STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 12, 2014

Yanga warejea toka Misri, Simba wawapa dole!

Yanga
WAKATI kikosi cha Yanga kilichotolewa kishujaa katika Ligi ya Mabingwa ya Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri, kikirejea nchini kutoka Cairo, watani zao Simba wamewapongeza kwa kiwango cha soka walichoonyesha mbele ya watetezi wa michuano hiyo ya Afrika.
Yanga iling'olewa kwa mikwaju ya penati 4-3 na watetezi hao baada ya kukubali kipigo cha 1-0 katika dakika 90 na kulingana magoli baada ya mechi ya kwanza wenyewe kushinda nyumbani idadi kama hiyo iliwasili leo na kupokewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe Said Mecky Sadiq.
RC huyo aliapongeza wachezaji na viongozi wa Yanga kwa namna walivyoipigania Tanzania, ingawa bahati haikuwa yao huku akiwataka wanaowasakama wachezaji hasa Said Bahanuzi kuacha jambo hilo kwa madai hata mastaa duniani hukosa penati na bado wanapongezwa na wadau wao.
Katika hali isiyotarajiwa Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga amenukuliwa akiwapongeza watani zao kwa mchezo waliouonyesha ugenini licha ya kushindwa kufikia rekodi yao ya kuwang'oa watetezi wa taji la Afrika,
Kamwaga alisema kila mtu ameona watani zao walivyopigana ingawa hawakuwa na bahati ya kupenya hatua hiyo na Simba kama wadau wengine wa soka wanapongeza na kuwakarisha kwenye ligi kuu.

Samuel Sitta ashinda kwa kishindo Uenyekiti Bunge la Katiba

http://www.dar24.com/wp-content/uploads/2013/05/sitta.jpg
Mhe Samuel Sitta
WAJUMBE 487 kati ya 563 wamemchagua Mbunge wa Urambo Mashariki na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta kuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba.
Sitaa aliyekuwa akipewa nafasi kubwa ya kushinda katika king'anyiro hicho alimwangusha mpinzani wake, Hashim Rungwe aliyeambulia kura 69, huku kura 7 ziliharibika katika uchaguzi uliofanyika jioni hii.
Kabla ya zoezi la kupigwa kura Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo, Pande Ameir Kificho aliwatangaza wagombea hao na kuwapa nafasi ya kujieleza kwa wajumbe ambapo Mzee Sitaa alifunika kwa kusisitiza kuwa falsafa yake ya Standard and Speed ipo pale pale katika kuihakikishia Tanzania inaopata Katiba Mpya na yenye kiwango kwa mujibu wa matakwa ya wananchi.
MICHARAZO Inampa heko zake Mhe Sitta na kumtakia kila la heri katika kazi yake hiyo kwani ni wazi wajumbe na watanzania kwa ujumla wanamuamini kutokana na ufanisi wake serikali na alipokuwa Mbunge wa Bunge la Tanzania.

Huu si wivu bali unyama na unyanyasaji

http://www.ippmedia.com/media/picture/large/shilogile-aug31-2013.jpg 
Na Mariam Kamgisha, Morogoro
MWANAMKE mmoja Juliana Wambura (24) mkazi wa kijiji cha Ruaha, ameuawa kwa kuchomwa kisu tumboni na mumewe.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile, alisema lilitokea juzi saa 2:00 usiku katika kijiji cha Ruaha tarafa ya Mikumi wilayani Kilosa.
Alisema marehemu aliuawa kinyama kwa kuchomwa na kisu tumboni  na mumewe  aliyefahamika kwa jina la  Fredi Ernest (34) mkazi wa Shirati Mara  na kupelekea utumbo wa mkewe kutoka nje.
Alisema chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi na mtuhumiwa baada ya kutekelea mauaji hayo amekimbia.
Katika tukio jengine alisema alisema Machi 8 mwaka huu saa 1:30 asubuhi, Gerry Joseph (23) alifariki dunia baada ya pikipiki aliyokuwa akiiendesha  kugonga mti.

Aidha alisema katika tukio jengine  gari aina ya Scania lililokuwa likiendeshwa na Juma Saidi (30) mkazi wa Dar es Salaam lilimgonga mtembea kwa miguu mwanamme asiyefahamika na kumsababishia kifo.

Sitta njia nyeupe Uenyekiti Bunge la Katiba

Samuel Sitta akiwa na fomu ya kuwania nafasi ya Uenyekiti Bunge Maalum la Katiba
WAKATI uchaguzi wa Mwenyekiti wa kudumu wa Bunge Maalumu la Katiba ukitarajiwa kufanyika leo, wagombea wawili waliojitokeza kutaka kuwania nafasi hiyo, wameenguliwa baada ya ya kushindwa kurudisha fomu ya kuwania nafasi hiyo kwa muda uliopangwa

Wajumbe hoa Dk Theria Uvisa pamoja na Danstan Chipaka walienguliwa katika kinyang’anyiro hicho kufuatia kushindwa kurudisha fomu za kugombea ambazo zilipaswa kurudishwa leo saa 4 asubuhi.

Kufuatia kuenguliwa kwa wajumbe hao, nafasi hiyo itawaniwa na Samwel Sitta pamoja  na Hashim Rungwe ambao ndiyo waliokidhi vigezo kwa kuchukua fomu na kurudisha kwa wakati.

Uchaguzi wa Mwenyekiti unatarajiwa kufanyika leo saa 10 jioni, ambapo baada ya kutangazwa matokeo kutatangazwa uchukuaji fomu kwa wajumbe watakaotaka kuwania nafgasi ya umakamo mwenyekiti.

Mpaka sasa anayetajwa kutarajiwa kuwania nafasi hiyo ya Makamu Mwenyekiti, ni Samia Suruhu.

Kwa mujibu wa kanuni za Bunge Maalumu la Katiba, Makamu Mwenyekiti wa Bunge anapaswa kutoka upande wapili wa muungano iwapo Mwenyekiti atakuwa amechaguliwa kutoka upande mwingine wa muungano hili kuleta usawa.
FK

TANZANIA BILA DAWA ZA KULEVYA INAWEZEKANA?!


KATIKATI ya mwaka jana iliyowahi kuchapishwa barua iliyoandikwa na kusainiwa na baadhi ya wafungwa wa dawa za kulevya waliopo China. Katika barua yao hiyo waliwataja baadhi ya wahusika na biashara hiyo waliopo nchini kwa majina yao na kumgusa mmoja wa Wabunge wa Tanzania, Mhe. Idd Azan ambaye alikanusha taarifa hiyo na kuapa yu tayari apigwe risasi hadharani kama atabainika anahusika.
Wakati hilo likiwa limesahulika, mfungwa mwingine ametuma barua akisisitiza kuwa Tanzania Bila Madawa ya Kulevya Inawezekana iwapo tu vigogo wahusika na biashara na mtandao huo watashughulikiwa kivipi?
Isome barua ya mfungwa huyo kama ilivyo;

DRUG FREE TANZANIA IS POSSIBLE

I write this letter on behalf of the Drug Free Tanzania Movement (Tanzanian Prisoners in Hong Kong jails). Today I write to you inspired by Dr. Harrison Mwakyembe “One of the men of goodwill in our current government”, with his renowned dedication and strong determination to dismantle drug trafficking networks in our nation. I also write on behalf of all men of goodwill to whom beauty is truth and truth and who eyes the beauty of genuine Drug Free Tanzania is more precious than silver or gold or diamond. My fellow compatriots, drug trafficking is still a fact in Tanzania. We must keep on building the momentum, we must keep up our campaign until next national election in 2015. We must keep revealing all those who involves in this illicit trade (from civilian, businessmen/women, law enforcement personnel and politicians). We must keep on confronting drug trafficking in its hidden and subtle forms.

