STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 2, 2013

Mazoezi ya Miss Kibaha 2013 yapamba moto


Mkufunzi wa Warembo wa Redd's Miss Kibaha Rehema Uzuwiya akizungumza na warembo hawo wakati wa mazoezi yao yanayo endelea katika ukumbi wa Vijana Kinondoni picha na www.burudan.blogspot.com

Warembo wa Redd's miss kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao

Warembo watakao wania taji la Redd's Miss Kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao yanayoendelea katika ukumbi wa vijana Kinondoni Dar es salaam picha na www.burudan.blogspot.com

Kivumbi ya UEFA Ndogo ni leo, Chelsea kupenya kwa Basel

http://www.thenewstribe.com/wp-content/uploads/2013/04/Chelsea-vs-FC-Basel-1.jpg
Vita hii ya Basel na Chelsea inatarajiwa kujirtudia tena usiku wa leo kwenye UEFA League

IKIWA na faida ya ushindi wa mabao 2-1 iliyopata ugenini dhidi ya Basel ya Uswiss, Chalsea itawakaribisha wageni wao hao kwenye nusu fainali ya pili ya Ligi Ndogo ya Ulaya katika pambano litakalochezwa uwanja wa Stanford Bridge, jijini London.
Chelsea am,bayo inashuka dimbani ikiwa na furaha ya ushindi wa mabao 2-0 iliyopata dhidi ya Swansea City katika Ligi Kuu ya England itahitaji ushindi au sare yeyote kuweza kufuzu fainali za michuano hiyo zitakazofanyika Mei 15.
Kocha wa Chelsea, Rafa Benitez ameweka bayana wameweka akili zao kwa ajili ya pambano hilo wakiwa na tahadhari kubwa kutokana na wapinzani wao kutotabirika akikumbukia walivyowaondoa michuanoni Tottenham katika mechi ya robo fainali.
Benitez amenukuliwa akisema watashuka dimbani wakiwa na dhamira kuu ya kuhakikisha wanapata ushindi katika mechi ya leo, lakini hawaipuuzii Waswisi hao ambao wametoka kupokea kichapo cha mabao 3-0 katika mechi ya ligi ya nyumbani kwao dhidi ya Luzern Jumapili iliyopita.
Naye kocha wa Basel Murat Yakin, amedai inahitgaji miujiza kidogo kuweza kuwaondosha Chelsea katika hatua hiyo ya nusu fainali na wao kutinga fainali.
Yakin alisema hata hivyo wachezaji wake wana ari kubwa na kujiamini kupita kiasi katika pambano hilo la leo dhidi ya kigogo kingine cha jiji la London baada ya awali kuiondosha Tottenham kwa mikwaju ya penati kufuatia kutoka sare ya mabao 4-4 katika mechi zote mbili.
Bila shaka ni suala la kusubiri kuona kama vijana wa darajani watatinga fainali ya pili mfululizo ya michuano ya Ulaya baada ya mwaka jana kucheza Ligi ya Mabingwa na kuiondosha patupu Bayern Munich waliotinga tena fainali hizo msimu huu baada ya jana kuing'oa kwa aibu Barcelona kwa mabao 7-0.
Pambano jingine la pili la nusu fainali ya marudiano usiku wa leo ni kati ya timu za Benfica na Fenerbache nchini Ureno.
Wenyeji hao walichezeas kichapo cha bao 1-0 ugenini nchini Uturuki wiki iliyopita, hivyo kuhitaji ushindi ili kuweka hai matumaini ya kucheza fainali hizo za UEFA Ndogo wiki mbili zijazo mjini Amsterdam, Uholanzi.

Redd's Miss Kigamboni 2013 kumekucha!

Somoe Ng'itu (wa pili toka kulia akiwa na wanahabari wenzake

FIFA yatengua uchaguzi wa TFF, kisa...!



Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limelitaka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuanza upya mchakato wa uchaguzi baada ya kubaini kasoro iliyotokana na ukosefu wa kutokuwepo vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadili.

FIFA ambayo ilituma ujumbe wake katikati ya mwezi uliopita kufanya utafiti kuhusu mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa TFF ambao ulisimamishwa baada ya baadhi ya wagombea kulalamika, imetaka uchaguzi ufanyike kabla ya tarehe 30 Oktoba 2013, lakini ukitanguliwa na mabadiliko ya katiba ambayo yatahusisha uundwaji wa vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadili.

Raiswa TFF, Leodegar Tenga aliwaambia waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa shirikisho hilo kuwa suala la Tanzania lilijadiliwa kwenye kikao cha Kamati ya Dharura ya FIFA kilichofanyika tarehe 28 Aprili 2013 na maamuzi yake kutumwa juzi kwa barua iliyosainiwa na KatibuMkuuwa FIFA, Jerome Valcke.

Baada ya kupokea barua hiyo, Rais wa TFF alifunga safari kwenda Dodoma jana kukutana na Mheshimiwa Waziri na Naibu wake pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT). 

“Matarajio yetu sote yalikuwa kupokea majina ya waliopitishwa ili tufanye uchaguzi. Kinyume chake tumepokea maagizo hayo. Hata hivyo tumeona kuwa hili ni jambo la kheri kwa vile siyo tu haki itatendeka bali pia itaonekana imetendeka.” alisema Tenga, ambaye alishatangaza kuwa hatagombea tena urais baada ya kuliongoza Shirikisho kwa vipindi viwili vya miaka minne kila kimoja.

“Lengo letu ni kuhakikisha maagizo hayo yanatekelezwa na uchaguzi kufanyika mapema iwezekanvyo kabla ya tarehe iliyotolewa. Yale mambo nayoweza kufanyika kwa pamoja yatafanyika ili tuharakishe utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na FIFA.”
Uchaguzi wa TFF ulipangwa kufanyik tarehe 23 na 24 Februari 2013 na ulikuwa ukielekea ukingoni, lakini baadhi ya wagombea walienguliwa katika hatua ya mwisho na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na ndipo walipo andika barua FIFA kuomba iingilie kati.

Rais Tenga alisema kuwa ujumbe wa FIFA ulikutana na pande zote zilizoathiriwa na mchakato wa uchaguzi na kwamba baada ya kukusanya taarifa hizo, maagizohayo ya FIFA sasa yatakuwa ni suluhisho la matatizo ya muda mrefu katika uendeshaji wa mpira wa miguu nchini.

