STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 20, 2013

NSSF YAIPIGA JEKI' ROCKY CITY MARATHON 2013

Mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini BMT, Dioniz Malinzi akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa mbio za Rocky Marathon.  
Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Juma Kintu akifafanua jambo wakati wa uzinduzi wa mbio za Rocky City Marathon uliofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo NSSF imedhamini mbio hizo kwa kutoa sh.milioni 15. 
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Suleima Nyambui.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza wakati wa uzinduzi wa mbio za Rocky Marathon 2013 Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel, akizindua rasmi mbio za Rocky City Marathon 2013 jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Juma Kintu ambao wamedhamini mbio hizo kwa kutoa sh.milioni 15. 
 Baadhi ya wadau.
Picha ya pamoja.
MSIMU wa tano wa mbio za Rock City Marathon umezinduliwa, ambapo mdhamini mkuu Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limetaka kuwepo kwa mgawanyo wa majukumu kwa mbio za umbali tofauti ili kuharakisha uendelezaji wa vipaji vya wanariadha nchini.

Rock City Marathon zinaratibiwa na Kampuni ya Capital Plus International (CPI), ambapo Ofisa Uhusiano wa NSSF inayodhamini mbio hizo kwa mwaka wa nne sasa, Juma Kintu aliliomba Shirikisho la Riadha Tanzania RT kugawana majukumu na wadau.

“Sisi kama NSSF tuko tayari kudhamini na kuchangia maendeleo ya riadha nchini, ndio maana tunasisitiza mgao wa majukumu kwa wakimbiaji wa umbali fulani kusimamiwa na taasisi au kampuni moja, ili kusaidia maendeleo ya haraka na makuzi sahihi ya vipaji,” alisema Kintu.

Pamoja na NSSF, wadhamini wengine wa Rock City Marathon 2013 zitakazofanyika jijini Mwanza Oktoba 27 ni pamoja na PPF, Airtel, African Barrick, Nyanza Bottlers, Sahara Media, Precission Air, Bank M, New Mwanza Hotel na Umoja.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel, aliyekuwa mgeni rasmi, alisema mchezo wa riadha nchini unaelekea kuangamia na jitihada za kuunusuru zinahitajika.

“Ni aibu kuwa mchezo wa riadha nchini unaelekea kufa wakati viongozi waliopewa mamlaka ya kuhakikisha unaendelea wanashuhudia. Ni wakati wa kuamka kuunusuru mchezo huu ambao katika miaka ya 1970 mpaka 1980 uliiletea nchi yetu heshima kubwa.

Kwa upande wake, Rais wa RT, Suleiman Nyambui aliwataka waratibu wa marathon kote chini kuhakikisha wanakuwa na mbio fupi za vijana ili kupanua wigo wa kuzalisha vipaji vipya, vitakavyoliletea sifa taifa na kushinda mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Naye Mgurugenzi Mtendaji wa Capital Plus, Ellen Otaru Okoedion, aliishukuru Serikali kwa ahadi ya ushirikiano, lakini akaitaka kuhakikisha inakaa mezani na (kina Nyambui) RT, ili kujadili njia sahihi zitakazofanikisha kupatikana kwa kina ‘Nyambui wapya.’

Aidha, Mratibu wa tukio hilo, Mathew Kasonta alisema kuwa mbio hizo zitajumuisha  kilometa tano kwa wakimbiaji kutoka katika makampuni, kilometa tatu kwa wenye ulemavu, kilometa tatu kwa watu wazima (zaidi ya miaka 55) na kilometa mbili kwa watoto wenye umri kati ya miaka 7 mpaka 10.

Msiba tena! Mwanajeshi mwingine wa Tanzania afariki Congo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdNJZZWb0uOyOr0xkZ4jESmQ2W9lpQ7JqPz7eO55Re1lTPE9x_VB50rB3ip7BdIvmzMXuzfPSrEPHFiXk3c58fxJmXG4R96K8IghFM_XbKsy5ZG0DVK8q3OsuweCkJUla56q1Cf65TPP5V/s640/mwamnyange.jpg
 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamnyange

MSIBA tena! Hizi ni habari za kusikitisha kusikia, ila ni kwamba  shujaa mwingine wa Tanzania amefariki dunia katika harakati za kulinda amani ya waafrika wenzetu. 
Habari zilizotolewa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) zinasema mwanajeshi anayetambulika kwa jina la Private Hugo Munga, ambaye alijeruhiwa kwenye shambulio lilisababisha Meja Khatibu kufariki dunia, naye amefariki.
Mwanajeshi huyo alikuwa nchini South Africa kwa ajili ya matibabu, lakini kwa bahati mbaya Tanzania imempoteza shujaa huyu. 
Mwili wake unatarajiwa kufikishwa hapa nyumbani kesho ukitokea nchini South Africa.
1j
2j

Polisi Dar wapiga marufuku maandamano ya Wapinzani, kisa...!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgTqetlsLeH_ScYXsPtt6WO1C0fCX-TowGb2uhPjHn6Tr5y1FeOFQlW2IKA6Gvj_SbkIxEdBwIkNjl_C_wq6S1VMWROlSa0pU8X4P2JHsx_PisWpU2abyDZBphoYSSGa0JX6_sKaf-j_NY/s1600/Kova1%252814%2529.jpg
Kamanda Suleiman Kova
JESHI la Polisi Jijini Dar es Salaam limeyapiga marufuku maandamano ya umoja wa vyama vya CUF, NCCR na CHADEMA yaliyopangwa kufanyika kesho Jumamosi.
Maandamano hayo yaliyokuwa  yamepangwa  kuanzia Tazara hadi Jangwani kisha Mwenge hadi Jangwani na sehemu mbalimbali .

Taarifa  iliyotolewa  na Kamanda Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova kupitia ITV   imeeleza kuwa Polisi wamechunguza na kugundua kwamba  maandamano  hayo  yataleta usumbufu kwa watu wengine na kwamba kwa kuwa lengo ni kufika Jangwani basi Viongozi wa vyama hivyo wawaambie wafuasi wao waende Jangwani bila Maandamano. 

Masogange aanza kufurahia 'uhuru' wa dhamana aliyopewa 'Kwa Mabida'

Mcheki katika picha hizi alizotupia leo mtandaoni



Picha hizi Amezipiga akiwa Gym leo asubuhi zinazidi kutoa ushahidi kuwa yupo Mtaani ...au jela za South Mambo ndio hivi ? We unasemaje?

