STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 21, 2015

Chelsea wabanwa, Man Utd yafa, Arsenal raha

Ben Mee rises above the Chelsea defence to equalise for Burnley against Premier League leaders Chelsea at Stamford Bridge
Ben Mee akiisawazishia Burnley bao kwa kichwa
Mee wheels away in celebration after finding the target with a header to level proceedings at Stamford bridge with 10 minutes left
Oyooooooooooo!
Manchester United must get used to their new style of play under Louis van Gaal, according to Gary Neville
hoi
Cazorla is congratulated by his team-mates as Arsenal looked to pick up an eighth win in nine games
Arsenal kwa raha zao
Wilfried Zaha skips past Nacho Monreal in the opening moments, and the England winger caused his full back plenty of problems
ilikuwa vita
QPR walip[okuwa wakizamishwa ugenini
WAKATI vinara wa Ligi Kuu ya England, Chelsea wakingángániwa nyumbani kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1, Mashetani Wekundu, Manchester United wamenyukwa mabao 2-1 na Swansea City, huku Arsenal ikingára ugenini kwa kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace.
Chelsea wakiwa kwenye uwanja wao wa Stanford Bridge walitangulia kuandika bao la kuongoza lililofungwa na beki wake Branslav Ivanovic katika ya 14 na wageni Burnley kuchomoa bao hilo dakika tisa kabla ya mchezo kumalizika kupitia kwa Ben Mee.
Chelsea itajilaulumu kwa kushindwa kuibuka na ushindi nyumbani kutokana na kutawala mchezo huo na washambuliaji wake Eden Hazard na Diego Costa wakikosa mabao ya wazi.
Sare hiyo imeifanya Chelsea kufikisha pointi 60 na kutoa fursa kwa wapinzani wao mabingwa watetezi Manchester City kupunguza pointi zilizokuwapo kwani mpaka muda huu wa mapumziko City wanaoongozxa mabao 3-0 dhidi ya Newcastle United.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Arsenal ikiwa ugenini imeshinda mabao 2-1, Manchester Utd ikipigwa 2-1 na Swansea City, wakati Aston Villa wameendelea kutetepa kwa kukubali kichapo cha 2-1 wakiwa nyumbani toka kwa Stoke City huku QPR wakilala ugenini 2-1 mbele ya Hully City na timu za Sunderland na West Bromwich wakitoka suluhu ya kutofungana.

Barcelona yazamishwa nyumbani na Malaga

Barcelona 0-1t Bat BA Malaga
Juanmi akiitungua Barcelona leo
Barcelona forward Lionel Messi (left) vies with Malaga's forward Samuel Castillejo (right) on Saturday
Messi hakufua dafu leo kwa Malaga siku chache kabla ya Barcelona kuvaana na Manchester City kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
KLABU ya Barcelona ikiwa dimba la nyumbani la Camp Nou imekubali kipigo cha bao 1-0 mbele ya Malaga katika mfululizo wa Ligi ya Hispania, La Liga.
Kipigo hicho cha nne kwa Barcelona msimu huu katika ligi hiyo kimezidi kuongeza ushindani wa mbio za ubingwa dhidi ya watetezi Real Madrid ambayo watashuka dimbani kesho wakiwa ugenini.
Bao pekee la wageni Malaga mbele ya Barcelona liliwekwa kimiani na  Juanmi katika dakika ya saba ya mchezo huo na kungángánia hadi mwisho na kuwaacha Barcelona wakiwa hoi nyumbani.
Mechi nyingine inayochezwa hivi sasa Valencia wakiwa ugenini waongoza bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Cardoba.

Jahazi la Mtibwa lazidi kuzama, Coastal hoi, Kagera yaua

Mtibwa Sugar iliyoipokea kichapo cha nne mfululizo leo kwa Mgambo JKT
http://api.ning.com/files/cPakA0chAEyfyqjZRP3k2djpZ9GyxNW23W69D7FY4fYhsuNz2vmH6gr7yEITcci18IdnTvIgOej4xydmYu8LtJiXW0uQDhCL/16.jpg
Kagera Sugar waliongára Kambarage kwa kuilaza Polisi Moro
Polisi Moro wliopoteza mchezo wa pili leo mbele ya Kagera Sugar baada ya wiki iliyopita kulala kwa Simba 2-0
Ndanda iliyotakata nyumbani Mtwara kwa kuilaza Coastal Union 1-0
JAHAZI la Mtibwa Sugar linazidi kuzama baada ya kufungwa 1-0 na Mgambo JKT ikiwa ni mechi ya nne mfululizo kupoteza katika Ligi kuu Tanzania Bara.
Kipigo hicho cha Mtibwa kimeifanya timu hiyo kuzidi kuporomoka kwenye msimamo wa ligi hiyo wakisaliwa na pointi zao 19 baad ya mechi 15.
Bao lililoizamisha Mtibwa katika pambano hilo lililochezwa katika uwanja wa Mkwakwani Tanga, liliwekwa kimiani na Malimi Busungu katika dakika ya 36 na kuifanya timu yao kufikisha pointi 17.
Katika mchezo mwingine ul;iochezwa Nangwanda Sijaona, wenyeji Ndanda waliinyuka Coastal Union kwa bao 1-0 lililowekwa kimiani na Jacob Massawe katika dakika ya 79.
Aidha Kagera Sugar wakwia uwanja wa Kambarage Shinyanga wanaoutumia kama uwanja wao wa nyumbani, iliendelea kutakata baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Moro.
Bao hilo pekee lililowapa ushindi Kagera na kuzidi kujikita nafasi ya tatu ikifikisha pointi 24 liliwekwa kimiani na Rashid Mandawa ambaye anafikisha bao lake la saba katika ligi hiyo, bao moja nyuma dhidi ya kinara wa mabao kwa sasa wa ligi hiyo Didier Kavumbagu wa Azam.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo mitatu, Yanga wakiwa uwanja wa Sokoine Mbeya kupapetana na Mbeya City, Simba watakuwa wageni wa Stand Utd mjini Shinyanga na Azam watauamana na Prisons Mbeya uwanja wa Chamazi.
Mechi hiyo ya Azam na maafande itachezwa saa 2 usiku na kila timu imetamba kujiandikishia ushindi katika pambano hilo.

