STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 18, 2014

Arsenal chupuchupu, Chelsea yaua, Southampton nouma

Arsenal walipotungulia mapema mabao kabla ya kuyarejesha
Alexis Sanchez (kushoto) akipongezwa kwa kufunga bao la kuongoza la Arsenal
Cesc Fabregas akishangilia bao lake wakati Chelsea wakishinda ugenini
Southampton celebrate
Southampton wakishangilia karamu yao ya mabao
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJ8gVj4IzJtst16bFSW_FamQning4RDHnfQOlk3S1lv7CaHgAJvnfydlnLb1oqRZ8Y_RYiOcVgXAYzeQqhG40uG3ylSssbREGAk_Z23vGsZQkGAT29YghLNR-XJbx03NmjYbznx1efM9g/s1600/1413638977348_Image_galleryImage_Manchester_City_s_Argenti.JPG
Kun Aguero akishangilia moja ya mabao yake manne mapema leo walipoiua Spurs
MSHAMBULIAJI Danny Welbeck ameendelea kuonyesha jinsi gani alivyo muhimu ndani ya Arsenal baada ya kuifungia timu hiyo bao katika dakika za lala salama na kuwaepushia wapiga mtutu hao wa Emirates kuambulia sare ya mabao 2-2 ikiwa nyumbani dhidi ya Hull City.
Welbeck aliyekuwa hapewi umuhimu wowote katika kikosi cha Manchester United na hivyo kuuzwa kwa Arsenal, alifunga bao hilo dakika za nyongeza kabla ya pambano kumalizika na kumpa nafuu meneja wake, Arsene Wenger.
Mshambuliaji huyo nyota wa England alifunga bao hilo akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Alexis Sanchez, ambaye alianza kuwafungia wenyeji  bao dakika ya 13 kwa kumalizia kazi ya Per Martesacker.
Wageni walifunga mabao yao katika dakika ya 17 kupitia Mohammed  Diamé kisha kuongeza la pili dakika chache baada ya kipindi cha pili kuanza kupitia kwa Abel Hernandez.
Katika mechi ya mapema leo, Sergio 'kun' Aguero aliisambaratisha Tottenham Hotspur waliowafuata nyumbani kwenye uwanja wa Etihad baa da ya kufunga mabao manne wakati wakiwazisha vijogoo hao wa London ya Kaskazini kwa mabao 4-1. Mabao mawili yakiwa kwa mikwaju ya Penati.
Chelsea ikiwa ugenini ilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace kwa mabao ya Oscar aliyefunga dakika ya sita kabla ya Cesc Fabrages kuongeza la pili dakika ya 51 na Campbell akaipatia bao la kufutia machozi wanyeji katika dakika ya 90.
Nayo Southampton ikiwa nyumbani iliwasambatarisha Sunderland kwa kuwafunga mabao 8-0 ikiwa ni rekodi ya kipigo kikubwa katika msimu huu wa ligi ya England, huku    Burnley ikiwa nyumbani ilifumuliwa mabao 3-1 na West Ham United na Everton walishinda nyumbani kwa mabao 3-0 dhidi ya Aston Villa.
Ushindi wa Southmpton umeifanya timu hiyo kufikia rekodi mojawapo ya mechi iliyokuwa na ushindi mnono ikienda sambamba na mechi nyingine tano tangu Ligi Kuu ilipoanza kutumika rasmi 1992 toka daraja la kwanza nchini humo..
Mechi nyingine za awali ni;
Manchester United 9-0 Ipswich, March 1995
Newcastle United 8-0 Sheffield Wednesday, September 1999
Tottenham Hotspur 9-1 Wigan Athletic, November 2009
Chelsea 8-0 Wigan Athletic, May 2010
Chelsea 8-0 Aston Villa, December 2012
Southampton 8-0 Sunderland, October  2014

Simba, Yanga debe tupu, Azam yaua, Mtibwa yabanwa

Mpambano wa watani ulivyokuwa uwanja wa Taifa leo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnGI0Fa_A1fReGNq630wAe-HUeAeC3CnzyXNWI0OAPfBgI-aka3Ybg_uU2XVpZaMurdewSapeGfrEvocd18umDQjB5vFdhDmsHEVhTWCSFg3rp4vfk7e-UZaT1IRvH4QtZHSFcKp6a8H7v/s1600/Picha+Simba.JPGhttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgNPa5lzs3_DyhJWIBPQ4eR7PVVwEV7kBsmZgbFj2NkFWHudak-xT3RA29hwYq_es9UcaOF5fj0I9w9hmoY_GT4jyCWZ2zMxmOX1zN7vws4XBFeRVRUgqalCm9eoug3LZYGSjq7wMFA9_PP/s1600/Yanga+leo+1.JPGWAPINZANI wa jadi wa soka Tanzania, Simba na Yanga zimeshindwa kutambiana katika pambano lao lililochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa, licha ya tambo za mapema kabla ya mchezo huo, huku Azam wakijikwea kileleni mwa msimamo wakiipiku Mtibwa Sugar waliobanwa mjini Morogoro.
Simba na Yanga ambazo zilikamiana na kutambiana kwa wiki kadhaa sasa, walishindwa kufungana katika pambano lililoshuhudia mtoto wa nyota wa zamani wa Mtibwa, Yanga na Taifa Stars, Manyika Peter, kipa Peter Manyika Jr aking;ara kwa kuinyima Yanga mabao kwenye uwanja huop wa Taifa.
Timu zote ilifanya kosa kosa za hapa na pale na has akwenye kipindi cha pili huku makocha wao, Marcio Maximo wa Yanga na Patrick Phiri wa Simba wakifanya mabadiliko ya wachezaji bila kuleta tija hadi dakika 90 za pambano lililochezeshwa vema na mwamuzi Israel Mujuni Nkongo.
Kwa matokeo hayo Yanga imefikisha pointi 7 na kushuka hadi nafasi ya nne wakiwapisha Coastal Union kukalia nafasi hiyo baada ya jioni ya leo kushinda mabao 2-0 dhidi ya Mgambo na kufikisha idadi kama hiyo ya pointi ila ikiwa na uwiano tofauti ya mabao, huku watani zao hiyo ikiwa ni sare yao ya nne msimu huu na ikifikisha mechi ya 10 katika ligi bila kuonja ushindi imefikisha pointi nne.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Azam waliwafyatua Mbeya City nyumbani kwao kwenye uwanja wa Sokoine kwa bao 1-0 na kufikisha idadi ya mechi 38 bila kupoteza katika Ligi Kuu..
Bao hilo liliwekwa kimiani na beki wake wa kati, Aggrey Morris kwa mkwaju wa adhabu kwenye dakika ya 19 na kuifanya mabingwa watetezi hao kukwea kileleni wakifikisha pointi 10 sawa na Mtibwa Sugar ambao walilazlmishwa suluhu mjini Morogoro na ndugu zao Polisi Moro kwenye uwanja wa Jamhuri.
Azam na Mtibwa zote zimefungana idadi ya pointi zikiwa na 10 kila moja, huku wakiwa na mabao sita kila moja na kufungwa moja, isipokuwa kiherufi Azam inawatangulia Wakata Miwa.
Kutoka Mkwakwani Tanga, Coastal Union imezidi kujiongezea pointi baada ya kuilaza Mgambo JKT kwa mabao 2-0.
Mabao ya washindi yalifungwa na Rama Salim kwa mkwaju wa penati kabla ya Kennedy Masumbuko kuongeleza la pili kwenye kipindi cha pili.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEheu2S3fe_9FoFd7hnk3AwEiXmoOP2ulk9Y13fiRJl12EdBwVuaIaC0y1ulilytUphp2lKiDBXt3tJkB_gfKPzweV4tFKqdIhBe-kGqjPOH6NhkBOCD0sjIxEJ00LhbAeNd57i_xQ_Yrxkh/s1600/20140913_160438.jpg
Ndanda waliopigwa nyumbani na Ruvu Shooting

