanzania maana kikanuni wasio watanzania hawaruhusiwi kujihusisha na uchaguzi wa TFF (rejea kifungu cha 9 cha kanuni za uchaguzi),pingamizi lake halikuambatana na udhibitisha wa uraia. Kwa nini alichukua maamuzi haya? Sipati jibu. Iweje mtu achukue maamuzi mazito ya kumkatia mtu rufaa kisha uishie kusaini karatasi na kuwaachia wengine wakusemee na usije hata kushuhudia kinachoendelea kama kweli una maslahi na madai yako? Waandishi wa habari mnisaidie kupata majibu.



Ndugu zangu ,mtoa pingamizi alidai haikuwa sahihi kupinga azimio la kubadili katiba ya TFF kwa njia ya waraka.Naomba nisistize mambo matatu:

1. Wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF wanawakilisha matakwa ya vyama vilivyowatuma kwenda kwenye mkutano mkuu wa TFF,na ndio maana chama cha mpira cha mkoa wa Kagera (KRFA) kiliitisha kikao cha kamati ya utendaji ili kamati iweze kutoa mwongozo kwa wajumbe wake kuhusu nini kifanyike kuhusu waraka ulioletwa na TFF, hivyo maamuzi yaliyotolewa ya kuukataa waraka huu yalikuwa ni maamuzi ya chama cha mpira mkoa wa Kagera na wala hayakuwa ni maamuzi ya Jamal Malinzi,iweje malinzi niadhibiwe kwa maamuzi haya,kwa nini usiadhibiwe mkoa mzima na mikoa yote iliyopinga waraka?hii ni haki kweli? Siamini kama kuna mjumbe wa mkutano mkuu aliyekiuka maamuzi ya kamati yake ya utendaji.

2. Katika mchakato wa kubadili katiba kwa njia ya waraka kilichokuwa kinagomba sio maudhui (content) ya mabadiliko ya Katiba bali utaratibu uliotumika kubadili Katiba. Swali la msingi tulilojiuliza wajumbe wa kamati ya utendaji KRFA ni kwamba je kwa mujibu wa Katiba ya TFF kifungu 22 na kifungu 30 wapi katiba inatamka kuwa inaweza kubadilishwa kwa njia ya waraka? Mpaka leo hilo jibu hakuna,labda aliyeniwekea pingamizi atusaidie kupata jibu la swali hili. Katiba ya TFF iko wazi kabisa inatamka kuwa Katiba itabadilishwa kwa njia ya Mkutano Mkuu tu (General Assembly).

3. Ni kweli FIFA iliagiza yafanyike mabadiliko ya Katiba ya kuingiza kipendele cha ‘club licencing’ katika Katiba ,lakini je FIFA katika agizo hilo ilisema Katiba ya TFF ivunjwe ili kutimiza azma hiyo? Ikumbukwe kuwa mwaka 2004 FIFA iliagiza TFF iingize kwenye Katiba kipengele cha Katibu Mkuu awe wa kuajiriwa badala ya kuchaguliwa,agizo hili lilitekelezwa kwa kupitishwa na Mktano Mkuu wa TFF,iweje leo utaratibu huu ukiukwe? Hata majuzi CAF walipotaka kubadili katiba ili Rais wa CAF atokane na wajumbe wa Kamati ya Utendaji jambo hili lilitekelezwa kwa kuitisha mkutano mkuu wa dharura uliofanyika Seychelles majuzi. Katiba ndio msingi mkuu wa uendeshajiwa TFF,nitaipigania siku zote.Huo ndio utaratibu,si CAF si FIFA si Vyama vya mpira vya nchi,hakuna anayebadili Katiba kwa njia ya waraka,kama kuna mwenye ushahidi aulete.



Kuengua jina langu eti kwa kuwa nilipinga waraka wa kubadili Katiba sio uamuzi sahihi.



Kuhusu uzoefu wa miaka mitano katika Uongozi:



Ikumbukwe kuwa katika uchaguzi mkuu wa TFF mwaka 2008 niligombea na jina langu lilikatwa na kamati ya uchaguzi ya TFF.Nilikata rufaa katika Kamati ya Rufaa ya TFF na kushinda . Hukumu hii ni halali hadi leo.Iweje leo hii miaka minne baadae Kamati hiyo hiyo ya rufaa (kubadili majina ya wajumbe sio kubadili taasisi) inione sina uzoefu?.Si hilo tu ,hata katika kujaza fomu namba moja ya kugombea niliambatanisha vielelezo vyote vya uzoefu wangu ikiwa ni pamoja na kudhibitisha kuwa katika kipindi cha miaka mine iliyopita nimekuwa:

-Mjumbe wa Baraza la michezo mkoa wa Dar es salaam.