Brethren, I am mindful that democracy as defined by Abraham Lincoln “is the government of the people, for the people and by the people”, and I am also mindful that if democracy is to live in our nation, politicians and their associates who involves in this Evil trade must be wiped and out of the Tanzania Political Map. If democracy is to live in our nation, drug trade must die, because democracy is people’s power and we (people) are not unmindful that drug trade is the universal Evil and anyone who associates himself with this Evil is an agent of the Devil. And since the ripple effect of drugs to our community as well as the international community is incalculable, we must eliminate all devil agents and their associates and their family members in our political map.

Every attempt to end our campaign by intimidation, by encouraging fellow inmates to inform, by using death threats toward us and our loved ones further cemented our campaign and brought sympathy for our cause from men and women of goodwill all over the nation.

The great appeal for the nation appears to lie in the fact that we (Tanzanian inmates in HK jails – “The Victims of the illicit trade”) have decided to break our silences and pray that The Almighty God shall give us strength to remain committed to this cause though we may face death.

We dared to dream of a better day in the midst of our sufferings and the nightmare that surrounded us. We have unequivocally declared our hatred for this most colossal of all Evils and we have publicly name and shame our ex-paymasters “the Drug Barons” most of them top brass businessmen and women, politicians, their associates and even law enforcement personnel. We have condemned all crooked politicians regardless of their political parties since we are not politically affiliated with any party.

When we started our campaign most of our brethren they told us we wouldn’t get here. They told us we cannot stop even a single Tanzanian courier coming into Hong Kong, Macau and the Mainland China. But it is now week twenty six (26) not a single Tanzanian courier has been arrested for drug trafficking here in Hong Kong Airport. (What a record? It was hardly to pass a week without several arrests).

And there were those who said that we would get here only over their dead bodies. All the nation knows that we are here and we aren’t going to let nobody turn us around.

So I write you today with the conviction that the illicit trade is on its death bed in Tanzania and the only thing uncertain about is how costly the drug barons and their political backers will make the funeral.

My dear fellow compatriots. Listen! The battle is in our hands. The battle is in our hands in Dar es Salaam, Dodoma and all over the United Republic of Tanzania. So let us be more than ever committed to this cause for better Tanzania. Let us march on the ballot boxes until all bad corrupted and drug related leaders disappear from the political arena. Let us march on the ballot boxes until those politician and their associates who has been barred from entering the United States for drug trafficking allegations and money laundering tremble away in silence.

Let us march on the ballot boxes, until we send to our Municipal councils and the House of parliament councilors and MP’s men and women who will not fear to do justice and walk humbly with their God.

Brethren, there are no broad highways to lead us easily and inevitably to quick solutions. We must keep going. We must be extremely vigilant with the drug enforcers and we must keep on spreading the news (about the dangers of trafficking drugs into HK, Macau and the Mainland China) to our fellow compatriots and we must keep on naming and shaming the Drug barons and their associates. And we shall not let anybody turn us around until we have a drug trafficking free society.

Your fellow compatriot languishing in Hong Kong jail.

Name: withheld Alias: Mckenga (TZA-Prisoner)

Date: 19-02-2014


Credit:Brother Danny

Wenger amponda Arjen Robben kwa udanganyifu

Arsenal's Laurent Koscielny (right) fouls Bayern Munich's Arjen Robben in the penalty area (PA Photos)
Arjen Robben akiwa amenguka ndani ya eneo la penati la Arsenal mbele ya Laurent Koscielny
MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amemponda winga nyota wa Bayern Munich, Arjen Robben kwa madai ya udanganyifu wa kujirusha ili kushawishi marefa kuipa penati timu yake.
Mfaransa huyo alisema kuwa Robben licha ya kuwa bonge la mchezaji anayemkubali, lakini pia amemsifia kuwa ni hodari wa kujirusha baada ya jana kuhusika na tukio la kujirusha langoni mwa Arsenal ili kushawishi penati kama alivyofanya kwenye mechi ya awali mjini London, japo penati hiyo ilikoswa.
Katika tukio hilo la awali, Mholanzi huyo alisababisha kipa wa Arsenal Wojciech Szczesny kutolewa nje ya dimba kwa kadi nyekundu kwa kile kilichoonekana kumchezea rafu mbaya Robben.
Jana winga huyo alirejea tena na kuipa timu yake penati dakika za lala salama ambayo ilipotezwa na Thomas Muller na kuinusuru Arsenal kuchezea kicha pili mfululizo kwa Bavarians hao ambao hata hivyo wamesonga mbele.
"Siwezi kupinga, Robben ni bonge la mchezaji, ila ni mjanja wa kulazimisha mambo kwa kupenda kwake kujirusha mbele ya mabeki ili aonekane kachezewa vibaya, haivutii," alisema Wenger baada ya mechi ya jana dhidi ya Bayern Munich, ambapo winga huyo alionekana kama kachezewa rafu na Laurent Koscielny.
Wenger alisema kama marefa wangekuwa wakimpa kadi ya njano, hadhani kama angerudia mchezo wake huo ambao alidai unapoteza mvuto wa soka kwani ni udanganyifu unaoziumiza timu nyingine wakati mwingine.

Manny Pacquiao nouma amchakaza Hatton

Pacquiao (kushoto) akimtandika mpinzani wake
MOJA ya pambano kali la kusisimua kabisa lilifanyika usiku wa kuamkia Jumapili ya Mei 3, 2009 huko Marekani kwenye ukumbi wa Las Vegas kati ya bondia Manny Pacquiao 'The PacMan' na Ricky Hatton maarufu kama Hitman.
Pacquiao alianza pambano hilo kwa kasi akishambulia ngumi lakini kwa tahadhari kubwa dhidi ya Hatton, ambaye si bondia wa kumtabiria, masabiki walikuwa wakipiga kelele kwa kushangailia wakati wote.
Kadiri randi ilivyokuwa ikisonga mbele ndivyo Pacquiao alivyokuwa akishambulia kwa kasi na kuonyesha ubora wa hali ya juu, alkuwa akipiga ngumi za kudonoa yaani 'jab' kali na kwa hesabu za hali ya juu na kufanikiwa kupenyeza ngumi nyingi kwa 'Hitman' akitumia jab na ngumi mkunjo za kulia yaani 'right hooks'.


Katika raundi hiyo ya kwanza Pacquiao alimkamata Hatton mara tatu kwa right hok zake kali zilizotua barabara katika kichwa chake na 'kumpotzea' kabisa Hatton katika raundi hiyo ambapo alikuwa akijitahidi kukwepa bila mafankio makubwa.


