STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 17, 2010

Jane Misso kuzindua albamu yake Diamond Jumapili







MSANII nyota wa muziki wa Injili nchini, Jane Misso kesho anatarajia kuzindua albamu yake mpya na ya pili ya 'Uinuliwe' akisindikizwa na wasanii mbalimbali wa miondoko hiyo wa ndani na nje ya nchi.
Uzinduzi wa albamu hiyo utakaoenda sambamba na kuachiwa hadharani video yake, umepangwa kufanyika mchana wa kesho kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Micharazo, Misso, ambaye ni mchungaji na mwalimu aliyewahi kufanya kazi nchini Uganda kabla ya kujikita kwenye miondoko hiyo na kuachia albamu yake ya kwanza ya 'Umoyo', alisema wasanii karibu wote watakaomsindikiza kesho wameshawasili jijini Dar es Salaam.
Misso aliwataja wasanii waliotua kwa ajili ya kumsindikiza katika uzinduzi wake ni pamoja na Mcongo, David Esengo, Peace Mhulu kutoka Kenya watakoshirikiana na nyota wa Kitanzania wa muziki huo na kwaya mbalimbali kumpambia onyesho lake.
Mwanamama huyo aliwataja wasanii wa Injili wa Tanzania watakaompiga tafu kesho ni Christina Shusho, Upendo Nkone, Martha Mwaipaja, Steve Wambura na Joseph Nyuki.
"Kwaya zitakazonisinidkiza ni pamoja na Joy Bring'res, The Whispers Band, AIC Chang'ombe na kwaya ya Watoto Yatima kutoka Dodoma inayoongozwa na mlemavu wa ngozi, Timotheo Maginga," alisema Misso.
Misso alisema albamu hiyo ina nyimbo sita na baadhi yake zinahamasisha wananchi juu ya ushiriki wao katika Uchaguzi Mkuu wa Taifa wa Urais, Ubunge na Udiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31.
Nyimbo zilizoibeba albamu hiyo ni 'Pokea Sifa', 'Motema', 'Nyosha Mkono Wako', 'Uinuliwe', 'Unaweza Yote' na 'Mimi Najua Neno Moja'.

Friday, September 10, 2010

Chagueni watu kwa sifa zao sio vyama-Sheikh Mapeyo

WAUMINI wa dini ya Kiislam na Watanzania kwa ujumla wameaswa kuchagua viongozi katika uchaguzi mkuu ujao bila kujali aina ya vyama vyao ilimradi ni watu wenye uchungu, uadilifu na dhamira ya kweli ya kuwakomboa.
Aidha waumini na watanzania wamehimiza kuhakikisha wanashiriki kwa wingi siku ya kupiga kura na kujichagulia viongozi wawatakao badala ya kusubiri kuchaguliwa kisha waje kulalama mambo yatakapokuwa yakienda kombo.
Wito huo umetolewa na Imamu wa Msikiti wa Mwenge Islamic Center, Sheikh Shaaban Mapeyo alipokuwa wakiwahutubia waumini baada ya swala ya Eid iliyoswaliwa msikini hapo, jijini Dar es Salaam.
Sheikh Mapeyo ambaye ni mgombea wa kiti cha Ubunge Jimbo la Kawe kupitia Chama cha Wananchi, CUF, alisema waumini wa Kiislam na wananchi kwa ujumla wasihadaiwe na propaganda za kuchagua viongozi kwa kuangalia chama bali wasifu wa mgombea kwa nia ya kujiletea maendeleo.
Alisema kuendelea kuchagua wagombea kwa kuzingatia chama ndio ambayo yamefanya Tanzania kuendelea kudumaa kwa muda mrefu kwa kuwa wapo baadhi ya wagombea hawana sifa za uongozi lakini wamechaguliwa kupitia vyama vyao.
"Waislam wakati tukizingatia 'darasa' tulilolipata kipindi cha Ramadhani ni vema tukajipanga kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao, tusiupuuze na muhimu ni kuhakikisha tunachagua watu wenye sifa na sio kuangalia chama," alisema.
Aliongeza kwa kuwataka waumini nao na watanzania kwa ujumla kushiriki kwa wingi kwenye uchaguzi huo kwa kujitokeza kupiga kura ili kuhakikisha wanajichagulia viongozi na makini watakaowaletea maendeleo ya maeneo yao.
"Bila kujali jinsia jitokezeni kwa wingi kushiriki kupiga kura Oktoba 31, puuzeni propaganda zinazosambazwa na baadhi ya watu kwamba kushiriki uchaguzi ni haramu, mtajiletea maendeleo vipi kama hampigi kura?" Alihoji.
Sheikh Mapeyo alisema mambo mengi hapa nchini yamekuwa yakienda kombo kwa sababu wananchi wengi wamekuwa sio makini katika kushiriki uchaguzi mkuu ambayo ndio silaha ya kujiletea maendeleo ya kweli.
Uchaguzi Mkuu wa kuchagua madiwani, wabunge na Urais utafanyika Oktoba 31 na kwa sasa wagombea wanaendelea na kampeni zao.

Mwisho

Monday, September 6, 2010

Mpeni kura Mkullo, namuamini mno-Dk KIkwete






RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni mgombea wa nafasi hiyo kwa tiketi ya CCM, Dk Jakaya Kikwete, amewaomba wakazi wa Jimbo la Kilosa, kumpa tena ubunge mgombea wa chama hicho na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo kwa madai anamuamini.
Aidha mgombea huyo aliwaomba wapiga kura wa majimbo mengine yaliyopo wilayani Kilosa kuhakikisha wanaipa kura CCM kupitia viti vya ubunge na udiwani ili kumrahisishia kazi ya kuongoza nchi kwa mara ya pili mfululizo.
Akiwahutubia wakazi wa wilaya ya Kilosa kwenye mkutano wake wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja uliopo njia panda Ilonga na Kimamba, Rais Kikwete alisema angependa kuona wakazi wa Kilosa wakimpa tena ubunge waziri Mkullo kwa vile ni mmoja wa mawaziri anayewaamini.
"Naombeni mnichagulie tena Mkullo kuwa Mbunge wa Kilosa kwa kuwa kumuamini kwangu ndiko kulikonifanya nimpe dhamana ya kuwa Waziri wa Fedha na Uchumi," alisema Dk Kikwete.
Dk Kikwete alisema, chini ya Mkullo Kilosa imeweza kupiga hatua kubwa ya maendeleo kwa serikali yake kushawishika kuidhinisha fedha za miradi ya maendeleo katika sekta za elimu, afya, maji, umeme na barabara.
Pia mgombea huyo wa Urais, aliwaomba wakazi wa wilaya hiyo kuwachagua pia wagombea wengine wa majimbo ya Gairo na Mikumi pamoja na wale wa udiwani wa kata zilizopo wilayani humo ili kumrahisishia kazi katika kuwaletea maendeleo katika maeneo yao.
Naye Mkullo, alipopewa nafasi ya kuwasalimia wapiga kura wake, aliwaomba wampigie kura na kumpa ubunge kwa mara ya pili ili aweze kukamilisha baadhi ya ahadi zake alizowatolea kwenye uchaguzi uliopita wa mwaka 2005.
"Sina cha ziada ila kuwaomba mnichague tena kwa awamu ya pili ya kiti cha jimbo la ubunge la Kilosa ili kutekeleza ahadi zangu na kuwaletea maendeleo kwa ujumla kwa sababu nia na sababu ninayo," alisema Mkullo.
Akisoma Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005, Katibu wa CCM wilayani Kilosa, Gervas Makoye, alisema asilimia kubwa zimetekelezwa au kuanza kutekelezwa na hivyo ni fursa ya wakazi wa mji humo kuhakikisha wanaichagua tena CCM Oktoba 31, ili kujiletea maendeleo ya kweli.

Mwisho

Sunday, September 5, 2010

Dk Kikwete akiri watumishi wake wengi ni wezi



MGOMBEA wa Urais wa Chama cha Mapinduzi, CCM, Dk Jakaya Kikwete, amekiri wazi kuwa, watumishi wengi wa Halmashauri ni wezi na ndio wanaokwamisha miradi mingi ya maendeleo.
Aidha mgombea huyo amesema kuwa watanzania wengi wanajitakia kupata maambukizo ya ugonjwa wa Ukimwi kwa kuendekeza starehe na 'kiherehere' cha kupapia mapenzi yasiyo salama licha ya hamasa mbalimbali zinazotokea juu ya kujikinga na maradhi hayo.
Dk Kikwete aliyasema hayo jana katika mkutano wake wa kuomba kura katika uchaguzi mkuu ujao na kuwanadi wagombea wa nafasi za udiwani na ubunge wa wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro.
Alisema kuwa, pamoja na juhudi za serikali chini ya CCM kutaka kuleta maendeleo kwa wananchi, wapoo baadhi yawatumishi wa Halmashauri ambao ni wezi na wanaoangalia masilahi yao kwa kuzifuja fedha za miradi katika maeneo yao.
"Watumishi wengi wa Halmashauri ni wezi na wanaokwamisha miradi ya maendeleo kwa kuzitumia vibaya fedha wanazopelekewa na serikali kwa ajili ya kuwainua wananchi katika sekta mbalimbali jambo ambalo ni baya," alisema Dk Kikwete.
Katika kukaribia na hilo, mgombea huyo alisema akipata nafasi ya kuchaguliwa tena atahakikisha anapambana nao kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kama ilivyo kauli mbiu yao kwa kuwa kufanya hivyo kutaondoa kikwazo cha kuwapelekea wananchi maendeleo.
Akizungumza suala la maambukizi ya Ukimwi, mgombea huyo wa CCM, alisema anaamini kuwa, ugonjwa huo unakingika na kuepukika iwapo wananchi wataamua kuzingatia mahubiri na makatazo ya viongozi wa kidini juu ya suala la zinaa.
Dk Kikwete alisema maambukizi mengi yaliyopo nchini ni kama wananchi wanajitakia wenyewe kwa kutawaliwa na kuendekeza starehe na kiherehere cha kukimbilia mapenzi yasiyo salama.
"Kama sio kiherehere ni vipi mwanafunzi badala ya kushughulika na masomo shuleni yeye anakimbilia mapenzi?" alihoji Dk Kikwete.
Alitoa ushauri kwa wananchi juu ya kuwa makini na ugonjwa huo kwa kuoa, kujizuia kuwa waaminifu au kutumia kinga.
Kwani kwa kutokufanya hivyo maambukizi yatazidi kuongezeka na taifa kupoteza nguvu kazi ilihali Tanzania Bila Ukimwi Inawezekana!
Alizungumzia dawa za kurefusha maisha ya waathirika, Dk Kikwete serikali yake inatoa dawa hizo bure na kudai kama kuna wanananchi wanaouziwa basi watakuwa wanaibiwa na wanapaswa kutoa taarifa ili wahusika washuighulikiwe.
Juu ya malaria, aliyodai seikali yake inaumia kuona wananchi wanakufa kwa ugonjwa huo kuliko hata Ukimwi na kudai wameweka mikakati ya kupambana nao kwa kuongeza ugawaji wa vyandarua, kupuliza dawa katika kila nyumba nchi nzima na kuhakikisha wanaua mbu wanaoambukiza ugonjwa huo.

