STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 6, 2013

Mussa Mgosi atua Mtibwa Sugar kumrithi Javu

Mussa Hassain Mgosi
MSHAMBULIAJI wa zamani wa klabu ya Simba Mussa Hassan Mgosi amejiunga rasmi na klabu ya Mtibwa Sugar ya Manungu Morogoro.

Mgosi ambaye msimu uliopita alikuwa akiitumikia klabu ya JKT Ruvu amejiunga na Mtibwa kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Akiongea na mtandao huu, kocha wa Mtibwa Sugar  Mecky Mexime amethibitisha kwamba klabu yake imemsajili mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba.
 
"Mgosi anakidhi vigezo vya mshambuliaji tunayemhitaji baada ya kuondoka wa Javu aliyejiunga na Yanga. Ameshaini mkataba wa mwaka mmoja na atajiunga na kambi ya maandalizi ya msimu mpya hivi karibuni."
 
Shafih Dauda

Kumekucha Tamasha la Idd Mosi Dar Live


Meneja wa Matukio wa Dar Live, Abdallah Mrisho (wa pili kulia) akiongea na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu burudani mbalimbali zitakazokuwepo Dar Live sikukuu ya Idd Mosi.
WASANII wa muziki watakaopanda katika jukwaa la kisasa la Dar Live sikukuu ya Idd Mosi pamoja na mabondia leo wamelonga na wanahabari kwenye mkutano uliowakutanisha ambao umefanyika katika hoteli ya Atriums iliyopo Sinza Afrikasana jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo wasanii wametambiana kila mmoja akitamba kuwa atamfunika mwenzake. Vilevile mabondia nao wametunishiana misuli hali inayoonyesha kuwa kutakuwa na bonge la burudani katika sikukuu hiyo ya Idd Mosi.
Katika sikukuu hiyo wasanii Ali Kiba, H-Baba, Chegge, Temba, Dogo Aslay, Bi. Cheka na Bendi ya Mapacha Watatu watashusha bonge la burudani na kuwapa raha mashabiki watakaohudhuria shoo hiyo. Kwa Upande wa masumbwi bondia Francis Miyeyusho atazipiga na Darius Lupupa kutoka nchini Zambia, Chupaki Chipindi atapigana na Ramadhan Kido. Vilevile mabondia wa kike Ester Kimbe na Irene Kimaro wataonyeshana moto siku hiyo.
(PICHA: SHAKOOR JONGO /GPL)
Mwanamuziki H – Baba akitamba mbele ya wanahabari (hawapo pichani) kuwa atafunika mbovu siku hiyo.

Mratibu wa mapambano ya ndondi, Abdallah Yasin ‘Ustaadh’ (kulia) akiongea na wanahabari. Kushoto ni Abdallah Mrisho.

Mwanamuziki Ali Kiba (kulia) akipeana ‘hi’ na Ustaadh wakati wa mkutano huo.
Bondia Francis Miyeyusho akitunisha misuli. Bondia huyu atapigana na Mzambia Darius Lupupa.

Bondia Chupaki Chipindi atakayezipiga na Ramadhan Kido.
Ramadhan Kido atakayepambana na Chupaki Chipindi siku hiyo.
Mabondia wa kike Ester Kimbe (kushoto) na Irene Kimaro wakijaribu kuzipiga.

Mabondia Francis Miyeyusho (kulia) na Ramadhan Kido (kushoto) wakifuatilia mkutano huo.
Chupaki Chipindi kutoka mkoani Iringa akiwa kwenye pozi.

Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano huo.
Bondia Ester katika pozi.
Bondia Irene naye akiwa kwenye picha ya pozi.
H – Baba katika pozi la kusimama.
Ester ndani ya gloves.

Rufaa 84 zakatwa Baraza la Ushidani

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2013/08/IMG_1843.jpg
Na Suleiman Msuya
KWA kipindi cha zaidi ya miaka sita tangu kuanzishwa kwa Baraza la Ushindani (FCT) jumla ya rufaa 84 zimesajiliwa 36 zimesikilizwa na kutolewa uamuzi na jopo la wajumbe waa Baraza hilo.
Hayo yamebainishwa Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uchumi wa FCT Nzinyangwa Mchany wakati akijibu swali la mwandishi wqa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
Alisema katika rufaa hizo 29 zilisitishwa kutokana na wahusika kuamua kuziondoa baada ya kufikia maamuzi ambayo baraza hilo halina mamlaka yakuingilia ambapo kwa sasa rufaa zinazoendelea kusikilizwa ni 19.
Mchany alisema Baraza la Ushindani limejipangia kusikiliza rufaa 24 kwa mwaka iwapo zitakuwepo lakini bado mwitikio ni mdogo hali ambayo inatajwa kuwa inachangiwa na uelewa mdogo kutoka katika jamii juu ya FCT.
“Baraza la Ushindani FCT limeanza kazi rasmi mwaka 2007 ambapo huwa tunapokea rufaa kutoka katika kwa watu na taasisi mbalimbali ambazo zinakuwa hazijaridhika na maamuzi ambayo yanatolewa na  mamlaka za udhibiti hapa nchini,” alisema.
Kwa upande wake Mwanasheria Mwandamizi Hafsa Said  alisema pamoja na mafanikio hayo madogo ambayo wameweza kuyapata tangu kuanza kwa FCT bado wana changamoto chache ambazo zinawakabili.
Alizitaja baadhi ya changamoto kuwa ni uchache wa majaji wa kusikiliza rufaa ambapo wamekuwa wakifanya kazi kwa muda maalumu (party time) kutokana na ukweli kuwa ni watumishi wa Mahakama ya Kuu nay a Rufaa.
Said alitaja changamoto nyingine ni ufahamu mdogo kwa jamii juu ya FCT ambapo wanajipanga kwa kushirikiana na mamlaka za udhibiti kutoa elimu hiyo ili wananchi na jamii kwa ujumla kutopoteza haki zao pale wanapoona kuna dalili za kuzikosa.
Pia alisema pamoja na changamoto hizo kupitia maamuzi yao wanayotoa ubora wa mamlaka za udhibiti umeongezeka jambo ambalo linaleta tija kwa jamii.
Alisema tangu waanze kupokea rufaa zinazotoka kwa taasisi na watu binafsi asilimia kubwa ya maamuzi yamekubalika ambapo ni maamuzi mawili tu ndio yaliendelea katika ngazi zingine za kimaamuzi.
Mwanasheria huyo Mwandamizi alitoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali ambazo zinasimamiwa na mamlaka kama TCRA, SUMATRA, EWURA, FCC na TCAA kujitokeza kukata rufaa iwapo watakuwa hawajaridhika na maamuzi yao.

