STRIKA

USILIKOSE

Sunday, October 13, 2013
Mauaji!: Mtangazaj ITV/Radio One apigwa risasi, ampoteza mama mzazi
Ufoo Saro (kulia) aliyepatwa na mkasa hivi punde |
Taarifa zinasema kuwa mchumba wa mtangazaji huyo aliyetajwa kwa jina la Ansel aliyekuwa nchini Sudan kikazi alitua nchini jana na kufikia kwa Ufoo lakini kukatokea mzozo ambao haukupata suluhisho.
Hivyo wawili hao waliongozana hadi kwa mama wa mtangazaji huyo kutafuta suluhu, asubuhi hii na kwa bahati mbaya hali ilikuwa tete na ndipo kijana huyo alipotoa bastola aliyokuwa nayo na kumtwanga mama mtu risasi ya kichwa iliyomuua papo hapo.
Kama hiyo haikutosha inaelezwa jamaa huyo alimtwanga risasi Ufoo kifuani na nyingine mguuni na kudhani amemuua kabla ya yeye mwenyewe kujilipua mwenyewe kwa risasi ya kidevuni na kumuua.
Tayari miili ya watu hao wawili yaani mama yake Ufoo na jamaa huyo imepelekwa Muhimbili sambamba na mtangazaji huyo anayeelezwa yupo katika hali mbaya kwa ajili ya kuhifadhiwa na matibabu zaidi.
Haifahamiki chanzo cha mauaji hayo licha ya kudaiwa huenda ni ugomvi wa kimapenzi na haifahamiki jamaa huyo huko Sudan anakodaiwa kuwa alikuwa akifanya kazi UN alikuwa kama nani japo inaelezwa huenda alikuwa mwanajeshi ambapo kabla ya kwenda huko aliwahi kuwa mpiga picha wa ITV na kufanya kazi Mahakama ya Kimataifa ya Arusha kabla ya kuomba kazi UN.
MICHARAZO inaendelea kufuatia kwa kina taarifa hii na itawafahamisha. Pia inamuombea kila la heri na salama mtangazaji huyo aweze kupona katika mkasa uliopata na kumpoa pole kwa msiba uliompata kwa kumpoteza mama yake mzazi.
Drogba aibeba Ivory Coast, waifyatua Senegal 3-1 WCQ

MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya taifa Ivory Coast, Didier Drogba alirejea kwa kishindo katika timu hiyo baada ya kuiongoza kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Senegal katika pambano la kwanza la mtoano wa kuwania nafasi tano za kutinga Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil.
Drogba aliitwa tena katika kikosi hicho baada ya awali kuwekwa kando na kusaidia kufunga bao la penati kabla ya Solomon Kalou kufunga la tatu huku la pili wageni wao wakijifunga wenyewe.
Ivory Coast 'The Elephants' sasa imeingia mguu mmoja ndani kwenye fainali hizo za Kombe la Dunia ikihitaji sare yoyote katika mechi ya marudiano baadaye kukihakikisha kucheza fainali hizo kubwa duniani.
Drogba aliitwa tena katika kikosi hicho baada ya awali kuwekwa kando na kusaidia kufunga bao la penati kabla ya Solomon Kalou kufunga la tatu huku la pili wageni wao wakijifunga wenyewe.
Ivory Coast 'The Elephants' sasa imeingia mguu mmoja ndani kwenye fainali hizo za Kombe la Dunia ikihitaji sare yoyote katika mechi ya marudiano baadaye kukihakikisha kucheza fainali hizo kubwa duniani.
Mlinzi wa Senegal Ludovic Sane aliizawadia wenyeji bao kabla ya Kalou kufunga bao la tatu na dakika za lala salama Papiss Demba Cisse aliifungia Senegal bao la kufutia machozi ambalo linaweza kuwa msaada kama Senegal itaenda kushinda nyumbani mabao 2-0 katika mechi ya marudiano.
Katika pambano jingine Burkina Faso wakiwa kwenye uwanja wao wa Agosti 4
waliwafunga Algeria 3-2 katika mchezo uliokuwa na upinzani wa aina yake .
Mabao ya Burkinabe yalifungwa na Jonathan Pitroipa , Aristide Bance na Djakaridja Kone huku Algeria wakifunga kupitia kwa Soufiane Feghouli na Carl Medjani. Bukinabe sasa wanahitaji sare yoyote katika mechi ya marudiano itakayofanyika ugenini kufuzu fainali hizo ikiwa ni kwa mara ya kwanza kwao.
Michezo hiyo ya kuwania fainali hizo za Kombe la Dunia hatua ya mwisho kwa nchi za Afrika zitaendelea tena leo kwa mabingwa wa Afrika Nigeria kuwa ugenini mjini Addis Ababa kupepetana na wenyeji wao Ethiopia, wawakilishi pekee wa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) huku timu iliyopenya baada ya Cape Verde kuenguliwa kwa udanganyifu Tunisia itaialika Cameroon na keshokutwa Jumanne Ghana watakuwa wenyeji wa Misri.
Mabao ya Burkinabe yalifungwa na Jonathan Pitroipa , Aristide Bance na Djakaridja Kone huku Algeria wakifunga kupitia kwa Soufiane Feghouli na Carl Medjani. Bukinabe sasa wanahitaji sare yoyote katika mechi ya marudiano itakayofanyika ugenini kufuzu fainali hizo ikiwa ni kwa mara ya kwanza kwao.
Michezo hiyo ya kuwania fainali hizo za Kombe la Dunia hatua ya mwisho kwa nchi za Afrika zitaendelea tena leo kwa mabingwa wa Afrika Nigeria kuwa ugenini mjini Addis Ababa kupepetana na wenyeji wao Ethiopia, wawakilishi pekee wa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) huku timu iliyopenya baada ya Cape Verde kuenguliwa kwa udanganyifu Tunisia itaialika Cameroon na keshokutwa Jumanne Ghana watakuwa wenyeji wa Misri.
Ashanti United yaona mwezi, yailaza Coastal Union 2-1
MABAO mawili yaliyofungwa na Tumba Sued moja likiwa la penati liliisaidia Ashanti United kupata ushindi wake wa kwanza katika Ligi Kuu Tanzania Bara na kujinasua mkiani wakiiachia Mgambo JKT ya Tanga.
Ashanti iliipata ushindi huo kwenye uwanja wa Chamazi kwa kuicharaza Coastal Union ya Tanga mabao 2-1, bao la ushindi likifungwa dakika za jioni na kulalamikiwa na Wagosi wa Kaya.
Tumba Sued beki wa kati mmoja wa wachezaji chipukizi wanaotoka ukoo wa wanasoka kaka zake wakiwa ni Said Swued 'Panucci' na Salum Sued 'Kussi' alifunga bao la kwanza kabla ya Coastal Union kusawazisha kwa mkwaju wa penati kupitia nahodha, Jerry Santo.
Mchezaji huyo mrefu aliyekuwa akicheza soka la kulipwa nchini China, aliiongezea Ashanti bao la pili dakika za lala salama kwa mkwaju wa penati na kuifanya Ashanti ifikishe pointi 5 sawa na Mgambo JKT, ambayo leo inashuka dimbani kuvaana na Mbeya City mjini Tanga.
Hata hivyo Ashanti wapo juu ikishika nafasi ya 13 kutokana na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa na kuiacha Mgambo ikiburuza mkia kwa sasa.
Matokeo ya mechi za jana pia zilibadilisha msimamo wa ligi kuu ambapo Yanga ilikwea hadi nafasi ya pili ikiwapumulia watani zao watakaovaana nao Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, huku Coastal ikijikuta ikiporomoka kwa nafasi moja hadi nafasi ya nane ikiiachia nafasi Ruvu Shooting ambaye hata hivyo jana haikushuka dimbani kwa leo leo itapepetana na Rhino Rangers ya Tabora kwenye uwanja wa Mabatini.
Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014 P W D L F A GD PTS
1. Simba 8 5 3 0 17 5 12 18
2. Yanga 8 4 3 1 15 8 7 15
3. Azam 8 3 5 0 11 6 5 14
4. Mbeya City 8 3 5 0 11 7 4 14
5. JKT Ruvu 8 4 0 4 9 7 2 12
6. Kagera Sugar 8 3 2 3 9 7 2 11
7. Ruvu Shooting 8 3 2 3 9 7 2 11
8. Coastal Union 8 2 5 1 7 5 2 11
9. Mtibwa Sugar 8 2 4 2 7 9 -2 10
10.Rhino Rangers 8 1 4 3 8 11 -3 7
11.Prisons 8 1 4 3 4 10 -6 7
12. Oljoro 8 1 3 4 6 10 -4 6
13.Ashanti 8 1 2 5 6 16 -10 5
14.Mgambo 8 1 2 5 2 13 -11 5
Wafungaji:
8- Tambwe Amisi (Simba
4- Didier Kavumbagu (Yanga), Peter Michael (Prisons), Kipre Tchetche (Azam), Elias Maguri (Ruvu Shooting)
3- Jerry Tegete, Hamis Kiiza (Yanga), Haruna Chanongo, Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Themi Felix (Kagera), Paul Nonga (Mbeya City), Salum Machaku (JKT Ruvu), Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Jerry Santo (Coastal Union), Tumba Sued (Ashanti Utd)
2- Haruna Moshi (Coastal Union), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Mwagani Yeya (Mbeya City), Mrisho Ngassa (Yanga), Godfrey Wambura (Kagera Sugar)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla,(Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki, Ramadhani Singano (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva, (Yanga), Iman Joel, Salum Majid, Mwalimu Musuku, Kamana Salum, Hussein Abdallah (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris, John Bocco, Joseph Kimwaga, Faridi Maliki (Azam), Steven Mazanda, Richard Peter, Peter Mapunda (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Shaaban Susan, Jerome Lembeli, Cosmas Ader, Said Dilunga (Ruvu Shooting), Masoud Ally, Shaaban Nditti, Shaaban Kisiga (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu, Paul Maono(OG) (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga, Hamis Msafiri (Mgambo JKT), Seleman Kibuta, Daud Jumanne, Maregesi Marwa, Clement Douglas (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary, Paul Malipesa, Expedito Kidulo, Nurdin Mohammed, Fikiri Mohammed (Oljoro JKT)
Ratiba za Ligi Kuu
Leo
Ruvu Shooting vs Rhino Rangers (-)
Mgambo JKT vs Mbeya City (-)
Azam vs JKT Ruvu (-)
Mtibwa Sugar vs Oljoro JKT (-)
Okt 16, 2013
Ashanti Utd vs Prisons (-)
Okt 19, 2013
Kagera Sugar vs Coastal Union (-)
Oljoro JKT vs Azam (-)
Mtibwa Sugar vs Mgambo JKT (-)
Mbeya City vs JKT Ruvu (-)
Ashanti Utd vs Ruvu Shooting
Okt 20, 2013
Simba vs Yanga
Ashanti iliipata ushindi huo kwenye uwanja wa Chamazi kwa kuicharaza Coastal Union ya Tanga mabao 2-1, bao la ushindi likifungwa dakika za jioni na kulalamikiwa na Wagosi wa Kaya.
Tumba Sued beki wa kati mmoja wa wachezaji chipukizi wanaotoka ukoo wa wanasoka kaka zake wakiwa ni Said Swued 'Panucci' na Salum Sued 'Kussi' alifunga bao la kwanza kabla ya Coastal Union kusawazisha kwa mkwaju wa penati kupitia nahodha, Jerry Santo.
Mchezaji huyo mrefu aliyekuwa akicheza soka la kulipwa nchini China, aliiongezea Ashanti bao la pili dakika za lala salama kwa mkwaju wa penati na kuifanya Ashanti ifikishe pointi 5 sawa na Mgambo JKT, ambayo leo inashuka dimbani kuvaana na Mbeya City mjini Tanga.
Hata hivyo Ashanti wapo juu ikishika nafasi ya 13 kutokana na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa na kuiacha Mgambo ikiburuza mkia kwa sasa.
Matokeo ya mechi za jana pia zilibadilisha msimamo wa ligi kuu ambapo Yanga ilikwea hadi nafasi ya pili ikiwapumulia watani zao watakaovaana nao Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, huku Coastal ikijikuta ikiporomoka kwa nafasi moja hadi nafasi ya nane ikiiachia nafasi Ruvu Shooting ambaye hata hivyo jana haikushuka dimbani kwa leo leo itapepetana na Rhino Rangers ya Tabora kwenye uwanja wa Mabatini.
Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014 P W D L F A GD PTS
1. Simba 8 5 3 0 17 5 12 18
2. Yanga 8 4 3 1 15 8 7 15
3. Azam 8 3 5 0 11 6 5 14
4. Mbeya City 8 3 5 0 11 7 4 14
5. JKT Ruvu 8 4 0 4 9 7 2 12
6. Kagera Sugar 8 3 2 3 9 7 2 11
7. Ruvu Shooting 8 3 2 3 9 7 2 11
8. Coastal Union 8 2 5 1 7 5 2 11
9. Mtibwa Sugar 8 2 4 2 7 9 -2 10
10.Rhino Rangers 8 1 4 3 8 11 -3 7
11.Prisons 8 1 4 3 4 10 -6 7
12. Oljoro 8 1 3 4 6 10 -4 6
13.Ashanti 8 1 2 5 6 16 -10 5
14.Mgambo 8 1 2 5 2 13 -11 5
Wafungaji:
8- Tambwe Amisi (Simba
4- Didier Kavumbagu (Yanga), Peter Michael (Prisons), Kipre Tchetche (Azam), Elias Maguri (Ruvu Shooting)
3- Jerry Tegete, Hamis Kiiza (Yanga), Haruna Chanongo, Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Themi Felix (Kagera), Paul Nonga (Mbeya City), Salum Machaku (JKT Ruvu), Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Jerry Santo (Coastal Union), Tumba Sued (Ashanti Utd)
2- Haruna Moshi (Coastal Union), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Mwagani Yeya (Mbeya City), Mrisho Ngassa (Yanga), Godfrey Wambura (Kagera Sugar)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla,(Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki, Ramadhani Singano (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva, (Yanga), Iman Joel, Salum Majid, Mwalimu Musuku, Kamana Salum, Hussein Abdallah (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris, John Bocco, Joseph Kimwaga, Faridi Maliki (Azam), Steven Mazanda, Richard Peter, Peter Mapunda (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Shaaban Susan, Jerome Lembeli, Cosmas Ader, Said Dilunga (Ruvu Shooting), Masoud Ally, Shaaban Nditti, Shaaban Kisiga (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu, Paul Maono(OG) (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga, Hamis Msafiri (Mgambo JKT), Seleman Kibuta, Daud Jumanne, Maregesi Marwa, Clement Douglas (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary, Paul Malipesa, Expedito Kidulo, Nurdin Mohammed, Fikiri Mohammed (Oljoro JKT)
Ratiba za Ligi Kuu
Leo
Ruvu Shooting vs Rhino Rangers (-)
Mgambo JKT vs Mbeya City (-)
Azam vs JKT Ruvu (-)
Mtibwa Sugar vs Oljoro JKT (-)
Okt 16, 2013
Ashanti Utd vs Prisons (-)
Okt 19, 2013
Kagera Sugar vs Coastal Union (-)
Oljoro JKT vs Azam (-)
Mtibwa Sugar vs Mgambo JKT (-)
Mbeya City vs JKT Ruvu (-)
Ashanti Utd vs Ruvu Shooting
Okt 20, 2013
Simba vs Yanga
Saturday, October 12, 2013
Simba yaendelea kung'ang'ania kileleni, Yanga yalipa kisasi Kaitaba
Simba walioshinda jijini Dar |
![]() |
Yanga iliyotakata mjini Bukoba kwa kuilaza Kagera Sugar |
Simba ilipata ushindi wa bao 1-0 katika pambano kali lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam dhidi ya maafande wa Magereza, Prisons-Mbeya na kufikisha jumla ya pointi 18.
Kiti cha Simba kilikuwa hatarini siku ya leo iwapo kama ingeteleza na matokeo iliyopata watani zao wa jadi mjini Bukoba, baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji wao Kagera Sugar.
Mkude alifunga bao hilo katika dakika ya 61 na kuiokoa timu yake kugawana pointi na Prisons iliyoonyesha upinzani mkubwa katika pambano hilo.
Bao hilo ambalo ni la tatu kwa Mkude katika orodha ya wafungaji mabao, lilikuwa likusubiriwa kwa hamu na mashabiki wa Simba ambao dakika 45 za kwanza walikuwa wanyonge na hasa walipokuwa wakipata matokeo ya pambano la mjini Bukoba.
Kwa ushindi huo Simba imesalia kileleni na kufuatiwa na Yanga ambao walipata mabao yake kupitia kwa Mrisho Ngassa aliyefunga kwa kichwa dakika moja tu baada ya pambano hilo kuanza bao lilidumu hadi mapumziko.
