BENDI kongwe za muziki wa dansi nchini, Msondo Ngoma na Mlimani Park 'Sikinde' ambazo zinatarajiwa kuonyeshana kazi wiki ijayo, zimetambiana kwa kila moja ikijinasibu kuizima nyingine katika onyesho lao la pamoja litakalofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.r
Msondo na Sikinde zitakutana tena Februari 18 ikiwa ni mara ya pili katika kipindi cha miezi miwili baada ya kuchuana awali Desemba 30 katika onyesho lililofanyika ndani ya ukumbi wa Mzalendo Pub, uliopo Millenium Tower, Makumbusho Dar es Salaam.
Wakati siku zikikaribia kabla ya pambano hilo, viongozi wa bendi hizo wameanza kurushiana vijembe kila upande ukitamba kuwazima wenzake.
Msemaji wa Msondo, Rajabu Mhamila "Super D', alisema wanaamini kama walivyowazima Sikinde katika onyesho lao la Desemba, ndivyo watakavyofanya wiki ijayo kutokana na kikosi chao kinachoundwa na wanamuziki vijana na wachapakazi.
"Tunajua kwa sasa Sikinde watakuwa wanatafuta namna ya kutukabili, lakini kwa kifupi watarajie kufunikwa kama tulivyofanya kwenye onyesho la Mzalendo Pub," alisema Super D.
Hata hivyo, Sikinde ambao walikuwa visiwani Zanzibar kwenye Tamasha la Sauti za Busara wamejinasibu kuwa Msondo hawana ubavu mbele yao na kuwataka mashabiki wa muziki waende Diamond Jubilee kushuhudia ukweli wa wanachokisema.
Katibu wa Sikinde, Hamis Milambo alisema Sikinde ni zaidi ya Msondo kutokana na kukamilika kila idara kuanzia safu ya uimbaji, wapiga magitaa na wapuliza tarumbeta walichodai watatumia kama silaha ya kuwazima mahasimu wao.
"Sisi ni kama Barcelona, tuna safu kali ya ushambuliaji nikimaanisha waimbaji na viungo mahiri ambao ni wapuliza ala za upepo sikuambii wapiga magita, sijui kama Msondo watafua dafu," alisema Milambo.
Milambo alisema bendi yao inatarajia kurejea leo mchana kuendelea na utambulisho wa vibao vyao vipya vinavyoandaliwa kwa ajili ya albamu yao ijayo.
STRIKA

USILIKOSE

Friday, February 11, 2011
Friday, February 4, 2011
Wasanii wa kike tujiheshimu-Regina

MMOJA wa waigizaji wa filamu anayekuja juu nchini, Regina Mroni amewaasa wasanii wenzake hususani wa kike, kujiheshimu na kuepukana kufanya matendo yanayowachafua mbele ya jamii pamoja na kuidhalilisha fani yao kuonekana kama kazi ya wahuni.
Mroni, aliyeng'ara kwenye filamu kama Trip to Amerika, Mastress, Siri y Mama, Aisha na nyinginezo, alisema kuna baadhi ya wasanii hasa wa kike wamekuwa wakiona raha kujianika utupu na kuhusishwa na skendo chafu, wakiamini wanakuza majina yao wakati wanajidhalilisha.
Alisema umaarufu wa msanii yeyote unapatikana kutokana na ubora na umahiri wa kazi zake na sio matendo machafu na hivyo kuwataka wasanii wa kike wajiamini, kujituma na kuithamini kazi yao ili jamii iwaheshimu.
"Wapo baadhi yetu wamekuwa wakijihusisha na matendo machafu na kuandikwa kila mara, kitu ambacho tofauti na fikra zao kuwa wanajijengea majina na umaarufu, wanajidhalilisha na kuonekana mbele ya jamii kama watu wasio na maadili kitu ambachio ni kibaya," alisema Mroni.
Mroni, aliyetumbukia kwenye fani hiyo miaka miwili iliyopita akitokea kwenye urembo ambapo aliwahi Miss Utalii Morogoro, Miss Ukonga, Miss Singida na kushiriki Miss Tanzania, alisema sanaa ni kazi kama kazi nyingine na wanaishiriki waithamini na kuipenda.
Alisema 'wavamizi' wachache kwenye fani hiyo wasio na vipaji ndio wanaojiachia na kujianika na mwisho wa siku wanadhalilika na kisha kupotea wakiwaacha wasanii wa kweli wakiendelea kutamba.
Mwisho
TAFF yapewa kifyagio kwa tamasha la filamu la Nyerere
SHIRIKISHO la Filamu Tanzania, TAFF, limepewa heko kwa ubunifu wake wa kuanzisha tamasha la filamu za Kibongo ambalo litafanyika Februari 14-19 jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo la kwanza kufanyika nchini kwa filamu za Kitanzania litafanyikia kwenye viwanja vya Leaders kwa kuzunduliwa na Rais Jakaya Kikwete na kufungwa na mke wa hayati baba wa taifa, Mwl Nyerere, Mama Maria Nyerere.
Baadhi ya wadau wa filamu wakiwemo wasanii wa fani hiyo wamesema kitendo cha TAFF kubuni tamasha hilo ni jambo la kupongezwa kwa vile litasaidia kuinua soko la kazi za wasanii wa kibongo, mbali na kutoa fursa kwa wananchi kupata mwamko wa kuzipenda kazi hizo.
"TAFF wamefanya jambo la maana ambalo wadau wa filamu Bongo tulikuwa tunalisubiri kwa muda mrefu, kitu cha muhimu waliendeleze kama mengine," alisema Leila Mwambungu wa Kimara.
Leila, alisema tamasha hilo linaweza kusaidia kuamsha hisia wa watanzania kupenda kazi za nyumbani kwa madai wapo wengine wanazichukulia poa filamu za Kibongo na kuhusudu kazi za Nigeria au Marekani.
Mtayarishaji wa filamu anayekuja juu, Husseni Ramadhani 'Swagger' alisema tamasha hilo ni kama njia ya wadau wa filamu kujitangaza na kuwahimiza wenzake kujitokeza kwa wingi kulishiriki kuanzia mwanzo wake hadi siku ya ufungwaji wake.
"Nafasi kama hizi ni muhimu kuzichangamkia, kwa kweli nalipongeza TAFF kwa kubuni kitu kama hiki, kwani itatusaidia wengine kujifunza makubwa zaidi ya yale tunayoyajua katika sanaa hiyo kutokana na ukweli tumesikia kuna mafunzo kadhaa yatakayotolewa hapo," alisema Swagger ambaye anatamba na filamu kama Hazina, Who is a Killer na sasa Bangkok Deal.
TAFF kupitia viongozi wake chini ya Rais Simon Mwakifamba, walitangaza kuanzisha kwa tamasha hilo litakalozinduliwa wiki ijayo na Rais Kikwete kwa ajili ya kuonyesha kazi za kitanzania pamoja na kupambwa na burudani kadhaa za sanaa na mada mbalimbali za kifani.
***
Tamasha hilo la kwanza kufanyika nchini kwa filamu za Kitanzania litafanyikia kwenye viwanja vya Leaders kwa kuzunduliwa na Rais Jakaya Kikwete na kufungwa na mke wa hayati baba wa taifa, Mwl Nyerere, Mama Maria Nyerere.
Baadhi ya wadau wa filamu wakiwemo wasanii wa fani hiyo wamesema kitendo cha TAFF kubuni tamasha hilo ni jambo la kupongezwa kwa vile litasaidia kuinua soko la kazi za wasanii wa kibongo, mbali na kutoa fursa kwa wananchi kupata mwamko wa kuzipenda kazi hizo.
"TAFF wamefanya jambo la maana ambalo wadau wa filamu Bongo tulikuwa tunalisubiri kwa muda mrefu, kitu cha muhimu waliendeleze kama mengine," alisema Leila Mwambungu wa Kimara.
Leila, alisema tamasha hilo linaweza kusaidia kuamsha hisia wa watanzania kupenda kazi za nyumbani kwa madai wapo wengine wanazichukulia poa filamu za Kibongo na kuhusudu kazi za Nigeria au Marekani.
Mtayarishaji wa filamu anayekuja juu, Husseni Ramadhani 'Swagger' alisema tamasha hilo ni kama njia ya wadau wa filamu kujitangaza na kuwahimiza wenzake kujitokeza kwa wingi kulishiriki kuanzia mwanzo wake hadi siku ya ufungwaji wake.
"Nafasi kama hizi ni muhimu kuzichangamkia, kwa kweli nalipongeza TAFF kwa kubuni kitu kama hiki, kwani itatusaidia wengine kujifunza makubwa zaidi ya yale tunayoyajua katika sanaa hiyo kutokana na ukweli tumesikia kuna mafunzo kadhaa yatakayotolewa hapo," alisema Swagger ambaye anatamba na filamu kama Hazina, Who is a Killer na sasa Bangkok Deal.
TAFF kupitia viongozi wake chini ya Rais Simon Mwakifamba, walitangaza kuanzisha kwa tamasha hilo litakalozinduliwa wiki ijayo na Rais Kikwete kwa ajili ya kuonyesha kazi za kitanzania pamoja na kupambwa na burudani kadhaa za sanaa na mada mbalimbali za kifani.
***
Ray, Kanumba na Msondo kila mtu kivyake
Ray ana 'Second Wife, Deception noma!
WAKATI filamu ya Family Disaster ikiendelea kutamba mitaani kwa sasa, msanii nyota wa fani hiyo nchini, Vincent Kigosi 'Ray', yupo mbioni kuachia kazi nyingine mpya iitwayo 'The Second Wife'.
Filamu hiyo ya kimapenzi, imewashirikisha wasanii kadhaa nyota pamoja na waigizaji chipukizi ambao wameibuliwa na kampuni iliyotayarisha filamu hiyo, RJ Production.
Miongoni mwa waigizaji walioshiriki filamu hiyo ni pamoja na Ray mwenyewe, Colleta Raymond, Aisha Bui, Riyama Ally, Msungu, Ramla na mtoto aitwae Aisha ambaye ni chupukizi.
Ray ameanika kwenye mtandao wake kuwa, filamu hiyo ambayo ameigiza kama muumini wa Kiislam ipo katika hatua ya mwisho kabla ya kuachiwa ni moja ya kazi yenye mafunzo makubwa kwa jamii.
"Kama nilivyofanya kwenye The Divorce ndani ya filamu hii mafunzo ni yale yale na mashabiki mkae mkao wa kula kupata uhondo," alisema Ray.
