STRIKA

USILIKOSE

Thursday, June 13, 2013
TFF yawafungia waamuzi watatu, kisa...!
Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefungia miezi mitatu waamuzi watatu walioshindwa kuchezesha mechi namba 32 ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kati ya Mpwapwa Stars ya Dodoma na Machava FC ya Kilimanjaro iliyokuwa ichezwe Juni 2 mwaka huu Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
TFF kupitia Kamati yake ya Waamuzi iliyokutana katika kikao chake cha Juni 12 mwaka huu kupitia taarifa mbalimbali za waamuzi wa RCL ilibaini makosa yaliyofanywa na baadhi ya waamuzi na kuyatolea uamuzi.
Waamuzi hao waliofungiwa ambao wanatoka mkoani Singida ni Jilili Abdallah, Amani Mwaipaja na Theofil Tegamisho. Wamefungiwa kwa kutoripoti katika kituo walichopangiwa (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma) na kutoa taarifa ya uongo kwa kushirikiana na Kamishna wa mechi hiyo.
Kanuni iliyotumika kuwafungia ni ya 28 kifungu (d) na (g) ya Ligi za TFF, na adhabu hiyo imeanza Juni 13 mwaka huu. Waamuzi hao pamoja na kamishna badala ya kwenda Uwanja wa Jamhuri, wao walikwenda kwenye Uwanja wa Mgambo ulioko Mpwapwa na kuandika ripoti iliyoonesha kuwa timu ya Machava FC haikufika uwanjani wakati wakijua kuwa mechi hiyo ilitakiwa kuchezwa katika Uwanja wa Jamhuri.
Mhe Sugu, Sir Nature kumpiga tafu Anaconda Nyumbani Lounge
![]() |
Jide katika pozi |
MMOJA wa waasisi wa muziki wa kizazi kipya nchini ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini-ChADEMA, Mhe. Joseph Mbilinyi, Sir Juma Nature na Komandoo Hamza Kalala ni baadhi ya watakaomsindikiza onyesho la Lady Jaydee 'Anaconda' katika maadhimisho ya miaka 13 tangu ajitose kwenye fani hiyo.
Onyesho hilo la Anaconda maarufu kama Binti Machozi a.k.a Comandoo litafanyika kwenye ukumbi wa Nyumbani Lounge kuanzia saa 3 usiku ambapo mwanadada huyo ameanika hadharani mipango mizima ya onyesho lake hilo.
Kwa mujibu Jide kupitia akaunti yake ya Twitter ni kwamba kesho atapigwa tafu na Mh Sugu, mmoja wa watu waliomuibua kisanii.
Jide ambae hivi karibuni ameachia wimbo mpya unaopatikana
kwenye album yake ‘Nothing but the truth’ inayoitwa Yahaya, amepost kupitia
kupitia ukurasa wake wa facebook na pia katika akaunti yake ya Twitter kuonesha
list ya wasanii watakaopanda jukwaani, na pia uwepo wa Sugu.
” Miaka 13 ya Lady JayDee, Ijumaa ya kesho shughuli inaanza
rasmi saa 3:00 usiku...Ukiskia paaaa ujue show imeisha
1. Prof Jay 2. Juma Nature 3. Grace Matata 4. Hamza Kalala
5. Wakazi na ugeni wa Mh. Joseph Mbilinyi a.k.a SUGU
Nyimbo zote unazozipenda zitalia tar 14 June, pale Nyumbani
Lounge sababu yaaaaa sababu yaaaaaa ?????????”
Sidhani kama utaikosa hafla hiyo ambayo itatumika pia kusimikwa rasmi kwa Jide jina la 'Komandoo' na mkongwe Hamza Kalala.
Ivory Coast wakitarajia kutua leo, tiketi za pambano la Stars kuanza kuuzwa kesho
![]() |
Wanaume wa Tanzania watakawakabili Tembo wa Ivory Coast Jumapili Taifa |
WAKATI timu ya Ivory Coast inatarajiwa kuwasili leo usiku (Juni 13 mwaka huu) kwa ndege maalum, tiketi kwa ajili ya mechi kati yake na Taifa Stars itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa zinaanza kuuzwa kesho mchana (Juni 14 mwaka huu) kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Vituo vitakavyotumika kwa mauzo hayo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.
Viingilio katika mechi hiyo ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika katika kundi C ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani, sh. 7,000 viti vya rangi ya bluu, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C, sh. 20,000 kwa VIP B wakati VIP A itakuwa sh. 30,000.
Pia viti 100 vilivyo katika sehemu ya Wageni Maalumu (VVIP) vitauzwa kwa sh. 50,000 kila kimoja. Tiketi hizo zitauzwa katika ofisi za TFF, na watakaonunua watapewa kadi maalumu zenye majina yao, majina ambayo pia watayakuta katika vita watakavyokaa. Kwa maana hiyo hakutakuwa pasi maalumu (free pass) za kuingia VVIP.
TFF yampongeza Rais mpya ZFA
![]() |
Rais wa TFF, Leodger Tenga |
Amesema ushindi aliopata Faina unaonyesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa ZFA walivyo na imani naye katika kuhakikisha maendeleo ya mpira wa miguu visiwani humo.
Rais Tenga amesema ni imani yake kuwa Rais Faina ataendeleza ushirikiano uliopo kati ya TFF na ZFA kwa ajili ya ustawi wa mpira wa miguu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kumtakiwa kila kheri katika wadhifa wake huo mpya.
Musonye afichua walijua Tanzania haitashiriki Kagame 2013
![]() |
Katibu Mkuu wa Musonye |
Akizungumza na NIPASHE kwa simu jana, Musonye alisema kuwa walishajua mapema kwamba Tanzania haiko tayari klabu zake zishiriki katika mashindano hayo yaliyopangwa kuanza Juni 18 hadi Julai 2 nchini Sudan, hivyo wataendelea na timu kutoka mataifa mengine.
"Tulijua mapema kwamba klabu za Tanzania hazitashiriki michuano hii baada ya serikali ya nchi hiyo kuingiwa na hofu ya usalama wa nchi ya Sudan ambako mashindano ya mwaka huu yanafanyika. Tutaendelea na timu ambazo ziko tayari kushiriki," alisema Musonye.
"Hata kama waziri asingesema leo (jana), tulishajua tangu mapema kuwa hawashiriki, lakini watambue kwamba michuano hii ina kanuni zake, ukizikiuka unaadhibiwa, aliongeza Katibu Mkuu huyo." Hata hivyo, Kenya ambayo ilikuwa inawakilishwa na klabu ya Tusker, nayo ilishatuma barua Cecafa kujitoa katika michuano hiyo.
Mashindano hayo yanayodhaminiwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, mwaka huu yamepangwa kuchezwa katika miji miwili ya Kadugli, uliopo Kordofan Kusini na Alfashery, uliopo Darfur Kaskazini, eneo ambalo kwa muda mrefu limekumbwa na vita vya wenyeji.
Juni Mosi mwaka huu akijibu hoja za wabunge walizozitoa katika kuchangia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bungeni mjini Dodoma, Waziri wa Wizara hiyo, Bernard Membe alisema kuwa hali ya usalama mjini Darfur ni ya wasiwasi kwa sababu watu wanaokwenda huko wanapokewa na vikosi vya magari ya jeshi na huvishwa nguo ambazo hazipenyezi risasi.
Timu tatu za Tanzania wakiwamo mabingwa watetezi wa kombe hilo, Yanga, mabingwa wa mwaka jana, Simba na Super Falcon ya Zanzibar ni miongoni mwa timu 13 zilizotakiwa kushiriki katika michuano hiyo mwaka huu.