-Mwenyekiti wa kamati ya mashindano chama cha mpira mkoa wa Pwani COREFA.

-Mjumbe wa mkutano mkuu wa mkoa wa Kagera

-Mwenyekiti wa chama cha mpira mkoa wa Kagera

Hii ni pamoja na kuongoza Yanga 2002-2005.

Hivi katika nafasi hizi za uongozi ipi ni ya kuongoza ‘bonanza’? Nimedhalilishwa sana.



HITIMISHO

Vyombo vya habari kupitia makala,tahariri na maoni ya wasikilizaji/wasomaji/watazamaji vimesifia sana awamu mbili za uongozi wa Bwana Leodeger Tenga.Bwana Tenga amesifiwa kwa umahiri wake wa kuleta utulivu katika sekta ya mpira wa miguu Tanzania.Amesifiwa kwa kujenga taasisi imara ambayo mhimili wake mkuu ni sekretarieti makini na kamati mbali mbali zilizo imara .Let him rise to the occasion,muda wa kuonyesha uongozi imara ni huu,historia itamhukumu kwa jinsi gani atasimamia suala hili,haki sio lazima itendeke lakini pia inatakiwa ionekane inatendeka.

Kamati ya utendaji ya TFF inayo mamlaka ya kubatilisha maamuzi haya kwa maslahi ya mpira wa Tanzania.Ninamshauri Rais wa TFF aitishe kikao cha dharura cha kamati ya utendaji ili kijadili hali hii na kunirudishia haki yangu ya kugombea urais wa TFF.

Nihitimishe kwa kuwaomba wadau wa mpira wa miguu Tanzania wawe watulivu wakati tukisubiri kupata ufumbuzi wa suala hili.



Mungu ibariki Afrika,

Mungu ibariki Tanzania.

Ahsanteni sana,



Jamal Emil Malinzi

Dar es salaam

13/02/2013


Yanga kuvuna nini leo kwa Lyon?

Kikosi cha Yanga kitakachovaana na African Lyon
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga jioni ya leo wanatarajiwa kuvaana na wanaoburuza mkia katika ligi hiyo, African Lyon katika mfululizo wa mechi za duru la pili pambano litakalofanyika kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Tayari kocha msaidizi wa Yanga, Fred Minziro ameweka bayana kwamba wanaingia dimbani leo kwa lengo la kushinda mchezo huo ili kuwakimbia Azam na kujiwekea mazingira mazuri ya kutwaa taji la msimu huu.
Yanga iliyolazimishwa sare ya bao 1-1 na Mtibwa Sugar katika mechi yake ya mwisho inalingana pointi na Azam waliopo nyuma yake ambao wapo mapumzikoni wakijiandaa na mechi yao ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Kikosi cha Yanga kinakutana na Lyon ambayo imekuwa na matokeo mabaya tangu kuanza kwa duru la pili wakiwapokea Polisi Moro katika nafasi ya mkiani.
Hata hivyo Yanga isitarajie wepesi katika mechi hiyo ya leo kutokana na rekodi zilizopo pale timu hizo mbili zinapokutanana ambapo Yanga hupata tabu kuifunga timu hiyo ya Lyon.
Mbali na mechi hiyo pia leo kutakuwa na mechi nyingine kadhaa katika viwanja wa Mkwakwani Tanga, JKT Mgambo itavaana na JKT Oljoro, Coastal Union itakuwa uwanja wa Kaitaba kuumana na Kagera Sugar, huku Toto African itakuwa nyumbani kuwakaribisha Polisi Moro na Mtibwa Sugar kuivaa Ruvu Shooting.

