STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 12, 2013

Ni vita vya Barca na Bavarian, Chelsea waangukia kwa Basel


MABINGWA wapya wa Ujerumani, Bayern Munich imeangukia mikononi mwa Barcelona katika mechi za hatua na Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, huku wapinzani wao Borussia Dortmund wakipangiwa Real Madrid.
Aidha Chelsea ya Uingereza timu pekee inayoiwakilisha Uingereza imepangwa kukwaruzana na Basel ya Uswiss katika mechi za Nusu Fainali ya UEFA Ndogo, huku Benfica ya Ureno na Fenarbeche ya Uturuki zikipangwa pamoja.
Kupangwa kwa droo hiyo iliyozitenganisha timu hasimu kutoka nchi moja inamaanisha kwamba fainali za mwaka huu ya Ligi ya Ulaya itazikutanisha timu za taifa moja baada ya kipindi kirefu.
Mechi za mkondo wa kwanza zinatarajiwa kucheza kati ya Aprili 23 na 24 na zile za marudiano zitachezwa Aprili 30 na Mei Mosi kabla ya fainali kupigwa uwanja wa Wembley Uingereza Mei 25.
Kwa mechi za UEFA Ndogo mkondo wa kwanza utaanza Aprili 25 na za mkondo wa pili Mei 2 kabla ya fainali Mei 15.
Barcelona watakuwa wageni wa wana fainali za mwaka jana katia mkondo wa kwanza kabla ya kurudiana wiki moja baadaye kwenye dimba lake la Camp Nou, kadhalika Wahispania wengine Real Madrid watasafiri pia Ujerumani kuvaana na wenyeji wao Dortmund kabla ya kurejea nyumbani katika mechi ya mkondo wa pili.
Kwenye mechi za UEFA Ndogo Chelsea wataanzia ugenini sawa na itakavyokuwa kwa Benfica na kurudiana na wapinzani wao kwenye viwanja vyao vya nyumbani dhidi ya Basel na Fenerbeche.

Kivumbi cha VPL kuendelea wikiendi, Simba, Yanga, Azam kuvuna nini?




Na Boniface Wambura
Ligi Kuu ya Vodacom inaendelea kesho (Aprili 13 mwaka huu) kwa mechi mbili zitakazochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, na Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Yanga itakuwa mwenyeji wa Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa wakati Uwanja wa Sokoine utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Tanzania Prisons na Ruvu Shooting.

Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Aprili 14 mwaka huu) kwa mechi kati ya wenyeji Azam na Simba. Mechi hiyo namba 155 itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika hatua nyingine, Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Shelisheli kuchezesha mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho kati ya Azam na AS FAR ya Morocco itakayofanyika Aprili 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Waamuzi hao ni Emile Fred atakayepuliza filimbi akisaidiwa na Steve Maire na Jean Ernesta. Mwamuzi wa mezani (fourth official) atakuwa Jean Claude Labrossa. Kamishna wa mechi hiyo ni Abbas Sendyowa kutoka Uganda.

Wakati huo huo, CAF imemteua Mtanzania Alfred Lwiza kuwa Kamishna wa mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho kati ya Liga Muculmana ya Msumbiji na Wydad Casablanca ya Morocco.

Mechi hiyo itakayochezwa kati ya Aprili 19,20 au 21 mwaka huu nchini Msumbiji itachezeshwa na waamuzi kutoka Zimbabwe wakiongozwa na Ruzive Ruzive.


UJUMBE WA FIFA KUWASILI APRILI 15




Na Boniface Wambura
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kuwatangazia wadau wa mpira wa miguu kuwa ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utawasili nchini Jumatatu (Aprili 15 mwaka huu) kwa ajili ya kushughulikia mchakato wa uchaguzi mkuu wa TFF.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka FIFA, ujumbe huo utaongozwa na Mkuu wa Idara ya Uanachama ya FIFA, Primo Covarro na utafanya kazi kwa siku tatu kuanzia siku ya ujio na kuondoka Aprili 18 mwaka huu.

Ukiwa nchini, ujumbe huo utakutana na wagombea uongozi walioathiriwa na uamuzi wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ambao waliomba mashauri yao yaangaliwe upya, wagombea ambao walikata rufani FIFA, Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Kamati ya Rufani na Sekretarieti ya TFF.

Wajumbe hao wangependa kukutana na waziri anayehusika na michezo, hivyo TFF imeiandikia Wizara ikipendekeza kuwa ujumbe huo ukutane na Waziri na wakuu wengine wa michezo Aprili 16 mwaka huu 2013 kabla ya kuanza kazi zao.

Wagombea watakaosikilizwa na ujumbe huo wa FIFA ni:
1.   Farid Salim Mbaraka Nahdi: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alienguliwa na Kamati ya Uchaguzi na baadaye rufani yake kwa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kutupwa na hali kadhalika ombi lake la kutaka shauri lake liangaliwe upya, kukataliwa.

2.   Elliud Peter Mvella: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na kukata rufani Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kabla ya maombi yake ya kutaka shauri lake kuangaliwa upya, kukataliwa.


3.   Mbasha Matutu: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi na kukata rufani ambayo pia ilitupwa kabla ya kuomba shauri lake liangaliwe upya, ombi ambalo lilikataliwa.

4.   Hamad Yahya: Mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa Bodi ya Ligi ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na kuondolewa. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ikatupa ombi lake.

5.   Jamal Emily Malinzi: Mgombea wa nafasi ya urais wa TFF ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, hivyo kuondolewa kwenye mchakato. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini likakataliwa. Hata hivyo, alikuwa ameshakata rufani FIFA.

6.   Michael Wambura: Mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais wa TFF ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na rufani yake kukataliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF. Hakuomba shauri lake liangaliwe upya, lakini alikata rufani FIFA.

Shirikisho linawaomba wote waliotajwa hapo juu kujiandaa kwa utetezi na maelezo ya kutosha na kwamba barua za kuwaita zinafuata. (Orodha ya waathiriwa na programu ya ujumbe wa FIFA imeambatanishwa)

Kigogo Yanga matatani, kisa...!