Mapema jana, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage alisema kuwa baada ya kuzungumza na Waziri Membe jana asubuhi Bungeni Mjini Dodoma na kuelezwa kuwa hali ya usalama Darfur ni mbaya, hayuko tayari kupeleka timu yake katika mashindano hayo.
"Nimezungumza na Waziri Membe na Naibu Waziri wa Wizara yenye dhamana na michezo (Amos Makalla) leo (jana). Waziri Membe amesema Sudan si shwari, hivyo klabu ya Simba haitapeleka timu katika michuano ya Kombe la Kagame mwaka huu. Hilo ndilo tamko rasmi la Simba baada ya kuhakikishiwa na waziri," alisema Rage, ambaye pia ni Mbunge wa Tabora Mjini (CCM).
Hata hivyo, simu ya Waziri Membe ilikuwa haipatikani jana kuzungumzia suala hilo. Tanzania ina kikosi maalum kinachoshiriki kulinda amani nchini Sudan.
Chanzo:NIPASHE
Diamond, Prezzo kupimana ubavu usiku wa Matumaini
![]() |
Diamond |
![]() |
Prezzo |
MSANII nyota wa Bongofleva, Naseeb Abdul a.k.a Diamond, atakuwa na fursa ya kuthibitisha makali yake dhidi ya nyota wa kizazi kipya wa Kenya, Jackson Makini a.k.a CMB Prezzo wakati wawili hao watakapopanda katika jukwaa moja kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Julai 7 mwaka huu.
Mratibu wa tamasha hilo Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’, alisema mpambano huo unatarajiwa kutegua kitendawili cha nani mkali kati ya wasanii hao kwenye ukanda wa Afrika Mashariki.
Alisema Diamond ambaye ana tuzo ya Msanii Bora wa Kiume ya Kilimanjaro, ataonyeshana ubavu na mkali Prezzo ambaye ana mashabiki wengi nchini Kenya, hivyo mpambano unatarajiwa kuwa mkali.
Abby alisema Prezzo ambaye ni mshiriki wa Big Brother msimu uliopita, alimwambia kuwa anatarajia kuona umati mkubwa wa mashabiki wake ukimuunga mkono siku hiyo kwa kuwa ndiyo mara yake ya kwanza kufanya shoo katika uwanja huo unaobeba zaidi ya mashabiki 60,000.
Aliongeza pia kwamba kutakuwa na mpambano utakaohusisha Kenya na Tanzania kwa upande wa ngumi ambapo mabondia kutoka nchi hizo mbili watazichapa.
Mabondia Patrick Amonte atatunishiana msuli na Thomas Mashali wakati Shadrack Machanje yeye atazichapa na Francis Miyeyusho.
Ukiachana na ngumi, pia bendi za Msondo Ngoma, Jahazi Modern Taarab na Sikinde zitakuwapo siku hiyo.
TMK Halisi na Wanaume Family watawafundisha mashabiki wao staili mpya za uchezaji, alisema.
“Hii itakuwa vita kali sana kwa kuwa ukiangalia stejini Diamond atapambana na mkali kutoka Kenya, huku kwenye ngumi nako kupo hivyohivyo ambako ni Wakenya vs Watanzania, hivyo patakuwa hapatoshi Julai 7.
“Sehemu ya mapato kama kawaida tutapeleka kwenye mfuko wa elimu kusaidia ujenzi wa mabweni ya wanafunzi.”
Messi, baba yake matatani wakihutumiwa kukwepa kodi
![]() |
Messi na baba yake |
MADRID, Hispania
MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Muargentina Lionel Messi na baba yake Jorge wanatuhumiwa na Mamlaka ya Kodi ya Hispania kukwepa kodi na kuikosesha serikali ya nchi hiyo mapato ya zaidi ya euro milioni nne (Sh. Bilioni 8.5).
Mwanasoka huyo bora wa mwaka wa Dunia na baba yake wanadaiwa kuficha sehemu ya mapato yao halisi ya miaka ya 2006, 2007, 2008 na 2009, kwa mujibu wa msemaji wa ofisi ya mwendesha mashtaka mjini Catalonia. Msemaji wa Barca hakuwa tayari kuzungumzia tuhuma hizo
Messi, ambaye atafikisha miaka 26 mwezi huu, ni miongoni mwa wanamichezo wanaolipwa mishahara mikubwa zaidi duniani, akiwa na mshahara wa zaidi ya dola za Marekani milioni 20 kwa mwaka (Sh. bilioni 32), kwa mujibu wa jarida la Forbes.
Mbali na mshahara mnono anaolipwa na Barca, Messi pia huingiza takriban dola za Marekani milioni 21 kwa mwaka (Sh. bilioni 33) kutokana na udhamini wa makampuni kadhaa yakiwamo ya Adidas, PepsiCo na P&G; na anakamata nafasi ya 10 katika orodha ya Forbes ya wanamichezo wanaoongoza kwa kuingiza fedha nyingi duniani.
Wednesday, June 12, 2013
Jaji Mark Bomani aipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba
![]() |
Jaji Mark Boman akizungumza mchana wa leo jijini Dar es Salaam |
Na Suleima Msuya.
WAKATI Taifa likiwa katika
mjadala juu ya rasimu ya katiba ijayo Mwanasheria Mkuu Mstaafu wa Serikali,
Jaji Mark Boman ameipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya Jaji Mstaafu
Joseph Warioba kwa kuja na rasimu nzuri na kuitaka kutoharakisha uwepo wa
katiba husika ili iweze kukidhi mahitaji ya wananchi.
Jaji Boman amesema
hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya
habari maelezo Jijini hapa.
Alisema mchakato
mzima wa kuandaa rasimu unahitaji umakini, uadilifu na kuhakikisha kuwa hakuna
misukumo yoyote ya kufanikisha suala hilo hivyo ni vyema wakahakikisha kuwa
mambo ya msingi yanayohusu jamii yanahusika.
Mwanasheria Mkuu
huyo Mstaafu alisema jambo ambalo linaonekana kugusa jamii kwa asilimia kubwa
ni kuhusu muungano, hivyo ni vyema tume ikafanya tathmini sahihi juu ya
utekelezaji wake ili kuhakikisha kuwa inakidhi kiu ya Watanzania.
Alisema kutokana na
rasimu hiyo ilivyochambuliwa na tume imejikita hasa kuhusu jinsi ya kuwa na
muungano wa nchi lakini ikajisahau kuwa ilikuwa ni fursa muhimu kwa wananchi
kuhusika moja kwa moja juu ya aina ya muungano wanaotaka na isiwe na maoni ya
wajumbe wa tume.
"Mimi kama
Mtanzania na pia mwanasheria mkongwe ambaye najua masuala ya nchi hii kwa upana
naamini tume imejitahidi kwa kiwango chake ila naona haipo sababu ya kukimbilia
kuwepo kwa katiba bila kuhakikisha kuwa mahitaji ya msingi hajatekelezwa hasa
ambayo yanagusa jamii," alisema.
Jaji Boman alisema
suala la muungano linahitaji mchango wa wadau hasa wananchi kwani ni jambo
ambalo linaweza kuweka muafaka wa hatma ya nchi kwa miaka ijayo.
Alisema ni vema
Tume ikatambua kuwa suala la muungano halihitaji maoni ya watu wachache kwani
ni wazi kuwa suala hilo limekuwa likiibua migogoro mingi kwa muda mrefu hasa
katika upande wa Zanzibar.