Kwa mujibu wa taarifa hizo kama filamu zake nyingine, 'The Second Wife' itasambazwa na kampuni ya Steps Entertainment.
Wakati huo huo filamu mpya ya Steven Kanumba iitwayo Deception, aliyoigiza pamoja na Bakari Makuka, Rose Ndauka na Patcho Mwamba imekuwa ikinunuliwa kama njugu tangu iigizwe sokoni mapema wiki hii.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Nipashe, filamu hiyo imekuwa ikigombewa kununuliwa sambamba na Pete ya Ajabu na Family Disaster ambayo ina karibu mwezi sasa sokoni.
***
Msondo wapeleka mpya Songea
BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo Ngoma, kesho inatarajiwa kuzitambulisha nyimbo zao mpya zinazoandaliwa kwa ajili ya albamu ya 2011 mjini Songea mkoani Ruvuma.
Msondo inayotamba na albamu ya ya Huna Shukrani, itatumbuiza kwenye ukumbi wa Serengeti Bar, mjini huo.
Kwa mujibu wa kiongozi wa bendi hiyo, Said Mabera 'Diblo' ni kwamba Msondo itatumbuiza kwenye ukumbi huo nyakati za usiku, wakati jioni watakuwepo kwenye dimba la Majimaji kushuhudia pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga na wenyeji Majimaji-Songea.
Mabera, alisema katika onyesho hilo, bendi yao itapiga nyimbo zao za zamani pamoja na zile mpya zinazoendelea kuandaliwa kwa ajili ya albamu yao ijayo.
"Tupo Songea na kesho tutafanya onyesho kwenye ukumbi wa Serengeti, wakazi wa Songea wakae mkao wa kupata uhondo mtupu," alisema Mabera mmoja wa wapiga solo mahiri nchini na mwanamuziki aliyedumu kwa muda mrefu Msondo tangu alipojiunga mwaka 1973.
Mabera alizitaja baadhi ya nyimbo watakazozipiga kwenye onyesho hilo ni pamoja na zile za albamu za Demokrasia ya Mapenzi, Ndoa Ndoana, Kilio cha Mtu Mzima, Piga Ua Talaka Utatoa, Kaza Moyo, Kicheko kwa JIrani na Huna Shukrani.
"Pia tutawapigia na kuzitambulisha nyimbo mpya za Lipi Jema, Dawa ya Deni, Kwa Mjomba Hakuna Urithi na Baba Kakura, yaani ni burudani kwa kwenda mbele," alisema.
Baadhi ya wanamuziki wa Msondo ambayo wiki iliyopita ilimpoteza mmoja wa waimbaji wake mahiri, Hamis Maliki 'Super Maliki' watakapanda jukwaani leo ni pamoja na Mabera, Roman Mng'ande, Huruka Uvuruge, Ibrahim Kandaya, Juma Katundu, Is'haka Katima, Eddo Sanga na wengineo.
***
WAKATI filamu ya Family Disaster ikiendelea kutamba mitaani kwa sasa, msanii nyota wa fani hiyo nchini, Vincent Kigosi 'Ray', yupo mbioni kuachia kazi nyingine mpya iitwayo 'The Second Wife'.
Filamu hiyo ya kimapenzi, imewashirikisha wasanii kadhaa nyota pamoja na waigizaji chipukizi ambao wameibuliwa na kampuni iliyotayarisha filamu hiyo, RJ Production.
Miongoni mwa waigizaji walioshiriki filamu hiyo ni pamoja na Ray mwenyewe, Colleta Raymond, Aisha Bui, Riyama Ally, Msungu, Ramla na mtoto aitwae Aisha ambaye ni chupukizi.
Ray ameanika kwenye mtandao wake kuwa, filamu hiyo ambayo ameigiza kama muumini wa Kiislam ipo katika hatua ya mwisho kabla ya kuachiwa ni moja ya kazi yenye mafunzo makubwa kwa jamii.
"Kama nilivyofanya kwenye The Divorce ndani ya filamu hii mafunzo ni yale yale na mashabiki mkae mkao wa kula kupata uhondo," alisema Ray.
Kwa mujibu wa taarifa hizo kama filamu zake nyingine, 'The Second Wife' itasambazwa na kampuni ya Steps Entertainment.
Wakati huo huo filamu mpya ya Steven Kanumba iitwayo Deception, aliyoigiza pamoja na Bakari Makuka, Rose Ndauka na Patcho Mwamba imekuwa ikinunuliwa kama njugu tangu iigizwe sokoni mapema wiki hii.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Nipashe, filamu hiyo imekuwa ikigombewa kununuliwa sambamba na Pete ya Ajabu na Family Disaster ambayo ina karibu mwezi sasa sokoni.
***
Msondo wapeleka mpya Songea
BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo Ngoma, kesho inatarajiwa kuzitambulisha nyimbo zao mpya zinazoandaliwa kwa ajili ya albamu ya 2011 mjini Songea mkoani Ruvuma.
Msondo inayotamba na albamu ya ya Huna Shukrani, itatumbuiza kwenye ukumbi wa Serengeti Bar, mjini huo.
Kwa mujibu wa kiongozi wa bendi hiyo, Said Mabera 'Diblo' ni kwamba Msondo itatumbuiza kwenye ukumbi huo nyakati za usiku, wakati jioni watakuwepo kwenye dimba la Majimaji kushuhudia pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga na wenyeji Majimaji-Songea.
Mabera, alisema katika onyesho hilo, bendi yao itapiga nyimbo zao za zamani pamoja na zile mpya zinazoendelea kuandaliwa kwa ajili ya albamu yao ijayo.
"Tupo Songea na kesho tutafanya onyesho kwenye ukumbi wa Serengeti, wakazi wa Songea wakae mkao wa kupata uhondo mtupu," alisema Mabera mmoja wa wapiga solo mahiri nchini na mwanamuziki aliyedumu kwa muda mrefu Msondo tangu alipojiunga mwaka 1973.
Mabera alizitaja baadhi ya nyimbo watakazozipiga kwenye onyesho hilo ni pamoja na zile za albamu za Demokrasia ya Mapenzi, Ndoa Ndoana, Kilio cha Mtu Mzima, Piga Ua Talaka Utatoa, Kaza Moyo, Kicheko kwa JIrani na Huna Shukrani.
"Pia tutawapigia na kuzitambulisha nyimbo mpya za Lipi Jema, Dawa ya Deni, Kwa Mjomba Hakuna Urithi na Baba Kakura, yaani ni burudani kwa kwenda mbele," alisema.
Baadhi ya wanamuziki wa Msondo ambayo wiki iliyopita ilimpoteza mmoja wa waimbaji wake mahiri, Hamis Maliki 'Super Maliki' watakapanda jukwaani leo ni pamoja na Mabera, Roman Mng'ande, Huruka Uvuruge, Ibrahim Kandaya, Juma Katundu, Is'haka Katima, Eddo Sanga na wengineo.
***
Extra Bongo yaivunjavunja Twanga Pepeta
NENO zuri la kusema ni kwamba African Stars 'Twanga Pepeta' imevunjwavunjwa baada ya wanamuziki wake nyota saba kuihama bendi hiyo kwa mpigo na kutua Extra Bongo 'Wana 'Next Level' iliyoingia rasmi kambini kujiwinda na albamu mpya ya pili.
Wanamuziki hao saba walitambulishwa rasmi leo asubuhi na Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki, ambapo alisema lengo la kuwanyakua wakali hao ni kutaka bendi yake iwe matawi ya juu na kuleta mabadiliko ya muziki wa dansi nchini.
Choki aliwatambulisha wanamuziki hao ambapo ni waimbaji wawili, wapiga gitaa wawili na madansa watatu akiwemo mkali Hassani Mussa 'Super Nyamwela'.
Mbali na Nyamwela aliyeitumikia Twanga kwa miaka 11 mfululizo bila kuhama ni Rogart Hegga 'Catapilla' na Saul Ferguson ambao ni waimbaji, Hosea Mgohachi mpuiga gita zito la besi na Godi Kanuti anayecharaza magita yote.
Wanenguaji wengine waliomfuata Nyawela Extra Bongo ni Otilia Boniface na Issack Burhan maarudu kama Danger Boy.
Choki alisema wanamuziki hao wote wana mikataba na bendi yao na mchana huu wanatarajia kuungana na wanamuziki wenzao kambini eneo la Mbezi Mwisho kujipanga kwa albamu mpya.
Alisema kambi hiyo ya muda wa wiki tatu itatumika kuwapa fursa wanamuziki hao wapya kuzoeana na wenzao kabla ya kuanza kufanya vitu vyao hadharani wakiwa wamezaliwa upya.
Mkurugenzi huyo aliyesema tukio kama hilo la kuibomoa Twanga liliwahi kumtokea miaka minne iliyopita alipochukuliwa wanamuziki wa idadi kama hiyo na ASET na kuifanya Extra Bongo 3x3 Kujinafasi kuzimika hadi ilipofufuka mwaka jana.
Alisema wanamuziki hao wapya wamenyakuliwa na Extra Bongo tayari kuziba nafasi za waliotemwa akiwemo rapa machachai Greyson Semsekwa na wenzake kadhaa.
Wakizungumza kwenye utambulisho huo, Ferguson na Nyamwela walisema wamekuja kuthibitisha thamani yao na mashabiki wa Extra Bongo watarajie makubwa.
"watarajie kazi bab'kubwa kwani tunafahamika kwa vipaji vya fani hii," alisema Ferguson.
Nyamwela aitema Twanga, adai miaka 11 imetosha
KIONGOZI wa muda mrefu wa madansa wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' Hassan Mussa 'Super Nyamwela', aliyetangazwa jana kujiunga na bendi ya Extra Bongo, amedai amefikia uamuzi huo kwa lengo la kutaka kubadilisha upepo baada ya kukaa bendi yke kwa miaka zaidi ya 10.
Akizungumza kwenye utambulisho wake na wenzake sita toka Twanga, Nyamwela alisema miaka 11 aliokaa ASET imemtosha na ndio maana ameondoka ili kuzaliwa upya.
Nyamwela alisema hata hivyo pamoja na kuondoka Twanga ikiwa ni bendi yake pekee kuifanyia kazi tangu alipochukuliwa toka kundi la Billbum, hawezi kuponda alikotoka kwa vile imemsaidia kwa mengi na kwa sasa akili yake ni kuwapa burudani mashabiki wa bendi yake mopya.