Ukingoni mwa raundi hiyo Hatton naye 'akazinduka' na kurusha makombora kadhaa kwa Pacquiao na kumfanya alalie kamba, Hatton mzaliwa wa Manchester akambana Pacquio na kumshambulia kwa right hook na left hook ambazo hata hivyo nyingi ziliishia katika mikono ya
Pacquiao.
Hatton akaendelea kumbana Pacquaio kweny kamba lakini mpinzani wake huyo akawa anatumia ngumi ndefu za kati aipiga tumbo na kifua na moja moja akitumbukiza katika uso wa Hatton na ngumi zote zilimwingia Hitman.


Ndipo ghafla alipojinasua kwenye kamba na kupiga ngumi mkunjo kali ya kulia yaani 'right hook' na Hitman akadondoka chini kama mzigo wa kuni katika raundi hiyo ya kwanza.


Umati ukalipuka kwa shangwe na hasa mashabiki wa Pacquiao, Hatton akajizoa chini na mwamuzi akamuhesabia hadi 8, akapanguza glavu zake na kusema yuko fit kuendele anapambano zikiwa zimesalia sekunde 46 raundi ya kwanza kumalizika.


Mwamuzi aliporuhusu tu pambano, Pacquaio hakukawia akamfuata kwa kasi Hatton na kumsukumia 'right hooks', na jabs za nguvu na ngumi nyoofu ya kushoto au 'straight lefts'.


Hatton kwa uzoefu wake akajaribu kujikinga lakini hakuweza kukinga ngumi zote kwani ngumi 5 zilimkamta barabara na kumfanya aone' double double' na ndipo Pacquio akakaza musuli wa mkono wa kushoto na kumtandika Hitman, ngumi kali iliyomwelemea na kujikuta akidondoka tena chini kwa mara ya pili katika raundi ya kwanza.


Ilikuwa ni bahati kwake wakati anakwenda chini zlikuwa zimesalia sekunde 7 na hivyo alivyoanza kuhesabiwa raundi ikawa imemalizika na ikawa ni dhahiri Hatton ameokolewa na kengele, mabondia wote wakaenda kwenye kona zao kufuta pumzi.


Raundi ya pili ilipoanza, Hatton alianza kwa kurusha jab zake nyingi na kutumia zaidi 'left hook' ambazo kadhaa zilimpata Pacquiao ambaye wakati fulani pamona na kupigwa ngumi za nguvu kichwani na kuonekana kulewa, lakini alikuwa na nguvu kiasi cha kushindwa kudondoka.


Pacquiao akawa anatumia ngumi za mnyooko yaani 'straight punch' , kisha akapiga jab ya kushoto akapiga tena ngumi ya kulia na kwa kasi ya ajabu, akaachia ngumi kali ya kushoto iliyompata Hatton na kumpeleka sakafuni.

Ngumi hiyo ilipigwa katikati ya ulingo wakati raundi ya pili inaelekea ukingoni, Hatton akajitutumua kujizoa pale chini kwa nia ya kutaka kuendelea kupigana kama alivyofanya kwenye raundi ya kwanza.

Akamudu kusimama kwa mbinde, mwamuzi akaruhusu pambano kuendelea baada ya kuwa amemhesabia Hatton naye kujibu kuwa ataendelea, Pacquiao hakukawia, akamfuata tena na kumcharaza konde kali la mkono wa kulia na Hatton akadondoka tena chini kama zigo la nyanya.


Safari hii mwamuzi Kenny Bayless hakujisumbua tena kumhesabia Hatton baada ya kumuona akihema kwa nguvu akiwa amelala chali na wala kutokuwa na dalilia ya kunyanyuka mapema, alibaki akipepesa macho pale chini.


Pambano likawa limemalizika katika raundi ya pili na Manny Pacquiao akawa bingwa kwa kumpoka ubingwa Hatton, akajiwekea rekodi ya mapambano 49 akipoteza 3 sare 2 huku 37 akishinda kwa KO na kuifanya rekodi ya Hatton iwe mapambano 45 akipoteza 2, huku 32 akishinda kwa KOs. Hakika hilo lilikuwa ni moja ya pambano bora la KO.

Hawa ndiyo wachezaji 10 wa Kiafrika wanaolipwa vyema

WAKATI Cristiano Ronaldo akitajwa kuwa mchezaji tajiri duniani akimfunika aliyekuwa akiishika nafasi hiyo kwa muda mrefu, David Beckham, pia akiwa ndiye mchezaji anayelipwa vyema duniani akiichezea Real Madrid.
Hata chini ni orodha ya wachezaji wanaovuta mkwanja mrefu katika klabu zao ambapo orodha hii imeanza na namba 10 kwenda namba moja.
John Obi Mikel HDTV Wallpaper
10. John Obi Mikel – $6.1 million

Nigerian John Obi Mikel joined the Premier League Club in 2006 to play midfielder for Chelsea, and has had an extremely successful career since. He has played for the Nigerian national team in the African Cup of Nations and FIFA World Cup in recent tournaments, and almost won the African Footballer of the Year Award in 2012.
http://1000goals.com/football-pictures/file/43/1600x1200/crop/michael-essien-wallpaper-real-madrid.jpg
9. Michael Essien – $6.9 million

Beginning his career with the Liberty Professionals in his home country of Ghana, Michael Essien burst onto the international stage when played for SC Bastia in France for several seasons. He joined Chelsea in 2005, and is on loan this season to Real Madrid. Essien has helped represent Ghana in numerous international competitions, including three African Cup of Nations tournaments and the FIFA World Cup.
http://e1.365dm.com/13/02/504x378/ChrisSambaQPR_2894520.jpg
8. Christopher Samba – $7.5 million

Congolese defender Christopher Samba moved around a fair amount early in his career, playing in the Premier League (with the Blackburn Rovers and Loftus Road), as well as for the Russian team, Anzhi Makhachkala. Earning more than $160,000 per week, Samba easily makes the list of highest-paid African footballers, and has helped represent Democratic Republic of the Congo in many international competitions.
http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/10/29/article-2479272-1824A2D100000578-997_634x476.jpg
7. Kolo Toure – $7.8 million

Ivorian Kolo Toure makes his living playing for Liverpool, though he got his start in Arsenal, where he played for seven years. He made more than 100 appearances for the Côte d’Ivoire national team, playing in the African Cup of Nations and FIFA World Cup tournaments. He also has a lucrative endorsement deal with Adidas to add to his already formidable salary. Toure’s younger brother, Yaya, also plays for the Côte d’Ivoire national team — and earns a lot more! Read on.

http://www.soccerwallpaper.mackafe.com/var/albums/Fr%C3%83%C2%A9d%C3%83%C2%A9ric-Kanout%C3%83%C2%A9-Wallpaper-Gallery/kanoute_goal_happy.jpg
6. Frédéric Kanouté – $8.4 million

Malian Frédéric Kanouté has played for the Chinese club Beijing Goan since June 2012, though he made a name for himself earlier playing for Lyon, West Ham, and Sevilla in Europe. He has played in three consecutive African Cup of Nations tournaments, and is consistently one of the most popular football players in Mali.
http://en.africatopsports.com/wp-content/uploads/2013/09/Emmanuel-Adebayor1.jpg
5. Emmanuel Adebayor – $13.5 million

Togo striker Emmanuel Adebayor has made his name in the English Premier League, playing for Arsenal and Manchester City before landing on his current team, Tottenham, in 2011. He is considered one of the most charitable athletes out there, committed to numerous projects around the world and particularly in his native Togo. Most notably, he started the SEA Foundation, a charity that helps to run educational, economic empowerment, and healthcare projects around Africa.