Alisisitiza kuwa
katika harakati za kutafua ufumbuzi juu ya sauala hilo la muungano ni vema tume
ikachukua maoni ya waliowengi ili kuhakikisha kuwa haja yao inatimia hata kama
wachache wenye uelewa watakuwa wanapinga.
Boman alisema dhana
kuhusu serikali tatu kuwa zitaongeza gharama za undeshaji wa Serikali ni
mtazamo finyu kwani kuna mifano ya nchi nyingi ambazo zimeungana na kuendeshwa
kwa mfumo huo na hakuna athari ya moja kwa moja ambayo imeonekana.
Alisema ni vyema
tume ikajikita kwa wananchi na kuachana na mitazamo ya baadhi ya viongozi wa
kisiasa ambao wengine wanaonekana kuwa yapo mambo ambayo wanataka yawepo kwa
maslahi yao na sio ya Taifa
Kwa upande mwingine
Jaji Boman ameiomba tume kuhakikisha kuwa rasimu hiyo ya katiba ya nchi inakuwa
na muongozo juu ya dira ya nchi, maslahi ya kijamii kwa jamii na mahitaji
muhimu yatajwe ili iwe ni muongozo sahihi kwa kiongozi yoyote ambaye atapata
kuongoza nchi.
Pia alisema ni
vyema rasimu hiyo ya katiba ianishe uwepo na uatambuzi wa rasilimali za nchi
ambazo kwa kiasi fulani zimeonekana kutumiwa kinyume na taratibu hivyo
kutowafaidisha wananchi kwa ujumla.
Alitolea mfano
suala la mikataba mibovu ambayo imekuwa ikiingiwa na Serikali iwapo kutakuwepo
na muungozo wa kikatiba juu ya suala la mikataba inaweza kuwa njia sahihi ya
kuwabana wahusika.
Alisema iwapo mambo
hayo ya msingi yakikosekana ni dhahiri kuwa kila kiongozi anaweza kufanya
anachotaka kutokana na mahitaji yake jambo ambalo ni kinyume na utawala
unavyotaka hasa katika ngazi ya nchi.
TNMC kuvishughulikia vyuo 'feki' vya uuguzi
Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Lena Mfalila akizungumza leo jijini Dar (picha:Audiface Jackson Blog) |
Aidha imeelezwa kuwa vyuo zaidi ya 200 nchini kote havina sifa ya kutoa mafunzo ya taaluma hiyo kwa kutokusajiliwa na TNMC.
Msajili
wa vyuo vya uuguzi na ukunga nchini Lena Mfalila alisema hadi sasa Baraza
linatambua uwepo wa vyuo 34 vinavyotoa mafunzo ya uuguzi nchini.
Mfalila alisema
ili mafunzo ya chuo yaweze kutambulika ni lazima kiwe kimesajiliwa, kiwe na
walimu wenye sifa pamoja kutumia mitaala inayotambuliwa na Baraza.
Aliwataka
wazazi na wanafunzi wote wanaohitaji kupata elimu katika vyuo mbalimbali hapa
nchini kuvichunguza kwanza kabla ya kujiunga navyo kwani wasipofanya hivyo
watakuwa wanapoteza muda wao.
“Lazima
wanaotaka kujiunga na chuo wanachotaka kusoma wahakikishe kama kimesajiliwa na baraza
chini ya sheria ya ‘Nursing and Midwifery’ ya mwaka 2010 na kuangalia mitaala yao
ya kufundishia,” alisema Mfalila.
Kwa
upande wa vyuo vinavyofundisha uuguzi, alisema Baraza limekumbana na changamoto
nyingi ikiwa ya kuibuka kwa vyuo ambavyo havitambuliki kisheria lakini
vinaendesha mafunzo kinyemela.
Aidha
alisema kutoka na malalamiko ya jamii
kuhudumiwa huduma duni ya uuguzi na ukunga zinazotolewa na watumishi wa afya ambao
wameajiriwa kutoka vyuo visivyotambulika,baraza
limetoa agizo kwa watumishi wa afya kutoa taarifa.
Ivory Coast kutua nchini kesho na nyota wote, ispokuwa Drogba
![]() |
Kikosi cha Ivory Coast, japo Didier Drogba hatakuja hiyo kesho |
Na Boniface Wambura
MSAFARA wa timu ya Taifa ya Ivory Coast (The Elephants) wa watu 80 wakiwemo wachezaji 27 unatarajiwa kuwasili nchini kesho (Juni 13 mwaka huu) kwa ndege maalum kwa ajili ya mechi dhidi ya Taifa Stars.
Mechi hiyo itachezwa Jumapili (Juni 16 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 9 kamili alasiri, na itachezeshwa na Charef Mehdi Abdi kutoka Algeria.
Kikosi hicho kitawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 2.50 usiku na kitafikia hoteli ya Bahari Beach iliyoko nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Timu hiyo inatarajia kuondoka saa chache baada ya mechi hiyo.
Wachezaji walioko katika kikosi hicho ni Abdoul Razak, Akpa Akpro Jean-Daniel Dave Lewis, Angoua Brou Benjamin, Arouna Kone, Aurier Serge Alain Stephane, Bamba Souleman, Barry Boubacar, Boka Etienne Arthur, Bolly Mathis Gazoa Kippersund, Bony Wilfried Guemiand, Cisse Abdoul Karim, Diarrassou Ousmane Viera na Dja Djedje Brice Florentin.
Doumbia Seydou, Gbohouo Guelassiognon Sylvain, Gosso Gosso Jean-Jacques, Kalou Salomon Armand Magloire, N’dri Koffi Christian Romaric, Sangare Badra, Serey Die Gnonzaroua Geoffroy, Sio Giovanni, Tiote Cheik Ismael, Toure Yaya Gnegneri, Traore Lacina, Ya Konan Didier, Yao Kouassi Gervais na Zokora Deguy Alain Didier.
Taifa Stars iko kambini hoteli ya Tansoma tangu iliporejea kutoka Marrakesh, Morocco ambapo leo na kesho itafanya mazoezi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 9 kamili alasiri. Ijumaa itapumzika, na itafanya mazoezi ya mwisho Jumamosi kwenye uwanja huo huo kuanzia saa 10 kamili.
Makocha wa timu zote mbili (Taifa Stars na The Elephants) watakutana na waandishi wa habari Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF kuzungumzia jinsi walivyojiandaa kwa mechi hiyo.
Kuziona Stars, Tembo wa Ivory Coast buku 5
![]() |
Stars na Ivory Coast zilipochuana siku za nyuma |
Na Boniface Wambura
KIINGILIO cha chini katika mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Ivory Coast (The Elephants) itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani.
Viti vya kijani katika uwanja huo wenye uwezo wa kumeza watazamaji 60,000 viko 19,648. Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu ambavyo viko 17,045 ni sh. 7,000. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 ni sh. 10,000.
Viingilio vya daraja la juu ni kama ifuatavyo; VIP C yenye watazamaji 4,060 ni sh. 15,000 wakati sh. 20,000 ni kwa VIP B yenye watazamaji 4,160. VIP A yenye watazamaji 748 kiingilio chake ni sh. 30,000.
Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo itakayoanza saa 9 kamili alasiri zitaanza kuuzwa siku mbili kabla ya mchezo (Ijumaa na Jumamosi) katika vituo vifuatavyo; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.
