STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 26, 2013

Kichanga cha siku nne chaokotwa shimoni alikokaa kwa siku 6



UKISHANGAA ya Mussa basi utayaona ya Firauni, usemi huu umethibitika Songea baada ya Mtoto Bahati Upendo mwenye siku 3 toka azaliwe aliyekuwa amewekwa kwenye mfuko wa mbolea kisha kutupwa kwenye shimo kuokolea akiwa hai licha ya kuishi shimoni humo kwa sita sita.
 
Ndani ya shimo hilo amekaa siku 6 bila kula wala kunywa hadi alipo okotwa na wasamaria wema...
Hivi sasa yuko Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma akiwa Salama  Salimini .
Yeyote Mwenye nafasi ya kumsaidia mtoto huyu anaweza kwenda moja kwa moja Hospitali au wasiliana na namba zifuatayo,  mchango  utafuatwa 0755061588 au 0755 731 234.
Dawati la Police Wanawake Mkoa wa Ruvuma wakiwa na Wauguzi kuangalia usalama wa Mtoto huyo aliye Tupwa. Kutoka kulia ni Muguzi Rukia Twahili anaye fuata Devota Umbela na aliye mshika mtoto Mwenyekiti wa Mtandao wa Police Wanawake Fadhila Chacha na wa mwisho kushoto ni A nna Chaima

Taifa Stars kwenda Ethiopia leo njiani kuifuata Morocco

 
Kikosi cha Stars
Na Boniface Wambura
KIKOSI cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kuondoka leo (Mei 26 mwaka huu) usiku kwenda Addis Ababa, Ethiopia ambapo itaweka kambi na kucheza mechi moja ya kirafiki kabla ya kwenda Morocco.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaondoka saa 5 usiku kwa ndege ya EgyptAir ikiwa na kikosi cha wachezaji 21 chini ya nahodha wake kipa Juma Kaseja.

Timu hiyo ikiwa Ethiopia, Juni 2 mwaka huu itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan ambapo siku inayofuata itaondoka kwenda Marrakech, Morocco kwa kupitia Cairo, Misri. Mechi hiyo ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech.

Mbali ya nahodha Kaseja, wachezaji wengine wanaoondoka katika kikosi hicho ambacho kina wiki sasa tangu kingie kambini jijini Dar es Salaam ni Mwadini Ally na Ally Mustafa ambao wote ni makipa.

Wengine ni Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Aggrey Morris, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd na Haruni Chanongo.

Wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu ambao wako na timu yao ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo watajiunga moja kwa moja na Stars jijini Marrakech, Juni 4 mwaka huu wakitokea Maputo, Msumbiji mara baada ya mechi yao ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Liga Muculumana ya huko.

Katika msafara huo wa Ethiopia benchi la ufundi la Stars linaundwa na Kim Poulsen (Kocha Mkuu), Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi),Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja wa timu), Dk. Mwanandi Mwankemwa (Daktari), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred Chimela (Mtunza vifaa).

Ommy Lax aachia mpya akisaka meneja

Ommy Lax katika pozi
MKALI wa wimbo wa 'Kioo Changu' alioimba na Matonya, Imani Omary 'Ommy Lax' ameachia wimbo mwingine mpya uitwao 'Wapotezee' huku akisaka meneja wa kuzisimamia kazi zake.
Akizungumza na MICHARAZO, Ommy Lax, alisema angependa kufanya kazi chini ya meneja ili kumuongoza katika majukumu yake baada ya mtu aliyekuwa akimtegemea ambaye ni mjomba wake, MP kuwa na majukumu mengine mazito binafsi.
"Natamani na ninasaka meneja wa kunisimamia kazi zangu, hivyo yeyote atakayekuwa tayari anaweza kuwasiliana nami tukae chini na kukubaliana, " alisema Ommy Lax.
Juu ya wimbo wake mpya, Ommy lax alisema ameimba na  mkali kutoka Watanashati, PNC na tayari umeanza kurushwa hewani.
Ommy Lax, alisema kazi hiyo mpya aliyorekodia kwa maprodyuza R Pino na The Timing, ni moja ya nyimbo kali kwa mwaka 2013.
Msanii huyo aliyejishughulisha na sanaa tangu akiwa shuleni na kutoa kazi ya kwanza mwaka 2006, alisema kwa sasa anajipanga kwa ajili ya kutoa  video ya wimbo huo.
"Kaka nimepakua wimbo mpya uitwao 'Wapotezee' nilioimba na PNC, ni moja ya kazi bomba siyo mchezo mashabiki wasubiri kuisikia hewani na sasa nafanya mipango ya video yake, lakini muhimu naomba mtu ajitokeze anipige tafu kama meneja," alisema.

Madabida mgeni tamasha la vipaji



MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida atakuwa mgeni rasmi katika tamasha la Mastaa chipukizi zaidi ya 320 litafanyika leo Jumapili 26, 2013 katika ukumbi wa Starlight Hotel kuanzia saa 4 asubuhi.

 

Peter Mwenda

                             

Mwenyekiti wa Shiwata, Caasim Taalib alisema Madabida ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) atapata nafasi ya kuona vikundi mbalimbali vya sanaa kikiwepo kikundi cha  Kaole, Splendid, Super Shine Taarab pamoja na wasanii mbalimbali wa Bongo Flava, Maigizo,Ngoma, Dansi na Sarakasi nao wamethibitisha kushiriki.
Taalib alisema wasanii wakongwe wa bongo flava walioalikwa ni Stara Thomas, Safi Theatre Group, Ommy G na waigizaji wakongwe wa Kaole na Splendid wataonesha umahiri wao katika fani ya sanaa Kauli Mbiu ikiwa ni Kilio cha Msanii .
Vikundi vingine vitakavyonesha vipaji vyao ni Kepteni  Shaibu, Tanzania Disabled, Uyoga Boga Village, Ndafu Arts Group, CGC, Magengistar Crew, Dodo Arts Group, Culture Arts Group, Wachapa Kazi Academy, Soweto Picture, Shiwata Commedy, Mwavionelachi, Manuari Arts Group, Tandale Morden Taarab na Begeja Wushu,
 Taalib alisema tamasha hilo ambalo limepata kibali cha Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pia wamealikwa Shirikisho la Sanaa za Maonesho Tanzania,Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF),Shirikisho la Muziki Tanzania na Shirikisho la Sanaa za maonesho Tanzania.
Mwenyekiti aliwaomba viongozi wengine wa bendi za muziki, taarab, vikundi vya sanaa,mapromota,maprodusa na wadau wote kushiriki katika tamasha hilo ili kujenga ushirikiano wa pamoja.
Peter Mwenda 
Ofisa Habari wa SHIWATA
0715/0752-222677

Kampuni ya Issere yatoa msaada wa jezi


Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Isere Sports, Abbas Ally Isere (kulia) akimkabidhi jezi seti moja mwakilishi, Dige Shaaban Nkusa kwa ajili ya timu ya vijana wa kijiji cha Mwembeni wilayani Kondoa ili kuimarisha michezo vijijini.

