KOCHA wa zamani wa klabu ya Yanga, Kennedy Mwaisabula, ameungana na kocha wa Mtibwa Sugar, Tom Olaba kuilalamikia kadi nyekundu aliyopewa kipa Shaaban Kado, siku chache kabla ya kuvaana na timu ya Simba.
Kado, anayeichezea pia timu ya taifa, Taifa Stars, alionyeshwa kadi hiyo katika mechi baina ya timu yake na Toto Afrika na kumfanya alikose pambano la kesho dhidi yao na Simba litakalochezwa kwenye uwanja wa Uhuru, jijini Dar.
Mwaisabula maarufu kama 'Mzazi' alisema kitendo cha Kado kulikosa pambano la kesho limepunguza ladha kutokana na ukweli kipa huyo ndiye mhimili wa Mtibwa Sugar na hivyo kuipungizia nguvu timu yake.
Kocha huyo aliyewahi kuzinoa timu kadhaa ikiwemo Bandari-Mtwara, Cargo, Twiga Sports, Villa Squad na TMK United, alisema kwa jinsi mazingira ya kadi hiyo ilivyotolewa huko Mwanza anahisi kama kuna 'mchezo mchafu'.
Alisema japo hana hakika, lakini huenda kadi hiyo imetolewa kwa nia ya kuidhofisha Mtibwa katika mechi yao ya kesho, kitu alichodai mambo kama hayo yanachangia kuporomosha kiwango cha soka la Tanzania.
"Nadhani ifikie wakati mambo kama haya ya ujanja ujanja kwa nia ya kuzibeba timu kubwa zikaachwa ili soka lisonge mbele, nimesikitishwa na kadi ya Kado kwa vile imepunguza msisimko kwa pambano lao na Simba," alisema.
Kauli ya Mwaisabula imekuja siku chache, tangu kocha wa Mtibwa, Mkenya Tom Olaba kulalamikia kadi hiyo iliyotolewa na mwamuzi Judith Gamba, akidai imeinyong'onyesha timu yake kwa ajili ya pambano hilo dhidi ya Simba.
Kado alipewa kadi na mwamuzi huyo baada ya kuilalamikia penati iliyopewa wenyeji wao, Toto Afrika ambapo pambano lilishia kwa Mtibwa kushinda 2-1.
STRIKA

USILIKOSE

Friday, February 25, 2011
Mabondia kuzipiga kuwachangia wahanga wa mabomu

MABONDIA mbalimbali kutoka mikoa tofauti wanatarajiwa kupigana katika michuano maalum kwa nia ya kusaka fedha za kuwasaidia wahanga wa milipuko ya mabomu ya Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam.
Michuano hiyo itakayochezwa sehemu nne tofauti ndani ya mikoa ya Dar, Pwani na Morogoro, imeratibiwa na kampuni ya Funiko Inc, chini ya uratibu wa mkurugenzi wake, Rowland Raphael Chulu 'Chen Lee Master'.
Chulu alisema michezo ya kwanza itafanyika kwenye ukumbi wa Hugho Tower Pub, Kigogo-Mburahati Machi 6, ambapo yeye atapigana na K kutoka Tanga pamoja na kusindikizwa na mapambano mengine ya utangulizi.
Aliwataja mabondia wengine watakaopigana siku hiyo ni Deus Tengwa atakayepigana na Kitonge wa Arusha, Abbas dhidi ya Abuu, Rahim Cobra na Abdul, Masoud Fighter dhidi ya Mrisho Mwana, Husseni Magali na Idd Rashid na Said Omary atapigana na Jembe wa Majembe.
"Pambano la pili litafanyika Machi 13 eneo la Bunju kwenye ukumbi wa Proud Tanzania, ambapo nitarudiana na K, na wiki inayofuata tutakuwa Bagamoyo kwenye ukumbi wa Police Mass ambapo nitachapana na Juma wa huko huko," alisema.
Alisema onyesho la tatu litachezwa kwenye ukumbi wa Makuti-Pub, Ifakara mkoani Morogoro kwa kuumana na Charles wa huko wakisindikizwa na michezo mingine ya utangulizi.
Chulu, aliyewahi kung'ara kwenye Kick Boxing kabla ya kutumbukia kwenye utayarishaji wa filamu nchini, alisema fedha zote zitakazopatikana kwenye maonyesho ya michezo hiyo zitapelekwa kwa wahanga.
Tangu tukio la milipuko ya mabomu litokee wiki mbili zilizopita watu mbalimbali wamekuwa wakitolea kuwasaidia wahanga, ambapo kesho kwenye uwanja wa Uhuru wasanii wa Bongofleva na wale wa filamu wataumana kusaka fedha za kuwasaoidia wahanga hao wa Gongo la Mboto.
Mwisho
Thursday, February 24, 2011
20% kuzindua Malumbano J'pili
MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abbas Hamis Kinzasa '20 Percent' anatarajia kuzindua na kuitambulisha rasmi albamu yake mpya iitwayo 'Ya Nini Malumbano' siku ya Jumapili.
Uzinduzi huo utakaosindikizwa na wasanii kadhaa nyota nchini unatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Club Masai, Oysterbay jijini Dar es Salaam chini ya utaribu wa kampuni ya King Kif Entertainment.
Akizungumza na Micharazo leo asubuhi, mkurugenzi wa kampuni hiyo, Sigfred Kimasa 'King Kiff', alisema maandalizi ya onyesho hilo yamekamilika ikiwemo wasanii nyota kibao kukubali kumsinidikiza mkali huyo ambaye anasifika kwa nyimbo zenye mafunzo na ujumbe mwanana.
"Msanii 20 Percent atazindua albamu yake ya Ya Nini Malumbano, akisindikizwa na wasanii kadhaa nyota, katika onyesho litakalofanyika Jumapili kwenye ukumbi wa Club Maisha," alisema.
Aliwataja wasanii watakaomsindikiza mkali huyo ambaye pia ni mahiri katika uigizaji filamu ni pamoja na 'swahiba' wake, Seleman Msindi 'Afande Sele'. Man Wter ambaye pia ni mtayarishaji wa albamu hiyo, Ney wa Mitego, Sajna, Linex na Uncle G.
Mbali na kibao cha Ya Nini Malumbano, albamu hiyo ya 20 Percent ina nyimbo nyingine kama Tamaa Mbaya ambao umekuwa ukitamba kwenye vituo kadhaa vya redio nchini, Neno la Mwisho na Nimerudi Salama.
Nyimbo nyingine ni Nyerere, Nia Yao, Mwema, Naficha, Kubadili Mwendo na Ya Nini Malumbano.
Hiyo ni albamu ya tatu ya msanii huyo ambaye anatamba pia na nyimbo za Money Money, Bangi na nyingine, awali alitoa albamu za Money Money na Mama Neema ambazo zinadaiwa kufanya vema sokoni licha ya nyimbo zake kumpa tuzo kadhaa za muziki nchini.
.
Tuesday, February 22, 2011
Dokii ana scandal na JB
MSANII nyota wa muziki na filamu, Ummy Wenceslaus 'Dokii' amefyatua kazi yake mpya iitwayo 'Scandal' iliyowashirikisha wakali kadhaa wa fani hiyo nchini.
Filamu hiyo inayozungumzia masuala ya mapenzi na hila za baadhi ya watumishi wa Mungu, inatarajiwa kuachiwa mitaani kuanzia mwezi ujao ikiwa imetungwa na Dokii mwenyewe na kuongozwa na Adam Kuambiana.
Akizungumza na micharazo, Dokii, aliyeng'ara na michezo ya kuigiza kupitia kituo cha ITV akiwa na kundi la Mambo Hayo, alisema ndani ya filamu hiyo aliyoitunga mwenyewe, kuna wasanii mahiri kama Jacob Stephen 'JB'.
"Baada ya kimya tangu nilipoachia filamu ya Money Transfer, nimekamilisha kazi mpya iitwayo Scandal' ambayo nimeigiza na wasanii kadhaa nyota akiwemo mkali, JB, Colleta Raymond, Tini White na wengine," alisema Dokii.
Dokii aliwataja wasanii wengine waliopo ndani ya filamu hiyo ni pamoja na Jacqueline Pentezel 'Jack wa Chuz', Ramadhani Ally 'Taff', Tini White, Kishoka na wengine.
"Ni filamu ya kusisimua kwa jinsi ilivyoigizwa na ujumbe uliopo ndani ya kazi hiyo mpya," alisema Dokii.
Dokii, ambaye pia ni muimbaji wa muziki wa Injili amewahi kutamba na filamu kama Yoland, Hard Love Moro, Bad Friend, My Nephew, Lonely Heart na nyinginezo.
Kwa muda mrefu msanii huyo alikuwa wakiwachanganya mashabiki wake wakidhani ni Mkenya kutokana na kupenda kwake kuigiza lafudhi ya taifa hilo, ingawa ukweli yeye ni mwenyeji wa mkoa wa Morogoro.
Mwisho
Msalaba Wangu upo kwa Teddy
MTUNZI anayekuja juu katika fani ya utunzi wa riwaya, Teddy Chacha, amejitosa kwenye filamu na kuibuka na kazi mpya iitwayo 'Msalaba Wangu'.
Filamu hiyo inayozungumzia masuala ya kijamii na hasa kuwepo kwa imani potofu juu ya watu wenye ulemavu, imeshirikisha 'vichwa' kadhaa nyota vya fani ya uigizaji nchini akiwemo Pembe, 'Bi Hindu' na Charles Magali 'Mzee Magali'.
Akizungumza na Micharazo, Teddy alisema filamu hiyo ni zao la moja ya hadithi zake zinazochapishwa kwenye magazeti mbalimbali likiwemo NIPASHE, ambapo inazungumzia familia moja inayomkataa mtoto wao aliyezaliwa mlemavu wa akili.
Teddy, alisema filamu hiyo ni kama simulizi la kweli kutokana na kisa alichowahi kusimuliwa na kusema ni moja ya kazi yenye kuelimisha na kuiasa jamii juu ya kuepukana na mila na desturi potofu.
"Ni moja ya kazi yenye mafunzo na hasa kutokana na wahusika kubeba uhusika wao kwa kiwango cha hali juu," alisema Teddy.
Aliongeza kuwa filamu hiyo aliyotunga na kuiongoza mwenyewe, imerekodiwa na kampuni ya Magambo Entertainment na kwa sasa inamalizwa kuhaririwa kabla ya kutafutiwa soko tayati kuwapa wadau wa filamu burudani yenye mafunzo kwao.
Teddy, aliwataja washiriki wa filamu hiyo ni pamoja na Pembe, Bi Hindu, Mzee Magali, mtoto Yasin Kamba ambaye ndiye mhusika mkuu, Mohammed Hamis, Josephine Joseph na wengine.
Filamu hiyo inayozungumzia masuala ya kijamii na hasa kuwepo kwa imani potofu juu ya watu wenye ulemavu, imeshirikisha 'vichwa' kadhaa nyota vya fani ya uigizaji nchini akiwemo Pembe, 'Bi Hindu' na Charles Magali 'Mzee Magali'.
Akizungumza na Micharazo, Teddy alisema filamu hiyo ni zao la moja ya hadithi zake zinazochapishwa kwenye magazeti mbalimbali likiwemo NIPASHE, ambapo inazungumzia familia moja inayomkataa mtoto wao aliyezaliwa mlemavu wa akili.
Teddy, alisema filamu hiyo ni kama simulizi la kweli kutokana na kisa alichowahi kusimuliwa na kusema ni moja ya kazi yenye kuelimisha na kuiasa jamii juu ya kuepukana na mila na desturi potofu.
"Ni moja ya kazi yenye mafunzo na hasa kutokana na wahusika kubeba uhusika wao kwa kiwango cha hali juu," alisema Teddy.
