STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 20, 2013

Mtangazaji aliyepigwa risasi aanza kufunguka juu ya mkasa wake, inatisha



Ufoo Saro akiwa na Rais Kikwete
MWANDISHI  wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro ambaye hivi karibuni alikumbwa na madhila ya kupigwa risasi na kujeruhiwa vibaya na mzazi mwenzie, ameanza kufunguka kidogo kidogo na kueleza kwa kina jinsi tukio zima lilivyotokea.  Akizungumza kwa sauti ndogo na taratibu na gazeti hili kando ya kitanda alicholazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, mwanahabari huyo alieleza kushangazwa na ujasiri na nguvu za aina yake ambazo zilimwezesha kutambaa na kujiburuza hadi eneo la karibu ya barabara ili kuomba msaada wa kukimbizwa hospitali.

Ufoo ambaye alionyesha dhahiri kutofurahishwa na baadhi ya taarifa zinazozingira tukio lake, alisema tayari alikuwa amewahakikishia polisi waliofika kumjulia hali hospitalini hapo kwamba alikuwa akisubiri afya yake iimarike kabla hajaeleza kwa kina kila anachokijua kuhusiana na tukio hilo.

“Alifika hapa kunijulia hali na kuangalia maendeleo yangu afande Msangi na nikasema nitakuwa tayari kueleza kila ninachokijua baada ya afya yangu kuimarika. Nasikitika kuna watu wanasema mambo wakifikia hatua ya kutaka kuonekana wananifahamu vizuri kuliko hata ninavyojifahamu mwenyewe,” alisema akionyesha kutofurahishwa na baadhi ya taarifa zinazoripotiwa kuhusu sakata lake.


Ufoo ambaye alifikishwa hospitalini hapo Jumapili ya wiki iliyopita kutokana na kujeruhiwa kwa risasi na mwanaume aliyezaa naye mtoto mmoja alisema anamshukuru sana Mungu kwa uzima alionao sambamba na kuelezwa kupata faraja kubwa na kutiwa moyo na mwajiri wake, ndugu, jamaa na marafiki.


Ufoo Saro kushoto akiwajibika
Mwanahabari huyo ambaye bado yuko chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuondoa risasi mwilini mwake siku chache zilizopita, amelazwa katika chumba cha peke yake ambacho ingawa kina seti ya televisheni alisema alikuwa haruhusiwi kuiangalia kwa ushauri na maelekezo ya madaktari.

Huku akionekana wa chini ya uangalizi mwingine wa karibu na wa kudumu wa muuguzi ambaye muda wote wa mazungumzo haya alionekana kuwapo katika chumba hicho, Ufoo alisema alikuwa ana mapenzi makubwa kwa mzazi mwenzake huyo ambaye alipoteza maisha katika tukio hilo.

“Nilimpenda sana Antheri. Alikuwa kijana mtaratibu na mpole sana. Najua kile kilichotokea ni shetani tu na binafsi nilishasamehe alfajiri ile ile baada ya tukio lile,” alieleza Ufoo ambaye pia alimpoteza mama yake mzazi katika mkasa huo.

TUKIO ZIMA LILIVYOTOKEA

Ufoo ambaye mara kadhaa katika mazungumzo na gazeti hili alionekana kukunja uso akiashiria kupata maumivu, alionyesha eneo la chini ya bega katika mkono wake wa kulia lililofungwa na bandeji ambalo alisema ndipo alipopigwa risasi ya kwanza wakati akigeuka na kujaribu kuepuka mauti muda mfupi baada ya Antheri kumfyatulia risasi zilizomkuta mama yake mzazi.

Ufoo Saro alipokuwa akitolewa kwenye chumba cha upasuaji Muhimbili
Akijaribu kuvuta kumbukumbu ya tukio lilivyoanza, Ufoo alisema mzazi mwenzake huyo alifika nyumbani kwake akitokea Sudan alikokuwa akifanya kazi usiku huo huo wa tukio na akamtaka kwenda kwa mama yake (Ufoo) eneo la Kibamba, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Kabla ya kufika Kibamba na kwa sababu ambazo Ufoo hakuzieleza, alimkariri mzazi mwenzake huyo akisema alikuwa amefikia uamuzi wa kujiua yeye na mtoto wao.

“Hata sijui ni nini kilitokea. Wakati tukitoka nyumbani Antheri alianza kwa kuniambia kwamba alikuwa amepanga kujiua yeye na mtoto wetu,” alisema Ufoo kabla ya kukaa kimya kwa sekunde kadhaa na kuendelea na simulizi yake ya kusikitisha.

Akiwa na sura ya ujasiri, Ufoo anasema pamoja na kumwambia maneno hayo bado Mushi alimsisitiza kwamba waende kwa mama yake (Ufoo) baadae warudi kumchukua mtoto wao japo Ufoo hakusema walitaka kwenda wapi baada ya hapo.

Alisema walipofika nyumbani kwa mama yake walikwenda moja kwa moja sebuleni na wakiwa wamekaa kwenye makochi baada ya salamu za hapa na pale ghafla Mushi akasimama akamwambia mama yake Ufoo kwamba; “Mama nimeishafanya maamuzi”

Kwa mujibu wa maelezo ya Ufoo, baada ya Mushi kutamka maneno hayo ghafla akaingiza mkono nyuma ya suruali  alikokuwa ameweka bastola  yake na kisha akaichomoa.

Katika maelezo yake Ufoo alisema baada ya kuichomoa bastola hiyo mama yake naye alisimama na kwenda kujaribu kumpokonya, kitendo hicho kilimfanya amiminiwe risasi mfululizo.

Alisema kuona hivyo aliamua kukimbia kuelekea jikoni ambapo Mushi alimuona na kuanza kumiminia risasi ambayo moja ilimpata eneo la mkono wa kulia ambayo ilitokezea mbele na kuchana titi la kulia.

Kwa mujibu wa Ufoo jeraha hilo halikumfanya akate tamaa ya kunusuru maisha yake kwani alijaribu kukimbia ingawa Antheri alifyatua risasi nyingine kadhaa ambazo zilimpata juu kidogo ya mgongo na kutokea tumboni ambazo zilisababisha aanguke chini

Akiendelea kusimulia, anasema ingawa alikuwa akivuja damu nyingi, na huku akijiburuza ardhini, Ufoo alisema wakati akitambaa aligeuka nyuma na akamuona Antheri akijielekeza bastola eneo la kidevu na alipofyatua risasi alianguka chini.

“Nikiwa chini nilimuona Antheri akijipiga risasi kidevuni na akaanguka chini, sikujua kilichofuata baada ya hapo kwani niliendelea kujiburuza ili kuokoa maisha yangu,” alisema Ufoo

ALIVYOJIOKOA

“Nyumbani kwetu, pale Kibamba si mbali sana na barabarani, wakati nikikaribia kufika barabarani wakati huo nikitokwa na damu nyingi huku nikihisi tumbo langu limejaa sana nilikutana na dada mmoja ambaye nilimuomba khanga ili nijifunge kuzuia damu zisitoke kwa wingi”.

Anasema dada yule alimpa khanga akajifunga na aliposogea barabarani alikutana na gari lililokuwa likiendeshwa na mwanamke mmoja.

“Nilipoona kuna gari linapita nikainuka kuomba msaada. Liliposimama nilimuona mwanamke akiendesha nikamweleza kwamba nilikuwa nimepigwa risasi na nilikuwa nikiomba msaada wake anikimbize hadi katika hospitali ya Tumbi na kwamba akifika pale tu aniache mlangoni.

“Si rahisi kuamini, yule mama alikataa kunisaidia akisema alikuwa akiwahi sehemu kumchukua mzazi. Sina la kusema niliamua kumsamehe tu yule mama ingawa niliumia sana,” alisema Ufoo.

Alisema muda mfupi tu baadaye alitokea kijana aliyekuwa na pikipiki, maarufu kwa jina la bodaboda ambaye alimuomba msaada wa kumkimbiza hospitali ya Tumbi na akakubali.

“Yule kijana aliniuliza iwapo nilikuwa ninao uwezo wa kujishikilia vizuri na niliposema nitaweza akanisaidia kupanda katika bodaboda.

“Wakati huo nilikuwa naona kama tumbo linazidi kujaa. Nikiwa kwenye pikipiki kuna wakati nilikuwa nikihisi kwamba naweza nikaishiwa nguvu na kuanguka katika barabara na kisha kupitiwa na gari na kupoteza maisha. Lakini nilipata ujasiri na kujishikilia,” alieleza kwa sauti ya chini.


Alisema anakumbuka wakati walipofika eneo la Kibaha ilipo mizani ya kupima uzito wa magari makubwa walikuta barabara ikiwa imejaa magari na yeye alimuomba dereva huyo wa bodaboda kupita hata nje ya barabara eneo la nyasi ili kumwahisha hospitalini jambo ambalo kijana yule alilifanya.

“Nilipofika eneo la mapokezi pale Tumbi nilimueleza muuguzi niliyemkuta kwamba nilikuwa nimejeruhiwa kwa risasi na nikamuomba asaidie kuokoa maisha yangu. Yule nesi alisita akitaka kwanza kupata kibali cha polisi (PF3) lakini nikaumuomba apigiwe simu, Kaimu Mganga Mkuu wa Tumbi, Dk. Dattan ambaye tunafahamiana”

“Baada ya muda mfupi Dk. Dattan alifika na nikamweleza yaliyonipata na mara moja nikaanza kuhudumiwa kwa kuniwekea dripu, na nikamsikia akiwaeleza wauguzi kwamba isingekuwa busara kwa hali niliyonayo kama wangeanza kuchukua picha za X-ray kwani hatua hizo zingeweza kusababisha kupoteza maisha,” alieleza akikumbuka yaliyojiri hapo Tumbi.

