STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, July 27, 2013

Kazi ataka wajumbe TFF wakamilishe Kazi aanze Kazi

Osman Kazi akiwa kazini katika pambano la Wabunge wa Simba na Yanga
MWAMUZI wa zamani wa kimataifa, Osman Kazi amewaomba wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa shirikisho la soka (TFF) kuhakikisha wanachagua viongozi bora ambao wataleta maendeleo ya mchezo huo nchini.
Aidha mwamuzi huyo amesema anajiandaa kurejea tena kwenye kazi yake baada ya kujiondoa kimya kimya tangu alipokumbwa na adhabu ya kifungo cha miezi mitatu kwa tuhuma za rushwa.
Akizungumza na MICHARAZO, Kazi alisema anawaomba wapiga kura wa TFF kutofanya makosa katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Septemba.
Kazi alisema kosa lolote litakalofanywa na wajumbe hao wa TFF kunaweza kuirejesha nyuma nchi kama ilivyokuwa miaka iliyopita kabla ya uongozi wa Rais anayemaliza muda wake, Leodger Tenga.
Alisema wapiga kura wahakikishe wanachagua viongozi ambao watakuwa na maono ya mbele ili nchi irejeshe heshima yake katika medani ya kimataifa katika mchezo huo ikiwemo kutoa waamuzi katika michuano ya kimataifa.
"Rai yangu kwa wajumbe wa TFF wahakikishe hawafanyi makosa kwa kuchagua viongozi watakaoturejesha nyuma, wawachague viongozi bora na makini na wenye uchungu wa kweli na mchezo wa soka badala ya kushinikizwa kuchagua watu kwa uwezo wao kifedha," alisema.
Kuhusu hatma yake ya uamuzi, Kazi alisema anajiandaa kurejea tena dimbani ila itategemea na aina ya viongozi watakaoingia madarakani TFF.
Alidai kama watakuwa ni wababaishaji, ni bora aendelee na uratibu wake wa matamasha na kama watakuwa ni wenye weledi atashiriki Copa Test ya Desemba.
"Bado nina miaka sita mbele kabla ya kustaafu rasmi kwa sheria za kimataifa za urefa, hivyo kama viongozi watanivutia kwa uwezo wao nitarejea kwa kuanza Cooper Test ya Desemba ili mwakani niwanie beji ya FIFA niliyovuliwa kimizengwe tangu mwaka 2005," alisema Kazi.

Serikali yaja na mikakati ya kuibua ajira 30,000 kwa wahitimu wa Vyuo Vikuu

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjH1bttKwptQaUumeTy5iQpTKX7qhgREzLaMpw_UjLldbYRkqeqi-I2EdgvtaLiMtAs04sNUGZBslW7C-tAE2PTEM0dxDbjDjE4XhZ78Jo0YZj9pO9h5YJiDKO3hNefCFXpxp64lVotQ-JE/s400/Waziri+wa+Kazi+na+Ajira+Bi.+Gaudentia+Kabaka.JPG
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudencia Kabaka

Na Suleiman Msuya
WIZARA ya Kazi na Ajira ipo katika mkakati wa kuanzisha programu ambayo itahusisha vijana waliomaliza vyuo vikuu na kuweza kuzalisha ajira 30,000 kwa kipindi cha miaka mitatu.
Hayo yamebainishwa na Msemaji wa Wizara hiyo Ridhiwan Wema wakati akizungumza na mwandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Alisema programu hiyo itatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na vyuo vya elimu ya juu nchini, taasisi za fedha na wabia wa maendeleo mbalimbali.
Wema alisema kwa kuanzia wake utaanza kwa kuendeleza programu ya mfano iliyoanzishwa na Idara ya kilimo, uchumi na biashara katika Chuo Kikuu cha Sokoine (DAEA-SUA) na hatimaye kuwafikia wahitimu wa vyuo vingine vya elimu ya juu.
Msemaji huyo alisema kwa kuanzia Serikali imekubaliana na Benki ya CRDB kuanzia utoaji wa mikopo kwa vijana mara utekelezaji wa programu utakapoanza.
“Tumekuja na programu mpya ambayo tunatarajia kuwa itaweza kuzalisha ajira 30,000 baada ya miaka mitatu na itagharimu shilingi bilioni 54.451 kwa kuhusisha vijana wa vyuo vikuu nchini wanaomaliza kwani takwimu zinaonyesha kila mwaka ni asilimia 48,” alisema.
Alisema madhumuni ya programu hiyo ni katika utekelezaji wa sera ya Taifa ya Ajira ya mwaka 2008 ya kuhamasisha uzalishaji wa kitaifa kufanikisha ajira kalimi  yenye kipato.
Wema alisema lengo la programu hiyo ambayo inahusisha vijana ni kuhakikisha kuwa vijana zaidi ya laki moja (100,000) wanapata ajira kupitia hatua mbalimbali kulingana na sifa zao.
Msemaji huyo pia lengo hilo ni kuongeza idadi ya vijana wanaomiliki shughuli rasmi za kiuchumi na wamejiajiri na kuajiri wengine, kukuza utamaduni wa kijasiriamali pamoja na ubunifu na kuhamasisha matumizi bora ya nguvu kazi.

