STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 2, 2014

Al Shaabab yawatimua Wakuu wa Usalama Kenya

Aliyekuwa Waziri wa Usalama, Joseph Ole Lenku
RAIS Uhuru Kenyatta amemwachisha kazi Waziri wa Usalama nchini Kenya, Joseph Ole Lenku na nafasi kumteua Joseph Nkaiseri, huku Mkuu wa Jeshi la Polisi,Inspekta Jenerali David Kimaiyo amejiuzulu wadhifa wake kutokana na shinikizo dhidi yake kutrokana na kudai kushindwa kutimiza wajibu wake kulinda Usalama nchini humo.
Rais Kenyatta alisema kuwa baada ya mazungumzo na Bw. Kimaiyo alikubali 'kustaafu' mapema kutoka kwa majukumu yake kwa sababu za kibinafsi.
Rais alitoa tangazo hilo wakati akihutubia taifa kufuatia shambulizi la hapo jana dhidi ya wachimba migodi 36 waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera Kaskazini ya Kenya.
Rais pia alitangaza kuwa amekubali ombi la Generali wa polisi David Kimaiyo kuachia wadhifa wake. Kimaiyo na Ole Lenku wamekuwa wakikabiliwa na shinikizo za kuachia ngazi kufuatia kukithiri kwa utovu wa usalama nchini.
Hatua ya kuwatimua kutoka katika nyadhifa zao wawili hao bila shaka litakuwa jambo la kuridhisha kwa wakenya wengi ambao wamekuwa wakilalamikia utovu wa usalama na kuwataka waondoshwe ofisini. Uteuzi wa Joseph Nkaisery kama waziri mpya wa usalama ni jambo jipya kwani atakuwa mwanasiasa wa kwanza kutoka kwa upinzani kuwa ndani ya serikali.
Alipokuwa anahutubia nchi,Rais Kenyatta aliwasihi wabunge kuongeza muda wa vikao vyao vya leo ili kumhoji na kumkagua Nkaisery aliyeteuliwa kuchukua nafasi ya waziri mpya wa usalama na maswala ya ndani ili wamuidhinishe.

Make Money at : http://bit.ly/copy_win

Liverpool, Manchester Utd kuvuna nini leo EPL, Arsenal kesho

http://cdn.footballtarget.com/wp-content/uploads/2013/10/Manchester-United-vs-Stoke-City.jpghttp://assets.lfcimages.com/uploads/8847__0257__leicester_prem_away_1000x600_517X310.jpg 
VUMBI la Ligi Kuu ya England (EPL) linatarajiwa kutimika tena leo kwa michezo sita, ambapo klabu za Liverpool na Manchester United zitakuwa viwanja tofauti kusaka pointi tatu muhimu.
Liverpool ambayo imekuwa na mwenendo mbaya msimu huu itakuwa uwanja wa ugenini kuvaana na Leicester City, wakati Mashetani Wekundu walioanza 'kuchangamka' watakuwa Old Trafford kuialika Stoke City.
Mechi nyingine za leo itazikutanisha timu za Burnley itakayokuwa nyumbani kuikaribisha Newcastle United, Swansea City wataialika QPR, wakayi Crystal Palace itaikaribisha Aston Villa na West Bromwich Albion itaialika West Ham United katika mchezo mwingine mkali.
Mashabiki wa kandanda watakuwa na hamu ya kufuatilia pambano la Mashetani Wekundu ambao mwishoni mwa wiki wlaipata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Hull City na kuingia kwenye Nne Bora.
Ingawa ushindi itakayopata leo timu hiyo inayonolewa na Mholanzi, Luis Van Gaal haiwezi kuwafanya wapande zaidi, lakini utawafanya wajichimbie zaidi katika nafasi hiyo ya nne kwani itafikisha pointi 25.
Moja pungufu ya ile ya Southampton ambayo wikiendi iliyopita ilitolewa nishai na Mabingwa watetezi Manchester City waliokwea hadi nafasi ya pili nyuma ya Chelsea.
Timu hizo zote tatu za Chelsea, Manchester City na Southampton zitashuka dimbani kesho kwenye mfululizo wa ligi hiyo maarufu duniani.
hiyo.
Liverpool baada ya kuzinduka mwishoni mwa wiki kwa kupata ushindi mwembamba dhidi ya Stoke City ni wazi wanahamu ya kuendeleza wimbi hilo ili kujenga imani kwa kocha Branden Rodgers.
Timu hiyo iliyomaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita kwa sasa ipo nafasi ya 11 baada ya ushindi huo wa Jumamosi nyumbani, itahitaji kushinda leo licha ya kuwa uwanja wa ugenini na timu ambayo ilicharazwa maba0 3-2 na QPR na kuachwa mkiani.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo minne, Arsenal itakuwa nyumbani uwanja wa Emirates kuikaribisha Southampton, Chelsea itaialika Spurs na City itaifuata Sunderland na Everton inayouguza kipigo cha mabao 2-1 ilichopewa ugenini na Spurs itaumana na Hull City.

Ajali Mlima Kitonga, basi latumbukia mtaroni na kuziba njia

 
Basi liitwalo Easy Bus lenye namba za usajili T 298 BLZ lililokuwa likitokea Lilongwe Malawi likiwa katika mtaro wa Mlima Kitonga.
 