Friday, February 20, 2015

Yamoto Band watua UK tayari kwa shoo wa kesho


Kikosi kizima cha Yamoto Band ndani ya jiji la London tayari kwa makamuzi ya jumamosi hii ndani ya ukumbi wa Royal Regency Monor Park London

Yamoto Band Touchdown London this morning., safe and sound.Now let's Get it...Let's Goooo. ..Made in East Africa 2015 ,Yamoto band Live in London Royal Regency Banquite .



Wakijiachia na mmoja wa mabosi wake







Enock Bella akiosha maji

Wacheza filamu nchini waonywa

Mlela akipeana mkono na Katibu Mtendani wa Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fisoo
Na Genofeva Matemu, Maelezo
WASANII wa filamu nchini wameshauriwa kutumia taaluma waliyonayo kupanua wigo wa filamu nchini na kuitangaza Tanzania duniani kote kwa kuzingatia matumizi mazuri ya lugha ya Kiswahili katika filamu wanazozitengeneza.
Rai hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu, Joyce Fisoo, juzi alipokutana na wasanii waliotarajia kuondoka jana kwenda Uingereza kurekodi filamu ya 'Sabasi' na Kampuni ya Didas Entertainment iliyopo nchini humo.
Fisoo alisema kuwa baadhi ya wasanii nchini wamekuwa makontena yanayopitisha biashara haramu kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine hivyo kuwaomba wasanii wanaokwenda Uingereza kuachana na tabia hiyo bali watumie fursa waliyoipata kuiwakilisha Tanzania vizuri na kutengeneza filamu bora itakayowawezesha kujulikana na kufungua fursa za kushirikishwa katika filamu na nchi nyingine duniani.
Aidha, Fisoo aliwataka wasanii hao kuheshimu sheria, kanuni na taratibu za Uingereza kwani kwa kufanya hivyo watakuwa mabalozi bora na kutoa nafasi kwa wasanii wengine kupata fursa hizo.
Naye Mama wa Didas Entertainment, Nuru Idrisa, aliwataka wasanii wa Bongo Movie waliopata nafasi ya kurekodi filamu na Didas Entertainment kujiheshimu na kuvaa mavazi ya staha yatakayostiri miili yao muda wote watakaokuwa nchini Uingereza kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wamelinda heshima ya nchi.
Akitoa neno la shukrani, msanii wa Bongo Movie, Yusuph Mlela, aliishukuru Bodi ya Filamu kwa kuwa bega kwa bega na wasanii na kuwaahidi wadau wa filamu nchini kazi bora na yenye tija katika jamii.
Filamu ya 'Sabasi' inatarajiwa kurekodiwa hivi karibuni nchini Uingereza na Kampuni ya Didas Entertainment na kuwashirikisha wasanii Mlela, Esha Buhet na Husna Athumani, na ni filamu ya pili kurekodiwa na kampuni hiyo na kuwashirikisha wasanii kutoka Tanzania. Filamu ya kwanza kurekodiwa na kampuni hiyo iliyowashirikisha wasanii kutoka Tanzania ni ile ijulikanayo kwa jina la 'Mateso Yangu Ughaibuni'.

Balotelli alianzisha tena Liverpool

3f
Muunganiko wa picha zilizochapishwa na Daily Mail zinazomuonyesha Balotelli na nahodha wake, Steven Gerrard
Balotelli akifunga penati yake
Balotelli took the ball off Liverpool captain Jordan Henderson and fellow striker Daniel Sturridge to take the penaltyMARIO Balotelli, aliifungia Liverpool mkwaju wa penati dakika tano kabla ya kumalizika kwa pambano lao dhidi ya Besiktas ya Uturuki, lakini ameibua mambo.
Kitendo chake cha kulazimisha kuipiga penati hiyo kimemtibua nahodha wa timu ya Liverpool Steven Gerrard anayemshutumu kwa utovu wa nidhamu.
Balotelli alifunga penalti hiyo na kuiwezesha Liverpool kuibuka washindi wa bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Ndogo ya Ulaya, katika uwanja wa Anfield.Hali hiyo ilijitokeza baada ya kushindwa kuelewana na nahodha wa mchezo huo Henderson na Daniel Sturridge juu ya nani abebe jukumu la kupiga penalti hiyo.
Gerrard amesema: "Henderson ni nahodha na Balotelli kwa kiasi fulani alionyesha kumkosea adabu katika hali hiyo."
Gerrard ambaye kwa sasa ni majeruhi, alikuwa mchambuzi katika matangazo ya mchezo huo kwenye televisheni ya ITV ya nchini Uingereza.
Katika mechi nyingine timu ya Tottenham Hotspur ililazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Fiorentina wakati Everton wakipata ushindi mnono wa mabao 4-1 ugenini dhidi ya Young Boys ya Uswisi.