4. Seydou Keita – $16.2 million

Malian midfielder Seydou Keita currently plays for the Chinese Super League club Dalian Aerbin FC, though he originally made it big during his four-year career with Barcelona. He is captain of the Malian national team and has helped represent his home country quite well in numerous African Cup of Nations tournaments.

http://foreverwestham.com/wp-content/uploads/2014/02/Didier-Drogba.jpg
3. Didier Drogba – $17.5 million

Ivorian star Didier Drogba is the all-time top scorer for the Côte d’Ivoire national team, and has lent his talents to various teams throughout his career. Finding stardom initially in the English Premier League in Chelsea, he then moved to the Shanghai Shenhua FC and finally to Galatasaray, where he plays now in the attacker position. Making more than $20,000 per match, his net worth only expands with the numerous endorsement deals he also has.
Yaya Touré
2. Yaya Toure – $20 million

The brother of aforementioned Kolo Toure, Yaya Toure earned $20 million in 2013, making the Toure brothers the highest-paid siblings in African sports. Playing midfielder for Manchester City, he developed an enormous fan base for his physical power and crystal clear technique. Earlier in his career, Toure played for youth clubs in Côte d’Ivoire before heading to Europe to play for the likes of Baveren, Olympiacos, and Barcelona.
Samuel Eto'o - Chelsea FC - 2013/14 Champions League matches for Chelsea.
1. Samuel Eto’o – $27 million

Perhaps the most recognized name in African sports, Cameroonian striker Samual Eto’o pulled home $27 million in 2013 playing for the Russican club Anzhi Makhachkala, though he recently signed a contract to play for Chelsea for the upcoming year. He brought his talents to various teams through the course of his career, including Real Madrid, RCD Mallorca, and Inter Milan, and has won African Player of the Year four times. He has helped represent Cameroon in numerous international competitions, and is on track to do so again this summer at the 2014 FIFA World Cup in Brazil.

Arsenal majanga, Ozil nje kwa majeraha

Arsenal's Mesut Ozil in action against Bayern Munich (AFP)
Mesut Ozil alipokuwa wakifanya mambo yake kabla ya kutolewa baada ya kuumia jana


HUENDA hii ikawa ni taarifa mbaya kwa mashabiki wa klabu ya Arsenal ambao wanaugulia kutolewa kwa timu yao kwenye hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana, baada ya kudokezwa kuwa huedna wakamkosa kiungo wao mahiri, Mesut Ozil aliyeumia katika pambano hilo la usiku wa jana
Meneja Arsene Wenger amethibitisha kuwa watakosa huduma za kiungo huyo aliyeumia katika mechi hiyo ikiwa ni siku chache baada ya kurejea kwenye kiwango chake na kuivusha Arsenal kwenye Nusu Fainali ya Kombe la FA.
Mchezaji huyo wa bei mbaya kwa klabu hiyo aliyolewa wakati wa mapumziko wakati matokeo yakiwa 1-1 na kocha Wenger amesema hana hakika itamchukua muda gani nje ya dimba, ila amekiri hatamtumia kwenye mechi yao ya Jumapili dhidi ya mahasimu wao wa London Kaskazini, Tottenham Hotspur.
"Linaonekana ni tatizo kubwa," alisema kocha huyo na kuongeza; "Sijui nitamkosa kwa muda gani, ila nina hakika hatacheza mechi ya Jumapili dhidi ya Spurs."
"Tutamfanyia vipimo kesho (leo) ili kujua tatizo lake lipo kwa kiasi gani ina atakuwa nje kwa wiki kadhaa. Natumaini halitakuwa tatizo kubwa sana," aliongeza kocha huyo toka Ufaransa.

Arsenal yang'oka, AC Milan aibu tupu Ligi ya Mabingwa Ulaya

Bastian SchweinsteigerAtletico Madrid's Diego Costa (R) celebrates with teammate Raul Garcia after scoring a goal against AC Milan during their Champions League last 16 second leg (Reuters)
Diego Costa akishangilia bao lake la Garcia

Jikaze wewe hii kazi ya kiume bana!
Atletico Madrid wakishangilia
Frank Ribery akichuana na wachezaji wa Arsenal
MABINGWA wa zamani wa Ulaya, AC Milan ya Italia imeyaaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kukung'utwa ugenini mabao 4-1 na Atletico Madrid ya Hispania, huku Arsenal ikitoka sare ya 1-1 ugenini lakini imekwama kutinga Robo Fainali  dhidi ya Bayern Munich.
Atletico ikiwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Vicente Calderon iliifumua Milan na kutinga hatua hiyo kwa jumla ya mabao 5-1 kwani mechi ya kwanza nchini Italia ilishinda 1-0.
Wenyeji waliwashtukiza wageni wao kwa bao la mapema la dakika tatu tu lililofungwa na nyota wa timu hiyo Diego Costa kabla ya Kaka kuisawazishia Milan bao dakika ya 27.
Hata hivyo Atletico iliongeza bao la pili dakika ya 40 kupitia kwa Turan na kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa 2-1.
Kipindi cha pili kilikuwa cha wenyeji baada ya kuongeza mabao mengine katika dakika ya 70 lililofungwa na Raul Garcia na Diego Costa aliongeza jingine dakika tano kabla ya pambano kiumalizika.
Katika mechi nyingine iliyochezwa kwenye uwanja wa Allianz Arena, mjini Munich nchini Ujerumani, watetezi wa taji hilo, Bayern Munich waliiondosha tena mashindanoni Arsenal ya England baada ya kutoka nao sare ya 1-1.
Arsenal ilikwama kufuzu hatua ya 16 Bora kwa mwaka wa tano mfululizo baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 nyumbani kwao wiki mbili zilizopita na hivyo sare ya jana imewafanya waage michuano hiyo kwa jumla ya mabao 3-1.
Wenyeji walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Bastian Schweinsteiger katika dakika ya 54 kabla ya Lukas  Podolski kuisawazishia wageni dakika tatu baadaye.
Kivumbi cha ligi hiyo kitaendelea leo kwa mechi nyingine mbili Barcelona itakuwa nyumbani kuikaribisha Manchester City ambayo katika mechi yao ya kwanza waliifumua kwa mabao 2-0 na pambano jingine ni kati ya PSG ya Ufaransa dhidi ya Bayer Leverkusen walioitambia kwao mabao 4-0.

Tuesday, March 11, 2014

Maafande wa Polisi Moro yarejea tena Ligi Kuu


TIMU ya soka ya Polisi Moro imekuwa timu ya kwanza kurejea Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kufanya vyema kweli Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL) kundi B, huku ikiwa imesaliwa na mechi mbili mkononi kuhitimisha mechi zake.
Polisi walioshuka daraja msimu uliopita sambamba na timu za Toto Africans na African Lyon ambazo nazo zinapigana kurejea zikiwa katika makundi mawili tofauti.