"Nimeondoka kwa kutaka kubadilisha upepo, mnanijua mie sina utamaduni wa kuhamahama, ila kwa kutaka kuleta mabadiliko katika fani na maisha yangu kwa ujumla nimeamua kuoka Twanga na watu wasinchukulie vingine natafuta maisha," alisema dansa huyo bingwa wa zamani wa Bolingo Dar.
Aliongeza kuwa kama alivyokuwa Twanga alipoipa mafanikio makubwa, ndivyo ambavyo amepania kufanya hivyo akiwa Extra Bongo ambao ameungana nao kambini kujiandaa kupakua albamu mpya.
"Nyamwela ni yule yule, ila kwa hapa Extra mashabiki wake watarajie mambo makubwa na mazuri zaidi, na imani kwa ushirikiano na wenzangu Extra Bongo itatisha," alisema Nyamwela.
Mbali na Nyamwela, katika utambulisho huo, pia madansa Otilia Boniface, Isaack Burhani nao walitambulishwa sambamba na wanamuziki, Rogart Hegga 'Catapillar', Saulo Ferguson, Hosea Mgohachi na God Kanuti waliokuwa Twanga Pepeta.
wanamuziki hao walitambulishwa kwa waandishi wa habai jana na Mkurugenzi wa bendi hiyo ya Extra Bongo, Ally Choki 'Kamarade'.
Saturday, December 18, 2010
Baba Diana a.k.a Lukasa kuzikwa kesho mjini Tanga
MWANAMUZIKI Mkongwe wa muziki wa dansi, Abuu Semhando 'Baba Diana', 57, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajili ya barabarani anatarajiwa kusafirishwa kesho kwenda wilayani Muheza, Tanga kuzikwa.
Kwa mujibu Meneja Masoko wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' aliyokuwa akiifanyia kazi marehemu huyo,Martin Sospeter ni kwamba Semhando aliyefahamika pia kama Lukasa enzi akiwa Super Matimila, atazikwa kesho nyumbani kwao Tanga, ingawa msiba upo Mwananyamala Kisiwani alipokuwa akiishi enzi za uhai wake.
Sospeter, alisema mwili wa marehemu kwa sasa upo Muhimbili na wanafanya mipango ya kuusafirisha kwenda kuzikwa kwao Tanga kesho alasiri.
"Marehemu anatarajiwa kusafirishwa kwao Tanga kwa ajili ya mazishi, ingawa kwa sasa msiba upo nyumbani kwake, Mwananyamala Kisiwani na mwili wake umeshapelekwa hospitali ya Muhimbili," alisema Sospter.
Meneja huyo alisema kuwa marehemu aliyezaliwa Oktoba 24, 1953 na kuanza muziki mwaka 1974 katika bendi ya Sola Tv kabla ya kupita bendi mbalimbali Twanga Pepeta aliyoiongoza kama Katibu wake, amewaachia pengo kubwa lisilozibika aslan.
"Ni pigo kwetu na tumeshtushwa na kuhuzunishwa na kifo chake cha ghafla," alisema Sospeter.
Kifo cha mkongwe huyo aliuyewahi kuzipigia bendi za Super matimila, Orchestra Toma Toma, Tango Musica, Diamond Sound 'Wana Kibinda Nkoy', Beta Musica kabla ya kuasisi Twanga Pepeta, kimekuja masaa machache tangu fani ya muziki kumpoteza Ramadhan MToro Ongalla aliyefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Dk Remmy alifariki Jumatatu na kuzikwa Alhamis, huku Semhando na wanamuziki wenzake wakishiriki mwanzo mwisho katika msiba huo.
Mwisho
Kwa mujibu Meneja Masoko wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' aliyokuwa akiifanyia kazi marehemu huyo,Martin Sospeter ni kwamba Semhando aliyefahamika pia kama Lukasa enzi akiwa Super Matimila, atazikwa kesho nyumbani kwao Tanga, ingawa msiba upo Mwananyamala Kisiwani alipokuwa akiishi enzi za uhai wake.
Sospeter, alisema mwili wa marehemu kwa sasa upo Muhimbili na wanafanya mipango ya kuusafirisha kwenda kuzikwa kwao Tanga kesho alasiri.
"Marehemu anatarajiwa kusafirishwa kwao Tanga kwa ajili ya mazishi, ingawa kwa sasa msiba upo nyumbani kwake, Mwananyamala Kisiwani na mwili wake umeshapelekwa hospitali ya Muhimbili," alisema Sospter.
Meneja huyo alisema kuwa marehemu aliyezaliwa Oktoba 24, 1953 na kuanza muziki mwaka 1974 katika bendi ya Sola Tv kabla ya kupita bendi mbalimbali Twanga Pepeta aliyoiongoza kama Katibu wake, amewaachia pengo kubwa lisilozibika aslan.
"Ni pigo kwetu na tumeshtushwa na kuhuzunishwa na kifo chake cha ghafla," alisema Sospeter.
Kifo cha mkongwe huyo aliuyewahi kuzipigia bendi za Super matimila, Orchestra Toma Toma, Tango Musica, Diamond Sound 'Wana Kibinda Nkoy', Beta Musica kabla ya kuasisi Twanga Pepeta, kimekuja masaa machache tangu fani ya muziki kumpoteza Ramadhan MToro Ongalla aliyefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Dk Remmy alifariki Jumatatu na kuzikwa Alhamis, huku Semhando na wanamuziki wenzake wakishiriki mwanzo mwisho katika msiba huo.
Mwisho
Buriani Baba Diana utakumbukwa daima
KIFO kimeumbwa kwa usiri mkubwa hata hujaji wake, pia huwa ni siri mno, kiasi ni vigumu kwa kiumbe chochote duniani kubaini lini atakumbana nacho.
Lau kisingekuwa na usiri katika suala la kifo, kwamtu kufahamu kitakufikia lini, wapi na kwa njia gani, sidhani kama kuna ambaye angekuwa akitoka nje siku ya ahadi yake kwa kuhofia kukutana nacho.
Ila kwa kuwa Mungu ana hekima na maana kubwa ya kukifanya kuendelea kuwa ni siri yake pekee yake duniani na ahera, kifo kinaendelea kuogopwa.
Ndio maana hata mwanamuziki gwiji wa muziki wa dansi, marehemu Marijani Rajabu 'Jabari la Muziki' enzi za uhai wake alitunga wimbo ulioelezea hamu yake ya kutaka kuwepo rufaa ya kifo ili mradi kuwarudisha wapendwa wetu wanaondoka ghafla bila kutarajiwa.
Abuu Semhando maarufu kama 'Baba Diana' au 'Lukasa' ambaye kwa siku zote nne za msiba wa mwanamuziki mwenzake, Ramadhani Ongolla 'Dk Remmy' alishiriki mwanzo mwisho hadi alipopumzishwa makaburini Sinza, Dar es Salaam, naye amefariki dunia.
Semhando, aliyekuwa mpiga dramu na Katibu wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' alifariki usiku wa kuamkia jana, ikiwa ni masaa machache tangu amzike mwenzake baada ya kupatwa na ajali mbaya ya barabarani.
Marehemu huyo alikumbwa na mauti hayo maeneo ya Mbezi Beach, akitokea kazini kwake baada ya kugongwa na gari akiwa anaendesha pikipiki na kujeruhiwa vibaya kichwani kabla ya kufa papo hapo.
Mwili wa mkongwe huyo aliyefanyia kazi bendi mbalimbali hapa nchini tangu miaka ya 1970 na aliyekuwa mpiganiaji wa haki za wanamuziki wenzake kama baadhi ya waliowahi kufanya nae kazi wanavyomueleza, uliohifadhiwa katika hospitali ya Muhimbili, utasafirishwa leo kwenda kuzikwa Muheza jiji Tanga.
Baadhi ya wanamuziki wa dansi nchini wamedai kushtushwa na kifo hicho cha ghafla cha Semhando, wakirejea kwamba walikuwa naye katika safari ya kumsindikiza Remmy aliyefariki Jumatatu na kuzikwa Alhamis, masaa machache kabla naye hajapatwa na mauti hayo.
Tshimanga Kalala Assosa, mtunzi na muimbaji aliyezipigia bendi mbalimbali kama Lipualipua, Le Kamalee, Fuka Fuka na Orchestra Marquis, alisema kama sio kuogopa kufuru, angeweza kusema Mungu ni kama amewaonea wanamuziki wa Tanzania wiki hii kwa vifo hivyo mfululizo.
"Naogopa kumkufuru Mungu, lakini misiba hii na hasa huu wa Semhando niliofahamishwa usiku wa manane kwa kupigiwa simu umeniuma kupindukia, ila sina jinsi kwa kuwa kazi ya Mungu haina makosa," alisema Assosa.
Assosa, alisema kuondoka kwa wakongwe hao ni kama uzindushi kwa waliosalia juu ya umuhimu wa kushikamana na kumcha Mungu, pamoja na kufanya maandalizi ya kusaka warithi wa nafasi zao katika muziki kwa sababu bila ya hivyo fani yao itatereka.
Ally Choki 'Mzee wa Farasi', aliyewahi kufanya kazi na Semhando wakati akiwa mwanamuziki na kiongozi wa Twanga Pepeta, alisema kifo cha Semhando ni pigo kwa familia ya marehemu, wadau wa muziki na hususani bendi yake ya Africana Stars kwa kuwa alikuwa nguzo.
"Sio siri ni msiba mkubwa na pengo kubwa katika muziki wa dansi na hasa Twanga Pepeta kwa vile nafahamu jinsi gani marehemu alivyokuwa 'roho' ya bendi hiyo, licha ya kwamba wapo waliokuwa wakimuona kama 'mnoko' fulani, namlilia milele Semhando," alisema Choki.
Choki alisema uzoefu wake katika fani ya muziki, ilimfanya marehemu kuwa mhimili wa bendi hiyo na muziki wa dansi kwa ujumla, akipigania masilahi ya wanamuziki wenzake na kusema hajui nani wa kuliziba pengo lake.
"Muhimu ni kumuombea kwa Mungu na pia kuiombea familia yake iwe na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi," alisema Choki.
Meneja wa Masoko wa bendi hiyo, Martin Sospeter, alisema kifo cha kiongozi mwenzao na mwanamuziki wao, ni pigo kubwa kutokana na kutokea kwake ghafla, lakini wanamuachia Mungu kwa kuwa alimpenda zaidi kuliko walivyompenda na kumthamini wao.
"Ni pigo kwetu na fani nzima ya muziki, tunajipanga kufanya maandalizi ya kumplekea mwenzetu katika makazi yake ya milele, ambapo atazikwa kesho (leo) nyumbani kwao mjini Tanga," alisema.