Nayo timu ya Ruvu Shooting wakiwa ugenini mjini Mtwara wamewatoa nishai wenyeji wao Ndanda Fc kwa kuwalaza mabao 3-1, mabao ya washindi yakiwekwa kimiani na Juma Nade, Abdurahman Mussa na Mathew. ilihali Kagera Sugar wakiwa nyumbani wamelazimishwa suluhu ya kutofungana na Stand United.
Ruvu waliovunja mwiko wa kutofunga bao lolote katika ligi ya msimu huu kwa kuilaza Ndanda mabao 3-1
Mtibwa iliyobanwa mbavu na Polisi na kutoka suluhu

Chelsea katika kibarua kizito England

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/03008/Chelsea4_3008183b.jpgVINARA wa Ligi Kuu ya England, Chelsea wataelekea kwa wapinzani wao jijini London Crystal Palace Jumamosi wakilenga kupanua mwanya wa alama tano walioweka kileleni mwa Ligi hiyo baada ya mapumziko ya kimataifa.
Palace walishangaza Chelsea, na klabu nyingine katika ligi, kwa kushinda dhidi ya Chelsea msimu uliopita na nahodha wa Blues John Terry amepuuzia mbali madai kwamba tayari mshindi wa ligi msimu huu amejulikana.
“Ni wazi (kwamba kinyang’anyiro cha ligi) hakijaisha,” amesema Mourinho.
“Klabu nyingine zimejipata katika nafasi kama hii. Ni vyema kuongoza lakini ukiwa juu, kila mtu hutaka kukuangusha.
“Hilo ndilo jambo zuri kuhusu Ligi ya Premia na ndio maana kila mtu huipenda. Timu zinalenga kutushambulia kwa sababu tuko juu na twacheza vyema.”
Mabingwa watetezi Manchester City, walio wa pili kwa sasa, watakuwa nyumbani dhidi ya Tottenham Hotspur na kiungo wa kati anayeichezea City kwa mkopo Frank Lampard amewaambia wachezaji wenzake wajihadhari dhidi ya Spur ambao wameanza kuamka.
“Huenda wanapitia kipindi cha mpito lakini nilifurahishwa sana na meneja wao (Mauricio Pochettino) alipokuwa Southampton na ikiwa anaweza kufanya hayo Tottenham, ambao bila shaka wana vipaji kwenye kikosi chao, watafana. Ni timu nzuri sana.”

Gallas atundika galuga kimataifa

http://purelyfootball.com/wp-content/uploads/2014/08/1756906_201007087783881-1.jpg 
BEKI wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa, aliyewahi kutamba na klabu za Arsenal na Tottenham Hotspur, William Gallas ametangaza kustaafu soka rasmi baada ya kupita miaka 19 akicheza mchezo huo. 
Gallas mwenye umri wa miaka 37 amesema alikuwa akijiambia mwenyewe kwamba anaweza kuendelea lakini anadhani wakati umefika sasa wa kuamua kutundika daruga. 
Mkongwe huyo ambaye alianza rasmi soka lake katika klabu ya Caen mwaka 1995, aemcheza mechi 84 za kimataifa akiwa na Ufaransa na kufunga mabao matano likiwemo bao la utata katika ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa mtoano dhidi ya Ireland uliowapa nafasi ya kushiriki Kombe la Dunia mwaka 2010. 
Gallas pia alicheza katika Kombe la Dunia mwaka 2006 nchini Ujerumani ambapo Ufaransa ilifungwa na Italia kwa changamoto ya mikwaju ya penati. 
Baada ya kuitumikia klabu ya Olympique Marseille kuanzia mwaka 1997 mpaka 2001, Gallas alihamia Chelsea ambako alishinda mataji ya Ligi Kuu mwaka 2005 na 2006 na kujiunga na Arsenal msimu uliofuata kabla ya kuhamia Tottenham Hotspurs mwaka 2010. 
Octoba mwaka jana Gallas alisaini mkataba wa mwaka mmoja na klabu ya Perth Glory inayoshiriki Ligi Kuu nchini Australia maarufu kama A-League.

WASANII WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA KILIMO KWANZA,

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghpa5vbwvmheywlGByFh8o7yO3Lc5-fMZmE0gO73qD27VxUBAhXb1yN7qEolYtIdZPYrCRKFKvR7QrWlUIS7-zb28hnDj9JlTvIe8GHj8K76kVfYhyphenhyphen1izNYfjmIKGjUEfdT4Yi-zGK0-dN/s1600/shiwata.JPG
Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Twalib
MCHUNGAJI wa Kanisa la KKKT, John Solomoni, ameshangazwa na kitendo cha idadi ndogo ya wasanii kujitokeza katika kununua mashamba ya bei rahisi yanayotolewa na Shirikisho la wasanii Tanzania(SHIWATA( yaliyopo Kijiji cha Ngarambe Wilayani Mkuranga.
Solomoni  ambaye pia ni Katibu wa kamati ya amani ya viongozi wa Dini mkoa wa Dar es Salaam,aliyasema hayo juzi katika hafla ya kuoneshwa mashamba kwa wasanii hao iliyoendana sambamba na maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
Alisema kitendo kilichofanywa nawasanii inaonesha ni jinsi gani bado haewajaanza kujitambua katika kutengenezamaisha yao ya mbeleni.
Alisema kiasi cha shilingi 200,000 kinachotozwa kwa ajili ya msanii kupata ekari moja na nusu ni kidogo sana ukilinganisha na thamani ya ardhi ilivyo sasa lakini anawashangaa kwa nini wasanii wameshindwa kujitokeza kama ilivyotarajiwa.
“Hapa nimeambiwa shirikisho lina wasanii zaidi ya 8000 wakiwemo wasanii wakubwa wenye majina lakini kwa nini ni 95 tu ndio wanunue mashamba hii ni aibu na kushindwa kujitambua nyie ni kina nani mbele ya jamii,”alisema Mchungaji Solomon.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Wilaya ya Mkuranga,Saada Mwaruka, alisema kama Wilaya watawapa ushirikiano wa hali na mali wasanii waliochukua mashamba hayo ikiwemo kuwakopesha pembejeo za kilimo.
Mwaruka alisema wanataka waone  eneo hilo linakuwa shamba darasa la kuigiwa mfano jambo litakalowaamsha vijana wa Mkuranga nao kujishughulisha na kilimo na kuona kilimo sio kazi ya waliokosa kazi bali ni moja ya njia za kuwainua kiuchumi.
Naye Mwenyekiti wa Shiwata, Cassim Taalib, alisema  wameamua kubuni mbinu hiyo ili kuwaondoa wasanii wa nchi hii katika umasikini.
Taalib alisema katika mashamba hayo kuna jumla ya ekari 500 kwa ajili ya kulima huku awali walitangulia kagawa eneo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba robo ekari kwa kila msanii lililopo maeneo ya Mwanzega huko huko Wilayani Mkuranga ili nao waweze kumiliki nyumba.
Alisema utaratibu huo ndio ulitumiwa na Mwalimu Nyerere wakati wa kuhamasisha vijiji vya Ujamaa ambako mpaka leo watu wameona matunda yake.

