STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 11, 2014

BFT yasogeza mbele mashindano ya Taifa hadi Nov 3.

http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/field/image/ngumilo.JPG?itok=lsVKoZrLMASHINDANO ya Taifa ya Ngumi za Ridhaa yaliyokuwa yafanyike mwezi ujao yameota mbawa baada ya Shirikisho la mchezo huo nchini (BFT) kutangaza kuyasogeza mbele hadi Novemba.
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga aliiambia MICHARAZO kuwa,  michuano hiyo iliyokuwa ianze kutimua vumbi lake kati ya Oktoba 8-14 sasa yataanza Novemba 3-8 kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wao.
Mashaga alisema alisema wameamua kuahirisha michuano hiyo ili kupisha mashindano ya ngumi ya kimataifa yanayoandaliwa na Chama cha Ngumi cha wilaya ya Temeke (TABA) ambayo yatafanyika mwezi ujao.
Katibu huyo alisema wameona siyo busara kuendesha michuano ya taifa na mashindano hayo ya kimataifa ambayo yamedhaminiwa na kampuni ya mtandao wa simu za mkononi ya Zantel.
"Tumeamua kuahirisha mashindano ya taifa ya ngumi hadi Novemba kupisha michuano ya kimataifa iliyoandaliwa na wanachama wetu mkoa wa Temeke, kuahirishwa huko kwa mwezi mzima ni fursa nzuri kwa mikoa kujipanga vema kabla ya kuja jijini Dar," alisema.
Mashaga alisema BFT inawatakia kila la heri timu za mikoa ambazo wameshawajulisha juu ya kuahirishwa kwa mashindano ya taifa, pia wakiipongeza Zantel kwa kujitolea kudhamini mashindano hayo ya kimataifa ya Temeke  kwa kutoa Sh. Milioni 10.
"BFT inawapongeza wadhamini wao na kuhimiza makampuni mengine kuiga mfano huo kwa lengo la kusaidia kuinua mchezo huo wa ngumi ambao umekuwa ukipambana kurejesha heshima ya Tanzania katika mazingira magumu," alisema Mashaga.
Katibu huyo wa BFT alisisitiza kuwa taratibu nyingine za mashindano ya Taifa yanaendelea kama kawaida na kwamba michuano hiyo itafanyikia kwenye uwanja wa Ndani wa Taifa.

Chicharito amvulia kofia Ronaldo, adai ni bora kuliko Messi

http://www.lapatilla.com/site/wp-content/uploads/2011/10/balon-de-oro-2011_323x216.jpg
MSHAMBULIAJI mpya wa Real Madrid, Javier Hernandez 'Chicharito' amesema tayari ameshawishika kwamba Cristiano Ronaldo ni bora zaidi ya Lionel Messi.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Mexico amejiunga na mabingwa hao wa Ulaya kwa mkopo wa msimu mmoja akitokea Manchester United muda mfupi kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.
Hata hivyo, Chicharito, ambaye alitua Old Trafford mwaka mmoja baada ya Ronaldo kutimkia Madrid, amesema tayari amedatishwa na mambo makubwa yanayofanywa na Mreno huyo mazoezini.
Bila ya shaka, Ronaldo ndiye bora," mshambuliaji huyo mwenye miaka 26 aliliambia gazeti la El Chiringuito.
"Katika muda mfupi niliokuwapo hapa, nimemuona yeye ndiye bora zaidi duniani.
"Si kwamba hufanya vyema sana katika mechi tu bali hata kila siku.
"Kwangu mimi, Cristiano ndiye bora zaidi. Messi yuko matawi hayo pia; baada ya Cristiano, anafuatia Muargentina yule."