Kwa mujibu wa Ufoo, akiwa bado ana fahamu alimsikia daktari aliyekuwa akimhudumia akiomba msaada wa gari la kubeba wagonjwa ili limchukue na kumkimbiza katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wito ambao ulijibiwa kwa maelezo kwamba lilikuwa halina mafuta.

Majibu hayo kwa mujibu wa Ufoo, yalisababisha daktari huyo aombe kuletewa gari la wagonjwa la wagonjwa maarufu (VIP) ambalo lililitwa na muda mfupi baadaye akapakizwa tayari kwa safari ya kukimbizwa Muhimbili.

Alisema wakati akikimbizwa Muhimbili anakumbuka namna alivyokuwa akipatwa na maumivu makali wakati wote gari ile ya wagonjwa ilipokuwa ikipanda matuta ya barabarani na kuna nyakati alikuwa akihisi kupoteza pumzi na kuishiwa nguvu. 


RAI

PSG yaua Ufaransa, Ibrahimovic akipiga bao la mwaka

Zlatan Ibrahimovic
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Ufaransa, PSG jana ilitoa kipigo cha mbwa mwizi wakati walipoisulubu Bastia kwa mabao 4-0 na kuiengua Monaco kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo kwa muda.
Mabao mawili ya kipindi cha kwanza kutoka kwa mshambuliaji 'mtukutu' kutoka Sweden Zlatan Abrahimovic moja likiwa la aina yake akiunganisha mpira kwa tiktak ya kisigino na kumtungia kipa wa Bastia.
Magoili mengine yalifungwa katika kipindi cha pili na Edinson Cavani na kuifanya PSG ikwee kileleni ikiwa na pointi 24.
Cavani aliifungia PSG bao la nne kwa mkwaju wa penati na kuzima matumaini ya wageni Bastia ambayo imeporomoka hadi nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi hiyo.

Hata hivyo huenda mabingwa hao wakaa kwa muda tu katika kiti hicho cha uongozi kabla ya kuwapisha Monaco ambayo muda mchache ujao itashuka dimba la ugenini kupepetana na Sochaux. Monaco ikishinda itarejea kileleni kwa tofauti na mabao ya kufunga na kufungwa.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo maarufu kama Ligue 1, juzi Ijumaa Nice iliinyoa Olimpique Marseille kwa bao 1-0, Reims ikilala nyumbani kwa mabao 2-1 mbele ya Toulouse, huku jana Ajaccio ikiwa nyumbani ilikubali kipigo cha bao 1-0 toka kwa Nantes, Evian TG nayo ikilala 2-1 nyumbani dhidi ya Guingamp, nayo Lille ikiicharaza Montpellier bao 1-0 na Rennes na Valenciennes zikitoka sare ya mabao 2-2.
Leo mbali na Monaco kuvaana na Sochaux ugenini, Saint Etienne itaialika Lorient na Olimpicque Lyon itapepetana na wageni wao Bordeaux.

Juma Luizio amchimbwa mkwara Tambwe

Juma Luizio (kushoto) alipokuwa katika mazoezi ya Taifa Stars nchini Uganda hiviu karibuni
MSHAMBULIAJI chipukizi anayekuja juu nchini anayeichezea Mtibwa Sugar, Juma Luizio 'Ndanda' amemchimba mkwara mkali wa mabao wa Simba Amissi Tambwe akimwabia asahau kuhusu kiatu cha dhahabu cha ufungaji bora msimu huu kwani hicho ni mali yake.
Luizio amesema anataka kuwa mfungaji bora msimu huu na kumuapia Tambwe kuwa atakula naye sahani moja.
Akizungumza na MICHARAZO hivi punde, Luizio ambaye jana alifunga mabao mawili wakati Mtibwa Sugar ikizamisha Mgambo JKT kwa mabao 4-1 na kufikisha jumla ya mabao saba moja nyuma ya Tambwe mwenye mabao nane, alisema lengo lake ni kufunga jumla ya mabao 17.
Chipukizi huyo aliyeanza kuitumikia timu ya wakubwa ya Mtibwa Sugar mwaka jana baada ya kupandishwa kutoka kikosi cha vijana, alisema amekuwa akitupia mipira nyavuni kwa lengo la kuwa Mfungaji Bora na kunyakua kiatu cha dhahabu.
Luizio alisema kila Mtibwa inapokuwa dimbani akili zake uziweka katika kutikisa nyavu na ndiyo maana amekuwa akifunga karibu kila mechi na kudai lengo ni kuwa mfungaji bora na siyo kuwasindikiza wenzake.
"Nafunga kwa sababu nataka kuwa mfungaji bora, nimepanga msimu huu nitupie jumla ya mabao 17 ambayo naamini yatanibebesha kiatu hicho, yakizidi haitakuwa neno," alisema.
Kuhusu kinara wa mabao kwa sasa Mrundi Amissi Tambwe wa Simba, Luizio alisema hana hofu naye kwani atamkamata na kumpita kutokana na kasi yake kuongezeka siku hadi siku.
Mshambuliaji huyo aliyewahi kuzichezea timu za Docks na Polisi Morogoro kabla ya kutua Mtibwa baada ya kung'ara kwenye michuano ya Taifa Cup na kuwa Mfungaji Bora namba mbili wa Uhai Cup mwaka uliopita, alisema ligi ni ngumu lakini atapigana kutimiza lengo.
Luizio alifichua siri ya mafanikio yake ya kufumania nyavu ni kuaminiwa na makocha na kuiga kwake mbinu za Zlatan Ibrahimovic anayemzimia.

Msiba! Mtangazaji Julius Nyaisanga 'Uncle J' hatunaye


Julius Nyaisanga enzi za uhai wake
TAARIFA zilizotufikia kutokana Morogoro zinasema kuwa, Mtangazajai nguli aliyewahi kutamba na vituo mbalimbali vya Radio kuanzia RTD, Radio One/ITV, Julius Nyaisangah 'Uncle J' amefariki dunia kutokana na kuugua kwa muda mrefu akiwa hospitali ya Mazimbu mjini humo.
Marehemu Nyaisanga anayekumbukwa kwa umahiri wake wa kutangaza taarifa habari na kuendesha vipindi vya Misakato na Klabu Raha Leo Show wakati yupo RTD na kisha kutisha na Mambo Mseto na Watoto Show akifahamika kama Babu wa Kimazichana akiwa Radio One, mpaka mauti yanamkumba alikuwa Mhairir Mtendaji wa Abood Media inayomiliki vituo vya Radio Abood na Abood Televisheni za mjini Morogoro.
Haijafahamika chanzo halisi cha mauti ya mtangazaji huyo, japo inaelezwa alikuwa akiigua kwa muda mrefu kisukari na Shinikizo la damu.
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na familia ya marehemu pamoja na wadau wote wa tasnia ya habari na kuwatakia subira katika kipindi hiki kigumu cha msiba.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema  Ameen

Saturday, October 19, 2013

Yanga watua Dar na matumaini kibao kuinyuka Simba kesho


MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imetua jijini Dar es Salaam leo ikitokea visiwani Pemba ilipoenda kuweka kambi kujiandaa na pambano lao la kesho dhidi ya Simba na kuapa 'mnyama' lazima afe kesho Taifa.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na mtandao wa klabu hiyo ya Yanga zinasema kuwa kikosi kamili cha mabingwa hao watetezi kimetua leo kikiwa na matumaini kibao ya kumchinja mnyama kesho katika pambano la kwanza la wapinzani hao wa jadi kwa msimu huu.
Taarifa hiyo inasema Yanga ilijifua asubuhi ya leo kabla ya kurejea jijini ikiwa ni maandalizi ya mwisho mwisho kwa ajili ya pambano hilo na kwamba kocha Ernie Brandts alisema hakuna mchezaji yeyote mgonjwa hali inayompa matumaini ya kucheka kesho.
"Sisi tumejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo huo, vijana wangu wapo safi kiafya, kifikra na morali ni ya hali ya juu, hivyo tuna kila sababu ya kuendeleza wimbi la ushindi ukizingatia uwezo wa kikosi chetu kwa ujumla hivi sasa" alinukuliwa Brandts Aidha Brandts alisema anatambua michezo ya watani wa jadi duniani kote huwa ni migumu lakini kwa sasa haoni sababu itakayowazuia kuibuka na ushindi katika mchezo huo japokuwa Simba timu nzuri pia.
Ushindi kwetu siku ya jumapili ni muhimu, ni muhimu kwa sababu tunapigania kutetea tena ubingwa wetu kwa awamu ya pili mfululizo, kikubwa tunawaomba wapenzi, washabiki na wanachama waje kwa wingi kuwashangilia vijana wao watakpokuwa wanapeperusha bendera ya watoto wa Jangwani.

