STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 10, 2014

Ramsey aiweka roho juu Arsenal

Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ballMASHABIKI wa klabu ya Arsenal wapo roho juu baada ya kiungo wao mahiri, Aaron Ramsey kuumia kifundo cha mguu na kuwa hatarisni kulikosa pambano la mwishoni mwa wiki dhidi ya Manchester City katika Ligi Kuu ya England.
Kiungo huyo alipata  majeruhi ya kifundo cha mguu katika ushindi wa Wales wa mabao 2-1 dhidi ya Andorra jana usiku baada ya kufanyiwa rafu na mchezaji wa Andorra ambapo alipatiwa matibabu, lakini akatolewa uwanjani.
Meneja wa timu, Chris Coleman alisema ukubwa wa  majeruhi utatangazwa saa 24 kuanzia jana usiku, na hali hiyo imempa maumivu ya kichwa, kocha Arsene Wenger
Chris Coleman alisema anaamini majeruhi ya Ramsey haiwezi kumuweka nje ya uwanja wa muda mrefu.

Kuziona Yanga, Azam buku 5 tu


KIINGILIO cha chini kwenye mechi ya Ngao ya Jamii kuashiria uzinduzi wa msimu mpya wa Ligi kati ya Azam na Yanga itakayochezwa Jumapili (Septemba 14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000.

Mechi hiyo itaanza saa 10 kamili jioni, na kiingilio hicho cha sh. 5,000 ni kwa viti vya rangi ya kijani na bluu vitakavyochukua jumla ya watazamaji 36,000 katika uwanja huo wenye viti 57,558.

Viingilio vingine katika mechi hiyo ambayo itatumia tiketi za elektroniki ni sh. 10,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000 kwa viti vya VIP C na B wakati viti vya VIP A kiingilio ni sh. 30,000.

MWAMUZI LUGENGE KUAGWA LEO
Mwamuzi wa daraja la kwanza (class one), Luteni Godwill David Lugenge aliyefariki dunia juzi (Septemba 7 mwaka huu) kwa ajali ya gari katika Wilaya ya Handeni mkoani Tanga anaagwa leo (Septemba 9 mwaka huu).

Mwili wa marehemu ambao umehifadhiwa katika Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) Lugalo, baadaye leo saa 6 mchana utapelekwa nyumbani kwa kaka yake Kimara Bucha jijini Dar es Salaam ambapo shughuli za kuaga zitafanyika kabla ya safari ya kwenda mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Luteni Lugenge ambaye mwishoni mwa wiki alishiriki mitihani ya utimamu wa mwili kwa waamuzi wa Ligi Kuu, akiwa na ndugu yake Christopher Alexander Lunyungu katika gari dogo walipata ajali hiyo wakati wakienda mkoani Kilimanjaro.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambalo limetoa ubani wa sh. 200,000 kwa familia ya marehemu kwenye shughuli ya kuaga itawakilishwa na mjumbe wake wa Kamati ya Utendaji ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi, Saloum Umande Chama.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Luteni Lugenge, Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu nchini (FRAT) na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Bwana ametoa, Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe

Yaillah Toba! Ajali nyingine tena yachukua roho za watu


 
 
 
JANGA la ajali za barabarani zimeendelea kupukutisha roho za watanzania baada ya basi la Super Feo lililokuwa linatokea Songea kwenda Mbeya kupata ajali na kusababisha vifo vya watu wawili na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa.
Ajali hiyo imetokea leo eneo la Sinangula wakati likimkwepa mwendesha baiskeli na kwenda kuvamia mti na kupinduka na taarifa za awali zinasema watu zaidi ya 34 wamejeruhiwa na wawili kufa jambo taarifa za sasa zinadai ni abiria watatu wamepoteza maisha.
Ajali hiyo ni mfululizo wa matukio yaliyoteketeza roho za watanzania huku tukielekea WIKI YA USALAMA BARABARANI inayotarajiwa kuadhimishwa mjini Arusha.
Tufunge na kuomba Mungu atuepushilie janga hili ambalo ni janga la kitaifa na linaloua pengine kuliko hata maradhi tishio nchini kwa sasa.
MICHARAZO inatoa pole kwa wote waliopoteza ndugu, jamaa na rafiki zao kwenye ajali zote zilizotokea ndani ya mwezi huu wa Septemba na mingine ya nyuma na kuwaombea kila la heri walioachwa na majeraha kupona haraka kwa uwezo wa AlLAH SW. Inshallah