Mama Mkwe wa Jennifer Mgendi kutolewa Sept 22

FILAMU mpya ya muimbaji nyota wa Nyimbo za Injili nchini, Jennifer Mgendi iitwayo 'Mama Mkwe' itatolewa rasmi Septemba 22 mwaka huu.
Akizungumza na MICHARAZO, Mgendi alisema filamu hiyo iliyokamilika hivi karibuni akiwa ameigiza na wakali wa filamu na miondoko ya Injili akiwamo Mussa Banzi na Bahati Bukuku itatoka mtaani siku hiyo.
Mgendi amewataka mashabiki wa filamu wasiikose filamu hiyo kutokana na kubeba ujumbe mwanana wenye mafunzo makubwa kwa jamii.
Alisema filamu hiyo iliyoongozwa na Mgeni Khamis na Chrissant Mhega wa Mega  Video Production imekamilika wiki iliyopita.
Mgendi anayetamba na albamu ya Hongera Yesu, alisema ndani ya filamu hiyo inayozungumzia mkasa wa mama mkwe anayemlilia mwanae wa kiume kumletea mjukuu na kuzua kizaazawa wamo pia Senga,Bi Bi Esther, Christine Matai, Husna Chobis. yeye (Mgendi)  na wengine ambao wameinoigesha vilivyo.
"Nimekamilisha filamu yangu mpya ya 'Mama Mkwe' ambayo nimeigiza mimi, Bahati (Bukuku) Christine Matai, Senga, Bi Esther, Mussa Banzi na wengine. Ni filamu yenye mafunzo makubwa kwa jamii na hasa mama wakwe wanaoingilia ndoa za watoto wao," alisema.
Kabla ya filamu hiyo, Jennifer amewahi kutamba na filamu kadhaa kama 'Chai ya Moto', 'Joto la Roho', 'Teke la Mama', na 'Pigo la Faraja'.

Ruvu Shooting kupimana ubavu na 94 KJ Lugalo leo jioni

TIMU ya maafande wa Ruvu Shooting inayojiandaa na Ligi Kuu Tanzania Bara jioni ya leo inatarajiwa kushuka dimba la Lugalo kuvaana na maafande wenzao wa 94 KJ katika mchezo wa kirafiki.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa muda mfupi uliopita na Afisa Habari wa timu hiyo, pambano hilo ni maalum kwa ajili ya kumpa nafasi kocha wao Mkenya Tom Olaba kuangalia mapunfugu wa kikosi chake dakika za mwisho mwisho kabla ya kujichimbia kuisubiri Ligi itakayoanza Septemba 20.
Timu hiyo ambayo ilimaliza katika nafasi ya sita msimu uliopita ikilingana pointi na Simba na Kagera Sugar kila moja ikiwa na 38, inasema wanaamini timu hiyo ya 94 KJ iliyopo Ligi Daraja la Kwanza itawapa mazoezi ya kutosha vijana wao katika pambano hilo la leo.
Ruvu iliyoingia kambini tangu Juni 9 imekuwa ikichgeza mechi kadhaa za kirafiki tayari kwa ajili ya Ligi Kuu ambapo watafungua dimba kwa kuumana na maafande wa Magereza, Prisons Mbeya katika pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Mabatini.
Msimu uliopita walifungua dimba na wapinzani wao hao na kuwanyuka mabao 3-0, kitu ambacho Bwire anaamini hata msimu huu mambo yatakuwa hivi hivyo katika pambano hilo la ufunguzi wa ligi Jumamosi ijayo.

Wednesday, September 10, 2014

Hii ni ajali nyingine iliyotokea asubuhi ya leo Lindi na kuua wawili

2fru
Ni taarifa ambayo imethibitishwa pia na kamanda Mpinga na kweli imehusisha kifaru cha Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) saa kumi na moja alfajiri ambapo kifaru kimoja chenye tairi kwenye msafara wa jeshi hilo kimeripotiwa kuacha njia na kugonga nyumba.
Shuhuda alieongea na Power Breakfast ya CloudsFM amesema ‘Imetokea Mnolela kijijini Lindi kwenye msafara huu wa jeshi ilitangulia Iveco moja na nyuma vifaru viwili na walipofika kwenye eneo la shule kuna kona mbaya sana ambayo mara nyingi magari huwa yanaanguka’
‘Kifaru kimoja kwenye huo msafara kilikosa njia na kuingia bondeni kikagonga nyumba ya kwanza kikamkanyaga mwenye nyumba kikagonga nyumba ya pili kikazama kwenye hiyo sebule, kwa harakaharaka waliofariki ni watatu, Wanajeshi watatu na mwenye nyumba ya kwanza na wengine ni majeruhi wa hali mbaya kabisa’
1fru
‘Msafara ulikua unatokea Mtwara kuelekea Nachingwea kwenye kambi kuu, hii kona ni kali na aliejenga hii barabara amebakiza baadhi ya changarawe hakufagia kwahiyo mtu akikaribia changarawe zile mtu zinamvuta, hiki kifaru chenye tairi kilikua kwenye spidi kubwa sana usio wa kawaida ikamshinda ndio akatumbukia bondeni’ – Shuhuda
‘Mmoja wa waliofariki ni mama mwenye nyumba ya kwanza ambae alikua amelala kwenye chumba cha mbele ndio alikanyagwa na kufariki papohapo, walioumia ni Wanajeshi waliokua wamekaa juu ya kifaru hicho, wamepelekwa kwenye hospital ya Mkoa wa Mtwara’ – Shuhuda
Kamanda Mpinga amethibitisha kutokea kwa hili tukio, unaweza kubonyeza play hapa chini kumsikiliza shuhuda mwenyewe na kamanda Mpinga.
Kwa msaada wa Millardayo.com