Marehemu Semhando ambaye majina yake kamili ni Abubakar Semhando, alizaliwa Oktoba 24, mwaka 1953 huko Muheza Tanga na kupata elimu ya msingi huko huko kwao, kabla ya kutumbukiza kwenye muziki miaka ya mwanzoni ya 1970.
Bendi yake ya kwanza kuifanyia kazi ni Sola TV ya jijini Dar mnamo mwaka 1974 kabla ya kutua Tanga International na kukaa nao hadi miaka ya 1980 alipohamia Super Matimila iliyokuwa chini ya Dk Remmy.
Aliihama Matimila na kutua Tomatoma Jazz akiwa na marehemu Adam Bakar 'Sauti ya Zege', kabla ya kuhamia Orchestra Safari Sound 'OSS' na kukaa nao hadi mwanzoni mwa miaka ya 1990 alipohamia Tango Musica, kisha kujiunga Vijana Jazz.
Baadae alitua Diamond Sound 'Wana Kibinda Nkoy' mwaka 1996 na kutunga kibao cha Neema kilichoipaisha bendi hiyo, miaka miwili baadae alihamia Beta Musica na kukaa nao kwa muda mfupi kabla ya kuhamia African Stars akiwa mmoja wa waasisi wake.
Amekuwa na bendi hiyo ya Twanga Pepeta tangu wakati huo hadi mauti yalipomkuta juzi akiwa ameshiriki kupiga dramu karibu nyimbo zote za albamu 10 za bendi hiyo kuanzia ile ya Kisa cha Mpenda hadi Mwana Dar es Salaam iliyozinduliwa mwaka huu.
Mwisho
BREAKING NEWS-ABUU SEMHANDO 'BABA DIANA' IS NO MORE


MWANAMUZIKI Mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Abuu Semhando 'Baba Diana' amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajali ya gari baada ya kugongwa akiwa kwenye pikipiki eneo la Africana, Mbezi jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana mapema zinasema kifo hicho kilitokea majira ya saa 9 usiku baada ya kugongwa na gari aina ya Benz lililomjeruhi vibaya sehemu ya kichwani.
Abuu aliyetamba miaka ya 1970 akiwa na bendi ya Vijana Jazz, amepatwa na mauti hayo ikiwa ni siku moja tu tangu ashiriki kumziba mkongwe mwenzake, Ramadhani Mtoro Ongalla 'Dk Remmy' aliyefariki Jumatatu na kuzikwa Alhamis.
Kwa hakika ni pigo kwa wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki na wadau wa muziki wa dansi kwa ujumla, ingawa Kazi ya Mola Haina Makosa kwa sababu alishatuambia mapema kwamba KILA NAFSI ITAONJA MAUTI, wametangulia sisi tu nyuma yao tuwadhaike na vifo vyao kwa vile hatujui saa au siku ambayo Malaikat Maut, Izraili atatupitia kuchukua AMANA.
INNALILLAH WAINNA ILAHI RAJIUN!
Thursday, December 16, 2010
Amer Lugunga Mwenyekiti Mpya Halmashauri ya Kilosa
DIWANI wa Kata ya Kimamba, wilayani Kilosa, Amer Lugunga, amefanikiwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo baada ya kuwaangusha wagombea wenzake wenzake wawili.
Wagombea walioangushwa na Lugunga, ni pamoja na Leonard Mapunda na mtu mwingine aliyetajwa kwa jina moja la Mbiza.
Katika mchuano huo uliofanyika kwenye ofisi za CCM wilaya ya Kilosa, Lugunga aliibuka mshindi kwa kuzoa jumla ya kura 40 kati ya 60 zilizopigwa kwenye kinyang'anyiro hicho kilichokuwa na ushindani mkali.
Mbiza alishika nafasi ya pili kwa kupata kura 17 na Mapunda aliambulia tatu tu.
Akizungumza na MICHARAZO mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi, Lugunga alisema atafanya kazi kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kuhakikisha Kilosa inaondokana na aibu iliyoighubika kwa sasa.
"Nawashukuru walionichagua, na ahadi yangu ni kwamba nitafanya kazi kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi, ili kuirejeshea heshima wilaya yetu iliyopewa hati chafu hivi karibuni kutokana na matumizi mabaya ya fedha za miradi ya maendeleo," alisema Lugunga.
Alipoulizwa juu ya 'zengwe' alilokuwa akiwekewa na baadhi ya wapinzani wake, Lugunga, alisema mambo yote yameisha na hana kinyongo na mtu.
Mwisho
Wagombea walioangushwa na Lugunga, ni pamoja na Leonard Mapunda na mtu mwingine aliyetajwa kwa jina moja la Mbiza.
Katika mchuano huo uliofanyika kwenye ofisi za CCM wilaya ya Kilosa, Lugunga aliibuka mshindi kwa kuzoa jumla ya kura 40 kati ya 60 zilizopigwa kwenye kinyang'anyiro hicho kilichokuwa na ushindani mkali.
Mbiza alishika nafasi ya pili kwa kupata kura 17 na Mapunda aliambulia tatu tu.
Akizungumza na MICHARAZO mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi, Lugunga alisema atafanya kazi kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kuhakikisha Kilosa inaondokana na aibu iliyoighubika kwa sasa.
"Nawashukuru walionichagua, na ahadi yangu ni kwamba nitafanya kazi kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi, ili kuirejeshea heshima wilaya yetu iliyopewa hati chafu hivi karibuni kutokana na matumizi mabaya ya fedha za miradi ya maendeleo," alisema Lugunga.
Alipoulizwa juu ya 'zengwe' alilokuwa akiwekewa na baadhi ya wapinzani wake, Lugunga, alisema mambo yote yameisha na hana kinyongo na mtu.
Mwisho
Extra Bongo yawanyatia akina Chokoraa

BAADA ya bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' kuwatimua kundini, wanamuziki wao nyota wawili, Khalid Chokoraa na Kalala Junior, uongozi wa bendi ya Extra Bongo, umeanza mipango ya kuwachukua wanamuziki hao kuimarisha kikosi chao.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Ally Choki, aliiambia MICHARAZO kuwa, tayari wameshaanza mazungumzo ya awali na wanamuziki hao ambao pia wanaunda kundi la Mapacha Watatu wakishirikiana na Jose Mara wa FM Academia.
Choki alisema walikuwa na mipango ya kuwachukua waimbaji hao kitambo kirefu,ila walikuwa wakisita kuhofia kutifuana na uongozi wa Twanga Pepeta, lakini kutimuliwea kwao kwa utovu wa nidhamu ni kama kumewarahisishia kazi.
"Kutimuliwa kwao Twanga Pepeta kumeturahisishia kazi ya kuwapata waimbaji hawa wenye vipaji vya aina yake na tumeshaanza mazungumzo ya awali, nadhani ndani ya wiki hii mambo yatakuwa shwari na wataanza kazi Extra Bongo," alisema Choki.
Choki aliongeza katika kuonyesha kuwa wapo karibu na wanamuziki hao na kuwakubali kwa kazi zao kupitia kundi lao la Mapacha watatu wanatarajia kufanya nazo onyesho la pamoja wakati wa Mkesha wa Mwaka Mpya na siku ya Mwaka Mpya wenyewe jijini Dar es Salaam.
Alisema onyesho la kwanza baina yao na Mapacha Watatu linalotamba na albamu ya 'Jasho la Mtu' litafanyika mkesha wa Mwaka Mpya, Vatican Hotel, Sinza na kisha siku ya Mwaka Mpya watakuwa wote pale TCC Chang'ombe.
"huwezi jua kwenye maonyesho hayo mawili yanaweza kutumiwa kama utambulisho wao ndani ya Extra Bongo," Choki alitania.
Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa, lengo la bendi yao ni kutaka kuona wanatamba kwenye muziki wa dansi nchini baada ya kurejea kwa mara ya pili baada ya kufariki enzi ikitumia miondoko ya 3x3.
Choki aliongeza wakati wakiwa, katika harakati hizo za kuwanyakua akina Chokoraa, aliyekuwa mmoja wa waasisi wa Extra Bongo ya awali, pia bendi yao inajiandaa kufanya uzinduzi wa albamu ya 'Mjini Mipango'.
Alisema uzinduzi uliofanyika Mei 25 mwaka huu ulikuwa ni wa bendi yao iliyofufuliwa upya na sio wa albamu kama baadhi ya watu walivyokuwa wanadhani na hivyo wanajipanga kuifanyia uzinduzi wake.
Choki alisema watazindua albamu hiyo yenye nyimbo sita ambazo baadhi zinaendelea kutamba kwenye vituo vya redio na runinga, huku wakiendelea kuandaa ya pili ambayo tayari baadhi ya nyimbo zake zimeshakamilika.
Dk Remmy kuzikwa leo

SAFARI ya mwisho ya hapa duniani kwa mwanamuziki nguli wa muziki wa dansi na ule wa Injili, Ramadhan Mtoro Ongalla 'Dk Remmy' aliyefariki mapema wiki hii, inatarajiwa kuhitimishwa rasmi leo atakapozikwa kwenye makaburi ya Sinza, jirani na nyumbani kwake.
Remmy, aliyezaliwa nchini Zaire (sasa DR Congo) miaka 63 iliyopita alifariki Jumatatu baada ya kuugua kwa muda mrefu atazikwa jioni ya leo kwenye makaburi hayo baada ya kuagwa kwa tamasha la muziki wa Injili kwenye viwanja vya Biafra, Kinondoni, jijini.
Mjomba wa marehemu, Mzee Makassy, alisema mwili wa marehemu utazikwa kwenye makuburi hayo jirani kabisa na mahali alipokuwa akiishi, Sinza kwa Remmy.
Marehemu Remmy aliingia nchini mwaka 1977 na kujiunga na bendi ya mjomba wake, Makassy Band na kutamba na kibao cha Siku ya Kufa kabla ya baadae kuhamis Super Matimila ambayo ilimpa umaarufu mkubwa kutokana na umahiri wake wa kutunga, kuimba na kupiga gita la solo ambapo alishiriki matamasha makubwa barani Ulaya mara kwa mara.
Hata hivyo miaka michache iliyopita alipata kiharusi na kupooza, ambapo aliamua kuokoka na kuanza kutumikia muziki wa Injili hadi mauti yalipompata akiwa ameacha mke na watoto kadhaa akiwemo mshambuliaji wa timu ya Azam, Kalimangonga 'Kally' Ongalla.