Vijana CUF wahimiza kuchangamkia uchaguzi mkuu

http://3.bp.blogspot.com/-Vg1FlLMzmC8/UGVoED0VOGI/AAAAAAAByBI/GI-uXRyYJ-s/s320/tz%7Dcuf.gif 
Na Suleiman Msuya 'Kipimo'
JUMUIYA ya Vijana ya Chama Cha Wananchi (JUVICUF) imewataka vijana wa chama hicho kujitokeza kugombea katika chaguzi za vijana pamoja na ule wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni nchini kote.
Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa (JUVICUF) Hamidu Bobali wakati akizungumza na mwandishi wa habari katika ofisi za chama cha CUF jijini Dar es Salaam.
Alisema chama kupitia (JUVICUF) kinatarajia kufanya chaguzi kuanzia matawi, kata, wilaya na Taifa ambapo wilaya 45 za Tanzania Bara na 10 za Zanzibar zitashiriki ili kupatikana kwa viongozi.
Bobali alisema mikakati (JUVICUF) ni kuhakikisha kuwa chama kinajijenga vizuri kuanzia ngazi za chini hasa ukizingatia kuwa ni wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwahimiza vijana wa CUF kujitokeza katika chaguzi zote za chama katika ngazi ya vijana ambazo zimeanza kufanyika sasa na mwezi ujao Novemba ili mwezi Desemba tuweze kufanya uchaguzi mkuu wa vijana Taifa”, alisema.
Bobali alisema uchaguzi huo wa Taifa unatarajiwa kuhusisha zaidi ya vijana 135 kutoka Bara na 120 kutoka Zanzibar ambao watotokana na chaguzi katika ngazi za Wilaya.
Alisema mikakati yao ni kuhakikisha kuwa wanakuwa na wawakilishi kutoka Wilaya zote za Tanzania Bara kama ilivyo Zanzibar ambayo italeta ushindani wa kisiasa hapa nchini.
Naibu Katibu huyo alisema pia JUVICUF inajipanga kufanya operasheni mbalimbali ambazo zitakuwa na lengo la kuhamasisha vijana kujitokeza katika chaguzi na ufahamu juu ya lengo la Wabunge wanaounga mkono Rasimu ya Jaji Warioba kutoka nje ya Bunge.
Alisema kuna hali ya sintofahamu kwa baadhi ya vijana na wananchi mbalimbali ya nini sababu ya wajumbe wa UKAWA kutoka nje ya Bunge hivyo JUVICUF inaona ni wakati muafaka wa kutoa elimu.
Bobali alisema ni vema vijana wa vyama vinavyounga mkono UKAWA kuendelea kuwa na umoja ili kuhakikisha kuwa juhudi za viongozi wao wa Kitaifa zinafikiwa ili waweze kukomboa Taifa.

Tuesday, September 9, 2014

Francis Cheka kuzipiga na Pascal Ndomba

Francis Cheka
Pascal Ndomba
BINGWA wa zamani wa Dunia wa WBF, Francis Cheka anatarajiwa kupanda ulingoni siku ya Novemba Mosi kupigana na bondia Pascal Ndomba katika pambano lisilo la ubingwa litakalofanyika mjini Morogoro.
Kwa mujibu wa Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC) Chaurembo Palasa, pambano hilo la uzito wa juu litachezwa kwenye uwanja wa Sabasaba mjini humo.
Palasa alisema TPBC imetoa baraka zote kwa pambano hilo litakalokuwa la raundi 10.
Rais huyo alisema mchezo huo na mingine ya utangulizi siku hiyo imeandaliwa na kampuni ya Cheka Promotion na mabondia watakawasindikiza wanatarajiwa kutangazwa baadaye.
Hilo litakuwa ni pambano la kwanza kwa mabondia hao kukutana na pia la kwanza kwa Cheka tangu bondia huyo alipopanda ulingoni mara ya mwisho  Aprili 19 mwaka huu alipopigana na bondia toka Iran Sajad Mehrabi  na kutoka naye sare kwenye ukumbi wa PTA.
Cheka ndiye bondia asiyepigika nchini kwa sasa akiwa amewatandika karibuni wapinzani wake wote tangu mwaka 2008 hajapigwa, ingawa anapotoka nje ya nchi amekuwa 'urojo'.

Newz Alert! Kaburi ya aliyekufa ajali ya mkoani Mara lafukuliwa

KABURI la mmoja kati ya watu waliopoteza maisha katika ajali mbaya iliyohusisha mabasi ya Mwanza Coach na J4 katika eneo la Sabasaba, Musoma, Mara limekutwa likiwa limefukuliwa na watu wasiojulikana leo asubuhi.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichofika katika eneo la makaburi ya Musoma Basi, ndugu wa marehemu aliyetajwa kwa jina la Juma Sai walienda asubuhi kuangalia kaburi ikiwa ni siku ya tatu tangu wafanye mazishi, ndipo walipokuta kaburi limefukuliwa na mbao zilizotumika kuhifadhi mwili kwa imani ya dini ya kiislamu zikiwa zimewekwa pembeni.

“Mwili wa marehemu bado uko ndani, watu wengi wako hapa na polisi wameimarisha hali ya usalama. Madaktari wameshafika hapa na wanafanya uchunguzi kuona kama kuna kiungo chochote kilichotolewa kwenye mwili wa marehemu. Inasikitisha sana.” Kimeeleza chanzo chetu cha kuaminika.

Ijumaa iliyopita, kulitokea ajali mbaya iliyohusisha magari matatu, mabasi ya kampuni ya Mwanza Coasch na J4 pamoja na gari dogo aina ya Landcruiser. Watu zaidi ya 40 walifariki na wengine 79 kujeruhiwa.