Lissu aponda uendeshaji wa Bunge, adai unakwamisha mengi ya maana

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh7-RqMhZYObN7yssSphvShWb4-noohMWpS-9fKfjYq9-a2R7Xz-srjovqDZ9GotCSbrnW7vv17aUlo9XPnNVAjodYGYnPkKGQSWQYzKhmMcl2bkgMEK3xC49D9gnIOeqlhXBydAVfiM8KX/s320/tundu+lissu.jpg
Tundu Lissu akiwa Bungeni
Na Suleiman Msuya
MBUNGE wa Jimbo la Singida Kaskazini Tundu Lissu amesema itakuwa maajabu kwa wabunge wa Bunge la sasa kufanya maajabu kutokana na mfumo wa uendeshaji wake.
Lissu alisema hayo jijini Dar es Salaam wakati akichangia katika kongamano linaloratibiwa na taasisi ya  Jukwaa la Jamii (Policy Forum) kila mwisho wa mwezi.
Alisema kumekuwepo na dhana kuwa wabunge ndio wanaweza kufanya maamuzi katika masuala ya kitaifa lakini kusema ukweli mfumo wa uendeshaji wake itakuwa jambo gumu kwa sasa.
Mbunge huyo ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni alisema ili Bunge hilo liweze kuwa na tija ni wakati muafaka kwa wananchi kufanya maamuzi sahihi pindi wanapopatiwa fursa hiyo.
“Jamani Watanzania napenda kuwaambia kuwa kwa mfumo wa Bunge hili la sasa wasitarajie kutokea maajabu kwani inabidi iwe hivyo ila wakati wa kufanya mabadiliko unakaribia,” alisema.
Lisu alisema dhana ya kuwa uchangiaji wa wabunge kuonekana wa mashaka unachangiwa na elimu alikanusha suala hilo na kusema mfumo mzima ndio chanzo cha matatizo hayo hivyo ni vema wananchi wakawa na subira ili kuhakikisha kuwa mabadiliko yanatokea.
Alisema elimu sio sababu ya kuonekana kwa uwezo mdogo kutokana na ukweli kuwa hakuna mtu yoyote ambaye anaweza kuwa mjuzi wa kila jambo.
Mbunge huyo alisema wabunge wengi hawana ofisi jambo ambalo linachangia kufanya kazi hata wakiwa baa hali ambayo haiwezi kuleta tija kwa maslahi ya nchi.
Alisema kumekuwepo na changamoto kubwa juu ya nguvu ya maamuzi kati ya Bunge na Serikali hali ambayo inachangia upande mmoja kujiona ndio wenye sifa ya kufanya maamuzi ya mwisho.
Lisu alisema Bunge limekuwa likinyimwa nafasi kutokana na dhana kuwa iwapo watakuwa na msimamo juu yabhoja Fulani ni dhahiri kuwa upo uwezekano wa Bunge kuvunjwa ambapo wabunge waliowengi wanaamini kuwa wanaweza wasirudi baada ya uchaguzi.
Kwa upande wake Mbunge wa Kisesa Luhanga Mpina alisema mfumo wa kuwasilisha bajeti bado unachangamoto nyingi ambazo zinahitaji kufanyiwa marekebisho ili kuhakikishakuwa bajeti inaleta tija kwa jamii.
Mpina alisema kumekuwepo na tabia ya kuwasilisha vitu nusu nusu wakati bunge likiendelea na vingine kutowasilishwa jambo ambalo linatia shaka juu ya nini kinafichwa katika mchakato huo.
Alizitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na kukosekana kwa ofisi ya Bunge ya bajeti, kutopatikana kwa vitabu vya mapato, uwazi juu ya matumizi ya misaada, taarifa za mkaguzi na zinginezo nyingi.
Mbunge huyo ambaye amekuwa na msimamo wa kujiamini pindi anapochangia hija zake Bungeni alisema ni vema kukawa na uwazi juu ya masauala ya katiba, uelewa na kuhakikisha kuwa wabunge wanashiriki kikamilifu tangu awali.

UNYAMA! Baba awauwa wanae wawili Kigoma, kisa mibangi!

Mauaji dhidi ya watoto kila kona. Hapa ni mwili wa mtoto Ayoub Agen ulipokuwa ukienda kuzikwa baada ya kuuwawa kinyama huko Rungwe mkoani Mbeya hivi karibuni. Watoto watafanyilia ukatili kama huo mpaka lini?
MATUKIO ya kikatili dhidi ya watoto wasio na hatia yamezidi kuendelea safari hii watoto wawili wachanga wamejikuta wakiuwawa kikatili na baba yao mzazi ambaye anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kigoma kwa mauaji hayo yaliyotokea juzi asubuhi katika kijiji cha Mvugwe wilayani Kasulu.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Kigoma, Fraiser Kashai, unyama huo ulifanywa na Majuto Thobias, 27 Jumatano asubuhi kwa kuwauwa watoto wake mwenyewe, mmoja akimchoma kisu na mwingine kichanga cha miezi mitatu kwa kumbamiza sakafuni na kumtoa uhai.
Kamanda huyo alisema majuto alimchoma kitu Loyce Majuto mwenye miaka miwili kifuani na kukishindilia hadi alipokata roho kabla ya kumgeukia kichanga kingine kilichokuwa kitandani chenye miezi mitatu kikiwa hakina jina bado na kumbamiza chini mara tatu hadi alipokufa.
Inaelezwa kuwa wakati mwanaume katili akifanya unyama huo, mkewe alikuwa nje akipika na aliposikia vilio vya wanae alikimbilia ndani na kukumkuta mtuhumiwa huyo akifanya ukatili huo kwa watoto wao.
Kamanda alisema mwanamke huyo aliamua kupiga mayowe kuita majirani baada ya kuwashuhudia wanawe wakiuwawa kikatili na ndipo walipofanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo na kumfikisha kituo cha Polisi.
"Inaelezwa kuwa mtuhumiwa huyo ambaye tunamshikilia alifanya ukatili huo kwa watoto wake kutokana na kile kinachoelezwa kuwa mtumiaji sugu wa dawa za kulevya aina ya bangi na kwamba upelelezi juu ya tukio hilo unaendelea kufanyika kabla ya kumfikisha mahakamani kwa makosa yanayomkabili" alisema.

Serikali yawakumbuka wanyonge


Na Suleiman Msuya
SERIKALI kupitia Wizara ya Sheria na Katiba ipo katika mchakato wa kutunga sheria ya Msaada wa Kisheria ambayo inalenga kuwasaidia wananchi na uwezo wa kulipia gharama zinazotozwa na Mawakili wa kujitegemea.
Hayo yamebainishwa Msemaji wa Wizara hiyo Farida Khalfan wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Alisema Wizara ya Sheria mwaka 2010 iliiunda kikosi kazi ambacho kilishirikisha wadau mbalimbali kufanya utafiti na kutoa mapendekezo juu ya mfumo sahihi ambao utakidhi hitaji kwa kila raia.
Msemaji huyo alisema baada ya kikosi kazi hicho kuwasilisha mapendekezo s.erikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria ilianza utaratibu wa kutunga sheria itakayojulikana kama (Sheria ya Msaada wa Kisheria)
Khalfan alisema maandalizi ya sheria hiyo yapo katika hatua za mwisho ambapo matarajio yao ni kuhakikisha kuwa sheria hiyo inawasilishwa Bungeni ifikapo Januari mwaka 2014.
“Tumekuwa tukifuatilia changamoto ambazo zinawakuta wananchi hasa katika masuala ya kisheria ila kutokana gharama kubwa ila tunaaamini kuwa mwakani utatuzi utakuwa ukipatikana,” alisema.
Alisema katika sheria hiyo itaunda chombo huru kitakachokuwa na majukumu mbalimbali ambayo ni kusajili taasisi zinazotoa msaada wa kisheria, kusajili watoa msaada wa kisheria, kuweka ubora wa viwango katika utoaji msaada wa kisheria na kuvisimamia.
Khalfan alisema pia chombo hicho kitasimamia nidhamu na maadili ya watoa huduma za msaada wa kisheria, kutambua wasaidizi wa kisheria na kutafuta fedha ili kutekeleza majukumu yake.
Alisema matoke ya kuwepo kwa sheria hiyo ni dhahiri kuwa watoa msaada wa kisheria atatakiwa kusajiliwa ili waweze kutoa huduma hiyo kupitia vituo vilivyosajiliwa kutoa msaada huo.
Msemaji huyo alisema kukosekana kwa sheria hiyo ndio sababu mojawapo ya kuwepo kwa watu wasio na sifa za kutoa huduma hiyo ambao wanatambulika kama (Bush Lawyers) ambao wamekuwa wakiwarubuni wananchi kuwa wanaweza kuwasaidia kisheria.
Alisema kupita kwa sheria hiyo kutasaidia jamii mbalimbali kama watoto, wajane na watu wote ambao wamekuwa wakipata shida ya msaada wa kisheria nchini kutokana na gharama kubwa zinazotozwa na wanasheria .