Bwana Alitoa Naye Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe. Micharazo tunamtakia safari njema aendako nasi tu nyuma yake kwa kuwa kila nafsi ni lazima ionje mauti.
Monday, December 13, 2010
Cheka, Maugo kumaliza Ubishi Dar

MABONDIA Francis Cheka 'SMG' na Mada Maugo 'King Maugo Jn' wanatarajia kumaliza ubishi baina yao watakapopigana kwenye ukumbi wa PTA jijini Dar es Salaam badala ya uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro.
Mratibu wa pambano hilo, Kaike Siraju, aliiambia MICHARAZO mapema leo kuwa, pambano la wababe hao wawili litafanyika Dar na sio Morogoro kama alivyokuwa akitaka iwe na kuingia kwenye mzozo na Mada Maugo.
Maugo, anayeshikilia taji la ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati, alitishia kutopigana na Cheka kama pambano hilo lingehamishiwa Morogoro.
Siraju, alisema wameangalia mambo mengi kabla ya kusitisha uamuzi wa kulibakisha pambano hilo Dar na kueleza kuwa maandalizi kwa ujumla yanaendelea vema ikiwemo mabondia wote kuendelea kujifua.
"Maandalizi ya pambano la Cheka na Maugo, yanaendelea vema na litafanyika Dar kama ilivyokuwa awali, baada ya jaribio la kulihamishia Moro kushindikana," alisema Siraju.
Siraju alisema pambano hilo la uzani wa Middle la raundi nane lisilo la kuwania Mkanda litakalofanyika Januari Mosi, mwakani, likisindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi.
Mratibu huyo aliitaja michezo ya utangulizi siku hiyo ni pamoja na pambano kati ya Mshihiri Kidira atakayezidunda na Deo Njiku, Jafari Majid dhidi ya Juma Afande na Hussein Mbonde atakayezichapa na Cosmas Cheka.
Michezo mingine ni ile ya Simba wa Tunduru ataonyeshana kazi na Albert Mbena, Arafati ‘Ngumi Jiwe’ atapambana na Juma Kihio wakati Sadik Momba atafunga kazi na Smoo Njiku.
Michezo yote hiyo inasimamiwa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBO na ni maalum kwa kukata mzizi wa fitina baina ya mabondia hao wanaotambiana kila mmoja akitamba ni bora kuliko mwenzie.
Mwisho
BREAKING NEWS-DK REMMY IS NO MORE

MWANAMUZIKI maarufu nchini aliyewahi kutamba na bendi za Makasy na Super Matimila kabla ya kuhamia kwenye muziki wa Injili, Ramadhani Mtoro Ongalla 'Dk Remmy' amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa tatizo la Ini, bado tunafuatilia kujua taratibu za mazishi yake.
Dk Remmy atakumbukwa kwa vibao vyake matata kama Nataka Mtoto, Siku ya Kufa, Muziki Sio Uhuni, Mambo kwa Soksi, Mrema, Mariam, Mwanza na kadhalika....!
Mungu Ilaze Roho ya Marehemu Mahali Pema. Amin
Friday, December 10, 2010
Sam wa Ukweli kuwasindikiza Mapacha Watatu J'3
MSANII anayekuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya, Salum Mohammed 'Sam wa Ukweli', anayetamba na kibao cha 'Sina Raha' anatarajia kulisindikiza kundi la muziki wa danis la 'Mapacha Watatu' katika onyesho la 'Usiku wa Sauti ya Kizazi Kipya cha Dansi' linalofanyika keshokutwa.
Onyesho hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Stereo Bar, Kinondoni jijini Dar es Salaam na Sam wa Ukweli, atakuwepo kulipamba onyesho hilo kwa vibao vyake murua kikiwemo cha 'Sina Raha' kinachotamba kwa sasa nchini.
Akizungumza na MICHARAZO, mratibu wa onyesho hilo, Sauda Mwilima, alisema onyesho hilo ni maalum kwa ajili ya kuwapa burudani mashabiki wa muziki wa dansi kupitia kundi hilo la Mapacha Watatu linaloundwa na waimbaji nyota watatu toka bendi za Africana Stars na Fm Academia.
Waimbaji hao wanaouunda kundi hilo linalotamba na albamu yao ya 'Jasho la Mtu' ni Khalid Chokoraa na Kalala Junior wa Twanga Pepeta pamoja na Jose Mara toka FM Academia.
"Katika kuwapa raha mashabiki wa muziki wanaojiandaa kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha 2011, nimeandaa Usiku wa Sauti ya Kizazi Kipya cha Dansi utakaofanyika Jumatatu ya Desemba 13, ambapo utapambwa na burudani toka kundi la Mapacha Watatu watakaosindikizwa na nyota wa muziki wa kizazi kipya, Sam wa Ukweli," alisema.
Sauda, alisema maandalizi ya onyesho lao yamekamilika kwa asilimia zote na kuwataka mashabiki kukaa mkao wa kula kupata burudani kabambe toka kwa wakali hao.
Munishi aja kuchangia yatima Bongo
MUIMBAJI nyota na mkongwe wa muziki wa Injili, Faustin Munishi anayeishi Kenya, anatarajia kutua nchini wiki ijayo kwa ajili ya kuja kutumbuiza kwenye tamasha maalum la muziki wa Injili la kuchangisha fedha kwa ajili ya yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Tamasha hiloi litakalofanyika kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama siku ya Desemba 26, limeandaliwa na asasi ya Keep a Child Alive, ambapo wasanii mbalimbali wa muziki wa injili wa ndani ya nje ya nchi wamealikwa kuja kulipamba.
Mratibu wa tamasha hilo, Godfrey Katunzi, aliiambia MICHARAZO kuwa, kati ya wasanii wa muziki wa Injili watakaotumbuiza siku hiyo ya 'Boxing Day' ni muimbaji mkongwe, Mtanzania Faustin Munishi, ambaye kwa miaka mingi anafanya shughuli zake nchini Kenya.
Katunzi, alisema mbali na Munishi anayetamba na vibao kama Chini ya Mwamba, Paulo na Sila, Amua Mwenyewe, Nimuogope Nani na nyingine, wengine watakaotumbuiza siku siku hiyo ni Dk Aaron, Jane Misso, Beatrice Muone na kwaya mbalimbali za jijini Dar es Salaam.
Mratibu huyo ambaye ni Katibu wa asasi hiyo ya Keep a Child Alive, alizitaja baadhi ya kwaya hizo ni ile ya New Life Church wanaotamba na albamu yao ya 'Sipati Picha', Tabata Menonite maarufu kama Wakunyatanyata na nyinginezo.
Katunzi alisema, lengo la tamasha hilo la injili ni kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia yatima na watoto hao wa mitaani walipiwe ada na kununuliwa vifaa na sare za shule pamoja na kutatua matatizo mbalimbali waliyonayo.
Aliwaomba watu binafsi na makampuni yenye uwezo kujitokeza kuwapiga tafu katika tamasha hilo, ili kutimiza malengo la kuwaonyesha upendo watoto hao, akidai jukumu la kusaidia na kulea yatima ni la watu wote bila kujali, dini, rangi, kabila au jinsia.
Levent kurekodi tatu mpya
BAADA ya ukimya mrefu tangu ilipofyatua albamu yao ya pili ya Mama Kabibi, bendi ya muziki wa dansi ya Levent Musica ya mjini Morogoro wiki ijayo itaingia studio kurekodi nyimbo tatu kwa ajili ya maandalizi ya albamu yao ijayo mpya.
Kiongozi wa bendi hiyo, Seleman Ramadhani 'Suzuki Sauti ya Malaika', aliiambia MICHARAZO jana kuwa nyimbo zitakazorekodiwa ni 'Pongezi Baba Madinda' na 'Mapenzi Maradhi' alizotunga yeye (Suzuki) na 'Mapenzi Sio Pesa' wa Steve Dokta.
Suzuki, alisema nyimbo hizo ni katyi ya nyimbo sita mpya za bendi hiyo zilizopangwa kurekodiwa kwa ajili ya albamu yao mpya na ya tatu ambayo wamepanga kuitoa mapema mwakani.
"Tupo katika maandalizi ya kwenda kurekodi nyimbo mpya tatu, tukiwa tunajiandaa kupakua albamu yetu ya tatu, kwa kweli kwa sasa Levent tupo kamili na tumepania," alisema Suzuki.
Mtunzi na muimbaji huyo, aliyerejea katika bendi hiyo baada ya kuikimbia kwa muda na kujiunga na Extra Bongo, alisema nyimbo nyingine tatu zimeshaanza kufanyiwa mazoezi na mara baada ya kumaliza kurekodi hizo za awali watarejea tena studio kukamilisha nyimbo hizo.
Kuhusu kikosi chao, Suzuki alisemakipo kamili, kila idara kuanzia safu ya unenguaji, wapiga ala na waimbaji ambao mbali na yeye yupo pia Steve Dokta na Salum Mzalamo 'Baba Mapacha'.
Bendi hiyo ya Levent ilianzishwa mwaka 2004 na imewahi kufyatua albamu mbili tu hadi sasa ambazo ni Rafiki ya 2006 na ile ya Mama Kabibi ya mwaka 2008 wakati bendi ikiwa chini ya Richard Malifa, alioyewahi kung';ara na bendi mbalimbali hapa nchini.
Kiongozi wa bendi hiyo, Seleman Ramadhani 'Suzuki Sauti ya Malaika', aliiambia MICHARAZO jana kuwa nyimbo zitakazorekodiwa ni 'Pongezi Baba Madinda' na 'Mapenzi Maradhi' alizotunga yeye (Suzuki) na 'Mapenzi Sio Pesa' wa Steve Dokta.
Suzuki, alisema nyimbo hizo ni katyi ya nyimbo sita mpya za bendi hiyo zilizopangwa kurekodiwa kwa ajili ya albamu yao mpya na ya tatu ambayo wamepanga kuitoa mapema mwakani.
"Tupo katika maandalizi ya kwenda kurekodi nyimbo mpya tatu, tukiwa tunajiandaa kupakua albamu yetu ya tatu, kwa kweli kwa sasa Levent tupo kamili na tumepania," alisema Suzuki.
Mtunzi na muimbaji huyo, aliyerejea katika bendi hiyo baada ya kuikimbia kwa muda na kujiunga na Extra Bongo, alisema nyimbo nyingine tatu zimeshaanza kufanyiwa mazoezi na mara baada ya kumaliza kurekodi hizo za awali watarejea tena studio kukamilisha nyimbo hizo.