Akina Samatta, Ulimwengu watinga Fainali Afrika

Mbwana Samatta atacheza Fainali ya Kombe la Shirikisho na timu yake ya TP Mazembe

Kikosi cha TP Mazembe kilichotangulia fainali za Kombe la Shirikisho Afrika
WASHAMBULIAJI nyota wa Tanzania, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wameweka rekodi baada ya timu yao ya TP Mazembe ya DR Congo kutinga hatua ya Fainali za Kombe la Washindi Afrika kutokana na ushindi wa bao 1-0 iliyopata jioni hii dhidi ya Stade Malien Bamako mjini Lubumbashi.
Bao pekee lililoipeleka fainali TP Mazembe na kuwafanya watanzania hao kuingia katika rekodi ya kukaribia kuwa Watanzania wa kwanza kunyakua taji kubwa barani Afrika, liliwekwa kimiani na Tresor Mputu kwa njia ya penati katika dakika ya 7 tu ya mchezo huo.
Kwa ushindi hio TP Mazembe imefuzu fainali kwa jumla ya mabao 3-1 baada ya mechi ya awali iliyochezwa mjini Bamako, Mali kushinda mabao 2-1.
Mabingwa hao wa zamani wa Afrika wanasubiri kujua itacheza na nani katika fainali ya michuano hiyo kati ya timu mbili za Tunisia, CA Bizertin itakayovaana na CSSfaxien kesho katika pambano la marudiano huku matokeo ya mechi ya kwanza yakiwa 0-0.

Kun Aguero aizamisha West Ham, Manchester City ikiua x3

Sergio 'Kun' Aguero

MABAO mawili ya mshambuliaji nyota wa Argentina, Sergio 'Kun' Aguero, yalitosha kuisaidia Manchester City kuizamisha West Ham kwa mabao 3-1 katika pambano lililomalizika hivi punde la Ligi Kuu ya England.
Wakiwa ugenini, Manchester City waliwashtua wenyeji wao kwa kupata bao la kuongoza lililofungwa katika dakika ya 16 kupitia Kun Aguero na kudumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili kilishiuhudia  Kun Aguero akiiongezea timu yao bao la pili dakika sita tu tangu kipindi hicho kianze kabla ya wenyeji West Ham kupata bao la kujifutia machozi kupitia kwa Ricardo Vaz Te dakika ya 58.
David Silva aliihakikishia Man City ushindi kwa kufunga bao la tatu dakika 10 kabla ya kumalizika kwa pambano hilo na kuifanya ichupe hadi nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo ikifikisha pointi 16 ikiwa nyuma ya timu ya Liverpool na Chelsea waliopo juu yao wakiifukuzia Arsenal inayoongopa baada ya jioni ya leo kupata ushindi mnono wa mabao 4-1 wakiwa nyumbani Emirates.

Arsenal. Chelsea zaua, Man Utd yabanwa Ozil nouma!

Making the difference: Ozil celebrates doubling Arsenal's advantage
Mesut Ozil ni kama anawauliza mashabiki 'Kuna Maswali...?'
Delight: Dejan Lovren's 89th minute equaliser earned Southampton a valuable point at Old Trafford
Tumnechomoaaaa, Southampton wakishangilia bao lao la kusawazisha dhidi ya Manchester United

Level: Eden Hazard netted the equaliser for the hosts
Eto'o akishangilia bao na wachezaji wenzake wa Chelsea

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester United imeendelea kudorora baada ya leo kubanwa mbavu nyumbani na Southampton, huku Arsenal na Chelsea zikifanya mauaji.
Manchester Utd inayonolewa na David Moyes, ilibanwa mbavu kwenye uwanja wa Old Trafford na kulazimishwa sare ya bao 1-1 na wageni wao waliochomoa bao dakika za lala salama na kuvuna pointi moja muhimu.
Robin van Persie alianza kuwafungia wenyeji bao dakika ya 26, lililodumu kwa hadi wakati wa mapumziko, kabla ya wageni kucharuka na kurejesha bao hilo dakika ya 89 kupitia Dejan Lavren.
Katika mechi nyingine zilizochezwa jioni hii, Arsenal imeendeleza rekodi ya kushinda mwechi mfululizo baada ya kuitafuna Norwich City kwa mabao 4-1 kama ilivyofanya Chelsea iliyoumana na Cardiff City.
Mesut Ozil aliendelea kuonyesha ni 'lulu' Arsenal kwa kufunga mabao mawili, huku magoli mengine yakifungwa na Jack Wilshere na Aaron Ramsey, huku bao la kufutia machozi la wageni kufungwa na Jonathan Howson.
Chelsea iliyokwea hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo kwa ushindi iliyopata nyumbani Stanford Bridge, ilifumania nyavu zake kupitia kwaEden Hazard aliyefunga mawili, Oscar na Mcameroon, Samuel Eto'o.
Mechi nyingine zilishuhudiwa Everton ikipata ushindi wa mabao 2-1 nyumbani dhidi ya Hull City, huku Swansea City 'ikiiua' kwa mabao 4-0 timu ya Sunderland na timu za Stoke City na West  Bromwich zilitoka suluhu ya kutofungana.

Azam, Mbeya City, Mtibwa 'zaua', Ashanti yazidi kujitutumua, Coastal yafa Kaitaba, Luizio, Maguri wampumulia Tambwe

Mbeya City walioendelea kuonyesha maajabu

Azam walioiengua Simba na kukalia kiti cha uongozi wa Ligi Kuu
Mtibwa waliishusha Yanga ikiendelea 'kuua' VPL
 VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba na watani zao wa jadi Yanga wanaotarajiwa kuvaana kesho, wameporomoshwa katika nafasi walizokuwa wakizishikilia baada ya Azam na Mbeya City kushinda leo.
Azam imekwea hadi katika nafasi ya kwanza na kuitoa Simba baada ya kuinyuka Oljoro JKT kwa bao 1-0 uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.
Ushindi huo wa ugenini uliopatikana kwa bao la mtokea benchi, Khamisi Mcha 'Vialli' imeifanya Azam kufikisha pointi 20 kutokana na mechi 10 sawa na Mbeya City ambayo ikiwa nyumbani kwao jijini Mbeya ilishinda bao 1-0 dhidi ya maafande wa JKT Ruvu.
Bao la Jeremiah John lilitosha kuwafanya wageni hao wa Ligi Kuu kuibuka na ushindia huo kwenye uwanja wa Sokoine na kuunga na Azam kileleni.
Timu hizo bado zinatofautiana mabao ya kufunga na kufungwa, Azam ikiwa na wastani mzuri.
Nao mabingwa wa zamani wa kandanda nchini, Mtibwa Sugar iliendelea kuzifanyia mauaji timu za majeshi baada ya jioni ya leo kuilipua Mgambo JKT kwa mabao 4-1 na kuiengua Yanga katika nafasi ya nne iliyokuwepo.
Mtibwa iliyopata ushindi wake wa tatu mfululizo, imefikisha jumla ya pointi 16 moja zaidi ya Yanga huku ikiwa na hazina kubwa ya magoli.
Magoli ya Mtibwa yalipachikwa wavuni na Nahodha Shaaban Nditti,Juma Luizio aliyefunga mawili na kumpumulia kinara wa mabao Amissi Tambwe wa Simba wakitofautiana kwa bao moja tu sasa. Luizio amefikisha mabao saba sawa na Elias Maguri aliyefunga mabao mawili jioni ya leo kuisaidia Ruvu Shooting kupata sare ya 2-2 dhidi ya Ashanti.
Bao jingine la Mtibwa lilifungwa na Mohammed Mkopi, huku Mgambo inayoburuza mkia kwa sasa ikipata bao la kufutia machozi kwa penati.
Katika mechi nyingine mkwaju wa penati uliopigwa na beki wa pembeni wa Kagera Sugar, Salum Kanoni uliisaidia timu yake kupata ushindi wa baoa 1-0 dhidi ya Coastal Union ya Tanga.
Hicho ni kipigo cha pili mfululizo kwa Coastal Union ambayo ilisafiri hadi kwenye uwanja wa Kaitaba kuwakabili wenyeji wao na kuwatungua bao hilo linaloifanya Kagera kufikisha pointi 14 na kushika nafasi ya saba.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea kesho kwa pambano moja tu la kukata na shoka kati ya Simba itakayoumana na Yanga katika mechi inayotarajiwa kuwa na ushindani mkali kutokana tambo na ubora wa timu hizo mbili.
Simba itashuka dimbani ikiwa na kumbukumbu wa kuchezea kichapo katika mechi yao ya mwisho dhidi ya watani wao hao Yanga waliowalaza mabao 2-0 kupitia 'mapro' Didier Kavumbagu na Hamis Kiiza 'Diego'.