Shaaban Dede bado amlilia Meddy Kitendawili

http://1.bp.blogspot.com/-cjdjW0iyNN0/TxQtbAxX1CI/AAAAAAAAUvc/JCJOdofxANw/s1600/Shaaban+Dede%252C+Msondo.JPG
Add caption

MTUNZI na muimbaji mahiri nchini, Shaaban Dede, amesema anaendelea kumkumbuka na kumlilia aliyekuwa 'swahiba' wake mkubwa, marehemu Mohammed Mpakanjia 'Meddy Kitendawili' aliyefariki karibu miaka mitano iliyopita.
Dede akizungumza na MICHARAZO, alisema licha ya ukaribu aliokuwa nao na marehemu Mpakanjia, lakini kukwama kwake kufanikisha mipango ya kufyatua albamu binafsi ya nyimbo zake za zamani humfanya amkumbuke zaidi.
Mwanamuziki huyo anayeiimbia Msondo Ngoma na aliyewahi kufanya kazi na bendi kama Mlimani Park, OSS na Bima Lee, alisema albamu hiyo ambayo ingekuwa na nyimbo sita na zingetolewa kwa mfuatano wa Vol, ilikuwa ifadhiliwe na Mpakanjia mipango iliyokuwa imeanza kabla ya swahiba wake huyo kukumbwa na mauti.
"Japo imepita miaka mitano takriban mitano sasa, bado  namkumbuka na kumlilia Meddy Kitendawili kwa mengio aliyonitendea na kuutendea muziki wa Tanzania. Ukiacha uswahiba wetu, pia kila nionapo nimeshindwa kufanikisha mipango ya kutoa albamu binafsi ya nyimbo zangu za zamani zilizotunga na kuimba katika bendi nilizopitia miaka ya nyuma naumia zaidi,"  alisema.
Dede alisema, hata hivyo anaendelea kupigana ili kufanikisha jambo hilo, hasa akisaka mfadhili mwingine wa kumpiga tafu.
Meddy Mpakanjia, aliyekuwa mume wa Mtangazaji na Mbunge maarufu wa Vijana, Amina Chipupa, alifariki Sept 14, 2009 miezi kadhaa tangu mkewe huyo kufariki wakati akiwa kwenye harakati za mapambano dhidi ya biashara ya dawa za kulevya.

Arsenal kusuka au kunyoa kwa Bavarian

Arsenal watashangilia leo Ujeruman kama hivi kwa Bavarians
 ARSENAL yenye morali baada ya kufanikiwa kutinga Nusu Fainali ya Kombe la FA, usiku huu itakuwa ugenini nchini Ujerumani kujaribu kupenya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mbele ya watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Bayern Munich.
Wakali hao wa London Kaskazini walitoka kuifumua Everton kwa mabao 4-1 katika mchezo wa Robo Fainali na leo itataka kuthibitisha kuwa msimu huu imepania angalau kuambuli mojawapo ya mataji ya ubingwa baada ya misimu karibu nane ikitoka patupu.
Ikiwa nyumba kwa mabao 2-0 ilipofumuliwa nyumbani na Bavarian, Arsenal itajarubuy kupambana na kuzika mzimu wa kutolewa kwenye 16 Bora kwa misimu karibu minne.
Msimu ulipita ni Bayern Munich iliyowakwamisha baada ya kuwatungua nyumbani kwao 3-1 kisha kupata ushindi Ujerumani kwa mabao 2-0 hata hivyo ikatoka kwa faida ya mabao ya ugenini, kitendo kilichomuudhi koca Arsene Wenger kiasi cha kulitaka Shirikisho la Ulaya, UEFA kuangalia upta sheria hiyo.
Arsenal imepewa nafasi kubwa ya kuitoa nishai Bayern kama ilivyofanya msimu uliopita, ila kazi ipo kwao kutokana na ubora na kiwango cha juu ilichonacho Bavarian kwa sasa, ikicheza mechi 16 na kufunga jumla ya mabao 26.
Wikiendi hii wakati Arsenal ikiigaragaza Everton, wenyewe waliichachafya  VfL Wolfsburg kwa mabao 6-1 ingawa kocha wake, Pep Guardiola amenukuliwa akiwahofia wapinzani wao na hasa kama wachezaji waop wataamua kuwaacha wamiliki mpira.
Kurejea katika kiwango kwa Mesut Ozil na majeruhi kadhaa katika kikosi cha Gunners kunawapa matumaioni makubwa mashabiki wa Arsenal kwamba leo watavunja mwiko wa kuishia 16t Bora kwa misimu minne mfululizo kwa kuing'oa Bayern Munich na kuivua taji la michuano hiyo.
Hata hivyuo Bayern wapo vyema na hasa baada ya kurejea kwa nyota wao, Frank Ribery aliyekuwa majeruhi kwa muda mrefu kumeiongezea chachu ya kuhakikisha wanatinga robo fainali na kuendeela kujipa matumaini ya kutetea taji hilo.
Mbali na mechi hiyo pia leo kuna mechi nyingine ambayo inaikutanishaAtletico Madrid itakayokuwa nyumbani kurejea na AC Milan ambayo walikubali kipigo nyumbani kwao katika mechi iliyopita ya kwanza.
Michezo mingine inatarajiwa kuchezwa kesho kwa pambano la kukata na mundu kati ya Barcelona itakayokuwa nyumbani kuikaribisha Manchester City waliotota katika mechi ya kwanza kwa mabao 2-0 na pia wikiendi hii kujikuta wakitupwa nje kwenye michuano ya FA baada ya kuzabuliwa na watetezi wa taji hilo, Wigan Athletic kwa mabao 2-1.
Pia kesho PSG iliyopata ushindi mnono wa mabao 4-0 ugenini itaialika Bayer Leverkusen mjini Paris ili kuhitimisha nafasi yake ya kutinga robo fainali.

Msondo Ngoma wamaliza Suluhu

Baadhi ya watunzi na waimbaji wa albamu mpya ya Msondo Ngoma, Eddo Sanga na Juma Katundu
BENDI kongwe ya Msondo Ngoma hatimaye imekamilisha kurekodi nyimbo zake za albamu yao mpya iitwayo 'Suluhu' na ipo katika hatua ya mwisho kwa ajili ya kuziachia hewani kutuliza 'mzuka' wa mashabiki wake.
Akizungumza na MICHARAZO, mmoja wa viongozi na mwanamuziki wa bendi hiyo, Shaaban Dede 'Super Motisha' alisema Msondo imekamilisha kurekodi nyimbo hizo kwa mtayarishaji Malone Linje baada ya kipindi kirefu cha danadana juu ya suala hilo.
Dede ambaye ndiye mtunzi wa wimbo uliobeba jina la albamu hiyo, alisema nyimbo hizo zinahaririwa kwa sasa kabla ya kuanza kurushwa hewani na viongozi kujipanga kwa ajili ya uzinduzi wake.
'Tunashukuru kwa sasa tumeshamaliza kurekodi albamu yetu mpya, mashabiki waliokuwa na kiu ya muda mrefu sasa kiu hiyo imeisha kwani mambo yamekamilika nawakati wowote zitaachiwa hewani baada ya kuhaririwa," alisema.
Nyimbo zilizopo katika albamu hiyo ni pamoja na 'Suluhu' alioutunga Dede, ' Lipi Jema' na 'Baba Kibene' za Eddo Sanga, 'Nadhiri ya Mapenzi' wa Juma Katundu, 'Kwa Mjomba Hakuna Urithi-Huruka Uvuruge na 'Machimbo' uliotungwa na bendi nzima.
Mara ya mwisho Msondo kutoa albamu ilikuwa miaka minne iliyopita walipoachia 'Huna Shukrani' ilikuja baada ya bendi hiyo kuzindua albamu yao ya 'Kicheko kwa Jirani' mwaka 2010.