Katika barua hiyo, FIFA imeiagizaTFF:
1.   Kuunda vyombo sahihi (Kamati ya Maadili itakayokuwa na vyombo viwili ambavyo ni cha kutoa maamuzi ya awali na cha rufaa) ambavyo mamlaka yake yatakuwa ni kushughulikia masuala ya ukiukwaji wa maadili;
2.   Kufanya mabadiliko ya katiba kwa kuzingatia uundwaji wa vyombo hivyo;
3.   Kuanza upya kwa mchakato wa uchaguzi wa Kamati ya Utendaji kwa kufungua milango kwa wagombea ambao walishachukua fomu na wagombea wapya:
4.   Shughuli hiyo ikamilike ifikapo tarehe 30 Oktoba 2013.
Katika kutekeleza hayo, TFF inatakiwa iitishe Mkutano Mkuu wa Dharura kwa ajili ya kufanya mabadiliko ya Katiba kwa ajili ya kuunda kamati hizo za maadili na Kanuni za Uchaguzi kabla ya kuendelea na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Kamati Mpya ya Utendaji.

Katika maoni yake FIFA imeeleza kuwa katika mchakato, Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliwaengua au kupitisha baadhi ya wagombea kwa kubaini kuwa walikiuka Ibara ya 9 (7) ya Kanuni za Uchaguzi na pia Ibaray a 29 (7) ya Katiba ya TFF ambavyo vinahusisha suala la kufungua kesi mahakamani, kufuja fedha za shirikisho na ukosefu wa uwajibikaji wa pamoja.

Hata hivyo, FIFA ilisema kuwa watu hao walitakiwa waadhibiwe kwanza na kamati husika (kamati za maadili) kabla ya kuenguliwa na kamati za uchaguzi za TFF.

“Kutokana na ukosefu wa kamati za maadili matokeo yake, mmoja wa wagombea amekuwa akienguliwa kwenye uchaguzi kila anapombea bila ya kujua adhabu yake ni ya muda gani,” inasema barua hiyo ya FIFA.

Rais Tenga ameagiza kuitishwa kwa kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji ya TFF kupokea maagizo ya FIFA na kupanga ratiba ya utekelezaji wake kwa lengo la kuhakikisha kuwa mchakato huu unatekelezwa mapema iwezekanavyo.


Shule 20 za Sekondari kuonyeshana ubabe Copa Coca Cola Ilala


JUMLA ya Shule 20 za Sekondari na Academia 10 za soka zinatarajiwa kuchuana katika mashindano ya Copa Coca Cola Wilaya ya Ilala yatakayoanza rasmi Mei 12 wilayani humo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Soka cha Ilala (IDFA) Daud Kanuti alisema timu hizo zitachuana kwenye viwanja vitatu tofauti vya Airwing-Ukonga, Shule ya Benjamini Mkapa, Ilala na Kinyerezi.
Alisema maandalizi ya michuano hiyo yanaendelea vyema ikiwamo kutolewa ratiba ya makundi ya timu hizo shiriki.
"Michuano yetu ya Coca Coca Cola Ilala inaanza rasmi Mei 12 mwaka huu kwa kushirikisha timu 20 za Shule za Sekondari na 10 za vituo vya kukuzia na kuendeleza soka, ambapo zitachuana katika viwanja vitatu tofauti,' alisema Kanuti.
Kanuti aliongeza wakati michuano hiyo ya Coca Coca ikianza Mei 12, Ligi Daraja la Tatu wilayani humo, itaanzaa kutimu vumbi lake Jumamosi Mei 4.
Alisema Ligi hiyo kuwaniwa bingwa wa Ilala na timu za kushiriki Ligi ya Kanda itashirikisha jumla ya timu 20 kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.
Katibu huyo alisema tayari timu zote zimeshapewa ratiba ya michuano hiyo itakayochezwa pia kwenye viwanja vitatu tofauti vilivyopo wilayani humo.

Kaseba kuzipiga na Mkenya mwezi ujao

Japhet Kaseba

BINGWA wa Taifa wa Ngumi za Kulipwa wa uzani wa Kati anayetambuliwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST), Japhet Kaseba anatarajiwa kupanda ulingoni mwezi ujao kupigana na bondia kutoka Kenya, Joseph Odhiambo Magudha katika pambano la kimataifa.
Pambano hilo litakalosindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi litaratibiwa na kampuni ya Bigright Promotion chini ya Ibrahim Kamwe.
Akizungumza na MICHARAZO Kamwe alisema pambano hilo litakalokuwa la raundi 10 litafanyika mwezi ujao jijini Dar es Salaam katika ukumbi na tarehe itakayotangazwa baadaye.
"Kampuni yetu imeandaa pambano la kimataifa litakalomkutanisha Japhet Kaseba dhidi ya Mkenya Joseph Magudha litakalofanyika mwezi Juni na kusindikizwa na michezo nkadhaa ya utangulizi," alisema Kamwe.
Kamwe alisema pambano hilo ni fursa nzuri ya Kaseba kurejea kwenye ngumi za kimataifa baada ya kutamba nyumbani aklitokea kwenye mchezo wa Kick Boxing alipokuwa bingwa wa Afrika na Dunia.
Mratibu huyo alisema maandalizi ya pambano hilo na mengine ya utangulizi yameanza ikiwamo kuwasainisha mikataba mabondia hao kwa ajili ya michezo hiyo ya mwezi Juni.
Alisema mabondia watakaosindikiza pambano hilo la Kaseba na Mkenya ni pamoja na Kamanda wa makamanda atakayezipiga na Ibrahim Maokola, Juma Seleman dhidi ya Issa Omar, Juma Fundi dhidi ya Moro Best na Yohana Matyhayo atakaychpana na Mkenya Joseph Onyango.
Mara ya mwisho kwa Kaseba kupanda ulingoni ni Machi mwaka huu alipopigana na Maneno Osward katika pambano la marudiano la ubingwa wa taifa, ambapo kama ilivyokuwa pigano lao la mwaka jana, Kaseba aliibuka mshindi kwa pointi.