Mwisho

Chagueni CCM Tanzania istawi-Dk Kikwete





MGOMBEA wa Urais wa kiteki ya CCM, Dk Jakaya Kikwete, amewataka wananchi kukichagua chama chake kwa mara nyingine ili kuistawisha nchi, kwa maelezo kwamba vyama vya upinzani vilivyopo ni vya msimu na havina uwezo wa kuongoza.
Dk Kikwete ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano aliyasema hayo leo alipokuwa akiwatuhubia wakazi wa wilaya ya Kilosa katika mkutano wa kampeni uliofanyika eneo la Wahanga wa Mafuriko lililopo njia panda ya Ilonga na Kimamba, mkoani Morogoro.
Rais Kikwete alisema kuwa, pamoja na kwamba wapinzani wamekuwa wakitoa kejeli dhidi ya utendaji wa CCM, ukweli ni kwamba vyama hivyo havina uwezo wa kuongoza na hivyo ni vema wananchi wakaichagua tena CCM kustawisha maendeleo yaliyopo.
Alisema pamoja na utitiri wa vyama vya upinzani, vingi vyake ni vya msimu tu, ambapo huibuka wakati wa uchaguzi na hasa wanapofanikiwa kuwapata wanaohama toka CCM.
"Wananchi wa Kilosa na Watanzania kwa ujumla nawaombeni muichague CCM kwa mara nyingine kwa kuwa ndio chama pekee bora kinachoweza kustawisha maendeleo ya nchi yaliyopo pamoja na kudumisha amani na utulivu, vyama vingi vya upinzani ni vya msimu tu na hasa vinapofanikiwa kuwanasa wanaohama toka CCM pale wanapogombea na kutochaguliwa," alisema Dk Kikwete.
Dk Kikwete alisema CCM imfanikiwa kutekeleza ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005 kwa asilimia kubwa katika nyanja na sekta za Afya, Elimu, Maji, Miundo Mbinu, Kilimo na Ufugaji na ikipewa nafasi tena itamalizia sehemu zilizobakia.
Alitoa mfano suala la elimu kwa wilaya ya Kilosa, imefanikiwa kuongeza majengo ya shule kuanzia chekechea hadi sekondari, ambapo alisema kwa mfanoi mwaka 2005 idadi ya wanafunzi katika sekondari ilikuwa ni 6969 ambapo kwa sasa idadi hiyo imefikia 17666 ikiwa ni ongezeko la zaidi ya wanafunzi 10,000.
Pia alisema juhudi hizo za kuboresha sekta hiyo zinaendana na kuongeza idadi ya walimu ambapop alisema mwaka 2005 idadi ya wahitimu wa ualimu nchi nzima ilikuwa ni 600 tu, lakini awamu ya nne imejitahidi na kufanya idadi hiyo kufikia 16,000.
Alisema, anafahamu idadi hiyo bado haikidhi hivyo serikali yake kupitia CCM inafanya mipango ya kuongeza walimu zaidi kupitia vyuo vyake na vile vya watu binafsi ili kufikia lengo sambamba na kuwezesha kupatikana kwa vitabu, maabara na nyumba za walimu.
Kuhusiana na vitabu,Dk Kikwete alisema tayari jitihada zimeshafanywa kwa kuomba msaada toka kwa nchi marafiki ikiwemo Marekani ambayo imejitolea kutoa jumla ya vitabu 800,000 vya masomo mbalimbali ya sekondari na mapema mwakani itapokea vitabu vingine zaidi ya Mil 2.4.
Alisema hayo na mengine ambayo yamekuwa yakifanywa na CCM tangu iwe madarakani hayawezi kufanywa na vyama vya upinzani na kuwataka wapiga kura kutofanya makosa Oktoba 31 watakapochagua viongozi kwa ajili ya miaka mitano ijayo.
Katika hatua nyingine, mgombea huyo alizungumzia suala la wahanga wa mafuriko yaliyoikumba wilaya hiyo mnamo Desemba mwaka jana, kuwa serikali ipo katika mpango wa kuwajengea nyumba za kudumu wahanga hao wanaishi kambini kwa sasa.
Dk Kikwete alisema kazi ya ujenzi wa nyumba hizo utafanywa na Jeshi la Kujenga Taifa, JKT, kwa lengo la kuwarejesha maisha ya amani na utulivu wakazi hao ambao kwa sasa wanaishi katika nyumba za mabati.
Pia alisema, serikali imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa bwawa jipya la Kidete pamoja na kujenga tuta jipya la kudhibiti maji ya Mto Mkondoa ambao aliutaja kuwa ndio tatizo lililosababisha mafuriko hayo yaliyoleta maafa makubwa.
Katika ziara yake ya kampeni wilayani humo, mgombea huyo wa CCM alikuwa akisimamishwa yeye na msafara wake na wananchi mbalimbali wa vijiji kwa ajili ya kumueleza kero zao.
Alipofika kata ya Dumila wananchi wa eneo hilo kupitia Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Dumila, Douglas Mwaigumila, walimueleza mgombea huyo juu ya kero zinazowakabili ambapo walizitaja ni huduma ya maji, afya, umeme na uporwaji wa ardhi yao ipatayo ekta 400 shutuma alizozipeleka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya yao.
Dk Kikwete aliwajibu wananchi hao kuwa serikali yao inayatambua kero hizo na tayari ilishaanza kuzitekeleza kwa awamu, huku akishangaa kusikia tukio la uporwaji huyo wa ardhi na kuahidi kulifuatilia.

Monday, August 23, 2010

Al Madina yafuturisha wanawake Dar, wakizundua ofisi



TAASISI ya Huduma za Kijamii ya Al Madinah, 'Al Madinah Social Services Trust' jana jioni ilizindua ofisi yao mpya kwenye jengo la BinSlum Plaza sambamba na kuwafuturisha futari wanawake wa Kiislam, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ally Hassani Mwinyi, Mama Sitti Mwinyi aliyeambana na Bi Khadija Mwinyi.
Shughuli hizo za uzinduzi na ufuturishwaji futari, iliandaliwa na Kamati ya Wanawake wa taasisi hiyo ya Al Madinah na kudhaminiwa na benki ya Stanbic na ilifanyika kwenye jengo hilo la Bin Slum lililopo mitaa ya Livingstone na Mkunguni, Kariakoo jijini Dar.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Wanawake wa Al Madinah, Hajat Mariam Dedesi, alisema hafla hiyo ya kuwafuturisha wanawake wa Kiislam ilikuwa na lengo kubwa la kujenga umoja na mshikamano pamoja na kutekeleza moja ya sunna iliyokokotezwa kwenye mfungo wa Mwezi wa Ramadhani ya watu kulishana kwa lengo la kupata dhawabu.
Mariam alisema mbali na hilo, lakini kubwa ni kutaka kutoa hamasa kwa wanawake wa Kiislam kuungana pamoja na kujitokeza kwa wajili ya kwenda Hijja kupitia taasisi yao ambayo inajishughulisha na huduma za kuwasafirisha mahujaji.
Alisema wanashukuru msaada mkubwa waliopewa na benki ya Stanbic, ambayo aliwahimiza wanawake nchini kote kujiunga nayo kwa lengo la kuweza kuhifadhia fedha zao bila ya riba na pia kupata mikopo itakayowawezesha kujianzishia na kuendesha miradi yao ya kimaendeleo kujikuza kiuchumi.
Naye mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Sheikh Ally Mbaraka, alitoa wito kwa waumini wote wanaotaka kwenda hija kujitokeza kujiandikisha na kulipia ada zao kupitia taasisi hiyo akidai ina huduma murua na gharama nafuu wakati wa kwenda na watakapokuwa hija.
Sheikh Mbaraka alisema huduma za malazi, usafiri kupitia Shirika la Ndege la Oman ni zenye kiwango cha hali juu na zitakazowawezesha mahujaji kutosafiri kwenda mbali na miji watakayofanyia hija zao.
Naye meneja wa Stanbic Bank, Bi Jennifer Hillal, alisema ni vema mahujaji na waumini wengine kuchangamkia kujiunga na benki yao kwa kuwa inazingatia miiko na sharia za kiislam kwa kutotoza riba ya aina yoyote.


Ukiondoa mgeni rasmi, Mama Sitti aliyeambatana na 'mkemwenza' Bi Khadija Mwinyi, wengine waliohudhuria ni Mwenyekiti wa

Waislam wahimizwa kujiunga na benki zisizotoza riba




WAUMINI wa dini ya Kiislam wamehimizwa kujiunga na mabenki kwa lengo la kuhifadhi fedha zao kwa salama pamoja na kuwawezesha kupata fursa ya kukopa fedha za kuendeshea shughuli zao za kimaendeleo na uchumi.
Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Kidini na Kijamii ya Al Madinah, Sheikh Ally Mbaraka, alipozungumza na Micharazo mara baada ya uzinduzi wa ofisi yao mpya eneo la Kariakoo, jijini Dar es Salaam.
Sheikh Mbaraka alisema ni vema waumini wa Kiislam wakajiunga na mabenki na hasa yasiyotoa riba kwa lengo la kupata fursa ya kukopa fedha ili kuanzisha miradi ya kimaendeleo na kiuchumi kujikwamua kimaisha.
Alisema kutokana na kujitokeza kwa mabenki kadhaa yanayoendesha shughuli zao kwa kuzingatia Sharia za Kiislam ni wasaa nzuri kwa waumini kujiunga nazo kuzilinda fedha zao salama na pia kupata faida bila kumuasi Mola wao.
Aliongeza kuwa taasisi yao inayohusika na masuala ya huduma za kijamii na kuratibu safari za Mahujaji, inawaomba waumini wanaotarajia kwenda Hija kuchangamka kujitokeza mapema kujiandikisha kwenye ofisi zao.
"Safari za Hija zinakaribia kuanza hivyo tunawahimiza waumini watakaoenda kuhiji kujitokeza mapema kujiandikisha ili kuwahi nafasi chini ya taasisi yetu ambayo inaendesha shughuli zake kwa kushirikiana na benki ya Stanbic itakayowawezesha mahujaji kutoa na kutuma fedha wakiwa hija," alisema.
Naye Meneja wa Huduma wa Benki ya Stanbic, Jennifer Hillal, alisema benki yao imeweka huduma mbalimbali zinazozingatia sharia ya kiislam kwa lengo la kuwawezesha watu wa imani hiyo kujiunga nao ili wanufaike na mikopo isiyo na riba pamoja na kusaidia kujiletea maendeleo ya kiuchumi.
Alisema benki yako yenye huduma ya ATM Visa Card ni muhimu kwa mahujaji kujiunga nayo kwa vile popote watakapokuwepo hata huko kwenye hija zao wataweza kupata huduma za kifedha kwa mfumo ule ule.
Pamoja na kuwahimiza kujiunga nao, pia aliwataka waumini hao na wananchi kwa ujumla kuingia kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 31 wakihakikisha unakuwa wa amani na utulivu.
Jennifer, alisema bila ya kuwepo kwa amani na utulivu hata wao wenye mabenki na watanzania kwa ujumla hawawezi kuendesha shughuli zao za kimaendeleo na kiuchumi kama inavyoshuhudiwa na mataifa mengine.

Mwisho

Mama Sitti Mwinyi ataka uchaguzi wenye amani na salama



WAKATI kampeni za wagombea wanaowania kinyang'anyiro cha uchaguzi zikiendelea nchini kote, Mke wa Rais wa Pili Mstaafu, Ally Hassani Mwinyi, Sitti Mwinyi, ameibuka na kuuombea uchaguzi huo uwe wa salama na amani.
Pia aliwahimiza wanawake nchini kote kuchangamkia uchaguzi huo kwa kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura ili kuhakikisha wanawachagua viongozi watakaosaidia kudumisha umoja na mshikamano.
Mama Sitti alitoa wito huo alipozungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa ofisi mpya ya Taasisi ya Kijamii ya Al Madinah, iliyoambatana na ufuturishwaji wa futari kwa wanawake wa Kiislam uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Alisema kuwa, wananchi bila kujali itikadi ya kidini au siasa wahakikishe kuwa uchaguzi mkuu ujao unafanyika kwa amani na utulivu wakiwa na maelewano kwa lengo la kudumisha umoja na mshikamano kwa watanzania wote.
"Nawasihi wananchi wote wake kwa waume bila kujali dini, kabila au itikadi za kisiasa washiriki uchaguzi mkuu kwa amani na salama wakiwa na maelewano, ili kudumisha umoja wetu," alisema.
Kauli kama hiyo ilitolewa pia na mke mkubwa wa Mwinyi, Bi Khadija, alihudhuria hafla hiyo iliyoandaliwa na Kamati ya Wanawake wa Al Madinah inayoongozwa na Hajat Mariam Dedesi na kudhaminiwa na Benki ya Stanbic.
Bi Khadija, alisema kwa kuwa Tanzania ni moja na wananchi ni wamoja ni vema wakashirikiana kuona uchaguzi wao unafanyika kwa amani na utulivu ili kuendeleza hali hiyo iliyozoeleka nchini.
Naye Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Wanawake ya Al Madinah, Mariam Dedesi alisema lengo la kuandaa futari hiyo kwa wanawake wenzao ni kujenga umoja na mshikamano na pia kusaidia kuhamasisha wenzao kujiunga na benki kwa lengo la kujiwezesha na hasa benki zisizo na riba.
Alisema kamati yao inawahamasisha wanawake kujiunga na mabenki yasiyo na riba ili kuweza kukopa fedha za kujianzishia miradi ya kimaendeleo ambazo itawakwamua kiuchumi wao na familia zao.