 

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Isere Sports imetoa vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. mil. 1.7 kwa ajili ya kuendeleza vijana katika wilaya ya Kondoa.

Akikabidhi vifaa hivyo jana, Mkurugenzi wa Masoko wa Isere Sports, Abbas Isere alisema ametoa vifaa hivyo ili kuwasaidia vijana kupenda michezo ili kujenga afya na kujikinga na vitengo cha kihalifu.


 

Abbas alisema vifaa alivyotoa ni kwa ajili ya vijiji vya Changaa kwa Mafunchi ambako wamepewa jezi, mipira na soksi, katika kijiji cha Mwembeni kata ya Hondomairo wilayani Kondoa wamekabidhiwa vifaa kama hivyo.

Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya vijana wa Changaa, Issa Lubuva alisema umefika wakati kwa wananchi waishio mijini kuwakumbuka vijana waliobaki nyumbani kwa kuwapatia vifaa vya michezo.

Naye Dige Shaaban aliyepokea vifaa kwa niaba ya kijiji cha Mwembeni alisema wachezaji wengi wapo vijijini lakini hawajapata fursa ya kuonesha vipaji vyao hivyo vifaa hivyo vitasaidia kutoa wachezaji kutoka wilaya ya Kondoa.

Abajalo kuonyeshana kazi na Kariakoo Lindi leo RCL







Na Boniface Wambura
Raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) inaendelea tena leo (Mei 26 mwaka huu) kwa mechi sita za kwanza zitakazochezwa katika miji sita tofauti.

Abajalo ya Dar es Salaam na Kariakoo ya Lindi zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam wakati Machava FC ya Kilimanjaro itakuwa mwenyeji wa Mpwapwa Stars ya Dodoma kwenye Uwanja wa Ushirika mjini Moshi.

Nayo Stand United FC ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida huku Polisi Jamii ya Bunda mkoani Mara ikimenyana na Biharamulo FC ya Kagera kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

Mjini Kigoma kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika ni kati ya wenyeji Saigon FC na Katavi Warriors ya Katavi wakati Njombe Mji itaikaribisha Kimondo SC ya Mbeya kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.

Twiga Stars waingia kambini

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9qCbvL7ACfY-W273M78SjNwShyphenhyphento0pGY0jocv4YwPbT2si8HWRgx-R_CH50plR4aAhjyvtlT_RlMM3p55WStyP9sBPLbjbDHdB-_SW_dqsAbqS6oRTd0nBZTJOMDGRyTRgcDxKE7WB-Zm/s1600/Pix-1.jpg
Kikosi cha Twiga Stars

 
Na Boniface Wambura
KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu (Twiga Stars), Rogasian Kaijage amewaita kambini wachezaji 30 ikiwa ni mwendelezo wa kuijenga na kuiimarisha timu hiyo.

Twiga Stars itakuwa na kambi ya siku kumi kuanzia Jumapili (Mei 26 mwaka huu) ambapo baadaye inatarajia kucheza mechi moja ya kirafiki kabla ya wachezaji kurudi kwenye klabu zao.

Kambi hiyo ni mwendelezo wa programu iliyopendekezwa na kocha kuijenga na kuiimarisha timu hiyo kwa vile haina mashindano mwaka huu, na itakuwa kambi ya pili baada ya ile iliyofanyika Machi mwaka huu.

Wachezaji walioitwa na klabu zao kwenye mabano ni Asha Rashid (Mburahati Queens), Aziza Mwadini (Zanzibar), Belina Julius (Lord Barden), Ester Chabruma (Sayari), Ester Mayala (TSC Academy), Eto Mlenzi (JKT), Evelyn Sekikubo (Mburahati Queens) na Fatuma Bushiri (Mburahati Queens).

Fatuma Hassan (Mburahati Queens), Fatuma Omari (Sayari), Flora Kayanda (Tanzanite), Hamisa Athuman (Marsh Academy), Hellen Peter (JKT), Maimuna Said (JKT), Mwajuma Abdallah (Tanzanite), Mwanahamisi Omari (Mburahati Queens), Mwanaidi Tamba (Mburahati Queens) na Mwapewa Mtumwa (Sayari).

Nabila Ahmed (Marsh Academy), Pulkeria Charaji (Sayari), Rehema Abdul (Lord Barden), Rukia Khamis (Uzuri Queens), Semeni Abeid (Tanzanite), Sharida Boniface (Makongo Sekondari), Sophia Mwasikili (Sayari), Therese Yona (TSC Academy), Vumilia Maarifa (Evergreen) na Zena Khamis (Mburahati Queens).

Miss Tabata 2013 waenda Mikumi



WASHIRIKI wa wa Dodoma Wine, Redd’s Miss Tabata 2013 leo wanatarajiwa kwenda kutembelea hifadhi ya taifa ya Mikumi.
Mratibu wa shindano hilo Godfrey Kalinga alisema warembo hao wataondoka na gari ya aina ya Toyota Double Coaster ikiwa na warembo 20 pamoja na walimu na viongozi wao.
Kalinga alisema ziara hiyo ina lengo la kukuza utalii wa ndani na kujenga ushirikiano miongoni mwao.
Alisema kuwa warembo hao pia watapata fursa ya kutembelea vivutio mbalimbali vilivyomo kwenye mbuga hiyo iliyoko mkoani Morogoro.
“Tutarudi Dar es Salaam Jumatatu kujiandaa na shindano letu litakalofanyika Ijumaa ijayo,” alisema Kalinga.
Kadhalika, Kalinga  alisema kuwa ziara hiyo imedhaminiwa na kampuni ya CXC Africa.
Shindano la kumsaka Miss Tabata  litafanyika Ijumaa ya Mei 31 katika ukumbi wa Da’ West Park, Tabata.
Wadhamini wa shindano hilo ni Nipashe, Redds, Dodoma Wine, Nipashe, Vayle Springs, Multichoice, Fredito Entertainment, Integrated Communications Limited, CXC Africa, Brake Point na Saluti5.
Warembo hao ni Madgalena Bhoke (21), Kabula Juma Kibogoti (20), Upendo Dickson Lema (22), Hidaya David Mwenda (22), Aneth Ndumbalo (19),  Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Musa Kitereja (19),  Rehema Kihinja (20),  Pasilida Mandali (21), Brath Chambia (23), Joaniter Kabunga (21), Recho Mushi (20),Caroline Sadiki (20) na  Suzan Daniel (18).
Anayeshikilia taji la Miss Tabata kwa sasa ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.
Miss Tabata inaandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts.