Ni fainali ya Wajerumani, Barca wapigwa tena nyumbani na Bayern

Arjen Robben akionyesha manjonjo ya ushindi

Aah hii aibu bana! Kipa wa Barcelona na beki wake wakiwa hoi

Wachezaji wa Bayern Munich wakipongeza baada ya kuisasambua Barcelona nyumbani kwao jana


Kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Gardiolla aliyetua Bayern Munich akishangilia ushindi wa timu yake mpya na Franky Ribbery


BARCELONA, Hispania
BAYERN Munich walitinga katika fainali ya kwanza ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya itakayokutanisha Wajerumani watupu wakati walipoisambaratisha Barcelona 3-0 kwenye Uwanja wa Nou Camp jana na kusonga mbele kwa jumla ya magoli 7-0.
Mabingwa hao wapya wa Ligi Kuu ya Ujerumani waliimaliza mechi mapema wiki iliyopita kwa ushindi wa 4-0 nchini Ujerumani na hapakuwa na namna ya kufufuka kwa Wahispania hao wakati Arjen Robben alipofunga goli la kuongoza dhidi ya kipa Victor Valdes katika dakika ya 49.
Kudhalilika kwa Barca kulikamilishwa mwishoni mwa mechi wakati Gerard Pique alipojifunga mwenyewe na Thomas Mueller, ambaye alifunga magoli mawili katika mechi yao ya kwanza, akapachika la tatu kwa kichwa.
Barca, kama Bayern ambao wanafukuzia taji la tano la Ulaya, wanategemea kipaji cha Lionel Messi, ambaye anarejea kutoka katika majeraha ya misuli ya nyuma ya paja na ambaye aliachwa benchi, lakini bila ya Mwanasoka Bora wa Dunia huyo hawakuwa na makali yoyote.
Bayern watacheza dhidi ya Borussia Dortmund katika mechi ya fainali kwenye Uwanja wa Wembley mjini London Mei 25 baada ya Dortmund kuitoa Real Madrid kwa jumla ya mabao 4-3 juzi Jumanne.

Cheka ni nouma amzima Mashali na kutibua rekodi yake ya kutopigika


Bondia Fransic Cheka Kushoto akipambani na Thomas Mshali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika sikukuu ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya kumi Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Cheka Kushoto akimshambilia kwa makonde ya nguvu Thomas Mshali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika sikukuu ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya kumi Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya nne Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya nne Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUTraundi ya nne Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' akishangilia ushindi uku akiwa amebebwa juu juu kama mkungu wa ndizi Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Cosmas Cheka kushoto akipambana na Charles Mashali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba siku ya mei mosi Cheka alishinda kwa ponti mpambano huo Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' akimsindikiza wakati wa kupigana bondia Ibrahimu Class 'King class Mawe wakati wa mpambano wake na amos mwamakula
Bondia Amos Mwamakula kushoto na Ibrahimu Class 'King Class mawe' wakisubili matokeo ambapo class alishinda kwa point Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Thomas Mashali kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Fransic Cheka katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT



Shomari kimbau akiwa na Cheka baada ya kumvisha ubingwa wa IBF Africa aliokuwa akiutetea
Kotoka kushoto ni Kocha wa mchezo wa ngumi Kimataifa Rajabu Mhamila 'Super D' mdau ambaye ajajulikana jina Mtaalishaji wa mpambano kati ya Fransic Cheka Vs Thomasi Mashali Adamu Tanaka 'Tunaluza' na MC wa mpambano huo COOL p
Rashidi Mhamila 'Ngade akiwa amepozi na Bad Boy wakati wa onesho hilo



BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa, Francis Cheka usiku wa kuamkia leo ameendeleza rekodi yake ya kuwapiga mabondia wenzake nchini baada ya kumtwanga kwa KO ya raundi ya 10 Thomas Mashali na kunyakua zawadi ya gari na kutetea taji lake la IBF-Afrika.
Cheka kwa kumpiga Mashali amefanikiwa kumvunjia rekodi mpinzani wake ya kutopigika nchini tangu ajitose kwenye ngumi hizo za kulipwa, ambapo kipigo cha jana kilikuwa cha kwanza kwake.
Mashali alikuwa na rekoidi ya kucheza mapambano 9 na kushinda nane na kutoka droo moja, lakini ukali wa ngumi za Cheka zilimfanya asalimu amri katika raundi hiyo ya 10 akiwa amebakisha mbili tu kumaliza mchezo huo uliokuwa wa raundi 12 la uzani wa Super Middle.
Ushindi huo wa Cheka umemfanya kuendeleza rekodi yake ya kuwapiga mabondia karibu wote nchini na kutowahi kupigwa katika ardhi ya Tanzania tangu mwaka 2008 akiwa amewachakaza karibu nyota wote nchini na Afrika Mashariki na Kati.
Cheka kwa kutetea taji lake sasa atapaswa kujiandaa kupambana tena na Mmalawi Chiotcha Chimwemwe aliyemtwanga kwa pointi walipoikutana katika pambano lililofanyika mjini Arusha ambapo alikuwa pia akitetea taji hilo alililotwaa kwa kumtwanga Mada Maugo, Aprili mwaka jana.

Wednesday, May 1, 2013

AZAM INA KILA SABABU ZA KUSHINDA MOROCCO

Khamis Mcha 'Vialli' nyota wa Azam katika pambano lao dhidi ya As Far Rabat jijini Dar na kuisha kwa 0-0

