STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 15, 2013

Ronaldo asaini mkataba mpya Madrid kulipwa donge nono kuliko Messi

 
KLABU ya Real Madrid imethibitisha kumalizana na nyota wao kutoka Ureno, Cristiano Ronaldo kwa kumsainisha mkataba mpya wa miaka mitano wa kuitumikia klabu hiyo.
Rais wa Madrid, Florentino Perez amethibitisha kuwa, Ronaldo ameongeza mkataba huo ambapo sasa atakuwa akilipwa mshahara wa euro mil. 17 kila mwaka.
Mshahara huo utamfanya Mreno huyo aliyewahi kutamba na Manchester United amzidi nyota wa dunia Lionel Messi wa Barca kwa euro mil. 1 na kiwango anacholipwa na klabu yake.
Kusaini kwa nyota huyo kumezima uvumi kwamba Ronaldo alikuwa njiani kutaka kuihama klabu hiyo ili kurejea England kukipiga Manchester iliyokuwa ikitajwa kutaka kumrejesha.

Unakikumbuka kikosi hiki? Kama ndiyo tueleze ni timu gani na kama vipi tupia majina ya wanaounda timu hii


Balotelli aiokoa Milan na kipigo cha ugenini

Mario Balotelli akishangilia bao

STRAIKA Mario Balotelli jana aliiokoa timu yake ya AC Milan isiaibike ugenini baada ya kufunga bao dakika za nyongeza na kuipa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Torino katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Italia Seria A.
Balotelli aliyetoka kuipeleka nchi yake kwenye michuano ya Fainali za Kombe la Dunia za mwakani, alifunga bao hilo kwa mkwaju wa penati dakika ya 90+6 na kuiepushia aibu Milan walioonekana kulala 2-1.
Kabla ya hapo Milan ilijipatia bao la kufutia machozi kupitia kwa Sulley Muntari baada ya wenyeji kutangulia kupata mabao mawili yaliyofungwa na D'Ambrosio na Cerci.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo mabingwa watetezi, Juventus wakiwa ugenini mjini Milan dhidi yasa Inter Milan waliambulia sare ya bao 1-1, huku Napoli ikipata ushindi wa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Atalanta, huku Fiorentina nayo ikilazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Cagliari.

Gareth Bale aanza na bao Real Madrid ikipata sare ugenini la liga

bale bale bale bale
NYOTA mpya wa Real Madrid na mchezaji ghali kuliko wote duniani, winga Gareth Bale usiku wa kuamkia leo alianza makeke yake katika klabu yake kwa kuifungia moja ya mabao yaliyoisaidia vinara hao wa Hispania wasiumbuke ugenini walipotoka sare ya 2-2 na Villareal.
Hiyo ilikuwa mechi ya kwanza kwa mchezaji huyo wa zamani wa Tottenham Hotspur na alionyesha uwezo mkubwa, akifunga bao hilo la kusawazisha baada ya wenyeji kuwatangulia Madrid kwa bao la Cani na kufanya hadi mapumziko timu hizo ziwe nguvu sawa ya bao 1-1.
Kipindi cha pili Cristiano Ronaldo aliiongezea Madrid bao ambalo hata hivuo lilikuja kurejeshwa na wenyeji kupitia kwa Giovani Dos Santos.
Katika mechi iliyochezwa mapema leo, Espanol ikiwa ugenini imeizabua Granada kwa bao 1-0 lilitupiwa kambani na Lanzarote.
Matokeo ya mechi nyingine zilizochezwa jana katika ligi hiyo maarufu kama La Liga, mabingwa watetezi Barcelona ikiwa nyumbani ilishinda mabao 3-2 dhidi ya Sevilla, shukrani ya mabao ya Dani Alves , Lionel Messi na Alexis Sanchez.
Wageni mabao yao yalitupiwa kimiani na Coke na Ivan Rakitic. Nao Atletico Madrid walipata ushindi wao wa nne mfululizo kwa kuwalaza Almeria mabao 4-2 na kuwaweka kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo wakati Levante walilazimishwa suluhu na Real Sociaded.

Warembo wa Miss Tanzania waitembelea DTL

Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' David Mgwassa akizungumza na waandishi wa habari baada ya warembo wanaowania taji la Miss Tanzania kufanya zihara katika Kampuni hiyo mwishoni juzi ambayo imedhamini mashindano hayo kupitia kinywaji chake cha Zanzi  .Picha na mpiga picha wetu
Baahi ya Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakichukua chakula wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' juzi   ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
Baahi ya Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakiwa kwenye pozi wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi'  juzi  Konyagi  ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
Meneja masoko  ya ndani na nje wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' ,Vimal Vaghmaria kushoto na meneja masoko wa ksampuni hiyo Joseph Chibhee wakigonganisha grass na Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania walipotembelea kiwandani  juzi Konyagi ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
Meneja masoko  ya ndani na nje wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' ,Vimal Vaghmariakatikati akiwa katika pozi na baadi ya washiriki wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania walipotembelea kiwandani  juzi konyagi  ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
 Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakiwa kwenye pozi wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi'  juzi konyagi ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu

Baahi ya Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakipata chakula wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi'    ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
NA MWANDISHI WETU

WAREMBO wanaowania taji la Miss Tanzania wametakiwa kupenda na kuthamini bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi mkuu wa Kiwanda cha Tanzania Distilleries (KONYAGI) Bw. David Mgwassa wakati akiongea na Warembo 30 wanaowani taji la Miss Tanzania walipotembelea kiwanda hicho jijini Dar es salaam.

"Nyinyi ni mabalozi wazuri wa kutangaza bidhaa za humu ndani  hivyo nawaomba sana mzipende na kuthamini sana bidhaa zote zinazozalishwa na viwanda vya ndani" alisema Bw. Mgwassa.