Katika vituo hivyo tiketi zitauzwa katika magari maalumu. Magari hayo pia yatafanya mauzo ya tiketi uwanjani siku ya mechi. Tunapenda kuwakumbusha watazamaji kutonunua tiketi mikononi mwa watu au katika maeneo yasiyohusika ili kuepuka kununua tiketi bandia, hivyo kukosa fursa ya kushuhudia mechi hiyo.
Utaratibu katika mechi hiyo utakuwa kama ilivyokuwa katika mchezo wa Simba na Yanga, ambapo hayataruhusiwa kuingia uwanjani isipokuwa kwa yale yatakayokuwa na sticker maalumu kutoka TFF.
Kitale, Montanabe wambeba Yosso
![]() |
Yosso katika pozi |
![]() |
Kitale katika pozi zake za 'kiteja' |
MCHEKESHAJI ambaye kwa sasa ni mpiga picha wa filamu , Mussa Rashid 'Yosso' amejitosa kwenye muziki akijiandaa kuibuka na wimbo uitwao 'Mwanangu' alioimba akishirikiana na Mussa Yusuf 'Kitale' namuimbaji wa Extra Bongo, Michael Athanas 'Montanabe'.
Akizungumza na MICHARAZO, Yosso, aliyewahi kutamba na igizo la 'Sekeseke' lililorushwa na kituo cha ITV wakati akiwa na kundi la Kambarage, alisema wimbo huo umekamilika na kwa sasa anafanya mipango ya kuachia hewani ili mashabiki wake wapate uhondo.
Yosso, alisema wimbo huo upo katika miondoko mchanganyiko na ndani mwake Kitale na Montanabe wamefanya mambo makubwa katika kuunogesha ikizingatiwa hivyo ndiyo kazi yake ya kwanza na hivyo hakupenda kuanza vibaya ndiyo maana ameshirikisha wakali hao.
"Katika kukiendeleza kipaji changu cha muziki nilichokuwa nacho tangu mdogo kabla ya kujitosa kwenye uiogizaji, nimekamilisha wimbo wangu uitwao 'Mwanangu' ambao nimeimba pamoja na Montanabe wa Extra Bongo na Kitale, ni bonge la 'ngoma'," alisema.
Alisema wakati wimbo huo ukiandaliwa kuachiwa hewani, pia tayari ameshaanza kutayarisha nyimbo nyingine ili mara baada ya kufyatua video yake iwe rahisi kwake kurejea studio kuwapakulia mashabiki wake burudani zaidi.
Yosso, anayeandaa kipindi cha Vituko Show kama mpiga, alisema anaamini wimbo huo mpya utaonyesha ni jinsi gani alivyojipanga katika ulingo huo wa muziki baada ya kutamba kwenye uigizaji akipitia makundi ya Mtandao Arts, Dar Talent na Kambarage.
Miaka 13 ya Kikosi sasa kuanzishwa Juni 21
![]() |
Kalapina kiongozi wa Kikosi cha Mizinga |
BAADA ya msiba wa Albert Magweha 'Ngwair' kusababisha kuahirishwa kwa onyesho maalum la maadhimisho ya miaka 13 ya kundi la Kikosi cha Mizinga, sasa onyesho hilo litafanyika Juni 21, huku idadi ya burudani ikiongezeka ikiwamo kuongezwa kwa Fid Q, Stereo na Hamidu.
Kiongozi wa Kikosi, Karama Masoud 'Kalapina' alisema baada ya kumpumzisha msanii mwenzao, sasa onyesho lao la miaka 13 ya Kikosi itafanyika Juni 21 kwenye ukumbi ule ule wa Msasani Club, kwa kila shabiki kujilipia Sh 5,000 ili kuhudhuria na kuburudishwa kwa tani yao na burudani zilizopangwa.
Kalapina alisema kati ya burudani zitakazosindikiza maadhimisho hayo mbali na wasanii mbalimbali kama Afande Sele, Nikki Mbishi, mshindi wa tuzo tatu za Kili Music 2013, Kala Jeremiah, Nash Mc wa LWP na Manzese Crew, pia mkalio Fid Q, Stereo na Dodo Hamidu 'Nyandu Tozi' watakuwepo.
"Pia tumepanga kufanya maonyesho ya uchoraji, kuimba Free Style, maonyesho ya mavazi na kutoa tuzo kwa wadau wote waliosaidia Kikosi cha Mizinga kufika hapa ilipo wakiwamo wanahabari, wadhamin, mashabiki an wengineo waliokuwa bega kwa bega na Kikosi tangu lianzishwe," alisema Kalapina.
Kalapina alisema ameona ni vyema kupeleka onyesho lake Juni 21 ili kutogongana na maonyesho ya wasanii wengine ambao yatafanyika wiki hii ambayo nayo yaliahirishwa kabla ya kifo cha Ngwair yakiwa yamepangwa kufanyika siku moja ya Mei 31 katika kumbi tatu tofauti.
Maonyesho hayo ni ya miaka 13 ya Lady Jaydee na lile la MwanaFA ambayo kama ilivyokuwa awali yote yafanyika siku moja Juni 14 yaani Ijumaa kwenye kumbi tofauti jijini Dar es Salaam.
Mwamuzi jela miezi 6 kwa kupanga matokeo ili apewe uroda
![]() |
Ali Sabbagh |
REFA wa kimataifa na maarufu nchini Lebanon, Ali Sabbagh amehukumiwa kwenda jela baada ya kukutwa na hatia ya kupanga matokeo ya michezo uwanjani kwa malipo na ngono.
Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari za nchini Singapore, mwamuzi huyo ambaye amekuwa akicheza mechi mbalimbali za kimataifa zikiwamo za kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia amekutwa na hatia hiyo yeye na wasaidizi wake wawili na mahakama moja nchini Singapore.
Sabbagh, 34 inadaiwa amekuwa akipanga matokeo kwa minajili ya kulipwa ujira wa ngono na wanawake aliokubaliana nao, jambo lililomshangaza jaji aliyekuwa akiisikiliza kesi hiyo na kutoa hukumu hiyo Jumatatu wiki hii akihojikama kesi hiyo tu katutwa na hatua je ni michezo mingapi amekuwa akilipwa ujira huyo wa kubadilisha mechi kwa ngono?
Wasaidizi wake waliohukumiwa miezi mitatu kila moja kwa makosa hayo ni Ali Eid, 33, na Abdallah Taleb, 37.
Inaelezwa waamuzi hao walikutwa na hatia ya kupanga matokeo katika pambano la Kombe la Shirikisho kwa nchi za Asia lililofanyika Aprili 3, kati ya klabu ya Singapore Tampines dhidi ya East Bengal ya India, iliyoshinda mabao 4-2 dhidi ya wenyeji wao.
Waamuzi hao wanadaiwa walifanya mipango hiyo wakishirikiana na mfanyabiashara anayesifika kwa dili za upangaji matokeo nchini Singapore, Ding Di Yang kwa kukubaliana na wanawake kupanga matokeo ya pambano kwa kulipwa mapenzi.
Wakili wa mwamuzi huyo, Gary Low, alisema haoni sababu ya mteja wake kuadhibiwa iwapo hakunufaika kifedha na mchongo huo anaoshutumiwa kuufanya ambao ni tuki jipya katika rushwa michezoni.
Simba yambakisha Kiemba, wamsubiri Ssenkoomi apone wampime
![]() |
Amri Kiemba |
BAADA ya tetesi za muda mrefu kwamba kiungo mahiri nchini wa Simba, Amri Kiemba ametua kwa mahasimu wa Msimbazi, Yanga kwa kitita cha Sh. Mil 38, hatimaye ukweli umebainikwa kuwa uvushi huo haukuwa wa kweli baada ya uongozi wa Simba kumsainisha kiungo huyo kwa kitita cha Sh. Mil. 35.