Kikosi Tegemeo cha Azam

Azam wakijifua mjini Rabat

Wachezaji wa Azam, walipokuwa wakijiandaa na pambano lao dhidi ya BYCII

Na Patrick Kahemela, Rabat
KIKOSI cha timu ya Azam Fc ipo mjini Rabat ikijiandaa kukabiliana na AS FAR kwenye mechi ya raundi ya mwisho ya 16 bora za kombe la shirikisho. Azam FC imetua hapa na wachezaji 23, benchi lote la ufundi isipokuwa Ibrahim shikanda pekee aliye masomoni Nairobi na uongozi karibu wote na kwa pamoja kama timu Azam FC ina dhamira ya kuifunga na kuisukuma nje ya mashindano timu ya AS FAR.
Kuna sababu sita zinazoifanya Azam FC iamini na ijiamini kuwa inaweza kushinda kwenye mtanange wa jumamosi hii. Sababu hizo ni maandalizi bora, wachezaji wazuri, Uongozi Mzuri, benchi bora la ufundi chini ya Stewart Hall, Mipango mizuri na dhamira ya kupata mafanikio. Makala hii itakayowajia katika sehemu tatu itachambua vipengele vilivyoaninishwa hapa chini.
MAANDALIZI MAZURI
Timu za Tanzania kwa miaka mingi zimekuwa zikishiriki mashindano ya kimataifa yanayoandaliwa na CAF, kwa Azam FC hii ni mara yake ya kwanza kupata nafasi hii. Lakini unaweza kuona utofauti mkubwa wa maandalizi kati ya Azam FC na timu nyingi za Tanzania na utofauti huo ndiyo unaoifanya Azam FC hadi sasa kuweza kucheza mechi tano pasi na kupoteza mchezo hata mmoja.
Azam FC baada ya kujua kuwa itawakilisha nchi kwenye mashindano ya kimataifa iliamua kufanya juhudi za makusudi za kujiandaa kwa kiwango cha mashindano hayo yanayoandaliwa na CAF.
Azam FC ilifanya ziara na kucheza mechi nane za kimataifa za kirafiki nje ya ardhi ya Tanzania, ilikwenda Kinshasa Congo DRC na kushiriki Congo Charity Cup ambako ilitwaa kikombe kabla ya kusafiri tena hadi Nairobi ambako ilipata nafasi ya kucheza mechi nyingine tatu.
Lengo la ziara hizi ilikuwa ni kuwapa ukomavu na uzoefu vijana wake ili wanapokuwa kwenye mashindano ya CAF hasa wanapocheza mechi za ugenini wasiwe na hofu. Hakika matunda ya ziara hizi tunayaona kwani Azam FC imeshinda ugenini mechi zake zote mbili za awali hadi sasa.
Maadalizi ya Azam FC kwenye mashindano haya pia yalihusisha utafutwaji na usajili wa wachezaji wenye viwango vya kuweza kucheza na kuisaidia timu, uboreshwaji wa kambi ya mazoezi ya Chamazi mapema kwa ajili ya kambi ya nyumbani, ununuzi wa vifaa bora vya mazoezi na kadhalika.
UWEZO WA WACHEZAJI
Timu ni wachezaji, bila ya wachezaji bora wenye nidhamu, viwango bora na malengo ni sawa na bure. Azam FC ililitambua hilo mapema… Azam FC haikukurupuka kusaka wachezaji kwa mkupuo, usajili wa wachezaji kwa ajili ya mashindano ya CAF ulifanyika kwa umakini kwa muda mrefu huku klabu ikijiwekea malengo ya kuwa na kikosi bora kitakochoweza kupambana na kuvifunga vigogo vya soka la Afrika.
Leo ukiwaangalia wachezaji 25 wa Azam FC waliosajiliwa kwenye mashindano ya CAF utaungana nami kuwa ni wachezaji sahihi kwa mashindano haya.
Wachezaji wa Azam FC wana nidhamu na vipaji vya hali ya juu. Wote wana viwango vya kuweza kuwemo kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania na kuanza kwenye kikosi cha kwanza. Hapa nitazungumzia sifa za wachezaji wa eneo la ulinzi tuu kwa ufupi… halafu muendelezo wa makala hii utawaletea wachezaji wa kiungo na baadaye washambuliaji.
MWADINI ALLY; Golikipa chaguo la kwanza la kikosi cha timu ya Taifa ya Zanzibar na sehemu ya kudumu ya kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania. Ana uzoefu mkubwa wa michezo ya kimataifa akiiongoza Zanzibar kushika nafasi ya tatu mara mbili kwenye mashindano ya CECAFA. Ni golikipa hodari ambaye Azam FC tunajivunia kuwa naye
AISHI MANULA, utasemaje juu ya kipaji cha kijana huyu toka Morogoro? Wengi wanamfananisha na golikipa wa zamani wa Tanzania na Simba Mohammed Mwameja. Aishi anajiamini, ana umbo zuri na kipaji kikubwa sana. Ndiyo maana haishangazi kwa nini yeye ni golikipa namba moja wa timu za vijana za taifa na chaguo namba tatu la Taifa Stars ya kocha Kim Poulsen
HIMID MAO; Ana miaka 20 tuu lakini ni mkongwe ndani ya kikosi cha Azam FC, Himid ni kiungo mwenye sifa za kukaba ambaye sasa anacheza kama beki wa kulia wa Azam FC. Hakuna aliyeshangaa jina lake lilipoitwa na Kim Poulsen kuwa sehemu ya wachezaji 30 bora nchini wanaonyemelea nafasi za walio timu ya Taifa. Himid Mao aliibukia kwenye mashindano ya Copa Cocacola na baadaye kuwa nahonda wa timu za taifa za Tanzania chini ya miaka 20. Kabla ya mwalimu wa wakati huo wa Azam FC Itamar Amorim kumpa nafasi kwenye kikosi cha kwanza akitokea Azam Academy. Himid anafanya vizuri sana kwenye kikosi cha Azam FC hadi sasa.
WAZIRI SALUM; huenda ndiye mchezaji mwenye kipaji kikubwa cha kumiliki mpira kuliko wachezaji wote nchini Tanzania kwa sasa. Waziri Salum, naye yumo kwenye daftari la kocha Kim Poulsen na ni mwanachama wa kudumu wa kikosi cha Zanzibar heroes. Mguu wake wa kushoto ni kama mkono wa paka kwani anaweza kufanya lolote na mpita kwa kutumia mguu huu. Ana mbinu za kukaba, ana krosi za hatari na chenga za maudhi. Ni hadhina kubwa kwa Azam FC na taifa la Tanzania
JOCKINS ATUDO; beki bora wa ligi kuu ya Kenya KPL msimu uliopita Jockins Atudo alitua Azam FC wakati wa dirisha dogo la Disemba mwaka jana ili kuimarisha ukuta wa Azam FC kwa ajili ya mashindano haya. Tangia atue Azam FC Atudo amethibitisha kuwa waliomchagua kuwa beki bora hawakukosea. Kocha wa zamani wa Harambee Stars James Nandwa alisema wakati tunataka maoni yake juu ya atudo kabla ya kumsajili kuwa ukiwa na beki kama Atudo unapata vitu viwili, kwanza uongozi ndani ya uwanja pili beki mwenye kipaji, nguvu, kimo na kujitolea… hakika kila kocha angependa kuwa na Atudo kwenye kikosi chake
LUCKSON KAKOLAKI; labda ndiye mchezaji mwenye busara zaidi kwenye kikosi cha Azam FC kiasi kwamba wachezaji wenzake wanamuheshimu na kumkubali kama kaka. Busara hizi za nje ya uwanja pia unaweza kuziona ndani ya uwanja mbapo Luckson amekuwa mhimili mkuu kwa Azam FC hasa pale eneo la ulinzi linapokabiliwa na majeruhi. Kiwango chake cha uchezaji kimekuwa cha uhakika wakati wote na hili alilithibitisha kwenye mechi ya awali dhidi ya AS FAR ambapo aliingia katika dakika ya sita baada ya Atudo kuumia na kucheza kwa ustadi mkubwa sana Luckson ni mchezaji mmoja wapo ambaye tunaweza kusema ana damu ya bluu (yaani ana damu yenye rangi ya Azam FC)
DAVID MWANTIKA; Tanzania tumejaaliwa kuwa na mabeki wazuri lakini hatujawahi kuwana beki wa kiwango cha David Mwantika tangia kuondoka kwenye ramani ya soka kwa Boniface Pawasa. Mwantika hapitiki kwa namna yoyote ile… Mwantika ana nguvu za asili na mwili uliojengeka. Wenyewe wanyakyusa wanamuita Bedui… Mwantika ana spidi ya upepo na amekuwa maarufu ndani ya wachezaji wa Tanzania lakini alikuwa na umaarufu mdogo nje kutokana na timu yake ya Prisons kutopewa nafasi sana na vyombo vya habari. Lakini ukikutana na washambuliaji wa ligi kuu watakuambia kuwa beki wanayemuogopa zaidi nchini ni David. Juzi kim Poulsen amemjumuisha kwenye kikosi chake na bila shaka wala wasiwasi Mwantika atavuka kwenye kikosi cha Young taifa Stars na kuingia kwenye kikosi cha kwanza cha Taifa Stars muda si mrefu
Katika makala zijazo, tutawaletea maelezo ya wachezaji waliosalia wa kiungo na ushambuliaji pamoja na sababu nyingine nne zilizosalia za kwa nini Azam FC itaifunga AS FAR ambazo ni UONGOZI BORA, BENCHI BORA LA UFUNDI, MIPANGO MIZURI, na DHAMIRA

