STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 25, 2013

MACHINGA WAONDOLEWA MANZESE OPERESHENI SAFISHA JIJI 

ASKARI WA JESHI LA POLISI KIKOSI CHA KUZUIA GHASIA AKIWA KATIKA DORIA LEO ENEO LA MANZESE


HALI HALISI KATIKA ENEO LA WAFANYABIASHARA ULINZI


BAADHI YA WAFANYABIASHARA WAKIWA HAWAJUI LA KUFANYA

ENEO LA MANZESE MITAA IKIWA WAZI

ASKARI WA MGAMBO WAKIWA KATIKA DORIA

MOJA YA MTAA ENEO LA MANZESE

WAKAAZI WAKIPITA MBELE YAN ASKARI

WAKAZI WAKIPITA ENEO LA BIASHARA LIKIWA WAZI

WAKAZI WAKIPITA ENEO LA BIASHARA LIKIWA WAZI


ASKARI WA JIJI WAKIWA PATRO ENEO LA MANZESE

KIJIKO CHA UJENZI WA BARABARA YA MWENDO KASI ENEO LA MANZESE
WAFANYABIASHARA ndogo ndogo (Machinga) waliokuwa wamehodhi eneo la Manzese wametimuliwa ikiwa ni muendelezo wa kusafisha jiji hasa katika kipindi hiki cha ujio wa Rais wa Marekani, Barrack Obama.
Hata hivyo taarifa za chinichini toka kwa baadhi ya watendaji wa Manispaa ya Kinondoni ni kwamba machinga hao wameondolewa kutokana na mkandarasi anayetengeneza barabara ya Morogoro kupata wakati mgumu katika kutekeleza majukumu yake kutokana na eneo kubwa kujaa wachuuzi hao kiasi cha kuwafanya wafanye kazi zao katika mazingira magumu.
MICHARAZO ilipita nyakati za mchana na kushuhudia barabara hiyo ikiwa nyeupe kukiwa hakuna biashara yoyote inayofanyika zaidi ya doria ya magari ya askari polisi, mgambo na walinzi shirikishi wengine, huku vijana waliozoea kuendesha biashara zao wakiwa wanawaangalia kwa chuki askari hao kwa kuwasababishia wakose riziki kwa doria wanalofanya.
Baadhi ya wananchi waliokuwa katika eneo hilo walionyesha kuunga mkono operesheni hiyo kwa sababu imewafanya watembee kwa kujinafasi japo wengine walikuwa wakihisi kutumuliwa kwa machinga hao kunaweza kusababisha hali ya uhalifgu kukithiri mitaani kwani vijana hao watakosa kazi za kuwaingizia riziki kama walivyokuwa wakifanya

Wagosi wa Kaya kufanya mkutano wao Jumapili jijini Tanga

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiWU79I62KhllZ9JxAvswIJciK6IQye_4ognmhrW0xbcEP87ox-7QWFaiLuUYATuwBH3vdt9ENM0COQXx-uiT1TYgnxjKXURDOmQoHsGK2kmS72juupLW78cIsGlHOzGfd_Xpvp5jbiiZk/s320/Coastal+Union+logo.JPG

WANACHAMA wa klabu ya soka ya Coastal Union ya jijini Tanga wanatarajiwa kufanya mkutano wa pamoja ulioitishwa na uongozi wa klabu hiyo utakapofanyika siku ya Jumapili.
Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi ilinukuliwa kwenye mtandao wa klabu hiyo ajenda kuu ya mkutano huo ni kujadili na kupanga mikakati ya ushiriki wao wa Ligi kuu Tanzania Bara inayaotarajiwa kuanza kivumbi chake Agosti mwaka huu.
Taarifa hiyto ya uongozi wa Coastal umewahimiza wanachama kujitokeza kwa wingi bila kujali wana kadi au la mradi kufanikisha mkutano huo na kujiweka mguu sawa wakiwa kitu kimoja ili kurejesha heshima iliyowapa ubingwa mwaka 1988.
Ebu jisomee mwenyewe taarifa hiyo hapo chini juu ya mkutano huo

Uongozi wa Coastal Union unawatangazia mashabiki wake walio ndani na nje ya nchi kuwa siku ya jumapili wiki hii June 30 kutakuwa na mkutano mkuu wa wanachama utakaofanyika mjini Tanga.

Mkutano huo ni muhimu kuhudhuria hata kama huna kadi ya uanachama, kwani itakuwa ni fursa pekee ya kupanga mikakati ya msimu ujao wa soka 2013/14 ili kuhakikisha kikosi imara cha wana Mangush kinaweka heshima ya soka nchini kwa kuchukua ubingwa kama walivyofanya mwaka 1988.

Uongozi unaweka wazi kuwa kwa yeyote ambaye ana malalamiko ama ushauri juu ya kuendesha timu ili kufikia mafanikio, basi ahudhurie kwenye mkutano ili kumaliza kiu yake na si kusema pembeni bila tija.

Siku hiyo mbali ya ajenda za kujenga timu pia kutakuwa na mikakati ya viongozi na kugawa majukumu kwa wanachama, pia kutajadiliwa namna ya kuhakikisha mashabiki walio mikoani na nje ya nchi wanatambulika rasmi na kukaribisha michango ya hali na mali kwa lengo moja tu, kuleta ushindi msimu ujao.

Tayari timu yetu imesharudi nyoyoni mwa wapenda soka, kilichobaki ni kuhakikisha hatuwavunji moyo wapenzi wetu cha kufanya ni kupata kadi ya uanachama ambazo zitatolewa siku hiyo, na pia kutawekwa utaratibu bora wa kuhakikisha timu inatunisha mfuko wa maendeleo.

Wanachama wengi wanawasiliana katika mitandao lakini hawajuani kwa sura hii itakuwa nafasi ya kipekee kuweza kujuana na kubadilishana mawazo, tayari wanachama wengi kutoka mikoa ya jirani wamethibitisha kuhudhuria mkutano huo, umebaki wewe tu.

Tuache kusemasema vipembeni tuelekee kwenye mkutano mkuu tarehe 30 June, 2013.

Cheka uso kwa uso na Mmarekani Dar



Bango linaloonyesha mapambano ya ngumi za kulipwa zinazotarajiwa kuwakutanisha wakali wa mchezo wenye sifa kubwa nchini.

Hatimaye mume wa Joyce Kiria aonekana hadharani

Bw.Henry Kileo akiwa na watuhumiwa wenzake wa mashtaka ya Ugaidi yanayowakabili wakati walipofikishwa Mahakama ya Hakimu mkazi mkoani Tabora kwa mara ya kwanza.
Wanachama wengine wa Chadema ambao wanahusishwa katika mashataka hayo ya Kigaidi ambapo imedaiwa kuwa watuhumiwa walifanya makosa hayo ya Ugaidi na kumjeruhi Bw.Mussa Tesha ambaye ni mwanachama wa CCM wakati wa kampeni za uchaguzi wa Ubunge wa jimbo la Igunga mnamo tarehe 9/9/2011 katika msitu wa Hanihani huko wilayani Igunga.
 Ulinzi katika Mahakama hiyo uliimarishwa ipasavyo.
 Henry Kileo akiwa ndani ya gari pamoja na watuhumiwa wenzake wanne wakisubiri kupelekwa Gereza la Mahabusu hadi watakapoletwa tena Mahakamani hapo mnamo tarehe 8/7/2013

Na Josephat Isango wa Tanzania Daima.