Makamui Mwenyekiti wa Yanga, Clement  Sanga
MAKAMU Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Clement Sanga, anatarajiwa kufikishwa mbele ya Kamati ya Nidhamu kufuatia kauli aliyoitoa hivi karibuni kuwa timu yao inayoongoza kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwamba inahujumiwa na ndiyo maana mechi yao dhidi ya JKT Oljoro imesogezwa mbele na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Awali, mechi hiyo ya Yanga dhidi ya Oljoro ilipangwa kufanyika juzi (Jumatano ya Aprili 10) lakini sasa itachezwa kesho Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema kuwa kauli kama za Sanga zinachangia kujenga chuki  zisizokuwa na sababu kati ya shirikisho hilo na mashabiki wa soka nchini.
Kwa sababu hiyo, Osiah alisema kuwa Sanga atatakiwa athibitishe ni kwa namna gani Yanga inahujumiwa baada ya kuwapo kwa mabadiliko hayo ya ratiba ambayo yalizihusu pia timu nyingine zinazoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara, zikiwamo za Simba na Azam ambazo sasa zitacheza Jumapili.
Osiah alisema kuwa anashangaa kusikia madai ya Sanga kuwa klabu hazijashirikishwa katika kufanya marekebisho hayo wakati ukweli ni kwamba klabu hizo ziliwakilishwa na viongozi wao walioko kwenye kamati ya ligi na timu yao ina mjumbe kwenye kamati hiyo.
Katibu huyo wa TFF alisema kuwa viongozi wa klabu walielezwa katika kikao kilichofanyika mapema kabla ya ligi kuanza kwamba kutakuwa na 'Super Week' katika hatua ya mwisho wa ligi ambayo itatekelezwa kupitia nafasi itakayopatikana katika kituo cha televisheni ya kulipia cha Afrika Kusini cha  Super Sport.
"Mnapotafuta wadhamini kuna wakati ni lazima mjitoe mhanga... na kuonekana kwetu kupitia Super Sport kumesaidia kuleta wadhamini wengi ambao tayari wamevutiwa na ligi yetu," alisema Osiah.
Katika mahojiano yake na vyombo vya habari hivi karibuni, Sanga alisema kuwa wao walikuwa tayari wameshaiandaa timu yao na kwa mabadiliko hayo ambayo hawaoni faida yake zaidi ya kuwapunguzia mashabiki viwanjani yamewapa hasara kubwa itokanayo na kuendelea kuiweka timu kambini.
Aliyewahi kuwa Afisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu na Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage waliwahi kuadhibiwa na TFF baada ya kukutwa na hatia ya kutoa kauli ambazo baadaye walishindwa kuzithibitisha.


Chanzo:NIPASHE

Matapeli wamhujumu rais wa IBF nchini

Rais wa IBF/USBA, Onesmo Ngowi
MATAPELI wa kimataifa wanaoingilia barua pepe na akaunti nyingine za watu mbalimbali wamemvamia rais wa hapa nchini wa Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF/USBA), Onesmo Ngowi na kutumia jina lake kwa nia ya kuwatapeli fedha watu mbalimbali anaojuana nao.
Jina la Ngowi ambaye pia ni Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, (TPBC), limetumiwa na matapeli hao kutuma ujumbe wa barua pepe kwa watu mbalimbali anaowasiliana nao, wahusika wakijifanya ni Ngowi na kuomba msaada wa fedha.
Katika barua pepe mojawapo iliyotumwa kwa mwandishi, inaeleza Ngowi alikuwa akiomba msaada wa Euro 2,950 (Sh. milioni 6.2) ili kumuwezesha kujinasua na tatizo lililomkumba akiwa nchini Ugiriki; jambo ambalo Ngowi amelilaani na kuwatahadharisha watu anaojuana nao kuwa wawe macho na matapeli hao.
"Matapeli wanatuma akaunti yangu (ya email) na kuomba pesa kwa watu mbalimbali... mimi siko Ugiriki na wala sijamuomba mtu fedha. Tafadhali naomba usijibu meseji hizo," alisema Ngowi kuelezea utapeli huo ambao umeshawakuta pia watu wengi.

TFF ipo tayari kukutana na Nsa Job utetezi wa Rushwa

Nsa Job (kulia)
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema liko tayari wakati wowote kukutana na mchezaji wa Coastal Union ya jijini Tanga, Nsa Job, ambaye alikiri hadharani kuwa aliwahi kupokea rushwa ya Sh.milioni mbili kutoka kwa kiongozi mmoja wa timu vigogo nchini ili asifunge magoli.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema katika barua yao waliyomuandikia mshambuliaji huyo hawakumpa siku maalumu lakini endapo nyota huyo atachelewa kujisalimisha atakumbushwa kabla ya kuchukuliwa hatua kupitia kamati husika.
"Tuliiweka wazi lakini tutamuandikia barua nyingine ya kumkumbusha na itakayofuata itakuwa imetoa muda fulani, ila tunaamini atatoa ushirikiano kama alivyokaririwa na gazeti (la NIPASHE)," alisema Katibu mkuu huyo.
Osiah alisema TFF inaamini mchezaji huyo atatoa ushirikiano kama alivyolieleza gazeti la NIPASHE lilipozungumza naye mapema wiki hii.
Aliongeza kwamba wanaamini akiwa wazi mhusika wa tuhuma hizo atajulikana na hatimaye adhabu itatolewa na kukomesha suala la rushwa katika soka la nchini.
Osiah alisema pia tayari Mkurugenzi wa Vipindi wa kituo cha redio cha Clouds ameahidi kuwapa ushirikiano katika kupata nakala ya kipindi kilichorushwa mahojiano na Nsa ambacho kilifanyika Aprili 3 mwaka huu.
Nsa alizungumza katika mahojiano na kituo cha redio hiyo akisema aliwahi kupokea rushwa lakini aliifungia timu yake goli pekee la ushindi.
Hata hivyo, hadharani, hakuitaja timu aliyokuwa anaichezea wakati huo wala timu aliyoifunga na wala jina la kiongozi aliyemhonga, ambaye alisema alianza kumsumbua kudai fedha zake pale “alipowatungua”.
Nyota huyo ambaye kwa sasa anafanya mazoezi binafsi baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti nchini India aliwahi kuchezea timu za Simba, Yanga, Moro United, Azam, Villa Squad na sasa Coastal Union zote zinazoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Nsa aliiambia NIPASHE kwamba atatoa ushirikiano kwa TFF kama alivyotakiwa na kwa sasa anajiandaa kwenda kukutana nao.
Alisema pia alipokea barua hiyo tangu wiki iliyopita na atafanya kila linalowezekana ili kutekeleza kile atakachoambiwa na wajumbe wa kamati hiyo.


CHANZO:NIPASHE.

Azam yamalizana na wachezaji wake iliyowasimamia kwa rushwa

 
Add caption



KLABU ya soka ya Azam ambayo Jumapili inatarajiwa kuvaana na Simba, imemalizana na wachezaji wake wanne iliyokuwa imewasimamisha kwa tuhuma za Rushwa kabla ya kusafishwa na TAKUKURU.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mtandao wa klabu ya Azam, imesema wachezaji wote wanne waliosimamishwa kupisha uchunguzi wa tuhuma za rushwa dhidi yao wameripoti kambini tayari kuikabili Simba SC siku ya jumapili

Kurejea kwa wachezaji hao kunamaliza mgogoro uliokuwepo na kudumu kwa takribani miezi mitano kufuatia shutuma za rushwa ambazo zilipelekwa takukuru kuchunguzwa ili kujua ukweli na uongozi wa Azam FC unaishukuru takukuru kwa kazi nzuri ambapo imegundulika kuwa wachezaji hao hawakuhusika na hivyo kusafishwa na chombo hicho chenye mamlaka ya kuchunguza tuhuma za rushwa.
Wachezaji hao wote wanatarajiwa kuwemo kwenye mchezo wa Jumapili dhidi ya Simba SC ikiwa mwalimu ataona inafaa na wapo katika hali nzuri kuweza kucheza.
Mchezo huo wa jumapili ni muhimu sana kwa Azam FC kwani ikishinda itaizidi Simba SC pointi 14 huku simba ikisaliwa na michezo minne na hivyo kumaanisha kuwa Kagera Sugar atabaki kuwa mpinzani pekee wa Azam FC katika kuwania nafasi ya pili.