Amesema kuwa TDL kupitia kinywaji cha Zanzi imeamua kudhamini shindano la Miss Tanzania kwa kiasi cha Milioni 40 ikiwa na lengo la kutangaza kinywaji hicho na pia kuboresha shindano hilo.

Kwa mujibu wa Bw. Mgwassa shindano la Miss Tanzania ni kielelezo muhimu kwa taifa hili na kuwataka warembo hao kutangaza milima kilimanjaro na pia kuitangaza Zanzi kuwa ni bidhaa bora kwa Watanzania kwa lengo la kuinua uchumi wa nchi.

"Nyinyi warembo naombeni sana  Zanzi iwe kwenye mawazo yenu kila siku na muitangaze Zanzi baada ya mlima kilimanjaro kwa kufanya hivyo basi uchumi wa nchiu pia utakua mzuri zaidi." alisema

Kwa upande wake meneja masoko wa TDL, Bw. Vimal Vaghmaria aliwataka warembo hao kuwa na nidhamu kubwa wanapokuwa kambini kwa lengo la kupata mrembo mwenye viwango vya juu na kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa.

"Sisi kama TDL kupitia kinywaji cha Zanzi tumemua kudhamini shindano hili la Miss Tanzania tukiamini kuwa nyinyi ni mabalozi wazuri wa kuitangaza kinywaji hichi na kuiletea sifa Tanzania" alisema Bw. Vaghmaria.

Katika ziara hiyo warembo walipata nafasi ya kujione shughuli mbalimbali za kiwanda hicho kuanzia mwanzo wa vinywaji vinapozalishwa hadi kwenye sehemu ya mwisho ya upakiaji.

JKT Ruvu hawakamatiki, Kavumbangu, Maguri, Kipanga wawanasa akina Tegete, Mkude katika magoli

Didier Kavumbagu
USHINDI wa tatu mfululizo uliopata JKT Ruvu katika Ligi Kuu Tanzania Bara imeifanya timu hiyo izidi kuchanja mbuga ikiongoza msimamo wa ligi hiyo na kuwa timu pekee ambayo haijapoteza mchezo wala kufungwa bao lolote mpaka sasa.
Ruvu inayonolewa na kipa wa zamani wa Tukuyu Stars na Yanga, Mbwana Makatta, iliitafuta Ashanti United jana kwa bao la Amos Mgisa na kuifanya ifikishe pointi 9 na magoli sita ya kufungwa huku yenyewe ikiwa na ukuta wa chuma kwa kutoruhusu kufungwa bao lolote.
Kikosi cha JKT Ruvu
Simba ambayo ilianza mechi zake kwa kulazimishwa sare ya wageni Rhino Rangers imechupa hadi nafasi ya pili kutokana na ushindi wa mechi yao ya jana dhidi ya Mtibwa Sugar, huku Ruvu Shooting ikiwa kwenye nafasi ya tatu kutokana na jana kuing'ata  Mgambo JKT.
Bao pekee lililofungwa na Elius Maguri lilitosha kuifanya maafande hao kufikisha pointi sita, huku mfungaji huyo akiingia kwenye orodha ya wafungaji watano wanaoongoza kwa sasa katika ligi hiyo kila mmoja akiwa na mabao mawili.
Maguri aliyesajiliwa na Ruvu Shooting toka Prisons ameungana na akina Jerry Tegete na Didier Kavumbagu wa Yanga, Jonas Mkude wa Simba, Saad Kipanga aliyeanza kuonyesha makeke licha ya ugeni wake katika ligi hiyo naye akiwa na mabao mawili baada ya jana kuisaidia timu yake ya Rhino kupata sare dhidi ya Olojoro JKT jijini Arusha.
Mchezaji mwingine aliye katika orodha hiyo ya wafungaji bora kwa sasa wakati ligi ikiwa ndiyo kwanza ipo raundi ya tatu ni Bakar Kombo wa JKT Ruvu.
Wakati Prisons ikiwa ndiyo timu pekee ambayo haijafanikiwa kufunga bao lolote mpaka sasa angalau wenyewe wameambulia pointi jana jijini Tanga mbele ya Coastal, kuliko Ashanti United ambayo licha ya kuwa na goli moja, lakini haijaonja furaha ya kumiliki pointi baada ya kupoteza mechi zake zote tatu.
Ilianza kwa kufungwa na Yanga mabao 5-1 kabla ya kunyolewa bao 1-0 katika mechi zilizofuata dhidi ya Mgambo na jana JKT Ruvu na kuwa ndiyo inayoburuza mkia ikizibeba timu zote za ligi hiyo yenye klabu 14.
Ashanti ni kati ya timu tatu zilizopanda daraja msimu huu sambamba na Rhino Rangers iliyokusanya pointi mbili mpaka sasa katika mechi zake tatu na Mbeya City iliyokaribia kuiadhiri mabingwa watetezi Yanga jana kwenye mechi yao ilioisha kwa sare ya 1-1 yenyewe ikiwa na pointi tano sambamba na klabu nyingine wakiwamo Yanga, Coastal Union na Azam.
Msimamo kamili wa ligi hiyo baada ya mechi ya jana ni kama ifuatavyo na wafungaji na ratiba ya mechi zijazo utachungulia hapo chini:

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014                                         
                                     P  W  D  L    F  A  GD PTS
1.  JKT Ruvu                 3    3   0   0   6   0    6    9
2.  Simba                       3    2   1   0   5   2    3    7
3.  Ruvu Shooting           3    2   0   1   5   2    3    6
4.  Yanga                        3    1   2   0   7   3   4    5
5.  Azam                        3    1    2   0   4   2   2    5
6.  Coastal Union            3   1    2    0   3   1  2    5
7.  Mbeya City                3   1    2    0   3   2   1   5
8.  Mtibwa Sugar             3   1    1   1    2   3  -1  4
9.  Mgambo                    3    1    0   2    1   3  -2   3
10. Rhino Rangers           3    0    2   1    3   5  -2   2
11. Kagera Sugar            3    0    2    1   1   2  -1   2
12. Oljoro                       3    0    1    2   1   4  -3   1
13. Prisons                      3    0    1    2   0   6  -6   1
14. Ashanti                      3    0    0    3   1   7  -6   0

Wafungaji:

2- Jerry Tegete, Didier Kavumbangu (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla, Jerry Santo (Coastal Union), Haruna Chanongo, Henry Joseph, Betram Mombeki (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva (Yanga), Iman Joel (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris (Azam), Mwagani Yeya, Steven Mazanda, Paul Nonga (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Ayoub Kitala, Jerome Lembeli (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Salum Machaku, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga (Mgambo JKT), Themi Felix (Kagera Sugar), Amir Omary (Oljoro JKT)

Mechi zinazofuata siku ya Jumatano 
Sept 18, 2013Prisons vs Yanga
Simba vs Mgambo JKT
Kagera Sugar vs JKT Oljoro
Azam  vs Ashanti United
Coastal Union  vs Rhino Rangers
Mtibwa Sugar  vs Mbeya City
Ruvu Shooting vs  JKT Ruvu

Mjini Magharib mabingwa wa Copa Coca Cola


MJINI Magharibi imetwaa ubingwa wa michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 upande wa wavulana baada ya jana (Septemba 14 mwaka huu) kuifunga Ilala bao 1-0.

Mechi hiyo ya fainali ilichezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam. Ilala iliwavua ubingwa Morogoro baada ya kuwafunga kwenye mechi ya nusu fainali kwa kuivua ubingwa Morogoro katika mechi iliyoamriwa kwa mikwaju ya penalti.

Kwa upande wa wasichana, Mwanza ndiyo imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 kwa njia ya penalti dhidi ya Ilala. Hadi muda wa kawaida wa mchezo huo uliochezwa jana (Septemba 14 mwaka huu) jioni Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es Salaam timu hizo zilikuwa suluhu.

Simba, Mtibwa waingiza Mil 102



Na Boniface Wambura
MECHI ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Mtibwa Sugar iliyochezwa jana (Septemba 14 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 95,080,000.

Watazamaji 16,507 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 15 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa wenyeji Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 23,018,077.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 14,503,728.81.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 11,704,107.18, tiketi sh. 2,548,890, gharama za mechi sh. 7,022,464.31, Kamati ya Ligi sh. 7,022,464.31, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 3,511,232.15 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 2,730,958.34.

Mbunge Mtemvu awaga magodoro Temeke Hospitali


 Mbunge wa temeke  Abbas Mtemvu akikabidhi kwa Lucy Sozigwa ambae ni katibu wa hospitali ya temeke  moja ya magodoro 30 yaliotolewa na kikundi cha akina mama wa  Neema Woman's Power (NWP).
 Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu akisalimiana na Mgeni Otto  katibu wa kikundi cha Neema Woman's Power(NWP) mara alipowasili katika hospitali ya Temeke.
 Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu akisalimiana na Moshi Ndungu ,mjumbe halmashauri tawi la Azimio.
Mbunge wa Temeke  Abbas Mtemvu akikabidhiwa magodoro 30 na Maryam Dedes ambae ni mwenyekiti wa kikundi cha Neema Woman's Power (NWP)

Mayweather Jr noumaa amtwanga Mmexico

Bondia Floyd Mayweather kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na  Canelo Alvarez wakati wa mpambano wao ambapo Mayweather alishinda kwa pointi 



Friday, September 13, 2013

Maskini Cape Verde, FIFA yaing'oa WC yaipa nafasi Tunisia


KIKOSI cha Cape Verde hakitashiriki mchuano wa kombe la dunia mwaka 2014 baada ya kubanduliwa nje ya kinyanganyiro cha kufuzu kwa dimba la dunia Mwakani kwa nchi za Afrika.
Kwa mujibu wa tovuti ya shirikisho la soka duniani FIFA, Cape Verde ilikosea kwakumshirikisha mchezaji aliyekuwa amepigwa marufuku katika mechi yao dhidi ya Tunisia Jumamosi iliyopita
Kwa mujibu wa FIFA Fernando Verela hakufaa kucheza katika mechi hiyo waliyoshinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Tunisia . FIFA sasa imebadilisha matokeo hayo na kuipa Tunisia ushindi mkubwa wa mabao 3-0.



Kauli hiyo imeipa Tunisia alama za kutosha kuipiku Cape Verde kutoka kileleni mwa kundi B ikiwa na alama 14 .Cape Verde ni ya pili na alama 14.
Shirikisho la soka la Cape Verde lilimetozwa faini ya dola $ 6400 Sadfa ni kuwa Cape Verde ilinufaika na alama za bwerere mapema mwakani Equatorial Guinea ilipoadhibiwa kwa kumshirikisha mchezaji kinyume na sheria za FIFA za uraiya wa wachezaji.
The Blue Sharks ya Visiwa vya Cape Verde walikuwa wamelazwa mabao 3-4 na Equatorial Guinea lakini FIFA ikabadilisha matokeo hayo kwani Emilio Nsue Lopez hakutimiza kanuni za uraiya wa taifa hilo .
Sasa Tunisia ndiyo itakayosonga mbele katika raundi ya mwisho itakayochezwa katika droo itakayofanyika Jumatatu tarehe 16.
Msimamo Mpya baada ya maamuzi ya FIFA
Kundi B
Tunisia - 14
Cape Verde - 9
Sierra Leone - 8
Eq Guinea - 2

BBC

DAR FILAMU FESTIVAL INAMTAMBULISHA LULU KWENU


TAMASHA Kubwa la Filamu litakaloandika historia ya tasnia ya filamu Tanzania la Dar Filamu Festival (DFF 2013) linamtambulisha Elizabeth Michael kama Official Actress for DFF 2013/14 katika muonekano mpya akiwa kama balozi wetu wa kwanza kutambulishwa kutoka DFF, alafu utapata muonekano wa Official Director/ Producer DFF 2013/2014 Vincent Kigosi ‘Ray the Greatest’.
Dar Filamu Festival 2013 awali ilitambulishwa kwa wadau na wanahabari wiki iliyopita na sasa tupo katika hatua nyingine ya kuwatangaza na kuwapa majukumu mabalozi wetu ambao ni Ray na Lulu katika kuhakikisha kampeni ya kupenda filamu za Kiswahili na kuzipa thamani zinafanikiwa na kuwa ni soko lenye nguvu zaidi katika tasnia ya filamu Ulimwenguni.
Tamasha la Dar Filamu Festival (DFF 2013) litafanyika katika viwanja vya CoICT- UDSM- Kijitonyama kuanzia tarehe 24 hadi 26 Septemba 2013, filamu za Kitanzania kama ufunguzi wa tamasha hilo zitaonyeshwa kwa kiingilio cha Bure kabisa  kiingilio chako ni kufika katika viwanja vya Posta pale Kijitonyama na kushuhudia filamu kutoka kwa wakali wa filamu Bongo Movie.
Sasa ni zamu yako kukutana na Lulu kisha kuongea naye kuhusu filamu na soko jipya la Filamu,  kupitia Projector kubwa  na kuona filamu kwa uzuri zaidi huku ukiburudika kwa kazi nzuri kutoka nyumbani.

Ilala yaifuata Mjini Magharib Fainali za Copa


TIMU ya Ilala imepata tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 upande wa wavulana baada ya kuivua ubingwa Morogoro katika mechi iliyoamriwa kwa mikwaju ya penalti.

Hadi muda wa kawaida wa mchezo huo uliochezwa leo (Septemba 13 mwaka huu) jioni Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es Salaam timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1.

Paul Ngowi ndiye aliyeanza kuifungia Ilala dakika ya 30, lakini Morogoro wakasawazisha dakika ya 50 kupitia kwa Omari Sultan. Katika changamoto ya mikwaju ya penalti, Ilala ilipata tatu dhidi ya mbili za Morogoro.

Ilala sasa itacheza fainali na Mjini Magharibi itakayofanyika kesho (Septemba 14 mwaka huu) kuanzia saa 9 alasiri.

Fainali hiyo ya wavulana itatanguliwa na ile ya wasichana kati ya Mwanza na Ilala itakayoanza saa 7 mchana. Mwanza imepata tiketi ya kucheza fainali baada ya leo kushinda nusu fainali ya pili dhidi ya Mbeya kwa mabao 3-0.

Mabao hayo katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume yamefungwa na Flora Fulgence dakika ya 47, Emiliana Akuti dakika ya 56 na Yulitha Masamu dakika ya 57.

Ngeta kuwakabidhi bendera Airtel Rising Stars

 
Na Boniface Wambura
TIMU ya Airtel Rising Stars ya Tanzania kwa wavulana na wasichana itakabidhiwa bendera kesho (Septemba 14 mwaka huu) tayari kwa safari ya Nigeria itakayofanyika keshokutwa alfajiri.

Hafla hiyo ya kukabidhi bendera kwa timu hiyo yenye kikosi cha wachezaji 32 itafanyika saa 5 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah ndiye atakayekabidhi bendera kwa kikosi hicho.

Sambazeni ujuzi wenu,Tenga awaambia wahitimu Grassroots

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodgar Tenga amewataka wahitimu wa kozi ya ukocha wa grassroots kusambaza ujuzi walioupata nje ya shule zao ili mradi huo uwe na manufaa nchi nzima.

Akifunga kozi hiyo iliyoshirikisha makocha 30 kutoka Tanzania Bara na Visiwani kwenye ukumbi wa TFF leo (Septemba 13 mwaka huu), Rais Tenga amewakumbusha kuwa mradi huo umelengwa kuenea nchi nzima katika kipindi cha miaka mitatu.

Mradi wa grassroots unalenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12, na kozi hiyo ilikuwa chini ya Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Govinder Thandoo kutoka Mauritius.

Washiriki waliohitimu kozi hiyo na kukabidhiwa vyeti ni Abdulkheir Khamis Mohamed (Kaskazini A), Ali Hamad Mohamed (Wete), Ali Khamis Ali (Wete), Amin Amran Yunus (Micheweni), Amina Mhando (Kibaha), Benito Mwakipesile (Kibaha), Deogratius Yesaya (Kibaha), Editha Katabago (Bagamoyo), Habiba Mulungula (Bagamoyo) na Irene Semng’indo (Kibaha).

Juma Omar Abdallah (Kaskazini A), Kassim Ibrahim Mussa (Mkoani), Khamis Haji Ali (Kusini Unguja), Khamis Hamad Rajab (Chakechake), Mahfoudh Abdulla Said (Wete), Marianus Nyalale (Bagamoyo), Maryam Suleiman Ali (Mjini Magharibi), Maryasa Juma Ali (Mjini Magharibi), Mohamed Ali Abdullah (Mjini Magharibi) na Mohamed Salim Omar (Micheweni).

Mohamed Seif Abeid (Mkoani), Ramadhan Kejeli (Bagamoyo), Rhobi Kibacho (Kibaha), Salim Suleiman Juma (Chakechake), Shaaban Naim Suleiman (Kusini Unguja), Shabani Rashid Masimbi (Bagamoyo), Talib Ali Rajab (Chakechake), Thabit Juma Makungu (Kusini Unguja), Yusuf Ali Issa (Mjini Magharibi), Zakia Choum Makame (Mjini Magharibi).

Hiyo ni kozi ya pili ya grassroots kufanyika nchini ambapo ya kwanza ilifanyika Desemba mwaka juzi.

Simba kamili gado 'kuiua' Mtibwa kesho, Owino, Dhaira watua

Joseph Owino
KLABU ya soka ya Simba imekamilika tayari kulipa kisasi kwa Mtibwa Sugar kesho katika pambano lao la Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya nyota wao wa kimataifa kutoka Uganda, Abel Dhaira na beki Joseph Owino kuwasili kikosini.

Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga aliliambia MICHARAZO kuwa, kikosi chao kipo 'kamili gado' kambini na kesho kitashuka dimba la Taifa, Dar es Salaam kwa nia ya kulipa kisasi kwa Mtibwa waliowanyuka na kuzoa pointi zote sita katika mechi mbili za msimu uliopita.

Kamwaga alisema benchi lao la ufundi limewahakikishia wachezaji wote wapo fiti kukiwa hakuna majeruhi na la furaha zaidi ni kurejea kwa mastaa wao wa Uganda, kipa Dhaira na beki Owino waliokuwa wameenda kwao kwa matatizo ya kifamilia.

"Tunashukuru kambi yetu ipo fiti na kwamba kikosi kimekamilika baada ya nyota wetu kutoka Uganda kutua nchini tayari kwa vita ya kesho, lengo likiwa kulipa kisasi dhidi ya Mtibwa sambamba na kuzoa pointi zitakazotuweka pazuri katika msimamo wa ligi," alisema.

Kamwaga alisema Simba inafahamu mechi ya kesho itakuwa ngumu na yenye upinzani mkali, lakini wamehakikishwa na benchi lao la ufundi pamoja na wachezaji wenye ari kuwa ushindi ni lazima Taifa kabla ya kusubiri mechi yao ijayo ya siku ya Jumatano dhidi ya Mgambo JKT.

Simba iliyoanza ligi hiyo kwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Rhino Rangers kisha kuifunga JKT Oljoro, ililala bao 1-0 jijini Dar es Salaam katika mechi yao ya pili dhidi ya mabingwa hao wa Tanzania  wa 1999 na 2000 baada ya awali kufungwa mabao 2-0 mjini Morogoro.

Baadhi ya nyota wa Mtibwa Sugar kama Salum Sued 'Kussi' na Salvatory Ntebe wametamba kuwa wamekuja  Dar kwa nia moja ya kuzoa pointi tatu pamoja na kuendeleza ubabe kwa vijana wa Msimbazi, licha ya kukiri litakuwa pambano la 'kufa mtu'.

Mtibwa kama ilivyo Simba na klabu nyingine tano zinazokamata nafasi ya pili nyuma ya JKT Ruvu ina pointi nne zilizotokana na sare ya 1-1 dhidi ya Azam na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya ndugu zao wa Kagera Sugar ambao kesho wapo Kagera kuumana na Azam.

Mechi nyingine za kesho ni kati ya Mbeya City na Yanga zitakazoumana uwanja wa Sokoine Mbeya, JKT Ruvu itakayokuwa wageni wa Ashanti Utd uwanja wa Chamazi, Coastal Union kuialika Prisons-Mbeya na JKT Oljoro itakayoikaribisha Rhino Rangers ya Tabora.

Tenga aipongeza Kamati ya Ligi

Rais wa TFF, Leodgar Tenga
Na Boniface Wambura
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodgar Tenga ameishukuru Kamati ya Ligi kwa usimamizi mzuri tangu ilipokabidhi Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) katika mzunguko wa pili msimu uliopita.

Amesema TFF iliamua kuanzisha Kamati ya Ligi kwa lengo la kutaka klabu zijisimamie zenyewe ili kuongeza ufanisi, jambo ambalo limeleta mabadiliko kwa vile hivi sasa hakuna matatizo katika kuwalipa marefa na makamisha wanaosimamia VPL na Ligi Daraja la Kwanza (FDL).

“Fedha za udhamini sasa zinakwenda moja kwa moja kwenye Kamati ya Ligi. Ni matarajio yangu kuwa ufanisi utaongezeka, kwani tumeanzisha jambo hili kwa lengo la kuleta tija, maendeleo na utulivu,” amesema Rais Tenga wakati akizungumza na Wahariri wa Michezo kutoka vyombo mbalimbali vya habari.

Rais Tenga amesema mahali penye utulivu na utawala bora watu wanakuwa na imani hasa katika masuala ya fedha, hivyo ni lazima kwa kampuni kuwekeza kwa vile kunakuwa hakuna vurugu.

Amesema ukiondoa Afrika Kusini na Angola katika ukanda huu wa Afrika Mashariki, Kati na Kusini, Ligi Kuu ya Tanzania ndiyo yenye udhamini mkubwa kupitia mdhamini wa ligi na udhamini wa matangazo ya televisheni.

Pia amesema kuanzia msimu ujao 2014/2015 klabu za Ligi Kuu hazitaruhusiwa kusajili wachezaji hadi zitakapowasilisha TFF ripoti zao za mapato na matumizi zilizokaguliwa (Audited accounts), hivyo klabu husika zijiandae kwa ripoti hizo za Januari hadi Desemba 2013.

Kuhusu tiketi za elektroniki, Rais Tenga amesema bado linafanyiwa kazi na CRDB ambayo ndiyo iliyoshinda tenda hiyo na liko katika hatua nzuri, kwani nia ya TFF na benki hiyo kuona kuwa linaanza haraka iwezekanavyo.