Bondia Djamel Dahou atua kuzipiga Moshi na Yazidu

http://mfs0.cdnsw.com/fs/Root/8ak85-IMG_0187.JPG
Bondia Djamel Dahou atakayepigana na Said Yazidu siku ya Ijumaa
BONDIA Djamel Dahou kutoka Algeria ametua nchini alfajiri ya jana tayari kwa ajili ya pambano lake la kuwania ubingwa wa Dunia dhidi ya Said Yazidu wa Tanzania litakalofanyika kesho mjini Moshi, Kilimanjaro.
Pambano hilo la raundi 12 litafanyika kwenye ukumbi wa YMCA na kusindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi likiwamo la kuwania ubingwa wa UBO Afrika.
Pigano hilo jingin la ubingwa wa UBO litakuwa kati ya Mtanzania Ali Ramadhan 'Alibaba' dhidi ya Mmalawi, Alick  Mwenda.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania, PST, litakalosimamia pambano hilo lililoandaliwa na kampuni ya Green Hill Promotion, Anthony Rutta alisema Dahou alitua alfajiri ya jana kwa Ndege ya Egypt Airways.
"Mpinzani wa Said Yazidu, Djamel Dahou ameshatua na anaelekea Kilimanjaro kwa ajili ya pambano lao la Septemba 12 kwenye ukumbi wa YMCA," alisema.
Rutta alisema pambano hilo litatanguliwa na michezo kadhaa ya utangulizi likiwamo la UBO Afrika la raundi 10 kati ya Alibaba na Mwenda wa Malawi.
Mengine ni kati ya Fatuma Yazidu dhidi ya Joyce Adam, Emmanuel Alex dhidi ya Ali Bugingo huku Pascal Bruno atazipiga na Cosmas Kibuga, George Allen atazipiga na Ssebo Husseni na Raymond Bwango dhidi ya Fadhil Mkinda.

Uholanzi yamtisha Sepp Blatter

http://vid.alarabiya.net/images/2014/07/27/837d0b74-5c15-435a-bd94-cc9250711bb9/837d0b74-5c15-435a-bd94-cc9250711bb9_16x9_600x338.jpgCHAMA cha Soka cha Uholanzi-KNVB kimedai kutompigia kura Sepp Blatter ambaye amethibitisha kugombea tena urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kwa kipindi cha tano. 
Rais wa KNVB Michael van Praag aliwaambia waandishi wa habari kuhusu msimamo wao huo jana lakini akakiri kuwa haoni kama kuna mtu anayeweza kumng’oa Blatter katika nafasi hiyo. 
Uholanzi mara kadhaa wamekuwa wakimpinga Blatter mwenye umri wa miaka 78 ambaye alichukua madaraka hayo kutoka kwa Joao Havelange mwaka 1998. 
Katika mkutano mkuu wa FIFA uliofanyika nchini Brazil kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia, KNVB ilimpasha Blatter kuwa anatakiwa astaafu huku wakimtaka kuwajibika kutoka kashfa mbalimbali zilizolikumba shirikisho hilo. 
Lakini Blatter anaonekana bado kutaka kuendelea kukomalia nafasi hiyo kwa kipindi kingine kitakachomaliza mwaka 2019 akiwa na umri wa zaidi ya miaka 83, baada ya rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA Michel Platini kuweka wazi kuwa hatagombea kiti hicho. 
Praag amesema bahati mbaya Platini amekataa kugombea kwani ndiye mtu pekee ambaye angeweza kusimama na Blatter.

