STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 5, 2014

Yanga kuivaa Alh Ahly J'2 usiku, kikosi kuondoka leo usiku

Kikosi cha Yanga kilichoibana Al Ahly kwa kuilaza 1-0 jijini Dar jumamosi iliyiopita
IMETHIBITIKA kuwa, wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Barani Afrika timu ya Young Africans itacheza mchezo wa marudiano siku ya jumapili jijini Cairo dhidi ya timu ya Al Ahly ukiwa ni mchezo utakaotoa picha halisi ni timu gani itasonga mbele katika hatua ya 16 bora.
Ikiwa ni takribani siku tano kabla ya kufanyika mchezo wenyewe wenyeji Al Ahly wameshindwa kuweka wazi ni uwanja gani utakaotumika kwa ajili ya mchezo huo huku Meneja wa klabu hiyo Abdoulazi akisema huenda mchezo ukachezwa jijini Cairo au Alexandria na kusema majibu kabili yatapatikana siku ya jumatano mchana.
Wenyeji wameiandalia timu ya Young Africans kufikia katika Hoteli ya Baron iliyopo maneneo ya Uwanja wa michezo wa kimataifa Cairo huku pia wakiipangia timu kufanya mazoezi katika uwanja wao uliopo eneno la Nasri City.
Katika mchezo wa awali uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Young Africans ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Al Ahly ambao ni mabingwa watetezi wa kombe hilo shukrani kwa bao la Nahodha wa timu Nadir Haroub "Cannavaro" aliyetikisha nyavu dakika ya 82 ya mchezo.
Mara baada ya mchezo huo kikosi cha mholanzi Hans Van der Pluijm kiliingia kambini jana jioni katika hotel ya Ledger Bahari Beach tayari kwa maandalizi ya mchezo marudiano ambapo timu imeendelea kufanya mazoezi katika uwanja wa Boko Beach Veterani.
Kuelekea mchezo huo wa jumamosi tayari uongozi wa Young Africans ulishaanza kufanya maandalizi ya safari ambayo inatarajiwa kuwepo kabla ya mwisho mwa wiki hii huku msafara ukitarajiwa na kuwa idadi ya watu 35, wakimwemo viongozi, benchi la ufundi pamoja na wachezaji 19.
Hali ya wachezaji ni nzuri, kiafya, fikra na morali ya kuelekea mchezo wenyewe bado ni kubwa kwani bench la ufundi na wachezaji wanaamini maandalizi wanayoyafanya yatasaidia kupelekea kupata ushindi katika mchezo huo na kuweza kusonga mbele katika hatua ya 16 bora.
Baadhi ya wachezaji wanaotarajiwa kuondoka usiku wa leo kuifuata Al Ahly ni makipa Deogratius Munishi 'Dida' na Juma Kaseja, Nadir Haroub 'Cannavaro, David Luhende, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Simon Msuva, Mrisho Ngasa, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, Juma Abdul, Frank Domayo, Mbuyu Twite, Rajab Zahir na Said Bahanuzi.
Okwi na Kiiza, wataungana na kikosi hicho Alhamisi wakitokea Lusaka, walipo na timu yao ya Taifa ya Uganda ( The Cranes) ambayo jana ilikuwa inacheza na Zambia (Chipolopolo) mechi ya kimataifa ya kirafiki.
Yanga inahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ili iweze kusonga mbele kwenye michuano hiyo.
Maandalizi ya sehemu ya kambi ambapo timu itafikia jijini Cairo tayari yanaendelea vizuri kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania ambapo kwa upande wa klabu ya Young Africans Afisa Habari Baraka Kizuguto tayari yupo nchini Misri kwa siku ya pili akiendelea kuweka mambo sawa.
Mchezo wa jumapili unatarajiwa kufanyika katika uwanja wa Arab Contractors uliopo jijini Cairo huku mechi hiyo ikichezwa bila ya mashabiki kufuatia Serikali ya Misri kuzuia mashabiki wa soka kutokana na mashabiki hao kufanya vurugu katika mchezo wa Fainal ya Super Cup dhidi ya CS Sfaxien na kupelekea askari kadhaa kujeruhiwa.

Wawili waongeza mkataba Arsenal na kumpa ahueni Wenger

350594_heroaBaada ya kupoteza mechi yake iliyopita ya ligi kuu ya England klabu ya Arsenal leo imewapa habari nzuri mashabiki wake baada ya kutangaza wachezaji wao wawili wameongeza mikataba ya kuendelea kuitumikia klabu hiyo.
Nahodha wa timu hiyo Mjerumani Per Mertesacker na kiungo Thomas Rosicky wote wametangazwa kuongeza mikataba yao.
“Tunayo furaha kutangaza kwamba Mertesacker na Rosicky wameongeza mikataba ya kuendelea kuwepo hapa,”  Arsene Wenger aliuambia mtandao rasmi wa klabu hiyo.
“Ni wachezaji wazuri na wenye uzoefu, na wameshaonyesha kila siku kwamba wanaweza kucheza kwenye level ya juu.’ – alimaliza Wenger.
Klabu hiyo hata hivyo haijatoa namba ya miaka kamili ya muda wa mikataba mipya.

Mourinho 'aizuga' Mancehster City mbio za ubingwa England

Jose Mourhino (kulia) na kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini  wakisalimiana enzi wakiwa Hispania
LONDON, England
KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amesema watakuwa wanabadilisha nafasi za mbio za ubingwa wa Ligi Kuu England na Manchester City kutokana na kikosi hicho cha Manuel Pellegrini kuwa na mechi mkononi.
Miamba hiyo ya Stamford Bridge inaizidi City kwa pointi sita baada ya mwishoni mwa wiki kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham, lakini mabingwa wa Kombe la Ligi (Capital One Cup) wana mechi mbili mkononi na wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa kuliko Chelsea.
Pellegrini anawinda mafanikio makubwa kwa kutwaa makombe matatu baada ya kuiongoza City kushinda 3-1 dhidi ya Sunderland Jumapili kwenye Uwanja wa Wembley na kutwaa ubingwa wa Capital One Cup, jambo ambalo Mourinho anasisitiza kuwa kocha huyo raia wa Chile yupo katika nafasi nzuri ya mbio za ubingwa.
"Ninapenda kuwa na bahati mkononi, na City tu ndiyo yenye bahati mkononi mwake," Mourinho alisema. "Kama nitashinda kila mchezo hadi mwishoni mwa msimu, zote 10 – kama hatutaweza labda hatutakuwa mabingwa.
"Kama [City] itashinda mechi zote 12 ilizo nazo, watakuwa mabingwa. Wana bahati mkononi mwao."