Simba wamembakisha kiungo huyo kwa mkataba wa miaka miwili na kwamba umeondoa hofu ya mchezaji huyo kuhamia kwa Yanga akiwa amerejesha kiwango chake na kuonyesha soka la aina yake kiasi cha kurejea timu ya taifa, Taifa Stars.
Kwa mujibu wa wakala wa Kiemba, Ulimwengu Hamim, kiungo huyo alisaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kuichezea Simba jana mchana.
Habari za Kiemba ambaye pia anakipiga timu ya taifa ‘Taifa Stars’ kurejea Yanga alikowahi kuitumikia miaka ya nyuma, ziliibua mjadala na kuwaweka katika wakati mgumu mashabiki wa Simba, ambao bado wana kumbukumbu nyota mwingine, Mrisho Ngasa, ambaye alikipiga Msimbazi nusu msimu na hatimaye kurejea Jangwani.
Awali, Kiemba alidai kuwa soka ndiyo ajira yake hivyo kupitia kwa wakala wake, angeangalia pa kwenda patakapomridhisha.
Kiemba hivi sasa yuko kwenye midomo ya wapenzi na mashabiki wa soka, hasa baada ya mwishoni mwa wiki kuonyesha kiwango cha juu katika mechi ya kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia, kati ya Stars na Morocco, ambako bao lake liliacha gumzo. Katika mechi hiyo, Stars ililala 2-1 ugenini.
Katika hatua nyingine, kocha mkuu wa Simba, Abdallah Kibadeni, amesema licha ya kuumia kwa beki wao wa kimataifa, Samuel Senkoomi, raia wa Uganda, wanamsubiri aweze kupona ili aendelee kumchunguza ili kuona kama anawafaa katika kikosi chao.
Senkoomi beki aliyetua Msimbazi akitokea URA, aliumia kifundo cha mguu katika mazoezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Kinesi jijini Dar es Saalam.
Kibadeni, akizungumza mara baada ya kumaliza mazoezi kwenye uwanja huo, alisema, wanatarajia kumtumia mchezaji huyo, ila mpaka kiwango chake kimvutie ili aweze kusajiliwa.
“Nimemtazama, ila bado sijamtazama vizuri, kwa kuwa siku mbili tu za mazoezi akaumia, nasubiri aweze kupona halafu nimwangalie kama atatufaa,” alisema Kibadeni.
Aidha alisema anatarajia kupata kikosi cha kwanza wiki ijayo, baada ya nyota walioko timu ya taifa kuungana na wenzao.
“Ningeishapata kikosi, ila nawangoja vijana waliokuwa timu ya taifa, nina imani wakija nitapata kikosi cha kwanza,” alisema.
Kibadeni, nyota wa zamani wa Simba, Majimaji na Taifa Stars, amerejea Msimbazi kuchukua mikoba ya Mfaransa, Patric Liewig, ambaye katupiwa virago kutokana na matokeo mabovu, akitokea Kagera Sugar.
Kijana mbaroni kwa kumchinja mfanyakazi mwenzake
Mwili wa Perpetua ulipotolewa katika shimo la taka na Polisi (Picha:Hisia za Mwananchi) |
![]() |
Kamanda Kova |
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari jana.
Alisema Philemon Laiza (27), mkazi wa Mikocheni B, anatuhumiwa kuhusika na mauaji ya Perptua Maina (30) kwa kumchinja na kisha kutelekeza mwili wake kwenye dampo la takataka.
Kova alisema mtuhumiwa anashikiliwa na Polisi na upelelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani.
Katika tukio la pili, alisema watu wawili; Isaya Mafuru (31) na Yusufu Machela (33), wanatuhumiwa kwa uporaji wa mali za raia wa Sweden, Gisela Bergstorm katika maeneo ya Coco Beach.
Katika tukio la lingine, alisema watu wanne, ambao ni Thenase Benjijimana (26), raia wa Burundi, Said Hassan (37), mkazi wa Mbande, Obadia Bukuku (25) na Benedict Mohamed (32) wakazi wa Tabata, wanatuhumiwa kwa kukutwa na gari ya wizi aina ya Noah T 157 BWC, pamoja na pikipiki aina ya Boxer T 568 CDL.
Wote kwa pamoja wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya upelelezi zaidi.
Hivi ndivyo alivyopumzishwa marehemu Kashi
Pichani juu ni mazishi ya msanii
ya mwigizaji Jaji Khamis 'Kashi' aliyefariki juzi mchana katika
Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar yaliyofanyika jana mchana majira
ya saa nane kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Marehemu
Kashi alikumbwa na umauti baada ya kuugua ghafla malaria na kifua.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Kashi mahali pema peponi. AMEN!
Tuesday, June 11, 2013
MABONDIA WA JIJI DAR, MORO KUPAMBANA JUMAPILI
KING CLASS MAWE |
Patrick Kavako'Baunsa' |
Bondia Patrick Anthony Kavako 'Baunsa' wa Morogoro ametamba kumsambalatisha Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mpambano wao wa raundi nane utakaofanyika siku ya jumapili june 16 katika ukumbi wa panandi panandi uliopo Ilala Bungoni Dar es salaam
Mpambano
huo ulioratibiwa na Kinyogoli Fondition kwa kushlikiana na PST itakuwa
chachu kwa vijana kuendelea kuupenda na kuucheza mchezo huo unaopendwa
na wengi nchini
mbali
ya mpambano uho kutakuwa na mapambano mengine ya kukata na shoka bondia
Abuu Mtambwe ataoneshana umwamba na Kassim Gamboo na Bondia mkongwe
kabisa Yohana Robart atamenyana na Mussa Sunga
Kocha huyo wa kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini,Rajabu
Mhamila ‘Super
D’ ametoa DVD mpya 3 kwa ajili ya mafunzo ya mchezo wa ngumi ndani yake
kukiwa na clips za mabondia wanaofanya vizuri Tanzania kama Thomas
Mashali vs Fransic Cheka na mambondia wengine mbalimbali
CD hizo zilizotengenezwa kwa umakini wa
ali ya juu ambazo zitakuwa chachu kwa ajili ya kuvutia wapenzi na
mashabiki mbalimbali kujua mchezo wa masumbi wakiwa wanangalia live mana
DVD hizo zina maelekezo ya sheria mbalimbali ambazo zinatumika katika
masumbwi
DVD hizo kwa sasa zinapatikana katika
makutano ya barabara ya Uhuru na Msimbazi au unaweza kuzipata jengo la
Azam lililopo mtaa wa Msimbazi karibu na kituo cha Polisi Post Gelezani
kwingine ni GYM ya Amana iliyopo Ilala au unaweza kuwasiliana na kocha
kwa simu 0713406938 ili uweze kupata DVD hizo kwa ajili ya kujifunza
zaidi mchezo huo
Mbali ya kupatikana katika maeneo hayo pia
katika mchezo mbalimbali ya masumbwi kutakuwa na CD na DVD za mafunzo wa mchezo
huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.
Aliongeza kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo katika CD na DVD
hizo ni ya Kalama Nyilawila
,Japhert Kaseba,Rashidi Matumla, Hassani Matumla,Thomas Mashali Dhidi ya
Francis Cheka, Mbwana Matumla na
Francis Miyeyusho,Japhert Kaseba na Maneno Oswald, Said Mundi na King Class Mawe.
mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether,
Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya
juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super
D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa
ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.