NASAHA ZA IJUMAA-SIRI SIRINI

Thursday, February 19, 2015

Ally Mustafa 'Barthez' ni Nouma sana!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2gWCT-X80QbEFaBLH3ow-j-DUBUoiESu7HybsUaOTaiK29nZu8xGcFRQwETVHpw-nbY11UkU2DDjhKczuGFnfxgBd_5QO8ZU6Kvpo1vd4IHZkFNaX3sIoyhhtPOFOXUbpjMPWPETf4lkv/s1600/35.jpg
Barthez mbele kushoto akiwaongoza wachezaji wenzakle wa Yanga
PAMBANO la Yanga dhidi ya Prisons-Mbeya lililochezwa uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya kwa vijana wa Jangwani wakiibuka na ushindi wa mabao 3-0 umezidi kumpandisha chati kipa Ally Mustafa 'Barthez' ambaye amedaka mechi sita mfululizo za Ligi Kuu Tanzania Bara bila kuruhusu bao lolote.
Kipa huyo aliyekuwa na wakati mgumu mbele ya kikosi cha Jangwani tangu Yanga ilipolazimishwa sare ya mabao 3-3 na Simba Oktoba mwaka juzi, hajafungwa bao lolote katika muda wa dakika 540 huku kwenye uwanja wa Sokoine akigeuka kuwa shujaa kwa kuokoa michomo mingi ya wachezaji wa Prisons.
Hizo ni mbali na dakika 90 za pambano la kimataifa la Kombe la Shirikisho Afrika ambapo Yanga ilishinda mabao 2-0 na yeye akiwa kwenye milingoni mitatu ya lango ya vijana wa Jangwani.
Barthez aliyesajiliwa na Yanga akitokea Simba, rekodi zake zinaonyesha kuwa ameshuka dimba katika mechi hizo kama ifuatavyo na kuwafunika makipa wote wa timu nyingine 13 zinazoshiriki ligi hiyo.
Jan 17, 2015Yanga vs Ruvu Shooting (0-0)
Jan 24, 2015Polisi Moro vs Yanga (1-0)
Feb 01, 2015Yanga vs Ndanda (0-0)
Feb 4, 2018Coastal Union vs Yanga (0-1)
Feb 08, 2015Yanga vs Mtibwa Sugar (2-0)
 Feb 14, 2015-Kimataifa
Yanga vs BDF XI (2-0)
Feb 19, 2015
Prisons vs Yanga (0-3)

FAINALI ZA DUNIA 2022 KUFANYIKA DESEMBA?

http://www.shalomlife.com/img/2014/12/27573/qatar_.jpg
MTANDAO mmoja barani Ulaya umetoa taarifa kuwa tayari muafaka umeshafikiwa kwa michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Qatar mwaka 2022 kufanyika katika kipindi cha Novemba na Desemba ili kuwepa joto kali katika kipindi cha kiangazi.
Wakiorodhesha vyanzo mbalimbali mtandao huo umedai kuwa uamuzi umeshafanyika kwani kikosi kazi kilichoteuliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kinatarajia kuwasilisha miezi hiyo katika kikao chao kitakachofanyika wiki ijayo jijini Doha kabla ya kamati ya utendaji haijakamilisha mpango huo wakati wa kikao cha mwezi ujao jijini Zurich.
Wiki tatu zilizopita, Katibu Mkuu wa FIFA Jerome Valcke katika mahojiano yake na radio moja nchini Ufaransa alisema Kombe la Dunia nchini Qatar linatakiwa kuandaliwa wakati wa majira ya baridi lakini kugongana na michuano ya Olimpiki ya kwenye baridi Februari mwaka 2022 pia ni hatihati.
Hata hivyo mpango huo haujafafanua kwa undani zaidi kuwa michuano ya Kombe la Shirikisho ambayo huchezwa mwaka mmoja kabla ya Kombe la Dunia kama nayo itasogezwa mbele kuepuka majira ya kiangazi.
Desemba mwaka jana Chama cha Vilabu barani Ulaya na Muungano wa Ligi za Soka barani humo vilipendekeza michuano hiyo ya Qatar kuchezwa kati ya May na Juni ili kutovuruga ratiba zingine za kawaida za msimu.
Uteuzi wa Qatar kuandaa fainali hizo na zile za mwaka 2018 nchini Russia zimeghubikwa na mizengwe na kuelezwa kujaa vitendo vya rushwa, ingawa FIFA imekuwa ikijitetea.

BAHANUZI, MAHUNDI WANG'ARA VPL

http://2.bp.blogspot.com/-ORUnNfNV-xE/VM0wOPMp6vI/AAAAAAABdBc/1sAbma_8dB4/s1600/BAHANUZI.jpg
Said Bahanuzi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2NUIe7-6s8hh3LAnWZphC1Sfmct-j1gnFK6vBlYl6-vWAkEms7KvbsXk8lsXx7as54qc9WOVhCaehk3-wlIYA3DXm_G5D2mryGl3IxaJ0IKhGMNNPLYmPUTtm0N9aOnG0wHywciFMsGQ/s1600/IMG_1197.jpg
Mahundi (kulia) akichuana na Niyonzima katika moja ya mechi ya Ligi Kuu
KIUNGO wa timu ya Coastal Union ya Tanga, John Mahundi amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Desemba 2014 wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mahundi alitoa mchango mkubwa kwa timu yake ya Coastal Union mwezi huo na kuchaguliwa na jopo la makocha linalofanya kazi ya kuchagua mchezaji bora wa kila mwezi.
Aidha mshambuliaji wa timu ya Polisi Morogoro, Said Bahanuzi 'Spider Man' amechaguliwa kuwa mchezaji bora mwezi Januari 2015.
Bahanuzi anayechezea timu ya Polisi Moro kwa mkopo akitokea timu ya Young Africans amekua na mchango mkubwa kwa timu yake tangu kujiunga nayo mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom nchini.
Kwa kuibuka wachezaji bora, Mahundi na Bahanuzi watazawadiwa fedha taslimu Sh. Mil. 1/ kwa kila mmoja kutoka kwa wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.
Jopo maalum la makocha waliopo katika viwanja vyote vinavyotumika kwa mechi za Ligi Kuu ndiyo wanaofanya kazi ya kuchagua mchezaji bora kwa kila mechi kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa.
Baadaye alama zao kujumlishwa ili kumpata mshindi wa mwezi.