Wavuvi wawili wauwawa kwa risasi wakivua samaki mtoni

Na   Walter Mguluchuma, Katavi
WATU wawili  James  Mauto  21 Mkazi wa Kijiji  cha  Ugala Wilaya ya Mlele   na  January  Marekani  18 Mkazi wa Kijiji  cha Mtapenda  Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele  mkoa  wa Katavi wameuwawa  kwa kupigwa  risasi   na Askari wa Geme Reserve wakati  wakiwa wanavua  samaki  ndani ya   Hifadhi  ya Pori la akiba la Ugala na mwenzao mmoja kujeruhiwa  kwa Risasi sehemu ya mbavu zake
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa  wa Katavi Dhahiri Kidavashari   tukio hilolilitokea hapo  Februari  28 mwaka huu majira ya saa  tisa Alasiri  ndani ya Hifadhi ya pori  la akiba la Ugala Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi 

Alieleza siku hiyo ya tukio    James Mauti  na  Januari Marekani walikuwa wakivua samaki ndani ya mto Ugala uliko kwenye  Hifadhi  ya pori la akiba la ugala wakiwa na mwenzao mmoja  aitwaye  Seif Juma  40  Mkazi wa kijiji  cha Mtapenda  Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele
Kamanda Kidavashari alisema  wakati wakiwa wanaendelea kuvua samaki ndani ya mto huo  alitokea Askari  wa Geme Reserve  ambae alikuwa amevalia sare   huku akiwa na silaha  bunduki  ambayo haikuweza kufahamika aina yake
Alisema Askari huyo aliwaamuru  wavuvi  hao wajisalimishe kwake  hata hivyo wavuvi  hao waliokuwa wakiendelea na uvuvi  kufutia amri hiyo ya Askari  waliamua kutupa nyavu zao walizokuwa wakivulia samaki  na kukimbia mbio  kila mmoja sehemu yake
Ndipo Askari huyo  alipoanza  kuwarushia  risasi  wavuvi  hao  na kuwauwa  kwa risasi James Mauto   na Januari  Marekani  na kumjeruhi Seif  Juma sehemu za  mgongoni na kwenye mbavu
Majeruhi  ambae ni Seif  Juma  alifanikiwa  kufika katika kijiji  cha Ugala  na  kutoa taarifa kijijini hapo kwa uongozi wa Serikali ya Kijiji juu ya tukio hilo  na aliweza kupatiwa msaada wa kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa ajiri ya matibabu
Kamanda Kidashari  alieleza  kuwa mvuvi huyo  ambae ni majeruhi  kwa kuhofia kukamatwa na kuhojiwa  na polisi  baada ya kufikishwa  Hospitali alitoroka  na mpaka sasa  haijajulikana mahari alipo na anatibiwa wapi majeraha yake ya risasi
Alisema  kutokana na tukio hilo kuhusishwa  na Askari  wa Geme  Reserve  katika hifadhi  hiyo  jeshi la polisi Mkoa wa Katavi  linawasiliana  na mkuu wa  kikosi cha  wanyama pori  mkoa wa Tabora  ambako ndio  walikuwa wametoka Akari waliohusika na tukio la mauwaji hayo
Alifafanua  kuwa  tayari mkuu wa Kikosi hicho  cha wanyama pori  ametuma kikosi chake kwenye eneo hilo la tukio  ilikubaini  ni Askari  gani waliokuwa kwenye  doria  eneo hilo  ili kuwabaini  na kisha  sheria ichukuwe mkondo wake  kwa askari  aliyehusika au waliohusika  kwa tukio la mauwaji hayo ya kinyama kwa binadamu hao.
Pambana na Climate Change

Petr Cech hakamatiki Tuzo ya Mchezaji Bora Czech

KIPA wa klabu ya Chelsea ya England, Petr Cech hashikiki katika Tuzo yta Mchezaji Bora wa Mwaka wa Jamhuri ya Czech baada ya kutangazwa tena kuwa mshindi wa mwaka 2013 ikiwa ni mara yake ya sita mfululizo kati ya saba aliyonyakua tuzo hiyo.
Cech (31) ameshinda tuzo hiyo kwa mara ya sita baada ya kupigiwa kura nyingi kutoka kwa wachezaji, makocha, viongozi wa shirikisho la soka na waandishi wa habari.
Kiungo wa Arsenal, Tomas Rosicky ameshika nafasi ya pili wakati mchezaji wa Freiburg, Vladimir Darida akishika ya tatu.
Kipa huyo ndiye tegemeo wa Chelsea inayopigana kunyakua ubingwa kwa msimu huu ikiwa chini na kocha aliyewahi kuipa mafanikio huko nyuma, Jose Mourinho.