Liverpool chupuchupu kwa Newcastle, Gerrard afunga la 100 EPL

Liverpool striker Daniel Sturridge heads in a goal against Newcastle
Sturridge akisawazisha bao la pili la Liverpool (Picha:BBC Sport)

NEWCASTLE United ikiwa dimba lake la nyumbani ya St Jamed Park ikicheza pungufu ya mchezaji mmoja kwa dakika 50, imeing'ang'ania Liverpool na kulazimisha sare ya mabao 2-2, wageni wakichomoa mara mbili ili kuambulia sare hiyo iliyowapeleka kileleni kwa muda kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England ikifikisha pointi 17, moja zaidi ya Arsenal itakayokuwa nyumbani kuialika Norwich City jioni hii.
Beki Yanga Mbiwa alijikuta akilimwa kadi nyekundu katika dakika ya 40 ya mchezo huo baada ya kumwamgusha Luis Suarez aliyekuwa akienda kumsalimia kipa wake Tim Krul wakati Newcastle ikiwa mbele kwa bao 1-0.
Kosa hilo la Yanga-Mbiwa, lilisababisha Liverpool kupata penati iliyotumbukizwa wavuni katika dakika ya 42 na nahodha Steven Gerrard, likiwa ni bao lake la 100 katika Ligi Kuu ya England.
Kabla ya Gerrard kupata bao hilo la kusawazisha, awali Newcastle ilikuwa mbele kwa bao lililofungwa na Yohan Cabaye katika dakika ya 23 akimalizia kazi nzuri ya Cheikh Tiote.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na wenyeji kujipatia bao la pili dakika ya 57 kupitia Paul Dummett , lakini katika dakika ya 72 mfungaji anayoongoza kwa kufumani nyavu kwa sasa EPL, Daniel Sturridge aliiepushia aibu Liverpool kwa kufunga bao la pili la kusawazisha na matokeo hayo kudumu hadi mwisho wa mchezo.
Hata hivyo Liverpool itakaa kwa muda kileleni kwani mechi mbalimbali zinaendelea kuchezwa jioni hii ambapo tayari Arsena wanaoongoza kwa bao 1-0 dhidi ya wageni wao Norwich, bao likifungwa na Jack Wilshere.

AS Roma yaizima Napoli 2-0

Mfungaji wa mabao yaliyoizamisha Napoli, Miralem Pjanic

KLABU ya AS Roma usiku wa kuamkia leo iliweza kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Italia Seria A baada ya kuwanyuka Napoli kwa mabao 2-0, mjini Roma.
Mabao mawili ya Miralem Pjanic yalitosha kuzima ubabe wa Napoli ambayo ilikuwa haijapoteza mechi yoyote katika ligi hiyo.
Mfungaji huyo alifunga mabao hayo katika dakika za nyongeza kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza na jingine la mkwaju wa penati dakika ya 71 yalifanya Roma kukaa kileleni ikiwa imejikusanyia jumla ya pointi 24, na kuiporomosha Napoli hadi nafasi ya tatu ikiipisha Juventus wanaolingana nao pointi 19 kushika nafasi ya pili.
Juventus leo inatarajiwa kushuka dimbani leo ugenini kuumana na Fiorentina katika mfululizo wa ligi hiyo, ambapo hata kama itapata ushindi bado haijaweza kuwaondoa Roma kileleni.

Simba ina nafasi kubwa kuitungua Yanga kesho, japo...!

Heka heka za Simba na Yanga

INGAWA viongozi na hata wanachama na mashabiki wa Yanga wana imani kubwa kwa timu yao kuibuka na ushindi kesho katika pambano la watani wa jadi linalofanyika kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, bado mabingwa watetezi hao wanapaswa kuwa makini kwani Simba ina nafasi kubwa zaidi ya kuiangusha Yanga.
Yanga wanaamini wana kikosi imara na kinachoweza kuwazima mapema Simba inayonolewa na kocha King Abdallah Kibadeni, lakini kwa mashabiki wa soka wanaofuatilia mechi za watani wa jadi bado Yanga ina kazi kubwa kwa Simba hata kama wanaonekana siyo imara zaidi ya vijana wa Jangwani.
Kama nilivyomnukuu winga wa zamani wa timu ya Yanga na TAMCO-Kibaha aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Wilaya ya Kinondoni (KIFA) Ramadhani Kampira Yanga wasipokuwa makini huenda kesho wakakoga kipigo bila kutarajia na kuleta mtafaruku mkubwa klabuni kwao.
Unajua kwanini?
Rekodi zinaonyesha kuwa wakati Yanga inapokuwa ikonekana kuwa imara na bora ndipo wanapoadhiriwa na Simba, kadhalika Simba inapoonekana kuwa ngangari zaidi huishia kuumia kwa watani zao hao.
Zipo baadhi ya mechi ambazo ukizifuatilia baina ya timu hizo zinaonyesha wakati klabu moja ikiwa juu kisoka na kuundwa na wachezaji wakali ndipo ilipokuwa aikiibishwa na ile iliyoonekana nyonge kuibuka kidedea.
Kwa mfano pambano baina ya timu hizo mwaka Julai 1988, Yanga ikihitaji sare ili kutwaa ubingwa na Simba iliyokuwa chovu ikisaka ushindi ili isihuke daraja, nini kilitokea? Yanga ililala kwa mabao 2-1.
Orodha ya mechi hizo ni ndefu lakini kwa uchache kuanzia miaka ya 1990 mpaka sasa utagundua ukweli huu na kinachosababisha kutokea kwa hali hiyo ni upande unaojiona bora na imara kujiamini kupita kiasi na mwishowe kukumbana na matokeo wasiyotarajiwa uwanjani kitu kinachoweza kuikuta Yanga kesho.
Kwa mfano hivi sasa Yanga inaoonekana kujiamini kupita kiasi hadi kufikia wanachama na wazee wa klabu hiyo kutangaza kwamba wataitungua Simba mabao 3-0, lakini wanasahau kuwa Simba siyo timu ya kubeza na inanolewa na makocha wenye kujua fitina za Simba na Yanga kwa ufasaha zaidi wakiwa wenyewe wameshawahi kucheza mechi za wapinzani hao enzi zao za uchezaji.
Kibadeni na msaidizi wake na hata kocha wa makipa, James Kisaka wanajua 'in and out' ya fitina za mechi za Simba na Yanga kulinganisha na Brandts na wasaidizi wake wengine ukimuondoa Fred Felix Minziro.
Sidhani kama Kibadeni na Julio watapenda kuadhiriwa na Yanga katika mechi ya kesho uwanja wa Taifa, ikizingatiwa kuwa kipigo chochote kwao kitawaondoa kileleni na kuwapisha watani zao kuwatangulia kutegemea na idadi ya mabao watakayofungwa.
Pia, imani yangu makocha hao watawajaza upepo wachezaji wao kupigana kiume ili kumbeba katika pambano hilo na kujihakikishia nafasi katika kikosi mbele ya Kibadeni ambaye huwa haangalii ukubwa wa jina la mchezaji zaidi ya nidhamu, kujituma uwanjani na mazoezini na namna ya kuisaidia timu.
Aina na wastani wa umri wa wachezaji waliopo Simba kulinganisha na Yanga unaweza kubaini kuwa Simba wana nafasi kubwa ya kuwapeleka Yanga mchakamchaka dimbani, iwapo tu wachezaji hao wa Simba watazingatia maelekezo ya walimu wao sambamba na kuonyesha vipaji vyao halisi walivyonavyo.
Kadhalika ipo imani iliyojengeka na kuaminika kwa wengi na hata wana Msimbazi wenyewe kwamba siku ya Jumapili ni SIKU YAO kama ilivyo kwa Yanga wanaoamini mechi ikichezwa JUMAMOSI asimilia zote kushinda ni LAZIMA.
Hata hivyo kwa vile soka halipo hivyo kwa kuangalia imani na historia ni vyema tusubiri tuone hiyo kesho kati ya vijana wa Jangwani na Msimbazi nani watakaolala mapema kwa aibu na wapi watakaokesha kwa furaha kushangilia ushindi?
Chini ni orodha ya mechi za watani hao wa jadi katika michuano ya Ligi tangu mwaka 1965 hadi Mei, 2013
JUNI 7, 1965
Yanga v Sunderland (Simba)
1-0
MFUNGAJI: Mawazo Shomvi dk. 15).

JUNI 3,  1966
Yanga v Sunderland (Simba)
3-2
WAFUNGAJI:
Yanga: Abdulrahman Lukongo dk. 54, Andrew Tematema dk 67, Emmanuel Makaidi dk. 83. Sunderland: Mustafa Choteka dk 24, Haji Lesso dk. 86.

NOVEMBA 26, 1966
Sunderland v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mustafa Choteka dk. 44.

MACHI 30, 1968
Yanga v Sunderland
1-0
MFUNGAJI: Kitwana Manara dk. 28.

JUNI 1, 1968
Yanga v Sunderland
5-0
WAFUNGAJI:
Maulid Dilunga dk. 18 (penalti), Dilunga dk. 43, Salehe Zimbwe dk. 54, Zimbwe dk. 89, Kitwana Manara dk. 86.

MACHI 3, 1969
Yanga v Sunderland
(Yanga ilipewa pointi za chee na ushindi wa mabao 2-0, baada ya Sunderland kugoma kuingia uwanjani).

JUNI 4, 1972
Yanga v Sunderland
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Kitwana Manara dk. 19,
Sunderland: Willy Mwaijibe dk. 11.

JUNI 18, 1972
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Leonard Chitete.

JUNI 23,  1973
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Haidari Abeid 'Muchacho' dk. 68.

AGOSTI 10, 1974
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Gibson Sembuli dk. 87, Sunday Manara dk. 97.
Simba: Adam Sabu dk. 16.
(Mechi ya kihistoria iliyochezwa Uwanja wa Nyamagana mjini Mwanza).

JULAI 19, 1977
Simba v Yanga
6-0
WAFUNGAJI:
Abdallah Kibadeni dk. 10, 42 na 89, Jumanne Hassan 'Masimenti' dk. 60 na 73, Selemani Sanga alijifunga dk. 20.