“Ninatarajia kuwepo kwa ajili ya kuwauzia DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika Mpambano ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi”, alisema Super D .
APPT Maendeleo yaifagilia Rasimu ya Katiba
![]() |
Rais wa APPT Maendeleo, Peter Kuga Mziray |
Kauli hiyo imetolewa na Rais Mtendaji wa APPT
Maendeleo Peter Kuga Mziray wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii leo
jijini Dar es Salaam.
Mziray alisema tangu rasimu hiyo izinduliwe rasmi
3/6/2013 kumekuwepo na mitazamo mbalimbali ya kuipongeza na kuipinga kwa baadhi
ya watu ambao kimantiki wanaipinga ni
watu wenye malengo yao ya kuwa Marais wa
Tanzania jambo ambalo linaelekea kufa.
Alisema Watanzania hasa wale wa Bara wamekuwa na
kilio cha miaka mingi cha kuhitaji uwepo wa Tanganyika kama ilivyo Zanzibar
lakini hawakusika jambo ambalo kwa sasa limepatiwa muafaka na Tume ya
Mabadiliko ya Katiba.
Rais Mtendaji alisema mapendekezo ya Tume ni mazuri
kwa asilimia kubwa kwani yamezingatia maoni ya watu wengi ambao walikuwa
wakihitaji rasimu ya katiba iwe hivyo bila kuogopa vivuli vya baadhi ya watu
ambao wamejionyesha dhahiri kutokubaliana nayo.
“Kimsingi naunga mkono mapendekezo ya Tume kwani
yamezingatia mahitaji ya Watanzania wote wa Bara na Visiwani na pia yana nia ya
kuhakikisha kuwa Tanzania inaendelea kudumu bila mitafaruku,” alisema.
Alisema wapo watu wameibuka na kusema Serikali tatu
zitakuwa ni kuongeza gharama kubwa kuziendesha jambo ambalo sio kweli kutokana
na ukweli kuwa kila nchi itakuwa ikitumia rasilimali zilizopo katika upande
wake na kuchangia Serikali ya Muungano ambayo haitakuwa kubwa.
Mziray alisema mapendekezo ya Tume yameaanisha mambo
muhimu katika muungano ambayo yapo saba jambo ambalo ni ishara tosha kuwa
hakukuwa na serikali kubwa kama inavyofikiriwa.
Mambo ayalitajwa kuhusika na muungano ni pamoja na
katiba na mamlaka ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, ulinzi na usalama wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania, uraia na uahamiaji, sarafu na benki kuu, mambo
ya nje, usajili wa vyama vya siasa na ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo na kodi
yatokanayo na mambo ya muungano.
Aidha alisema rasimu hiyo imeenda mbali pale
ilipoweka wazi kuwa ili mgombea wa Urais atangazwe anapaswa kushinda kura
ambazo zitampatia 50 ya kura zote, pamoja na wagombea wa Urais kupata haki ya
kuenda mahakamani kupinga matokeo.
Rais Mtendaji huyo pia alisema kupunguzwa kwa
madaraka na kuwajibishwa kwa wabunge ambao hawafanyi kazi katika majimbo yao ni
jambo muhimu ambalo Tume inapaswa kupongezwa kutokana na umuhimu wake hasa
ukizingatia kuwa baadhi ya wawakilishi wa wananchi wamekuwa wakiishi mijini
zaidi.
Maziray alisema pamoja na mapendekezo hayo ya tume
ni vema mabaraza ya katiba yakapendekeza adhabu ambazo zinaweza kutolewa kwa
utoro unaofanywa na wabunge jambo ambalo linaweza kurejesha hadhi ya Bunge
ambalo kila siku linaonekana lipo wazi.
Kwa upande mwingine Mziray ameiomba Serikali kuanza
mchakato wa uwepo wa Katiba ya Tanganyika ili iweze kuendana na mchakato wa
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jambo ambalo litarahisisha uwepo kwa
serikali hiyo.
Alisema bila kuwepo kwa Katiba ya Tanganyika itakuwa
ngumu kutekeleza mapendekezo ya Tume ambayo yanahitaji kuwepo kwa Serikali tatu
ambazo ni Tanganyika, Zanzibar na Tanzania.
Rais Mtendaji alisema mchakato huo hautakuwa na kazi
ngumu kwani ukweli unaonyesha kuwa maoni mengi ambayo yapo katika rasimu na
yalioachwa yalikuwa yanahusu serikali ya Tanganyika.
Vita ya Ally Choki, Asha Baraka yafika pabaya
MKURUGENZI wa Extra Bongo Ally Chocky ametoa kauli nzito kuhusu waajiri wake wa zamani, Asha Baraka na Baraka Msilwa.
Katika maongezi yake Chocky alisema katika watu asiowapenda duniani ni Asha Baraka (Mkurugenzi wa ASET) na Baraka Msilwa (Mwenyekiti wa ASET). Asha Baraka na Baraka Msilwa ni mtu na kaka yake.
Kiongozi huyo wa Extra Bongo akaenda mbali zaidi kwa kusema: “Nikifa leo hii Asha Baraka na Baraka Msilwa wasije kwenye mazishi yangu, na kama watanitangulia wao na mimi sitakwenda kwenye mazishi yao.
“Nina uhakika leo hii nikipata matatizo au nikifa Asha na Msilwa watafurahi, sasa kuna haja gani ya watu kama hao kuja kwenye mazishi yangu.
“ASET ni kama simba wako tayari kukutafuna hadi macho, nimetafakari kwa muda mrefu sana nimevumilia mengi sana lakini nimeshindwa na sasa natamka rasmi, Nikifa wasinizike.”
Chocky ameorodhesha sababu nyingi sana za kufikia hatua hiyo lakini miongoni mwa sababu zake ni hizi tatu:
Kwanza kitendo cha Aset kumpeleka mahakamani kumdai gari, pili Aset kukataa kurudisha pesa za Miraji Shakashia na tatu ni ASET kutothamini michango ya wasanii walioizalishia pesa nyingi.
Chocky ansema kitendo cha Aset kumpeleka mahakamani kumdai gari ambalo walimpa mwenyewe kilimkera sana.
“Mtu anapokupeleka mahakamani maana yake ni kwamba yupo tayari hata ufungwe, ukifungwa maana yake ni kila kitu kwenye maisha yako kinaharibika.
“Gari walinipa wenyewe na maandishi yapo kwamba nikimaliza mkataba wangu gari litakuwa la kwangu.
Lakini badala yake wakanigeuzia kibao na kwenda kunidai mahakamani kwamba nimeiba gari.
Kuhusu Shakashia, Chocky amesema mwanamuziki huyo alichukua shilingi milioni tano za Extra Bongo ili ajiunge nayo na akasaini mkataba wake.
“Lakini badala yake Shakashia akaingia mitini na pesa zetu, Aset wakasema watazirudisha wao na sasa wanakuja na hadithi mpya.
“Wanasema hawawezi kurudisha hizo pesa eti kwa vile wananidai, wanasahau kuwa mkataba wa Shakashia ni kati yeke na Extra Bongo na sio Ally Chocky.
“Hata kama kipo wanachonidai hiyo ni kati ya Chocky na Aset na haiingii akilini kuliingiza suala la Shakashia ndani yake.
“Huu ni utapeli na inatoa picha kuwa Aset walimtumia Shakashia kufanya utapeli huu, lakini wajue kuwa mwisho wa siku atakayeathirika ni Shakashia mwenyewe,” alisema Chocky.