Taifa Stars dimbani leo Namibia bila Samatta, Ulimwengu

Taifa Stars
Mbwana Samatta (kulia) atakayelikosa pambano la leo nchini Namibia

TIMU ya Taifa (Taifa Stars), itawakosa nyota wake wanaocheza soka nje ya nchi katika mechi ya kirafiki ya Kimataifa dhidi ya Namibia itakayochezwa leo kwenye Uwanja wa Sam Nujoma jijini Windhoek nchini humo.
Hatua hiyo inakuja baada ya Shirikisho la Soka nchini (TFF) kushindwa kupata usafiri wa uhakika wa kuwarejesha ndani saa 24 katika klabu yao, washambuliaji Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu wanaoichezea TP Mazembe ya DR Congo pamoja na Mwinyi Kazimoto anayeichezea Al-Makhiya ya Qatar.
Stars ya TFF (iliyoteuliwa na shirikisho hilo badala ya kocha), iliondoka nchini juzi alfajiri ikiwa chini ya Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi wa shirikisho hilo, Salum Madadi, aliyeshika kwa muda nafasi ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Mdenmark Kim Poulsen, ambaye alitimuliwa wiki iliyopita.
Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, aliliambia NIPASHE jijini Dar es Salaam jana kuwa, Stars itashuka dimbani bila ya wachezaji wake wanaosakata kabumbu la kulipwa nje ya nchi, Ulimwengu, Samata  na Kazimoto.
Alisema wachezaji hao wanakosekana baada ya TFF kukosa ndege ya kuwarudisha katika timu zao ndani ya saa 24 baada ya mechi hiyo kumalizika kama Kanuni za Fifa zinavyoelekeza.
"Ndege tulizopata zinapita Nairobi kwenda Lubumbashi Machi 8, wakati Samata na Ulimwengu wana mechi muhimu ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwishoni mwa wiki," alisema Wambura.
Aidha, Wambura alisema Stars itawakosa wachezaji Hassan Mwasapili na Edward Charles ambao wamekosa hati za kusafiria (passport).
Kutokana na kukwama kwa nyota hao, Stars sasa imebaki na wachezaji 15 wakiwamo makipa Mwadini Ally (Azam) na Shaban Kado (Coastal) aliyeitwa kuziba nafasi ya Ivo Mapunda (Simba) aliyefiwa na baba yake mzazi wiki iliyopita.
Mabeki ni Erasto Nyoni, Said Moradi na Aggrey Morris (Azam), Abdi Banda (Coastal) na Michael Aidan (Ruvu Shooting), wakati viungo ni Amri Kiemba (Simba), Jonas Mkude (Simba) na Himid Mao kutoka Azam FC.
Washambuliaji ni Athanas Mdamu (Alliance Mwanza), Haruna Chanongo (Simba), Khamis Mcha (Azam), Ramadhan Singano (Simba) na Juma Luizio kutoka Mtibwa Sugar.

Tuesday, March 4, 2014

Young Hassanally kuzindua Nyongo Mkaa na Ini

* Uzinduzi kufanyika Ijumaa Travertine Hotel
* Khadija Kopa, Jokha Kassim,Mwanahawa Ally ndani
Muimbaji Hassani Ally 'Young Hassanally'
Mwanahawa Ally naye atakuwepo ukumbini kumsindikiza Young Hassanally
Khadija Kopa (kushoto) naye atakuwepo Travertine Hotel
MALKIA wa Mipasho nchini, Khadija Kopa, Mwanahawa Ally na Jokha Kassim wanatarajiwa kusindikiza uzinduzi wa albamu mpya binafsi ya muimbaji nyota wa muziki wa taarab nchini anayeliimbia kundi la King's Modern Taarab, Hassan Ally 'Young Hassanally'.
Uzinduzi huo wa albamu hiyo inayofahamika kwa jina la 'Nyongo Mkaa na Ini' utafanyika siku ya Ijumaa kwenye ukumbi wa hoteli maarufu iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO, Young Hassanally, alisema mbali na waimbaji hao mahiri nchini, pia uzinduzi huo utasindikizwa na kundi la King's Modern Taarab maarufu kama 'Wana Kijoka'.
Hassanally, alisema ameamua kuwashiriki wakali hao katika uzinduzi wake ili kuunogesha na kuwapa burudani mashabiki wa muziki wa mwambao.
"Siku ya Ijumaa natarajia kuzindua albamu yangu ya pili mpya iitwayo 'Nyongo Mkaa na Ini' ambapo nitasindikizwa na wakali wa muziki wa mwambao Afrika Mashariki na Kati, Al-hanisa Khadija Kopa, Mwanahawa Ally 'B52' na Jokha Kassim pia kundi langu la King's Modern litakuwapo ukumbini Magomeni kunisindikiza," alisema.
Hiyo ni albamu ya pili binafsi ya staa huyo baada ya awali kuzidnua albamu ya 'Aibu Yao Aibu Yetu' na  aliongeza kuwa maandalizi yote ya uzinduzi huo yamekamilika na kwa sasa kinachosubiriwa na siku ya uzinduzi huo ili mashabiki wapate burudani, huku akitaja viingilio ni Sh. 5000 tu kila kichwa.

Ridhiwani Kikwete kuitetea CCM-Chalinze, ambwaga Madega

Ridhiwani Kikwete (kulia)
Kuelekea uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani lililoachwa wazi baada ya mbunge wake SAID BWANAMDOGO kufariki hivi karibuni Chama cha Mapinduzi kimefanya kura ya maoni ili kumpata mrithi wa Jimbo hilo atakayechuana na wagombea kutoka vyama vingine.

Katika kura hiyo ya maoni wagombea watatu wamejitokeza kuwania nafasi ya ubunge wa Jimbo la Chalinze kupitia chama cha CCM akiwemo mbunge wa zamani wa Jimbo hilo RAMADHAN MANENO, mwenyekiti wa zamani wa Yanga IMANI MADEGA na mdau mkubwa wa soka hapa nchini na mwanachama wa Yanga RIDHIWANI KIKWETE.
Baada ya kura kupigwa RIDHIWANI KIKWETE ndiye amepata Baraka za wanaCCM kuingia kwenye kinyang’anyiro cha Ubunge kwa kumpa kura 758 huku IMANI MADEGA akishika nafasi ya pili kwa kupata kura 335 na RAMADHAN MANENO akishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 206.
SHAFFIH DAUDA

Steve Nyerere aja na Snake Kingdom

Hii ndiyo kazi mpya ya Steve Nyerere itakayosambazwa na Proin Promotions
MWENYEKITI wa Bongo Movie Unity (BMU), Steven Mengele 'Steve Nyerere' anajiandaa kuiachia hadharani filamu yake mpya kwa mwaka 2014 iitwayo 'Snake Kingdom'.
Akizungumza na MICHARAZO, Steve Nyerere alisema filamu hiyo ya kijamii ameigiza na wakali wenzake kama Chuchu Hans, Mayasa Mrisho, Cathy Rupia, Bi Terry 'Mama Nyamayao' na wengine.
Steve Nyerere alisema filamu hiyo ni ya aina yake na kuwataka mashabiki kujiandaa kupata uhondo mara itakapoachiwa mtaani hivi karibuni chini ya kampuni mpya na inayokuja kwa kasi katika kusambaza kazi za wasanii wa filamu nchini ya Proin Promotions.
Mchekeshaji huyo anayeigiza sauti za viongozi mashuhuri, alisema 'Snake Kingdom' ni filamu iliyozalishwa na kampuni yake iliyowahi kutoa filamu kama 'Mwalimu Nyerere', 'My President', 'My Son', 'Mke Mwema' na nyingine.