OKTOBA 7, 1979
Simba v Yanga
3-1
WAFUNGAJI:
Simba: Nico Njohole dk. 3, Mohammed Bakari 'Tall' dk. 38, Abbas Dilunga dk.72. Yanga: Rashidi Hanzuruni dk. 4.

OKTOBA 4, 1980
Simba v Yanga
3-0
WAFUNGAJI: Abdallah Mwinyimkuu dk. 29, Thuwein Ally dk. 82, Nico Njohole dk. 83.

SEPTEMBA 5, 1981
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Juma Hassan Mkambi dk. 42

APRILI 29, 1982
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Rashid Hanzuruni dk 2.

SEPTEMBA 18, 1982
Yanga 3-0 Simba
WAFUNGAJI:
Omar Hussein dk. 2 na 85, Makumbi Juma dk. 62.

FEBRUARI 10, 1983
Yanga v Simba.
0-0

APRILI 16, 1983
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Charles Mkwasa dk. 21, Makumbi Juma dk. 38, Omar Hussein dk. 84, Simba; Kihwelu Mussa dk. 14.

SEPTEMBA 10, 1983,
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Lila Shomari alijifunga dk. 72, Ahmed Amasha dk. 89.

SEPTEMBA 25, 1983
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk. 75,
Simba: Sunday Juma dk. 72.

MACHI 10, 1984
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 72.
Simba: Idd Pazi kwa penalti dk 20.

JULAI 14, 1984
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 39.
Simba: Zamoyoni Mogella dk. 17

MEI 19, 1985
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 6
Simba: Mohammed Bob Chopa dk. 30.

AGOSTI 10, 1985
Yanga v Simba
2-0

MACHI 15, 1986
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 44
Simba: John Hassan Douglas dk. 20.

AGOSTI 23, 1986
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila dk. 9, Malota Soma dk. 51
Yanga: Omar Hussein dk. 5.

JUNI 27, 1987
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Edgar 'Fongo' Mwafongo dk. 36.

AGOSTI 15, 1987
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Abeid Mziba dk. 14.

APRILI 30, 1988
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Justin Mtekere dk. 28
Simba: Edward Chumila dk. 25.

JULAI 23, 1988
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila 21, John Makelele dk. 58
Yanga: Issa Athumani dk. 36.

JANUARI 28, 1989
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Issa Athumani dk. 4, Abeid Mziba dk. 85
Simba: Malota Soma dk. 30.

MEI 21, 1989
Yanga v Simba
0-0

MEI 26, 1990
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mavumbi Omari dk 6.

OKTOBA 20, 1990
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk 33, Thomas Kipese dk. 82, Sanifu Lazaro dk. 89
Simba: Edward Chumila dk. 58.

MEI 18, 1991
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Said Sued 'Scud' dk.  7.

AGOSTI 31, 1991
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Said Sued Scud.

OKTOBA 9, 1991
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Athumani China dk. 3, Abubakar Salum 'Sure Boy' dk. 54.

NOVEMBA 13, 1991
Yanga v Simba
2-0

APRILI 12, 1992
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Kenneth Mkapa dk. 10.

SEPTEMBA 26, 1992
Simba v Yanga
2-0

OKTOBA 27, 1992
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Damian Morisho Kimti.

MACHI 27, 1993
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Said Mwamba Kizota dk. 47 na 57
Simba: Edward Chumila dk. 75.

JULAI 17, 1993
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Dua Said dk. 69.

SEPTEMBA 26, 1993
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Dua Said dk. 13.

NOVEMBA 6, 1993
Simba v Yanga
0-0

FEBRUARI 26, 1994
Yanga v Simba
2-0
MFUNGAJI: Mohammed Hussein 'Mmachinga' na James Tungaraza 'Boli Zozo'.

JULAI 2, 1994
Simba v Yanga
4-1
WAFUNGAJI:
Simba: George Masatu, Athumani China, Madaraka Selemani, Dua Saidi Yanga; Constantine Kimanda.

NOVEMBA 2, 1994
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Madaraka Selemani dk. 71

NOVEMBA 21, 1994
Simba v Yanga
2-0
WAFUNGAJI: George Lucas dk. 18, Madaraka Selemani dk. 42.

MACHI 18, 1995
Simba v Yanga
0-0

OKTOBA 4, 1995
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Mchunga Bakari dk. 79,
Yanga: Mohamed Hussein ÔMmachingaŐ dk. 40.

FEBRUARI 25, 1996
Yanga v Simba
2-0

SEPTEMBA 21, 1996
Yanga v Simba
0-0

OKTOBA 23, 1996
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk. 46

NOVEMBA 9, 1996
Yanga v Simba
4-4
WAFUNGAJI:
Yanga: Edibilly Lunyamila (penalti) dk. 28, Mustafa Hozza alijifunga dk 64, Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Sanifu Lazaro dk. 75.
Simba: Thomas Kipese dk. 7, Ahmed Mwinyimkuu dk. 43, Dua Saidi dk. 60 na 90.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

APRILI 26, 1997
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 16
Simba: Abdallah Msamba sekunde ya. 56

AGOSTI 31, 1997
Yanga v Simba
0-0

OKTOBA 11, 1997
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 52
Simba: George Masatu dk. 89
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya)

NOVEMBA 8, 1997
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Sekilojo Chambua dk. 85
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma)

FEBRUARI 21, 1998
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Akida Makunda dk. 46
Simba: Athumani Machepe dk. 88

JUNI 7, 1998
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 28
Simba: Abuu Juma (penalti) dk. 32

MEI 1, 1999
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idd Moshi dk. 59, Kalimangonga Ongala dk. 64, Salvatory Edward dk. 70, Simba: Juma Amir dk. 12.

AGOSTI 29, 1999
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Bakari Malima dk. 49, Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk 71

JUNI 25, 2000
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Steven Mapunda dk. 59 na 72
Yanga: Idd Moshi dk. 4.

AGOSTI 5, 2000
Yanga v Simba
2-0
MFUNGAJI: Iddi Moshi 37 na 47. (Alifunga mabao hayo, akitoka kwenye fungate ya ndoa yake)

SEPTEMBA 1, 2001
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Joseph Kaniki dk. 76

SEPTEMBA 30, 2001
Simba v Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
Simba: Joseph Kaniki dk. 65,
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 86
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza)

AGOSTI 18, 2002
Simba v Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
Simba: Madaraka Selemani 65
Yanga: Sekilojo Chambua (penalti). dk. 89

NOVEMBA 10, 2002
Simba v Yanga
0-0

SEPTEMBA 28, 2003

Simba v Yanga
2-2
WAFUNGAJI:
Simba: Emmanuel Gabriel dk. 27 na 36
Yanga: Kudra Omary dk. 42, Heri Morris dk. 55

NOVEMBA 2, 2003
Simba v Yanga
0-0

AGOSTI 7, 2004
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Shaaban Kisiga dk. 64, Ulimboka Mwakingwe dk. 76
Yanga: Pitchou Kongo dk. 48

SEPTEMBA 18, 2004
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Athumani Machuppa dk. 82

APRILI 17,  2005
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Nurdin Msiga dk. 44, Athumani Machupa dk. 64,
Yanga: Aaron Nyanda dk. 39
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

AGOSTI 21, 2005
Simba v Yanga
2-0
MFUNGAJI: Nico Nyagawa dk. 22 na 56
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

MACHI 26, 2006
Simba v Yanga.
0-0

OKTOBA 29, 2006
Simba v Yanga
0-0

JULAI 8, 2007
Simba v Yanga
1-1 (dakika 120)
WAFUNGAJI:
Simba: Moses Odhiambo (penalti dk. 2)
Yanga: Said Maulid (dk. 55).
(Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya sare hiyo).
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

OKTOBA 24, 2007:
Simba Vs Yanga
1-0
Mfungaji: Ulimboka Mwakingwe
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

APRILI 27, 2008:
Simba Vs Yanga
0-0

OKT 26, 2008
Yanga Vs Simba
1-0
MFUNGAJI: Ben Mwalala dk15.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

APRILI  19, 2009
Simba Vs Yanga
2-2
WAFUNGAJI:
SIMBA: Ramadhan Chombo dk 23, Haruna Moshi dk 62
YANGA: Ben Mwalala dk48, Jerry Tegete dk90
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

OKTOBA 31, 2009
Simba Vs Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mussa Hassan Mgosi dk 26
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

APRILI 18, 2010
Simba Vs Yanga
4-3
WAFUNGAJI:
SIMBA: Uhuru Suleiman dk 3, Mussa Mgosi dk 53 na 74, Hillary Echesa dk 90+
YANGA: Athumani Iddi dk 30, Jerry Tegete dk 69 na 89

OKTOBA 16, 2010:
Yanga Vs Simba
1-0
MFUNGAJI: Jerry Tegete dk 70

MACHI 5, 2011
Simba Vs Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
YANGA: Stefano Mwasyika (penalti) dk 59.
SIMBA:  Mussa Mgosi dk 73.

OKTOBA 29, 2011
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Davies Mwape dakika ya 75


MEI 6, 2012
Simba 5-0 Yanga
WAFUNGAJI:
Emmanuel Okwi dk 1 na 65, Patrick Mafisango pen dk 58, Juma Kaseja pen dk 69 na Felix Sunzu pen dk 74.