Aliongeza kuwa filamu hiyo aliyotunga na kuiongoza mwenyewe, imerekodiwa na kampuni ya Magambo Entertainment na kwa sasa inamalizwa kuhaririwa kabla ya kutafutiwa soko tayati kuwapa wadau wa filamu burudani yenye mafunzo kwao.
Teddy, aliwataja washiriki wa filamu hiyo ni pamoja na Pembe, Bi Hindu, Mzee Magali, mtoto Yasin Kamba ambaye ndiye mhusika mkuu, Mohammed Hamis, Josephine Joseph na wengine.
Aisha Bui: Kisura anayetamba Bongo Movie

HANA muda mrefu tangu atumbukie kwenye faini ya uigizaji, lakini makali yake kupitia baadhi ya kazi alizoshiriki, zimemfanya Aisha Fat'hi maarufu kama Aisha Bui, kuwa tishio kwa waigizaji wakongwe wa kike.
Mwenyewe anakiri aliingia rasmi kwenye fani hiyo mwaka juzi kutokana na kuvutiwa na Wema Sepetu, licha ya kudai alipenda uigizaji licha ya kutowahi kujaribu tangu alipokuwa mdogo.
"Wema ndiye aliyechangia kujiingiiza kwangu kwenye filamu kutokana na kuvutiwa nae, ila tangu utotoni nilikuwa naipenda fani hiyo sambamba na ile ya uchoraji," alisema.
Alisema alipenda sana kuchora utotoni, kipaji ambacho anaamini kama angekiendeleza angefika mbali kwa vile alikuwa mahiri kuliko maelezo.
Filamu yake ya kwanza kumtangaza mwanadada huyo ni My Book, kisha kushiriki zingine kama Saturday Morning, Better Days, Not Without My Son, Continous Love na sasa ameibuka na Second Wife.
Aisha anayependa kuogelea, kufanya mazoezi na kupika, alisema kati ya kazi zote alizoshiriki ile ya Saturday Morning ndio filamu bomba kwake kwa jinsi alivyoigiza kwa umahiri.
"Saturday Morning, ndiyo picha kali kwangu wala sio siri," alisema kisura huyo.
Akiwa na ndoto za kuja kuwa muigizaji wa kimataifa, Aisha anasema hakuna anachochukia maishani mwake kama dharau ya uongo.
"Uongo na kufanyiana dharau ni vitu nisivyopenda maishani mwangu,"
Aisha Fat'hi aliyezaliwa mwaka 1983, alisema fani ya filamu nchini inazidi kupiga hatua, ingawa alisema bado haijawa na tija ya kutosha kutokana na kuwepo kwa wizi wa wajanja wachache.
Kisura huyo ambaye waliwahi kuhusishwa na marehemu Meddy Mpakanjia, hajaolewa wala
hana mtoto na mipango yake ni kujikita zaidi katika fani hiyo ili afike mbali ikiwezekana aje kumiliki kampuni yake binafsi ya kuzalisha filamu.
"Hizi ndizo ndoto zangu, kutamba kimataifa na kuja kumiliki kampuni yangu binafsi," alisema.
Aisha, alisema kwa umri wake na kiu ya mafanikio aliyokuwa nayo naamini atafika huko
akutakapo, muhimu Mungu amjalie umri na afya njema.
Saturday, February 19, 2011
Nyalawila apigiwa debe, Cheka ajipanga
MAPROMOTA wa Ngumi za Kulipwa nchini, wameombwa kujitokeza kumuandalia pambano la utetezi Bingwa wa Dunia wa WBF, Karama Nyalawila, ili asipoteze taji hilo.
Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBO, Yasin 'Ustaadh' Abdalla, alisema ili kumuepushia Nyalawila asipoteze taji lake alilotwaa mwishoni mwa mwaka jana nchini Ukraine ni vema mapromota wakajitokeza kumuandalia pambano la utetezi.
Ustaadh, alisema kwa kanuni zilizopo katika mchezo huo, bingwa yeyote akikaa muda mrefu bila kupigana, hupoteza sifa ya kushikilia taji na hivyo anahofia yasije yakamkuta Nyalawila.
"TPBO tunawaomba waratibu wa michezo ya ngumi za kulipwa nchini kumuandalia pambano Nyalawila ili kutetea taji na kuepuka kulipoteza taji hilo lenye hadhi kubwa katika mchezo huo duniani," alisema Usraadh.
Rais huyo alisema oganaizesheni yake ipo tayari kufanya kazi na promota yeyote atakayekuwa tayari kumuandalia bingwa huo wa WBF pambano hilo kwa lengo la kutaka Tanzania iendelee kung'ara kimataifa.
Alisema kwa kitambo kirefu mabondia wa Tanzania wameshindwa kung'ara kimataifa na hivyo ni vema Nyalawila, Francis Cheka na wengine wanaoshikilia mataji wakawa wanapewa kipaumbele kuandaliwa michezo.
Katika hatua nyingine, bingwa wa dunia wa WBC, UBO, ICB, Francis Cheka, anajifua kujiandaa na pambano lake la kuwania taji la IBF litakalofanyika April 2, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Micharazo toka Morogoro, Cheka, alisema pambano lake litafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee na atapigana na Mmarekani, Marcus Upshaw.
"Natarajia kupanda ulingoni April 2 kwa kuzichapa na Mmarekani ambaye jina lake limenitoka, katika kuwania mkanda wa IBF uzito wa kilo 72," alisema.
Hilo litakuwa pambano la kwanza kwa Cheka tangu alipomshindwa kwa pointi Bingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Mada Maugo katika pambano lisilo la mkanda lililochezwa Januari Mosi, kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar.
Mwisho
Msama Promotion yawasaidia Wahanga wa Mabomu Gongo la Mboto
WAHANGA wa milipuko ya mabomu yaliyotoka eneo la Gongo la Mboto, wameendelea kupewa misaada, baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka nchini, Alex Msama kutoa misaada ya vyakula.
Misaada hiyo yenye thamani ya karibu Sh. Mil. 3, ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Msama kupitia kituo cha runinga cha Cloud's, kwa lengo la kufikishwa kwa waathirika na milipuko hiyo iliyotokea katikati ya wiki kwenye kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania, JWTZ, kikosi cha 521 KJ.
Msama alisema kama sehemu ya jamii walioguswa na tukio la milipuko hiyo ya mabomu wameamua kutoa misaada hiyo kuitikia wito wa serikali, huku akiwahimiza watu wengine wenye uwezo kufanya hivyo.
"Tusiiachie serikali pekee yake kufanya kazi hii, ndio maana sisi kama sehemu ya jamii tumeamua kutoa msaada huu japo mdogo, lakini uwasaidie wenzetu walioathirika na tukio hilo linalosikitisha," alisema Msama.
Msaada huo uliotolewa ni magunia manne ya Mchele, Unga wa Ngano gunia 10, gunia mbili za Maharage na Sukari pamoja na ndoo mbili za mafuta ya Gunia za maharage na ndoo mbili za mafuta ya kupikia.
Msama alisema, pamoja na msaada huo, kamati yao inafanya mipango zaidi ya kuongeza misaada yao kwa wahanga hao kwa nia ya kuisaidia serikali na asasi nyingine zilizojitolea kwa hali na mali kuwafariji waathirika wa mabomu hayo.
Tukio la ulipukaji wa mabomu la Gongo la Mboto ni la pili katika kipindi cha karibu miaka miwili, baada ya awali kulipuka April 29, mwaka juzi kambi nyingine ya jeshi eneo la Mbagala, pia jijini Dar es Salaam.
Katika tukio hilo la pili, karibu watu 20 wakiwemo watoto wameripotiwa kupotea uhai wao, huku wengine wanaokadiriwa kufikia 400 wakijeruhiwa, mbali na kusababisha uharibifu wa mali na miundo mbinu kadhaa.
Tayari serikali imetangaza kuwalipa fidia wote walioathirika na tukio hilo, ambalo lilitokea majira ya usiku, siku ya Jumatano na kuleta taharuki kwa wakazi wengi wa jijini na wale wa mikoani.
Mwisho
Tuesday, February 15, 2011
TAMAGSARAI na mikakati yao dhidi ya uboreshwaji masoko
KUTOKANA na kuona hawana sauti ya pamoja na mahali pa kusemea matatizo na kero zinazowakabili katika shughuli zao, wauzaji wa mazao ya nafaka katika soko maarufu la Tandale waliamua kuunda umoja wao kama njia ya kupigania na kutetea haki zao.
Umoja huo wa wauza nafaka hao unafahamika kwa kifupi kama TAMAGSARAI ambao ni kifupi cha Umoja wa Wauza Nafaka na Wawekezaji wa Soko la Tandale kwa lugha ya Kiingereza na ulianzishwa rasmi mwaka 2000 ingawa usajili wake ulipatikana mwaka 2003.
Malengo makubwa ya umoja huo ulioasisiwa na watu 45 chini ya Uenyekiti wa Abeid Hamad Lunda na katibu Abdul Kambaya, mbali na kuwa sauti ya pamoja katika utatuzi wa kero na matatizo yao, pia kutaka kubadilisha mazingira na hali ya soko hilo na mengine Tanzania.
Mwenyekiti wa sasa wa umoja huo, Juma Dikwe, alisema masoko mengi nchini likiwemo lao la Tandale yana mazingira duni, machafu na hayavutii, kiasi kwamba yamekuwa yakikimbiwa na baadhi ya watu wanaoenda kwenye masoko ya kisasa maarufu kama 'Super Market'.
Dikwe, alisema kitu cha kinachowauma ni kwamba pamoja na masoko kuwa katika mazingira duni na machafu, kosi na ushuru utozwa kila siku na hazijulikani wapi zinapoenda wakati zilihitajiwa kuboresha masoko husika.
"Tunalipishwa kodi na ushuru, tegemeo letu fedha hizo zingerudi tena kwetu kwa kuboresha maeneo yetu ya kazi, lakini cha ajabu masoko yanakuwa machafu na kuhatarisha maisha yetu," alisema Dikwe.
Mwenyekiti huyo, alisema hata hivyo wanashukuru miaka karibu 10 tangu umoja wao uanzishwe wameweza kuielewesha serikali na kusaidia kuboresha soko lao na wanapigana zaidi kuona masoko mengine nayo yanakuwa katika na mazingira mazuri ya kufanyia kazi.
Alisema karibu masoko yote nchini hufanana kimazingira na hivyo ni vema yakafanyiwa marekebisho kuendana na wakati, ili kusaidia biashara kufanyika vema na kusaidia kuinua kipato cha wafanyabiashara, wakulima na taifa kwa ujumla.
Tangu umoja huo ulipoanzishwa hadi sasa una wanachama 105 ikiwa ni ongezeko la wanachama zaidi ya 60 kwa kipindi cha miaka saba iliyopita, huku ukiwa umesaidia kuandaa semina na mafunzo mara tatu kwa lengo la kuwaelimisha wanachama wao.
Semina ya kwanza ilifanyika mwaka 2007 iliyohusumu Elimu ya Utawala Bora iliyowahusisha viongozi wa serikali za mitaa na wanachama wao kwa lengo la kusimamia utekelezaji wa shughuli za serikali kwa ufanisi ikiwemo sekta ya masoko.
Kisha mwaka 2009 waliandaa mafunzo mengine yaliyohusu ufuatiliaji wa fedha za umma zilizotengwa kwa ajili ya sekta ya Masoko na mwaka huu waliandaa nyingine iliyohusu Usimamiaji wa Miradi na Rasilimali za Masoko ikiwa ni mradi wa miaka mitatu mfululizo.
Dikwe, alisema mradi huo, semina na mafunzo ya awali yaliandaliwa na umoja wao kwa msaada na ufadhili wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii, The Foundations for Civil Society na imekuwa ikiwahusisha wanachama wao na wachuuzi wengine wa masoko ya jijini Dar es Salaam.