 
Foleni kubwa iliyosababishwa na basi hilo baada ya kuingia mtaroni na kuziba njia.
BASI la abiria la Easy Bus lenye namba za usajili T 298 BLZ  linalofanya safari zake kati ya Malawi na Tanzania limepata ajali katika Mlima Kitonga, mapema leo baada ya kutumbukia kwenye mtaro.
Hata hivyo jambo la kushukuru Mungu ni kwamba hakuna mtu aliyepoteza maisha yake, japo ajali hiyo imesababisha foleni kubwa katika barabara hilo inayosifika kwa kona zake katika mlima huo.
Kwa mujibu wa mashuhuda, chanzo cha gari hilo kutumbukia mtaroni ni kufuatia kupata hitilafu na hatimaye uamuzi wa kuliegesha kando ukafanyika kisha abiria wote wakashuka ili kusubiri marekebisho hayo. 
Haikupita muda mrefu baada ya abiria kushuka gari lilikosa balansi, likaanza kurudi kinyumenyume na kisha kuingia mtaroni. 

Rais Kikwete amteua CAG mpya, ni Prof Mussa Juma Assad


cag_clip 
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Mussa Juma Assad kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Taarifa iliyotolewa, Jumatatu, Desemba Mosi, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, inasema kuwa uteuzi wa Bwana Assad ulianza Novemba 5, mwaka huu, 2014.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa Bwana Assad ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 2, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.
Kabla ya uteuzi wake, Bwana Assad alikuwa Profesa Mshiriki, Idara ya Uhasibu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi ya Bwana Ludovick Utouh ambaye amestaafu kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma.
Profesa Assad ni msomi, mwenye weledi, ujuzi na uzoefu mkubwa wa uhasibu na udhibiti wa fedha ambaye ana Shahada ya Uzamivu wa Uhasibu (PHD in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Southampton, Uingereza mwaka 2001 na Shahada ya Uzamivu katika Udhibiti wa Fedha (MA in Financial Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City, Jamhuri ya Ireland mwaka 1991.Kusoma zaidi bofya
Profesa Assad pia ana Stashahada ya Kitaaluma ya Uhasibu (Professional Diploma in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City mwaka 1990 na Shahada ya Biashara (Bachelor of Commerce) ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam mwaka 1988.
Pamoja na uzoefu wa kitaaluma, Profesa Assad anao uzoefu mkubwa katika eneo la uhasibu na ukaguzi. Alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) kwa miaka saba (2007 – 2014); ni Rais na Mjumbe wa Chama cha Wahasibu Afrika (Pan African Federation of Accountants) tangu mwaka 2012; na ni mjumbe wa Bodi kadhaa za Wakurugenzi nchini Tanzania.
Katika kumteua Profesa Assad kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Rais anayo imani kubwa kuwa elimu, weledi, ujuzi na uzoefu ambao Profesa Assad anao utamwezesha kutekeleza vema majukumu ya nafasi hiyo muhimu sana katika utawala bora wa nchi yetu.

Irene Uwoya, JB, Richie kupamba uzinduzi Family Singers J'mosi

WASANII nyota wa filamu nchini, Irene Uwoya, Jacob Stephen 'JB' na Single Mtambalike 'Richie' wanatarajiwa kupamba uzinduzi wa albamu ya pili ya Kikundi cha Waimbaji wa Injili cha 'Family Singers' utakaofanyika siku ya Jumamosi.
Uzinduzi huo wa albamu hiyo iitwayo 'Usilie' utafanyika kwenye ukumbi wa PTA-Sabasaba, Temeke Dar es Salaam na utapambwa na shushuli za upimaji bure wa afya kwa wananchi mbalimbali sambamba na burudani ya muziki toka kwa waimbaji mbalimbali wa muziki wa Injili na wasanii hao wa Bongo Movie.
Mkurugenzi wa kikundi hicho kilichopo chini ya Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA), Daniel Misheto Jr, aliiambia MICHARAZO kuwa wasanii wa Bongo Movies wamethibitisha kuwapiga tafu katika uzinduzi huo ambao mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Misheto alisema kuwa maandalizi kuelekea uzinduzi huo yanaendelea vema na idadi wa watakaosindikiza ikizidi kuongezeka na kudai mbali na wasanii wa Bongo Movies, pia wazee wa Buguruni nao wamethibitisha kuwepo katika uzinduzi huo ambao utaenda sambamba na zoezi la kuwapima afya na kuwatibia watu bure kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 6 mchana kabla ya huduma ya uimbaji kushika kasi.
Baadhi ya waimbaji Injili watakaosindikiza onyesho hilo ni Leah Moody, mshindi wa BSS, Vocapella, Martha Mwaipaja, AIC (T) Vijana Chang'ombe, Accasia Singers, Papson Mistaki wa Kenya na Frank Hume kutoka Marekani.

Kun Aguero anyakua tuzo ya Mashabiki 2014

Sergio Aguero picked up Player of the Year award with girlfriend Karina Tejeda
Sergio Aguero akiwa na tuzo yake kwa pamoja na mpenzi wake, Karina Tejeda
STRIKA nyota wa klabu ya Manchester City, Sergio 'kun' Aguero ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa Shirikisho la Mashabiki jana.
Mpachika mabao huyo wa mabingwa wa Ligi Kuu ya England na washindi wa pili wa Kombe la Dunia, Argentina, alishinda tuzo hiyo katika hoteli ya St Pancras Renaissance mjini London, England.
Nahodha wa Manchester United na England, Wayne Rooney na winga wa Real Madrid na Wales, Gareth Bale pia walikuwemo kwenye kinyang'anyiro cha tuzo hiyo sambamba na nyota wengine wa Ligi Kuu England, Thibaut Courtois, Branislav Ivanovic, Vincent Kompany, Pablo Zabaleta, Angel di Maria, Cesc Fabregas, Eden Hazard, Mesut Ozil, Yaya Toure, Sergio Aguero na Diego Costa.