Miyeyusho kumvaa Mzambia Dar Live siku ya Idd Mosi

Bondia Francis Miyeyusho kushoto akitia saini mkataba wa makubaliano ya kucheza siku ya sikukuu ya Idd Mosi dhidi ya Darius Lipupa wa Zambia mpambano utakaopigwa katika ukumbi wa Dar Live kushoto ni Rais wa TPBO LIMITED Yassin Abdallah 'Ustaadh'  

Bondia Francis Miyeyusho kushoto akitia saini ya Dole Gumba  mkataba wa makubaliano ya kucheza siku ya sikukuu ya Idd Mosi na Darius Lipupa wa Zambia mpambano utakaopigwa katika ukumbi wa Dar Live kushoto ni Rais wa TPBO LIMITED Yassin Abdallah 'Ustaadh'  

Rais wa TPBO LIMITED Yassin Abdallah 'Ustaadh' kushoto akimkabidhi kiasi cha pesa bondia Francis Miyeyusho kama sehemu ya maandalizi ya mpambano wake utakaofanyika siku ya Sikukuu ya Idd katika ukumbi wa Dar Live 

Friday, July 26, 2013

RAIS KIKWETE ACHIMBA MKWARA MAJAMBAZI, WAHAMIAJI HARAMU





RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho ameamuru majambazi na wahamiaji haramu wote katika mikoa mitatu nchini kujisalimisha katika muda wa siku 14 kuanzia leo, Ijumaa, Julai 26, 2013 kabla ya kuanza kwa operesheni kubwa kuliko zote katika historia ya Tanzania nyenye lengo la kukomesha ujambazi katika mikoa hiyo na kukamata wahamiaji haramu.

Rais Kikwete ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu amesema kuwa leo ametoa amri kwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama nchini kuanza maandalizii ya operesheni hiyo na hatimaye kuiendesha katika Mikoa ya Kagera, Kigoma na Geita.

Majambazi wanateka magari, wanaua watu wetu, wanapora mali zao. Watanzania hawawezi kuendelea kuishi kwa hofu, woga na taabu katika nchi yao wenyewe. Tutawasaka majambazi misituni, tutawasaka majumbani, tutachimbua ardhini kutafuta hata silaha zilizofukiwa chini,” amesema Rais Kikwete.

Rais Kikwete ametoa amri hiyo mchana wa leo, Ijumaa, Julai 26, 2013 wakati alipohutubia wananchi wa mjini Biharamulo, Mkoani Kagera, kabla ya kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kagoma, Wilaya ya Muleba kwenda Lusahuga, Biharamulo.

Rais Kikwete ametoa amri hiyo kufuatia matukio ya mara kwa mara na yasiyokuwa na mwisho ya majambazi kuteka mabasi, kuua watu na kupora mali zadi katika mikoa hiyo, hali ambayo imesababisha malalamiko ya wakazi wa mikoa hiyo.

Rais Kikwete ameaambia wananchi: “Tumeamua kukomesha upuuzi huu katika mikoa ya Kagera, Kigoma Geita. Leo nimetoa maagizo kwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama – Jeshi la Wananchi, Jeshi la Polisi, Uhamiaji na Usalama wa Taifa kuandaa operesheni maalum, operesheni kubwa kuliko zote tokea tupate uhuru. Upuuzi huu hauwezi kuendelea.”

Ameongeza Rais Kikwete na kuwaambia wananchi: “Nawaamuru majambazi wote, wenye kumiliki silaha kinyume cha sheria na wahamiaji haramu wote wajisalimishe katika wiki mbili kuanzia leo. Wajisalimishe wao pamoja na silaha zao. Baada ya hapo, tunaanzisha operesheni ambayo haijapata kuonekana katika historia ya nchi yetu.”

Amesisitiza Rais Kikwete: “Sitanii, sina mzaha na hili. Nimechoka. Nalisema hili mchana, macho makavu. Nawaambia majambazi watafute kazi nyingine, kazi hii hailipi tena. Kwa wale majambazi na wahamiaji haramu kutoka nchi za jirani, waanze safari ya kurejea kwao.”

Rais Kikwete ameonya: “Na hata wale wanaoishi na kulea majambazi na wahamiaji haramu nao wajisalimishe. Na ole wao majambazi watakaojaribu kuwapiga risasi askari wetu. Watakiona cha mtema kuni.”

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

Uzinzi wamfikisha kiongozi CHADEMA kortini


RORYA,Tanzania
MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Rorya mkoani Mara ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Tai kupitia Chama hicho, Masirori Kyorang  amefikishwa Katika Mahakama ya Mwanzo Shirati kujibu mashitaka ya ugon Kwa mujibu wa kesi hiyo, Kyorang anadaiwa kushikwa ugoni na mke wa mlinzi wa Mbunge wa Jimbo la Rorya wakiwa gesti ya Triple Kabwana katika mji mdogo wa  Shirati, suiku wa kuamkia jana.

Akisomewa Mashitaka hayo  jana Julai 24, na Mwendesha Mashitaka wa Polisi mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Shirati Dock Nyatega , ambapo ilidaiwa kuwa mheshimiwa Masirori alikamatwa  mida ya saa 3 usiku, katika chumbani akiwa na mke wa mlinzi huyo wa Mbunge wa Jimbo la Rorya aliyejulikana kwa jina Pendo Omolo.