Huwezi kuamini! Kaole Sanaa Group 'lafufuka' na Kipusa

Issa Kipemba 'Kipemba' aliyepigana kuirejesha tena Kaole Sanaa
Mmoja wa waasisi wa Kaole Sanaa, Bi Chuma Suleiman 'Bi Hindu' aliyecheza igizo la 'Kipusa'
Unamkumbuka Mzee wa Mabreka? Swebe Santana naye ndani dah!
JANA niliwaacha na maswali mengi juu ya taarifa inayokuwa ikiuliza unalikumbuka kundi la Kaole Sanaa Group, kundi lililochangia kupatikana kwa asilimia kubwa ya mastaa wanaotamba kwenye Bongo Movie.
Kundi hilo lililoasisiwa na kuundwa na wasanii wakongwe wa maigizo waliotamba kupitia Radio Tanzania (RTD) na lililokuja kutamba na michezo yao ya kwenye runinga kupitia kituo cha ITV kabla ya kuhamisa TVT (sasa TBC1) lilikuwa kama 'limekufa' hasa baada ya mastaa wake kuhamia kwenye filamu.
Hata hivyo mmoja wa mastaa wake, Issa Kipemba na wenzake kadhaa walikaa chini na kutafakari ili kulirejesha tena kwa nguvu kundi hilo.
Vikao kadhaa vilivyowahusisha baadhi ya waasisi wake kama Chuma Suleiman 'Bi Hindu' na wengine hatimaye kundi hilo limeanza kurekodi igizo lao jipya kwa ajili ya kuwarejesha burudani mashabiki wake ambayo waliikosa kwa kipindi kirefu.
Igizo hilo ambalo hata hivyo bado halijafahamika litaonyeshwa katika kituo gani cha runinga kwa sasa nchini, utafahamika kwa jina la 'Kipusa' ambapo sehemu kubwa ya tamthilia hiyo imesharekodiwa sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO mmoja wa nyota wa kundi hilo Adam Malele 'Swebe Santana' alisema tamthilia hiyo imewashirikisha asilimia kubwa ya nyota za zamani wa kundi hilo.
Swebe aliwataja baadhi ya nyota hao akiwamo yeye ni pamoja na Rashid Mwinshehe 'Kingwendu', Issa Kipemba 'Kipemba', Abdallah Mkumbira 'Muhogo Mchungu' na Ndimbango Misayo 'Thea'.
"Pia igizo hilo limewashirikisha Khadija Yahya 'Davina', Bi. Star, Happiness Stancelaus ‘Nyamayao’, Mzee Chap Chapuo,Davina, Bi Star, Bi Hindu, Mama Nyamayao na wengine," alisema Swebe.
MICHARAZO ilikuwa wa kwanza kudokeza kuwepo kwa mipango ya kurejeshwa upya kwa kundi hilo baada ya kuwafumania Lango la Jiji wakifanya vikao na sasa imethibitika suala hilo ni kweli tupu.
Taarifa zaidi na wasifu wa washriki walioucheza mchezo huo MICHARAZO itaendelea kuwajuza kila mara.

TFF/TWFA kutoa mafunzo maalum Siku ya Wanawake


Mwenyekiti wa TWFA, Linnah Mhando
KATIKA kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani na kudhamini mchango wa wanawake katika michezo Shirikisho la Soka ya Wanawake Tanzania (TWFA) ikishirikiana na TFF itaendesha mafunzo maalum.
Mwenyekiti wa TWFA, Linnah Mhando amesema shirikisho lake kupitia Kamati ya Wanawake ya mpira wa miguu kwa wanawake, wanatambua umuhimu wa siku ya wanawake duniani.
“Mpira wa miguu kwa wanawake ni moja ya michezo inayokuwa kwa kasi katika bara la Afrika na hata hapa nyumbani. Idadi ya wasichana wanoshiriki katika mpira wa miguu imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.
Katika kusheherekea  siku ya wanawake duniani mwaka 2014. Sherehe rasmi zitafanyika katika mkoa wa Tanga
TFF /TWFA wanaamini kuwa ili kuwa na kiwango kizuri na maendeleo katika mpira wa miguu wanawake  ni lazima kuanza na vijana wadogo hivyo basi Shirikisho na chama cha mpira wa miguu Tanga limeandaa mafunzo kwa walimu wapatao 30 toka shule15 za mkoa wa Tanga.
Walimu hao watapatiwa mafunzo kwa siku mbili na tarehe 08/03/2014 kutakuwa na Tamasha la Grassroot litakalojumusha jumla ya wanafunzi wapatao 1000 toka shule husika.
Ni matumaini ya shirikisho kuwa mafunzo hayo na tamasha la grassroot litaleta mwamko wa mpira wa miguu katika mkoa wa Tanga na hamasa kwa watoto wa kike,wasichana na kina mama katika ushiriki wa mpira wa miguu wanawake.