KAIMU Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mkoa wa  Dar es Salaam, Henry Kilewo, anashikiliwa  na polisi , akihusishwa na  tukio la kumwagiwa tindikali, Musa Tesha. Tesha alimwagiwa tindikali na watu wasiojulikana Septemba 9, mwaka juzi kwenye kampeni ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga, uliomuweka madarakani Dk. Kafumu Dalali.
Akizungumza juzi na Tanzania Daima kabla ya kufika makao makuu ya Jeshi la Polisi, Kilewo alisema hajui anachoitiwa na kwamba anatekeleza wito wa jeshi hilo kuwa afike ofisini kwao. “Sijui ninachoitiwa, nimepigiwa simu naenda kutekeleza wito, nimesha wataarifu mawakili wangu ninaowaamini, kwa kuwa chochote kinaweza kutokea cha msingi Watanzania wapenda mageuzi waniombee kwa Mungu,” alisema Kilewo.
Wakili wa Kilewo, Peter Kibatala, alisema baada ya mteja wake kuhojiwa kwa muda wa saa tano juzi alielezwa kuwa anapelekwa Igunga, mkoani Tabora kuunganishwa na watuhumiwa wengine katika kesi ya kutumia tindikali na kujeruhi.
Kibatala alisema anasikitishwa na hatua ya jeshi hilo kumnyima dhamana mteja wake ilhali kosa wanalomtuhumu linadhaminika na kwamba hayo ni matumizi mabaya ya madaraka kumzuia mtu kwa zaidi ya saa 24 pasipo kumfikisha mahakamani. Wengine wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kutumia tindikali na kudhuru watu ni pamoja na  Oscar Kaijage wa Shinyanga na Evodius Justinian wa Bukoba.
Evodius Justinian alikamatwa na  Jeshi la Polisi mjini Bukoba na kushikiliwa kwa siku kadhaa kabla ya  kusafirishwa hadi jijini Dar es Salaam. Kabla ya kusafirishwa na kufikishwa jijini Da r es Salaam, Justinian alieleza kuteswa na kupigwa na askari waliokuwa wakimzuia katika vituo mbalimbali kuanzia mjini Bukoba.
Joyce Kiria alipoandamana kushinikiza serikali imuonyeshe mumewe yupo wapi baada ya ukimya tangu afikishwe kituo kikuu cha Polisi Dar.

Maajabu ya Mungu! Msaidie mama huyu kuwaokoa watoto wake


MWANAMKE mmoja mkazi wa Kijiji cha Kasumuru, Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya, Grace Joel Lwesha (19), amelia baada ya kujifungua watoto walioungana.


Akizungumza na waandishi wetu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Jengo la Watoto, Grace alilia kutokana na kile alichodai kujifungua watoto walioungana wakati yeye ni maskini.


Watoto hao mapacha wa kiume, Eliudi na Elikana wameungana sehemu ya makalio hivyo kulazimika kutumia sehemu moja ya haja kubwa.

Grace aliwaambia waandishi wetu kwamba, watoto hao walizaliwa katika Hospitali ya Kyela, Februari 20, mwaka huu wakiwa na miguu miwili na mikono miwili kila mmoja.


“Baada ya kujifungua Machi mosi nilihamishiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya kwa uchunguzi zaidi ili waweze kujua ni jinsi gani watakavyotenganishwa,” alisema.


Hata hivyo, hospitali hiyo ya mkoa haikufanikiwa badala yake Machi 16, walimhamishia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo kuanzia hapo mpaka sasa anafanyiwa maandalizi kwa ajili ya safari ya kupelekwa nchini India kwa upasuaji.

 “Ninawapenda sana watoto wangu hawa pamoja na kwamba wapo katika hali hii, ndugu zangu walipokuja hospitalini kuniona akiwema mama yangu walinifariji na kunisihi nisiwachukie nizidi kuwapenda.

“Kuwatunza ni kazi ngumu sana kwani mara nyingi wamekuwa wakininyima usingizi kwa sababu wamekuwa wakilala kwa nyakati tofauti.

“Nakumbuka siku niliyojifungua mume wangu alikosa raha lakini sasa anawapenda kwani amejua kuwa hii ni zawadi kutoka kwa Mungu.

 “Maisha yetu ni magumu kwani tunatoka kwenye familia maskini, kazi yetu ni kilimo cha kutumia jembe la mkono hivyo bado kuna mahitaji mengi nashindwa kumudu.


Nichukue nafasi hii kuwaomba msaada Watanzania wote walioguswa na tukio hili,” alisema Grace.

Grace alifunga ndoa na Erick William Mwakyusa Desemba 23, 2010 na katika ndoa yao wamejaliwa kupata mtoto mmoja aitwaye Lide (3) na hao mapacha ni uzao wake wa pili.

Mama huyo anaomba msaada kwa mtu yeyote aliyeguswa na habari hii atume mchango wake kupitia namba 0753308525 ambayo ni ya mumewe au aende kumuona Muhimbili.

Askari Polisi 114 watimuliwa kazi, kisa....!

http://2.bp.blogspot.com/-HFY83aRnIf0/UQlOtZQQmPI/AAAAAAAAAKw/J1v9b9t_vE4/s640/12-Naibu+Waziri+wa+Mambo+ya+Ndani+ya+Nchi+Pereira+Ame+Silima+akijibu+hoja+mballimbali+za+wizara+yake+Bungeni.JPG
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima
http://www.gushit.com/files/bookmark_photos/8e1effe441L.jpg
IGP, Said Mwema

JUMLA ya askari  wa 114 wa Jeshi la Polisi wamefukuzwa kazi kutokana na makosa mbalimbali ya ukiukwaji wa maadili ya kazi zao na baadhi yao wakiwa wamefikishwa mahakamani katika kipindi cha mwaka 2007-2010.
Takwimu hizi zimefichuliwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima wakati  akijibu swali la Mbunge wa Baraza la Wawakilishi (CCM), Jaku Hashim Ayoub.
Mbunge huyo alitaka kujua serikali ina mpango gani wa kudhibiti vitendo vya baadhi ya askari kuwabambikia kesi raia kinyume na misingi ya haki za binadamu.
Pia alitaka kujua serikali imewachukulia hatua gani za kinidhamu na kisheria askari waliojihusisha na vitendo hivyo ili iwe fundisho kwa askari wengine.
Akijibu, Silima alisema serikali ina mikakati ya kukabiliana na kudhibiti vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu na utawala bora pamoja na vitendo vya baadhi ya askari kuwabambikia kesi na kuwatishia raia ili wasifuatilie kesi zao vituoni.
“Kuanzia mwaka 2007 hadi 2010 jumla ya askari 114 wamefukuzwa kazi kwa makosa mbalimbali ya ukiukwaji wa maadili na maadhi yao wamefikishwa mahakamani” alisema.
Hata hivyo, alisema mafanikio ya jeshi la polisi yanategemea upatikanaji wa taarifa za matukio hayo kutoka kwa wananchi ambao wanatendewa vitendo hivyo na baadhi ya askari ambao siyo waaminifu.

Hivi karibuni askari karibu 10 nchini waliripotiwa kutimuliwa kazi kwa makosa mbalimbali ikiwemo wale waliokuwa wakitumia fuvu la mtu kuwapakazia kesi wananchi katika mkoa wa Morogoro.