MSD yatataka uwekezaji zaidi sekta ya dawa

BOHARI ya Dawa nchini (MSD) imetoa rai kwa wawekezaji kuwekeza katika sekta ya viwanda vya kuzalisha dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara ili kuhakikischa kuwa nchi inapiga hatua kiuchumi.
Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MSD Isaya Mzoro wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Alisema kutokana na ukweli kuwa asilimia 80 ya dawa, asilimia 95 ya vifaa tiba na vitendanishi vya maabara asilimia 100 huagizwa kutoka nje hali ambayo inachangia fedha nyingi kufaidisha nchi zingine.
Mzoro alisema ni vema wawekezaji wan je na ndani wakajitokeza kuwekeza katika viwanda ambavyo vitajihusisha na uzalishaji wa mahitaji yote ambayo yanahusu afya ya binadamu hapa nchini.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema kabla ya kuanzishwa MSD hapa nchini kulikuwa na viwanda vya kutengeneza dawa zaidi ya saba lakini hadi sasa ni viwanda viwili ambavyo vinafanyan kazi hivyo kusababisha Serikali kuagiza dawa kutoka nje.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwaomba watu kutoka nje au ndani ya nchi kuwekeza katika sekta hii ya uzalishaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwani ni fedha nyingi ambazo zinaenda nje kwa lengo hilo,” alisema.
Aidha alisema pamoja na changamoto hiyo kubwa ya ukosefu wa viwanda MSD imefanikiwa kufikisha huduma za ununuzi, uhifadhi na usambazaji wa huduma zao kwa asilimia 75 jambo ambalo linawapa matumaini kwa siku za karibuni.
Mzoro alisema MSD kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali ina mpango wa kupanua maghala kwa kukamilisha ujenzi wa awamu ya pili ili kuongeza nafasi za kuhifadhi dawa na vifaa tiba.
Alisema MSD inatumia mfumo wa EPICOR 9 tangu mwezi Agosti 2012 ambapo wanatoa mafunzo endelevu kwa watumishi wao ili waweze kutoa huduma kwa haraka na kwa ufanisi.
Kwa upande mwingine Kaimu Mkurugenzi huyo alisema MSD inakabiliwa na changamoto nyingi kama ongezeko kubwa la mahitaji ya dawa ukilinganisha na uwezo serekali, ucheleweshaji wa kufikishwa pesa MSD kutoka hazina, Halmashauri kutotumia vyanzo vingine vya fedha, uhaba wa viwanda vya dawa nchini.
Changamoto nyingine taratibu za ununuzi kuchukua muda mrefu na baadhi ya zahanati na vituo vya afya kutopeleka maombi ya dawa na vifaa tiba katika kanda za MSD kama utaratibu unavyohitaji.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema matarajio yao ni kushirikisha sekta binafsi katika kusambaza dawa na vifaa tiba, kubandika orodha ya dawa na vifaa tiba vilivyokabidhiwa vituoni, kuendelea kuweka nembo ya serikali kwenye vidonge, kushirikisha sekta binafsi katika kutoa huduma ya dawa na vifaa tiba na waganga kuwasilisha maombi mapema.