TFF kuwaadhibu wawili Twiga Stars

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) linatafakari hatua zaidi za kinidhamu dhidi ya wachezaji wawili wa kikosi cha Twiga Stars walioondolewa kwenye timu hiyo na Kocha Rogasian Kaijage. Kocha Kaijage aliwatimua kambini wachezaji Mwapewa Mtumwa na Flora Kayanda kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu wakati Twiga Stars ikijiandaa kwa mechi ya marudiano ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Zambia.
Twiga Stars ilipoteza mechi ya kwanza ugenini mabao 2-1 na kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya marudiano iliyochezwa Februari 28 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex, hivyo kutolewa katika mashindano hayo kwa jumla ya mabao 3-2.
“TFF tunaunga mkono hatua iliyochukuliwa na Kocha Kaijage dhidi ya wachezaji hao wakongwe wa Twiga Stars, kwani katika shughuli yoyote ile inayohitaji ufanisi nidhamu ni kitu cha kwanza,” imesema taarifa ya TFF.
Twiga Stars itacheza mechi za mchujo za michezo ya 11 ya Afrika (All Africa Games) ambayo itafanyika mwakani nchini Congo Brazzaville.

Sikia hii! Mchungaji akataza waumini wake wasivae Ch**pi


UKISIKIA Mwisho wa Dunia haupo mbali ndiko huku, Mchungaji mmoja nchini Kenya amewapiga marufuku waumini wake wa kike kuvaa nguo za ndani waendapo kufnya ibada ndani ya kanisa analoliongoza ili wampokee YESU wakiwa huru.
Mchungaji huyo Mkenya amenukuliwa nchini mwake kuwa waumini wanapaswa kuwa huru kimwili na kiroho wakati a kumpokea Bwana hivyo wanapaswa kutovaa nguo za ndani.
Ebu soma taarifa hiyo hapo nchini uone maajabu ya mwisho wa dunia na wanaojifanya wachungaji wa Kondoo za BWANA.
KENYAN Pastor Orders Female Congregants To Attend Church Without Putting On Bras & Panties For Christ To Enter Their Lives 'Freely'

A Kenyan pastor has ordered his female congregants to go to the church 'free' - That
is without bras and panties for Christ to enter their
lives.

According to kenyan-post.com, Reverend Njohi of the Lord's Propeller Redemption Church in Nairobi reportedly advised female worshippers against
wearing any undergarments to the church, calling them ungodly.

In a meeting chaired by him, a law was passed banning the wearing of inner wears.

Njohi claims that when going to church, people need to be free in 'body' and 'spirit' to receive Christ.

He went ahead to warn members of dire consequences if they secretly put on their inner wears.

Mothers were also advised to do same and check their daughters when coming to church on Sundays so as to receive Christ too.

Duh, Vibaka Nouma kweli wamliza Ally Choki

Ally Choki 'Mzee wa Ambulance' aliyelizwa na vibaka
AMA kweli kwenye msafara wa mamba kenge hawakosekani. Mkurugenzi wa bendi ya muziki wa dansi Extra Bongo Next Level 'Kamarade' 'wazee wa Kimbembe' Ally Choki alijikuta akimwaga machozi baada ya watu wanaodhaniwa kuwa vibaka kujipenyeza wakati wa uzinduzi wa albamu ya 'Mtenda Akitendewa' Februari 22 mwaka huu na kumuibia saa ya silva yenye thamani ya dola 300 sawa na sh.500,000.
Extra Bongo ilizindua albamu hiyo ndani ya Ukumbi wa Dar Live Mbagala jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mamia ya mashabiki na wadau wa muziki wa dansi ambapo Choki aliingia ukumbini akiwa ndani ya gari la kubeba wagonjwa 'Ambulance' na kulakiwa juu kwa juu.
Choki, alieleza, tukio la kuibiwa lilimkuta wakati akishuka kwenye ambulance ambapo ndani ya kundi la mashabiki waliompokea kulikuwepo na vibaka waliofanikwa kumvua saa hiyo pasipo yeye kujitambua.
"Kwa kweli saa yangu inaniuma sana nililetewa zawadi na rafiki yangu kutoka Qatar lakini ndo hivyo vibaka wameniingiza mjini alisema Choki kwa masikitiko na kuongeza.
"Wakati nimepanda jukwaani ndiyo nikashtukia nimelambwa saa, bahati nzuri simu na vitu vyangu vingine vya thamani nilikuwa nimeviacha kwa mlinzi wangu vinginevyo hali maumivu yangekuwa makali zaidi ya hivi.
Tukio la Choki kuibiwa linakumbusha tukio jingine lililowahi kutokea miaka kadhaa nyuma kwa aliyekuwa rapa wa bendi ya Tanzania One Theatre (TOT) Papii Kocha 'Mtoto wa Mfalme' kuporwa cheni na vibaka akiwa jukwaani wakati wa uzinduzi wa moja ya albamu za bendi hiyo katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.
Aidha Choki alisema atatoa zawadi ya sh.300,000 kwa mtu yoyote atakayeweza kufanikisha kupatikana kwa saa hiyo huku akitaka aliyeiba kumrejeshea kiroho safi na atampatia kiasi hicho cha fedha pasipo kufikishwa kwenye vyombo vya dola.
"Nimeamua kutoa zawadi kwa atakayewezesha niipate saa yangu au kwa aliyechukua kuirudisha kwangu, hii ni sababu nilikuwa naipenda sana alieleza.

Samuel Sitta ndiye Mwenyekiti wa Bunge la Katiba

  CCM waridhia awanie uenyekiti Bunge la Katiba
  Samia Hassan Suluhu kuwania umakamu
Mhe Samuel Sitta
WAJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamemaliza ‘mnyukano’ wa muda mrefu wa vigogo wa kuwania uenyekiti wa kudumu wa Bunge hilo, baada ya kutoa baraka zote kwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kugombea nafasi hiyo.

Wakati Waziri Sitta akipewa baraka hizo na wajumbe hao kupitia Kamati ya Uongozi ya Wabunge wa CCM, Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge, ameripotiwa kuamua kutogombea nafasi hiyo.

Pia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Hassan Suluhu, amepitishwa na kamati hiyo kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Kudumu wa Bunge hilo kutokea Zanzibar.

NIPASHE lilimtafuta Sitta jana kueleza kupitishwa na chama chake, lakini alisema kuwa hakuwa kwenye mkutano huo hadi mwisho. “Niliingia kwenye kikao na kutoka mapema, sijui kama uamuzi huo umefikiwa,” alisema.