Mwisho

Aisha Sururu ataka umoja jumuiya za Kiislam

MWENYEKITI wa Taifa wa Jumuiya ya Wanawake wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania, BAKWATA, Aisha Sururu, ameziomba taasisi za Kiislam nchini kushikamana na kuombea uchaguzi mkuu uwe wa amani na utulivu.
Sururu, ambaye ni mgombea wa udiwani wa Viti Maalum CCM, alisema umoja na mshikamano ndio silaha pekee ya kuifanya Tanzania kuendelea kuwa nchi ya amani na utulivu na kuzikumbusha jumuiya hizo Kiislama kuidumisha.
Mwenyekiti huyo aliyasema hayo alipozungumza na Micharazo jana jijini Dar es Salaam na kudai taasisi na jumuiya hizo zina wajibu mkubwa wa kuwa mfano kwa wengine kwa kuwa na umoja na mshikamano bila kubaguana.
Alisema kujumika pamoja kwa viongozi na wafuasi wa jumuiya mbalimbali za kiislam katika hafla ya ufuturishwaji futari uliofanywa na Taasisi ya Al Madinah ni moja ya dalili njema za umoja miongoni mwao aliotaka udumishwe milele.
Alisema umoja huo hautafaa kama hawatashirikiana kwa ajili ya kuiombea nchi kufanya uchaguzi mkuu Oktoba 31 kwa amani na utulivu ili kuendeleza hali ya utilivu iliyopo nchini kwa miaka mingi.
"Kama kiongozi wa jumuiya ya wanawake ya BAKWATA nilikuwa nahimiza umoja na mshikamano kwa jumuiya zingine kuiombea Tanzania ifanye uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu ili tuishi na raha mustarehe," alisema.
Sururu, alisema kwa kuwa lengo la kila Mtanzania ni kuona amani na utulivu unaendelea kudumu basi ni vema wananchi wakashikamana na kutokubali kuwaachia wachache wawavuruge kwani majuto yake ni makubwa baadae.
Aliongeza kuwa, pamoja na kuhimiza umoja huo, pia anawaomba wananchi waliojiandikisha kupiga kura kujitokeza siku ya uchaguzi mkuu, Oktoba 31 kuchagua viongozi wanaowataka na kuwaamini kwa mustakabali wa nchi na maisha yao kwa ujumla.
Juu ya wagombea waliopitishwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi huo, Sururu aliwataka wafanye kampeni za kistaarabu kwa kumwaga sera zao ili kuwashawishi wananchi wawapigie kura siku ya kufanya hivyo.
Hafla hiyo ya kufuturishwa kwa wanawake wa Kiislam ilidhaminiwa na Benki ya Stanbic
Mwisho

Sunday, August 22, 2010

Wagombea Kilosa kuanza kampeni Agosti 26





WAGOMBEA wa CCM wanaowania viti vya Ubunge na Udiwani wilaya ya Kilosa wanatarajia kuanza rasmi kampeni zao Agosti 26 mwaka huu, wakati mgombea wao wa Urais, Rais Jakaya Kikwete atakapoenda kuzindua kampeni hizo jimbo la Mikumi.
Katibu wa CCM-Kilosa, Gervase Makoye, alisema wagombea wa CCM wataanza kampeni zao rasmi siku hiyo wakati rais atakapozuru Mikumi kuendelea kujikampenia kuomba kura za wananchi kwa uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 31.
Makoye alisema, wagombea wote watatu wa majimbo matatu yaliyopo wilayani kwao watahudhuria kampeni hiyo kabla ya kila mmoja kutawanyika jimboni mwake kuanza kuomba kura za wananchi wa maeneo yao.
Katibu huyo alisema baada ya Rais kuzindua Mikumi Agosti 26, siku inayofuata atakuwa Kilosa kisha kumalizia Gairo na kuwaacha wagombea wahusika wakiendelea na kampeni zao.
Jimbo hilo la Mikumi linawaniwa na Abdulsalaam Nahad Suleiman 'SAS', ambaye alisema amejipanga kuhakikisha anaibuka kidedea kwenye kinyang'anyiro hicho kinachowaniwa na wagombea wengine wa vyama vya mbalimbali vya upinzani.
Naye mgombea wa Jimbo la Kilosa, Mustafa Mkullo alisema yeye ataanza rasmi kampeni zake Agosti 27 baada ya Rais kuzindua kampeni za wilaya hiyo huko Mikumi na hapo ndipo atakapoanika kila kitu juu ya ukweli kuhusu alichowafanyia wakazi wa jimbo hilo na yale ambayo amepania kuyaendelea na kufanya mengine mapya.
Mkullo alisema mbali na hilo, lakini pia atazitumia siku 70 za kampeni hizo kuweka bayana juu ya tuhuma dhidi yake kuwa yeye sio raia wa Tanzania bali ni Mmalawi, madai aliyodai yametolewa na mmoja wa waliokuwa wagombea wenzake asiyekubali matokeo.
"Kampeni zangu nitazianza Agosti 27 na hapo ndipo nitapata fursa nzuri ya kusema kila kitu juu ya mipango yangu ya maendeleo kwa wakazi wa jimbo langu na pia kuweka hadharani madai juu ya tuhuma za utata wa uraia wangu," alisema Mkullo.
Mgombea wa Gairo, Ahmed Shabiby, yeye alisema yupo vema na atajinadi ili kuomba ridhaa ya wakazi wa jimbo hilo kumpa tena nafasi ya kuwatumikia kama walivyompa katika uchaguzi mkuu uliopita wa mwaka 2005.

Masilahi ya Ubunge ndio chanzo cha watu kuchafuana-Chayeka



MASILAHI makubwa wanayolipwa na kuyapata Wabunge, yanaelezwa ndio chanzo cha mfarakano miongoni mwa wana CCm kiasi cha kufikia kuchafuana wakipakaziana masuala ya utata wa uraia na mambo mengine yakudhalilishana.
Hayo yamesemwa na aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya wa Tarime, Raphael Chayeka, alipozungumza na Micharazo wilayani Kilosa, ambapo alisema masilahi manono wanayolipwa wabunge ndiyo yanayofanya kila mmoja kupigana kufa na kupona kuona anakuwa mbunge.
Chayeka alisema hali hiyo ya tamaa na uchu iliyowanayo watu wengi wanaojitosa kwenye siasa ndio wanaopelekea wanaoangushwa kuwachafua wenzao kwa minajili ya kuona wanapata nafasi ya kuteuliwa, kitu alichodai sio uungwana katika dunia ya wastaarabu.
Alisema donge nono la kwenye masuala ya ubunge na siasa kwa ujumla ndiyo inayofanya kila mtu sasa bila kujali wa kada gani kutaka kuwa mwanasiasa na hasa ubunge na pale wanaposhindwa kwenye kura ndipo wanapoibuka kuwachafua wengine.
"Masilahi manono yaliyopo kwenye Ubunge na Siasa kwa ujumla ndio yanayopelekea watu kuchafuana na kupakaziana mambo mabaya, lakini kama sio hivyo wala yasingetokea hayo yaliyojitokeza miaka ya hivi karibuni," alisema Chayeka.
Naye Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kilosa, Alhaj Shaweji Abdallah naye alisema ifike wakati wanachama wa CCM na wagombea wengine wawe waungwana kwa kubali matokeo badala ya kuwapakazia wenzao masuala ambayo yanayowadhalilisha wengine bila sababu ya msingi.
Wazee hao walitoa kauli hizo wakati wakimtetea mgombea ubunge wa jimbo la Kilosa na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo aliyevumishiwa kuwa sio raia wa Tanzania bali ni mtu wa Malawi kitu kilichomshangaza waziri mwenyewe kwa madai anatambue yeye ni raia.

Mwisho

Friday, August 20, 2010

Ligi ya TFF Kilosa kuanza mwezi ujao


LIGI ya Soka ya TFF Wilaya ya Kilosa, inatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi ujao ambapo fomu za ushiriki wa ligi hiyo zitaanza kutolewa Septemba 15 mwaka huu.
Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Wilaya ya Kilosa, KIDFA-Kilosa, Anthony Malipula, alisema ligi yao inatarajiwa kushirikisha timu zaidi ya 20 kati ya klabu zote 57 zilizosajiliwa wilayani humo.
Malipula, alisema fomu hizo za usajili zitakaponza kutolewa klabu zitalazimika kulipa ada ya Sh 30000 badala ya 50000 iliyowekwa kwa lengo la kutoa nafasi klabu nyingi zaidi kujitokeza tofauti na msimu uliopita.
"Ligi yetu ya TFF inatarajiwa kuanza mwishoni mwa Septemba kwenye Uwanja wa Halmashauri ya Kilosa na fomu zitaanza kutolewa Septemba 15 kwa gharama ya Sh. 30,000 badala ya 50,000." alisema.
Katibu huyo alisema ligi yao ya msimu uliopita ilishirikisha timu 18 ambapo klabu ya Mvumi Stars ndio walioibuka mabingwa na kuiwakilisha wilaya yao katika Ligi ya TFF Mkoa wa Morogoro na kuishia kushika nafasi ya pili kwenye kundi lao na kukwama kwenda kushiriki Ligi ya TFF ngazi ya Taifa iliyomalizika hivi karibuni.

Mwisho

Tuesday, August 3, 2010

Phiri awatuliza Simba, atua na kuomba radhi * Aahidi ushindi Agosti 14



KOCHA mkuu wa Simba, Patrick Phiri, alirejea nchini jana mchana kwa ajili ya kuendelea na kibarua chake cha kuwafundisha mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Bara na akawaomba radhi mashabiki wa timu hiyo kwa kuchelewa kujiunga na timu.
Akizungumza mara baada ya kuwasili, Phiri alisema kuwa matatizo ya kifamilia yaliyokuwa yanamkabili ndio yalifanya achelewe kuripoti kambini na anaahidi kwamba hatarajii jambo hilo tena.
Phiri alisema kuwa haikuwa rahisi kwa yeye kuondoka na kuiacha familia yake bila ya kutatua matatizo aliyokuwa nayo (hakuyaweka wazi) na kwamba kwa muda wote alikuwa akiwafahamisha viongozi wa Simba kuhusu maendeleo yake.
"Najua kwamba nimechelewa, nawaomba mnisamehe, nitatumia muda uliobakia kuinoa timu ili ifanye vizuri katika Ligi Kuu na mashindano ya kimataifa mapema mwakani," alisema kocha huyo ambaye alilakiwa na baadhi ya wanachama kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.
Alisema kuwa pamoja na kuchelewa lakini pambano dhidi ya watani zao, anaamini watashinda kwa vile timu yao ni nzuri kuliko watani zao.
Simba na Yanga zinatarajiwa kupepetana kwenye pambano la Ngao za Hisani kuzindua msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara, mechi itakayochezwa Agosti 14.
Phiri aliondoka jijini Dar es Salaam na kuelekea Zanzibar kuungana na timu ambayo imeweka kambi tangu wiki iliyopita ikiwa chini ya makocha Syllersaid Mziray, Suleiman Matola na Amri Said.
Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Godfrey Nyange 'Kaburu' aliliambia gazeti hili kwamba mkataba wa kocha huyo umebakiza miezi michache na baada ya kumalizika uongozi utafanya upya mazungumzo naye kabla ya kuongeza mkataba mwingine.
Simba iliyopangwa kuanza ligi kwa kucheza na African Lyon, itacheza mechi ya kirafiki na Express ya Uganda Jumapili kwenye Uwanja wa Uhuru.