Shilole kukomaa na jiji videoni hivi karibuni

Zuwena Mohammed 'Shilole'
MUIGIZAJI nyota wa filamu anayejishughulisha pia na muziki, Zuwena Mohammed 'Shilole' yupo mbioni kuachia video ya wimbo wake unaoendelea kutamba wa 'Nakomaa na Jiji'.
Akizungumza na MICHARAZO leo, Shilole alisema video hiyo iliyorekodiwa nchini Marekani alipoenda ziarani hivi karibuni kwa sasa inahaririwa kabla ya kuachiwa hewani mashabiki waone namna anavyokomaa na jiji.
Shilole alisema tofauti na nyimbo za nyuma kama 'Lawama', ' Dada Dume', 'Dudu' au 'Paka la Baa' ambazo zipo katika miondoko ya 'Chakacha' safari hii ametoka kivingine katika Bongofleva kuonyesha uwezo alionao katika fani hiyo ya muziki.
"Wakati wimbo wangu wa 'Nakomaa na Jiji' ukiendelea kuwa gumzo kwa sasa, nakamilisha mipango ya kuachia video yake hivi karibuni ili kuwapa raha mashabiki wangu," alisema Shilole.
Mkali huyo, alisema video hiyo aliipiga katika jiji la New York alipoenda Marekani na kwamba kila kitu kimekamilisha kwa ajili ya kuhakikisha anaiachia mapema iwezekanavyo.
Pia alisema kutoka hadharani kwa video ya 'Nakomaa na Jiji' itakuwa fursa yake nyingine ya kujiandaa kutoa kazi nyingine katika mtindo wa 'bandika bandua'  ili kuwapa raha mashabiki wake.
Shilole alisema ana hazina kubwa ya muziki katika stoo yake na ndiyo maana kila mara anawaangushia mashabiki wake nyimbo mpya kali kama alivyofanya katika kazi zilizopita ambapo kabla ya 'Nakomaa na Jiji' alikuwa gumzo na wimbo wa 'Paka wa Baa'.

Side Boy Usimdharau Usiyemjua

Msanii Side Boy katika pozi
MSANII wa miondoko ya Bongofleva anayejishughulisha na ujasiriamali, Said Salim 'Side Boy Mnyamwezi', anayetamba na wimbo wa 'Hujafa Hujaumbika' yupo mbioni kuachia kazi mpya iitwayo 'Usimdharau Usiyemjua'.
Akizungumza na MICHARAZO, Side Boy alisema wimbo huo aliorekodi katika studio za Pamoja Records, ni utangiulizi wa nyimbo za albamu yake ya tatu anayotarajia kuitoa hivi karibuni.
Side Boy aliyewahi kutamba na nyimbo kama 'Kua Uone', 'Jifungue Salama' na 'Pongezi wa Kikwete', alisema wimbo huo mpya ameuimba peke yake yake tofauti na kazi yake iliyopita ya Hujafa Hujaumbika alioimba na wasanii Best Naso na Aunty Ezekiel 'Gwantwa'.
"Baada ya kutamba na 'Hujafa Hujaumbika' kwa sasa najiandaa kuachia wimbo wa 'Usimdharau Usiyemjua' ambao nimeimba pekee yangu na ni utambulisho wa albamu yangu ya tatu inayokuja," alisema.
Side Boy alisema albamu hiyo ijayo inayofuata baada ya zile za 'Kua Uone' na 'Acha Waseme' itatoka ikiwa na cd mbili kwa moja ikijumuisha video na audio, ili kuwapa raha mashabiki wake na wale wa muziki wa ujumla.
"Albamu yangu ijayo ambayo bado sijaipa jina itatoka ikiwa na CD mbili,. moja video na nyingine au audio ili mashabiki wasisumbuke," alisema.,
Msanii huyo aliyewahi kufanya kazi pamoja na kundi la TMK Wanaume Family, japo hakuwa 'membaz' wa kundi hilo, alisema mashabiki wake wajiandae kupata ladha mpya toka kwake kutokana na albamu hiyo ya tatu anavyoiandaa kwa sasa itakayokuw ana nyimbo nane.

Kibudu cha Msechu kuandaliwa Kenya

Peter Msechu
 Na Elizabeth John

HATIMAYE ngoma inayokwenda kwa jina la ‘Kibudu’ liyoimbwa na mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Peter Msechu, imeanza kutamba katika vituo mbalimbali vya redio kutokana na ujumbe wa mashairi yaliyomo ndani yake.

Mbali ya kutamba na kibao hicho, mkali huyo alishawahi kutamba na kibao chake cha ‘Relax’, ‘Kumbe’ ambavyo vilifanya vizuri zaidi mbali na kuwa na vibao vingi ambavyo vilimtambulisha katika tasnia ya muziki huo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Msechu alisema katika kazi hiyo kamshirikisha mkali wa muziki huo, Ally Nipishe na kwamba tayari imeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Alisema kibao hicho kakitengeneza katika studio ya Ufundi Production chini ya mtayarishaji wake mahiri, Fundi Samuel.
“Naomba mashabiki wangu wakipokee vizuri kibao hicho ambacho natarajia kukifanyia video yake Nairobi, Kenya,” alisema.

Msechu aliwataka mashabiki wake wakae mkao wa kula kwa ajili ya video hiyo ambayo anatarajia kuitoa mwinzoni mwa mwezi ujao ikiwa ni pamoja na nyimbo nyingine nyingi zinazofuata.

Awamu ya kwanza usajili wa wachezaji wakamilika



Na Boniface Wambura
HATUA ya kwanza ya usajili wa wachezaji kwa msimu wa 2013/2014 imefungwa rasmi jana (Agosti 5 mwaka huu) ambapo klabu zote za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zimewasilisha usajili wa vikosi vyao ndani ya wakati.

Baadhi ya klabu zimefanya makosa madogo madogo katika usajili ambapo zimepewa siku ya leo (Agosti 6 mwaka huu) kufanyia marekebisho kasoro hizo. 