Mwantumu Mahiza aapishwa kuwa Skauti Mkuu wa Tanzania

 Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania mteule Mhe. Mwantumu Mahiza akisubiri kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akijiandaa kuvishwa skafu na skauti kabla ya kumuapisha Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza akisubiri kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akivishwa skafu na skauti kabla ya kumuapisha Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza akisubiri kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza akisubiri kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka sahihi baada ya kumuapisha Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza baada ya kumuapisha Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi vitendea kazi Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
   Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
   Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim, Jaji Kiongozi Fakih Jundu na Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza pamoja na viongozi wa maskatu na skauti  baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza na familia yake baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza pamoja na waheshimiwa wabunge ambao ni maskauti  baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na skauti Ismail Aden Rageh na wabunge maskauti  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza pamoja na wanachama wa UWT wilaya ya Ilala  baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza na viongozi wa skauti nchini baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na skauti Livingstone Lusinde ambaye pia ni Mbunge wa Mtera  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 23, 2013

Majambazi waua walinzi wawili wakipora fedha kituo cha mafuta

Kaimu Kamanda Mkuu wa Polisi Mkoa wa Njombe, Focus Malengo

WATU wanaosadikiwa kuwa ni majambazi, wamewaua kwa kuwapiga risasi walinzi wawili  wa kampuni binafsi ya ulinzi ya Makambako Security Guard katika mji mdogo wa Makambako mkoani Njombe.
Tukio hilo lilitokea jana saa 12:30 asubuhi baada ya watu hao kuvamia kituo cha kuuzia mafuta cha Oryx cha mjini hapa.
Walinzi waliouawa wametajwa kuwa ni Chesco Mpogole (30) na Damas Sanga (28), wakazi wa Ubena na Uhuru mjini hapa.
Mbali na watu hao kuuawa, pia majambazi hayo yamemjeruhi vibaya Meneja wa Kituo hicho, Jonas Msengi (43), mkazi wa Mji Mwema ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Misheni ya Ilembula kwa matibabu.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Njombe, Focus Malengo, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Kamanda Malengo alisema majambazi hayo yalivamia kituo hicho kwa kutumia usafiri wa pikipiki na kujifanya wateja wa kununua mafuta.
“Lakini wakiwa tayari wameuziwa mafuta ya Sh. 5,000, yalitoa noti ya Sh. 10,000, hivyo mhudumu aliyewahudumia Ibrahim Manga, alikwenda kwa mwenzake Mwanaidi Kalinga (32) kwa ajili ya kufuata chenji,” alisema Kamanda Malengo.
Aliongeza kuwa wakati jambazi moja likisubiria chenji, mwingine aliwafuata walinzi hao na kuwashambulia kwa kuwapiga risasi na kusababisha vifo vyao papo hapo.
Kamanda Malengo alisema baada ya kufanya mauaji hayo, majambazi hayo yalimfuata Meneja Msengi, ambaye wakati huo alikuwa akiingia ofisini kwake na kuanza kumshambulia.
“Lakini pia majambazi hayo yalipora kiasi cha kati ya Shilingi milioni sita na saba kwa taarifa za awali kwani wamiliki wa kituo hiki wanaendelea kufanya hesabu zao,” alisema Kamanda Malengo.

After Death ya Kanumba kuachiwa hadharani Julai 30

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEis_FnvkJ3vrjIRirZl9Qxb0BdfdsIQOCGQIcqOV2__0kfCDRjnU1KnQlIoCR3nyI5i-BS2k8HEbNq1Vcn_QcZlXS3S5qzbXof7eyCdW71O0Q0WyQVcEVz5ILvAToRDjFipfsZ9UUF30TI/s1600/Kanumba1.jpeg

FILAMU iliyoandaliwa maalum kwa ajili ya kumuenzi marehemu Steven Kanumba iitwayo 'After Death' na iliyozinduliwa rasmi katika maadhimisho ya mwaka mmoja tangu msanii huyo aage dunia inatarajiwa kuachiwa mtaani mwezi ujao.
Filamu hiyo iliyotungwa na tayarishwa na msanii Jacklyne Wolper na kuongozwa na Leah Richard 'Lamata' ilipangwa kutolewa mwezi huu wa Juni, lakini Lamata aliiambia MICHARAZO kwamba kazi hiyo itaachiwa rasmi Julai 30 mwaka huu.
Lamata alisema wameamua kusogeza muda wa kuiingiza sokoni kutokana na foleni kubwa iliyopo kwa wasambazaji na pia kujipanga kuweza kuwafikia mashabiki karibu wote nchini, ikiwa ni siku chache baada ya kuiachia hadharani filamu ya "my Princess'.
"Baada ya kuachia 'My Princess' tunajipanga kuitoa hadharani 'After Death' filamu maalum iliyotengenezwa kwa ajili ya kumuenzi Kanumba, tumepanga kuiachia Julai 30," alisema Lamara.
Ndani ya filamu hiyo imeshirikisha wasanii chipukizi walioibuliwa na marehemu Kanumba kama Patrick na Jennifer, wamo pia Branco, Uncle D, Shamsa Ford, Wolper, Mainda, Patcho Mwamba, Stanley Msungu na wengine ambao walikuwa wakiigiza na msanii huyo.
Kanumba alifariki Aprili 7 mwaka jana baada ya kuanguka katika kilichoelezwa ugomvi baina yake na mpenzi wake, Elizabeth Michael 'Lulu'  na kuacha majonzi kwa mashabiki na wale waliokuwa wakifanya naye kazi kutokana na ufanisi wake katika tasnia ya filamu na uigizaji kwa ujumla.

Jordi Alba ajishangaa kuwa 'Man of the Match'

http://en.rian.ru/images/17604/24/176042404.jpg

BEKI wa timu ya taifa ya Hispania, Jordi Alba amejishangaa kwa kuweza  kufunga mabao mawili na kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mechi baada ya kuisaidia timu yake kushinda 3-0 dhidi ya Nigeria katika mechi yao ya mwisho ya makundi ya Kombe la Mabingwa wa Mabara 2013 juzi usiku.
Mlinzi huyo wa kushoto wa Barcelona alifunga goli kali la juhudi binafsi mapema kipindi cha kwanza kabla ya kutupia la tatu baada ya kukimbia kutokea katikati ya uwanja na kumpiga chenga kipa Vincent Enyeama katika dakika za mwisho.
"Si kawaida kwangu kufunga magoli mawili katika mechi moja," Alba aliwaambia waandishi wa habari. "Nadhani hii ni mara ya kwanza.
"Hii ni mpya kwangu, kwa sababu, kama ulivyosema, mara nyingi tuzo hii (ya mchezaji bora wa mechi) hupewa washambuliaji au wale walio mbele katika mechi kubwa. Najivunia kupata tuzo hii."
Kocha Vicente del Bosque alilalamikia hali ya hewa mjini Fortaleza Jumapili jioni, na Alba alikiri kwamba joto limekuwa likiziathiri timu katika michuano hiyo.
"Tulisikia joto katika mechi nzima, ilikuwa ni joto sana," aliendelea. "Miguu yako inaungua... Lakini iko hivyo kwa timu zote."
Hispania sasa itacheza dhidi ya Italia katika nusu fainali katika mechi ambayo ni kama marudio ya fainali ya Euro 2012, ambayo Hispania ilishinda 4-0, lakini Alba amesisitiza kwamba timu yake ni lazima iwe katika kiwango cha juu ili kuishinda timu ya kocha Cesare Prandelli.
"Dhidi ya timu kama Italia hujui nini kitatokea," alisema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. "Wanajipanga vyema nyuma na wanajua kukaa na mpira.
"Watakuwa wagumu kwetu, kama ambavyo wamekuwa kila siku. Tunapaswa kudumusha staili yetu ya kucheza na kutoruhusu magoli nyuma."

Shasta aonja utamu wa penzi la H-Mbizo


MUIGIZAJI wa kike wa filamu nchini, Leah Mussa 'Shasta' amefuata mkondo wa shoga zake Shilole na Snura kwa kujitosa kwenye muziki akikamilisha wimbo wake wa kwanza uitwao 'Utamu wa Penzi' ambao amemshirikisha Hamis Mbizo 'H-Mbizo'.
Akizungumza na MICHARAZO Shasta alisema wimbo huo upo hatua ya mwisho kabla ya kukamilika akiwa ameurekodia katika studio za prodyuza More Fire aliyetengeneza wimbo wa Snura uitwao 'Majanga'.
Alisema kuingia kwake kwenye muziki siyo kwa kubahatisha kwani tangu utotoni alikuwa akijishughulisha na muziki akiimba kanisani na shuleni na mpaka sasa yeye ni mwalimu wa muziki na anaimba kwaya ya kanisa lake la Sabato, ila hakuifanya kazi hiyo  kibiashara kutokana na kutingwa na majukumu ya uigizaji wa filamu.
"Wengine wanaweza kuhisi landa nimevamia fani ya uimbaji, hapana mimi ni mwanamuziki kamili nikianza kuimba kanisani na shuleni tangu nikiwa mdogo na hata sasa naimba kwaya kanisani, ila kwa vile nataka kuwaonyesha wengine kwamba watu tuna vipaji zaidi ya kimoja ndiyo maana nimeamua kutoka na wimbo huo wa 'Utamu wa Penzi' kisha kufuatiwa na nyimbo nyingine," alisema Shasta.
Nyota huyo wa filamu ya 'Kisasi cha Mzimu', 'Julia', 'Deception', 'Ongwana', Pete ya Ajabu na nyingine, alisema mara baada ya kuachia hewani wimbo huo klabla ya kuanza kwa mfungo wa mwezi wa Ramadhani unaoanza wiki mbili zijazo ataanza mipango ya kukamilisha video yake kabla ya kutoa kazi mpya hapo baadaye.

Kipemba, Mapigo 7 wahamasisha ulipaji kodi Ujiji-Kigoma


      
Msanii Yasini Mapigo Saba akiwa na Issa Kipemba
    
MUIGIZAJI nyota wa zamani wa kundi la Kaole Sanaa, Issa Kipemba 'Kipemba' akishirikiana na msanii Yassini  Mapigo Saba wa mkoani Kigoma, wameendesha kampeni ya kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa wakazi wa manispaa ya kigoma Ujiji.

Kampeni hizo zilizoambatana na burudani ya ngoma asilia, vichekesho na uigizaji, ziliandaliwa na ofisi ya Manispaa ya mji huo wa Ujiji –Kigoma kupitia mradi wa Tanzania Strategic Cities Project (TSCP) chini ya Mstahiki Meya Bakari Beji.

Alisema alijikuta akishiriki kampeni zilizoambatana na utoaji wa elimu ya ulipaji wa kodi za manispaa hiyo kwa ajili ya kuongeza chachu ya maendeleo alipoenda kwa likizo fupi na kama msanii alijiona ana dhima ya kuisaidia jamii yake.

"Nilikuwa nimeenda kusalimia nyumbani na kukuta uhamasishaji huo na mie kushiriki kama msanii na mwenyeji wa Ujiji na tumefanya kazi kubwa nikishirikiana na msanii mkongwe wa Kigoma, Mapigo Saba," alisema.

Naye mstahiki meya wa manispaa ya Kigoma ujiji  alithibitisha kufanyika kwa kampeni hizo akidai zilikuwa zina lengo la kuchochea hamasa kwa wakazi wa mji huo kujenga tabia ya kulipa kodi zilizopo katika manispaa yao ili kuongeza kasi ya maendeleo ya manispaa yao.

"Ni kweli Kipemba na wasanii wengine akiwamo Mapigo Saba walikuwa hapa kuendesha kampeni ya elimu na uhamasishaji wa ulipaji wa kodi za manispaa na kwa kiasi kikubwa wamefanya kazi kubwa na tunasubiri utekelezaji toka kwa wananchi," alisema  Mstahiki Meya Beji.

Aidha mweka hazina wa manispaa hiyo ndugu Edward Malima alianisha kodi zilizoahamasishwa kwa wananchi wa Kigoma - Ujiji kuwa ni pamoja na kodi za Majengo, Ushuru wa Huduma ya Mji, Maegesho ya magari, Masoko na Vizimba, Hoteli na Nyumba za wageni (guest), na Mabango ya Matangazo.

Ndugu Malima alitilia mkazo kwa kutofautisha kodi za maegesho ya magari na ile ya Stendi za mabasi ambapo alitanabahisha umuhimu wa ulipaji wa kodi hizo kwa ustawi na maendeleo ya mji wa Kigoma Ujiji huku akitoa mifano lukuki ya maendeleo ya sasa ya manispaa hiyo ukilinganisha na hapo nyuma.

Kipute cha Ligi Kuu msimu wa 2013-2014 kuanza Agosti 24

http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2012/11/Vodacom-Premier-League.jpg

PAZIA la Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2013/2014 unatarajiwa kuanza Agosti 24 mwaka huu ambapo timu zote 14 zitashuka dimbani kwenye viwanja tofauti kusaka pointi tatu muhimu, imefahamika.
Akizungumza jijini jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi, Wallace Karia, alisema kuwa tarehe hiyo imeshapitishwa katika kalenda ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na tayari pia mechi za ligi hiyo zimeshapangwa lakini hazijathibitishwa na kamati yake kama taratibu zinavyoeleza.
Karia alisema kuwa tayari 'wataalamu' ambao huhusika na zoezi la kupanga ratiba za mechi wameshakamilisha zoezi hilo lakini kamati yake ndiyo inasubiriwa kupanga siku ya kukutana ili kuithibitisha.
"Ligi itaanza tarehe 24 Agosti ila nani ataanza na nani ndiyo bado hatujapitisha, tukishakutana na kupitia hilo kwa kuzingatia mazingira yetu ya timu kusafiri ndiyo itatolewa hadharani. Tutakuwa makini sana kwa sababu hatutaki makelele yaliyojitokeza mwaka jana na miaka ya nyuma yaendelee," alisema Karia ambaye ameshasema kuwa atawania cheo cha Makamu wa Rais katika uchaguzi ujao wa shirikisho hilo utakaofanyika Septemba.
Hata hivyo, Karia alisema kuwa suala la wadhamini wa ligi hiyo bado halijakamilika lakini kubwa wanachotaka ni kuona ni klabu zinafaidika na udhamini utakaopatikana.
Alisema kuwa kamati yake inatarajia kukutana Julai 3 asubuhi ili kupitia taarifa za msimu uliopita na kupata washindi wa tuzo mbalimbali na jioni yake washindi hao watatangazwa na kutunukiwa.
"Tumepanga tukutane siku hiyo hiyo ya tuzo ili habari zisivuje, kwa sababu kila mtu na kifua chake cha kuweka mambo…  hadi sasa ni bingwa, mshindi wa pili na wa tatu ndiyo wanajulikana. Lakini kocha bora na tuzo nyingine tutajua siku hiyo baada ya kuangalia na kuthibitisha rekodi tulizonazo," aliongeza Karia.
Kabla ya kuanza kwa ligi hiyo, bingwa mtetezi Yanga na mshindi wa pili, Azam watakutana katika mechi ya kuwania Ngao ya Jamii kama kanuni za ligi zinavyosema.
Timu 14 za msimu ujao wa ligi ni pamoja na Yanga, Azam, Simba, Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, Coastal Union, JKT Oljoro, JKT Ruvu, Ruvu Shooting, Mgambo Shooting, Prisons na zilizopanda daraja ambazo ni Mbeya City, Ashanti na Rhino Rangers ya Tabora.

NIPASHE

TFF yamlilia Mathias Kissa yaipa pole Cosmopolitan

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-oqDTfx6eD3GS-91kZ027R1B7KN3FGOluw6ENwQnLjL8AcgR3WMUBHEwNYC-7_iYXwCHXik-lPqq5I6uVkLtL9IPhfuHikd5tKT2P8aiJe9V2_NWhU7eF7mjzi-rdjo5azW2MsUoYmjjK/s320/tff_LOGO.jpg
Na Boniface Wambura
Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mchezaji wa zamani wa timu za Cosmopolitan na Taifa Stars, Mathias Kissa (84) kilichotokea leo alfajiri (Juni 24 mwaka huu) kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.

Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani enzi zake, Kissa akiwa na timu ya Tabora alitamba katika michuano ya Kombe la Taifa wakati huo ikiitwa Sunlight Cup. Alikuwa akicheza katika nafasi ya ulinzi.

Baadaye alijiunga na Cosmoplitan ya Dar es Salaam, na pia kuwa mchezaji wa timu ya Taifa ambapo enzi zake akiwa na wachezaji kama Yunge Mwanansali wakiiwakilisha Tanganyika na baadaye Tanzania Bara walitamba katika michuano ya Kombe la Chalenji wakati huo ikiitwa Gossage, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.

Kissa ambaye alipata tuzo ya mchezaji bora wa karne kwa upande wa Tanzania, tuzo inayotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) alikuwa ndiye mchezaji msomi kupita wote wakati akichezea timu ya Taifa akiwa amehitimu elimu ya Darasa la Kumi.

Kwa mujibu wa binti yake, Erica, marehemu ambaye pia aliwahi kuwa mjumbe wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi (stroke) alioupata miaka mitano iliyopita, na kisukari. Baadaye alipata kidonda ambacho ndicho kilichosababisha kifo chake.

Msiba uko nyumbani kwa marahemu, Masaki, Mtaa wa Ruvu karibu na Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST). Maziko yatafanyika keshokutwa, Jumatano (Juni 26 mwaka huu) kwenye makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Kisa, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na klabu ya Cosmopolitan na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Mungu aiweke roho ya marehemu Kisa mahali pema peponi. Amina

Monday, June 24, 2013

VODACOM KUKABIDHI ZAWADI LIGI KUU BARA JULAI 3

Meneja Uhusiano wa nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza tarehe ya utoaji wa zawadi za ligi kuu ya Vodacom zitakazotolewa Julai 3 jijini Dar es Salaam.  Zawadi hizo ni za jumla ya Sh. milioni 200 zitakazotolewa kwa vipengele mbalimbali kwa timu za ligi hiyo.
WADHAMINI wakuu wa Ligi Kuu ya soka ya Tanzania Bara Kampuni ya Vodacom imetangaza kuwa itakabidhi zawadi kwa washindi wa ligi hiyo Julai 3 jijini Dar es salaam.

Vodacom imesema ilikuwa ikisubiri kumalizika kwa hekaheka za timu ya taifa - Taifa Stars za kusaka nafasi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil hali iliyochelewesha tukio la kukabidhi zawadi hizo kwa mabingwa pamoja na wote waliofanya vema katika msimu wa 2012/2013.
.
"Tulikuwa tukisubiri wakati mwafaka wa kufanya hivyo kwani tangu kumalizika kwa ligi mwezi uliopita mwelekeo wa taifa ulikuwa ni kuipa ari na nguvu timu yetu ya taifa katika kusaka tiketi ya kufuzu kushiriki fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil," alisema Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim.

Mwalim amesema maandalizi yote ya tukio hilo yamekamilika kwani hakukuwa na sababu nyingine ya kutokabidhi zawadi mara tu baada ya ligi kumalizika zaidi ya timu ya taifa - Taifa Stars.

Mwalim amesema hafla ya utoaji wa zawadi inahitaji ushiriki wa wadau mbalimbali wa soka nchini wakiwamo wachezaji wa klabu ambao miongoni mwao wamo kwenye kikosi cha Stars, viongozi wa TFF na walimu wa timu ya taifa ambao wote hao kwa pamoja walikuwa na jukumu moja tu la kuhakikisha Stars inafuzu kwenda Brazil na hivyo isingekuwa vema kuingiza maandalizi ya jambo jingine katikati ya juhudi hizo.

Mwalim ametumia nafasi hiyo kuzishukuru klabu pamoja na Shirikisho la Soka (TFF) na kamati ya ligi kwa uvumulivu wao wakati wote ambapo Vodacom ilikuwa ikisubiri kupatikana kwa muda mwafaka wa kukabidhi zawadi.

"Tendo la kukabidhiwa zawadi ni moja ya matendo makuu kabisa kwa yeyote anayeshinda, tumeona uvumilivu mkubwa na wenzetu walituelewa wakati tulipowashauri kutoa nafasi kwa Stars bila kuharibu concentration ya taifa. Tumeonesha umoja wetu."
Vodacom itakabidhi zawadi za fedha taslimu takribani Sh. milioni 200 kwa mabingwa Yanga na Azam, Simba na Kagera Sugar zilizoshika nafasi ya pili hadi ya nne.

Mbali ya mabingwa timu ya Yanga ambayo itakabidhiwa fedha taslimu Sh milioni 70, wengine watakaotunukiwa ni wachezaji mmoja mmoja walioonesha umahiri kwenye maeneo yao.

Wengine watakaonufaika na zawadi za fedha ni kipa bora, mwamuzi bora, mwalimu bora, timu iliyoonyesha nidhamu na mfungaji bora, ambaye ni Kipre Tchetche wa Azam.

Vodacom imekuwa ikiidhamini ligi kuu ya soka ya Tanzania bara kwa zaidi ya misimu mitano sasa huku ikiiwezesha ligi hiyo kuimarika na kuwa ya ushindani kadri miaka inavyosonga mbele.

Balotelli kuikosa Hispania Nusu Fainali ya Kombe la Mabara

Mario Balotelli 'Super Mario'
MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya taifa ya Italia 'Azzurri' Mario Balotelli, atalikosa pambano la Nusu Fainali ya Kombe la Mabara dhidi ya Hispania siku ya Alhamis kutokana na kuwa majeruhi.
Balotelli aliumia na kutoka uwanjani wakati Italia ikichezea kichapo cha mabao 4-2 toka kwa Brazili Jumamosi iliyopita na kuungana na wachezaji wengine wa Azzurri watakaolikosa pambano hilo ambao ni  Andrea Pirlo na Riccardo Montolivo.
Kukosekana kwa Balotelli kunamfanya kocha wa timu hiyo ya Italia, Cesare Prandelli kuwa katika mtihani mkubwa katika pambano hilo dhidi ya Mabingwa wa Ulaya na Dunia, Hispania walioinyoa Nigeria jana usiku kwa mabao 3-0 na kumaliza mechi za makundi bila kupoteza mechi.
Mshambuliaji huyo mtukutu mwenye umri wa miaka 22 na anayeichezea AC Milan katika michuano hiyo amefunga mabao mawili mpaka sasa. na atakosa fursa ya kuisaidia timu yake iliyokumbana na kipigo cha aibu katika Fainali ya Kombe la Ulaya Euro Cup 2012 pale Hispania walipowanyoa kwa mabao 4-0.
Nusu Fainali nyingine ya michuano hiyo itachezwa keshokutwa kati ya Brazil ya Neymer na Uruaguay ya Luis Suarez ambao usiku wa kuamkia leo walitoa kipigo cha mabao 8-0 kwa Tahiti iliyoweka rekodi ya kushiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza ikifungwa mechi zote tatu za makundi na kufunga bao moja tu huku yenyewe ikiruhusu jumla ya mabao 24.

Mzee Mandela hali yazidi kuwa tete

Mzee Mandela (kulia) akiwa na rais Jacob Zuma wakati hali yake ilipokuwa ikianza kutengemaa kabla ya kuelezwa imebadilika kiasi cha kuwa tishio
HALI ya Afya ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini na Mwanasiasa anayeheshimika duniani kote, Mzee Nelson Mandela inaelezwa kuwa tete.
Madaktari wanaomtibu Mwanaharakati huyo aliyeleta ukumbozi katika nchini ya Afrika Kusini, wamesema hali ya Mzee Mandela imekuwa siyo nzuri kwa saa 24 zilizopita na kwamba kwa sasa yu mahututi.
Habari hizo zimekuja kupitia taarifa iliyotolewa na ofisi ya rais ya Afrika Kusini zikisema kuwa bado Mzee Mandela ameendelea kusalia hospitalini mjini Pretoria kwa siku ya kumi na sita akitibiwa mapafu yaliyosababisha tatizo kwenye mfumo wake wa upumuaji.
Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma alimtembelea Rais Mstaafu huyo jana jioni na kuzungumza na jopo la matatibu wanaomtibia.
Baadaye Rais Zuma alirejea kauli yake ya kulitaka taifa na dunia kumuombea Mzee Mandela apate nafuu kwa hali aliyonayo.

Soggy Doggy Anter atangaza kuwania ubunge Jimbo la Segerea analoshikilia Makongoro Mahanga

Soggy Doggy Anter akiwajibika jukwaani

MSANII nguli wa muziki wa kizazi kipya nchini, Anselm Tryphone Ngaiza, 'Soggy Doggy Anter' ametangaza nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Segerea, Dar es Salaam kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015.
Soggy Doggy ameweka bayana mipango yake hiyo ha kuwania kiti cha ubuinge cha jimbo hilo kinachoshikiliwa kwa sasa na Mhe. Makongo Mahanga kupitia akaunti yake ya Facebook ambapo aliandika;
"Shikamoo Mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga, imetosha sasa nadhani ni zamu yangu kuwatumikia wana-segerea 2015 kupitia CHADEMA" mwisho wa kunukuu. Pia kwenye ukurasa wake wa twitter imesomeka ivyo ivyo.
Msanii huyo alisema ameamua kujitosa kwenye siasa kupitia CHADEMA, kwa sababu ndicho chama pekee anachokiona kinachoweza kufanya mabadiliko kwenye jamii kwa sasa.

Azam waanza kujifua,10 pekee wahudhuria Morad kimyaaa

Wachezaji wa Azam walipokuwa wakijiandaa na mechi za Kombe la Shirikisho Afrika hivi karibuni
WACHEZAJI 10 pekee ndiyo waliohudhuria mazoezi ya timu ya Azam yaliyoanza leo kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.
Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo wachezaji wengi 16 wameshindwa kuhudhuria siku ya kwanza ya mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika kwenye uwanja wao wa Chamazi, kutokana na sababu mbalimbali huku beki Said Murad akiwa hana taarifa yoyote ya udhuru uliomfanya asiwepo mazoezini.
Taarifa hiyo imesema wachezaji walianza mazoezi asubuhi ya leo ni pamoja na Malika Ndeule, Brian Umony, Jabir Aziz, Waziri Salum, Gaudence Mwaikimba, Luckson Kakolaki, Samih Haji Nuhu, Seif Abdallah Karihe, Wandwi Jackson na Ibrahim Mwaipopo
Wachezaji wengine 16 wamekosekana kutokana na kuomba ruksa kwa matatizo waliyonayo ya kifamilia wakiomba kuanza mazoezi wiki ijayo ambao ni  David Mwantika aliye na matatizo ya kifamilia kama ilivyo kwa Omary Mtaki anayeuguza baba yake na Himid Mao aliyefiwa na baba yake mkubwa.
"Mchezaji pekee ambaye hakufika mazoezini na hakuna taarifa zozote juu ya kukosekana kwake ni Said Morad Mweda," taarifa hiyo inasomeka hivyo kuelezea kushindwa kujitokeza kwa beki huyo wa kati ambaye alisimamishwa na wenzake watatu kwa tuhuma za Rushwa kabla ya kusafishwa na TAKUKURU na kurejeshwa kikosi mwishoni mwa msimu uliopoita japo hakucheza hata mechi moja.
Moradi alisimamishwa na aliyekuwa nahodha, Aggrey Morris, kipa Deo Munishi na beki wa pembeni Erasto Nyoni.

Kibadeni akana kumtimua Kaseja Msimbazi

Kocha King Abdallah Kibadeni
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnmGiUBH2n-4bYq2A7G-O5Mg7eMw2R8U3g_2gTLIHmOvOciOk4zkgnhEV0ZbsJdpep3-YAmE7L8q-zXX7P9cJDnYcQoRAUfq3BK2wnYkoqAoZu9sLMdhdazbFee-dXHAlY_7VkAk1INgo/s1600/JUMA_KASEJA%5B1%5D.JPG
Kipa Juma Kaseja
KOCHA wa Simba, Abdallah Kibaden 'King', ameibuka na kukanusha vikali uvumi kwamba ni yeye ndiye aliyemtimua kipa chaguo la kwanza wa timu hiyo na Taifa Stars, Juma Kaseja baada ya kumtema katika orodha ya nyota wanaotarajia kuwamo katika kikosi chake cha msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Badala yake, Kibaden ambaye pia ni mchezaji nyota wa zamani wa 'Wekundu wa Msimbazi' aliyewahi pia kuandika rekodi kwa kuifikisha fainali ya Kombe la Shirikisho wakati akiifundisha mwaka 1993, amefichua kuwa Kaseja hakuwamo katika orodha ya wachezaji aliokabidhiwa na uongozi wa klabu yake hiyo.
Akizungumza na jana, Kibadeni, alisema wakati akikabidhiwa majina ya wachezaji wa timu hiyo ili aanze kuwanoa, jina la Kaseja halikuwamo na hivyo yeye hawezi kulirejesha kwa maamuzi yake binafsi.
"Sijamkata mimi, ila jina lake sikupewa. Hicho ndicho ninacheweza kukieleza... mambo mengine ni ya ndani ya klabu," alisema Kibaden, mshambuliaji nyota wa zamani wa timu hiyo aliyerejea kuwafundisha baada ya kuihama klabu aliyoiongoza msimu uliopita ya Kagera Sugar.
Alisema kwa sasa tayari ameshapata wachezaji 25 atakaokuwa nao katika msimu ujao wa ligi, huku akiwataja nyota wa kigeni kuwa ni wawili na wote wanatokea Uganda.
"Kikosi changu hakitazidi nyota 25, na wageni hadi leo (jana) ni kipa Abel Dhaira na beki Senkoomi (Samuel), mipango mingine ya ndani ni ya kiufundi. Mazoezi tunayoendelea nayo ni ya kawaida na wengi waliokuja kujaribiwa hawajanishawishi kuwachukua," aliongeza Kibaden.
Naye Kaseja ambaye aliwahi kusema kitambo kuwa hahofii kutemwa Simba, alisema kuwa hivi sasa anachofanya ni kuendelea kujiweka 'fiti' ili atumikie vizuri taifa kwa sababu yeye na wenzake wa kikosi cha timu ya taifa (Taifa Stars) wana kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa wanashinda katika mechi ijayo dhidi ya Uganda na kujiweka katika mazingira mazuri ya kufuzu kwa fainali zijazo za kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN).
"Jamani kuhusiana na Simba siwezi kusema lolote kwa sasa... ila maisha ni popote," alisema nahodha huyo wa Taifa Stars ambaye wiki iliyopita alishuhudiwa akiwa katika mazoezi ya timu ya vijana ya Simba B, akishauriana na kocha msaidizi wa timu hiyo, Amri Said.
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage hakutaka kueleza wazi suala la Kaseja na badala yake akasema kuwa hivi sasa, suala la nani asajiliwe na nani aachwe liko katika mamlaka ya kamati yao ya ufundi inayoshirikiana na benchi lao la ufundi.
Rage alisema vigezo vya kusajili mchezaji ni muhimu zaidi kutekelezwa na makocha na kisha kamati ya utendaji itakuwa ya  mwisho kwa lengo la kutoa baraka.
 