Kipindi cha kilianza kwa wenyeji Kagera Sugar kusawazisha bao dakika mbili baada ya kuanza kwa kipindi hicho, lakini Yanga ilidhihirisha kuwa ilipania kuilipa kisasi na kufuta unyonge wake mbele ya Kagera kila wanapokutana Kaitaba kwa kuongeza bao la pili.
Mganda Hamis Kiiza 'Diego' alifunga bao hilo katika dakika ya 57, goli linalomfanya afikishe jumla ya mabao matatu mpaka sasa katika ligi ya msimu huu, ikiwa ni wiki moja kabla ya timu yake ya Yanga kukabiliana na Simba katika pambano la watani wa jadi litakalochezwa Okt. 20.
Ushindi huo wa Yanga umeifanya mabingwa watetezi hao kufikisha pointi 15, tatu nyuma ya Simba na iwapo itafanikiwa kushinda katika mechi yao ya Jumapili ijayo, huenda vijana hao wa Jangwani wakakikalia kiti cha uongozi baada ya kuenguliwa walipoyumba katika ligi hiyo.
Golden Bush, Pugu Veterani kuvaana kesho Kinesi
Ticotico (kushoto) katika moja ya mechi zao za maveterani |
WAKALI wa soka la maveterani jijini Dar es Salaam, Golden Bush Veterani kesho asubuhi inatarajiwa kuvaana na Pugu Veterani katika pambano la kukata na shoka la kirafiki litakalochezwa kwenye uwanja wa Kinesi, Ubungo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi wa Golden Bush inayoundwa na wakali za zamani wa Simba na Yanga, mechi hiyo ni ya kumaliza mzizi wa fitina baada ya tambo za muda mrefu, huku wakali hao wa soka la jiji wakiwatisha Pugu kwamba wajiandae kupokea kipigo kikali hiyo kesho.
Taarifa ya Golden Bush kupitia Msemaji na mlezi wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' inasomeka hivi:
Wadau,
Kutokana
na vipigo vya mfululizo kutoka kwa wapinzani wetu wakiwepo Pugu
Veterans, na tambo nyingi kutoka kwa wapinzani wetu hapa jijini, Golden
bush tumelazimika kuomba mechi ya kirafiki ya marudiano na Pugu
Veterans, game itapigwa uwanja wa Kinesi maarufu kama St James Park siku
ya jumapili asubuhi. Kwakutambua umuhimu ya game hii, uongozi wetu
umeitisha kikao cha dharula kesho baada ya mazoezi asubuhi ili kuweka
mikakati kabambe ya kurudisha heshima ya timu yetu ambayo mpaka sasa
inatambulika kama mabingwa wa jiji la Dar es Salaam. Timu yetu
imekamilika kabisa hakuna majeruhi hakuna mgonjwa hakuna mgogoro, uwanja
uko sawa kamati ya ufundi inamaalizia kazi yake kwa kushirikiana na
Walimu wetu. Tumejiwekea lengo la kufunga magoli mengi iwezekanavyo ili
kuvunja rekodi ya kufunga magoli.
Aidha
ningependa kutoa taarifa kwamba timu yetu imeimarika zaidi mara baada
ya Juma Kaseja, Said Swedi ,Mwarami Mohamed na Shadrack Nsajigwa
kurejea kwenye timu yetu. karibuni mje muone soka la hali ya juu sana
huku likihanikizwa na ufundi wa vijana wa zamani chini ya kocha wetu
Madaraka Selemani “Mzee wa kiminyio”
Baada ya game ya jumapili, timu itakuwa kwenye maandalizi ya mwisho kabisa kwenda kucheza mechi za kirafiki visiwani Zanzibar.
Asanteni kwa kunisikiliza.
Onesmo Waziri “Ticotico” Mchezaji Mwandamizi
Mimi ndiye niyeyaruhusu Rai, Mwananchi-Waziri Makalla
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mhe. Amos Makalla 'Mtu wa Watu' |
Katika habari iliyochapishwa jana na gazeti moja la kila siku (siyo NIPASHE), lilinukuu agizo la serikali likionya mmiliki wa Mtanzania kuzingatia ratiba ya kutoa gazeti lao kila siku ya Alhamisi, la Rai na mmiliki wa Mwananchi, kuacha kuchapisha gazeti lao katika mtandao kama amri ya kufungiwa ilivyoainishwa.
Hata hivyo, wakati kauli za Waziri na Naibu wake, Makala, zikitofautiana, gazeti la Mwananchi limemaliza adhabu yake jana ya kufungiwa kwa siku 14.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Naibu waziri Makala, alisema yeye ndiye aliruhusu Gazeti la Mwananchi kuendelea na utoaji wa taarifa/habari kwenye tovuti yake, pia Gazeti la Rai kutoka kila siku.
“Ninalazimika kutoa ufafanuzi kwa njia ya maandishi kutokana na kupigiwa simu nyingi na waandishi wa habari kuhusiana na tamko jipya la Mkurugenzi wa Habari – Maelezo, Assah Mwambene kuhoji uhalali wa Gazeti la Mwananchi kuwa online na Gazeti la Rai kutoka kila siku, badala ya mara moja kwa wiki (Alhamisi),” alisema.
Makala alisema Oktoba 4, alifanya mazungumzo na viongozi wa Kampuni ya Mwananchi Communication Ltd (MCL) na New Habari Corporation (2006) Ltd kwa upande mmoja na msajili wa magazeti kwa upande mwingine.
Alisema katika kikao hicho cha pamoja na viongozi wa Magazeti ya Mwananchi na Mtanzania waliomba waziri apitie upya adhabu iliyotolewa kwa magazeti hayo, ambapo yeye (Makala) aliwaambia kwamba mwenye mamlaka juu ya suala hilo ni waziri mwenye dhamana na masuala ya habari pekee.
Kuhusu ombi la Mwananchi kuwa online na Gazeti la Rai kutoka kila siku badala ya kutoka siku ya Alhamisi, alisema New Habari walieleza kuwa siku zilizopita waliwahi kuomba kwa maandishi kwamba gazeti la Rai litoke kila siku. Maelezo ya Naibu Msajili wa Magazeti katika kikao hicho yalikuwa kwamba, kulikuwa na tatizo la kiufundi katika kurejea maombi hayo na akakiri kuwa hakuna kinachozuia gazeti la Rai kutoka kila siku. Kutokana na maelezo hayo mimi niliridhia gazeti hilo sasa liruhusiwe kutoka kila siku.
Aidha, alisema kuhusu gazeti la Mwananchi kuwa online, Naibu Msajili alisema hakuna sheria yoyote inayoweza kuzuia gazeti hilo kuwa online ila aliwataka lisionekane gazeti zima kama lilivyo, pia wabadili nembo (Master Head) kwa kuweka ya MCL na siyo ya gazeti husika ambalo limefungiwa. “Pia baada ya maelezo hayo niliridhia gazeti hilo liwe mtandaoni kwa kuzingatia angalizo lililotolewa na Naibu Msajili wa Magazeti,” alisema.
Alisema hoja ya tatu ilikuwa ni ile ya Serikali kupitia Idara ya Habari - Maelezo kuwa na uhusiano mzuri na vyombo vya habari, ili kuepuka misuguano isiyo ya lazima, ambapo pendekezo hilo alilipokea na kuliwasilisha kwa Waziri wa Habari kwa hatua zaidi, likiwamo suala la kupitia upya adhabu na ushauri wa kujenga uhusiano na vyombo vya habari.
Aliongeza kuwa masuala ya gazeti la Mwananchi kuwa online na Rai kutoka kila siku, alilitolea uamuzi siku hiyo hiyo. “Na uamuzi ni kwamba niliwaruhusu baada ya kuridhika kwamba hakukuwa na ukiukwaji wa sheria yoyote uliofanywa na waombaji.”
“Nimeamua kuweka sawa jambo hili kutokana na taarifa ya Mkurugenzi wa Maelezo ambayo ninaamini kwamba kutolewa na kusambazwa kwake ni kukosekana kwa mawasiliano kati yake kwa upande mmoja na Mhe. Waziri, Naibu waziri na Naibu Msajili wa Magazeti kwa upande mwingine.
“Hivyo aliyeruhusu Gazeti la Mwananchi kuwa online na Rai ni mimi na ndiyo maana kuanzia tarehe 5/10/2013 Gazeti la Rai lilianza kuchapwa kila siku na kusambazwa, na Gazeti la Mwananchi likaanza kuwa mtandaoni kwa kuzingatia maelekezo ya Naibu Msajili wa Magazeti,” alisema katika taarifa hiyo.