Coastal yaibana Yanga, Lyon byebye VPL

Yanga iliyobanwa uwanja wa Taifa

maafande wa JKT Oljoro waliolazikisha suluhu kwa Ruvu Shooting

Coastal waliochelewesha sherehe za ubingwa za Yanga

Afican Lyon iliyoshuka rasmi Ligi Kuu baada ya kunyukwa na Mtibwa Sugar Manungu
WAKATI Mabingwa wapya wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga wakishikwa kwenye uwanja wa Taifa na Coastal Union ya Tanga kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1, African Lyon imezama rasmi Ligi Daraja la Kwanza baada ya kulazwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar.
Yanga ambayo inakamilisha tu ratiba ya ligi hiyo baada ya Ijumaa iliyopita kutawazwa mabingwa baadaya Azam kung'ang'aniwa na Coastal na kyutoka sare ya 1-1, ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata bao kupitia Jerry Tegete kabla ya Coastal kusawazisha dakika chache baadaye kupitia kwa Abdi Banda na kuzifanya timu hizo ziende mapumziko zikiwa nguvu sawa hali iliyoendelea hadi dakika 90 zilipoisha na hivyo kugawana pointi moja moja na Yanga kufikisha pointi 57 na Coastal 35.
Katika mechi nyingine iliyochezwa uwanja wa Chamazi, JKT Ruvu walijikuta wakizama kwa kulazwa mabao 2-1 na Prisons ya Mbeya, huku uiwanja wa Mabatini Mlandizi wenyeji Ruvu Shooting walibanwa na JKT Oljoro kwa kutofungana.
African Lyon inayoburuza mkia ilijihakikishia kucheza Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao kwa kutunguliwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar katika pambano jingine lililochezwa uwanja wa Manungu, mjini Turiani. Mabao yoye ya washindi yakiwekwa kimiani na mshambuliaji nyota Hussein Javu katika dakika ya 30 na 59.
Mechi nyingine ya ligi hiyo ilichezwa mjini Morogoro kati ya Polisi Moro dhidi ya wageni wao Kagera Sugar iliyoisha kwa wenyeji kushinda bao 1-0 na kuifanya timu hiyo kuendelea kuvuta pumzi kusubiri kuona hatma yao katika ligi hiyo kwa kufikisha pointi 22 sawa na Toto African..

Mikoa 18 yapata mabingwa wake


Na Boniface Wambura
Mikoa 18 kati ya 27 ya kimpira tayari imeshapata mabingwa wao kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa itakayoanza Mei 12 mwaka huu chini ya usimamizi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Timu tatu za juu katika Ligi hiyo ya Mabingwa zitapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao (2013/2014). Ligi ya FDL ina jumla ya timu 24 ambapo tatu katika ligi hiyo zilizoshuka daraja msimu huu ni Moro United ya Dar es Salaam, Small Kids ya Rukwa na Morani FC ya Manyara.

Mabingwa waliopatikana hadi sasa na mikoa yao kwenye mabano ni Abajalo SC (Dar es Salaam 2), Biharamulo FC (Kagera), Flamingo SC (Arusha), Friends Rangers (Dar es Salaam 3), Katavi Warriors (Katavi), Kiluvya United (Pwani), Kimondo FC (Mbeya) na Machava FC (Kilimanjaro).

Wengine ni Magic Pressure FC (Singida), Mbinga United (Ruvuma), Mji Njombe (Njombe), Polisi Jamii Bunda FC (Mara), Red Coast FC (Dar es Salaam 1), Rukwa United (Rukwa), Saigon FC (Kigoma), TECKFOLT FC ya Kilombero ambayo ni Shule ya Sekondari (Morogoro) na UDC FC ya Ukerewe (Mwanza).

Kila klabu inatakiwa kulipa ada ya ushiriki ambayo ni sh. 100,000 wakati usajili wa wachezaji wa timu hizo ni uleule uliofanyika katika Ligi ya Mkoa na unatakiwa kuwasilishwa TFF kwa ajili ya uthibitisho. TFF inapenda kusisitiza kuwa hakuna usajili mpya wa wachezaji kwa ajili ya ligi hiyo.

Mtanzania mwingine aula Norway


Na Boniface Wambura
Shirikisho la Mpira wa Miguu Norway (NFF) limetuma maombi ya kupatiwa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Mtanzania Godfrey Mlowoka ili aweze kucheza mpira nchini humo.

NFF inamuombea hati hiyo Mlowoka ili aweze kujiunga na klabu ya Ekne IL kama mchezaji wa ridhaa ambapo klabu yake ya zamani aliyokuwa akiichezea nchini imetajwa kuwa Sadani.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanyia kazi maombi hayo na mara taratibu zote zitakapokamilika hati hiyo ya uhamisho itatumwa nchini Norway.

Azam waendelea kujiwinda Morocco

Kocha Stewart Hall akiwanoa wachezaji wake Morocco


WAWAKILISHI pekee wa Tanzania katika michuano ya kimataifa, Azam ambayo iko jijini Rabat kwa ajili ya mechi ya marudiano ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho dhidi ya AS FAR Rabati ya huko inaendelea vizuri na mazoezi.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari Msaidizi wa Azam FC, Jaffer Idd maandalizi yanakwenda vizuri kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Jumamosi (Mei 4 mwaka huu).

Msemaji huyo alisema wachezaji wana ari kubwa ya kuwapa raha watanzania na kuomba wazidi kuimbea kila la heri ili kupata ushindi Jumamosi na kutinga hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo ya pili kwa ukubwa Afrika.

