STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 14, 2013


SIMBA, AZAM HAKUNA MBABE, YANGA YAPUMUA KILELENI

 Mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa akichuana na beki wa Azam FC, John David katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilifunga mabao 2-2 (Picha na Habari Mseto Blog)  
 Mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa akimtoka beki wa Azam FC, Joockins Atudo wakati wa mchezo wa Ligi Kuu  Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana. Timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.
 Wachezaji wa Simba wakishangilia baada ya kuapata bao la pili.
Kiungo wa timu ya Simba, Abdallah Seseme akiwatoka wachezaji wa Azam FC, Himid Mao (kulia) na Salum Abubakar wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Timu hizo zimetoka sare ya mabao 2-2.

LICHA ya tambo nyingi kabla ya pambano lao timu za Simba na Azam jioni ya leo zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na kuwafanya vinawa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga kupumua.
Yanga mabo mashabiki wake leo walionyesha kioja kwa kuwashangilia watani zao Simba dhidi ya Azam, wanapumua kwa vile Azam inayowafukuza kwenye mbio za ubingwa imepunguza pengo la pointi moja tu na kuipa nafasi Yanga kuhitaji pointi tano tu kati ya mechi zake nne zilizosalia kutangaza ubingwa msimu huu.
Yanga yenyewe ina pointi 52 wakati Azam waliopo nafasi ya pili wana pointi 47, huku kjwa sare hiyo ya leo Simba imeendelea kusalia kwenye nafasi ya nne akiwa na pointi 36.
Ramadhani Singano 'Messi' ndiye aliyeipa Simba uongozi wa mabao katika pambano hilo lililochezeshwa na mwamuzi Oden Mbaga kwa kufunga mabao mawili katika dakika ya 10 na 14 akimalizia kazi murua iliyofanywa kwa ushirikiano wa Mrisho Ngassa na Haruna Changono.
Dakika ya 29 Kipre Tchetche aliifungia Azam bao la kwanza baada ya Khamis Mcha kuangushwa akielekea kumsalimia kipa Abel Dhaira na kumfanya afikishe bao la 15 msimu huu.
Dakika mbili baadaye kocha wa Azam, Stewart Hall alionyeshwa kadi nyekundu kwa kumtolea lugha chafu mwamuzi kutokana na maamuzi yake na hadi mapumziko matokeo yalikuwa mabo 2-1.
Kipindi cha pili Azam walionyesha uhai zaidi kwa kushambulia lango la Simba na kufanikiwa kupata bao la pili na la kusawazisha dakika ya 72 kupitia kwa Humphrey Mieno.
Kwa matokeo ya pambano hilo lililokuwa likisubiriwa kwa hamu kutokana na tambo zilizokuwa zikitolewa na pande zote mbili na mkasa ulioibuka baada ya mechi yao ya kwanza ambapo Simba walishinda mabao 3-1 na kupelekea Azam kusimamisha wachezaji wake wanne kwa tuhuma za rushwa, msimamo upo hivi;


                                       P     W     D     L     F     A     D     PTS
    1.  Young Africans       22    16     4     2    40    12    28    52
    2. Azam                      23    14     5     4    41    19    22    47    
    3 . Kagera Sugar         22    10     7     5    25    18    7      37     
    4.  Simba                     22     9     9     4     32    21    11    36
    5.  Mtibwa Sugar         23     8     9     6     26    24     2     33   
    6. Coastal Union          22     8     8     6     23    20     3     32    
    7.  Ruvu Shooting         23     8     6     9     21    22    -1    30     
    8.  JKT Oljoro FC       23     7     7     9     22     27    -5    28     
    9. Tanzania Prisons       24     6     8    10    14     21    -7    26    
    10.JKT Mgambo         22     7     3     12    14     22    -8    24
    11.Ruvu Stars              21     6     4     11     19     34   -15   22
    12. Toto Africans         24     4    10    10     22     32   -10   22
    13. Polisi Morogoro     23     3    10    10     11     21    -10  19    
    14.  African Lyon         23     5     4     14     16     35    -19  19

WAWILI WAFA KATIKA AJALI KAGERA


 

Magari yaliyohusika na ajali hiyo iliyotokea jana jioni huko Ngara, Kagera

Watu wawili wamefariki dunia  papo hapo na wengine wawili kujeruhiwa baada ya gari aina ya Mercedec benz lenye namba ya usajili T 908 ABZ semitrailer lililokuwa ikitokea nchini Burundi, kuacha njia leo(April 13,2013) muda wa saa 12 jioni na kupinduka katika eneo la Kumuyange nje kidogo ya mji wa Ngara mkoani Kagera.

Kamanda wa Polisi wilaya ya Ngara  Abel Mtagwa amewataja watu hao waliofarki katika ajali hiyo kuwa ni Edward Filimon alie kuwa akiendesha pikipiki yake yenye namba za usajiri T 756 BZJ na abiria wake ambae hadi sasa haja fahamika jina lake.
Kamanda Mtagwa amewataja majeruhi wa ajari hiyo kuwa ni Dereva wa gari hilo Hajji Omary Ibrahim(29) mkazi wa gongolamboto jijini Dar es salaam na tingo wake aliyejulikana kwa jina la Kambi simba(40).
Kamanda Mtagwa ameongeza kuwa katika ajal i hiyo nyumba moja mali ya Bi.Bibiana John (58) imegongwa na gari hilo na kuharibika.
Aidha Kamanda Mtagwa amesema kuwa chanzo cha ajari hiyo ni  gari hilo kufeli  mfumo wa Breki  jambo ambalo Dereva wake alishindwa kulimudu kuliendesha ndipo lilipanda mtaro na kubomoa nyumba hiyo. 
 
Aidha Majeruhi wa Ajali hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Murugwanza wilayani Ngara.
 