CHANZO:
NIPASHE
Kivumbi cha FDL kuendelea wikiendi hii
KIVUMBI cha Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa makundi yote matatu kinatarajiwa kuendelea wikiendi hii ambapo kundi B litakuwa na mechi moja tu kati ya Lipuli na Mlale JKT itakayochezwa kesho (Oktoba 12 mwaka huu) katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa.
Transit Camp itakwaruzana na Tessema katika Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi wakati Polisi Dar itaumana na African Lyon kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam katika mechi za kundi A zitakazochezwa kesho (Oktoba 12 mwaka huu).
Mechi nyingine ya kundi hilo itachezwa keshokutwa (Oktoba 13 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam kwa kuzikutanisha Friends Rangers na Villa Squad.
Timu zote nane za kundi C zinashuka viwanjani kesho (Oktoba 12 mwaka huu) kusaka pointi tatu. Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Polisi Dodoma na JKT Kanembwa ya Kigoma.
Pamba na Mwadui zitacheza katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, Polisi Tabora itaikaribisha Toto Africans kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora wakati uga wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma utatumika kwa mechi kati ya Polisi Mara na Stand United ya Shinyanga.
Simba, Yanga vitani Ligi Kuu Tanzania Bara
* Yanga yaapa kisasi Kaitaba, Prisons kuishusha Simba kileleni?
Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inakamilisha raundi ya nane kesho (Oktoba 12 mwaka huu) kwa mechi tatu zitakazochezwa Dar es Salaam na Bukoba mkoani Kagera.
Simba ina fursa ya kuendelea kukamata usukani wa ligi hiyo iwapo itaishinda Tanzania Prisons ya Mbeya katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni. Tanzania Prisons inayofundishwa na Jumanne Chale inashika nafasi ya kumi na moja katika msimamo wa ligi hiyo.
Ili iendelee kupanda katika nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi hiyo iliyoanza Agosti 24 mwaka huu, Tanzania Prisons ambayo katika mechi yake iliyopita ugenini ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mgambo Shooting inalazimika kuifunga Simba.
Licha ya sare ya bao 1-1 katika mechi yake iliyopita dhidi ya Ruvu Shooting, Simba inayoongoza kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya Azam na Mbeya City matokeo mazuri katika mchezo huo ni muhimu kwao kama ilivyo kwa wapinzani wao Tanzania Prisons.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 ambapo tiketi zitauzwa uwanjani kwenye magari maalumu kuanzia saa 4 kamili asubuhi.
Mabingwa watetezi Yanga wao watakuwa mjini Bukoba kwenye Uwanja wa Kaitaba kuwakabili wenyeji Kagera Sugar wanaofundishwa na Mganda Jackson Mayanja akisaidiwa na Mrage Kabage.
Kagera ambayo inapishana na Yanga kwa tofauti ya pointi moja ilipoteza mechi iliyopita dhidi ya JKT Ruvu baada ya kulala kwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Azam Complex. Wakati Yanga ikiwa katika nafasi ya nne kwa pointi 12, Kagera Sugar ni ya sita kwa pointi kumi na moja.
Iwapo Kocha Ernst Brandts atawaongoza vijana wake wa Yanga kuibuka na ushindi katika mechi hiyo na Simba kufanya vibaya kwenye mechi dhidi ya Tanzania Prisons huenda akakamata uongozi wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 14.
Mwamuzi Zakaria Jacob wa Pwani ndiye atakayechezesha mechi kati ya Ashanti United na Coastal Union itakayopigwa Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.
Raundi ya tisa ya ligi hiyo inaanza keshokutwa Jumapili (Oktoba 13 mwaka huu) kwa mechi kati ya Ruvu Shooting na Rhino Rangers (Mabatini, Mlandizi), Mgambo Shooting na Mbeya City (Mkwakwani, Tanga), Azam na JKT Ruvu (Azam Complex, Dar es Salaam) na Mtibwa Sugar na Oljoro JKT (Manungu, Turiani).
Mechi zitakazooneshwa moja kwa moja (live) na Azam TV kupitia TBC1 wikiendi hii ni kati ya Simba na Tanzania Prisons itakayochezwa Jumamosi katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na ile kati ya Azam na JKT Ruvu itakayofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Azam Complex.
![]() |
Simba itakayokuwa Taifa kuilika Prisons Mbeya |
![]() |
Yanga watakaokuwepo Kagera ili kulipa kisasi kwa Kagera Sugar |
Kagera Sugar watakubali 'kufa' nyumbani Kaitaba? |
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inakamilisha raundi ya nane kesho (Oktoba 12 mwaka huu) kwa mechi tatu zitakazochezwa Dar es Salaam na Bukoba mkoani Kagera.
Simba ina fursa ya kuendelea kukamata usukani wa ligi hiyo iwapo itaishinda Tanzania Prisons ya Mbeya katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni. Tanzania Prisons inayofundishwa na Jumanne Chale inashika nafasi ya kumi na moja katika msimamo wa ligi hiyo.
Ili iendelee kupanda katika nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi hiyo iliyoanza Agosti 24 mwaka huu, Tanzania Prisons ambayo katika mechi yake iliyopita ugenini ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mgambo Shooting inalazimika kuifunga Simba.
Licha ya sare ya bao 1-1 katika mechi yake iliyopita dhidi ya Ruvu Shooting, Simba inayoongoza kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya Azam na Mbeya City matokeo mazuri katika mchezo huo ni muhimu kwao kama ilivyo kwa wapinzani wao Tanzania Prisons.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 ambapo tiketi zitauzwa uwanjani kwenye magari maalumu kuanzia saa 4 kamili asubuhi.
Mabingwa watetezi Yanga wao watakuwa mjini Bukoba kwenye Uwanja wa Kaitaba kuwakabili wenyeji Kagera Sugar wanaofundishwa na Mganda Jackson Mayanja akisaidiwa na Mrage Kabage.
Kagera ambayo inapishana na Yanga kwa tofauti ya pointi moja ilipoteza mechi iliyopita dhidi ya JKT Ruvu baada ya kulala kwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Azam Complex. Wakati Yanga ikiwa katika nafasi ya nne kwa pointi 12, Kagera Sugar ni ya sita kwa pointi kumi na moja.
Iwapo Kocha Ernst Brandts atawaongoza vijana wake wa Yanga kuibuka na ushindi katika mechi hiyo na Simba kufanya vibaya kwenye mechi dhidi ya Tanzania Prisons huenda akakamata uongozi wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 14.
Mwamuzi Zakaria Jacob wa Pwani ndiye atakayechezesha mechi kati ya Ashanti United na Coastal Union itakayopigwa Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.
Raundi ya tisa ya ligi hiyo inaanza keshokutwa Jumapili (Oktoba 13 mwaka huu) kwa mechi kati ya Ruvu Shooting na Rhino Rangers (Mabatini, Mlandizi), Mgambo Shooting na Mbeya City (Mkwakwani, Tanga), Azam na JKT Ruvu (Azam Complex, Dar es Salaam) na Mtibwa Sugar na Oljoro JKT (Manungu, Turiani).
Mechi zitakazooneshwa moja kwa moja (live) na Azam TV kupitia TBC1 wikiendi hii ni kati ya Simba na Tanzania Prisons itakayochezwa Jumamosi katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na ile kati ya Azam na JKT Ruvu itakayofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Azam Complex.
Nyalla wenzake wapeta TFF, washinda rufaa zao
KAMATI ya Rufani ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imewarejesha warufani wote watatu katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa Kamati mpya ya Utendaji ya TFF utakaofanyika Oktoba 27 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Samwel Nyalla, Ayubu Nyaulingo na Ayoub Nyenzi walikata rufani mbele ya Kamati hiyo inayoongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Bernard Luanda kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF kuwaondoa katika uchaguzi huo ambapo wote wanagombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji kuwakilisha kanda mbalimbali.
Akisoma uamuzi wao leo (Oktoba 11 mwaka huu) mbele ya Waandishi wa Habari kwenye ofisi za TFF, Jaji Luanda amesema baada ya kusikiliza hoja za Mrufani Nyalla walipitia Kanuni za Uchaguzi za TFF na kugundua yafuatayo;
Ibara ya 10(3) imeweka masharti makuu mawili ya ujazaji wa fomu za kugombea uongozi. Fomu hiyo ni lazima iwe na saini ya mgombea na ni lazima ithibitishwe na viongozi wa shirikisho.
Kamati imepitia Kanuni za Uchaguzi haijaona sehemu fomu hiyo ya uongozi imeambatanishwa ili kuifanya kuwa Kanuni ya Uchaguzi. Ni maoni ya Kamati kuwa ni vizuri fomu za kugombea zikawa ni sehemu ya Kanuni za Uchaguzi.
