STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 6, 2014

Shigongo afafanua madhara ya Ugonjwa wa Ini


Shigongo akizungumza kwa masikitiko jinsi watu wengi walivyo kwenye hatari ya kufa kwa ugonjwa wa ini.

…Akiwa na jopo la madaktari. Kushoto ni Dk. Mtebe Majigo, Mganga Mkuu wa Amana, Meshack Shing'wela (wa pili kulia) na Daktari Kiongozi Andrew Method.

Ndeonasio Towo kutoka Damu Salama akielezea umuhimu wa wananchi kupima damu kubaini maradhi mbalimbali bila kusahau virusi vya homa ya ini.
Mwakilishi kutoka SD Tanzania ambao ni wadau wa ugonjwa huo, Phillip Sawe, akielezea umuhimu wa kupima mapema ugonjwa huo kabla mwili haujashambuliwa.
Daktari Kiongozi wa Hospitali ya Amana, Andrew Method (kulia) akisistiza jambo.
Mapaparazi kazini.
Shigongo akimueleza jambo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana.
Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdalah Mrisho (kushoto) na Mwakilishi kutoka Sanofa, Edwin Kisimbo, wakifuatilia kwa makini kilichokuwa kikiendelea.
Dk. Majigo (wa pili kulia) akielezea ugonjwa huo unavyoambukiza kwa njia ambazo huambukiza Ukimwi.
Meshack Shing'wela akifafanua jambo.
…Akimshukuru Shigongo kwa kuanzisha kampeni za kutokomeza ugonjwa huo.
MKURUGENZI wa Kampuni ya Global Publishers Ltd, Eric Shigongo, na wadau mbalimbali wa afya leo walizungumzia madhara ya ugonjwa hatari wa homa ya ini kwenye mkutano na wanahabari uliofanyika Hospitali ya Mkoa wa Ilala, Amana Jijini Dar.
Miongoni mwa wadau waliokuwa kwenye mkutano huyo ni madaktari mbalimbali, Sanofa ambao huhusika na vipimo vya ugonjwa huo, Damu Salama ambao huhusika na upimaji wa damu na SD Tanzania.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL)

Ujerumani, England, Ureno zaua kirafiki Ulaya


article-2574068-1C10556200000578-473_634x396
Ujerumani wakishangilia goli lao dhidi ya Chile
Ronaldo akipambana na kuweka rekodi ya mabao dhidi ya Cameroon walioizabua 5-1

Messi alishindwa kuibeba Argentina dhidi ya Romania
Italia walitepeta kwa Hispania 1-0, Diego Costa akiichezea timu yake hiyo kwa mara ya kwanza

Sturridge akishangilia bao liliuloibeba England jana
UJERUMANI usiku wa jana imefanikiwa kuizabua Chile kwa kuwalaza bao 1-0, huku England nayo ikipata ushindi kama huo kwa Denmark, na Brazili ikiifanyizia Afrika Kusini kwa kuifunga kwao mabao 5-0.
Bao la Ujerumani katika mechi yake na Chile lilifungwa na Mario Gotze aliyeshirikiana vyema na Mesut Ozil.
Matokeo mengine ya michezo ya kirafiki ya kimataifa inayotambuliwa na FIFA iliyochezwa jana na alfajiri ya leo Hispania iliilaza Italia baop 1-0 na kudhihirisha haikuiotea kwenye Fainali za Ulaya walipoisasambua mabao 4-0 mpaka kumfanya Mario Balotelli kumwaga chozi.
Mexixo na Nigeria zenyewe zilishindwa kufungana, Ivory Coast ikitoka sare ya mabao 2-2  na Belgiaum, huku Ureno ikiifumua Cameroon kwa mabao 5-1 Cristiano Ronaldo akifunga mawili na kuweka rekodi ya kuwa mfungaji wenye mabao mengi kwa timu ya taifa lake akimzidi Pauleta.
amabaoUshirikiano wa kiungo wa Bayern Munich Mario Gotze na kiungo wa Arsenal Mesut Ozil ulizaa matunda jana usiku katika mchezo wa kirafiki baina ya Ujerumani dhidi ya Chile.
Wachezaji wawili walishirikiana vizuri katika goli la ushindi lilofungwa na Gotze kutoka na pasi nzuri ya mwisho ya Ozil. Mchezo ulimalizika kwa matokeo ya 1-0.