Waamuzi wa soka kunolewa Dar

http://www.eatv.tv/media/picture/large/waamuzi(4).jpg
Baadhi ya waamuzi wakiwa uwanjani
WAAMUZI na waamuzi wasaidizi 22 wameteuliwa kushiriki semina na mtihani wa utimamu wa mwili kwa robo ya kwanza ya mwaka huu itakayofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Machi 14 hadi 16.

Semina hiyo inashirikisha waamuzi wote wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na wale wa ngazi ya juu (elite) kutoka Tanzania Bara za Zanzibar.

Waamuzi hao ni Charles Simon (Dodoma), Dalila Jafari (Zanzibar), Ferdinand Chacha (Mwanza), Hamis Chang’walu (Dar es Salaam), Helen Mduma (Dar es Salaam), Israel Mujuni (Dar es Salaam), Issa Vuai (Zanzibar), Janeth Balama (Iringa), Jesse Erasmo (Morogoro), John Kanyenye (Mbeya) na Jonesia Rukyaa (Bukoba).

Josephat Bulali (Zanzibar), Lulu Mushi (Dar es Salaam), Martin Saanya (Morogoro), Mfaume Nassoro (Zanzibar), Mohamed Mkono (Tanga), Mwanahija Makame (Zanzibar), Ngaza Kinduli (Zanzibar), Oden Mbaga (Dar es Salaam), Ramadhan Ibada (Zanzibar), Samwel Mpenzu (Arusha) na Waziri Sheha (Zanzibar).

Wakufunzi wa semina hiyo ambao wanatambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) ni Joan Minja na Riziki Majala.

Mawakala wa wachezaji kutahiniwa April 3

MTIHANI kwa ajili ya watu wanaotaka kuwa mawakala wa wachezaji wanaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utafanyika Aprili 3 mwaka huu saa 4 kamili asubuhi ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (FIFA). Kwa wanaotaka uwakala huo wanatakiwa kujisajili ambapo watapewa kanuni mbalimbali za FIFA na TFF ili waweze kujiandaa kikamilifu kwa mtihani huo utakaokuwa na sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ya mtihani huo ni maswali kutoka FIFA wakati nyingine ni kutoka TFF.
Tanzania ina mawakala watatu tu wa wachezaji wanaotambuliwa na FIFA. Mawakala hao ni Ally Saleh, John Ndumbaro na Mehdi Remtulla.

Babi apewa unahodha Malaysia

Photo: Thamani.yangu na uwezo .wangu na nithamu yangu ndio inayonifanya .nipewe ukepten..ndani ya nchi na nje ya .nchi..nawatakia kila la heri YANGA..
Babi (kushoto-mbele) akiwa na kitambaa cha unahodha
KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa nchini Malaysia, Abdi Kassim 'Babi' ameteuliwa kuwa nahodha wa timu ya UiTM inayoshiriki Ligi Kuu ya nchi hiyo.

Babi alipewa unahodha huo wiki iliyopita alipoingoza timu hiyo katika mchezo dhidi ya 'vibonde' wa ligi hiyo Perlis na kupoteza mchezo huo wa ugenini kwa kulala mabao 2-1.

Kiungo huyo wa zamani wa Taifa Stars, aliiambia MICHARAZO kuwa nidhamu na kiwango bora cha soka alichokionyesha tangu atue katika timu hiyo ndicho kilichofanya apewe cheo hicho na kusema anamshukuru Mungu.

"Ninajisikia fahari kupewa cheo hicho baada ya viongozi na wachezaji kuridhika na uwezo wangu uwanjani na nidhamu kubwa niliyonayo ni furaha kwangu hasa ikizingatiwa nipo ughaibuni," alisema Babi.

Kuhusu mechi yao ya Ijumaa, Babi alisema walifungwa kimchezo katika pambano hilo la ugenini lililochezwa kwenye uwanja wa Darul Aman mjini Alor Setar, likiwa pambano lao la tatu mfululizo kupoteza. Wako katika nafasi ya tisa wakiwa na pointi nne tu.

"Tumefungwa kimchezo na kwa muda kulikuwa na mgogoro wa kiuongozi ambao kwa sasa umeisha na tunajipanga kwa mechi yetu ya Ijumaa hii tutakayocheza nyumbani," alisema Babi, nahodha wa zamani wa Yanga.


UiTM itaumana na DRB-Hicom katika mechi ambayo Babi ametamba kwamba timu yake wataibuka na ushindi katika mechi hiyo itakayochezwa uwanja wa Mini UiTM, katika mji wa Shan Alam.

Babi aliyewahi kuzichezea pia Mtibwa Sugar, Azam na KMKM kabla ya kutimkia Malaysia alikosaini mkataba wa mwaka mmoja, alisema ligi ya nchi hiyo ni ngumu na imejaa ushindani tofauti na alivyofikiria mwanzoni.

Ajali yachukua roho ya mmoja wengine wajeruhiwa

Gari la Hood likiwa limepinduka na majeruhi wakipigania uhai wao
Abiria wakiwa hawaamini kama wamenusurika kifo
AJALI zimeendelea kutikisa Tanzania, baada ya Basi la Hood linalofanya safari zake kutoka Arusha kwenda Mbeya, namba za usajili T.488 AXV aina ya Scania kupata ajali mbaya leo asubuhi na kusababisha kifo cha mtu mmoja na abiria wengine karibu 20 kujeruhiwa.

Ajali hiyo imetokea majira ya saa tatu katika, barabara ya Same - Mwanga, Kijiji cha Kiverenge wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro ambapo taarifa za awali zinasema  kuwa chanzo chake ni kupasuka kwa tairi ya mbele.

Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Robert amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema katika ajali hiyo alifariki Abiria mmoja aliyemtaja kwa jina la Joshua Likumbia, Raia wa Kenya, ambaye alikuwa akisafiri kuelekea jijini Mbeya.

Kamanda Boaz amesema majeruhi katika ajali hiyo ambao ni 16, akiwemo dereva wa Basi, Fadhili Hashim wamelazwa katika Hospitali ya wilaya ya Same na Hospitali ya Rufaa mkoani Kilimanjaro, KCMC.