OKT 3, 2012
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
SIMBA: Amri Kiemba dk 3,
YANGA: Said Bahanuzi dk 64

MEI 6, 2013
Simba 0-2 Yanga
WAFUNGAJI:  Didier Kavumbagu dk 5 na Hamis Kiiza dk 62

Huyu ndiye Wema Isaac Sepetu 'Beautiful Onyinye'

Wema Sepetu oct 2013 
Swali: Wema ni nani?
Jibu: Wema Sepetu is a girl, i can say a Lady mwenye umri wa miaka 24 kutoka familia ya Isack Abraham Sepetu, a darling, a libra.. a girl who is very ambicious, i love my self…

Swali: Siku yako ya kwanza shuleni ilikuaje?
Wema: Siku ya kwanza tumeenda nikakutana na msichana flani hivi anaitwa Shubira nakumbuka mpaka leo, alikua rafiki yangu wa kwanza tulikutana shuleni nilikua na miaka minne… tumekaa nikaanza kulia kwa sababu ilikua sehemu mpya, mazingira mapya baada ya hapo tukazoea.

Swali:Shule ilikua vipi kipindi unasoma?
Wema: Naweza kusema kipindi ambacho niko shule, Mwalimu wangu sijawahi kukaa hata siku moja kumfikiria mara mbili na haijawahi kutokea kwamba hata mwalimu akaweza kufanya labda matamanio au kutaka kitu chochote, hamna kitu kama hicho

Swali: Utafanya nini ikitokea umerudi shule?
Wema: Ningepata nafasi ya kurudi shule, academic nini uniform na nini… ningejaribu kuifanya more fun, a place where everybody can be just himself or herself and just be Wema Sepetu kwa sababu right now this is my time!!

Swali: Ni nani ambaye uko karibu nae kwenye familia yenu?
Wema: Dada yangu wa kwanza kuzaliwa anaitwa Tunu, tunakwenda sawa kwenye many many ways, kipindi mama yangu alivyonizaa aliumwa akalazwa hivyo dada yangu ndio akawa ananihudumia kama mtoto wake, ananinywesha uji… anahakikisha nimekunywa maziwa on time na mpaka leo ananiita my baby and I call her my mami… mtu wa pili ni dada yangu wa tatu, she is my bestfriend… baba yangu atabaki kuwa baba yangu tu, mama yangu ni my guardian Angel, my heart my darling.
Swali: Ulishawahi kugombana na ndugu zako?
Wema: Yeah nimegombana na dada yangu mpaka sasa hivi hatuongei, sio kitu chepesi….

Swali: Unaamini Mama yako ni mkorofi?
Wema: Linapokuja swala la mama yangu huwezi ukasema kwamba ni mkorofi lakini hapendi nikikosea wala kufanya kitu ambacho sicho…. kutokupenda kwake inafikia point anakua na hasira sana alafu njia ya kuonyesha hasira yake ndio level ya juu, yeye anafikiria kwamba anatengeneza ila badala ya kutengeneza ndio anaharibu.

Wema akiwa na mama yake
Swali: Wema ni mkorofi?
Wema: Mimi sio mkorofi, mtu ambae hanijui ndio ataniita mkorofi ukishanijua yani tutafika mbali lakini usiponijua na hujui ninachonitaka ndio tatizo.

Swali: Unajisikiaje kuwa Wema Sepetu?
Wema: Kuwa Wema Sepetu sio kitu rahisi, haiwezi kuwa kama watu wanavyofikiria  na haitakua hivyo kwa sababu ni maisha ambayo naishi, ni mpaka uone maisha ninayoishi ndio unielewe… yani hata kujaribu kuieleza ili uielewe napata tabu… mashabiki wangu wananielewa sana na uhusiano wangu na wao ni mzuri na ni tofauti na uhusiano kati yangu na familia yangu’

Swali: Unachukulia vipi unaposemwa ama kuandikwa vibaya?
Wema: Katika vitu vyangu ambavyo mtu wa nje anaweza kuviona kama vile… Mungu wangu Wema ana nini, mi navichukulia kama changamoto… mi naona kuna kitu special kuhusu mimi, kwa nini wasiseme watu wengine?

Swali: Unaamini wewe ni mrembo?
Wema: I am beautiful, naamini kwamba mimi ni beautiful kwa sababu nina pure heart… ni kitu Mwenyezi Mungu alichonibariki nacho.


Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu, Kuna maswali....?!

Swali: Kitu gani unachojivunia kwamba kinakutofautisha na wasanii wengine?
Wema: Ninachojivunia… uelewa wangu, I am very very smart.. ni mtu ambae ukiniambia kitu, fasta…. na hata kama sijui kitu, kujiua itanichukua muda mfupi, ability kusimama na kuongea na nikasikika, lugha…. hivyo ni vitu ambavyo najivunia sana

Swali: Unavuta sigara?
Wema: Ndio, ninapokua na msongo wa mawazo sana huwa nafanya hivyo  ili kuondoa mawazo na inaweza kutokea mara moja kwa mwezi.

Swali: Ni kweli kwamba wewe ni limbukeni wa umaarufu?
Wema: Sijaacha ustaa uniendeshe, unajua kuna wale watu wanaacha ustaa uwameze mpaka wanabadilisha kuongea, watu wengine wanaacha ule ustaa unawaendesha mwisho wa siku unaanza kuishi maisha ambayo hawana inafika point unaishi kama mtumwa mwisho wa siku unaishi maisha ambayo huna, unaanza kuumia Mungu wangu nimeshazoea kuishi maisha yale,  ishi vile ambavyo unaweza… huna pesa, huna! mimi ni mtu ambae ninaweza kuamka nasikia hamu ya kula mihogo, nafanya kitu ninachopenda na sio anachotaka mwingine’

Swali: Gucci na Vanny ni kina nani kwako?
Wema: My precious, kipenzi changu ni Vanny, katakufanya tu ukapende…. Gucci staa anajifanyaga kama yeye mtu tu wa kuchil!

Swali: Unaamini katika ushirikina?
Wema: Ushirikina najua kwamba upo, uchawi kama uchawi upo worldwide ila sipendi kujishirikisha manake sitaki siku moja kuwa mtumwa, mimi mtoto wa Kiislamu nafanya kisomo nachinja kila baada ya muda so naamini ukifanya hivyo unajikinga na vitu vingi.
Swali: Umeshawahi kurogwa?
Wema: Nimeshawahi kurogwa, imeshawahi kunitokea kabisa yani… ni kitu kingine ambacho huwa sipendi kukizungumzia.

Swali: Ulishawahi kwenda kwa Mganga?
Wema: Siwezi kuficha, wamekuja wengi ambao wanataka kunipeleka wengine mpaka kuniletea Waganga nyumbani kwangu lakini Quran mimi ndio mganga wangu namba moja.

Swali: Unafikiri kuna Wasanii wenzako ambao wanakuchukia?
Wema: Unategemea nini once ukishakua katika spotlight, hautegemei kuwa na watu wazuri karibu yako lazima wengine watakua ni wabaya na sio kila mmoja atakua anakuchekea kwa uzuri, wengine sio kutoka moyoni, wanakuchekea tu kwa sababu hawana choice.

Swali: Nani alikua mpenzi wako wa kwanza?
Wema: Sitaki kumtaja bwana….
wema na Diamond
Swali: Inasemekana unapenda mahusiano ya kimapenzi na watu maarufu?
Wema: Sio kwamba Wema anapenda kuwa na wapenzi maarufu, ni field ambayo tuko, tuko kwenye kiwanda kimoja kwa hiyo kwangu imekua iko hivyo, ni watu ambao mtakua mna interest zinaendana..

Swali: Umeshawahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na watu wangapi?
Wema: Wanne, watano au Wanaume sita hehhehe!!

Swali: Mlianza vipi mapenzi na Diamond?
Wema: Tulikua na hii Chemistry inaendana ilikua crazy, baada ya yeye kuniandikia msg kwenye facebook na kuniambia ananipenda, ni mtu ambae nilipata uzoefu mapenzi yanaweza kuwaje, nilipitia kwenye furaha na huzuni nikiwa na yeye…. kilichotokea kimetokea

Swali: Kuna ushindani wowote kati yako na Diamond?
Wema: Once upon a time kulikua na Diamond na Wema, na hawa watu walifall inlove…. watu wanajaribu sana kutulinganisha au tunaonekana tunashindana labda kwa sababu yeye anafanya vizuri kwenye industry yake na mimi nafanya vizuri kwenye industry yangu, mi sijawahi hata siku moja kushindana na Diamond…. mi kuimba siwezi.

Wema na Kajala
Swali: Kajala Masanja ni nani kwako?
Wema: Kajala ni rafiki, dada…. ndugu ambae hayuko kwenye ukoo wa Sepetu lakini uhusiano wangu na wake kwenye urafiki toka mwanzo sidhani kama nimewahi kuwa na uhusiano huu na mtu yeyote, watu wanadhani kwamba nimeanza kumjua juzi… tokea mwaka 2007 mi nimeanza kumfahamu Kajala mpaka tukawa marafiki sana hadi tunajikuta tumevaa sare.

Swali: Wazo la kumtolea Kajala dhamana ya milioni 13 lilitoka wapi?
Wema: Nilimuangalia Kajala analia pale kizimbani, aidha ilipwe faini au aende jela…. kilikua ni kitu ambacho hakijapangwa, ilikua suprise kwetu wote ila nilichokua nataka ni Kajala kuwa huru kwa hiyo kilichoweza kufanyika kilifanyika.