Kuhusu kikosi chao, Suzuki alisemakipo kamili, kila idara kuanzia safu ya unenguaji, wapiga ala na waimbaji ambao mbali na yeye yupo pia Steve Dokta na Salum Mzalamo 'Baba Mapacha'.
Bendi hiyo ya Levent ilianzishwa mwaka 2004 na imewahi kufyatua albamu mbili tu hadi sasa ambazo ni Rafiki ya 2006 na ile ya Mama Kabibi ya mwaka 2008 wakati bendi ikiwa chini ya Richard Malifa, alioyewahi kung';ara na bendi mbalimbali hapa nchini.
Msondo yamuombea Gurumo
WAKATI hali yake ikizidi kuwa tete, uongozi wa bendi ya Msondo Ngoma umemuombea dua njema na kuwataka Watanzania kuzidi kumuombea kiongozi wao na muimbaji mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Maalim Muhidin Gurumo aliyelazwa hospitalini kwa matatizo ya mapafu.
Msemaji wa bendi hiyo, Rajabu Mhamila 'Super D', alisema wanamuziki na uongozi mzima wa Msondo umekuwa ukiendesha dua maalum kila siku kumtakia kila la heri na afueni, Gurumo ili aweze kurejea tena jukwaani.
Super D, alisema Msondo bado inamhitaji mno Gurumo kutokana na umahiri wake katika muziki na uongozi kwa ujumla na kuwaomba mashabiki wao na wadau wa muziki wa ujumla kuzidi kumuombea mwanamuziki huyo mkongwe awe kupona haraka.
"Kwa kweli tunamuombea sana mwenzetu aweze kupona na tunawasihi watanzania bila kujali dini, rangi au kabila na ushabiki wa muziki, wamuombee kamanda Gurumo, Mwenyezi Mungu amfanyie tahafif apone haraka," alisema Super D.
Super D, alisema pamoja na kumuombea kiongozi wao huyo, bendi yao bado inaendelea na maonyesho yao kama kawaida pamoja na kufanya maandalizi ya kufyatua albamu yao mpya.
Alisema kwa leo Jumamosi bendi yao itakuwa kwenye bonanza lao kwenye viwanja vya Sigara, TCC- Changombe na kesho Jumapili watawachezesha wapenzi wa muziki miondoko yao ya Msondo kwenye onyesho litakalofanyika Max Bar, Bungoni Ilala jijini Dar es Salaam.
"Hatuwezi kuacha maonyesho, tunaendelea na shoo huku tukizidi kumuombea mwenzetu, leo (jana) Ijumaa tutakuwa Postal Club, Jumamosi tunaendelea na bonanza letu pale TCC-Chang'ombe na tutamalizia wikiendi yetu kwenye ukumbi wa Maxi Bar, Ilala," alisema.
Msondo inayotamba na albamu ya HUna Shukrani iliyotoka mwaka jana, ipo katika maandalizi ya kutoa albamu mpya ambapo hadi sasa tayari imeshaachia nyimbo tatu ambazo ni Dawa ya Deni, Lipi Jema na Mjomba.
Ally Choki awafunda wanamuziki wenzake
NYOTA wa muziki wa dansi nchini, Ally Choki amewafunda wanamuziki wenzake akiwataka wajenge tabia ya kuwa na shukrani wakikumbuka mazuri wanayofanyiwa na bendi wanazozihama badala ya kuziponda na kutaja mabaya tu.
Choki alisema tabia ya wanamuziki wanaohama bendi kuponda na kukashfu kule watokapo sio tu zinavunja umoja, ila inajenga uhasama miongoni mwa wasanii na wamiliki na mwisho wa siku ni kudidimiza muziki ambao umekuwa ukisaidia vijana wengi kupata ajira zao.
Akizungumza na MICHARAZO, Choki, alisema yeye binafsi pamoja na kutamba kimuziki nchini, katu hawezi kusahau fadhila na mazuri aliyofanyiwa na Asha Baraka, kitu alichotaka hata wasanii wengine wawe na moyo wa namna hiyo wa kukumbuka fadhila.
Choki alisema amelazimika kusema hayo kutokana na baadhi ya wasanii walioihama bendi yake kusambaza maneno ya kashfa juu yake na bendi yake, wakati kabla ya kuhama walikuwa wakifanyiwa fadhila zilizowafanya wamuone kama 'Mungu-Mtu'.
"Siwalazimishi, lakini nawaasa wanamuziki wenzake na wasanii kwa ujumla kuwa na shukrani kwa mazuri wanayofanyiwa na makundi yao, kuhama hakukatazwi, lakini sio kwa kukashfu au kuponda tu, kwani ndiko kunakodumaza muziki," alisema Choki.
Aliongeza kama sio kuwa na moyo wa kutaka muziki wa dansi usonge mbele na kusaidia vijana wengine wenye vipaji kupata riziki kupitia ajira ya sanaa hiyo, asingeanzisha na kuendesha bendi ya Extra Bongo na badala yake angekuwa mwanamuziki wa kujitegemea ili ale kuku kwa raha.
"Kwa jina na umaarufu nilionao ndani na nje ya nchi naweza kuendesha shughuli zangu za muziki kama solo artist, lakini naguswa na kupenda kusaidia wengine kutokana, ili kulifanya jina langu liendelee kutajwa katika mchango wa muziki huu," alisema.
Choki, alisema hata leo Mbaraka Mwinshehe na Marijab Rajab pamoja na kufa wanatajwa kwa sababu waliwasaidia wengi kupitia bendi zao hali ambayo anatamani naye iwe hivyo milele.
Dance Music Competition laiva
USAILI wa wasanii chipukizi wa muziki wa dansi watakaoshiriki shindano la kusaka nyota wapya wa muziki huo nchini, kupitia shindano la 'Dance Music Competation' unatarajiwa kuanza rasmi Desemba 20-21 kwenye ukumbi wa Afri Center, Ilala jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa shindano hilo, Seleman Mathew alisema maandalizi ya mchakato huo umeshaanza kwa kuanza kutoa fomu za ushiriki kwa wanaopenda kushiriki mchuano huo kuzichangamkia kabla ya usaili huo utakaoendeshwa na majaji wanne.
Mathew aliwataja majaji hao kuwa ni wanamuziki wakongwe wa muziki huo nchini, Ally Choki wa Extra Bongo, Tshamanga Kalala Assosa wa Bana Marquiz, Nyota Waziri wa Kilimanjaro Band 'Wana Njenje' na Abdul Salvador 'Father Kidevu' wa Hisia Kali Band.
'Mchujo wa kusaka vijana kwa ajili ya shindano letu na nyota wapya wa muziki wa dansi utaanza rasmi Desemba 20-21 kwenye ukumbi wa Afri Center Ilala kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 11 jioni, na watakaopenya wataingia kwenye kinyang'anyiro hicho," alisema Mathew.
Alisema kinyang'anyiro cha shindano hilo kitaanza Januari 16 kwa washiriki kuingia kambini na kupigiwa kura hadi atakapopatikana mshindi katika fainali zitakazofanyika Machi 6 mwakani.
Mathew, beki za zamani wa timu za Simba, Yanga, Plisner na Ndovu-Arusha, alisema lenye lengo la shindano hilo ni kuibua wanamuziki wapya wa dansi na kuendeleza muziki huo nchini kuwabadili vijana wengi kuona hakuna muziki mwingine zaidi ya Bongofleva tu.
Alisema washiriki wanaotaka kushiriki wanapaswa kuwa katika kundi la kuanzia wasanii watano hadi saba wenye uwezo wa kuimba nyimbo za muziki wa dansi na kuongeza kwa wale ambao hawana makundi pia wanaruhusiwa muhimu wawe na uwezo katika muziki huo.
Alisema fomu za ushiriki wa shindano hilo zinapatikana kwenye ukumbi wa Afri Center kwa gharama ya Sh 3,000 na kuwataka wenye vipaji hivyo kuchangamkia nafasi hiyo, huku akiwataka wadhamini kujitokeza kuwapiga tafu kufanikisha shindano hilo la kwanza nchini kwa muziki huo.
Mratibu wa shindano hilo, Seleman Mathew alisema maandalizi ya mchakato huo umeshaanza kwa kuanza kutoa fomu za ushiriki kwa wanaopenda kushiriki mchuano huo kuzichangamkia kabla ya usaili huo utakaoendeshwa na majaji wanne.
Mathew aliwataja majaji hao kuwa ni wanamuziki wakongwe wa muziki huo nchini, Ally Choki wa Extra Bongo, Tshamanga Kalala Assosa wa Bana Marquiz, Nyota Waziri wa Kilimanjaro Band 'Wana Njenje' na Abdul Salvador 'Father Kidevu' wa Hisia Kali Band.
'Mchujo wa kusaka vijana kwa ajili ya shindano letu na nyota wapya wa muziki wa dansi utaanza rasmi Desemba 20-21 kwenye ukumbi wa Afri Center Ilala kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 11 jioni, na watakaopenya wataingia kwenye kinyang'anyiro hicho," alisema Mathew.
Alisema kinyang'anyiro cha shindano hilo kitaanza Januari 16 kwa washiriki kuingia kambini na kupigiwa kura hadi atakapopatikana mshindi katika fainali zitakazofanyika Machi 6 mwakani.
Mathew, beki za zamani wa timu za Simba, Yanga, Plisner na Ndovu-Arusha, alisema lenye lengo la shindano hilo ni kuibua wanamuziki wapya wa dansi na kuendeleza muziki huo nchini kuwabadili vijana wengi kuona hakuna muziki mwingine zaidi ya Bongofleva tu.
Alisema washiriki wanaotaka kushiriki wanapaswa kuwa katika kundi la kuanzia wasanii watano hadi saba wenye uwezo wa kuimba nyimbo za muziki wa dansi na kuongeza kwa wale ambao hawana makundi pia wanaruhusiwa muhimu wawe na uwezo katika muziki huo.
Alisema fomu za ushiriki wa shindano hilo zinapatikana kwenye ukumbi wa Afri Center kwa gharama ya Sh 3,000 na kuwataka wenye vipaji hivyo kuchangamkia nafasi hiyo, huku akiwataka wadhamini kujitokeza kuwapiga tafu kufanikisha shindano hilo la kwanza nchini kwa muziki huo.