Vyanzo mbalimbali vya NIPASHE kutoka ndani ya kikao hicho vinaeleza kuwa, uamuzi wa kamati hiyo ulifikiwa baada ya kuwaita viongozi hao na kuwahoji kwa nyakati tofauti iwapo wana nia ya kugombea nafasi hizo au la.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, Waziri Sitta na Waziri Suluhu, walipitishwa kwa kauli moja kuwania nafasi hizo, baada ya kamati hiyo kujiridhisha kwamba, wamekidhi sifa.

Mbali na Sitta, Suluhu na Chenge, chanzo hicho kilieleza kuwa mwingine, ambaye aliitwa na kuhojiwa na kamati hiyo ni Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, aliyefahamika kwa majina la Mwajuma Mgeni, ambaye hata hivyo, naye kama Chenge aliamua kutogombea nafasi hiyo.

Kabla ya kamati hiyo kutoa baraka hizo, kiongozi pekee aliyejitokeza hadharani na kutangaza azma ya kuwania nafasi hiyo ni Sitta pekee.

Sitta alisema anataka kuwania nafasi hiyo ili apate fursa ya kutimiza kwa vitendo ndoto ya Rais Jakaya Kikwete ya kuhakikisha Tanzania inapata katiba bora.

Imeelezwa kuwa wajumbe kadhaa walipendekeza jina la Sitta lipitishwe pasipo kuwapo mgombea mwingine, kwa maelezo kuwa wana-CCM wengine waliokuwa wanatajwa, wanaonekana kutokuwa na uwezo wa kulimudu Bunge hilo.

“Tumetoka kwenye kikao cha wajumbe wa CCM na kwa namna ya pekee, imekubalika kwamba Sitta ndiye anayefaa kwa uenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,” kilieleza chanzo kimojawapo kwa sharti la kutokutajwa jina lake gazetini.

“Kama chama kimeonyesha imani yake kwa Sitta, na kwa mujibu wa Sheria, Makamu wake anatakiwa kutoka Zanzibar ambapo jina la Samia Suluhu limepitishwa ndani kwa wajumbe wa CCM,” kilieleza chanzo hicho.

Sitta amekuwa akitajwa ndani na nje ya Bunge Maalum la Katiba, kwamba anafaa kuchukua nafasi hiyo kutokana na rekodi nzuri aliyoiacha alipokuwa Spika wa Bunge la Tisa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

ZENGWE LA SERIKALI TATU
Hata hivyo, waliokuwa wanampinga Sitta waliibua hoja kwamba mwanasiasa huyo mkongwe, amekuwa na mwelekeo wa kutaka kuwapo kwa serikali tatu, hoja aliyoipinga mara kadhaa akisema uamuzi wowote kuhusu hatima ya Katiba Mpya na hususani mfumo wa utawala utakavyokuwa, vitaamriwa na Watanzania.

HAKUNA MARIDHIANO
Katika hatua nyingine, matumaini ya kufikia maridhiano yatakayowezesha kupatikana kwa katiba mpya, yamezidi kufifia.

Hiyo ni baada ya wajumbe wa Bunge hilo kutoka vyama vya upinzani na makundi ya kijamii na wale wanaotoka CCM kuendelea kuvutana kuhusu utaratibu utakaotumiwa kupata uamuzi katika vikao vya Bunge hilo.

Katika mvutano huo, wajumbe wa CCM wanataka utaratibu utakaotumiwa kupata uamuzi katika vikao vya Bunge hilo uwe wa kura ya wazi, huku wale wanaotoka katika vyama vya upinzani na wa baadhi wanaotoka katika makundi ya kijamii wakitaka utumike wa kura ya siri.

Msimamo wa wajumbe kutoka vyama vya upinzani na makundi ya kijamii, ulifikiwa kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika kikao chake kilichofanyika juzi.

Chanzo chetu kutoka ndani ya kikao cha wajumbe wa CCM zinaeleza kuwa baadhi ya wajumbe walilalamikia kile walichokiita mjadala wa Rasimu ya Kanuni za Bunge Maalumu kuachwa kuhodhiwa na wapinzani bungeni.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, baadhi ya wajumbe katika kikao hicho walitoa mfano wakisema uundwaji wa Kamati ya Kanuni za Bunge Maalumu, ambao walidai kuwa imeachiwa kuhodhiwa na wapinzani.

Mbunge huyo alieleza pia kuwa wajumbe wengine katika kikao hicho walidai kwamba hata Rasimu ya Kanuni ya Bunge Maalumu ya Mwaka 2014 zimetungwa kwa kuwabeba wapinzani.

Alieleza kuwa kuwa baadhi ya wajumbe katika mjadala huo, walitaka kumjua waliyemuita “mchawi” aliyesababisha hali hiyo.

MKAKATI WA KUTEKA BUNGE
Mtoa taarifa wetu alieleza kuwa baada ya majadiliano yaliyochukua takriban saa sita, hatimaye kikao kilifikia maamuzi mbalimbali, ikiwamo namna wajumbe watahakikisha utaratibu wa kupata uamuzi katika Bunge hilo kwa kura ya siri unadhibitiwa.

Alieleza kuwa jambo lingine, ambalo lilitolewa uamuzi na kikao hicho, linahusu namna ya kumdhibiti mwenyekiti wa muda wa Bunge hilo, Pandu Ameir Kificho.

Chanzo hicho kilisema udhibiti huo utalenga zaidi katika maelekezo yoyote yatakayotolewa na mwenyekiti huyo wakati wa kusimamia mjadala wa rasimu ya kanuni hizo hadi azimio la kuzipitisha litakapotolewa na Bunge hilo.

Kilisema kuwa maamuzi hayo pia yalipinga ushauri uliotolewa na Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela, wakati akichangia mjadala wa rasimu ya kanuni hizo wiki iliyopita, kwamba ushauri huo hauna maslahi na chama.

Chanzo hicho kilieleza kuwa kikao hicho pia kilipitisha maamuzi ya kujengwa mazingira ya kuahirishwa makusudi kikao cha Bunge cha jana asubuhi, kama ilivyotokea.