"Mradi huu Usimamiaji wa Rasilimali za Masoko, ni wa miaka mitatu na tunashirikisha wachuuzi wa masoko karibu yote ya wilaya tatu za mkoa wa Dar es Salaam kwa vile matatizo ya masoko yanafanana kwa kiasi kubwa," alisema.
Mbali na kuendesha miradi na semina hizo, TAMAGSARAI pia huwasaidia wanachama wao wanapopata matatizo kama ya kufiwa na mengineyo kupitia fedha zinazopatikana toka kwa wafadhili wao na zile za michango ya ada inayotozwa kwa kila mmoja wao.
Pia husimama kama wadhamini kwa wanachama wao katika hupatikanaji wa mikopo toka kwa asasi za kifedha, ili kurahisisha kuboresha shughuli zao na kuihimiza serikali kuboresha masoko kwa kujenga mabanda ambayo yanakithi haja ya matumizi ya binadamu.
"Mabanda mengi yaliyopo kwenye masoko yetu ni mafupi na hayana ubora na imekuwa chanzo cha vifo vya wanachama na wachuuzi wengine kutokana na magonjwa ya kuambukiza kama Kifua Kikuu, na Kipindupindu na Homa ya Matumbo nyakati za mvua," alisema.
Alisema kwa takwimu za haraka kwa kipindi cha miaka saba, wanachama na wachuuzi wenzao 15 kati ya 50 walioathirika kwa ugonjwa wa Kifua Kikuu walifariki, huku wengine wakinusurika vifo wakati wa msimu wa mvua kutokana na ugonjwa wa Kipindupindu.
"Kwa kweli soko la Tandale na mengineyo nchini ni machafu na yanatisha nyakati za mvua na ndio maana TAMAGSARAI tumekuwa tukipigania kuboreshwa kwake, ili kuwaokoa watumiaji wake yaani wauzaji na wateja ambao wengi wanayakambia na kutukosesha mapato," alisema.
Moja ya mikakati yao kwa sasa ni kutaka kuunganisha nguvu zaidi katika umoja wao na kupanua huduma zao kutoka soko la Tandale tu na kuwa la nchi nzima likiunganisha wachuuzi na wauzaji wote wa nafaka, kwa lengo la kuwa na sauti moja yenye nguvu.
Pia wanajaribu kusaka mbinu na kuwaelimisha wanachama wao na wachuuzi wengine kwa ujumla juu ya upakiaji na uuzaji wa bidhaa zao katika hali ya kisasa ili kuvutia wateja hata wale ambao wanayachukulia masoko mengi kama ya watu wanyonge na wasio na hadhi.
"Tuimeshaanza kuwapa mafunzo wanachama wetu ili kupakia bidhaa zao kisasa, badala ya kuendelea kutoa huduma kizamani ambayo inachangia watu kukimbilia Super Market wakiona ni usasa zaidi, ingawa bidhaa ni zile zile na pengine zetu ni bora zaidi, " alisema.
Msisitizo wa umoja huo wenye safu kamili ya uongozi uliochaguliwa baada ya kuongozwa kwa muda na viongozi waasisi ni kuitaka serikali kutumia kodi na ushuru wanaotoza kwenye masoko kuboresha mazingira na masoko hayo kusaidia ajira na vipato vya watumiaji wake.
"Pia tunataka fedha zinazotengwa na serikali kwa ajili ya kuboresha huduma za masoko zitumike kwa malengo yaliyowekwa badala ya kufanyiwa ubadhilifu na wachache wenmye jukumu la kusimamia masoko," alisema Dikwe.
Aliongeza, pia ni vema masoko yakamilikishwa kwa vyama au wafanyabiashara wenyewe badala ya kuachiwa mawakala ambao wapo kifedha zaidi bila kuangalia uboreshaji wa mazingira ya masoko hayo kulingana na kodi na ushuru wanaotoza kila siku sokoni hapo.
Safu nzima ya umoja huo ambao kwa sasa unasaka soko la bidhaa zao nje ya nchi ni Mwenyekiti wake ni Juma Dikwe, Makamu wake, Juma Janga, Abdul Kambaya ndiye ni Katibu, wakati Sadiki Kubiga niu Mhazini.
Mwisho
Saturday, February 12, 2011
Vijana wahimizwa kujifunza uongozi, ujasiriamali
VIJANA wa Kitanzania wamehimizwa kujitosa kwenye masuala ya uongozi na ujasiriamali kwa lengo la kuja kuwa tegemeo la taifa hapo baadae.
Wito huo umetolewa na uongozi wa Chuo cha Viongozi wa Afrika, African Leadership Academy (ALA), kilichopo Afrika Kusini wakati wakitangaza ofa maalum ya kuwasomesha kwa muda wa miaka miwili bure wahitimu wa sekondari na vijana wa Kitanzania.
Mkurugenzi wa Usajili wa chuo hicho, Ivy Mwai, amesema kutokana na hali ilivyo duniani kwa sasa ni vema vijana wakajifunza masuala ya uongozi na ujasiriamali ili kuweza kujisaidia wenyewe na nchi yao kwa ujumla.
Mwai alisema vijana wenye ndoto za kuwa viongozi au wajasiriamali ni lazima wajisomee fani hizo kisha kujitokeza bila hofu yoyote kwa lengo la kuiletea nchi maendeleo.
"Vijana wa Kitanzania wenye vipaji vya uongozi na ndoto za kuwa wajasiriamali wajitokeze hadharani ili wapate ujuzi na uzoefu kwa manufaa ya taifa hapo baadae," alisema Mwai.
Mwai, alisema kutokana na kupenda kuona nchi za kiafrika zinapiga hatua kubwa kimaendeleo chuo chao kimetoa ofa Tanzania kwa kuwasomesha watakaojisajili na kufuzu kwenye mchujo utakaofanyika Mei mwaka huu.
Alisema usajili wa wahitimu hao wa sekondari na vijana wenye sifa utaanza kufanyika kuanzia mwezi ujao na watakaoshinda watatangazwa Mei kabla ya kwenda kujiunga na chuo hicho.
"Lengo letu ni kutaka kuona Tanzania na nchi za Kiafrika zinakuwa na viongozi wenye uchungu wa kuziletea mabadiliko nchi yao kimaendeleo na hivyo tumeamua kutoa ofa maalum kwa vijana wa hapa," alisema.
Mwai alisema kijana yeyote mwenye umri kati ya miaka 16-19 wanaweza kuichangamkia ofa hiyo itakayoambatana na kusaidiwa kutafutiwa vyuo vikuu vya kimataifa pale watakapofanya vema kwenye masomo yao ALA kwa kujaza fomu kupitia barua pepe admissions@africanleadershipacademy.org.
Mmoja wa wanafunzi wa Kitanzania aliyewahi kupata ofa kama hiyo ya ALA, Julius Shirima, ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Chama cha Wajasiriamlia Mkoa wa Dar es Salaam, DARECHA, alisema vijana hawapaswi kuipoteza bahati hiyo.
Wito huo umetolewa na uongozi wa Chuo cha Viongozi wa Afrika, African Leadership Academy (ALA), kilichopo Afrika Kusini wakati wakitangaza ofa maalum ya kuwasomesha kwa muda wa miaka miwili bure wahitimu wa sekondari na vijana wa Kitanzania.
Mkurugenzi wa Usajili wa chuo hicho, Ivy Mwai, amesema kutokana na hali ilivyo duniani kwa sasa ni vema vijana wakajifunza masuala ya uongozi na ujasiriamali ili kuweza kujisaidia wenyewe na nchi yao kwa ujumla.
Mwai alisema vijana wenye ndoto za kuwa viongozi au wajasiriamali ni lazima wajisomee fani hizo kisha kujitokeza bila hofu yoyote kwa lengo la kuiletea nchi maendeleo.
"Vijana wa Kitanzania wenye vipaji vya uongozi na ndoto za kuwa wajasiriamali wajitokeze hadharani ili wapate ujuzi na uzoefu kwa manufaa ya taifa hapo baadae," alisema Mwai.
Mwai, alisema kutokana na kupenda kuona nchi za kiafrika zinapiga hatua kubwa kimaendeleo chuo chao kimetoa ofa Tanzania kwa kuwasomesha watakaojisajili na kufuzu kwenye mchujo utakaofanyika Mei mwaka huu.
Alisema usajili wa wahitimu hao wa sekondari na vijana wenye sifa utaanza kufanyika kuanzia mwezi ujao na watakaoshinda watatangazwa Mei kabla ya kwenda kujiunga na chuo hicho.
"Lengo letu ni kutaka kuona Tanzania na nchi za Kiafrika zinakuwa na viongozi wenye uchungu wa kuziletea mabadiliko nchi yao kimaendeleo na hivyo tumeamua kutoa ofa maalum kwa vijana wa hapa," alisema.
Mwai alisema kijana yeyote mwenye umri kati ya miaka 16-19 wanaweza kuichangamkia ofa hiyo itakayoambatana na kusaidiwa kutafutiwa vyuo vikuu vya kimataifa pale watakapofanya vema kwenye masomo yao ALA kwa kujaza fomu kupitia barua pepe admissions@africanleadershipacademy.org.
Mmoja wa wanafunzi wa Kitanzania aliyewahi kupata ofa kama hiyo ya ALA, Julius Shirima, ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Chama cha Wajasiriamlia Mkoa wa Dar es Salaam, DARECHA, alisema vijana hawapaswi kuipoteza bahati hiyo.
SOMA MAELEZO KUKIJUA VEMA CHUO CHA ALA
African Leadership Academy is a world-class, pan-African secondary institution that aims to educate and develop outstanding students into principled, ethical leaders for Africa. It is an A level school, enrolling students aged 15-19 who are in their last two years of secondary and they sit the Cambridge International Examinations. The school, located in Johannesburg, South Africa seeks students who have demonstrated leadership, have good consistent academic performance, have an entrepreneurial/problem solving spirit, are involved in their communities and have a passion for Africa.
AFRICAN LEADERSHIP ACADEMY - AT A GLANCE
Our Mission
African Leadership Academy (ALA) seeks to transform Africa by developing and supporting future generations of African leaders. Opened in September 2008, African Leadership Academy brings together the most promising 16 -19 year old leaders from all 54 African nations for an innovative two-year program designed to prepare each student for a lifetime of leadership on the continent. Students are selected to attend the Academy based on merit alone and complete a unique curriculum with a focus on Leadership, Entrepreneurship, and African studies. ALA graduates attend the world’s finest universities and will lead Africa toward a peaceful and prosperous future. ALA is a non-profit institution located on the outskirts of Johannesburg, South Africa.
Our Team
African Leadership Academy was founded in 2004 by Fred Swaniker, Chris Bradford, Peter Mombaur, and Acha Leke. The founding team brings considerable experience as educators, entrepreneurs, consultants, and corporate executives in Africa and throughout the world. Our Advisors and Directors are internationallyrecognized luminaries in business, leadership development, secondary education, and social entrepreneurship.
These include Carly Fiorina, the former CEO and Chairwoman of Hewlett-Packard; Isaac Shongwe, Chairman of the African Leadership Initiative in South Africa; Futhi Mtoba, Chairwoman of Deloitte & Touche South Africa; Sir Sam Jonah, formerly President of Anglogold Ashanti; Jon Cummings, Director at McKinsey & Company; Ralph Townsend, Headmaster of Winchester College (UK); Ed Brakeman, retired Managing Director of Bain Capital; James Mwangi, CEO of Equity Bank, Kenya and Tunde Folawiyo, Executive Director of The Yinka Folawiyo Group, Nigeria. ALA also has a larger network of like-minded mentors, partners, and leaders to provide alumni with the long-term support system needed to lead Africa toward equitable and lasting development.
Our Successes
• In June 2005, ALA launched a pilot summer program to test and refine its concept and curriculum.
By 2008, more than 500 young leaders from 40 countries had participated in this innovative program.