Wema wakati wa kesi yake iliyomalaza mahabusu
Swali: Ulijisikiaje siku tatu ulizolala Mahabusu?
Wema: Haikua nzuri kabisa, ni siku tatu mbaya kwenye maisha yangu… hakuna binadamu ambae hapendi uhuru, kwanini nilimsaidia Kajala na kupata nguvu ya kutoa hizo milioni 13? kwa sababu nimekuepo hapo… mimi siku tatu zilikua balaa sasa mwenzangu mwaka mmoja naa? ingekuaje? hata kama nisingemsaidia Kajala alafu Kajala ndio angekaa miaka hiyo 7 sijui 8 jela mimi nisingeweza kuishi, sio Wema Sepetu alivyo’

Swali: Best Werema ni nani katika kampuni yako?
Wema: Bestizzo ni blogger wangu na mpiga picha wangu, anarun kila kitu kinachohusu kampuni kwenye social network Website nini…

Swali: Kwanini uliamua kufanya nae kazi?
Wema: Kipindi cha kwanza niliona kumpa kazi ingeleta matatizo flani lakini nikafikiria, namjua Bestizzo alikua akifanya kazi kwa Diamond na alikua mfanyakazi mzuri, sijui ni kitu gani kilimfanya aondoke kwa Diamond kwa sababu mimi wakati sikua kwenye uhusiano mzuri na Diamond, Best bado alikua kwa Diamond na kipindi hicho hata bado nilikua sijafungua kampuni, hata alikua haniombi kazi ila alihitaji nimuunganishe na wengine’

Wema akiwa na Kadinda
Swali: Uko vipi na Tinny Dad, Pettman na Martin Kadinda?
Wema: Tiny na Petti ni watu wangu wa karibu sana, nimewajua kwa muda mrefu na wananijua na ninawajua.. Kadinda kabla ya kuwa meneja wangu alikua rafiki yangu, hakua rafiki yangu wa hivyo… tulikua hatuonani hata miezi sita lakini tukikutana namwambia yote yaliyopita, mwaka juzi ndio Martin akasema ngoja niwe Meneja wako, hatukua hata na mikataba mwanzoni… tukajaribisha na tukafanikiwa mpaka leo niko nae.


credit: millardayo

Jambazi la kike lapigwa kichwa kudhibitiwa lisipore fedha


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas
JARIBIO la kupora fedha katika kituo cha M-Pesa lililofanywa na Anita Kaburu (27),  pamoja na mwenzake wakitumia bastola na bunduki, lilishindikana baada ya mteja mmoja kumpiga kichwa na kufanikiwa kumdhibiti.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, alisema jana kuwa Anita ambaye ni mkazi wa Usa River wilayani Arumeru, alivamia kituo cha M-Pesa kinachomilikiwa na Stela Mrema akiwa na mwanamume mmoja.

Alisema watu hao wanaodaiwa kuwa ni majambazi, baada ya kufika kwenye kituo cha huduma hiyo maeneo ya Shamsi jijini hapa majira ya saa 6:00 mchana wakijifanya wateja,  ghafla mmoja wao (Anita) alichomoa bastola kwenye mkoba wake na mwenzake akatoa bunduki na kuamrisha wapewe fedha.

“Baada ya kuingia walijifanya kuhitaji huduma ya M-Pesa, ghafla yule mwanamke alitoa bastola kwenye mkoba wake na mwanaume naye alitoa bunduki na kuwaamuru watoe pesa na simu… ndipo yule mteja alimpiga kichwa yule mwanamke na kisha kupiga kelele za kuomba msaada hivyo walifanikiwa kumdhibiti,” alisema.

Hata hivyo, alisema mwenzake alifanikiwa kukimbia. Alisema baada ya polisi kumtaka Anita awataje wenzake, polisi waliwakamata watuhumiwa wanne waliokuwa wamepanga kufanya uporaji huo.

Kamanda Sabas aliwataja waliokamatwa kuwa ni Abdulahman Jumanne Idd (27) ambaye ni mwangalizi wa Kampuni ya Ulinzi ya KK na mkazi wa Shamsi, Simon Martine au Mapanki (45) mkazi wa Kwa Mrombo, Hashimu Ally (30) ambaye ni mpanda milima na mkazi wa Ngarenaro na Charles Luangano (24) ambaye pia ni mlinzi wa kampuni ya ulinzi ya KK.

Alisema watuhumiwa hao baada ya kufanyiwa upekuzi walikamatwa na bunduki aina ya shotgun, bastola aina ya bereta na risasi sita za bastola. Alisema watafikishwa mahakamani Jumatatu.
CHANZO: NIPASHE

Mdogo wa Super Nyamwela akwaa kashfa nzito


Juma Nyamwela (nyuma) anayedaiwa kulawiti mtoto

MNENGUAJI wa kiume wa Mashujaa Band, Juma Nyamwela (Nyamwela Jr) amekamatwa na polisi kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa kiume wa umri wa miaka sita.

Kwa sasa mnenguaji huyo yupo kituo cha polisi cha Mabatini Kijitonyama jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku ya tatu tangu akamatwe kwa tuhuma hizo.

Habari za uhakika kutoka kituoni hapo zinasema katika maelezo ya awali, mnenguaji huyo amekiri kosa.

Chanzo cha Chetu kimeeleza kuwa huenda mnenguaji huyo akafikishwa mahakamani siku ya Jumatatu.
Nyamwela Jr (wa tatu toka kulia) akiwa na wasanii wenzake wa Mashujaa
 Nyamwela ambaye ni mdogo wake na Super Nyamwela wa Extra Bongo, aliwahi kuitumikia TOT Plus kabla ya kujiunga na Mashujaa Band. 

Mwaka 2007 aliibuka bingwa wa mashindano ya dansa bora wa kiume yaliyoandaliwa na Usher Family na kujinyakulia zawadi ya gari.

Source:- Salute5

Friday, October 18, 2013

Miss Universe Tz 2013 akabidhiwa bendera

MREMBO wa Miss Universe Tanzania 2013 Betty Boniface Omara amekabidhiwa bendera leo na Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Khamis Kagasheki.

Zoezi hili limefanyika katika ukumbi wa mkutano wa wizara hiyo tayari kwa safari yake ya kwenda kwenye mashindano ya Miss Universe yatakayofanyika Moscow nchini Urusi mapema mwezi Novemba.

Akimkabidhi bendera huku akimpongeza waziri Kagasheki pia amemtakia mafanikio mema huko aendako.

Betty pia aliwaahidi watanzania kuwa mbali na kurudi na ushindi lakini pia ataenda kuitangazia dunia kuacha kutumia nakshi(Mapambo) yanayotumia pembe za ndovu ili kumaliza tatizo la ujangili nchini.

Zoezi la kukabidhiwa bendera lilifanyika likishuhudiwa na Mkurugenzi wa Kitaifa Miss Universe Tanzania Maria Sarungi Tsehai.

Mashindano ya Miss Universe Tanzania 2013 yamedhaminiwa na hifadhi ya Taifa Tanapa na Mrembo Betty Boniface ameshaanza kutangaza hifadhi hizi kwa njia mbalimbali hapa nchini na nje ya nchi.
 Mrembo wa Miss Universe Tanzania 2013 Betty Boniface Omara akipokea bendera ya taifa leo kutoka Waziri Maliasili na Utalii, Hamisi Kagasheki.

Mbeya City, Azam kuing'oa Simba kileleni VPL?

Vijana wa Mbeya City
Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea kutimua vumbo kesho (Oktoba 19 mwaka huu) kwa mechi tano huku Mbeya City ikiikaribisha JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, ambapo ushindi wowote unaweza kukwea kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo kwa mara ya kwanza.
 

Timu hiyo iliyopanda daraja msimu huu ina pointi 17 sawa na Azam ambayo nayo ina nafasi ya kuing'oa Simba kama itaifunga Oljoro JKT wanaoumana nao jijini Arusha.

Simba wanaoongoza msimamo wa ligi hiyo kwa sasa ikiwa na pointi 18 na yenyewe itashuka dimbani Jumapili kuwakaribisha watani zao Yanga katika uwanja wa Taifa.


Mbali na mechi ya Mbeya City na JKT Ruvu na ile ya Oljoro dhidi ya Azam mechi nyingine zitazkazochezwa kesho ni Mtibwa Sugar na Mgambo Shooting (Uwanja wa Manungu, Turiani), Ashanti United na Ruvu Shooting (Azam Complex Chamazi, Dar es Salaam) na Kagera Sugar dhidi ya Coastal Union (Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba).

Wakati huo huo, Ligi Daraja la Kwanza (FDL) nayo inaendelea katika viwanja nane kesho (Oktoba 19 mwaka huu) huku Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam ukiwa mwenyeji wa mchezo kati ya African Lyon na Friends Rangers.

Nayo Villa Squad itacheza na Green Warriors katika Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Polisi Morogoro na Kimondo (Uwanja wa Jamhuri, Morogoro), Lipuli na Kurugenzi (Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa) na Mkamba Rangers dhidi ya Majimaji (Uwanja wa CCM Mkamba, Morogoro).