SIMBA, YANGA MWISHO WA TAMBO LEO TAIFA

Simba
Yanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-gq39K7CdJepat14klzaYSKkbOOhTk4agTfimjq9e_T_i79-pSKFHrC001eHuYXQ6J66Ddn1velG_DzJ9mP9Z6oGjeZC2ZIPr2Rc51jI6a4QvPo15HKLVYLKybQY2AbSGUsgkhBIKlL0/s1600/katuni_watani.jpg
Katuni ya Chris Katembo nayo inazungumza je nani ataibuka mbabe leo Taifa?
BAADA ya tambo, kejeli na majigambo ya muda mrefu baina ya Simba na Yanga, hatma yote inatarajiwa kufahamika leo baada ya pambano lao litakalofanyika kwenye uwanja wa Taifa.
Simba na Yanga zinakutana katika pambano la 78 la Ligi Kuu tangu mwaka 1965, huku Yanga wakiwa wababe wa Simba kwa kushinda mara 29 dhidi ya 22 za watani zao wanaotokea kambini nchini Afrika Kusini.
Timu hizo zinakutana leo kwenye dimba hilo huku Simba wakionekana wachovu zaidi kulinganisha na Yanga msimu huu wakikamata nafasi ya 10 baada ya mechi za raundi tatu, wakati wapinzani wao wakiwa nafasi ya tatu wakitofautiana kwa pointi tatu.
Simba haijashinda pambano lolote kati ya 9 iliyochezwa kumalizia msimu uliopita na katika mechi za msimu huu, zaidi ya kuambulia sare tu.
Hata hivyo pambnano la watani huwa haliamuliwi kwa kuangalia rekodi kama hizo, kwani lolote huweza kutokea na kushangaza wale wanaotabiri labda kwa kuangalia udhaifu wa timu.
Mashabiki wa Yanga kwa sasa ni kama wanashangilia ushindi dhidi ya watani zao, lakini soka ni baada ya dakika 90 kwani lolote linaweza kutokea na kushangaa Simba wanaoonekana wanyonge kuibuka na ushindi dhidi ya watani zao.
Yanga inapewa nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi kwenye mchezo huo kutokana na matokeo waliyoyapata kwenye michezo mitatu ya kwanza ya ligi kuu ya Bara ukilinganisha na sare tatu mfululizo za mtani Simba.
Yanga iliyoshinda michezo miwili, ina ponti tatu zaidi ya Simba kutokana na kufungwa na viongozi wa ligi Mtibwa katika mechi ya ufunguzi wa msimu.
Tayari makocha wa timu zote mbili wamekuwa wakitoa kauli tofauti kwa wiki kadhaa kuonyesha namna pambano hilo lisivyotabirika kirahisi.
Marcio Maximo amekuwa akisisitiza kuwa mashabiki waende uwanjani kuona kitakachotokea, bila kuweka bayana kama ana hakika Yanga kushinda ila anasisistiza kuwa wamejiandaa vya kutosha, wakati Patrick Phiri  ametadharisha na kusema ni mchezo huo utakuwa wa aina yake.
"Wenzetu wana matokeo mazuri zaidi yetu kwa kuwa wameshinda michezo miwili mfululizo laikini hilo haliwapi uhakika wa ushindi," alinukuliwa Phiri.
Phiri alisema anajua mapungufu ya wapinzani wao na kikosi chake kipo tayari kwa mchezo huo huku 'akiita' mashabiki kujaa kwa wingi uwanjani.
"Mashabiki (wa Simba) wasiwe na wasiwasi... tumejipanga vizuri kwa mchezo huu na kambi yetu ya Afrika Kusini imetusaidia.Tutapambana kupata ushindi.," alisema.
Kwa matokeo ya hivi karibuni, Simba tangu walipoifunga Yanga mabao 5-0 katika mechi ya kufungia msimu wa 2011-2012 haijashinda tena zaidi ya kuambulia sare na kuchapwa kama ilivyokuwa ligi ya kufungia msimu wa 2012-2013 walipolala mabao 2-0.
Timu hizo zinakutana huku kila moja ikiwa na idadi kubwa ya majeruhi ambao huenda wakakosekana uwanjani.
Simba ina uhakika wa kumkosa golikipa wake Hussein Sharif 'Casillas' huku pia mlinda mlango namba moja, Ivo Mapunda akiwa na uwezekano mdogo wa kuanza hivyo golikipa yosso Manyika Peter anatarajiwa kuanza golini.
Kwa upande wa Yanga, huenda ikamkosa kiungo wao nyota Haruna Niyonzima aliyeumia enka kwenye mazoezi ya timu hiyo wakati nahodha Nadir Haroub 'Canavaro' ambaye aliumia Jumapili akiwa na kikosi cha timu ya taifa na kushonwa nyuzi tatu ataangaliwa afya yake mpaka muda mfupi kabla ya mechi.
Katika mbili za msimu uliopita, timu hizo zilishindwa kutambiana baada ya mechi ya awali kuisha kwa sare ya 3-3 na waliporudiana Aprili mwaka huu walifungana bao 1-1, Yanga wakilazimika kuchomoa 'usiku' kwa bao ya Simon Msuva, kama watani zao walivyochimoa mabao matatu katika ligi ya duru la kwanza.

