STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 29, 2016

Waganda kuziamua Taifa Stars v Harambee Stars

NA ALFRED LUCAS, NAIROBI
WAAMUZI watatu wa soka kutoka Uganda, ndio wakaochezesha mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Taifa Stars ya Tanzania na Harambee Stars ya Kenya utakaofanyika leo Jumapili kwenye  Uwanja wa Moi Kasarani jijini Nairobi, Kenya.
Waamuzi hao watakaochezesha mchezo huo utakaoanza saa 10.00 jioni na kurushwa moja kwa moja na Kituo cha Televisheni cha Azam Tv kwa kushirikishi na Shirika la Utangazaji la Kenya (KBC) ni Brian Nsubuga atakayepuliza kipenga na wasaidizi wake ni Bugembe Hussein upande wa kulia (line 1) na Katenya Ronald kwa upande wa kushoto (line 2).


Kamishna wa mchezo atakuwa Amir Hassan kutoka Somalia ambako Meneja wa Uwanja wa Moi Kasarani, Lilian Nzile amesema kwamba mazingira uwanja ni mazuri na mipango yote ya mchezo huo imekaa vema ikiwa ni pamoja na usalama uliothibitishwa pia na Kanali wa Jeshi la Polisi, Muchemi Kiruhi OCS wa Kasarani.

Kwa upande wa Kocha Mkuu Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro inayozalishwa na Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL), Charles Boniface Mkwasa atawakosa washambuliaji wake watatu katika kikosi ambacho kitaivaa Harambee Stars.

Washambuliaji hao ni Mbwana Samatta kutoka Genk ya Ubelgiji, Thomas Ulimwengu anayechezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC) na John Bocco ambaye ni majeruhi wa mguu aliumia wakati wa fainali za Kombe la FA kati ya Yanga na Azam Jumatano wiki hii.

“Madaktari wamempa Bocco saa 72 za mapumziko. Bila shaka kabla ya kucheza na Misri atakuwa amepona,” alisema Mkwasa leo Mei 28, 2016 asubuhi na kuongeza kuwa Samatta ametuma taarifa kukosa mchezo dhidi ya Kenya kwa kuwa ana ratiba ya kucheza mchezo muhimu Mei 30, mwaka huu na matarajio ni kujiunga na timu Juni 1, 2016 kabla ya kuivaa Misri Juni 4, mwaka huu.

Kwa upande wa Ulimwengu, uongozi wa TP Mazembe nao waliomba kumtumia Ulimwengu katika mchezo wa ushindani wa mpinzani wake AS Vita. TP Mazembe na AS Vita ni timu pinzani huko DRC Congo na uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ukaridhia na Mkwasa sasa amejipanga kukiandaa kikosi bila nyota hao mahiri.

“Katika mchezo huu sitakuwa na professionals (wachezaji wa kulipwa),” alisema Mkwasa ambaye jioni ya leo ameahidi kutoa kikosi cha nyota 11 watakaonza dhidi ya Kenya kesho.

Kwa sasa anaangalia namna ya kuipanga vema safu yake ya ulinzi baada ya kumkosa Kelvin Yondani anayetumikia adhabu ya kuonywa mara mbili kwa kadi ya njano hivyo kutojumuishwa kwenye mipango mchezo dhidi ya Misri. Mabeki anaotarajiwa kuanza nao ni Juma Abdul upande wa kulia na Mohammed Hussein upande wa kushoto.

Walinzi wakaoachukua nafasi ya Yondani na Nadir Haroub Cannavaro ambaye hakuongozana na timu katika safari ya Kenya ni Erasto Nyoni, Aggrey Morris na David Mwantika huku viungo wa kati wanaotarajiwa kupangwa ni Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude na pembeni ni Farid Mussa na Shiza Kichuya. Washambuliaji watakaotikisa Kenya katika mchezo wa kesho ni Elisu Maguli na Ibrahim Ajib.

“Kipa anaweza kuanza Dida (Deo Munishi) au Aishi Manula. Lakini hao niliokutajia ni proposed team (kikosi tarajiwa), lakini hasa nani anaaza kesho nitakutajia jioni ya leo mara baada ya mazoezi pale Moi Kasarani,” alisema Mkwasa aliyeonekana kujiamini na mipango yake kama lilivyo jina lake la umaarufu la Master.

“Nimeiandaa timu kucheza mifumo miwili ambayo ni 4-3-3 ambao ni mfumo wa kushambuliaji na pale tutakapokuwa tuna-defense (tunazuia) basi mfumo utakuwa ni 4-5-1,” alisema Mkwasa.

Katika mchezo wa kesho Mkwasa anayesaidia na Hemed Morocco na Manyika Peter anayewanoa makipa atapata nafasi ya kubadili wachezaji hadi sita ambao ni utaratibu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kwa mechi za kirafiki za kimataifa kadhalika makubaliano katika mkutano wa kabla ya mchezo wa kesho.

Stars iliwasili Nairobi, Kenya jana asubuhi na kupokewa na wenyeji Shirikisho la Soka Kenya iliyowapeleka hoteli ya Nairobi Safari Club iliyoko mtaa wa Koinange, katikati ya jiji la Nairobi ambako mchana kabla ya kwenda mazoezi ilitembelewa na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dk. John Haule aliyewahakikishia usalama  timu hiyo licha ya kuwako kwa taarifa za kuvamiwa.

“Msaada wowote mnaotaka na chochote mnachohitaji tunaomba mtutaarifu tujue namna ya kuwasaidia. Msiwe na wasiwasi kabisa. Hata kama hamjaipenda hoteli, semeni,” alisema Dk. Haule ambaye aliitakia timu mafanikio mazuri katika mchezo wa dhidi ya Harambee na ule wa Mafarao wa Misri.

Viongozi wa msafara wa Taifa Stars, Ahmed Mgoyi na Omar Walii walimweleza Balozi DK. Haule kuridhika na kambi na kwamba hawakupata tatizo lolote hali ilivyo hadi sasa.

Real Madrid vidume Ulaya, yaikandamiza tena Atletico

http://theblogfc.com.au/wp-content/uploads/2014/08/real-madrid-champions-league.jpg KLABU ya Real Madrid usiku wa kuamkia leo Jumapili, imefanikiwa kutwaa taji lake la 11 la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuilaza kwa mikwaju ya penalti 5-3  mahasimu wao, Atletico Madrid.
Real na Atletico zilimaliza muda wa dakika 120 zikiwa nguvu sawa ya kufungana bao 1-1 katika mchezo mkali wa fainali uliochezwa Uwanja wa San Siro, Milan, Italia.
Kipa Keilor Navas Gamboa alijitanua vizuri langoni na Juan Francisco Torres Belen ‘Juanfarn’ akaona lango dogo na kugongesha nguzo ya pembeni penalti ya nne ya Atletico.
Cristiano Ronaldo akaenda kwa kujiamini kupiga penalti ya mwisho ya Real Madrid na kumtungua kipa Jan Oblak wa Atletico kuwapa Magalactiico taji la 11 la Ligi ya Mabingwa.
Wengine waliofungaa penalti za Real Madrid ni Lucas Vazquez, Marcelo, Gareth Bale na Sergio Ramos, wakati Atletico zimefungwa na  Antonio. Griezmann, Gabi na Saul.
Nahodha wa Reald Madrid, Sergio Ramos akiinua taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuifunga Atletico Madrid kwa penalti 5-3 usiku huu Uwanja wa San Siro PICHA ZAIDI GONGA HAPA   

Mchezo huo uliochezeshwa na marefa wa England, Mark Clattenburg aliyesaidiwa na Simon Beck na Jake Collin, Real Madrid walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa beki wake na Nahodha, Sergio Ramos dakika ya 15 aliyemalizia mpira wa kichwa wa winga Gareth Bale.
Baada ya bao hilo, Real waliuteka mchezo na kupeleka mashambulizi mengi langoni mwa Atletico, lakini bahati haikuwa yao.
Kipindi cha pili, kocha Diego Simeone wa Atletico alianza na mabadiliko, akimpumzisha kiungo Muargentina mwenzake Augusto Matias Fernandez na kumuingiza kiungo Mbelgiji Yannick Ferreira Carrasco.
Mabadiliko hayo yalikuwa msaada kwa kikosi cha Simeone, kwani ni Carrasco aliyekwenda kuisawazishia Atletico dakika ya 79, akimalizia pasi ya Juan Francisco Torres Belen, maarufu kama Juanfran.
Bao hilo ‘likauamsha’ upya mchezo huo, timu zote zikicheza ka nguvu na kasi kusaka bao la ushindi, lakini dakika 90 zikamalizika kwa sare ya 1-1.
Awali ya hapo, mshambuliaji hatari wa Atletico Madrid, Antonio Griezmann alipaisha mkwaju wa penalti dakika ya 48 baada ya Fernando Torres kuangushwa na Pepe kwenye boksi.
Kocha Mfaransa, Zinadine Zidane aliwapumzisha Karim Benzema, Daniel Carvajal na Toni Kroos kipindi cha pili na kuwaingiza Isco, Danilo na Lucas Vazquez.
Katika dakika 30 za nyongeza timu zote zilicheza kwa tahadhari mno na mwishoni mwa mchezo, Simeone akawatoa Filipe Luis na Koke na kuwaingiza Lucas Hernandez na Thomas Teye Partey.
  Kwa ushindi huo Real inafikisha mataji 11 ya Ligi ya Mabingwa, mengine ikitwaa misimu ya 1955–1956, 1956–1957, 1957–1958, 1958–1959, 1959–1960, 1965–1966, 1997–1998, 1999–2000, 2001–2002 na 2013–2014.

Saturday, May 28, 2016

United? Mawe subiri mshtukizwe na Zlatan Ibrahimovic


http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2014/0605/fc_ibrahimovic_rh_1296x729.jpg&w=738&site=espnfcMSHAMBULIAJI wa KImataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic amekuwa akihusishwa na kutaka kutua Manchester United ili kuungana na Kocha wake wa zamani, Jose Mourinho, lakini wakala wake wamesema klabu atakayojiunga nayo itashangaza wengi.
Wakala wa mchezaji huyo, Mino Raiola, alisema Straika huyo ambaye mkataba wake na PSG imeisha hakuna anayejua atatua wapi na hivyo mashabiki wasubiri kushtukizwa tu.
Nahodha huyo wa Sweden mwenye miaka 34, kwa sasa anaendelea na maandalizi ya kuiongoza timu yake katika michuano ya Fainali za Kombe la Ulaya itakayoanza Juni 10 nchini Ufaransa.
"Sidhani kama atajiunga na United, na wala hakuna anayelala Sweden kwa sasa hakuna anayejua kitakachotokea," alisema Raiola.
Wakala huyo alisema bila shaka mwisho wa yote watu watashangazwa na maamuzi ya mkali huyo kwa klabu atakayojiunga nayo kwa msimu ujao.
"Bado hatuajamua, lakini itashangaza wengi mwishowe. Watu wanazungumza kuhusu United, ila ukweli utafahamika tu na ndio maana hatusemi mengi kwa waandishi wasubiri waone wenyewe," alisema wakala huyo.

Mascherano, Higuain wajipa tumaini kwa Messi Copa America 2016

http://static.dnaindia.com/sites/default/files/styles/half/public/2016/05/28/465312-messi-injury.jpg?itok=WVjhADzW
Messi akisaidiwa kutoka uwanjani jana Ijumaa alipoumia katika mechi yao ya kirafiki dhidi ya Honduras
HOFU tupu. Kuumia kwa nyota wa Argentina, Lionel Messi kumezua hofu miongoni mwa wachezaji wa timu yake ya taifa inayojiandaa na fainali za michuano ya  Copa America zitakazoanza mwezi ujao nchini Marekani.
Javier Mascherano na Gonzalo Higuain kwa nyakati tofauti wamenukuliwa wakisema kuwa wana matumaini nahodha wao huyo, Lionel Messi atakuwa fiti kabla ya kuanza kwa fainali za Copa America 2016.
Messi aliumia jana Ijumaa katika mechi za kirafiki ya kimataifa dhidi ya Honduras na kusababisha hofu kubwa kwa wachezaji, mashabiki wa Argentina.
Mwanasoka huyo bora wa dunia, alitolewa Uwanjani baada ya kudondoka vibaya na kujiumiza mgongo na mbavu zake kwenye mjini San Juan waliposhinda bao 1-0.
Kocha Mkuu wa Argentina, Gerardo Martino alisema yu tayari kupokea taarifa zozote juu ya majeraha ya Messi, wakiwa wanakabiliwa na mchezo wa ufunguzi dhidi ya watetezi Chile Juni 6.
Hata hivyo mchezaji mwezake wa Barcelona Javier  Mascherano amesema anatumaini Messi atapona haraka na kurejesha Uwanja kwa ajili ya michezo ya Copa America.
Kauli kama hiyo ilitolewa pia na mfungaji wa bao pekee katika mchezo huo wa Honduras, Gonzalo Hiuguain, alisema anaamini tatizo lililompata nyota wao halitakuwa kubwa kiasi cha kumkosa kwenye michuano hiyo migumu.

Spurs yakimbilia Wembley kwa Uefa Champion League ijayo

https://static.guim.co.uk/sys-images/Sport/Pix/columnists/2015/1/28/1422488355275/tottenham-010.jpgKLABU YA Tottenham Hotspur imetangaza kuwa itacheza mechi zake za Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani kwenye Uwanja wa Wembley.
Spurs ipo katika maandalizi ya kuukarabati Uwanja wao wa White Hart Lane, hivyo imeona ni vema mechi zake za UEFA ikacheza. katika Uwanja huo wa Taifa wa Uingereza wa Wembley.
Timu hiyo iliyomaliza Ligi Kuu ya England msimu huu kwa kushika nafasi ya tatu imethibitisha taarifa hizo leo Jumamosi kwa sababu ya upishaji wa matengenezo na upanuzi wa uwanja wao.

Chama cha Soka cha Uingereza (FA) kimewapa ofa pia timu hiyo kucheza mechi zao zote za Ligi Kuu za nyumbani na na zile michuano mingine ya makombe ya Uingereza kwenye Uwanja huo wa maarufu wa Wembley.

'Juventus? Hapana Dani Alves hajasaini bhana!'

http://static.pulse.ng/img/football/origs4099488/8810481433-w980-h640/danialves-cropped-nghtlocydwb61j2jec4boxnqp.jpgWAKALA wa beki kisiki wa Barcelona, Dani Alves amekanusha taarifa kuwa mteja wake amesaini mkataba wa awali na Juventus, japo amekiri kuwa mabingwa hao wa Italia na klabu nyingine zinamwinda mchezaji huyo. 
Vyombo vya habari nchini Hispania viliripoti juzi kuwa beki huyo wa Barcelona anatarajiwa kuondoka baada ya kutimukia timu hiyo kwa miaka nane na kwenda Turin kwa mkataba wa miaka mitatu. 
Hata hivyo, wakala wake ambaye pia amewahi kuwa mke wake, Dinorah Santa Ana da Silva alikanusha taarifa hizo akidai hazina ukweli wowote. 
Dinorah aliongeza kuwa hakuna klabu yoyote ambayo Alves aliyosaini nayo mpaka sasa kwani amehamishia nguvu zake zote katika timu ya taifa ya Brazil ambayo inakabiliwa na michuano ya Copa America inayotarajiwa kuanza mapema mwezi ujao. 
Wakala huyo aliendelea kudokeza kuwa, ni kweli amekutana na Juventus lakini sio wao peke yao bali ameshakutana pia na klabu nyingine, ila hakuna dili lolote lililoafikiwa mpaka sasa.

Kocha Benitez akomaa na Newcastle United 'mchangani'

Benitez Akisaini Mkataba huo wa kumweka Newcastle United Miaka 3Wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari juu ya kuongeza Miaka 3 kuifundisha Klabu hiyo ya Newcastle UnitedKwenye Mkutano na Waandishi huko St. James Park
KOCHA Rapa Benitez amesaini mkataba wa miaka mitatu wa kuendelea kuinoa Newcastle United licha ya klabu hiyo maarufu England kushuka daraja msimu huu.
Benitez alisaini mkataba huo baada ya mkataba wake wa muda mfupi wakati akipambana kuiokoa Newcastle isizame kumalizika. Kocha huyo ameahidi kuirejesha timu hiyo Ligi Kuu ya England akiamini alicheleweshwa kukabidhiwa timu wakati ikiwa na hali mbaya. VIjana hao wa Benitez walimaliza msimu kwa kutoa kipigo kitakatifu kwa Tottenham Hotspur na kuinyima nafasi ya kumaliza ikiwa ya pili na badala yake kuwaacha mahasimu wao wa London ya Kaskzini, Arsenal wakiibamba nafasi hiyo nyuma ya Leicester City walikuwa mabingwa wapya wa England.

Simba jeuri bwana, yamlipa Mosoti na kuwaokoa Wakimataifa

http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/02/musoti.jpg
Mosoti
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEijkioCMLTxbWmSc7Or2shgbE674AVVOh8YREydnX4Y5pvner4ydWT610U0c1usyjR8IfbiAf_g6S3i-E4u_ylGIZCrsSr_-gUGX0_JaOfiXiQo9pb9KI0WWeEJyEj_SnYTR4TR7HnQCUGb/s1600/HANS+POPPE.jpg
Zakaria Hanspoppe
YAEPUSHA ugomvi. Klabu ya Simba imemaliza utata baada ya kumlipa chake, aliyekuwa beki wao wa kati, Mkenya Donald Mosoti na kujiepusha kushushwa daraja na pia kuikoa Tanzania isifungiwe na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).
Simba imemlipa Mosoti fedha zake za malimbikizo ya usajili na fidia nyingine zinazokaribia Sh Milioni 64.2 Mei 19 mwaka huu ikiwa ni wiki moja na ushei kabla ya siku ya mwisho waliyopewa na FIFA kabla ya kuchukuliwa hatua za kukiuka maamuzi ya Baraza la Usuluhishi la klabu Shirikisho hilo la Dunia.
Kabla ya Simba kulipa fedha hizo ambazo Mosoti amethibitisha kupata taarifa mapema wiki hii, Yanga kupitia Msemaji wake, Jerry Muro, ilitaka Simba iwapelekee nyaraka za deni inalodaiwa na Mosoti ili walipe kupitia Mamilioni ya fedha walizovuna kupitia michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika hatua ya makundi.
Siku chache baada ya Muro kutoa kauli hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, Zakaria Hans Poppe alisema klabu yao ina uwezo wa kulipa fedha hizo na isingehitaji msaada kutoka kokote.
Mosoti aliiburuza Simba FIFA kutokana na kuvunja mkataba wake wa kuichezea klabu hiyo kienyeji na hata ilipotolewa hukumu ya kumlipa Mkenya huyo, Simba ilipuuza ndipo mapema mwezi huu FIFA iliiagiza TFF kuilazimkisha Simba imlipe Mosoti ndani ya mwezi mmoja la sivyo Iishushe Daraja na yenyewe (TFF) itafungiwa kwa michuano ya kimataifa, jambo ambalo lingeizuia Yanga kucheza hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho.

Friday, May 27, 2016

Ratiba nzima ya Yanga na wenzake Kombe la Shirikisho Afrika


Yanga kikosi
Mashabiki

 Round 1

June 17
FUS RabatAl Ahly Tripoli


Kawkab MarrakechEtoile Sahel


MazembeMedeama


MO BejaiaYoung Africans
Round 2

Juni 28 Al Ahly TripoliKawkab Marrakech


Etoile SahelFUS Rabat


MedeamaMO Bejaia


Young AfricansMazembe
Round 3

Julai 15 Etoile SahelAl Ahly Tripoli


Kawkab MarrakechFUS Rabat


MO BejaiaMazembe


Young AfricansMedeama
Round 4

Julai 26 Al Ahly TripoliEtoile Sahel


FUS RabatKawkab Marrakech


MazembeMO Bejaia


MedeamaYoung Africans
Round 5

Agosti 12Al Ahly TripoliFUS Rabat


Etoile SahelKawkab Marrakech


MedeamaMazembe


Young AfricansMO Bejaia
Round 6

Agosti 23FUS RabatEtoile Sahel


Kawkab MarrakechAl Ahly Tripoli


MazembeYoung Africans


MO BejaiaMedeama

Kijana anusurika kufa kwa kujirusha kutoka mnara wa simu

Kijana Mmoja (picha) Jijini Mwanza amenusurika kifo baada ya kujirusha kutoka katikati ya mnara wa simu.
Tukio hilo limetokea hii leo na kuvuta watu wengi waliofika kumshuhudia kijana huo ambae amepanda katika mnara huo tangu majira ya asubuhi na kukatalia mnarani hadi majira ya saa sita mchana.
Mashuhuda wa tukio hilo ambao pia ni marafiki wa karibu na kijana huyo, wamesema huenda kijana huyo amefikia maamuzi hayo kutokana na ugumu wa maisha ambao amekuwa akiulalamikia huku wengine wakisema ni kutokana na kuathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya ikiwemo gundi ambayo amekuwa akiyatumia.
Akizungumza kwa niaba ya Kamanda wa jeshi la uokoaji na zima moto mkoani Mwanza, mmoja wa maafisa wa uokoaji Mussa Kaboni, amsetoa rai kwa makampuni yenye minara ya simu kuimarisha ulinzi katika minara hiyo ili kuondoa hatari inayoweza kujitokeza kutoka kwa raia wasio wema.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walionekana kuchukizwa na kitendo cha kijana huyo na kusikika wakifoka kwa hasira na makelele ya hali ya juu "rukaa, ruka sasa, jirushe kama wewe ni mwanaume" hali ambayo ilikuwa ikimuongezea morari kijana huyo na hivyo kujirusha kweli kutoka katikati ya mnara huo.
Baada ya kijana huyo kujirusha kutoka katikati ya mnara hadi chini, alipoteza fahamu na kukimbizwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mwanza, Sekour Toure kwa ajili ya huduma ya kwanza.
Credit:Mwanaharakati Mzalendo

Fomu za Uchaguzi Yanga zadoda Karume

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrzE3bbtu7GRPgGN93LhICuCjwQRZE3vqY_pGiWVkAF9jOSdE1Vzs2La-FJH2SHaflrratFARxI8Kpk9nWsIf5KHY24cksHhFC4MeNgvfpBsCC8hqwZR4sJoE1lsIf5F2cNVttMU0iWYcp/s1600/Page+2.JPG
Manji (kati)n akitetea na Cannavaro na Chuji misimu kadhaa ya nyuma ya Ligi Kuu Bara
FOMU za Uchaguzi Mkuu wa Yanga zimesuswa baada ya kushindwa kujitokeza hata mwanachama mmoja wa klabu hiyo kuchukua ili kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.
Kamati ya Uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ilitangaza leo Ijumaa ndio siku ya kufunguliwa kwa zoezi hilo, lakini mpaka jioni hii hakuna aliyejitokeza, huku kukiwa na taarifa kwamba Yanga wameugomea uchaguzi huo.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Alloyce Komba amedokeza kuwa, hakuna aliyejitokeza kuchukua fomu, lakini akiamini muda bado kwani wana siku 5 za zoezi hilo kufikia tamati.
Hata hivyo MICHARAZO imenasa taarifa kuwa, uchaguzi huo umesuswa na wana Yanga baada ya kutaka usifanyike kipindi hiki ambacho klabu yao itakuwa kwenye pilikapilika za kuelekea kwenye mechi zao za kimataifa ya Kombe la Shirikisho.
Yanga imepangwa Kundi A na timu za MO Bejaia ya Algeria, TP Mazembe ya DR Congo na Medeama ya Ghana na itaanza mechi zao siku mbili kabla ya kuvaana na Bejaia mjini Algiers, Algeria.
Uchaguzi wa Yanga umepangwa kufanyika Juni 15, lakini uongozi wa klabu hiyo ukitaka ufanyike tarehe moja na uchaguzi wao mdogo uliofanyika Julai 15, 2012 na kumuingiza Mwenyekiti na tajiri wao, Yusuf Manji.

Ronaldo kwa vijembe hajambo, awakejeli Barcelona kimtindo

http://u.goal.com/2890500/2890552.jpgHEBU msikieni CR7. Straika nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amesema kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya itakuwa na thamani kubwa zaidi kuliko mataji mawili yaliyonyakuliwa na wapinzani wao, Barcelona msimu huu.
Ronaldo aliye na umri wa miaka 31 aliyekuwa majeruhi katika wiki za karibuni na kumfanya akose mechi ya nusu fainali ya mkondo wa kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester City ni kama amewapiga kijembe wapinzani wao hao.
Hata hivyo juzi aliwaondoa hofu mashabiki wa timu hiyo akidai kuwa atakuwa fiti kwa asilimia 100 kwa ajili ya fainali hiyo dhidi ya Atletico Madrid.
Akihojiwa Ronaldo amesema kama wakishinda taji hillo la Ligi ya Mabingwa itakuwa ni thamani kubwa zaidi kwao kuliko mataji mawili ya Barcelona waliyoshinda hivi karibuni, kwani taji la michuano hiyo ya Ulaya liko katika ndoto za kila mchezaji. Klabu hasimu za jiji la Madrid, Real Madrid na Atletico Madrid zitakutana kesho Jumamosi katika fainali ya tatu zilizozikutanisha timu za Hispania na mechi ya fainali ya pili baina yao baada ya mwaka juzi 2014 kukutana na Real kushinda 4-1.

Kaka akumbukwa Brazil, aitwa kuziba pengo la Costa

http://www.fantasista10.co.uk/wp-content/uploads/2015/03/Kaka-orlando1.jpg
Kaka akiwajibika kwa klabu yake ya Orlando
BADO wamo. Straika mkongwe wa Brazil anayeichezea klabu ya Orlando City, Kaka ameitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi yake kwa ajili ya michuano ya Copa America akichukua nafasi ya Douglas Costa.
Costa mwenye umri wa miaka 25, amepata majeraha ya misuli ambayo yatamfanya akose michuano hiyo maalumu ya kuadhimisha miaka 100 toka kuanzishwa kwake. Kaka mwenye umri wa miaka 34 ameichezea Brazil mechi 91 na kufunga mabao 29 katika kikosi hicho.
Costa alikuwa sehemu ya kikosi cha Bayern Munich ambacho kimeshinda taji la Bundesliga na Kombe la Ujerumani katika msimu wa mwisho wa Pep Guardiola na timu hiyo.
Brazil imepangwa kufungua pazia la Copa America kwa kucheza na Ecuador katika Uwanja wa Rose Bowl huko Pasadena, California Juni 4 mwaka huu, huku mechi zao nyingine mbili za kundi B zitakuwa dhidi ya Haiti na Peru.

Yanga yaibania Simba kucheza kimataifa

Yanga
Simba
 MWAKA wa hasara ni wa hasara tu. Baada ya ndoto za kucheza fainali za michuano ya Nile Basin iliyopangwa kufanyika Sudan kupotea hewani, Simba imeikosa tena fursa nyingine ya kushiriki michuano ya kimataifa mwaka huu.
Simba ilikuwa ikijipa matumaini ya kuwemo kwenye michuano ya Kombe la Kagame iliyopangwa kufanyika kuanzia mwezi ujao nchini, lakini michuano hiyo sasa haitafanyika tena Tanzania baada ya TFF kuchomoa kuiandaa.
Shirikisho hilo la Soka Tanzana, limetangaza kutoandaa michuano hiyo  inayohusisha timu za nchi wanachama wa Shirikisho la Soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), maarufu kama Kombe la Kagame kwa mwaka 2016 kama ilivyopendekezwa.
Sababu za TFF ya kutoandaa fainali hizo ni kwa kubanwa na ratiba ya michuano ya kitaifa na kimataifa.
Awali mkutano mkuu wa CECAFA, uliamua Zanzibar iwe mwenyeji wa michuano ya Kagame.
Baadaye kwa sababu zilizo nje ya uwezo wa ilionekana Zanzibar hawataweza kufanya.
Baada ya hapo TFF ilianza kuangalia uwezekano wa mashindano haya kwa kumshirikisha mabingwa wa 2015/16 ambao ni Yanga.
Kutokana na ratiba ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAFCC) iliyotolewa na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), kipindi ch Juni hadi Agosti, 2016 Yanga watakuwa na kwenye michuano ya CAF hatua ya makundi hivyo ushiriki wao CECAFA utakuwa mgumu ilihali michuano ya CECAFA imepangwa kufanyika Juni na Julai, mwaka huu.
Watetezi wa taji hilo ni Azam na tayari Yanga ilikuwa ikisita kushiriki na kutoa nafasi kubwa kwa Simba kubeba jukumu, lakini kwa hali ilivyo watabidi wasubiri sana.

Dani Alves ainyima ubingwa Real Madrid Ulaya

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2016/05/17/16/344C8FAD00000578-0-image-a-60_1463500208098.jpg
Dani Alves
https://cdn2.vox-cdn.com/thumbor/7-e7Hp4ZSgo6fGmgV0DLxHNGWuQ=/0x25:3000x2025/1310x873/cdn0.vox-cdn.com/uploads/chorus_image/image/49093871/GettyImages-515165792.0.jpg
Atletico Madrid
KUELEKEA kwenye Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itakayochezwa kesho Jumamosi, Beki wa Barcelona, Dani Alves amekiri kuwa angependelea zaidi Atletico Madrid ishinde taji hilo kuliko mahasimu wao Real Madrid.
Atletico na Madrid zitavaana kesho, katika mechi ya kisasi kwea kocha Diego Simeone ambaye alifungwa kwenye fainali ya mwaka juzi na mabingwa hao wa kihistoria wa michuano hiyo ya Ulaya kwa mabao 4-1.
Atletico walio chini Diego Simeone ndio waliowang’oa mabingwa watetezi Barcelona katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kabla ya kuitoa tena Bayern Munich kwenye hatua ya nusu fainali.
Madrid ndio timu pekee iliyopo mbele ya Atletico kwasasa ikiwa ni kama marudiano baada ya ile fainali ya mwaka 2014 ambapo Madrid waliibuka kidedea kwa kushinda mabao 4-1 katika muda wa nyongeza.
Hata hivyo, Alves ana mawazo tofauti katika fainali hiyo itakayofanyika katika Uwanja wa San Siro jijini Milan nchini Italia kwani anadhani Atletico wanastahili zaidi taji hilo kuliko Madrid. Alves amesema Atletico ni timu ambayo imepambana sana mpaka kufikia hapo walipo hivyo anadhani wanastahili taji hilo

Juventus kumng'oa Mascherano Nou Camp

http://ghettoradio.co.ke/wp-content/uploads/2015/10/javier-mascherano.jpgMABINGWA wa Italia, Juventus imepanga kumng'oa Kiungo mahiri wa Barcelona, Javier Mascherano.
Inadaiwa kuwa Muargentina huyo amekubali dili la kujiunga na mabingwa wa Serie A.
Duru za kimichezo zinasema kuwa, nyota huyo wa kimataifa wa Argentina amefanya mazungumzo na Juventus na anajiandaa kuhamia jijini Turin kiangazi hiki.
Mpaka sasa inadaiwa kuwa hakuna makubaliano yoyote kati ya Barcelona na Juventus na mabingwa hao wa Hispania wanahisiwa kutokuwa na mpango wowote wa kumuachia kiungo huyo mwenye umri wa miaka 31.
Mascherano alijiunga na Barcelona mwaka 2010 akitokea Liverpool na kufanikiwa kushinda mataji manne ya La Liga na mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa Camp Nou.

Ufaransa yaapa fainali za Euro 2016

http://gdb.voanews.com/23C9424D-B2D5-4DD1-BDCC-2F282A62DD35_cx23_cy23_cw62_w987_r1_s_r1.jpgUTAWALA wa nchi ya Ufaransa umesema kuwa inatarajia kuweka polisi zaidi ya 60,000 ili kulinda usalama katika michuano ya Euro 2016 itakayopanza Juni 10 wakiapa kuwa watafanya kila wawezalo kuhakikisha wanazuia shambulio lolote la kigaidi katika kipindi chote cha mashindano hayo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi hiyo, Bernard Cazeneuve ndiye aliyetoa kauli hiyo baada ya Uwanja wa Ufaransa uliopo jijini Paris ambao ndio utatumika kwa ajili ya mechi ya ufunguzi na fainali, kuleta rabsha Jumamosi iliyopita kabla ya fainali ya Kombe la Taifa.
Moshi mkubwa uliohisiwa kuwa bomu ulilipuka ndani ya uwanja na kusababisha mashabiki kuchanganyikiwa na kukimbia hovyo kuelekea milango ya kutoka nje ya uwanja.
Akihojiwa Waziri huyo amesema tukio la Jumamosi iliyopita halihusiani na maandalizi yao kwani waandaaji walikuwa tofauti.
Waziri huyo aliongeza kuwa katika michuano ya Euro 2016 inayotarajiwa usalama utakuwa ni kipaumbele chao cha kwanza ili kuhakikisha hakuna tukio lolote hatarishi ya kigaidi litakaloweza kutokea.

Jose Mourinho atambulishwa rasmi Man United

Jose Mourinho poses with a Manchester United shirt after being confirmed as the club's new manager
Jose Mourinho akitua rasmi Man United
YAMETIMIA. Hatimaye klabu ya Manchester United imemtangaza na kumtambulisha rasmi Kocha Jose Mourinho kuwa kocha wao mkuu na kumpa kandarasi ya miaka mitatu.
Mourinho, mwenye miaka 53 ametangazwa na klabuni na kuchapishwa picha akiwa na jezi za klabu yake mpya ambayo ilikuwa ikimsaka tangu alipotemwa Chelsea katikati ya msimu uliomalizika wa EPL.
Kocha huyo alisaini mkataba huo jana jioni baada ya mazungumzo ya siku tatu kabla ya kutambulishwa akiwa kavalia suti kali nyeusi jambo linaloashiria kuwa, Special One sasa ni mali ya Mashetani Wekundu na wapinzani wao wajipange kwa mikakati anayokuja nayo kocha huyo mjuzi.
Moja ya mikakati inayotajwa kuwa mikononi mwa Mourinho ni kumnyakua Willian anayekipiga Chelsea ambaye alinunuliwa na kocha huyo wakati akiinoa klabu hiyo ya The Blues.

Sunday, May 22, 2016

HIVI NDIVYO LIGI KUU BARA 2015-2016 ILIVYOISHA RASMI

Mabingwa Yanga

Simba washindi wa tatu
Majimaji iliyoigomea Yanga mjini Songea
PAZIA la Ligi Kuu Bara limefungwa rasmi jioni hii ikishuhudia timu tatu za jijini la Tanga, Coastal Union, African Sports na Mgambo JKT zikishuka rasmi kwa kushika nafasi tatu za chini, huku Simba ikishindwa kuvunja mwiko wa kukamata nafasi ya pili tangu ilipotwaa ubingwa wake wa mwisho wa Ligi Kuu msimu wa 2011-2012 ikizidiwa ujanja na Azam.
Sports maarufu kama Wana Kimanumanu walilala mabao 2-0 mbele ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Manungu Complex, Turiani Morogoro, wakati Wagosi wa Kaya Coastal ikilala tena mabao 2-0 Mkwakwani Tanga mbele ya Prisons-Mbeya licha ya kwamba ilishashuka mapema katika ligi hiyo.
Mgambo JKT ilishindwa kukomaa kujiokoa kama misimu mitatu iliyopita ilivyopambana baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Azam na kujikuta pointi zake kutotosha kuiokoa isirudi Ligi Daraja la Kwanza baada ya kucheza mfululizo tangu ilipopanda mwanzoni mwa miaka ya 2010.
Simba ikiwa Uwanja wa Taifa ilishindwa kuhimili vishindo vya JKT Ruvu na kulala mabao 2-1 ikiiacha Azam ikitwaa zawadi ya mshindi wa pili nyuma ya Yanga ikiwa msimu wa tano mfululizo kwa Wanalambalamba kutotoka kwenye Mbili Bora ya ligi hiyo tangu mwaka 2011-2012.
Mjini Songea Majimaji ikiwa Uwanja wake wa Majimaji, ililazimishwa sare ya mabao 2-2 na Mabingwa Yanga, huku ikishuhudiwa Ally Mustafa Barthez akifunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu, huku Paul Nonga akiifungia Yanga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu tangu aliposajiliwa katika dirisha dogo mwishoni mwa mwaka jana.
Toto Africans imenusurika kushuka daraja licha ya kufungwa bao 1-0 na Stand United Uwanja wa CCM Kirumba, kama ambavyo Kagera Sugar ilivyoponea kwa Wana Shinyanga wengine Mwadui FC waliowazabua mabao 2-0.
Mbeya City ikiwa nyumbani ilishindwa kulipa kisasi cha kufungwa mabao 4-1 na Ndanda katika mchezo wao wa kwanza mjini Mtwara kwa kutoka suluhu kwenye Uwanja wa wa Sokoine, Mbeya.
Kwa namna msimamo ulivyo, Yanga iliyotwaa ubingwa mbali na kunyakua Kombe na Medali, pia imevuta mkwanja upatao Sh. 81,345,723/= kama washindi wa kwanza, wakati Azam  ikizoa Sh. 40,672,861/= za ushindi wa pili.
Simba yenyewe imevuta donge la Sh. 29,052,044/= kwa kushika nafasi ya tatu wakati Prisons iliyokuwa ya nne ikiipiku Mtibwa Sugar imeweka kibindoni Sh. 23,241,635/=
Kadhalika kumalizika kwa ligi hiyo kumempa nafasi Amissi Tambwe wa Yanga kuibuka kinara wa mabao msimu huu akifunga jumla ya 21 na kujihakikishia zawadi ya Sh. 5,742,940/= mbele ya Hamis Kiiza wa Simba aliyekuwa akiongoza kwa muda mrefu kabla ya kupoteza makali yake.

Matokeo kamili na msimamo wa mwisho wa Ligi hiyo ni kama ifuatavyo;



Msimamo wa Ligi Kuu Bara:

                            P  W   D   L   F    A  Pts

1. Yanga               30 22  7   1  70  20  73

2. Azam                30 18 10  2  47  24 64

3. Simba               30 19  5   6  45  17 62

4. Prisons              30 13 12  5  29  22 51

5. Mtibwa              30 14  8   8  33  21 50

6. Mwadui FC         30 11  8  11 29  29 41

7. Stand Utd          30 12  4  14 28  29 40

8. Mbeya City        30  9   8  13 32  34 35

9. Ndanda             30  7  14  9  28  31 35

10.Majimaji           30  9   8  13 22  40 35

11.JKT Ruvu          30  8   8  14 31  43 32

12.Toto Africans     30  7   9  14 26  40 30

13.Kagera Sugar    30  8   7  15 23  34 31

14.Mgambo           30  6  10 14 24  36 28

15.African Sports   30  7   5  18 13  34 26

16.Coastal Union    30  5  7   18 15  41 22
 
Wafungaji: 
 
21-Amissi Tambwe               (Yanga)
19-Hamis Kiiza                      (Simba)
17-Donald Ngoma                (Yanga)
16-Jeremiah Juma               (Prisons)
15-Elias Maguli                      (Stand)
12- Kipre Tchetche                 (Azam)
10-John Bocco                       (Azam)
     Atupele Green              (Ndanda)
9-  Ibrahim Ajib                     (Simba)
     Shiva Kichuya               (Mtibwa) 
     Simon Msuva                  (Yanga)
 8- Shomary Kapombe          (Azam)
     Fully Maganga            (Mgambo)
 
7- Mbaraka Yusuf              (Kagera) 
    Mussa Kiumbu           (JKT Ruvu)
    Waziri Junior                     (Toto)
       Saady Kipanga          (JKT Ruvu) 
6- Danny Mrwanda         (Majimaji) 
  
  AbdulRahman Mussa (JKT Ruvu)
5-Said Bahanuzi               (Mtibwa)
    Samuel Kamuntu       (JKT Ruvu)
    Miraji Athuman                  (Toto)
    Jerry Tegete                 (Mwadui)
    Thabani Kamusoko         (Yanga)
    Mohammed Mkopi      (Prisons)
    Raphael Alpha                (Mbeya)
    Didier Kavumbagu           (Azam)
   Paul Nonga                       (Yanga)

4- Aziz Gillah                   (Mgambo)
    Juma Abdul                      (Yanga)  
    Edward Christopher         (Toto)
3- Michael Aidan            (JKT Ruvu)
    Haruna Moshi                (Mbeya)
    Pastory Athanas              (Stand)
    Adam Miraj                    (Coastal)
    Kiggy Makassy             (Ndanda)
    Omar Mponda             (Ndanda)
    Peter Mapunda           (Majimaji)
   Danny Lyanga                 ( Simba)
   Babu Ally                        (Kagera)
   Mzamiru Yasin               (Mtibwa)
   Bryson Raphael            (Ndanda)
   Joseph Mahundi            (Mbeya)
   Deus Kaseke                  (Yanga)
   Mudathir Yahya              (Azam)
   Kelvin Sabato              (Mwadui)
   Alex Kondo                   (Ndanda) 
2-Malimi Busungu              (Yanga)
   Ally Myovela                 (Prisons)
   Mohamed Ibrahim       (Mtibwa)
   Ally Shomary                (Mtibwa)
   Fabian Gwanse             (Mwadui)
   Jabir Aziz                      (Mwadui)
   Nassor Kapama             (Coastal)
   Thabit Khamis            (JKT Ruvu)
   Frank Domayo                  (Azam)
   Abslim  Chidiebele       (Coastal)   
   Hamad Mbumba            (Sports)
   Ditram Nchimbi     (Mbeya City)
   Kassim Selembe               (Stand)
   Nizar Khalfan                (Mwadui)
   Juma Mahadhi              (Coastal)
   Paul Ngway                    (Kagera)
   Farid Mussa                      (Azam) 
   Japhet Mkala                     (Toto)
   Chande Magoya         (Mgambo)
   Ally Ramadhani               (Sports)
   Salum Kabunda             (Mwadui)
   Kelvin Yondani                 (Yanga)  
   Salim Mbonde              (Mtibwa)
   Abdallah Juma              (Mbeya)
   Stamili Mbonde          (Majimaji)
   Omar Issa                        (Sports)
   Jumanne Alfadhil          (Prisons)
   Hassan Materema         (Sports)
   Frank William                (Prisons)
   Bolly Ajali Shaibu        (Mgambo) 
   Jaffar Ramadhani             (Toto)