Thursday, April 11, 2013

Chelsea yafa ugenini lakini yatinga nusu fainali UEFA ndogo


Wachezaji Chelsea wakimpongeza Torres kwa kufunga bao akuongoza
LICHA ya kupokea kipigo cha mabao 3-2 kutoka kwa wenyeji wao Rubin Kazan ya Russia, Chelsea ya Uingereza imekuwa timu ya kwanza muda mfupi uliuopita kufuzu hatua ya nusu fainali ya UEFA Ndogo.
Chelsea imefanikiwa kufuzu hatua hiyo kutokana na ushindi mnono wa mabao 3-1 iliyopata katika mechi yao ya wali iliyochezwa 'darajani' mjini London hivyo kupenya kwa jumla ya mabao 5-4.
Fernando Torres aliiandikia Chelsea bao la kuongoza dakika chache baada ya kuanza kwa pambano hilo kwa kumalizia kazi nzuri ya Frank Lampard, goli lililodumu hadi wakati wa mapumziko kabla ya wenyeji kusawazisha dakika ya 51  Marcano.
Victor Moses mmopja wa wafungaji wa mabao katika pambano la wiki iliyopita baina ya timu hizo aliiongezea Chelsea bao la pili dakika nne baadaye kabla ya wenyeji kusawazisha katika dakika ya 62 kupitia kwa Gokdeniz Karadeniz kabla ya Bibras Natcho kufunga bao la ushindi kwa mkwaju wa penati dakika ya 75.
Michezo mingine ya ligi inatarajiwa kuchezwa muda mfupi ujao kwenye viwanja vingine vitatu tofauti kupata timu tatu za kuungana na Chelsea katika hatua hiyo ya nusu fainali.

Jahazi la African Lyon lazidi kuzama VPL


Kikosi cha African Lyon kilichozamishwa leo jioni
JAHAZI la timu ya African Lyon jioni ya leo limeendelea kuzama baada ya kubamizwa mabao 3-1 na Azam katika pambano pekee lililochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, jijini Dar es Salaam.
Kipigo hicho kimezidi kuifanya Lyon kusalia nafasi nafasi ya 13 ikijiweka pabaya katika kuepuka kushuka daraja tofauti na tambo zilizokuwa zikitolewa awali kuwa ni vigumu kwao kushuka daraja, kwani wamesaliwa na pointi 19 tu
Mabao yalioinyong'onyesha Lyon yalitupiwa kimiani na nyota wa Azam, Mcha Khamis ‘Vialli’ katikam dakika ya 9 kabla ya mfungaji kinara wa mabao wa VPL, Kipre Tchetche kuongeza mengine mawili katika dakika ya 28 na 61.
Bao pekee la Lyon lilifungwa na Adam Kingwande katika kipindi cha kwanza na kufanya wakati wa mapumziko matokeo yawe mabao 2-1.


                                          P      W     D     L     F      A     GD     PTS
    1.  Young Africans         21     15     4     2    37     12    +25     49
    2. Azam                         22     14     4     4    39     17     +22     46   
    3. Kagera Sugar            22     10     7     5    25     18     +7      37    
    4. Simba                        21     9      8     4     30     19    +11     35
    5. Mtibwa Sugar            23     8      9     6     26     24     +2      33  
    6. Coastal Union            22     8     8      6     23     20     +3     32   
    7.  Ruvu Shooting           22     8     6     8     21     19     +2     30    
    8.  JKT Oljoro FC            22     7     7     8     22     24     -2     28    
    9. JKT Mgambo              22     7     3     12     14     22     -8     24
    10.Tanzania Prisons      23      5     8     10     12     21     -9     23   
    11.Ruvu Stars                21     6     4     11     19     34     -15     22
    12. Toto Africans           24     4     10     10    22     32     -10     22
    13.  African Lyon            23     5     4     14     16     35     -19     19
     14. Polisi Morogoro      23     3     10     10     11     21     -10     19   
 

Ruvu Shooting yaitahadharisha TFF Kamati za Ushindi zinazoibuka sasa Ligi Kuu

IKIWA safarini mkoani Mbeya kwa ajili ya pambano lao lijalo dhidi ya wenyeji wao, Prisons ya Mbeya, uongozi wa timu ya Ruvu Shooting umeliomba Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kuwa makini na Kamati ya Ushindi za klabu mbalimbali zilizoundwa wakati Ligi Kuu Tanzania Bara ikielekea ukingoni.
Uongozi huo wa Ruvu umedai kuwa, kamati hizo huenda zikatumika vibaya katika upangaji na hulazimishaji wa matokeo viwanjani kutokana na ukweli kamati hizo mara nyingi huusisha viongozi wa FA mkoa na hata ofisi za wakuu wa mikoa husika wanaoweza kutumia vibaya nafasi zao kuzibeba timu zao hasa zikiwa kwao.
Akizungumza na MICHARAZO hivi punde, Msemaji wa klabu hiyo, Masau Bwire alisema kamati ya kusaka ushindi kwa timu za ligi kuu, siyo tatizo ila hofu yao namna zinavyoundwa wakati huu ligi ikielekea ukingoni na baadhi yao ni zile timu ambazo zipo katika hali mbaya kwenye ligi hiyo.
Bwire alisema, ingekuw vyema wakafuatilia kwa ukaribu mechi za mwisho za ligi hiyo ili kuepusha hujuma kwa timu nyingine, ili ligi imalizike salama kama ilivyoanza.
"Hatupingi kuundwa kwa hizi kamati kwa baadhi ya timu, lakini zinatutia hofu kwa namna zinavyoundwa kila mara timu zikiwa katika nafasi mbaya na hasa ligi ikielekea ukingoni, mbaya zaidio hujumuisha watu wenye nyadhifa ambazo wanaweza kutumika kuwatisha au kuwalazimisha waamuzi kutengeneza matokeo ya kuzibeba timu hizo," alisema Bwire.
Alisema kwa vile vyama vya mikoa (FA) ni wanachama wa TFF na majukumu yao ni kuhakikisha utekelezwaji wa sheria 17 za soka zinatumika uwanjani, hadhani ni sahihi nao kuingizwa kwenye kamati hizo kwani wanaweza kulaumiwa inapotokea dosari kwenye mechi ndani ya mikoa yao.
Aliongeza kuwa ni vyema kamati hizo zingekuwa zikiundwa mapema na kufanya kazi kuzisaidia timu zao kuliko sasa ambako imekuwa kama fasheni na kuleta hisia mbaya hasa wakati huu watanzania wakiwa na hisia kali juu ya vitendoi vya rushwa michezoni.
Juu ya pambano lao lijalo Bwire alisema kikosi chao kipo safarini lakini wakiwa na morali wa kupata ushindi mjini Mbeya, cha muhimu akiiomba TFF kuhakikisha wanausimamia kwa ukamilifu mchzeo huo ili kusiwepo na matukio kama waliyokutana nao jana kwenye pambano lao na Polisi Moro lililoisha kwa suluhu ya 0-0.