Ramsey aiweka roho juu Arsenal

Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ball
Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Twisted it: Chris Coleman says he hopes Ramsey's injury wasn't enough to keep him out for too long
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=6083#sthash.pLeuLv8H.dpuf
Going down: Ramsey picked up a suspected ankle injury while battling for the ballMASHABIKI wa klabu ya Arsenal wapo roho juu baada ya kiungo wao mahiri, Aaron Ramsey kuumia kifundo cha mguu na kuwa hatarisni kulikosa pambano la mwishoni mwa wiki dhidi ya Manchester City katika Ligi Kuu ya England.
Kiungo huyo alipata  majeruhi ya kifundo cha mguu katika ushindi wa Wales wa mabao 2-1 dhidi ya Andorra jana usiku baada ya kufanyiwa rafu na mchezaji wa Andorra ambapo alipatiwa matibabu, lakini akatolewa uwanjani.
Meneja wa timu, Chris Coleman alisema ukubwa wa  majeruhi utatangazwa saa 24 kuanzia jana usiku, na hali hiyo imempa maumivu ya kichwa, kocha Arsene Wenger
Chris Coleman alisema anaamini majeruhi ya Ramsey haiwezi kumuweka nje ya uwanja wa muda mrefu.

Kuziona Yanga, Azam buku 5 tu


KIINGILIO cha chini kwenye mechi ya Ngao ya Jamii kuashiria uzinduzi wa msimu mpya wa Ligi kati ya Azam na Yanga itakayochezwa Jumapili (Septemba 14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000.

Mechi hiyo itaanza saa 10 kamili jioni, na kiingilio hicho cha sh. 5,000 ni kwa viti vya rangi ya kijani na bluu vitakavyochukua jumla ya watazamaji 36,000 katika uwanja huo wenye viti 57,558.

Viingilio vingine katika mechi hiyo ambayo itatumia tiketi za elektroniki ni sh. 10,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000 kwa viti vya VIP C na B wakati viti vya VIP A kiingilio ni sh. 30,000.

MWAMUZI LUGENGE KUAGWA LEO
Mwamuzi wa daraja la kwanza (class one), Luteni Godwill David Lugenge aliyefariki dunia juzi (Septemba 7 mwaka huu) kwa ajali ya gari katika Wilaya ya Handeni mkoani Tanga anaagwa leo (Septemba 9 mwaka huu).

Mwili wa marehemu ambao umehifadhiwa katika Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) Lugalo, baadaye leo saa 6 mchana utapelekwa nyumbani kwa kaka yake Kimara Bucha jijini Dar es Salaam ambapo shughuli za kuaga zitafanyika kabla ya safari ya kwenda mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Luteni Lugenge ambaye mwishoni mwa wiki alishiriki mitihani ya utimamu wa mwili kwa waamuzi wa Ligi Kuu, akiwa na ndugu yake Christopher Alexander Lunyungu katika gari dogo walipata ajali hiyo wakati wakienda mkoani Kilimanjaro.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambalo limetoa ubani wa sh. 200,000 kwa familia ya marehemu kwenye shughuli ya kuaga itawakilishwa na mjumbe wake wa Kamati ya Utendaji ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi, Saloum Umande Chama.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Luteni Lugenge, Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu nchini (FRAT) na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Bwana ametoa, Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe

Yaillah Toba! Ajali nyingine tena yachukua roho za watu


 
 
 
JANGA la ajali za barabarani zimeendelea kupukutisha roho za watanzania baada ya basi la Super Feo lililokuwa linatokea Songea kwenda Mbeya kupata ajali na kusababisha vifo vya watu wawili na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa.
Ajali hiyo imetokea leo eneo la Sinangula wakati likimkwepa mwendesha baiskeli na kwenda kuvamia mti na kupinduka na taarifa za awali zinasema watu zaidi ya 34 wamejeruhiwa na wawili kufa jambo taarifa za sasa zinadai ni abiria watatu wamepoteza maisha.
Ajali hiyo ni mfululizo wa matukio yaliyoteketeza roho za watanzania huku tukielekea WIKI YA USALAMA BARABARANI inayotarajiwa kuadhimishwa mjini Arusha.
Tufunge na kuomba Mungu atuepushilie janga hili ambalo ni janga la kitaifa na linaloua pengine kuliko hata maradhi tishio nchini kwa sasa.
MICHARAZO inatoa pole kwa wote waliopoteza ndugu, jamaa na rafiki zao kwenye ajali zote zilizotokea ndani ya mwezi huu wa Septemba na mingine ya nyuma na kuwaombea kila la heri walioachwa na majeraha kupona haraka kwa uwezo wa AlLAH SW. Inshallah

