STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 18, 2014

Tamasha la Magari kufanyika Leaders

http://swahili.cri.cn/mmsource/images/2008/12/10/20080718094020385b.jpg 
Na Suleiman Msuya
KAMPUNI ya  Jast Tanzania Limited kwa kushirikiana na Jossekazi Auto Garage and General supplier wameandaa tamasha la kwanza la Magari la aina yake, linalojulikana kwa jina la Automobile Clinic, ambalo linatarajiwa kufanyika kwa siku mbili mfululizo katika viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam.
Tamasha hilo limelenga katika kutoa huduma ya kitaalamu ya kiufundi kwa wenye magari (Checkup and Fix) kutoka kwa mafundi stadi ambao wamebobea katika fani ya ufundi wa makenika katika aina tofauti tofauti za magari.
Akizungumza na vyombo vya habari, kwenye ukumbi wa habari Maelezo, Joseph Mgaya mmiliki wa Jossekazi Auto garage amesema tamasha hili lina lengo kuwakutanisha mafundi stadi na wenye magari, kwa gharama nafuu sana ya shillingi elfu ishirini tu.
Mgaya alisema huduma hizo ambazo zilipaswa kugharimu kiasi kikubwa sana cha pesa kwa wenye magari, kitatolewa kwa bei nafuu ili kwa makusudi tu ya kukutanisha mafundi hao na wenye magari,.
Alisema pamoja na Wateja kutengenezewa Air condition na kujaziwa gesi, kufanyiwa Electronical scan diagnosis, Kuchekiwa Matairi, kuchekiwa Battery, na kupata ushauri wa kiufundi kuhusu gari zao, pia tamasha hilo litakuwa ni sehemu ya kukutanisha watu na kupata burudani. 
Mgaya alisema, Mafundi wapatao 50 waliobobea katika fani ya ufundi magari, wamepatikana baada ya kufanyiwa usaili wa kina na kupitia mchujo na semina elekezi ili kuweza kuhudumia magari yanayokadiriwa kufika zaidi ya 6000 kwa siku hizo mbili.
Pamoja na hayo, Mgaya alisema “ Tumeandaa warsha maalum kwa kina dada, tunatambua kuwa asilimia kubwa ya waendesha magari barabarani hivi sasa ni kina dada, tunataka waelewe ni nini cha kufanya pindi atakapopatwa na hitilafu kwenye gari mabarabarani. “
Elimu hii ambayo wameiita ‘Auto First Aid’, alisema itasaidia kupunguza uharibifu zaidi kwenye magari yao,  alisema wakati mwingine kwenye deshboord ya gari kuna kuwa na alama za hatari, lakini kwa kuwa gari inatembea wanawake wengi wamekua wakipuuzia alama hizo na matokeo yake wanasababisha hasara kubwa zaidi.
“Pamoja na kuwafundisha alama za hatari na nini cha kufanya pindi waonapo alama hizo pia Tutawafundisha kubadilisha matairi, na nini chakufanya na kuwa nacho ikitokea gari limewaharibikia njiani. “ alisema Mgaya.
Mgaya ambaye amefanikiwa sana katika ufundi wa AC za magari, Ndege, na Meli, aliongeza kuwa fani ya ufundi makenika ni kazi ya kuheshimika kama zilivyo kazi nyingine, na kuongeza kuwa anaiona fursa kubwa kwa vijana wanaomaliza elimu ya juu.
“Siku hizi magari yote kuanzia Mwaka 2005 kwenda juu yanatumia vifaa maalum vya computer na internet, pamoja na kuwa maelezo yanakuja kwa lugha ya kingereza, ufundi spana wa kurithishwa hivi sasa hauna nafasi,”alisema.
“Tofauti na zamani ukifeli form 4, unapelekwa kwenye ufundi hali hivi sasa imebadiliilka fani hii inahitaji wasomi na watu wanaoweza kubadilika na kurudi shuleni kila mara, kama computer matoleo ya magari kila mwaka yanakuja na vitu tofauti, hivi sasa break hazina annoying sound, break zikiisha utaona kwenye dashboard, kutengeneza lazima useme user manual ya kingereza na u download soft ware kwenye internet,” alisema Mgaya na kusistiza vijana waingie kwenye fani hii. 
Aidha Mkurugenzi wa Jast Tanzania Limited, Jahu Mohammed Kessy, Mratibu wa Tamasha hilo walisema kuwa, Automobile Clinic litakuwa zaidi ya Tamasha.
“Katika kuhakikisha tunautumia muda wa wateja wetu vizuri, wakati gari inafanyiwa ufundi, kutakuwa na huduma nyingine za ziada zitakazo patikana siku hizo mbili, kutakuwa na vinywaji, vyakula kama nyama choma, na michezo ya watoto, kutakuwa na huduma ya kulipia ya kuoshewa magari, kusafishiwa taa, na baadhi ya vifaa kama Fire extinguisher, manukato ya gari, Triangle na kadhalika vitauzwa hapo uwanjani,” 
Jahu alisema Tiketi zitauza kabla, na kwamba tiketi hizo zitakuwa katika mfano wa sticker ya kubandika kwenye magari, na zitapatikana katika vituo vyote vya kuweka mafuta vya TSN, Supermarket zote za TSN, Kwenye ofisi za Millembe insurance, Bon to shine, BM hair cutting salon, na Mlimani City.
“Hakutakuwa na Kiingilio kwa watu, lakini badala yake kwa magari, magari yenye sticker pekee ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia na kupata huduma hizo, tunashauri wenye kununua sticker wafike mapema kwani watakao fika kwanza ndio watakao hudumiwa,”
Jahu alisema katika kurudisha kwa jamamii, mafundi hao hamsini baada ya Tamasha watatembelea kwenye hospitali ya CCBRT kusaidia wakina mama wenye matatizo ya fistula.
Tamasha hilo limedhaminiwa na Milembe insurance, Wambi lube oil distributor, TSN, Binslum tires company Limited, I view, Cocacola, Dreams Limited, Hugo Domingo, Olduvai Bay Wash, 0-60 autogarage, Meku Auto spear part, Dick Sound, Brand Tiger, Clouds FM, Auto Beats, Neh Catering, Pamoja na Lim Painting and decorating.