Udaku Specially

Maskini, Kisura huyu kumbe alijinyonga

Ripoti: Mwimbaji wa kike wa Marekani aliyekutwa amekufa nyumbani kwake alijinyonga
POLISI wa Los Angeles wameeleza kuwa mwimbaji wa kike wa Marekani, Simone Battle aliyekutwa amekufa nyumbani kwake wiki iliyopita alijiua kwa kujinyonga.
Sababu ya kifo chake imetajwa siku mbili baada ya polisi kuanza uchunguzi kufuatia tukio hilo lililotokea kusini mwa Hollywood.
Simone Battle aliwahi kuwa mshiriki wa shindano la kuimba la X Factor na kufika katika hatua ya fainali, pia alikuwa member wa kundi la G.R.L.

Rais Yoweri Museveni wa Uganda kutua nchini kesho

http://media.web.britannica.com/eb-media/05/61705-004-8486B3D5.jpg 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RAIS wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, anatarajiwa kuwasili nchini siku ya Jumatano asubuhi, tarehe 10 Septemba, 2014 kwa ziara ya kikazi ya siku moja.

Katika ziara hiyo nchini, Mhe.Museveni atakuwa na mazungumzo na mwenyeji wake, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ikulu, Dar es Salaam. Rais Museveni ataondoka baadaye siku hiyo hiyo kurejea nyumbani.

IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI,
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Didier Zakora atundika daluga kuichezea Tembo wa Ivory Coast

http://images.supersport.com/2014/5/Didier-Zokora-100615-Gestures-R300.jpg 
http://futboler.tv/wp-content/uploads/2014/05/fft99_mf1310873.jpegKIUNGO nyota wa timu ya taifa ya Ivory Coast, Didier Zokora ametangaza kustaafu soka ya kimataifa baada ya kuitumikia timu ya taifa kwa zaidi ya miaka 10. Maestro kama anavyofahamika kwa mashabiki wa soka nchini mwake, alisema anadhani ni muda muafaka kuwapisha wengine kuitumikia timu hiyo.
"Baada ya miaka 15 ya kucheza soka ya kiwango cha juu, nafikiri ni wakati wa mimi kufikia tamati ya soka soka ya kimataifa" amesema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 katika mashindano maalum yaliyoandaliwa kwa heshima yake mjini Abidjan kitongoji cha Williamsville."Ni wakati wa kutoa nafasi kwa vijana wadogo. Katika mechi na Sierra Leone, nimeona wachezaji wadogo ambao wanaweza kuchukua nafasi," aliongeza.
Zokora alianza kuichezea timu hiyo tangu mwaka 2000 na amekuwa na rekodi ya kucheza mechi 121.
Amecheza fainali tano za Kombe la Mataifa ya Afrika mfululizo 2006, 2008, 2010, 2012 na 2013, mbali na  Kombe la Dunia mara tatu mfululizo 2006, 2010 na 2014.
Kiungo huyo mkabaji, kwa sasa anachezea klabu ya Akhisar Belediyespor ya Uturuki, baada ya kuchezea klabu nyingine za Racing Genk ya Ubelgiji, Saint-Etienne ya Ufaransa, Tottenham Hotspur ya England, Sevilla ya Hispania na Trabzonspor ya Uturuki pia.
Ni matunda ya akademi ya ASEC Mimosas ya mwaka 1998 ambao walishinda taji la Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kuifunga Dynamos ya Zimbabwe kwenye fainali, michuano ambayo pia Yanga SC ilishiriki.
Zokora ambaye majina yake kamili ni
Déguy Alain Didier Zokora alizaliwa Desemba 14, 1980) ni gwiji mwingine wa Ivory Coast kustaafu kwa sasa baada ya Nahodha wa zamani, Didier Drogba anayechezea Chelsea.

Diamond, Yami Alade kuangusha ya pamoja Coke Studio Africa

STAA wa Mdogomdogo na My Number One, Diamond Platnumz amerejea tena kwenye msimu wa pili wa kipindi cha Coke Studio Africa na awamu hii atatangeneza 'pea' na mkali wa Johnny, Yemi Alade kutoka nchini Nigeria.
Kwa mujibu wa taarifa za kwenye mtandao, Diamond ni msanii wa nne mwaka huu kutoka Tanzania aliyeshiriki kwenye kipindi hicho kinachorekodiwa jijini Nairobi, Kenya.
Wengine waliowahi kushiriki ni pamoja na Vanessa Mdee aliyerekodi na Burna Boy wa Nigeria, Joh Makini aliyerekodi na Chidinma wa Nigeria na Shaa aliyerekodi na Jacky Chandiru wa Uganda.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Yemi aliyekuja nchini hivi karibuni aliweka picha yake akiwa na Diamond katika na kudokeza anavyojisikia furaha kufanya kazi na mshindi huyo wa tuzo saba kwa mpigo wa Kili Music Awards-2014.
#wonderment! With the infamous ubertalented six-abbs superstar Diamond….@diamondplatnumz
#iAmHumbled #thankYouCokeStudio, ForThe Opportunity God bless AFrica.. #cokeastudioafrica
@cokestudioafrica @dresomes Nosa @chocolatecity
Diamond has been singing your song all morning@audumaikori.
Naye Diamond katika picha akiwa na mrembo huyo
ameandika:
Na dem ake Johny @yemialade , ushaelewa nini kinaendelea si eti????….. (jus me and Johny’s
Girlfriend…You allready know what it is ryt???… Cc@yemialade