Toto Africans na Mwadui (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza), Polisi Dodoma na Polisi Tabora (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma), wakati Polisi Mara na pamba zitacheza kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

Magari Maalum tu, pambano la Simba na Yanga J2

Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura
MAGARI yenye shughuli maalumu tu ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia uwanja wakati wa mechi ya Simba na Yanga itakayochezwa keshokutwa (Jumapili) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi itaanza saa 10 kamili jioni, na kila timu inaruhusiwa kuingia na magari matatu tu; gari la timu na mengine mawili ya viongozi. Ukaguzi wa kuingia uwanjani ni kwa watu wote, kwani utaratibu huo si wa kumdhalilisha mtu bali lengo lake ni kuhakikisha usalama.
Vilevile watu hawataruhusiwa kuingia uwanjani na mifuko ya aina yoyote ikiwemo mabegi, isipokuwa kwa waandishi wa habari wanaotumia mabegi hayo kwa ajili ya kubebea kamera zao. Pia hakuna wafanyabishara watakaoruhusiwa kufanya biashara katika maeneo yanayozunguka uwanja.
Kwa washabiki watakaokuwa katika mazingira ya kuwa kero kwa wenzao wakiwemo walevi hawataruhusiwa kuingia uwanjani, pamoja na wale wenye silaha kama bastola ambapo wakikamatwa wafikishwa polisi na baadaye kufunguliwa mashtaka kortini.
Barabara ya Uwanja wa Taifa itafungwa kuanzia saa 2 asubuhi upande wa Chang’ombe, hivyo washabiki wanatakiwa kununua tiketi zao mapema kesho (Jumamosi) ambapo zitaanza kuuzwa katika vituo mbalimbali kuanzia saa 4 asubuhi.
Vituo hivyo ni mgahawa wa City Sports Lounge, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala, Uwanja wa Uhuru, mgahawa wa Brake Point uliopo Kijitonyama na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.

TFF bado ina kinyongo na Shafii Dauda yamchinja, ikitangaza majina wagombea uchaguzi mkuu, mwenyewe adai hakubali

Shafii Dauda 'Tishio' akiwa kwenye shughuli zake za habari
 KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imetangaza orodha ya mwisho ya wagombea wa uchaguzi wa TFF na wa Bodi ya Ligi (TPL Board) utakaofanyika baadaye mwezi huu, 'ikimchinja' tena Shafii Dauda katika kinyang'anyiro hicho.
Uchaguzi wa Bodi ya TPL utafanyika Oktoba 25 mwaka huu wakati ule wa TFF utafanyika Oktoba 27 mwaka huu. Kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa TPL Board na ule wa TFF zimeanza leo (Oktoba 18 mwaka huu)  zitamalizika siku moja kabla ya uchaguzi saa 10 kamili alasiri. Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Hamidu Mbwezeleni amewataja wagombea kwa upande wa TPL Board kugombea uenyekiti ni Hamad Yahya Juma (Mtibwa Sugar), Makamu Mwenyekiti ni Said Muhammad Said Abeid (Azam). Wanaowania ujumbe wa Bodi ya Uendeshaji ni Kazimoto Miraji Muzo (Pamba) na Omary Khatibu Mwindadi (Mwadui).
Wagombea kwenye uchaguzi wa TFF ni Athuman Jumanne Nyamlani na Jamal Emily Malinzi (Rais), Imani Omari Madega, Ramadhan Omar Nassib na Wallace Karia (Makamu wa Rais).
Kwa upande wa wajumbe wa Kamati ya Utendaji ni Kalilo Samson (Kanda namba 1- Geita na Kagera), Jumbe Odessa Magati, Mugisha Galibona, Samwel Nyalla na Vedastus Lufano (Kanda namba 2- Mara na Mwanza), Epaphra Swai na Mbasha Matutu (Kanda namba 3- Shinyanga na Simiyu).
Ali Mtumwa, Elley Simon Mbise na Omar Walii Ali (Kanda namba 4- Arusha na Manyara), Ahmed Idd Mgoyi na Yusuf Hamis Kitumbo (Kanda namba 5- Kigoma na Tabora), Ayubu Nyaulingo na Blassy Mghube Kiondo (Kanda namba 6- Katavi na Rukwa), Ayoub Shaibu Nyenzi, David Samson Lugenge, John Exavery Kiteve, Lusekelo Elias Mwanjala (Kanda namba 7- Iringa na Mbeya).
James Patrick Mhagama na Stanley William Lugenge (Kanda namba 8- Njombe na Ruvuma), Athuman Kingombe Kambi, Francis Kumba Ndulane na Zafarani Mzee Damoder (Kanda namba 9- Lindi na Mtwara), Hussein Zuberi Mwamba, Stewart Ernest Masima, Charles Komba (Kanda namba 10- Dodoma na Singida), Farid Nahdi, Geofrey Irick Nyange, Juma Abbas Pinto, Riziki Juma Majala) na Twahil Twaha Njoki (Kanda namba 11- Morogoro na Pwani).
Davis Elisa Mosha, Khalid Abdallah Mohamed (Kanda namba 12- Kilimanjaro na Pwani), Alex Crispine Kamuzelya, Kidao Wilfred Mzigama, Muhsin Said Balhabou na Omary Isack Abdulkadir (Kanda namba 13- Dar es Salaam).
Mbwezeleni amewataka wagombea kufanya kampeni bila kukashfu wenzao, kwani Kanuni ya Uchaguzi za TFF toleo la 2013 inatoa fursa kwa Kamati ya Uchaguzi kuwaondoa wagombea wa aina hiyo kwenye uchaguzi.
Aliyekuwa mgombea wa Ujumbe wa Kanda ya 13, Shafii Dauda ametoswa licha ya kulipa faini aliyotakiwa kulipa ndani ya siku tatu na Kamati ya Maadili ya Rufaa.
Akihojiwa muda mfupi uliopita na kituo cha Uhuru Fm, Shafii amesema hakubali hata kidogo na ameshaanza mchakato wa kupeleka malalamiko yake FIFA kwa madai kuna mchezo mchafu amefanyiwa na kamati hiyo ya uchaguzi ya TFF.
Shafii alisema tangu awali kulikuwa na zengwe kwa lengo la kuwabeba wagombea fulani kutetea nafasi zao na dai kwamba hana uzoefu ni sababu tu, lakini alisema hakubali haki yake ipotee bure na Jumapili atakwea pipa kwenda Zurich makao makuu ya FIFA kupeleka mashtaka yake.
Baadhi ya wadau wa soka waliozungumza na MICHARAZO wamedai kushtushwa na maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF wakidai ni kama kutaka kuleta malumbano yasiyokuwa na sababu yoyote.

Thursday, October 17, 2013

Simba yapumua, Mombeki arejea dimbani kuivaa Yanga J'2

Hii ndiyo kazi ya Mombeki kuwaokotesha mipira mabeki na kipa
KLABU ya soka ya Simba imepumua na kuwa na matumaini makubwa ya kumtumia mshambuliaji wake mrefu na mwenye nguvu, Betram Mombeki aliyekuwa akitajwa huenda asiwepo kwenye pambano lao na watani za Yanga.
Mombeki alitajwa yupo katika hatihati ya kulikosa pambano hilo la watani wa jadi litakalochezwa kwenue uwanja wa Taifa siku ya Jumapili baada ya kujiumiza mazoezi katika kambi ya timu hiyo iliyopo Bagamoyo.
Hata hivyo habari njema kwa wanachama na mashabiki wa Simba ni kwamba mshambuliaji huyo aliyesajiliwa na Simba akitokea Pamba ya Mwanza, amerejea tena uwanjani na kuna uwezekano mkubwa Jumapili atashirikiana na mfumani nyavu mahiri, Amissi Tambwe kuichachafya ngome ya Yanga.
Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga aliiambia MICHARAZO kuwa, Mombeki amerejea tena uwanjani baada ya hali yake kutengemaa na kuwapa matumaini makubwa ya kushuka dimbani Jumapili kuiangamiza Yanga.
Kamwaga alisema hata hivyo kikosi chao bado kitaendelea kukosa huduma za wachezaji wao nyota kama Henry Joseph, Issa Rashid 'Baba Ubaya' na Miraj Adam.
"Tunashukuru hofu ya kumkosa Mombeki imeondoka baada ya mshambuliaji huyo kurejea tena dimbani, japo Simba itawakosa Henry Joseph ambaye hayupo kambini, Baba Ubaya, Miraj Adam na Abdallah Seseme ambao ni majeruhi," alisema Kamwaga.
Kamwaga alisema kikosi chao kina morali na ari kubwa ya kushinda mechi ya Jumapili, licha ya kudai litakuwa pambano gumu.
Pia alisema katika kuwatia motisha wachezaji ili kuigaragaza Yanga kwenye uwanja wa Taifa, viongozi na 'matajiri' wa Simba wanatarajia kuteta na wachezaji siku ya Jumamosi kwa lengo la kuwaweka sawa kisaikolojia pamoja na kuwatia morali zaidi ili kuwashinda Yanga.
"Viongozi na matajiri wa Simba wataitembelea kambi na kuzungumza na wachezaji kati ya Ijumaa na Jumamosi ili kuwaweka sawa na kuhakikisha Yanga anakufa Jumapili Taifa," alisema Kamwaga.
Simba na Yanga zitakutana katika mchezo huo, huku Simba ikiwa na deni la kulipa kisasi cha kipigo walichopewa katika mechi yao ya mwisho ya ligi iliyopita iliyochezwa Mei mwaka huu ambapo Yanga ilishinda mabao 2-0.