Juve, PSG waua Ulaya, Man U, Madrid vitani leo

Juventus stun Celtic Park thanks to Matri's early strike and temporarily silence one of the most partisan crowds in European football. The goal came following a dreadful defensive error from Efe Ambrose, who helped Nigerian win the Africa Cup of Nations just last Sunday.
Wachezaji wa Juventus wakishangilia moja ya mabao yao
WAKATI mashabiki wasoka dunia wakiwa na hamu  kushuhudia pambano kabambe kati ya Manchester United na Real Madrid, timu za Juventus na PSG usiku wa kuamkia leo wameanza vema mechi zao mtoano Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Juvetus ya Italia ikiwa ugenini nchini Scotland ilipata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Celtic na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu robo fainali ya michuano hiyo.
Bao la mapema la dakika tatu toka kwa Alessandro Matri na mengine ya kipindi cha pili yaliwafanya 'kibibi' hicho cha Turin, kwenda kuisubiri Celtic katiak mechi ya marudiano ikiwa haina presha kubwa.
Mabao mengine ya Juvetus, vinara wa Ligi ya Seria A yalitupiwa kambani na Claudio Marchisio katika dakika ya 77 na Mirko Vucinic dakika saba kabla ya pambano hilo kumalizika.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana usiku, Valencia ya Hispania ilijikuta ikichezea kichao cha mabao 2-1 wakiwa nyumbani kutoka kwa wenyeji wao PSG ya Ufaransa.
PSG, ilijikuta hata hivyo ikimaliza pambano hilo vibaya kwa kumpoteza nyota wake Zlatan Ibrahimovic aliyelimwa kadi nyekundu dakika za lala salama.
Michuano hiyo inatarajiwa kuendelea usiku wa leo kwa mechi nyingine mbili, Manchester United ya Uingereza itasafiri mpaka Madrid, Hispania kuivaa Real Madrid katika pambano linalosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka duniani,
Pambano hilo linasubiriwa kwa hamu kutokana na hali ilizonazo timu hizo mbili ambazo zinanolewa na makocha waliowahi kuwa wapinzani wakubwa katika Ligi Kuu ya Engaland, Jose Mourinho na Sir Alex Ferguson.
Mechi nyingine inayochezwa leo itazikutanisha pia timu za Shakhtar dhidi ya Borrusia Dotmund, itakayokuwa ugenini nchini Ukraine
Utamu wa pambano hilo unachagizwa na 'vita' ya makocha waliowahi kuwa wapinzani baada ya kupewa kadi ya pili ya njano.lijikuta akimaliza mchezo huo vibaya kwa kulipwa kadi nyekundu dakika za lala salamai.

Tuesday, February 12, 2013

Diamond, Lady Jay dee watajwa kama vibopa Bongo kwa wasanii

When it comes to money, Bongo music is one of the most lucrative but you’d never tell that listening to the artistes pour their hearts out for their loved ones. Bongo Flavour acts rake in the money in truck loads and they don’t spend it on bling only, they invest their money. Sylvia Ambani and Herieth Makwetta looked at some of the richest acts in Tanzania.





NASEEB ABDUL (DIAMOND)

He stayed in the shadows for long looking for a break but now that the limelight has been trained on him, he has proved that he belongs at the top of the music charts. He finally made a debut in 2009 with his hit song “Kamwambie”.

He is one of the most expensive musicians not just in Tanzania but the region and this does not seem to put promoters off as he is on the stage on a weekly basis. Want him for a show, you will have to pay him $4000 (Sh350,000). And that’s after a bargain.

This has enabled him to make a fortune for himself in a very short period of time. He owns mansions in Tanzania, acres of land, cars and shops.



JUDITH WAMBURA (LADY JAY DEE)



She started her music career at the end of the 1999. She is one of the most respected Tanzanian artistes and has remained humble through her success. She is very hard working and this has led her to accumulate a good fortune to her name.



Her garage pays homage to a Nissan Murano, a Toyota Coaster minibus, Toyota Prado among others. She of course can’t own all those and rent. She owns a mansion. She also invests heavily and owns a band by the name Machozi.




JOSEPH HAULE (PROFESSOR JAY)

He began his music career in 1990 with a group called the Hard Blasters. It is this band that started the music style known as ‘muziki wa kizazi kipya’. The artiste has acquired his wealth through the many shows he does internationally.

He owns a beachfront mansion which has an in-built studio, drives a modest Toyota Spacio but don’t let that fool you, it’s not that he can’t afford fuel because he makes good money from his music and owns several parcels of land and is also a serious investor.



JUMA NATURE (KIROBOTO)

He is one of the long timers who are still relevant in the music scene. He has been able to make a name for himself since his days in the male group artists TMK when he was under Mkubwa Fela. He later left and formed his own group called ‘Wanaume Halisi’.

He owns a fleet of taxis that operate in Dar es Salaam; he owns acres of land and a home.



AMBWENE YESAYA (AY)

He started his music career back in 2000 with the group East Coast. The group later split and he continued to do his solo music together with his close friend Hamisi Mwinjuma (Mwana FA). They are still close friends and have been friends for more than ten years.

AY likes to keep his personal life private and stays away as much as he can from the cameras. All the camera shyness may fool you but he is one of the richest artistes in Tanzania. He has derived his wealth from the many shows he does and the international events that pay him handsomely. He has a collection of cars, a clothing line with his name and several boutiques.

He is the owner of Unity Entertainment Company which produces programmes like the famous ‘Mkasi’ which is broadcasted on East Africa Television. He recently did a collabo with Lil Romeo that got some good reception across the continent.

Source: Kenya’s The Nation via wavuti

Uchaguzi wa FRAT upo palepale Siku ya Wapendanao

Na Boniface Wambura
UCHAGUZI Mkuu wa viongozi wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT) unafanyika Februari 14 mwaka huu mjini Morogoro kama ulivyopangwa, tofauti na taarifa wanazopewa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa chama hicho.