Waziri Mukangara mgeni rasmi Redd's Miss Tanzania

Vimwana wanaotarajiwa kuchuana kesho kwenye shindano la Redd's Miss Tanzania 2013
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika shindano la urembo la taifa mwaka huu 'Redd's Miss Tanzania 2013' litakalofanyika kesho kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar se Salaam.
Gazeti la kila siku la NIPASHE linalochapishwa na Kampuni ya The Guardian Ltd ni miongoni mwa wadhamini wa shindano hilo litakalotoa mwakilishi wa nchi katika fainali za Urembo za Dunia (Miss World).
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga, alisema jana wanatarajia  kiongozi huyo wa serikali kushuhudia shindano hilo na kwamba amesharidhia kuwa mgeni rasmi.
Lundenga alisema kila kitu kimekamilika na kuwataka wadau wa sanaa ya urembo kusubiri kushuhudia shindano lililo bora zaidi ya miaka iliyopita.
"Maandalizi yamekamilika na kama ni chakula, sasa kinachosubiriwa ni kukila tu," alisema kwa kifupi mratibu huyo ambaye kampuni yake imekuwa ikiandaa shindano hilo tangu 1994.
Alisema shindano hilo litapambwa na burudani kutoka kwa mshindi wa tuzo ya mwanamuziki bora wa kike nchini, Judith Wambura 'Lady Jay Dee' ambaye kwa sasa anatamba na vibao vyake vya Yahaya na Joto Hasira, Mike Rose wa Uganda na kikundi cha ngoma za asili cha Mama Afrika.
Shindano hilo linatarajiwa kushirikisha warembo 30 kutoka sehemu mbalimbali nchini watakaowania taji linaloshikiliwa na Brigitte Alfred, kutoka Kanda ya Kinondoni jijini ambaye kwa sasa yuko Indonea akijiandaa kupanda jukwaani kuwania taji la dunia ifikapo Septemba 28, mwaka huu.
Hata hivyo, warembo watano wameshatinga hatua ya 15 bora baada ya kutwaa mataji madogo yaliyoshindanishwa wakiwa kambini.
Warembo hao ni Severina Lwinga, kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam ambaye ni Redd's Miss Personality, Prisca Clement (Redd's Miss Tanzania Talent), Clara Bayo (Redd's Miss Sports Woman ), Happiness Watimanywa (Redd's Miss Photogenic) na Narietha Boniface ambaye ni Redd's Miss Tanzania Top Model.
Mshindi wa taji hilo mwaka huu atabeba dhamana ya kuiwakilisha nchi katika shindano la urembo la dunia mwakani na zawadi ya Sh. milioni nane pamoja na gari lenye thamani ya Sh. milioni 15.

Homa ya pambano la Man Utd, City yaanza

http://img.thesun.co.uk/aidemitlum/archive/01507/kompany_1507398a.jpg
Vincent Kompany
http://www.independent.co.uk/incoming/article8668976.ece/BINARY/original/wayne-rooney.jpg
Wayne Rooney


KATIKA kile kinachoonekena kama ni kuanza kupanda kwa 'homa ya pambano' baina ya wapinzani wa mji wa Manchester, Manchester United na Manchester City waachezaji wa timu hizo wameanza kutambiana.
Beki nmahiri wa Manchester City, Vincent Kompany amesema anasubiri kwa hamu kucheza dhidi ya Wayne Rooney keshokutwa Jumapili na anatumai kwamba mshambuliaji huyo wa Manchester United atakuwa katika kiwango chake cha juu.
Rooney amefunga magoli matatu katika mechi mbili tangu aliporejea katika kikosi kwa kwanza baada ya kupata jeraha la katika paji la uso lililomweka nje ya uwanja lakini nahodha huyo Man City alipuuza mitazamo kwamba anatamani kuona kiwango cha mshambuliaji huyo kinakuwa chini katika mechi yao ya mahasimu wa mji wa Manchester Jumapili.
"Hapana. Unahitaji kucheza dhidi ya wachezaji walio katika kiwango chao cha juu kabisa," aliwaambia waandishi wa habari. "Hivyo ndivyo ninavyoona. Daima nataka kucheza dhidi ya wachezaji wanaokuwa katika kiwango chao bora kabisa.
"Nina furaha sana kwa Wayne kwamba yuko katika kiwango cha juu. Huu ndiyo utamu wa Ligi kuu ya England, unacheza dhidi ya washambuliaji wakubwa wakati wote, lakini kuna wachezaji wengi wa kuchunga katika timu zote."
David Moyes na Manuel Pellegrini wanaelekea katika mechi yao ya kwanza ya watani wa jadi wa mji wa Manchester wakiwa kama makocha wa timu hizo, ingawa Mscotland huyo alishinda mechi nne mfululizo kwenye Uwanja wa Etihad baina ya mwaka 2008 na 2010 wakati akiifundisha Everton.
Lakini Kompany haamini kama matokeo hayo ya zamani yana mchango wowote katika kitakachotokea Jumapili.
"Ni timu tofauti, ni msimu tofauti na naweza kusema kwamba huwezi kutabiri matokeo ya mechi hii ya watani wa jadi," aliongeza. "Hakuna mtu aliyetabiri kwamba tungeshinda 6-1 kwenye Uwanja wa Old Trafford (katika msimu wa 2011-12), kwamba wangetufunga kwenye Uwanja wa Etihad au kwamba tungeshinda Old Trafford (msimu uliopita). Nadhani hicho ndicho mashabiki wanachopenda. Mechi isiyotabirika.
"Ni mechi ambayo daima unaisubiri. Sidhani kama watu wa mjini Manchester tu bali duniani kote wanajiandaa kufurahia mechi hiyo.
"Ni mechi ambayo inavutia kwa mengi. Sijawahi kuichukulia poa na najiona kubarikiwa kucheza katika mechi hizo. Unafanya kila uwezalo kuhakikisha unacheza vyema katika mechi hizi."
 





Tottenham, Swansea, Fiorentina 'zaua' Ulaya

Goal king: Jermain Defoe scored twice in the first half as Spurs cruised to victory
Defoe akishangilia moja ya mabao yake ya jana
Up and running: Swansea celebrate after Wilfried Bony scored the club's first European goal
Swansea City wakishangia moja ya mabao yao yalioizamisha Valencia
WAKATI Swansea wakishinda ugenini dhidi ya wenyeji wao Valencia ya Hispania, 'Vijogoo' vya Londo ya Kaskazini, Tottenham Hotspur wenyewe wameikandika Tromso kwa mabao 3-0 ikiwa nyumbani katika mechi za Ligi ndogo ya UEFA.
Valencia iliyomaliza mchezo huo ikiwa pungufu baada ya mchezaji wake Adil Rami kutolewa dakika 10 kabla ya pambano kuisha ilijikuta ikilala nyumbani kwa mabao ya Wilfried Bony, Michu na Jonathan de Guzman.
Katika mchezo wa Spurs dhidi ya Tromso, washindi walipata mabao yake kupitia Jermain Defoe aliyefunga mara mbili na jingine la Christian Eriksen.
Mechi nyingine  timu ya St. Gallen iliishinda 2 - 0 dhidi ya Kuban' Krasnodar,        Dinamo Zagreb ikalala nyumbani 2-1 mbele ya Chornomorets kama ilivyokuwa kwa PSV iliyonyukwa mabao 2-0 nyumbani na Ludogorets.
Nayo timu ya Salzburg iliisasambua Elfsborg kwa mabao 4-0, Standard Liège ikalala 2-1 kwa Esbjerg, Zulte-Waregem na Wigan zikatoka suluhu, Maribor ikalala 5-2 kwa Rubin Kazan' na Fiorentina ikashinda nyumbani 3-0 djhidi ya Paços de Ferreira.
Mechi nyingine matokeo yake ni kama ifuatavyo;
Pandurii Târgu Jiu  0-1 Dnipro Dniprop…    
Eintracht Fran…    3-0  Bordeaux    
Maccabi Tel Aviv    0-0  APOEL    
Dynamo Kyiv     0-1  Genk    
Thun     1-0  Rapid Wien    
Freiburg    2-2  Slovan Liberec    
Estoril     1-2  Sevilla    
Real Betis    0-0  Olympique Lyonnais
Vitória Guimarães   4-0  Rijeka    
Apollon     1-2 Trabzonspor    
Lazio     1-0  Legia Warszawa
Sheriff    0-0  Anzhi    
PAOK     2-1  Shakhter Karagandy    
Maccabi Haifa   0-1 AZ      