Kuhusu kutothamini wasanii waliozalishia pesa nyingi kampuni, Chocky anasema wasanii walipota ASET na kuizalishia pesa hawana chochote walichopewa kulingana na thamani ya kile walichokizalisha. “Sio pesa tu bali hata heshima pia hakuna,” alifafanua Chocky.
Chocky akazama zaidi na kuwataja wakongwe kama Shem Karenga na Kasongo Mpinda ambao waliwahi kufanya kazi katika familia ya kina Asha Baraka kupitia bendi za MK Group na MK Beats.
“Wako wapi Kasongo Mpinda na Shem Karenga, Kasongo aliwatengenezea pesa nyingi kupitia MK Group “Ngoma za Magorofani” huku Shem Karenga akiwatengenezea utajiri katika MK Beats “Tukunyema”.
“Lakini hebu tujiulize wako wapi hawa wazee na wana kipi cha kujivunia?” alihoji Chocky.
Haikuishia hapo, tuliamua kumpigia Asha Baraka ambaye naye alikuwa na yake ya kujibu kuhusu mapigo ya Chocky.
Asha Baraka amesema hayo ni mambo ya kike na kwamba kuzikana si tija.
Asha Baraka akasema: “Hata mimi sina mpango wa kwenda kwenye mazishi yake na yeye pia asije kwenye mazishi yangu.
“Hivi kuzikana ni nini? Wazazi wangu walifariki na Chocky hakuja kuzika, kilipungua nini? Halafu mi nikifa sitaona na yeye akifa sitaona kwahiyo hiyo siyo ishu, wamanyema wenzangu watatosha kunizika hata wasanii wote wasipokuja achilia mbali huyo Chocky.
“Nilimzikia wazazi wake na hakuliona hilo kwahiyo hata tusipozikana hakipungui kitu.
“Chokcy tunamdai gari na pesa shilingi milioni 13, kwenda mahakamani ni sehemu ya kudai haki na yeye kama anaona amedhulumiwa kuhusu pesa za Shakashia basi aende mahakamani.”
Asha Baraka alimtaka Chocky aelewe kuwa baadhi ya wasanii wa Twanga ni virusi na watammalizia pesa zake bure.
“Wako wasanii wamelelewa vizuri, wamefanyiwa mengi na Twanga na wanaelewa utu kwahiyo akijipendekeza kwao atapoteza pesa zake bure.
“Hao ni virusi wetu, wanatuletea taarifa zote za kila mtu anapotaka kuwachukua.
Asha Baraka amesema kama ni roho mbaya Chocky ndio anaoongoza kwa roho mbaya.
“Alikaa yeye na kamati yake yenye wakiwemo mpaka wafanyakazi wa umma na kuzoa wanamuziki wa Twanga”
Anawataja wasanii wa Twanga waliowahi kuchukuliwa na Extra Bongo ni pamoja na Ferguson, Rogart Hegga, Hosea, Otilya, Nyamwela, Danger Boy, Aisha Madinda, Maria Soloma, Subrina pamoja na Kanuti ambaye baadae alirudisha pesa zao na kubakia Twanga.
Asha Baraka anawataja wasanii wengine wenye damu ya Aset ambao wako Extra Bongo ni Ephraim Joshua, Martin Kibosho, Athanas, Banza Stone na yeye mwenyewe Chocky.
“Kwa mfumo huo utaona wazi kuwa Extra Bongo inapumua kwa nguvu ya Aset lakini sisi hatujasema kitu, kama ni kutoa kauli ya kutozikana basi sisi ndio tulipaswa kuwa wa kwanza,” alifafanua Asha.
“Tunajua pia kuwa Chocky alihusika kushawishi usajili wa Chaz Baba Mashujaa Band akiamini kuwa kwa kuondoka Chaz Twanga itakufa,” aliongeza
Asha Baraka amemtaka Chocky aonyeshe mfano wa namna ya kulea wasanii kwa kuwapa maisha mazuri wanamuziki waandamizi kama Banza na Rogart.
“Asiangalie mambo ya Aset, ajitazame yeye anaishi vipi na Banza anaishi vipi, badala ya kutoa milioni tano kumnunua Shakashia, angemnunulia japo Corola Banza au Rogart.
“Chocky aitishe mkutano wa waandishi wa habari halafu mimi na yeye twende na mikataba ya wasanii inayoonyesha mishahara na marupurupu tuone nani analea vizuri wasanii.
“Mimi nilifanya kazi Bima na sijajengewa nyumba wala kununuliwa gari, silalamiki kwa kuwa haikuwa sehemu ya makubaliano yetu.
“Kama Chocky anadhani muziki unalipa kiasi cha kumnunulia kila mtu gari na nyumba basi atuonyeshe mfano kupitia Extra Bongo.
“Kila baya linalomfika basi mchawi ni Aset, mbona mimi naumwa mguu na sijawahi kusema ni Chocky?
“Chocky akapime afya yake apate ukweli, tunajua rekodi ya sehemu alizopita, sasa asije akadondoka akasema ni Aset …akapime kwanza” alimaliza Asha Baraka.
Asha Baraka amesema hayo ni mambo ya kike na kwamba kuzikana si tija.
Asha Baraka akasema: “Hata mimi sina mpango wa kwenda kwenye mazishi yake na yeye pia asije kwenye mazishi yangu.
“Hivi kuzikana ni nini? Wazazi wangu walifariki na Chocky hakuja kuzika, kilipungua nini? Halafu mi nikifa sitaona na yeye akifa sitaona kwahiyo hiyo siyo ishu, wamanyema wenzangu watatosha kunizika hata wasanii wote wasipokuja achilia mbali huyo Chocky.
“Nilimzikia wazazi wake na hakuliona hilo kwahiyo hata tusipozikana hakipungui kitu.
“Chokcy tunamdai gari na pesa shilingi milioni 13, kwenda mahakamani ni sehemu ya kudai haki na yeye kama anaona amedhulumiwa kuhusu pesa za Shakashia basi aende mahakamani.”
Asha Baraka alimtaka Chocky aelewe kuwa baadhi ya wasanii wa Twanga ni virusi na watammalizia pesa zake bure.
“Wako wasanii wamelelewa vizuri, wamefanyiwa mengi na Twanga na wanaelewa utu kwahiyo akijipendekeza kwao atapoteza pesa zake bure.
“Hao ni virusi wetu, wanatuletea taarifa zote za kila mtu anapotaka kuwachukua.

Asha Baraka amesema kama ni roho mbaya Chocky ndio anaoongoza kwa roho mbaya.
“Alikaa yeye na kamati yake yenye wakiwemo mpaka wafanyakazi wa umma na kuzoa wanamuziki wa Twanga”
Anawataja wasanii wa Twanga waliowahi kuchukuliwa na Extra Bongo ni pamoja na Ferguson, Rogart Hegga, Hosea, Otilya, Nyamwela, Danger Boy, Aisha Madinda, Maria Soloma, Subrina pamoja na Kanuti ambaye baadae alirudisha pesa zao na kubakia Twanga.
Asha Baraka anawataja wasanii wengine wenye damu ya Aset ambao wako Extra Bongo ni Ephraim Joshua, Martin Kibosho, Athanas, Banza Stone na yeye mwenyewe Chocky.
“Kwa mfumo huo utaona wazi kuwa Extra Bongo inapumua kwa nguvu ya Aset lakini sisi hatujasema kitu, kama ni kutoa kauli ya kutozikana basi sisi ndio tulipaswa kuwa wa kwanza,” alifafanua Asha.
