STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 13, 2014

'HATUITAKI KATIBA MPYA PENDEKEZWA'

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema hakiikubali Katiba inayopendekezwa kwa kuwa haina maslahi ya wananchi wa Zanzibar.
Badala yake chama hicho kimewataka Wazanzibari waikatae Katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba (BMK).
Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa CUF ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja vya Demokrasia vya Kibanda Maiti, mjini Zanzibar.
“Wananchi, Katiba haikubaliki kwa Wazanzibari, mimi mwenzenu siikubali, sijui nyinyi wenzangu?” alihoji Maalim Seif na wananchi kuitikia kuwa nao hawaikubali.
Alisema kuwa miongoni mwa mambo yanayoipokonya Zanzibar hadhi yake ni Katiba inayopendekezwa kumpokonya Rais wa Zanzibar mamlaka ya kugawa mikoa, tofauti na Katiba ya Zanzibar ya sasa. 
Alisema kwa maana hiyo Rais wa Muungano anachukua mamlaka ya Rais wa Zanzibar na anaweza kuteuliwa wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya wa Zanzibar. 
“Kwa mabadiliko hayo ya rasimu ya Chenge, Rais wa Muungano anaweza kututeulia Sheha wa Shehia ya Mtoni Zanzibar kutoka Bukoba,” alisema Maalim Seif huku akishangiliwa na wanachama na wafuasi wa CUF.
Maalim Seif alisema Katiba ya Zanzibar na marekebisho yake ya mwaka 2010 iko sahihi kabisa na inazingatia matakwa ya Makubaliano ya Muungano.
Alisema hayuko tayari kuona rasimu hiyo inakubalika na kwamba Wazanzibari hawataki kuiona.
Alisema hakubaliani na kauli za baadhi ya watu waliosema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) inaridhishwa na mchakato wa Katiba mpya.
“Nataka kuwambia hakuna kikao chochote cha SMZ kilichokaa na kusema tunaijadili rasimu, kama kuna mtu anataka kusema eti Smz imeridhishwa aseme mwenyewe binafsi na siyo Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alisema Maalim Seif.
Maalim Seif aliisifu Rasimu ya Jaji Joseph Warioba ambayo ndiyo ilizingatia matakwa ya Watanzania walio wengi na kwamba pamoja na awali Wazanzibari kupendekeza muundo wa Muungano wa mkataba, lakini kwa busara ya tume hiyo waliikubali muundo wa serikali tatu.
Maalim Seif alisema anahutubia mkutano huo akiwa na furaha kubwa kutokana na umma ulioteremka katika viwanja vya Kibandamaiti, na hiyo ni sababu tosha na ujumbe kuwa hawaitaki Katiba inayopendekezwa.
“Ndugu yangu, rafiki yangu Rais Jakaya Kikwete ufahamu kuwa umma huu uliohudhuria Kibandamaiti ni ujumbe tosha kuwa Katiba hiyo hawaitaki, na mwambia Rais Kikwete kuwa Katiba hii hatuikubali,” alisema Maalim Seif. 
Maalim Seif alisema Katiba bora ni ile inayozingatia maoni ya wananchi. 
“Lakini Rais (Rais Jakaya Kikwete), Katiba yenu mmeweka upande maoni ya wananchi, mmejifungia wenyewe, mmeipitisha wenyewe na mmeichezea ngoma wenyewe”, alisema. 
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui, alisema wajumbe saba wa Bunge Maalum la Katiba waliopiga kura ya Hapana hadharani kukataa rasimu hiyo ni mashujaa wa Zanzibar na Wazanzibari wote wanapaswa kuwapa heshima kubwa.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF, Salum Bimani, alisema wananchi wa Zanzibar wameshaamua na hawatarejea nyuma zaidi ya kuiondoa CCM mwaka 2015 na kuipa Zanzibar mamlaka kamili.
Bimani alisema msiwape kura viongozi wa CCM ambao wanauza nchi ya Zanzibar huku wakicheza ngoma.
“Kwa Shilingi 300,000 watu hawa wanadiriki kuuza nchi, hawa waliopiga kura za ndiyo ni madalali wa Zanzibar, hata wale waliopiga kura za siri pia ni madalali,” alisema Bimani.
Alisema wanasheria wawili wameitetea Zanzibar na wakafikwa na masahiba mazito.
Aliwataka wanasheria hao kuwa Jaji Walfgong Dourado na Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliyefutwa kazi, Masoud Othman Masoud.
Bimani alisema Wazanzibari wapo pamoja nao katika kuhakikisha Zanzibar inabaki na wale wenye nia mbaya wajue kwamba Zanzibar wataitapika watake wasitake. 
Mansour alisema naendelea kuwa muumini wa Maridhiano ya Zanzibar. Katiba hii ni yao wenyewe si ya Wazanzibari.
“Baada ya kuona umma huu uliohudhuria katika mkutano huu tunapaswa kumhofia Mwenyezi Mungu,” alisema.
“Naendelea kumuunga mkono Maalim Seif Sharif Hamad, ni kiongozi asiyekuwa mnafiki anajitambua na hatawaliwi na utawala wa Dodoma, anatawaliwa na Wazanzibari wenyewe na matakwa na matumaini yao,” alisema na kuwataka Wazanzibari wasiwe na hofu kwani hawawezi kufungwa wote wako wengi sana, wakati umefika. 
“Tumeungana kwa hiari yetu, tukakubali kwa hiari yetu, sisi si watumwa wa mtu yoyote, tumefungwa tumefukuzwa makazini kwa sababu ya nchi hii, hatuwezi kurudi nyuma,” alisema.
Alieleza kuwa watu wasishangae kumuona Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano, Mzee Nassoro Moyo, amesimama kwenye jukwa anatetea nchi yake.
Mzee Moyo alisema Wazanzibari hawakubalini kuona watu wanataka kuichukua nchi yao ovyo ovyo.
Mkutano huo ambao ni wa kwanza kuhutubia na Maalim Seif tangu BMK limalize kazi yake na kuwasilisha rasimu kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, ulihudhuriwa na maelefu ya wananchi huku baadhi yao wakibeba mabango.
Baadhi ya mabango hayo yalibeba ujumbe usemao “Wapige mabomu rasimu yao hatuitaki, Hongera Othman Masoud, Katiba ya vijisenti (Chenge) hatuitaki”. 
Katika hatua nyingine, Maalim Seif alikanusha taarifa kwenye mitandao kuwa hatajiuzulu wadhifa huo na ataendelea kukiongoza CUF kushika madaraka na kushika Serikali ya Umoja wa Kitaifa katika uchaguzi mkuu wa mwakani, akiwa kwenye nafasi hiyo.
Maalim alisema taarifa zilizoenezwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa baada ya kufukuzwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Masoud Othman Masoud, naye amejiuzulu Umakamu wa Kwanza ni uzushi mtupu.
CHANZO: NIPASHE

CAF yaichomolea Morocco AFCON 2015

http://static.goal.com/243400/243477_heroa.jpgSHIRIKISHO la Soka Afrika, CAF, limeichomolea Morocco wenyeji wa Fainali za Afrika za mwakani, ambao waliomba kuahirishwa kwa michuano hiyo kwa hofu ya ugonjwa wa EBOLA.
CAF wamesisitiza kuwa fainali hizo za mataifa ya Afrika 2015 itaendelea kama ilivyopanga licha ya hofu ya wenyeji dhidi ya ugonjwa huo hatari.
Morocco waliomba shindano hilo liahirishwa kufuatia mripuko wa ugonjwa huo ambao umeua watu zaidi ya 4,000 baada ya maafisa wa afya nchini humo kuonya kuendelea kwa fainali hizo kwa madai yanaweza kuendeleza uambukizaji zaidi.
Mshauri wa Waziri wa Michezo wa Morocco, Mohammed Ouzzine, alieleza taifa hilo la magharibi mwa bara hilo lina wasiwasi kuandaa shindano hilo linalochukua wiki tatu.
“Matakwa ya Morocco na wakaazi wake pamoja na wale wa bara Afrika yanadunisha linguine lolote. Morocco wamewasilisha ombi hilo kufuatia ushauri muhimu kutoka maafisa wa afya.
“Hatuwezi hatarisha maisha ya watu kwa kuendelea kuandaa shindano hili kwani msingi wa tahadhari unafaa kufuatwa,” mshauri Hamid Faridi aliambia stesheni ya redio, Atlantic Jumamosi.
Kwa majibu, Caf walitoa taarifa wakitofautiana na wenyeji hao huku Afrika Kusini wakilengwa kama waandalizi wa dharura ikiwa Morocco watajiondoa.
“Caf wanadhibitisha hakuna badiliko kwenye ratiba ya shindano hili. Tungependa kukumbusha kwamba tangu dimba la kwanza la 1975, shindano hili halijawahi chelewa au kuhairishwa,” taarifa ya utawala huo wa kandanda ilisema.
Mataifa ya Afrika magharibi, Guinea, Liberia na Sierra Leone yameadhirika zaidi na mkurupuko wa sasa wa Ebola. Guinea na Sierra Leone bado wanawania tiketi za Morocco 2015.
Afrika Kusini waliokoa jahazi la shindano hilo 1996 na mwaka jana.

ARSENAL MAJANGA, MAJERUHI WAZIDI KUONGEZEKA

http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/003/042/640/hi-res-a01b8eaefd6aaec9613b24d358507950_crop_north.jpg?w=630&h=420&q=75KLABU ya Arsenal imezidi kupata pigo baada ya nyota wake kadhaa kupata majeraha, kufuatia kuumia kwa beki Laurent Koscielny aliyelazimika kujiondoa kwenye mazoezi ya timu yake ya kitaifa ya Ufaransa.
Beki huyo wa kati amejitoa Les Blues kutokana na maumivu ya ukano wa kisigino.

Meneja Arsene Wenger amepigwa na pigo moja baada ya lingine ikiwa ni mechi saba tu ndani ya msimu mpya huku ambapo sasa Koscielny anajiunga na nyota wenzake Danny Welbeck, Mathieu Debuchy, Mikel Arteta, Olivier Giroud, David Ospina, Aaron Ramsey na Yaya Sanogo kwenye zahanati.

Siku mbili baada ya Ujerumani kutangaza kiungo nyota Mesut Ozil atalazimika kutocheza kati ya wiki 10 na 12, Wenger ameongezewa tumbo joto na habari kuwa beki Koscielny amejiondoa kutoka mechi za Ufaransa dhidi ya Ureno na Armenia kwenye msururu wa kufuzu Kombe la Euro la 2016, huku Danny Welbeck naye akiiumia wakati England ikishinda 1-0.
Shirikisho la Ufaransa limeandika kwenye anwani yao ya mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa Koscielny anauguza uvimbe wa ukano wake wa kisigino.

Kocha Nigeria aweweseka kipigo cha Sudan, aomba radhi

http://mobifootball.com/wp-content/uploads/2013/08/B13FEGB0345.jpgKOCHA wa timu ya taifa ya Nigeria, Stephen Keshi bado yuko katika mshangao kufuatia kipigo walichopata kutoka kwa Sudan katika mchezo wa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika. 
Super Eagles walishindwa kucheza kwa kiwango chao cha juu na kujikuta wakichapwa bao 1-0 katika Uwanja wa Manispaa jijini Khartoum katika mechi za kuwania Fainali za Kombe la Afrika mwakani. 
Keshi amesema kikosi chake kingeweza kuibuka na ushindi katika mchezo huo kama nafasi walizotengeneza zingetumika ipasavyo lakini haraka aliwaomba radhi mashabiki wa Nigeria kwa kupoteza mchezo huo. 
Kocha huyo amesema inabidi aombe radhi kwani mashabiki wa Nigeria walikuwa na imani kubwa na timu yao kuibuka na ushindi. 
Mbali na Keshi lakini pia golikipa na nahodha wa Super Eagles Vincent Enyeama naye aliwaomba radhi mashabiki kwa kipigo hicho na niaba ya wachezaji wenzake na kuahidi kufanya vyema katika michezo yao inayofuata.

Dk Ndumbaro yamkuta, afungiwa miaka 7 katika soka

BAADA ya tetezi zilizokuwa zikizagaa kwamba huenda Mwanasheria wa klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara, Dk Damas Ndumbaro yupo kitanzini na huenda akaadhibiwa kwa kauli alizotoa hivi karibuni kuhusiana na makato ya 5% zilizotakiwa na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, hatimaye imethibitika kuwa kweli.
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imemfungia Dk Ndumbaro kujihusisha na mambo ya soka kwa muda wa miaka saba na faini ya kiasi cha fedha.
Ndumbaro ambaye aliingia katika mzozo mkubwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi wiki iliyopita baada ya TFF kuagiza kila klabu kukatwa asilimia tano za mapato yatokanayo na udhamini wa klabu hizo wanaoupata kutoka kwa Vodacom, wadhamini wakuu wa ligi kuu ya Tanzania Bara, na Azam TV.
Ndumbaro alikimbilia katika vyombo vya habari na kusema wazi kuwa, klabu zimemuagiza kuwaambia TFF kuwa havipo tayari na havitakubali jambo hilo litokee, huku akijiamini na kuchambua baadhi ya vipengele na mambo ya sheria, Ndumbaro alivuka mipaka pale aliposema kuwa wanatafuta wastani wa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF na kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais wa shirikisho, Malinzi.
Kikao cha juzi cha kamati ya nidhamu kimefikia uamuzi wa kumfungia, Ndumbaro na kumlilipisha faini kwa sababu, Ndumbaro ambaye alizungumza kama wakili wa klabu za ligi kuu kupitia,.
TFF imedai Ndumbaro amekanwa na klabu ingawa taarifa zinaeleza si kweli kwa kuwa viongozi wa klabu 12 walisaini kumpitisha kuwa wakili wao.

Sunday, October 12, 2014

TCRA waitoza faini, yaipa onyo Times FM, kisa...!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgUCfyBMCPGb1kGs84BKKyY7GJqi99M0X_vtw7Se01slrZVrI959nyXlBWA-Ym_pkRRrzOuXM2LwxbpBD_zgni4015OzXit1Vg3SgqfjKu5zNEbYsgFW3mz2W3nbR59ivFs9sk1oE-utYw/s1600/CIMG5207.JPG
Mtangazaji wa Mitikisiko ya Pwani wa Times FM, Dida akiwa kazini
KAMATI ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imetoa onyo kali kwa kituo cha Redio cha Times Fm, pamoja na faini ya kulipa kiasi cha Sh milioni 1, kutokana na kukiuka vifungu vya maadili na kanuni za utangazaji, vilivyopo katika leseni ya utangazaji inayotolewa na mamlaka hiyo.
 
Akisoma hukumu hiyo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Margareth Munyagi, alisema ‘ Times Fm’ imepewa adhabu hiyo baada ya watangazaji wake kukiuka taratibu zilizowekwa na mamlaka hiyo, kwa kutangaza hewani maneno yanayokiuka maadili ya utangazaji.
 
Munyagi alisema kwa nyakati tofauti kupitia kipindi chake cha ‘Hatua tatu’ kilichorushwa saa 3 hadi saa 5 asubuhi na ‘Mitikisiko ya Pwani’, kilichorushwa mchana wa Agosti 29 mwaka huu, watangazaji wa vipindi hivyo walisikika wakizungumzia dondoo zilizolenga kuhamasisha ngono bila kuzingatia muda huo ambao watoto wengi wanaweza kusikiliza.
 
Alisema kiutaratibu muda ambao dondoo hizo zilikuwa zikitangazwa, si muda muafaka kwa kuwa vipindi hivyo pia vingewezwa kusikilizwa na watoto na kwamba muda wa dondoo kama hizo kutolewa unapaswa kuanzia saa 3 usiku hadi saa 11 alfajiri.
 
Aidha alisema utetezi uliotolewa na Mkurugenzi wa Redio hiyo, Leule Nyaulawa haukidhi haja mbali na kulipokea shitaka lililotolewa dhidi yao.
 
Nyaulawa alisema suala la kupata watangazaji wazuri Tanzania bado ni changamoto kutokana na vyuo vingi kuzalisha watangazaji wasio na uwezo mzuri.
 
Pia alisema kupitia kwa utetezi wake watakwenda kulifanyia kazi suala hilo ili kuepusha kurudiwa kwa kosa kama hilo na mengine yaliyopo katika leseni za utangazaji huku kamati hiyo ikitoa muda wa mwezi mmoja kwa Times Fm kulipa faini hiyo au kukata rufaa kama haikuridhika na uamuzi uliotolewa dhidi yao.

Ureno yafumuliwa na Ufaransa, Benzema zaidi ya Ronaldo

http://level3.soccerladuma.net/cms2/image_manager/uploads/News/179201/7/default.jpg
Benzema akifunga bao la kuongoza la Ufaransa
http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/10/11/1413055734828_lc_galleryImage_Portugal_s_Cristiano_Rona.JPG
Ronaldo akilalamika
https://media.zenfs.com/en_GB/Sports/Eurosport/1330493-28603425-2560-1440.jpg
Wachezaji wa Ufaransa wakimpongeza Pogba baada ya kufunga bao la pili la nchi yake wakiilaza Ureno 2-1
TIMU ya taifa ya Ufaransa imeitambia Ureno kwa kuilaza mabao 2-1 katika pambano la kirafiki la kimataifa, huku ikishuhudiwa nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo akishindwa kumaliza pambano kwa kuumia goti.
Mwanasoka Bora huyo wa dunai alitoka uwanjani dakika ya 76 baada ya kuumia akiwa ameshuhudia mchezaji mwenzake ambaye hivi karibuni alimwagia sifa akidai ndiye namba 9 Bora duniani akiwa amefunga bao moja na Paul Pogba akifunga la pili.
Benzema anayecheza na Ronaldo katika klabu ya Real Madrid alifunga bao la kuongoza dakika ya tatu tu kabla ya Pogba anayecheza Juventus kuongeza la pili dakika ya 65 na Ureno ilipata la kufutia machozi dakika ya 78 lililofungwa na mtokea benchi Ricardo Quaresma kwa mkwaju wa penati.

England wachonga kwa kuikung'uta San Marino

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02367/lennon_2367930b.jpgKOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson amesema amefurahishwa na utulivu wa kikosi chake wakati wakitafuta mbinu za kuifunga San Marino katika mchezo wa kufuzu michuano ya Ulaya uliofanyika katika Uwanja wa Wembley. 
Uingereza ilikwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao mawili kabla ya kluongeza mengine matano katika kipindi cha pili na kuwafanya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 katika mchezo huo. 
Hudgson amesema kikosi chake kifanya kazi ngumu kuipenya ngome ya San Marino iliyowapa usummbufu lakini utulivu na subira kwa wachezaji wake vilifanya mchezo huo kuja kuonekana rahisi. 
Mabao ya Uingereza katika mchezo huo yalifungwa na beki Phil Jagielka, nahodha Wayne Rooney aliyefunga kwa penati, Danny Welbeck, Andros Townsend na bao la kujifunga wenyewe lililofungwa na Alessandro Della Valle aliyebabatizwa na mpira uliopigwa na Rooney. 
Ushindi huo unawapeleka Uingereza kileleni mwa msimamo wa kundi E kwa tofauti ya mabao dhidi ya Lithuania baada ya timu zote hizo kushinda mechi zao mbili walizocheza.

Dk Ndumbaro kitanzini, TFF yaomba radhi kwa upotoshwaji

Add caption

KIKAO cha dharura cha Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kimefanyika jana kujadili matukio ya hivi karibuni, hasa mwenendo wa wadau wa Bodi ya Ligi. Shirikisho linatoa tamko kwa umma kama ifuatavyo:

1. Kamati ya Utendaaji imesikitishwa na taarifa za upotoshaji kuhusu kanuni mpya za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), hivyo inaomba radhi kwa wadau ambao wameguswa na kusumbuliwa na matukio hayo.

2.Kufuatia matukio hayo, Sekretarieti ya TFF kwa niaba ya Kamati ya Utendaji, imefungua mashtaka kwenye Kamati ya Nidhamu dhidi ya Dk. Damas
Ndumbaro ambaye ni mjumbe wa Bodi ya Ligi na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Klabu ya Simba. Pia wadau wote waliohusika na upotoshaji huo
wakiwemo wafanyakazi wa TFF na Bodi ya Ligi watashughulikiwa kulingana na nafasi zao.

3.Kutokana na madai ya klabu kuhusu vipengele kadhaa vya Kanuni za Ligi Kuu 2014/15, Kamati ya Utendaji imepanga kukutana na viongozi wa klabu za Ligi Kuu siku ya Jumamosi, Oktoba 18 mwaka huu ili kuwasikiliza na kushauriana kuhusu changamoto za kikanuni na uendeshaji wa mashindano kwa ujumla.

4.Kamati ya Utendaji itaendelea kuboresha Kanuni za Uendeshaji Bodi ya Ligi (Governing Regulations) ili kuweka uwiano wa utendaji na kuepusha tofauti
kati ya Bodi ya Ligi, vilabu na TFF. Aidha Kamati ya Utendaji itafanya kila linalowezekana kuboresha ligi kwa kuijengea uwezo Bodi ya Ligi kwa lengo la
kuwa na ligi zinazoendeshwa kisasa (Professional Leagues).

HUYU NDIYE MISS TANZANIA WA 20

MISS Tanzania mpya Sitti Abass Zuberi Mtemvu akipunga mkono mara baada ya kuvikwa taji hilo usiku wa kuamkia leo katika shindano lililoshirikisha warembo 30 na kufanyika ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam. Sitti Mtemvu ametwaa taji hilo lililokuwa likishikiliwa na Happyness Watimanywa na kuwa mrembo wa 20 tangu shindano hilo liliporejeshwa tena nchini mnamo mwaka 1994 na kutwaliwa na Aina Maeda.

Mrembo wa Redd's Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu akiwa katika picha ya pamoja na Mshindi wa pili, Lillian Kamazima (kulia) na Mshindi wa Tatu, Jihhan Dimachk mara baada ya kutawazwa rasmi usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar es Salaam. Sitti Mtemvu alianza kwa kunyakua Redds Miss Chang'ombe na baadaye Redds Miss Temeke. Sitti ni binti wa Mbunge wa Temeke, Mhe. Abbas Mtemvu.
Picha zote na Othman Michuzi.
Redd's Miss Tanzania aliemaliza muda wake,Happiness Watimanywa akimpisha crown,Redd's Miss Tanzania wa sasa,Sitti Mtemvu.

























Tuesday, October 7, 2014

Dk Ndumbaro kuburuzwa Kamati ya Nidhamu kisa...!

http://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/06/ndumbalo1.jpg
Dk Damas Ndumbaro, Mwanasheria wa Klabu 14 za Ligi Kuu zinazopinga agizo la TFF kuwakata asilimia 5 za fedha za wadhamini wao
SAKATA la vilabu 14 vinavyoshiriki Ligi Kuu ya Bara kupitia kwa mwanasheria wao, Dk Damas Ndumbaro, kupingana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) juu ya kukatwa asilimia tano ya fedha za wadhamini wa ligi hiyo na kutishia kutoshiriki ligi na zitapiga kura ya maoni ya kutokuwa na imani na Rais wa TFF, Jamal Malinzi, ikiwa TFF itatekeleza azma yake, limechukua sura.
Mapema wiki iliyopita, Malinzi aliagiza timu hizo kukatwa kiasi hicho cha pesa kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Soka (FDF) ambapo klabu husika zikiwemo Simba na Yanga zimepinga hatua hiyo na kutishia kutocheza ligi kuu kama agizo hilo litatekelezwa na Bodi ya Ligi.
Sasa kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika inaelezwa kwamba Shirikisho la soka nchini limefikia hatua ya kumpeleka mwanasheria huyo Damas Ndumbaro kwenye Kamati ya Nidhamu ya shirikisho hilo kutokana na kitendo chake alichokifanya mwishoni mwa wiki iliyopita.

Credit:Shafii Daud

CAF yaitosa Tanzania AFCON 2017

http://i2.cdn.turner.com/cnn/dam/assets/140823175408-afcon-trophy-story-top.jpgSHIRIKISHO  la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefahamishwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuwa Tanzania haitaweza kuwa mwenyeji wa Fainali za Afrika- AFCON 2017 kwa kuwa haijawahi kuandaa fainali zozote za vijana Afrika. Fainali hizo ni zile za vijana wenye umri chini ya miaka 17 na 20.
Hivyo, TFF inaelekeza nguvu zote katika kuandaa Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka U17 mwaka 2019.
Tunapenda kuchukua fursa hii kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanazania, Jakaya Kikwete kwa kututia moyo katika kuomba uenyeji wa AFCON 2017.
Pia tunamshukuru Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara kwa juhudi binafsi alizozionyesha katika jitihada za Tanzania kuomba uenyeji wa AFCON 2017.
TFF inaamini kwa dhati kuwa uenyeji wa Afrika U17 2019 utaifungulia Tanzania milango ya kuandaa mashindano makubwa zaidi.

Newz Alert! Mwanasheria Mkuu ZNZ afutwa kazi

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Othman Masoud amefutwa kazi na Rais wa Zanzibar, Dk Mohammed Ali Shein.
Taarifa kutoka visiwani humo zinasema kuwa Mwanasheria huyo aliyeamua kutumia demokrasia yake katika Bunge la Katiba kwa kupigia kura za ndiyo na hapana vipengele na ibara za Rasimu ya Katiba Mpya amefutwa kazi usiku huu.
Inaelezwa maamuzi hayo ya Dk Shein yamekuja ikiwa imesalia saa chache kabla ya rasimu huyo kukabidhiwa kwa viongozi wakuu wa nchi kesho mjini Dodoma na nafasi yake imeelezwa inazibwa na aliyekuwa Mwansheria Mkuu Msaidizi, Said Hassan Said.
hata hivyo haikuelezwa sababu ya kufutwa kazi kwa Mwanasheria huyo ambaye kwa baadhi ya wajumbe na wananchi wa visiwani humo wanamuona kama 'Msaliti' kwa alichokifanya kwenye Bunge Katiba lililomalizika hivi karibuni.

Mkude, Mgeveke waongezwa Stars


http://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/05/IMG_7000.jpgKATIKA kuhakikisha wanapata ushindi katika mechi yao ya Jumapili dhidi ya Benin, Kocha Mart Nooij ameongeza wachezaji watatu kwenye kikosi cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ili kukiongezea nguvu.
Taifa Stars inajianda kukabiliana na Benin katika mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)  itakayofanyika Jumapili (Oktoba 12 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Wachezaji walioongezwa ni kiungo Jonas Mkude na mlinzi Joram Mgeveke kutoka timu ya Simba, pamoja na mlinzi Gadiel Michael wa Azam.

WANYARWANDA KUZIHUKUMU STARS v BENIN

taifa stars 2014

MAREFA kutoka Rwanda ndiyo watakaochezesha mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kati ya Taifa Stars na Benin itakayofanyika Jumapili jijini Dar es Salaam. Hakizimana Louis ndiye atakayeongoza waamuzi hao wa FIFA kwa kupuliza filimbi kwenye mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 jioni. 
Atasaidiwa na Simba Honore na Niyitegeka Jean Bosco.
Mechi hiyo itatanguliwa na ile ya viongozi wa dini- Kiislamu vs Kikristo kudumumisha upendo, amani na ushirikiano itakayoanza saa 9 kamili alasiri. 

Tiketi za elektroniki zitakazotumika kwa mechi hiyo tayari zimeanza kuuzwa kwa kiingilio cha sh. 4,000 na sh. 10,000.

Arsene Wenger apuuzia sakata lake na Mourinho


KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kamwe hajutii kumsukuma kocha wa Chelsea, Jose Mourinho katika mechi ya juzi zikiwa ni dakika 20 tu tangu mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Stamford Bridge kuanza kuchezwa.
Wawili hao walitibuana baada Gary Cahill kumchezea rafu mbaya winga mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez na Wenger kukasirishwa na uamuzi wa Mourinho wa kuonyesha kumtetea Cahill.
Hata hivyo, kama si juhudi za refa Martin Atkinson na mwamuzi wa akiba Jonathan Moss kujaribu kuwasuluhisha zingepigwa kavu kavu.
"Cha kujutia nini baada ya hilo? Nilitaka kwenda kutoka (pointi) A hadi B na mtu fulani akanitibua bila kuonyesha ishara ya mapokeo," Wenger alisema.
"B ilikuwa ni kuangalia kama Sanchez aliumia. Ilikuwa ni kusukumwa? Kidogo. Unaweza kuona kama ukweli nimejaribu kumsukuma."
Wenger anasema alimsukuma "kidogo" Mourinho.
Hata hivyo walitenganishwa na mwamuzi wa akiba Jon Moss na refa Atkinson, lakini haitarajiwi FA kuwachukulia hatua zaidi.
Mourinho alisema alitaka "kusahau" kuhusu tukio hilo na Mfaransa huyo, na akasisitiza hakufanya lolote baya.
"Inauma kwa sababu hii ni mechi kubwa, klabu kubwa, mpinzani mkubwa,na mechi muhimu kwa timu zote. Hali hii inaufanya mchezo kuwa na hisia,'' alisema.
"Nimefanya makosa mengi sana katika soka, lakini si kipindi hiki kwa sababu nilikuwa katika eneo langu la kiufundi na halikuwa kosa langu. Mchezo umekwisha. Mwisho wa stori."
Uhusiaano wa makocha hao wawili umekuwa wa maneno maneno katika mechi kwa kipindi kilichopita, kwa Mourinho kumpachika Wenger "mtaalam wa kufeli" hiyo ilikuwa Februari mwaka huu.
Mourinho pia alisema hahofii uamuzi wa kitabibu baada ya Thibaut Courtois kuhaha kutokana na kukwaruzana na mshambuliaji wa Kimataifa wa Chile Sanchez na kwamba pengo hilo likiwamo litazibwa na Petr Cech.

Esha Buheti achekelea tuzo mbili kwa mpigo

Esha Buheti akiwa na tuzo yake ya ACVCA-2014
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiVLR6SKy55g1ZgzkaXh0gpsrnv1_T8oa6EBwc7LrSGGG6KbSjBI5WwFEbyB69EgDwDS4spNTr4l3syPUdQ8KGG3x-33z7oUTejlSRFKTZkmTpdbBaYjKLLVlJaOzLLQcpKyKLUYcQM44vG/s1600/2.jpg
Esha Buheti katika pozi
MSHINDI wa Tuzo za filamu za Action & Cuts Viewers Choice (ACVCA-2014) Esha Buheti amesema mafanikio aliyopata kwa kipindi kifupi katika tasnia hiyo imetokana na kipaji cha kuzaliwa, kujituma na kujiheshimu mbele ya jamii.
Esha alisema, amejisikia faraja kuona ndani ya kipindi kisichozidi miezi mitatu akinyakua tuzo ya pili baada ya ile ya ZIFF-2014 (Tamasha la Kimataifa la Filamu la Zanzibar) na katu hatavimba kichwa badala yake kuongeza bidii afike mbali zaidi.
Mrembo huyo alisema kuwashinda nyota wa filamu kama Chuchu Hans, Salma Jabu 'Nisha', Shamsa Ford na Blandina Chagula 'Johari' siyo kazi ndogo na kusisitiza anashukuru wote waliopigia kura za kutosha na kunyakua tuzo hiyo ya pili.
"Kwa kweli nimejisikia faraja kubwa kwa lililonitokea, sikuamini kama ningeweza kuibukia mshindi mbele ya washindani wangu ambao naamini ni wakali. Hii ni changamoto kwangu kundelea kufanya vyema ili nitambe kimataifa," alisema.
Muigizaji huyo alishinda tuzo hiyo wiki iliyopita katika kipengele cha Muigizaji Bora Msaidizi, ikiwa ni miezi mitatu tangu alipotwaa tuo ya Muigizaji Bora wa Kike wa ZIFF-2014 kupitia filamu ya 'Mimi na Mungu Wangu' anayoitaja kama kazi bomba kwake.

Hammer Q kuweka kibakuli chake videoni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPuXhtoeR4zztOCIdP7ZAekZVHi6Yl2h8tpe5fFNe4ECtPzhUsg7Z-Na338MBN_tvxM5xrs2kGZ0v9Fn6DnsJSOz75hXNxqqYAL7QbNtlUvMB7tp7ZN4t-71MOswqFm3nnUcz3wFF5r6g/s1600/Hammer+Q.jpgMUIMBAJI mahiri wa muziki wa taarab, Hammer Q ameachiwa wimbo wake binafsi uitwao 'Kibakuli', ambao anajipanga kuutengenezea video yake mapema hivi karibuni.
Hammer Q aliyewahi kutamba kwenye muziki wa kizazi kipya na wimbo wa 'Lady' kabla ya kuhamia kwenye taarab, ameachiwa wimbo huo uliopo kwenye mduara.
Wimbo huo umetengenezwa na mtayarishaji aitwae Anta Nation na  umeanza kutamba kwenye redio na mitandao ya kijamii.
Msanii huyo amesema kwa sasa anafanya mchakato ili kutengeneza video ya wimbo huo mapema kuwapa burudani zaidi mashabiki wake.
Hammer Q mbali na kufanya muziki kama 'solo artist' pia analiimbia kundi maarufu na miondoko ya mduara ya Zanzibar la Offside Trick sambamba na kufanya kazi na mkewe Salha Abdallah 'Salha wa Hammer'

Ligi ikienda mapumziko, Yanga yapumua, Mtibwa Sugar inatisha

Yanga wanaenda mapumziko wakipumua nafasi ya tatu
Coastal Union bado wanajikongoja

Watetezi Azam wakiporomoka hadi nafasi ya pili wakiwapisha Mtibwa kuwaongoza
Mtibwa timu pekee iliyoshinda mechi zake 100%

Ruvu Shooting ndiyo ambayo haijafunga bao hata mmoja mpaka sasa. Ni kwamba pengo la Maguli (kushoto) halijapata mrithi wa kuliziba?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgboM03iAUZPCYvuYadSX-DrgxLYiOqanpQRh7w9oQyCDx_BclL4a6oF2VrzSbdjwrhAhFHPKlzRnMprs771Eep9DtnpEeGeoC5KrCHMmrC1wfNHGwyf56QiZMMSUqM8AmM2gVywZA6S2I/s1600/HMB_8265.JPG
Simba wataivaa Yanga mechi ijayo ikiandamwa na mdudu wa sare
RAUNDI ya tatu ya Ligi Kuu Tanzania Bara umemalizika  mwishoni mwa wiki na kushuhudia jumla ya mabao 44 yakitinga wavuni, huku mshambuliaji wa Azam Didier Kavumbangu akiongoza kwa kupachika mabao manne kati ya hayo.
Kavumbagu aliyetua Azam akitokea Azam anafuatiwa kwa karibuni na Ally Shomari wa Mtibwa mwenye mabao matatu kiisha kufuatiwa na wachezaji wanne wenye mabao mawili kila mmoja.
Timu yenye fowadi kali mpaka sasa wakati lihi ikienda mapumziko kwa wiki moja ni Mtibwa Sugar na Ndanda FC zenye mabao sita kila moja, kisha kufuatiwa na Azam yenye mabao matano kisha Yanga na Simba zikafuatia zikiwa zimetumbukiza kimiani mabao manne kila moja.
Pamoja na kuwa kinara wa kufunga mabao Ndanda pia ndiyo timu yenye ukuta mwepesi ikiruhusu mabao sita mpaka sasa ikifuatiwa na timu za Stanmd United na Polisi waliopanda pamoja ligi ya msimu huu zikiwa zimeruhusu mabao matano.
Ruvu Shooting ndiyo timu iliyo na safu butu mpaka sasa ikiwa haijafunga bao lolotewakifuatiwa na Mbeya City, Mgambo na JKT Ruvu wenye bao moja moja.
Ukuta wa chuma wa ligi hiyo mpaka sasa ni ule wa klabu ya Mbeya City ambayo haujaruhusu bao lolote kwake huku Mtibwa Sugar na Azam zikifuata kwa kufungwa bao moja tu kila moja.
Yanga ambayo ilianza kwa kipigo katika ligi ya msimu huu imechupa toka maeneo ya kati hadi nafasi ya tatu wakiwaacha watani zao watakaoumana nao katika mechi yao ijayo wakiwa na pointi tatu wakishika nafasi ya 10.


MSIMAMO KAMILI WA LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                               P   W    D    L    F    A   GD   Pts

01. Mtibwa Sugar     03  03   00  00  06   01  +5   09
02. Azam                 03  02   01  00  05   01  +4   07
03.Yanga                  03  02   00  01  04   04  00   06
04. Mbeya City          03  01  02  00  01   00  +1   05
05.Kagera Sugar       03  01  01   01  03   02 +1   04
06. Prisons                03  01  01   01  03  02  +1  04
07.Coastal Union       03  01  01   01  04  04   00  04
08.Stand Utd             03  01  01   01  03   05  -2   04
09. Ndanda Fc           03  01  00   02  06    06  00  03
10.Simba                  03  00  03   00  04    04  00  03
11. Mgambo JKT       03  01  00   02   01    02  -1  03
12. Polisi Moro          03  00   02  01   03    05   -2  02
13.JKT Ruvu             03  00   01  02   01   04   -3  01
14. Ruvu Shooting     03  00  01   02  00   04   -4  01

http://static.goal.com/462500/462526_heroa.jpg
Didier Kavumbangu  (kushoto) akipongezwa na wenzake
Wafungaji Bora:
4- Didier Kavumbagu(Azam)


3-
Ally Shomari (Mtibwa)


2-
Shaaban Kisiga (Simba), Nassor Kapama (Ndanda), Ame Ally (Mtibwa), Rashind Mandawa (Kagera)


1- Emmanuel Okwi, Amissi Tambwe (Simba), Coutinho, Kelvin Yondan, Haruna Niyonzima, Simon Msuva (Yanga), Deo Julius (Mbeya City), Danny Mrwanda, Nicolaus Kabipe, Bakari (Polisi-Moro),  Salum Kanoni,  (Kagera), Aggrey Morris  (Azam), Ernest Joseph, Paul Ngalema, (Ndanda), Jacob Mwaitalako, Ibrahim Kihaka, Laurian Mpalile (Prisons), Lutimba Yayo, Rama Salimu, Joseph Mahundi, Hussein Sued, (Coastal), Ramadhani Pella (Mgambo), Mussa Mgosi (Mtibwa), Jabir Aziz (JKT Ruvu), Salum Kamana, Heri Mohammed, Mussa Said(Stand Utd)