Yanga, Coastal Union hapatoshi leo Taifa


Mabingwa wapya wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga

WAKIWA tayari na uhakika, mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu 2012/13 Yanga, wanashuka katika dimba la Taifa jijini Dar es Salaam leo kuvaana na Coastal Union ya Tanga, kila mmoja akitamba kutaka kulinda heshima yake mbele ya mwenzake.
Yanga licha ya kuwa bingwa tayari, imedai itateremka katika dimba hilo kuibuka na pointi tatu muhimu ili kulinda heshima na hadhi yao kama vigogo vya soka hapa nchini na Afrika Mashariki na Kati.
Kiburi hicho cha Yanga kinatokana na maandalizi ya mwisho waliyoyafanya wiki hii katika gym ya Quality Center pamoja na mazoezi kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Loyola, Mabibo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa klabu hiyo, Baraka Kiziguto, kikosi kizima kipo fiti kwa ajili ya mechi mbili zilizosalia na kudai kuwa, Salum Telela aliyekuwa anasumbuliwa na nyama za paja naye kajumuika na wenzake.
Coastal kwa upande wao wametamba kuwa lengo lao kubwa katika pambano dhidi ya Yanga ni kunyakua pointi tatu sambamba na kutibua sherehe za ubingwa wao waliotwaa Ijumaa iliyopita baada ya kuwabana Azam na kutoshana nao nguvu ya kufungana bao 1-1 mjini Tanga.
Coastal wapo nafasi ya sita katika msimamo ikitanguliwa na timu za Simba na Mtibwa Sugar, ikiwa na pointi 34 iwapo itaisimamisha Yanga itaweza kufikisha pointi 37 na kushika nafasi ya tano ila itategemea na matokeo ya pambano la Mtiwa sugar dhidi ya African Lyon linaloichezwa pia jioni ya leo.
Nayo Kagera Sugar iliyo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo itakuwa mgeni wa Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro huku Azam Complex Chamazi, maafande wa JKT Ruvu na Tanzania Prisons watapigishana kwata, wakati Ruvu Shooting itakuwa nyumbani kwenye uwanja wake Mabatini Mlandizi, Pwani kuwakabili ndugu zao Oljoro JKT ya Arusha.

Cheka, Mashali kumaliza ubishi leo PTA

Mabondia Francis Cheka (kulia) na Thomas Mashali wakiwa na Rais wa IBF/USBA, Onesmo Ngowi na Promota wa pambano lao, Tanaka Juma kabla ya kupima uzito jana
 
MABONDIA Francis Cheka 'SMG' na Thomas Mashali 'Simba Asiyefugika' leo wanatarajiwa kumaliza ubishi baina yao wakati watakapopanda ulingoni kuzipiga katika pambano la kimataifa la kuwania ubingwa wa IBF-Afrika.
Cheka na Mashali walioipimwa afya na uzito wao jana asubuhi na kukutwa wote wana kilo 74 watapigana katika pambano hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam ambalo litasindikizwa na mapambano mengine 10 ya utangulizi.
Mabondia hao walitambiana jana wakati wa zoezi hilo la upimaji afya na uzito kila mmoja akitamba kuwa ni lazima leo ataibuka na ushindi kutwaa taji hilo pamoja na gari aina ya Noah watakayoigombania.
Cheka ndiye bingwa mtetezi wa taji hilo alililolitwaa mwaka jana kwa kumpiga Mada Maugo na ametamba kwamba hana hofu na Mashali ambaye ni bingwa wa Afrika Mashariki na Kati.
Mratibu wa pambano hilo, Yasin Abdallah 'Ustaadh' alisema kila kitu kimekaa sawa kwa ajili ya pambano hilo na kwamba  litachezeshwa na mwamuzi Jon Shipanuka kutoka Zambia na kusawidiwa na majaji Daud Chikwanje wa Malawi, Steve Okumu wa Kenya na Ismail Sekisambu wa Uganda.
Msimamizi mkuu atakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Viwango na Ushindi wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBC, Boniface Wambura anayemwakilisha Rais wa IBF/USBA, Onesmo Ngowi ambaye ndiye aliyekuwa asimamie pambano hilo anatarajiwa kwenda Ghana kusimamia pambano jingine la kimataifa.

Real Madrid watupwa nje Ligi ya Ulaya licha ya ushindi wa nyumbani

Kipa Ike Casillas, akimliwaza Sergio Ramos aliyekuwa akilia baada ya Madrid kung'olewa kwenye nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya jana usiku

LICHA ya kupigana kiume na kujipatia mabao 2-0 dhidi ya Borussia Dortmund, kocha Jose Mourinho na vijana wake wa Real Madrid wamejikuta wakishindwa kutimiza ndoto za kucheza fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya ili kusaka taji la 10 kwa kutupwa nje ya michuano hiyo kwa jumla ya mabao 4-3.
Madrid ikiwa dimba la nyumbani la Santiago Bernabeu, nchini Hispania ilikuwa ikihitajika kupata ushindi wa mabao 3-0 ili kuing'oa Dortmund, lakini uwezo wao uliishia kwa kuambulia mabao hayo mawili ambayo hata hivyo hayawajasaidia kutokana na mechi ya awali wiki iliyopita kunyukwa mabao 4-1.
Mabao ya ushindi kwa Madrid jana yaliwekwa kimiani dakika za lala salama baada ya wageni wao kuwabana kipindi kizima cha kwanza na nusu ya kile cha pili kwa kutofungana.
Karim Benzema aliiandikia Madrid bao dakika ya 83 akimalizia kazi ya Mesut Ozil kabla ya dakika tano baadaye Sergio Ramos kuongeza la pili na kuwapoa wenyeji imani ya kupata bao jingine la kuwavusha hatua hiyo ya nusu fainali.
Hata hivyo hadi filimbi ya mwisho ya mwamuzi Howard Webb kutoka England ikilia kuashiria kumalizika kwa pambano hilo wenyeji Madrid walikuwa washindi wa 2-0, lakini ushindi ambao haukuwasaidia kutinga fainali ya michuano hiyo na kuiacha Dortmund wakitangulia kumsubiri mshindi wa nusu fainali nyingine ya leo.
Nusu fainali hiyo inazikutanisha timu za Barcelona ya Hispania itakayoikaribisha Bayern Munich ya Ujerumani, ikiwa na deni la kipigo cha mabao 4-0 ilichopewa wiki iliyopita ilipocheza ugenini.
Kama ilivyokuwa kwa Madrid, Barcelona inayokaribia kutwaa ubingwa wa La Liga, itakuwa na kazi pevu ya kuwaondosha Wajerumani hao ambao msimu huu wameonekana kuwa moto wakiwa tayari wameshanyakua taji la Bundesliga hata kabla ligi haijamalizika.