“Tunajua pia kuwa Chocky alihusika kushawishi usajili wa Chaz Baba Mashujaa Band akiamini kuwa kwa kuondoka Chaz Twanga itakufa,” aliongeza
Asha Baraka amemtaka Chocky aonyeshe mfano wa namna ya kulea wasanii kwa kuwapa maisha mazuri wanamuziki waandamizi kama Banza na Rogart.
“Asiangalie mambo ya Aset, ajitazame yeye anaishi vipi na Banza anaishi vipi, badala ya kutoa milioni tano kumnunua Shakashia, angemnunulia japo Corola Banza au Rogart.
“Chocky aitishe mkutano wa waandishi wa habari halafu mimi na yeye twende na mikataba ya wasanii inayoonyesha mishahara na marupurupu tuone nani analea vizuri wasanii.
“Mimi nilifanya kazi Bima na sijajengewa nyumba wala kununuliwa gari, silalamiki kwa kuwa haikuwa sehemu ya makubaliano yetu.
“Kama Chocky anadhani muziki unalipa kiasi cha kumnunulia kila mtu gari na nyumba basi atuonyeshe mfano kupitia Extra Bongo.
“Kila baya linalomfika basi mchawi ni Aset, mbona mimi naumwa mguu na sijawahi kusema ni Chocky?
“Chocky akapime afya yake apate ukweli, tunajua rekodi ya sehemu alizopita, sasa asije akadondoka akasema ni Aset …akapime kwanza” alimaliza Asha Baraka.
MPEKUZI HURU
Bosi Masinde 'kulifufua' kundi la Shirikisho Msanii Afrika
Bosi Masinde katika pozi |
Masinde, alisema wazo la kulirejesha upya kundi hilo katika 'uhai' baada ya kuzimika miaka kadhaa iliyopita inatokana na ushawishi anaopata kwa baadhi ya wasanii wenzake wa zamani pamoja na mashabiki ambao walikunwa na maigizo ya kundi hilo wakati likiwa kileleni.
Akizungumza na MICHARAZO, Masinde alisema Shirikisho Msanii Afrika halijafa kimoja, ila liligawanyika pande mbili mara baada ya yeye kujiweka kando na kulifanya kundi hilo lizimike tofauti na iliovyotamba enzi zake likitesa kituo cha ITV.
"Nimekuwa nikiombwa na baadhi ya wasanii nami nafikiria kama nirejeshe majeshi na kulifufua upya kundi hilo ambalo lifukuzana sambamba na Kaole Sanaa kama fitina hazijaingia na kuilisambaratisha," alisema Masinde.
Mshindi huyo wa tuzo ya Muigizaji Bora wa Mwaka wa ZIFF-2012, alisema anajihisi ana wajibu wa kuwarejeshea mashabiki wao burudani kama walivyoipata kupitia michezo kadhaa ilizotamba enzi zao kiasi cha kundi hilo kuwa 'gumzo' la jiji mbali na kuibua nyota kibao.
Enzi za kundi hilo lilitamba na michezo kama 'Tamu Chungu', 'Gumbizi', 'Hatia', 'Dumaza' na mingine huku likiwaibua mastaa wa sasa wa filamu nchini kama akina Amanda, Mama Kawele, Bakar Makuka, Aunty Ezekiel, Nyatawe na wengineo.
Machava yapeta RCL, kipute cha raundi ya 3 wikiendi hii
Na Boniface Wambura
MICHEZO ya kwanza za hatua ya tatu ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kuwania nafasi tatu za kupanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao zitachezwa Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) wakati za marudiano zitachezwa Jumatano ya Juni 19 mwaka huu.
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana leo (Juni 11 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za michezo iliyopita na kufanya uamuzi mbalimbali ikiwemo mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars na Machava FC ambayo haikuchezwa.
Machava FC ambayo ilishinda mechi ya kwanza iliyochezwa mjini Moshi kwa mabao 2-0 inaendelea katika hatua ya tatu kwa vile haikuhusika katika kukwamisha mchezo wa marudiano uliopangwa kuchezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma (DOREFA) kiliuhamishia mchezo huo kwenye Uwanja wa Mgambo mjini Mpwapwa kinyume na maelekezo ya Kamati ya Mashindano ya TFF. Kamati katika kikao chake cha awali iliekeleza kuwa mechi zote za RCL zitachezwa makao makuu ya mikoa isipokuwa kwa Morogoro ambapo timu ya Techfort FC iliruhusiwa kutumia Uwanja wa CCM Mkamba mjini Ifakara.
Hivyo timu nane zilizofuzu kucheza raundi hiyo ni Friends Rangers ya Dar es Salaam, Kariakoo ya Lindi, Katavi Warriors ya Katavi, Kimondo SC ya Mbeya, Machava ya Kilimanjaro, Njombe Mji ya Njombe, Polisi Jamii ya Mara na Stand United FC ya Shinyanga.
Wakati timu nyingine zimefuzu kwa kushinda mechi zao za raundi ya mbili, Njombe Mji imeingia hatua hiyo kwa kuwa timu yenye uwiano mdogo wa kufungwa (best looser) katika hatua ya pili.
Katika hatua hiyo mechi ni ifuatavyo; Kariakoo vs Friends Rangers, Machava FC vs Stand United FC, Polisi Jamii vs Katavi Warriors, na Kimondo SC vs Njombe Mji. Timu zilizoanza kutajwa ndizo zinazoanzia nyumbani.
Vilevile Kamati ya Mashindano imeagiza Kamishna wa mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars vs Machava FC, Mwijage Rugakingira wa Tanga ambaye alikwenda Uwanja wa Mgambo badala ya Uwanja wa Jamhuri kinyume na maelekezo ya TFF aondolewe kwenye orodha ya makamishna.
Pia waamuzi wa mechi hiyo ambao nao walikwenda Mpwapwa badala ya Dodoma Mjini wamepelekwa Kamati ya Waamuzi ya TFF kwa ajili ya kuchukuliwa hatua kutokana na tukio hilo.
Kamati ya Mashindano imekumbusha kuwa RCL ni mashindano yanayosimamiwa na TFF, hivyo maelekezo yoyote kuhusiana na mashindano hayo pia yatatoka TFF na si mahali pengine popote. Hivyo, msimamizi wa kituoa hana mamlaka ya kubadili uwanja.
Hatua ya nne ya RCL itachezwa kati ya Juni 23 na 23 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 29 na 30 mwaka huu.
Waaljeria kuzihukumu Stars, Ivory Coast
Kocha Kim Poulsen akiwoanyesha kwa vitendo wachezaji wa Stars |
Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limeteua waamuzi kutoka Algeria kuchezesha mechi kati ya Taifa Stars na Ivory Coast itakayofanyika Jumapili saa 9 alasiri kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Waamuzi hao watakaochezesha mechi hiyo ya kundi C kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil wataongozwa na Charef Mehdi Abid atakayepuliza filimbi. Atasaidiwa na Hamza Hammou na Bouabdallah Omari wakati mezani atakuwa Sofiane Bousseter.
Abdi na wezake wanatarajiwa kutua nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 12 asubuhi kwa ndege ya EgyptAir. Mtathmini wa waamuzi ni Athanase Nkubito kutoka Rwanda ambaye atatua nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 12 jioni kwa ndege ya RwandAir.
Kamishna wa mechi hiyo ni Bernard Mfubusa kutoka nchini Burundi ambapo atawasili nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 3.35 asubuhi kwa ndege ya Kenya Airways. Maofisa wote hao wa mechi hiyo watarejea makwao Jumatatu (Juni 17 mwaka huu).
Subscribe to:
Posts (Atom)