• In June 2006, co-founders Fred Swaniker and Chris Bradford were named Echoing Green Fellows and described as two of the “15 best emerging social entrepreneurs in the world.”
• In April 2007, ALA secured a state-of-the art campus on the outskirts of Johannesburg to serve as the home of the institution.
• In June 2010, 93 students of the Inaugural Class graduated, many with full scholarships to attend top universities around the world.
• In July 2010, ALA sent offers of admission to 105 students from 33 countries, out of a pool of over 2,000 applicants. For the first time applicants from Guinea, the Gambia, Tunisia and Rwanda, were admitted to the Academy.
• In 2010, ALA students gained entrance into leading universities in USA, Europe and Africa such as Harvard, Oxford, Stanford, University of Cape Town and Ashesi University, Ghana.
• In 2010, ALA students received over $9.5 million in scholarship money to attend university.
Your Role
African Leadership Academy offers like-minded individuals and organizations a growing global network of local chapters and strategic partnerships committed to fostering our vision. To learn more, please contact admissions@africanleadershipacademy.org.
Campus Address
1050 Printech Ave, Honeydew 2040 South Africa
Postal Address
Postnet Suite 413, Private Bag X1
Northcliff 2115 South Africa
Phone: +27 11 699 3000 Fax: +27 11 252 6190
Email: info@africanleadershipacademy.org
First Ready Development 695 (Incorporated under Section 21) T/A African Leadership Academy
Directors: Peter B. Mombaur, Dr. Achankeng Leke, Frederick K. Swaniker
Reg. No. 2005/005377/08 - VAT No. 4670224122 - PBO No. 930020187
Gauteng Department of Education Reg. No. 400286
www.africanleadershipacademy.org
$9.5 million in University Scholarship Money Awarded to Outstanding
African Leadership Academy Graduates in 2010
The following are examples of just some of the leading universities that ALA students have been admitted to in 2010:
Fatoumata Fall, SENEGAL
University attending: Harvard University, USA
Also admitted to: Massachusetts Institute of Technology (MIT) (USA)
Subject: Engineering
Samuel Gichohi, KENYA
University attending: Princeton University, USA
Subject: Computer Science
Ifedolapo Omiwole, NIGERIA
University attending: Yale University, USA
Also admitted to: Oxford University (UK)
Subject: Economics
Mbali Zondi, SOUTH AFRICA
University attending: Barnard College, USA
Also admitted to: Ithaca College (USA), Lake Forest College (USA)
Subject: Journalism
Nkululeko Zigizendoda Yeni, SOUTH AFRICA
University attending: Yale University, USA
Also admitted to: Amherst College (USA), Colgate University (USA), Harvard University (USA),
University of Virginia (USA)
Subject: International Relations
Felix Tetteh, GHANA
University attending: Ashesi University, Ghana
Also admitted to: The College of Idaho (USA)
Subject: Business Economics & Music
Campus Address
1050 Printech Ave, Honeydew 2040 South Africa
Postal Address
Postnet Suite 413, Private Bag X1
Northcliff 2115 South Africa
Phone: +27 11 699 3000 Fax: +27 11 252 6190
Email: info@africanleadershipacademy.org
First Ready Development 695 (Incorporated under Section 21) T/A African Leadership Academy Directors: Peter B. Mombaur, Dr. Achankeng Leke, Frederick K. Swaniker
Reg. No. 2005/005377/08 - VAT No. 4670224122 - PBO No. 930020187
Gauteng Department of Education Reg. No. 400286
www.africanleadershipacademy.org
Dagbedji Fagnisse, CÔTE D’IVOIRE
University attending: Duke University, USA
Subject: Engineering
Awarded: Robertson Scholarship
Mehdi Oulmakki, MOROCCO
University attending: Dartmouth College, USA
Also admitted to: Amherst College (USA), Northeastern University (USA), Pomona College (USA)
Subject: Mathematics
Marie Shabaya, KENYA
University attending: University of Durham, London, UK
Also admitted to: Royal Holloway (UK), University of London (UK), School of Oriental and African
Studies (UK)
Subject: Economics
Imelda Rweyemamu, TANZANIA
University attending: Jacobs University Bremen, Germany
Also admitted to: Indiana University-Purdue University Indianapolis (USA)
Subject: Engineering
Rumbidzai Gondo, ZIMBABWE
University attending: Colby College, USA
Subject: History
Mariam Doumbia, MALI
School attending: Miss Hall’s School, Massachusetts, USA
Subject: Gap Year Program
Awarded: ASSIST-USA Gap Year Scholarship
AFRICAN LEADERSHIP ACADEMY - AT A GLANCE
Our Mission
African Leadership Academy (ALA) seeks to transform Africa by developing and supporting future generations of African leaders. Opened in September 2008, African Leadership Academy brings together the most promising 16 -19 year old leaders from all 54 African nations for an innovative two-year program designed to prepare each student for a lifetime of leadership on the continent. Students are selected to attend the Academy based on merit alone and complete a unique curriculum with a focus on Leadership, Entrepreneurship, and African studies. ALA graduates attend the world’s finest universities and will lead Africa toward a peaceful and prosperous future. ALA is a non-profit institution located on the outskirts of Johannesburg, South Africa.
Our Team
African Leadership Academy was founded in 2004 by Fred Swaniker, Chris Bradford, Peter Mombaur, and Acha Leke. The founding team brings considerable experience as educators, entrepreneurs, consultants, and corporate executives in Africa and throughout the world. Our Advisors and Directors are internationallyrecognized luminaries in business, leadership development, secondary education, and social entrepreneurship.
These include Carly Fiorina, the former CEO and Chairwoman of Hewlett-Packard; Isaac Shongwe, Chairman of the African Leadership Initiative in South Africa; Futhi Mtoba, Chairwoman of Deloitte & Touche South Africa; Sir Sam Jonah, formerly President of Anglogold Ashanti; Jon Cummings, Director at McKinsey & Company; Ralph Townsend, Headmaster of Winchester College (UK); Ed Brakeman, retired Managing Director of Bain Capital; James Mwangi, CEO of Equity Bank, Kenya and Tunde Folawiyo, Executive Director of The Yinka Folawiyo Group, Nigeria. ALA also has a larger network of like-minded mentors, partners, and leaders to provide alumni with the long-term support system needed to lead Africa toward equitable and lasting development.
Our Successes
• In June 2005, ALA launched a pilot summer program to test and refine its concept and curriculum.
By 2008, more than 500 young leaders from 40 countries had participated in this innovative program.
• In June 2006, co-founders Fred Swaniker and Chris Bradford were named Echoing Green Fellows and described as two of the “15 best emerging social entrepreneurs in the world.”
• In April 2007, ALA secured a state-of-the art campus on the outskirts of Johannesburg to serve as the home of the institution.
• In June 2010, 93 students of the Inaugural Class graduated, many with full scholarships to attend top universities around the world.
• In July 2010, ALA sent offers of admission to 105 students from 33 countries, out of a pool of over 2,000 applicants. For the first time applicants from Guinea, the Gambia, Tunisia and Rwanda, were admitted to the Academy.
• In 2010, ALA students gained entrance into leading universities in USA, Europe and Africa such as Harvard, Oxford, Stanford, University of Cape Town and Ashesi University, Ghana.
• In 2010, ALA students received over $9.5 million in scholarship money to attend university.
Your Role
African Leadership Academy offers like-minded individuals and organizations a growing global network of local chapters and strategic partnerships committed to fostering our vision. To learn more, please contact admissions@africanleadershipacademy.org.
Campus Address
1050 Printech Ave, Honeydew 2040 South Africa
Postal Address
Postnet Suite 413, Private Bag X1
Northcliff 2115 South Africa
Phone: +27 11 699 3000 Fax: +27 11 252 6190
Email: info@africanleadershipacademy.org
First Ready Development 695 (Incorporated under Section 21) T/A African Leadership Academy
Directors: Peter B. Mombaur, Dr. Achankeng Leke, Frederick K. Swaniker
Reg. No. 2005/005377/08 - VAT No. 4670224122 - PBO No. 930020187
Gauteng Department of Education Reg. No. 400286
www.africanleadershipacademy.org
$9.5 million in University Scholarship Money Awarded to Outstanding
African Leadership Academy Graduates in 2010
The following are examples of just some of the leading universities that ALA students have been admitted to in 2010:
Fatoumata Fall, SENEGAL
University attending: Harvard University, USA
Also admitted to: Massachusetts Institute of Technology (MIT) (USA)
Subject: Engineering
Samuel Gichohi, KENYA
University attending: Princeton University, USA
Subject: Computer Science
Ifedolapo Omiwole, NIGERIA
University attending: Yale University, USA
Also admitted to: Oxford University (UK)
Subject: Economics
Mbali Zondi, SOUTH AFRICA
University attending: Barnard College, USA
Also admitted to: Ithaca College (USA), Lake Forest College (USA)
Subject: Journalism
Nkululeko Zigizendoda Yeni, SOUTH AFRICA
University attending: Yale University, USA
Also admitted to: Amherst College (USA), Colgate University (USA), Harvard University (USA),
University of Virginia (USA)
Subject: International Relations
Felix Tetteh, GHANA
University attending: Ashesi University, Ghana
Also admitted to: The College of Idaho (USA)
Subject: Business Economics & Music
Campus Address
1050 Printech Ave, Honeydew 2040 South Africa
Postal Address
Postnet Suite 413, Private Bag X1
Northcliff 2115 South Africa
Phone: +27 11 699 3000 Fax: +27 11 252 6190
Email: info@africanleadershipacademy.org
First Ready Development 695 (Incorporated under Section 21) T/A African Leadership Academy Directors: Peter B. Mombaur, Dr. Achankeng Leke, Frederick K. Swaniker
Reg. No. 2005/005377/08 - VAT No. 4670224122 - PBO No. 930020187
Gauteng Department of Education Reg. No. 400286
www.africanleadershipacademy.org
Dagbedji Fagnisse, CÔTE D’IVOIRE
University attending: Duke University, USA
Subject: Engineering
Awarded: Robertson Scholarship
Mehdi Oulmakki, MOROCCO
University attending: Dartmouth College, USA
Also admitted to: Amherst College (USA), Northeastern University (USA), Pomona College (USA)
Subject: Mathematics
Marie Shabaya, KENYA
University attending: University of Durham, London, UK
Also admitted to: Royal Holloway (UK), University of London (UK), School of Oriental and African
Studies (UK)
Subject: Economics
Imelda Rweyemamu, TANZANIA
University attending: Jacobs University Bremen, Germany
Also admitted to: Indiana University-Purdue University Indianapolis (USA)
Subject: Engineering
Rumbidzai Gondo, ZIMBABWE
University attending: Colby College, USA
Subject: History
Mariam Doumbia, MALI
School attending: Miss Hall’s School, Massachusetts, USA
Subject: Gap Year Program
Awarded: ASSIST-USA Gap Year Scholarship
JE WEWE UNAPENDA UONGOZI NA KUWA MJASIRIAMALI SOMA HAPA
CHUO CHA UONGOZI AFRIKA, AFRICAN LEADERSHIP ACADEMY CHA AFRIKA KUSINI KINASAKA WAHITIMU WA SEKONDARI NA VIJANA WENYE UMRI USIOZIDI MIAKA 19 KWA AJILI YA KUINGIA KWENYE MCHAKATO WA KUPATA OFA YA KUSOMESHWA UONGOZI NA UJASIRIAMALI PAMOJA NA KUFANYIWA MIPANGO SCHOLARSHIP KWA VYUO VIKUU VYA KIMATAIFA.
MCHAKATO HUO UNAANZA RASMI MWEZI UJAO NA MAJINA YA WATAKAOVUKA MCHUJO HUO YATATANGAZWA RASMI MEI MWAKA HUU.