Yanga wafanya mauaji Mbeya, Azam yabanwa

Yanga
Msuva na Coutinho walipokuwa wakijiandaa kuiangamiza Prisons-Mbeya

Azam
Azam walishindwa kushangilia kama hivi leo kwa Ruvu Shooting
KLABU ya Yanga imeendeleza rekodi yake ya kugawa dozi kwa wapinzani wao katika Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kuilaza Prisons-Mbeya kwa mabao 3-0 na kukwea kileleni mwa msimamo wakiiengua Azam.
Azam waliokuwa uwanja wa Mabatini-Mlandizi wameshindwa kutamba kwa kulazimishwa suluhu mbele ya maafande wa Ruvu Shooting na kutoa nafasi kwa Yanga kuwaacha kwa pointi mbili kileleni.
Kwa suluhu iliyopata kwa Ruvu, imeifanya mabingwa watetezi Azam kufikisha pointi 26 na kushuka hadi nafasi ya pili licha ya timu zote mbili kulingana mechi zote zikicheza michezo 14 kila moja.
Yanga ikicheza kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya walipata ushindi huo murua na uliowafanya kufikisha pointi 28 baada ya kupata mabao yake mawili katika kipindi cha kwanza na jingine kipindi cha pili.
Mabao hayo yaliwekwa kimiani na Simon Msuva aliyefunga dakika ya tatu tu ya mchezo kabla ya Coutinho kuongeza la pili.
Msuva alirudi tena kambani kwa kufunga bao la tatu kipindi cha pili na kumfanya afikishe jumla ya mabao sita akibakisha mabao mawili kumkuta Didier Kavumbagu wa Azam mwenye mabao nane.
Yanga wataendelea kusalia jijini humo kwa ajili yua kusubiri pambano lake la Jumapili dhidi ya Mbeya City kabla ya kutimka zao Botswana kuwafuata BDF XI kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika mchezo wao wa kwanza uliochezwa mwishoni mwa wiki, Yanga iliitambia BDF kwa kuilaza mabao mawili yote yakiwekwa kimiani na Mrundi, Amissi Tambwe.

Wednesday, February 18, 2015

Yanga, Azam vitani tena viwanja tofauti kesho

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/09/DSC02166.jpg
Yanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdDjGKemN2sVnPU1l723rHo-UtuVjBZ673i-L4ZgSmKzLiH8dPrkov8VclFd1qQYP1c48z_omeSmeZFlSwvlBweJ0Ous2ja2z3bmlzGANL_dA-GQmz780dcej0AwtKL-Z13vKA-TDyjsQ/s1600/HERM5672-1.JPG
Azam
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam pamoja na wapinzani wao wakuu katika mbio za kuwania ubingwa wa msimu wa 2014-2015, Yanga kesho wanatarajiwa kushuka viwanja tofauti kusaka nafasi ya kujiimarisha kileleni mwa msimu wa ligi hiyo.
Yanga waliopo Mbeya wanatarajiwa kuvaana na Prisons katika pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Sokoine, wakati Azam watakabiliana na maafande wa Ruvu Shooting katika pambano linalotarajiwa kuwa kali litakalochezwa kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Timu hizo mbili zilizotoka kwenye majukumu yao ya kuiwakilisha taifa katika michezo ya kimataifa ya Ligio ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho zote zipo kileleni zikiwa na pointi 25, Azam akitangulia kwa kuwa na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa kulinganisha na wapinzani wao.
Azam wanarejea kwenye ligi hiyo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi mnono wa mabao 5-2 kwenye uwanja wa Chamazi dhidi ya Mtibwa Sugar, wakati Yanga ikitoka kuwafyeka Mtibwa mabao 2-0.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alinukuliwa mapema jana kuwa kikosi chao kipo tayari jijini Mbeya kugawa dozi kwa maafande hao wa Magereza kabla ya kumalizia kazi kwa Mbeya City Jumapili na kuanza safari ya kuwafuata Wabotswana wa BDF XI kwa mechi ya marudiano ya kimataifa.
Azam wenyewe kupitia Meneja wao, Jemedari Said imetamba kuitoa nishai Ruvu Shooting kabla ya mechi yao ya mwisho ya ligi kuanza safari kuelekea Sudan kurudiana na El Merreikh katika Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo katika mchezo wa kwanza uliochezwa Jumapili walishinda mabao 2-0.
Licha ya Yanga na Azam kutamba kujiandaa kugawa dozi kwa wapinzani, timu za Ruvu Shooting na Prisons inayoburuza mkia nazo zimetamba hawatakubali kufa kikondoo katika mechi hizo za kesho kwani hata wao wanazihitaji pointi tatu toka kwa vigogo hao.
Msemaji wa Ruvu Masau Bwire na Kocha wa Prisonsa, David Mwamaja walisema kwa nyakti tofauti kuwa wanahitaji ushindi kuliko kitu kingine katika mechi hizo za kesho kwa lengo la kujiweka katika nafasi nzuri ndani ya ligi hiyo iliyoanza  kushika kasi kwa mechi za duru la pili.