HIZI NDIZO RATIBA ZA LEO ZA LIGI KUU TANO MAARUFU DUNIANI


http://modelsportsfan.com/wp-content/uploads/2013/08/EPL-La-Liga-Bundeliga-Serie-A-Logo.jpghttp://www.informationng.com/wp-content/uploads/2012/10/63751112_5738e41b-fd90-4ceb-bf30-b450f5664095.bmp 
LONDON,
Ratiba ya ligi kuu ya soka ya Uingereza ya LEO 

Man City        v Tottenham    (8:45) 
Arsenal        v Hull City    (11:00) 
Burnley        v West Ham
Palace       v Chelsea    (11:00) 
Everton        v Aston Villa
Newcastle    v Leicester
Southampton    v Sunderland

MADRID,
Mechi katika ratiba ya La Liga, ligi kuu ya soka ya Hispania, LEO:
Levante        v Real Madrid    (11:00) 
Athletic        v Celta Vigo
Barcelona    v Eibar        (3:00) 
Cordoba        v Malaga

ROME,
Ratiba ya ligi kuu ya soka ya Italia, Serie A, LEO: AS Roma        v Chievo Verona
Sassuolo        v Juventus

MUNICH,
Mechi za Bundesliga, ligi kuu ya soka ya Ujerumani, LEO:
Cologne        v Dortmund
Bayern        v Werder Bremen
Mainz        v FC Augsburg
Hanover 96    v Gladbach
Freiburg        v VfL Wolfsburg
Stuttgart    v Leverkusen 
Schalke 04    v Hertha Berlin

PARIS,
Mechi za Ligue 1, ligi kuu ya soka ya Ufaransa, za LEO:
FC Lorient    v St Etienne
Monaco        v Gaillard
Metz            v Stade Rennes
Nantes        v Stade Reims
Lille        v Guingamp
Nice            v Bastia

DAVIDO WA NIGERIA AZUA SONGOMBINGO BONGO

http://www.redpepper.co.ug/wp-content/uploads/2014/07/Davido-1.jpg
MSANII nyota wa Nigeria, Davido ameibua songombingo la aina yake baada ya kuvifanya vituo maarufu vya redio nchini Times FM na Claoud's FM kuburuzana mahakamani.
Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Dar es Salaam imemzuia msanii kutoka
Nigeria, Adedeji Adelek maarufu kama 'Davido' kuperform katika tamasha la
Fiesta linaloandaliwa na Clouds Fm na Prime Promotion, October 18,2014.
Amri hiyo imetolewa jana (October 17) na hakimu mkazi wa mahakama ya kisutu mheshimiwa D. Kisoka kufuatia maombi ya dharura yaliyowasilishwa
mahakamani hapo na Times Fm Radio na Times Fm Promotion.
Times Fm Radio na Times Fm Promotion walipeleka maombi ya dharura
mahakamani hapo wakiitaka mahakama kumzuia msanii huyo kuperform katika
tamasha hilo kwa kuwa licha ya BASATA (Baraza La Sanaa Tanzania) kukataa
kutoa kibali cha msanii huyo kwa maelezo kuwa tayari alikuwa
ameshachukuliwa kibali cha kuperform nchini November 1 kwenye tamasha
lililoandaliwa na Times Fm Radio,  Clouds Fm na Prime Times Promotion
waliendelea na taratibu zote bila kujali zuio hilo la BASATA.
Times Fm Radio na Times Fm Promotion waliiomba mahakama kuidhinisha madai
yao dhidi ya Clouds Fm, Prime Promotion na mkurugenzi wa kampuni
inayomsimamia Davido, HKN Music.
Madai hayo ni pamoja na kulipwa fidia ya gharama na usumbufu
waliosababishiwa na walalamikiwa kadiri Mahakama itakavyoona inafaa.
Mahakama imetoa amri kuwa msanii huyo amezuiwa kufanya onesho hilo October
18,2014 hadi pale ufumbuzi wa kesi hiyo utakapopatikana mhakamani hapo.
Awali, Davido alisikika katika matangazo ya Times Fm Radio akieleza kuwa
atakuja Tanzania November 1 kwa ajili ya kufanya onesho linaloandaliwa na
kituo hicho cha radio lililopewa jina la 'The Climax'.
 

Thursday, October 16, 2014

Algeria yafuzu Fainali za AFCON 2015 yaitungua Malawi 3-0

Algeria prove why they are the top ranked side in AfricaTIMU ya taifa ya Algeria imeweka rekodi ya kuwa nchi ya kwanza kufuzu katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco baada ya kupata ushindi murua wa mabao 3-0 dhidi ya Malawi katika mechi za kundi D.
Vijana wa kocha Christian Gourcuff wameweka rekodi ya kushinda mechi zake zote mpaka sasa kukiwa kumesaliwa mechi mbili kabla ya mechi za makundi kumalizika.
Mabao ya washindi hao waliong'olewa kwenye raundi ya pili ya Fainali za Kombe la Dunia za 2014 na waliokuja kuwa Mabingwa wapya, Ujerumani yaliwekwa kimiani naYasine Brahimi  dakika ya pili, Riyad Mahrez dk ya 45 na Islam Slimani Dk ya 55.
Katika mechi nyingine ya michuano hiyo kundi B lilishuhudiwa Ethiopia ikiwa ugenini mjini Bamako iliicharaza wenyeji Mali kwa mabao 3-2 na kujiweka pazuri kabla ya mechi mbili za mwisho dhidi ya Algeria na Malawi.
Bakary Sako alianza kufungua milango ya pambano hilo kwa kuwafungia wenyeji bao la kuongoza dakika ya 31 kabla ya wageni kurejesha na kuongeza la pili kupitia kwa wachezaji wao Oumed Oukri na Getaneh Kebede na Mali kuchomoa na kufanya matokeo kuwa 2-2 kwa bao la Mustapha Yatabare dakika dakika ya 69.

Bao la ushindi la Ethiopia lilifungwa na Abebaw Butako Bune, huku Angola ikiwa nyumbani ilipata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Lesotho katika mechi ya Kundi C.
Bastos alianza kuwaandikia wenyeji bao dakika ya pili kabla ya Ary Papel kuongeza la pili dakika ya 33 na kufanya hadi mapumziko matokeo kuwa 2-0 na kwenye kipindi cha pili Tsoanelo Koetle alijifunga katika dakika ya 47 na Love akapigilia msumari wa mwisho kw akuifungia Palancas Negras bao dakika ya 57.
nazo timu za Burkina Faso na Gabon zilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1 Jonathan Pitroipa akiifungia Burkinabe na wageni kuchomoa kupitia kwa Malick Evouna dakika ya 76.
Cape Verde waliendelea kuweka ugumu katika Kundi F baada ya kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Msumbiji kwa bao la Heldon katika dakika ya 75 na kuifanya wenyeji kufikisha pointi 9, huku Msumbiji wakisalia kwenye nafasi ya tatu ikiwa na pointi 5 sawa na Zambia walioshinda nyumbani mabao 3-0 dhidi ya Niger.
Nayo timu ya Tunisia ilifuata nyayo za majirani zao Misri walioishinda Botswana kwa mabao 2-0 nyumbani baada ya kuilaza Senegal bao 1-0 bao lilifungwa 'jioni' na Ferjani Sassi na kuifanya Tunisia kuongoza msimamo wa kundi hilo wakiwa na pointi 10 wakifuatiwa na Senegal wanaokamata nafasi ya pili wamiwa na pointi saba wakiitangulia Misri wenye pointi 6 wakiwa nafasi ya tatu.