MSHAMBULIAJI NEYMAR ASAINI MIAKA MITANO FC BARCELONA


 

Neymar akichuana na Messi wakati wa mechi yao ya fainali ya Kombe la Dunia la Klabu baina ya Barca na Santos mwaka juzi
Neymar akichuana na Glen Johnson wakati wa mechi baina ya timu ya taifa ya Brazil na England

Neymar (katikati) akikimbizwa na Gary Cahill (kulia) na Smalling (kushoto)

Neymar akionyeshana shughuli na Tom Cleverly
Karibu Barca mwana.... Neymar akipongezana na Lionel Messi baada ya mechi yao ya fainali ya Kombe la Dunia la Klabu mwaka juzi. 

BARCELONA imefanikisha kumsajili mshambuliaji wa Santos, Neymar kwa dau linalokadiriwa kuwa euro milioni 28 leo.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil atajiunga na Barcelona kwa mkataba wa miaka mitano baada ya kukataa ushawishi wa Real Madrid, ambao wanaamini kwamba walitoa ofa nono ya euro milioni 35.

Mshambuliaji huyo ataingiza malipo binafsi ya euro milioni 7 kwa mwaka, ambayo licha ya kwamba ni pungufu ya ambayo angepata Real Madrid, yatamshuhudia akipata malipo ya ziada kutokana na maafikiano ya mkataba na kampuni ya kimataifa ya vifaa vya michezo ya Nike.

Neymar amekuwa katika rada za klabu nyingi kubwa za Ulaya kwa miaka kadhaa baada ya kung'aa Amerika Kusini na aliingia kuwania tuzo ya Ballon d'Or mwaka 2013.

Nyota huyo amekuwa akihusishwa na klabu kadhaa kubwa kama Chelsea, Bayern Munich na PSG, lakini Barcelona imeziacha mbali sana klabu hiyo kwa kupewa nafasi kubwa zaidi ya kumnasa nyota huyo mwenye umri wa miaka 21.

Mabingwa hao wapya wa La Liga, hata hivyo, wamewapiku mahasimu wao Real katika kumsajili Neymar ambaye atajiunga nao katika kipindi hiki cha usajili kujiandaa na msimu ujao wa 2013-14.

Kama sehemu ya dili hilo, Barcelona imeafiki kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Santos zenye thamani ya euro milioni 2 kila moja, hivi karibuni, moja kila bara - Amerika Kusini na Ulaya.

Klabuni Nou Camp, Mbrazil huyo atajiunga na nyota wenzake wanaotokea katika bara ya Amerika Kusini kama Lionel Messi, Alexis Sanchez, Javier Mascherano na nyota wenzake wa timu ya taifa ya Brazil, Dani Alves na Adriano.

Neymar alipata kusema siku za nyuma kwamba anataka kusubiri kuhamia Ulaya hadi baada ya fainali za Kombe la Dunia 2014, lakini kutokana na mkataba wake kumalizika mwakani, Santos wamelazimika kumuuza ili mchezaji huyo waliyemlea tangu mdogo asije kuondoka bure.  

Bayern Munich waizima Dortmund na kutwaa Ubingwa Ulaya

Top of the pile: Bayern Munich are the Champions of Europe for a fifth time after beating Borussia Dortmund
Wachezaji wa Bayern wakishangilia na taji lao la Ulaya jana

Dutch delight: Arjen Robben settled the Champions League final with a late, late strike
Aerjen Robben akishangilia bao lake
HUU ni msimu ni Bayern Munich! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya mabingwa hao wa Ujerumani kunyakua taji la Ligi ya Ulaya usiku wa kuamkia leo kwa kuwanyuka mahasimu wao Borussia Dortmund kwa mabao 2-1.
Winga wa Kiholanzi, Arjen Robben ndiye aliyewahakikishia wakali hao wa Ujerumani ambao wamekuwa na msimu mzuri mwaka huu kwa kufunga bao dakika za lala salama la pambano hilo.
Robben alifunga bao katika pambano hilo la fainali lililochezwa kwenye uwanja wa Wembley, London nchini England na kuipa Bayern taji hilo lililokuwa halina mtu baada ya waliokuwa mabingwa watetezi, Chelsea kulitema mapema.
Mholanzi huyo alifunga bao hilo tamu dakika ya 89, na pia ndiye aliyetoa pasi ya bao la kwanza la mabingwa hao wapya wa Ulaya lilitumbukizwa kimiani na Mario Mandzukic katika dakika ya 60.
Dortmund iilijipatia bao lake dakika saba baada ya kutanguliwa kufungwa na wapinzani wao kupitia mkwaju wa penati wa Ilkay Gundogan baada ya Mario Reus kuangushwa langoni mwa Bayern na Dante.

Saturday, May 25, 2013

Majambazi waliopora fedha Dar wanaswa

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limewakamata watuhumiwa wa ujambazi watano wanaodaiwa kupora sh milioni 46 za mfanyabiashara wa bia wilayani Temeke, Ivon Urio.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Suleiman Kova, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa tano asubuhi na watuhumiwa wote wamekiri kuhusika na tukio hilo, na kumtaja mwenzao John Tesha kwamba ndiye aliyekimbia na fedha hizo.
Kova aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Bernards Mashamba, Steven Thadeo, Adams Isudor, Johns Benja na Sultanis Kipensa huku juhudi za kumtafuta mwenzao aliyekimbia zikiendelea.
Alisema pesa hizo zilikuwa zimewekwa katika boksi kwa ajili ya kupelekwa benki ya BOA ghafla mfanyabiashara huyo akavamiwa na watuhumiwa hao waliokuwa na bunduki kubwa moja na bastola mbili wakitumia pikipiki mbili aina ya Boxer mojawapo ikiwa na namba za usajili T 311 CGE rangi nyekundu.
Kova alitaja maeneo waliyokamatiwa majambazi hao ni Chamanzi, Manzese, Keko, Kongowe Kizinga na Mtoni Mtongani.
Katika hatua nyingine, Kova alisema pikipiki 300 zimekamatwa kati ya hizo 201 ni aina ya Boxer ambazo zinasadikiwa kuwa kwa kiasi kikubwa zinatumiwa na majambazi.
Aliongeza kuwa wanaandaa utaratibu wa kuzipaka rangi pikipiki zote kama zilivyo teksi ili zijulikane wilaya zinakotoka na wamiliki wake.
Kamanda Kova alisema mpango huo utasaidia kudhibiti uhalifu na ajali zinazotokea mara kwa mara.    