Matokeo Mengine ni kama ifuatavyo
Japan     4 - 2     New Zealand    
Iran     1 - 2     Guinea    
Russia     2 - 0     Armenia    
Bulgaria     2 - 1     Belarus    
South Africa     0 - 5     Brazil    
Algeria     2 - 0     Slovenia    
Namibia 1-1 Tanzania
Greece     0 - 2     Korea Republic    
Hungary     1 - 2     Finland    
Montenegro     1 - 0     Ghana    
Czech Republic     2 - 2     Norway    
Israel     1 - 3     Slovakia    
Bosnia-Herzegovina     0 - 2     Egypt    
Cyprus     0 - 0     Northern Ireland    
Colombia     1 - 1     Tunisia    
Turkey     2 - 1     Sweden    
Romania     0 - 0     Argentina        
Ukraine     2 - 0     United States    
Austria     1 - 1     Uruguay    
Switzerland     2 - 2     Croatia    
Germany     1 - 0     Chile    
Republic of Ireland   1 - 2     Serbia    
Belgium     2 - 2     Côte d'Ivoire    
Poland     0 - 1     Scotland    
Wales     3 - 1     Iceland    
France     2 - 0     Netherlands    
England     1 - 0     Denmark    
Australia     3 - 4     Ecuador    
Portugal     5 - 1     Cameroon    
Spain     1 - 0     Italy    
Honduras     2 - 1     Venezuela    
Mexico     0 - 0     Nigeria        
Costa Rica     2 - 1     Paraguay

Yanga wapaa kuifuata Al Ahly ikijiamini

KIKOSI cha wachezaji 18 na viongozi wa klabu ya Yanga wameodnoka nchini usiku wa kuamkia leo kuelekea Misri kwa ajili ya pambano lao la marudiano dhidi ya Al Ahly wakijiamini wanaenda kumaliza kazi.

Msafara huo umeondoka bila nyota wake kutoka Uganda,Hamis Kiiza na Emmanuel Okwi waliokuwa nchini Zambia kuichezea timu yao ya taifa Uganda The Cranes ambao walilala 2-1 kwa wenyeji wao Chipolopolo.
Hata hivyo wachezaji hao wanatarajiwa kuungana nao wenzao nchini Misri baadaye leo mchana wakitokea Zambia tayari kuivusha Yanga kwenye hatua ya 32 na kuipeleka katika 16 Bora mbele ya mabingwa wateteziu hao wa Ligi ya Mabingwa Afrika na mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo.
Wachezaji waliondoka kwenda kuiua Al Ahly ni  Ally Mustapha ‘Barthez’, Juma Kaseja, Deogratius Munishi ‘Dida’, Nadir Haroub ‘Cannavaro, Juma Abdul, Kelvin Yondani, Mbuyu Twite, Oscar Jushua, Nizar Alfan, Franck Domayo, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Mrisho Ngasa, Said Bahanuzi, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, David Luhende na Jerry Tegete.
Kwa mujibu wa uongozi wa Yanga mpaka sasa hawajajua mechi yao itakayochezwa Jumapili usiku itafanyika kwenye uwanja gani baada ya uongozi wa Al Ahly kuficha taarifa hizo mpaka jana mchana.
Hata hivyo, Afisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto aliyetangulia Cairo alsema huenda  mchezo huo ukachezwa kwenye Uwanja wa Arab Contractors uliopo jijini Cairo. na kwamba maandalizi ya kuipokea timu yao inaendelea vyema kujipanga kuivaa wenyeji wao ambao hawaamini mpaka sasa kama walefungwa na timu ya Afrika Mashariki .

Cannavaro atamba Yanga itafanya maajabu Cairo

 
NAHODHA wa klabu ya Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' amesema kwamba kikosi chao kitafanya maajabu kwenye mechi yao ya marudiano dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi ya Klabu Bingwa Afrika, Al Ahly ya Misri siku ya Jumapili.
Yanga itaumana na Al Ahly katika mechi yao ya marudiano ya hatua ya kwanza itakayochezwa usiku wakiwa na ushindi wa 1-0 waliopata katika pambano lao la awali jijini Dar es Salaam kupitia goli lililofungwa kwa kichwa katika dakika ya 82 na nahodha huyo.
Akizungumza na MICHARAZO, Cannavaro alisema wanajua wa mchezo huo utakuwa ni mgumu, lakini wanaenda Cairo kuhakikisha wanatimiza ndoto zao za kuivusha Yanga kwenye 16 Bora.
"Tutaenda kupambana japo tunatarajia ushindani mkubwa baada ya kuwafunga hapa nyumbani," alisema beki huyo wa kati.
Cannavaro alisema wachezaji karibu wote watakaokuwa kwenye msafara wao uliotarajiwa kuondoka usiku wa jana, wamepania kuhakikisha Yanga inaing'oa Al Ahly na kurejea kilichowahi kufanywa na watani zao Simba mwaka 2003.
Katika mwaka huo Simba iliwafunga waliokuwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa, Zamalek pia ya Misri kisha kwenda kukubali kipigo cha 1-0 ugenini na kufanya timu hizo zikipigiane penalti na Simba kushinda kwa mikwaju 3-2.
"Tupo tayari kwa vita na Inshallah tutapambana mpaka kieleweke mjini Cairo kwa sababu tumepania kuifikisha mbali timu yetu, " alisema Cannavaro.
Bao la Cannavaro alililofungwa kwa kichwa cha kuchupia liliiwezesha Yanga kuvunja uteja kwa timu za Afrika Kaskazini zikiwamo kutoka Misri uliodumu kwa miaka zaidi ya 30 na watalazimika kupata japo sare ugenini ili kusonga mbele.