Thursday, September 19, 2013

Maskini! Watoto wa3 wa familia moja wateketea kwa moto



WATOTO watatu wa familia moja wenye umri kati ya miaka miwili na sita, mmoja wao mwanafunzi wa shule ya awali, wamekufa baada ya nyumba walimokuwa wamelala kuungua moto.

Tukio hilo lililozua simanzi kubwa, lilitokea katika Kijiji cha Lushamba, Wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza, saa 5:00 usiku wa kuamkia Septemba 16, mwaka huu.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Careen Yunus, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, ingawa hakuwa tayari kutoa maelezo zaidi.

Mama mzazi wa watoto hao anadaiwa kuwaacha watoto hao na kwenda kwa rafiki yake, ambaye mahusiano yao hayakutajwa.

Kitendo hicho ambacho kiliwaudhi wanakijiji na kutaka kumvamia, kumshambulia na kumuua mama huyo.

Hata hivyo, mama huyo alinusurika baada ya uongozi wa kata hiyo chini ya Afisa Mtendaji wake, Amos Mabula, kuingilia kati na kutuliza hasira za wananchi hao.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Bulyaheke, Mabula, aliwataja watoto waliofariki dunia katika ajali hiyo kuwa ni Joseph Alfonce (6),  mwanafunzi wa Shule ya Awali Kanyala; sofia Alfonce (4) na Ndeva Alfonce (2).

Mama wa watoto hao, Naomi Kilembi (25), anashikiliwa na polisi kwa mahojiano.

Mumewe, Alfonce Budanda, ambaye walijaliwa kuzaa watoto wanne, akiwamo mwenye umri wa miezi mitano aliyekuwa ametoka na mama yake usiku huo, wakati tukio hilo linatokea alikuwa safarini.

Mabula alisema akiwa mlinzi wa amani katika kata hiyo, baada ya wananchi kukusanyika eneo la tukio wakiwa na hasira, mama wa watoto hao alitokea, huku watoto wakiwa wameshateketea kwa moto.

Alisema kuwa alichukua hatua baada ya mama huyo kukiri mbele yake kuwa alikuwa ametoka usiku na kuwaacha watoto hao.

Awali, Diwani wa Kata hiyo, Bagesi Ngele, akizungumzia tukio hilo, alisema tabia hiyo haiwezi kuruhusiwa kuendelea.

Alisema tukio hilo lingeweza kuzuilika kama hatua zingechukuliwa kunzia kwa familia yenyewe kwani kitendo cha kuwaacha watoto peke yao huku kukiwa moto ni cha hatari ikizingatiwa ilikuwa nyumba

TFF yatoa siku 14 kuiona mikataba ya makocha VPL, FDL


Kocha wa Azam na wasaidizi wake inatakiwa mikataba yao TFF

Brandts wa Yanga na Minziro nao wanatakiwa mikataba yao itue TFF
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa siku 14 kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na za Ligi ya Daraja la Kwanza (FDL) kuwasilisha mikataba ya makocha wao.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana Septemba 12 mwaka huu imebaini klabu nyingi hazijawasilisha mikataba ya mabenchi yao ya ufundi, kitu ambacho ni matakwa ya kikanuni. Siku hizo 14 zimetolewa kuanzia Septemba 17 mwaka huu.

Kwa klabu ambazo zitashindwa kuwasilisha mikataba hiyo na vielelezo vingine ndani ya mudau huo zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni.


Simba, Mgambo wavuna Sh. Mil 58


Na Boniface Wambura
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Mgambo Shooting Stars iliyochezwa jana (Septemba 18 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 58,365,000.

Watazamaji 10,241 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 23 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa wenyeji Simba kuibuka na ushindi wa mabao 6-0.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 13,839,327.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,903,135.59.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,036,946.16, tiketi sh. 2,548,890, gharama za mechi sh. 4,222,167.70, Kamati ya Ligi sh. 4,222,167.70, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,111,083.85 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,641,954.10.

Baby Madaha alamba 'bingo' Kenya

Baby Madaha
Bosi Mpya wa Madaha, Joe Kariuki
MSHIRIKI wa zamani wa BSS, Baby Madaha amelamba 'bingo' baada ya kuingia mkataba wa miaka miwili wa kufanya kazi na kampuni na Candy n Candy Records ya nchini Kenya wenye thamani ya Sh. Mil 20 za Kenya ambazo ni sawa na Sh. Mil 50 za kitanzania.
Mbali na donge hilo, pia kampuni hiyo inayoongozwa na Mkurugenzi wake, Joe Kariuki imepa msanii huyo anayetamba kwenye fani ya muziki na filamu nchini, gari aina ya Audi TT.
Akizungumza na MICHARAZO, Baby alisema mkataba huo aliingia hivi karibuni na kampuni hiyo na tayari ameshafyatua kazi mpya kupitia kampuni hiyo iitwao 'Summer Holiday' ambao anatarajia kuizindua rasmi Oktoba 6 jijini Dar es Salaam.
Baby alisema uzinduzi huo utakaoambatana na 'party' ya kusherehekea mafanikio yake kisanii itafanyika kwenye ukumbi wa Dar Live na kusindikizwa na burudani za wasanii mbalimbali.
"Nimeingia mkataba wa miaka miwili wa kufanya kazi nchini Kenya kupitia kampuni ya Candy n Candy ambayo mbali na fedha pia wamenipa usafiri na tayari nimeshatoa kazi chini yao  iitwayo Summer Holiday iliyoanza kutamba kwenye vituo vya Channel O na MTV," alisema.
Msanii huyo aliyeibuliwa na shindano la BSS 2008, alisema anajisikia fahari kuwa msanii wa kwanza wa kike nchini kupata mkataba mnono kama huo nchini Kenya na imani yake ni mwanzo wa safari yake kuelekea kwenye kilele cha mafanikio kimuziki.