Bingwa wa FDL kujulikana J2 Taifa

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mwadui Shinyanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhX4CPi_gLzDiNDFJxODqQK-bun_Lz_-fqogmOSBafonpNyQztxKsciMrA9kx7T2CAkfa14juJT5WVK1BxZPxkqTuD40uPWHMTtpatpKUHMvQpdWau2Aw3yYJfbYrgwYFAnwHWaIEFpT7c/s1600/sports.JPG
Aficans Sports 'Wana Kimanumanu
KLABU za African Sports  ya Tanga na Mwadui FC ya Shinyanga zinatarajiwa kucheza mchezo wa fainali  kusaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) siku ya Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
African Sports waliibuka washindi wa kwanza katika Kundi A, na Mwadui FC washindi wa kwanza Kundi B watacheza mchezo huo wa fainali ambapo Bingwa atapewa zawadi ya Kombe na medali, hali kadhalika kwa msindi wa pili.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Baraka Kizuguto alisema kwa mujibu wa Kanuni, ni lazima apatikane mshindi mmoja ambaye ni bingwa.
“Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ilimalizika mwishoni mwa wiki kwa timu nne kupanda Ligi Kuu kwa kila kundi kutoa timu mbili, Kundi A ni African Sports na Majimaji FC, Kundi B ni timu za Mwadui FC na Toto Africans,”alisema.
Alisema  timu za Green Worriors na Villa Squad zimeteremka  Daraja la pili baada ya kushika nafasi za mwisho kwenye msimamo wa Ligi Daraja la Kwanza, Villa Squad kutoka Kundi A na Green Warriors Kundi B.
Katika hatua nyingine, Rais wa TFF  Jamal Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa Wenyekiti wa klabu ya African Sports (Tanga) , Majimaji (Ruvuma),  Mwadui (Shinyanga) na Toto Africans ya Mwanza kwa timu zao kupanda Ligi Kuu ya Vodacom (VPL).
 Katika salamu zake  Malinzi alisema klabu hizo zinapaswa kujipanga na kufanya maandalizi kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom 2015/2016, kwani VPL ni ngumu kutokana na timu zote kuwa na ushindani mkubwa wa kutafuta matokeo mazuri kuepeuka kushuka daraja.
 Kwa niaba ya TFF, familia ya mpira na watanzania kwa ujumla wanawapa pongezi timu za African Sports, Majimaji, Mwadui na Toto Africans kwa kupanda Ligi Kuu ya Vodacom na kuwatakia maandalizi mema ya VPL 2015/2016,” alisema.

KWA UCHAFU HUU ELIMU TANZANIA ITAPANDA KWELI?!



Haifahamiki ni wanafunzi wa shule gani ya Sekondari, lakini hii ni taswira ya kitu gani kinachoendelea katika shule zenu nyingi na sababu ya kupatikana kwa division ziro lukuki

Rais wa FIFA alaani ubaguzi wa mashabiki wa Chelsea

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02939/sepp-blatter_2939007b.jpg
Rais wa FIFA, Sepp Blatter aliyekerwa na kitendo chga kibaguzi kilichofanywa na amshabiki wa Chelsea dhidi ya mtu mweusi mjini Paris.
PARIS, Ufaransa
RAIS wa Shirikisho la Kimataifa la Soka Sepp Blatter amewalaumu mashabiki wa klabu ya Chelsea, kwa kitendo chao cha kumzuia mtu mweusi kuingia ndani ya treni huku wakiimba nyimbo za kibaguzi jijini hapa.
Blatter amelaaini kitendo hicho kilichofanywa na baadhi ya mashabiki hao wa Chelsea cha ubaguzi wa rangi dhidi ya mtu huyo mweusi na kumzuia kuingia katika treni jana Jumanne.
Baadhi ya mashabiki wa Chelsea wameonekana katika mkanda wa video wakizuia mlango wa treni kabla hawajamsukuma mtu huyo huku wakiimba nyimbo za kibaguzi: 
"Sisi wabaguzi, sisi wabaguzi na hicho ndicho tunachokitaka."
Tukio hilo lilitokea baada ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya uliofanyika jijini hapa na Chelsea kutoka sare ya kufungana bao 1-1 na Paris Saint-Germain kwenye uwanja wa Parc des Princes, huku klabu hiyo ikijibu haraka kuwa kitendo hicho sio cha kiungwana.
Ni wiki moja tu baada ya kocha wa zamani wa AC Milan Milan Arrigo Sacchi kutoa kauli kuwa "kuna weusi wengi" katika ligi ya vijana ya Italia, ambapo Blatter akijibu matukio yote hayo katika mtanda wake wa kijamii wa Twitter.
Matukio ya kibaguzi katika michezo yamekuwa kama ugonjwa sugu, huku adhabu dhidi ya wahusika yakielezwa kuruhusu kuendelea kuyahamasisha.