Kamanda Boaz ameendelea kufafanua kuwa majeruhi hao nane wamelazwa Same huku wengine 8 wakikimbizwa mjini Moshi katika hospitali ya KCMC kutokana na hali zao kuwa mbaya ambapo watatu kati yao wakia wamelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Ratiba ya VPL yapanguliwa tena

Na Boniface Wambura
BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeifanyia marekebisho ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) ambapo sasa itamalizika Aprili 19 mwaka huu badala ya Aprili 27 mwaka huu. 
Marekebisho hayo yamefanyika ili kutoa fursa kwa timu ya Taifa, Taifa Stars, kujiandaa kwa mechi za mchujo la Kombe la Afrika 2015 ambapo itacheza raundi ya awali Mei mwaka huu.
Kutokana na marekebisho hayo, Yanga itacheza na Prisons (Uwanja wa Taifa) Machi 26 mwaka huu katika mechi ya raundi ya 17 wakati Machi 19 mwaka huu kwenye uwanja huo huo ni Yanga na Azam.
Machi 15 mwaka huu kutakuwa na mechi mbili; Azam na Coastal (Azam Complex), na Mtibwa Sugar itacheza na Yanga (Jamhuri). Mgambo na Azam zitacheza Machi 26 mwaka huu Mkwakwani, na Aprili 9 mwaka huu Yanga itaialika Kagera Sugar (Taifa).
Raundi ya 22 itaanza Machi 22 mwaka huu kwa mechi kati ya Kagera vs Prisons (Kaitaba), JKT Ruvu vs Mbeya City (Azam Complex), na Rhino vs Yanga (Ali Hassan Mwinyi). Machi 23 mwaka huu ni Simba vs Coastal (Taifa), Mgambo vs Mtibwa (Mkwakwani), Ruvu Shooting vs Ashanti (Mabatini) na Azam vs Oljoro (Azam Complex).
Machi 29 mwaka huu itaanza raundi ya 23 kwa mechi kati ya Ashanti vs Oljoro (Azam Complex) wakati Machi 30 ni Mbeya City vs Prisons (Sokoine), Kagera vs Ruvu Shooting (Kaitaba), Mtibwa vs Coastal (Manungu), JKT Ruvu vs Rhino (Azam Complex), Azam vs Simba (Taifa), na Mgambo vs Yanga (Mkwakwani).
Raundi ya 24 inaanza Aprili 5 mwaka huu kwa Kagera vs Simba (Kaitaba), Ashanti vs Mbeya City (Azam Complex). Aprili 6 mwaka huu ni Coastal vs Mgambo (Mkwakwani), Oljoro vs Prisons (Sheikh Kaluta Amri Abeid), Rhino vs Mtibwa (Ali Hassan Mwinyi), Ruvu Shooting vs Azam (Mabatini) na Yanga vs JKT Ruvu (Taifa).
Aprili 12 mwaka huu inaanza raundi ya 25 kwa Mtibwa vs Ruvu Shooting (Mabatini), Coastal vs JKT Ruvu (Mkwakwani), Prisons vs Rhino (Sokoine). Aprili 13 mwaka huu ni Mgambo vs Kagera (Mkwakwani), Simba vs Ashanti (Taifa), Mbeya City vs Azam (Sokoine) na Oljoro vs Yanga (Sheikh Kaluta Amri Abeid).
Raundi ya 26 ni Aprili 19 mwaka huu kwa Rhino vs Ruvu Shooting (Ali Hassan Mwinyi), Mbeya City vs Mgambo (Sokoine), Prisons vs Ashanti (Jamhuri, Morogoro), JKT Ruvu vs Azam (Azam Complex), Oljoro vs Mtibwa (Sheikh Kaluta Amri Abeid), Coastal vs Kagera (Mkwakwani) na Yanga vs Simba (Taifa).

Monday, March 10, 2014

Mpiga Drums Extra Bongo awashtua Wajumbe Bunge la Katiba

Mpogoro Machine akikaanga chipa mazoezi ya Extra Bongo
MPIGA dramu wa bendi ya Extra Bongo 'Wana Kimbembe', Wenceslaus Chitalula 'Mpogoro Machine', amewaomba Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kufanya kile walizotumwa na wananchi.
Mwanamuziki huyo alisema malumbano na muda unaopotezwa na wajumbe hao kwenye bunge hilo mjini Dodoma ni kutowatendea haki wananchi wanaosubiri kuona wanawasaidia kupata Katiba Mpya.
Mpogoro alisema anashindwa kufahamu iweje tangu wajumbe hao wakutane Dodoma karibu mwezi mzima unafika sasa wameshindwa kupata muafaka ili mchakato wa kuijadili rasimu ya katiba uanze.
Alisema ni lazima wajumbe hao watambue kuwa wameteuliwa na Rais na kutumwa na wananchi kuhakikisha Tanzania inapata Katiba Mpya yenye kukidhi matakwa ya watanzania hivyo wafanye kazi yao.
"Malumbano yanayoendelea kwenye Bunge kiasi cha kushindwa kufanya kile walichotumwa kwa hakika ni kutomtendea haki Rais na wananchi waliowatuma kwenda kuipatia nchi katiba mpya,' alisema.
Kumekuwa na malumbano ya baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo na kusababisha kila mara kuahirishwa kuanza kazi inayosubiriwa kwa hamu na watanzania kitu ambacho kimezua lawama kila kona ya nchi.

TFF yaiomba radhi serikali, ila yaapa kufa na 'wahuni' Taifa

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgOwi8JlabIoxGmPjw0ajGnnjyghJpOiAcjEg49cjFUyOVaYL5xsBWUM5viTvW1dhxFIWd38S_8PJgsQXwERt1iEAVMMJOWVP59_f0VmOMPJmLqCnLDeDKKJjGGT7W-hIe_4QFZ-OxDLhAu/s1600/8.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjDAqMNfB8sT1Kd3J3S3e3BzZvFIkoYfeHckcsPzbSrO-WE9mcigQc-SDLezqEyxG9Hv2t4qwZ069BFQ1KnZVvPn5IZSiNAaAW-7P_DfjjSYkHTeVMyU4zIvdIVmLy_jBiptshByI4RtkYS/s1600/9.jpgSHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limelaani vikali fujo na uhabirifu wa mali unaofanywa na washabiki viwanjani wakati mechi mbalimbali zikiwemo zile za kimataifa na ligi za hapa nchini.
TFF  imeiomba radhi Serikali kwa uharibifu wa viti uliotokea kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga ya Tanzania na Al Ahly ya Misri iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Machi 1, mwaka huu.
Imesema uharibifu huo wa viti umesababisha hasara ya Sh. milioni 15 kwa wamiliki wa uwanja huo ambao ni Serikali. TFF tutalipa fedha hizo kwa Serikali kutokana na uharibifu huo.
“Tunaendelea kuchunguza tukio hilo, huku tukijiandaa kutoa adhabu kwa klabu na washabiki husika kulingana na kanuni zetu. Adhabu itakuwa kali ili iwe fundisho kwa wengine,”imesema taarifa ya TFF.
Kwa mujibu wa Serikali, viti 10 viling’olewa na kutupwa ovyo ovyo uwanjani wakati vingine 40 viliathirika kutokana na vurugu za watazamaji hao na TFF imekubali kubeba dhamana ya kulipa uharibifu huo kwa kuwa wao ndio wenye dhamana ya kusimamia mechi za kimataifa na ndiyo walioomba idhini ya kutumika uwanja huo kwenye mechi hiyo.
“Kwa vile sasa baadhi ya washabiki, wapenzi na wanachama wa klabu mbalimbali nchini wanataka kufanya suala la uharibifu kuwa la kawaida na mazoea, Serikali inakusudia kuchukua mapato yote ya mchezo husika endapo kutatokea uharibifu,”.
“Pia kuruhusu uwanja kutumiwa bila watazamaji kwa baadhi ya mechi, na kutoruhusu uwanja huo kutotumika kabisa kwa baadhi ya mechi,”imesema taarifa ya TFF.