Kwa mujibu wa Katibu wa Kamati ya Uchaguzi ya FRAT, Damas Ndumbaro, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa FRAT wanatakiwa kufika Morogoro keshokutwa (Februari 12 mwaka huu) . Pia wapiga kura na wagombea wanatakiwa kulipia ada za uanachama kwa mwaka 2013 kabla ya uchaguzi.

Wagombea ni Army Sentimea na Said Nassoro (uenyekiti) wakati wanaoomba nafasi ya Makamu Mwenyekiti ni Juma Chaponda, Juma Mpuya na Tifika Kambimtoni.

Abdallah Mitole, Charles Ndagala na Hamis Kisiwa wanawania ukatibu mkuu, nafasi ya Mhazini inagombewa na Jovin Ndimbo. Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ni Kamwaga Tambwe wakati nafasi ya uwakilishi wanawake yupo Isabela Kapera.

Wagombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ni Emmanuel Chaula na Samson Mkotya.

Kampeni za uchaguzi TFF zasitishwa kisa,,,

TAARIFA KWA UMMA

UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA NA TANZANIA PREMIER LEAGUE BOARD (TPL)



KUSITISHA ZOEZI LA KAMPENI

12/02/2013



1. Kamati ya Uchaguzi, kwa mamlaka iliyonayo kupitia Kanuni za Uchaguzi za TFF Ibara ya 3(1), 6(1) (g) na (l), 10(5), 11(6) inayosomeka pamoja na Ibara ya 14(1) na (2) na pia Ibara ya 26(5) na (6), imesitisha zoezi la kampeni za uchaguzi wa TFF na TPL Board lililokuwa lianze kesho tarehe 13/02/2013 hadi hapo itakapowatangazia, ili kuhakikisha kuwa mchakato wa uchaguzi unakidhi kikamilifu matakwa ya Kanuni za Uchaguzi na Katiba ya TFF.



2. Tarehe za Uchaguzi Mkuu wa TFF na TPL Board zinabaki kama zilivyopangwa.



3. Taarifa hii inazingatia pia Ibara ya 2(4) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF inayoagiza uongozi uliopo madarakani kuendelea na kutekeleza majukumu ya Shirikisho hadi hapo mchakato wa uchaguzi utakapokamilika.



Deogratias Lyatto

MWENYEKITI

KAMATI YA UCHAGUZI TFF

YANGA KUSAKA POINTI ZA KUIACHA AZAM KWA LYON KESHO

Kikosi cha Yanga

Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inamaliza raundi ya 16 kesho kwa mechi kati ya wenyeji African Lyon dhidi ya Yanga itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi Martin Saanya kutoka Morogoro inakutanisha timu zenye mazingira tofauti. Wakati Yanga wakiwa ndiyo vinara wa ligi hiyo kwa pointi 33, African Lyon ambayo sasa inanolewa na Salum Bausi inakamata mkia ikiwa na pointi tisa tu.
Nayo Toto Africans iliyopo katika nafasi ya 12 itaikaribisha Polisi ya Morogoro kwenye Uwanja wa CCM Kirumba-Mwanza katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Jacob Adongo wa Musoma. Katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000 utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Mgambo Shooting na Oljoro JKT.
Nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Maxime ambaye sasa ni kocha wa Mtibwa Sugar ataiongoza timu yake hiyo katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani, Morogoro. Ni kwenye uwanja huo huo ambapo Mtibwa Sugar katika mechi yao iliyopita walichapwa mabao 4-1 na Azam.

Shaa wa Wakilisha achia mpya akiapa raha kwa mashabiki


Msanii Shaa katika pozi

MWANADADA mkali wa muziki wa kizazi kipya, Sarah Kais 'Shaa', aliyekuwa kimya kwa kitambo, ameibuka na 'ngoma' mpya iitwayo 'Promise', akiapa kuwapa raha zaidi mashabiki wake.
Shaa, mkali aliyeibuliwa na shindano la Coca Cola Pop Star na kuja kuunda kundi la pamoja na wakali wenzake wawili, Langa na Witness lililoitwa 'Wakilisha', alisema wimbo huo mpya ni salamu kwa mashabiki wake 2013.
Msanii huyo alisema baada ya kimya tangu aachie wimbo wake uitwao 'Siri ya Penzi', amefyatua ngoma hiyo mpya akiwa mbioni kuendelea kufyatua moja moja ili kuwapa raha mashabiki wake.
"Hizi ni salamu zangu za 2013, nimeachia 'Promise' na kwa sasa najipanga kwa ajili ya vitu vingine vikali ili kuonyesha kuwa 'Shaa' bado nipo na ukali wangu ni ule ule," alisema Shaa.
Msanii huyo alisema kwa sasa anafanya kazi chini ya usimamizi wa Babu Tale na umeneja wa Master J na kwamba mashabiki wake waliomiss kitambo watarajie makubwa zaidi kuliko ilivyokuwa siku za nyuma.