Vijana CUF wahimiza kuchangamkia uchaguzi mkuu

http://3.bp.blogspot.com/-Vg1FlLMzmC8/UGVoED0VOGI/AAAAAAAByBI/GI-uXRyYJ-s/s320/tz%7Dcuf.gif 
Na Suleiman Msuya 'Kipimo'
JUMUIYA ya Vijana ya Chama Cha Wananchi (JUVICUF) imewataka vijana wa chama hicho kujitokeza kugombea katika chaguzi za vijana pamoja na ule wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni nchini kote.
Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa (JUVICUF) Hamidu Bobali wakati akizungumza na mwandishi wa habari katika ofisi za chama cha CUF jijini Dar es Salaam.
Alisema chama kupitia (JUVICUF) kinatarajia kufanya chaguzi kuanzia matawi, kata, wilaya na Taifa ambapo wilaya 45 za Tanzania Bara na 10 za Zanzibar zitashiriki ili kupatikana kwa viongozi.
Bobali alisema mikakati (JUVICUF) ni kuhakikisha kuwa chama kinajijenga vizuri kuanzia ngazi za chini hasa ukizingatia kuwa ni wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwahimiza vijana wa CUF kujitokeza katika chaguzi zote za chama katika ngazi ya vijana ambazo zimeanza kufanyika sasa na mwezi ujao Novemba ili mwezi Desemba tuweze kufanya uchaguzi mkuu wa vijana Taifa”, alisema.
Bobali alisema uchaguzi huo wa Taifa unatarajiwa kuhusisha zaidi ya vijana 135 kutoka Bara na 120 kutoka Zanzibar ambao watotokana na chaguzi katika ngazi za Wilaya.
Alisema mikakati yao ni kuhakikisha kuwa wanakuwa na wawakilishi kutoka Wilaya zote za Tanzania Bara kama ilivyo Zanzibar ambayo italeta ushindani wa kisiasa hapa nchini.
Naibu Katibu huyo alisema pia JUVICUF inajipanga kufanya operasheni mbalimbali ambazo zitakuwa na lengo la kuhamasisha vijana kujitokeza katika chaguzi na ufahamu juu ya lengo la Wabunge wanaounga mkono Rasimu ya Jaji Warioba kutoka nje ya Bunge.
Alisema kuna hali ya sintofahamu kwa baadhi ya vijana na wananchi mbalimbali ya nini sababu ya wajumbe wa UKAWA kutoka nje ya Bunge hivyo JUVICUF inaona ni wakati muafaka wa kutoa elimu.
Bobali alisema ni vema vijana wa vyama vinavyounga mkono UKAWA kuendelea kuwa na umoja ili kuhakikisha kuwa juhudi za viongozi wao wa Kitaifa zinafikiwa ili waweze kukomboa Taifa.

Tuesday, September 9, 2014

Francis Cheka kuzipiga na Pascal Ndomba

Francis Cheka
Pascal Ndomba
BINGWA wa zamani wa Dunia wa WBF, Francis Cheka anatarajiwa kupanda ulingoni siku ya Novemba Mosi kupigana na bondia Pascal Ndomba katika pambano lisilo la ubingwa litakalofanyika mjini Morogoro.
Kwa mujibu wa Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC) Chaurembo Palasa, pambano hilo la uzito wa juu litachezwa kwenye uwanja wa Sabasaba mjini humo.
Palasa alisema TPBC imetoa baraka zote kwa pambano hilo litakalokuwa la raundi 10.
Rais huyo alisema mchezo huo na mingine ya utangulizi siku hiyo imeandaliwa na kampuni ya Cheka Promotion na mabondia watakawasindikiza wanatarajiwa kutangazwa baadaye.
Hilo litakuwa ni pambano la kwanza kwa mabondia hao kukutana na pia la kwanza kwa Cheka tangu bondia huyo alipopanda ulingoni mara ya mwisho  Aprili 19 mwaka huu alipopigana na bondia toka Iran Sajad Mehrabi  na kutoka naye sare kwenye ukumbi wa PTA.
Cheka ndiye bondia asiyepigika nchini kwa sasa akiwa amewatandika karibuni wapinzani wake wote tangu mwaka 2008 hajapigwa, ingawa anapotoka nje ya nchi amekuwa 'urojo'.