Chuji, Kaseja warejeshwa Stars





KIPA mahiri wa klabu ya soka ya Simba na kiungo nyota wa Yanga ambao waliondolewa kwenye timu ya taifa na Mbrazil, Marcio Maximo, wamerejeshwa kikosini humo na kocha mpya wa timu hiyo, Mdenmark, Jan Poulsen.
Akizungumza katika mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari tangu alipowasili nchini Jumamosi usiku kwa ajili ya kurithi mikoba ya kocha Mbrazili Marcio Maximo aliyemaliza muda wake, Poulsen, alisema kuwa alipata taarifa za wachezaji hao na wengine waliowahi kuichezea timu hiyo, lakini ameamua kuwarejesha wawili hao ili kuwapa nafasi ya pili.
"Nimewapa nafasi ya pili ya kuonyesha vipaji vyao, hata kwangu pia, nidhamu ni sehemu ya vigezo vya wachezaji ninaowahitaji, kama watashindwa kuendana na sera zangu nitawaondoa, Boban (Haruna) sijamwita kwa sababu kwa sasa hana timu anayoichezea," alisema kocha huyo.
Mdenmark huyo alisema kwavile yeye ni mgeni na hawafawahamu wachezaji, alianza na wachezaji wa kikosi kilichocheza na timu ya taifa ya Brazili katika mechi ya kirafiki kwa kujua kwamba lazima ndio watakaokuwa wachezaji bora zaidi, kisha akaomba pia majina ya wachezaji wa vikosi vya nyuma na akaulizia kiwango cha kila mmoja hivi sasa na ndipo alipowabaini Kaseja, Chuji na Boban na wengineo.
Alisema wachezaji ambao walikuwepo katika kikosi kilichocheza na Brazil lakini hajawaita, imekuwa hivyo kutokana na kushuka kwa viwango vyao lakini endapo watarejesha viwango vyao atawaita tena huku akianza pia kuangalia vipaji vipya.
Alisema kuwa mipango yake ya muda mfupi ni kuhakikisha Stars inafuzu kucheza fainali zijazo za Kombe la Mataifa ya Afrika na kutwaa ubingwa wa Kombe la Chalenji.
Hata hivyo, alisema hajaja na miujiza na kwamba mafanikio hayapatikani mdomoni bali kila mdau kwa nafasi yake kujituma na kutimiza jukumu lake.
"Mafanikio haya yote hayawezi kupatikana kwa maneno, Kenya nao wanasema wanayataka, Uganda pia wanasema hivyo hivyo, lililo muhimu ni wachezaji kujituma, tunatakiwa tushirikiane kuanzia wachezaji, wadhamini, klabu... sio mimi peke yangu nitakayefanikisha," alisema kocha huyo.
Aliitaja mipango yake ya muda mrefu kuwa ni kuendesha mafunzo mbalimbali kwa makocha wa nchini na kusimamia maendeleo ya timu za vijana ambazo ndio msingi wa mafanikio ya nchi zote zilizoendelea katika mchezo huo.
Alisema kuwa wachezaji 27 aliowaita wataripoti kambini leo jioni na kuanza mazoezi kesho kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Misri 'The Pharaos' itakayofanyika katika jiji la Cairo Agosti 11.
Kikosi kamili alichokiita ni Kaseja, Jackson Chove, Shabani Kado, Shadrack Nsajigwa, Salum Kanoni, Stephano Mwasika, Juma Jabu, Idrissa Rajab, Nadir Haroub 'Cannavaro', Kevin Yondani, Aggrey Morris na Erasto Nyoni.
Wachezaji wengine ni Nurdin Bakari, Abdulhalim Humoud, Henry Joseph, Chuji, Nizar Khalfan, Jabir Aziz, Kigi Makasi, Abdi Kassim 'Babi', Uhuru Suleiman, Suleiman Kassim, Mrisho Ngassa, John Bocco, Mussa Hassan 'Mgosi', Jerryson Tegete na Danny Mrwanda.
Rais wa TFF, Leodegar Tenga, amewataka wadau kumpa ushirikiano kocha huyo mpya na kuongeza kwamba mafanikio hayaji kwa njia ya mkato.
Tenga alisema kuwa kocha huyo atafanya kazi kwa muda wa miaka miwili na akasisitiza kuwa Tanzania haina desturi ya kubadilisha makocha kama nguo.
Alisema pia kwa sasa, kocha huyo atasaidiwa na makocha Juma Pondamali na Syllvester Marsh.
Kaseja alipopigiwa jana alikataa kuzungumzia chochote kuhusiana na maamuzi ya kocha huyo mpya. "Nimesikia taarifa hizo, ila sina chochote cha kusema," alisema.

'Vigogo', Mawaziri wa JK 'chali' CCM







MAWAZIRI kadhaa wa Serikali ya Awamu ya Nne na wabunge wengi waliomaliza muda wao, wameshindwa kuongoza katika mchakato wa kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM), zilizopigwa juzi kuteua wagombea wa ubunge, ingawa wanachosubiri ni kwa sasa ni hatma yao katika vikao vya juu vya chama hicho.

Baadhi ya mawaziri walioanguka katika kinyang'anyiro hicho ni aliyekuwa Mbunge wa Nkenge,Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Diosdorus Kamala pamoja na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendera wa Korogwe Mjini, huku kukiwa na taarifa kwamba Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo, naye ameshindwa kuongoza katika Jimbo la Mbulu.

Mbali na hao, wabunge wengine maarufu wameanguka akiwemo aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM, Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais, John Malecela wa Mtera, ambaye ameshindwa kushika nafasi ya kwanza ambayo ingempa nafasi ya moja kwa moja ya uteuzi, ingawa wakati mwingine matokeo hayo hubadilishwa na vikao vya juu vya CCM.
Kwa mujibu wa Katibu wa CCM Mkoa huo, John Barongo,Malecela alimbwagwa na Katibu wa CCM wilaya ya Tarime, Livingstone Lusinde ambaye ameongoza kwa kupata kura 5,810 huku Malecela akiwa na kura 5,379.

Jimbo la Mpwapwa, George Lubeleje ambaye ameliogoza jimbo hilo kwa miaka 20, ameangushwa na Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Gregory Teu,Lubeleje aliyeambulia kura 4,830 huku Teu akiongoza kwa kura 7,777.

Jimbo la Chilonwa, matokeo ya awali yanaonesha Hezekiah Chibulunje anaongoza kwa kura 5,267 ambapo Joel Mwaka akiwa na kura 3,848, katika kata 8 kati ya kata 13.

Barongo alifafanua kuwa, kwa upande wa Jimbo la Kondoa Kaskazini, matokeo ya awali yalionesha kuwa Zabein Mhita alikuwa akiongoza ra 6,211, Mohamed Rashid akiambulia kura 2,116.

Jimbo la Kondoa Kusini, matokeo ya awali ya kata 11 kati ya kata 20, mtangazaji wa zamani wa TBC, Juma Nkamia alikuwa akiongoza kwa kura 4,249 huku akifuatiwa na Paschal Degera kura 632 huku aliyekuwa Katibu wa Bunge, Damian Foka akiambulia kura 545.

Jimbo la Kibakwe, George Simbachawene alikuwa akiongoza kwa kupata kura 8,824 akifuatiwa na Acray Galawika mwenye 2,537.Jimbo la Bahi, Donald Mejiti aliongoza kwa kupata kura 2,627 akifuatiwa na Omar Baduel mwenye kura 2,268.

Jimbo la Dodoma Mjini ambalo lilikuwa na wagombea 19, Peter Chiwanga alikuwa akiongoza kwa 3,183 katika kata 18 kati ya kata 37, huku akifuatiwa na David Malole mwenye kura 2,479 naaliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Adam Kimbisa akipata kura 2,141.

Kwa upande wa Dar es Salaam, matokeo mengi yalikuwa hayajafika katika ofisi za wilaya. Matokeo ya awali katika Jimbo la Temeke yanaonesha kuwa Abass Mtemvu alikuwa anaongoza katika kata nne za Miburani, Sandali na Mtoni.

Alifuatiwakwa mbali na Salimu Chicago wakati Hiza Tambwe katika kata hizo aliambulia nafasi ya tatu. Katika Jimbo la Kigamboni, Faustine Ndungulile alikuwa anaongoza katika kata za Vijiweni, Kimbiji na Mbagala Kuu.

Katika jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu anaongoza na kuwaacha wapinzani wake kwa mbali huku katika Jimbo la Ukonga, Godwin Barongo anaongoza katika kata za Gongo la Mboto, Ukonga, Pugu na Kitunda.

Kwa upande wa Jimbo la Kinondoni aliyekuwa anaongoza ni Idd Azzan ambaye matokeo ya awali katika kata za Kijitonyama, Kigogo, Hananasif pamoja na Mwananyamala huku Shy-Rose Bhanji akimfuatia kwa karibu. Kura za majimbo ya Segerea, Kawe na Ubungo yanatarajiwa kutolewa leo.

Mkoani Kilimanjaro, Mbunge aliyemaliza muda wake katika Jimbo la Vunjo, Aloyce Kimaro, ameanguka baada ya kushika nafasi ya pili kwa kubwagwa na Wakili Crispin Meela.

Akitangaza matokeo hayo, Katibu wa CCM mkoani Kilimanjaro, Stephen Kazidi alisema katika Jimbo la Vunjo, Kimaro alipata kura 3,194, Meela kura 7,162 huku wagombea wengine akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Taifa, James Kombe akipata kura 1,110 na Thomson Moshi kura 788.

Jimbo la Moshi Mjini aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kiusa katika Manispaa ya Moshi, Buni Ramole alishinda kwa kura 1,554 huku wagombea wengine na kura zao katika mabano wakiwa Thomas Ngawaiya (1,539), Justine Salakana (1,152), Gibson Lyamuya (269) na Joseph Mtui (208). Wengine ni Onesmo Ngowi (127), Peter Njambi (110), Athumani Mwariko (109) na Askofu Pius Ikongo (91).

Jimbo la Moshi Vijijini, Dk. Cyril Chami aliongoza kwa kupata kura 9,196 huku mpinzani wake wa karibu, Ansy Mmasi akipata kura 2,791.

Jimbo la Mwanga, Mbunge anayemaliza muda wake, Profesa Maghembe alipata kura 10,743, Joseph Thadayo kura 6,889 na Karia Magalo alipata kura 252.

Hata hivyo, Katibu huyo wa CCM Mkoa, amesema Ngawaiya ameandika barua akilalamika kwamba baadhi ya wanachama wamezuiwa kupiga kura jambo lililomnyima kura ambazo zingempa ushindi.

Jimbo la Rombo, Kazidi alisema Basil Mramba ameongoza kwa kura 8,389, Netburga Masikini kura 2,946, Lemunge Lesfory kura 854 na Stambul Vitus kura 779.

Jimbo la Same Magharibi, Dk. Mathayo David ameongoza kwa kura 14,281, sawa na asilimia 95, akifuatiwa na John Singo kura 608, Ali Kibwede kura 65 na Lameck Shogholo kura 61.

Jimbo la Hai, Mbunge anayemaliza Fuya Kimbita aliongoza kwa kura 3,725, akifuatiwa na Dastan Mallya (2,649), Aziz Waziri (2,384), Christopher Awinia (1,149), Masumba Meena (939), Lazaro Swai (728), Neema Massawe (456) na Gasper Ngido.

Katika Jimbo la Siha, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri alipita bila kupingwa ndani ya CCM.

Jimbo la Same Mashariki, Mbunge aliyemaliza muda wake, Anne Kilango Malecela, ameongoza kwa kupata kura 7,514 akifuatiwa na mpinzani wake mkubwa, Michael Kadede aliyepata kura 1,804.

Mkoani Singida, Singida Mjini, Mbunge aliyemaliza muda wake, Mohammed Dewji aliongoza kwa kishindo kwa kupata kura 8,997, sawa na asilimia 95, Hawa Ngulume kura 390 na Mariam Msawira 35.

Jimbo la Iramba Mashariki, Mgana Msindai ameshindwa baada ya kupata kura 3,005 huku aliyeongoza ni Salome Mwambu aliyepata kura 3,635, jimbo hilo lilikuwa na wagombea tisa.

Jimbo la Iramba Magharibi, aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Juma Kilimbah, amebwagwa pia baada ya kupata kura 3,788 ukilinganisha na aliyeongoza, Lameck Mwigulu mwenye kura 3,834.

Jimbo la Kwimba, Mbunge anayemaliza muda wake, Bujiku Sakila amekiri kushindwa na akizungumza kwa simu na gazeti hili jana kutoka Ngudu, makao makuu ya Wilaya ya Kwimba, alisema atakuwa tayari kumuunga mkono mgombea wa CCM, Shanif Mansoor ambaye ni Mhasibu wa CCM mkoa wa Mwanza.

“Kwanza nimeshindwa vibaya, lakini niseme kutoka rohoni mwangu kabisa ni mfumo wa uchaguzi wa kura za maoni ndiyo ulionifanya nishindwe, lakini sitakuwa na malalamiko makubwa maana nikiyatoa kitahitajika, “evidence,“ na mimi sikushindwa kwa kukosa sifa za kuwa Mbunge ila ni system ya uchaguzi ilivyokuwa, kulikuwa na rushwa sana hapa Kwimba
lakini mkamataji hakuwepo,” alisema.