Mtuhumiwa Masirori alikana Mashitaka yake na kupata Dhamana hadi kesi yake itakapotajwa tena Julai  29 , ambapo Mke huyo Pendo amekwenda Nyumbanio kwao hadi Shauri hilo litakapoanza kusikilizwa na kubaini Ukweli wake baada ya Ushahidi kutolewa Mahakamani alisikika akisema Hakimu Nyatega .
 Habari hii imeandikwa na Samson Chacha, 0788312145, 0762219255

Arsenal njia nyeupe kumnasa Suarez ni baada ya Real kujiondoa kwenye mbio za kumwania



KLABU ya Arsenal ipo katika nafasi nzuri ya kumnyakua mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez baada ya Real Madrid kujiondoa kwenye mbio za kumwania mchezaji huyo kutoka Uruguay.
Duru za michezo zilizonukuu chanzo kutoka ndani ya Santiago Bernabeu, zinasema kuwa bosi mpya wa Real Madrid, Carlo Ancelotti hana mpango wa kuongeza mshambuliaji mwingine baada ya kumuuza Gonzalo Higuain kwa Napoili ya Italia wiki hii.
Ancelotti anaamini kwamba silaha alizonazo katika safu yake ya mbele ikiongozwa na Cristiano Ronaldo na Karim Benzema inatosha kabisa kuua wapinzani wake.
Kocha huyo wa zamani wa Chelsea pia anataka kuwapa nafasi makinda wanaoichezea timu ya taifa ya Hispania u21, Jese Rodriguez na Alvaro Morata ndiyo maana hana sababu ya kunyakua strika mwingine.
Chanzo hicho kilichonukuliwa na gazeti la michezo la Marca, kimesema " Tunaimani kubwa kwa Jese na Morata wataziba nafasi hiyo. Ni wazuri sana. Hatuna haja ya kusaini mshambuliaji mwingine mpya,"
Kwa maana hiyo ni kwamba njia ipo nyeupe wa Arsenal kumnyakua mchezaji huyo baada ya mbio za muda mrefu.

After Death ya kumuenzi Kanumba kutolewa hadharani Jumanne


FILAMU maalum kwa ajili ya kumuenzi marehemu Steven Kanumba iitwayo 'After Death' inatarajiwa kuachiwa rasmi mtaani kuanzia kesho.
Filamu hiyo iliyotungwa na Jacklyne Wolper na kuongozwa na Leah Richard 'Lamata' kama njia ya kuenzi kipaji na mchango wa marehemu Kanumba imeshirikisha wasanii kadhaa nyota waliowahi kufanya kazi na mkali huyo aliyefariki mwaka mmoja uliopita.
Akizungumza na MICHARAZO muda mfupi uliopita, Lamata alisema filamu hiyo iliyozinduliwa siku ya kumbukumbu ya kifo cha Kanumba Aprili 7 mwaka huu itaachiwa kesho Jumanne baada ya taratibu zote kukamilika kwa wasambazaji wao.
Alisema anaamini filamu hiyo itarejesha kumbukumbu za majonzi kwa mashabiki wa marehemu Kanumba, lakini pia watapata burudani baada ya kupita mwaka mmoja tangu wampoteze nyota huyo aliyekuwa akitamba kimataifa.
"Hayawi hayawi sasa yamekuwa, ile filamu ya kumuenzi marehemu Kanumba iliyochezwa na wakali karibu wote waliowahi kufanya kazi na mkali huyo iitwayo 'After Death' itaachiwa rasmi siku ya Jumanne ya Julai 30," alisema Lamata.
Lamata aliwataja baadhi ya wasanii waliocheza filamu hiyo ni pamoja na chipukizi walioibuliwa na Kanumba, Hanifa Daud 'Jenifer' na Othman Njaidi 'Patrick'.
Pia ndani yake wamo wakali kama Ruth Suka 'Mainda', Samsha Ford, Stanley Msungu, Patcho Mwamba, Ben Branco, Wolper, Irene Paul, Uncle D aliyeshabiana na marehemu Kanumba na wengineo.

Stars kushambulia mwanzo mwisho kesho, kaseja kukaa langoni Chuji, Bocco ndani



Na Boniface Wambura
MOJA ya mikakati ya Taifa Stars kwenye mechi ya kesho (Julai 27 mwaka huu) dhidi ya Uganda kuwania kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Tatu za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini ni kushambulia kwa muda mwingi wa mchezo.

Kocha Kim Poulsen amesema maandalizi ya Taifa Stars jijini Mwanza kwa ajili ya mechi hiyo ambayo Uganda inaongoza kwa bao 1-0 yalikuwa mazuri, lakini mabao ni muhimu hivyo watashambulia bila kusahau kulinda lango lao.

“Unapocheza mechi za aina hii za nyumbani na ugenini, huku mwenyeji akiwa anaongoza mabao yana maana kubwa katika mechi. Mabao yanabadili mchezo na pia wachezaji kifikra,” amesema Kim akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Mt. Zion ambayo Stars imefikia.

Amesema katika mechi ya kwanza walitengeneza nafasi nyingi lakini hawakuzitumia, hivyo wamekuwa wakifanya mazoezi ya kushambulia, jinsi ya kutengeneza nafasi, na jinsi ya kumalizia.

“Hivyo tuko hapa (Kampala) kwa ajili ya kufunga, ni lazima tufunge ili tuweze kuendelea na mashindano. Lakini ngome yetu nayo ni lazima iwe makini ili kutoruhusu bao,” amesema Kim na kuongeza kuwa kikosi chake cha kwanza ni lazima kitakuwa mabadiliko kutoka na Mwinyi Kazimoto kuingia mitini na Shomari Kapombe kwenda kwenye majaribio Uholanzi.

Amesema angalau kutakuwa na mabadiliko kwa kuingiza sura mbili mpya katika kikosi cha kwanza, na kuongeza kuwa wachezaji wanafahamu umuhimu wa mechi hiyo kwani timu ikienda kwenye Fainali za CHAN itakuwa manufaa kwao binafsi.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefanya mazoezi ya mwisho leo jioni Uwanja wa Mandela ulioko Namboole ambao utatumika kwa ajili ya mechi hiyo kesho.

Mechi hiyo itaanza saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki na itachezeshwa na waamuzi kutoka Madagascar wakiongozwa na Kanoso Abdoul Ohabee wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Andirvoavonjy Pierre Jean Eric. Mwamuzi msaidizi namba mbili ni Jinoro Velomanana Ferdinand huku Andriamiharisoa Hubert Marie Bruno akiwa mwamuzi wa mezani (fourth official). Kamishna wa mechi hiyo namba 38 ni Ismail Kamal kutoka Ethiopia.

Stars inatarajiwa kupangwa hivi; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, David Luhende, Aggrey Morris, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Salum Abubakar, Frank Domayo, John Bocco, Amri Kiemba na Mrisho Ngasa.

Hii ndiyo Ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2013-2014

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjJxOTyB99VtpqbPwxU2WK_mBVt2aJduuEaZWfhDMaKd8N3qJfKPpq8NjDtvmXwOn8ITwk3QzDisfmzEGHplUnR0t35sAqEmb96RBDSv1fAq3HwuR8omUomwPg35259yi_nsEq4eXtSTdw/s1600/ratiba+vpl.JPG

Suarez ruksa kuteta na Arsenal, ila...!