Barafu, Mzee Majuto waja na Daladala pamoja na Monalisa

Kava la filamu mpya ya msanii Barafu
Barafu
BAADA ya kuwatumikia wenzake kwa muda mrefu, hatimaye msanii mahiri wa filamu, Seleman Abdallah 'Barafu' ameibuka na kazi yake binafsi iitwayo 'Daladala' inayozungumzia mikasa, vituko na kero zote zilizopo ndani ya usafiri huo wa umma.
Ndani ya filamu hiyo, mkali huyo ameigiza na wasanii wakongwe nchini kama Amri Athuman 'King Majuto', Yvonne Cherly 'Monalisa' na wengine.
Akizungumza na MICHARAZO Barafu anayefahamika pia kama 'Mzee wa Land Rover', alisema hiyo ni kazi ya kwanza kwake kuuitoa kupitia kampuni yake iitwayo 'Mtafuna Films Production' na ni 'serious comedy'.
Barafu alisema, anatarajiwa kuitoa hadharani filamu hiyo wiki mbili zijazo, na kuwataka mashabiki kujiandaa kupata burudani na 'kuvunjika mbavu' kwa namna walivyoiigiza filamu hiyo na hasa vimbwanga vya Mzee Majuto.
"Kwa wale ambao wavijua vituko vya Mzee Majuto wajiandae kuumia zaidi kwa namna mzee huyo, mimi na Monalisa tulivyofanya mambo makubwa katika filamu hii ya 'Daladala'," alisema.
Barafu alisema baada ya kutoka kwa 'Daladala' ataanza maandalizi ya kazi zake nyingine kupitia kampuni yake mbali na zile za kushirikishwa na wenzake ambazo alidai hawezi kuziacha.

Chelsea hoi darajani, Barca 'yaua', Arsena yatakata

All smiles: Messi celebrates his opener with defener Dani Alves
Messi akishangilia moja ya mabao yake usiku wa kuamkia leo
Sulley Muntari
Sulley Muntari akishangilia bao la ushindi la Ac Milan alilofunga lala salama
Matchwinner: Marco Streller (second right) steals in at the near post to head Basle's decisive second goal
Basel wakijipatia bao la pili lililoizamisha Chelsea 'darajani' huku Mourhino akipewa ujumbe kupitia mabango kwamba Mata atatakiwa awe uwanjani na siyo kwenye benchi.
 Rumblings of discontent: A Chelsea fan shows his displeasure at Juan Mata's lack of first-team action
WAKATI Jose Mourinho na vijana wake wa Chelsea wakianguka 'darajani' kwa kulala mabao 2-1 mbele ya Basel ya Uswisi, Lionel Messi ameendelea kuboresha rekodi yake ya mabao baada ya kufunga 'hat trick' wakati Barcelona ikiizamisha Ajaz kwa mabao 4-0.
Chelsea ilikumbana na kipigo hicho na kuifanya icheze mechi nne bila kupata ushindi, japo walianza kutangulia katika mechi hiyo iliyochezwa Stanford Bridge kupata bao kupitia Oscar kabla ya Basel kusawazisha mabao yote katika kipindi cha pili.
Mabao ya washindi hao ambao wamekuwa wakizisumbua timu kubwa kila mara katika michuano hiyo, yalifungwa na Salah dakika ya 71 na Streller dakika ya 82.
Katika mechi nyingine Barcelona ikiwa uwanja wake wa nyumbani iliisasambua Ajax ya Uholanzi kwa kuishindilia mabao 4-0, huku 'mchawi mweupe' Messi akitumbukiza mara tatu na kuondoka na mpira wake nyumbani.
Bao jingine la mabingwa hao wa Hispania lilifungwa na Gerard Pique, ilihali Arsenal wakiwa ugenini nchini Ufaransa walitakata baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Olympique Marseille nao Ac Milan ikiwa nyumbani ilifunga Celtic mabao 2-0.
Mecchi nyingine matokeo yake ni Schalke 04 kuilaza Steau Bucharest mabao 3-0, Napoli kuitafuna Borussia Dotmund ya Ujerumani mabao 2-1 nchini Italia, kadhaalika Atletico Madrid wakitakata nyumbani kwa kuilaza Zenit kwa mabao 3-1na Porto ya Ureno kushinda ugenini mbele ya wenyeji wa Austria Wien.

Mabao 58 yafungwa Ligi Kuu, Tambwe nouma Ashanti, Prisons angalau sasa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhSAUn1hwkMI3BcBcVeWb4YPc0cKNG2217o1rBuA9t_YRDuDqEfojRYqpc29if8_8ljHN5fIIGwDFx3hdNQ8y8cAo4E9tHnw8BP3Wr4L1T4iGcr2gWQ3Ua9aWJGULdoHdk_r9la7cxPVzw/s1600/DSC_0072.jpg
Tambwe Amissi

JUMLA ya mabao 58 yametinga wavuni mpaka sasa Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa imemaliza raundi nne tangu ilipoanza rasmi Agosti 28 mwka huu, huku Mrundi Tambwe Amisi akiongoza orodha ya wafungaji baada ya jana kutupia mabao manne pekee yake wakati Simba ikiichinja Mgambo JKT kwa mabao 6-0.
Mfungaji Bora huyo wa michuano ya Kombe la Kagame, anafukuziwa na wachezaji wa Yanga na Simba, Jerry Tegete na Haruna Chanongo wenye mabao matatu kila mmoja, huku wachezaji sita wengine wakiwa kwenye nafasi ya tatu na mabao mawili kila mmoja.
Wachezaji hao ni Didier Kavumbagu wa Yanga, Saad Kipanga wa Rhino Rangers, Bakar Kondo wa JKT Ruvu, Elias Maguri (Ruvu Shooting), Jonas Mkude wa Simba na Jerry Santo (Coastal Union).
Safu ya mbele ya Simba ndiyo mpaka sasa inaonekana kuwa kali baada ya kutumbukiza wavuni mabao 11 ikifuatiwa na watani zao Yanga wenye mabao nane, huku timu ya Prisons ndiyo yenye safu butu ya ushambuliaji ikitupia bao moja tu wavuni, ikizidiwa na timu za Oljoro JKT na Ashanti yenye mabao mawili kila moja.
Wakati ukuta wa JKT Ruvu ukiwa mgumu kupitika, ule wa maafande wenzao wa Mgambo JKT ndiyo 'nyanya' baada ya kuruhusu mabao 9 mpaka sasa ikifuatiwa na Ashanti (8) na Prisons iliyofungwa mabao 7.
Mashabiki wa soka watarajie mabadiliko makubwa ya orodha ya ufungaji na hata kwenye msimamo wa Ligi Kuu ambao kwa sasa unaoongozwa na Simba mwishoni mwa wiki wakati ligi hiyo itakapoendelea kwa timu zote 14 kushuka tena dimbani, huku pambano linalosubiriwa kwa hamu likiwa ni Yanga na Azam.
Chini ni msimamo wa sasa wa Ligi hiyo na orodha ya wafungaji mabao;

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014                                            P  W  D  L    F  A  GD  PTS
1. Simba                         4   3   1   0   11 2  9   10
2. JKT Ruvu                   4   3   0   1   6  1   5    9
3.  Ruvu Shooting           4   3   0   1   6  2   4    9
4.  Yanga                        4   1   3   0   8  4   4    6
5.  Azam                         4   1   3   0   5  3   2    6
6.  Coastal Union            4   1   3   0   4  2   2    6
7.  Mbeya City                4   1   3   0   3   2   1   6
8.  Kagera Sugar             4   1   2   1   3   3   0   5
9.  Mtibwa Sugar            4   1   2   1   2  3   -1   5
10.Rhino Rangers            4   0   3   1   4  6   -2   3
11. Mgambo JKT           4   1   0   3   1   9  -8   3
12. Prisons                      4   0   2   2   1   7  -6   2
13. Oljoro  JKT              4   0   1   3   2   6  -4   1
14. Ashanti United           4   0   1   3   2   8  -6   1