BASATA yampongeza Diamond kwa kutwaa tuzo 3 za CHOMVA 2014

http://api.ning.com/files/Ct4BimYh7MjWwN3GDSYmz7wODwHWnN6B6NKofKrjboEN10YJnN3x6S3mquF1uzO9XyFNuVQVglyDwmavxGdZK*GQlLJBilOZ/04diamondtuzo4.jpgBARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) kama msimamizi na mratibu wa sekta ya Sanaa nchini linapenda kutoa pongezi za dhati kwa Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nassib Abdul maarufu kama Diamond kwa kushinda tuzo tatu kwa mkupuo za CHOMVA zinazoendeshwa na kituo maarufu cha luninga cha Channel 0 chenye makao makuu yake Afrika Kusini.
Tuzo alizoshinda Diamond ni pamoja na Most Gifted East African Artist, Most Gifted Afro Pop video na ile ya Most Gifted New Comer. 
Kushinda kwa Diamond katika tuzo hizo kubwa barani Afrika na kuwashinda wasanii wengine wenye ‘majina makubwa’ ni ishara kwamba muziki wetu unakubalika ndani na 
Baraza linatoa wito kwa wasanii na wadau wote wa muziki kuzidisha ubunifu, bidii na weledi katika kazi wanazozifanya ili wasanii wengi zaidi waweze kuchomoza katika tuzo na majukwaa mbalimbali ya kimataifa kwa lengo la kujitangaza na kukuza soko la kazi zao kimataifa.
Aidha, Baraza linaendelea kuwakumbusha na kuwasisitiza wadau wa muziki na Sanaa kwa ujumla hususan wakuzaji Sanaa (mapromota) kuendelea kujenga mazingira rafiki kwa wasanii wetu kufanya kazi kwa ubora na weledi lakini pia kwa upendo na furaha ili kujenga daraja zuri kwa wasanii wengi zaidi kung’ara kwenye ngazi za kimataifa.
Ni imani ya Baraza kwamba, ushindi huu wa kihistoria wa Diamond utakuwa chachu kwa wadau wote wa Sanaa nchini hususan wasanii katika kujituma na kuhakikisha hawaridhiki na mafanikio waliyonayo. 
Ni matumaini ya Baraza kwamba wasanii na wadau wote wa Sanaa wataendelea kutambua umuhimu wa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji sekta sambamba na kutambuliwa na Serikali.
Sanaa ni kazi, tuipende na kuithamini

TPBO-Limited yafichua siri ya mabondia wa Tz kupigwa ughaibuni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEix_ikFUVQYo2XFuYXtUqvjRzHYr5VnfbR27zD1v1mQO9vDKcyGTWjAyDe3E9fbTST0rnQCVDupyg8mHUY0b4E6Sd-_s4zemsQTsSDaMD7Fz_DjHVmpMzcqxBTIkpxN200Ne6-sNZjJDms7/s1600/IMG_0009.JPG
Rais wa TPBO-Ltd, Yasin 'Ustaadh' Abdallah
RAIS wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO-Ltd) Yasin Abdallah 'Ustaadh' amefichua siri za mabondia wengi wa Tanzania kushindwa kufanya vema kwenye mapambano yao ya kimataifa nje ya Tanzania, akidai inachangiwa na maandalizi duni na pia kutohimili kucheza mbele ya umati mkubwa wa watazamaji.
Ustaadh, alisema siyo kweli kama mabondia wa Tanzania wanapigwa na kupoteza michezo yao nje ya nchi kwa sababu ya hujuma, bali ni kutokana na kutojiandaa vema kwa utamaduni uliipo miongoni mwa mabondia wengi nchini kutotambua kama ngumi za kulipwa ni biashara zinazohitaji wahusika kuzingatia miiko, maadili na nidhamu ya hali ya juu kufikia mafanikio ya wenzao wanaotamba duniani.
"Siyo kama wanapigwa kwa hila, wengi huwa hawafanyi maandalizi mazuri, hukurupuka tu kwenda nje kupigana na mwishowe kutia aibu imefika wakati sasa mabondia wakazinduka na kujitambua," alisema Ustaadh.
Alitoa maoni yake kufuatia bondia Fadhili Majiha kupigwa kwa KO ya raundi ya 3 kwenye pambano la utangulizi wakati Manny Pacquiao akitetea taji lake la WBO mbele ya Chris Algieri, ambapo Ustaadh alisema inawezekana kucheza mbele ya umati mkubwa na kukosa kwake maandalizi yamechangia kupata matokeo mabaya kulinganisha na yale aliyopata Russia alipoenda kupigwa kwa pointi.
Kwa muda mrefu mabondia wa Tanzania wamekuwa wakipata matokeo mabaya kwenye mapambano yao nje ya Tanzania, kiasi cha kuzushiwa kuwa huenda ni 'dili' zinazofanywa na baadhi ya mawakala wa mabondia wanaotoa ofa ya Watanzania kwenda kupigana katika nchi zao ili kulinda na kuboresha rekodi  za mabondia wanaowasimamia, wakishirikiana na viongozi wa mchezo huo nchini.
Hata hivyo mara kadhaa viongozi wa vyama vya ngumi za kulipwa wamekuwa wakikanusha kuwepo kwa suala hilo na kusisitiza kuwa mabondia wa Tanzania wanapigwa kwa sababu ya maandalizi ya zima moto na kutokuwa na mameneja wa kuwasimamia.