'Simba hatuhusiki uvunjwaji wa viti Taifa'

UONGOZI wa Klabu ya Soka ya Simba umesema kuwa hauhusiki na vurugu za kuvunja viti zilizotokea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati Yanga inacheza mechi yake ya mabingwa wa Ligi ya Klabu Bingwa Afrika, Al Ahly ya Misri.
Simba ilisema jana kuwa imeamua kutoa taarifa hiyo kutokana na kuwapo kwa 'uvumi' kwamba klabu hiyo huenda ikapigwa faini kufuatia baadhi ya mashabiki wake kudaiwa kuvunja viti siku ya mchezo huo.
Baadhi ya picha zilizoonekana kwenye vyombo vya habari zilionyesha mashabiki waliovaa jezi nyekundu na wengine njano wakirushiana viti na kuacha kushangilia.
Afisa Habari wa klabu hiyo, Asha Muhaji, alisema kuwa mashabiki wa Simba hawawezi kuvunja viti kwa sababu mechi hiyo ilikuwa inawahusu wapinzani wao, Yanga na Al Ahly.
Muhaji alisema kuwa si kila shabiki aliyevaa jezi nyekundu ni wa Simba kwa sababu rangi hiyo inavaliwa na klabu mbalimbali za hapa nchini kama Coastal Union, Small Simba na Al Ahly iliyokuwa inashiriki mchezo huo.
"Sisi tunaamini waliofanya vurugu ni mashabiki wa Al Ahly ambao ndio walikuwa na wapinzani wa Yanga, inashangaza Simba tunatajwa kuhusika na vurugu hizo katika mechi tusiyokuwa na maslahi nayo," alisema Muhaji.
Aliongeza kwamba Simba inataka kuweka wazi kuwa vurugu zilizofanyika katika mchezo huo haziwezi kuhusishwa na klabu yao kwa namna yoyote.
Mara kadhaa mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, amekuwa akisisitiza mashabiki wa soka kuwa wazalendo pale timu mojawapo inapokuwa inapeperusha bendera ya nchi kushangilia na kuacha mazoea ya kuzomea.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesema linaendelea kufanya uchunguiz juu ya tukio hilo kabla ya kutoa tamko, japo imelaani vurugu hizo na kuwaonya mashabiki kuwa wastaarabu kwa kuwa uwanja wa Taifa siyo wa klabu chache bali ni wa Watanzania wote.