Kwa vile Kanuni za Uchaguzi za TFF za 2013 pia hazijaainisha nini adhabu kwa mgombea aliyekosea kujaza Fomu namba 1 ya kugombea uongozi, Kamati inaona itakuwa si haki kumnyima mgombea nafasi ya kushiriki katika uchaguzi kwa vile tu fomu yake haijajazwa vipengele vyote.
Nyalla aliondolewa kwenye uchaguzi na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa maelezo kuwa si mtu makini anayeweza kutekeleza majukumu yake kikamilifu baada ya kushindwa kujaza Fomu namba 1 kipengele cha 15 kinachohusu malengo ya mgombea uongozi.
Kwa upande wa Nyaulingo ambaye aliondolewa kwa kukosa uzoefu uliothibitika kulingana na Ibara ya 29(3) ya Katiba ya TFF na Kanuni ya 9(3) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF, Kamati ya Rufani imeamua ifuatavyo;
Kamati ya Rufani ya Uchaguzi imepokea sababu za rufani na imepata fursa ya kusikiliza hoja na maelezo kutoka kwa Mrufani juu ya sababu zake alizozitoa kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi.
Mrufani alifafanua historia yake katika masuala ya michezo kuanzia alipokuwa anasema Chuo Kikuu kuanzia 2005-2009 na pia ushiriki wake kama mchezaji wa Rukwa United iliyowahi kushiriki Ligi ya Mkoa wa Rukwa na ligi nyingine za kitaifa.
Kwa kusoma maana ya ‘Familia ya TFF’ iliyoko kwenye utangulizi wa Katiba ya TFF, pamoja na Ibara ya 29(3) na 29(6) ya Katiba hiyo, Kamati imejiridhisha kuwa Mrufani ana sifa za kugombea uongozi wa Shirikisho na amekidhi kigezo cha sifa za ugombea.
Ameshiriki kwenye mchezo wa mpira wa miguu kama mchezaji na mtawala, hivyo kutimiza kigezo kilichohitajika cha ushiriki katika uongozi na utawala wa mchezo wa mpira wa miguu kwa muda usiopungua miaka mitano.
Kwa kuzingatia hayo, Kamati ya Rufani ya Uchaguzi inaruhusu rufani ya Mrufani. Uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi umetenguliwa na Mrufani anapewa nafasi ya kushiriki katika uchaguzi.
Kuhusu Ayubu Nyenzi aliyeondolewa kwa kukosa uzoefu kwa mujibu wa Ibara ya 29(3) ya Katiba ya TFF na Kanuni ya 9(3) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF, na pia kushindwa kuthibitisha uraia wake mbele ya Kamati ya Uchaguzi, Kamati ya Rufani katika uamuzi wake imesema;
Imepokea sababu za rufani na imepata fursa ya kusikiliza hoja na maelezo kutoka kwa Mrufani juu ya sababu zake alizozitoa kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi.
Baada ya uchambuzi wa kina, Kamati imeona kuwa kulingana na maelezo yaliyotolewa na Mrufani na viambatanisho vilivyowasilishwa, Kamati haina shaka kuhusu uraia wake. Uthibitisho wa uraia unapaswa kufanywa kwa umakini na taasisi yenye mamlaka ya kiserikali kufanya hivyo.
Kamati pia imejiridhisha kupitia Fomu namba 1 iliyojazwa na kusainiwa na Mrufani kuwa kuanzia mwaka 2004 mpaka 2010, Nyenzi ameshika nyadhifa za utawala wa mpira wa miguu na hasa katika klabu ya Yanga, uzoefu unaomfanya kuwa na sifa ya kugombea nafasi ya uongozi katika TFF kulingana na Ibara ya 29(3) ikisomwa pamoja na Ibara ya 29(6).
Kwa kuzingatia hayo, Kamati ya Rufani ya Uchaguzi inaruhusu rufani ya Mrufani. Uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi umetenguliwa na Mrufani atashiriki katika uchaguzi wa TFF kwa nafasi anayogombea.
Wakati huo huo, Kamati ya Rufani ya Maadili ya TFF inakutana keshokutwa (Oktoba 13 mwaka huu), kufanyia mapitio (revision) ya uamuzi wa Kamati ya Maadili kwa waombaji uongozi wanane kama ilivyoombwa na Sekretarieti ili kutoa mwongozo wa utekelezaji wa uamuzi huo.
Samwel Nyalla, Ayubu Nyaulingo na Ayoub Nyenzi walikata rufani mbele ya Kamati hiyo inayoongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Bernard Luanda kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF kuwaondoa katika uchaguzi huo ambapo wote wanagombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji kuwakilisha kanda mbalimbali.
Akisoma uamuzi wao leo (Oktoba 11 mwaka huu) mbele ya Waandishi wa Habari kwenye ofisi za TFF, Jaji Luanda amesema baada ya kusikiliza hoja za Mrufani Nyalla walipitia Kanuni za Uchaguzi za TFF na kugundua yafuatayo;
Ibara ya 10(3) imeweka masharti makuu mawili ya ujazaji wa fomu za kugombea uongozi. Fomu hiyo ni lazima iwe na saini ya mgombea na ni lazima ithibitishwe na viongozi wa shirikisho.
Kamati imepitia Kanuni za Uchaguzi haijaona sehemu fomu hiyo ya uongozi imeambatanishwa ili kuifanya kuwa Kanuni ya Uchaguzi. Ni maoni ya Kamati kuwa ni vizuri fomu za kugombea zikawa ni sehemu ya Kanuni za Uchaguzi.
Kwa vile Kanuni za Uchaguzi za TFF za 2013 pia hazijaainisha nini adhabu kwa mgombea aliyekosea kujaza Fomu namba 1 ya kugombea uongozi, Kamati inaona itakuwa si haki kumnyima mgombea nafasi ya kushiriki katika uchaguzi kwa vile tu fomu yake haijajazwa vipengele vyote.
Nyalla aliondolewa kwenye uchaguzi na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa maelezo kuwa si mtu makini anayeweza kutekeleza majukumu yake kikamilifu baada ya kushindwa kujaza Fomu namba 1 kipengele cha 15 kinachohusu malengo ya mgombea uongozi.
Kwa upande wa Nyaulingo ambaye aliondolewa kwa kukosa uzoefu uliothibitika kulingana na Ibara ya 29(3) ya Katiba ya TFF na Kanuni ya 9(3) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF, Kamati ya Rufani imeamua ifuatavyo;
Kamati ya Rufani ya Uchaguzi imepokea sababu za rufani na imepata fursa ya kusikiliza hoja na maelezo kutoka kwa Mrufani juu ya sababu zake alizozitoa kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi.
Mrufani alifafanua historia yake katika masuala ya michezo kuanzia alipokuwa anasema Chuo Kikuu kuanzia 2005-2009 na pia ushiriki wake kama mchezaji wa Rukwa United iliyowahi kushiriki Ligi ya Mkoa wa Rukwa na ligi nyingine za kitaifa.
Kwa kusoma maana ya ‘Familia ya TFF’ iliyoko kwenye utangulizi wa Katiba ya TFF, pamoja na Ibara ya 29(3) na 29(6) ya Katiba hiyo, Kamati imejiridhisha kuwa Mrufani ana sifa za kugombea uongozi wa Shirikisho na amekidhi kigezo cha sifa za ugombea.
Ameshiriki kwenye mchezo wa mpira wa miguu kama mchezaji na mtawala, hivyo kutimiza kigezo kilichohitajika cha ushiriki katika uongozi na utawala wa mchezo wa mpira wa miguu kwa muda usiopungua miaka mitano.
Kwa kuzingatia hayo, Kamati ya Rufani ya Uchaguzi inaruhusu rufani ya Mrufani. Uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi umetenguliwa na Mrufani anapewa nafasi ya kushiriki katika uchaguzi.
Kuhusu Ayubu Nyenzi aliyeondolewa kwa kukosa uzoefu kwa mujibu wa Ibara ya 29(3) ya Katiba ya TFF na Kanuni ya 9(3) ya Kanuni za Uchaguzi za TFF, na pia kushindwa kuthibitisha uraia wake mbele ya Kamati ya Uchaguzi, Kamati ya Rufani katika uamuzi wake imesema;
Imepokea sababu za rufani na imepata fursa ya kusikiliza hoja na maelezo kutoka kwa Mrufani juu ya sababu zake alizozitoa kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi.