Hispania yaifumua Macedonia 5-1 bila Diego Costa, David Silva nouma

Silva na Paco Alcacer wakipongezana baada ya kinda hilo (9) kufunga bao
Breaking away: Cesc Fabregas escapes a challenge from Macedonian midfielder Stefan Spirovski as Spain exerted their authority in the midfield areas
Utanivunja nyonga bure! Mtaalam Cesc Fabregas akimpeleka mtu chini
MABINGWA watetezi wa Kombe la Mataifa ya Ulaya, Hispania ikiwa bila mshambuliaji wao nyota Diego Costa anayesumbuliwa na majeraha ya nyama za Paja, usiku wa kuamkia leo ilitoa onyo kwa wapinzani wake baada ya kuifumua Macedonia kwa mabao 5-1 katika mechi za kuwania fainali hizo za Uero 2016.
Mchezaji aliyechukua nafasi ya Costa, Paco Alcacer , 21 aliitenda haki kwa kuifungia Hispania bao la pili katika dakika ya 17 akimalizia krosi pasi safi ya Cesc Fabregas.
Bao la kwanza la wababe hao wa zamani wa Dunia, lilitumbukizwa wavuni na Sergio Ramos  kwa panalti dakika ya 16 baada ya David Silva kuangushwa kwenye eneo la hatari.
Macedonia walijipatuia bao lao la kufutia machozi katika dakika ya 28 baada ya Juanfran kufanya madhambi na Agim Ibraimi akafunga kwa kumtungua Iker Casillas.
Sergio Busquets aliiandikia Hispania bao la tatu sekunde chache kabla ya kwenda mapumziko, huku mabao mengine ya ushindi huo mnono kwa Hispania yakiwekwa kimiani na David Silva katika dakika ya 50 na Pedro aliyepigilia msumari dakika za lala salama.

Danny Welbeck aibeba England michuano ya kuwania Euro 2016

At the double: Danny Welbeck wraps up victory for EnglandMSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Danny Welbeck usiku wa kuamkia leo amethibitihs aubora wake baada ya kuipa England ushindi wa 2-0 dhidi ya Uswisi ugenini katika mechi ya kuwania kufuzu Euro 2016. Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United, alifunga mabao hayo katika dakika za 59 na 90 na kumfanya kocha Roy Hodgson aondoke na furaha uwanjani.
Welbeck aliyekuwa hana nafasi katika kikosi cha kwanza cha Mashetani Wekundu alinyakuliwa na Arsene Wenger mwishoni mwa msimu wa usajili kwa mkopo.

Lulu Kayage atamba kumtandika mtu Sept 27

 Kocha mkongwe wa mchezo wa masumbwi nchini akimwelekeza bondia Lulu Kayage jinsi ya kukupa ngumi wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa kupambana na Fatuma Yazidu mpambano utakaofanyika September 27 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam picha na SUPER D BLOG
 Bondia Lulu Kayage kulia akielekezwa jinsi ya kupiga makomde mazito na Kocha Habibu Kinyogoli 'Masta' wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa kupambana na Fatuma Yazidu Septermber 27 katika ukumbi wa frends Corner Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BLOG
Bondia Juma Biglee kushoto akioneshana umwamba na Lulu Kayage wakati wa mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Ilala Amana Dar es salaam Lulu anajiandaa na mpambano wake na Fatuma Yazidu utakaofanyika Septermber 27 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Picha na SUPER D BLOG
Bondia Lulu Kayage kushoto akipambana na Juma Biglee wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa kupambana na Fatuma Yazidu september 27 Dar es salaam Picha na SUPER D BLOG
Bondia Lulu Kayage kushoto akifanya mazoezi ya kuimalisha misuli ya tumbo wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa kupambana na Fatuma Yazidu september 27 katika ukumbi wa frends corene manzese Dar es salaam kushoto ni Titus Jonson Picha na SUPER D BLOG
Na Mwandishi Wetu

 

lulu kayage
BONDIA Lulu Kayage yupo katika mazoezi makali kwa ajili ya kupambana na bondia Fatuma Yazidu Septermber 27 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam

akizungumza wakati akiwa mazoezini katika kambi ya ilala amana Dar es salaam amemtahadhalisha mpinzani wake kufanya mazoezi ya kutosha kwani yeye kwa sasa yupo fiti kupita kiasi na akuna bondia wa kike kwa Tanzania hii mwenye uzito wake anaeweza kumsumbua kwa sasa kwani ana uzoefu mkubwa na wakutosha

aliongeza kwa kusema kuwa jinsi anavyosimamiwa mazoezi na jopo la makocha wake wanao ongozwa na kocha mkongwe nchini Habibu Kinyogoli 'Masta' kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' na Kondo Nassoro ambao wanamuhimiza kila wakati kufanya mazoezi ya kutosha na ndio wana muongeza moyo zaidi kwa ajili ya kufanya mazoezi