Wafungaji:

4- Tambwe Amisi (Simba)
3- Jerry Tegete (Yanga), Haruna Chanongo (Simba)
2- Didier Kavumbangu (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Jerry Santo (Coastal Union)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla, (Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva (Yanga), Iman Joel, Salim Majid (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris, Kipre Tchetche (Azam), Mwagane Yeya, Steven Mazanda, Paul Nonga (Mbeya City), Laurian Mpalilem, Peter Michael (Prisons-OG), Ayoub Kitala, Jerome Lembeli, Cosmas Ader (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Salum Machaku, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga (Mgambo JKT), Themi Felix, Godfrey Wambura, Maregesi Marwa (Kagera Sugar), Amir Omary, Shaibu Nayopa (Oljoro JKT)

Matokeo ya mechi za awali


Agosti 24, 2013
Yanga vs Ashanti United (5-1)
Mtibwa Sugar vs Azam (1-1)
Oljoro JKT vs Coastal Union (0-2)
Mgambo JKT vs JKT Ruvu (0-2)
Rhino Rangers vs Simba (2-2)
Mbeya City vs Kagera Sugar (0-0)
Ruvu Shooting vs Prisons (3-0)

Agosti 28, 2013
Mtibwa Sugar vs Kagera Sugar (1-0)
Rhino Rangers vs Azam (0-2)
JKT Ruvu  vs Prisons (3-0)
Mbeya City vs Ruvu Shooting (2-1)
Mgambo  vs Ashanti United (1-0)
Oljoro JKT vs Simba (0-1)
Yanga  vs Coastal Union (1-1)

Sept 14, 2013

Simba  vs Mtibwa (2-0)
Coastal Union  vs Prisons (0-0)
Ruvu Shooting va Mgambo JKT (1-0)
Oljoro JKT vs Rhino Rangers (1-1)
Mbeya City  vs Yanga (1-1)
Kagera Sugar vs Azam (1-1)
Ashanti United  vs JKT Ruvu (0-1)


Sept 18, 2013
Prisons vs Yanga (1-1)
Simba vs Mgambo JKT (6-0)
Kagera Sugar vs JKT Oljoro (2-1)
Azam  vs Ashanti United (1-1)
Coastal Union  vs Rhino Rangers (1-1)
Mtibwa Sugar  vs Mbeya City (0-0)
Ruvu Shooting vs  JKT Ruvu (1-0)

Ratiba ya mechi zijazo mwishoni mwa wiki hii
Jumamosi
Mgambo JKT vs Rhino Rangers
Prisons vs Mtibwa Sugar
Simba vs Mbeya City
Kagera Sugar vs Ashanti United

Jumapili:

 JKT Ruvu vs Oljoro JKT
Azam  vs Yanga
Coastal Union v Ruvu Shooting 

Wednesday, September 18, 2013

Ray, Lulu kunogesha Dar Filamu Festival 2013

http://thumbp4-ne1.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AO9WimIAAAfiUjk68wAAAJhFJXY&midoffset=2_0_0_1_1304473&partid=5&f=1215&fid=Inbox&w=480&h=331
Stanford Kihore (kati) akizungumza huku Lulu kushoto akiwa makini
TASNIA ya filamu Tanzania inakua kwa kasi sana kila kunapokucha lakini pengine ni tasnia pekee ambayo imekuwa na changamoto nyingi, na sintofahamu kwani ndio tasnia ambayo imekosa mtiririko wa matukio ambayo huwa kama motisha kwa wadau na wasanii wa filamu kwa muda mrefu tasnia ya filamu hakuna tuzo zozote takribani miaka sita zilipofanyika tuzo za Vinara 2007/8.

Tuzo na matamasha ya filamu ni vitu ambavyo uchochea sana ubora na ukuaji wa filamu katika tasnia ndio maana sehemu yoyote yenye mafanikio ya filamu lazima utawaliwa na matamasha ya sinema, ukiangalia filamu za kibongo ni nyingi sana na zimekuwa zikizalishwa na kutolewa kwa wingi na kuingia sokoni kwa kasi bila kuwa na mizania yoyote jambo linalotuchelewesha na kushindwa kufikia medani za kimataifa.

Hivi karibuni tamasha kubwa la filamu limezinduliwa na linatarajia kufanyika kuanza tarehe 24 hadi 26 Septemba 2013 katika viwanja wa CoICT- UDSM- Posta Kijitonyama Tamasha litaambatana utoaji wa  Semina kwa wadau wa filamu, kuonesha filamu za kitanzania kwa watu wote bure kwa siku tatu,Kutakua na filamu nne kwa siku kuanzia saa kumi na mbili jioni mpaka saa tano usiku.

Tamasha hilo linaloitwa Dar Filamu Festival (DFF 2013/14) linajenga histori mpya katika tasnia ya filamu kutokana na sera ya tamasaha lenyewe ambalo limekusudia kutoa fursa na kuwajengea uzoefu watayarishaji wa filamu sambamba na wasanii na kubaini umuhimu wa kuwa na matamasha, DFF pia imekusudia kutumia fursa ya kufanya Lugha ya Kiswahili bidhaa yenye mlengo wa kibiashara.

Filamu zitakazoonyeshwa ni zile ambazo zimetumia kuigizwa kwa Lugha ya Kiswahili tu, kwa kuanza ni filamu za Tanzania tu ndiyo zitakazorushwa katika Projecta kubwa kwa siku tatu  kwa jioni kuanzia saa kumi na mbili hadi saa tano usiku, hiyo ni sehemu muhimu sana na kubwa kwani hiyo ni fursa nyingine ya kuongeza mauzo badala ya njia moja tu ya kuuza Dvd pekee.

Ni Tanzania pekee ndiyo ambayo utegemea sana mauzo ya aina moja tofauti na nchi zilizoendelea ambazo kuna aina nyingi za ufanyaji wa biashara ya filamu, ikiwa soko kama uuzaji wa filamu katika majumba ya sinema tukio ambalo huwa la kwanza kabisa, filamu kuonyeshwa awali kabisa kabla ya kuingia  mtaani, filamu ikitoka kila kitu ni biashara.

Katika Dar Filamu Festival 2013/14 inastahili pongezi kwani pia inajenga hadhi kwa waigizaji wetu tayari wasanii ambao wamekuwa na mchango mkubwa wanakuwa mabalozi wa tamasha hilo, msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’ anasimama kama mwigizaji wa kike anayewakilisha wasanii wenzake kama balozi anayebeba wengine na alama ya tamasha .