TFF YAOMBA MASHABIKI KUZISAPOTI SIMBA, AZAM KIMATAIFA

Tanzania Football Federation
Affiliated to FIFA, CAF and CECAFA
Karume Memorial Stadium, Uhuru/Shaurimoyo Road
P.O. Box 1574, Dar es Salaam, Tanzania
. Telefax: + 255-22-2861815
E-mail:
tfftz@yahoo.com . Website: www.tff.or.tz
 
 
 

 
 
 
Release No. 026
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 12, 2013
WASHABIKI WAZIUNGE MKONO AZAM, SIMBAShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaka washabiki wa mpira wa miguu kujitokeza kwa wingi wikiendi hii kuzishangilia timu za Azam na Simba zitakazocheza mechi za mashindano ya Afrika jijini Dar es Salaam.
Nguvu ya washabiki ni muhimu katika kuziweza timu hizo kufanya vizuri katika mechi hizo za nyumbani dhidi ya Al Nasir Juba ya Sudan Kusini na Club Libolo ya Angola.
Azam itacheza Jumamosi (Februari 16 mwaka huu) dhidi ya Al Nasir katika mechi ya Kombe la Shirikisho wakati Simba itaikabili Club Libolo kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayofanyika Jumapili. Mechi zote zitachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
LYON, YANGA KUUMANA UWANJA WA TAIFALigi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inamaliza raundi ya 16 kesho (Februari 13 mwaka huu) kwa mechi kati ya wenyeji African Lyon dhidi ya Yanga itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo itakayochezshwa na mwamuzi Martin Saanya kutoka Morogoro inakutanisha timu zenye mazingira tofauti. Wakati Yanga wakiwa ndiyo vinara wa ligi hiyo kwa pointi 33, African Lyon ambayo sasa inanolewa na Salum Bausi inakamata mkia ikiwa na pointi tisa tu.
Nayo Toto Africans itaikaribisha Polisi ya Morogoro kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Jacob Adongo kutoka Musoma. Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000 utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Mgambo Shooting na Oljoro JKT.
Nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Maxime ambaye sasa ni kocha wa Mtibwa Sugar ataiongoza timu yake hiyo katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani, Morogoro. Ni kwenye uwanja huo huo ambapo Mtibwa Sugar katika mechi yao iliyopita walichapwa mabao 4-1 na Azam.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Baby Madaha kutega videoni kidigitali

Baby Madaha katika pozi

LICHA ya kulia na mfumo wa digitali akidai unawalaza kwa kazi zao kutotangazika kama zamani, msanii mahiri wa muziki na filamu nchini, Baby Madaha, ameachia video ya wimbo mpya uitwao 'Nitege'.
Akizungumza na MICHARAZO, Baby alisema video hiyo iliyotengenezwa na watalaam Tudd Thomas na Nash Disigner, siku yoyote anatarajia kuisambaza ili irushwe hewani na vituo vya runinga.
Alisema ameona haja jinsi zaidi ya kutoa video hiyo, kutokana na ukweli ilikuwa imeshakamilika wakati Tanzania ikiingia kwenye digitali.
"Katika muziki nimetoa video ya Nitege, lakini shaka na namna itakavyotangazika ukilinganisha na kazi zangu za nyuma kutokana na mfumo mpya wa urushwaji wa matangazo ya kidigitali,"alisema Madaha.
Alisema mashabiki wao wameshindwa kumudu kununua ving'amuzi, hivyo anakuwa na mashaka na kazi yake itatangazika vipi, ingawa ameamua kukomaa hivyo hivyo.

KIVUMBI LIGI YA MABINGWA ULAYA KUANZA KUTIMKA LEO

Ronaldo akishangilia moja ya mabao yake ambapo kesho atakivaa kikosi chake za zamani Manchester United

KIVUMBI cha hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya kinaanza leo kwa kushuhudiwa timu nne kuanza kusaka tiketi ya kutinga robo fainali ya michuano hiyo.
Celtic ya Uskochi itakuwa uwanja wa nyumbani kuwakaribisha mabingwa wa Italia, Juventus, huku Valencia watamenyana na vinawa wa Ligi ya Ufaransa Paris Saint Germani.
Mechi zote hizo zitachezwa kuanza saa 4;45 usiku kwa saa za Afrika Mashariki, kabla ya kesho mashabiki wa soka ulimwengu kuishuhudia dunia 'ikisimama' kwa muda kupisha pambano la Real Madrid ya Hispania dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya England, Manchester United.
Pambano hilo linasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa timu zote kutokana na uwepo wa Criastian Ronaldo aliyewahi kuichezea na kuipa mafanikio Manchester United ambapo leo atakuwa akiiongoza Real kusaka ushindi kabla ya mechi ya marudiano mwezi ujao.
Pambano jingine la leo litazikutanisha timu za Shakhtar Domestic dhidi ya Borrusia Dortmund ya Ujerumani.