Lulu aliongeza kuwa mchezo wa masumbwi nchini wasichana wanaojitokeza ni wachache sana hivyo kukosa msisimko wa kila wakati kucheza wasichana kwa wasichana hivyo kuomba wasichana mbalimbali wajitokeze kufanya mazoezi na kucheza mchezo kwa  ajili ya afya pia ni kwa ajili ya ajira kumbuka mchezo wa ngumi ni ajira kama una uwezo wa kufanya vizuri

siku hiyo pia kutakuwa na mpambano mkali utakao wakutanisha Nassibu Ramadhani na Mohamed Matumla mwingine ni Sadiki Momba na Adam Ngange, Issa Omari na Juma Fundi
siku hiyo pia kutakuwa zikiuzwa DVD mpya za masumbwi ambazo zinaonesha mafunzo mbalimbali ya mchezo wa ngumi yanavyoanza hatua kwa hatua

mpaka kujua kitu kamili katika mchezo huo pia kunakuwa na mapambano ya mabondia mabigwa wa dunia wa mchezo huo kama Floyd Maywether, Manny Paquaio,mike Tyson, Mohamed Alli pamoja na mabambano ya ngumi ya ndani

Marco Reus bado majanga matupu Dortmund kumkosa wiki nne

KLABU ya Borussia Dortmund imethibitisha kuwa Marco Reus anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki nne baada ya kupata majeruhi ya kifundo cha mguu katika mchezo wa kufuzu michuano ya Ulaya mwakani dhidi ya Scotland.
Mshambuliaji alikosa michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil kutokana na majeruhi ya kifundo cha mguu aliyopata mwishoni mwa msimu uliopita na sasa inaonekana tatizo limejirudia kwa kujitonesha. 
Hata hivyo Dortmund katika taarifa yake wamedai kuwa majeruhi hayo aliyopata Reus, 25 siyo makubwa sana kama yale yaliyopita. 
Reus sasa anakabiliwa na changamoto ya kuwa fiti kwa ajili mechi za kufuzu za Ujerumani zinazofuata ambazo zitakuwa dhidi ya Poland na Jamhuri ya Ireland katikati ya Octoba mwaka huu.

Maskini! Ajali yaua Diwani wa CCM Iringa

GARI aina ya Toyota Coaster iliyokuwa ikifanya safari zake kutoka Ludewa Mjini kuelekea Lupingu baada ya kupata ajali iliyoondoa uhai wa Diwani wa Viti Maalum CCM Kata ya Lupingu, Prisca Kayombo (Zaruta).
Diwani wa Viti Maalum CCM Kata ya Lupingu, Prisca Kayombo (Zaruta) wa tatu kushoto enzi za uhai wake akiwa na Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe (wa kwanza kushoto), Katibu wake Stan Gowele (wa pili kushoto) na wananchi wengine wa Ludewa wakijiandaa kunyanyua nguzo ya umeme wiki mbili zilizopita.
Baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo wakiwashushwa katika Hospitali ya Wilaya Ludewa, mkoani Iringa leo.
Majeruhi wakiwa katika Hospitali ya Wilaya Ludewa.
Wananchi wa Kata ya Ludewa wakiwa hospitalini hapo kuwaona majeruhi wa ajali.

DIWANI wa Viti Maalum CCM Kata ya Lupingu, Prisca Kayombo (Zaruta) amekufa papo hapo huku watu wengine kadhaa wakijeruhiwa vibaya katika ajali mbaya ya gari iliyotokea leo asubuhi huko Ludewa mkoani Iringa.

Mashuhuda wa ajali hiyo walidai kuwa chanzo chake ni gari hilo ambalo walikuwa wakisafiria kutoka Lupingu - Ludewa kufeli breki na hivyo kupinduka .

Inadaiwa baada ya gari hilo aina ya Toyota Coaster inayojulikana kwa jina la DMX kufeli breki dereva aliwataka abiria kutulia ndani ya gari hilo ila diwani huyo hakuweza kufanya hivyo na kuamua kuchukua maamuzi magumu ya kutaka kuruka katika gari hilo ambapo wakati akiruka alimsukuma utingo wa basi hilo na hivyo wote wawili utingo na diwani kufunikwa na gari hilo na kupelekea kifo cha diwani huku utingo akiwa mahututi baada ya kubanwa na gari hilo.

"Diwani amepoteza maisha wakati akiwa njiani kuelekea kujumuika na wananchi wake katika shughuli ya maendeleo ya kuchimba mashimo ya nguzo za umeme kuelekea kijijini kwake Lupingu" Alisema mmoja wa abiria.

Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe ameeleza kusikitishwa na kifo cha diwani huyo kutokana na mchango wake mkubwa aliouonyesha enzi wa uhai wakati kwa kushiriki vema na wananchi wa kata yake katika zoezi la kufyeka na kuchimba mashimo ya nguzo za umeme kwenda Lupingu.

Alisema kuwa anakumbuka ni wiki mbili pekee zimepita toka diwani huyo alipoungana nae katika uchimbaji wa mashimo ya nguzo za umeme kwenda kijiji cha Ntumbati na kuwa hata wakati ajali hiyo inamkuta bado alikuwa katika harakati za kuwatumikia wananchi wake.