Ajuza watatu wachinjwa kama kuku Bunda wakituhumiwa uchawi

Matukio kama haya ya watu kujichukulia sheria mikononi na kuwauwa wenzao kwa kuwachoma moto yamekithiri katika jamii na ndiyo yaliyosababisha ajuza watatu kuuwawa kikatili usiku wa kuamkia leo huko Bunda, Mara
MAUAJI ya kikatili yametokea usiku wa kuamkia leo wilayani Bunda, mkoani Mara baada ya watu wenye hasira wa kijiji cha Kasaula kuwauwa kwa kuwachinja kama Kuku kisha kuwachoma moto ajuza watatu kwa kuwatuhumu wanajihusisha na vitendo vya kishirikina.
Pia watu hao mbali na kuwaua kikatili vibibi hivyo kwa tuhuma kwamba walimuua kijana mmoja aitwaye Sale Ligolo, walichoma moto na kuteketeza nyumba walizokuwa wakiishi wazee hao pamoja na kupora kuku waliokuwa wakiwafuga na kuatafuna kumaliza hasira zao.
Kwa mujibu wa wa taarifa ya mwandishi Masau Bwire aliyepo Bunda kwa sasa, tukio hilo limetokea usiku wa kumakia leo baada ya watu hao wenye hasira kuwasaka ajuza hao baada ya kuwepo tuhuma kwamba walishirikiana kumuua kijana huyo hivi karibuni.
Inaelezwa kijana huyo alikufa kwa kugongwa na gari, lakini dereva aliyemgonga alidai hakuona kama alimgonga mtu ila mbwa na pia inaelezwa  tangu azikwe kijana huyo alikuwa akirejea kwa mkewe na kumuita nyakati za usiku pamoja na kusumbua familia yao akitaka apewe chakula na ndipo wanafamilia hao walipoamua kwenda kwa mganga kuchunguza tukio hilo.
Inaelezwa ndipo walipotajiwa majina ya wanavijiji watatu wa kijiji hicho ambao hata hivyo walitoroka kwenda vijiji vya jirani pamoja na familia zao kabla ya usiku wa leo kuvamiwa walipokuwepo na kuangushiwa adhabu hizo za kinyama.
Wa kwanza kushambuliwa na kuuwa ni bibi aitwaye Bi Mgala ambaye alikimbilia kijiji cha jiorani kwa rafikie aitwaye Bi Laya, ambapo walimtaka miguu yote miwili na kumtenganisha kichwa na kiwiliwili kabla ya kumchoma moto ambapo hata hivyo kitu cha ajabu ni kwamba ziliungua nguo zake tu huku mwili ukiwa upo vile vile.
Baadaye walimgeukia Bi Laya aliyekuwa akitaka kuwatoroka na kumfanyia unyama kama rafikie kwa kile walichodai kwa kosa la kumhifadhi Bi Mgala kwa kuamini huenda wanafanya shughuli za kishirikina pamoja na baadaye kurudi Kasaula na kumnasa Bi Chausiku na kumfanyia kama walivyowafanyia ajuza hao wengine kisha kuchoma nyumba tatu.
Bibi wa tatu wanayemtuhumu pia kwa ushirikina, ametimka kijijini hapo, lakini nyumba yake imeteketezwa pamoja na kuku waliokuwa wakiwafuga kuporwa na watu hao na kutumia moto waliouwasha katika nyumba hizo kuwachoma na kuwala kwa hasira.
Kamanda wa Polisi wa Bunda, Mika David Nyange amethibitisha juu ya tukio hilo la kusikitisha na kwamba wanedelea na upelelezi kwa nia ya kuwasaka waliohusika na kitendo hicho cha kujichukulia sheria mikononi.

Friday, May 24, 2013

Baada ya kung'ara Gor Mahia, Ivo Mapunda awindwa na Tusker

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgcOsm-7zdR8dd1_VaKXsG_pBGttOec_6nguW8rxdX0f25fGFel_h1i8t__5lKCqSGd3tP8YSGwX1MS8JUGnUEQ-6eDQgXlYYQaO-VxDlPnOlnnAqByjy6zuTcYxXENkjTNjtlTc7tBatOJ/s400/IVO-MAPUNDA.jpg
Ivo Mapunda
KIPA nyota wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Ivo Mapunda anayeidakia Gor Mahia ya Kenya, amesema yupo katika harakati ya kuhamia kwa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Kenya, Tusker.
Hata hivyo kipa huyo aliyewahi kuichezea Bandari-Kenya kabla ya kutua Gor Mahia, alisema anasubiri kwanza kumalizika kwa mkataba wake mwishoni mwa mwaka huu kuamua hatma yake.
Alisema kocha wa Tusker, Robert Matano alimpigia simu mara baada ya kung'ara katika pambano la marudiano la Nusu Fainali ya 8 Bora ili kujua mkataba wake ukoje kabla ya kumvuta Tusker.
Mapunda aliyechaguliwa Mchezaji Bora wa pambano hilo lililoisha kwa suluhu ya kutofungana, lakini Tusker ikisonga mbele kwa ushindi wa bao 1-0 iliyopata katika mechi ya awali, alisema iwapo Tusker itamvutia kimasilahi atahamia kwa mabingwa hao wa ligi.
"Nitaangalia masilahi kwanza kama jamaa nibaki Gor Mahia au kujiunga na Tusker, ila nasubiri kwamba mkataba wangu na klabu yangu ya sasa uishe Desemba mwaka huu," alisema Mapunda.
Kuhusu mafanikio anayoyapata akiwa Kenya, kipa huyo aliyewahi kuidakia Prisons Mbeya na St George ya Ethiopia alisema yanamfariji mno baada ya kupuuzwa nyumbani akionekana kaisha.
"Nafurahia mno kupata mafanikio ugenini na kuthaminika naamini Mungu ataendelea kunisaidia zaidi na kutamba," alisema.
Mapunda ambaye amekuwa chaguo la kwanza katika kikosi cha Gor Mahia anatarajiwa kuiongoza timu yake Jumapili ikiwa ugenini katika mji wa Mumias dhidi ya Western Stima katika mechi ya Ligi.