Ecuador yaingia Top 10 ya FIFA, England yaporomoka, Tanzania yapaa



NCHI ya Ecuador imeweka hostoria kwa kufanikiwa kuingia kwa mara ya kwanza kwenye Top 10 ya orodha timu bora duniani kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA.
Kwa mujibu wa orodha iliyotangazwa na FIFA, Ecuador imeshika nafasi hiyo kutokana na ushindi wa mechi mbili mfululizo walizocheza ndani ya mwezi uliopita.
Mechi hizo ni pamoja na ile ya kirafiki ya kimataifa dhidio ya El Salvador waliposhinda mabao 5-0 na ile ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Paguguay waliowalaza mabao 4-1.
Wakati Ecuador wakitinga hatua hiyo, Russia wamejikuta wakiporomoka, huku Croatia wakitinga hadi nafasi ya nne katika msimamo wa orodha hiyo mpya ya FIFA baada ya kushinda mechi zake mbili dhidi ya Wales na Serbia.
Orodha hiyo mpya ya FIFA inaoonyesha timu ya Hispania imeendelea kuongoza msimamo ikifuatiwa na Ujerumani kisha Argentina na Ureno ikikamilisha orodha ya timu Tano Bora ikitoka nafasi ya saba.
Colombia imeendelea kusalia kwenye nafasi ya sita huku England ikifuatia ikiporomoka kwa nafasi tatu, Italia imeshika nafasi ya nane baada ya kushuka kwa nafasi tatu na Uholanzi walioshuka nafasi moja wameshika nafasi ya tisa mbele ya Ecuador.
Katika orodha ya nchi za Afrika, Ivory Coast imeendelea kuongoza ikiwa ipo nafasi ya 12 duniani, ikifuatiwa na majirani zao Ghana walipo nafasi ya 22 duniani ikishika nafasi ya pili Afrika.
Zilizopo kwenye Top 10 ni Mali, Nigeria, Algeria, Tunisia, Zambia, Burkina Faso, Guinea ya Ikweta na Cameroon. Kwa ukanda wa CECAFA, Uganda imeendelea kuwa kinara ikifuatiwa na Tanzania iliyopanda kwa nafasi tatu toka 119 duniani hadi ya 116 huku Afrika ikiwa nafasi ya 33.

Pan Africans kwafukuta moto, IDFA yaamua kuingilia kati

Jengo la makao makuu ya klabu ya Pan African
WANACHAMA wa klabu ya Pan African wameushtaki uongozi wao kwa Chama cha Soka Wilaya ya Ilala (IDFA) kwa madai ya kukiuka katiba wakishindwa kuitisha mikutano tangu walipoingia madarakani mwaka 2009.
Kwa mujibu wa barua yao kwenda ya Machi 30, 2012 kwenda kwa Katibu Mkuu wa IDFA, wanachama hao wa Pan wanadai tangu uongozi wao ulipoingia madarakani Aprili 18, 2009 hawajaitisha mkutano wowote wala kushirikisha wanachama katika baadhi ya maamuzi waliyoamua kuyafanya.
Taarifa hiyo iliyosainiwa na mmoja wa wanachama wa klabu hiyo kwa niaba ya wenzake, Abbas Ally (kadi namba 0075), imedai mbali kutoshirikishwa katika maamuzi yanayofanywa na uongozi huo, pia klabu imekuwa haina ofisi.
"Japo jingine linalotutisha ni klabu kutokuwa na ofisi wake tuna jengo letu ambalo uongozi umelipangisha lote kiasi sisi wanachama kukosa mahali pa kupata huduma za klabu au kupata taarifa na kulipia ada za uanachama," taarifa hiyo ilisema.
Iliongeza kwa kuiomba IDFA kama mlezi wa klabu za Ilala kuushinikiza uongozi kuitisha mkutano wa wanachama na wao (IDFA) wakiwepo kama shahidi juu ya uongozi lazima uwasilishe mambo manne kwao siku hiyo.
Moja na mambo hayo ni ripoti ya mapato na matumizi kwa kipindi chote walichokaa madarakani na ukaguzi juu ya mapato hayo, taarifa ya sababu zilizoufanya uongozi huo kupangisha jengo lote kiasi cha kukosa ofisi na  mengine.
MICHARAZO liliutafuta uongozi wa Pan kufafanua madai hayo, ambapo  Makamu Mwenyekiti, Ally Hemed alisema asingeweza kuzungumzia suala hilo badala yake akataka atafutwe Katibu Mkuu wake Saad Mateo ambaye simu zake hazikupatikana hewani.
Hata hivyo Katibu Mkuu wa IDFA, Daud Kanuti ilithibitisha juu ya kupokea barua ya wanachama hao wa Pan na kudai kamati yao ya Utendaji ilishakutana na kuamua kuziita pande mbili zinazosigana kukaa meza moja kuzungumza.
Kanuti alisema kikao hicho kitafanyika Jumamosi ili kuzisikiliza pande zote mbili kwa kuipitia katiba ya klabu hiyo kisha kutoa maamuzi yatakayoleta suluhu ndani ya klabu hiyo kongwe nchini.

Lyon kuendeleza maajabu leo mbele ya Azam?


Kikosi cha African Lyon

Azam Fc
TIMU ya soka ya Azam leo inatarajiwa kushuka dimbani kuvaana na African Lyon, inayopigana kuepuka kushuka daraja katika pambano pekee litakalochezwa kwenye uwanja wa Chamazi.
Lyon ambayo katika mechi yake iliyopita ilifanya maajabu kwa kuilaza Coastal Union na kuondoka mkiani, hali inayofanya mashabiki kutaka kuona kama itaendeleza ubabe huo au la.
Pambano na kwamba Lyon hiyo ni mechi yake muhimu, lakini pia kwa Azam ni muhimu zaidi katika mbio zake za kutaka kuwaengua Yanga kileleni na kuweka rekodi ya kuwa mabingwa wapya nchini.
Azam ipo nafasi ya pili nyuma ya Yanga ikiwa na pointi 43, sita zaidi ya vinara hao na iwapo itashinda itapunguza pengo hilo hadi kuwa tatu kabla ya kuvaana na Simba Jumapili uwanja wa Taifa.
Makocha wa timu hizo mbili zenye upinzani wa jadi kutoka wilaya ya Temeke, wametamba kuhakikisha wanaibuka na ushindi ili kutimiza malengo yao tofauti.
Kocha wa Azam, Muingereza Stewart Hall, alinukuliwa akisema wataingia uwanjani bila kuidharau Lyon licha ya kusaka ushindi ili kujiweka pazuri katika harakati zao za ubingwa.
Naye kocha wa Lyon, Charles Otieno, alitamba kwamba wamejipanga kushinda mchezo wa leo ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kuepuka kurudi Ligi Daraja la Kwanza.
Kikosi cha Lyon mpaka sasa kimejikusanyia pointi 19 wakilingana na Polisi Moro wanaoshikilia mkia kwa tofauti ya uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Ili kujua nani atakayekuwa ametimiza malengo ni kusubiri mpaka baada ya dakika 90 za pambano hilo pekee kwa siku ya leo.

Messi aivusha Barca nusu fainali, Juve wakiona cha moto nyumbani

 
Pedro akishangilia bao lake la kusawazisha dhidi ya PSG jana usiku

NYOTA wa kimataifa wa Argentina, Lionel Messi usiku wa kuamkia leo alionyesha ni namna gani alivyo chachu ya mafanikio ya timu yake baada ya kuiwezesha Barcelona kufuzu nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Messi aliyeingia kipindi cha pili wakati wenyeji Barca wakiwa nyuma kwa bao 1-0, alibadilisha taswira nzima ya mchezo huo uliochezwa uwanja wa Camp Nou na kuipa timu yake sare ya bao 1-1 dhidi ya wageni PSG ya Ufaransa.