"Ludewa tumempoteza diwani mchapa kazi na aliyependa kujituma muda wote na hata wakati mwingine diwani huyo alikuwa akifanya kazi ngumu kama mwanaume kwa kubeba nguzo za umeme kwa kushirikiana na mimi na wananchi wake.....kwa kweli kifo chake ni pigo kubwa ndani ya CCM na kwa wananchi wa kata nzima ya Lupingu"

Kwani kati ya madiwani waliokuwa bega kwa bega na wananchi wao na mbunge ni pamoja na diwani huyo ambaye alikuwa mstari wa mbele kuona Kata ya Lupingu inapata umeme wa uhakika baada ya miaka zaidi ya 50 ya Uhuru bila umeme .

Mbunge Filikunjombe alisema atamkumbuka diwani huyo kutokana na mchango wake mkubwa katika maendeleo na vile alivyofanya kazi na wananchi wote bila kujali itikadi zao za vyama.

Mkuu wa wilaya ya Ludewa, Juma Madaha amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo iliyosababisha kifo cha diwani huyo na kuwa ajali hiyo ilitokea majira ya saa 2 asubuhi .

(PICHA / STORI: FRANCIS GODWIN, IRINGA)

Monday, September 8, 2014

Waliokufa ajali ya Airbus ni wanne tu


AJALI mbaya iliyotokea mjini Gairo ikihusisha basi la Airbus lililokuwa likitokea Dar kuelekea Tabora imedaiwa kusababisha vifo vya watu wanne tu na wengine kadhaa kujeruhiwa tofauti na taarifa za awali toka kwa waliokuwa kwenye tukio hilo kuwa zaidi ya watu 10 walikuwa wamekata roho.
Ajali hiyo ambayo imekuja siku chache baada ya roho za watu 39 kupotea kwenye ajali ilitokea mkoani Mara ikihusisha magari matatu, ilielezwa ilitokea majira ya asubuhi baada ya basi la Airbus kupinduka mara kadhaa na kuharibika huku baadhi ya abiria wakijeruhiwa vibaya na kutupwa nje na kuleta hofu kubwa.
Hata hivyo jeshi la Polisi la Morogoro limethibitisha waliokufa ni abiria wanne tu na siyo zaidi ya idadi hiyo na majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali mbalimbali mjini Dodoma na Morogoro.

Babu Seya kaachiwa Huru nani kasema?!


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwRW3gfI8pIOBdf65LIaHBQzTJ_1ntCBcOUCbVgGXfnYmqtU3SHV7m-AwX-0lbIjBGHCaHue_ZEMjMXIbUG_yEMgBpwzHNRoPzdrO-7TdW4Ty2zIlsJ0rEa-XwtfKBbMj9-yR0jH_ECJA/s640/bauseya.jpg
Babu Seya na mwanae Papii Kocha
TANGU majira ya mchana kuna taarifa zilizagaa kwamba Babu Seya na mwanae Papi Kocha walikuwa wameachiwa huru na kuanza kusambazwa ujumbe mfupi wa simu za mkononi na kwenye mitandao ya kijamii.
Hata hivyo Jeshi la Magereza limefunguka na kuweka bayana juu ya ukweli wa taarifa hizo kama taarifa yao inavyosomeka hapo chini;
Hivi sasa kuna taarifa zimesambaa kupitia Ujumbe mfupi wa simu (SMS) na mitandao ya kijamii zikihusisha kuachiliwa huru kwa wafungwa wawili wanaotumikia Kifungo cha Maisha gerezani. Wafungwa hao wanaotajwa ni Nguza Vicking(Maarufu kwa jina Babu Seya) na Johnson Nguza(Maarufu kwa jina la Papii Kocha).

Napenda kuufahamisha Umma wa Watanzania kuwa taarifa hizo zote zilizotolewa kupitia njia hizo ni za Uongo na uzushi mkubwa na zinalenga kuipotosha jamii kwani wafungwa hao wapo gerezani na wanaendelea kutumikia adhabu ya kifungo cha Maisha gerezani kwa mujibu wa Sheria.

Jeshi la Magereza nchini linatoa onyo kali kwa watu kujiepusha na uhalifu huo na linawataka wale wote wanaotumiwa ujumbe wa aina hiyo waepuke kuusambaza ujumbe huo kwa wengine bali waufute, kwani kuendelea kuusambaza ni kosa kisheria.

Aidha, Jeshi la Magereza linaendelea na uchunguzi wa kina ili kuwabaini wanaosambaza ujumbe huo likishirikiana na Vyombo vingine muhimu kwa lengo la kuwakamata wahalifu hao ili mkondo wa Sheria uchukue nafasi yake.

Imetolewa na;
Lucas Mboje, Mkaguzi wa Magereza,
Afisa Habari wa Jeshi la Magereza,
Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
DAR ES SALAAM.
Septemba 8, 2014