Taifa Stars angalau, yatoka sare ya 1-1 ugenini Namibia

Na Prince Akbar, Windhoek, Namibia
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania Taifa Stars imetoka sare ya kufungana bao 1-1 na Namibia katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki unaotambuliwa na Fifa uliochezwa Jumatano usiku kwenye uwanja wa Sam Nujoma nchini Namibia.
Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika,timu hizo zilikuwa bado hazijafungana na kocha Salum Madadi akafanya mabadiliko katika kipindi cha pili kwa kuwatoa Erasto Nyoni, Ramadhani Singano ‘Messi’ na juma Luizio na nafasi zao kuchukuliwa na Michael Aidan, Athanas Mdam na khamisi Mcha ‘Vialli’.
Kikosi cha kwanza cha Timu ya Taifa, Taifa Stars kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo dhidi ya Timu ya Taifa ya Namibia, Brave Warriors na kutoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mchezaji wa Taifa Stars, Jonas Mkude  (katikati) akijaribu kupiga mpira katikati ya wachezaji wa timu ya taifa ya Namibia ‘Brave Warriors’ wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu hizo mbili katika uwanja wa Sam Nujoma  jana usiku. Tumu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mlinzi wa Taifa Stars, Saidi Morad  (kulia) akiwania mpira na mchezaji wa timu ya taifa ya Namibia ‘Brave Warriors’ Lous Jereme  wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu hizo mbili katika uwanja wa Sam Nujoma jana usiku. Tumu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mlinzi wa Taifa Stars, Erasto Nyoni (kulia) akijaribu kuudhibiti mpira mbele ya mchezaji wa timu ya taifa ya Namibia ‘Brave Warriors’ Puriza Hosea wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu hizo mbili katika uwanja wa Sam Nujoma  jana usiku. Tumu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Stars, inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager ndio walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 86 baada ya kona  iliyopigwa na Khamisi Mcha ‘Vialli’ aliyetokea benchi na kuingia moja kwa moja nyavuni bila kuguswa.
Namibia walisawazisha bao hilo katika dakika ya tano ya muda wa nyongeza baada ya kutimu dakika 90 za kawaida, lililofungwa na Nekundi Haleluya Panduleni kwa adhabu.
Refa wa mechi hiyo aliingia lawamani kwa kuzidisha muda kupita kiasi, kwani mwamuzi wa mezani alionyesha dakika tano za nyongeza lakini muamuzi alichezesha dakika tano nyingine hivi kuwawezesha Namibia kupata bao.
Lakini katika hali ya kushangaza waamuzi toka nchini Zambia na msimamizi wa mechi toka nchini Afrika Kusini waliopangiwa kuchezesha mchezo huo hawakutokea, na badala yake shirikisho la soka Namibia NFA, wakaamuru mchezo huo uchezeshwe na waamuzi wa Namibia kwa makubaliano ya pande zote mbili.
Mwalimu Salum Madadi alisema licha ya kuwakosa wachezaji wengi nyota, kikosi hiki kilipigana hadi dakika ya mwisho na ameridhishwa na matokeo yaliyopatikana.
Wachezaji walioshindwa kujiunga na kikosi cha Stars ni Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu na Mwinyi Kazimoto ambao hawakuruhusiwa na vilabu vyao kutokana na kukosekana na usafiri wa kuwarudisha vilabuni kwa muda unaotakiwa.
Wengine walioshindwa kufika ni Edward Charles na Hassan Masapili ambao hati zao za kusafiri hazikuwa zimekamilika. Viwango
Matokeo haya huenda yakaiweka Stars kwenye nafasi nzuri ya viwango vya Fifa kwa kupata sare ugenini.
BIN ZUBEIRY