PSG walitangulia kupata bao kupitia Javier Pastore na kuwapa wakati mgumu wenyeji waliokuwa wameelemewa licha ya  Xavi Hernendez kuweka rekodi ya kupiga pasi sahihi kwa asilimia 100 katika pambano hilo.

Mara baada ya kuingia uwanjani Messi aliifanya PSG kupoteza mwelekeo na yeye kutumia nafasi hiyo kutoa pasi murua kwa David Villa ambaye alimpasia Pedro aliyefunga bao la kusawazisha dakika ya 71.

Hata hivyo Barca wamefanikiwa kufuzu kwa sheria ya bao la ugenini baada ya kupata sare ya mabao 2-2 ugenini wiki iliyopita na hivyo kufanya matokeo ya jumla kuwa mabao 3-3 na kuiondosha PSG kwenye michuano hiyo.

Katika pambano jingine ambalo lilichezwa mjini Turin, Italia wenyeji na vinara wa ligi kuu ya Seria A, Juventus walishindwa kutamba nyumbani baada ya kunyukwa mabao 2-0 na Bayern Munich ya Ujerumani.

Ushindi huo wa Munich umeifanya timu hiyo kufuzu nusu fainali ikiungana na timu za Real Madrid, Borussia Dortmund na Barcelona kwa jumla ya mabao 4-0.

Katika mechi yao iliyopita iliyochezwa nchini Ujerumani, Juve walilala kwa mabao 2-0.

Bayern ilipata ushindi huo ugenini kupitia mabao yaMario Mandzukic aliyefunga katika dakika ya 64 akimalizia mpira wa faulo uliopigwa na kiungo Bastian Schweinsteiger kabla ya Claudio Pizarro kufuinga bao la pili dakika ya 90.

Hatma ya timu zipi zitakazokutana katika hatua hiyo inatarajiwa kufahamika kesho Ijumaa itakapotangazwa droo ndogo huku kukiwa na hofu Wahispania na Wajerumani waliofuzu hatua hiyo kukutana wenyewe kwa wenyewe.


Golden Bush Fc haikamatiki Ligi ya TFF-Kinondoni

TIMU ya soka ya Golden Bush imezidi kuchanja mbuga kwenye Ligi Daraja la Nne wilaya ya Kinondoni, baada ya juzi kupata ushindi wa nne mfululizo  kwa kuwalaza TP Afrika kwa mabao 3-1 katika mfululizo wa ligi hiyo.
Ushindi huo wa juzi katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Itihad, Mwananyamala jijini Dar es Salaam limeifanya Golden Bush kuongoza msimamo wa kundi lake na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya pili ya michuano hiyo ninayochezwa kwenye viwanja mbaliumbali wilayani humo.
Golden Bush inayonolewa na nyota wa zamani wa soka nchini, Shija Katina na Madaraka Seleman, ilipata ushindi huo wa nne kupitia mabao yaliyofungwa na wachezaji wake nyota, Kenan Mwashinde aliyefunga mawili na Mrisho aliyefunga bao jingine.
Kabla ya ushindi huo wa juzi, Golden Bush ilianza ligi hiyo kwa kishindo kwa kuipa kipigo kitakatifu timu za Victoria ya Kijitonyama kwa kuwatandika mabao 6-1 kabla ya kuilazaa Makumbusho Talents kwa magoli 3-1 na kuizima Katabazi  na kufanya waongoze msimamo wa kundi lao wakiwa na pointi 12.

Wednesday, April 10, 2013

Prisons yazinduka, Toto, Mtibwa ngoma nzito

Kikosi cha Prisons Mbeya

WAKATI timu ya Toto African ikijitutumua mjini Manungu na kulazimisha sare ya mabao 2-2, vijana wa maafande wa Prisons Mbeya imezinduka nyumbani kwa kuicharaza Mgambo JKT ya Tanga kwa bao 1-0,
Toto ambayo kupitia kocha wake, John Tegete waliwatupia lawama waamuzi wa pambano hilo kwa kuyakataa mabao yao mawili na kisha wenyeji kupewa penati ya kitatanishi na kufanya Mtibwa kuongoza mabao 2-0 hadi wakati wa mapumziko.
Tegete alisema walifanikiwa kurejesha mabao hayo kipindi cha pili na kuambulia pointi moja iliyowafanya waendelee harakati zao za kujinusuru kushuka daraja.
Nao Prisons ikicheza nyumbani na kuilaza Mgambo kwa bao 1-0 katika pambano jingine la Ligi Kuu Tanzania Bara lililochezwa kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya, huku maafande wa Polisi Morogoro walishindwa kutamba nyumbani kwa kulazimishwa suluhu na Ruvu Shooting  kwenye uwanja wa Jamhuri.
Matokeo ya ya mechi hizo yameifanya Prisons kuchupa hadi nafasi ya 10 ya msimamo wakiishusha JKT Ruvu, huku Toto na Polisi wameendelea kusalia katika nafasi zao za awali, ila Mtibwa imeiporomosha Coastal Union kwa kufikisha pointi 33.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea kesho kwa pambano moja tu litakalowakutanisha wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Azama itakayoikaribisha African Lyon.
Mechi hiyo itachezwa kwenye uwanja wa Chamazi ambapo matokeo yoyote kwa Azam itaelekea kupunguza pengo lake la pointi dhidi ya vinara wa ligi hiyo Yanga.
 1.  Young Africans     21     15     4     2     37     12     +25    49 
2.  Azam                     21     13     4     4     36     16     +20    43    
3 . Kagera Sugar         22     10     7     5     25     18     +7      37     
4.  Simba                     21      9     8     4     30     19     +11     35
5.  Mtibwa Sugar         23      8     9     6     26     24     +2      33   
6. Coastal Union          22      8     8     6     23     20     +3     32    
7.  Ruvu Shooting        22      8     6     8     21     19     +2     30     
8.  JKT Oljoro FC        22      7     7     8     22     24      -2     28     
9. JKT Mgambo           22      7     3    12    14     22      -8     24
10.Tanzania Prisons     23      5     8     10     12     21     -9    23          11.Ruvu Stars               21     6     4     11     19     34     -15   22
12. Toto Africans          24    4    10     10     22     32     -10   22
13.  African Lyon         22     5     4     13     15     32     -17   19
14. Polisi Morogoro      23     3     10   10     11     21     -10   19

            

Rungu la TFF yazikong'ota Villa Squad, Kocha Rhino Rangers


Na Boniface Wambura
KAMATI ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imempiga faini ya sh. 400,000 na kumfungia mechi sita Kocha wa Rhino Rangers, Renatus Shija kwa kushiriki vitendo vinavyoashiria imani za ushirikina na kumdhihaki mwamuzi kwenye mechi za Ligi Daraja la Kwanza (FDL).

Adhabu hizo zimetolewa kwa mujibu wa kifungu cha 31(1)(a) na (b) cha Kanuni za FDL ambapo Kocha huyo aliyeipandisha daraja Rhino Rangers kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) alifanya vitendo hivyo kwenye mechi mbili tofauti.

Mechi hizo ni kati ya Kanembwa JKT na Rhino Rangers iliyochezwa Februari 23 mwaka huu Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma, na ile kati ya Rhino Rangers na Morani iliyochezwa Machi 17 mwaka huu Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Pia klabu ya Rhino Rangers imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na Polisi Wanajeshi- MP kuwapiga walinzi milangoni kwenye mechi hiyo dhidi ya Kanembwa JKT ili kupisha washabiki wa timu hiyo waingie bure uwanjani.

Mchezaji wa timu ya Pamba ya Mwanza, Leonard Nahole amepigwa faini ya sh. 200,000 na kufungiwa mechi nne baada ya kumrushia chupa ya maji mwamuzi kwa madai amependelea kwenye mechi dhidi ya Polisi Tabora iliyochezwa Machi 16 mwaka huu.

Nao wachezaji Joseph Mapalala, Yohana Mirobo, Noel Makunja, Mkome Pastory na Rudenzi Kilinga wa Polisi Mara wamepigwa faini ya sh. 200,000 kila mmoja na kufungiwa mechi tatu kwa kufanya vitendo vinavyoshiria ushirikina na kumkimbiza mwamuzi kwenye mechi dhidi ya Morani iliyochezwa Machi 9 mwaka huu. Adhabu za wachezaji hao ni kwa mujibu wa kifungu cha 27(1)(g) cha Kanuni za FDL.

Klabu ya Villa Squad imepigwa faini ya sh. 150,000 kwa kuchelewa uwanjani kwenye mechi yake dhidi ya Ashanti United wakati Majimaji imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na washabiki wake kufanya vurugu kwenye mechi dhidi ya Mbeya City iliyochezwa Uwanja wa Majimaji.

Vilevile Msimamizi wa Uwanja wa Majimaji aliyetambulika kwa jina moja la Mapunda aliwatukana waamuzi kwenye mechi hiyo, na suala lake litafikishwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF kwa ajili ya hatua za kinidhamu.

Pia uongozi wa Uwanja wa Mafinga unaotumiwa na timu ya daraja la kwanza ya Kurugenzi umetakiwa kuufanyia marekebisho, vinginevyo hautatumika kwa mechi za FDL msimu ujao.

MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kesho (Aprili 11 mwaka huu) litakuwa na Mkutano na Waandishi wa Habari. Mkutano huo utafanyika saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF.

Barca, PSG ni kufa ama kupona leo, Juve kuizua Bayern?


Messi alipoichachafya PSG wiki iliyopita


BARCELONA, Hispania
LIONEL Messi ameondolewa kutoka kuwa wa kwanza katika orodha ya nyota wa kikosi cha Barcelona hadi kuwa wa mwisho wakati klabu yake ikilazimika kusubiri taarifa ya mwisho ya daktari kuhusiana na hali yake kabla ya kuteremka dimbani katika mechi yao ya marudiano ya robo fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Paris St Germain (PSG) itakayochezwa kwenye Uwanja wa Nou Camp leo.
Mwanasoka huyo bora wa mwaka wa Dunia anaendelea kuuguza jeraha la msuli wa paja alilopata mjini Paris wiki iliyopita, wakati alipofunga katika mechi yao ya kwanza iliyomalizika kwa sare ya 2-2, ingawa Barca walithibitisha kuwa wanaweza kufanya vizuri pia bila kuwa naye baada ya kuisambaratisha Real Mallorca kwa mabao 5-0 katika mechi yao ya La Liga, Ligi Kuu ya Hispania Jumamosi.
Licha ya kuchezesha kikosi dhaifu, vinara hao wa La Liga walionyesha kiwango cha juu kwenye Uwanja wa Nou Camp kutokana na 'hat-trick' ya Cesc Fabregas na mabao mengine mawili kutoka kwa Alexis Sanchez lakini PSG ni wagumu kulinganisha na 'vibonde' Mallorca wanaokamata mkia kwenye msimamo wa La Liga.
Barca wanaopewa nafasi kubwa ya kusonga mbele wanafukuzia taji lao la nne la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya katika misimu nane na Messi ndiye huwabeba kwa kuwatoka mabeki wa upinzani kwa chenga katika mechi zao kubwa na kuwatengenezea wenzake nafasi za kufunga au kuifanya mwenyewe kazi hiyo ya kupachika mabao.
Ule uwapo wa Messi tu uwanjani huwachanganya wapinzani kisaikolojia, wakiumiza vichwa juu ya namna ya kumdhibiti.
Muargentina huyo alifanya mazoezi mepesi ya viungo Jumapili na vyombo vya habari vya Hispania viliripoti kwamba alikuwa ni mmoja wa wachezaji waliojitokeza kufanya mazoezi juzi licha ya timu hiyo kuwaruhusu wachezaji wote kupumzika .
Huku wakiwa tayari wamejihakikishia kutwaa ubingwa wa La Liga kutokana na kuongoza kwa tofauti ya pointi 13 dhidi ya mahasimu wao Real Madrid wanaokamata nafasi ya pili wakati kila timu ikiwa imebakiza mechi nane, kocha  Tito Vilanova anaweza kuiongoza timu hiyo leo dhidi ya PSG.
Vilanova pia anatarajiwa kuamua ni nani amchezeshe na Gerard Pique katika sehemu ya ulinzi wa kati baada ya Javier Mascherano kuwa nje kutokana na jeraha na Carles Puyol yuko shakani kucheza baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti.
Beki yosso asiye na uzoefu, Marc Bartra alicheza vizuri na Pique Jumamosi lakini beki kiraka wa pembeni, Adriano Correia anakaribia kuwa 'fiti' na hivyo anaweza kucheza au kupangwa tena kwa kiungo Alex Song katika nafasi hiyo ya beki wa kati.
"Tutaangalia wachezaji gani tulio nao dhidi ya PSG," kocha msaidizi wa Barca, Jordi Roura alisema jana.

SILVA APONA
Beki wa kati aliye tegemeo PSG, Thiago Silva amejumuishwa kikosini kufuatia unafuu alio nao wa jeraha la goti alilolipata katika mechi yao ya kwanza dhidi ya Barca na kukosa mechi ya Jumamosi waliyoshinda 2-0 dhidi ya Rennes kwenye Ligue 1, Ligi Kuu ya Ufaransa.
Kocha wa PSG, Carlo Ancelotti alikuwa na wachezaji saba wa kikosi cha kwanza ambao aliwaanzisha benchi au kutowajumuisha kabisa katika kikosi kilichochea Jumamosi wakati wakijiandaa kwa mechi ya leo.
Ancelotti, hata hivyo, atakuwa na kazi ya kuziba pengo la kiungo wake 'ngangaro' Blaise Matuidi ambaye ataikosa mechi ya leo kwa sababu ya kutumikia adhabu.
David Beckham anatarajiwa kuanza baada ya kuonyesha kiwango cha juu katika mechi yao ya kwanza, huku viungo wengine wakitarajiwa kuwa kati ya Muitalia Marco Verratti na Mfaransa Clement Chantome.
Kiungo wa kimataifa wa Italia, Thiago Motta anaweza pia kuziba nafasi ya Matuidi lakini hadi sasa amecheza mechi moja tu katika kipindi cha zaidi ya miezi miwili iliyopita kwa sababu ya jeraha.
Kiwango cha juu alichoonyesha Jeremy Menez dhidi ya Rennes hakitoshi kumfanya apate namba katika kikosi kitakachoanza na kuwaweka kando Ezequiel Lavezzi au Lucas Moura. Beki wa kati, Alex amepona pia jeraha la goti na amejumuishwa kikosini.
"Tunapaswa kuichukulia kuwa ni siku muhimu kwetu. Tuko katika hatua isiyokuwa ya kawaida kwetu," mkurugenzi wa michezo wa PSG, Leonardo aliviambia vyombo vya habari vya Ufaransa.
"Barcelona wako katika mwaka wa 20 wa mradi wa kujenga timu yao. PSG imeanza ukurasa mpya katika historia yao lakini timu yao imeanza kujifua pamoja miezi 20 tu iliyopita."
Mechi nyingine ya robo fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya leo itakuwa ni kati ya Bayern Munich na Juventus. Katika mechi yao ya kwanza wiki iliyopita, Bayern waliutumia vyema uwanja wao wa nyumbani baada ya kuibuka na ushindi wa 2-0. 