Naibu Waziri huyo wa zamani aisema kwa jinsi alivyoona mazingira ya uchaguzi wilayani Kwimba, alisema Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) hawakufanya kazi yao barabara ya kudhibiti rushwa katika uchaguzi huo wa kura za maoni kwa madai kuwa rushwa katika jimbo hilo ilikuwa kubwa, kiasi cha kuifafanisha Takukuru na mtoto mdogo na wagombea watu wazima.

Jimbo la Ilemela, Mbunge wake, Anthony Diallo ameongoza kwa kupata kura 6,601. Wagombea wengine na kura zao ni Pastory Masota (2,159); John Buyamba (1,837); Samson Maganga (519); Darius Ngocho (450); DC mstaafu Jared Gachocha (365); Ashery Gasabire (357) na Shadrack Fereshi (343).

Katika Jimbo la Sengerema, kwa mujibu wa Katibu wa CCM, Maiko Kahuruda alisema jana kuwa mbunge ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alikuwa anaongoza kwa wingi wa kura akifuatiwa kwa karibu na Francisco Shejamabu.

Kwa Jimbo la Buchosa, Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Dk. Charles Tizeba alikuwa anaongoza akifuatiwa na Eric Shigongo na Mbunge aliyekuwa anashikilia jimbo hilo, Samuel Chitalilo alikuwa wa tatu.

Jimbo la Misungwi, Kahuruda alisema Charles Kitwanga “Mawe Matatu” alikuwa akiongoza kwa kupata kura 9,104 katika kata tisa kati ya 27 zilipokewa matokeo yake huku akifuatiwa na Mbunge aliyemaliza muda wake, Jacob Shibiliti na Madoshi Makene akishika nafasi ya tatu.

Majimbo ya Sumve na Magu, matokeo yao yalikuwa yakiendelea kukusanywa, wakati katika Jimbo la Nyamagana, matokeo ya awali yaliyotolewa jana na Katibu wa CCM Wilaya, Musa Matoroka yalionesha kuwa Mbunge wa sasa, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha alikuwa anaongoza kwa kupata kura 8,627, akifuatiwa na John Marogori aliyepata kura 2420.

Wagombea wengine na kura zao kwenye mabano ni Joseph Kahungwa (1,941); David Mtetemera (570); Wilson Swalala (492); Robert Masunya (396); Stephen Deya (286); Maseke Magaiwa (315); Stephen Deya (286); Abdi Chakechake(271); William Mvanga (220); Boniface Kahangara (162); na Ibrahim Lukumay (124).

Jimbo la Ukerewe, Mbunge aliyemaliza muda wake, Balozi Gertrude Mongella ameongoza kwa kura 6,666 na akifuatiwa na Josephat Lyato aliyepata kura 4,140. Wagombea wengine na kura zao kwenye mabano ni Msafiri Nyandiga (3,530); Oswald Mwizarubi (2,362); Mtani Chitanda (1,822); Deus Tungaraza (967); Ernest Kamando (642); Majige Munyu (284) na Mwibure

Kazi (104).

Jimbo la Busega, aliyekuwa anaongoza ni Dk. Titus Kamani ambaye alikuwa amemuacha mbali sana Dk. Raphael Chegeni

ambaye ni Mbunge anayemaliza muda wake.

Katika Jimbo la Busanda, Mbunge wa sasa, Lolensia Bukwimba alikuwa akiongoza. Jimbo la Nyang’hwale, Mbunge

anayemaliza muda wake, James Musalika ameshika nafasi ya tatu kwa kura 1,200 wakati DC wa Kilombero, Evarist Ndikilo

ana kura 3,125 na aliyeongoza ni Hussein Gulamali kwa kura 4,449.

Mkoani Shinyanga, Jimbo la Shinyanga Mjini, aliyeongoza kwa mujibu wa Katibu wa CCM Mkoa, Mohammed Mbonde, ni

Stephen Masele akiwaangusha wagombea wengine akiwamo aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na

Mbunge mtetezi, Dk. Charles Mlingwa na Mbunge mwingine wa Viti Maalumu, Joyce Masunga;

Jimbo la Solwa aliyeongoza ni Ahmed Salum; Jimbo la Meatu ni Salum Khamis ‘Mbuzi’; Jimbo la Kishapu ni Suleiman Nchambi’s na Jimbo la Bariadi Magharibi ni Andrew Chenge.

Katibu huyo wa CCM Mkoa aliwataja wengine waliongoza ni Emmanuel Luhahula (Bukombe); Peter Bunyungoli (MaswMashariki); Simon Robert (Maswa Magharibi); Martin Makondo (Bariadi Mashariki); Luhaga Mpina (Kisesa); James Lembeli (Kahama). Katika Jimbo Mbogwe, Augustine Masele anaongoza kwa kura nyingi.

Jimbo la Nkenge, Mbunge aliyemaliza muda wake, Dk. Diodorus Kamala ameanguka kwa kushika nafasi ya pili baada ya nafasi ya kwanza kuchukuliwa na Asumpta Mshamu.

Kamala ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, amepata kura 6,184 wakati Mshama amepata kura

9,055. Wagombea wengine ni Dickson Balyagati (4,123), Julius Rugemarila (771), Charles Katarama (410), Ismail

Suleiman (239) na Amani Kajuna kura 146.

Jimbo la Ngara, Mbunge wa sasa, Profesa Feetham Banyikwa alikuwa anashika nafasi ya tatu kwa kuwa na kura 2,112,

wakati anayeongoza ni Deo Ntukamazima akiwa na kura 3,954 akifuatiwa na Alex Gashaga mwenye kura 3,838.

Jimbo la Chato, Mbunge wa sasa ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk. John Magufuli alikuwa akiongoza kwa kura 8,305 akifuatiwa na Dk. Lukanima mwenye kura 810.

Jimbo la Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki amepita bila kupingwa.

Jimbo la Kyerwa, Mbunge aliyemaliza muda wake, Eustace Katagira ameongoza kwa kura nyingi. Hata hivyo, takwimu hazikuweza kupatikana haraka kutokana na tawi mojawapo katika Kata ya Businde kuendelea kukamilisha taratibu za uchaguzi kabla ya kuunganisha matokeo yote.

Jimbo la Karagwe ambalo pia mchakato wa kuunganisha takwimu uliendelea hadi jioni, matokeo yanaonesha mbunge aliyemaliza muda wake, Gosbert Blandes ameshinda kwa kura nyingi. Aliyeshika nafasi ya pili ni Karim na ya tatu ni Profesa Ngalinda.

Jimbo la Bukoba Vijijini ambako hadi jana jioni matokeo ya kata 20 kati ya 29 yalishapatikana, Jasson Rweikiza

ameongoza kwa kura 18,212. Mbunge aliyemaliza muda wake, Nazir Karamagi ameshika nafasi ya pili kwa kura 4,111 na

kufuatiwa na Novatus Nkwama mwenye kura 4,111.

Wagombea wengine ni Muzamir Kachwamba aliyepata kura 816 na Kamalu Mustafa amepata kura 600.

Mbunge wa sasa wa Biharamulo Magharibi, Oscar Mukasa ameongoza kwa kura nyingi akifuatiwa na Agricola Magoho na

Hamidu Nzomukunda.

Kwa upande wa Muleba Kusini, ingawa hadi jioni mchakato wa kuunganisha kura za kata zilizochelewa ulikuwa

ukiendelea, Profesa Anna Tibaijuka ndiye alitajwa kuibuka mshindi kwa kura nyingi akiwaacha mbali Mbunge wa sasa,

Wilson Masilingi aliyeshika nafasi ya pili. Nafasi ya tatu imeshikwa na Alfred Tibaigana.

Maswa Magharibi, Amani Nzugile Jidulalamabambasi, amefariki dunia jana wakati akiwa njiani kutoka Hospitali ya

Wilaya ya Maswa kwenda Rufaa Bugando kwa uchunguzi na matibabu zaidi baada ya kuwa amelazwa katika hispitali hiyo ya

wilaya tangu Julai 29, mwkaa huu.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dk. Amos Mremi alisema mwanasiasa huyo alikuwa amelazwa kwenye hospitali hiyo

kutokana na uvimbe mkubwa uliojitokeza katika sehemu zake za siri na kutokana na hali yake ilivyokuwa ilibidi apewe

rufaa ya kweda Bugando kwa uchunguzi na matibabu, na jana akiwa njiani kwenda Mwanza pamoja na muuguzi mmoja kwenye

gari la wagonjwa, alifikishwa hadi katika mapokezi ya Bugando, lakini mara tu kufika hospitalini, iligundulika kuwa

amefariki dunia.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Bugando, Dk. Charles Majinge alithibitisha kutokea kwa kifo hicho na kwamba alifikishwa

mapokezi akiwa tayari amefariki dunia, mwili wake ulitarajiwa kurejeshwa wilayani Maswa kwa ajili ya mazishi.

Mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa kiongozi wa UDP, alishika nafasi ya tatu nyuma ya Robert na Shibuda, miongoni mwa

wagombea tisa waliojitokeza.

Jimbo la Chalinze, aliyeongoza ni Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Said Bwanamdogo aliyepata kura 8,144 akifuatiwa na

aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Imani Madega mwenye kura 4,193; Mbunge aliyemaliza muda wake, Ramadhan

Maneno kura 3,623. Jimbo hilo lilikuwa na wagombea 10.

Jimbo la Bagamoyo, Mbunge wa sasa Dk. Shukuru Kawambwa ambaye pia ni Waziri wa Miundombinu, ameongoza kwa kura

6,576, akiafuatiwa Dk. Andrew Kasambala mwenye kura 1,061.

Wabunge waliomaliza muda wao, Dk. Ibrahimu Msabaha (Kibaha Vijijini), Dk. Zainabu Gama (Kibaha Mjini); Profesa

Idrisa Mtulya (Rufiji), nao wameanguka.

Wabunge wa zamani waliopeta katika kinyang'anyiro hicho ni Adam Malima (Mkuranga); Abdul Malombwa (Kibiti) na

Abdulkarim Shah (Mafia)

Wagombea wapya waliochomoza na Silvesta Koka (Kibaha Mjini); Hamidu Abuu (Kibaha Vijijini); Seleman Jafo (Kisarawe)

na Dk.Seif (Rufiji).

Hata hivyo, baada ya matokeo hayo kutangazwa, aliyekuwa Mbunge wa Kibaha Mjini, Dk. Gama aliwasilisha barua kwa

Katibu wa CCM Mkoa wa Pwani, Sauda Mpambalyoto akipinga matokeo ya jimbo lake kwa madai ya uchaguzi kutawaliwa na

mchezo mchafu na rafu za hapa na pale kwa baadhi ya wagombea.

Jimbo la Kasulu Mjini, Neka Raphael ameongoza kwa kura 672 akifuatiwa na Gidion Bunyaga (510); Askofu Gerald Mpango (306); Twalib Mangu (270) na Agnes Nyowola (225).

Jimbo la Kasulu Vijijini, Daniel Nsanzugwanko alikuwa akiongoza kwa kura 1,560 akifuatiwa na Kafonogo Mayengo (625) na Patrick Nyembele (420).

Jimbo la Manyovu, Albert Obama alikuwa akiongoza kwa kura 770; James Japhet (667); Eliadory Kavejuu (300); Betwel Ruhega (300) na mbunge anayemaliza muda wake, Kilontsi Mporogomyi (260).

Jimbo la Muhambwe, Jamal Tamim alikuwa akiongoza kwa kura 2,921 akifuatiwa na Richard Kigaraba (); Mbunge wa sasa, Felix Kijiko (1,523); mbunge wa zamani Arcardo Ntagazwa (577) na Edgar Mkosomali (922).

Mkoani Iringa, hatima ya wabunge Joseph Mungai, Monica Mbega, Jackson Makweta, Profesa Raphael Mwalyosi, Benito

Malangalila na Yono Kevela, kurudi kwa mara nyingine tena katika vikao vya Bunge lijalo, kutategemea zaidi maamuzi ya juu ya vikao vya CCM, baada ya taarifa za awali kuonesha kuwa wameshindwa kura za maoni.

Hata hivyo, mpaka tunakwenda mitambani ofisi za chama za majimbo hayo zilikuwa hazijatoa taarifa rasmi, na Katibu wa CCM wa Mkoa, Mary Tesha alipoulizwa, alisema ofisi yake inaendelea kupokea matokeo kutoka katika majimbo yote ya uchaguzi.

Taarifa za awali za uhakika kutoka katika majimbo hayo zinaonesha kwamba wakati Mahamudu Mgimwa ameibuka kidedea katika Jimbo la Mufindi Kaskazini lililokuwa likiongozwa na Mungai, Deo Sanga (Jah People) ameibuka kidedea katika Jimbo la Njombe Kaskazini lililokuwa likiongozwa na Makweta.

Mbega (Iringa Mjini) ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro atalazimika kurudi haraka iwezakanavyo mkoani humo

kuendelea na majukumu mengine ya kiserikali baada ya kushindwa katika kura hizo zilizompa ushindi aliyekuwa Katibu

Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Frederick Mwakalebela.

Mwakalebela anaongoza kwa kuwa na kura 3,897, Mbega 2,989 na Yahaya Msigwa 1,217. Ludewa, Mbunge wa sasa Profesa

Mwalyosi amebanwa na Deo Filikunjombe ambaye matokeo ya awali yanaonesha amepata kura zaidi ya 6,000 huku Profesa

Mwalyosi akipata kura zaidi ya 4,000.

Dalali maarufu Kevela wa Njombe Magharibi, naye anadaiwa yuko katika wakati mgumu dhidi ya Mbunge aliyemtangulia

Thomas Nyimbo, huku taarifa kutoka Jimbo la Mufindi Kusini nazo zimethibitisha kwamba Benito Malangalila naye

ameshindwa kuongoza katika kura za maoni za jimbo hilo. Mendradi Kigola anaongoza katika jimbo hilo.

Katika Jimbo la Kilolo, Venance Mwamoto ameshindwa kumpiku Mbunge aliyemaliza muda wake, Profesa Peter Msolla

aliyepata zaidi ya kura 18,000 dhidi ya kura zake zinazodaiwa kuwa zaidi ya 3,000.

Jimboni Makete, mbunge aliyemaliza muda wake, Dk. Benelith Mahenge amejihakikishia kurudi bungeni kwa awamu ya pili,

kama ilivyo kwa Njombe Kusini kwa Naibu Spika, Anne Makinda.

Kutoka Isimani, Katibu wa CCM wa wilaya ya Iringa, Luciano Mbosa alisema jana kwamba William Lukuvi ameshinda kura hizo kwa kujinyakulia kura 7,996 dhidi ya kura 533 za Festo Kiswaga, 286 za Leonard Mwali na Yahaya Mtete aliyepata kura 176.

Huko Kalenga, Mbosa alisema shughuli ya ujumlishaji kura inaendelea hata hivyo taarifa za awali zinaonesha kwamba Dk William Mgimwa amepata kura 2,819 akifuatiwa na Abbas Kandoro aliyepata kura 2,353 na Hafsa Mtasiwa aliyepata kura

1,553.

Mkoani Mbeya, Mbarali, Mbunge anayemaliza muda wake, Estherina Kilasi amekuwa wa tatu akiwa na kura 614, huku

akiongoza Modestus Kilufi kura 1,521 na wa pili ni Burton Kihaka (1,322). Ileje ni Aliko Kibona (5,844), Ambonesigwe

Mbwaga (2,200) na Godfrey Msongwa (2,004).

Lupa, Mbunge aliyemaliza muda wake, Victor Mwambalaswa ameongoza kura 6,135 dhidi ya aliyewahi kuwa Mbunge na

Waziri, Njelu Kasaka (4,135). Songwe, Mbunge aliyemaliza muda wake, Dk. Guido Sigonda amepata kura 780; aliyeongoza

ni Philipo Mulugo (7,100); Paul Ntwina (1,618) na Hamad Juma (962).

Kyela, Mbunge ambaye alikuwa kinara katika mapambano ya ufisadi, Dk. Harrison Mwakyembe ameongoza kwa kura 7,681 dhidi ya George Mwakalinga (574) na Elias Mwanjala (512).

Rungwe Mashariki, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya ameongoza kwa kupata kura 4,240 dhidi ya Stephen Mwakajumulo (228). Rungwe Magharibi, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa ameongoza kwa kura 6,974, dhidi ya Richard Kasesela (5,843) na Frank Magoba (1,379).

Mbeya Mjini, Mbunge aliyemaliza muda wake, Benson Mpesya ameongoza dhidi ya Mbunge wa Kuteuliwa, Thomas Mwang’onda kwa kupata kura 5,586 dhidi ya kura 3,362.

Mbeya Vijijini, Mbunge aliyemaliza muda wake, Mchungaji Luckson Mwanjale ameongoza kwa kura 7,353 dhidi ya kura 1,902 za Andrew Saile.

Mkoani Tabora, Jimbo la Urambo Mashariki, Samuel Sitta alikuwa akiongoza kwa kura 6,130 dhidi ya Masoud Maswanya

mwenye kura 2,432 na Ali Karavina kura 464. Jimbo la Urambo Magharibi (sasa Kaliua), Profesa Juma Kapuya anaongoza

kwa kura 5.656 dhidi ya Ramadhan Kalla mwenye kura 751.

Jimbo la Nzega, Hussein Bashe alikuwa akiongoza kwa kura 6,815 na Lucas Selelii ambaye niMbunge aliyemaliza muda

wake, ana kura 1,420.

Jimbo la Bukene, Mbunge aliyemaliza muda wake, Teddy Kasella-Bantu ana kura 1,968 na Suleiman Zeddy ana kura 1,727.

Sikonge ni George Kakunda anaongoza kwa kura 1,570 dhidi ya Mbunge anayemaliza muda wake, Said Nkumba mwenye kura

1,365.

Tabora Mjini, Ismail Aden Rage anaongoza kwa kura 4,145 dhidi ya Mwanne Mchemba ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu

mwenye kura 2,985 na mbunge wa jimbo hilo, Siraju Kaboyonga ana kura 835.

Mkoani Lindi, Jimbo la Mchinga, Said Mtanda alikuwa akiongoza katika kata nane kati ya 10, kwa kuwa na kura 3,768

dhidi ya kura 1,577 za Mbunge aliyepita, Mudhihir Mudhihir.

Jimbo la Nachingwea, Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe ameongoza kwa kura 5,887, akifuatiwa na DC wa

zamani wa Bukoba Mjini, Albert Mnali (3,912), Elias Masala (1,844), Maokola Majogo (1,191), Ally Mpelemba (450),

Fulgence Mpelembe (126) na Benito Ng’itu (266).

Mkoani Katavi, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amepita bila kupingwa katika Jimbo la Mlele (zamani Mpanda Mashariki),

lakini wabunge watatu wa zamani wameanguka.

Jimbo la Sumbawanga Mjini, Aeshy Hillaly ameongoza kwa kupata kura 867 dhidi ya Mbunge wa Viti Maalumu, Elieta

Switi 155; Edson Makallo (54); James Kusulo (26); Frolence Mtepa (25); Emmanuel Msingezi (18); Joseph Malikawa

(38).

Jimbo la Nkasi Kaskazini, ameongoza Mohamed Keissy (1,557); Hiporitus Matete (1,173), DED wa Kilosa, Ephrem

Kalumalwendo (1,003), mbunge anayemaliza muda wake, Ponsiano Nyami (695), S. Khamsin (319) na V. Konga (51). Jimbo

la Nkasi Kusini, aliyeongoza ni Desderius Mipata (719); Joseph Walingozi (348); Emmanuel Sungura (45); J. Mwanansau

(23); Joseph Kitakwa (58).

Jimbo la Kwela, ameongoza Ignas Malocha (5,772); Meja January Kisango (1,772); Didas Mfupe (1,669); Steven

Chambanenje (796); Patrick Maufi (329); Solomon Jairos (66) na Bendicto Chapewa (227). Jimbo la Kalambo, Josephat

Kandege ameongoza kwa kura (5,597) dhidi ya Ludovick Mwananzila (4,061) na Paul Mwanandeje.

Mkoani Mtwara, Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia ameongoza katika Jimbo la

Mtwara Vijijini huku Vita Kawawa akiongoza Jimbo la Namtumbo.Mkoani Tanga, Bendera ameshindwa na Yussuf Nasir kwa

kupata kura 2,258 dhidi ya Nasir aliyeongoza kwa kura 2,513.

Pangani, Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, ameshinda Mbunge aliyemaliza muda wake, Risherd Abdallah kwa kura 4,391 dhidi ya 2,442.

Tanga Mjini, Omar Nundu ameongoza kwa kura 7,445 dhidi ya Harith Mwapachu aliyepata kura 2,156 ambaye ni Mbunge aliyemaliza muda wake.

Wakati huo huo, aliyekuwa Mbunge wa Tarime kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Charles Mwera ameshindwa kutetea kiti hicho baada ya kubwagwa na mwanachama mwenzake, Mwita Waitara ambapo Waitara alipata kura

131 akifuatiwa na Mwera aliyepata kura 113. Wagombea John Heche kura 92 na Philipo Nyanchini aliyepata kura 10.

Upande wa Viti Maalumu kwa wagombea wa Chadema Tarime aliyeshinda ni Mary Nyagabona aliyepata kura 58 na kuwashinda Ester Matiko aliyepata kura 54, wengine ni Tekra Johanes kura nne na Mwenyekiti wa Wanawake wa Chadema Taifa, Leticia Mosore hakupata kura.

Tuesday, July 27, 2010

DC mikononi mwa Takukuru *Anawania ubunge viti maalum *Akamatwa na wapambe wake, fedha gesti

MKUU wa Wilaya ya Kasulu, Betty Machangu, ni miongoni mwa mavuno mapya ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) katika operesheni ya kukamata wagombea ubunge wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya kugawa fedha.

Machangu alikamatwa juzi na maofisa wa Takukuru mkoani Kilimanjaro pamoja na vigogo wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) wa mkoani wa Kilimanjaro
na wa Wilaya ya Moshi Vijijini.

Mkuu huyo wa wilaya ambaye amejitosa kwenye kinyang’anyiro cha kusaka ubunge kupitia viti maalum mkoani Kilimanajro, alikamata na kuhojiwa kisha kuachiwa.

Machangu anadaiwa kutoa rushwa kwa wajumbe wa UWT mkoa ili wamchague.

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Kilimanjaro, Alexander Budigila, aliwataja
watuhumiwa wengine kuwa ni Katibu wa UWT mkoa, Mariam Kaaya, Katibu wa
UWT wilaya ya Moshi, Hadija Ramadhani, mfanyabiashara wa Moshi
mjini, Hawa Sultani na dereva wa gari alilokuwa wakitumia, Swalehe
Twalibu.

Alisema Takukuru ilipokea taarifa kutoka kwa raia mwema za kuwepo vitendo vya rushwa katika nyumba ya kulala wageni ya Safari Resort, ambapo walikuwa wakigawa rushwa ya fedha na vitu kwa wajumbe kwa kila mmoja kuingia mmoja mmoja kuanzia majira ya saa 8:30 mchana.

Tarifa hiyo ilionyesha kuwa mgombea huyo na wafuasi wake walikuwa wakigawa fedha kiasi cha Sh. 100,000 na 50,000, kanga, asali na vipeperushi na kadi za wajumbe wa mkutano mkuu wa UWT mkoa.

“Tuliizingira nyumba hiyo kuanzia majira ya saa nane hadi saa 10 ndipo tulipoingia ndani na kuwataka kufungua chumba namba 24 ambako
mgombea huyo na viongozi hao walikuwa wamejifungia huku dereva wa gari
lenye namba za usajili T 688 APQ aina ya Mitsubishi ambaye alikuwa anaimarisha ulinzi kwa kila anayefika,” alisema

Alisema walikaa kimya hadi saa 1:30 bila kufungua na ndipo maafisa wa
Takukuru walipojitambulisha na kugonga mlango kwa nguvu zaidi na
majira ya saa 2:15 usiku, ambapo ndipo walifanikiwa kuingia ndani na
kuwakuta watu wanne.

Alisema baada ya upekuzi walikuta Sh. 400,000 kwenye pochi ya katibu wa UWT, pea nne za vitenge, vipeperushi vya kumnadi mgombea
huyo, kadi za wajumbe wa mkutano mkuu wa UWT mkoa ambazo zilitumbukizwa
kwenye chombo cha kuingiza maji chooni (tanki la chooni).

Alisema pia walikamata Sh.100,000 zikiwa kwenye pochi ya mgombea huyo, ambazo ziliwekwa kwenye bahasha na kuandikwa majina, lakini baada ya kuhisi watakamatwa walizitoa kwenye bahasha na
kuzichanachana na kisha kuzitupa chini ya uvungu wa kitanda.

Budigila alisema pia kwenye pochi ya katibu huyo walikuta vipeperushi
vya mgombea mwingine Regina Chonjo ambaye pia ni Mwenyekiti wa UWT mkoa na walifanikiwa kulikamata gari hilo ambalo ni mali ya mgombea huyo.

Machangu akizungumza na wanahabari alisema kuwa majira ya saa 10 ndio
alikwenda kwenye baa hiyo kwa lengo la kupata chakula cha mchana na kwamba baada ya kufika alitafuta mahali penye utulivu, ili azungumze
na viongozi na msaidizi wake kabla ya kwenda kwenye mkutano wa kampeni.

Alisema walikosa pa kukaa na kumua kwenda kukaa chumbani na hakukua na
rushwa yoyote iliyotolewa kwa kuwa kila mmoja alikuja na mkoba wake na
hata kama angetaka kutoa rushwa angewafuata majumbani mwao.


Takukuru yashikiria saba

Wakati huo huo, Takukuru inawashikilia na kuwahoji watu saba waliodaiwa kuwa mabalozi, wajumbe wa vijiji na makatibu wa CCM katika kata ya Shirimatunda ambao wanadaiwa walikuwa wakila na kunywa na mgombea
udiwani mmoja.

Habari zinasema baada ya maafisa wa Takukuru kufika watu hao walikimbia akiwemo mgombea huyo na kwamba walifanikiwa kuwakamata watu hao kati
ya 30 waliokuwa wamekaa na mgombea huyo wakiwa na kikao cha kushawishi
mgombea huyo kupitishwa.

Kamanda wa Takukuru mkoani hapa alisema uchunguzi wa kina wa matukio hayo yote unaendelea na baada ya kukamilika watafikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa mujibu wa sheria.

Dodoma wataka
matokeo yafutwe

Baadhi ya wagombea udiwani wa Viti Maalum kupitia UWT katika Wilaya ya Dodoma Mjini, wametaka matokeo yafutwe na uchaguzi urudiwe kutokana na uchaguzi huo kutofanyika kwa haki.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi ya CCM mkoa, mmoja wa wagombea hao, Catherine Mbiligwa, alisema uchaguzi huo haukuwa wa huru na haki kutokana na mmoja wa wasimamizi uchaguzi (jina tunalo) kutoa kauli za matusi kwa wagombea na wajumbe waliokuwepo kwenye uchaguzi huo.

Alisema moja ya sababu za kuomba uchaguzi huo kurudiwa ni kutokana na wagombea hao kutopata nafasi ya kuhesabu kura zao wala kuweka mawakala wao.

“Tulipojaribu kumuomba tuweke mawakala wetu kama haki yetu, tulifukuzwa kama mbwa na askari pamoja na katibu wa UWT wakishirikiana na msimamizi wa uchaguzi,” alisema.

Aidha, mgombea huyo alisema wakati wa kupiga kura pia hapakuwa na masanduku ya kutosha ya kuwekea kura, badala yake kura nyingine zililazimika kufungwa kwenye kanga za wajumbe.

Mgombea mwingine, Mwajuma Yame, alisema mbali na kutotendewa haki katika uchaguzi huo, pia hapakuwapo na uwiano wa nafasi za viti maalum kwa kila tarafa.

“Kila tarafa inatakiwa kuwa na madiwani watatu wa viti maalum, lakini tarafa zingine zina kata chache tofauti na Dodoma Mjini ambapo kuna kata takribani 20, lakini nafasi za viti maalum ni nne tu…Tunaomba uwiano,” alisema.

Akampeni harusini

Mgombea udiwani anaye maliza mda wake katika Kata ya Tambukareli Manispaa ya Dodoma, Edward Lamali, amejikuta akifanya kampeni katika ukumbi wa harusi.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Hall Cross, ambapo diwani huyo aliteuliwa na ndugu kutambulisha wageni pamoja na kuwapa nasaha maharusi katika maisha yao ya ndoa.

Diwani huyo alitoa utambulisho huo kama alivyoagizwa, lakini kabla ya kuhitimisha alianza kupiga kampeni kwa kuwataka wageni waalikwa kumpigia kura za maoni wakati utakapowadia.

Aliwaomba wamchague kwa mara nyingine ili aendelee kuyamalizia mambo ambayo alikuwa ameshaanza kuyatekeleza kwa kipindi kilichopita.

Mwangunga akumbana na Loliondo jimboni Ubungo
Mgombea wa ubunge Jimbo la Ubungo, Shamsa Mwangunga, amezidi kubanwa na wanachama baada ya kuambiwa kuwa kama alishindwa kuwasaidia Wamasai wa Loliondo mkoani Arusha wasinyang'anywe ardhi na mwekezaji, atawezaje kutatua kero zinazowakabili wananchi wa Mabibo, jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa wanachama wa CCM alimbana mgombea Mwangunga ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii kwenye mkutano wa kujinadi wagombea uliofanyika Mabibo na kukutanisha matawi manne.

“Ukiwa kama Waziri wa Maliasili na Utalii ulishindwa kuwasaidia wafugaji hao ambao serikali ilidai kuwa waliingia eneo la hifadhi ya Taifa je, utaweza kutusaidia sisi?” alihoji mwanachama huyo.

Baada ya kuulizwa swali hilo, Mwangunga alishangaa kisha alimjibu kuwa wafugaji hao ndiyo waliovunja sheria na kuingia eneo la hifadhi hivyo serikali iliwaondoa kwa kuzingatia sheria.

Hata hivyo, mwanachama huyo alionekana kutoridhika na jibu hilo ingawa alilikubali na kukaa chini ili kumpa mwenzake aendelee kuuliza
swali lingine.

Maghari ya kifahari yatumika

Wakati huo huo, wagombea wa CCM wamezidi kuonyeshana ufahari wa kuwa na magari ya gharama wakati wa kampeni zao zinazoendelea maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam licha ya chama chao kuwataka wasitumie vyombo hivyo na badala yake wapande basi moja.

Baadhi ya magari hayo yaliyoonekana kuvinjari maeneo ya mikutano ni yenye namba za usajili, T 626 AEX aina ya Toyota Land Cruiser Prado, T 780 AZJ aina ya Nissan Patrol na T257 AQT Toyota Land Cruiser VX ambayo yalikuwa yakitumiwa na wagombea katika jimbo la Segerea.

Katika jimbo la Ubungo nalo, Mwangunga alionekana akiwa ndani ya gari lake aina ya Land Cruiser huku wagombea wenzake wakiwa kwenye basi la pamoja kama chama kilivyowataka kufanya.

Akizungumza na NIPASHE siku ya kwanza ya kuanza kampeni hizo, Katibu Msaidizi wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Abihudi Shilla, alisema wagombea wote hawaruhusiwi kutumia magari yao wala kuvaa suti au nguo nyingine tofauti na zile za chama.

Alisema chama kimeweka utaratibu huo ili wagombea wote waonekane wapo sawa kwa wanachama badala ya kila mmoja kufanya mbwembwe za kila aina ili kuwakoga wanachama.

Shy-Rose aibuka
na staili mpya

Mchakato wa kura za maoni kwa wagombea wa CCM Jimbo la Kinondoni umeendelea kuwa na vituko na moja ya matukio na vituko hivyo ni mmoja wa wagombea kutembea kwa gwaride mbele ya wanachama na kuwapigia magoti kuomba kura.

Mgombea huyo, Shy-Rose Bhanji, jana alitumia staili hiyo katika ukumbi wa DDC Magomeni Kondoa alipokuwa akiomba kura kutoka kwa wanaCCM wakazi wa Kata ya Ndugumbi.

Bhanji alitembea kwa gwaride wakati wa kujitambulisha na kupiga magoti kabla ya kuondoka kwa gwaride na kushangiliwa kwa makofi mengi.

Akijibu swali aliloulizwa la jinsi gani ataweza kupambana na dawa za kulevya na kitu gani alichowafanyia vijana kichama, Bhanji alisema kuwa atatetea kero mbalimbali ikiwemo ya kudhibiti matumizi ya dawa za kulevya kwa vijana, kusaidia wajane kwa kuunda vikundi vya maendeleo.


Kigamboni wazozana

Kampeni katika Jimbo la Kigamboni jana zilikumbwa na mzozo baada wagombea ubunge kutaka kuwabana makatibu wa matawi na wanachama wao kususia kikao cha kampeni.

Matukio hayo yametokea katika mikutano ya katika Kata za Kibada na Mjimwema wakati wagombea hao walipokwenda kujinadi kwa wanachama.

Katika kata ya Kibada, wagombea ubunge walifika katika eneo la mkutano majira ya saa 4:00 asubuhi, lakini walijikuta wakiwa peke yao bila ya kupokewa na wenyeji, baada ya viongozi na wanachama kutokuwepo eneo hilo.

Kutokana na hali hiyo, baadhi walionekana kuja juu wakidai kuna dalili ya kuchezewa rafu, kwa sababu haiwezekani wasione hata mwanachama mmoja akiwa eneo la mkutano.

Juhudi za kusubiri wapiga kura ziligonga ukuta, baada ya mratibu wa kampeni hizo, Jimbo la Kigamboni, Sophia Kinega, kuwaagiza wagombea hao kujinadi mbele ya wanachama 50 pekee kati ya wapigakura 1,500 waliotakiwa kuwepo kwenye mkutano huo.

Akielezea tukio hilo, Mratibu huyo alisema hali hiyo ilisababishwa na makatibu wa matawi kususia kutoa taarifa kwa wanachama wao kwa sababu zisizoeleweka.

“Kwa kweli ni hali ya kusikitisha, nimewasiliana na katibu wa kata, lakini ameniambia makatibu wa matawi wamesusa na ndio maana hata wanachama hawakufika, jambo hili ni baya na ni lazima nilifikishe mbele,” alisema Kinega.

Mjumbe mmoja aliyejitaja kwa jina la Mohamed Namwogo, alisema kwa ujumla taarifa ya kuwepo kwa mkutano huo waliipata usiku na kusababisha wengi wao kushindwa kufika.


Nusura wapigane mkutanoni

Katika hatua nyingine, wagombea watatu nusura wapigane ngumi kwa madai kuwa mgombea mmoja alikuwa akieneza maneno yanayohusiana na ubaguzi wa kikabila.

Wagombea hao, John Kibaso na Magige Kiboko walimtuhumu Kazimbaya Makwega kwa kueneza maneno yanaoonyesha ishara ya kuwatenga kwa sababu wao wanatoka Mkoa wa Mara.

Tukio hilo lilitokea katika kituo cha Kata ya Mjimwema kabla ya kuanza kwa mkutano, ambapo wagombea hao walionekana kupandwa na hasira na kutishia kumtwanga ngumi kwa maelezo kuwa wamechoshwa na maneno yake.

“Haiwezekani bwana kila akisema utamsikia huyu mtu wa Musoma, sasa u-Musoma wetu unakuja vipi hapa, usitubabaishe bwana,” alisema Kibaso kwa hasira na kumfuata Makwega sehemu aliyokuwa amesimama.

Baada ya kuona hali imekuwa mbaya, baadhi ya wagombea waliingilia kati na kuwaingiza ndani ya gari wagombea hao na kuwasihi wapunguze jazba kwani wote ni wamoja.

Hata hivyo, wagombea wote walijinadi mbele ya wanachama na kuelezea mikakati na mipango yao ikiwa watachaguliwa.