Kilieleza kuwa uamuzi huo ulipitishwa ili kuwapa fursa wajumbe wa CCM kuifanya marekebisho rasimu ya kanuni hizo kama wanavyotaka.

NDIYO DHIDI YA SIRI

Chanzo hicho kilieleza pia kuwa uamuzi mwingine uliofikiwa na kikao hicho ulitaka lazima mwenyekiti wa muda wa Bunge hilo ahakikishe upitishaji wa vifungu vya rasimu ya kanuni hizo unafanyika kwa kura za wajumbe kupaza sauti za ndiyo au hapana.
 

Katibu wa wajumbe wa CCM, Jenista Mhagama, hakupatikana jana kuzungumzia yaliyojiri katika kikao chao cha juzi na hata alipopigiwa, simu yake ilikuwa inaita bila majibu.
 
CHANZO: NIPASHE

Inatisha jamaa afukua kaburi na mwanamke akiwa uchi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjzMYECCwkRKCFGbps0HoMYnLTH_Qnj1FT7Lc8nRmd6SQUU_iopPLSDtZrhMxlJqwdEv1hBiLOV3Fs1G4dPx8oHT59kcCtTbMznrMoHiZBiLDy-JI7LOQzK-Fx1WsVNz5jA8b1Zw9jA7npz/s1600/4680222.jpg
MKAZI wa kijiji cha Ikola  Wilaya ya Mpanda Mkoa  wa Katavi  Richard  Clavery  34 amefikishwa  Mahakamani  katika mahakama ya Wilaya ya Mpanda kujituhuma za kufanya vitendo vya ushirikina  wa kufukua kaburi la mwanamke aliyekufa.
Mtuhumiwa  alifikishwa kizimbani hapo Februari   25 mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa   na kusomewa mashitaka na mwendesha mashitaka  Godfrey  Luzabila
Mwendesha mashitaka alidai  Mahakamani hapo kuwa  mtuhumiwa  alitenda kosa hilo hapo Februali   18 mwaka huu majira ya saa nne usiku nyumbani kwa  Lenada  Sakafu
Mwendesha mashitaka   Luzabila  aliiambia mahakama kuwa siku  hiyo ya tukio  mtuhumiwa alifika nyumbani kwa Lenana  Sakafu  na kufukua  maiti ya mdogo wake na Lenada  aitwaye Tabu Omera  ambae alikuwa amefarii  siku tatu kabla ya tukio  hili
Aliendelea kuieleza Mahakama   siku hiyo  Lenada  alikuwa nyumbani  kwake pamoja na   majirani na ndugu  zake wakiendelea kuomboleza msiba  ghafla alitokea  mtoto wake aitwaye  Brandina  na kuwaeleza  kuwa ameona mtu nje akifukua kaburi la marehemu   ambae alikuwa amezikiwa  kwenye eneo la nyumba yao
Alieleza ndipo watu hao walipoamua kutoka nje   na kumkuta  mtuhumiwa  Richard  Clavery   akifukua kaburi  hilo huku akiwa  amevua nguo zake zote  ambazo alikuwa amezitundika kwenye msalaba  wa kaburi  hilo  na walipomsemesha mtuhumiwa  alijifanya kupandisha majini
Mtuhumiwa  baada ya kusomewa mashitaka  alikana   na Hakimu Mkazi Mfawidhi  Chiganga Ntengwa aliharisha kesi hiyo hadi hapo machi 6 na mtehumiwa alipelekwa rumande  baada ya kushindwa kutimiza masharti ya mdhamana ambapo alitakiwa adhaminiwe na mtu mmoja kwa  dhamana ya shilingi milioni  moja

Monday, March 3, 2014

Je, unalikumbuka kundi la Kaole Sanaa? Basi kaaeni chonjo

Issa Kipemba aliyekuwa akicheza kama Mshakunaku
Kingwendu Kingwendulile
Davina

Hii achana nayo, Issa Kipemba nouma

Issa Kipemba, Chini ni kazi yake mpya iliyopo njiani siyo ya kuikosa hii

Yanga kuivaa Al Ahly Cairo bila mashabiki

MAMLAKA za usalama nchini Egypt katika jiji la Cairo zimewaonya mashabiki wa Al Ahly kutoingia katika uwanja Cairo kuhudhuria mechi ya raundi ya pili ya CAF Champions league kati ya Al Ahly dhidi ya Young Africans S.C.  itakayochezwa mnamo March 9.
Katika taarifa iliyotolewa jana Jumapili, polisi wa Cairo walisema kwamba itapambana na jaribio lolote la mashabiki kujaribu kuingia uwanjani.

Azmi Megahed, msemaji wa FA ya Misri, alisema raia hawatoruhusiwa kuhudhuria mechi hiyo kutoka sababu za kiusalama.

Jumamosi wiki iliyopita, polisi walipambana na mashabiki wa Zamalek White Knights ambao walijaribu kuingia katika uwanja wa Cairo kuangalia mchezo kati ya Zamalek dhidi ya mabingwa wa Angola Cabo Schrob. Fujo hizo zilipelekea kwa kukamatwa kwa mashabiki 33.
SHAFIH DAUDA

Kumekucha Sikinde ebu sikia vibao vyao vipya

Baadhi ya waimbaji wa Sikinde
Baadhi wa wapuliza ala za upepo, Hamis Mirambo na Mbaraka Othman
BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Mlimani Park 'Wana Sikinde Ngoma ya Ukae' imekamilisha vibao vyake vitatu vipya kwa ajili ya albamu yao mpya ya 'Jinamizi la Talaka'.
Kibao cha kwanza cha Jinamizi la Talaka baadhi yenu mmeshaushikia katika vituo vya redio kwa vile ulirekodiwa toka mwaka jana, lakini vingine viwili vya Mkwezi na Deni Nitalipa mtakuwa hamjavisikia.
Wala usichokechungulia hapa mtandao wao wa https://www.hulkshare.com/sikinde, ambapo unaweza kuzisikiliza Online na kutoa maoni ama ushauri ili kuboresha ama kufanyia marekebisho nyimbo hizo kabla ya kuzinduliwa rasmi wakati wa kuadhimisha miaka 36 tangu kuanzishwa kwake.