Maskini Malinzi atupwa uchaguzi wa TFF


KATIBU Mkuu wa zamani wa Yanga na aliyeekuwa mgombea wa nafasi ya Urais katika Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi ametupwa katika kinyang'anyiro hicho kinachoitarajiwa kufanyika Februari 24.

Kuenguliwa kwa Malinzi, kunaifanya nafasi hiyo ya kusaka mrithi wa Rais wa sasa wa TFF, Leodger Tenga kusaliwa na mgombea mmoja pekee ambaye ni Makamu wa Rais, Athuman Nyamlani.
Malinzi (kulia) alipokuwa akirejesha fomu za kuwania urais wa TFF
Uamuzi wa kumuengua Malinzi umetolewa jana na Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ya shirikisho hilo iliyokuwa ikipitria pingamizi mbalimbali ambapo Nyamlani alisalimika baada ya kuonekana kuwa utumishi wake serikalini haumzuii kuwa mgombea.
Wengine walioenguliwa ni Michael Wambura aliyekuwa akigowania nafasi ya Makamu wa Rais na Ahmed Yahya aliyekuwa akiwania nafasi ya uenuekiti wa Bodi ya Ligi.
Imeelezwa kuwa Malinzi ameenguliwa kwa sababu ya kukosa uzoefu katika uongozi.
Akizungumza jana baada ya kupata taarifa hiyo, Malinzi alisema kuwa amechoshwa na vikwazo.
Malinzi ambaye katika uchaguzi wa mwaka 2008 alipitishwa kuwa mgombea akichuana na rais wa sasa anayemaliza muda wake, Leodgar Tenga, alinukuliwa jana akisema amechoshwa na pingamizi na vikwazo ambavyo amewekewa kuhusiana na mchakato huo wa kuwania cheo hicho cha juu.
Alisema mapema jana kabla ya kutangazwa rasmi kwa maamuzi hayo kuwa ataheshimu maamuzi yatakayotolewa na kamati hiyo kwa sababu lengo lake la kuwania uongozi TFF ni kutaka kutoa mchango wake katika kuendeleza soka la Tanzania ambalo bado wadau wana kiu ya kupata mafanikio.
"Nimechoka na hali inavyoendeshwa, mimi siendi kuomba kazi, siendi kuomba ajira, siendi kufanya biashara, lengo langu ni kutoa mchango wangu katika kusukuma soka letu," Malinzi ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Mkoa wa Kagera (KRFA) alisema.
Alisema kwamba moja ya sababu zilizomfanya awanie nafasi hiyo ni kutokana na uzoefu alionao.
Malinzi aliwekewa pingamizi na baadaye kukatiwa rufaa na Agape Fue dhidi ya Kamati ya Uchaguzi TFF kupinga kumpitisha akisema kwamba kiongozi huyo hana uzoefu.
John Bocco 'Adebayor' aliyerejea toka kwenye majeruhi

TIMU ya soka ya Azam imesema ipo tayari kuwavaa Al Nasir Juba ya Sudan Kusini, hasa baada ya kurejea dimbani kwa washambuliaji wake waliokuwa majeruhi, Kipre Tchetche na John Bocco 'Adebayor'.
Azam na Al Nasir wanatarajiwa kuvaana Jumamosi kwenye uwanja wa Chamazi, likiwa ni pambano la awali la michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Afisa Habari wa Azam, Jaffer Idd Maganga aliiambia MICHARAZO jana kuwa, kikosi chao kimeshaingia kambini tangu jana asubuhi baada ya kutoka Morogoro ilipotoka kuiadhibu Mtibwa Sugar kwa kuilaza mabao 4-1 katika mechi ya Ligi Kuu.
Jaffer, alisema maandalizi waliyofanya wakati wakijiandaa na duru la pili la Ligi Kuu kwa kucheza michuano ya Mapinduzi na kusafiri katika nchi za DR Congo na Kenya yameiivisha Azam kimataifa.
Alisema kinachowapa faraja zaidi ni kupona kwa washambuliaji wao nyota, Kipre Tchetche ambaye Jumapili aliifungia Azam mabao mawili kati ya manne yaliyoizamisha Mtibwa, huku Bocco akiwa ameanza kufanya mazoezi mepesi na wenzake.
"Kwa kweli Azam tupo kamili gado kukabiliana na wageni wetu Al Nasir Juba, furaha zaidi ni kurejea kwa nyota wetu waliokuwa majeruhi kadhalika kikosi kina ari kubwa kwa ajili ya mechi hiyo ya Kombe la Shirikisho," alisema Jaffer.
Aliongeza japo Bocco ameanza kujifua mazoezi na wenzake bado hawajajua kama ataweza kucheza katika pambano hilo,  kwa madai inategemea maamuzi ya kocha wao John Stewart Hall.
Azam inashiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya msimu uliopita kushika nafasi ya pili kwen ye Ligi Kuu Tanzania Bara nyuma ya Simba ambao watashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.
Simba wenyewe watashuka dimbani Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, kuumana na Libolo ya Angola kabla ya kurudiana nao wiki mbili zijazo ugenini nchini Angola.
Kikosi cha Azam kitakachoshuka dimbani Jumamosi kuivaa Al Nasir Juba