Yanga yampa mkataba wa mwaka mmoja Mbrazil Emerson

EMERSON AKISAINI MKATABA WA MWAKA MMOJA KUICHEZEA YANGA MBELE YA MTAALAMU WA MAMBO YA IT NA MSEMAJI WA YANGA, BARAKA KIZUGUTO.
KLABU ya soka ya Yanga imemsainisha mkataba wa mwaka mmoja kiungo mkabaji mpya kutokla Brazil,  Emerson De Oliveira Neves Roque.
Tukio la usainiwaji wa mkataba huo wa mwaka mmoja lilifanyika jana baada ya kiungo huyo kuliridhisha benchi la ufundi la klabu hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotangazwa na mtandaop wa klabu ya Yanga benchi la ufundi liliridhika na uwezo wake,na mchezaji mwenyewe kufikia makubaliano hayo ya kuwatumikia watoto wa Jangwani.

Baada ya kufanya mazoezi kwa siku nne mfululizo chini ya makocha Marcio Maximo, Leonardo Neiva na makocha wazawa Salavatory Edward, Shadrack Nsajigwa kwa pamoja wameridhiswa na uwezo wake na kuomba apewe kandarasi la kuitumikia klabu ya Young Africans.
Emerson aliyekua akichezea katika timu ya Bonsucesso iliyopo daraja la pili kwenye jimbo la Rio de Janeiro anachukua nafasi ya mshambuliaji Geilson Santos "Jaja" ambaye ameshindwa kureje nchini kutokana na matatizo ya kifamilia na kuomba klabu ya Young Africans imuache.
Kocha wa Young Africans Marcio Maximo amesema wamerizishwa na uwezo na kiungo mkabaji Emerson na kusema ataisaidia timu katika michuano mbali mbali ya Ligi na Kimataifa.
Ujio wa Emerson unafanya klabu ya Young Africans kufikisha jumla ya wachezaji watano wa kimataifa, wengine wakiwa ni Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima, Hamis Kizza na Andrey Coutinho.

Klabu za Simba, Yanga zapigwa vijembe

http://ehabari.com/wp-content/uploads/2014/12/7a19Simba-Yanga.jpgUONGOZI wa Ruvu Shooting umezipiga 'madogo' klabu za Simba na Yanga kwamba zimekuwa mahiri katika kuviza vipaji vya soka vya wachezaji nchini kutokana na kuwasajili kwa papara kila wanapong'ara katika timu nyingine, kisha kushindwa kuwatumia.
Aidha uongozi huo umewazindua wachezaji vijana kuwa makini na kuzikimbilia klabu hizo hata kama ni kweli zina masilahi makubwa miongoni mwa klabu za soka za Afrika Mashariki, lakini ni vema pia wakaangalia vipaji vyao.
Akizungumza na MICHARAZO, msemaji wa Ruvu Masau Bwire, alisema Simba na Yanga ni klabu za 'kuviza' vipaji ndiyo maana asilimia kubwa ya wachezaji waliokuwa nyota katika klabu zao wanaposajiliwa na klabu hizo hufifia na hata kuzimika kama baadhi yao ambao licha ya kusajiliwa kwa mamilioni ya fedha wamekuwa watu wa kukaa benchi.
"Ni lazima wachezaji wanaozikimbilia Simba na Yanga wajiulize mara mbili, ni kweli zina mvuto wa kifedha lakini vipaji vyao ni muhimu, kuna maana gani kusajiliwa kwa mamilioni ya fedha kisha ukaishia kukaa benchi na mwishowe kutemwa ukiwa haina thamani," alihoji.
Bwire alisema wapo wachezaji kadhaa waliokuwa waking'ara nje ya Simba na Yanga, lakini walipotua katika timu hizo wamekuwa hawana maana yoyote wakiishia kuwa wasugua benchi kisha kuachwa kwa kudaiwa kushuka viwango na wanaposajiliwa na timu nyingine zinazowapa nafasi ya kucheza hurejea kwenye viwango vyao na klabu hizo kubwa kuwavizia tena kutaka kuwasajili.
Baadhi ya wachezaji wamekuwa wakizikimbilia Simba na Yanga kwa sababu ya usajili wa donge nono, lakini mrundikano wa wachezaji wengi mastaa umewafanya kuishia kukalia benchi na kushuka viwango kabla ya kutemwa, kitu kinachodaiwa kinachangia kudidimiza soka la Tanzania.

RT kuamua hatma yao Desemba 6

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgF-lOhMYrCVlKenUdlFeY7QpbkcfwIJuaSC7FRgOrlXV1EJeCdVq0X8PHDRiN_zLwblmyeveKZjHa8mlDA2bS2ynAPJPiO9n0eTW0O5zXJ3aS4QS-pNbzMwCxd3_BYkbSpnr_Oyf4Eadk/s1600/IMG_9856.JPG
Katibu Mkuu wa RT, Suleiman Nyambui
SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT) linatarajiwa kufanya kikao cha Kamati ya Utendaji ambacho kitapitia na kujadili maoni ya mikoa wanachama wao kwa ajili ya Rasimu ya Katiba Mpya ya shirikisho hilo.
Katibu Mkuu wa RT, Suleiman Nyambui aliiambia MICHARAZO kuwa, awali kikao hicho kilikuwa kifanyike juzi Jumapili ila kilisogezwa mbele kwa sababu ya kutoa fursa kwa mikoa kuwasilisha maoni yao.
Nyambui alisema ni mikoa saba tu ambayo ilikuwa imewasilisha maoni yao tofauti na idadi ya mikoa wanachama wa shirikisho hilo ambayo ni 25.
"Kikao cha Kamati ya Utendaji cha RT kilichokuwa kifanyika Novemba 30 kimesogezwa mbele hadi Desemba 6 na ajenda zake zitakuwa ni kupitia na kujadili maoni ya mikoa juu ya Rasimu ya Katiba Mpya," alisema Nyambui.
Nyambui alisema ajenda nyingine ni kujadili maendeleo ya jumla ya mchezo huo na namna ya kuukwamua ili kuweza kufanya vema kwenye mashindano ya kimataifa yaliyopo mbele yao. Mikoa iliyowasilisha maoni yao mpaka sasa ni Dar es Salaam, Arusha, Mara, Mbeya, Majeshi, Tanga na Morogoro.