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02489/luis-suarez_2489623b.jpg
LONDON, Uingereza
LUIS Suarez ataruhusiwa kufanya mazungumzo na Arsenal baada ya klabu hiyo ya London kufikisha ofa ya paundi milioni 40 lakini Liverpool haiko tayari kumuuza mshambuliaji huyo hadi bei ya paundi milioni 50 itakapofikiwa.
Ofa iliyoweka rekodi ya Arsenal ya paundi milioni 40 jumlisha paundi moja ilikataliwa na Liverpool lakini Suarez sasa anataka kufanya mazungumzo na klabu hiyo ya London.
Ripoti nyingine zinasema mshambuliaji huyo amewaambia maafisa wa Liverpool kwamba anataka kujiunga na Arsenal na anajiandaa kuwasilisha barua ya kuomba kuondoka Anfield.
Ofa ya paundi milioni 40 inamaanisha kwamba kipengele cha kuvunjia mkataba wake kimefikiwa na hivyo ni lazima Liverpool imfahamishe kuhusu ofa hiyo na sasa yuko huru kuzungumza na Arsenal.
Arsenal wanajiandaa kumlipa Suarez mshahara wa paundi 150,000 (Sh. milioni 364) kwa wiki kwa mkataba wa miaka mitano.
Lakini Liverpool haiko tayari kumuuza hadi Arsenal watakapoongeza ofa yao.
Juzi Jumatano, Suarez aliichezea Liverpool kwa mara ya kwanza tangu tukio maarufu la kumng'ata mkononi beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic msimu uliopita, akiingia kutokea benchi katika dakika 18 za mwisho za mechi yao ya kirafiki waliyoshinda 2-0 dhidi ya Melbourne Victory kwenye Uwanja wa MCG.
Huku Liverpool ikiongoza kwa goli 1-0, Suarez alipika goli la pili la timu hiyo wakati alipomtengea mchezaji mpya Iago Aspas katika dakika za lala salama.
Baada ya mechi hiyo kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers alisema: "Hakuna kipya cha kueleza, yeye (Suarez) ni mchezaji wa Liverpool na ndani ya wiki chache zijazo tunahitaji kumrejeshea kasi yake."
Rodgers hata hivyo, alimkumbusha Suarez deni alilonalo kwa mashabiki wa Liverpool ambao walisimama upande wake kwa misimu miwili ambayo ametawaliwa na matukio ya utata.
"Sapoti aliyopata kutoka kwa mashabiki na watu wa mji wa Liverpool haipimiki," Rodgers aliongeza.
"Katika kipindi hicho alikosa mechi nyingi za timu kutokana na sababu mbalimbali. Watu walisimama upande wake kama mtoto wao na hakika walikuwa wakimtetea. Chochote kitakachotokea katika wiki zijazo jambo hilo litabaki akilini mwake kwa sababu ni mambo ambayo huwezi kuyasahau."
Liverpool sasa wamekataa ofa mbili kutoka Arsenal, ambao wamedhamiria kuimarisha safu yao ya ushambuliaji, wakati Real Madrid, ambao tayari wamemuuza Gonzalo Higuain kwa Napoli, bado pia wanamhitaji nyota huyo wa Uruguay licha ya kwamba hawajapeleka ofa yoyote.
Kufuatia ofa mpya ya Arsenal, mmiliki wa Liverpool, John Henry aliwakebehi katika ukurasa wake wa Twitter kwa kuandika: "Unadhani wanavuta/puliza nini kule Emirates?"
Haijawa wazi kama kama Henry anazungumzia majaribio ya Arsenal kutaka kumsajili Suarez au kiasi cha ofa wanazotuma.
Wakati Liverpool wanadhamiria kumbakisha Suarez, ambaye alifunga magoli 30 katika mechi 44 za klabu hiyo msimu uliopita, ugumu wao unatarajiwa kulegea kama kama ofa hiyo itazidi kuongezwa. Kama ofa ya Arsenal itakubaliwa, itakuwa ni zaidi ya mara mbili ya kiwango cha juu cha pesa walichotoa kumnunua mchezaji.
Arsenal, ambao ofa yao ya kwanza kwa Suarez ilikuwa ni paundi milioni 30, walilipa paundi milioni 17.5 kumnunua winga wa Sevilla, Jose Antonio Reyes mwaka 2004.
Suarez anataka kuondoka Anfield ili akacheze soka la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya licha ya kwamba alisaini kurefusha mkataba wake Liverpool mwaka jana tu.
Uvumi ulianza kukua kuhusu hatma ya Suarez tangu alipofungiwa mechi 10 mwishoni mwa Aprili kwa kumng'ata Ivanovic.
Mshambuliaji huyo amebakisha mechi sita za kutumikia katika kifungo chake na pia alifungiwa mwaka 2011 baada ya kukutwa na hatia ya kumfanyia vitendo vya kibaguzi beki wa Manchester United, Patrice Evra.
Suarez alijiunga na Liverpool akitokea Ajax Januari 2011 kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 22.7.
Wachezaji walionunuliwa na Arsenal kwa pesa nyingi zaidi ni Jose Antonio Reyes (paundi milioni 17.5 kutoka Sevilla), Santi Cazorla (paundi milioni 16, Malaga), Andrey Arshavin (paundi milioni 15, Zenit St Petersburg), Sylvain Wiltord (paundi milioni 13, Bordeaux) na Thierry Henry (paundi milioni 11, Juventus).

Simba, Coastal kuvaana Mkwakwani J2


TIMU ya soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam inatarajiwa kuvaana na 'ndugu' zao, Coastal Union ya Tanga katika pambano la kirafiki na kujiandaa na Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Agosti 24 litakalochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani siku ya Jumapili.
Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema lengo la mechi hiyo ni pamoja na kuwaandaa wachezaji wao kabla ya kuanza kampeni ya kuwania kurejesha taji lao walilolipoteza kwa mahasimu wa jadi, Yanga.
Alisema mechi hiyo itatoa nafasi kwa mashabiki wa Simba waliopo jijini Tanga kuwafahamu wachezaji wapya waliosajiliwa kwa ajili ya msimu mpya.
Alisema mara baada ya mechi hiyo wachezaji wa Simba watarejea jijini Dar es Salaam kujiandaa na mechi nyingine dhidi ya timu ya Kombaini ya Majeshi itakayopigwa Agosti 3 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Coastal itavaana na Simba ikiwa na kumbukumbu ya kuinyuka URA kwa bao 1-0, huku Simba ikiwa inauguza kipigo toka kwa Wakusanya ushuru hao wa Uganda waliowadungua mabao 2-1.