CHUO HIKI KIMEKUWA KIKITOA OFA NA KUWASAIDIA WANAFUNZI NA VIJANA WA KIAFRIKA, AMBAPO WALIOPIOTIA KATIKA CHUO HICHO BAADHI YAO KWA SASA WANASOMA MAREKANI, UJERUMANI NA NCHI ZINGINE ZA ULAYA NA AMERIKA.
KWA MAELEZO ZAIDI MNAWEZA KUJIUNGA SASA KUPITIA admissions@africanleadershipacademy.org.
MCHAKATO HUO UNAANZA RASMI MWEZI UJAO NA MAJINA YA WATAKAOVUKA MCHUJO HUO YATATANGAZWA RASMI MEI MWAKA HUU.
CHUO HIKI KIMEKUWA KIKITOA OFA NA KUWASAIDIA WANAFUNZI NA VIJANA WA KIAFRIKA, AMBAPO WALIOPIOTIA KATIKA CHUO HICHO BAADHI YAO KWA SASA WANASOMA MAREKANI, UJERUMANI NA NCHI ZINGINE ZA ULAYA NA AMERIKA.
KWA MAELEZO ZAIDI MNAWEZA KUJIUNGA SASA KUPITIA admissions@africanleadershipacademy.org.
Friday, February 11, 2011
Sikinde, Msondo zaanza tambo, zitakutana Februari 18
BENDI kongwe za muziki wa dansi nchini, Msondo Ngoma na Mlimani Park 'Sikinde' ambazo zinatarajiwa kuonyeshana kazi wiki ijayo, zimetambiana kwa kila moja ikijinasibu kuizima nyingine katika onyesho lao la pamoja litakalofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.r
Msondo na Sikinde zitakutana tena Februari 18 ikiwa ni mara ya pili katika kipindi cha miezi miwili baada ya kuchuana awali Desemba 30 katika onyesho lililofanyika ndani ya ukumbi wa Mzalendo Pub, uliopo Millenium Tower, Makumbusho Dar es Salaam.
Wakati siku zikikaribia kabla ya pambano hilo, viongozi wa bendi hizo wameanza kurushiana vijembe kila upande ukitamba kuwazima wenzake.
Msemaji wa Msondo, Rajabu Mhamila "Super D', alisema wanaamini kama walivyowazima Sikinde katika onyesho lao la Desemba, ndivyo watakavyofanya wiki ijayo kutokana na kikosi chao kinachoundwa na wanamuziki vijana na wachapakazi.
"Tunajua kwa sasa Sikinde watakuwa wanatafuta namna ya kutukabili, lakini kwa kifupi watarajie kufunikwa kama tulivyofanya kwenye onyesho la Mzalendo Pub," alisema Super D.
Hata hivyo, Sikinde ambao walikuwa visiwani Zanzibar kwenye Tamasha la Sauti za Busara wamejinasibu kuwa Msondo hawana ubavu mbele yao na kuwataka mashabiki wa muziki waende Diamond Jubilee kushuhudia ukweli wa wanachokisema.
Katibu wa Sikinde, Hamis Milambo alisema Sikinde ni zaidi ya Msondo kutokana na kukamilika kila idara kuanzia safu ya uimbaji, wapiga magitaa na wapuliza tarumbeta walichodai watatumia kama silaha ya kuwazima mahasimu wao.
"Sisi ni kama Barcelona, tuna safu kali ya ushambuliaji nikimaanisha waimbaji na viungo mahiri ambao ni wapuliza ala za upepo sikuambii wapiga magita, sijui kama Msondo watafua dafu," alisema Milambo.
Milambo alisema bendi yao inatarajia kurejea leo mchana kuendelea na utambulisho wa vibao vyao vipya vinavyoandaliwa kwa ajili ya albamu yao ijayo.
Msondo na Sikinde zitakutana tena Februari 18 ikiwa ni mara ya pili katika kipindi cha miezi miwili baada ya kuchuana awali Desemba 30 katika onyesho lililofanyika ndani ya ukumbi wa Mzalendo Pub, uliopo Millenium Tower, Makumbusho Dar es Salaam.
Wakati siku zikikaribia kabla ya pambano hilo, viongozi wa bendi hizo wameanza kurushiana vijembe kila upande ukitamba kuwazima wenzake.
Msemaji wa Msondo, Rajabu Mhamila "Super D', alisema wanaamini kama walivyowazima Sikinde katika onyesho lao la Desemba, ndivyo watakavyofanya wiki ijayo kutokana na kikosi chao kinachoundwa na wanamuziki vijana na wachapakazi.
"Tunajua kwa sasa Sikinde watakuwa wanatafuta namna ya kutukabili, lakini kwa kifupi watarajie kufunikwa kama tulivyofanya kwenye onyesho la Mzalendo Pub," alisema Super D.
Hata hivyo, Sikinde ambao walikuwa visiwani Zanzibar kwenye Tamasha la Sauti za Busara wamejinasibu kuwa Msondo hawana ubavu mbele yao na kuwataka mashabiki wa muziki waende Diamond Jubilee kushuhudia ukweli wa wanachokisema.
Katibu wa Sikinde, Hamis Milambo alisema Sikinde ni zaidi ya Msondo kutokana na kukamilika kila idara kuanzia safu ya uimbaji, wapiga magitaa na wapuliza tarumbeta walichodai watatumia kama silaha ya kuwazima mahasimu wao.
"Sisi ni kama Barcelona, tuna safu kali ya ushambuliaji nikimaanisha waimbaji na viungo mahiri ambao ni wapuliza ala za upepo sikuambii wapiga magita, sijui kama Msondo watafua dafu," alisema Milambo.
Milambo alisema bendi yao inatarajia kurejea leo mchana kuendelea na utambulisho wa vibao vyao vipya vinavyoandaliwa kwa ajili ya albamu yao ijayo.
Friday, February 4, 2011
Wasanii wa kike tujiheshimu-Regina

MMOJA wa waigizaji wa filamu anayekuja juu nchini, Regina Mroni amewaasa wasanii wenzake hususani wa kike, kujiheshimu na kuepukana kufanya matendo yanayowachafua mbele ya jamii pamoja na kuidhalilisha fani yao kuonekana kama kazi ya wahuni.
Mroni, aliyeng'ara kwenye filamu kama Trip to Amerika, Mastress, Siri y Mama, Aisha na nyinginezo, alisema kuna baadhi ya wasanii hasa wa kike wamekuwa wakiona raha kujianika utupu na kuhusishwa na skendo chafu, wakiamini wanakuza majina yao wakati wanajidhalilisha.
Alisema umaarufu wa msanii yeyote unapatikana kutokana na ubora na umahiri wa kazi zake na sio matendo machafu na hivyo kuwataka wasanii wa kike wajiamini, kujituma na kuithamini kazi yao ili jamii iwaheshimu.
"Wapo baadhi yetu wamekuwa wakijihusisha na matendo machafu na kuandikwa kila mara, kitu ambacho tofauti na fikra zao kuwa wanajijengea majina na umaarufu, wanajidhalilisha na kuonekana mbele ya jamii kama watu wasio na maadili kitu ambachio ni kibaya," alisema Mroni.
Mroni, aliyetumbukia kwenye fani hiyo miaka miwili iliyopita akitokea kwenye urembo ambapo aliwahi Miss Utalii Morogoro, Miss Ukonga, Miss Singida na kushiriki Miss Tanzania, alisema sanaa ni kazi kama kazi nyingine na wanaishiriki waithamini na kuipenda.
Alisema 'wavamizi' wachache kwenye fani hiyo wasio na vipaji ndio wanaojiachia na kujianika na mwisho wa siku wanadhalilika na kisha kupotea wakiwaacha wasanii wa kweli wakiendelea kutamba.
Mwisho
TAFF yapewa kifyagio kwa tamasha la filamu la Nyerere
SHIRIKISHO la Filamu Tanzania, TAFF, limepewa heko kwa ubunifu wake wa kuanzisha tamasha la filamu za Kibongo ambalo litafanyika Februari 14-19 jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo la kwanza kufanyika nchini kwa filamu za Kitanzania litafanyikia kwenye viwanja vya Leaders kwa kuzunduliwa na Rais Jakaya Kikwete na kufungwa na mke wa hayati baba wa taifa, Mwl Nyerere, Mama Maria Nyerere.
Baadhi ya wadau wa filamu wakiwemo wasanii wa fani hiyo wamesema kitendo cha TAFF kubuni tamasha hilo ni jambo la kupongezwa kwa vile litasaidia kuinua soko la kazi za wasanii wa kibongo, mbali na kutoa fursa kwa wananchi kupata mwamko wa kuzipenda kazi hizo.
"TAFF wamefanya jambo la maana ambalo wadau wa filamu Bongo tulikuwa tunalisubiri kwa muda mrefu, kitu cha muhimu waliendeleze kama mengine," alisema Leila Mwambungu wa Kimara.
Leila, alisema tamasha hilo linaweza kusaidia kuamsha hisia wa watanzania kupenda kazi za nyumbani kwa madai wapo wengine wanazichukulia poa filamu za Kibongo na kuhusudu kazi za Nigeria au Marekani.
Mtayarishaji wa filamu anayekuja juu, Husseni Ramadhani 'Swagger' alisema tamasha hilo ni kama njia ya wadau wa filamu kujitangaza na kuwahimiza wenzake kujitokeza kwa wingi kulishiriki kuanzia mwanzo wake hadi siku ya ufungwaji wake.
"Nafasi kama hizi ni muhimu kuzichangamkia, kwa kweli nalipongeza TAFF kwa kubuni kitu kama hiki, kwani itatusaidia wengine kujifunza makubwa zaidi ya yale tunayoyajua katika sanaa hiyo kutokana na ukweli tumesikia kuna mafunzo kadhaa yatakayotolewa hapo," alisema Swagger ambaye anatamba na filamu kama Hazina, Who is a Killer na sasa Bangkok Deal.
TAFF kupitia viongozi wake chini ya Rais Simon Mwakifamba, walitangaza kuanzisha kwa tamasha hilo litakalozinduliwa wiki ijayo na Rais Kikwete kwa ajili ya kuonyesha kazi za kitanzania pamoja na kupambwa na burudani kadhaa za sanaa na mada mbalimbali za kifani.
***
Tamasha hilo la kwanza kufanyika nchini kwa filamu za Kitanzania litafanyikia kwenye viwanja vya Leaders kwa kuzunduliwa na Rais Jakaya Kikwete na kufungwa na mke wa hayati baba wa taifa, Mwl Nyerere, Mama Maria Nyerere.
Baadhi ya wadau wa filamu wakiwemo wasanii wa fani hiyo wamesema kitendo cha TAFF kubuni tamasha hilo ni jambo la kupongezwa kwa vile litasaidia kuinua soko la kazi za wasanii wa kibongo, mbali na kutoa fursa kwa wananchi kupata mwamko wa kuzipenda kazi hizo.
"TAFF wamefanya jambo la maana ambalo wadau wa filamu Bongo tulikuwa tunalisubiri kwa muda mrefu, kitu cha muhimu waliendeleze kama mengine," alisema Leila Mwambungu wa Kimara.
Leila, alisema tamasha hilo linaweza kusaidia kuamsha hisia wa watanzania kupenda kazi za nyumbani kwa madai wapo wengine wanazichukulia poa filamu za Kibongo na kuhusudu kazi za Nigeria au Marekani.
Mtayarishaji wa filamu anayekuja juu, Husseni Ramadhani 'Swagger' alisema tamasha hilo ni kama njia ya wadau wa filamu kujitangaza na kuwahimiza wenzake kujitokeza kwa wingi kulishiriki kuanzia mwanzo wake hadi siku ya ufungwaji wake.
"Nafasi kama hizi ni muhimu kuzichangamkia, kwa kweli nalipongeza TAFF kwa kubuni kitu kama hiki, kwani itatusaidia wengine kujifunza makubwa zaidi ya yale tunayoyajua katika sanaa hiyo kutokana na ukweli tumesikia kuna mafunzo kadhaa yatakayotolewa hapo," alisema Swagger ambaye anatamba na filamu kama Hazina, Who is a Killer na sasa Bangkok Deal.