Baada ya uchambuzi wa kina, Kamati imeona kuwa kulingana na maelezo yaliyotolewa na Mrufani na viambatanisho vilivyowasilishwa, Kamati haina shaka kuhusu uraia wake. Uthibitisho wa uraia unapaswa kufanywa kwa umakini na taasisi yenye mamlaka ya kiserikali kufanya hivyo.
Kamati pia imejiridhisha kupitia Fomu namba 1 iliyojazwa na kusainiwa na Mrufani kuwa kuanzia mwaka 2004 mpaka 2010, Nyenzi ameshika nyadhifa za utawala wa mpira wa miguu na hasa katika klabu ya Yanga, uzoefu unaomfanya kuwa na sifa ya kugombea nafasi ya uongozi katika TFF kulingana na Ibara ya 29(3) ikisomwa pamoja na Ibara ya 29(6).
Kwa kuzingatia hayo, Kamati ya Rufani ya Uchaguzi inaruhusu rufani ya Mrufani. Uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi umetenguliwa na Mrufani atashiriki katika uchaguzi wa TFF kwa nafasi anayogombea.
Wakati huo huo, Kamati ya Rufani ya Maadili ya TFF inakutana keshokutwa (Oktoba 13 mwaka huu), kufanyia mapitio (revision) ya uamuzi wa Kamati ya Maadili kwa waombaji uongozi wanane kama ilivyoombwa na Sekretarieti ili kutoa mwongozo wa utekelezaji wa uamuzi huo.
Wanahabari wakumbushwa kuomba vitambulisho WC 2014
![]() |
Mwisho wa kupokea maombi hayo itakuwa Januari 31 mwakani, hivyo kwa waandishi wanaotaka kupata vitambulisho hivyo ni lazima wawe na akaunti ya FIFA Media Channel pamoja na utambulisho wa mtumiaji wa akaunti hiyo (user ID).
Kwa mujibu wa FIFA, kila nchi itapewa idadi maalumu ya nafasi kwa waandishi (waandishi wa kawaida pamoja na wapiga picha) baada ya mechi za mchujo za Kombe la Dunia kumalizika ambapo vigezo mbalimbali vitazingatiwa ikiwemo nchi kufuzu kwa fainali hizo.
Hivyo, nchi ambayo itakuwa imefuzu itakuwa na nafasi zaidi kulinganisha na zile ambazo hazitakuwa na timu katika fainali hizo za Brazil.
Mgawanyo wa nafasi zitakazotolewa kwa Tanzania utapangwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kulingana na maombi yatakayokuwa yamewasilishwa FIFA kupitia FIFA Media Channel.
TFF inatoa mwito kwa waandishi wa habari za mpira wa miguu ambao hawana akaunti FIFA Media Channel kuhakikisha wanakuwa nayo mapema ili waweze kutuma maombi yao.
Filama ya Dasmila karibuni kutoka hadharani
FILAMU mpya ya Dasmila inatarajia kuingia sokoni mwishoni mwa mwezi huu. Akizungumza jijini Dar, Mkurugenzi wa DJ Marketing & Promotion ambao ndio wasambazaji wa kazi hiyo, Haulle
Daniel amesema kazi hiyo ime kamilika kwa asilimia zote hivyo wapenzi
wa filamu wakae mkao wa kula kwani imewashirikisha wasanii wengi akiwemo
Shamsa Frod,Jack Pentzel, Elias Mkali, Shaban Dicosta na wasanii
wengine wanaotamba katika anga za filamu nchini. Filamu hiyo ya mapenzi ambayo kuna mambo mbalimbali ya kuelimisha jamii ya kitanzania ambapo Dasmila
aliyeuawa kipindi cha nyuma kidogo, arudi tena kama mzimu, na mengi
yanatokea. Fuatilia.. Familia, vichekesho na vimbwanga, mapenzi, kukosa
uaminifu, visa na mikasa kibao ambayo
yatapatikana katika filamu hiyo, ambayo imetengenezwa kwa ubora wa ali
ya juu na itakayokuwa ikisambazwa na kampuni ya kizalendo ya DJ
Marketing ya jijini Dar es salaam.
Friday, October 11, 2013
Kocha Wailes ampaisha Gareth Bale
![]() |
bale akiwa amebebwa na Ronaldo |
Alisema: "Sitaki kuingia katika mijadala kuhusu thamani yake, lakini ninaloweza kusema sasa ni kwamba Bale hayuko mbali sana na matawi aliyopo Cristiano Ronaldo na Messi."
Toshack pia alisema winga huyo wa zamani wa Tottenham hahusiki kwa lolote katika kiwango kikubwa cha pesa kilicholipwa ili kumhamishia Real Madrid, akisema: "Mchezaji si wa kulaumiwa kwa ada ya euro milioni 100 iliyolipwa ili kumsajili. Kama klabu mbili husika zimeafikiana bei hiyo, hayo ni makosa yao."
Pia aliwataka watu wawe wavumilivu kwa nyota huyo ili azoee mazingira mapya. "Alikuwa na bahati mbaya hakujifua katika kipindi cha kujiandaa na msimu, kutokatana na mvutano uliokuwapo baina ya Tottenham na Real Madrid, lakini Bale ni mchezaji mzuri. Hakuna sababu yoyote ya kutilia shaka uwezo wa Gareth Bale, nawahakikishia," alisema kwa kujiamini.
Kocha huyo wa Wales pia alizungumzia hali ya vipaji vinavyoibukia Real. "Kwa mfano watu kama Illarramendi, Isco au wachezaji yosso wa El Castilla (Real Madrid B), kama wakiangalia benchi la Ancelotti na Zidane linaleta matumaini. Kwa sasa ni wakati mgumu kwao kwa sababu Barcelona wanafanya vyema, huku Madrid wakiwa nyuma yao kwenye msimamo, lakini wanahitaji kupewa muda,” alisema kocha huyo Wales.
Thursday, October 10, 2013
Eid El Hajj kusherehekewa J'5 BAKWATA watoa taarifa
![]() |
![]() |
HATA hivyo wakati BAKWATA wakitoa taarifa hiyo ni kwamba kwa wale wanaofuata mwezi muandamo wa kimataifa ni kwamba Waislam watafunga Arafah kuwaunga mkono mahujaji siku ya Jumatatu na kuisherehekea sikukuu Jumanne itakayokuwa Oktoba 15, yaani siku moja kabla ya ile iliyotangazwa na BAKWATA.
Funga ya Arafah ni muhimu kwa waumini wa kiislam ambao hawakubahatika kwenda Hijja kwani kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (SAW) kufunga Swawm siku ya
'Arafah kwa sababu ni kufutiwa madhambi ya miaka miwili; mwaka uliopita
na baada yake (Hadiyth katika Swahiyh Muslim).
Hivyo MICHARAZO inawakumbusha waumini wa dini hiyo kutoisahau swaumu hiyo, japo tumesisitizwa kufunga tangu Mfungo tatu unapoingia katika makundi ya mwanzoni, lakini kwa wale walioshindwa kutekeleza ibada hiyo shime wasiiache Arafah kwa manufaa yao ya kidunia na Ahera Inshallah
Minziro:Msituchonganishe Yanga
Minziro alitoa kauli hiyo alipoigiwa simu na MICHARAZO kujua msafara mzima wa timu yao kuelekea Bukoba kuumana na Kagera Sugar siku ya Jumamosi na iwapo kama walimjumuisha beki wa kati Kelvin Yondani aliyeripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba alikirofichana na kocha mkuu, Ernie Brandts kiasi cha kuvua jezi na kutupa chini kisha kususia mazoezi.
Kocha huyo, nyota wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, alisema hakuna tukio lolote lililotokea baina ya Yondani na kocha mkuu na ndiyo maana mchezaji huyo yupo kwenye msafara wa wachezaji 21 kwa ajili ya kuivaa Kagera Sugar kwenye uwanja wa Kaitaba.
"Ndugu yangu huyo aliyekuambia kwamba Yondani kagombana na kocha ana yake, na ningependa kuwaambia wazi Yanga hatutaki mtuchonganishe, tupo shwari na hivi sasa tumetua Bukoba salama," alisema Minziro.
Alisema Yondani ni miongoni mwa wachezaji 21 wa Yanga walioenda Bukoba kuhakikish Yanga itaibuka na ushindi dhidi ya wenyeji wao ambao anakiri huwa wasumbufu kwenye dimba lao la nyumbani.
"Msitugombanishe kabisa, tupo shwari tayari kwa kuisulubu Kagera, tumekuja kusaka ushindi huku hivyo tuacheni," alisisitiza Minziro.