Mgambia wa Simba kujaribiwa wiki mbili kabla ya mkataba

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/12/mboob.jpg
MSHAMBULIAJI mpya aliyetua Simba, Omary Mboob kutoka nchini Gambia, amepewa wiki mbili kwa ajili ya kufanya majaribio na kikosi hicho na kama akifuzu atasajiliwa kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo kwenye mechi zijazo za Ligi Kuu Bara.
Mboob amewasili nchini juzi kimya kimya na jana aliripoti mazoezi katika Uwanja wa Sigara, Chang'ombe jijini Dar es Salaam na kuanza mazoezi rasmi.
Akizungumza jana, Kocha Mkuu wa Simba, Mzambia Patrick Phiri, alisema wamempa wiki mbili mchezaji huyo kutokana na kwamba hajawahi kumuona katika mechi zake alizowahi kucheza.
"Tumempa wiki mbili za mazoezi ili tumuone kama anafaa au hafai, akifuzu atasajiliwa," alisema Phiri.
Alisema mshambuliaji huyo ni tofauti na Mganda Dan Sserunkuma ambaye atasajiliwa moja kwa moja kutokana na kwamba wameshawahi kumuona akiwa na timu yake katika baadhi ya mechi za kimataifa na nchini yake.
Phiri alisema baada ya wiki mbili watajua kama kiwango cha mchezaji huyo kinaweza kuisaidia timu kuanzia mzunguko wa nane wa Ligi Kuu unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 26, mwaka huu.
Kwa upande wa mazoezi kwa ujumla, alisema yanaendelea vizuri kutokana na wachezaji kujifua kwa bidii kuelekea mechi ya 'Nani Mtani Jembe 2' dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga Desemba 13, mwaka huu.

Ommy Lax achekelea video yake kupokewa vema

MSANII anayekuja kwa kasi nchini, Iman Omari 'Ommy Lax' amesema amefurahi namna mashabiki wa muziki walivyoipokea video yake mpya ya wimbo uitwao 'Mimi na Wewe' ambao inaendelea kutamba kwa sasa katika vituo mbalimbali vya runinga.
Ommy anasema jambo hilo limemtia nguvu na kujipanga kuandaa kazi nyingine mpya ili kuzidi kuwapa burudani mashabiki wake, sambamba na kulitangaza jina lake.
Video hiyo mpya ya Ommy Lax imetengenezwa na Zolla D, na 'audio' yake imetengenezwa katika studio za Bokaz Entertainment chini ya Man DVD.
Kabla ya video hiyo msanii huyo aliyejitumbukiza kwenye sanaa hiyo mwaka 2006 alitamba na video za nyimbo za 'Kioo Changu' alioimba na Matonya na 'Wapotezee' aliyomshikisha PNC.

Dokii asisitiza, 'Sijam-beep mtu Uchaguzi Mkuu 2015'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjnoMKLupYtlqQbGVaMutBdYjiLDa_mTiB1b27_5dckqSFFO_3yEs6iO6nO9RgKk6rh8A8pH149EjrqLLJhL5hoLNlSUmoNeQjV6qnkBsvva7m50eRarf7ZV0SGQER1CqbvXFwyBQ0Y-tE/s1600/dokii%2525202%255B1%255D.JPG

MWANAMITINDO na muigizaji mahiri wa filamu nchini, Ummy Wenceslaud 'Dokii' amesema kauli yake ya kutaka kuwania ubunge siyo ya utani na kwamba ‘hajambeep’ yeyote bali amedhamiria kweli 2015 kuingia bungeni.
Akizungumza na MICHARAZO, Dokii alisema tofauti na wasanii wenzake ambao wamekuwa wakitangaza nia ya kujitosa kwenye siasa kisha kuishia njiani yeye hatanii na kwamba uchaguzi ujao atakuwa miongoni mwa wanawake watakaowania ubunge jimboni.
"Sitanii na wala ‘simbeep’ mtu, nimenuia kabisa kujitosa kwenye mbio za uchaguzi wa 2015, nautaka ubunge wa Kilosa na ninaamini ninaweza nikipewa nafasi na chama changu cha CCM," alisema Dokii.
Dokii ambaye pia ni muimbaji muziki, alitangaza nia yake hiyo wiki mbili zilizopita, lakini baadhi ya mashabiki wake wanadhani ni kauli kama zilizowahi kutolewa na wasanii mbalimbali akiwamo JB, King Majuto, Steve Nyerere, Shilole na wengine lakini wasioaminika kama watajitosa kwenye uchaguzi huo.
Katika bunge la sasa linaloelekea ukingoni wapo wasanii kadhaa walitwaa viti vya ubunge akiwamo mmoja wa waasisi wa Bongofleva nchini, Joseph Mbilinyi 'Sugu' ambaye ni Mbunge wa Mbeya-Chadema, huku muimbaji Vick Kamata akiwa Mbunge-CCM Viti Maalum.

Marehemu Senzo Meyiwa atinga Tano Bora tuzo za CAF 2014

http://www.timeslive.co.za/sport/soccer/2014/10/27/senzo-meyiwa6/ALTERNATES/crop_630x400/Senzo+MeyiwaALIYEKUWA nahodha na kipa tegemeo wa timu ya taifa ya Afrika Kusini 'Bafana Bafana' na klabu ya Orlando Pirates, Senzo Meyiwa aliyeuwawa na majambazi mwezi uliopita ni miongoni mwa nyota waliotinga Tano Bora ya Tuzo ya Mwanasoka Bora Anayecheza Soka barani Afrika.
Kipa huyo aliyeuwawa kwa kupigwa risasi akiwa kwa hawara yake, ametangazwa katika orodha hiyo ya mwisho iliyotolewa na Shirikisho la Soka Afrika, CAF.
Wengine wanaochuana na marehemu huyo ni  Akram Djahnit, El Hedi Belamieri wote wa Algeria na E.S. Setif, Fakhreddine Ben Youssef wa Tunisia na C.S. Sfaxien na Firmin Mubele Ndombe wa DRC na AS Vita.

Yaya Toure aongoza orodha ya mwisho Mwanasoka Bora Afrika 2014

http://www.football-marketing.com/wp-content/uploads/2012/01/PUMA-Yaya-Toure.jpg
KIUNGO nyota wa Manchester City na timu ya taifa ya Ivory Coast, Yaya Toure ameongoza orodha ya wachezaji watano walioingia Fainali za kuwania Tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika 2014.
Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limetoa orodha ya mwisho ya wachezaji hao watano wanaowania tuzo hiyo ambayo awali ilikuwa na wachezaji 25.
Mtetezi wa tuzo hiyo anayetarajiwa kutwaa kwa marta ya nne anachuana na Wanigeria wawili, Mghana mmoja na Mgabon.
Orodha hiyo inaonyesha kuwa Toure anachuana na  Vincent Enyeama na Ahmed Musa wote wa Nigeria, Mghana Asamoah Gyan na Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon.
Toure alitwaa tuzo hiyo miaka mitatu iliyopita na kama akifanikiwa kuitwaa tena msimu huu, atakuwa amefikia rekodi ya Mcameroon Samuel Eto, ambaye ameitwaa mara nne.
Mshindi atatangazwa jijini Lagos, Nigeria Alhamis Januari 8, 2015

Kocha Manchester Utd akerwa ratiba kuelekea X-mass Mwaka Mpya

http://www.nerdoholic.com/wp-content/uploads/2014/07/Van-Gaalmoyes1.jpg
Kocha Luis Van Gaal
RATIBA ya Ligi Kuu na michuano mingine nchini England kuelekea Sikukuu ya Krismasi inaonyesha kumkera Kocha wa Manchester United, Louis Van Gaal.
KOcha huyo ameonyesha kutofurahishwa na ratiba ya Ligi Kuu itakavyokuwa katika kipindi cha sikukuu hiyo na ile ya Mwaka mpya.
Kuna uwezekano mkubwa United ikacheza mechi nne ndani ya siku tisa katika kipindi cha kati ya Desemba 29 mpaka Januari 3 kutegemeana na ratiba ya Kombe la FA itakavyokuwa. 
Ratiba katika Ligi Kuu inaonyesha kuwa watakuwa wenyeji wa Newcastle United Desemba 26, kabla ya kucheza wa ugenini dhidi ya tottenham Hotspurs siku mbili baadae na siku ya mwaka mpya watapepetana na Stoke City. 
Akihojiwa Van Gaal amesema ana mke, watoto na wajukuu na hawezi kuwaona katika kipindi cha krismasi lakini alitaka kufanya kazi katika Ligi Kuu hivyo anapaswa kuzoea hali iliyopo. 
Van Gaal amesema hafurahishwi na suala hilo lakini hawezi kubadilisha na hadhani kama ni jambo zuri kwa wachezaji pia.

Stars Maboresho yaingia kambini Bulyanhulu kuiwinda Burundi

https://silajilimbu.files.wordpress.com/2014/10/savedpicture-2014103164047.jpghttp://tff.or.tz/wp-content/uploads/2014/11/Star-U-23.jpgKIKOSI cha pili cha timu ya taifa, maarufu kama Taifa Stars Maboresho kimeingia kambini Bulyanhulu mkoani Shinyanga kujiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi itakayochezwa Desemba 9 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Ikiwa chini ya Kocha Mart Nooij, Stars Maboresho itapiga kambi mkoani humo hadi Desemba 6 mwaka huu ambapo itarejea jijini Dar es Salaam tayari kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa. Wachezaji walioingia kambini ni Abubakar Ally (Coastal Union), Abubakar Ally Mohamed (White Bird), Aishi Manula (Azam), Andrew Vicent (Mtibwa Sugar), Atupele Green (Kagera Sugar), Edward Charles (Yanga) na Emmanuel Semwanda (African Lyon).
Gadiel Michael (Azam), Hashim Magoma (Stand United), Hassan Banda (Simba), Hassan Mwasapili (Mbeya City), Joram Mgeveke (Simba), Kassim Mohamed Simbaulanga (African Lyon), Kelvin Friday (Azam) na Makarani Ally (Mtibwa Sugar).
Miraji Adam (Simba), Mohamed Hussein (Simba), Muzamir Ally (Mtibwa Sugar), Omari Nyenje (Ndanda), Pato Ngonyani (Yanga), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Said Hamisi (Simba), Salim Hassan Mbonde (Mtibwa Sugar) na Shiza Ramadhan (Mtibwa Sugar).
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linaishukuru kampuni ya kuchimba madini ya Acacia Mining PLC (zamani African Barrick Gold PLC) kwa kufadhili kambi ya Stars kupitia mgodi wa Bulyanhulu.

Yacine Brahimi ndiye Mwanasoka Bora wa Afrika wa BBC 2014

 
http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Yacine+Brahimi+Algeria+v+Armenia+International+DPgMxDsahSgl.jpgNYOTA wa Algeria anayeichezea Porto ya Ureno, Yacine Brahimi ndiye mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika 2014.
Brahimi alitangazwa kushinda tuzo hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na Yaya Toure wa Manchester City jana.
Tuzo hizo uandaliwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza,BBC na Brahimi, 24, anakuwa mchezaji wa kwanza kutoka Algeria kushinda tuzo hiyo ambayo hupigiwa kura na mashabiki kutoka pande mbalimbali za bara la Afrika. 
Akihojiwa mara baada ya kukabidhiwa tuzo yake Brahimi amesema ni heshima kubwa kwake kushinda tuzo hiyo muhimu na anawashukuru watu wote nchini kwake na popote pale ambao walimpigia kura. 
Brahimi alikuwa akichuana na Yaya Toure na Gervinho kutoka Ivory Coast, Pierre-Emerick Aubameyang kutoka Gabon na Vincent Enyeama kutoka Nigeria.

Ronaldo, Messi, Neuer wapambanishwa Ballon d'Or 2014

 
SHIRIKISHO la Soka Duniani, FIFA limetangaza orodha ya wachezaji watatu watakaogombea tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Dunia, Ballon d’Or. Wachezaji hao waliopenya katika mchujo wa wachezaji 23 ni mtetezi wa tuzo hiyo nyota wa Ureno na klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo, Lionel Messi wa Argentina na klabu ya Barcelona na Manuel Neuer wa Ujerumani na timu ya Bayern Munich. Sherehe za utoaji tuzo inatarajiwa kufanyika Januari 12 mwakani huku Ronaldo akiwa ndio mshindi wa mwaka jana. Kwa upande wa wanawake walioteuliwa kugombea tuzo hiyo ni pamoja na Nadine Kessler wa Ujerumani, Marta wa Brazil na Abby Wambach kutoka Marekani. Kwa upande wa makocha walioteuliwa kugombea tuzo ni pamoja na Carlo Ancelotti wa Real Madrid, Joachim Loew aliyeiwezesha Ujerumani kunyakuwa Kombe la Dunia na kocha wa Atletico Madrid Diego Simeone.

Monday, December 1, 2014

Inter Milan yapigwa 4-2 na Roma, Gervinho atupia moja

http://www.iberita.com/wp-content/uploads/2014/11/Jadwal-Liga-Italia-2014-Terbaru-Pekan-Ini-30-November-dan-1-2-Desember-2014.jpg
AS Roma wakishangilia moja ya mabao yao yaliyoizamisha Inter Milan
KLABU ya Inter Milan usiku wa jana imeshindwa kufurukuta nyumbani kwa AS Roma baada ya kubanduliwa mabao 4-2 katika pambano kali la Ligi Kuu ya Italia, Serie A.
As Roma iliwakaribisha wapinzani wao kwa bao la dakika ya 21 kupitia kwa Gervinho kabla wa wageni hao kusawazisha kupitia kwa Ranocchia dakika ya 36.
WWEnyeji waliongeza bao la pili dakik achache baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kupitia kwa Holebas kabla ya funga nikufunge kuendelea kwa Inter Milan kurejesha bao hilo kwa mkwaju wa Osvaldo dakika ya 57.
Magoli mawili ya Pjanic ya dakika ya 60 na 90 yaliisaidia wenyeji kuibuka na ushindi huo na kuendelea kuwafukuza Juventus waliopo kileleni wakitofautiana pointi tatu, Juve wakiwa na 34 na Roma 31 zote zikiwa zimecheza mechi 13kila moja.

Macho vya Vishal, Pingu videoni, audio njiani

Pingu na Vishali katika pozi

Vishali
BAADA ya kuachia video ya 'Macho' inayoendelea kutamba hewani, msanii Vishal Milanzi 'Vishal' yupo katika maandalizi ya kutengeneza kazi nyingine mpya atakayoanza kuirekodi mara baada ya kurusha hewani 'audio' ya wimbo huo wa Macho alioimba na mzoefu Pingu.
Akizungumza na MICHARAZO, Vishal alisema alitanguliza video hewani na wiki ijayo ndiyo ataachia 'audio' kabla ya kuanza mipango ya kurekodi kazi nyingine mapya akimshirikisha pia Pingu mmoja wa wasanii wa muda mrefu nchini anayetamba na nyimbo mbalimbali.
"Niliamua kutanguliza video hewani, kabla ya 'audio' yake na ninashukuru mashabiki wameikubali kazi na imenitia moyo wa kuanza kutengeneza kazi nyingine mpya. Kazi hizo zitafuata baada ya 'audio' ya 'Macho' kutoka," alisema Vishal.
Msanii huyo alidokeza kuwa wimbo huo atakaouachia hewani wiki ijayo umerekodiwa studio za Triple One Records kwa Kizo One na video yake imetengenezwa Rubby Videos na ‘Audio' na zitatengenezwa katika studio nyingine kwa lengo la kuipa vionjo tofauti.