Balozi mwingine Vincent Kigosi ‘Ray’ ambaye akiwa kama mtayarishaji na muongozaji aliyechangia ukuaji wa tasnia ya filamu Tanzania, tamasha limempa nafasi kama official Producer and Director  kwa tamasha kuwaweka mbele wasanii wetu ni njia nyingine ya biashara kwao, mara nyingi kuna changamoto nyingi kwa wasanii wetu pamoja na kuwa na wafuasi wengi bado hawapati nafasi za matangazo.

“Nimefurahia sana kuchaguliwa kama Balozi wa Dar Filamu Festival na ninafuraha sana kwani kwanza kabisa ni kuonyesha uzalendo kwa kuwa na tamasha la filamu linalotuhusu sisi kama watengenezaji filamu za Kiswahili Lugha ambayo wenzetu wakenya na nchi nyingine wanakitumia vizuri na kuwaingizia fedha, huku sisi tukibaki maskini,”anasema Ray.

Mratibu wa tamasha hilo Staford Kihore anasema kuwa katika kufanikisha hilo DFF inakuwa ni chachu ya maendeleo ya tasnia ya filamu Tanzania, huku tukisema kuwa Dar Filamu Festival 2013 kwa kauli mbiu ya ‘Ubora wa Filamu Zetu’ ikiwa ni njia ya kuwakutanisha wadau wote kwa pamoja na kuwa jukwaa linalojenga tasnia ya filamu inayokua kila siku huku pia tamasha likitoa njia nyingine ya soko jipya.

“Kwa tamasha hili la awali tutaonyesha filamu za hapa Tanzania pekee ikiwa ni utambulisho wa Dar Filamu Festival kwa mara ya kwanza kwenu wanahabari, miaka ijayo Tamasha litahakikisha linashirikisha filamu kutoka sehemu mbalimbali zinazotumia Lugha ya Kiswahili  kutoka popote Ulimwenguni,” anasema Staford Kihore.

“Mimi kama Balozi wa Dar Filamu Festival ninaona fahari sana kwa ukuaji wa tasnia ya filamu tunaomba watu waliunge mkono tamasha hili kwani sisi tunapiga hatua katika tasnia ya filamu, wadau waje katika viwanja vya Posta wajionea filamu pia filamu yangu ya Foolish Age itaonyeshwa tena bure kabisa nashukru sana kuchaguliwa waigizaji tupo wengi,”anasema Lulu.

Akiongea na FC mratibu wa Tamasha hilo Staford Kihore pia amesema kuwa katika kuzingatia maendeleo ya tasnia ya filamu siku tatu hizo kila siku imepewa jina kwa filamu zitakazoonyeshwa kuanzia Tarehe 24th September, 2013 siku ya Jumanne ambayo ndio siku ya ufunguzi utakuwa ni usiku wa Bongo Movie Classics, 25th September, 2013 ni usiku wa Quality Nights.

Na ile siku ya mwisho tarehe 26th September, 2013 itakuwa ni Stars Nights siku ambayo kutakuwa na wasanii wetu mbalimbali ambao wanajenga soko hilo la Bongo movie filamu, Tamasha hili linapambwa na wasanii wote wakiwakilishwa na wasanii wenzao wawili ambao ni Vincent Kigosi ‘Ray’ kama Official Producer and Director  for DFF 2013 na Elizabeth Michael ‘Lulu’ kama Official Actress for DFF 2013.

Pia tamasha litaambatana na utoaji wa semina kwa wadau wa filamu kwa asubuhi ambapo madarasa  yataendeshwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Sanaa tarehe 24 September, 2013 masomo ya Uandishi wa Muswada, Uigizaji na  Uongozaji wa filamu yatafundishwa kwa washiriki, 25th September 2013 Siku nzima Makapuni ya Utengenezaji filamu yataonyesha na kutangaza kazi zao kwa wadau mbaliambali.

Tarehe 26th September 2013 ni siku muhimu sana kwani Taasisi kama vile TRA, Bodi ya Ukaguzi wa filamu na michezo ya kuigiza, Wasambazaji wa filamu na taasisi nyingine watakutana katika jukwaa la majadiliano kuhusu mustakabali wa tasnia ya filamu, pia filamu kadhaa zitaonyeshwa na kujadiliwa na wadau watakaokuwepo matukio yote ya asubuhi yatafanyika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Idara ya Sanaa.

Kampuni ya Haak Neel Production na Filamucentral mtandao wa habari za filamu ndio waandaaji  wa tamasha hilli la Dar Filamu Festival (DFF) 2013,  kwa kushirikia na taasisi kama Bodi ya Filamu na ukaguzi wa michezo ya kuigiza Tanzania, Tanzania Film Federation (TAFF), UDSM- PFA, MFDI, Swahiliwood, Global Publishers.

Na makapuni ya usambazaji wa filamu Steps Entertainment Ltd, Leo Media na kampuni mpya ya usambazaji ya Proin Promotion ambayo imeanza hivi karibuni na kuonyesha dhamira ya kusaidia tasnia ya filamu, pia unaweza kupata habari zaidi kupitia mtandao wa www.dff.or.tz

Baada ya kuja tamasha la filamu ambalo limepokelewa vema na wadau wote ni kama moja ya kuelekea katika Nyanja za kimataifa ni wakati ambao pia Serikali na taasisi nyingine kuunga mkono na kuhamasisha uwepo wa tuzo za ndani, ambazo hazipo kwa muda mrefu tofauti na fani ya muziki ambayo kila aina yake imekuwa na tuzo, pia hivi karibu wadau walikutana kwa kujadili suala la sera ya Filamu.

Kwa shirikisho la wasanii wa filamu Tanzania (TAFF) kuweka mjadala huo ni hatua mojawapo wa kufungua njia ya kuelekea katika medani za kimataifa, pengine sera ya filamu ikiwepo itasaidia tasnia ya filamu kukua zaidi na kuwa rasmi tofauti na ilivyo sasa wadu wadai hivyo.

Tambwe aanza mambo Simba, JKT chali, Azam, Yanga mmmh!