HATIMAYE HARUNA NIYONZIMA ASAINI MIAKA MIWILI YANGA SC


Uongozi wa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Vodacom  klabu ya Young Africans leo umekata mzizi wa fitina kwa kiungo mchezeshaji kutoka nchini Rwanda Haruna Niyonzima kuendelea kuitumikia timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili kufuatia kumalizika kwa mkataba wake awali.
Akiongea na waandishi wa habari makao ya klabu ya Yanga, katibu mkuu Lawrence Mwalusako amesema wameamua kumuongezea mkataba mchezaji huyo kufuatia kuuhitaji mchango wake kwani katika kipindi chake cha miaka miwili ameonyesha kiwango cha hali ya juu na kutoa mchango mkubwa.
 Mwalusako amesema kumekua yakiongelewa mengi juu ya mchezaji wetu Niyonzima, baadhi ya vyombo vya habari vimekua vikitoa taarifa za kupotosha juu yake ukweli leo umedhihirika kwamba Niyonzima ni mchezaji wa Yanga na ataendelea kuitumikia kwa miaka miwili.
Haruna Niyonzima alijiunga na Yanga kwa mara ya kwanza Julai 2011 akitokea katika timu ya APR nchini Rwanda ambapo katika miaka yake miwili aliyoichezea timu ya Yanga amefanikiwa kuisadia kupata makombe mawili ya ubingwa wa Ligi Kuu 2012-2013 na Kombe la Kagame 2011-2012.
Naye Niyonzima amesema anawashukuru wanachama, washabiki na wapenzi wa klabu ya Yanga kwa kuwa naye muda wote, Yanga ni nyumbani kwangu kwani najisikia furaha kuichezea timu hii na malengo yangu ni kuisadia ili iweze kufanya vizuri katika upatashindano ya kimataifa.
Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya klabu ya Yanga Abdallah BinKleb amesema palikua na propaganda nyingi juu ya Niyonzima, lakini ukweli ndio huu Niyonzima ataendelea kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka miwili.
"Tunautambua mchango wake alioutoa kwa miaka mwili kwani ameweza kutupatia vikombe viwili vya Ligi Kuu ya Vodacom na Kombe la Kagame hivyo tumemuongezea mkataba wa miaka miwili tena ili aendelee kutoa mchango wake na kuisadia timu katika michezo ya kimataifa" alisema BinKleb.

Credit:Global Publishers

Banana Zorro, Khadija Kopa kupamba Miss Ukonga kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhWIQs31cc1ObyFSwZFkTslMrCrqe8JOHfVCu5nkNNQIMV-QitnF79eyi9AgiPQKx9mq3a7k7lemiNEE0Y6epiRyqHRbVYnrCXUJvSOY0_6ingI_jceO6O3ekt0BiFPfLJBng9Pq07XD6o/s400/IMGP0489.JPG
Banana Zorro na mmoja wa waimbaji wake wa B-Band wakitumbuiza

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhOH8NqF9z-_bsGqNP4n7EmBzCzeCozBhgE-FpTw7JPWKIK3AMrIKZOl0OcZt7XFra7Cgs0XElATkb75G19PbU0rCcdIdYf0Jb2yiqhyphenhyphenPJ38iRmtyFJ8YyEVicrcy3cSiVPESCxSnCSigU/s1600/kopa.jpg
Khadija Kopa
WASANII nyota nchini Banana Zorro na bendi yake ya B-Band pamoja na Malkia wa Mipasho, Khadija Kopa kesho wanatarajiwa kuwasinidikiza warembo 17 watakaochuana kuwania taji la urembo la Redd's Miss Ukonga 2013, litakalofanyika jijini Dar es Salaam.
Warembo hao watachuana kwenye shindano litakalofanyika kwenye ukumbi wa Wenge Garden na kusindikizwa na burudani ya wasanii hao wanaotamba nchini na nyimbo mbalimbali.
Mratibu wa shindano hilo, Rashid Kazumba aliiambia MICHARAZO kuwa jumla ya warembo 17 watachuana kuwania taji hilo sambamba na kuwania nafasi ya kuwania ushiriki wa shindano la Miss Ilala litakalofanyika baadaye.
Kazumba alisema maandalizi kwa ujumla kwa ajili ya kinyang'anyiro hicho yamekamilika na kwamba inasubiriwa tu kuona nani atakayeibuka kidedea usiku wa kesho.
Aliwataja baadhi ya warembo watakaochuana katika shindano hilo lililodhaminiwa na makampuni kadhaa nchini ni pamoja na Glory Jigge, Happiness Jackson, Flosek Mwakanyamale, Annatolia Raphael, Musnat Hassan, Gift Swai, Natasha Mohamed, Vanessa Magule, Queen John, Martha Gewe, Nancy Obasi, Mwanamkasi Bakari na Diana Joachim.



Klabu za Ligi Kuu kupigwa msasa kuhusu usajili wa TMS




Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeandaa semina ya usajili kwa njia ya mtandao (Transfer Matching System-TMS) kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom kwa ajili ya msimu wa 2013/2014.

Semina hiyo itafanyika Jumamosi (Mei 25 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF saa 3 kamili asubuhi ikishirikisha watu wawili kutoka kila klabu ambao ni TMS Manager, na ofisa mwingine wa klabu.

Klabu za ligi hiyo zinazotakiwa kuhudhuria semina ya usajili ni Ashanti United, Azam, Coastal Union, JKT Ruvu, Kagera Sugar, Mbeya City, Mgambo Shooting, Mtibwa Sugar, Oljoro JKT, Rhino Rangers, Ruvu Shooting, Simba, Tanzania Prisons na Yanga.

Semina hiyo huenda ikazisaidia klabu za ligi hiyo ambao mara kadhaa wamekuwa wakiingia mkenge katika zoezi la usajili wa wachezaji kutokana na mfumo huo mpya kuwakanganya kama ilivyojitokeza msimu huu ulioisha katika usajili wa mchezaji Mbuyi Twitte aliyegombewa Simba na Yanga.

Banka kuitema Bandari-Kenya, huenda akarejea nyumbani au....!