TAFF kupitia viongozi wake chini ya Rais Simon Mwakifamba, walitangaza kuanzisha kwa tamasha hilo litakalozinduliwa wiki ijayo na Rais Kikwete kwa ajili ya kuonyesha kazi za kitanzania pamoja na kupambwa na burudani kadhaa za sanaa na mada mbalimbali za kifani.
***
Ray, Kanumba na Msondo kila mtu kivyake
Ray ana 'Second Wife, Deception noma!
WAKATI filamu ya Family Disaster ikiendelea kutamba mitaani kwa sasa, msanii nyota wa fani hiyo nchini, Vincent Kigosi 'Ray', yupo mbioni kuachia kazi nyingine mpya iitwayo 'The Second Wife'.
Filamu hiyo ya kimapenzi, imewashirikisha wasanii kadhaa nyota pamoja na waigizaji chipukizi ambao wameibuliwa na kampuni iliyotayarisha filamu hiyo, RJ Production.
Miongoni mwa waigizaji walioshiriki filamu hiyo ni pamoja na Ray mwenyewe, Colleta Raymond, Aisha Bui, Riyama Ally, Msungu, Ramla na mtoto aitwae Aisha ambaye ni chupukizi.
Ray ameanika kwenye mtandao wake kuwa, filamu hiyo ambayo ameigiza kama muumini wa Kiislam ipo katika hatua ya mwisho kabla ya kuachiwa ni moja ya kazi yenye mafunzo makubwa kwa jamii.
"Kama nilivyofanya kwenye The Divorce ndani ya filamu hii mafunzo ni yale yale na mashabiki mkae mkao wa kula kupata uhondo," alisema Ray.
Kwa mujibu wa taarifa hizo kama filamu zake nyingine, 'The Second Wife' itasambazwa na kampuni ya Steps Entertainment.
Wakati huo huo filamu mpya ya Steven Kanumba iitwayo Deception, aliyoigiza pamoja na Bakari Makuka, Rose Ndauka na Patcho Mwamba imekuwa ikinunuliwa kama njugu tangu iigizwe sokoni mapema wiki hii.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Nipashe, filamu hiyo imekuwa ikigombewa kununuliwa sambamba na Pete ya Ajabu na Family Disaster ambayo ina karibu mwezi sasa sokoni.
***
Msondo wapeleka mpya Songea
BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo Ngoma, kesho inatarajiwa kuzitambulisha nyimbo zao mpya zinazoandaliwa kwa ajili ya albamu ya 2011 mjini Songea mkoani Ruvuma.
Msondo inayotamba na albamu ya ya Huna Shukrani, itatumbuiza kwenye ukumbi wa Serengeti Bar, mjini huo.
Kwa mujibu wa kiongozi wa bendi hiyo, Said Mabera 'Diblo' ni kwamba Msondo itatumbuiza kwenye ukumbi huo nyakati za usiku, wakati jioni watakuwepo kwenye dimba la Majimaji kushuhudia pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga na wenyeji Majimaji-Songea.
Mabera, alisema katika onyesho hilo, bendi yao itapiga nyimbo zao za zamani pamoja na zile mpya zinazoendelea kuandaliwa kwa ajili ya albamu yao ijayo.
"Tupo Songea na kesho tutafanya onyesho kwenye ukumbi wa Serengeti, wakazi wa Songea wakae mkao wa kupata uhondo mtupu," alisema Mabera mmoja wa wapiga solo mahiri nchini na mwanamuziki aliyedumu kwa muda mrefu Msondo tangu alipojiunga mwaka 1973.
Mabera alizitaja baadhi ya nyimbo watakazozipiga kwenye onyesho hilo ni pamoja na zile za albamu za Demokrasia ya Mapenzi, Ndoa Ndoana, Kilio cha Mtu Mzima, Piga Ua Talaka Utatoa, Kaza Moyo, Kicheko kwa JIrani na Huna Shukrani.
"Pia tutawapigia na kuzitambulisha nyimbo mpya za Lipi Jema, Dawa ya Deni, Kwa Mjomba Hakuna Urithi na Baba Kakura, yaani ni burudani kwa kwenda mbele," alisema.
Baadhi ya wanamuziki wa Msondo ambayo wiki iliyopita ilimpoteza mmoja wa waimbaji wake mahiri, Hamis Maliki 'Super Maliki' watakapanda jukwaani leo ni pamoja na Mabera, Roman Mng'ande, Huruka Uvuruge, Ibrahim Kandaya, Juma Katundu, Is'haka Katima, Eddo Sanga na wengineo.
***
WAKATI filamu ya Family Disaster ikiendelea kutamba mitaani kwa sasa, msanii nyota wa fani hiyo nchini, Vincent Kigosi 'Ray', yupo mbioni kuachia kazi nyingine mpya iitwayo 'The Second Wife'.
Filamu hiyo ya kimapenzi, imewashirikisha wasanii kadhaa nyota pamoja na waigizaji chipukizi ambao wameibuliwa na kampuni iliyotayarisha filamu hiyo, RJ Production.
Miongoni mwa waigizaji walioshiriki filamu hiyo ni pamoja na Ray mwenyewe, Colleta Raymond, Aisha Bui, Riyama Ally, Msungu, Ramla na mtoto aitwae Aisha ambaye ni chupukizi.
Ray ameanika kwenye mtandao wake kuwa, filamu hiyo ambayo ameigiza kama muumini wa Kiislam ipo katika hatua ya mwisho kabla ya kuachiwa ni moja ya kazi yenye mafunzo makubwa kwa jamii.
"Kama nilivyofanya kwenye The Divorce ndani ya filamu hii mafunzo ni yale yale na mashabiki mkae mkao wa kula kupata uhondo," alisema Ray.
Kwa mujibu wa taarifa hizo kama filamu zake nyingine, 'The Second Wife' itasambazwa na kampuni ya Steps Entertainment.
Wakati huo huo filamu mpya ya Steven Kanumba iitwayo Deception, aliyoigiza pamoja na Bakari Makuka, Rose Ndauka na Patcho Mwamba imekuwa ikinunuliwa kama njugu tangu iigizwe sokoni mapema wiki hii.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Nipashe, filamu hiyo imekuwa ikigombewa kununuliwa sambamba na Pete ya Ajabu na Family Disaster ambayo ina karibu mwezi sasa sokoni.
***
Msondo wapeleka mpya Songea
BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo Ngoma, kesho inatarajiwa kuzitambulisha nyimbo zao mpya zinazoandaliwa kwa ajili ya albamu ya 2011 mjini Songea mkoani Ruvuma.
Msondo inayotamba na albamu ya ya Huna Shukrani, itatumbuiza kwenye ukumbi wa Serengeti Bar, mjini huo.
Kwa mujibu wa kiongozi wa bendi hiyo, Said Mabera 'Diblo' ni kwamba Msondo itatumbuiza kwenye ukumbi huo nyakati za usiku, wakati jioni watakuwepo kwenye dimba la Majimaji kushuhudia pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga na wenyeji Majimaji-Songea.
Mabera, alisema katika onyesho hilo, bendi yao itapiga nyimbo zao za zamani pamoja na zile mpya zinazoendelea kuandaliwa kwa ajili ya albamu yao ijayo.
"Tupo Songea na kesho tutafanya onyesho kwenye ukumbi wa Serengeti, wakazi wa Songea wakae mkao wa kupata uhondo mtupu," alisema Mabera mmoja wa wapiga solo mahiri nchini na mwanamuziki aliyedumu kwa muda mrefu Msondo tangu alipojiunga mwaka 1973.
Mabera alizitaja baadhi ya nyimbo watakazozipiga kwenye onyesho hilo ni pamoja na zile za albamu za Demokrasia ya Mapenzi, Ndoa Ndoana, Kilio cha Mtu Mzima, Piga Ua Talaka Utatoa, Kaza Moyo, Kicheko kwa JIrani na Huna Shukrani.
"Pia tutawapigia na kuzitambulisha nyimbo mpya za Lipi Jema, Dawa ya Deni, Kwa Mjomba Hakuna Urithi na Baba Kakura, yaani ni burudani kwa kwenda mbele," alisema.
Baadhi ya wanamuziki wa Msondo ambayo wiki iliyopita ilimpoteza mmoja wa waimbaji wake mahiri, Hamis Maliki 'Super Maliki' watakapanda jukwaani leo ni pamoja na Mabera, Roman Mng'ande, Huruka Uvuruge, Ibrahim Kandaya, Juma Katundu, Is'haka Katima, Eddo Sanga na wengineo.
***
Extra Bongo yaivunjavunja Twanga Pepeta
NENO zuri la kusema ni kwamba African Stars 'Twanga Pepeta' imevunjwavunjwa baada ya wanamuziki wake nyota saba kuihama bendi hiyo kwa mpigo na kutua Extra Bongo 'Wana 'Next Level' iliyoingia rasmi kambini kujiwinda na albamu mpya ya pili.
Wanamuziki hao saba walitambulishwa rasmi leo asubuhi na Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki, ambapo alisema lengo la kuwanyakua wakali hao ni kutaka bendi yake iwe matawi ya juu na kuleta mabadiliko ya muziki wa dansi nchini.
Choki aliwatambulisha wanamuziki hao ambapo ni waimbaji wawili, wapiga gitaa wawili na madansa watatu akiwemo mkali Hassani Mussa 'Super Nyamwela'.
Mbali na Nyamwela aliyeitumikia Twanga kwa miaka 11 mfululizo bila kuhama ni Rogart Hegga 'Catapilla' na Saul Ferguson ambao ni waimbaji, Hosea Mgohachi mpuiga gita zito la besi na Godi Kanuti anayecharaza magita yote.
Wanenguaji wengine waliomfuata Nyawela Extra Bongo ni Otilia Boniface na Issack Burhan maarudu kama Danger Boy.
Choki alisema wanamuziki hao wote wana mikataba na bendi yao na mchana huu wanatarajia kuungana na wanamuziki wenzao kambini eneo la Mbezi Mwisho kujipanga kwa albamu mpya.
Alisema kambi hiyo ya muda wa wiki tatu itatumika kuwapa fursa wanamuziki hao wapya kuzoeana na wenzao kabla ya kuanza kufanya vitu vyao hadharani wakiwa wamezaliwa upya.
Mkurugenzi huyo aliyesema tukio kama hilo la kuibomoa Twanga liliwahi kumtokea miaka minne iliyopita alipochukuliwa wanamuziki wa idadi kama hiyo na ASET na kuifanya Extra Bongo 3x3 Kujinafasi kuzimika hadi ilipofufuka mwaka jana.
Alisema wanamuziki hao wapya wamenyakuliwa na Extra Bongo tayari kuziba nafasi za waliotemwa akiwemo rapa machachai Greyson Semsekwa na wenzake kadhaa.
Wakizungumza kwenye utambulisho huo, Ferguson na Nyamwela walisema wamekuja kuthibitisha thamani yao na mashabiki wa Extra Bongo watarajie makubwa.
"watarajie kazi bab'kubwa kwani tunafahamika kwa vipaji vya fani hii," alisema Ferguson.
Nyamwela aitema Twanga, adai miaka 11 imetosha
KIONGOZI wa muda mrefu wa madansa wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' Hassan Mussa 'Super Nyamwela', aliyetangazwa jana kujiunga na bendi ya Extra Bongo, amedai amefikia uamuzi huo kwa lengo la kutaka kubadilisha upepo baada ya kukaa bendi yke kwa miaka zaidi ya 10.
Akizungumza kwenye utambulisho wake na wenzake sita toka Twanga, Nyamwela alisema miaka 11 aliokaa ASET imemtosha na ndio maana ameondoka ili kuzaliwa upya.