Sunday, September 14, 2014

Manchester United yaanza Ligi yaifumua QPR

Di Maria akishangilia bao lake
1410710470161_lc_galleryImage_14th_September_2014_Barcl
Furaha ya ushindi Manchester wakifurahia baada ya kuypata moja ya mabao yao
Mata akishangilia bao lake
NYOTA wapya wa Manchester United, Ander Herrera na Angel di Maria walithibitisha thamani yao baada ya kuiwezesha timu yao kupata ushindi wa kwanza msimu huu katika mashindano kwa kuilaza QPR kwa mabao 4-0 katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Di Maria aliwainua mashabiki wa Old Trafford kwa kufunga bao la kwanza katika dakika ya 24 kabla ya Herrera kupachika la pili katika dakika ya 36 akimalizia kazi ya nahodha Wayne Rooney.
Dakika moja kabla ya mapumziko, nahodha huyo Rooney alifunga bao la tatu akimalizia kazi murua ya Herrera na bao la mwisho la vijana wa Luis Van Gaal lilifungwa na Juan Mata katika dakika ya 58 kwa kazi safi ya Di Maria aliyeonyesha ubora wake na kuifanya Mashetani Wekundu kupumua baada ya kuanza vibaya ligi na msimu mzima kwa ujumla.
Radamel Falcao aliingia uwanjani katika kipindi cha pili na kuonyesha makeke yake ikiwa ni mara ya kwanza tangu asajiliwe kutoka Monaco.

Yanga ya Maximo kiwangoo! yaiua Azam x3

Mrisho Ngassa akijaribu kumtoka Erasto Nyoni wa azam (Picha zote kwa hisani ya Habari Mseto )
Kikosi cha Azam kilichozimwa Taifa leo
Kikosi ch Yanga kilichotwaa Ngao ya Hisani leo kwa kuilzaza Azam
 KLABU ya Yanga iliyo chini ya kocha Marcio Maximo wa Brazil, jioni ya leo imetuma salamu kwa klabu nyingine za Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifumua bila huruma watetezi wa ligi hiyo, Azam mabao 3-0 katika pambano la Ngao ya Hisani lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa.
Yanga ikiwa katika kiwango cha juu na kuwafunika wapinzani wao, walithibitisha kuwa bado ni wababe wa Azam katika mechi ya Ngao ya Hisani baada ya kuifdunga kwa msimu wa pili mfululizo kwani msimu uliopita waliitambia kwa bao 1-0.
Mabao yaliyoizamisha Azam waliotwaa ubingwa wa ligi msimu uliopita bila ya kupoteza mchezo wowote yalitumbikizwa wavuni na Gelinson Santana 'Jaja' aliyefunga mabao mawili na kuzima ngebe za mashabiki waliokuwa wakimzomea kabla ya Simon Msuva kufunga jingine akitokea benchi kumpokea Nizar Khalfan.
Kipigo hicho cha Azam kimevunja rekodi ya kocha Joseph Omog pamoja na vijana wao ambao walikuwa wakifurahia kushinda au kutoka sare bila kupoteza mchezo wowote tangu mwaka jana katika mashindano nchini Tanzania.

Hofu yatanda Arsenal kuumia kwa Debuchy

Gunners manager Arsene Wenger has admitted that Mathie Debuchy's injury 'doesn't look good'
Arsenal defender Mathieu Debuchy screams in pain after injuring his ankle against Manchester CityKLABU ya Arsenal ipo katika hofu kubwa baada ya beki wake wa kulia Mathieu Debuchy ameumia vibaya na haijajulikana bado  atakaa nje ya kiwanja  kwa muda gani  .
Kocha  Arsene Wenger amesema majeraha ya  Debuchy’s  ‘Hayaonyeshi' kupona upesi na kuna hitajika kufanyika uchunguzi wa kina zaidi waweze kugundua atakaa nje kwa muda gani .
Mchezaji huyo alianguka vibaya na kukanyaga kifundo chake cha mguu wa kushoto katika kipindi cha pili cha mchezo kati ya Arsenal na Manchester City ulioisha kwa sare ya 2-2.
Debuchy, 29 alijiunga na  Arsenal katika majira ya kiangazi akichukua nafasi ya Bacary Sagna,aliyejiunga na  Man City, na alicheza vizuri katika mechi na klabu yake ya zamani katika uwanja Emirates.