Barcelona yaipumia Real Madrid, Messi apigwa

Otamendi falls to the floor in theatrical fashion, but Neymar had forcefully moved his head towards the Valencia man's jaw
Kulaaa! Neymar akimlamba kichwa beki wa Valencia aliyemchezea kitemi kabla
Players of both Valencia and Barcelona then got involved in a heated discussion after the incident
Mzozo baina ya wachezaji wa Valencia na Barcelona
Messi looks to get Barcelona on the attack during the second half of their clash with ValenciaKLABU ya Barcelona imezidi kuwapumulia wapinzani wao Real Madrid baada ya usiku wa jana kupata ushindi mwembamba ugenini dhidi ya Valencia huku nyota wake Lionel Messi akipigwa na chupa uwanjani.
Barcelona walioivaa Valencia katika uwanja wa Mestalla walipata ushindi huo kupitia bao la 'jioni' lililofungwa na Sergio Busquets dakika ya 90, kabla ya Lionel Messi kupigwa na chupa. Katika pambano hilo lilishuhudiwa undava ukitembezwa uwanjani kwatai Neymar alipompiga kichwa Nicolas Otamendi baada ya beki huyo kuanza kumcheza ‘kitemi’ Mbrazil huyo. Otamendi alimchezea kibabe Neymar kwenye eneo la hatari, lakini alipokwenda kumuinamia kumuomba msamaha, alilambwa kichwa ‘kishikaji’ kabla ya kuibuka mzozo uliohusisha wachezaji wote.
Hata hivyo Neymar hakuchukuliwa hatua zozote na refa wa pambano hilo, David Fernandez.
Ushindi huo umeifanya Barcelona kufikisha pointi 31, mbili nyuma ya Real Madrid wanaoongoza msimamo ambao walishinda mabao 2-1 ugenini siku ya Jumamosi dhidi ya Malaga.

Mkurugenzi Zugo Sports ahimiza wanawake kujifunza Martial Arts

Zuwena Idd Kipingu akionyesha umahiri kwa kunyanyua chuma katika gym yake
WANAWAKE na wasichana wamehimiza kujenga utamaduni ya kupenda kujifunza na kucheza michezo ya mapigano kwa lengo la kuwasaidia kuwaepusha na matukio la kudhalilishwa mitaani.
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Klabu ya Michezo ya Zugo, Zuwena Idd Kipingu, alipozungumza na blogu hii na kudai ili kuepukana na kubakwa au kuporwa na unyanyasaji mwingine wasichana na wanawake wanapaswa kujifunza na kucheza michezo ya mapigano (Martial Arts).
Zuwena alisema michezo hiyo mbali na kuwaweka kuwa fiti pia itawasaidia kwa ulinzi wao binafsi pale wanapovamiwa au kukumbana na wahalifu mahali popote.
"Wanawake na wasichana wamekuwa wakifanyiwa uonevu na baadhi ya wanajamii kwa kuwaona ni wanyonge na legelege ni fursa yao kujifunza michezo kama ya karate, Judo, Kung-fu au ngumi ili kujiweka fiti na kukomesha unyanyasaji dhidi yao," alisema.
Mkurugenzi huyo ambaye pia ni Mwakilishi wa Wanawake, Maendeleo ya Vijana na Ajira kwa Wachezaji wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT) alisema klabu yake ipo tayari kuwapa mafunzo wanawake wanaohitaji kufanya hivyo.
"Klabu yangu ya Zugo Sports, inafundisha michezo mbalimbali, lakini wengi wao ni wanaume, nilidhani ni wakati wanawake na wasichana wakachangamka ili kujisaidia kwa mambo mengi."
Alisema mbali na kupata ulinzi binafsi katika matukio madogo madogo, lakini pia michezo itawafanya wawe na afya njema pamoja na kujitengenezea mazingira mazuri ya ajira.
Mwanadada huyo mwenye mkanda mweusi katika mchezo wa Taekwondo na aliyewahi kung'ara kwenye michezo ya kunyanyua vitu vizito na ngumi, alisema wanawake wasijiweke nyuma.
"Wasijiweke nyuma au kutishwa na madai kwamba ukicheza michezo kama hiyo hataweza kuzaa, huo ni uongo mimi nimeanza michezo hii mwaka 1980 na nina watoto saba kwa sasa," alisema.
Aliongeza kuwa, michezo ni afya, hivyo ni wajibu hata kwa wazazi kuwazoesha watoto wao kuicheza ili kuiweka miili yao salama na kuepukana na maradhi madogo madogo.

Sunday, November 30, 2014

Juventus yazidi kujichumbia kileleni Italia

Juventus celebrateAndrea PirloMABINGWA watetezi wa Serie A ya nchini Italia, Juventus, imezidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo baada ya usiku huu kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Torino.
Katika pambano hilo lililochezwa kwenye mjini wa Turin, wenyeji walijikuta wakimaliza mchezo huo wakiwa pungufu baada ya beki waoStephan Lichtsteiner kulimwa kadi nyekundu kutokana na kupewa kadi ya pili ya njano.
Wenyeji hao walitangulia kuandika bao mapema kupitia kwa Arturo Vidal kwa mkwaju wa penati iliyotolewa na mwamuzi dakika ya 15 kabla ya wageni wao kurejesha bao hilo dakika saba baadae kupitia kwa Bruno Peres.
Wakati wengi wakidhani matokeo yangeisha kwa sare ya 1-1, kiungo mkongwe  Andrea Pirlo aliifungia Juventus bao muhimu la ushindi dakika za lala salama na kuifanya 'Kibibi' cha Turin, kufikisha jumla ya pointi 34 kutokana na michezo 13.
MUda mchache ujao wanaoshikilia nafasi ya pili AS Roma wenye pointi 28 watakuwa nyumbani kuwakaribisha Inter Milan katika pambano linalotarajiwa kuwa kali.