Kanumba, apania uzinduzi wa Off Side DR Congo
NYOTA wa filamu nchini, Stephen Kanumba, ametamba kuwa uzinduzi wa kazi mpya aliyotoa pamoja na Vincent Kigosi 'Ray' iitwayo 'Off Side' utakaofanyika wiki ijayo nchini DR Kongo, utakuwa wa aina yake kutokana na jinsi walivyojiandaa kuwapa raha mashabiki wao nchini humo.
Uzinduzi wa filamu hiyo iliyowarejesha tena wawili hao pamoja tangu walipotoa Ophra miaka miwili iliyopita, unatarajiwa kufanyika kati ya Desemba 15-20 katika miji miwili ya nchi hiyo ya Goma na Bukavu.
Akizungumzia uzinduzi huo, Kanumba, alisema wamepania kufanya kweli ili kusuuza nyoyo za mashabiki wao lukuki waliopo katika nchini hiyo na Ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Kati na pia kutaka kujitengenezea majina yao katika anga la kimataifa.
"Hii ni nafasi ambayo haipaswi kuichezea na ndio maana tunaenda kamili kuwapa raha mashabiki wetu wakati wa uzinduzi huo, ili kujitangaza kimataifa," alisema Kanumba.
Kanumba, atakayeambatana na washiriki vinara wa filamu hiyo, Ray, Irene Owoya, Aunty Ezekiel na mtoto Jennifa aliyecheza filamu za This is It na Uncle JJ, alisema maandalizi yao ya kwenda kufanya uzinduzi huo yamekamilika na kwamba wakati wowote wiki ijayo watatua nchini humo kufanya mambo.
"Tunaendelea vema na maandalizi ya shughuli hiyo na tunawasihi wakazi wa Kongo wakae mkao wa kula kupata klitu roho inapenda kqwani tutafanya onyesho la jukwaani la dakika kama 30 ili kukonga nyoyo zao," alisema.
Katika filamu hiyo ya kimapenzi, Kanumba amecheza kama kijana maskini anayelazimishwa mapenzi na mke wa tajiri kitu ambacho kinamletea kizaazaa cha aina yake.
Kanumba alisema mara baada ya uzinduzi huo wa Kongo wataenda Burundi kabla ya kurejea nchini kwa ajili ya kuitoa hadharani kupitia kampuni ya Steps Entertainment ambayo ndiyo yenye kibali cha kuisambaza kazi hiyo.
Huba wana Bangkok Deal
BAADA ya kutamba na filamu ya Hazina, kampuni ya Huba, ipo mbioni kufyatua kazi mpya iitwayo Bangkok Deal ambayo imeshirikisha nyota kadhaa wa fani hiyo nchini.
Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Husseni Ramadhan 'Swagger' aliiambia NIPASHE jana kuwa, wapo hatua ya mwisho ya upigaji wa picha za filamu hiyo ambayo ameshirikishwa mkali Charles Magali.
Swagger alisema ndani ya filamu hiyo mbali na Mzee Magali, pia kuna wachina walioshirikishwa katika kuipa ladha kulingana na simulizi ya kazi hiyo aliyodai italeta mapinduzi ya fani hiyo nchini.
"Walioishuhudia Hazina na kazi nyingine tulizofyatua kupitia kampuni hii ni chamtoto tu, Bangkok Deal ni kazi isiyo na maelezo, tuombe tumalize na kuiingiza sokoni mashabiki ndio watakaijaji," alisema.
Swagger, alisema pamoja na kuendelea kurekodi filamu hiyo, pia kampuni hiyo tayari imeshaanza maandalizi ya kazi nyingine itayofahamika kwa jina la Hofu Tupu, aliyopanga kuitoa mapema mwakani.
Swagger aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya kupitia makundi ya 2 Wise Boy na The Crime Busters, alisema ndani ya filamu hizo wasanii wakali na wanaotamba katika fani hiyo wameshirikishwa.
Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Husseni Ramadhan 'Swagger' aliiambia NIPASHE jana kuwa, wapo hatua ya mwisho ya upigaji wa picha za filamu hiyo ambayo ameshirikishwa mkali Charles Magali.
Swagger alisema ndani ya filamu hiyo mbali na Mzee Magali, pia kuna wachina walioshirikishwa katika kuipa ladha kulingana na simulizi ya kazi hiyo aliyodai italeta mapinduzi ya fani hiyo nchini.
"Walioishuhudia Hazina na kazi nyingine tulizofyatua kupitia kampuni hii ni chamtoto tu, Bangkok Deal ni kazi isiyo na maelezo, tuombe tumalize na kuiingiza sokoni mashabiki ndio watakaijaji," alisema.
Swagger, alisema pamoja na kuendelea kurekodi filamu hiyo, pia kampuni hiyo tayari imeshaanza maandalizi ya kazi nyingine itayofahamika kwa jina la Hofu Tupu, aliyopanga kuitoa mapema mwakani.
Swagger aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya kupitia makundi ya 2 Wise Boy na The Crime Busters, alisema ndani ya filamu hizo wasanii wakali na wanaotamba katika fani hiyo wameshirikishwa.
Monday, December 6, 2010
Mapacha Watatu, Sam wa Ukweli kupimana Ubavu Dar
KUNDI la Mapacha Watatu linaloundwa na waimbaji mahiri nchini, Khalid Chokoraa, Jose Mara na Kalala Junior wanatarajia kuonyeshana kazi na msanii anayekuja juu katika miondoko ya muziki wa kizazi kipya Sam wa Ukweli.
Mapacha hao watatu na Sam wa Ukweli watakutanishwa kwenye onyesho la pamoja lifahamikalo kama 'Usiku wa Sauti za Kizazi Kipya cha Dansi' litakalofanyika Desemba 13, jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa onyesho hilo, Sauda Mwilima, aliiambia Micharazo kuwa, onyesho hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Stereo Bar, Kinondoni na wasanii hao wataonyesha umahiri wao.
Mwilima alisema onyesho hilo linawagusa Mapacha Watatu, watakaofanya vitu vyao kwa kutoa burudani na watasindikizwa na msanii Salum Mohamed 'Sam wa Ukweli' anayetamba na ngoma yake iitwayo 'Sina Raha'.
"Usiku wa Sauti ya Kizazi Kipya cha Dansi utaporomoshwa na Mapacha Watatu, wakisindikizwa na shoo ya ukweli mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini Sam wa Ukweli, yaani ni usiku usio wa kawaida," alisema Mwilima.
Mwilima ambaye ni mtangazaji wa kituo cha runinga cha Star Tv, alisema maandalizi ya onyesho hilo yanaendelea vema na kuwataka mashabiki wa muziki kukaa mkao wa kula kupata uhondo toka kwa wakali hao.
Kundi hilo la Mapacha Watatu linaundwa na waimbaji hao toka bendi hasimu za African Stars 'Twanga Pepeta' na FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma'.
Mwisho
Mapacha hao watatu na Sam wa Ukweli watakutanishwa kwenye onyesho la pamoja lifahamikalo kama 'Usiku wa Sauti za Kizazi Kipya cha Dansi' litakalofanyika Desemba 13, jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa onyesho hilo, Sauda Mwilima, aliiambia Micharazo kuwa, onyesho hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Stereo Bar, Kinondoni na wasanii hao wataonyesha umahiri wao.
Mwilima alisema onyesho hilo linawagusa Mapacha Watatu, watakaofanya vitu vyao kwa kutoa burudani na watasindikizwa na msanii Salum Mohamed 'Sam wa Ukweli' anayetamba na ngoma yake iitwayo 'Sina Raha'.
"Usiku wa Sauti ya Kizazi Kipya cha Dansi utaporomoshwa na Mapacha Watatu, wakisindikizwa na shoo ya ukweli mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini Sam wa Ukweli, yaani ni usiku usio wa kawaida," alisema Mwilima.
Mwilima ambaye ni mtangazaji wa kituo cha runinga cha Star Tv, alisema maandalizi ya onyesho hilo yanaendelea vema na kuwataka mashabiki wa muziki kukaa mkao wa kula kupata uhondo toka kwa wakali hao.
Kundi hilo la Mapacha Watatu linaundwa na waimbaji hao toka bendi hasimu za African Stars 'Twanga Pepeta' na FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma'.
Mwisho
Mkulo: Nimewasamehe walionichafua, ila sintowasahau
WAZIRI wa Fedha na Uchumi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kilosa, Mustafa Mkulo, amesema pamoja na kuwasamehe wale wote waliompakazia mabaya wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, bado hawezi kuwasahau hadi anaingia kaburini.
Pia, amewataka wanachama wa CCM na wananchi wa Kilosa kwa ujumla, kuzika tofauti zao zilizosababishwa mchakato wa uchaguzi mkuu, ili kuweza kushikamana kuijenga wilaya na jimbo lao la Kilosa liweze kuwa mfano wa kuigwa nchini.
Akizungumza kwenye mapokezi na hafla ya kupongezwa kuteuliwa tena kuwa waziri, Waziri Mkulo, alisema kashfa alizokuwa akipewa akidaiwa sio raia wa Tanzania na kejeli zingine ni vitu ambavyo vilimuumiza, ila amewasamehe wote waliomfanyia jambo hilo.
Waziri alisema hata hivyo pamoja na kuwasamehe wahusika, katu hatawasahau kwa vile walimpa wakati mgumu na kumnyima raha, kitu alichodai kitaendelea kubaki kichwani mwake hadi kifo.
Alisema wale walioanzisha na kueneza maneno hayo na waliomtusi, wasimuogope kwa sababu anafahamu siasa ni mchezo usio na simile na wenye kuhitaji uvumilivu mkubwa kitu alichoweza kukimudu na ndio maana amewasamehe kwa yote.
"Walionitusi na kunizushia kwamba mie sio raia na wengine kufikia hata kumhusisha mke wangu, wote nimewasamehe, ila kwa hakika sintowasahau, muhimu nataka kuwaambia wahusika wasiwe na hofu juu yangu yale yamepita kwani najua siasa ndivyo zilivyo," alisema Mkulo.
Alisema kama sio mambo ya siasa, kwa hakika angeweza kuwafungulia mashtaka na kudai fidia kubwa wahusika wote waliomchafua kipindi cha kura za maoni ndani ya CCM na hata kwenye uchaguzi mkuu uliompa ushindi wa kishindo yeye Mkulo na chama chake.
Waziri Mkulo, alisema kwa kuwa uchaguzi umeshapita kwa sasa yeye ni mbunge wa wakazi wote wa Jimbo la Kilosa na hivyo atawatumikia wananchi wote kwa ajili ya kuwaletea maendeleo, akiomba kupewa ushirikiano wa kutosha kufanikisha aliyopanga kwa miaka mitano ijayo.