Jeshi Nigeria ladai kuua Boko Haram 300

http://d.ibtimes.co.uk/en/full/1418176/nigeria-boko-haram-2000-feared-killed-after-baga-attacked-second-time-days.png
baadhi ya wapiganaji wa Boko haram wakiwa 'kamili' na zana zao
ABUJA, Nigeria
ZAIDI ya wanamgambo 300 wa kundi la Boko Haram wameuawa katika zoezi la kijeshi huko Kaskazini-Mashariki ya Nigeria, limesema jeshi la Nigeria.
Baadhi ya askari wamekamatwa na silaha kadhaa zimeharibiwa, alisema msemaji wa jeshi hilo, Chris Olukolade.
Pia katika tukio hilo askari wawili walipoteza maisha yao na wengine 10 walijeruhiwa wakati wa zoezi hilo la siku mbili huko katika jimbo la Borno, aliongeza.
Hatahivyo, vifo hivyo havijathibitishwa.
Jeshi la Nigeria lilituhumiwa katika siku zilizopita kuwa limekuwa likitoa taarifa za uongo kuhusu kujeruhiwa kwa maadui.
Boko Haram wamevamia raia huku wakiwaua maelfu wa askari tangu kundi hilo lianzishe vurugu kwa ajili ya kuanzisha taifa lao la kiislamu mwaka 2008.
Nigeria, Chad, Cameroon na Niger hivi karibuni vimeunda jeshi la muungano na kudai kuwa limekuwa likifanya vizuri dhidi ya Boko Haramu.
Tisho la kundi hilo linaelezwa ndiyo sababu ya kuahirishwa kwa Uchaguzi Mkuu wa nchini huo uliokuwa ufanyike Jumamosi iliyopita na kupelekwa mbele hadi majuma sita yaani Machi 28.

Rooney aomba radhi kwa kujirusha

http://a2.fssta.com/content/dam/fsdigital/fscom/Soccer/images/2015/02/18/021815-Soccer-Manchester-United-Rooney-PI-CD.vadapt.620.high.0.jpgGOLIKIPA wa klabu ya Preston, Thorsten Stuckmann amesema Wayme Rooney alimuomba radhi kwa jinsi alivyodanganya na kupata penati katika mchezo wao dhidi ya Manchester United waliofungwa mabao 3-1. Rooney alianguka katika eneo la hatari baada ya kile kilichoonekana kama kuguswa na Stuckmann. Stuckmann alikaririwa na gazeti la The Sun akidai kuwa Rooney alimfuata na kumuomba radhi kwani ilikuwa nafasi yake ya kupata penati na alilazimika kuitumia.
Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza alifunga penati hiyo na kuihakikishia nafasi United ya kucheza hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la FA dhidi ya Arsenal.
Kitendo hicho cha Rooney kilizua mjadala mkubwa miongoni mwa wachambuzi wa soka lakini aliungwa mkono na kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo Roy Hodgson na mchezaji mwenzake wa zamani Phil Neville ambao walidai alijirusha ili kumkwepa golikipa.
Stuckmann mwenye umri wa miaka 33 amesema suala hilo liko wazi kuwa ile haikuwa penati lakini walipewa kwa sababu wenyewe ni United na kama ingekuwa mchezaji wao ndiye angefanya vile hadhani kama angepewa mkwaju huo.

Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin

Mourinho akiri sare ilikuwa kama zali kwa PSG

http://images.dailystar-uk.co.uk/dynamic/58/photos/879000/161879.jpg
Kipa aliyeibeba Chelsea jana ugenini dhidi ya PSG
MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amekiri kikosi cha kilikuwa na bahati kupata sare ya bao 1-1 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya timu 16 bora dhidi ya Paris Saint-Germain. 
Katika mchezo huo Branislav Ivanovic ndiye aliyeifungia Chelsea bao la kuongoza kabla ya Edinson Cavani hajasawazisha. 
Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Mourinho amesema ukiona jinsi golikipa wake Thibaut Courtois alivyokuwa akiokoa michomo mingi ya wapinzani hakuna shaka kuwa ilikuwa bahati kwao kuibuka na ushindi. 
Mourinho amesema sasa karata iko upande wao kwani mchezo huo utaamuliwa katika Uwanja wa Stamford Bridge baada ya wiki mbili zijazo.

Rais Kikwete apangua Ma-DC, Mwakalebela, Kisu waula!

https://pamelamollel.files.wordpress.com/2013/02/frederick-mwakalebela.jpg
Mwakalebela

http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2011/12/kiss.jpg
Shaaban Kissu (kulia)