Newz Alert! Kaburi ya aliyekufa ajali ya mkoani Mara lafukuliwa

KABURI la mmoja kati ya watu waliopoteza maisha katika ajali mbaya iliyohusisha mabasi ya Mwanza Coach na J4 katika eneo la Sabasaba, Musoma, Mara limekutwa likiwa limefukuliwa na watu wasiojulikana leo asubuhi.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichofika katika eneo la makaburi ya Musoma Basi, ndugu wa marehemu aliyetajwa kwa jina la Juma Sai walienda asubuhi kuangalia kaburi ikiwa ni siku ya tatu tangu wafanye mazishi, ndipo walipokuta kaburi limefukuliwa na mbao zilizotumika kuhifadhi mwili kwa imani ya dini ya kiislamu zikiwa zimewekwa pembeni.

“Mwili wa marehemu bado uko ndani, watu wengi wako hapa na polisi wameimarisha hali ya usalama. Madaktari wameshafika hapa na wanafanya uchunguzi kuona kama kuna kiungo chochote kilichotolewa kwenye mwili wa marehemu. Inasikitisha sana.” Kimeeleza chanzo chetu cha kuaminika.

Ijumaa iliyopita, kulitokea ajali mbaya iliyohusisha magari matatu, mabasi ya kampuni ya Mwanza Coasch na J4 pamoja na gari dogo aina ya Landcruiser. Watu zaidi ya 40 walifariki na wengine 79 kujeruhiwa.

Udaku Specially

Maskini, Kisura huyu kumbe alijinyonga

Ripoti: Mwimbaji wa kike wa Marekani aliyekutwa amekufa nyumbani kwake alijinyonga
POLISI wa Los Angeles wameeleza kuwa mwimbaji wa kike wa Marekani, Simone Battle aliyekutwa amekufa nyumbani kwake wiki iliyopita alijiua kwa kujinyonga.
Sababu ya kifo chake imetajwa siku mbili baada ya polisi kuanza uchunguzi kufuatia tukio hilo lililotokea kusini mwa Hollywood.
Simone Battle aliwahi kuwa mshiriki wa shindano la kuimba la X Factor na kufika katika hatua ya fainali, pia alikuwa member wa kundi la G.R.L.

Rais Yoweri Museveni wa Uganda kutua nchini kesho

http://media.web.britannica.com/eb-media/05/61705-004-8486B3D5.jpg 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RAIS wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, anatarajiwa kuwasili nchini siku ya Jumatano asubuhi, tarehe 10 Septemba, 2014 kwa ziara ya kikazi ya siku moja.

Katika ziara hiyo nchini, Mhe.Museveni atakuwa na mazungumzo na mwenyeji wake, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ikulu, Dar es Salaam. Rais Museveni ataondoka baadaye siku hiyo hiyo kurejea nyumbani.

IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI,
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Didier Zakora atundika daluga kuichezea Tembo wa Ivory Coast

http://images.supersport.com/2014/5/Didier-Zokora-100615-Gestures-R300.jpg 
http://futboler.tv/wp-content/uploads/2014/05/fft99_mf1310873.jpegKIUNGO nyota wa timu ya taifa ya Ivory Coast, Didier Zokora ametangaza kustaafu soka ya kimataifa baada ya kuitumikia timu ya taifa kwa zaidi ya miaka 10. Maestro kama anavyofahamika kwa mashabiki wa soka nchini mwake, alisema anadhani ni muda muafaka kuwapisha wengine kuitumikia timu hiyo.
"Baada ya miaka 15 ya kucheza soka ya kiwango cha juu, nafikiri ni wakati wa mimi kufikia tamati ya soka soka ya kimataifa" amesema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 katika mashindano maalum yaliyoandaliwa kwa heshima yake mjini Abidjan kitongoji cha Williamsville."Ni wakati wa kutoa nafasi kwa vijana wadogo. Katika mechi na Sierra Leone, nimeona wachezaji wadogo ambao wanaweza kuchukua nafasi," aliongeza.
Zokora alianza kuichezea timu hiyo tangu mwaka 2000 na amekuwa na rekodi ya kucheza mechi 121.
Amecheza fainali tano za Kombe la Mataifa ya Afrika mfululizo 2006, 2008, 2010, 2012 na 2013, mbali na  Kombe la Dunia mara tatu mfululizo 2006, 2010 na 2014.
Kiungo huyo mkabaji, kwa sasa anachezea klabu ya Akhisar Belediyespor ya Uturuki, baada ya kuchezea klabu nyingine za Racing Genk ya Ubelgiji, Saint-Etienne ya Ufaransa, Tottenham Hotspur ya England, Sevilla ya Hispania na Trabzonspor ya Uturuki pia.
Ni matunda ya akademi ya ASEC Mimosas ya mwaka 1998 ambao walishinda taji la Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kuifunga Dynamos ya Zimbabwe kwenye fainali, michuano ambayo pia Yanga SC ilishiriki.
Zokora ambaye majina yake kamili ni
Déguy Alain Didier Zokora alizaliwa Desemba 14, 1980) ni gwiji mwingine wa Ivory Coast kustaafu kwa sasa baada ya Nahodha wa zamani, Didier Drogba anayechezea Chelsea.