Breaking Newz! Nigeria yamtimua Stephen Keshi, Amodu amrithi

http://ynaija.com/wp-content/uploads/2013/10/Nigerias-coach-Stephen-Ke-011.jpg
Stephen Keshi akiwa amebebwa alipotwaa ubingwa wa Afrika
https://thetbjoshuafanclub.files.wordpress.com/2009/12/amodu1.jpg
Shaibu Amodu anayemrithi Keshi kartika Super Eagles

SHIRIKISHO la Soka la Nigeria, NFF, kimetangaza kumfuta kazi aliyekuwa kocha Mkuu wa Super Eagles, Stephen Keshi ikiwa ni saa chache tangu aiongoze timu hiyo kupata ushindi wa mabao 3-1 nyumbani dhidi ya Sudan katika mechi ya kuwania Fainali za Kombe la Afrika za 2015.
Kocha za zamani wa timu hiyo Shaibu Amodu ndiye aliyepewa mikoba ya kuuiongoza Super Eagles katika mechi zilizosalia za kundi lake.
Keshi, nyota wa zamani wa timu hiyo amekuwa kocha wa Nigeria tangu mwaka 2011 na alifanikiwa  kuipeleka Super Eagles kwenye Fainali za Kombe la Dunia na kuishia nao raundi ya pili na inaelezwa tangu fainali hizo hakuwa na mkataba wowote licha ya kuendelea kuinoa timu hiyo aliyoipa ubingwa wa Afrika fainali za mwaka jana zilizofanyika nchini Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa NFF, maamuzi ya kutimuliwa kwa Keshi yamekuja baada ya Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo kukutana jana.
"Kwa manufaa ya soka la Nigeria na kiu kubwa ya kushiriki fainali za mwaka 2015 kamati imeamua kuachana na Keshi na benchi lake lote la ufundi," taarifa ya NFF ilisomeka hivyo.
Badala ya keshi NFF imemtaja Amodu aliyewahi kuinoa timu hiyo katika vipindi vinne tofauti mara ya mwisho ikiwa ni mwaka 2008-2010.
Vipindi vingine ambayo Shaibu Amodu aliwahi kuiongoza timu hiyo ni mwaka 1994-95, 1998-99, 2001-2002, Mei Mwaka jana alikuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Soka nchini humo kabla ya kupata kazi kama hiyo katika klabu na kutema nafasi yake hadi alipoitwa leo na NFF kuwa Kocha Mkuu kwa mara ya tano.

Maafa makubwa Misri! Bomu lalipuliwa Mahakamani jiji Cairo

An injured man arrives at the Helal hosp 
BOMU lililotengenezwa kienyeji huko Cairo, Misri limelipuka karibu na mahakama kuu siku ya Jumanne tarehe 14 mwaka huu na kujeruhi watu 12 ambapo gari na maduka yaliliyokuwa karibu ya eneo hilo la tukio yameharibika.
Haikufahamika vizuri kama lengo lilikuwa ni la kumuua mtu mmoja au kufanya tu uharibifu kwa sababu hii ni mara ya pili tukio kama hili limetokea huko Cairo chini ya mwezi mmoja.
Ripoti zinasema bomu ambalo lililipuka mwezi uliopita karibu na wizara ya mambo ya nje lililoua polisi watatu, lilisababisha uhalifu mkubwa ambao haukutokea kwa muda mrefu mjini Cairo.
Shambulizi hilo la bomu lilianzishwa na kundi la Jeshi la Kiislamu liitwalo Ajnad Misr ambapo inasemekana ongezeko la mashambulizi ya majeshi ya Kiislamu yamezidi kwenye nchi hiyo toka mkuu wa jeshi aitwae Abdel Fattah al-Sisi ampindue Rais Mohamed Morsi mwaka jana baada ya wananchi kupinga utawala wake.
Baada ya kumpindua Rais Mohamed Morsi mkuu huyo wa jeshi Abdel Fattah alivunja udugu wa Kiislamu uliokuwa chini ya Mohamed Morsi ambapo serikali ililitangaza kuwa ni kundi la kigaidi.

Kocha Hispania aanza kuaga, kutema timu baada ya Euro Cup

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/10/01/1412176952043_wps_10_Spain_s_head_coach_Vicent.jpg
Kocha Del Bosque
KOCHA wa Hispania, Vicente Del Bosque amesema ataachia ngazi ya kukinoa kikosi hicho cha timu ya taifa baada ya michuano ya Euro 2016 itakayofanyika nchini Ufaransa.
Del Bosque (63), ameshuhudiwa akipata mafanikio ya dhahabu kwa umri wake huo katika soka la Hispania, baada ya kushinda Kombe la Dunia  2010 na michuano ya Ulaya (Euro 2012) katika historia ya jina lake kwenye timu ya taifa.
Hata hivyo, Hispania ilianza kudorora katika Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil na kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Slovakia ilichokipata Alhamisi ni cha kwanza katika mechi 36 za kuwania kufuzu kuanzia 2006 -- kimemfanya Del Bosque kuanza kukosolewa kwa mara ya kwanza tangu alipotwaa mikoba ya kuinoa timu hiyo mwaka 2008 kutoka kwa Aragones.
Baada ya kutolewa kwenye Kombe la Dunia, kocha huyo mkuu wa Hispania, Del Bosque alionekana kuzama zaidi katika vipaji vya timu ya taifa ya makinda kwa kuviandaa kwa ajili ya Euro 2016. Tayari Del Bosque ameiongoza Hispania katika michuano mikubwa ya kimatifa mitatu na kushinda miwili tangu alipoanza kuinoa 2008.
"Nadhani Euro 2016 itakuwa michuano yangu ya mwisho kama kocha mkuu wa Hispania," aliiambia  Redio Nacional de Espana.
"Tutaona nini kitatokea wakati tutakapokwenda Ufaransa. Kinadharia, hii ni michuano yangu ya mwisho."
Del Bosque si mtu pekee ambaye yupo katika presha kubwa katika kikosi hicho cha 'La Roja', pia kipa wa Real Madrid, Iker Casillas amepoteza nafasi yake ambayo imetwaliwa na mlinda mlango wa Manchester United, David De Gea wakati  walipoibuka na ushindi wa 4-0 dhidi ya Luxembourg Jumapili.
Casillas (33), amekuwa akikosolewa na vyombo vya habari vya Hispania kutokana na kiwango chake katika Kombe la Dunia na dhidi ya Slovakia, huku pia uwezo wake ndani ya klabu ukizua mjadala, jambo linalomfanya kipa wa kimataifa wa Costa Rica Keylor Navas kuanza kuivizia nafasi yake.