“Tiketi za elektroniki zimechelewa kuanza kwa sababu ambazo haziwezi kuzuilika, lakini CRDB imeshatengeneza miundombinu katika karibu viwanja vyote. Kulitokea uchelewaji katika kuleta printer (mashine za kuchapia), zilizokuja hazikuwa zenyewe. Kwa upande wa Uwanja wa Taifa, system (mfumo) iliyopo inatofautiana na ile ya CRDB. Hivyo sasa tunaangalia uwezekano wa zote mbili zitumike kwa pamoja, kwa sababu Uwanja wa Taifa una system yake tayari. Printer zimeshafika, tunataka ili suala lisitucheleweshe,” amesema.

620 wapitishwa kucheza FDL, wanne Ndanje akwama


Na Boniface Wambura
KAMATI ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imethibitisha usajili wa wachezaji 620 kati ya 624 wa timu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inayoanza kutimua vumbi kesho (Septemba 14 mwaka huu).

Wachezaji wanne ambao usajili wao umezuiwa mpaka watakapokamilisha taratibu ni Emmanuel Simwanza Namwando wa African Lyon, Godfrey Bonny Namumana (Lipuli FC), na Enyinna Darlington na Chika Keneth Chukwu wote wa Mwadui FC ya Shinyanga.

Darlington na Chukwu ambao wote ni Wanigeria wamezuiwa mpaka watakapowasilisha vibali vya kufanya kazi nchini kutoka Idara ya Uhamiaji wakati Namumana aliyekuwa akicheza nchini Nepal bado hajapata Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC).

Nayo African Lyon imetakiwa kufikia muafaka na AYOSA Academy ambayo Namwando anatoka juu ya usajili kabla ya kuanza kumtumia mchezaji huyo.

Klabu ambazo zimemaliza nafasi zote 30 usajili katika FDL ni Friends Rangers FC ya Dar es Salaam, na Stand United FC ya Shinyanga wakati iliyosajili wachezaji wachache zaidi ni Burkina Faso FC. Klabu hiyo ya Morogoro imesajili wachezaji 19 tu.

Vilevile Kamati hiyo vilevile imethibitisha usajili wa wachezaji wanane wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) waliosajiliwa katika hatua ya pili ya usajili iliyoanza Agosti 14 hadi 30 mwaka huu.

Wachezaji hao ni Samir Ruhava na Amani Simba (Ashanti United), Robert Machucha na Said Ndutu (Yanga U20), Ayoub Masoud na Abdallah Selemani (Coastal Union U20), Ramadhan Kipalamoto (Simba U20) na Henry Joseph (Simba) ambaye tayari Hati yake Uhamisho wa Kimataifa (ITC) imeshawasili.

Vita vya Ligi Kuu vyaanza tena, Simba, Yanga kuvuna nini?


Yanga watawafunga mdomo Mbeya City kesho jijini Mbeya?

Vijana wa Kibadeni wataizuia Mtibwa jijini Dar?
 Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) inaingia raundi ya tatu kesho (Septemba 14 mwaka huu) kwa timu zote 14 kushuka viwanjani huku masikio ya washabiki wengi yakielekezwa kwenye mechi kati ya Simba na Mtibwa Sugar na ile kati ya Mbeya City na Yanga.

Simba inaikaribisha Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Dominic Nyamisana kutoka Dodoma. Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000 viti vya bluu na kijani, sh. 8,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000.

Pia Azam TV itautumia mchezo huo kwa ajili ya mazoezi (broadcast training) kwa wafanyakazi wake. Hivyo mechi hiyo haitarekodiwa au kuoneshwa moja kwa moja.

Katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, shughuli itakuwa kati ya mabingwa watetezi Yanga na wenyeji wao Mbeya City SC. Mwamuzi Andrew Shamba kutoka Pwani ndiye atakayepuliza filimbi wakati Kamishna wa mechi hiyo James Mhagama kutoka Songea.

Mechi nyingine za ligi hiyo ni Coastal Union na Tanzania Prisons (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Ruvu Shooting na Mgambo Shooting (Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani), Oljoro JKT na Rhino Rangers (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha), Kagera Sugar na Azam (Uwanja wa Kaitba, Bukoba), na Ashanti United na JKT Ruvu (Uwanja wa Azam Complex,

Mjini Magharib yaifyatua TMK na kutinga fainali za Copa Coca Cola

TIMU ya Mjini Magharibi imepata tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 upande wa wavulana baada ya kuing’oa Temeke kwenye nusu fainali iliyochezwa leo (Septemba 13 mwaka huu) asubuhi Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es Salaam.

Ushindi wa mabao 2-0 yaliyofungwa dakika za 30 na 63 kupitia Juma Ali Yusuf ndiyo yaliyoipa Mjini Magharibi tiketi ya kucheza fainali itakayofanyika kesho (Septemba 14 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kuanzia saa 9 alasiri.

Mjini Magharibi itacheza fainali hiyo na mshindi wa nusu fainali ya pili inachezwa leo jioni kwenye uwanja huo huo kati ya mabingwa watetezi Morogoro na Ilala.

Kwa upande wa wasichana Ilala imetinga fainali baada ya kuifunga Kinondoni mabao 2-0 katika nusu fainali ya kwanza. Mabao ya washindi yalifungwa dakika ya 27 na Fatuma Bahau wakati Happiness Lazoni alifunga la pili dakika ya 39.

Nusu fainali ya pili kwa wasichana itakuwa kati ya Mwanza na Mbeya.

30 waitwa kambi ya Twiga Stars

Kikosi cha Twiga Stars
Na Boniface Wambura
Kocha Mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage ameita kambini kikosi cha wachezaji 30, wengi wao wakiwa vijana ikiwa ni mwendelezo wa programu ya kujenga timu hiyo.

Kambi hiyo itakuwa jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 15 hadi 26 mwaka huu. Vijana wengi wamejumuishwa ikiwa ni hatua ya mwanzo ya kuandaa timu itakayocheza mechi za mchujo za Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20.