Nyamwela alisema hata hivyo pamoja na kuondoka Twanga ikiwa ni bendi yake pekee kuifanyia kazi tangu alipochukuliwa toka kundi la Billbum, hawezi kuponda alikotoka kwa vile imemsaidia kwa mengi na kwa sasa akili yake ni kuwapa burudani mashabiki wa bendi yake mopya.
"Nimeondoka kwa kutaka kubadilisha upepo, mnanijua mie sina utamaduni wa kuhamahama, ila kwa kutaka kuleta mabadiliko katika fani na maisha yangu kwa ujumla nimeamua kuoka Twanga na watu wasinchukulie vingine natafuta maisha," alisema dansa huyo bingwa wa zamani wa Bolingo Dar.
Aliongeza kuwa kama alivyokuwa Twanga alipoipa mafanikio makubwa, ndivyo ambavyo amepania kufanya hivyo akiwa Extra Bongo ambao ameungana nao kambini kujiandaa kupakua albamu mpya.
"Nyamwela ni yule yule, ila kwa hapa Extra mashabiki wake watarajie mambo makubwa na mazuri zaidi, na imani kwa ushirikiano na wenzangu Extra Bongo itatisha," alisema Nyamwela.
Mbali na Nyamwela, katika utambulisho huo, pia madansa Otilia Boniface, Isaack Burhani nao walitambulishwa sambamba na wanamuziki, Rogart Hegga 'Catapillar', Saulo Ferguson, Hosea Mgohachi na God Kanuti waliokuwa Twanga Pepeta.
wanamuziki hao walitambulishwa kwa waandishi wa habai jana na Mkurugenzi wa bendi hiyo ya Extra Bongo, Ally Choki 'Kamarade'.
Saturday, December 18, 2010
Baba Diana a.k.a Lukasa kuzikwa kesho mjini Tanga
MWANAMUZIKI Mkongwe wa muziki wa dansi, Abuu Semhando 'Baba Diana', 57, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajili ya barabarani anatarajiwa kusafirishwa kesho kwenda wilayani Muheza, Tanga kuzikwa.
Kwa mujibu Meneja Masoko wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' aliyokuwa akiifanyia kazi marehemu huyo,Martin Sospeter ni kwamba Semhando aliyefahamika pia kama Lukasa enzi akiwa Super Matimila, atazikwa kesho nyumbani kwao Tanga, ingawa msiba upo Mwananyamala Kisiwani alipokuwa akiishi enzi za uhai wake.
Sospeter, alisema mwili wa marehemu kwa sasa upo Muhimbili na wanafanya mipango ya kuusafirisha kwenda kuzikwa kwao Tanga kesho alasiri.
"Marehemu anatarajiwa kusafirishwa kwao Tanga kwa ajili ya mazishi, ingawa kwa sasa msiba upo nyumbani kwake, Mwananyamala Kisiwani na mwili wake umeshapelekwa hospitali ya Muhimbili," alisema Sospter.
Meneja huyo alisema kuwa marehemu aliyezaliwa Oktoba 24, 1953 na kuanza muziki mwaka 1974 katika bendi ya Sola Tv kabla ya kupita bendi mbalimbali Twanga Pepeta aliyoiongoza kama Katibu wake, amewaachia pengo kubwa lisilozibika aslan.
"Ni pigo kwetu na tumeshtushwa na kuhuzunishwa na kifo chake cha ghafla," alisema Sospeter.
Kifo cha mkongwe huyo aliuyewahi kuzipigia bendi za Super matimila, Orchestra Toma Toma, Tango Musica, Diamond Sound 'Wana Kibinda Nkoy', Beta Musica kabla ya kuasisi Twanga Pepeta, kimekuja masaa machache tangu fani ya muziki kumpoteza Ramadhan MToro Ongalla aliyefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Dk Remmy alifariki Jumatatu na kuzikwa Alhamis, huku Semhando na wanamuziki wenzake wakishiriki mwanzo mwisho katika msiba huo.
Mwisho
Kwa mujibu Meneja Masoko wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' aliyokuwa akiifanyia kazi marehemu huyo,Martin Sospeter ni kwamba Semhando aliyefahamika pia kama Lukasa enzi akiwa Super Matimila, atazikwa kesho nyumbani kwao Tanga, ingawa msiba upo Mwananyamala Kisiwani alipokuwa akiishi enzi za uhai wake.
Sospeter, alisema mwili wa marehemu kwa sasa upo Muhimbili na wanafanya mipango ya kuusafirisha kwenda kuzikwa kwao Tanga kesho alasiri.
"Marehemu anatarajiwa kusafirishwa kwao Tanga kwa ajili ya mazishi, ingawa kwa sasa msiba upo nyumbani kwake, Mwananyamala Kisiwani na mwili wake umeshapelekwa hospitali ya Muhimbili," alisema Sospter.
Meneja huyo alisema kuwa marehemu aliyezaliwa Oktoba 24, 1953 na kuanza muziki mwaka 1974 katika bendi ya Sola Tv kabla ya kupita bendi mbalimbali Twanga Pepeta aliyoiongoza kama Katibu wake, amewaachia pengo kubwa lisilozibika aslan.
"Ni pigo kwetu na tumeshtushwa na kuhuzunishwa na kifo chake cha ghafla," alisema Sospeter.
Kifo cha mkongwe huyo aliuyewahi kuzipigia bendi za Super matimila, Orchestra Toma Toma, Tango Musica, Diamond Sound 'Wana Kibinda Nkoy', Beta Musica kabla ya kuasisi Twanga Pepeta, kimekuja masaa machache tangu fani ya muziki kumpoteza Ramadhan MToro Ongalla aliyefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Dk Remmy alifariki Jumatatu na kuzikwa Alhamis, huku Semhando na wanamuziki wenzake wakishiriki mwanzo mwisho katika msiba huo.
Mwisho
Buriani Baba Diana utakumbukwa daima
KIFO kimeumbwa kwa usiri mkubwa hata hujaji wake, pia huwa ni siri mno, kiasi ni vigumu kwa kiumbe chochote duniani kubaini lini atakumbana nacho.
Lau kisingekuwa na usiri katika suala la kifo, kwamtu kufahamu kitakufikia lini, wapi na kwa njia gani, sidhani kama kuna ambaye angekuwa akitoka nje siku ya ahadi yake kwa kuhofia kukutana nacho.
Ila kwa kuwa Mungu ana hekima na maana kubwa ya kukifanya kuendelea kuwa ni siri yake pekee yake duniani na ahera, kifo kinaendelea kuogopwa.
Ndio maana hata mwanamuziki gwiji wa muziki wa dansi, marehemu Marijani Rajabu 'Jabari la Muziki' enzi za uhai wake alitunga wimbo ulioelezea hamu yake ya kutaka kuwepo rufaa ya kifo ili mradi kuwarudisha wapendwa wetu wanaondoka ghafla bila kutarajiwa.
Abuu Semhando maarufu kama 'Baba Diana' au 'Lukasa' ambaye kwa siku zote nne za msiba wa mwanamuziki mwenzake, Ramadhani Ongolla 'Dk Remmy' alishiriki mwanzo mwisho hadi alipopumzishwa makaburini Sinza, Dar es Salaam, naye amefariki dunia.
Semhando, aliyekuwa mpiga dramu na Katibu wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' alifariki usiku wa kuamkia jana, ikiwa ni masaa machache tangu amzike mwenzake baada ya kupatwa na ajali mbaya ya barabarani.
Marehemu huyo alikumbwa na mauti hayo maeneo ya Mbezi Beach, akitokea kazini kwake baada ya kugongwa na gari akiwa anaendesha pikipiki na kujeruhiwa vibaya kichwani kabla ya kufa papo hapo.
Mwili wa mkongwe huyo aliyefanyia kazi bendi mbalimbali hapa nchini tangu miaka ya 1970 na aliyekuwa mpiganiaji wa haki za wanamuziki wenzake kama baadhi ya waliowahi kufanya nae kazi wanavyomueleza, uliohifadhiwa katika hospitali ya Muhimbili, utasafirishwa leo kwenda kuzikwa Muheza jiji Tanga.
Baadhi ya wanamuziki wa dansi nchini wamedai kushtushwa na kifo hicho cha ghafla cha Semhando, wakirejea kwamba walikuwa naye katika safari ya kumsindikiza Remmy aliyefariki Jumatatu na kuzikwa Alhamis, masaa machache kabla naye hajapatwa na mauti hayo.
Tshimanga Kalala Assosa, mtunzi na muimbaji aliyezipigia bendi mbalimbali kama Lipualipua, Le Kamalee, Fuka Fuka na Orchestra Marquis, alisema kama sio kuogopa kufuru, angeweza kusema Mungu ni kama amewaonea wanamuziki wa Tanzania wiki hii kwa vifo hivyo mfululizo.
"Naogopa kumkufuru Mungu, lakini misiba hii na hasa huu wa Semhando niliofahamishwa usiku wa manane kwa kupigiwa simu umeniuma kupindukia, ila sina jinsi kwa kuwa kazi ya Mungu haina makosa," alisema Assosa.
Assosa, alisema kuondoka kwa wakongwe hao ni kama uzindushi kwa waliosalia juu ya umuhimu wa kushikamana na kumcha Mungu, pamoja na kufanya maandalizi ya kusaka warithi wa nafasi zao katika muziki kwa sababu bila ya hivyo fani yao itatereka.
Ally Choki 'Mzee wa Farasi', aliyewahi kufanya kazi na Semhando wakati akiwa mwanamuziki na kiongozi wa Twanga Pepeta, alisema kifo cha Semhando ni pigo kwa familia ya marehemu, wadau wa muziki na hususani bendi yake ya Africana Stars kwa kuwa alikuwa nguzo.
"Sio siri ni msiba mkubwa na pengo kubwa katika muziki wa dansi na hasa Twanga Pepeta kwa vile nafahamu jinsi gani marehemu alivyokuwa 'roho' ya bendi hiyo, licha ya kwamba wapo waliokuwa wakimuona kama 'mnoko' fulani, namlilia milele Semhando," alisema Choki.
Choki alisema uzoefu wake katika fani ya muziki, ilimfanya marehemu kuwa mhimili wa bendi hiyo na muziki wa dansi kwa ujumla, akipigania masilahi ya wanamuziki wenzake na kusema hajui nani wa kuliziba pengo lake.
"Muhimu ni kumuombea kwa Mungu na pia kuiombea familia yake iwe na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi," alisema Choki.
Meneja wa Masoko wa bendi hiyo, Martin Sospeter, alisema kifo cha kiongozi mwenzao na mwanamuziki wao, ni pigo kubwa kutokana na kutokea kwake ghafla, lakini wanamuachia Mungu kwa kuwa alimpenda zaidi kuliko walivyompenda na kumthamini wao.
"Ni pigo kwetu na fani nzima ya muziki, tunajipanga kufanya maandalizi ya kumplekea mwenzetu katika makazi yake ya milele, ambapo atazikwa kesho (leo) nyumbani kwao mjini Tanga," alisema.
Marehemu Semhando ambaye majina yake kamili ni Abubakar Semhando, alizaliwa Oktoba 24, mwaka 1953 huko Muheza Tanga na kupata elimu ya msingi huko huko kwao, kabla ya kutumbukiza kwenye muziki miaka ya mwanzoni ya 1970.
Bendi yake ya kwanza kuifanyia kazi ni Sola TV ya jijini Dar mnamo mwaka 1974 kabla ya kutua Tanga International na kukaa nao hadi miaka ya 1980 alipohamia Super Matimila iliyokuwa chini ya Dk Remmy.
Aliihama Matimila na kutua Tomatoma Jazz akiwa na marehemu Adam Bakar 'Sauti ya Zege', kabla ya kuhamia Orchestra Safari Sound 'OSS' na kukaa nao hadi mwanzoni mwa miaka ya 1990 alipohamia Tango Musica, kisha kujiunga Vijana Jazz.