Paul Scholes ampigia 'salute' Jack Welshere

http://i1.mirror.co.uk/incoming/article2168562.ece/alternates/s2197/England-v-Scotland-International-Friendly.jpg
Jack Welshere
KIUNGO nyota wa zamani wa England aliyewahi kutamba na klabu ya Manchester United, Paul Scholes anaamini kwamba Jack Wilshere ameongezeka ubora na sasa ndiye mchezaji bora zaidi katika kikosi cha timu ya taifa ya England.
Welshere, 22, ambaye alicheza kwa dakiia zote 180 za mechi mbili za timu ya taifa ya England za kuwania kufuzu kwa fainali za Euro 2016 ambazo walishinda dhidi ya San Marino na Estonia, alipata kukosolewa na gwiji huyo wa Manchester United kwa kushindwa kuongezeka ubora tangu alipoingia katima kikosi cha kwanza cha Arsenal.
Lakini Scholes sasa amemsifu Wilshere, ambaye alipewa jukumu la kucheza katikati ya kiungo na kocha Roy Hodgson, na gwiji huyo wa Man U mwenye umri wa miaka 39 amefurahishwa na pasi zilizokuwa zikitolewa na kiungo huyo.
“Nadhani Jack Wilshere alikuwa na mechi mbili nzuri sana za England wiki iliyopita,” Scholes aliandika kwenye gazeti la Independent. “Naweza kwenda hatua moja mbele na kusema kwamba, kwa sasa, Wilshere ndiye mchezaji bora wa England.
“Amebadilika na ameongeza kitu katika uchezaji wake. Alikuwa ni mtu wa pasi fupi tu, lakini sasa anaweza kupiga pasi ndefu pia.”

Hivi ndivyo Suzuki Sauti ya Malaika alivyozikwa jana jijini Dar

https://fbcdn-sphotos-h-a.akamaihd.net/hphotos-ak-xpf1/v/t34.0-12/10735860_387830028030788_699106094_n.jpg?oh=4a4a71a5e704c6de8d13b86213f578a6&oe=544077E5&__gda__=1413518840_3735b6aa646908122422cde63a7ff273
Waombolezaji wakifukia kaburi ya marehemu Suzuki wakati wa mazishi yake jana kwenye makaburi ya Magomeni Kagera
Mwili wa marehemu Suzuki ulipokuwa ukihifadhiwa jana
Mwili wa Suzuki ukihifadhiwa katika makaburi ya Kagera

Waombolezaji wakiwa makini kufuatilia mazishi ya Suzuki

Baadhi ya woambolezaji walioshiriki mazishi ya Suzuki
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhFhXutATUb6_ogGzQhP1FoqA9uKARlTfPORgEC6yTP-kCm0Wggg8WAt_Ne5GzHPzDDHbaEikGcRE9B53AYkJ-gMmL1fkvt6KkDpCYYUY_zS9m_vVA16ZWnOLkQV38zDGrRyVxrngyVxX8/s400/P1211580.jpg
Suzuki Sauti ya Marehemu enzi za uhai wake
MWILI wa mwanamuziki nyota wa zamani wa bendi za Tabora Jazz, Mikumi Sound, Levent Musica na Extra Bongo, Suleiman Ramadhan 'Suzuki' au Sauti ya Malaika hatimaye umepumzishw akatika mazishi yaliyofanyika jana jioni kwenye makaburi yaliyopo eneo la Kagera.
Mwili huo ulizikwa saa 10:30 mara baada ya kuswaliwa kwenye Msikiti wa Rahman Kagera Mikoroshini na kusindikizwa na wanamuziki wenzake wachache na waumini wengine ambao wlaifurika kumhifadhi muimbaji huyo aliyefariki usiku wa juzi kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari.
MICHARAZO iliwashuhudia wanamuziki wachache waliojitokeza kumsindikiza mwenzao huku baadhi ya waliokuwa mabosi wake wa zamani wakiwa wameingia mitini.
Miongoni mwa wanamuziki walioshiriki mazishi hayo mwanzo mwishoni ni Ramadhan Mhoza 'Pentagone', Athanas Montanabe, Adam Mbombole, Frank Kaba 'Kaba Tano' Redock Sura ya Mauzo, Hosea Mgohachi, dansa wa zamani wa Chino Loketo, Bob Kissa na wengine.
Aidha kulikuwa na wasanii wengine mbalimbali wa muziki ambao walishiriki kumsindikiza mwenzao, huku majina makubwa ya wasanii ambao waliwahi kufanya kazi na marehemu Suzuki wakiwa wameingia mitini.

TFF yapangua kiduchu ratiba Ligi Daraja la Kwanza (FDL)

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXBt0R5Pi-ynZE0lUwMuVOoucOGlhDsPIsBIaGAiajuQXwnnQ3ouUqzqLpkbGZdozVZKBB0vK7XL15pWWM0MF2OQWhhvfPiIxQw-fpCI7V6a5Jbi8Fy89wLz6es-PsG5pO3dt0uQLfunnH/s640/Wambura1_2_339a2.jpg
MECHI nne za Kundi A la Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zimefanyiwa marekebisho ili kutoa fursa ya matumizi ya Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam.


Timu za African Lyon na Kimondo ambazo awali zilikuwa zicheze Oktoba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani, sasa zitacheza Oktoba 26 mwaka huu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.


Nayo mechi ya Polisi Dar es Salaam na Majimaji ya Songea iliyokuwa ichezwe Oktoba 26 mwaka huu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, sasa itachezwa Oktoba 27 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.


Mechi ya Friends Rangers na Ashanti United iliyokuwa ichezwe Mabatini mkoani Pwani, Oktoba 26 mwaka huu, sasa itachezwa Uwanja wa Karume, Oktoba 28 mwaka huu.

Pia mechi ya Lipuli na JKT Mlale iliyokuwa ichezwe Oktoba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa, imesogezwa mbele kwa siku moja. Mechi hiyo sasa itachezwa Oktoba 26 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Uchaguzi mdogo Bodi ya Ligi Nov 15

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/10/DSC03338.jpgMKUTANO  Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) utafanyika Novemba 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo moja ya ajenda ni uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi moja ya uongozi kwenye bodi hiyo.


Nafasi hiyo ya ujumbe kwenye Kamati ya Uendeshaji ya TPLB iliyokuwa ikishikiliwa na Kazimoto Muzo imebaki wazi baada ya klabu yake ya Pamba ya Mwanza kushuka daraja kutoka la Kwanza hadi la Pili.