Na Rahim Junior, Dodoma 
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Jakaya Kikwete ameendelea kufanya panga pangua katika serikali yake baada ya kufanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya kwa kuwateua Ma-DC wapya 27, kuwahamisha vituo vya kazi 64 na wengine 42 amewabakisha kwenye vituo vyao vya awali.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, leo mchana, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema mabadiliko hayo yamesababishwa na kuwepo kwa nafasi wazi 27 ambazo zilitokana na wakuu wa wilaya watatu kufariki dunia; kupandishwa cheo wakuu wa wilaya watano, kupangiwa majukumu mengine wakuu wa wilaya saba na kutenguliwa kwa uteuzi wa wakuu wa wilaya 12.
Hata hivyo, Waziri Mkuu alisema, Rais  Kikwete amewabadilisha vituo vya kazi wakuu wa wilaya 64 na kuwabakiza kwenye vituo vyao vya zamani wakuu wa wilaya 42.
Wakuu wa Wilaya wapya 27 walioteuliwa ni; Mariam Ramadhani Mtima anayeenda Ruangwa; Dk. Jasmine B. Tiisike anayeenda Mpwapwa; Pololeti Mgema (Nachingwea); Fadhili Nkurlu anayeenda Misenyi; Felix Jackson Lyaniva anayeenda Rorya na Katibu Mkuu wa zamani wa TFF, Fredrick Wilfred Mwakalebela anayeenda wilaya ya Wanging’ombe.
Wengine na vituo vyao kwenye mabano ni Zainab Rajab Mbussi (Rungwe); Francis K. Mwonga (Bahi); Kanali Kimiang’ombe Samwel Nzoka (Kiteto), Husna Rajab Msangi (Handeni), Emmanuel J. Uhaula (Tandahimba); Mboni Mhita (Mufindi); Hashim S. Mgandilwa (Ngorongoro); Mariam M. Juma (Lushoto); Thea Medard Ntara (Kyela); Ahmad H. Nammohe (Mbozi); Mtangazaji wa TBC, Shaaban Kissu (Kondoa) na Stephen Zelothe (Musoma).
Wengine ni Pili Moshi (Kwimba); Mahmoud A. Kambona (Simanjiro); Glorius B. Luoga (Tarime); Zainab R. Telack (Sengerema); Bernard Nduta (Masasi); Zuhura Mustafa Ally (Uyui); Paulo Makonda (Kinondoni); Mwajuma Nyiruka (Misungwi) na na Maftah Ally Mohamed (Serengeti).
Waliotenguliwa uteuzi wao lakini watapangiwa majukumu mengine ni'; Brig. Jenerali Cosmas Kayombo aliyekuwa Simanjiro; Kanali Ngemela E. Lubinga (aliyekuwa Mlele); Juma S. Madaha (aliyekuwa Ludewa); Mercy E. Silla (aliyekuwa Mkuranga); Ahmed R. Kipozi (aliyekuwa Bagamoyo); Mrisho Gambo (aliyekuwa Korogwe) na Elinas A. Pallangyo (aliyekuwa Rombo).
Waziri Mkuu pia aliwataja Wakuu wa Wilaya 12 ambao uteuzi wao umetenguliwa kutokana na sababu za umri, kiafya na kuimarisha utendaji Serikaini na wilaya zao kwenye mabano kuwa; ni James K. Ole Millya (Longido); Elias Wawa Lali (Ngorongoro); Alfred Ernest Msovella (Kongwa); Danhi Beatus Makanga (Kasulu); Fatma Losindilo Kimario (Kisarawe); Elibariki E. Kingu (Igunga); Dk. Leticia Moses Warioba (Iringa); Evarista N. Kalalu (Mufindi); Abihudi M. Saideya (Momba); Martha J. Umbulla (Kiteto); Khalid J. Mandia (Babati) na Elias Goroi (Rorya).

Monday, February 16, 2015

Polisi Zanzibar, KMKM yaendeleza uteja Afrika

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi59R0MYcrxWHLeSNnC_vM50rvpo6pW4S079-xz073BM1qMzHu78BZ3M2A6-Rcffg0AKuCNlGJTx77XuEspNUQTYpSZxeIwClivBXmTswWbLyuGBKDZoXuu3mnXKpUwrCIZ62qjbxpxVhkw/s640/4.jpg
KMKM waliokufa 2-0 Sudan
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiLCWb5BqldkVTcFvaO8san-9Nhbw4RdsAVAbuN1u3556K_TvVv67OvOYjoXCPZ7VpusnafOOpJiS6SLaDK-7wNEixcgcnDUbt54qaR2jof0UEU-xKJdBd0IUmCqdrNsyokdr0MSy0kmIY/s1600/IMG_3886.JPG
Polisi waliopigwa 'mkono' nchini Gabon
WAKATI wawakilishi wa Tanzania Bara, Azam na Yanga wakiwapa raha mashabiki wao, KMKM na Polisi Zanzibar zimeendelea kuwasononesha mashabiki wa soka wa visiwa hivyo baada ya kugeuzwa 'urojo' katika mechi zao za kimataifa zilizochezwa mwishoni mwa wiki.
Polisi wanaoiwakilisha Zanzibar kwenye Kombe la Shirikisho Afrika kama Yanga, ilikutana na kipigo cha mabao 5-0 toka kwa Moumana ya Gabon wakati mabingwa wa visiwani, KMKM wakilala 2-0 nchini Sudan kwa Al Hilal na kujiweka katika mazingira magumu ya kusonga mbele kwenye michuano hiyo.
Tangu Zanzibar ilipopata uanachama wa Shirikisho la Soka Afrika CAF, 2004, imekuwa ikifanya vibaya kwenye uwakilishi wa klabu kwa timu zao kuondolewa hatua za awali.
KMKM na Polisi maarufu kama Wazee wa Tunisia' watakuwa na mtihani mgumu swa na kupanda mlima mrefu kuweza kuzitoa Mounana na Al Hilal katika mechi zao za marudiano wakati wakiwa nyumbani.
Hiyo ni tofauti na wawakilishi wa Tanzania Bara, Yanga na Azam wenye kazi nyepesi kwenye mechi zao za marudiano wiki mbili zijazo ugenini dhidi ya timu za BDF XI ya Botswana na El Merreikh ya Sudan.
Yanga ilianza kwa kuizabua BDF kwa mabao 2-0 juzi kwenye Kombe la Shirikisho, kabla ya Azam kufuata mkumbo huo kwa kuilaza El Merreikh kwa idadi kama hiyo jana kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
Matokeo mengine ya michuano ya hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika yapo hivi;
Al Ahli Tripoli     1 - 0     Smouha
COB     2 - 0     Moghreb Tétouan        
Raja Casablanca     4 - 0     Diables Noirs
St Michel United     1 - 1     Mamelodi Sundowns       
KCCA     1 - 0     Cosmos de Bafia        
Gor Mahia     1 - 0     CNaPS Sport        
Al-Malakia     0 - 2     Kano Pillars  
Recreativo do Libolo  3 - 1     Sanga Balende      