CHANZO:MWANA AFRIKA

Simba, Azam. ni vita ya kisasi leo taifa

Simba

Azam

SIMBA na Azam jioni ya leo wanatarajiwa kushuka dimbani kumenyana katika pambano pekee la Ligi Kuu Tanzania Bara inayoelekea ukingoni huku, ambalo limetabiriwa na wengi kama vita ya kisasi baina ya timu hizo.
Timu hizo zitakutana kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kila moja ikiwa na malengo tofauti, Azam kulipa kisasi ya kipigo cha mabao 3-1 ilichopewa kwenye pambano lao la kwanza lililosababisha iwasimamishe wachezaji wake wanne kwa tuhuma za kuihujumu kupitia rushwa.
Simba wenyewe wakaikabilia Azam wakiwa na hasira za kutuhumia na rushwa sakata ambalo lilimalizwa nna Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kabla ya kuibuka ikitaka kulipwa fidia ya Bilioni 1 kwa tuhuma hizo nzzito.
Pia Simba inashuka uwanja wa Taifa ikiwa inataka kulinda heshima yake katika ligi ya msimu huu kutokana nna ukweli imeshatemeshwa ubingwa na ipo hatua chachee kukosa hata nafasi ya uwakilishi wa nchi katika michuano ya Kimataifa mwakani.
Tayari kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' ametamka wazi kwamba wanashuka dimbani leo kwa lengo moja tu la kutaka kulinda heshima yao mbele ya Azam na pia kuhakikisha wanamaliza ligi wakiwa katika nafasi nzuri baada ya kutemeshwa taji.
Azam mbali na kuhitaji kulipa kisasi kwa Simba ikiamini kwamba mechi ya kwanza walifungwa kwa hila, lakini pia inasaka ushindi ili kuifukuzia Yanga kileleni ambayo jana ilitakata kwa kupata ushindi wa mabao 3-0 mbele ya maafande wa JKT Oljoro na kuzidi kujichimbia kwenye nafasi ya kwanza.
Yanga mbali na kuendelea kuongoza na kuongeza pendo la pointi dhidi yake na Azam, pia imejihakikisha nafasi ya kushiriki michuano ya Afrika mwakani mpaka sasa kati ya nafasi mbili za uwakilishi wa nchi.
Kwa kuangalia mazingira hayo, huku Azam wakijinafasi kwamba kiu yao ni kutwaa ubingwa msimu huu na kuweka rekodi, ni wazi pambano la jioni litakuwa ni patashika nguo kuchanika.
Wachezaji wanne waliohusishwa na tuhuma za rushwa baada ya pambano hilo la duru la kwanza, nahodha wa zamani Aggrey Morris, Said Morad, Erasto Nyoni na kipa Deo Munishi 'Dida' tayari wameripoti kambini katika kikosi cha timu hiyo wakielezwa wanaweza kushuka dimbani leo kuwakabili 'Mnyama'.
Hata hivyo kwa mazingira yalivyo huenda ikawa vigumu kwa wachezaji hao kucheza pambano hilo ikizingatiwa kwamba ni Simba hao hao waliowaponza hata kuingia matatani kabla ya kusafishwa na TAKUKURU.
Mashabiki wa soka watakuwa na hamu kubwa ya kuona kipi kitakachotokea katika mechi hiyo baada ya dakika 90 huku macho na masikio yakielekezwa kwa washambuliaji nyota wa Azam, Kipre Tchetche na John Bocco 'Adebayor'.
Tchetche anaangaliwa kutokana na kasi yake ya ufungaji mabao akifunga karibu kila mechi tangu arejee dimbani katika duru la pili, huku Adebayor kwa bahati yake ya kuitungia Simba kila timu hizo zinapokutana.
Bila shaka kujua nani atakayecheza ua kulia leo taifa ni suala la kusubiri kuona baada ya dakika 90 za pambano hilo la kusisimua.

MIUJIZA:ABIRIA ZAIDI YA 100 WANUSURIKA KIFO AJALI YA NDEGE

































  
ZAIDI ya abiria 100 wamenusurika kimiujiza katika ajali ya ndege iliyoanguka muda mfupi baada ya kuruka hewani kando ya pwani ya bali, nchini Indonesia.
Mashuhuda wa tukio hilo lililoikumba ndege ya Lion Jet iliyoanguka ikitoka kuruka kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa Ngurah Rai nje kidogo ya mji wa Denparsar walisema walisema manusura wa ajali hiyo walionekana kuhamanika wakati wakiokolewa kutoka kwenye ndege hiyo iliyozama baharini kwa futi kadhaa.
Inaelezwa ndege hiyo ilikuwa imebebea jumla ya abiria 101 na watumishi wapatao saba wakati ikianguka majini kutoka umbalio wa Mita 50 juu.

Saturday, April 13, 2013

Prisons yazidi kukimbia janga la kushuka daraja


MAAFANDE wa Prisons Mbeya wamezidi kupigana kuepa janga la kushuka daraja baada ya kuinyoa Ruvu Shooting kwa mabao 2-0 katika pambano lililochezwa jioni ya leo mjini Mbeya.

Ushindi huo ni wa pili mfululizo baada ya Jumatano iliyopita kuicharaza Mgambo JKT, ulipatikana kwenye uwanja wa Sokoine na kuifanya Prisons kuchupa kwa nafasi moja toka nafasi ya 10 haid ya 9.
Hata hivyo bado Prisons ina kibarua cha kuhakikisha wanashinda mechi zao mbili zilizosalia dhidi ya JKT Ruvu na Kagera Sugar kujihakikishia kusalia Ligi Kuu msimu ujao.
Habari kutoka Mbeya zinasema kuwa Mabingwa hao wa zamani wa Tanzania walipata ushindi huo kwa magoli ya kipindi cha pili yaliyowekwa yote kimiani na mchezaji wake aliyekuw shujaa leo, Elias Maguli.Maguli alifunga bao la kwanza kwa shuti akiunganisha pasi murua ya mchezaji mwenzake katika dakika ya 53 kabla ya kuongeza jingine dakika tano baadaye kwa mkwaju wa penati baada ya beki mmoja wa Ruvu kuunawa mpira langoni mwake.
Kwa matokleo hayop Prisons imefikisha pointi 26 na kuishuka Mgambo katika nafasi ya tisa na kukalia wao nafasi hiyo.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena kesho kwa pambano kati ya Azam na Simba litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa.