NIPASHE

CHADEMA yafichua njama nzito dhidi yao

Mussa Tesha aliyemwagiwa tindikali katika uchaguzi mdogo wa Igunga
Viongozi Wakuu wa CHADEMA (kulia) Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuna mpango mchafu wa kuwabambikizia viongozi wakuu wa chama hicho kesi ya kumwagiwa Tindikali kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Musa Tesha.
Viongozi wanaoandaliwa mpango huo ni Mwenyekiti, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, Mnyika alisema mpango huo unafanyika kwa lengo la kukidhoofisha chama chao kinachowapa wakati mgumu CCM.
Alisema hivi sasa baadhi ya makachero wa polisi wamekuwa wakiwakamata vijana na kuwalazimisha kukiri kwa kuandika au kuandikiwa maelezo kuwa viongozi hao waliwatuma kummwagia tindikali Tesha wakati wa uchaguzi mdogo wa Igunga mwaka 2011.
Mnyika alisema wafuasi wao waliokamatwa na polisi kwa kuhusishwa na tukio hilo wameshinikizwa kusema Mbowe, Slaa, Lissu na yeye ndio waliowatuma kummwagia tindikali Tesha.
Alisema jambo hilo linaendeshwa kisiasa, ambapo wafuasi wanne wameshatiwa mbaroni na kuwalazimisha kuwataja viongozi wakuu wa CHADEMA kuhusika na uhalifu huo.
Mnyika aliwataja waliokamatwa ni pamoja na Evodius Justinian, aliyeshikiliwa kwa siku mbili mjini Bukoba, na baadaye akapelekwa Mwanza kabla ya kufikishwa Dar es Salaam.
Alisema zoezi hilo lilifanyika kwa kificho na mtuhumiwa huyo baadae alifikishwa Igunga.
Alibainisha kuwa taarifa za kada huyo kupelekwa Dar es Salaam  zilikuwa za kificho kwani wakili wake, Nyaronyo Kicheere aliyeongozana na ndugu wa mtuhumiwa huyo walipofika Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam walielezwa amepelekwa Makao Makuu.
Mnyika alisema mara baada ya Evodius kuonana na wakili wake, Kicheere, siku hiyo alieleza unyama aliofanyiwa na jeshi hilo wakati wote wa mahojiano mkoani Mwanza na Dar es Salaam.
Katika maelezo yake yaliyoshuhudiwa na Ofisa wa Polisi Makao Makuu, Advocate Nyombi, Evodius alisema kuwa baada ya kutolewa mjini Bukoba kwa siri bila ndugu zake kujua, alipelekwa jijini Mwanza na kuhojiwa bila kuruhusiwa kuonana na wakili wake.
Kada huyo akisimulia unyama aliofanyiwa alisema:  “Nimepigwa na polisi Mwanza, nikiwa chooni Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam wakati naletwa huku, polisi wakaniambia mimi ni mtu hatari sana, niseme nilifanya nini Igunga na kama najua mkanda wa Lwakatare.
“Nikiwa Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam niliomba kwenda chooni, waliingia pamoja na mimi wakanipiga sana, nimeshaandika maelezo kwa kulazimishwa, niliomba kuwa na wakili wakanikatalia.”
Aliongeza kuwa akiwa Dar es Salaam alihojiwa aseme ukweli kuhusu video ya Lwakatare. Akawajibu kuwa ilifanyiwa uhariri na Ludovick, lakini akapigwa makofi na askari wakaagiza nyaya za umeme za kutesea.
“Waliposimama kuleta nyaya za umeme, kwa kuhofia mateso ya umeme nikasema hii video ni yangu. Ninaumwa sana tumbo la kuhara damu, natumia dawa nilizonunuliwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Mkoa wa Kagera tarehe 4 Aprili,” alisema.
Mnyika alisema mtuhumiwa wa pili aliyeteswa ili akubali kuandika kuwa Mbowe, Slaa, Lissu na Mnyika walimtuma akammwagie tindikali Tesha ni Seif Kabuta aliyekamatwa Mwanza.
Alisema Kabuta baada ya kukataa kukiri kuwa viongozi wake wanahusika na matendo hayo, walimfungia katika chumba maalumu wakamleta mke wake, mama yake na mkwe wake na kumtesa mbele yao ili akiri kuwa Mbowe na wenzake walimtuma kummwagia Tesha tindikali.
Mnyika alisema mtuhumiwa wa tatu aliyekamatwa kuhusishwa na tindikali ni Oscar Kaijage wa Shinyanga mjini, ambaye awali alipokamatwa aliambiwa ni kwa sababu kuna pesa zimepotea kwa njia ya simu, na yeye alikuwa anajishughulisha na uwakala wa pesa kwa njia ya mitandao ya M-pesa na Z-pesa.
Alisema mtuhumiwa huyo alipokutanishwa na makachero wa polisi makao makuu, naye alilazimishwa aseme kuwa Mbowe, Slaa, Lissu na Mnyika walimtuma akammwagie Tesha tindikali.
Mnyika alisema mtuhumiwa wa nne ni Rajab Kihawa, aliyetumiwa wasichana kuitwa akiwa Dodoma, ambaye aliombwa akubali kupewa shilingi milioni 30, kama alivyolipwa Ludovick ili aseme kuwa Mbowe na wenzake waliwatuma kummwagia tindikali Tesha.
Mtuhumiwa wa mwisho ni Henry Kilewo, Katibu wa CHADEMA wa Wilaya ya Kinondoni, na Katibu wa Makatibu wa CHADEMA Kanda Maalumu ya Dar es Salaam anayeshikiliwa na polisi.
Polisi wanamtuhumu Kilewo kummwagia tindikali Tesha wakati wa uchaguzi mdogo wa Igunga mwaka 2011.
Kilewo alishikiliwa na polisi kuanzia Ijumaa iliyopita na baada ya kuhojiwa alichukuliwa kwa kificho kupelekwa Mwanza kwa ndege ili aweze kuunganishwa katika kesi hiyo ya Igunga leo.
Mnyika alisema Kilewo amesafirishwa bila wakili wake kuwa na taarifa kuwa amepelekwa Mwanza, wala mke wake aliyeambiwa ampelekee  chakula, lakini alipofika polisi aliambiwa mume wake hayupo.
Mmoja wa mawakili wanaokwenda Igunga kuwatetea Kilewo na wenzake, Profesa Abdallah Safari alisema wameshitushwa kusikia wateja wao wamelazimishwa kutoa maelezo ili kuwahusisha viongozi wakuu wa CHADEMA.
Alibainisha kuwa kutokana na kesi hiyo kuonekana kujaa masuala ya kisiasa, atashirikiana na mawakili wenzake ambao ni Peter Kibatala na Gasper Mwalyela na kama itakapolazimika watawaongeza Mabere Marando, Kicheere, Method Kimomogoro na Lissu.
Aliongeza kuwa imefika hatua itabidi atumie kifungu cha sheria cha 102, ili kujenga dhana ya kutiliwa shaka kwani viongozi wote wa CHADEMA sasa wamefunguliwa kesi katika maeneo mbalimbali nchini, huku wale wa CCM wakiachwa.
Profesa Safari alitolea mfano Mbunge wa Tabora mjini, Ismail Aden Rage, ambaye alipatwa na hatia katika uchaguzi wa Igunga na alipaswa kufungwa miaka mitatu bila fidia, lakini DPP amekalia faili lake hadi sasa.
Aliongeza kuwa mambo hayo yanajitokeza kutokana na CHADEMA kumtaja ofisa wa usalama anayeitwa Shaali Ally kuwa ndiye aliwatafuta vijana wa chama hicho akiwemo Ahmed Sabula na wenzake.
Alibainisha kuwa Machi 29, mwaka huu vijana hao waliitwa na Shaali katika chumba cha hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam, akiwataka wakubali kutumika kwa kutoa taarifa za vikao vya CHADEMA, kuwasilisha kwake nyaraka za kamati kuu na kueleza mipango ya chama katika kesi ya Lwakatare.
Kwenye mpango huu, ofisa huyo wa usalama wa taifa ambaye Marando alisema anamfahamu vizuri, alimuahidi Sabula kiasi cha sh milioni 30 na kwamba fedha hizo angelipwa kama ujira kwa kukubali kutoa ushahidi dhidi ya Lwakatare.