Fabregas afunguka ya moyoni kuhusu Chelsea

http://e1.365dm.com/14/07/800x600/Fabregas_3179732.jpg?20140728165853
Sikuwahi kuota kuja kuzaa uzi wa Chelsea kabisa aisee....dunia inabadilika sana
CESC Fabregas amekiri kwamba hakuwahi kufikiria hata mara moja kama angekuja kuitumikia klabu yake ya sasa ya Chelsea.
Kiungo huyo wa zamani wa Arsenal na Barcelona, alisema wazo la kuitumikia klabu hiyo chini ya Jose Mourinho lilikuwa halifikiriki katika kipindi cha nyuma. 
Fabregas aliyerejea tena kwenye Ligi Kuu katika kipindi cha usajili wa majira ya kiangazi baada ya kushindwa kupata namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha Barcelona, alisema kama mtu angemuambia miaka mitano nyuma kwamba atakwenda kucheza Chelsea chini Mourinho ni jambo ambalo asingeamini lakini maisha yanabadilika. 
Kiungo huyo alidai alianza kufikiria kuondoka Barcelona baada ya fainali ya Kombe la Mfalme ambayo walifungwa na Real Madrid ambapo baada ya kuzungumza na mkurugenzi wa michezo Andoni Zubizarreta aliona kama amewapunguzia bugudha kutokana na kauli yake. 
Baada ya hapo alimuomba wakala wake amtafutie timu nyingine na Chelsea wakatoa ofa ambapo baada ya kuzungumza na Mourinho na kumwambia mambo anayohitaji akaona hapo ndio patakapomfaa.

Mwamuzi afa ajalini, TFF yamlilia

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhmRpmlPP9xJpBS_8mLZgKPLic2CoFHDnUT8GcHzIpatlFFo_XCz6NyaPIHEvMTTpcnILwpDDOKuRpWx7EePjClPxJ3LrbQ_Eais1BNmwIRmy2yv_eSiPMEEdCtgKP-2adLWq6lJncprglB/s640/Wajumbe.jpg
Luteni Lugenge (kushoto) enzi za uhai wake
 SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mwamuzi wa daraja la kwanza (class one), Luteni  David Lugenge kilichotokea jana (Septemba 7 mwaka huu) kwa ajali ya gari katika Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.
Luteni Lugenge ambaye mwishoni mwa wiki alishiriki mitihani ya utimamu wa mwili kwa waamuzi wa Ligi Kuu alikuwa na ndugu yake Christopher Alexander Lunyungu katika gari dogo wakienda mkoani Kilimanjaro.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Handeni, Peter Juma, Luteni Lugenge alikuwa akimsindikiza mwenzake aliyekuwa anakwenda kujitambulisha kwa wakwe zake watarajiwa.
Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu kwani Luteni Lugenge alikuwa ni mmoja wa waamuzi wanaoinukia nchini, hivyo mchango wake ulikuwa bado unahitajika. Hivyo tutamkumbuka daima.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Luteni Lugenge, Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu nchini (FRAT) na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Yanga waendelea kumkomalia Emmanuel Okwi, sasa wamshtaki FIFA

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspoppe (kulia) akimtambulisha mshambuliaji Emmanuel Okwi kurejea katika klabu hiyo jijini Dar es Salaam jana. Picha: Halima Kambi 
SIKU moja baada ya Shirikisho la soka Tanzania, TFF kumtangaza mchezaji Emmanuel Okwi kuwa huru na hivyo anaweza kusajiliwa na klabu ya Simba, uongozi wa Yanga umesema haujakubali.
Uongozi wa Yanga umesema utatinga katika Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kupinga maamuzi ya Kamati ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kumtangaza Emmanuel Okwi kuwa ni mchezaji huru na anaweza kuichezea Simba.
Baada ya kukutana jijini Dar es Salaam juzi kupitia masuala mbalimbali ukiwamo mgogoro wa kimkataba kati ya Yanga na Okwi, kamati hiyo ilisema imebaini kwamba mkataba kati ya pande hizo mbili ulikuwa umevunjika.
Hata hivyo, Yanga wamepinga maamuzi hayo na katika taarifa yao iliyotolewa na Kaimu Ofisa Habari, Baraka Kizuguto jana saa 7:08 mchana, klabu hiyo ya Jangwani imejipanga kuyakatia rufaa maamuzi hayo.
Kizuguto alisema Mwenyekiti wa Kamati  ya Sheria ya Yanga, Sam Mapande amesema hawajaridhishwa na maamuzi ya TFF huku akidai yanakinzana na shitaka zima la mchezaji huyo.
Katika maelezo yake yaliyochapishwa kwenye mtandao wa klabu ya Yanga jana mchana, Mapande alidai kuwa Kamati ya TFF imeamua sakata la Okwi kinyume cha malalamiko yao kwani hakukuwa na lalamiko la mchezaji huyo kuhusiana na malipo ya fedha zake za usajili.
Alisema wameshangaa kuona kamati hiyo ya TFF inaamua kusikiliza kesi ambayo haikuwa mbele yao na kutoa maamuzi yanayoshangaza.
“Kwanza, kesi yenyewe ilikuwa haijamalizika, walituambia tuwasilishe vielelezo kuhusiana na kitendo cha mchezaji huyo kufanya mazungumzo na klabu ya Misri, lakini cha kushangaza maamuzi yametolewa, hili limetushangaza sana,” alisema Mapande katika taarifa hiyo.
Alisema mazingira yalikuwa yameandaliwa kuibeba Simba na Okwi kwani hata malalamiko yao kwa Simba hayakusikilizwa. “Malalamiko yetu yalikuwa wazi kabisa, yapo kimaandishi, hatukuwahi kulalamikiwa, suala la fedha za usajili la Okwi limetoka wapi, kama lilikuwapo, mbona hatujajulishwa kimaandishi kama utaratibu ulivyo?” Alihoji Mapande.
Alisema kamati hiyo kumruhusu mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo Zacharia Hanspoppe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba kuwamo katika kikao hicho ni kinyume cha taratibu za Fifa kupitia kifungu namba 19 kinachoeleza mgongano wa kimaslahi.
Lakini, katika maelezo ya Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF, yaliyotolewa juzi usiku kupitia kwa Kaimu Karibu Mkuu wa TFF, Boniface Wambura, Yanga ilikiuka kipengele namba 8 kuhusu malipo ya ada ya usajili katika mkataba huo wa pande mbili.
Wambura alieleza kuwa Yanga ikiwa mwajiri, haikutekeleza kipengele hicho cha kimkataba hadi kufikia Juni 27, mwaka huu ilipoandika barua TFF kuomba mkataba huo uvunjwe. Kwa maana hiyo Okwi ni mchezaji huru, hivyo yuko huru kujiunga na timu yoyote.
"Mkataba ni uhusiano kati ya mwajiri (Yanga) na mwajiriwa (Okwi), kamati imebaini kuwa uhusiano huo haupo, hivyo hakuna mazingira ya pande hizo mbili kuendelea kufanya kazi pamoja," inasomeka sehemu ya taarifa hiyo iliyotolewa na Wambura juzi.
Wambura ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, alisema kuwa pamoja na Yanga kuwasilisha pingamizi la kuwapo mmoja wa wajumbe katika kikao kwa sababu za kimaslahi (conflict of interests) (Hanspoppe), walifahamishwa kuwa kilichokuwapo mbele ya kamati ni mgogoro wa kimkataba kati ya Yanga na Okwi, na si usajili.
Pia lilijitokeza suala la Okwi kutakiwa na klabu ya Wadi Degla ya Misri. Kamati imeiagiza Sekretarieti ya TFF kulifanyia uchunguzi suala hilo na kulitolea taarifa katika kikao kijacho.
Wambura alidai kuiwa mjumbe huyo (Hanspoppe) hakushiriki katika kuchangia hoja na kutoa maamuzi na kwamba uamuzi wa kamati ulifanyika baada ya majadiliano, hivyo hakukuwa na suala la kupiga kura.
Okwi raia wa Uganda, ambaye juzi alikuwapo wakati mkataba huo ukipitiwa na kamati pamoja na wawakilishi wa Yanga, alisaini mkataba wa miaka miwili na nusu kuitumikia timu hiyo ya Jangwani akitokea SC Villa ya Uganda.