Yanga, Azam leo hapatoshi Taifa katika Ngao ya Jamii

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0OMIi84tDpx05S0PI2fuo0AE_ulzrjGm81vlt-VnfTTM5dO-IxD-GT-W5iOY3rW6KOsIt72oAKVP2adJndh_oTt8BMN6leXVkHUnX5tP_KMFYkNc362P0lRT8ck1Iz7KiBY4fWKa1aGKV/s1600/YANGAVSAZAM.jpgMWISHO wa tambo na mikwara baina ya Azam na Yanga ni leo wakati klabu hizo mbili zitakapopepetana kwenye mechi ya Nf\gao ya Jamii kuashiria kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Timu hizo zitapambana kwenye uwanja wa Taifa, huku zote zikiwakosa baadhi ya nyota wake kutokana na kuwa majeruhi.
Yanga inatarajiwa kumkosa kiungo wake mahiri, Andrey Coutinho aliyeumia katika mechi ya kirafiki dhidi ya Polisi Dar es Salaam kwenye uwanja wa sekondari ya Loyola.
Mshambuliaji huyo alipatwa na maumivu hayo wakati alipokuwa akijaribu kupiga mpira na hivyo kushindwa kuendelea na mchezo. Timu hizo zilitoka suluhu.
Azam ambao walilala bao 1-0 katika mechi kama hiyo kwa msimu uliopita, haitakuwa na huduma ya nahodha wake, John Bocco Adebayor aliye majeruhi pia, kwa mujibu wa Meneja wa Azam Said Jemedari.
“Tunao majeruhi wawili, ambao hawatakuwepo kwenye programu ya mchezo wa Ngao ya Jamii, ambao ni beki Waziri Salum na nahodha wetu, John Bocco,”alisema Jemedari.
Timu hizo zinakutana baada ya mwaka jana kushuhudia Azam wakiipindua Yanga na kuwanyang'anya ubingwa wakiwa hawajapoteza mchezo wowote.
Mechi hiyo itaanza saa 10 kamili jioni, na kiingilio hicho cha sh. 5,000 ni kwa viti vya rangi ya kijani na bluu vitakavyochukua jumla ya watazamaji 36,000 katika uwanja huo wenye viti 57,558.
Viingilio vingine katika mechi hiyo ambayo itatumia tiketi za elektroniki ni sh. 10,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000 kwa viti vya VIP C na B wakati viti vya VIP A kiingilio ni sh. 30,000.

Simba yabanwa na Ndanda Fc Mtwara

Simba SC
Ndanda Fc
SIMBA imeendelea kwenda mwendo wa kusuasua katika mechi zake za kujiandaa kwa michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya jana kulazimishwa kutoka suluhu na Ndanda FC.
Katika mechi hiyo ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, vijana wa Ndanda waliwabana vyema wapinzani wao katika vipindi vyote viwili.
Sare hiyo imekuja siku chache baada ya Simba kuchapwa bao 1-0 na URA ya Uganda katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kama ilivyokuwa katika mechi dhidi ya URA, mshambuliaji Emmanuel Okwi alishindwa kuonyesha makeke yake kutokana na kubanwa vyema na mabeki wa Ndanda. Okwi aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Abdalla Seseme.

Warembo Miss Tanzania 2014 wawasili kambini

Na Father Kidevu 
Wanyange 30 wanao wanbia taji la Redd's Miss Tanzania 2014 leo wameingia kambini tayari kwa safari ya fainali za Miss Tanzania 2014 zitakazo fanyikia mapema mwezi Oktoba jiji Dar es Salaam.


Warembo hao waliowasdili kwa muda tofauti kuanzaia saa 12 alfajiri ya leo na kupokelewa na waandaaji wa Miss Tanzania katika hoteli ya JB Belmont iliyopo katikati ya jiji la maraha la Dar. 
Warembo kutoka Kanda ya Ziwa walitia fora pale warembo hao walipowasili kambini hapo wakiwa ndani ya gari ya Mshindi wa Kanda ya Ziwa ambayo alizawadiwa hivi kjaribuni katika shindano lao.
 Warembo wa Kanda ya Ziwa wakiteremka katika gari lao baada ya kuwasili na inaelezwa waliendesha kutoka jijini Mwanza.
 Warembo wa Kanda ya Ziwa wakijiandikisha baada ya kuwasili kambini.
 Warembo wakielekea chumba cha mkutano.
 Warembo wakiwa katika chumba cha semina ambapo maelezo mbalimbali ya ka,mbi yao yalitolewa.

Shinji Kagawa aanza na mguu mzuri Borussia Dortmund

Japan international Shinji Kagawa (right) celebrates after his goal at the WestfallonstadionKIUNGO mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Shinji Kagawa amedhihirisha ukali wake baada ya kurejea Borussia Dortmund kwa kishindo kwa kuisaidia timu hiyo kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Freiburg katika Ligi Kuu ya Ujerumani Bundesliga.
Kagawa aliyekaribishwa vyema na mashabiki wa klabu hiyo kwa mabango na bendera ya Japan, alifunga bao moja na kuchangia nyingine lililokuwa la kwanza kwa timu yake lililotumbukizwa wavuni na Adrian Ramos.
Ramos alilipa fadhila kwa kumtengeneza Mjapani huyo aliyepachika bao la pili katika ya 41 na kuifanya wenyeji kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-0.
Bao la tatu la Dortmund iliyoimuuza Kagawa kwa Mashetani WEkundu kabla ya kumrudisha hivi karibuni liliwekwa kimiani katika kipindi cha pili na Aubameyang  dakika ya 78 kabla ya wageni kupata bao la kufutia machozi dakika ya 90 kupitia Sorg.

Real Madrid yafa nyumbani, Neymar aibeba Barcelona La Liga


Atletico Madrid's Arda Turan scores
Kitu hicho! Atletico Madrid wakiwaadhibu wenyeji wao
Cristiano Ronaldo
Hawaamini kama ni kweli wamepigwa
Cristiano Ronaldo scored a penalty in Real Madrid's 2-1 defeat against Atletico Madrid on Saturday
Ronaldo akifunga mkwaju wake wa penalti
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Hispania, Atletico  Madrid wameendeleza ubabe wake kwa Real Madrid baada ya kuinyuka  mabao 2-1 Uwanja wa Bernabeu mjini Madrid, katika mchezo wa ligi hiyo.
Atletico waliwashtukiza wenyeji wao kwa kuandika bao la kuongoza dakika ya 10 tu ya mchezo huo kupitia kwa Tiago.
Wenyeji walicharuka na kusawazisha dakika sita baadaye kupitia kwa Cristiano Ronaldo aliyefunga kwa penalti na kufanya hadi mapumziko mambo yawe 1-1.
Atletico walirejea tena nyavuni mwa wenyeji wao kwa kuandika bao la pili na la ushindi katika dakika ya 76 kupitia kwa Arda Turan aliyemaliza kazi nzuri ya Raul Garcia. 

Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Barcelona walipta ushindi nyumbani dhidi ya Athletico Bilbao kwa kuwalaza mabao 2-0.
Mabao yote ya wenyeji wakiwekwa kimiani katika kipindi cha pili na nyota wa Kibrazil, Neymar.
Ijumaa timu za Almeria na Cordoba zilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1, wakati katika mechi nyingin e za jana,Malaga na Levante zilishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu huku Celta Vigo na Real Sociedad zikitoka 2-2.

Coastal, Mtibwa kuzionolea makali Simba, Yanga

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEih8GIhwPpFvx9y37-dG5TLICcp_KCiphSP1VYgwX79MDr9R3tnTWyceiGkEuX9A89bxtFoklDDQtYSmrAox361CSsxPLNO0QiOzOiXFjYBym8OfCB3s-9GgU3KnI0_8FXHv919Cb0oO1Xk/s640/DSCN0138.jpg
Coastal Union
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgbodZ0IJ3DDDukQkZOD3uBBhFnRyS_36bTNfa2lByCz4hi3do7n2ffnbHwJPZ7M927cjrGC4zHIdMWa_k0r-eR3D8YaAO8lvvkkH17E8Xf7I_WhVKdmiJ87gem7uKakkwoXHDsRcIjqCQC/s640/MTIBWA+SUGAR.jpg
Mtibwa Sugar
MABINGWA wa zamani wa soka nchini Coastal Union ya Tanga na Mtibwa Sugar ya Morogoro zinatarajiwa kupimana ubavu leo katika pambano la kirafiki litakalochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani.
Mechi hiyo ni ya mwisho mwisho kwa klabu hizo kabla ya kujichimbia kambini kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza rasmi Jumamosi.
Kocha mkuu wa Coastal, Yusuph Chipo ametamba kuwa mchezo huo utakuwa kipimo kizuri kwa timu yake ambayo ilijichimba Pemba, na kugawa dozi nene kwa timu pinzani za Zanzibar ilizocheza nayo ambazo kisoka ni tofauti na timu za Tanzania Bara.
Chipo alisema huo utakuwa ni mchezo kwa kikosi chake kabla ya kuinolea makali Simba watakaofungua nao dimba Jumapili.
Mkenya huyo alisema pia mechi hiyo ni nafasi yake ya kupata kikosi cha kwanza kabla ya kuelekea kwenye Ligi Kuu.
"Baada ya mchezo wa Jumapili na Mtibwa Sugar nitatoa tathmini ya wachezaji, ikiwemo kupata kikosi cha kwanza katika timu,"alisema Chipo.
Kwa upande wa Mtibwa kupitia Msemaji wake, Thobias Kifaru naye alitamba kwamba mechi hiyo ni muhimu kwa benchi lo la ufundi kujiweka tayari kuinza ligi kuikaribisha Yanga kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro siku ya Jumamosi ijyo.
"Tupo kamili kwa ajili ya kuonyesha burudani kwa mashabiki wa Tanga sambamba na kuipa makali timu yetu kabla ya kuvaana na Yanga," alisema Kifaru.

Nyatawe 'awafunda' wenzake, ataka wajiheshimu

MUIGIZAJI mahiri wa filamu nchini aliyewahi kutamba na makundi ya Shirikisho Msanii Afrika, Happy Mkamwa 'Nyatawe' amewataka wasanii wenzake wa kike kupenda kujiheshimu na kujithamini ili nao waheshimiwa na kuthaminiwa na jamii.
Aidha aliwataka wasanii nchini kwa ujumla kuwa wabunifu na kuumiza vichwa ili kutoa kazi ambazo zitabamba anga la kimataifa.
Akizungumza na MICHARAZO, Nyatawe alisema wasanii wa kike wanapaswa kujitambua wao ni  nani ndani ya jamii na hivyo kuwa mfano bora kuanzia mavazi yao, matendo na hata kwa kauli zao ili kujijengea heshima mbele ya jamii inayowazunguka.
Alisema kuendelea kufanya mambo ya ovyo yanawashushia heshima na kufanya wadharaulike.
"Wasanii wa kike wa leo ndiyo wazazi na walezi wa kesho wa familia hivyo ni wajibu wetu kuwa makini kwa kila tunalofanya au kulitamka, ili kujenga heshima na hadhi zetu," alisema.
Pia aliwakumbusha wasanii kupenda kuwa wabunifu katika kazi zao pamoja na kujituma kwa bidii ili mwishowe waje kutamba kimataifa badala ya kuridhika na mafanikio ya nyumbani.

Sikinde sasa kuzindua Jinamizi lao Oktoba

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgyQvJbNPmPY9Zp7MmXibkXD186MC54L8sZ79WM1IZ_KxdV5R5Wh9ZWSAd3-nx1OZIXAfVweaIncxaslL1wDR3VQuRmdKX2u7M6swKmwLhBJ4W2tcShvII75vxkD5IjN7HNy3v0uowGg6s/s1600/sikinde.JPGBENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Mlimani Park 'Sikinde' inatarajia kuzindua albamu  yake mpya ya 'Jinamizi la Talaka' mwishoni mwa Oktoba baada ya kushindwa kufanya hivyo  mwezi uliopita.
Aidha bendi hiyo inatarajiwa kufanya ziara ya kimuziki katika mikoa ya Morogoro na Dodoma  wiki ijayo kwa ajili ya kuzitambulisha nyimbo zao mpya za albamu hiyo kwa mashabiki wa mikoa  hiyo.
Msemaji Msaidizi wa Sikinde, Emmanuel Ndege aliiambia MICHARAZO kuwa baada ya kukwama  kufanya uzinduzi wao Agosti kama ilivyokuwa imetangazwa, Sikinde sasa inatarajiwa kuzindua  albamu yao mpya katika maadhimisho ya miaka 38 ya kuanzishwa kwa bendi hiyo.
Ndege alisema kwa sasa wanaendelea kufanya mchakato wa wadhamini kabla ya kutangaza rasmi  tarehe ya jambo hilo, japo alisisitiza itakuwa mwishoni mwa Oktoba.
"Uzinduzi wa albamu yetu mpya utafanyika Oktoba sambamba na maadhimisho ya miaka 38  tangu kuanzishwa kwa Sikinde," alisema Ndege.
Pia aligusia juu ya ziara ya kimuziki wanaotarajia kuifanya wiki ijayo katika mikoa ya Morogoro na  Dodoma ili kutambulisha nyimbo zao mpya kwa mashabiki wa bendi hiyo wa mikoa husika.
"Tupo katika maandalizi ya kwenda kuzitambulisha nyimbo za albamu yetu mpya katika mikoa ya  Dodoma na Morogoro, tukiwa huko pia tutakumbushia nyimbo za zamani za bendi hiyo zilizoipa  Ubingwa wa Muziki wa Dansi Tanzania," alisema Ndege

Saturday, September 13, 2014

Newz Alert! Jengo analohubiria TB Joshua laporomoka Nigeria


Watu kadhaa wanahofiwa kufariki mjini Lagos Nigeria baada ya jengo moja linalohusishwa na muhubiri mashuhuri nchini humo TB Joshua kuanguka.

Ripoti zinasema kuwa miili kadhaa imetolewa katika vifusi vya jengo hilo.
church collapses
Shirika la kusimamia dharura nchini humo NEMA ,limesema kuwa jengo hilo ni la nyumba za kulala za wanachama wa kanisa la All Nations katika wilaya ya Ikotun.
Jengo hilo la ghorofa mbili lilikuwa likiongezwa ghorofa nyengine mbili lilipoanguka.
Maelfu ya watu mara nyingi uhudhuria maombi yanayoongozwa na TB Joshua anayejulikana kama mtume,kwa kuwa wanavutiwa na uwezo wake wa kuwaponya watu

Bright Mbwilo: Mwanasoka Afande anayetesa ktk muziki wa Injili


Kava la albamu ya Afande Bright kama linavyoonekana kwa anayehitaji kupata burudani hiyo anaweza kuwasiliana naye kupitia namba zinazoonekana pembeni au  barua pepe

Afande Bright Mbwilo katika pozi

NDOTO zake za utotoni zilikuwa aje kuwa mmoja wa nyota wa soka nchini kutokana na kuupenda mchezo huo anaoendelea kuucheza mpaka sasa akiwa na klabu ya Polisi-Pwani.
Kiu kubwa ya mafanikio katika soka ndiyo iliyomfanya Bright Job Mbwilo kuanza kucheza tangu akisoma Shule ya Msingi Magoye-Makete na baadaye Songwe Mbeya.
Hata alipojiunga na masomo ya Sekondari katika Shule ya Kilombero Day ya Ifakara na baadaye Iyula-Mbozi bado alikuwa akisakata kandanda na kuamini ndoto zake zitatimia.
Haikuwa ajabu kwake kuanza kupata umaarufu akiwa Songwe Stars akicheza kama mshambuliaji na wakati mwingine kiungo au beki wa kati kabla ya kutua Oljoro JKT iliyomsaidia kupata mafunzo ya kijeshi.
Mafunzo hayo yaliyofahamika kama Operesheni Kasi Mpya yalimpa ajira JKT kabla ya kuhamishiwa Mafinga JKT.
Kambi ya Mafinga ilikuwa na kikundi cha sanaa na Mbwilo maarufu kama Afande Bright alianza kujifunza kuimba baada ya wenzake kugundua kipaji kikubwa cha muziki alichonacho.
Kipindi kifupi alijipatia umaarufu na kuteuliwa kuwa mwalimu kwa wenzake katika masuala ya utunzi baada ya kutunga nyimbo za Uhamasishaji za 'Mwanzilishi wa JKT' na 'Naipenda Nchi Yangu'..
"Safari yangu kimuziki ilianzia hapo na kujitosa muziki wa kizazi kipya kabla ya mwishoni mwa mwaka jana hasa nilipoteuliwa na Shaibu Issa kujiunga JKT Ruvu nikitokea Rhino ya Mafinga mwaka 2007."

 
KIPAJI
Mwaka 2008 alinyakuliwa na Prisons Mbeya na kupata mafunzo Magereza huku akiichezea timu hiyo katika Ligi Kuu msimu wa 2009 kabla ya kuhamishiwa Iringa.
Akiwa Iringa alijiunga na Polisi Iringa kabla ya kwenda kusomea Ukutubi Chuo cha Sanaa cha Bagamoyo na kuanza kushiriki matamasha ya muziki na kufunguliwa neema.
Matamasha hayo yalimfanya apate nafasi ya kurekodi wimbo wake wa kwanza wa Bongofleva uitwao 'Tanzania' aliomshirikisha Mirror.
Baada ya hapo alirekodi nyimbo nyingine kadhaa zilizokuja kuzaa albamu yake ya kwanza iliyofahamika kama Tanzania iliyokuwa na nyimbo nane.
Baadhi ya nyimbo hizo ni; 'Ndani ya Dancehall', 'Zako Style', 'Kiza Kinene', 'Jakaya', 'Nimedata', 'Hawapendi', 'Watanzania', 'Nikiachwa leo' na 'Leave Me Alone'.
Novemba mwaka alipohitimu Stashahada ya Ukutubi, alirejea kwao Mbeya na kuwa miongoni mwa wachezaji waliojaribiwa na Mbeya City kwa ajili ya usajili.
Hata hivyo kwa namna ya ajabu wakati akiendelea na mazoezi ili kusubiri kutangazwa watakaosajiliwa aliugua ghafla kichwa.

 
MATESO
Mbwilo anayezishabikia Chelsea, Barcelona na JKT Ruvu anasema kichwa kilimpa mateso makubwa, licha ya kuzunguka hospitali kadhaa kubwa ikiwamo ya Aga Khan.
"Mateso niliyopata kwa maumivu ya kichwa yaliyoshindwa kubainika katika hospitali zote nilizoenda kutibiwa kiasi cha kukata tamaa na kutamani kujiua kwa kujirusha ghorafani."
Anasema siku aliyokusudia kujiua ilitokea miujiza kwa kuokolewa na mama zake kabla ya kupelekwa kanisani kuombewa na ndipo ikawa sababu ya kupona kwake na kumpokea Yesu.
"Baadhi ya waumini wa kanisa hilo walibaini mimi nilikuwa mmoja wa waimbaji wa muziki wa kizazi kipya na kunishawishi kumuimbia Bwana na sikuwa na hiyana," anasema.
Anasema kupitia ufadhili wa Papaa Delinson alirekodi albamu nzima ya Asante Bwana yenye nyimbo nane ambazo ameanza kuzitengenezea video kupitia kampuni ya HMC ya mjini Moshi.
Nyimbo za albamu ya msanii huyo anayeshukuru soka kumpa ajira jeshini ni 'Asante Bwana', 'Upendo', 'Vita', 'Hamjui', 'Itakuwaje', 'Twakuheshimu', 'Jinsi Gani' na 'Vita Remix'
Mbwilo anasema ndoto zake kumtumikia Mungu kwa kadri awezavyo ili kurejesha shukrani kwa wema aliomtendea kwa kumuokoa na kifo na tayari ameanzisha kundi liitwalo Makomandoo wa Yesu.
Kundi hilo linalotoa huduma katika makongamano na makanisani linaundwa na wasanii watatu akiwamo yeye (Afande Bright), mdogo wake Robert Mbwilo na Eliah Michael.
Pia anatamani kulitanua kundi hilo na kusaidia wasanii wenye vipaji vya sanaa ili kuisaidia serikali kupunguza tatizo la ajira kwa madai kuwa asilimia kubwa ya vijana kwa sasa wamejiajiri kwenye sanaa.

 
WITO
Mbwilo mwenye ndoto za kufika mbali kisanii anawataka wasanii wenzake kuwa wabunifu na kuacha    kujikita kwenye matumizi ya dawa za kulevya kadhalika wajitambua kama waelimishaji umma.
Pia ameiomba serikali kutunga sheria kali zitakazoweza kumkomboa msanii kupitia jasho lake sawia na kumwezesha kujiweza kisha ndipo wawakamua 'kodi' kinyume na inavyofanyika sasa.
"Huwezi kumkama Ng'ombe bila kumpa malisho, serikali imekuwa ikimbana na kumkamua msanii kupitia stika bila msanii kuanza kukusanya mapato, hii ni ajabu na inakatisha tamaa," anasema.
Mbwilo mwenye mke na mtoto mmoja hupenda kula wali kwa maharage na kunywa Fanta anamshukuru familia yake yote hasa mama yake mzazi Mwalimu Nesi Mziho, Papa Delinson na Enock Masanja wa HMC Production aliyebeba jukumu la kumrekodi video.
"Namshukuru sana Enock Masanja kwa kukubali kubeba jukumu la kurekodi na kusambaza video ya albamu yangu, pia Papaa Denilson na familia yangu nzima kwa kunisapoti kwa hali na mali pamoja na wanasoka wenzangu wote." anasema askari Magereza huyo.