Banka (kushoto) akiwa na wachezaji wenzake wa Kitanzania wanaocheza wote Bandari-Kenya
KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa nchini Kenya, Mohammed Banka amesema hafikirii kuongeza mkataba mpya na timu yake ya Bandari Kenya bila kueleza sababu.
Banka, alisema kuna mambo mawili kichwani mwake baada ya kuisha kwa mkataba wake na klabu hiyo yenye maskani yake Mombasa, ama arejee nyumbani au kujiunga na timu nyingine.
Kiungo huyo alisema mkataba wake unatarajiwa kuisha miezi miezi mwili ijayo na hivyo hajaamua kuongeza mkataba mpya zaidi ya kutaka kuondoka klabuni hapo.
"Tunamalizia duru la kwanza Jumapili kwa kuumana na Sofapaka na mimi ndiyo namalizia mkataba wangu na sifikirii kuongeza tena zaidi ya kurudi nyumbani au kusonga mbele," alisema Banka.
Mchezaji huyo aliyekuwa miongoni mwa walioipandisha Ligi Kuu timu hiyo ambayo kwa sasa ipo nafasi ya sita kwenye msimamo wa timu 16, alisema haoni sababu ya kubaki Bandari bila kufafanua.
Hata hivyo hivi karibuni mchezaji huyo alidokeza kuna mambo hayapo sawa hasa suala la masilahi tofauti na makubaliano yaliyokuwepo kati yake na uongozi wa timu hiyo ilipopanda daraja.


TFF yasisitiza wenyeviti wa FA ndio wasimamizi wa RCL




Na Boniface Wambura
WAKATI mechi za kwanza za raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zinachezwa wikiendi hii, Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imesisitiza kuwa wasimamizi wa mechi za ligi hiyo ni wenyeviti wa mikoa wa vyama vya mpira wa miguu.

Kamati hiyo chini ya uenyekiti wa Ramadhan Nassib ilikutana jana (Mei 23 mwaka huu) kupitia ripoti za makamishna kwa mechi za raundi ya kwanza ya RCL iliyomalizika wikiendi ya Mei 18 na 19 mwaka huu.

Kuhusu viwanja vinavyotumika kwa ligi hiyo, Kamati imesema vitaendelea kuwa vile vya makao makuu ya mikoa, na kwa vile vilivyokuwa vimeombwa vifanyiwe marekebisho ili viweze kukaguliwa kwa ajili ya RCL msimu ujao. Pia imeitaka mikoa kuendelea kuboresha viwanja vinavyotumika sasa, lakini vina upungufu.

Vilevile Kamati imebaini kuwa zimekuwepo pingamizi kuhusu usajili wa wachezaji ambapo imesema haiwezi kujadili pingamizi hizo kwa vile mikoa yote haikuwasilisha usajili wa wachezaji wa klabu husika uliofanyika mikoani kama ilivyoagizwa na kuelekezwa na TFF.

Hata hivyo, Kamati imeitaka mikoa ambayo klabu zao zimefanikiwa kuingia raundi ya pili kuwasilisha usajili huo haraka.

Pia Kamati imebaini kuwa zipo baadhi ya klabu ambazo zimekata rufani kuhusu usajili wa baadhi ya wachezaji, na kusisitiza kilichowasilishwa ni pingamizi kwa vile kwa mujibu wa kanuni masuala ya uwanjani hayakatiwi rufani. Hivyo, Kamati imeshauri klabu zilizokata rufani zilirejeshewe ada zilizolipa kwa ajili hiyo.

Makamishna na waamuzi wanaosimamia mechi za RCL wamekumbushwa kuwa ili mchezaji aruhusiwe kucheza mechi ni lazima awe na leseni yake (kadi ya usajili), vinginevyo asiruhusiwe kucheza mechi husika.

Mechi za RCL zinaendelea wikiendi hii ambapo zote zitachezwa Jumapili (Mei 26 mwaka huu) isipokuwa mechi kati ya Friends Rangers ya Dar es Salaam na African Sports ya Tanga itakayochezwa Jumamosi (Mei 25 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi.

Nayo mechi kati ya Abajalo ya Dar es Salaam na Kariakoo ya Lindi iliyokuwa ichezwe Jumamosi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam sasa itachezwa Jumapili kwa vile siku hiyo uwanja huo utatumika kwa mazoezi ya Taifa Stars.

Mechi nyingine za RCL zitakazochezwa Mei 26 mwaka huu ni Machava FC ya Kilimanjaro dhidi ya Mpwapwa Stars ya Dodoma kwenye Uwanja wa Ushirika mjini Moshi, Stand United FC ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida.

Polisi Jamii ya Bunda mkoani Mara na Biharamulo FC ya Kagera zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma. Mjini Kigoma kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika ni kati ya wenyeji Saigon FC na Katavi Warriors ya Katavi.

Nayo Kimondo SC ya Mbeya itakuwa mgeni wa Njombe Mji ya Njombe katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe. Mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu.

Timu zitakazofuzu kucheza raundi ya tatu zitacheza mechi za kwanza kati ya Juni 8 na 9 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakuwa kati ya Juni 15 na 16 mwaka huu.

Sasa ruksa kwa Dk Slaa kuoana na mchumba wake Josephine Mushumbuzi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhraC9iZRYXVNVm9NqNkpaKtt00FJUrgjJ20tjW7uw8VZAV2l2xCsa2DxseokFhXxi8XHjbYkrN-G5Eg6GQDuB3gFAvn1GOFpzsh9m1YKJAyhTzhVERBpIPmei-IZLLqnakhleRVhkl1XA/s640/dkt+slaa.jpg
Dk Slaa (kulia) na mchumba wake, Josephine Mushumbuzi


HATIMAYE Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, imetupilia mbali rufaa iliyokuwa imekatwa na aliyekuwa mume wa Josephine Mshumbusi, ambaye ni mchumba wa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk Wilbroad Slaa, Mahimbo baada ya kuiona rufaa hiyo haina msingi wowote kisheria.



Hukumu hiyo ya rufaa ya  madai ya ndoa Na.32/2012 ilitolewa jana na Hakimu Aniseth Wambura ambapo alisema mahakama yake imefikia uamuzi huo wa kuitupa rufaa hiyo kwasababu haina mantiki ya kisheria.



Hakimu Wambura alisema mahakama yake imekubalina na hukumu iliyotolewa Aprili 2012 na Mahakama ya Mwanzo Sinza katika kesi ya madai talaka iliyokuwa imefunguliwa na Mshumbusi anayetetewa na wakili wa kujitegemea Philemon Mutakyamilwa  dhidi ya Maimbo ambapo mahakama hiyo ya chini ilitangaza kuwa hakukuwa na ndoa baina ya watu hao kwasababu Maimbo alikuwa ni mzinzi, simwaminifu katika ndoa yake na alikuwa akimtesa mkewe.