Hivyo kesho (Agosti 7 mwaka huu) majina ya vikosi vyote yatabandikwa kwenye mbao za matangazo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa ajili ya kipindi cha pingamizi kitakachomalizika Agosti 12 mwaka huu.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa itakutana Agosti 13 na 14 mwaka huu kupitia na kufanyia uamuzi usajili wa wachezaji wenye matatizo.

Hatua ya pili ya usajili itaanza tena Agosti 14 mwaka huu ikihusisha wachezaji ambao watakuwa hawajasajiliwa katika Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu na wale kutoka nje ya Tanzania. 

Hivyo, dirisha la uhamisho kwa wachezaji wa kimataifa litafungwa baada ya hatua ya pili ya usajili kumalizika Agosti 29 mwaka huu.

TFF yaridhia 3 Pillars ya Nigeria kucheza Bongo



Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetoa baraka zote kwa timu ya 3Pillars Football Club ya Nigeria kucheza mechi za kirafiki nchini baada ya kupata idhini ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la Nigeria (NFF).

Awali tuliikatalia timu hiyo kucheza mechi za kirafiki nchini kwa vile haikuwa na barua kutoka NFF, lakini sasa Shirikisho hilo limetoa idhini hiyo. Pia ziara yake haikuwa inaratibiwa na wakala wa mechi anayetambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) au mwanachama wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Klabu hiyo kutoka Jimbo la Lagos ilipanga ziara hiyo kwa kuwasiliana na chama cha mpira wa miguu cha jimbo hilo ambacho nacho kilitakiwa kuomba idhini NFF kwa niaba ya 3Pillars.

Hivyo timu hiyo inaweza kucheza mechi, kwani ziara hiyo sasa inaratibiwa na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) ambaye ni mwanachama wetu.

Tunapenda kukumbusha kuwa watu pekee wanaotakiwa kuandaa mechi za kirafiki za kimataifa ni mawakala wa mechi wanaotambuliwa na FIFA au wanachama wa TFF.

Monday, August 5, 2013

Njemba yanusurika kufa kisa ujambazi

Jambazi likiwa hoi baada ya kichapo kutoka kwa wanachi.
Jambazi hilo likihojiwa.
Mmoja wa wanausalama (mwenye tisheti yenye mistari) akiwa na bastola aliyokutwa nayo jambazi huyo.
Wananchi wakiwa eneo hilo la tukio.
Wanausalama wakishauriana jambo kabla ya kulipiga pingu jambazi na kulipeleka hospitali.
Baada ya kichapo kikali jambazi lilipelekwa katika hospitali ya Mwananyamala kwa matibabu.

GPL

Chimwemwe atua Dara na kutamba kumnyuka Cheka

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Best Man Promotion, Zumo Makame (katikati) akiwatambulisha mabondia wawili kutoka Malawi,  Chiotcha Chimwemwe (kulia) na Bgright Mdoka (kushoto) kwa waandishi wa habari tayari kwa mapambano yao ya Agosti 10. Cimwemwe  atapambana na Cheka wakati Mdoka atazipiga na Jitu Samia. Mwingine katika picha ni promota wa Chimwemwe, Steven Msiska. (Na Mpiga Picha Wetu)

Na Mwandishi Wetu
BONDIA nyota wa ngumi za kulipwa wa Malawi, Chimwemwe Chiotcha amewasili nchini na kutamba atamtwanga bondia alisyekuwa na mpinzani Tanzania, Francis “SMG” Cheka katika pambano lao la uzito wa super-middle lililopangwa kufanyika Jumamosi kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Chimwemwe ambaye hajawahi kupoteza pambano nchini Malawi zaidi ya kupigwa kwa pointi na Cheka Desemba 27 mwaka jana, alisema kuwa amekuja kulipiza kisasi huku akiponda matokeo ya awali kuwa Cheka alibebwa sana.
Alisema kuwa hajui ni ushindi wa aina gani atakaoupata kwa bondia huyo, kwani Knock Out (KO) au Technical Knock Out (TKO) utokea ulingoni tu na wala si ushindi wa kupangilia. “Nimekuja hapa kushinda na wala si vinginevyo, nakuja Cheka amejiandaa sana, sikuridhika na matokeo ya awali na ndiyo maana nimeamua kuja kurudiana naye, najua nitaibuka na ushindi,” alisema Chimwemwe.
Alifafanua kuwa si kweli kuwa kila bondia aliyepigana na Cheka na kushindwa kuwa hajui ngumi za kulipwa zaidi ya hofu tu kutoka kwa mabondia hao. Mimi nimedhamilia kufanya kweli na ninajua nitashinda, hii ni fursa yangu,” alisema Chimwemwe ambaye ni mwanajeshi wa Jeshi la Malawi.
Mkurugenzi wa kampuni ya Best Man Promotion inayoaandaa pambano hilo, Zumo Makame alisema kuwa maandalizi ya pambano yamekamilika na siku hiyo kutakuwa na mapambano makali nay a kusisimua.
Makame aliyataja mapambano hayo kuwa, Deo Njiku atawania ubingwa wa Taifa wa Shirikisho la Masumbwi la PST dhidi ya Cosmas Cheka, Rashid “Snake Man” Matumla atazichana na Maneno “Mtambo wa gongo “ Oswald na bondia mwingine kutoka Malawi, Bright Mdoka atazipiga na Jitu Samia.
Mapambano mwngine kwa mujibu wa Makame ni Nasibu Mkude atapigana na Juma Kihiyo katika uzito wa super welter bout, Juma Afande v Epson (featherweight) na  Karim Mandonga dhidi ya Ramadhan Agogo katika uzito wa superwelter.