Mrundi Tambwe Amisi akishangilia moja ya mabao yake leo uwanja wa Taifa (Pix:Bin Zubeiry)
MABAO manne ya nyota wa kimataifa wa Simba, Tambwe Amisi kutoka Burundi yameiwezesha Wekundu wa Msimbazi kukalia usukani wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuitafuna Mgambo JKT kwa mabao 6-0.
Simba ilipata ushindi huo mnono kwenye pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kufikisha jumla ya pointi 10 na mabao 11 ikiwaengua JKT Ruvu iliyokuwa ikiongoza.
Simba imekwea kileleni baada ya waliokuwa vinara JKT Ruvu kulala bao 1-0 mbele ya ndugu zao Ruvu Shooting katika pambano jingine lililochezwa kwenye uwanja wa Mabatini-Mlandizi.
Mabao mengine ya leo ya Simba yaliwekwa kimiani mshambuliaji anayezidi kuja juu nchini wa klabu hiyo ya Simba, Haruna Chanongo. Kwa kufunga mabao hao manne Tamwe ameweka rekodi ya aina yake ya kuwa mchezaji wa kwanza kwa misimu mitatu kufunga zaidi ya mabao mawili katika mechi moja pia kukwea kwenye nafasi ya kwanza ya ufungaji mabao akiwaacha nyuma akina jerry Tegete na Chanongo wenye mabao matatu kila mmoja.
Wakati Simba ikichekelea ushindi huo wa kishindo jijini Dar mabingwa watetezi Yanga waliokuwa mjini Mbeya walijikuta wakipata sare ya tatu mfululizo baada ya Prisons kuwagomea.
Jerry Tegete alitangulia kuipatia bao Yanga kabla ya wenyeji kusawazisha dakika ya 77 kupitia Peter Michael na kufanya mechi hiyo iliyochezw auwanja wa Sokoine kuisha kwa sare ya 1-1.
Waliokuwa vinara wa ligi hiyo, JKT Ruvu walijikuta wakiangukia pua mbele ya Ruvu Shooting kwa kulazwa bao 1-0 katika mechi iliytochezwa uwanja wa Mabatini, Pwani.
Katika pambano jingine lililochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, wenyeji Azam ilijikuta wakilazimishwa sare ya bao 1-1 na Ashanti United.
Azam walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia mfungaji bora wa ligi iliyopita, Kipre Tchetche dakika ya 20 ya mchezao kabla ya Anthony Matangalu kuisawazishia Ashanti dakika ya 78.
Katika mechi nyingine zilizochezwa leo Coastal Union ikiwa jijini Tanga imenusurika kipigo baada ya nahodha wake Jerry Santo kusawazisha bao na kufanya wagosi hao wa Kaya kutoka sare ya 1-1 na Rhino Rangers ya Tabora.
Nao Kagera Sugar wakiwa nyumbani kwao uwanja wa Kaitaba walmechomoza na ushindi wa mabao 2-1 dakika za jioni dhidi ya JKT Oljoro, huku Mtibwa Sugar kwenye uwanja wao wa Manungu, walibanwa mbavu na Mbeya City na kwenda nao suluhu ya kutofungana.

Tuesday, September 17, 2013

Hawa ndiyo wanawake vinara wa dawa za kulevya!

KUNA dhana iliyojengeka kuwa wanawake ni watu laini, wapole na wasioweza kufanya mambo ya hatari. Hata hivyo pia kuna wengine wanadai kuwa wanawake ni daraja hatari sana. Machoni huonekana laini lakini wanaweza kutenda mambo ambayo ni vigumu kwa mtu wa jinsia ya kiume kuyafanya. Biashara ya madawa ya kulevya inahitaji watu hatari, katili, wenye roho isiyotishika. Huwezi amini miongoni mwa watu wanaonekana jamali na wapole usoni ndiyo wakali katika biashara hiyo. Wasome vigogo 10 wanawake duniani wanaotisha kwa biashara ya 'bwimbwi' a.k.a ugoro, unga sembe nk
Mireya Moreno Carreon.
Nancy Botwin katika ‘siriz’ yake ya Weeds kwenye TV, anajaribu kuonesha jinsi mwanamke anaweza kuwa hatari katika biashara ya bangi na madawa ya kulevya kwa jumla, hata hivyo katika uhalisia, hajawafikia hata chembe wanawake hawa hatari ambao wameitikisa dunia.
Hawa ni maharamia 10 wauza unga, wametengeneza fedha nyingi na kila mmoja ameshahusika kwa namna moja au nyingine na mauji. Kwa muuza madawa ya kulevya, kitendo cha kutoa roho ya mtu kipo jirani yake sana.
1. GRISELDA BLANCO
Inawezekana huyu ndiye akawa muuza unga mwanamke katili, mwenye uwezo mkubwa kuliko wote kuwahi kutokea katika historia ya dunia. Ameshahusika na mauaji ya watu zaidi ya 200. Ni raia wa Colombia, akiwa na miaka 11, tayari alishahusika na tukio la utekaji wa mtoto. Baadaye alihamia Marekani, kwenye Jimbo la Florida ambako alitengeneza mtandao wa madawa ya kulevya ambao ulimpa utajiri mkubwa.

2.  SANDRA AVILA BELTRAN
Ni raia wa Mexico, alizaliwa mwaka 1960. Aliwahi kupewa jina la Mungu wa Kike wa Madawa ya Kulevya. Vyombo vya habari nchini mwake vikamwita Malkia wa Pacific. Serikali za Marekani na Mexico zinamtaja kuwa kiungo wa magenge ya unga ya Sinaloa Cartel la Mexico na Norte del Valle Cartel la Colombia. Anadaiwa kujipatia mabilioni ya dola kwa usafirishaji wa unga kati ya Colombia, Mexico na Marekani. Kwa sasa yupo gerezani nchini Mexico kwa kosa la utakatishaji wa fedha haramu.

3. ANGIE SANCLEMENTE VALENCIA
Ni raia wa Colombia, aliwahi kushika taji la urembo la taifa katika nchi hiyo lakini alinyang’anywa baada ya kubaini ameshaolewa. Mume wake alikuwa mmoja wa vinara wa unga na walipoachana, alitumia njia zilezile kujipatia utajiri haramu. Alikuwa na genge kubwa la wasafirishaji wa cocaine na kila mtu alimlipa dola 5,000 kwa safari moja. Alisafirisha zaidi Argentina, Uingereza na Mexico. Ana umri wa miaka 35, yupo gerezani Argentina tangu Oktoba 27, 2010.

4. KATH PETTINGILL
Alizaliwa mwaka 1935. Jina lake la utani ni Bibi Kizee Shetani (Granny Evil). Ni mwenyeji wa Jiji la Melbourne, Australia. Alianza kama kahaba kabla ya kugeukia madawa ya kulevya. Alipoteza jicho moja baada ya kupigwa risasi katika moja ya matukio ya uharamia, akimtetea binti yake, Vicky, aliyekuwa anadaiwa dola 300 na maharamia wenzake. Nguvu ya mtandao wa unga aliyoitengeneza, ni hatari na imehusika na mauaji mengi nchini Australia.

5. ENEDINA ARELLANO FELIX
Katika genge ambalo lilikuwa linaongozwa na kaka zake, Ramon na Eduardo, mwanzoni yeye alishika nafasi ya umeneja wa fedha. Baada ya Ramon kuuawa na Eduardo kukamatwa, alishika uongozi. Maofisa usalama wa Mexico waliwahi kukiri kwamba Enedina ndiye alikuwa dira ya kaka zake. Ana umri wa miaka 52, ni msomi mwenye shahada ya uhasibu. Marekani imempiga marufuku kuingia nchini humo. Amebadili mfumo na sasa anaendesha kazi zake kisayansi,
hakuna fujo za magenge ya wahuni kiasi kwamba inakuwa ngumu kumtia hatiani.

6.  BLANCA CAZARES SALAZAR
Ni raia wa Mexico, alianza kujihusisha na utakatishaji wa fedha haramu, aliponogewa akajikita kwenye unga. Ana umri wa miaka 37. Biashara yake ameitanua na yupo makini sana. Anaongoza mtandao mkubwa wenye makundi 42. Ni ngumu kumkamata kwa sababu hahusiki moja kwa moja. Marekani imempiga marufuku kuingia nchini humo.

7. MARIA JIMENEZ
Ana umri wa miaka 27. Alikuwa kiongozi wa genge lililokufa la La Tosca. Baada ya kufanya biashara kwa muda mrefu, alikamatwa mwaka jana nchini kwake Mexico kwa tuhuma za usafirishaji wa unga na mauaji. Baadaye alikiri kuua watu 20 na mpaka sasa yupo jela.

8.  EDITH LOPEZ LOPEZ
Anajulikana kama Malkia wa Kusini. Amekuwa kinara wa madawa ya kulevya tangu alipoolewa na haramia wa unga, Raul Nunez Morales, maarufu kama The Cowboy. Tangu mwaka 2000, Edith amebaki kuwa mmoja kati ya wanawake tisho kwa biashara hiyo haramu duniani.

9. THELMA WRIGHT
Alishirikiana na marehemu mumewe, Jackie Wright katika biashara ya unga kati ya miaka ya 1980 na 1990. Mwaka 1986, mumewe aliuawa, kwa hiyo akashika usukani kwa kulisuka genge lao la Black Mafia ambalo lilifanya matukio mengi. Hata hivyo, kwa kuhofia maisha ya mtoto wake, Jackiem,  kuharibika, aliachana na kazi hiyo na kufanya shughuli nyingine halali. Ni mara chache sana kutokea.

10. MIREYA MORENO CARREON
Ndiye mwanamke pekee kushika nafasi ya juu kwenye Genge la Zetas. Ndani ya kipindi kifupi alifanya matukio mengi ya utakatishaji wa fedha haramu na usafirishaji wa unga. Akiwa nchini kwake, Mexico, mwaka 2010, maofisa usalama wa siri walimkamata akiwa akiwa na gari lenye cocaine na bangi na mpaka leo yupo korokoroni.

Sheikh Ponda akwama kupata dhamana Morogoro



  Sheikh Ponda Akishuka kwenye basi la Magereza tayari kuingia Mahakamani Kusikiliza kesi yake inayomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoani Morogoro.
Sheikh Ponda anashtikiwa katika Mahakama hiyo akikabiliwa na Mashtaka Matatu ambayo inadaiwa aliyatenda Mkoani Morogoro katika Mkutano hadhara mwezi uliopita.
Kiongozi huyo wa umma wa Kiislam Tanzania amenyimwa dhamana na hivyo kurejeshwa tena rumande mpaka kesi yake itakaposomwa tena Oktoba  Mosi.






 Sheikh Ponda akiwa Chini ya Ulinzi Mkali wakati akiingia Mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoani Morogoro.




 
Sheikh Issa Ponda akiingia Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoani Morogoro leo kusikiliza kesi yake






 Wafusi wa Sheikh Ponda wakiwa wakiwa mahakamani leo kusikiliza kesi ya Kiongozi wao iliyokuwa imetajwa mahama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro.


Ulinzi mkali ukiwa umeimarishwa mahakamani leo wakati kesi hiyo ikiendelea mjini Morogoro.

Newz Alert: Shule ya Ilboru yafungwa, kisa...!

Waziri Majaliwa alipowahi kwenda kuutuliza mgogoro wa wanafunzi wa Ilboru mwaka jana
TAARIFA zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa, serikali imeamua kuifunga kwa muda usiojulikana Shule Maalum ya vipaji ya Ilboru ya jijini Arusha, baada ya kuwepo kwa tishio la kuchomwa moto kutokana na mgogoro uliodumu kwa muda mrefu shuleni hapo.
Imedokezwa wanafunzi wapatao wanne wanahojiwa kutokana na tishio hilo huku wengine karibu 800 wamerudishwa makwao mpaka watakapotangaziwa vinginevyo.
Tangu mwaka jana shule hiyo imekuwa na mgogoro baina ya wanafunzi na uongozi wake kiasi Naibu waziri wa Tamisemi (Elimu), Kassim Majaliwa kulazimika kuingilia kati, lakini hali haijatengemaa hadi hivi karibuni tena kiliponuka tena.

Msiba tena! Prince Ahmed Mgeni hayupo nasi afariki Zenji

Prince Ahmed Mgeni

TASNIA ya sanaa imeendelea kupata misiba baada ya muimbaji nyota wa zamani wa Zanzibar Stars, Prince Ahmed Mgeni kufariki dunia visiwani Zanzibar na jioni hii alitarajiwa kuzikwa.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka visiwani humo zinasema kuwa, marehemu Mgeni aliyetamba na kuziba nafasi ya Mzee Yusuf alipojiengua katika kundi hilo na kuunda Jahazi, alifariki usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Mnazi Mmoja alipokuwa amelazwa.
Taarifa za awali zinasema marehemu alikuwa akisumbuliwa na kifua kikuu (TB) na kulazwa hospitalini hapo kwa muda mrefu.
Mpaka mauti yalipomkuta jana marehemu Mgeni alikuwa mwanamuziki wa kundi la Zanzibar Njema Taarab.
Kifo cha msanii huyo ni muendelezo wa misiba katika tasnia ya sanaa kuanzia mwishoni mwa mwaka jana ambapo imeshuhudiwa waigizaji na waimbaji wakipoteza uhai kwa sababu mbalimbali ikiwamo ajali na maradhi. Mungu aiweze mahali pema peponi roho ya marehemu Ahmed Mgeni na MICHARAZO inawapa pole familia, ndugu, jamaa na rafiki wa msanii huyo pamoja na wadau wote wa sanaa Tanzania. 

Sunday Kayuni kuhudhuria kozi ya wakufunzi CAF

Sunday Kayuni
MKURUGENZI wa Ufundi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Sunday Kayuni atashiriki warsha ya wakufunzi wa makocha wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) itakayofanyika kuanzia Oktoba 22-24 mwaka huu.

Warsha hiyo iliyoandaliwa na CAF kwa ajili ya wakufunzi wake itafanyika nchini Cameroon. Wakufunzi 18 wa CAF kwa upande wa makocha watahudhuria warsha hiyo.

Madhumuni ya warsha hiyo ni kuainisha majukumu yao, kubadilishana uzoefu. Pia kuwapa methodolojia mpya ya ufundishaji na muongozo kuhusu mfumo wa leseni za makocha ambao watautumia katika nchi wanazotoka.

Mbali ya Kayuni Tanzania, wakufunzi wengine ni Ahmed Babiker (Sudan), Amadou Shaibu (Nigeria), Boy Bizzah Mkhonta (Swaziland), Duodu Fred Osam (Ghana), Edussei Anthony (Ghana), Fathi Nossir (Misri), Faouzy Altaisha (Sudan) na Fran Hilton Smith (Afrika Kusini).

Wengine ni Francis Oti-Akenteng (Ghana), Honour Janza (Zambia), Kasimawo Laloko (Nigeria), Mahmoud Saad (Misri), Paul Hamilton (Nigeria), Serame Letsoaka (Afrika Kusini), Shawky Abdel Shafy (Misri), Thondoo Govinder (Mauritius) na Ulric Mathiot (Seychelles),