Diamond, Yami Alade kuangusha ya pamoja Coke Studio Africa

STAA wa Mdogomdogo na My Number One, Diamond Platnumz amerejea tena kwenye msimu wa pili wa kipindi cha Coke Studio Africa na awamu hii atatangeneza 'pea' na mkali wa Johnny, Yemi Alade kutoka nchini Nigeria.
Kwa mujibu wa taarifa za kwenye mtandao, Diamond ni msanii wa nne mwaka huu kutoka Tanzania aliyeshiriki kwenye kipindi hicho kinachorekodiwa jijini Nairobi, Kenya.
Wengine waliowahi kushiriki ni pamoja na Vanessa Mdee aliyerekodi na Burna Boy wa Nigeria, Joh Makini aliyerekodi na Chidinma wa Nigeria na Shaa aliyerekodi na Jacky Chandiru wa Uganda.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Yemi aliyekuja nchini hivi karibuni aliweka picha yake akiwa na Diamond katika na kudokeza anavyojisikia furaha kufanya kazi na mshindi huyo wa tuzo saba kwa mpigo wa Kili Music Awards-2014.
#wonderment! With the infamous ubertalented six-abbs superstar Diamond….@diamondplatnumz
#iAmHumbled #thankYouCokeStudio, ForThe Opportunity God bless AFrica.. #cokeastudioafrica
@cokestudioafrica @dresomes Nosa @chocolatecity
Diamond has been singing your song all morning@audumaikori.
Naye Diamond katika picha akiwa na mrembo huyo
ameandika:
Na dem ake Johny @yemialade , ushaelewa nini kinaendelea si eti????….. (jus me and Johny’s
Girlfriend…You allready know what it is ryt???… Cc@yemialade

Hispania yaifumua Macedonia 5-1 bila Diego Costa, David Silva nouma

Silva na Paco Alcacer wakipongezana baada ya kinda hilo (9) kufunga bao
Breaking away: Cesc Fabregas escapes a challenge from Macedonian midfielder Stefan Spirovski as Spain exerted their authority in the midfield areas
Utanivunja nyonga bure! Mtaalam Cesc Fabregas akimpeleka mtu chini
MABINGWA watetezi wa Kombe la Mataifa ya Ulaya, Hispania ikiwa bila mshambuliaji wao nyota Diego Costa anayesumbuliwa na majeraha ya nyama za Paja, usiku wa kuamkia leo ilitoa onyo kwa wapinzani wake baada ya kuifumua Macedonia kwa mabao 5-1 katika mechi za kuwania fainali hizo za Uero 2016.
Mchezaji aliyechukua nafasi ya Costa, Paco Alcacer , 21 aliitenda haki kwa kuifungia Hispania bao la pili katika dakika ya 17 akimalizia krosi pasi safi ya Cesc Fabregas.
Bao la kwanza la wababe hao wa zamani wa Dunia, lilitumbukizwa wavuni na Sergio Ramos  kwa panalti dakika ya 16 baada ya David Silva kuangushwa kwenye eneo la hatari.
Macedonia walijipatuia bao lao la kufutia machozi katika dakika ya 28 baada ya Juanfran kufanya madhambi na Agim Ibraimi akafunga kwa kumtungua Iker Casillas.
Sergio Busquets aliiandikia Hispania bao la tatu sekunde chache kabla ya kwenda mapumziko, huku mabao mengine ya ushindi huo mnono kwa Hispania yakiwekwa kimiani na David Silva katika dakika ya 50 na Pedro aliyepigilia msumari dakika za lala salama.