 Msimamo wa Ligi hiyo baada ya mechi za leo jioni;

                                        P     W     D    L     F     A     D     PTS
    1.  Young Africans     22     16    4     2    40   12    +28     52
    2.  Azam                     22     14    4     4    39   17    +22     46    
    3.  Kagera Sugar         22     10    7     5    25   18    +7       37     
    4.  Simba                     21     9     8     4     30   19   +11      35
    5.  Mtibwa Sugar        23      8     9     6     26   24    +2      33   
    6. Coastal Union         22     8     8     6     23    20    +3      32    
    7.  Ruvu Shooting       23     8     6     9     21     22     -1     30     
    8.  JKT Oljoro FC       23     7     7     9     22     27     -5     28     
    9. Tanzania Prisons     24     6     8    10    14     21     -7     26    
   10.JKT Mgambo          22     7     3    12    14     22     -8     24
   11.Ruvu Stars              21     6     4     11    19     34     -15   22
   12. Toto Africans        24     4     10    10    22    32     -10    22
   13.  African Lyon       23     5      4     14    16     35     -19   19
   14. Polisi Morogoro    23     3     10    10    11     21     -10   19    
             

Yanga yaitemesha Simba ubingwa, yaikwangua JKT Oljoro 3-0

Vinara wa ligi kuu Yanga walioivua Simba taji jioni ya leo
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imeendelea kudhihirisha wamepania kutwaa taji la msimu huu baada ya jioni hii kuikwangua JKT Oljoro ya Arusha mabao 3-0 katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Ushindi huo uliopatikana kwa mabao ya kipindi cha kwanza yameifanya Yanga kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 52 na kuivua rasmi Simba ubingwa kutokana na kufikisha pointi 52 ambazo haziwezi kufikiwa na Wana Msimbazi.
Simba ambayo itashula kesho dimbani kuumana na Azam yenyewe ina pointi 35 na kama itashinda mechi zake zote itafikisha pointi 50 tu.
Mabao yalioifanya Yanga kulishika taji la ubingwa kwa mkono mmoja na kusubiri mwingine iwapo Azam wanaowafukuzia watateleza katika mechi zake yaliwekwa kimiani na beki Nadir Haroub 'Cannavaro' katika dakika ya 5 tu ya mchezo kabla ya Simon Msuva kufunga la pili dakika ya 19 na Hamis Kiiza 'Diego' kuongeza la tatu dakika mbili kabla ya mapumziko.
Pambano hilo lililochezeshwa na mwamuzi Amon Paul wa Mara lilihuhudia kadi kadhaa za njano zikitolewa kwenye mchezo huo na mpaka dakika 90 zinamalizika Yanga walikuwa wababe mbele ya maafande hao kwa ushindi huo wa mabao 3-0.

Supersport yakwama kurusha live mechi za VPL

PRESS RELEASE



Na Boniface Wambura
MECHI tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.

Kwa mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.

Mechi hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba, Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17 mwaka huu jijini Tanga.

Tatizo hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi hiyo ya Kenya.

Tshunungwa amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo. SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.

Pia TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport watakuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa.

ZA LEO LEO

Friday, April 12, 2013

Ni vita vya Barca na Bavarian, Chelsea waangukia kwa Basel


MABINGWA wapya wa Ujerumani, Bayern Munich imeangukia mikononi mwa Barcelona katika mechi za hatua na Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, huku wapinzani wao Borussia Dortmund wakipangiwa Real Madrid.
Aidha Chelsea ya Uingereza timu pekee inayoiwakilisha Uingereza imepangwa kukwaruzana na Basel ya Uswiss katika mechi za Nusu Fainali ya UEFA Ndogo, huku Benfica ya Ureno na Fenarbeche ya Uturuki zikipangwa pamoja.
Kupangwa kwa droo hiyo iliyozitenganisha timu hasimu kutoka nchi moja inamaanisha kwamba fainali za mwaka huu ya Ligi ya Ulaya itazikutanisha timu za taifa moja baada ya kipindi kirefu.
Mechi za mkondo wa kwanza zinatarajiwa kucheza kati ya Aprili 23 na 24 na zile za marudiano zitachezwa Aprili 30 na Mei Mosi kabla ya fainali kupigwa uwanja wa Wembley Uingereza Mei 25.
Kwa mechi za UEFA Ndogo mkondo wa kwanza utaanza Aprili 25 na za mkondo wa pili Mei 2 kabla ya fainali Mei 15.
Barcelona watakuwa wageni wa wana fainali za mwaka jana katia mkondo wa kwanza kabla ya kurudiana wiki moja baadaye kwenye dimba lake la Camp Nou, kadhalika Wahispania wengine Real Madrid watasafiri pia Ujerumani kuvaana na wenyeji wao Dortmund kabla ya kurejea nyumbani katika mechi ya mkondo wa pili.
Kwenye mechi za UEFA Ndogo Chelsea wataanzia ugenini sawa na itakavyokuwa kwa Benfica na kurudiana na wapinzani wao kwenye viwanja vyao vya nyumbani dhidi ya Basel na Fenerbeche.

Kivumbi cha VPL kuendelea wikiendi, Simba, Yanga, Azam kuvuna nini?




Na Boniface Wambura
Ligi Kuu ya Vodacom inaendelea kesho (Aprili 13 mwaka huu) kwa mechi mbili zitakazochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, na Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Yanga itakuwa mwenyeji wa Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa wakati Uwanja wa Sokoine utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Tanzania Prisons na Ruvu Shooting.

Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Aprili 14 mwaka huu) kwa mechi kati ya wenyeji Azam na Simba. Mechi hiyo namba 155 itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika hatua nyingine, Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Shelisheli kuchezesha mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho kati ya Azam na AS FAR ya Morocco itakayofanyika Aprili 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Waamuzi hao ni Emile Fred atakayepuliza filimbi akisaidiwa na Steve Maire na Jean Ernesta. Mwamuzi wa mezani (fourth official) atakuwa Jean Claude Labrossa. Kamishna wa mechi hiyo ni Abbas Sendyowa kutoka Uganda.

Wakati huo huo, CAF imemteua Mtanzania Alfred Lwiza kuwa Kamishna wa mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho kati ya Liga Muculmana ya Msumbiji na Wydad Casablanca ya Morocco.

Mechi hiyo itakayochezwa kati ya Aprili 19,20 au 21 mwaka huu nchini Msumbiji itachezeshwa na waamuzi kutoka Zimbabwe wakiongozwa na Ruzive Ruzive.


UJUMBE WA FIFA KUWASILI APRILI 15




Na Boniface Wambura
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kuwatangazia wadau wa mpira wa miguu kuwa ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utawasili nchini Jumatatu (Aprili 15 mwaka huu) kwa ajili ya kushughulikia mchakato wa uchaguzi mkuu wa TFF.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka FIFA, ujumbe huo utaongozwa na Mkuu wa Idara ya Uanachama ya FIFA, Primo Covarro na utafanya kazi kwa siku tatu kuanzia siku ya ujio na kuondoka Aprili 18 mwaka huu.

Ukiwa nchini, ujumbe huo utakutana na wagombea uongozi walioathiriwa na uamuzi wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ambao waliomba mashauri yao yaangaliwe upya, wagombea ambao walikata rufani FIFA, Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Kamati ya Rufani na Sekretarieti ya TFF.

Wajumbe hao wangependa kukutana na waziri anayehusika na michezo, hivyo TFF imeiandikia Wizara ikipendekeza kuwa ujumbe huo ukutane na Waziri na wakuu wengine wa michezo Aprili 16 mwaka huu 2013 kabla ya kuanza kazi zao.

Wagombea watakaosikilizwa na ujumbe huo wa FIFA ni:
1.   Farid Salim Mbaraka Nahdi: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alienguliwa na Kamati ya Uchaguzi na baadaye rufani yake kwa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kutupwa na hali kadhalika ombi lake la kutaka shauri lake liangaliwe upya, kukataliwa.

2.   Elliud Peter Mvella: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na kukata rufani Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kabla ya maombi yake ya kutaka shauri lake kuangaliwa upya, kukataliwa.


3.   Mbasha Matutu: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi na kukata rufani ambayo pia ilitupwa kabla ya kuomba shauri lake liangaliwe upya, ombi ambalo lilikataliwa.

4.   Hamad Yahya: Mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa Bodi ya Ligi ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na kuondolewa. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ikatupa ombi lake.

5.   Jamal Emily Malinzi: Mgombea wa nafasi ya urais wa TFF ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, hivyo kuondolewa kwenye mchakato. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini likakataliwa. Hata hivyo, alikuwa ameshakata rufani FIFA.

6.   Michael Wambura: Mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais wa TFF ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na rufani yake kukataliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF. Hakuomba shauri lake liangaliwe upya, lakini alikata rufani FIFA.

Shirikisho linawaomba wote waliotajwa hapo juu kujiandaa kwa utetezi na maelezo ya kutosha na kwamba barua za kuwaita zinafuata. (Orodha ya waathiriwa na programu ya ujumbe wa FIFA imeambatanishwa)

Kigogo Yanga matatani, kisa...!

Makamui Mwenyekiti wa Yanga, Clement  Sanga
MAKAMU Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Clement Sanga, anatarajiwa kufikishwa mbele ya Kamati ya Nidhamu kufuatia kauli aliyoitoa hivi karibuni kuwa timu yao inayoongoza kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwamba inahujumiwa na ndiyo maana mechi yao dhidi ya JKT Oljoro imesogezwa mbele na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Awali, mechi hiyo ya Yanga dhidi ya Oljoro ilipangwa kufanyika juzi (Jumatano ya Aprili 10) lakini sasa itachezwa kesho Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema kuwa kauli kama za Sanga zinachangia kujenga chuki  zisizokuwa na sababu kati ya shirikisho hilo na mashabiki wa soka nchini.
Kwa sababu hiyo, Osiah alisema kuwa Sanga atatakiwa athibitishe ni kwa namna gani Yanga inahujumiwa baada ya kuwapo kwa mabadiliko hayo ya ratiba ambayo yalizihusu pia timu nyingine zinazoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara, zikiwamo za Simba na Azam ambazo sasa zitacheza Jumapili.
Osiah alisema kuwa anashangaa kusikia madai ya Sanga kuwa klabu hazijashirikishwa katika kufanya marekebisho hayo wakati ukweli ni kwamba klabu hizo ziliwakilishwa na viongozi wao walioko kwenye kamati ya ligi na timu yao ina mjumbe kwenye kamati hiyo.
Katibu huyo wa TFF alisema kuwa viongozi wa klabu walielezwa katika kikao kilichofanyika mapema kabla ya ligi kuanza kwamba kutakuwa na 'Super Week' katika hatua ya mwisho wa ligi ambayo itatekelezwa kupitia nafasi itakayopatikana katika kituo cha televisheni ya kulipia cha Afrika Kusini cha  Super Sport.
"Mnapotafuta wadhamini kuna wakati ni lazima mjitoe mhanga... na kuonekana kwetu kupitia Super Sport kumesaidia kuleta wadhamini wengi ambao tayari wamevutiwa na ligi yetu," alisema Osiah.
Katika mahojiano yake na vyombo vya habari hivi karibuni, Sanga alisema kuwa wao walikuwa tayari wameshaiandaa timu yao na kwa mabadiliko hayo ambayo hawaoni faida yake zaidi ya kuwapunguzia mashabiki viwanjani yamewapa hasara kubwa itokanayo na kuendelea kuiweka timu kambini.
Aliyewahi kuwa Afisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu na Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage waliwahi kuadhibiwa na TFF baada ya kukutwa na hatia ya kutoa kauli ambazo baadaye walishindwa kuzithibitisha.


Chanzo:NIPASHE

Matapeli wamhujumu rais wa IBF nchini

Rais wa IBF/USBA, Onesmo Ngowi
MATAPELI wa kimataifa wanaoingilia barua pepe na akaunti nyingine za watu mbalimbali wamemvamia rais wa hapa nchini wa Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF/USBA), Onesmo Ngowi na kutumia jina lake kwa nia ya kuwatapeli fedha watu mbalimbali anaojuana nao.
Jina la Ngowi ambaye pia ni Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, (TPBC), limetumiwa na matapeli hao kutuma ujumbe wa barua pepe kwa watu mbalimbali anaowasiliana nao, wahusika wakijifanya ni Ngowi na kuomba msaada wa fedha.
Katika barua pepe mojawapo iliyotumwa kwa mwandishi, inaeleza Ngowi alikuwa akiomba msaada wa Euro 2,950 (Sh. milioni 6.2) ili kumuwezesha kujinasua na tatizo lililomkumba akiwa nchini Ugiriki; jambo ambalo Ngowi amelilaani na kuwatahadharisha watu anaojuana nao kuwa wawe macho na matapeli hao.
"Matapeli wanatuma akaunti yangu (ya email) na kuomba pesa kwa watu mbalimbali... mimi siko Ugiriki na wala sijamuomba mtu fedha. Tafadhali naomba usijibu meseji hizo," alisema Ngowi kuelezea utapeli huo ambao umeshawakuta pia watu wengi.

TFF ipo tayari kukutana na Nsa Job utetezi wa Rushwa

Nsa Job (kulia)
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema liko tayari wakati wowote kukutana na mchezaji wa Coastal Union ya jijini Tanga, Nsa Job, ambaye alikiri hadharani kuwa aliwahi kupokea rushwa ya Sh.milioni mbili kutoka kwa kiongozi mmoja wa timu vigogo nchini ili asifunge magoli.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema katika barua yao waliyomuandikia mshambuliaji huyo hawakumpa siku maalumu lakini endapo nyota huyo atachelewa kujisalimisha atakumbushwa kabla ya kuchukuliwa hatua kupitia kamati husika.
"Tuliiweka wazi lakini tutamuandikia barua nyingine ya kumkumbusha na itakayofuata itakuwa imetoa muda fulani, ila tunaamini atatoa ushirikiano kama alivyokaririwa na gazeti (la NIPASHE)," alisema Katibu mkuu huyo.
Osiah alisema TFF inaamini mchezaji huyo atatoa ushirikiano kama alivyolieleza gazeti la NIPASHE lilipozungumza naye mapema wiki hii.
Aliongeza kwamba wanaamini akiwa wazi mhusika wa tuhuma hizo atajulikana na hatimaye adhabu itatolewa na kukomesha suala la rushwa katika soka la nchini.
Osiah alisema pia tayari Mkurugenzi wa Vipindi wa kituo cha redio cha Clouds ameahidi kuwapa ushirikiano katika kupata nakala ya kipindi kilichorushwa mahojiano na Nsa ambacho kilifanyika Aprili 3 mwaka huu.
Nsa alizungumza katika mahojiano na kituo cha redio hiyo akisema aliwahi kupokea rushwa lakini aliifungia timu yake goli pekee la ushindi.
Hata hivyo, hadharani, hakuitaja timu aliyokuwa anaichezea wakati huo wala timu aliyoifunga na wala jina la kiongozi aliyemhonga, ambaye alisema alianza kumsumbua kudai fedha zake pale “alipowatungua”.
Nyota huyo ambaye kwa sasa anafanya mazoezi binafsi baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti nchini India aliwahi kuchezea timu za Simba, Yanga, Moro United, Azam, Villa Squad na sasa Coastal Union zote zinazoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Nsa aliiambia NIPASHE kwamba atatoa ushirikiano kwa TFF kama alivyotakiwa na kwa sasa anajiandaa kwenda kukutana nao.
Alisema pia alipokea barua hiyo tangu wiki iliyopita na atafanya kila linalowezekana ili kutekeleza kile atakachoambiwa na wajumbe wa kamati hiyo.


CHANZO:NIPASHE.

Azam yamalizana na wachezaji wake iliyowasimamia kwa rushwa

 
Add caption



KLABU ya soka ya Azam ambayo Jumapili inatarajiwa kuvaana na Simba, imemalizana na wachezaji wake wanne iliyokuwa imewasimamisha kwa tuhuma za Rushwa kabla ya kusafishwa na TAKUKURU.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mtandao wa klabu ya Azam, imesema wachezaji wote wanne waliosimamishwa kupisha uchunguzi wa tuhuma za rushwa dhidi yao wameripoti kambini tayari kuikabili Simba SC siku ya jumapili

Kurejea kwa wachezaji hao kunamaliza mgogoro uliokuwepo na kudumu kwa takribani miezi mitano kufuatia shutuma za rushwa ambazo zilipelekwa takukuru kuchunguzwa ili kujua ukweli na uongozi wa Azam FC unaishukuru takukuru kwa kazi nzuri ambapo imegundulika kuwa wachezaji hao hawakuhusika na hivyo kusafishwa na chombo hicho chenye mamlaka ya kuchunguza tuhuma za rushwa.
Wachezaji hao wote wanatarajiwa kuwemo kwenye mchezo wa Jumapili dhidi ya Simba SC ikiwa mwalimu ataona inafaa na wapo katika hali nzuri kuweza kucheza.
Mchezo huo wa jumapili ni muhimu sana kwa Azam FC kwani ikishinda itaizidi Simba SC pointi 14 huku simba ikisaliwa na michezo minne na hivyo kumaanisha kuwa Kagera Sugar atabaki kuwa mpinzani pekee wa Azam FC katika kuwania nafasi ya pili.

Thursday, April 11, 2013

Chelsea yafa ugenini lakini yatinga nusu fainali UEFA ndogo


Wachezaji Chelsea wakimpongeza Torres kwa kufunga bao akuongoza
LICHA ya kupokea kipigo cha mabao 3-2 kutoka kwa wenyeji wao Rubin Kazan ya Russia, Chelsea ya Uingereza imekuwa timu ya kwanza muda mfupi uliuopita kufuzu hatua ya nusu fainali ya UEFA Ndogo.
Chelsea imefanikiwa kufuzu hatua hiyo kutokana na ushindi mnono wa mabao 3-1 iliyopata katika mechi yao ya wali iliyochezwa 'darajani' mjini London hivyo kupenya kwa jumla ya mabao 5-4.
Fernando Torres aliiandikia Chelsea bao la kuongoza dakika chache baada ya kuanza kwa pambano hilo kwa kumalizia kazi nzuri ya Frank Lampard, goli lililodumu hadi wakati wa mapumziko kabla ya wenyeji kusawazisha dakika ya 51  Marcano.
Victor Moses mmopja wa wafungaji wa mabao katika pambano la wiki iliyopita baina ya timu hizo aliiongezea Chelsea bao la pili dakika nne baadaye kabla ya wenyeji kusawazisha katika dakika ya 62 kupitia kwa Gokdeniz Karadeniz kabla ya Bibras Natcho kufunga bao la ushindi kwa mkwaju wa penati dakika ya 75.
Michezo mingine ya ligi inatarajiwa kuchezwa muda mfupi ujao kwenye viwanja vingine vitatu tofauti kupata timu tatu za kuungana na Chelsea katika hatua hiyo ya nusu fainali.

Jahazi la African Lyon lazidi kuzama VPL


Kikosi cha African Lyon kilichozamishwa leo jioni
JAHAZI la timu ya African Lyon jioni ya leo limeendelea kuzama baada ya kubamizwa mabao 3-1 na Azam katika pambano pekee lililochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, jijini Dar es Salaam.
Kipigo hicho kimezidi kuifanya Lyon kusalia nafasi nafasi ya 13 ikijiweka pabaya katika kuepuka kushuka daraja tofauti na tambo zilizokuwa zikitolewa awali kuwa ni vigumu kwao kushuka daraja, kwani wamesaliwa na pointi 19 tu
Mabao yalioinyong'onyesha Lyon yalitupiwa kimiani na nyota wa Azam, Mcha Khamis ‘Vialli’ katikam dakika ya 9 kabla ya mfungaji kinara wa mabao wa VPL, Kipre Tchetche kuongeza mengine mawili katika dakika ya 28 na 61.
Bao pekee la Lyon lilifungwa na Adam Kingwande katika kipindi cha kwanza na kufanya wakati wa mapumziko matokeo yawe mabao 2-1.


                                          P      W     D     L     F      A     GD     PTS
    1.  Young Africans         21     15     4     2    37     12    +25     49
    2. Azam                         22     14     4     4    39     17     +22     46   
    3. Kagera Sugar            22     10     7     5    25     18     +7      37    
    4. Simba                        21     9      8     4     30     19    +11     35
    5. Mtibwa Sugar            23     8      9     6     26     24     +2      33  
    6. Coastal Union            22     8     8      6     23     20     +3     32   
    7.  Ruvu Shooting           22     8     6     8     21     19     +2     30    
    8.  JKT Oljoro FC            22     7     7     8     22     24     -2     28    
    9. JKT Mgambo              22     7     3     12     14     22     -8     24
    10.Tanzania Prisons      23      5     8     10     12     21     -9     23   
    11.Ruvu Stars                21     6     4     11     19     34     -15     22
    12. Toto Africans           24     4     10     10    22     32     -10     22
    13.  African Lyon            23     5     4     14     16     35     -19     19
     14. Polisi Morogoro      23     3     10     10     11     21     -10     19   
 

Ruvu Shooting yaitahadharisha TFF Kamati za Ushindi zinazoibuka sasa Ligi Kuu

IKIWA safarini mkoani Mbeya kwa ajili ya pambano lao lijalo dhidi ya wenyeji wao, Prisons ya Mbeya, uongozi wa timu ya Ruvu Shooting umeliomba Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kuwa makini na Kamati ya Ushindi za klabu mbalimbali zilizoundwa wakati Ligi Kuu Tanzania Bara ikielekea ukingoni.
Uongozi huo wa Ruvu umedai kuwa, kamati hizo huenda zikatumika vibaya katika upangaji na hulazimishaji wa matokeo viwanjani kutokana na ukweli kamati hizo mara nyingi huusisha viongozi wa FA mkoa na hata ofisi za wakuu wa mikoa husika wanaoweza kutumia vibaya nafasi zao kuzibeba timu zao hasa zikiwa kwao.
Akizungumza na MICHARAZO hivi punde, Msemaji wa klabu hiyo, Masau Bwire alisema kamati ya kusaka ushindi kwa timu za ligi kuu, siyo tatizo ila hofu yao namna zinavyoundwa wakati huu ligi ikielekea ukingoni na baadhi yao ni zile timu ambazo zipo katika hali mbaya kwenye ligi hiyo.
Bwire alisema, ingekuw vyema wakafuatilia kwa ukaribu mechi za mwisho za ligi hiyo ili kuepusha hujuma kwa timu nyingine, ili ligi imalizike salama kama ilivyoanza.
"Hatupingi kuundwa kwa hizi kamati kwa baadhi ya timu, lakini zinatutia hofu kwa namna zinavyoundwa kila mara timu zikiwa katika nafasi mbaya na hasa ligi ikielekea ukingoni, mbaya zaidio hujumuisha watu wenye nyadhifa ambazo wanaweza kutumika kuwatisha au kuwalazimisha waamuzi kutengeneza matokeo ya kuzibeba timu hizo," alisema Bwire.
Alisema kwa vile vyama vya mikoa (FA) ni wanachama wa TFF na majukumu yao ni kuhakikisha utekelezwaji wa sheria 17 za soka zinatumika uwanjani, hadhani ni sahihi nao kuingizwa kwenye kamati hizo kwani wanaweza kulaumiwa inapotokea dosari kwenye mechi ndani ya mikoa yao.
Aliongeza kuwa ni vyema kamati hizo zingekuwa zikiundwa mapema na kufanya kazi kuzisaidia timu zao kuliko sasa ambako imekuwa kama fasheni na kuleta hisia mbaya hasa wakati huu watanzania wakiwa na hisia kali juu ya vitendoi vya rushwa michezoni.
Juu ya pambano lao lijalo Bwire alisema kikosi chao kipo safarini lakini wakiwa na morali wa kupata ushindi mjini Mbeya, cha muhimu akiiomba TFF kuhakikisha wanausimamia kwa ukamilifu mchzeo huo ili kusiwepo na matukio kama waliyokutana nao jana kwenye pambano lao na Polisi Moro lililoisha kwa suluhu ya 0-0.

Ecuador yaingia Top 10 ya FIFA, England yaporomoka, Tanzania yapaa



NCHI ya Ecuador imeweka hostoria kwa kufanikiwa kuingia kwa mara ya kwanza kwenye Top 10 ya orodha timu bora duniani kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA.
Kwa mujibu wa orodha iliyotangazwa na FIFA, Ecuador imeshika nafasi hiyo kutokana na ushindi wa mechi mbili mfululizo walizocheza ndani ya mwezi uliopita.
Mechi hizo ni pamoja na ile ya kirafiki ya kimataifa dhidio ya El Salvador waliposhinda mabao 5-0 na ile ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Paguguay waliowalaza mabao 4-1.
Wakati Ecuador wakitinga hatua hiyo, Russia wamejikuta wakiporomoka, huku Croatia wakitinga hadi nafasi ya nne katika msimamo wa orodha hiyo mpya ya FIFA baada ya kushinda mechi zake mbili dhidi ya Wales na Serbia.
Orodha hiyo mpya ya FIFA inaoonyesha timu ya Hispania imeendelea kuongoza msimamo ikifuatiwa na Ujerumani kisha Argentina na Ureno ikikamilisha orodha ya timu Tano Bora ikitoka nafasi ya saba.
Colombia imeendelea kusalia kwenye nafasi ya sita huku England ikifuatia ikiporomoka kwa nafasi tatu, Italia imeshika nafasi ya nane baada ya kushuka kwa nafasi tatu na Uholanzi walioshuka nafasi moja wameshika nafasi ya tisa mbele ya Ecuador.
Katika orodha ya nchi za Afrika, Ivory Coast imeendelea kuongoza ikiwa ipo nafasi ya 12 duniani, ikifuatiwa na majirani zao Ghana walipo nafasi ya 22 duniani ikishika nafasi ya pili Afrika.
Zilizopo kwenye Top 10 ni Mali, Nigeria, Algeria, Tunisia, Zambia, Burkina Faso, Guinea ya Ikweta na Cameroon. Kwa ukanda wa CECAFA, Uganda imeendelea kuwa kinara ikifuatiwa na Tanzania iliyopanda kwa nafasi tatu toka 119 duniani hadi ya 116 huku Afrika ikiwa nafasi ya 33.

Pan Africans kwafukuta moto, IDFA yaamua kuingilia kati

Jengo la makao makuu ya klabu ya Pan African
WANACHAMA wa klabu ya Pan African wameushtaki uongozi wao kwa Chama cha Soka Wilaya ya Ilala (IDFA) kwa madai ya kukiuka katiba wakishindwa kuitisha mikutano tangu walipoingia madarakani mwaka 2009.
Kwa mujibu wa barua yao kwenda ya Machi 30, 2012 kwenda kwa Katibu Mkuu wa IDFA, wanachama hao wa Pan wanadai tangu uongozi wao ulipoingia madarakani Aprili 18, 2009 hawajaitisha mkutano wowote wala kushirikisha wanachama katika baadhi ya maamuzi waliyoamua kuyafanya.
Taarifa hiyo iliyosainiwa na mmoja wa wanachama wa klabu hiyo kwa niaba ya wenzake, Abbas Ally (kadi namba 0075), imedai mbali kutoshirikishwa katika maamuzi yanayofanywa na uongozi huo, pia klabu imekuwa haina ofisi.
"Japo jingine linalotutisha ni klabu kutokuwa na ofisi wake tuna jengo letu ambalo uongozi umelipangisha lote kiasi sisi wanachama kukosa mahali pa kupata huduma za klabu au kupata taarifa na kulipia ada za uanachama," taarifa hiyo ilisema.
Iliongeza kwa kuiomba IDFA kama mlezi wa klabu za Ilala kuushinikiza uongozi kuitisha mkutano wa wanachama na wao (IDFA) wakiwepo kama shahidi juu ya uongozi lazima uwasilishe mambo manne kwao siku hiyo.
Moja na mambo hayo ni ripoti ya mapato na matumizi kwa kipindi chote walichokaa madarakani na ukaguzi juu ya mapato hayo, taarifa ya sababu zilizoufanya uongozi huo kupangisha jengo lote kiasi cha kukosa ofisi na  mengine.
MICHARAZO liliutafuta uongozi wa Pan kufafanua madai hayo, ambapo  Makamu Mwenyekiti, Ally Hemed alisema asingeweza kuzungumzia suala hilo badala yake akataka atafutwe Katibu Mkuu wake Saad Mateo ambaye simu zake hazikupatikana hewani.
Hata hivyo Katibu Mkuu wa IDFA, Daud Kanuti ilithibitisha juu ya kupokea barua ya wanachama hao wa Pan na kudai kamati yao ya Utendaji ilishakutana na kuamua kuziita pande mbili zinazosigana kukaa meza moja kuzungumza.
Kanuti alisema kikao hicho kitafanyika Jumamosi ili kuzisikiliza pande zote mbili kwa kuipitia katiba ya klabu hiyo kisha kutoa maamuzi yatakayoleta suluhu ndani ya klabu hiyo kongwe nchini.

Lyon kuendeleza maajabu leo mbele ya Azam?