Alidokeza kuwa kwa maandalizi waliyofanya dhidi ya mchezo huo ana imani kubwa ya kuibuka na ushindi Jumamosi licha ya kutarajia upinzani mkali wa wenyeji wao hao walkiowatungua katika mechi kama hiyo ya msimu uliopita iliyochezwa Oktoba 8, 2012 ambapo Yanga walilala kwa bao 1-0.
P Square kutua Bongo na wasanii 13
![]() |
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa,(kulia) akisisitiza jambo katika mkutano wake leo na wanahabari kuhusu ujio wa P Square. Kushoto ni Mtangazaji, Hillary Daud 'Zembwela'. |
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hoteli ya Hyatt jijini Dar, mtangazaji wa kituo hicho, Hillary Daudi maarufu kama Zembwela alisema show hiyo itakuwa ya aina yake.
“Wote tunatambua namna kundi hili linavyofanya vizuri ndani na nje ya bara la Afrika, licha ya kutoa burudani kwa mashabiki, pia litatoa fursa kwa wasanii wa ndani kujifunza kutoka kwa wasanii hawa vijana ambao wamepata mafanikio makubwa kutokana na kazi yao ya muziki,” alisema.
“Hii itakuwa ni fursa ya kipekee kwa wasanii wetu wa Bongo kujifunza kwa kuangalia wenzao wanavyofanya kazi.”Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa, alisema Vodacom inafurahi kuendelea kuwa sehemu ya kutoa burudani kwa jamii ya Watanzania na safari hii ikiwaleta wasanii ambao ni kipenzi cha Watanzania wengi.
“Siku zote Vodacom imeendelea kuwa chaguo la kwanza kwa Watanzania, kuanzia katika burudani na hata huduma nyingine za mawasiliano na kijamii. Tunaendelea kuunga jitihada za kuwainua wasanii wetu wa ndani kwa kuwapatia fursa ya kujifunza kutoka kwa wasanii wenzao wakubwa waliofanyikiwa kufanya kazi zao Kimataifa,” alisema.
“Kwa wateja wa Vodacom ambao pia ni mashabiki wa wasanii hawa ambao wanatamba na kibao chao kitamu cha ‘Personally’ kwa sasa wanayo fursa ya kufurahia nyimbo hizi kwa kuzidownload au kuzitumia kama miito ya simu (RBT) na kuweza kujishindia tiketi za onesho hilo. Natoa wito kwa Watanzania wapenda burudani kutembelea ukurasa wetu wa Facebook na Twitter kwa taarifa zaidi na kujua namna ya kujishindia tiketi za onesho hilo.”
Henry, Redondo, Baba Ubaya kuwakosa Prisons
Henry Joseph |
Redondo |
NYOTA watatu wa Simba, Issa Rashid 'Baba Ubaya', Henry Joseph na Ramadhani Chombo 'Redondo' wamefahamika hawatakuwepo kwenye pambano kati ya timu yao na Prisons-Mbeya siku ya Jumamosi.
Baba Ubaya atalikosa pambano hilo kwa sababu ya kuwa majeruhi sawa na ilivyo kwa kiungo mkabaji Abdallah Seseme na beki wa pembeni Miraj Adam waliovishwa POP.
Henry na Redondo watakosekana katika mechi hiyo kutokana na kuenguliwa kwenye kambi ya timu hiyo iliyopo Bamba Beach, Kigamboni.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga ni kwamba klabu yao imekuwa na utaratibu wa kuingia kambini kila wanapokabiliwa na mechi na wachezaji wanaofanya vyema kwenye mechi iliyopita na mazoezini ndiyo hujumuishwa kambini kutokana na mapendekezo ya makocha.
Kamwaga alisema hivyo kwa mtazamo wa makocha wao, Henry na Redondo hawakuwaridhisha na ndiyo maana wameungana na makinda wengine waliosajiliwa katika kikosi hicho kutoitwa kambini.
"Huu ni utaratibu wa kawaida na umekuwa ukitumiwa tangu alipokuwepo kocha Patrick Liewig, huwa nasema Simba ya sasa ni 'Simba-LUKU', yaani kadri unavyonunua umeme ndivyo utakavyoutumia na wachezaji kadri wanavyofanya vyema ndivyo wanavyopimwa na makocha," alisema.
Kamwaga alisema hajaelewa ni kwa nini baadhi ya vyombo vya habari vimeliona tukio la kutoitwa kambini kwa akina Redondo na Henry kuwa kitu cha ajabu wakati ni utaratibu uliopo siku zote Simba.
"Klabu imesajili wachezaji 36 wakiwamo wale wa U20, na kambini huingia wachezaji 25 hasa wanaofanya vyema na kushawishi makocha, hivyo kuachwa kwa akina Henry na Redondo sidhani kama ni issue kubwa wakati msimu uliopita tulikuwa tunaingia kambini bila akina Boban, Kazimoto na watu hawakusema lolote," alisema Kamwaga.
Simba ina kibarua kigumu mbele ya Prisons ambayo imeonyesha kuzinduka hivi sasa ili kuweza kulinda nafasi yao kileleni kwani tayari inapumuliwa na timu za Azam na Mbeya City na iwapo itateleza na Yanga kushinda Kagera siku ya Jumamosi inaweza kuwaengua katika nafasi hiyo.
Mechi nyingine kwa wikiendi hii ni zile zitakazochezwa Jumapili kwa Ashanti kuvaana na Coastal Union kenye uwanja wa Chamazi, Ruvu Shooting kuvaana na Rhino Rangers uwanja wa Mabatini-Mlandizi, Mgambo JKT kujiuliza kwa Mbeya City jijini Tanga, Azam kuwaalika JKT Ruvu kwenye uwanja wa Taifa wakati Mtibvwa itapepetana na Oljoro JKT kwenye mashamba ya Miwa ya Manungu Turiani Morogoro.
Kibadeni kupasua la rohoni kesho Msimbazi
![]() |
Kocha wa Simba Abdallah Kibadeni akiwa kwenye mazoezi ya timu hiyo |
Akizungumza na MICHARAZO, Kibadeni alisema amelazimika kuitisha mkutano huo kutokana na baadhi ya magazeti kuripoti taarifa 'mbaya' dhidi ya kambi yake na benchi nzima la Simba kitu alichodai kinachafua taswira ya Simba na kuleta sintofahamu miongoni mwa wanachama na mashabiki wao.
Kibadeni aliyeichukua timu hiyo baada ya Mfaransa Patric Liewig kutimuliwa alisema mkutano huo utafanyika majira ya saa 5 asubuhi ya kesho kwenye makao makuu ya klabu hiyo mtaa wa Msimbazi.
"Kuna baadhi ya wanahabari wamekuwa wakituchonganisha Simba, hivyo nimeitisha mkutano kesho nizungumze kuweka mambo sawa, kadhalika kuelezea maandalizi ya jumla dhidi ya pambano leo na Prisons," alisema Kibadeni maarufu kama King Mputa.
Kibadeni aliongeza kuwa, kuanza sasa wanahabari watakaotaka kujua chochote kuhusu Simba ni lazima wapate taarifa hizo kwa Msemaji wa Klabu, Ezekiel Kamwaga hata yale ya ufundi ambapo atakuwa anawauliza benchi la ufundi na kutoa majibu kwa wanahabari ili kuhofia kuivuruga Simba inayoongoza Ligi Kuu kwa sasa ikiwa na pointi 15.
Naye Msemaji wa Simba, Kamwaga alithibitisha kuwepo kwa mkutano huo wa kesho, akidai kocha wao hajafurahia na baadhi ya taarifa zinazoripotiwa zinazoonekana kama zina lengo la kuivuruga timu yao.
Hatimaye Mwananchi lamaliza kifungo kuanza kutoka tena kesho
GAZETI LA MWANANCHI LATOKA KIFUNGONI
Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications limited(MCL)Tido Mhando akizungumza na waandishi wa habari jijini kuhusu kuanza uchapishaji wa gazeti la Mwananchi kuanzia Oktoba 11, lililokuwa limefungiwa kwa wiki mbili. Kulia ni Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, Denis Msacky na Meneja Masoko wa Kampuni hiyo,Bernard Mukasa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications limited(MCL)Tido Mhando akizungumza na waandishi wa habari jijini kuhusu kuanza uchapishaji wa gazeti la Mwananchi kuanzia Oktoba 11, lililokuwa limefungiwa kwa wiki mbili. Kulia ni Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, Denis Msacky na Meneja Masoko wa Kampuni hiyo,Bernard Mukasa.