Maajabu! Chatu amzidi ujanja Mamba

 Nyoka huyo alijipinda kwa Mamba na kumbana hadi akafa
 Nyoka alimvuta Mamba na kumtoa ndani ya Maji
 Chatu huyo alianza kumla Mamba na kushangaza wakazi
Baada ya mlo huo mkubwa Nyoka alijiendea zake
Chatu ameshinda vita vikali dhidi ya Mamba Kaskazini mwa mji wa QueensLand, kupigana na Mamba, kumpinda na kisha kumla.
Tukio hilo lilishuhudiwa katika ziwa Moondarra, karibu na mlima Isa na kunaswa kwa kamera na wakazi wa eneo hilo siku ya Jumapili.
Nyoka huyo mwenye urefu wa futi 10, alijipinda kwa Mamba na kuanza kupambana naye majini.
Hatimaye, Nyoka huyo alifanikiwa kumshinda Mamba na kumtoa nje ya maji na kisha kumla.
Tiffany Corlis,mkazi wa eneo hilo, alishuhudia pambano hilo na kupiga picha hizi.
"lilikuwa jambo la ajabu sana, '' aliambia BBC
"Tulimuona Nyoka akipambana na Mamba , alifanikiwa kumbana mamba hasa katika sehemu ya miguu ya ili kumdhibiti.''
"Pambano lilianzia ndani ya maji. Mamba alikuwa anajaribu kuweka kichwa chake juu ya maji wakati mmoja ingawa Nyoka alikuwa amembana sana.''
"Baada ya Mamba kufa nyoka alijikunjua, na kuja mbele ya Mamba huyo na kuanza kumla,'' alisema Tifanny.
Bwana Corlis alisema kuwa ilimchukua nyoka muda wa robo saa kumla mamba huyo.
''Bila shaka Nyoka huyo alishiba vyema, na hatujui alikokwenda, baada ya mlo wake,'' alisema mama huyo ambaye hakutaka kusuburi kumuona Nyoka tena.
Mtu mwingine aliyeshuhudia pambano hilo Alyce Rosenthal, alisema kuwa wanyama hao wawili walipambana kwa karibu saa 5. Hatimaye wote walionekana kuchoka.
''Sio kitu unachoweza kuona kila siku,'' alisema Alyce.
BBC SWAHILI

Mkenya Lupita Nyong'o aweka historia anyakua tuzo ya Oscar


Lupita Nyong'o akiwa na tuzo yake


Lupita akishow kwenye red carpet
MKENYA Lupita Nyong'o, ameweka historia baada ya kufanikiwa kunyakua tuzo maarufu duniani ya Oscar.

Tuzo hizo za 86 za Academy Awards 2014 maarufu kama oscars zilifanyika Dolby Theathre pande za Hollywood 
Mshiriki pekee toka pande za Afrika Mashariki, Mkenya Lupita Nyong’o ndiye ametunyanyua ile kinoma noma baada ya kuondoka na tuzo katika kipengele cha best supporting actress kupitia movie yake ya '12 Years a Slave'

Lupita ambaye aliwashinda waigizaji wenzie kama Jennifer Lawrence kupitia movie yake ya American hustle , Sandra Burlock kupitia movie yake ya Gravity, Lupita alipata shangwe za hatari wakati jina lake linatajwa kuwa mshindi wa tuzo hizo.
Hongera Lupita Nyong'o Watz mpooooo?!

Pambano la Simba, Ruvu laingiza Mil 20

PAMBANO la Ligi Kuu ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Ruvu Shooting iliyochezwa jana (Machi 2 mwaka huu) imeingiza sh. 20,610,000 ambapo kila klabu ilipata mgawo wa sh. 4,402,492 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 3,143,898.31.
Katika mchezo huo Simba iliweza kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 na kuendelea kusalia kwenye nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na Azam yenye pointi 40 na kufuatiwa na Yanga yenye 38 kisha Mbeya City inayokamata nafasi ya tatu ikiwa na pointi 36.
Katika hatua nyingine mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya Mlale JKT na Lipuli iliyokuwa ichezwe Machi 9 mwaka huu Uwanja wa Majimaji mjini Songea sasa itachezwa Machi 5 mwaka huu.
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imefanya mabadiliko hayo ili kuipunguzia gharama timu ya Lipuli ya Iringa ambayo jana (Machi 2 mwaka huu) ilicheza mechi mjini Songea dhidi ya Majimaji.


Yanga, Al Ahly zavuna Mil. 488/- Taifa

MBIOOOO
MECHI ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga na Al Ahly kutoka Misri iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki imeingiza sh. 448,414,000.
Mapato hayo yametokana na watazamaji 50,202 waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo kwa viingilio vya sh. 7,000, sh. 13,000, sh. 25,000 na sh. 35,000. Yanga ilishinda mechi hiyo kwa bao 1-0.
Mgawo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ni sh. 68,402,135.59, gharama za kuchapa tiketi ni sh. 10,343,219, waamuzi na kamishna sh. 14,665,930 na matangazo sh. 15,679,000.
Uwanja sh. 50,898,557.31, gharama za mchezo sh. 33,932,371.54, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)/Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 33,932,371.54 wakati Yanga ilipata mgawo wa sh. 220,560,415.01.

Stars yatua salama Namibia

KIKOSI cha Taifa Stars kimeondoka leo alfajiri kwenda Windhoek, Namibia kwa ajili ya mechi ya kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) dhidi ya wenyeji itakayochezwa Machi 5 mwaka huu.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ina msafara wa watu 25 unaoongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Timu imefikia hoteli ya Safari jijini humo.
Mechi hiyo itachezwa kwenye Uwanja wa Sam Nujoma, na kikosi cha Taifa Stars kipo chini ya Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madadi ambaye ana leseni A ya ukocha inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
Namibia (Brave Warriors) inayofundishwa na kocha Ricardo Mannetti imeingia kambini jana (Machi 2 mwaka huu) kwa ajili ya mechi hiyo ambayo tiketi zake zilianza kuuzwa Februari 28 mwaka huu.