Juve maarufu kama kibibi kizee cha Turin watakuwa wakihitaji ushindi mnono ili kuwang'oa mabingwa hao wapya wa Ujerumani ambao msimu huu wameonekana kuwa moto mkali.

Filamu ya After Death kutolewa hadharani Mei



FILAMU maalum kwa ajili ya kumuenzi marehemu Steven Kanumba iitwayo 'After Death' iliyozunduliwa kwa kishindo wakati wa hafla ya 'Kanumba Day' inatarajiwa kuachiwa rasmi mwezi ujao.
Kwa mujibu wa waandaaji, filamu hiyo itatoka Mei kwa lengo la kutoa fursa ya kazi mpya ya marehemu Kanumba ya 'Love & Power' iliyozinduliwa pamoja Aprili 7 kwenye viwanja vya Leaders itambe sokoni ikitarajiwa kuachiwa rasmi sokoni Ijumaa hii.
Muongozaji wa filamu hiyo ilitungwa na Jacklyne Wolper, Leah Richard 'Lamata', alisema licha ya mashabiki waliofika Leaders kushuhudia uzinduzi wa filamu hizo kuitaka kuinunua, walikwama kwa vile muda wake wa kuitoa bado.
Lamata alisema mashabiki hao wanapaswa kuwa na subira mpaka mwezi ujao kazi hiyo itakapoachiwa rasmi kulingana na ratiba iliyopo.
"Tunashukuru tumefanikiwa kuwaonjesha ladha na kupokewa vyema kwa filamu hii, lakini mashabiki wanapaswa kusubiri hadi Mei tutakapoiachia rasmi," alisema Lamata.
Filamu hiyo inayoakisi maisha baada ya Kanumba kufariki, imewashirikisha wasanii kadhaa wakiwamo chipukizi waliotamba katika 'This is It' na 'Uncle JJ', Khanifa Daud 'Jennifer' na Othman Njaidi 'Patrick'.
Wengine walioigiza filamu hiyo ni Philemon Lutwazi 'Uncle D', Irene Paul, Patcho Mwamba, Mainda Suka, Shamsa Ford, Jacklyne Wolper na Stanley Msungu.

Victoria Sound yakamilisha mpya za albamu yake

 
Mwinjuma Muumin anayeiongoza Victoria Sound

BENDI ya Victoria Sound imekamilisha wimbo mpya wa albamu yao ya kwanza wanayotarajia kuitoa hivi karibuni, pia wakiwa mbioni kurekodi video yao ya pili ya wimbo wa 'Mwisho wa Siku'.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Mwinjuma Muumin 'Kocha wa Dunia' aliiambia MICHARAZO jana kuwa wimbo unaokamilisha albamu umetungwa na muimbaji wao Januari Mavoko haujapewa jina na unaendelea kufanyiwa mazoezi.
Muumin alisema wimbo huo utarekodiwa siku chache zijazo ili kukamilisha jumla ya nyimbo sita na sebene moja kama bonasi kwa mashabiki zitakazokuwa katika albamu ya kwanza.
"Victoria Sound tunaendelea kuufanyia mazoezi wimbo mpya unaokamilisha albamu yetu uliotungwa na Januari Mavoko, ikiwa ni siku chache tangu tutoke kurekodi wimbo wa 'Maisha' uliotungwa na Atosha One," alisema Muumin.
Alisema kuwa Victoria wameamua kurekodi video ya wimbo mmoja mmoja mpaka wamalize zote saba kabla ya uzinduzi baadaye mwaka huu.
Kwa sasa bendi hiyo imerekodi na 'kushuti' video ya wimbo wa 'Shamba la Bibi' ambao mbali na huo pia wamesharekodi nyimbo za 'Utafiti wa Mapenzi' utunzi wa Muumin, 'Mama Bahati' wa Yohana Mbatizaji na 'Maisha'.

Sunzu, Kazimoto warejesha Msimbazi

Sunzu (kulia)
WAKATI wachezaji Felix Sunzu na Mwinyi Kazimoto wakirejea katika kikosi cha Simba kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Azam utakaofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, kikosi cha timu hiyo kinaingia kambini leo Bamba Beach, Kigamboni.
Sunzu na Kazimoto walitarajiwa jana jioni kuanza mazoezi na wachezaji wenzao kwenye Uwanja wa Kinesi, Sinza jijini na lengo la kuwarejesha baada ya kuomba msamaha ni kukiongezea nguvu kikosi kitakachopambana kuivaa Azam.
Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema jana kuwa wachezaji wote wataingia kambini leo asubuhi na wanaamini kambi hiyo itawaongezea morali ya kufanya vizuri katika mechi hiyo.
Mtawala alisema kuwa maandalizi  ya mechi hiyo yamekamilika na wachezaji wamepatiwa mahitaji yote muhimu kuelekea mchezo huo muhimu kwa timu yao ambayo imeshapoteza matumaini ya kutwaa ubingwa.
"Kila kitu kinachotakiwa kuandaliwa kimeshafanyiwa kazi na wachezaji wote wanaingia kambini kesho saa nne asubuhi, tunaamini wakiwa huko watapata utulivu na kumsikiliza mwalimu," alisema Mtawala.
Naye daktari wa Simba, Cosmas Kapinga, alisema jana kuwa beki tegemeo wa timu hiyo, Shomary Kapombe, ameshapona na jana jioni alitarajiwa kuanza mazoezi na wenzake.
Kapinga alisema kwamba vipimo vya mwisho vya uchunguzi alivyofanyiwa juzi Jumatatu vimeonyesha kuwa eneo la mfupa kati ya bega na kifua lililokuwa na maumivu limepona.
Simba itashuka dimbani Jumapili ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Azam walioutapata katika mechi yao ya mzunguko wa kwanza iliyofanyika Oktoba 27 mwaka jana.
Mabingwa watetezi Simba ni wa nne katika msimamo wa ligi wakiwa na pointi 35 wakati Azam ambao ni wenyeji wa mechi ya Jumapili wako kwenye nafasi ya pili wakiwa na pointi 43 huku Yanga ndiyo vinara kwa pointi 49.