Chanzo:GAZETI LA NIPASHE

Rais wa Tandale aja na filamu ya Mbagala


=============================


KIBAO cha 'Kwetu Mbagala' kinachozidi kutamba nchini cha msanii Naseeb Abdul 'Diamond' a.k.a 'Rais wa Tandale' kinatarajiwa kutengenezewa filamu itakayopewa jina hilo hilo la 'Mbagala'.
Akizungumza na Blog hii, Diamond, alisema tayari ameshaanza maandalizi ya kufyatua filamu hiyo ambayo itawashirikisha wasanii nyota wa fani hiyo akiwemo Jacqueline Wolper.
Diamond alisema lengo la kutoa filamu hiyo ni kutaka kufafanua ukweli juu ya kibao chake ambacho kimekuwa kikilalamikiwa na baadhi ya wapenzi na mashabiki wa fani hiyo wakazi wa eneo hilo la jijini wakidai amewadhalilisha.
"Baada ya kibao changu cha 'Mbagala' kutamba, natarajia kuja na filamu yenye jina hilo ambayo itawashirikisha wasanii kadhaa nyota, akiwemo Wolper, mimi mwenyewe na wengineo ambao wataifanya iwe ya kiwango," alisema Diamond.
Aliongeza kuwa kutoka kwa filamu hiyo kutamaliza 'ubishi' juu ya ukweli kama kibao chake cha 'Mbagala' kilikuwa kinalenga kuwadhalilisha wakazi wa Mbagala au alitumia jina hilo kupata vina vya wimbo huo, ilihali alikuwa akilenga maskani yake ya Tandale alipokulia.
"Mengi yamesemwa juu ya kibao hiki, lakini itakapotoka filamu yake ndio watu watajua mimi sikuwa na nia mbaya ya kusanifu kitongoji hicho, ila nililazimika kutumia jina lake kufikisha ujumbe juu ya mkasa wa kimapenzi na eneo letu nililokulia la Tandale," alisema

RATIBA LIGI KUU YA VODACOM 2010-2011







IFUATAYO NI RATIBA YA LIGI KUU YA VODACOM, VPL- 2010-2011 ILIYOTOLEWA NA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA, TFF, AMBAYO INATARAJIWA KUANZA AGOSTI 21, MWAKA HUU;


JUMAMOSI, Agosti 21
African Lyon v Simba
Polisi Dodoma v Yanga
AFC v Azam
Majimaji v Mtibwa Sugar
Toto African v Ruvu Shooting
Kagera Sugar v JKT Ruvu

JUMAMOSI, Agosti 28
Majimaji v African Lyon
Polisi Dodoma v Mtibwa Sugar
Kagera Sugar v Ruvu Shooting
Toto African v JKT Ruvu

JUMAMOSI, Septemba 4
Polisi Dodoma v Toto African
JKT Ruvu v Majimaji
African Lyon v AFC

JUMAMOSI, Septemba 11
AFC v Yanga
Azam v Simba

JUMATANO, Septemba 15
Kagera Sugar v Azam
Mtibwa Sugar v Yanga
Simba v Ruvu Shooting

Jumamosi Septemba 18
Toto African v Azam
Yanga v Majimaji
Ruvu Shooting v AFC
Mtibwa Sugar v Kagera Sugar

JUMAPILI, Septemba 19
Simba v Polisi Dodoma

JUMATATU, Septemba 20
African Lyon v JKT Ruvu

JUMATANO, Septemba 22
Ruvu Shooting v POlisi Dodoma
Yanga v Kagera Sugar
Majimaji v AFC

ALHAMISI, Septemba 23
JKT Ruvu v Mtibwa Sugar

IJUMAA, Septemba 24
Azam v African Lyon

JUMAMOSI, Septemba 25
Simba v Toto African
Majimaji v Polisi Dodoma

JUMAPILI, Septemba 26
Yanga v Ruvu Shooting

JUMATATU, Septemba 27
African Lyon v Kagera Sugar
AFC v Toto African

JUMANNE, Septemba 28
Azam v JKT Ruvu

JUMATANO, Septemba 29
Mtibwa Sugar v Simba

JUMAMOSI, Oktoba 2
Mtibwa Sugar v Toto African
Ruvu Shooting v African Lyon
Kagera Sugar v Polisi Dodoma
AFC v JKT Ruvu
Majimaji v Azam

JUMAMOSI, Oktoba 16
Simba v Yanga

JUMATANO, Oktoba 20
Simba v AFC
Mtibwa Sugar v Azam
Polisi Dodoma v African Lyon
Toto African v Kagera Sugar
Ruvu Shooting v Majimaji

ALHAMISI, Oktoba 21
JKT Ruvu v Yanga

JUMAMOSI, Oktoba 23
JKT Ruvu v Simba
Ruvu Shooting v Mtibwa Sugar
AFC v Polisi Dodoma
Toto African v African Lyon

JUMAPILI, Oktoba 24
Azam v Yanga
Kagera Sugar v Majimaji

JUMATANO, Oktoba 27
Toto African v Majimaji
Mtibwa Sugar v AFC
Yanga v African Lyon
Polisi Dodoma v Azam
Kagera Sugar v Simba

ALHAMISI, Oktoba 28
JKT Ruvu v Ruvu Shooting

IJUMAA, Oktoba 29
African Lyon v Mtibwa Sugar

JUMAMOSI, Oktoba 30
Azam v Ruvu Shooting

JUMAPILI, Novemba 7
Polisi Dodoma v JKT Ruvu
AFC v Kagera Sugar
Majimaji v Simba
Yanga v Toto

2011
JUMAMOSI, Januari 15
Azam v Kagera Sugar
Toto African v Polisi Dodoma
Majimaji v JKT Ruvu
AFC v African Lyon
Ruvu Shooting v Simba

JUMAPILI, Januari 16
Yanga v Mtibwa Sugar

JUMANNE, Januari 18
Simba v Azam

JUMATANO, Januari 19
Mtibwa Sugar v Polisi Dodoma
Ruvu Shooting v Kagera Sugar

ALHAMISI, Januari 20
African Lyon v Majimaji

IJUMAA, Januari 21
Yanga v AFC
JKT Ruvu v Toto African

JUMAMOSI, Januari 22
Yanga v Polisi Dodoma

JUMAPILI, Januari 23
Simba v African Lyon

JUMATATU, Januari 24
Azam v AFC

JUMATANO, Januari 26
Ruvu Shooting v Toto African
Mtibwa Sugar v Majimaji
JKT Ruvu v Kagera Sugar

JUMATANO, Februari 2
Azam v Toto African

JUMAMOSI, Februari 5
Majimaji v Yanga
Kagera Sugar v Mtibwa Sugar
AFC v Ruvu Shooting
Polisi Dodoma v Simba
JKT Ruvu v African Lyon

JUMAPILI, Februari 13
AFC v Majimaji
Mtibwa Sugar v JKT Ruvu
Polisi Dodoma v Ruvu Shooting

JUMATANO, Februari 16
African Lyon v Azam
Toto African v Simba
Kagera Sugar v Yanga

JUMAPILI, Februari 20
Kagera Sugar v African Lyon
Toto African v AFC
Polisi Dodoma v Majimaji
JKT Ruvu v Azam

JUMATANO, Februari 23
Toto African v Mtibwa Sugar
African Lyon v Ruvu Shooting
Polisi Dodoma v Kagera Sugar

JUMAPILI, Februari 27
Simba v Mtibwa Sugar

JUMATATU, Februari 28
Ruvu Shooting v Yanga

JUMANNE, Machi 1
JKT Ruvu v Ruvu Shooting

JUMATANO, Machi 2
Azam v Majimaji

JUMAMOSI, Machi 5
Yanga v Simba

JUMATANO, Machi 9
Kagera Sugar v Toto African
African Lyon v Polisi Dodoma
Majimaji v Ruvu Shooting

JUMAMOSI, Machi 12
AFC v Simba
Yanga JKT Ruvu

JUMAPILI, Machi 13
Azam v Mtibwa Sugar

JUMATANO, Machi 16
African Lyon v Toto African
Polisi Dodoma v AFC
Majimaji v Kagera Sugar
Mtibwa Sugar v Ruvu Shooting

JUMAMOSI, Machi 19
Majimaji v Toto African

JUMAPILI, Machi 27
Simba v Kagera Sugar

JUMATANO, Machi 30
Yanga v Azam
Ruvu Shooting v JKT Ruvu
AFC v Mtibwa Sugar

JUMAPILI, Aprili 2
Simba v JKT Ruvu

JUMATATU, Aprili 3
African Lyon v Yanga

ALHAMISI, APrili 7
Azam v Polisi Dodoma

JUMAMOSI, Aprili 9
JKT Ruvu v Polisi Dodoma

JUMAPILI, Aprili 10
Mtibwa SUgar v African Lyon
Kagera Sugar v AFC
Toto African v Yanga
Ruvu Shooting v Azam
Simba v Majimaji

Wanamichezo wauota ubunge 2010

MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Ismail Rage anaongoza orodha ya wanamichezo waliojitosa kwenye mchakato wa kuwania kuteuliwa kuwa wagombea na viti vya ubunge katika uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba 31.
Rage anawania jimbo la Tabora Mjini kwa tiketi ya CCM, ambalo linashikiliwa kwa sasa na Juma Kaboyoga ambaye anakitetea kiti hicho.
Wanamichezo wengine wanaotaka ubunge ni pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mchezo Netiboli, CHANETA, Shy Rose Bhanji anayewania Jimbo la Kinondoni, Seneta wa zamani wa Yanga, Nasor Duduma na Mwenyekiti aliyemaliza muda wake katika klabu hiyo Imani Madega wao wamejitosa kwenye mbio hizo wakiwania Jimbo la Chalinze.
Wengine ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Frrdirick Mwakalebela, aliyejitosa jimbo la Iringa Mjini, mkimbiaji bingwa wa zamani, John Bura aliyejitosa Jimbo la Karatu, Mkurugenzi wa Simba, Aziz Aboud aliyeomba katika jimbi la Morogoro Mjini.
Phares Magese, Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Kikapu nchini, TBF, aliyejitosa Jimbo la Kigamboni.
Pia katika kinyang'anyiro hicho cha mbio za siasa, Mtangazaji wa Mtangazaji wa Channel Ten, Cyprian Msiba amejitosa Jimbo la Mwibara.
Majina ya wagombea wateule wa viti vya ubunge ndani ya CCM yanatarajiwa kutangazwa Agosti 1 baada ya kukamilika kwa kura za maoni za wanachama wa chama hicho.

Cheka amlaumu meneja wake

BINGWA wa dunia wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na mashirikisho ya ICB na UBO Francis Cheka amemlaumu meneja wake Juma Ndambile kwa kushindwa kumuandalia mapambano. Aidha, amedai anajuta kuingia nae mkataba ambao "unamfunga" bila faida.
Akizungumza na Micharazo, Cheka alisema katika kipindi cha mwaka mmoja alioingia mkataba na meneja huyo, ameshakosa michezo kadhaa ikiwemo pambano la kimataifa lililokuwa lifanyike Uingereza pamoja na mengine ya ndani.
Cheka, alisema hajui ni kwa nini meneja huyo anashindwa kumsaidia katika hilo wakati anatambua kuishi kwake kunategemea ngumi.
"Kwa kweli huwa najuta kwa nini niliingia mkataba na meneja huyu kwa jinsi anavyonizibia riziki zangu wakati hanitafutii mapambano ya kuniwezesha kuingiza fedha na pia kupima kiwango changu," alisema Cheka.
Aliongeza kuwa hata suala la malipo ya mishahara aliyokubaliana naye imekuwa ikilegalega na kusisitiza huenda asiongeze mkataba mpya na meneja huyo mara mkataba wa sasa utakapomaliza Desemba mwaka huu.
Hata hivyo Ndambile alisema madai ya Cheka ni ya "kitoto" kwa sababu yeye ni meneja na sio promota.
Wakati akiingia mkataba na bondia huyo alimlipa mishahara ya muda wa miezi sita pamoja na fedha nyingine za ziada kwa ajili ya dharura, alisema Ndambile.
Aliasema alimlipa mishahara ya miezi sita ambayo ni shilingi milioni 1.2 na kumpa dola za kimarekani 1,500 za maandalizi ya michezo atakayoipata na hivyo kushangazwa na tuhuma kwamba anamzungumza kumlipa chake.
"Anachokisema ni utoto, mimi sio promota ni meneja wake na unajua kazi za umeneja, hivyo sijui anataka nimfanyie nini," alisema Ndambile.
"Pia amekuwa akipata mapambano kibao, lakini amekuwa akiyakwepa kiasi cha kuwakera hata wadhamini waliojitolea kwa ajili yake."
Alisema bado anaendelea kumtambua Cheka kama bondia wake na ataendelea kumsimamia atakapopata mapambano kama mkataba unavyojieleza.