Hivyo, wagombea wa nafasi hiyo ni kutoka kwenye klabu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL). 
Klabu hizo zina nafasi mbili kwenye Kamati ya Uendeshaji ya TPLB ambapo nyingine inashikiliwa na Omari Mwindadi wa klabu ya Mwadui ya Shinyanga.

Nigeria yazinduka, Ivory Coast hoi, Cameroon wanusa AFCON 2015

http://images.performgroup.com/di/library/Goal_Nigeria/e0/cf/nigeria-vs-sudan-abuja_1ro9umbg2xq9b1qgpib297xiqm.jpg?t=349299433&w=940
Nigeria walipoisulubu Sudan mjini Abuja
http://www.goal-news.com/wp-content/uploads/2014/10/Asamoah-Gyan-Ghana-e1413339163729.jpg
Ghana wakishangilia moja ya mabao yao
http://nilsenreport.ca/wp-content/uploads/2014/06/Ivory-Coast-World-Cup-tea-010.jpg
Ivory Coast iliyokufa kwa DR Congo
http://www.goolfm.net/wp-content/uploads/2014/10/s64.jpg
Cameroon walionusa fainali za AFCON 2015

MABINGWA watetezi wa Kombe la Afrika, Nigeria imelipiza kisasi kwa Sudan kwa kuilaza mabao 3-1, wakati Ivory Coast ikifumuliwa mabao 4-3, huku Uganda ikigawa pointi tena kwa Togo kwa kukubali kipigo cha bao 1-0 kwenye mechi za kuwania kucheza Fainali za Kombe la Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.
Nigeria mabyo ilitoka kupigwa mabao 2-0 na Sudan kwenye mechi iliyochezwa wikiendi iliyopita, ikiwa mjini Abuja waliwakomalia wapinzani wao na kupata ushindi huo muhimu na kufufua matumaini yao ya kwenda kutetea taji hilo Morocco kwa mabao ya Ahmed Mussa aliyefunga mawili dakika ya 48 na 90 na jingine la Aaron Olanare.
Bao la kufutia machozi la Sudan lilifungwa na Mohammed Salah Ibrahim dakika ya 56.
Katika mechi nyingine za mashindano hao Ghana ilipata ushindi mnono nyumbani dhidi ya Guinea waliotoka nao sare siku chache zilizopita.
Mabao ya washindi yalifungwa na Asamoh Gyan aliyefunga dakika ya 16 kabla ya Ander Ayew 'Pele' kuongeza la pili kwa mkwaju wa penati dakika ya 58 na Agyemang-Badu kufunga la tatu dakika za jioni, huku wapinzani wao wakipata bao kupitia kwa Mohammed Yattara.
Uganda ikiwa mjini Lome Togo, ilishinda kulip[a kisasi kwa wenyeji wao kwa kukubali tena kicvhapo cha bao 1-0 na kuzidi kuwaweka pabaya katika mbio za kwenda Morocco.
Bao lililoiangamiza Uganda The Cranes lilifungwa na Serge Akakpo dakika ya 70 na kuifanya Togo kupanda hadi nafasi ya pili katika kundi hilo la E ikiwa na pointi 6, ikishusha Uganda inayosaliwa na pointi zake nne.
Katika mechi za kundi F, Zambia iliendeleza ubabe kwa kuinyuka Niger mabao 3-0 katika pambano lililiochezwa mjini Lusaka kupitia mabao ya Rainford Kalaba, Emmanuel Mayuka na Kenned Mweene aliyefungwa kwa penatui.
Nayo Misri ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Botswana wakirejea ushindi kama huo walioupata katika mechi iliyopita siku chache zilizopita wakiwa ugenini.
Mabao ya washindi yalifungwa na Amr Gamal na Mohammed Salah, huku Cameroon ikizinduka na kuinyuka Sierra Leone kwa mabao 2-0 kupitia mabao ya mapema ya Leonard Kweuke na Stephane Mbia na kuifanya tuimu hiyo inuse fainali hizo za mwakani kwa kufikisha pointi 10 ikifuatiwa na Ivory Coast ambayo walikung'utwa mabao 4-3 na DR Congo katika mechi iliyosisimua.
Magoli ya DR Congo yalifungwa na Neeskens Keban dk ya 21, Junior Kabananga dk ya 35 na Jeremy Bokila dakika ya 36 na 89 huku magoli ya wageni waliocheza pungufu baada ya kumpoteza Yannick Kessie aliyetolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 47, yalipachikwa wavuni na Mwanasoka Bora wa Afrika Yaya Toure na Solomon Kalou aliyefunga mawili.

Wednesday, October 15, 2014

Suarez akiri ilikuwa vigumu kukiri kosa la kumng'ata Chiellini

http://vertienteglobal.com/wp-content/uploads/2014/06/luis-suarez-anota-gol.jpghttp://img2.timeinc.net/people/i/2014/news/140707/luis-suarez-600.jpgSTRIKA nyota wa Barcelona, Luis Suarez amesema ilikuwa ngumu kukubaliana na ukweli wa kumng’ata beki wa Italia Giorgio Chiellini katika michuano ya Kombe la dunia nchini Brazil. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay aliyejiunga na Barcelona akitokea Liverpool kwa kitita cha Pauni Mil. 75 alifungiwa miezi minne kutokana na tukio hilo. 
Akihojiwa strika huyo amesema alikuwa akiona vigumu kukubali alichokifanya kwani yeye ni binadamu kama walivyo wengine. 
Suarez, 27, amesema alikuwa hataki kumsikiliza yeyote au kuongea na yeyote kwa sababu alikuwa hataki kukubaliana na ukweli. 
Suarez alimuomba radhi Chiellini Juni 30 zikiwa zimepita siku sita toka afanye tukio baada ya Uruguay kushinda bao 1-0 dhidi ya Italia, msamaha ambao ulipokelewa na beki huyo na kueleza matumaini yake kama Shirikisho la Soka Duniani-FIFA lingeweza kumpunguzia adhabu hiyo. 
Kabla kuomba radhi Suarez alikanusha kwa kudai kuwa aliteleza bahati mbaya na usoni mwa Chiellini na kumuangukia jambo ambalo lilikuwa kama vichekesho kwani tukio hilo lote lilionekana katika picha za video.