“Baada ya mahakama yangu kusikiliza hoja za mwomba rufaa na mjibu rufaa ,mahakama hii imefikia uamuzi wa kukubali hoja za Mshumbisi kuwa kwa tabia ile ya mbaya ya uzinzi na ukosefu wa uaminifu katika ndoa yake hapakuwepo na ndoa baina yao hivyo mahakama yake inatangaza kuwa hukumu ya mahakama ya Mwanzo Sinza ambayo iliivunja ndoa hiyo ilikuwa hukumu sahihi “alisema hakimu Wambura.



Akizungumza na mwandishi wa habari hizi baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo wakili Mutakyamilwa alisema amefurahishwa na hukumu hiyo kwani mahakama imetenda haki  kwasababu kesi hiyo ya madai ya talaka ilikuwa na msukumo wa siasa chafu zilizokuwa na lengo chafu la kumchafulia jina mteja wake(Mshumbusi) ambaye kwa sasa ni mzazi mwenzie Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk.Wilbroad Slaa.
Kutokana na hali ni wzi kwamba Dk Slaa sasa wanaweza kuoana na mpenzi wake huyo waliyezaa naye mtoto mmoja.

Chegge, Mhe Temba wanaswa na Maringo 7


Mhe Temba na Chegge

Maringo Saba katika pozi
MCHEKESHAJI anayetamba kwenye kipindi cha Mizengwe, Rashid Costa 'Maringo 7' amewajumuisha wakali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Said Chegge, Mheshimiwa Temba na 'bosi' wao Saidi Fella kwenye filamu yake anayotarajia kuitoa hivi karibuni.
Maringo 7 aliyewahi kutamba na michezo ya kuigiza ya kwenye runinga akiwa na kundi la Shirikisho Msanii Afrika, alisema filamu hiyo itafahamika kwa jina la 'Papaa' na atawashirikisha wakali hao na nyota wengine wa filamu nchini.
"Nipo katika maandalizi ya mwisho ya kukamilisha filamu yangu mpya itakayoitwa 'Papaa' ambayo mbali na kucheza mimi na nyota wengine wa filamu, pia ndani mwake kutakuwa na Said Fella, Mhe. Temba, Said Chegge na YP," alisema Maringo 7.
Maringo 7, alisema ana imani kazi hiyo itathibitisha kipaji alichonacho katika sanaa ya uigizaji na muziki, fani anazozifanya kwa wakati mmoja kwa sasa.

Salha, Hammer Q watoa albamu ya Mke na Mume

Salha Abdallah na mumewe Hammer Q
MUIMBAJI nyota wa taarab wa kundi la Dar Modern, Salha Abdallah akishirikiana na mumewe Husseni Mohammed 'Hammer Q' wamekamilisha kurekodi nyimbo tatu mpya kwa ajili ya kutoa albamu yao.
Akizungumza na MICHARAZO, Salha ambaye 'amelitosa' kundi la Five Star lililokuwa limetangaza kumnyakua hivi karibuni, alisema nyimbo mbili kati ya hizo zipo katika miondoko ya taarab na wimbo mwingine upo katika mahadhi ya mchiriku.
Salha aliyeripotiwa kupewa kipigo kikali na mumewe huyo kiasi cha kulazwa hospitalini kabla ya kusameheana, alizitaja nyimbo hizo tatu kati ya nne walizopanga kuwamo katika albamu hiyo kuwa  ni 'Tunaoana', 'Safiri Salama' na 'Nisamehe Tusonge Mbele'.
"Wimbo wa 'Nisamehe Tusonge Mbele' upo katika mahadhi ya Mchiriku na nyingine zipo katika miondoko ya taarab na kibao cha mwisho ambacho tutakirekodi baadaye ni ule wa 'Subhana Heri'," alisema Salha.
Muimbaji huyo aliyeingia kwenye fani hiyo mwaka 2008 kwa kuvutiwa na sauti tamu ya marehemu Mariam Khamis, alisema wameanza kutoa albamu hiyo lakini mipango yao ya baadaye kuja kuanzisha kundi lao ili kuepuka kuwatumikia watu.
"Tuna mipango ya kuja kuanzisha kundi letu wenyewe baada ya kufanya kazi kwa watu kwa kipindi kirefu bila ya kupata mafanikio yoyote ya maana," alisema Salha

TP Mazembe yamnyakua kocha wa Mali


https://lh6.googleusercontent.com/-VEtRhDY7qrI/UZzx8PeR2fI/AAAAAAAAlAE/izjc83pUpI8/patrice-carteron-dijon5.jpg?imgmax=800
Kocha Patrice Carteron

LUBUMBASHI, Congo DR
KAMPENI za Mali za kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia zilipaa juzi Jumatano wakati kocha wao Patrice Carteron  aliposaini mkataba wa miaka miwili na klabu ya TP Mazembe ya Congo.
Mali, ambayo chini ya kocha huyo Mfaransa ilimaliza ya tatu katika fainali ya Mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini, ina mechi za kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Rwanda na Benin Juni 9 na Juni 16.
"Tunamtambua Patrice Carteron kama kocha wa Mali," rais wa shirikisho la soka la nchi hiyo Hamadoun Kola Cisse alisema katika mahojiano na kituo cha radio cha Ufaransa.
"Yuko katika mkataba hadi mwakani lakini kwa kwenda kusaini mkataba mwingine anajiweka matatani," Cisse alisema.
Katika muda huo huo wa mahojiano, beki wa zamani wa klabu za St Etienne na Sunderland, Carteron (42) alikuwa alikuwa akitambulishwa hadharani kwenye Uwanja wa Mazembe mjini Lubumbashi.
"Hatuna pingamizi kwa Carteron kuiongoza Mali katika mechi zao mbili zijazo Juni licha ya kusaini mkataba nasi," mwenyekiti Moise Katumbi alisema.