Tanzania yaanza vibaya michuano ya Wavu Uganda


Athuman Rupia (kulia) akiwa na mchezaji mwenzake wa timu ya taifa ya wavu
TIMU ya taifa ya mchezo wa Wavu ya Wanaume ya Tanzania jana ilianza vibaya michuano ya Kanda ya Tano kuwania kufuzu fainali za kimataifa za mchezo huo FIVB World Cup 2014 zitakazofanyika Poland baada ya kutandikwa na Wakenya kwa seti 3-0.
Michuano hiyo ya Kanda ya Tano Afrika, inafanyika nchini Uganda kwenye uwanja wa MTN Sports uliopo Lugogo jijini Kampala ikishirikisha timu nne wakiwamo wenyeji Uganda.
Kwa mujibu wa mmoja wa wachezaji wa timu hiyo, Athuman Rupia aliyezungumza na MICHARAZO kwa njia ya simu asubuhi hii kutoka Uganda, ni kwamba Tanzania ilishindwa kufuruka kwa Wakenya kutokana na hali ya uchovu waliokuwa nao baada ya kutua nchini humo majira ya asubuhi na jioni kushuka dimbani.
"Tumeanza vibaya michuano ya Kanda ya Tano kuwania Fainali za Kombe la Dunia baada ya kufungwa sti 3-0 na Wakenya, ila tunaamini uchovu umechangia kipigo chetu na tunajipanga kwa mechi zilizosalia dhidi ya Burundi na wenyeji Uganda," alisema Rupia anayeichezea pia timu ya Jeshi Stars.
Jumla ya timu za taifa za nchi nne tu kati ya sita zilizotarajiwa kushiriki michuano hiyo ndizo zinazochuana jiji Kampala baada ya  wakali kutoka Sudan na Rwanda kujioengua dakika za lala salama na kuziacha Kenya, Uganda, Tanzania na Burundi zikionyeshana kazi kuwania nafasi tatu za Kanda hiyo ya Tano.

Thursday, July 25, 2013

Hatimaye Javu atua rasmi Jangwani

Mshambuliaji mpya wa timu ya Yanga Hussein Javu














HATIMAYE klabu ya soka ya Yanga imekamilisha usajili wa mshambuliaji nyota wa timu ya Mtibwa Sugar, Hussein Javu ambapo mchezaji huyo asubuhi ya leo alianza mazoezi Jangwani.
Javu ambaye alikuwa akisisitiza kuwa alikuwa hajasaini kokote licha ya kutangazwa alishasajiliwa na klabu hiyo, zoezi lake la kutua Jangwani lilikamilika leo na kuungana na wenzake katika  mazoezi kwenye uwanja wa shule ya sekondari Loyola Mabibo jijini Dar es salaam.
Hussein Javu amesajili Young Africans kwa mkataba wa miaka miwili ambapo atavaa jezi za watoto wa Jangwani mpaka mwishoni mwa msimu wa 2014/2015.
Usajili wa Javu unafikisha idadi ya washambuliaji sita mpaka sasa wakiwemo Didier Kavumbagu, Jerson Tegete, Said Bahanuzi, Shaban Kondo (mpya - Msumbiji) na Realintus Lusajo (mpya kutoka Machava FC - Moshi).
Kikosi cha Mholanzi Ernie Brandts kinaendelea na mazoezi kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom unaotarajiwa kuanza agosti 24 kwa kufungua dimba na timu ya Ashanti United iliyopanda msimu huu.
Agosti 17-2013  Young Africans itacheza mchezo wa Ngao ya Hisani na timu ya Azam FC katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam ikiwa ni ishara ya ufunguzi wa pazia la Ligi Kuu kwa msimu wa 2013/2014.
Mpaka sasa klabu ya Yanga imekamilisha usajili wa wachezaji saba (7) wapya ambao ni:
1. Deogratius Munishi 'Dida' -  Huru Azam FC (Golikipa)
2.Rajab Zahir -  Huru Mtibwa Sugar  (Mlinzi wa kati)
3.Hamis Thabit - Huru Ureno (Kiungo)
4.Shaban Kondo - Huru Msumbiji (Mshambuliaji)
5.Mrisho Ngassa - Huru Azam FC (Kiungo mshambuliaji)
6.Reanlintus Lusajo - Huru Machava FC (mshambuliaji)
7. Hussein Javu - Mtibwa Sugar (mshambuliaji)
Kikosi kinaendelea na mazoezi katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola kila siku saa 2 asubuhi na wachezaji waliopo katika timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars) wanatarajiwa kuungana na wenzao katika mazoezi siku ya jumatatu.

Young SC

Hivi ndivyo ilivyokuwa Siku ya Mashujaa Tanzania

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka ngao na sime katika mnara wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa katika kambi ya jeshi ya Kaboya, Bukoba, mkoani Kagera leo Julai 25, 2013


Viongozi wa dini wakisoma dua kwenye maadhimisho hayo. Pembeni ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Mohamed Ali Shein, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali, Jaji Mkuu Mheshimiwa Chande Othman na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Othman Makungu




Rais Jakaya Kikwete akitembelea makaburi ya mashujaa waliopoteza maisha wakati wa vita na Nduli Iddi Amini wa Uganda

                                  Rais JK akisalimiana na askari wastaafu




Maskini Kibosile wa Home Shopping Centre!


MFANYABIASHARA maarufu na Mmiliki wa maduka ya Home Shopping Center (HSC), Said Mohamed Saad, ambaye wiki iliyopita alimwagiwa tindikali maeneo ya Msasani City Mall, jijini Dar es Salaam, sasa yuko Afrika Kusini kwa matibabu zaidi .

Wiki iliyopita majira ya saa moja jioni, mfanyabiashara huyo alimwagiwa tindikali na mtu mmoja ambaye hakufahamika na mara baada ya kutenda tukio hilo, mhusika alikimbia huku mlinzi wa eneo hilo akijaribu kumkimbiza pasipo mafanikio baada ya kuteleza na kuanguka.

Hatua hiyo ilitoa mwanya kwa mtuhumiwa kutoroka eneo la tukio kwa kutumia usafiri aina ya pikipiki.

Hapo awali ilidaiwa kuwa Saad alikuwa anaweza kuzungumza japo amefungwa mashine sehemu ya pua kwa ajili ya kumsaidia kupumua.  Matukio ya watu kumwagiwa tindikali yameonekana kushamiri nchini katika siku za hivi karibuni.

Tukio la kumwagiwa tindikali mmiliki huyo wa Home Shopping Centre, limekuja ikiwa ni takribani wiki mbili tangu Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha, Said Juma Makamba naye ajeruhiwe vibaya usoni kwa kumwagiwa maji maji yanayosadikiwa kuwa ni tindikali majira ya usiku akiwa nyumbani kwake.SOURCE BOFYA HAPA

Vialli kuwakosa Uganda The Cranes Jumamosi?

Vialli (kati) anayeweza kuikosa Uganda Jumamosi

Na Boniface Wambura
TIMU ya taifa, Taifa Stars imewasili salama hapa Kampala tayari kwa mechi ya marudiano ya mchujo dhidi ya Uganda (The Cranes) kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Tatu za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.