Ronaldo alibeba Ureno, Ujerumani bado gonjwa Ulaya

http://i.ytimg.com/vi/TevIMI1W8NI/0.jpg
Ronaldo akishangilia bao lake lililoiua Denmark nyumbani kwao
http://www.101greatgoals.com/wp-content/uploads/2014/10/Screen-Shot-2014-10-14-at-23.54.46.png
Wachezaji wa Ireland wakishangilia bao lao la kusawazisha dhidi ya Ujerumani
http://www.theglobeandmail.com/sports/soccer/article21090950.ece/BINARY/w620/510260433_534397343.JPG
Mabingwa wa Dunia, Ujerumani wakihenyeka uwanjani dhidi ya Jamhuri ya Ireland
WAKATI Mabingwa wa Kombe la Dunia Ujerumani wakiwa hawajatulia, Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo usiku wa jana aliifungia timu yao ya Ureno bao pekee lililowapa ushindi dhidi ya Denmark uwanja wa ugenini katika mbuio za kuwania Fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya Euro 2016.
Ujerumani inayouguza kichapo cha mabao 2-0 ilichopewa na Poland wikiendi iliyopita ilishindwa kulinda bao lake na kujikuta wakilazimishwa sare ya baoa 1-1 nyumbani na Jamhuri ya Ireland waliochomoa bao 'jioni'.
Ton Kroos aliiandikia wenyeji bao la kuongoza dakika ya 71, lakini wageni walikaza msuli na kulirejesha dakika za nyongeza kupitia John O'shea na kufanya timu hizo kugawana pointi huku Poland wakilazimishwa sare ya mabao 2-2 na Scotland ikiwa nyumbani.
Matokeo ya mechi nyingine ni kwamba Ureno ikiwa ugenini iliizabua Denmark kwa bao 1-0 lililofungwa na nahodha wake Cristioano Ronaldo katika dakika ya lala salama mashabiki wakiamini kuwa timu hizo zimetoka suluhu na kuifanya Ureno kufikisha jumla ya pointi tatu na kushika nafasi ya tatu.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo, Gibraltar imeendelea kutoa takrima baada ya kugongwa nyumbani mabao 3-0 na Georgia, San Marino kulazwa mabao 4-0 nyumbani na Uswisi, wakati Visiwa vya Faroe walilala nyumbani pia kwa bao 1-0 kutoka kwa Hungary, Finland ikafa pia nyumbani kwa mabaop 2-0 kw akipigo cha Romania na Ugiriki ikaendeleza unyonge kwa timu zilizocheza nyumbani jana kwa kulazwa mabao 2-0 na Ireland ya Kaskazini.

Kivumbi Afrika, Nigeria vs Sudan, Uganda v Togo hapatoshi!!

https://media.premiumtimesng.com/wp-content/files/2014/06/Eagles-Getty-images.jpg
Watetezi Nigeria
http://static.pulse.ng/img/incoming/origs3188111/4750486101-w980-h640/The-Sudanese-national-team.jpg
Sudan
http://www.goal-news.com/wp-content/uploads/2014/10/Guinea-vs-Ghana.jpg
Ghana
http://www.redpepper.co.ug/wp-content/uploads/2014/08/1.-EBOLA-OR-NOT-The-Cranes-are-ready-to-fly-to-Morocco-Picture-by-John-Batanudde-445x350.jpg
Uganda watacheka kama hivi leo kwa Togo
VUMBI la michuano ya kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON-2015 linatarajiwa kuendelea kutimka leo wakati mechi kadhaa zitapigwa kwenye mataifa mbalimbali barani Afrika.
Cameroon iliyong'ang'aniwa katika mechi iliyopita na Sierra Leone itakuwa nyumbani kurudiana na majirani zao hao, wakati Togo iliyoiduwaza Uganda The Cranes mjini Kampala itaialikia wapinzani wao hao katika pambano la kusisimua.
Mabingwa watetezi waliofumuliwa mjini Khartoum na wenyeji wao Sudan itajiuliza nyumbani huku Angola na Lesotho zitaonyeshana kazi mjini Luanda.
Mechi nyingine za makundi hayo zitakuwa kama ifuatavyo;
Ghana vs    Guinea
Zambia vs    Niger
Côte d'Ivoire vs    Congo DR   
Egypt vs Botswana   
Cape Verde Islands vs Msumbiji
Mali vs Ethiopia
Burkina Faso vs    Gabon
South Africa vs    Congo
Tunisia vs    Senegal   
Algeria vs    Malawi

Msiba! Muimbaji wa zamani Extra Bongo afariki dunia

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQc1H5GJ4HwdiXPaWbq-vVhWG0Bm2Vi87Ia9OXMQL5oKZR41D0Hvg8X4TGWY439EgCeIYuWHEJPboaoLwTISvctf3TKJVmvXtVjQFjLJQQRltQP02J05yvMNyCViL0_9LwVpTL8swJgrs/s400/P1191212.JPG
Suzuki enzi za uhai wake
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhFhXutATUb6_ogGzQhP1FoqA9uKARlTfPORgEC6yTP-kCm0Wggg8WAt_Ne5GzHPzDDHbaEikGcRE9B53AYkJ-gMmL1fkvt6KkDpCYYUY_zS9m_vVA16ZWnOLkQV38zDGrRyVxrngyVxX8/s400/P1211580.jpg
Seleman Ramadhan Suzuki Sauti ya Malaika enzi za uhai wake
MWANAMUZIKI nyota wa zamani wa bendi za Mikumi Sound, Levent Musica na Extra Bongo 'Wana Next Level', Suleiman Ramadhani 'Suzuki Sauti ya Malaika' amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua muda mrefu.
Kwa mujibu wa mwanamuziki mwenzake ambaye alikuwa akifuatilia afya yake kipindi akiugua, Ramadhani Mhoza 'Pentagone' ameiambia MICHARAZO, Suzuki amefariki akiwa nyumbani eneo la Magomeni Kagera, jijini Dar es Salaam na huenda akazikwa leo au kesho.
Pentagone aliyefanya kazi na mwanamuziki huyo aliyekuwa na uwezo wa kutunga, kuimba na kurapu  katika bendi za Levent Musica 'Wazee wa Kumuvuzisha' na Extra Bongo, alisema Suzuki alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari na alikuwa akitibiwa nyumbani kwa dawa za kienyeji.
"NIlitaka kukutaarifu kubwa swahiba yetu Suzuki hatunaye kwani amefariki usiku wa leo na kwa sasa tunaangalia mipango ya mazishi kwa kuwasiliana na ndugu zake wa karibu," alisema Pentagone ambaye kwa sasa anaiimbia African Stars 'Twnaga Pepeta'.
Enzi za uhai wake, Suzuki anayetokea Kigoma alitamba na bendi za Tabiora Jazz kabla ya kutua Morogoro katika bendi ya Mikumio Sound iliyowahi kutamba na albamu ya Mlinzi wa Godown kabla ya kuitua Levent Musica na baadaye yeye na wanamuziki wenzake watatu, Bob Kissa, Pentagone na Athanas Montanabe walihamia kwa mpigo Extra Bongo na kupakua albamua ya Mjini Mipango.
Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi na MICHARAZO inatoa pole kwa wote walioguswa kwa namna moja au nyingine na msiba huio na kuwaomba kuwa na moyo wa Subira kwa kukumbuka kuwa 'Kila Nafsi Itaonja Mauti' na Sisi ni wa Mola na Kwake Hakika Tutarejea'.