Kikosi cha African Lyon

Azam Fc
TIMU ya soka ya Azam leo inatarajiwa kushuka dimbani kuvaana na African Lyon, inayopigana kuepuka kushuka daraja katika pambano pekee litakalochezwa kwenye uwanja wa Chamazi.
Lyon ambayo katika mechi yake iliyopita ilifanya maajabu kwa kuilaza Coastal Union na kuondoka mkiani, hali inayofanya mashabiki kutaka kuona kama itaendeleza ubabe huo au la.
Pambano na kwamba Lyon hiyo ni mechi yake muhimu, lakini pia kwa Azam ni muhimu zaidi katika mbio zake za kutaka kuwaengua Yanga kileleni na kuweka rekodi ya kuwa mabingwa wapya nchini.
Azam ipo nafasi ya pili nyuma ya Yanga ikiwa na pointi 43, sita zaidi ya vinara hao na iwapo itashinda itapunguza pengo hilo hadi kuwa tatu kabla ya kuvaana na Simba Jumapili uwanja wa Taifa.
Makocha wa timu hizo mbili zenye upinzani wa jadi kutoka wilaya ya Temeke, wametamba kuhakikisha wanaibuka na ushindi ili kutimiza malengo yao tofauti.
Kocha wa Azam, Muingereza Stewart Hall, alinukuliwa akisema wataingia uwanjani bila kuidharau Lyon licha ya kusaka ushindi ili kujiweka pazuri katika harakati zao za ubingwa.
Naye kocha wa Lyon, Charles Otieno, alitamba kwamba wamejipanga kushinda mchezo wa leo ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kuepuka kurudi Ligi Daraja la Kwanza.
Kikosi cha Lyon mpaka sasa kimejikusanyia pointi 19 wakilingana na Polisi Moro wanaoshikilia mkia kwa tofauti ya uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Ili kujua nani atakayekuwa ametimiza malengo ni kusubiri mpaka baada ya dakika 90 za pambano hilo pekee kwa siku ya leo.

Messi aivusha Barca nusu fainali, Juve wakiona cha moto nyumbani

 
Pedro akishangilia bao lake la kusawazisha dhidi ya PSG jana usiku

NYOTA wa kimataifa wa Argentina, Lionel Messi usiku wa kuamkia leo alionyesha ni namna gani alivyo chachu ya mafanikio ya timu yake baada ya kuiwezesha Barcelona kufuzu nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Messi aliyeingia kipindi cha pili wakati wenyeji Barca wakiwa nyuma kwa bao 1-0, alibadilisha taswira nzima ya mchezo huo uliochezwa uwanja wa Camp Nou na kuipa timu yake sare ya bao 1-1 dhidi ya wageni PSG ya Ufaransa.

PSG walitangulia kupata bao kupitia Javier Pastore na kuwapa wakati mgumu wenyeji waliokuwa wameelemewa licha ya  Xavi Hernendez kuweka rekodi ya kupiga pasi sahihi kwa asilimia 100 katika pambano hilo.

Mara baada ya kuingia uwanjani Messi aliifanya PSG kupoteza mwelekeo na yeye kutumia nafasi hiyo kutoa pasi murua kwa David Villa ambaye alimpasia Pedro aliyefunga bao la kusawazisha dakika ya 71.

Hata hivyo Barca wamefanikiwa kufuzu kwa sheria ya bao la ugenini baada ya kupata sare ya mabao 2-2 ugenini wiki iliyopita na hivyo kufanya matokeo ya jumla kuwa mabao 3-3 na kuiondosha PSG kwenye michuano hiyo.

Katika pambano jingine ambalo lilichezwa mjini Turin, Italia wenyeji na vinara wa ligi kuu ya Seria A, Juventus walishindwa kutamba nyumbani baada ya kunyukwa mabao 2-0 na Bayern Munich ya Ujerumani.

Ushindi huo wa Munich umeifanya timu hiyo kufuzu nusu fainali ikiungana na timu za Real Madrid, Borussia Dortmund na Barcelona kwa jumla ya mabao 4-0.

Katika mechi yao iliyopita iliyochezwa nchini Ujerumani, Juve walilala kwa mabao 2-0.

Bayern ilipata ushindi huo ugenini kupitia mabao yaMario Mandzukic aliyefunga katika dakika ya 64 akimalizia mpira wa faulo uliopigwa na kiungo Bastian Schweinsteiger kabla ya Claudio Pizarro kufuinga bao la pili dakika ya 90.

Hatma ya timu zipi zitakazokutana katika hatua hiyo inatarajiwa kufahamika kesho Ijumaa itakapotangazwa droo ndogo huku kukiwa na hofu Wahispania na Wajerumani waliofuzu hatua hiyo kukutana wenyewe kwa wenyewe.


Golden Bush Fc haikamatiki Ligi ya TFF-Kinondoni

TIMU ya soka ya Golden Bush imezidi kuchanja mbuga kwenye Ligi Daraja la Nne wilaya ya Kinondoni, baada ya juzi kupata ushindi wa nne mfululizo  kwa kuwalaza TP Afrika kwa mabao 3-1 katika mfululizo wa ligi hiyo.
Ushindi huo wa juzi katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Itihad, Mwananyamala jijini Dar es Salaam limeifanya Golden Bush kuongoza msimamo wa kundi lake na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya pili ya michuano hiyo ninayochezwa kwenye viwanja mbaliumbali wilayani humo.
Golden Bush inayonolewa na nyota wa zamani wa soka nchini, Shija Katina na Madaraka Seleman, ilipata ushindi huo wa nne kupitia mabao yaliyofungwa na wachezaji wake nyota, Kenan Mwashinde aliyefunga mawili na Mrisho aliyefunga bao jingine.
Kabla ya ushindi huo wa juzi, Golden Bush ilianza ligi hiyo kwa kishindo kwa kuipa kipigo kitakatifu timu za Victoria ya Kijitonyama kwa kuwatandika mabao 6-1 kabla ya kuilazaa Makumbusho Talents kwa magoli 3-1 na kuizima Katabazi  na kufanya waongoze msimamo wa kundi lao wakiwa na pointi 12.