Monday, February 11, 2013

ALIYEPIGWA RISASI NA ASKARI POLISI AKATWA MGUU

      
 Na  Antony Sollo  -  Kishapu.

HALI si shwari katika mgodi wa mwadui,wananchi wamezidi kuuawa na kujeruhiwa kwa risasi huku Serikali ikiwa haina majibu kuhusu kashfa zinazotokea katika  mgodi huo jambo ambalo hadio sasa wananchi wana mpango wa kuvamia mgodi huo kwa lengo la kuharibu mali za mgodi huo.
 
Kufuatia hali hiyo,wananchi wa vijiji vinavyozunguka eneo la mgodi huo wanajipanga kufanya vurugu kubwa katika mgodi huo ili kulipiza kisasi kufuatia kushambuliwa kwa vijana watano ambao waliingia mgodini humo hivi karibuni kama ilivyoripotiwa na Tanzania daima na hatimaye kupigwa risasi na kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za miili yao huku mmoja wa vijana hao bwana Geroge Joseph akikatwa mguu.
Hali hii ni mwendelezo wa taarifa nyingi za kuuawa na kujeruhiwa kwa raia  lakini hakuna ufuatiliaji wowote kutoka kwa viongozi wa Serikali hususani vyombo vya ulinzi na usalama kama jeshi la polisi jambo ambalo kwa siku chache zijazo kama hali hii haitarekebishwa watanzania tukashuhudia mapigano makubwa kati ya walinzi wa mgodi na wananchi.
Matukio haya yamegubikwa na usiri mkubwa huku Viongozi mbalimbali wakiendelea kutupiana mpira na kushindwa kueleza bayana juu ya ukweli wa matukio haya na kibaya zaidi majeruhi aliyepata ulemavu huo bwana George Joseph akiwatuhumu viongozi hao akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kishapu kwa kushindwa kufika kwa muda muafaka kumuona na kumuombea ruhusa kwa uongozi wa mgodi ili aende kupata matibabu.
 