Mjumbe CCM, awapasha wajumbe Tume ya Katiba

Mjumbe wa CCM, Evod Mmanda
MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (MNEC) Evod Mmanda amewataka Wajumbe wa Tume ya Katiba kuacha kufanya kazi ya kujibu mapungufu yaliyopo katika rasimu hiyo kwani huu ni wakati wa Mabaraza kufanya kazi ya kurekebisha na kupendekeza.
Mmanda alitoa kauli hii wakati akiongea na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam ambapo alisema ameshuhudia baadhi ya wajumbe wa Tume wakitoa maelekezo kwa wajumbe wa mabaraza jinsi ya kutoa maoni.
Alisema ni vema Tume hiyo ikatambua kuwa wakati wao wa kuandaa rasimu umepita na sasa ni wakati wa kuyapa fursa mabaraza kutokana sheria inavyotaka jambo ambalo ni muhimu kuheshimiwa.
Mjumbe huyo wa Mkuatano Mkuu alisema CCM wanaamini kuwa fursa zikipatikana upo uwezekano wa kupatikana na kwa katiba ambayo itakuwa na maslahi na Taifa hivyo kuingilia maoni ya watu ni kinyume na katiba inavyotaka.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwaasa wajumbe wa Tume ya Katiba kuwa wakati huu ni wakuwaachia wajumbe wa mabaraza kutoa maoni na mapendekezo yao hivyo kukaa na kujibu hoja hizo wakati wanatakiwa kusubiri ni kwenda kinyume na sheria inayowaongoza,: “ alisema.
Mmanda alisema iwapo wajumbe watatumia nafasi elekezi kuwashawishi wajumbe wa mabaraza kukubaliana na mapendekezo yao ni dhahiri kuwa kutakuwepo na katiba ambayo ina mitazamo ya watu wachache.
Alisema kuna mapungufu mengi ambayo yameonekana katika rasimu hiyo hivyo ni wakati muafaka kwa jamii na vijana kwa ujumla kutumi nafasi zao kutoa maoni ambayo yataweza kusaidia kizazi cha leo na kijacho.
Mjumbe huyo ambaye alionyesha dhahiri kutokuunga mkono wa uwepo wa Serikali tatu aliishutumu tume kwa kuweka maoni hayo kwa kile alichodai kuwa haikuwa sehemu ya muuongozo wao kufanya.
Aliweka bayana kuwa yeye ni muumini mkuwa wa serikali mbili hivyo hakuona sababu ya kuwepo mapendekezo juu ya aina ya muungano na kuwataka wachangiaji kupitia nafasi mbalimbali kuwa makini kwa maslahi ya Taifa.
Mmanda alitoa rai kwa vijana wa CCM kuwa watumie nafasi yao kuhakikisha kuwa katiba ijayo inakuwa na maboresho yesnye tija na kuacha tabia ya kuwa katika mitazamo ya watu amabao wanaweza kuwa na maslahi yakiuongozi.

Umeme Majanga! Mabwawa yote ya kuzalisha umeme yakauka

Prof.  Muhongo
Na Suleiman Msuya
WAZIRI wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amesema takwimu zinonyesha kuwa kwa sasa hamna bwawa lolote la maji ya kuzalisha umeme ambalo lenye maji ya kutosha ya kuzalisha umeme wa kutosha hapa nchini.
Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam wakati akijibu swali la mwandishi habari hii aliyetaka kujua ni kwanini Serikali haikutaka kutumia Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) ili kuzalisha umeme pamoja na kwamba tafiti zinaonyesha kuwa lingeweza kuzalisha umeme wa zaidi ya megawati 3500 iwapo kungekuwepo na uwekezaji.
Profesa Muhongo alisema upo uwezekano wa tafiti kuonyesha hivyo ila kwa sasa serikali ipo katika harakati za kuleta umeme ambao utaweza kumfikia kila Mtanzania kwa gharama ndogo bila tatizo lolote.
Alisema serikali iliwataka RUBADA kutoa taarifa za uhakika kuhusu uwepo wa maji ya uhakika ambayo hayataweza kupungu jambo ambalo halijafanyika hadi sasa hivyo wao kama wasimamia sera mikakati yao ni kuhakikisha kuwa wanatatua matatizo makubwa ya umeme yaliyopo.
“Mimi kila siku napokea taarifa kutoka kwa wasaidizi wangu na wanasema hakuna bwawa hata moja ambalo lina maji ya kutosha ya kuzalisha umeme hivyo kwa sasa ni vema jamii ikajua kuwa sisi tunajikita katika vyanzo ambavyo havina changamoto,” alisema.
Waziri huyo alisema wao kama serikali wamejikita katika uwekezaji wa uzalishaji wa umeme wa gesi, jua, makaa ya mawe na vyanzo vingine ambavyo ni vizuri na rahisi katika uzalishaji wa umeme.
Alisema iwapo mvua zitanyesha wanaweza kufikiria vyanzo hivyo kama njia ya kutatua tatizo ila kwa sasa macho na nguvu zao zipo katika vyanzo hivyo ambavyo amevitaja kwani havina gharama kubwa ya uzalishaji.
Profesa Muhongo alisema mikakati ya Serikali ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2015 kunakuwepo zaidi ya uniti 2000 za umeme ambazo zinazalishwa hapa nchini hali ambayo itachangia kukuza uchumi.
Aidha akizungumzia maamuzi ya kuleta gesi mkoani Dar es Salaam kutoka mtwara alisema hilo ni jambo ambalo halina mjadala kwani Dar es Salaam ndipo mahali penye chanagamoto nyingi za umeme pamoja na uzalishaji mkubwa wa bidhaa mbalimbali.
Muhongo alisema suala la kwanini usambazaji usianze katika mikoa ambayo bado haijapata huduma ya umeme wa uhakika alibainisha kuwa lengo la Serikali ni kufikisha huduma hiyo kwa jamii yote bila ubaguzi ila kwa sasa watafikisha Dar es Salaam na maeneo mengine yatafuata.