Wakati wa mchakato wa kura za maoni, Waziri Mkulo alivumishiwa kuwa yeye si raia wa Tanzania na kikundi cha watu waliojiita Wazee wa Kilosa, ambao walikuja kurukwa na uongozi wa Baraza la Wazee la wilaya hiyo waliodai hawakumtuma mhusika aliyeanzisha chokochoko hizo.
Pia baada ya kushinda kiti hicho cha Ubunge kwa mara ya pili, baadhi ya watu walidaiwa kuapa kuwa asingekuwa miongoni mwa wateule wa Baraza Jipya la Mawaziri, kitu kilichoenda kinyume kutokana na Rais Jakaya Kikwete kumtangaza kuendelea kushikilia wizara hiyo ya Fedha.
Pia, amewataka wanachama wa CCM na wananchi wa Kilosa kwa ujumla, kuzika tofauti zao zilizosababishwa mchakato wa uchaguzi mkuu, ili kuweza kushikamana kuijenga wilaya na jimbo lao la Kilosa liweze kuwa mfano wa kuigwa nchini.
Akizungumza kwenye mapokezi na hafla ya kupongezwa kuteuliwa tena kuwa waziri, Waziri Mkulo, alisema kashfa alizokuwa akipewa akidaiwa sio raia wa Tanzania na kejeli zingine ni vitu ambavyo vilimuumiza, ila amewasamehe wote waliomfanyia jambo hilo.
Waziri alisema hata hivyo pamoja na kuwasamehe wahusika, katu hatawasahau kwa vile walimpa wakati mgumu na kumnyima raha, kitu alichodai kitaendelea kubaki kichwani mwake hadi kifo.
Alisema wale walioanzisha na kueneza maneno hayo na waliomtusi, wasimuogope kwa sababu anafahamu siasa ni mchezo usio na simile na wenye kuhitaji uvumilivu mkubwa kitu alichoweza kukimudu na ndio maana amewasamehe kwa yote.
"Walionitusi na kunizushia kwamba mie sio raia na wengine kufikia hata kumhusisha mke wangu, wote nimewasamehe, ila kwa hakika sintowasahau, muhimu nataka kuwaambia wahusika wasiwe na hofu juu yangu yale yamepita kwani najua siasa ndivyo zilivyo," alisema Mkulo.
Alisema kama sio mambo ya siasa, kwa hakika angeweza kuwafungulia mashtaka na kudai fidia kubwa wahusika wote waliomchafua kipindi cha kura za maoni ndani ya CCM na hata kwenye uchaguzi mkuu uliompa ushindi wa kishindo yeye Mkulo na chama chake.
Waziri Mkulo, alisema kwa kuwa uchaguzi umeshapita kwa sasa yeye ni mbunge wa wakazi wote wa Jimbo la Kilosa na hivyo atawatumikia wananchi wote kwa ajili ya kuwaletea maendeleo, akiomba kupewa ushirikiano wa kutosha kufanikisha aliyopanga kwa miaka mitano ijayo.
Wakati wa mchakato wa kura za maoni, Waziri Mkulo alivumishiwa kuwa yeye si raia wa Tanzania na kikundi cha watu waliojiita Wazee wa Kilosa, ambao walikuja kurukwa na uongozi wa Baraza la Wazee la wilaya hiyo waliodai hawakumtuma mhusika aliyeanzisha chokochoko hizo.
Pia baada ya kushinda kiti hicho cha Ubunge kwa mara ya pili, baadhi ya watu walidaiwa kuapa kuwa asingekuwa miongoni mwa wateule wa Baraza Jipya la Mawaziri, kitu kilichoenda kinyume kutokana na Rais Jakaya Kikwete kumtangaza kuendelea kushikilia wizara hiyo ya Fedha.
CCM Kilosa waambiana kweli, wapashana kuacha majungu
UONGOZI wa Chama cha Mapinduzi, CCM, Wilaya ya Kilosa, umewataka wanachama wake waache majungu na mifarakano na badala yake washikamane kukijenga chama chao pamoja na kuwapa ushirikiano wa kutosha viongozi walioshinda kwenye uchaguzi mkuu uliopita.
Viongozi wakuu wa chama hicho, Mwenyekiti Christopher Wegga na Katibu wake, Gervas Makoye walitoa wito huo kwa nyakati tofauti wakati wa mapokezi na sherehe ya kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Kilosa, Mustafa Mkulo kuchaguliwa tena kuwa Waziri wa Fedha na Uchumi zilizofanyika wilayani humo.
Makoye, aliyehutubia katika mkutano wa mapokezi ya Mkulo, yaliyofanyika kwenye uwanja wa CCM wilayani hapo, alisema kwa kuwa uchaguzi mkuu umeshamalizika ni vema wanachama wa chama hicho wakazika tofauti zao na kushirikiana na walioshinda kukijenga chama chao.
Katibu huyo, alisema pamoja na uchaguzi huo kumalizika na chama chao kuzoa ushindi wa kishindo, bado wapo baadhi ya wanachama wanaendeleza majungu na maneno kitu alichodai haisaidii.
Alisema wanaofanya hivyo ni wanachama waliozoea kupiga mizinga (kuomba hela) na kuwataka wenye tabia hiyo kubadilika kwa sababu chama hakitawavumilia.
"Wanachama wa CCM na wana Kilosa kwa ujumla acheni kupiga maneno, acheni majungu tushikamane kukijenga chama, tuwape ushirikiano wa kutosha viongozi walioshinda kwa sababu uchaguzi umeisha na hivyo tunapaswa kuvunja kambi zetu tuwe kitu kimoja," alisema.
Naye Mwenyekiti wa chama hicho, Christopher Wegga, akihutubia kwenye hafla ya kupongeza Waziri Mkulo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Babylon, alisema kuendeleza majungu na tofauti baada ya uchaguzi ni kukwaza maendeleo ya wilaya yao na kuwataka wananchi kushirikiana.
Alisema binafsi anampongeza Waziri Mkulo kwa kurejeshwa kwenye cheo chake cha uwaziri na kuwapongeza wazee walioandaa sherehe hiyo.
Sherehe hiyo ya kumpongeza Mkulo, iliandaliwa na Baraza la Wazee wa Kilosa, ambapo Mwenyekiti wake, Raphael Chayeka, alisema wamefurahishwa mno na kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kumrejesha Mbunge wao kwenye nafasi hiyo kwa imani Kilosa itapata maendeleo zaidi.
"Imani yetu ni kwamba cheo ulichopewa ni fahari kwetu wana Kilosa, wewe ni kama Rais wetu na tunaamini Kilosa itasonga mbele, tunakutakia kila la heri mna mafanikio," alisema Chayeka.
Waziri Mkulo, aliwashukuru wazee hao, wanachama na wananchi wa Kilosa kwa ujumla kwa kuonyesha imani yake kwake na kuwaahidi kuwasaidia kuwaletea maendeleo ili miaka mitano ijayo Jimbo hilo libadilike na litofautiane kuliko miaka mitano iliyopita.
Ila alisema jambo la muhimu ni wananchi bila kujali itikadi za vyama, dini, jinsia, kabila kushirikiana pamoja katika kupigania wilaya yao iondokane na vitendo vinavyorudisha nyuma maendeleo yao.
****
Na Badru Kimwaga, Aliyekuwa Kilosa
WAZIRI wa Fedha na Uchumi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kilosa, Mustafa Mkulo, amesema pamoja na kuwasamehe wale wote waliompakazia mabaya wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, bado hawezi kuwasahau hadi anaingia kaburini.
Pia, amewataka wanachama wa CCM na wananchi wa Kilosa kwa ujumla, kuzika tofauti zao zilizosababishwa mchakato wa uchaguzi mkuu, ili kuweza kushikamana kuijenga wilaya na jimbo lao la Kilosa liweze kuwa mfano wa kuigwa nchini.
Akizungumza kwenye mapokezi na hafla ya kupongezwa kuteuliwa tena kuwa waziri, Waziri Mkulo, alisema kashfa alizokuwa akipewa akidaiwa sio raia wa Tanzania na kejeli zingine ni vitu ambavyo vilimuumiza, ila amewasamehe wote waliomfanyia jambo hilo.
Waziri alisema hata hivyo pamoja na kuwasamehe wahusika, katu hatawasahau kwa vile walimpa wakati mgumu na kumnyima raha, kitu alichodai kitaendelea kubaki kichwani mwake hadi kifo.
Alisema wale walioanzisha na kueneza maneno hayo na waliomtusi, wasimuogope kwa sababu anafahamu siasa ni mchezo usio na simile na wenye kuhitaji uvumilivu mkubwa kitu alichoweza kukimudu na ndio maana amewasamehe kwa yote.
"Walionitusi na kunizushia kwamba mie sio raia na wengine kufikia hata kumhusisha mke wangu, wote nimewasamehe, ila kwa hakika sintowasahau, muhimu nataka kuwaambia wahusika wasiwe na hofu juu yangu yale yamepita kwani najua siasa ndivyo zilivyo," alisema Mkulo.
Alisema kama sio mambo ya siasa, kwa hakika angeweza kuwafungulia mashtaka na kudai fidia kubwa wahusika wote waliomchafua kipindi cha kura za maoni ndani ya CCM na hata kwenye uchaguzi mkuu uliompa ushindi wa kishindo yeye Mkulo na chama chake.
Waziri Mkulo, alisema kwa kuwa uchaguzi umeshapita kwa sasa yeye ni mbunge wa wakazi wote wa Jimbo la Kilosa na hivyo atawatumikia wananchi wote kwa ajili ya kuwaletea maendeleo, akiomba kupewa ushirikiano wa kutosha kufanikisha aliyopanga kwa miaka mitano ijayo.
Wakati wa mchakato wa kura za maoni, Waziri Mkulo alivumishiwa kuwa yeye si raia wa Tanzania na kikundi cha watu waliojiita Wazee wa Kilosa, ambao walikuja kurukwa na uongozi wa Baraza la Wazee la wilaya hiyo waliodai hawakumtuma mhusika aliyeanzisha chokochoko hizo.
Pia baada ya kushinda kiti hicho cha Ubunge kwa mara ya pili, baadhi ya watu walidaiwa kuapa kuwa asingekuwa miongoni mwa wateule wa Baraza Jipya la Mawaziri, kitu kilichoenda kinyume kutokana na Rais Jakaya Kikwete kumtangaza kuendelea kushikilia wizara hiyo ya Fedha.
Mwisho
Mwisho
Subscribe to:
Posts (Atom)