Tuesday, April 30, 2013

Simon Mberwa kuzihukumu Yanga, Coastal Union

Wachezaji wa Yanga wataendelea kushangilia ushindi kama hivbi kesho kwa Coastal Union?

Na Boniface Wambura
MWAMUZI Simon Mberwa ndiye atakayezichezesha timu za Yanga na Coastal Union katika pambano lao namba 172 la Ligi Kuu Tanzania Bara inayoingia raundi ya 25 kesho kwa michezo mitano tofauti katika miji ya Dar es Salaam, Turiani, Morogoro na Mlandizi.

Licha ya kuwa tayari Yanga imetawazwa kuwa mabingwa wa VPL msimu huu (2012/2013), mechi dhidi ya Coastal Union itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni moja kati ya zitakazovuta macho na masikio ya washabiki wa mpira wa miguu nchini.

Mechi hiyo namba 172 itachezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka Pwani akisaidiwa na Said Mnonga na Charles Chambea wote wa Mtwara wakati mwamuzi wa mezani atakiwa Hashim Abdallah wa Dar es Salaam. Kamishna wa mechi hiyo ni David Lugenge kutoka Iringa.

Viingilio katik mechi hiyo itakayoanza saa 10.15 jioni ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 8,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000. Tiketi zitauzwa uwanjani siku ya mchezo.

Mtibwa Sugar itakuwa mwenyeji wa African Lyon katika mechi namba 170 itakayochezeshwa na mwamuzi Dominic Nyamisana wa Dodoma kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro. Nayo Kagera Sugar iliyo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo itakuwa mgeni wa Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam na wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 7,000 uko tayari kwa mechi kati ya JKT Ruvu na Tanzania Prisons. Nayo Ruvu Shooting itakuwa nyumbani kwenye uwanja wake Mabatini ulioko Mlandizi, Pwani kuikabili Oljoro JKT kutoka Arusha.

Mtanzania apewe ITC ya kucheza Msumbiji


Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Yusuf Kunasa kucheza nchini Msumbiji.

Shirikisho la Mpira wa Miguu cha Msumbiji (FMF) lilituma maombi TFF kumuombea hati hiyo Kunasa anayekwenda kujiunga na timu ya Estrela Vermelha da Beira inayocheza Ligi Kuu nchini humo.

Kunasa ambaye msimu huu hakuwa na timu (free agent) amejiunga na timu hiyo akiwa mchezaji wa ridhaa (amateur). Zaidi ya wachezaji kumi kutoka Tanzania hivi sasa wanacheza katika klabu mbalimbali nchini Msumbiji.

Simba na Polisi Moro wavuna Mil 18 tu!


 
Na Boniface Wambura
PAMBANO namba 163 la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa juzi (Aprili 28 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Simba kuibuka ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Polisi Morogoro limeingiza sh. 18,014,000.

Watazamaji 3,145 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 3,564,252.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 2,747,898.31.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 2,841 na kuingiza sh. 14,205,000 wakati idadi ndogo ya washabiki ilikuwa ya kiingilio cha sh. 20,000 kilichovutia washabiki 36 na kuingiza sh. 720,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 1,812,331.75, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 1,087,399.05, Kamati ya Ligi sh. 1,087,399.05, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 543,699.53 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 422,877.41.

Coastal Unioni kutibua sherehe za ubingwa Jangwani kesho?




Coastal Union
KIVUMBI cha Ligi Kuu Tanzania Bara kinatarajiwa kuendelea tena kesho kwa michezo sita, likiwamo la Mabingwa wapya wa ligi hiyol, Yanga dhidi ya wagosi wa Kaya, Coastal Union walioapa kuwatibulia wana Jangwani sherehe zao za ubingwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga ilitawazwa kuwa mabingwa Ijumaa iliyopita baada ya wapinzani wao wa karibu Azam kulazimishwa sare ya bao 1-1 na wagosi hao wa kaya waliokuwa kwenye uwanja wao wa Mkwakwani-Tanga.
Uongozi wa Yanga na benchi la ufundi la timu hiyo, liemsisitiza kuwa kunyakua kwao ubingwa hakuwafanyi walegeze makali yao ambapo tangu kuanza kwa duru la pili hawajapoteza mechi yoyote.
Hata hivyo kocha wa Coastal, Hemed Morocco amenukuliwa juzi akisema kuwa wamekuja Dar kwa ajili ya kutibua furaha ya ubingwa ya Yanga na kwamba mabingwa hao wasitarajie mteremko kwani lengo lao kuona wakimaliza ligi wakiwa kwenye Tatu au Nne Bora.
Wakati Yanga na Coastal zikitambiana hivyo kabla ya kuvaana kesho Dar, michezo mingine itakayochezwa kesho ni pamoja na lile la Mtibwa Sugar dhidi ya 'vibonde' Agfrican Lyon ambayo imeshashuka daraja, japo bado hawajatangazwa rasmi na TFF kama desturi.
Timu hizo zitaumana kwenye uwanja wa Manungu Complex, Turiani, ambapo Mtibwa itakuwa ikisaka pointi za kuwafukuzia ndugu zao, Kagera Sugar waliopo nafasi ya tatu katika msimamo.
Kagera wenyewe watakuwa ugenini mjini Morogoro kuvaana na Polisi Moro ambayo kama ilivyo kwa Lyona na Toto ni kama zimeshajikatia tiketi ya kurudi Ligi Daraja la Kwanza ilikoicheza msimu uliopita kabla ya kupanda Ligi Kuu msimu huu.
Polisi na Lyon zote zina pointi 19 kila moja na hata zikishinda mechi zao za mwisho zitafikisha pointi 25 ambazo zimerukwa na asilimia kubwa ya timu zinazoshiriki ligi hiyo itakayofikia tamati yake Mei 18.
Pambano jingine la kesho litazikutanisha timu za maafande za Ruvu Shooting itakayokuwa nyumbani kuwakabili wageni wao JKT Oljoro kwenye uwanja wa Mabatini-Mlandizi Pwani.
Tayari Afisa Habari wa Ruvu, Masau Bwire alemchimba mkwara kwamba vijana wao wapo tayari kutoa dozi kwa Oljoro kabla ya kuwakabilia Simba Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, baada ya mechi yao ya awali kusogezwa mbele kitatanishi dakika za lala salama kabla ya kuanza kwake.
Bwire alisema lengo lao ni kuhakikisha mechi zao nne zilizosalia wanazishinda zote na kuwa fanya wamalize msimu wakiwa na pointi 42 zinazoweza kuwaweka katyika nafasi ya Tatu Bora au Nne msimu huu.
Mchezo wa mwisho kwa kesho utachezwa kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam kwa maafande wa JKT Ruvu watakapowakaribisha askari wenzao wa Magereza, Prisons-Mbeya ambazo hazina cha kupoteza kwenye msimamo wa ligi hiyo kutokana na kwamba zote hazina nafasi ya ubingwa wala kushuka daraja.
Msimamo wa Ligi hiyo kwa sasa ni kama ifuatayvyo:


                             P      W     D     L     F      A     D     Pts
Young Africans      24    17     5     2     44     13    31    56
Azam                    24    14     6     4     42     20    22    48    
Kagera Sugar        23    11     7     5     26     18     8     40     
Simba                   23    10     9     4     34     22    12     39
Mtibwa Sugar       24     9      9     6     27     24     3      36   
Coastal Union       24     8    10     6     24     21     3      34    
Ruvu Shooting      23     8     6      9     21     22     -1     30     
JKT Oljoro FC    24     7     7     10    22     28     -6     28     
Tanzania Prisons   24     6     8     10    14     21     -7     26    
Ruvu Stars           24      7     5     12    20     37     -17   26
JKT Mgambo       23     7     4     12    15     23     -8     25
Toto Africans       25      4     10   11    22     33     -11    22
African Lyon        24      5     4     15     16    36     -20     19
Polisi Morogoro   24      3    10    11     12    23     -11     19    
             

Mourinho na vijana wake kuvuna nini leo Ulaya?

http://www.footballtarget.com/wp-content/uploads/2012/11/real-madrid-vs-borussia-dortmund-match-preview-champions-league.jpg
KOCHA Jose Mourinho na vijana wake wa Real Madrid leo wana kibarua kizito cha kuudhibitishia dunia kwamba soka lina maajabu yake watakapowakaribisha Borussia Dortmund nyumbani kwao, Santiago Bernabeu katika nusu fainali ya marudiano wakiwa na deni la kipigo cha mabao 4-1 walichopewa ugenini.
Mourinho na vijana wake walichezea kichapo cha mabao 4-1 ugenini nchini Ujerumani katika pambano la kwanza la Nusu Fainali ya michuano hiyo na hivyo leo watalazimika kulipa kisasi ili  kutinga fainali na kusaka taji la 10 na la kwanza tangu mwaka 2002.

Madrid watahitajika kushinda mabao 3-0 ili kutinga fainali za Ulaya baada ya misimu kadhaa ya ukame wa taji hilo tangu ilipotwa mara ya mwisho mwaka 2002.
Hata hivyo huenda isiwe kazi rahisi kwa vijana wa Santiago Bernabeu kutokana na ukweli wapinzani wao wapo vyema msimu huu licha ya kutemeshwa taji la ubingwa wa Bundesliga na Bayern Munich.
Dortmund wanasaka heshima baada ya kutwaa taji hilo mara ya mwisho mwaka 1997, hivyo huenda hawatakubali kuipoteza nafasi waliyopata safari hii kwa mabao manne ya Robert Lewandowski aliyefunga katika pambano la awali wiki iliyopita.
Wakati hatma ya Madrid na Dortmund ikitarajiwa kufahamika usiku wa leo, mabingwa wengine wa zamani wa Ulaya, Barcelona na Bayern Munich zenyewe zitakuwa na kibarua kingine kesho nchini Hispania.
Barcelona iliyocheze kichapo cha aibu wiki iliyopita ugenini kwa kulala kwa mabao 4-0 itakuwa nyumbani kujaribu kutupa karata yake kwa wageni wao ambao msimu huu wanatisha kisoka barani Ulaya.
Ikiwategemea nyota wake kama Xavi, Iniesta, Cesc Fabregas na Lionel Messi, Barca itakuwa na kazi pevu kulipiza kisasi na kutaka kupenya katika pambano hilo ili kucheza fainali Mei 25 itakayochezwa kwenye uwanja wa Wembley, Uingereza.
Je, ni Wahispania au Wajerumani watakaoenda London kwenye fainali hizo? Tusubiri tuone maana soka lina maajabu yake.

Bi Hindu ashirikishwa Fungate la Kifo



MTUNZI wa riwaya na simulizi za kusisimua anayezidi kuja juu nchini, Ramadhan Yahya, ameamua kugeukia fani ya filamu akifyatua kazi iitwayo 'Fungate la Kifo', iliyowashirikisha wasanii mbalimbali akiwemo nyota wa Kaole Sanaa, Chuma Suleiman 'Bi Hindu'.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Yahya aliyewahi kutamba na vitabu kama 'Uchawi Uliosumbua Maisha Yangu, 'Bibi Yangu Mchawi', na 'Katikati ya penzi' alisema filamu hiyo mpya imekamilika na inafanyiwa mipango ya kuanza kuisambaza.
Yahya alisema hiyo ni filamu yake ya pili baada ya ile ya 'Uchawi Uliotesa Maisha Yangu' iliyotokana na kitabu chake cha awali na imewashirikisha wasanii mchanganyiko wazoefu na chipukizi.
Aliwataja baadhi ya wasanii hao ni Chuma Suleiman maarufu kama 'Bi Hindu', Maua Mbwana na wasanii wengine wanaoibukiwa kwenye fani hiyo.
"Baada ya filamu yangu ya kwanza kufanya vyema kwa sasa natarajia kuja na filamu ya 'Fungate la Kifo' ambayo imeshirikisha wasanii mchanganyiko," alisema Yahya.
Aliongeza kuwa, tofauti na filamu ya awali 'Fungate la Kifo' ataisambaza mwenyewe kwa kile alichodai filamu ya awali hakuambulia cha maana cha kujivunia.
"Nitaisambaza mwenyewe, maana watu tunaowaamini wanatuumiza mno, tunatumia gharama kubwa kuzalisha filamu, lakini malipo tunayoambulia ni mkia wa mbuzi, tunawanufaisha wao, najaribu mwenyewe nione inakuwaje," alisema.
Aidha mtunzi huyo wa hadhithi na mchora katuni, alisema kwa sasa anafanya mipango ya kusaka mfadhili wa kusimamia kazi zake ili fedha zitakazopatikana katika sanaa yake aziwekeze kwa kuanzisha asasi ya kuwasaidia yatima, wajane na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.

MAZOEZI YA MISS KIBAHA 2013 YAZIDI KUPAMBA MOTO

Mkufunzi wa Warembo wa Miss Kibaha Rehema Uzuwiya akizungumza na warembo hawo wakati wa mazoezi yao yanayo endelea katika ukumbi wa Vijana Kinondoni

Warembo wa miss kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao

Warembo watakao wania taji la Miss Kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao yanayoendelea katika ukumbi wa vijana Kinondoni Dar es salaam