Danny Welbeck aibeba England michuano ya kuwania Euro 2016

At the double: Danny Welbeck wraps up victory for EnglandMSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Danny Welbeck usiku wa kuamkia leo amethibitihs aubora wake baada ya kuipa England ushindi wa 2-0 dhidi ya Uswisi ugenini katika mechi ya kuwania kufuzu Euro 2016. Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United, alifunga mabao hayo katika dakika za 59 na 90 na kumfanya kocha Roy Hodgson aondoke na furaha uwanjani.
Welbeck aliyekuwa hana nafasi katika kikosi cha kwanza cha Mashetani Wekundu alinyakuliwa na Arsene Wenger mwishoni mwa msimu wa usajili kwa mkopo.

Lulu Kayage atamba kumtandika mtu Sept 27

 Kocha mkongwe wa mchezo wa masumbwi nchini akimwelekeza bondia Lulu Kayage jinsi ya kukupa ngumi wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa kupambana na Fatuma Yazidu mpambano utakaofanyika September 27 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam picha na SUPER D BLOG
 Bondia Lulu Kayage kulia akielekezwa jinsi ya kupiga makomde mazito na Kocha Habibu Kinyogoli 'Masta' wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa kupambana na Fatuma Yazidu Septermber 27 katika ukumbi wa frends Corner Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BLOG
Bondia Juma Biglee kushoto akioneshana umwamba na Lulu Kayage wakati wa mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Ilala Amana Dar es salaam Lulu anajiandaa na mpambano wake na Fatuma Yazidu utakaofanyika Septermber 27 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Picha na SUPER D BLOG
Bondia Lulu Kayage kushoto akipambana na Juma Biglee wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa kupambana na Fatuma Yazidu september 27 Dar es salaam Picha na SUPER D BLOG
Bondia Lulu Kayage kushoto akifanya mazoezi ya kuimalisha misuli ya tumbo wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa kupambana na Fatuma Yazidu september 27 katika ukumbi wa frends corene manzese Dar es salaam kushoto ni Titus Jonson Picha na SUPER D BLOG
Na Mwandishi Wetu

 

lulu kayage
BONDIA Lulu Kayage yupo katika mazoezi makali kwa ajili ya kupambana na bondia Fatuma Yazidu Septermber 27 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam

akizungumza wakati akiwa mazoezini katika kambi ya ilala amana Dar es salaam amemtahadhalisha mpinzani wake kufanya mazoezi ya kutosha kwani yeye kwa sasa yupo fiti kupita kiasi na akuna bondia wa kike kwa Tanzania hii mwenye uzito wake anaeweza kumsumbua kwa sasa kwani ana uzoefu mkubwa na wakutosha

aliongeza kwa kusema kuwa jinsi anavyosimamiwa mazoezi na jopo la makocha wake wanao ongozwa na kocha mkongwe nchini Habibu Kinyogoli 'Masta' kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' na Kondo Nassoro ambao wanamuhimiza kila wakati kufanya mazoezi ya kutosha na ndio wana muongeza moyo zaidi kwa ajili ya kufanya mazoezi

Lulu aliongeza kuwa mchezo wa masumbwi nchini wasichana wanaojitokeza ni wachache sana hivyo kukosa msisimko wa kila wakati kucheza wasichana kwa wasichana hivyo kuomba wasichana mbalimbali wajitokeze kufanya mazoezi na kucheza mchezo kwa  ajili ya afya pia ni kwa ajili ya ajira kumbuka mchezo wa ngumi ni ajira kama una uwezo wa kufanya vizuri

siku hiyo pia kutakuwa na mpambano mkali utakao wakutanisha Nassibu Ramadhani na Mohamed Matumla mwingine ni Sadiki Momba na Adam Ngange, Issa Omari na Juma Fundi
siku hiyo pia kutakuwa zikiuzwa DVD mpya za masumbwi ambazo zinaonesha mafunzo mbalimbali ya mchezo wa ngumi yanavyoanza hatua kwa hatua

mpaka kujua kitu kamili katika mchezo huo pia kunakuwa na mapambano ya mabondia mabigwa wa dunia wa mchezo huo kama Floyd Maywether, Manny Paquaio,mike Tyson, Mohamed Alli pamoja na mabambano ya ngumi ya ndani