Stars ambayo iliwasili ikitokea jijini Mwanza ilipokuwa imepiga kambi ya siku kumi kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itakwenda Afrika Kusini mwakani imefikia hoteli ya Mt. Zion iliyoko eneo la Kisseka katikati ya Jiji la Kampala.

Kocha Mkuu wa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, Kim Poulsen ameridhishwa na kiwango cha hoteli hiyo, kwani ndiyo ambayo timu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) ilifikia Novemba mwaka jana ilipokuja Kampala kushiriki michuano ya Kombe la Chalenji inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).

Stars ambayo ilitiwa chachu na Rais Jakaya Kikwete alipokutana nayo Uwanja wa Ndege wa Mwanza wakati ikiondoka kuja Kampala, na kuitakia kila la kheri itafanya mazoezi yake ya mwisho kesho (Julai 26 mwaka huu) Uwanja wa Mandela kujiandaa kwa mechi ya Jumamosi.

Kocha Kim amesema ingawa mechi hiyo ni ngumu, lakini kikosi chake kimejiandaa kuikabili Uganda kwani wachezaji wako wako vizuri na ari kwa ajili ya mechi iko juu.

Wachezaji wote wako katika hali nzuri, isipokuwa Khamis Mcha aliyekuwa na maumivu ya goti, lakini kwa mujibu wa madaktari wa timu anaendelea vizuri kwani tayari wanampa mazoezi mepesi.

Kikosi cha kamili cha Stars ilichoko hapa kinaundwa na makipa Juma Kaseja, Mwadini Ali na Ali Mustafa. Mabeki ni Aggrey Morris, David Luhende, Erasto Nyoni, Kelvin Yondani, Nadir Haroub na Vincent Barnabas.

Viungo ni Amri Kiemba, Athuman Idd, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Khamis Mcha, Mudhathir Yahya, Salum Abubakar na Simon Msuva. Washambuliaji ni John Boko, Juma Luizio na Mrisho Ngasa.

Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen atakuwa na Mkutano na Waandishi wa Habari siku ya Jumatatu (Julai 29 mwaka huu). Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi katika ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

JUma Fundi, Nasibu Ramadhani hapatoshi Idd Pili

IMG_4971
Mabondia Juma Fundi (kushoto) na Nasibu Ramadhani (kulia) wakinyakuliwa mikono na mratibu wa pambano lao la Idd Pili

BONDIA Nassibu Ramadhani na Juma Fundi ambao ni wapinzani wa jadi wanatarajiwa kuvaana kayika pambano litakalofanyika siku ya Idd Pili, huku wakitambiana.
Mabondia hao watavaana kwenye ukumbi wa Friends Corners katika pambano la kumaliza ubishi baina yao baada ya kutambiana kwa muda mrefu kila mmoja akijinasibu kuwa ni mkali zaidi ya mwenzake.
Pambano hilo litakalokuwa la raundi 10 linaratibiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST).
Bondia Nasibu Ramadhani amesema hana hofu na mpinzani wake kwa sababu anamuona mwepesi kwa vile alishampinga na kutwaa ubingwa wa Dunia wa WB-Forum.
"Anayeniumiza kichwa katika uzito wa Bantam ni Francis Miyeyusho pekee, wengine nawaona wa kawaida tu," alisema Nasibu.
Bondia huyo alisema Fundi atarajie kipigo kikali toka kwake kwani amejiandaa vyema ili kuendeleza rekodi ya ubabe kwa mpinzani wake huyo.
Hata hivyo Fundi alisema yeye hana maneno mengi anasubiri kwa hamu siku ya pambani lifike ili aweze kuzima kilimilimi cha Nasibu.
"Tunaandikia mate ya nini wakati wino upo, tusubiri Idd Pili kisha tujue nani mbabe kati yangu na Nasibu, nimejiandaa kufanya vyema siku hiyo," alisema.

Falcao akana kuwa 'kijeba'

Falcao (kushoto) alipokuwa Atletico Madrid
PARIS, Ufaransa
MSHAMBULIAJI mpya wa klabu iliyorejea Ligi Kuu nchini Ufaransa ya Monaco, Radamel Falcao amekanusha ripoti zinazodai kwamba alidanganya kuhusu umri wake, huku vyombo mbalimbali vya habari vikidai mfumania nyavu huyo ni 'kijeba' akiwa kazaliwa mwaka 1984 tofauti na unaofahamika wa 1986.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia, ambaye alikamilisha uhamisho wa kutua Monaco katika kipindi hiki cha usajili kwa ada ya uhamisho ya euro milioni 60 mwezi Juni, anatuhumiwa kudanganya tarehe yake ya kuzaliwa kufuatia kutolewa kwa rekodi zake za shule ambazo zinaonyesha kwamba mshambuliaji huyo ana umri wa miaka 29.
Kwa mujibu wa rekodi za usajili za mshambuliaji huyo za Fifa, Falcao alizaliwa Februari 10, 1986 lakini kituo cha televisheni cha Noticias Uno cha Colombia kimedai kuwa nyota huyo alizaliwa miaka miwili kabla.
Hata hivyo, nyota huyo wa zamani wa Atletico Madrid alitumia ukurasa wake wa Twitter kukanusha uvumi huo, ambao aliuelezea kuwa ni "upuuzi mtupu".
Aliandika: "Nimeshangazwa na ripoti hizi mpya zilizozunguka umri wangu, na madai haya ni upuuzi mtupu."
"Napenda kukanusha madai haya na naufunga rasmi mjadala huu."
Falcao alipata uhamisho wake wa pesa nyingi wa kutua Monaco baada ya kufunga magoli 70 katika mechi 90 akiwa na Atletico aliyodumu nayo kwa misimu miwili tu.