JK awatia moyo Stars kwa Morocco

Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Taifa Stars jana Ikulu

Wachezaji wa Stars wakijifua kwa mazoezi

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, amewaambia wachezaji wa timu ya taifa ya soka (Taifa stars) kwamba wanaweza kuwafunga tena Morocco katika mechi yao ya marudiano ya kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia 2014 mjini Marrakech kama walivyowafunga jijini Dar es Salaam katika mechi yao ya awali.
Stars watarudiana na Morocco Juni 7 katika mechi yao ya nne ya hatua ya makundi baada ya kuwashushia kipigo kilichoishangaza "dunia ya soka" cha magoli 3-1 katika katika mechi yao ya awali jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na timu hiyo wakati alipoialika Ikulu kwa ajili ya mlo wa mchana jana, Rais Kikwete alisema: "Maadamu mliwashinda mara ya kwanza, hakikisheni mnawashinda tena kwa kuwa mkishinda tunafurahi sana na mkishindwa tunanyong’onyea sana."
Rais Kikwete aliiambia timu hiyo kuwa uwezo waliouonesha katika mechi ya kwanza ya kuwania kufuzu kwa fainali hizo dhidi ya Gambia ambayo walishinda 2-0, na kisha kuisambaratisha Morocco 3-1, zinathibitisha uwezo mkubwa walionao Watanzania katika mchezo huo na kwamba cha muhimu ni kujiamini.
Aidha, amempongeza kocha wa timu hiyo Kim Poulsen pamoja na Kamati ya Ushindi ya Taifa stars kwa kuisaidia timu hiyo kwa hali na mali ili iweze kushinda na hatimaye iweze kufuzu kwa mara ya kwanza katika historia kucheza fanali za Kombe la Dunia. Stars itahitaji kucheza mechi tano kishujaa ili kwenda Brazil 2014.
Naye Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Fenella Mukangara alisema serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa michezo nchini ili kupambana na changamoto zinazoikabili timu hiyo ili kuiwezesha kufanya vizuri.
Kwa upande wake kocha Poulsen alimshukuru Rais Kikwete kwa kuwakaribisha na kuwatia moyo ambapo aliahidi kuifundisha vizuri timu hiyo ili kuhakikisha kuwa wanafanya makubwa.
Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, nahodha wa  timu hiyo, Juma Kaseja alimshukuru Rais Kikwete na kuahidi kuhamasishana kujituma kwenye mazoezi na hatimaye kutimiza ndoto za Watanzania.
Taifa Stars iko Kundi C la kufuzu kwa Kombe la Dunia 2014, ikiwa na pointi 6, moja nyuma ya vinara, Ivory Coast. Morocco ni ya tatu kwenye msimamo wa kundi hilo ikiwa na pointi mbili na Gambia inaburuta mkia ikiwa na pointi moja.

Yanga kujipima kwa Rayon kabla ya kwenda Darfur kutetea Kagame


Kikosi cha Yanga
MABINGWA watetezi wa mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), Yanga wanatarajia kucheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Rwanda, Rayon kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza mwezi ujao.
Akizungumza jana, Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako, alisema kuwa wamepokea barua ya mwaliko huo kutoka kwa mratibu wa mechi hiyo lakini bado hawajathibitisha hadi kocha Mholanzi Ernie Brandts atakapotoa maelekezo.
Mwalusako alisema kwamba mechi hiyo wakiipata itakuwa ni nzuri kwa kuwaandaa wachezaji kuelekea Sudan na vile vile ni nafasi kwa Yanga kuwapa heshima mashabiki wake wa kanda ya ziwa kuiona timu baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Bara.
"Ni kweli taarifa za mechi hiyo tunayo, lakini majibu rasmi hatutawapa na siku ya mchezo pia haijapangwa ila wamependekeza iwe mapema mwezi ujao," alisema Mwalusako.
Naye mmoja wa viongozi wa Rayon, Clever Kazungu, alithibitisha timu yake kupokea mwaliko huo na kusema kwamba wako tayari kuja nchini endapo watafikia makubaliano na waandaaji wa mchezo.
Kazungu alisema tayari wameambiwa kuwa watalipiwa gharama ya malazi, chakula na posho ya wachezaji kwa siku watakazokuwa hapa nchini.
Yanga itaanza kampeni za kutetea ubingwa wa Kombe la Kagame kwa kuivaa Express ya Uganda katika mechi ya kundi C itakayofanyika Juni 20 kwenye Uwanja wa Elfasher saa nane mchana wakati Simba iliyopangwa kundi A itashuka dimbani siku inayofuata kuivaa El Mereikh.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Bara watashuka tena dimbani Juni 22 mwaka huu kuikabili Ports na watakamilisha mechi za hatua ya makundi Juni 25 kwa kuvaana na Vital'O.
Simba watashuka tena kusaka ubingwa wa michuano hiyo Juni 23 kwa kupambana na APR na watamaliza dhidi ya Elman Juni 26.
Yanga pia huenda ikawavaa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Zanzibar, KMKM, katika mechi nyingine ya kirafiki inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Thursday, May 23, 2013

Shinji Kagawa aipa taji Borussia Dortmund

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6qnMGGtEdfljwGsrw8rCwj7Az3DybB28VZLR1sfi1mmYGfENc0OAMvIk91kA-UOfpfSkxBVypEs7biZVLGjf9QjGPv1VGFTXYprResinbb3klLzzYOUfYrXyXIVyyW2YP87McxG1lYi4/s1600/Shinji+Kagawa+wallpapers.jpeg
Shinji Kagawa katika uzi wa Manchester United

 

http://ballsybanter.com/wp-content/uploads/2012/06/Cologne-v-Borussia-Dortmund-Shinji-Kagawa-cel_2739644.jpg
Shinji Kagawa alipokuwa akiichezea Borussia Dortmund

 

KIUNGO wa kijapani anayeichezea Manchester United, Shinji Kagawa ametoa turufu yake kwa klabu yake ya zamani Borussia Dortmund kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya katika fainali itakayochezwa Jumamosi nchini Uingereza.

Kagawa aliyetua Manchester United msimu uliopita akitokea Dortmund kwa dau la Pauni Milioni 12, alisema anadhani Borussia wataifunga Bayern Munich kwenye fainali za michuano hiyo itakayochezwa katika uwanja wa Wembley.

Pia mchezaji huyo alisema mafanikio iliyopata Dortmund msimu huu kwenye michuano hiyo ya Ulaya licha ya kupoteza ubingwa wa ligi ya Ujerumani, itawachochea Man Utd kufanya vyema kwa msimu ujao wa Ligi hiyo ya Mabingwa Ulaya.

Pamoja na kupoteza taji la nyumbani Dortmund wamekuwa na mafanikio makubwa katika michuano hiyo ya Ulaya licha ya wali kutopewa nafasi kubwa kama klabu nyingine zilizong'olewa au kama ilivyo kwa mahasimu wao Bayern Munich.

Kagawa aliyecheza kwa mafanikio makubwa katika klabu hiyo ya Ujerumani, alisema Dortmund inacheza kwa kujituma na ina wachezaji ambao wanajua wajibu wao uwanjani, licha ya kuimwagia sifa pia Bayern akidai ni timu kubwa na yenye bahati katika soka.