Mangasport     1 - 0     Bantu         
LLB Académic     0 - 0     Kabuscorp        
Séwé Sport     1 - 2     Kaloum Star
Real de Banjul     1 - 1     BYC
Pikine     1 - 0     Etoile Filante
MC El Eulma     1 - 0     Kedus Giorgis
Kaizer Chiefs     2 - 1     Township Rollers
Fomboni Club     0 - 1     Big Bullets
Azam     2 - 0     Al Merreikh 
Enyimba     3 - 0     Buffles de Borgou
Liga Muçulmana     0 - 0     APR
Mbabane Swallows     1 - 1     ZESCO United
USM Alger     3 - 0     Foullah Edifice
Al Hilal Omdurman     2 - 0     KMKM
Matokeo ya Kombe la Shirikisho Afrika;
Al-Ghazal     0 - 1     Petrojet
URA     3 - 2     Elgeco Plus
Benfica Luanda     2 - 0     Le Messager Ngozi
RSB Berkane     2 - 1     Onze Créateurs
Petite Rivièr…     1 - 2     Ferroviário Beira
Côte d'Or     2 - 3     Dedebit
RC Bobo-Dioulasso     0 - 1     Warri Wolves
Volcan Club     0 - 1     Petro de Luanda
Young Africans     2 - 0     BDF XI
Panthère     0 - 1     Rayon Sports
MC Alger     0 - 0     Sahel 
Leones Vegetar…     1 - 0     Dolphins
Étoile du Congo     1 - 2     FC MK
BV Wits     3 - 0     Royal Leopards
Khartoum 3     1 - 0     Power Dynamos
Sofapaka     1 - 2     Platinum
Al-Ittihad     6 - 1     Elect-Sport
Unisport Bafang     1 - 0     Olympique Ngor
Mounana     5 - 0     Polisi
Hearts of Oak     1 - 0     Police
Togo Port     2 - 0     CARA Brazzaville
ASO Chlef     2 - 0     Kamboi Eagles
Horoya     1 - 0     Fassell

Sikiliza ngoma mpya ya Shaa iitwayo For You


KOCHA JULIO AWAUMBUA WALIOMBEZA

Kocha jamhuri Kihwelu 'Julio'
KOCHA Jamhuri Kihwelu 'Julio' ni maarufu kwa kuwa mzungumzaji na mtu mwenye tambo nyingi zinazokera, lakini kwa kitendo alichofanya cha kuipandisha Ligi Kuu timu ya Mwadui Shinyanga mwaka mmoja baada ya kubaniwa na TFF ni kama amewaumbua wabaya wake.
Waliombeza na kumtimua ndani ya Simba katikati ya msimu uliopita wakati Simba ikiwa nafasi ya nne pamoja na bosi wake Abdallah Kibadeni 'King' huenda sasa wakatafuta mahali pa kuficha sura zao kwa aibu baada ya Julio kufanya kweli kwa kuirejesha Mwadui Ligi Kuu baada ya miaka zaidi ya 30 tangu ishuke daraja.
Msimu uliopita mara baada ya kutemwa na Simba, Julio alipewa mikoba ya kuinoa timu hiyo na kumaliza vinara wa kundi lao na kuonekana kama wamepanda daraja kabla ya TFF kuwaengua kutokana na rufaa ya JKT Kanembwa kuwaacha nafasi ya tatu nma ya pili ikitwaliwa na Stand United kama utani.
Kocha huyo aliyewahi kutamba na klabu mbalimbali ikiwamo Pilsner na Simba na timu ya taifa, akiwa mmoja wa mabeki mahiri wa kati, hakukata tamaa na badala yake alisuka kikosi chake na kuwezesha kupata msimu huu baada ya kumaliza kinara wa kundi lao wakifuatiwa na Toto Africans ambao nao wanarejea ligi chinio ya kocha John Tegete.
Akihojiwa mara baada ya kupata ushindi wa mabao 4-3, Julio alituma salamu zake kwa vigogo vya Ligi Kuu kuwa wajiandae kupata upinzani mkali msimu wa 2015-2016 kwani Mwadui haitacheza chini ya Nafasi ya Tatu Bora.
"Wajiandae tunakuja, tunajipanga kuhakikisha tunakuwa miongoni mwa timu Tatu Bora," alisema Julio hata ikiwa ligi yenyewe bado haijaanza.
Julio mmoja wa makocha wenye elimu ya juu ya ukocha na ambaye amekuwa akipata mafanikio licha ya utamaduni wa kupuuzwa kwa makocha wazalendo wanaotumiwa kama 'spea tairi' ameuthibitishia umma kwamba makocha Wazalendo wanaweza.
Mbali na kutwaa mataji kama mchezaji wa Simba, Julio pia ameshatwaa ubingwa wa Kombe la taifa kama kocha wa timu ya soka ya Ilala iliyoundwa na nyota wa Simba na Yanga kama ambavyo kikosi chake cha Mwadui kilivyoundwa na wakali wa timu hizo ambao walipigana na kuibeba kurudi Ligi Kuu msimu ujao.
MICHARAZO inampongeza Julio na timu yake sambamba na kuzipongeza timu zote nne za Majimaji Songea, Africans Sports na Totyo Africans kwa kurejea tena ligi kuu baada ya muda mrefu kuwa nje ya lifgi hiyo kubwa nchini.
Jambo la muhimu jipangeni mapema sasa ili msije mkainusa na kurejea tena ligi daraja la kwanza kama ambavyo imekuwa ikishuhudiwa kwa baadhi ya timu zinazopanda ligi hiyo na kudumu kwa msimu mmoja.