Sheria bila Sera 'miyeyusho' mitupu kwa maendeleo ya jamii


Na Suleiman Msuya
KITENDO cha kuwepo kwa sheria bila sera kimetajwa kama moja ya chanzo cha kukwamisha na kudididimiza jitihada za kuleta maendeleo kwenye jamii hapa nchini.
Hayo yamebainishwa na Dk. Frateline Kashaga wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
Alisema kumekuwepo kwa utaratibu wa kuwepo kwa sheria bila sera jambo ambalo ukiliangalia kiundani ndicho chanzo kikubwa kinachokwamisha juhudi za kupigania maendeleo hapa nchini kwa utekelezaji haupo.
Dk. Kashaga ambaye pia ni Mwahadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu Cha  Dar es Salaam tawi la (DUCE) alisema ni vema amichakato hiyo ikaenda kwa pamoja ili iweze kuleta tija kwa Taifa.
“Nimekuwa nikifuatilia mara kwa mara sheria zetu ambazo zinaundwa nimegundua mapungufu mengi ambapo kubwa zaidi ni ukosefu wa sera kwa wakati huku sheria ikiwepo kwa muda mrefu jambo ambalo linanishangaza,” alisema.
Mwahadhiri huyo Mwandamizi alisema huu ni wakati muafaka kwa jamii ya wanataaluma kutafakari kwa kina juu ya changamoto hiyo na kuja na mapendekezo ambayo yatakuwa na manufaa kwa nchi.
Alisema ni muhimu kwa Taifa likahakikisha kuwa kunakuwepo kwa sera sahihi ambazo zitafaidisha jamii kwani kutokana na takwimu kunaonyesha nchi zilizoendfelea ndizo zinafaidika kwa rasilimali za nchi.
Dk. Alisema zaidi ya dola bilioni 150 zinapotea kutoka bara la Afrika takribani kila mwaka katika mazingira ambayo hayakubaliki hali ambayo inaonyesha dhahiri kuwa ni ukosefu wa sera sahihi za kusimamia rasilimali za nchi.
Kashaga alisema ni vema Tanzania na Afrika kwa ujumla wakatengeneza sera za kimkakati ambazo zitaweza kufanya mataifa yao kufaidika na rasilimali zilizopo kwa kipindi kirefu.
Aidha mmoja wa changiaji aliweka bayana kuwa uvutiaji wa wawekezaji katika bara la Afrika takwimu zinaonyesha kuwa bara la Afrika linaingiza dola bilioni 130 kwa mwaka kutoka nje ambapo lenyewe linapeleka zaidi ya dola trilioni mbili uwioano ambao sio sahihi.

Makamba awataka vijana kuwania nafasi za uongozi


Mhe. January Makamba

Na Suleiman Msuya
MLEZI wa Shirikisho la Vijana wa Vyuo Vikuu wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia January Makamba amewataka vijana nchini kujitokeza na kushiriki katika nafasi mbalimbali za uongozi kuanzia ngazi za mitaa hadi Taifa.
Makamba aliyasema hayo Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wanafunzi wa vyuo vikuu katika kongamano la kujadili rasimu ya Katiba ambayo kwa sasa ipo kwenye mchakato wa mabaraza.
Alisema vijina wanapaswa kutambua kuwa ufumbuzi wa mahitaji yao yao ni pamoja na wao kushiriki moja kwa moja katika kugombea nafasi za uongozi ambazo zinapatikana na kuacha tabia ya kulalamika.
Naibu Waziri alisema ili Taifa liweze kupiga hatua ni dhahiri kuwa mchango wa vijana hasa wasomi unahitajika kwani ndio chachu ya kuleta maendeleo katika nchi na wananchi kwa ujumla.
“Kimsingi vijana wa Tanzania wamekuwa walalamikaji bila kuwajibika ila napenda kuwapa usia huu kuwa njia ya kukomboa Taifa ni sisi kushiriki katika nafasi mbalimbali za uongozi na kiutumishi ili tuwe sehemu ya maendeleo,” alisema.
Mlezi huyo alitolea mfano wa Nabii Musa wakati alipoulizwa na Mungu mkononi ameshikilia nini ambapo alimjibu fimbo na kumtaka aiweke chini fimbo hiyo ambayo ilibadilika kuwa nyoka na baadae ilibadilika kuwa fimbo tenda hivyo taaluma zao ziwe ni fimbo kwa kusaidia maendeleo ya Taifa.
Alisema fursa zilizopo nchini zinahitaji vijana kushiriki kikamilifu ili ziweze kuwa na tija kwani kuendelea kusubiri kutachangia nchi kupoteza rasilimali nyingi ambazo zipo.
Naibu Waziri alisema iwapo vijana watakuwa washiriki katika uongozi ni dhahiri kuwa viongozi sahihi wenye uzalendo na uadilifu wanaweza kupatikana bila kuwepo kwa lawama za ufisadi na kashfa nyingine nyingi ambazo zimekuwa zikiibuliwa.
Akizungumzia juu ya kongamano hilo alisema CCM imejipanga kikamilifu ili kuhakikisha kuwa vijana wanashiriki katika majadiliano yoyote ambayo yanahusu Taifa kwa lengo kuu kwamba wao ndio wasimamizi wa rasilimali za nchi.
Makamba alisema vijana wanapaswa kutumia fursa hiyo kuwasilisha hoja ambazo zitasaidia nchi na kuachana na tabia ya kulalamika mara kwa mara bila kuja na suluhisho