Ni shidaa leo England, Arsenal uso kwa uso na watetezi Man City


KIVUMBI cha Ligi Kuu ya England, kinatarajiwa kuendelea tena wikiendi hii baada ya kupisha michezo ya Kimataifa wiki mbili zilizopita ambapo leo Jumamosi Arsenal itavaana na watetezi Manchester City.
Mwezi uliopita, Arsenal iliichapa Man City Bao 3-0 Uwanjani Wembley kwenye Mechi ya kufungua pazia Msimu mpya kugombea Ngao ya Hisani lakini kwenye Ligi Arsenal wameshinda Mechi moja na kutoka Sare Mechi 2 zilizopita.
Nao Man City walianza kwa ushindi katika Mechi mbili za kwanza lakini kwenye Mechi yao ya mwisho Uwanjani kwao Etihad walitandikwa 1-0 na Stoke City.
Mbali ya Mechi hii, Chelsea, ambao wanaongoza Ligi kwa kushinda Mechi zao zote 3, watakuwa kwao Stamford Bridge kucheza na Swansea City ambao ndio wamefungana nao kileleni na ambao pia wameshinda Mechi zao zote 3.
Lakini Chelsea huenda wakamkosa Straika wao Diego Costa mwenye  mabao manne na aliyeshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi Agosti kutokana na kuwa majeruhi.

RATIBA kamili ipo hivi:
Leo Jumamosi
14:45 Arsenal v Man City
17:00 Chelsea v Swansea
17:00 Crystal Palace v Burnley
17:00 Southampton v Newcastle
17:00 Stoke v Leicester
17:00 Sunderland v Tottenham
17:00 West Brom v Everton
19:30 Liverpool v Aston Villa
Kesho Jumapili
18:00 Man United v QPR
Jumatatu
22:00 Hull v West Ham

Steve Nyerere abwanga manyanga Bongo Movie Unity kama Mtitu

http://api.ning.com/files/ZZRe-BUg83mT6Wyu86ZmDINS*-9-PEciDm-LquUgZ8-ItEbclBzA4sJFyXnJzi40YGDHA2Fg4GGg3Ljg2km*PE0f884ZqnJu/SteveNyerere_full.jpg 
MUIGIZAJI na mchekeshaji anayenakili sauti za watu mashuhuri, Steve Nyerere aliyekuwa Rais wa Klabu ya Bongo Movie Unity ameamua kujiuzulu nafasi hiyo.
Steve ameeleza uamuzi wake kupitia Instagram bila kutoa sababu zilizopelekea kujiuzulu kwake.
“Napenda kuwashkulu ndugu zangu wote wasaniii wenzangu kaka zangu mama zangu rafiki zangu mimi pamoja na family yangu nimeamua kujiuzuru uongozi wa bongo move nabaki kuwa mwanachama wa kawaida naimani tulifurahi pamoja tukauzunika pamoja na daima tutakuwa pamoja.” 
Uamuzi wa Steve Nyerere umepokelewa kwa hisia tofauti na wapenzi wa filamu za kitanzania ambao wengine wamemtaka kutofanya hivyo huku wakitaja ‘majungu’ na kusemwa kama chanzo cha yote.
“Khaaaaaaa asa @stevenyerere2 kujihuzur sio suluhisho la tatizo kaanza willy umefata ww sasa c kamat nzima itajiuzur!?? Why mnashindwa kukaa km wasanii mkasuluhisha penye makosa mambo yakaendelea? Majungu yapo kila sehem kusemwa kupo kila sehem @stevenyerere2 mnapoelekea bongomovie kila mtu atakaa mwenyewe wallah.” Ameandika shabiki anaetumia jina la Neyjd.

Yanga wakubali yaishe kwa Twite yawaita Fc Lupopo mezani

http://api.ning.com/files/3I-9LvQkoOSAPbzeGPW5yP6OSfiIe*zDKxvTvEruLBnPGhxkE3j8HJX2IRwtbIWsugVPQAhAda5j3SU7tPM2CI5dsqk6mOCF/MBUYUTWITESALAMAJAMANIPIXNO5.jpg
Mbuyu Twite
UONGOZI wa klabu ya Yanga umesema umeshangazwa na wenzao wa timu ya a FC Lupopo ya JK Kongo kudai Mbuyi Twite alijiunga nao kwa mkopo, hata hivyo wameamua kuwaita mezani kumaliza mambo kiutu uzima tofautis na tisho la Lupopo kutaka kukimbilia FIFA kushtaki.
Akizungumza na Waandishi wa habari jana, Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Beno Njovu, alisema Yanga haikumsajili Twite kwa mkopo.
Akifafanua zaidi, Njovu, alisema Lupopo inataka ilipwe fedha zaidi mara baada ya Yanga kumuongezea mkataba Twite baada ya ule wa awali kumalizika.
"Mbali na malalamiko mengine ya wenzetu, pia wanataka walipwe pesa baada ya Twite kuongezewa mkataba.. lakini kwenye mkataba hakuna makubaliano kama hayo wakati tunamchukua Twite," alisema Njovu.
Aidha, alisema kuwa ili kuweka mambo sawa, Yanga imewasiliana na viongozi wa Lupopo ambao siku yoyote kuanzia leo watawasili nchini kwa ajili ya mazungumzo.
"Tumewapigia simu hao jamaa na watawasili nchini kuanzia kesho, tutakaa kuwaelewesha na naamini tutaelewana..., ila nataka muelewe kuwa hatukumchukua Twite kwa mkopo," aliongezea kusema Njovu.