Wednesday, October 9, 2013
Diamond, Wema Sepetu, kitu na box
BAADA YA kuzikanusha taarifa kwamba amerudiana na zilipendwa wake, Wema Sepetu imefahamika wazi kwamba Diamond Platnumz sasa ni kitu na box na mlimbwende huyo.
aada ya habari kuenea kuwa Diamond PLatnumz amerudiana na Awali kulikuwa na taarifa wawili hao wamerudiana walipokuwa Malaysia Diamond alipoenda kutumbuiza na Wema kwa shughuli zake binafsi, lakini msanii huyo wa muziki wa kizazi kipya alikanusha.
Hata hivyo picha zilizonaswa zimewaonyesha wawili hao walikuwa wakiuhadaa umma kwani hakuna ubishi ni ng'ari ng'ari mwanzo mwisho.


Baadhi ya picha hizo, moja inawaonesha Diamond na Wema wakiwa wamevaa mapajama (nguo za kulalia) sehemu kama hotelini hivi na nyingine ikimuonesha Diamond akim-kiss Wema wakiwa kitaa. Lakini Diamond ni real boyfriend wa Penny
Nini nitakachofuata...TUSUBIRI!
BaabKubwa
aada ya habari kuenea kuwa Diamond PLatnumz amerudiana na Awali kulikuwa na taarifa wawili hao wamerudiana walipokuwa Malaysia Diamond alipoenda kutumbuiza na Wema kwa shughuli zake binafsi, lakini msanii huyo wa muziki wa kizazi kipya alikanusha.
Hata hivyo picha zilizonaswa zimewaonyesha wawili hao walikuwa wakiuhadaa umma kwani hakuna ubishi ni ng'ari ng'ari mwanzo mwisho.


Baadhi ya picha hizo, moja inawaonesha Diamond na Wema wakiwa wamevaa mapajama (nguo za kulalia) sehemu kama hotelini hivi na nyingine ikimuonesha Diamond akim-kiss Wema wakiwa kitaa. Lakini Diamond ni real boyfriend wa Penny
Nini nitakachofuata...TUSUBIRI!
BaabKubwa
Mbeya City yazidi kupepea, Azam, Mtibwa Sugar wazinduka
![]() |
Mbeya City |
WAKATI Azam ikizinduka na kuondoka na 'mdudu' wa sare baada ya kuitungua Mgambo JKT mabao 2-0, wageni wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Mbeya City ya jijini Mbeya imeendelea kutakata baada ya kuisasambua Rhino Rangers nyumbani kwao mjini Tabora kwa kuilaza mabao 3-1.
Ushindi wa timu hizo mbili zimezifanya ziisogelee Simba kwa kufikisha pointi 14, moja pungufu na zile ilizonazo vinara hao ambao leo hawakushuka dimbani.
Azam ilipata ushindi huo kwenye uwanja wa Chamazi na shukrani zikienda kwa kinda Faridi Mussa Maliki na Kipre Tchetche na kuipeleka Azam hadi nafasi ya pili mbele ya Mbeya City wakizidi kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Katika mechi nyingine, Ruvu Shooting imetoshana nguvu dhidi ya maafande wenzao wa Oljoro JKT baada ya kutoka sare ya mabao 2-2, mabao ya timu hizo yakifungwa na Elias Maguri wa Ruvu na Fikiri Mohammed wa Oljoro waliyofunga kila mmoja mawili.
Nao mabingwa wa zamani wa Tanzania, Mtibwa Sugar imezinduka nyumbani kwao Manungu Morogoro baada ya kuwatungua JKT Ruvu mabao 2-1 na kujivuta hadi nafasi ya tisa.
Mabao mawili ya Juma Luizio yalitosha kuibeba Mtibwa ambao mwishoni mwa wiki walinyanyaswa na Yanga kwa kulazwa mabao 2-0, na mkongwe Salum Machaku akiifungia JKT bao pekee la kufutia machozi.
Mfanyabiashara mwingine amwagiwa Tindikali, safari hii Arusha

MFANYABIASHARA mkazi wa Sakina jijini Arusha, Japhet Minja anadaiwa kumwagiwa kitu kinachosadikiwa kuwa ni tindikali na watu wasiofahamika na kuachwa na majeraha usoni na mikononi.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Arusha zinasema kuwa Minja alikumbwa na tukio hilo eneo la Shamsi Kata ya Elarai baada ya kumwagiwa kimiminika hicho na kuachwa na maumivu makali.
Akizungumza katika hospital ya Seriani alikola wa, Minja ambae ni mfanyabiashara adai alisimamishwa na watu waliomtaka kuongozana nao kwa ajili ya masuala ya kibiashara na ghafla wakiwa njiani ghafla alizuiwa na watu hao waliofunga njia na kumdhuru.Daktari wa zamu aliyempokea mgonjwa huyo Godbless Masawe amesema walimpokea
mgonjwa huyo jana asubuhi akiwa na fahamu lakini baadae hali ilibadilika na
kulazimika kumpeleka katika chumba cha wagonjwa mahututi na kwa sasa Minja anaendela vyema kwa sasa.
Yaillah Toba, Ajali nyingine tena yahusisha magari matatu
GA
Lori
la Mizigo likiwa limeacha njia leo, baada ya kugongana na basi katika
eneo la Kabuku mkoani Tanga na kuyahusisha magari matatu katika ajali
hiyo. (Picha na Francis Dande)
Askari wa usalama barabara wakiwa katika eneo la tukio.
Baadhi ya watu wakishuhudia ajali iliyoyakutanisha malori mawili pamoja na basi la abiria lenye namba za usajili T 158 BXG, iliyotokea leo katika eneo la Kabuku, mkoani TangaUchaguzi Bodi ya Ligi wapigwa dochi, Rufaa za wagoimbea TFF kupitiwa kesho
Na Boniface Wambura
UCHAGUZI wa viongozi wa Bodi ya Ligi Tanzania (TPL Board) sasa utafanyika Oktoba 25 mwaka huu badala ya Oktoba 18 mwaka huu.
Kamati
ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imesogeza
mbele uchaguzi huo kutokana na maombi ya Kamati ya Ligi kwa vile baadhi
ya wajumbe wa Baraza la Bodi hiyo kuwa vilevile wajumbe wa Mkutano Mkuu
wa TFF.
TFF
itafanya Mkutano Mkuu wake Oktoba 26 mwaka huu ambao utakuwa na ajenda
za kawaida kama zilivyoainishwa katika Katiba yake wakati ajenda ya
uchaguzi itakuwa Oktoba 27 mwaka huu.
Wagombea
uongozi TPL Board ni Hamad Yahya Juma anayewania nafasi ya Mwenyekiti
wakati Makamu Mwenyekiti ni Said Muhammad Abeid. Wanaowania nafasi za
ujumbe katika Kamati ya Uongozi ni Kazimoto Miraji Muzo na Omar Khatib
Mwindadi.
Kamati
ya Uchaguzi ya TFF chini ya Mwenyekiti wake Hamidu Mbwezeleni
inatarajia wakati wowote kutangaza tarehe ya kuanza kampeni kwa wagombea
katika uchaguzi huo. Baraza la Bodi linaundwa na wajumbe 38 ambao ni
wenyeviti 14 wa klabu za Ligi Kuu na wenyeviti 24 wa klabu za Daraja la
Kwanza.
Wakati huo huo Kamati
ya Rufani ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
inayoongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Bernard Luanda
itakutana keshokutwa (Oktoba 10 mwaka huu) kusikiliza rufani
zilizowasilishwa mbele yake.
Waombaji
uongozi watatu wamekata rufani katika Kamati ya Jaji Luanda wakipinga
kutopitishwa kugombea katika uchaguzi wa TFF, uamuzi uliofanywa na
Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa ajili ya uchaguzi huo utakaofanyika Oktoba
27 mwaka huu.
Warufani
ni Samwel Nyalla aliyeondolewa kugombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji
kupitia Kanda namba 2 ya mikoa ya Mara na Mwanza kwa kutojaza kikamilifu
fomu namba 1 ya maombi ya kugombea uongozi TFF kwa kutoonesha malengo
yake.
Ayoub
Nyaulingo yeye anapinga kuondolewa kugombea ujumbe wa Kamati ya
Utendaji kupitia Kanda namba 6 (Katavi na Rukwa) kwa kutokuwa na uzoefu
uliothibitika wa miaka mitano katika uongozi wa mpira wa miguu.
Naye
Ayoub Nyenzi amekata rufani kupinga kuondolewa kugombea ujumbe wa
Kamati ya Utendaji kuwakilisha Kanda namba 7 (Iringa na Mbeya) kwa
kushindwa kuthibitisha uraia wake.
Subscribe to:
Posts (Atom)