Baadae alitua Diamond Sound 'Wana Kibinda Nkoy' mwaka 1996 na kutunga kibao cha Neema kilichoipaisha bendi hiyo, miaka miwili baadae alihamia Beta Musica na kukaa nao kwa muda mfupi kabla ya kuhamia African Stars akiwa mmoja wa waasisi wake.
Amekuwa na bendi hiyo ya Twanga Pepeta tangu wakati huo hadi mauti yalipomkuta juzi akiwa ameshiriki kupiga dramu karibu nyimbo zote za albamu 10 za bendi hiyo kuanzia ile ya Kisa cha Mpenda hadi Mwana Dar es Salaam iliyozinduliwa mwaka huu.
Mwisho
BREAKING NEWS-ABUU SEMHANDO 'BABA DIANA' IS NO MORE


MWANAMUZIKI Mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Abuu Semhando 'Baba Diana' amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajali ya gari baada ya kugongwa akiwa kwenye pikipiki eneo la Africana, Mbezi jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana mapema zinasema kifo hicho kilitokea majira ya saa 9 usiku baada ya kugongwa na gari aina ya Benz lililomjeruhi vibaya sehemu ya kichwani.
Abuu aliyetamba miaka ya 1970 akiwa na bendi ya Vijana Jazz, amepatwa na mauti hayo ikiwa ni siku moja tu tangu ashiriki kumziba mkongwe mwenzake, Ramadhani Mtoro Ongalla 'Dk Remmy' aliyefariki Jumatatu na kuzikwa Alhamis.
Kwa hakika ni pigo kwa wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki na wadau wa muziki wa dansi kwa ujumla, ingawa Kazi ya Mola Haina Makosa kwa sababu alishatuambia mapema kwamba KILA NAFSI ITAONJA MAUTI, wametangulia sisi tu nyuma yao tuwadhaike na vifo vyao kwa vile hatujui saa au siku ambayo Malaikat Maut, Izraili atatupitia kuchukua AMANA.
INNALILLAH WAINNA ILAHI RAJIUN!
Thursday, December 16, 2010
Amer Lugunga Mwenyekiti Mpya Halmashauri ya Kilosa
DIWANI wa Kata ya Kimamba, wilayani Kilosa, Amer Lugunga, amefanikiwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo baada ya kuwaangusha wagombea wenzake wenzake wawili.
Wagombea walioangushwa na Lugunga, ni pamoja na Leonard Mapunda na mtu mwingine aliyetajwa kwa jina moja la Mbiza.
Katika mchuano huo uliofanyika kwenye ofisi za CCM wilaya ya Kilosa, Lugunga aliibuka mshindi kwa kuzoa jumla ya kura 40 kati ya 60 zilizopigwa kwenye kinyang'anyiro hicho kilichokuwa na ushindani mkali.
Mbiza alishika nafasi ya pili kwa kupata kura 17 na Mapunda aliambulia tatu tu.
Akizungumza na MICHARAZO mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi, Lugunga alisema atafanya kazi kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kuhakikisha Kilosa inaondokana na aibu iliyoighubika kwa sasa.
"Nawashukuru walionichagua, na ahadi yangu ni kwamba nitafanya kazi kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi, ili kuirejeshea heshima wilaya yetu iliyopewa hati chafu hivi karibuni kutokana na matumizi mabaya ya fedha za miradi ya maendeleo," alisema Lugunga.
Alipoulizwa juu ya 'zengwe' alilokuwa akiwekewa na baadhi ya wapinzani wake, Lugunga, alisema mambo yote yameisha na hana kinyongo na mtu.
Mwisho
Wagombea walioangushwa na Lugunga, ni pamoja na Leonard Mapunda na mtu mwingine aliyetajwa kwa jina moja la Mbiza.
Katika mchuano huo uliofanyika kwenye ofisi za CCM wilaya ya Kilosa, Lugunga aliibuka mshindi kwa kuzoa jumla ya kura 40 kati ya 60 zilizopigwa kwenye kinyang'anyiro hicho kilichokuwa na ushindani mkali.
Mbiza alishika nafasi ya pili kwa kupata kura 17 na Mapunda aliambulia tatu tu.
Akizungumza na MICHARAZO mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi, Lugunga alisema atafanya kazi kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kuhakikisha Kilosa inaondokana na aibu iliyoighubika kwa sasa.
"Nawashukuru walionichagua, na ahadi yangu ni kwamba nitafanya kazi kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi, ili kuirejeshea heshima wilaya yetu iliyopewa hati chafu hivi karibuni kutokana na matumizi mabaya ya fedha za miradi ya maendeleo," alisema Lugunga.
Alipoulizwa juu ya 'zengwe' alilokuwa akiwekewa na baadhi ya wapinzani wake, Lugunga, alisema mambo yote yameisha na hana kinyongo na mtu.
Mwisho
Extra Bongo yawanyatia akina Chokoraa

BAADA ya bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' kuwatimua kundini, wanamuziki wao nyota wawili, Khalid Chokoraa na Kalala Junior, uongozi wa bendi ya Extra Bongo, umeanza mipango ya kuwachukua wanamuziki hao kuimarisha kikosi chao.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Ally Choki, aliiambia MICHARAZO kuwa, tayari wameshaanza mazungumzo ya awali na wanamuziki hao ambao pia wanaunda kundi la Mapacha Watatu wakishirikiana na Jose Mara wa FM Academia.
Choki alisema walikuwa na mipango ya kuwachukua waimbaji hao kitambo kirefu,ila walikuwa wakisita kuhofia kutifuana na uongozi wa Twanga Pepeta, lakini kutimuliwea kwao kwa utovu wa nidhamu ni kama kumewarahisishia kazi.
"Kutimuliwa kwao Twanga Pepeta kumeturahisishia kazi ya kuwapata waimbaji hawa wenye vipaji vya aina yake na tumeshaanza mazungumzo ya awali, nadhani ndani ya wiki hii mambo yatakuwa shwari na wataanza kazi Extra Bongo," alisema Choki.
Choki aliongeza katika kuonyesha kuwa wapo karibu na wanamuziki hao na kuwakubali kwa kazi zao kupitia kundi lao la Mapacha watatu wanatarajia kufanya nazo onyesho la pamoja wakati wa Mkesha wa Mwaka Mpya na siku ya Mwaka Mpya wenyewe jijini Dar es Salaam.
Alisema onyesho la kwanza baina yao na Mapacha Watatu linalotamba na albamu ya 'Jasho la Mtu' litafanyika mkesha wa Mwaka Mpya, Vatican Hotel, Sinza na kisha siku ya Mwaka Mpya watakuwa wote pale TCC Chang'ombe.
"huwezi jua kwenye maonyesho hayo mawili yanaweza kutumiwa kama utambulisho wao ndani ya Extra Bongo," Choki alitania.
Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa, lengo la bendi yao ni kutaka kuona wanatamba kwenye muziki wa dansi nchini baada ya kurejea kwa mara ya pili baada ya kufariki enzi ikitumia miondoko ya 3x3.
Choki aliongeza wakati wakiwa, katika harakati hizo za kuwanyakua akina Chokoraa, aliyekuwa mmoja wa waasisi wa Extra Bongo ya awali, pia bendi yao inajiandaa kufanya uzinduzi wa albamu ya 'Mjini Mipango'.
Alisema uzinduzi uliofanyika Mei 25 mwaka huu ulikuwa ni wa bendi yao iliyofufuliwa upya na sio wa albamu kama baadhi ya watu walivyokuwa wanadhani na hivyo wanajipanga kuifanyia uzinduzi wake.
Choki alisema watazindua albamu hiyo yenye nyimbo sita ambazo baadhi zinaendelea kutamba kwenye vituo vya redio na runinga, huku wakiendelea kuandaa ya pili ambayo tayari baadhi ya nyimbo zake zimeshakamilika.
Dk Remmy kuzikwa leo

SAFARI ya mwisho ya hapa duniani kwa mwanamuziki nguli wa muziki wa dansi na ule wa Injili, Ramadhan Mtoro Ongalla 'Dk Remmy' aliyefariki mapema wiki hii, inatarajiwa kuhitimishwa rasmi leo atakapozikwa kwenye makaburi ya Sinza, jirani na nyumbani kwake.
Remmy, aliyezaliwa nchini Zaire (sasa DR Congo) miaka 63 iliyopita alifariki Jumatatu baada ya kuugua kwa muda mrefu atazikwa jioni ya leo kwenye makaburi hayo baada ya kuagwa kwa tamasha la muziki wa Injili kwenye viwanja vya Biafra, Kinondoni, jijini.
Mjomba wa marehemu, Mzee Makassy, alisema mwili wa marehemu utazikwa kwenye makuburi hayo jirani kabisa na mahali alipokuwa akiishi, Sinza kwa Remmy.
Marehemu Remmy aliingia nchini mwaka 1977 na kujiunga na bendi ya mjomba wake, Makassy Band na kutamba na kibao cha Siku ya Kufa kabla ya baadae kuhamis Super Matimila ambayo ilimpa umaarufu mkubwa kutokana na umahiri wake wa kutunga, kuimba na kupiga gita la solo ambapo alishiriki matamasha makubwa barani Ulaya mara kwa mara.
Hata hivyo miaka michache iliyopita alipata kiharusi na kupooza, ambapo aliamua kuokoka na kuanza kutumikia muziki wa Injili hadi mauti yalipompata akiwa ameacha mke na watoto kadhaa akiwemo mshambuliaji wa timu ya Azam, Kalimangonga 'Kally' Ongalla.
Bwana Alitoa Naye Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe. Micharazo tunamtakia safari njema aendako nasi tu nyuma yake kwa kuwa kila nafsi ni lazima ionje mauti.
Monday, December 13, 2010
Cheka, Maugo kumaliza Ubishi Dar

MABONDIA Francis Cheka 'SMG' na Mada Maugo 'King Maugo Jn' wanatarajia kumaliza ubishi baina yao watakapopigana kwenye ukumbi wa PTA jijini Dar es Salaam badala ya uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro.
Mratibu wa pambano hilo, Kaike Siraju, aliiambia MICHARAZO mapema leo kuwa, pambano la wababe hao wawili litafanyika Dar na sio Morogoro kama alivyokuwa akitaka iwe na kuingia kwenye mzozo na Mada Maugo.
Maugo, anayeshikilia taji la ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati, alitishia kutopigana na Cheka kama pambano hilo lingehamishiwa Morogoro.
Siraju, alisema wameangalia mambo mengi kabla ya kusitisha uamuzi wa kulibakisha pambano hilo Dar na kueleza kuwa maandalizi kwa ujumla yanaendelea vema ikiwemo mabondia wote kuendelea kujifua.
"Maandalizi ya pambano la Cheka na Maugo, yanaendelea vema na litafanyika Dar kama ilivyokuwa awali, baada ya jaribio la kulihamishia Moro kushindikana," alisema Siraju.
Siraju alisema pambano hilo la uzani wa Middle la raundi nane lisilo la kuwania Mkanda litakalofanyika Januari Mosi, mwakani, likisindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi.
Mratibu huyo aliitaja michezo ya utangulizi siku hiyo ni pamoja na pambano kati ya Mshihiri Kidira atakayezidunda na Deo Njiku, Jafari Majid dhidi ya Juma Afande na Hussein Mbonde atakayezichapa na Cosmas Cheka.
Michezo mingine ni ile ya Simba wa Tunduru ataonyeshana kazi na Albert Mbena, Arafati ‘Ngumi Jiwe’ atapambana na Juma Kihio wakati Sadik Momba atafunga kazi na Smoo Njiku.
Michezo yote hiyo inasimamiwa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBO na ni maalum kwa kukata mzizi wa fitina baina ya mabondia hao wanaotambiana kila mmoja akitamba ni bora kuliko mwenzie.
Mwisho
Subscribe to:
Posts (Atom)