Halima Mdee aibuka kidedea CHADEMA, asema la moyoni

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2012/09/HalimaMdee.jpg
MWANASIASA machachari ambaye pia ni Mbunge wa Kawe Halima Mdee CHADEMA amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la wanawake wa Chama hicho (BAVICHA) unaoendelea katika ukumbi wa Mlimani City.
Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Mdee aliwaasa wanawake kwa wanawake kuwa wamoja badala ya kupigana vijembe wao kwa wao ili maendeleo ya mwanamke yaweze kupatina na na kuondokana na mfumo dume
“Nimezoea kuona watu wanaotukashifu ni wa upande wa pili kutokana na mfumo dume uliojengeka na sio wanawake wenyewe kukashifiana,” alisema.
Alisema mwanamke ana nguvu ya kuleta mabadiliko na kueleza kuwa, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kipo madarakani kwa sababu kinawatumia wanawake na kutaka nao kuungana na kuwa kitu kimoja.
“Mwanamke ana nguvu ya kuleta mabadiliko, bila kuwatumia  hakuna ushindi na wanawake siku zote wanamsimamo na sio wasaliti hata kidogo,” alisema Mdee.
Aidha aliwataka wanawake wakafanye kazi majimboni kwa umoja licha ya kufahamu wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa fedha.
“Harakati zetu sio za starehe na hata ikiwezekana pindi mnapokuwa majimboni bila kujali mnalala wapi, mnatumia choo cha ‘pasipoti size’ ili mradi ushindi unapatikana,” alisema.
Akitangaza matokeo hayo katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam jana, Arcado Ntagazwa, alisema Mdee alipata kura 165 akifuatiwa na Janeth Rithe 35, Sophia Mwakagenda 18, Chiku Abwao 15, Lilian Wassira 11 na Rebecca Magwishe kura 4.
Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti upande wa Bara, alitangazwa Hawa Mwaifunga aliyejinyakulia kura 136 akifuatiwa na Victoria Benedict kura 99.
Nafasi ya Makamu Mwenyekiti Zanzibar ilichukuliwa na Hamida Abdalah Huewishi aliyepata kura 194 akifuatiwa na Mariamu Msabaha kura 36.

Hivi ndivyo wahitimu wa la 7 Brain Trust School walivyoagwa jana

Skauti walioongoza maandamano wa kuingia kwenye eneo la tukio
Ni wakakamavu kudhihirisha ni mashujaa wa kesho
Kwa mwendo wa pole mbele tembeaaaaaa!

Matarumbeta yalikuwapo kusapoti sherehe hizo
Wahitimu wakielekea kwenye eneo la tukio



Maandamano fulani ya kuonyesha furaha yao ya kuhitimu Darasa la Saba
Mkuu wa Shule ya Msingi, Neville Marandu akizungumza machache, huku Mkuu wa Shule za Brain Trust, Irene Makinda (pembeni yake kulia) akiwa bize


Hawa nao walikuwapo kushuhudia kila kitu kwa umakini zaidi
Baadhi ya wazazi na walezi waliohudhuria sherehe hizo jana Yombo Vituka

Wazazi na walezi wakiwa makini kufuatilia kila tukio katika mahafali hayo
Hakuna aliyetaka kupitwa na jambo au asimuliwe na mtu



Gift Marandu akisoma shairi mbele ya hadhira kwa umahiri mkubwa

Kama Mwanamalenga katika ughani mashairi
Dada zao wa Sekondari nao walikuwapo kuwapa mkono wa kwaheri

Kwa herini wadogo zetu, heri twawatakia, makini muwapo makwenu....
Dada zao wa Sekondari wakiendelea kuwaburudisha kwa kuwaimbia ngonjera na nyimbo

Ikawa zamu ya wahitimu wenyewe kuingia kilingeni kuonyesha umahiri wao
Kwa kujiamini wahitimu wakiingia uwanjani kuangusha burudani la mwisho mwisho


Kazi ikaanza kwa kuimba wimbo
Wakaangusha na ngonjera

Mashairi pia yalikuwapo
Wahitimu wa Elimu ya msingi wa Shule ya Brain Trust wakiendeleza kutoa burudani

Samuel Robert (kulia) akawaongoza wenzake kuangusha njongera
Dogo achana naye ana kipaji cha kughani acha bhana!


Kwa mbwembwe ndiyo kabisaaaaa
 

Ikawa zamu ya mwanadada naye kuonyesha makeke yake

Skauti nao wakaingia uwanjani kuonyesha umahiri wao katika sanaa hiyo
Hayaaaa twende

Ni nyuma geuka, kulia geuka kwa ukakamavu kama maafande
 






Ikaja zamu ya mwnafunzi huyo wa Chekechea Mereciana Ronald ambaye aliangusha burudani ya kufa mtu
Anacheza kwa pozi taratibu kama hataki

Kadri mzuka ulivyokuwa ukimpanda ndivyo alivyoongeza makeke kwa kunengua muziki
 

Akachanganya kasi we kama Aisha Madinda

Hapo chachaaaa! Yebaaaa
Mkuu wa Shule ya Msingi Brain Trust, Neville Marandu akisoma wasifu wa shule
Mgeni rasmi ikafika zamu yake kutoa nasaha zake ni Richard Mngomo wa Tanzania Printers
Msiridhike na kumaliza kwenu la Saba bado mna kazi kubwa mbele yenu, ndivyo alivyowanasihi wahitimu
Wahitimu wakaanza kukabidhiwa vyeti vyao

Immaculata Justine Limonga, naye alitunukiwa cheti na mgeni rasmi wa mahafali hayo
Ilikuwa furaha kwa wahitimu baada ya kukabidhiwa vyeti vyao
Immaculata Justine akiwa katika picha mbalimbali na familia yake baada ya kukabidhiwa cheti cha kuhitimu darasa la saba katika shule ya Brain Trust

Anafanyiwa surprise
 

Pokea keki ya zawadi mwanangu

Mdogo mtu anampokea keki ya zawadi

Daa nitaifaidije hiii
Akifurahia zawadi ya Mwanafunzi Mwenye Nidhamu na Msafi kuliko wote Brain Trust School