Chanzo:TANZANIA DAIMA

Mwanamke Iringa ateketeza watoto wa jirani yake kwa wivu wa mapenzi

Picha hii haihusiani na habari hii, ila inaonyesha taswira ya nyumba iliyoteketea kwa moto
 MWANAMKE mmoja anayefahamika kwa jina la Taraji Muenzi, 31, mkazi wa kijiji cha Mwatasi, wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, anashikiliwa na jeshi la Polisi mkoani humo kwa kosa la kuichoma nyumba ya jirani yake na kuwateketeza watoto wawili waliokuwa ndani mwake pamoja na vitu vyote katika nyumba hiyo kwa kilichoelezwa wivu wa mapenzi.
Habari kutoka mkoani humo zinasema watoto walioteketezwa wakiwa ndani ya nyuma hiyo ni Faraji, 6 na Jacob, 3 ambao walikuwa watoto pekee wa Subira Kisitu aliyekuwa akituhumiwa na mtuhumiwa huyo kuwa anatembea na mumewe.
Inaelezwa kuwa Taraji kwa muda mrefu alikuwa akimtuhumu jirani yake kumuibia mume na kumchimba mkwara kwamba atamfanyizia, kiasi cha uongozi wa eneo lao kuitisha kikao na kumtwanga faini ya Sh 10,000 aliotakiwa kuilipa juzi, Juni 22 siku aliyofanya tukio hilo.Inaelezwa uongozi wa kitongoji hicho kiliamua kumtoza faini baada ya wiki iliyopita kumvamia jirani yake nyumbani kwake na kumwagia mboga na kusisitiza kuwa kuna kitu atakachomfanyia ambacho hatasahau maishani kama siyo kwa kumuua kwa sumu basi kwa kumchomea moto nyumba yake.
Hata hivyo inaelezwa kuwa jana juzi usiku akiamini kuwa jirani yake yupo ndani na wanawe aliamua kuichoma moto nyumba hiyo, ila kwa bahati mbaya jirani zake alikuwa klabuni akipata kinywaji na hivyo watoto pekee waliokuwa wamelala ndani ndiyo waliougua na kufa pamoja na mali zote.
Kamanda wa Polisi wa Iringa, Ramadhani Mungi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza wanamshikilia mwanamke huyo ili kumfikisha mahakamani kwa kitendo alichokmifanya ambacho kimeacha gumzo kijiji cha Mwatasi, huku familia ya watoto ikiwa katika majonzi makubwa ya kupoteza watoto wao.

Sunday, June 23, 2013

Mbunge Sugu amuomba radhi Waziri Mkuu, kisa...!

Mhe Sugu
Waziri Mkuu, Mhe. Pinda
BAADA ya kauli yake iliyoibua mjadala mkubwa nchini dhidi ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda kufuatia majibu yake aliyoyatoa wiki iliyopita Bungeni kwa kutaka Polisi kuendelea kuwapiga raia, Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe Joseph Mbilinyi 'Sugu', aomba radhi.
Sugu amemuomba radhi mhe Pinda na watanzania kwa ujumla kwa lugha aliyotumia katika kuonyesha hisia zake juu ya kauli aliyoitoa mhe Pinda bungeni.
Kupitia akaunti yake ya Facebook, Mbunge huyo machachari amenukuliwa akiwaomba radhi Watanzania waliokerwa na kauli yake iliyodai kwamba Tanzania haijawahi kuwapata Waziri Mkuu kama Mhe. Pinda kwa kusema;
"Ndugu watanzania, naombeni radhi kwa tusi nililolitoa kwa mhe Pinda, kwani nilikua nimeghafirika, halikuwa kusudio langu kumtukana mmoja wa viongozi wa nchi."

Kiemba, Sure Boy ndiyo Wanasoka Bora Tanzania 2012

Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah akimpa tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi, Salum Abubakar 'Sure Boy' wa Azam

KIUNGO nyota wa timu ya Simba na Taifa Stars, Amri Kiemba amefanikiwa kutwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Tanzania iliyotolewa na Chama cha Wanasoka Tanzania, SPUTANZA, katika hafla iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es salaam.
Kiemba amenyakua tuzo hiyo iliyodhaminiwa na kampuni ya Pepsi kwa ufanisi wake kwa msimu uliopita ambapo amekuwa katika kiwango cha juu akiisaidia kuifungia simba mabao 8 kwa msimu uliopita huku akiibeba Stars katika mechi zake za kimataifa.
Naye kiungo mwenye mapavu ya mbwa, Abubakar Salum 'Sure Boy' alinyakuwa tuzo ya Mwanasoka Bora Chipukizi, tuzo ambayo alistahili kutokana na umahiri wa mchezaji huyo anayeichezea Azam na Taifa Stars.
Wengine walionyakua tuzo katika hafla hiyo ni kipa wa Mtibwa, Hussein Sharrif 'Casillas' aliyekuwa Kipa Bora wa Mwaka na kocha Mecky Mexime wa Mtibwa.
MICHARAZO inawapa pongezi wote waliotwaa tuzo hizo na kuwatakia mafanikio mema, kadhalika inawapa heko SPUTANZA na wadhamini wa tuzo hiyo ya kwanza kuandaliwa na chama hicho.