Japanese anogewa ughaibuni

Japanese kikazi zaidi

Amina Ngaluma 'Japanese' akifurahia maisha Ughaibuni
MUIMBAJI nyota wa zamani wa bendi mbalimbali nchini ikiwamo Double M Sound, African Revolution 'Wana Tamtam', Amina Ngaluma 'Japanese' amesema hana mpango wa kurejea nchini kwa sasa kutokea ughaibuni anakofanya shughuli zake za muziki na bendi ya Jambo Survivors kwa madai muziki wa Tanzania umejaa 'wizi mtupu'.
Akizungumza na MICHARAZO kutoka Thailand walipoweka maskani yao ya kudumu, Ngaluma alisema haoni ya sababu ya kurudi nyumbani kwa sasa wakati maisha yamemnyookea ughaibuni akiwa na bendi hiyo inayopiga muziki asilia na iliyoweka maskani ya kudumu nchini humo.
"Kwa kweli sifikirii kurudi nyumbani leo wala kesho, hii ni kutokana na kuona tofauti kubwa ya kuthaminika kwa wanamuziki kati ya huko na hapa tulipo tukiendeleza makamuzi na bendi ya Jambo Survivors," alisema Japanese aliyetamba na wimbo wa 'Mgumba II'.
Ngaluma alisema muziki wa Tanzania umeshindwa kuwanufaisha wanamuziki wake kutokana na kuwapo kwa unyonyaji kuanzia kwa wamiliki wa bendi mpaka wadau wanaousimamia kama wasambazaji na hata wananchi wanaowaibia wasanii kazi zao bila kujali wala kuwahurumia wanavyovuja jasho lao.

Noma! Ronaldo ndiye mchezaji tajiri duniani

NYOTA wa Ureno anayeichezea Real Madrid, Cristiano Ronaldo ndiye mwanasoka tajiri kuliko wote duniani.
Kwa mujibu wa mtandao wa Goal.com, nahodha huyo watimu ya taifa ya Ureno ndiye kinara katika orodha hiyo iliyotangazwa leo.
Mkali huyo amerithi nafasi hiyo ya kwanza iliyokuwa ikishikiliwa na David Beckham kwa muda mrefu kabla hajastaafu soka msimu uliopita. 
Ronaldo ambaye alisaini mkataba mnono zaidi na Real Madrid miezi kadhaa iliyopita amempita mshindani wake Lionel Messi na mwanasoka anayelipwa zaidi kimshahara Wayne Rooney.
Samuel Eto'o ndiye Mwaafrika pekee aliyeingia kwenye listi ya wanasoka matajiri zaidi duniani.
Hii ndiyo orodha kamili:
1. Cristiano Ronaldo £122m
2. Lionel Messi £120.5m
3. Samuel Eto'o £70m
4. Wayne Rooney £69m
5. Kaka £67.5m
6. The Neymar family £66m
7. Ronaldinho £64m
8. Zlatan Ibrahimovic £57m
9. Gianluigi Buffon £52m
10.Thierry Henry £47m
SOURCE: Goal.

Ronaldo azidi kuipaisha Real Madrid

High flying: Cristiano Ronaldo hurdles Levante's goalkeeper Keylor Navas
Ronaldo akiwajibika uwanjani
MSHAMBULIAJI Cristiano Ronaldo usiku wa jana alisaidia timu yake kuzidi kujichimbia kileleni baada ya kufunga moja ya mabao yaliyoisaidia Madrid kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Levante.
Real Madrid imefikisha pointi 67 na kuwakimbia Atletico Madrid wenye pointi 64 timu zote zikiwa zimecheza mechi 29.
Ronaldo alifunga bao hilo katika dakika ya 11 akiunganisha kona ya Angel Di Maria kabla ya kumtengenezea pande zote Marcelo aliyefunga bao la pili.
Bao la tatu la vinara hao lilitiwa kimiani na Karabellas dakika ya 81.
Katika mchezo huo Levente walipata pigo baada ya David Navarro kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kosa la kumchezea vibaya Ronaldo katika dakika ya 49.
Barcelona ambayo juzi ilikandikwa na vibonde Real Valledolid ipo katia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 63 na kutishia amani utetezi wa taji lake la La Liga msimu huu.

Maskini Yanga yakwama Misri, matuta yawatoa Afrika

LICHA ya kutolewa, lakini Yanga inastahili pongezi kwa kupigana kiume mbele ya mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa wa Afrika, Al Ahly baada ya kung'olewa kwa mikwaju ya penati katika pambano la marudiano lililochezwa usiku wa jana.
Yanga ilipambana kwa dakika 90 na kujikuta wakilala kwa bao 1-0 na kufanya matokeo ya jumla kuwa 1-1 na hivyo kuingia kwenye hatua ya upigaji wa penati ambapo ilionekana dhahiri walikuwa wakielekea kufuzu baada ya Deo Munishi Dida kudaka penati mbili za Wamisri.
Dida aliyeonyesha ushupavu mkubwa alidaka penati za Saed Mowaeb na Hossan Ashour huku zile za Abdalllah Said, Gedo, Mahmoud Trezeguet na Mohamed Nagieb zilimpita.
Hata hivyo Oscar Joshua alikosa penati naye na baadaye Bahanuzi aliyekuwa akimalizia mikwaju ya penati tano tano, alipaisha mkwaju wake wakati wachezaji wenzake wakijiandaa kushangilia kuwavua ubingwa Al Ahly na kuongezwa penati moja moja.
Katika hatua hiyo Mbuyi Twite alilizamisha jahazi la Yanga baada ya kukosa mkwaju wake na kuwafanya mabingwa watetezi hao kufuzu hatua ya pili na kutarajia kukutana na waarabu wenzao kutola Libya, Al Ahli Benghazi.
Kwa wastani Yanga ilikuwa imejiandaa kuweka rekodi kwa soka la uhakika na umakini mkubwa iliyooonyesdha katika mchezo huo kwa kuwabana wenyeji wao kwenye uwanja wa  Border Guard mjini Alexandria.
Kipindi cha kwanza kiliisha kwa sare ya kutofungana  kabla ya wenyeji kupata bao dakika za jioni baada ya mabeki wa Yanga kujichanganya kuokoa mpira uliokwamishwa na  Sayed Moawad. dakika ya 71.
Ndipo ikaja hatua ya kupigiana penati baada ya dakika 90 kumalizika kwa matokeo hayo yaliyofanya timu hizo kuwa nguvu sawa kwani Yanga ilishinda bao 1-0 nyumbani wiki iliyopita na zikaja penati na Yanga wakapata penati zao kupitia nahodha Nadir Cannavaro, Emmanuel Okwi na Didier Kavumbagu.
Kung'olewa kwa Yanga kumehitimisha safari ya timu za Tanzania kwenye michuano ya kimataifa baada ya awali Azam, KMKM na Chuoni kung'oka raundi ya awali katika Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho.