STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 2, 2015

Wife wa Ali Kiba avuja mtandaoni, msikilize hapa


Maradhi ya Moyo ya Diamond hadharani usikilize hapa


Newz Alert! Francis Cheka ahukumiwa miaka mi3 jela

Cheka (kulia) katika mikutano ya mapambano yake pembeni yake ni promota Omar Kimbau
BONDIA nyota wa ngumi za kulipwa nchini aliyewahi kuwa Bingwa wa Dunia wa WBF, Francis Cheka 'SMG' mwenye maskani yake mjini Morogoro amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela.
Kwa mujibu wa kituo cha redio cha EFM kipindi cha Sports Headquarter, Cheka amehukumiwa adhabu hiyo baada ya kukutwa na hatia ya kumpiga meneja wake katika shughuli zake za biashara ya ukumbi wa Vijana Social mjini Morogoro anayedaiwa kumuingiza mjini kiasi kikubwa cha fedha kiasi cha kufikia kuchapana naye.
Akizungumza na kituo hicho baba mzazi wa Francis Cheka amesema haikuwa sahihi kwa mwanae kupewa hukumu hiyo na badala yake wangekaa na kuzungumza ili kuyamaliza matatizo hayo.
Mzee huyo alienda mbali zaidi na kusema kuwa kuna watu wenye chuki na mwanae wameitumia kesi hiyo ya muda mrefu kutimiza malengo yao lakini pia mzee huyo ameelezea hisia zake kwa wakazi wa Morogoro kutoa sapoti ndogo kwa mwanae.
Taarifa zinasema kuwa Cheka amehukumiwa adhabu hiyo leo JUmatatu Februari 2, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro.
EFM.

Shaa kutoa mpya, video ya Subira bado yakwama

WAKATI video ya wimbo wake wa 'Subira' ikiwa inaendelea kupigwa danadana bila kuachiwa tangu itengenezwe, msanii Sarah Kais 'Shaa' yupo njiani kuachia kazi mpya.
Akizungumza na MICHARAZO mapema leo, Meneja wa msanii huyo Said Fella 'Mkubwa' alisema kuwa katikati ya mwezi huu Shaa ataachia kazi mpya kulingana na utaratibu waliojiwekea.
Akiwa chini ya Mkubwa na Wanae, Shaa ameshaachia nyimbo mbili za 'Sugua Gaga' na 'Subira' na hivi karibuni akiwa Kenya kikazi alitoa wimbo mpya uitwao 'Njoo' akishirikiana na mkenya Redsan.
"Tupo katika maandalizi ya mwisho kabla ya Shaa kuingia studio kutengeneza kazi mpya," alisema Fella na kufafanua juu ya video ya wimbo wa 'Subira' ambao ina muda mrefu tangu itangazwe itaachiwa hadharani bila mafanikio.
"Video hiyo imeshakamilika kitambo ila bado ipo mikononi mwa Adam Juma aliyeitengeneza, tukikabidhiwa tutaiachia mara moja," alisema Fella.
Alipoulizwa sababu ya kucheleweshwa kwa video hiyo alisema kuna mambo ambayo hawajaridhishana katika video hiyo ya 'Subira' ambayo ilitengenezwa mwishoni mwa mwaka jana kabla ya Shaa hajaenda Kenya.

Chegge, Mhe Temba, Madee kuzindua video zao Escape One

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhRcuFMHdCOMH-6MJo0M0ke2rBniv8pPETU5_l3lk5chotAEkEwbjahckMWz6qtRuRnbCvvvfPLQcoQci2-PeTusKm9ik3rwx6oDiF6JkqNCZ27dc2yH8EhHF2u85Rr1GwBubQzST4gDeI/s1600/Madee+-+Vuvula.jpgWASANII nyota nchini Mhe Temba, Chegge na Madee wanatarajiwa kuzindua rasmi video ya nyimbo zao mpya walizorekodiwa nchini Afrika Kusini wakimshirikisha Dj Maphorisa wa Uhuru.
Meneja wa wasanii hao, Said Fella aliliambia MICHARAZO kuwa, uzinduzi wa video hizo utafanyika siku ya Jumamosi  kwenye ukumbi wa Escape One, Mikocheni.
Fella alisema Madee atazindua video ya wimbo wake uitwao 'Vuvula' wakati Chegge na Mhe Temba watazindua 'Kaunyaka' ambazo zinafanya vema kwenye vituo vya radio na televisheni.
Meneja huyo alisema uzinduzi huo utapambwa na burudani za wasanii kadhaa nyota watakaousindikiza akiwataja baadhi kuwa ni Diamond, Yamoto Band, Jux, Vanessa Mdee, Shaa na wengine.
"Madee, Chegge na Mheshimiwa Temba wanatarajia kuzindua video za nyimbo zao zinazoendelea kutamba hewani kwa sasa, uzinduzi utafanyika Escape One na utasindikizwa na wasanii kadhaa nyota akiwamo Diamond, Shaa, Vee Money na wengine," alisema Fella.

Costa ajitetea, adai hakukanyaga kwa makusudi

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/03178/CostaButt_3178918b.jpg
Diego Costa akizinguana na Martin Skrtel
MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Diego Costa amesema hakuwa na nia yeyote ya makusudi kumkanyaga mchezaji wa Liverpool Emre Can.
Chama cha Soka Uingereza-FA kilimtwanga adhabu kwa vurugu kutokana na tukio hilo lililotokea katika mchezo wa nusu fainali ya mkondo wa pili wa Kombe la Ligi Jumanne iliyopita jambo ambalo Costa amelipinga.
Costa mwenye umri wa miaka 26 amesema jambo kubwa ni wakati akienda nyumbani kwake kulala na kujua kuwa hakufanya jambo lolote baya.
Strika huyo wa kimataifa wa Hispania amesema hakuwa na nia ya makusudi kutenda kitendo kile kwani ilikuwa bahati mbaya.
Hata hivyo Costa amesema amekubali na kuheshimu adhabu aliyopewa, japo  amesisitiza hakufanya vile kwa makusudi.

Baada ya kuwakosa Ndanda, Yanga kumalizia hasira Mkwakwani

Yanga
BAADA ya jana kushindwa kupata ushindi kama walivyoahidi mbele ya Ndanda Fc ya Mtwara, Yanga itaifuata Coastal Unioni nyumbani kwa Mkwakwani Tanga wakiwa na dhamira moja tu ya kupata pointi tatu.
Yanga ililazimishwa suluhu na Ndanda jana katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara iliyochezwa jkwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuwafanya washindwe kukalia kiti cha uongozi wa ligi hiyo unaoshikiliwa na Azam waliopo DR Congo, japo imerejea katika nafasi ya pili walioshushwa Jumamosi na Mtibwa Sugar.
Sare hiyo ya jana imeifanya Yanga kufikisha pointi 19 baada ya mechi 11, mbili nyuma ya Azam waliolingana nao kimichezo ambao kesho wanatarajiwa kumalizia mechi zao nchini Congo baada ya juzi kulazimisha sare ya 2-2 dhidi ya wenyeji wao TP Mazembe.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alisema wanatarajia kwenda Tanga kwa mechi tyao ya Jumatano wakiwa na nia mopja ya kuhakikisha wanapata ushindi kama ilivyofanya wiki iliyopita mjini Morogoro walipowafunga maafande wa Polisi kwa bao 1-0.
Muro alisema wanatambua pambano hilo litakuwa gumu kutokana na ukweli Coastal Union watakuwa nyumbani na hawajafanya vema katika mechi zao za karibuni, lakini wao hawatajali hilo zaidi ya kupata ushindi ili kujiweka katika nafasio nzuri ya kunyakua taji hilo.
"Matokeo dhidi ya Ndanda ni ya kawaioda katika mchezo na sasa tunajipanga kwa mechi ijayo dhidi ya Coastal Union tutakaowafuata Mkwakwani kwa dhamira moja ya kuvuna pointi," alisema Muro.
Tangu ligi iendelee tena baada ya mapumziko ya Novemba 9, Yanga imevuna pointi  sita tu katika mechi nne ilizocheza mpaka sasa baada ya kutoka sare ya 2-2 na Azam kisha kulazimishwa suluhu na Ruvui Shooting kabla ya kuwazabua Polisi Moro na kubanwa na Ndanda.

Renard awasifu Algeria licha ya kuwang'oa AFCON

http://zambianintelligencenews.com/wp-content/uploads/2013/08/Renard.jpg
Kocha wa Ivory Coast
KOCHA wa timu ya taifa ya Ivory Coast Herve Renard amedai kuwa, wapinzani wao Algeria walikuwa wazuri zaidi yao licha ya kuwafunga bao 3-1 katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
Renard ambaye aliwahi kuipa Zambia ubingwa wa michuano hiyo alisema kuwa, kikosi chake jana usiku kilikuwa dhaifu licha ya ushindi huo ulioiwezesha kutinga hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo.
Washindi wa mchezo huo ndio walikuwa wa kwanza kupata bao lililowekwa kimiani na mchezaji mpya wa Manchester City Wilfried Bony, ambaye pia ndiye aliyefunga la pili baada ya Mualgeria El Arbi Hillel Soudani kusawazisha.
Gervinho aliihakikishia Ivory Coast ushindi baada ya kufunga bao la tatu katika dakika za majeruhi katika mchezo huo uliofanyika jijini hapa na kuihakikishia timu hiyo nafasi ya kusonga mbele.
Renard alisema kuwa wapinzani wao hao kutoka Afrika ya Kaskazini walikuwa wazuri, lakini walishindwa kutumia nafasi zao vizuri.
"Kwa upande wa soka, mbinu, Algeria walikuwa bora zaidi yetu, " alisema Renard alipozungumza na waandishi wa habari mara baada ya mchezo huo.
Timu hiyo sasa itavaana na DR Congo walioiondosha Congo kwa mabao 4-2, timu nyingine iliyofuzu nusu fainali ni Ghana iliyoicharaza Guinea kwa mabao 3-0 na sasa watacheza na wenyeji Guinea ya Ikweta keshokutwa.
Naye Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Algeria Christian Gourcuff aliunga mkono maneno ya mwenzake, ambapo alisisitiza kuwa timu iliyoshinda haikuwa bora.
"Hii sio timu bora iliyoshinda. Kwa upande wa mchezo, tulicheza vizuri lakini bahati haikuwa yetu, " alibainisha Gourcuff.
"Wachezaji wa Ivory Coast hawakupata nafasi nyingi. Hawakustahili kushinda."
Gourcuff pia alitupia lawama ubora wa kiwanja, na kusema kuwa lilikuwa kosa lao kukubali kufungwa na Ghana baada ya kukubali bao la dakika za mwisho na kumaliza wa pili katika Kundi C kwani wangeshinda wangekuwa wa kwanza na wangeikwepa Ivory Coast katika robo fainali.
"Lakini ikiwa tumecheza mechi 10, lakini haujafungwa mara 10, ni wazi sisi ni timu bora…”

Sunday, February 1, 2015

Real Madrid yamtoa nishai David Moyes

Bale (centre) takes Real Sociedad's Yuri Berchiche at Bernabeu stadium in Madrid
Bale akipambana mbele ya vijana wa Real Sociedad
KOCHA wa zamani wa Manchester United, David Moyes anayeinoa kwa sasa Real Sociaded hana hamu na vinara wa La Liga, Real Madrid baada ya kuwashuhudia vijana hao wa Santiago Bernabeu wakiitoa nishai timu yake kwa kuicharaza mabao 4-1 katika pambano la Ligi Kuu ya Hispania usiku wa jana.
Moyes aliyeiongoza Sociaded kuilaza Barcelona bila kutarajiwa hivi karibuni alishuhudia vijana wake wakipotea Bernabeu licha ya kutangulia kufunga la mapema dakika ya kwanza tu tangu kuanza kwa mchezo huo.
Aritz Elustondo aliiandikia wageni bao dakika ya kwanza akimalizia kazi nzuri ya Rubén Pardo kabla ya James 'Bond' Rodríguez kulisawazisha dakika mbili baadaye akimlazia kazi ya Marcelo.
Beki mfungaji wa Real Madrid, Sergio Ramos aliionmgeza timu yake bao la pili dakika ya 37 na kudumu hadi mapumziko wenyeji wakiwa mbele kwa mabaoi 2-1.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa, Karim Benzema aliwapa furaha mashabiki wa Real Madrid ambao walimkosa nahidha wao, Cristiano Ronaldo anayetumikia adhabu ya kandi nyekundu aliyopata katika mechi hiyo iliyopita kufanya undava uwanjani aliingozea timu hiyo bao la tatu dakika ya 52 akiunganisha krosi ya Gareth Bale.
Benzema alirudi tena kambani dakika ya 76 akifunga bao la nne na kuifanya Real Madrid kuzidi kujikuta kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo wakiwa na pointi 51 baada ya kucheza mechi 20, pointi nne zaidi ya wanaowafukuzia Barcelona wanaocheza leo na Atletico Madrid walioshinda jana ugenini kwa mabao 3-1.
Matokeo mengine ya mechi hiyo, Rayo Vallecano ilikubali kichapo nyumbani cha mabao 2-1 mbele ya wageni wa Deportivo La Coruna, Atletico Madrid wakishinda ugenini mabao 3-1 dhidi ya Eibar, Granada wakishinda nyumbani bao 1-0 dhidi ya Elche na Celta Vigo wakiilaza Cordoba kwa bao 1-0.
Ligi hiyo itaendelea tena leo kwa michezo ifuatayo;
Levante vs  Athletic Bilbao (saa 8 mchana)
Almería vs Getafe (saa 1 usiku)
Sevilla vs Espanyol (saa 3 usiku)
Barcelona vs Villarreal (saa 5 usiku)

Yanga, Ndanda hapatoshi leo Taifa

Yanga
Ndanda FC
KLABU ya soka ya Yanga leo watakuwa na kibarua kigumu mbele ya Ndanda Fc ya Mtwara katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Yanga ambayo imetoka kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Moro itawakaribisha Ndanda kwenye dimba la Taifa, jijini Dar es Salaam huku wageni hao wa ligi ambao walitoka kuwatoa nishai Kagera Sugar.
Vijana wa Jangwani ambao walikuwa nafasi ya pili katika msimamo kabla ya mechi zilizochezwa jana, wametamba kushinda mchezo huo wakiwa na nia ya kujiweka pazuri kwenye mbio zao za kurejesha taji hilo.
Yanga inayonolewa na kocha Hans van der Pluijm ina pointi 18 baada ya mechi 10 wakati wapinzani wao wakikamata nafasi ya 12 wakiwa na pointi 13 wakianza kuchanganya kasi tofauti na walipoianza ligi hiyo.
Kocha wa Ndanda, Meja Abdul Mingange alinukuliwa kuwa anatarajiwa upinzani mkali toka kwa Yanga, lakini vijana wake wapo tayari kupigana ili kuendeleza wimbi lao la ushindi baada ya kushinda mechi iliyopita.
Yanga itakayoiwakilisha Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho, inakabiliwa na mechi nyingine ngumu katikati ya wiki dhidi ya Coastal Union.
Mechi hiyo ya Yanga na Coastal Union itachezwa siku ya Jumatano  kwenye uwanja wa Mkwakwani, ikiwa ni mechi ya kiporo baina ya timu hizo baada ya mechi ya awali kuahirishwa ili Yanga ishiriki Mapinduzi Cup.
Wanayanga wanahamu ya kutaka kuona timu yao ikipata matokeo mazuri leo na mechi ya Jumatano baada ya awali kuzinguliwa na sare mbili mfululizo dhidi ya Azam na Ruvu Shooting kabla ya kuilaza Polisi.
Pambano jingine litakalochezwa leo katika mfululizo wa ligi hiyo ni lile la Ruvu Shooting watakaoikaribisha Stand United ya Shinyanga kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani.
Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire ametamba kuwa vijana wao wanaonolewa na kocha Tom Olaba wapo tayari kuvuna pointi tatu baada ya kuwatioa nishai na kuvunja mwiko wa Mtibwa wa kutofungwa katika ligi walipowazabua mabao 2-1 wiki iliyopita ikiwa ni siku chache walipong'ang'ania Yanga na kutoka 0-0.

DR Congo, wenyeji watangulia Nusu Fainali Afrika

Javier Balboa akishangilia moja ya mabao ya wenyeji Guinea ya Ikweta
Referee Rajindraparsad Seechurn is shielded from angry Tunisia players by security personal
Polisi wakimuokoa refa baada ya wachezaji wa Tunisia kuchukizwa na penati waliopewa wenyeji dakika za jioni
Guinea's midfielder Javier Balboa (bottom-R) celebrates with teammates after scoring their second goal
Wenyeji Guinea ya Ikweta wakishangilia ushindi wao dhidi ya Tunisia
Democratic Republic of the Congo's forward Jeremy Bokila (C) celebrates his goal in Bata
DR Congo wakipongezana walipowaduwaza majirani zao Congo-Brazzaville
Mbokani and Sagesse Babele go flying as they compete for the ball in a hotly contested game
Ilikuwa kama Vita baina ya Congo-Brazzaville na DR Congo
TIMU za DR Congo na wenyeji Guinea ya Ikweta zimekuwa timu za kwanza kufuzu Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kushinda mechi zao za Robo Fainali bila kutarajiwa.
DR Congo walityoka nyuma ya mabao 2-0 na kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Congo-Brazzaville katika mchezo uliochezwa mapema kabla ya wenyeji kuwang'oa kwenye muda wa ziada mabingwa wa zamani wa Afrika Tunisia kwa mabao 2-1.
Congo-Brazzaville walianza kuwashtua majirani zao dakika 10 baada ya kuanza kwa kipindi cha pili pale Ferebory Dore alipofunga bao la kuongoza kabla ya Thievy Bifouma kuongeza la pili dakika ya 62 baada ya kutokea piga nikupige langoni mwa DR Congo.
Hata hivyo DR Congo hawakukata tamaa baada ya kufungwa mabao hayo mawili na badala ake kucharuka na kurejesha bao moja baada ya jingine kupitia wachezaji wake nyota, Dieumerci Mbokani aliyefunga mabao mawili katika dakika ya 65 na 90, Jeremy Bokila dakika ya 75, na   Joel KImwaki aliyefunga bao la tatu dakika ya 81 na kuivusha timu yao nusu fainali tangu 1988.
Katika meechi ya pili iliyochezwa pia kwenye uwanja huo wa Bata usiku wenyeji waliwaduwaza Tunisia kwa kuwalaza mabao 2-1 wakichomoa bao dakika ya jioni na kumaliza dakika 90 kwa sare ya 1-1 kabla ya kufunga bao la ushindi kwenye muda wa nyongeza wa dakika 30.
Tunisia walianza kuandika bao lililokuwa likionekana kama limewavusha hatua ya nusu fainali kupitia kwa Ahmed Akaichi katika dakika ya 70, lakini Guinea ya Ikweta ilichomo dakika za ziada za pambano hilo kabla ya halijamalizika kupitia kwa Javier Balboa aliyefunga kwa penati, iliyozua zogo kwa wachezaji wa Tunisia kumlalamikia mwamuzi kiasi cha Polisi kuamua kuingilia kati kumuokoa mwamuzi huyo.
Dakika ya 102 Balboa tena aliwatoa kimasomaso wenyeji wa kufunga bao la pili ambalo lilidumu hadi mwisho wa mchezo na kuifanya Guinea ya Ikweta kufuzu kwa mara ya kwanza hatua hiyo na sasa wanasubiri mshindi kati ya Ghana na Guinea wanaocheza leo kwenye robo fainali nyingine wa michuano hiyo.
DR Congo wenyewe watasubiri kujua watacheza nani hatua ya nusu fainali kati ya Ivory Coast na Algeria ambazo zitakamilisha mechi za robo fainali usiku wa leo kwenye uwanja wa Malabo.

Saturday, January 31, 2015

Bingwa wa Taifa Wanawake kuzoa Mil.3

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhENRxfiE96-KL4ns71WPE2_XM1rUPglyqgf7sij2rgovmDsZi8fpyZJd_YZoswfB67v51e2xA3AoMNgNjzrK728L5tHgcMEVDmQ1vzukkgCK7lD5lb9wuNnWnoNjKAXtEuumAvIqQElrU/s1600/MUKA.jpg
Waziri Dk Fenella Mukangara atakayekuwa mgeni rasmi katika fainali za Kombe la Taifa la Wanawake
Na Boniface Wambura 
BINGWA wa michuano ya Kombe la Taifa Wanawake, inayodhaminiwa na kampuni ya Proin na atapata Kombe na fedha taslimu Sh. Milioni 3. 
Aidha, katika michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini, mshindi wa pili atapata Sh. Milioni 2, wakati mshindi wa tatu atapata Sh. Milioni 1.
Fainali ya Kombe la Taifa Wanawake itazikutanisha Pwani na Temeke kesho Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam na mashabiki wataingia bure.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye mechi hiyo itakayoanza Saa 10.15 jioni, ikichezeshwa na refa wa FIFA, Jonesia Rukyaa na kuonyeshwa moja kwa moja na televisheni ya Azam.
Marefa wasaidizi wanatarajiwa kuwa Hellen Mduma, Agnes Alphonce, na Mwanahamisi Matiku wakati Kamisaa atakuwa Ingridy Kimario. Timu za Ilala na Kigoma zitacheza mechi ya utangulizi kutafuta mshindi wa tatu kuanzia saa 8.00 mchana.

Bayern Munich waonja kipigo Bundesliga

Bas Dost scores
Bayern walivyokuwa wakiangamizwa na Wolfsburg
Pep Guardiola
Kocha wa Beyern Munich, Pep Guardiola akiwa haamini kama vijana wake wamemuangusha ugenini
MABINGWA watetezi wa Bundesliga, Bayern Munich jana ilikiona cha moto ugenini baada ya kunyukwa mabao 4-1 na Wolfoburg kikiwa ndicho kipigo cha kwanza kwao kwa msimu huu katika ligi hiyo.
Mabao mawili yaliyofungwa na Bas Dost katika dakika ya nne na 45 na mengine ya Kelvin De Bruyne ya dakika za 53 na 73 yalitosha kuwazima wababe hao wa Ujerumani ambao walipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 55 kupitia kwa Juan Bernat.
Licha ya kipigo hicho Bayern wameendelea kukalia kiti cha uongozi wa ligi hiyo wakiwa na pointi 45 na wapinzani wao waliowatoa nishai Wolfsburg waking'ang'ania nafasi ya pili wakiwa na pointi 37.
Ligi hiyo inaendelea jioni hii kwa michezo kadha kabla ya kesho kumalizia michezo mingine ya wikiendi hii.












Newcastle Utd yainyuka Hull City, Man Utd waongoza 3-0 HT

Sammy Ameobi (right) is congratulated after scoring for Newcastle
Wachezaji Newcastle waksihangilia moja ya mabao yao
Ahmed Elmohamady of Hull City punches the ball into the Newcastle net
Hekaheka langoni mwa Newcastle
Sammy Ameobi shoots to score for Newcastle
Sammy Ameobi akifunga bao la pili la Newcastle
KLABU ya Newcastle United ikiwa ugenini imetoa kipigo cha mabao 3-0 kwa wenyeji wao Hull City katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu ya England.
Newcastle walianza kuandika bao la kwanza dakika ya 40 kupitia kwa Remy Cabella kabla ya kuongeza bao la pili dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kupitia kwa Sammy Ameobi na katika dakika ya 78 Yoan Gouffran alimaliza udhia kwa kufunga bao la tatu na kuipa ushindi muhimu Newcastle United.
Kwa sasa michezo kadhaa ipo mapumziko huku Spurs wakiongoza mabao 2-0 dhidi ya West Bromwich, Everton ikiwa ugenini wanaongoza bao 1-0 dhidi ya Crystal Palace, Liverpool dhidi ya West Ham Utd wapo 0-0, Manchester United wanaongoza 3-0 dhidi ya Leiceister City uwanja wa Old Trafford, Stoke City wakiwa nyumbani wanaongoza 2-1 dhidi ya QPR na Sunderland wakiwa mbele kwa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Burnley.

Mnyama 'yaua' Taifa, Mbeya City yalala Moro 1-0

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQw0Q6Z99EoVWkyx9Yf4-SQu6v6ms0PaPb_sKenOOroi-QKbRnmecjHWsCkMjBGp9Gme9kVSLBI6loRiDVMNpxjyOidGhsx9k3uN8L4NzFcmC9SUT8cQrLUnJwL2a4pbDoK4TypzmK_ig/s1600/_HMB7014.JPG
Simba
JKT Ruvu
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/IMG-20140920-WA005311.jpg
Mbeya City iliyolala Morogoro

BAADA ya kuwaweka roho juu mashabiki wao, Simba jioni ya leo imezinduka mbele ya JKT Ruvu baada ya kuifunga JKT Ruvu mabao 2-1 na kupanda hadi nafasi ya saba.
Mabao mawili ya mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Dan Sserunkuma yameisaidia Simba kupata ushindi wake wa tatu katika Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye uwanja wa Taifa na Simba walianza kuandika bao mapema kabla ya JKT Ruvu kurejesha na kwenda mapumziko matokeo yakiwa bao 1-1.
Bao la Simba lililofungwa na Sserunkuma liliwekwa kimiani katika dakika ya pili tu ya pambano hilo akiunganisha krosi pasi ya Emmanuel Okwi.
Hata hivyo JKT Ruvu walikuja kusawazisha bao hilo dakika ya 19 kwa George Minja kuunganisha kwa kichwa mpira wa Jabir Aziz na kufanya timu ziende mapumziko zikiwa nguvu sawa.
Sserunkuma aliihakikishia Simba ushindi baada ya kufunga bao la pili katika dakika ya tatu baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kewa kichwa akiwahi mpira wa krosi ya Okwi na kusaidia Simba kulipa kisasi kwa maafande hao ambao waliwafunga mabao 3-2 walipokutana mara ya mwisho.
Kwa ushindi huo Simba imefikisha pointi 16 na kuchupa kutoka nafasi ya 11 hadi nafasi ya saba.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo Mtibwa Sugari imejikuta ikichupa hadi nafasi ya pili ya msimamo ikiziengua Yanga na JKT Ruvu baada ya kupata suluhu ya bila kufungana dhidi ya Coastal Union.
Mtibwa Sugar ilipata sare hiyo uwanja wa Mkwakwani Tanga na kufikisha pointi 18 sawa na ilizonazo Yanga waliokuwa wa pili ambao wanashuka hadi nafasi ya tatu japo kesho itashuka dimbani kuumana na Ndanda na kuwa na nafasi ya kukwea kileleni.
Nayo timu ya Polisi Moro imefanikiwa kuinyuka Mbeya City bao 1-0 ikiwa ni sikui chache tangu Mbeya City kutoka  kuilaza Simba 2-1 katikati ya wiki kwenye mechi yao ya kiporo kilichochezwa uwanja wa Taifa.
Mjini Mbeya wenyeji Prisons ililazimishwa sare ya 1-1 na wageni wao Kagera Sugar katika mchezo unaodaiwa ulikuwa mkali na wa kusisimua wenyeji walianza kuzinguliwa kwa bao la Rashid Mandawa kabla ya kuchomoa dakika 15 kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kupitia Nurdin Chona..
Katika mfululizo wa ligi hiyo kesho, Yanga itaikaribisha Ndanda kwenye uwanja wa Taifa wakati Ruvu Shooting wataialika Stand United ya Shinyanga kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani.

Friday, January 30, 2015

NGOMA MPYA YA MATONYA-HOMA YA JIJ

Ngoma mpya ya Matonya - Homa Ya Jiji.mp3 @Hulkshare:

Chelsea yakaribia kumnasa Cuadrado

http://resources2.news.com.au/images/2015/01/27/1227198/061530-6ca4ddec-a5bb-11e4-a11e-9d15a37a8504.jpg
Juan Cuadrado anayekaribia kutua Chelsea
VINARA wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Chelsea ipo katika hatua za mwisho kukamilisha dili la Pauni Mil. 23.3 ili  kumsajili winga wa Fiorentina Juan Cuadrado, 26.
Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia tayari ameshafikia makubaliano kuhusu mambo yake binafsi na Chelsea na kwa sasa klabu ziko katika hatua za mwisho kukamilisha uhamisho huo.
Inakadiriwa kuwa Chelsea watatoa kitita cha Pauni Mil.26.8 kwa ajili ya winga huyo kiasi ambacho ndio kilichowekwa na klabu yake hiyo ya Italia sambamba na kudaiwa kuwa mbioni kumtoa kwa mkopo kinda lake Mohamed Salah, 22 kwa klabu hiyo ya Fiorentina ikiwa ni sehemu ya kukamilisha dili hilo.
Hata hivyo, Salah ambaye ni winga wa kimataifa wa Misri bado hajaamua kama anataka kwenda kucheza Serie A au sehemu gani nyingine.
Aidha imedokezwa kuwawinga nyota wa Chelsea, Andre Schurrle yupo katika mazungumzo ya kutua klabu ya Bundesliga,Wolfsburg.

HII NDIYO TANZANIA BHANA YENYE AMANI NA UTULIVU!


Simba katika mtihani mwingine, kulipa kisasi kwa JKT kesho?

Simba watavuna nini kesho kwa JKT
JKT Ruvu kuendeleza machungu Msimbazi?
WAKATI Kocha Msaidizi wa Simba, Seleman Matola akiomba kuachia ngazi mwenyewe ndani ya klabu hiyo, timu hiyo kesho itakuwa na kibarua kingine kigumu mbele ya maafande wa JKT Ruvu katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.
Katika mechi ya mwisho baina ya timu hizo msimu uliopita, Simba ilicharazwa mabao 3-2 na maafande hao hali inayofanya mechi ya kesho miongoni mwa mechi zitakazochezwa katika viwanja tofauti kuwa ni kama vita ya kisasi.
Simba na JKT wataumana kwenye uwanja wa Taifa, huku timu hizo zikiwa na matokeo tofauti katika mechji zao zilizopita, Simba ikitoka kupokea kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City wakati JKT Ruvu wakilazimishwa sare ya 1-1 na Mgambo JKT.
Mechi nyingine zitakazopigwa kesho ni pamoja na zile za timu za Coastal Union dhidi ya Mtibwa Sugar mchezo utakaochezwa uwanja wa Mkwakwani Tanga, huku Prisons Mbeya itawalika Kagera Sugar uwanja wa Sokoine Mbeya na Polisi Moro waliotoka kucharazwa bao 1-0 na Yanga wataialika Mbeya City uwanja wa Jamhuri.
Mechi ya Mgambo JKT na Azam yenyewe imeahirishwa kwa kuwa Azam wapo DR Congo wakicheza mechi za kirafiki za michuano maalum.
Ligi hiyo itaendelea Jumapili kwa michezo miwili Yanga itaikaribisha Ndanda ya Mtwara na Ruvu Shootimng itavaana na Stand United kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani.
Mpaka sasa katika ligi hiyo Azam wapo kileleni wakiwa na pointi 21 wakifuatiwa na Yanga wenye pointi 18 sawa na JKT Ruvu.
Katika hatua nyingine uongozi wa Simba umesema umepata taarifa za Kocha Msaidizi wa timu yao Seleman Matola kutokana na kile kinachoelezwa kuwa kuitingwa na majukumu, japo inaelezwa kusakamwa na baadhi ya wanachama na viongozi wa klabu hiyo ni sababu ya Matola kuamua kubwaga manyanga.
Uongozi wa Simba kupitia Rais wake, Evance Aveva umesema kuwa umemtaka kocha huyo kuandika maombi yake kimaandishi ili kuyajadili na kutoa maamuzi, sambamba na kutoa sababu ya timu yao kuwa na matokeo mabaya katika mechi za karibuni kuwa inatokana na uchovu wa wachezaji kucheza mfululizo.
Wakati ligi ikiingia kwenye raundi ya 13 wikiendi hii chini ni msimamo na orodha ya wafungaji mpaka sasa.
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                                P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Azam                 11  06  03  02  15  08  07   21
02. Yanga                10  05  03  02  12   07  05  18
03. JKT Ruvu           12  05  03  04   12   11  01  18
04. Mtibwa Sugar     10  04  05  01  13  07  06   17
05. Coastal Union    11  04  04   03  10   08  02  16
06. Polisi Moro         12  03  06  03   09  09  00  15
07. Mbeya City         11   04  03  04  08   09  -1   15
08. Ruvu Shooting    12  04  03   05   07   09  -2  15
09. Kagera Sugar     12  03  05  04   09   10   -1  14
10. Mgambo JKT      11  04  02  05   06    10  -4  14
11. Simba                11  02  07   02   11   10  01  13
12. Ndanda Fc          12  04  01   07  12    17  -5  13
13. Stand Utd           12  02  05   05   07   14  -7  11
14. Prisons               11  01  06   04   08   10  -2   09
Wafungaji:

7- Didier Kavumbagu(Azam)
6- Samuel Kamuntu (JKT Ruvu)
5-Ame Ali (Mtibwa), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Danny Mrwanda (Yanga)
4- Rama Salim (Coastal),  Simon Msuva (Yanga),  Emmanuel Okwi (Simba)
3- Ally Shomari (Mtibwa),  Jacob Massawe (Ndanda), Nassor Kapama (Ndanda)

Gerrard Pique, Shakira wapata mtoto wa pili

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/08/Shakira-Gerard-Pique-Milan.jpg
Shakira na Pique wakiwa na Milan
BEKI wa Barcelona, Gerard Pique na mwanamuziki nyota Shakira wamepata mtoto wao wa pili aliyezaliwa usiku wa jana.
Shakira alijifungua mtoto wa kiume bila matatizo yeyote katika hospitali ya Quiron Tecknon iliyopo jijini Barcelona.
Pique, 27 na mwanamuziki huyo wa Pop kutoka Colombia mwenye umri wa miaka 37, walitoa taarifa hizo muda mfupi kabla ya usiku wa manane.
Jina la mtoto ambaye amezaliwa miaka miwili baada ya wawili hao kupata mtoto wao wa kwanza aitwaye Milan Piqué Mebarak, ni Sasha Piqué Mebarak.
Wawili hao wamekuwa pamoja toka mwaka 2010 walipokutana katika michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika nchini Afrika Kusini.

Diego Costa majanga! Afungiwa England

The Spain striker celebrates his goal in the 2-0 Premier League win over West Ham
Diego Costa aliyefungiwa mechi tatu kwa kosa la kumtimba Emre Can
STRIKA mkali wa klabu ya Chelsea, Diego Costa amefungiwa mechi tatu kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa Liverpool Emre Can.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 anatarajiwa kuukosa mchezo wa Ligi Kuu kati ya timu yake na Manchester City utakaochezwa Stamford Bridge kesho pamoja na mechi dhidi ya Aston Villa na Everton. Chama cha Soka cha Uingereza-FA kilimtwanga adhabu hiyo ambayo Costa aliipinga kuhusiana na tukio lake alilofanya katika dakika ya 12 ya mchezo wa nusu fainali ya mkondo ya pili wa Kombe la Ligi uliofanyika Jumanne iliyopita.
Costa aliyesajiliwa kwa kitita cha Pauni Mil. 32, ameshafunga mabao 17 katika mechi 19 za Ligi Kuu alizocheza simu huu.
Tukio hilo halikuonwa na waamuzi lakini lilinaswa katika picha za video na FA kutumia kama ushahidi wa kumtia adabu mshambuliaji huyo ambaye alikuwa akitetewa na kocha wake, Jose Mourinho.

ROBO FAINALI AFCON 2015 NI VITA TUPU!

*Wakongo kumaliza ubishi kesho, Ghana, Guinea balaa

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/74471000/jpg/_74471882_161377467.jpg
Taji linalosubiri mbebaji wake
http://static.allsports.com.gh/img/incoming/origs3434059/431253271-w1280-h960/DR-Congo-National-team.jpg
DR Congo
http://www.redpepper.co.ug/wp-content/uploads/2015/01/eq.jpg
Wenyeji Guinea ya Ikweta
FAINALI za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON- 2015) yamefikia patamu wakati kesho timu nane zilizofanikiwa kupenya kutoka kwenye makundi zitaanza kutupa karata zao katika mechi za Robo Fainali kuwania kucheza Nusu Fainali baadaye wiki ijayo.
Guinea ambayo ililinagana kila kitu na Mali katika nafasi ya pili ya Kundi D lililoongozwa na Ivory Coast jana ilipenya kwa kupitia turufu ya kura na kurejesha matukio matatu kama hayo kuwahi kushuhudiwa kwenye michuano mikubwa duniani ya Kombe la Dunia 1954 na 1990 pamoja na Kombe la Mataifa mwaka 1988.
Guinea na Mali zilishindwa kutambiana katika mechi yao ya mwisho kwa kutoka sare ya 1-1 ikiwa ni sare zao za tatu baada ya awali kufanya kama hivyo mbele ya Ivory Coast na Cameroon iliyooaga mashindano kwa kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa vinara wa kundi hiyo Tembo wa Ivory.
Ndipo Shirikisho la Soka Afrika (CAF) likaamua kuzipambanisha timu hizo katika kapu la sadakarawe na Mali kuangusha kuwapisha wenzao kuendelea ambapo sasa Guinea wamepangwa kuumana na Ghana katika mechi ya tatu ya Robo fainali itakayochezwa siku ya Jumapili jioni.
Mechi zitakazochezwa kesho kwa mujibu wa ratiba ni Congo Brazzaville dhidi ya wapinzani wao wa jadi DR Congo pambano litakalochezwa saa 1 jioni kwenye uwnaja wa Bara kabla ya wenyeji Guinea ya Ikweta kupepetana na Tunisia katika mechi isiyotabirika kutokana na timu hizo kumaliza katika uwiano sawa kwenye makundi yao.
Wakongo wameshakutana mara tano katika michezo mbalimbali ya karibuni tangu mwaka 2000 na timu hizo zimeshindw akutambiana kwa kila mmoja kushinda mara mbili na kutoka sare moja.
Kupenya kwa Guinea kwa kutupia turufu ya sadakarawe inakumbusha michuano ya fainali za Kombe la Dunia za mwaka 1954 wakati Ugiriki ilipowazidi kete Uholanzi
Katika fainali hizo Ugiriki na Hispania zililingana katika kundi lao na turufu ikawabeba Ugiriki kwenda kwenye fainali na tuykio hilo lilijirudia tena kwenye fainali za mwaka 1990 Ireland iliibwaga Uholanzi katika zoezi kama hilo.
Katika fainali za Afrika za mwaka 1988 Algeria ilipenya mbele ya Ivory Coast baada ya kulingana kila kitu.
Mbali na michezo hiyo ya kesho, Jumapili kutakuwa michezo miwili kubwa linalosubiriwa kwa hamu kubwa ni Ivory Coast dhidi ya Algeria litakalochezwa usiku wa saa 4:30 huku Tembo wakiwa na wasiwasi na hali ya kiafya ya nahodha wao, Yaya Toure.
Timu zitakazofuzu hatua hiyo zitakutana kwenye nusu fainali zitakazochezwa katikati ya wiki kabla ya kufahamika timu mbili zitakazocheza Fainali itakayopigwa Februari 8 na kupatikana kwa bingwa mpya wa michuano hiyo baada ya wlaiokuwa watetezi Nigeria kukwama kwenye kwenye fainali hizo za Guinea ya Ikweta.

VUMBI LA LIGI KUU ENGLAND WIKIENDI HII LIPO HIVI

http://www.footballgate.com/wp-content/uploads/2014/09/barclays-english-premier-league-wallpaper-2014-2015-790x444.jpgKIVUMBI cha Ligi Kuu England kinatarajiwa kuendelea tena wikiendi hii baada ya wiki iliyopita kusimama kupisha Raundi ya nne ya Kombe la FA na mechi za Nusu Fainali ya Kombe la Ligi (Capital One).
Chelsea ambao wamefanikiwa kufuzu Fainali za Kombe la Ligi kwa kuvaana na Tottenham Hotspur Machi Mosi kwenye uwanja wa Wembley, itashuka dimbani kesho kuvaana na Mabingwa Watetezi, Manchester City.
Kwa mujibu wa ratiba ya mechi hizo za wikiendi hii Kesho kutakuwa na mechi nane zitakazokutanisha timu 16 kabla ya Jumapili kushuhudiwa mechi mbili tu ambazo zitazikutanisha timu nne.
Mechi za kesho zipo hivi:
Hull City15:45 Newcastle United
Crystal Palace  18:00  Everton
Liverpool  18:00 West Ham United
Manchester Utd 18:00 Leicester City
Stoke City    18:00 Queens Park Rangers
Sunderland  18:00  Burnley      
West Bromwich 18:00 Tottenham Hotspur   

Chelsea  20:30 Manchester City
Jumapili:

Arsenal     16 : 30     Aston Villa     
Southampton   19:00 Swansea City

KUMEKUCHA SIMBA! WANACHAMA WATAKA MKUTANO

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi1rzqcYY91IP82IKEyguMFJWPC4hCQgVwYhX3RKM0wUWMMuRH11c_EXojxJd1liCSgl-5xR3eMAFwHxHQxLf1A63zvgEBMnmQv-b_GOPlE8nQo6YIctaW4NKlP7YZhAd43uG-OnVBeNiY/s1600/hans+poppe+na+aveva.jpg
Rais Evance Aveva akiwa na Mwenyekiti wa kamati ya usajili Zakaria Hanspop
KUFUATIA timu yao kupata kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa wageni Mbeya City kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam juzi, wanachama wa klabu ya soka ya Simba wanautaka uongozi wa klabu yao kuitisha mkutano mkuu wa dharura ili kujadili mwenendo mbaya wa kikosi chao kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Simba juzi ilipoteza mechi yake ya pili msimu huu na kuangukia katika nafasi ya 11 kwenye msimamo ligi hiyo ya timu 14 ikiwa imetoka sare mara saba na kushinda mechi mbili tu.
Akizungumza kwa niaba ya wanachama wenzake, Mwenyekiti wa Tawi la Mpira Pesa lililoko Magomeni jijini Dar es Salaam, Ustadh Masoud, alisema kwamba wanauomba uongozi kuitisha mapema mkutano ili waweze kupata suluhisho kabla ya 'jahazi' halijazidi kuzama.
Masoud alisema kwamba kupitia mkutano wa wanachama, wanaamini watafahamu kinachosababisha timu yao kufanya vibaya kwenye mechi zake za ligi na kupoteza matumaini ya kutwaa ubingwa.
Alisema pia wamebaini ndani ya uongozi hakuna umoja na baadhi yao wanaingilia majukumu ya watu wengine.
"Mwenendo wa timu hauturidhishi kabisa, ndiyo maana tumeomba viongozi waitishe mkutano wa dharura, tayari tumeshapeleka barua kuwaomba mkutano haraka," alisema mwenyekiti huyo wa kundi maarufu na lenye nguvu ndani ya Simba.
Aliongeza kwamba pia hawana imani na baadhi ya viongozi waliopo kwenye benchi la ufundi na kuutaka uongozi ulifanyie kazi.
Mashabiki wa klabu hiyo na wanachama walisikika wakisema baada ya mechi yao ya juzi kuwa Simba si shule ya soka, ni klabu kubwa inayopaswa kupigania mataji hivyo viongozi wanapaswa kusajili wachezaji walioiva tayari na kwamba vijana waingizwe wachache taratibu kupewa uzoefu tofauti na ilivyo sasa.
Simba juzi iliwatumia yosso saba Manyika Peter, Hassan Isihaka, Mohamed Hussein 'Tshabalala', Jonas Mkude, Twaha Ibrahim, Ibrahim Hajib na Ramadhani Singano.
Rais wa Simba, Evans Aveva, alisema kuwa amepata taarifa za wanachama hao kuomba mkutano na kueleza kwamba mkutano utafanyika kwa kufuata programu iliyoandaliwa na si vinginevyo.
Aveva alisema kwamba Kamati ya Utendaji itakutana kupanga siku ya mkutano si kwa kufuata maelekezo ya wanachama.
"Mkutano utafanyika kwa kufuata programu, tutakutana wakati wowote ili kupitisha tarehe ya mkutano, hatuwezi kufanya kitu kilichoko nje ya utaratibu na kalenda ya mwaka," alisema.
Rais huyo alisema pia yeye binafsi hafurahishwi na matokeo hayo na kuwataka wanachama na mashabiki kuwa watulivu kwenye kipindi hiki.
"Tunawapa wachezaji wetu kila kinachotakiwa, ila matokeo yanayopatikana si mazuri, inatuuma na kutuchanganya sisi pia," alisema Aveva.
Baada ya kichapo cha juzi, Simba inaendelea na mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mechi yake dhidi ya JKT Ruvu itakayofanyika kesho kwenye Uwanja wa Taifa jijini.

Uwanja wa Real Madrid kubadilishwa jina

http://www.larbes.com/photos/2010/1023-1110/large/image045.jpg
Uwanja wa Santiago
KLABU ya Real Madrid inajipanga kubadili jina la Uwanja wake wa Santiago Bernabeu ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya udhamini na Kampuni ya Kimataifa ya Uwekezaji ya Petroli-IPIC yenye maskani yake Umoja wa Falme za Kiarabu. Wawili walikubali kushirikiana katika mkataba unaoaminika kuwa na thamani ya euro milioni 500 itakazovuna Madrid katika kipindi cha miaka 20 ijayo kuanzia Octoba mwaka huu. Mkataba huo unajumuisha haki ya kubadili jina la uwanja ambao umekuwa nyumbano kwa timu hiyo toka mwaka 1947. Uwanja huo pia ndio uliochezewa mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1982. Sasa inaaminika uwanja huo utakuwa ukiitwa The Abu Dhabi Santiago Bernabeu. Rais wa klabu hiyo Florentino Perez amesizitiza kuwa urithi wa uwanja huo utaheshimiwa kwa kuendelea kubaki na neno Santiago Bernabeu. Perez amesema dhumuni kubwa la udhamini huo ni pamoja na kuukarabati upya uwanja huo na kuuongeza mpaka kufikia uwezo wa kubeba mashabiki 91,000 kutoka 81,000 wa hivi sasa