Kaijage amesema pamoja na malengo hayo kwa timu ya vijana, bado maana kubwa inabaki kuandaa Twiga Stars iliyo imara kwa ajili ya mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Amesema Twiga Stars haikabiliwi na mashindano yoyote mwaka huu, hivyo lengo ni kuijenga upya ndiyo maana haichezi michezo ya kimataifa ya kirafiki hadi itakapofika wakati wake.

Utaratibu huo ulianza kuanzia kambi ya Machi mwaka huu, na ndio umezaa timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 ambayo sasa itashiriki mashindano ya Kombe la Dunia.

Wachezaji walioitwa ni Amina Ally (Lord Barden, Pwani), Asha Rashid (Mburahati Queens, Dar es Salaam), Belina Julius (Lord Barden, Pwani), Donisia Daniel (Lord Barden, Pwani), Esther Chabruma (Sayari Queens, Dar es Salaam), Eto Mlenzi (JKT, Dar es Salaam) na Evelyn Sekikubo (Mburahati Queens, Dar es Salaam).

Fatuma Bushiri (Simba Queens, Dar es Salaam), Fatuma Hassan (Mburahati Queens, Dar es Salaam), Fatuma Issa (Evergreen, Dar es Salaam), Fatuma Mustafa (Sayari Queens, Dar es Salaam), Fatuma Omari (Sayari Queens, Dar es Salaam), Flora Kayanda (Tanzanite, Dar es Salaam) na Gerwa Lugomba (Umisseta, Kanda ya Ziwa).

Hamisa Athuman (Marsh Academy, Mwanza), Maimuna Hamisi (Airtel Rising Star, Ilala), Maimuna Said (JKT, Dar es Salaam), Mwanahamisi Omari (Mburahati Queens, Dar es Salaam), Mwapewa Mtumwa (Sayari Queens, Dar es Salaam), Pulkeria Charaji (Sayari Queens, Dar es Salaam) na Rehema Abdul (Lord Barden, Pwani).

Sabahi Hashim (Umisseta, Zanzibar), Semeni Abeid (Tanzanite, Dar es Salaam), Sharida Boniface (Makongo Sekondari, Dar es Salaam), Sofia Mwasikili (Sayari Queens, Dar es Salaam), Tatu Idd (Lord Barden, Pwani), Therese Yona (TSC Academy, Mwanza), Vumilia Maarifa (Evergreen, Dar es Salaam), Yulitha Kimbuya (Marsh Academy, Mwanza) na Zena Khamis (Mburahati Queens, Dar es Salaam). 

Yanga wapewa wiki 2 kuwalipa akina Nsajigwa

Nsajigwa (2) akiwa ameshikwa na Godfrey Taita
Na Boniface Wambura
KLABU ya soka ya Yanga imepewa siku 14 kuanzia leo (Septemba 13 mwaka huu) kuwalipa waliokuwa wachezaji wake msimu uliopita, nahodha Shadrack Nsajigwa na Stephen Mwasika wanaoidai klabu hiyo jumla ya sh. milioni 15.5.

Uamuzi huo umefanywa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana jana (Septemba 12 mwaka huu) ambapo pamoja na mambo mengine ilisikiliza madai ya wachezaji hao.

Fedha hizo ni ada ya usajili ambayo klabu hiyo ilikubaliana na wachezaji hao wakati ikiwasainisha mikataba. Yanga imeshawalipa sehemu ya fedha walizokubaliana na kiasi hicho ndicho bado hakijalipwa. Nsajigwa anadai sh. milioni 9 wakati Mwasika ni sh. milioni 6.5.

Baba wa Ozil kuishtaki Real Madrid

Ozil na baba yake
Mesut Ozil

MADRID, Hispania
BABA wa Mesut Ozil, Mustafa, ametishia kuchukua hatua za kisheria kufuatia taarifa za katika vyombo vya habari nchini Hispania kudai kwamba kiungo huyo Mjerumani alikuwa akiathiriwa kipaji chake na matatizo ya nje ya uwanja wakati akiwa Real Madrid.
Mapema wiki hii, gazeti la Hispania liitwalo ABC, ambalo lina mahusiano na rais wa Real, Florentino Perez, liliripoti kuwa rais huyo wa Madrid anaamini kwamba Ozil "hakuwa vizuri kiweledi na alikuwa akichanganywa na wanawake na maisha ya kujirusha usiku".
Lakini baba wa kiungo huyo Mjerumani amejia juu tuhuma hizo akisema Perez anajaribu kumfanya kiungo huyo aliyetua Arsenal kuwa mbuzi wa kafara.
"Kwa sababu tu ana pesa nyingi haimaanishi kwamba yeye ni mtu wa heshima," baba wa Ozil alikaririwa na gazeti la Bild. "Na Perez si mtu wa heshima.
"Mesut anatumiwa kama mbuzi wa kafara sasa lakini baba yake nipo. Nitaingia mchezoni. Tutatetea upande wetu kisheria.
"Kama Mesut alikuwa na maisha yasiyozingatia weledi Madrid, kwanini sasa alikuwa akichezeshwa kila siku? Wanataka kumlaumu sasa kwa vile mashabiki na wachezaji wenzake wamekasirika (kuuzwa kwake)."
Ozil, ambaye alifunga ama kutoa pasi ya magoli 108 katika mechi 159 akiwa na Madrid, alikamilisha uhamisho wa aina yake katika siku ya mwisho na kutua Arsenal kwa ada ya paundi milioni 40, jambo lililowakera wachezaji wenzake wengi akiwamo Cristiano Ronaldo.