Joseph Owino 'aota' mbawa Msimbazi


Joseph Owino alipokuwa akiichezea Simba
JUHUDI za viongozi wa klabu ya Simba kutaka kumrejesha beki wa zamani wa timu hiyo, Joseph Owino kutoka Mamlaka ya Mapato ya Uganda (URA), zimegonga mwamba baada ya kukosekana pesa za kumlipa.
Mbali ya kukosekana kwa pesa anazotaka mchezaji huyo, uongozi wa URA  umegoma kumuuza Owino kwa Simba kwa vile amepata ofa nzuri ya kwenda kucheza soka ya kulipwa Qatar, Vietnam na China.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, wameshafanya mazungumzo na Owino na kukubaliana naye mambo kadhaa, lakini dau analotaka ni kubwa.
Hata hivyo, Hanspope hakuwa tayari kutaja dau hilo, lakini alisisitiza kuwa bado wanaendelea na juhudi za kutafuta pesa ili waweze kukamilisha usajili wa mchezaji huyo.
Owino aliichezea Simba msimu wa 2009/2010 akiwa na Emmanuel Okwi na Hilaly Echessa kutoka Kenya na kuiletea mafanikio makubwa, lakini aliachwa msimu uliofuata baada ya kuumia goti.
Baada ya kuumia, beki huyo mahiri alipelekwa India kupatiwa matibabu na aliporea nchini alijiunga na Azam FC, lakini alishindwa kuichezea kutokana na kukosa namba na kuamua kurejea Uganda.
Owino alionyesha umahiri mkubwa katika mechi mbili za kirafiki za kimataifa, ambazo URA ilicheza dhidi ya Simba na Yanga. Katika mechi hizo zilizochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, URA iliichapa Simba mabao 2-1 kabla ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Yanga.
"Kimsingi tumeshazungumza na Owino na ameikubali ofa tuliyompa ili aweze kurudi tena Simba, lakini bado kuna masuala yanayohusu pesa, ambayo hatujayakamilisha,"alisema Hanspope.
Mwenyekiti huyo wa kamati ya usajili ya Simba alisema, kutokana na benchi la ufundi kuvutiwa na kiwango cha beki huyo, watafanya kila wanaloweza kuhakikisha anarejea Msimbazi na kucheza katika ligi kuu msimu ujao.
Wakati Simba ikiwa katika mikakati hiyo, Meneja wa URA, Sam Okabo amesema hawawezi kumruhusu Owino arejee Simba kwa sababu ampata ofa nzuri Marekani na Asia.
Okabo alisema jana kuwa, si rahisi kwa Owino kurejea Simba kama viongozi wa klabu hiyo wanavyotaka kwa vile mchezaji huyo ni lulu kwa sasa na anawindwa na klabu nyingi.
Kwa sasa, Simba imesaliwa na wachezaji wawili wa kigeni, Abel Dhaira na Hamis Tambwe baada ya uongozi kuvunja mkataba wa Mussa Mudde na pia kusitisha mpango wa kumsajili Robert Ssenkoom kutokana na benchi la ufundi kutoridhishwa na kiwango chake.
Katika hatua nyingine, Hanspope amesema mshambuliaji mpya wa timu hiyo, Hamis Tambwe kutoka Burundi anatarajiwa kuwasili nchini Jumanne na kujiunga na timu hiyo kwenye kambi yake iliyopo Mbamba Beach, Kigamboni, Dar es Salaam.

LIWAZO

Ajali ya treni yaua 78, wengine 140 Hispania

Watu 20 wamepoteza maisha


WATU zaidi ya 70 wamefariki na wengine 140  katika ajali mbaya ya treni inayoenda kasi ilitokea Kaskazini Magharibi ya Hispania.
Abiria hao walifariki wakati wakisafiri na treni hiyo kabla ya kupata ajali na kwamba baadhi ya majeruhi hali zao ni mbaya.
Moja ya mabehewa limeonekana likiwa linawaka moto na jingine kukatika katikati kwenye eneo la ajali hiyo karibu na Santiago De Compostela ambapo treni hiyo ilikuwa ikisafiri kuelekea Ferrol Northwest nchini humo.

Msondo yaingia studio, kula Idd Dar, Zenji

Baadhi ya wanamuziki wa Msondo Ngoma wakiwajibika
BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki' imetumia muda wake wa mapumziko kuingia studio kurekodi nyimbo zilizosalia za albamu yao, huku ikiweka bayana ratiba nzima ya Sikukuu za Idd el Fitri.
Msemaji wa bendi hiyo, Rajabu Mhamila 'Super D' aliiambia MICHARAZO kuwa, wameona ni vyema kuutupia muda wa likizo ya mfungo wa Ramadhani kurekodi nyimbo za albamu yao ambayo inasubiriwa kwa muda mrefu na mashabiki wao.
Super D, alisema nyimbo zinazorekodiwa kwa sasa katika studio moja ya jijini Dar es Salaam ni Lipi Jema na Baba Kibebe zilizotungwa na Eddo Sanga, Kwa Mjomba Hakuna Urithi wa Huruka Uvuruge, Nadhiri ya Mapenzi wa Juma Katundu na Machimbo.
Wimbo wa Machimbo umeingia kwenye albamu hiyo baada ya kuondolewa kwa kibao kilichokuwa kimetungwa na aliyekuwa muimbaji wao, Isihaka Katima 'Papa Upanga' uitwao 'Dawa ya Deni' na kibao cha mwisho cha albamu hiyo kilichobeba jina wa Suluhu wenyewe ulishakamilika kitambo.
Aidha Super D aliweka wazi kwamba bendi yao katika shamrashamra za Sikukuu za Idd el Fitri, watatambulisha baadhi ya nyimbo mpya katika maonyesho yatakayofanyika kwenye ukumbi wa  DDC Kariakoo kwa onyesho la Idd Mosi na Idd Pili watakamua TCC Chang'ombe kabla ya kuvuka bahari kuelekea Zanzibar kwa onyesho la Idd Tatu pale Gymkhan.
"Idd Mosi tutakamua ngome ya zamani ya wapinzani wetu, DDC Kariakoo na siku inayofuata tutaila Idd viwanja vya TCC Chang'ombe kisha kwenda Zanzibar kumalizia sikukuu," alisema Super.

Kikosi kuweka Zogo lao videoni

Karama Masoud 'Kalapina'
KUNDI la Kikosi cha Mizinga kilichoadhimisha miaka 13 tangu kuanzishwa kwake hivi karibuni, kimekamilisha video ya wimbo wao unaotamba hewani wa 'Zogo la Mtaa'.
Kiongozi wa kundi hilo linalopiga muziki wake katika miondoko ya Hip Hop, Karama Masoud 'Kalapina' aliiambia MICHARAZO kuwa, video hiyo ipo mbioni kuachiwa wakati wowote.
Kalapina alisema mashabiki wa kikosi waliokuwa na hamu ya kuona video hiyo wajiandae kupata burudani.
"Kikosi kimekamilisha video ya wimbo wa 'Zogo la Mtaa' na hivi karibuni itaachiwa hewani, ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 13 ya Kikosi," alisema Kalapina.
Msanii huyo alisema mbali na video hiyo, pia kundi lao lenye maskani yake Kinondoni Block 41, linaendelea pia kuuza fulani na vifaa vingine vyenye nembo yao ya Kikosi.
"Pia tumefufua duka letu la Kikosi lililopo Block 41 ambapo tunauza t-sheti, na vifaa vingine," alisema Kalapina.
Kundi hilo la Kikosi cha Mizinga, lilianzishwa rasmi mnamo mwaka 1997 baada ya kusambaratika kwa kundi lililomuibua Kalapina liitwalo School Face Gangster lililokuwa likiundwa na wasanii watatu.