Serena Williams atwaa taji la US Open

Williams akilala chini kwa furaha uwanja wa Arthur Ashe Arena baada ya kumshinda Caroline Wozniacki
MCHEZA tennis Serena Williams wa Marekani ametwaa ubingwa wa US Open.
Williams ameshinda katika mchezo uliofanyika usiku wa kuamkia leo baada ya kumtwanga Caroline Wozniacki wa Denmark kwa ushindi wa moja kwa moja.

Mpambano huo wa fainali ulipigwa mjini New York ambapo Serena ameshinda kwa seti 6-3, 6-3 na kujinyakulia ubingwa huo kwa mara ya 6.

Kwa sasa Serena ndiye mchezaji nambari 1 duniani kwa mchezo huo na pia bingwa mara 18 wa Grand Slam, amekuwa bingwa wa kombe hilo mara tatu mfululizo tangu mwaka 2012.

Wozniacki ambaye ni rafiki wa karibu wa Serena alimpongeza rafiki yake huyo baada ya mchezo na kusema alistahili ushindi huo kutokana na jinsi alivyocheza.
Over the moon: Serena Williams celebrates her US Open victory with a jump for joy with the trophy
Serena Williams akishangilia ushindi wa US Open dhidi ya Caroline.
Overwhelmed: Serena Williams drops to the court after beating Caroline Wozniacki for the US Open title
Serena Williams akianguka kwa furaha baada ya kumchapa Caroline Wozniacki katika US Open
Formidable: Williams dominated as she claimed an 18th career Grand Slam title
Passion: Williams screams in anguish despite being well in control of the match from the outset 
Out of reach: Wozniacki stretches for a forehand as she falls to Williams in 75 minutes
Kashindwa kufikia malengo: Wozniacki akijinyoosha msuli dhidi ya Williams dakika ya 75
Good spirits: Wozniacki and Williams share a laugh after the presentation in New York
Wozniacki na Williams wakionyesha tabasamu jijini New York

Sepp Blatter athibitisha kutetea kiti FIFA

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani,FIFA Sepp Blatter amethibitisha kuwa atakitetea kiti chake katika uchaguzi ujao wa shirikisho hilo. 
Akihojiwa jijini Manchester, Blatter 78 alithibitisha uamuzi wake japo alidai atatoa taarifa rasmi katika mkutano mkuu wa kamati ya utendaji ya FIFA utakaofanyika Septemba 25 na 26. 
Tayari rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA Michel Platini ameshatangaza kutogombea nafasi hiyo ya Blatter. 
Blatter ambaye amekuwa katika kiti hicho cha FIFA tangu mwaka 1998 amesema amechukua uamuzi huo kwa vile kazi alioianza anaona bado haijamalizika.