'Unga' wachelewesha safari ya Mark Band

Rashid Pembe (kushoto) akiwa na mwanamuziki wenzake wa Mark Band

SAKATA la kubambwa kila uchao kwa Watanzania nje ya nchi kwa tuhuma za kujihusiaha na dawa za kulevya limesababisha safari ya Mark Band kwenda Chile na Peru ichelewe kutokana na ugumu wa kuzipata visa za kuingia katika nchi hizo.
Mark Band iliyojikita na kupiga muziki asilia kwenye mahoteli ya kitalii, ilikuwa itimke nchini wiki iliyopita, lakini zoezi la upatikanaji wa visa za kuingia nchini humo kupitia balozi zilizopo Kenya na Afrika Kusini limeichelewesha safari hiyo kwa wakati.
Mkurugenzi wa bendi hiyo iliyoanzishwa mwaka 2006, Rashid Pembe 'Profesa' alisema tangu Tanzania ichafuke kutokana na kukamatwa kwa raia wake wakihusisha na dawa za kulevya imekuwa usumbufu kwa watu wengine kiasi cha wao kucheleweshewa safari yao.
"Yaani kwa sasa hakuna Mtanzania anayeaminiwa anapotaka kwenda nje ya nchi au kuingia katika taifa jingine kwa kudhaniwa ni wale wale wanaojihusisha na dawa za kulevya, hata sisi imekuwa tabu kupata visa kwa wakati na kufanya tukwame kuondoka mapema," alisema.
Hata hivyo, alisema zoezi la kupata visa za kuingia katika nchi hizo wanazoenda kutumbuiza kwa mualiko maalum limekamilika na wanamaliza mambo madogo kabla ya wiki ijayo kuondoka nchini.
"Nadhani tutaondoka wiki ijayo kwani karibu kila kitu kimekaa vyema kwa sasa japo ratiba yetu ilishavurugwa kwa kuchelewa kuzipata visa," alisema.
Kwa siku za karibuni Tanzania imekuwa ikichafuka kimataifa kutokana na baadhi ya raia wake wakiwamo wasanii na wanamichezo kuripotiwa kutiwa mbaroni katika mataifa mbalimbali kwa tuhuma za kujihusisha na usafirishaji wa dawa za kulevya.
Baadhi ya walioripotiwa  kunaswa ni pamoja na video queen na nduguye, Agness Gerald  'Masogange' na Mellisa Erdwad, strika wa zamani wa Simba, Joseph Kaniki na bondia wa ukoo wa Matumla, Mkwinda na Mbwana Matumla mbali na watanzania wengine kadhaa.

Waziri Mulugo aahidi Mil 2 kwa Mbeya City wakiitungua Yanga kesho

http://kifltd.files.wordpress.com/2012/01/01_12_enn75u.jpg
Naibu Waziri Philipo Mulugo

Kikosi cha Mbeya City
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiSJsNsHjk8oZes4gIRZJMglBDLy-cqJ__Id6KV6ouVjbXYivTnjTaWyCOanYX5Ih6OyrwPaHjkzm8Gxz-fLOi_cbctliSDX9r5rqi82IUo5V_Wg7As77JRaNzSAHzEH_bs5dPA0IN52NbE/s1600/IMG_8317.JPG
Kikosi cha Yanga

NAIBU Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo ametanga kutoa dau la Sh Milioni 2 kwa kikosi cha Mbeya City iwapo watafanikiwa kuifunga Yanga katika pambano lao la Ligi Kuu Tanzania Bara linalochezwa kesho kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.
Aidha Waziri huyo ameamua kufunga safari kutoka jijini Dar es Salaam kuelekea mkoani Mbeya kwa ajili ya kuipa sapoti timu hiyo ya Mbeya City katika mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa kandanda mkoani humo.
Waziri Mulugo alisema amefunga safari hiyo ili kuhakikisha timu hiyo ya Mbeya City inapata ushindi dhidi ya mabingwa watetezi hao, Yanga ambao wameshatangaza vita dhidi ya timu hiyo wakitamba wameenda mkoani humo kuzoa pointi sita zikiwamo tatu za mechi ya leo.
Mechi nyingine ambayo Yanga imetangaza kuipigia hesabu ni ile ya Jumatano dhidi ya Prisons Mbeya iliyoanza ligi hiyo vibaya.
Waziri Mulugo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songwe  mkoani humo, alisema kwa vile anaamini Mbeya City ni timu nzuri na iwapo ikipata sapoti itafanya maajabu katika mechi hiyo ya kesho na nyingine za ligi hiyo iliyokuw amesimama kwa wiki mbili mfululizo.
Alisema kutokana na hilo ndilo maana amefunga safari kwenda Mbeya kuisapoti timu hiyo na kuahidi kuwapa Sjh Mil 2 iwapo watafanikiwa kuifunga Yanga, aliyokiri ni moja ya timu kubwa yenye uzoefu, lakini bado haamini kama inaweza kufua dafu kwa Mbey City katika mechi hiyo.
"Naifahamu Yanga ni timu nzuri yenye wachezaji wazuri, lakini katika mchezo wa Jumamosi naamini kabisa watabugizwa mabao mengi ya Mbeya City, iliyonilazimu kufunga safari kuja kuisapoti ili ishinde na wakifanya hivyo nitawapa Sh. Mil 2 taslim kama zawadi yao," alisema.
Mbeya City inayonolewa na kocha mzoefu, Juma Mwambusi inashiriki ligi hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kupanda daraja ikiwa na timu nyingine mbili za Rhino Rangers ya Tabora na Ashanti United ya Dar es Salaam na mpaka sasa ina pointi nne kutokana na mechi mbili ilizocheza.
Ilianza kwa kutoka sare ya bila kufungana na Kagera Sugar kabla ya kuicharaza Ruvu Shooting kwa mabao 2-1 katika mechi yao ya mwisho zote zilizochezwa uwanja wa Sokoine kabla ya ligi kusimama kupisha pambano la kimataifa la Taifa Stars dhidi ya Gambia.