Azam yaanza vibaya Sauzi, yapigwa 3-0

Na Bin Zubeiry
AZAM FC imeanza vibaya ziara yake ya mechi za kujipima nguvu mjini hapa, baada ya kufungwa mabao 3-0 na wenyeji, Kaizer Chiefs katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa mazoezi wa wa timu hiyo, eneo la Nachurena.
Azam iliyoondoka nchini jana mchana kwa ndege ya Shirika la Afrika Kusini, kuja Johannesburg, Afrika Kusini kuweka kambi ya wiki mbili kujiandaa na msimu mpya, katika mchezo wa leo iliathiriwa na uchofu wa safari na hali ya hewa ya baridi, hivyo kucheza chini ya kiwango.
Azam FC

Timu hiyo yenye maskani yake, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, iliyoondoka na kikosi chake kizima, kasoro wachezaji wawili tu majeruhi, kiungo Mkenya, Humphrey Mieno na mshambuliaji Mganda, Brian Umony, imefikia katika hoteli ya Randburg Towers.
Azam jana ilifanya mazoezi yake ya kwanza kwenye Uwanja wa Wits University asubuhi na jioni na Kocha Mkuu wa timu hiyo, Muingereza Stewart Hall amefurahishwa na mazingira ya kambi na Uwanja wa mazoezi.
Baada ya mchezo wa leo, Azam itashuka tena dimbani Agosti 7, kumenyana na Mamelodi Sundowns kabla ya kuivaa Orlando Pirates Agosti 9 na Agosti 12 itamaliza ziara yake kwa kumenyana na Moroka Swallows.
Azam inatarajiwa kurejea nchini Agosti 13 tayari kwa mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii kuashiria kufungua pazia la msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Yanga SC, Agosti 17, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Safari hii Azam, washindi wa pili mara mbili mfululizo wa Ligi Kuu wamepania kutwaa Ngao mbele ya Yanga, baada ya mwaka jana kufungwa na Simba SC na kocha Muingereza Stewart Hall anajiandaa kikamilifu kwa ajili hiyo.   

Azam kuikabili Kaizer Chiefs 'Bondeni'

Wachezaji wa Azam wakiwa katika picha tofauti nchini Afrika Kusini, jioni hii wataumana na Kaizer Chiefs


MAKAMU bingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), Azam wanaanza rasmi ziara ya mechi za kirafiki nchini Afrika Kusini leo kwa kuikabili timu ya Kaiser Chiefs ambayo inacheza Ligi Kuu ya nchi hiyo (PSL).
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Azam, Jaffer Idd aliyefutana na timu hiyo, mechi hiyo inachezwa jijini Johannesburg, likiwa ni pambano la kwanza kati ya manne ambayo Azam itajipima nguvu nchini humo ilipoenda kuweka kambi ya muda kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu inayoanza Agosti 24.
Mechi nyingine ambazo Azam itacheza ni ya keshokutwa dhidi ya Orlando Pirates, Mamelodi Sondowns na Moroka Swallows.

Hatimaye Katiba ya TFF yapita kwa Msajili

Rais wa TFF, Leodger Tenga na katibu wake, Angetile Osiah
Na Boniface Wambura
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amemshukuru Msajili wa Klabu na Vyama vya Michezo nchini kwa kusajili Katiba ya TFF toleo la 2013 kutokana na marekebisho yaliyofanywa na Mkutano Mkuu Maalumu uliofanyika Julai 13 mwaka huu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Dar es Salaam leo (Agosti 5 mwaka huu), Rais Tenga ameishukuru Serikali, Msajili, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, Naibu wake Amos Makala na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kwa ushirikiano ambao wametoa kwa TFF katika kufanikisha suala hilo.

Amesema baada ya kupokea usajili huo, kinachofuata ni Katibu Mkuu wa TFF kumwandikia rasmi Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ili aanzishe mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa TFF.

Kuhusu kauli ya Naibu Waziri Makala kuwa marekebisho hayo yasingeweza kusajiliwa kwa sababu hayakufuata Katiba ya TFF, Rais Tenga amesema alikuwa ana haki ya kusema hivyo kwa sababu hakuwepo kwenye Mkutano huo, na kuongeza:

“Makala hakuwepo kwenye mkutano ndiyo maana alisema hivyo. Ana haki ya kuuliza, nina hakika sasa atakuwa ameeleweshwa na ameelewa kwa sababu ni msikivu. Kuhusu marekebisho hayo kupigiwa kura, hilo lisingewefanyika kwa sababu hakukuwa na mjumbe aliyepinga marekebisho,” amesema.

Rais Tenga amesema marekebisho hayo yalipitishwa kwa kauli moja (unanimous) hivyo hakukuwa na sababu ya kuanza kunyoosha mikono kupiga kura, kwa maana hiyo mkutano ulipitisha marekebisho kwa asilimia 100 wakati Katiba ilikuwa ikihitaji theluthi mbili tu.

“Hakukuwa na dispute (mabishano) kuhusu marekebisho, isipokuwa wajumbe walitumia muda mwingi kuboresha kanuni na kutoa ushauri wa aina ya watu ambao wangeingia kwenye kamati mbalimbali zikiwemo zile mpya za Maadili,” amesema.

Ameongeza kuwa kwa vile wote walioingia kwenye Mkutano Mkuu huo Maalumu ni watu wa mpira wa miguu wasingeweza kupinga marekebisho kwa vile yametokana na maagizo ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

“Labda itokee aliyeingia kwenye mkutano alikosea njia. Mtu yeyote wa mpira wa miguu ni lazima afahamu kuwa maagizo ya FIFA ni lazima yatekelezwe, na Katiba ya TFF inasema hivyo,” amesema Rais Tenga.

Pia Rais Tenga amewataka wapenzi wa mpira wa miguu kushawishi watu wenye sifa na uwezo wa kuongoza kujitokeza kwa wingi wakati Kamati ya Uchaguzi itakapotangaza mchakato na tarehe ya uchaguzi huo.

Huyu ndiye 'Tanzania One' Juma Kaseja

Kipa Juma Kaseja akiwa na Katibu wa kituo cha yatima cha New Life Orphans Home Hamad Kombo walipokitembelea kituo hicho jana ambapo watoto walipagawa naye wakionyesha wanaomfuatilia kupita maelezo.

Ebu niambie wewe msimu huu unaenda wapi? Ashanti au Fc Lupopo? Kaseja akiteta jambo na Mlezi wa klabu ya Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' huku wachezaji wenzake wakisikiliza kwa makini na watoto wakiwa bado wana hamu ya kufurahia naye kama wanvyoonekana kando yake kwa ndani..

Huyo hana lolote anaenda zake Mbeya City? Kaseja akiteta na beki wa zamani wa Yanga na Reli, Yahya Issa huku Ticotico na Faraji wakisikiliza.
Kaseja mkekani na watoto
Akimakinika na watoto ambao baadhi walikuwa wakimshangaa


Kwani hiyo simu inauzwa kiasi gani? Ni kama dogo huyo anamuuliza Kaseja
Watoto wakiwa sambamba na Kaseja

Kaseja akizungumza na watoto waliotaka kupiga naye picha jana kwenye kituo cha kulelea yatima cha New Life Orphans Home
Yaani kila mtoto alitaka kuwa karibu na Kaseja

Kaseja na mlezi wa Golden Bush, Onesmo 'Waziri Ticotico' aliyembeba mtoto katikapicha ya pamoja na watoto.
 
Sheikh huwezi kutoka bila kupiga picha na miye! Katibu wa kituo cha kulelea yatima, Hamad Kombo(kati) akiwa pichani na Kaseja (kushoto)
HUENDA kipa Juma Kaseja ndiye mchezaji anayetambuliwa na kufahamika kirahisi nchini iwe kwa watoto ama hata wanawake ambao mara nyingi huwa siyo wafuatiliaji wa soka.
Mara kadhaa katia mahojiano yangu na wasanii au wanamichezo hasa wa kike wanaoshabikia soka wengi humtaja Kaseja kama mchezaji wanayemjua kwa umahiri wake, wengine huwa ni Mrisho Ngassa, Ally Mustafa 'Barthez', Athuman Idd 'Chuji' na wakati mwingine Emmanuel Okwi japo kwa sasa hayupo nchini.
Kitu gani kinachomfanya Kaseja awe kivutio na gumzo midomoni mwa watu, kama ambavyo ilivyo sasa baada ya kutemwa na Simba? Sina shaka ni umahiri wake dimbani, nidhamu na kule kujiweka chini licha ya usupa staa alionao.
Jana wakati timu ya Golden Bush FC ilipowatembelea yatima wa kituo cha New Life Orphans Home, Kaseja ndiye aliyekuwa gumzo kwa watoto na hata uongozi wa kituo hicho na kuomba kupiga naye picha, huku kipa wa Mbeya City, Aman Simba akifananishwa na Chuji kwa mzuzu aliokuwa nao.
Hata wakati wenzake wakiwa wamekaa kwenye mabenchi na viti, Kaseja alijichanganya na watoto katika mkeka kabla ya baadaye wachezaji wenzake wakati wa kupiga picha ya pamoja na watoto kuungana naye kwenye mkeka.