Real Madrid yafuzu nusu fainali kwa kipigo, Dortmund yawafuata

Ronaldo akishangilia bao lake la kwanza usiku wa jana
MABINGWA wa kihistoria wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Real Madrid usiku wa kuamkia leo imefuzu hatua ya Nusu Fainali ya michuano ya mwaka huu ikipokea kipigo ugenini cha mabao 3-2 toka kwa Galatasaray ya Uturuki.
Real chini ya kocha wao Jose Mourinho walifanikiwa kufuau hatua hiyo kwa faida ya mabao iliyopata katiika mechi ya nyumbani wiki iliyopita walipoizima Galatasaray kwa mabao 3-0 hivyo kufuzu kwa jumla ya mabao 5-3.
Nyota wa klabu hiyo ya Hispania, Mreno Cristiano Ronaldo ndiye aliyesaidia kuiokoa Real Madrid baa ya kufunga mabao mawili moja kila kipindi na kusaidia kuivusha timu yake hatua hiyo.
Ronaldo alifunga bao la kuongoza dakika saba tu ya mchezo huo uliochezwa Uturuki  na kufanya hadi mapumziko matokeo yawe bao 1-0.
Kipindi cha pili wenyeji waliingia wakiwa wamecharuka na kusawazisha bao kupitia kwa Emmanuel Eboue katika dakika ya 57, kabla Wesley Sneijder hajaongeza bao la pili dakika ya 70.
 
Wesley Sneijder, akishangilia bao lake dhidi ya Real Madrid
Katika dakika ya 72, Didier Drogba aliifungia Galatasaray bao la tatu kabla ya  Ronaldo kufunga  goli la pili la kufutia machozi la Real Madrid dakika ya 90.
Katika pambano jingine la michuano hiyo lililochezwa usiku wa jana nchini Ujerumani wenyeji Borussia Dotmund walifanikiwa kusonga mbele kwenye michuano hiyo baada ya kuwalaza wageni wao mabao 3-2.
Borussia Dortmund wakipongezana kufuzu nusu fainali dhidi ya Malaga

Wageni walionyesha kama wangewaadhiri wenyeji wao baada ya kutangulia kupata bao dakika ya 25 kupitia Joaquin kabba ya Robert Lewandowski kusawazisha dakika tano kabla ya mapumziko.
Eliseu aliiongezea Malaga bao la pili dakika ya 82 na kuwafanya wageni hao kuamini wamemaliza kazi katika pambano hilo kabla ya wenyeji wao kucharuka na kuandika mabao mawili dakika za nyongeza.
Iliwachukua dakika mbili tu za ziada kwa wenyeji hao kujipatia mabao hayo mawili kupitia kwa Marco Reus kumalizia kazi nzuri ya Felipe Santana kabla ya Santana kutupia la pili na kuwavusha mabingwa hao wa Ulaya wa mwaka 1997 kuungana na Real Madrid kucheza hatua ya nusu fainali.

Tuesday, April 9, 2013

WATU WAMETOKA MBALI, RAIS MPYA WA KENYA ALIPOKUWA 'KINDA'

RAIS Mpya wa Kenya, Uhuru Kenya aliyeapishwa leo nchini humo, huenda akiiona picha hii itamkumbusha mbali. Hapa ni alipokuwa mdogo akiwa ameshikwa mkono na baba yake Jomo Kenyatta wakati huo akiwa rais wa taifa hilo.Nyuma ya Kenya mwenye suti nyeusi ni aliyekuja kuwa Rais wa Pili wa Kenya, Daniel Arap Moi. Jamani watu tunatoka mbali nyie acheni!

Yanga, kocha Toto waadhibiwa na TFF kwa 'ukora'

Kikosi cha Yanga
Kocha wa Toto, Athuman Bilal 'Bilo'

Na Boniface Wambura
KLABU ya Yanga na Kocha Msaidizi wa timu ya Toto Africans, Athuman Bilali wamepigwa faini ya sh. 500,000 kila mmoja kutokana na makosa mbalimbali katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inayoendelea nchini.

Adhabu hizo zimetolewa na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana Jumapili (Aprili 7 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za waamuzi na makamishna kwa michezo namba 108 hadi 171.

Yanga imepigwa faini hiyo baada ya kupata kadi tano za njano katika mechi dhidi ya Kagera Sugar iliyochezwa Februari 7 mwaka huu. Vilevile Kagera Sugar imepigwa faini ya sh. 100,000 kwa kuchelewa kufika kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre match meeting) dhidi ya African Lyon iliyochezwa mjini Bukoba, Februari 23 mwaka huu.

Naye Kocha Bilali amepigwa faini hiyo na kufungiwa mechi tatu za ligi hiyo kwa kumshambulia kwa maneno kocha wa timu pinzani, hali iliyosababisha mwamuzi amtoe kwenye benchi la wachezaji. Alifanya tukio hilo kwenye mechi kati ya Toto Africans na Tanzania Prisons iliyochezwa Aprili 3 mwaka huu jijini Mwanza.

African Lyon na Simba zimepigwa faini ya sh. 500,000 kila moja kwa kushindwa kuchezesha timu zao za U20 kwenye mechi za utangulizi wakati zilipocheza na Oljoro JKT na Coastal Union, Machi mwaka huu kwenye viwanja vya Azam Complex na Uwanja wa Taifa.

Suala la Meneja wa Coastal Union, Akida Manchai kumshambulia kwa maneno yasiyo ya kiungwana Makamu Mwenyekiti wake Steven Mnguto baada ya kwenye mechi kati ya African Lyon na Coastal Union iliyochezwa Machi 30 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex limepelekwa Kamati ya Nidhamu kwa ajili ya hatua za kinidhamu.

Adhabu zote zimetolewa kwa mujibu wa Kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom.

Kivumbi cha Ligi Kuu kutimka tena kesho


Na Boniface Wambura
TIMU ya Polisi Morogoro inapambana na Ruvu Shooting katika moja kati ya mechi tatu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zitakazochezwa kesho (Aprili 10 mwaka huu). Matokeo ya mechi hiyo yanatarajia kutoa mwanga kama Polisi inaweza kubaki kwenye ligi hiyo msimu ujao.

Timu hiyo itakuwa nyumbani Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro katika mechi hiyo itakayochezeshwa na Ibrahim Kidiwa kutoka Tanga akisaidiwa na Godfrey Kihwili na Ephrony Ndissa wa Arusha.

Polisi Morogoro inayonolewa na Adolf Rishard inakamata nafasi ya mwisho ikiwa na pointi 18 tu na imebakiza mechi tatu dhidi ya Simba, Kagera Sugar na Coastal Union.

Mechi nyingine za kesho ni kati ya Tanzania Prisons iliyo nafasi ya 12 ikiwa na pointi 20 dhidi ya Mgambo Shooting. Mwamuzi Hashim Abdallah wa Dar es Salaam ndiye atakayechezesha mechi hiyo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya. Mgambo ina pointi 24 na iko katika nafasi ya tisa.

Mwamuzi Said Ndege wa Dar es Salaam atachezesha mechi kati ya wenyeji Mtibwa Sugar na Toto Africans itakayofanyika Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro. Toto Africans ya Kocha John Tegete ina pointi 21 ikiwa nafasi ya 11 wakati Mtibwa Sugar iko nafasi ya tano na pointi zake 32.

Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Aprili 11 mwaka huu) kwa mechi moja kati ya Azam na African Lyon itakayofanyika Uwanja wa Azam Complex.