Hali hii inatokana na kwamba mgonjwa majeruhi huyo alikuwa akishikiliwa na uongozi wa mgodi huo kwa tuhuma za kuingia mgodini isivyo halali jambo lililosababisha kumchelewesha kwenda kupata matibabu hivyo kuharibika kwa mguu wake na hatimaye kukatwa.
Kijana huyo alilazwa katika hospitali ya mgodi wa mwadui tangu tarehe 9/01/2013 huku akiwa chini ya ulinzi wa askari wa mgodi huo lakini kukiwa hakuna huduma zilizokuwa zikitolewa jambo lililosababisha aombe kupewa rufaa bila mafanikio ambapo na hatimaye ndugu walifanikiwa kumuondoa hospitalini hapo kwa kutumia nguvu na kumpeleka hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza ambako amelazwa hadi sasa.
Akilalamikia viongozi wa Serikali mgonjwa huyo Bwana George Joseph anasema”ndugu mwandishi,Mkuu wa Wilaya ya Kishapu ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya alikuwa ni mtu wa kwanza kumjulisha juu ya tukio hili na aliahidi kufika hospitalini lakini hakufanya hivyo hadi sasa nimethirika na kuwa mlemavu kwa kukatwa mguu wangu.
Kuhusu kauli ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga kuwa hana taarifa,inashangaza na inasikitisha sana kwani askari waliokuwa wamekuja hapa kwa ajili ya kufanya operesheni walitoka mkoani Shinyanga.
Askari waliofika  kunichukua maelezo nao pia walitoka ofisi ya upelelezi ya Mkoa wa Shinyanga hata operesheni hii huandaliwa na Mkoa,je haya madai kwamba hana na taarifa yana lengo gani kama si kuficha ukweli wa jambo hili? na anafanya hivyo kwa faida ya nani amehoji bwana George.
Wakiongea na Tanzania daima wananchi waliozungumzia tukio hili walisema ndugu mwandishi, kwa kweli kuna idadi kubwa sana ya watu waliouawa na kujeruhiwa katika mgodi huu lakini hatuoni viongozi wetu wakifuatilia masuala haya sijui hawana uchungu na wananchi ambao ndiyo rasrimali ya taifa hili.
Kwa sasa tukio hili limetupa hofu kubwa na sasa tunaiomba Serikali ijiandae kuona machafuko makubwa kwa vile tumechoshwa na vitendo hivi katika maeneo yetu.
tuna mpango wa kwenda kuvamia mgodi na kuchoma ofisi mbalimbali pamoja na kufanya uharibifu mkubwaili kuibua na kuweka wazi manyanyaso tunayofanyiwa na mawekezaji wa mgodi wa Williamson mwadui maana kuna usiri mkubwa mno kuhusu matukio ya unyanyasaji wa wananchi wa Maganzo na vitongoji vyake. 
Akiongea na waandishi wa habari waliotembelea Ofisi za SHILEMA zilizopo katika mji mdogo wa Maganzo, Katibu Msaidizi wa SHILEMA bwana Hamza Yusuph amesema watu wengi wamepoteza maisha na viungo vyao kwa sababu ya kuingia mgodini mwadui pasipo na uhalali wa kuingia mgodini humo,wote tunajua kuwa kuingia mgodini ni kosa la jinai,lakini pia  hatua za watendaji wa jeshi la Polisi  kujichukulia sheria mkononi zinatokana sheria na mamlaka ipi?
 Kwa nini watu hawa wasikamatwe na kufikishwa mbele ya sheria kuliko kufanya ukiukwaji huu wa sheria na kusababisha wimbi la vijana walemavu kuongezeka! Vitendo hivi havikubaliki kabisa alisema bwana Selemani mkaji wa kitongoji cha majimaji mji mdogo wa Maganzo.
Bwana Yusuph amewalalamikia pia viongozi wa kisiasa wanaotumia mwavuli wa kisiasa katika masuala yanayohusu maisha ya watu ili kujijengea umaarufu katika nyakati za uchaguzi huku akiwalaumu viongozi wa kamati ya mzunguko wa mwadui kwa kujali masilahi yao  binafsi na kusahau kwamba wao ni wawakilishi wa wananchi.
Akizungumzia fedha zinazotolewa mgodini hapo bwana Yusuph amesema haelewi kama fedha hizo zinatolewa kama zawadi  au ni wajibu wa kampuni katika kuihudumia jamii hususani huduma za msingi kama Elimu,Afya,Miundo mbinu,Maji,Umeme naBarabara kama ilivyo katika maeneo mengine.
Bwana Yusuph amelaumu pia Serikali kwa kushindwa kuweka wazi mikataba ya Makampuni ya uchimbaji wa madini nchini kwa kuwa wananchi hadi sasa hawaelewi mambo mbalimbali zikiwemo haki zao dhidi ya makampuni ya uwekezaji katika maeneo yao.
 
Tanzania daima ilibisha hodi katika Ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Bwana Justine Sheka na kufanya mahojiano naye ambapo alianza kwa kusema,ndugu mwandishi,sisi kama viongozi wa Serikali Wilayani Kishapu tunashangazwa na uongozi wa mgodi wa Mwadui kwa kuendesha shughuli zake kwa ubabe na usiri katika mapato yanayotokana na mgodi huo.
 
Hadi sasa uingiaji ndani ya mgodi huo una urasimu mkubwa kiasi kwamba hata Mbunge wa Jimbo anapohitaji kuingia na kuangalia utendaji wa shughuli za mgodi huo zinavyofanyika ni shida,unaingia ukiwa chini ya ulinzi mkali na mara nyingine yapo madai kuwa ni lazima utoe taarifa mapema kwa uongozi wa mgodi.
 
Lakini pia amesikitishwa na jinsi Serikali ilivyofanya siri kuhusu uwakilishi wake katika kukagua uzalishaji wa madini na namna ya kupata taarifa mbalimbali ili kuweza kuona kama kweli mali inayopatikana ndiyo inayotolewa taarifa  kama ilivyo katika maeneo mengine yaliyo na migodi.
Inasemekana ni muda mrefu mgodi wa Mwadui umekuwa ukiendesha shughuli za uchimbaji wa madini Wilayani Kishapu bila kuwa na mwakilishi wa Serikali ambaye anafanya ukaguzi jambo linalohofiwa kuporwa kwa madini na kuisababishia Hasara Serikali.
Kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga bwana Evarist Mangala alipotafutwa kujibu malalamiko juu ya tuhuma zinazotolewa na mgonjwa aliyekatwa mguu bwana George Joseph alisisitiza kwamba bado hana taarifa lakini akashauri kwamba mgonjwa aandike barua ya malalamiko juu ya tukio hilo ili aweze kulifanyia kazi.
 
CHANZO:Francis Godwin