Wednesday, March 5, 2014

Yanga kuivaa Alh Ahly J'2 usiku, kikosi kuondoka leo usiku

Kikosi cha Yanga kilichoibana Al Ahly kwa kuilaza 1-0 jijini Dar jumamosi iliyiopita
IMETHIBITIKA kuwa, wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Barani Afrika timu ya Young Africans itacheza mchezo wa marudiano siku ya jumapili jijini Cairo dhidi ya timu ya Al Ahly ukiwa ni mchezo utakaotoa picha halisi ni timu gani itasonga mbele katika hatua ya 16 bora.
Ikiwa ni takribani siku tano kabla ya kufanyika mchezo wenyewe wenyeji Al Ahly wameshindwa kuweka wazi ni uwanja gani utakaotumika kwa ajili ya mchezo huo huku Meneja wa klabu hiyo Abdoulazi akisema huenda mchezo ukachezwa jijini Cairo au Alexandria na kusema majibu kabili yatapatikana siku ya jumatano mchana.
Wenyeji wameiandalia timu ya Young Africans kufikia katika Hoteli ya Baron iliyopo maneneo ya Uwanja wa michezo wa kimataifa Cairo huku pia wakiipangia timu kufanya mazoezi katika uwanja wao uliopo eneno la Nasri City.
Katika mchezo wa awali uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Young Africans ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Al Ahly ambao ni mabingwa watetezi wa kombe hilo shukrani kwa bao la Nahodha wa timu Nadir Haroub "Cannavaro" aliyetikisha nyavu dakika ya 82 ya mchezo.
Mara baada ya mchezo huo kikosi cha mholanzi Hans Van der Pluijm kiliingia kambini jana jioni katika hotel ya Ledger Bahari Beach tayari kwa maandalizi ya mchezo marudiano ambapo timu imeendelea kufanya mazoezi katika uwanja wa Boko Beach Veterani.
Kuelekea mchezo huo wa jumamosi tayari uongozi wa Young Africans ulishaanza kufanya maandalizi ya safari ambayo inatarajiwa kuwepo kabla ya mwisho mwa wiki hii huku msafara ukitarajiwa na kuwa idadi ya watu 35, wakimwemo viongozi, benchi la ufundi pamoja na wachezaji 19.
Hali ya wachezaji ni nzuri, kiafya, fikra na morali ya kuelekea mchezo wenyewe bado ni kubwa kwani bench la ufundi na wachezaji wanaamini maandalizi wanayoyafanya yatasaidia kupelekea kupata ushindi katika mchezo huo na kuweza kusonga mbele katika hatua ya 16 bora.
Baadhi ya wachezaji wanaotarajiwa kuondoka usiku wa leo kuifuata Al Ahly ni makipa Deogratius Munishi 'Dida' na Juma Kaseja, Nadir Haroub 'Cannavaro, David Luhende, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Simon Msuva, Mrisho Ngasa, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, Juma Abdul, Frank Domayo, Mbuyu Twite, Rajab Zahir na Said Bahanuzi.
Okwi na Kiiza, wataungana na kikosi hicho Alhamisi wakitokea Lusaka, walipo na timu yao ya Taifa ya Uganda ( The Cranes) ambayo jana ilikuwa inacheza na Zambia (Chipolopolo) mechi ya kimataifa ya kirafiki.
Yanga inahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ili iweze kusonga mbele kwenye michuano hiyo.
Maandalizi ya sehemu ya kambi ambapo timu itafikia jijini Cairo tayari yanaendelea vizuri kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania ambapo kwa upande wa klabu ya Young Africans Afisa Habari Baraka Kizuguto tayari yupo nchini Misri kwa siku ya pili akiendelea kuweka mambo sawa.
Mchezo wa jumapili unatarajiwa kufanyika katika uwanja wa Arab Contractors uliopo jijini Cairo huku mechi hiyo ikichezwa bila ya mashabiki kufuatia Serikali ya Misri kuzuia mashabiki wa soka kutokana na mashabiki hao kufanya vurugu katika mchezo wa Fainal ya Super Cup dhidi ya CS Sfaxien na kupelekea askari kadhaa kujeruhiwa.

Wawili waongeza mkataba Arsenal na kumpa ahueni Wenger

350594_heroaBaada ya kupoteza mechi yake iliyopita ya ligi kuu ya England klabu ya Arsenal leo imewapa habari nzuri mashabiki wake baada ya kutangaza wachezaji wao wawili wameongeza mikataba ya kuendelea kuitumikia klabu hiyo.
Nahodha wa timu hiyo Mjerumani Per Mertesacker na kiungo Thomas Rosicky wote wametangazwa kuongeza mikataba yao.
“Tunayo furaha kutangaza kwamba Mertesacker na Rosicky wameongeza mikataba ya kuendelea kuwepo hapa,”  Arsene Wenger aliuambia mtandao rasmi wa klabu hiyo.
“Ni wachezaji wazuri na wenye uzoefu, na wameshaonyesha kila siku kwamba wanaweza kucheza kwenye level ya juu.’ – alimaliza Wenger.
Klabu hiyo hata hivyo haijatoa namba ya miaka kamili ya muda wa mikataba mipya.

Mourinho 'aizuga' Mancehster City mbio za ubingwa England

Jose Mourhino (kulia) na kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini  wakisalimiana enzi wakiwa Hispania
LONDON, England
KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amesema watakuwa wanabadilisha nafasi za mbio za ubingwa wa Ligi Kuu England na Manchester City kutokana na kikosi hicho cha Manuel Pellegrini kuwa na mechi mkononi.
Miamba hiyo ya Stamford Bridge inaizidi City kwa pointi sita baada ya mwishoni mwa wiki kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham, lakini mabingwa wa Kombe la Ligi (Capital One Cup) wana mechi mbili mkononi na wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa kuliko Chelsea.
Pellegrini anawinda mafanikio makubwa kwa kutwaa makombe matatu baada ya kuiongoza City kushinda 3-1 dhidi ya Sunderland Jumapili kwenye Uwanja wa Wembley na kutwaa ubingwa wa Capital One Cup, jambo ambalo Mourinho anasisitiza kuwa kocha huyo raia wa Chile yupo katika nafasi nzuri ya mbio za ubingwa.
"Ninapenda kuwa na bahati mkononi, na City tu ndiyo yenye bahati mkononi mwake," Mourinho alisema. "Kama nitashinda kila mchezo hadi mwishoni mwa msimu, zote 10 – kama hatutaweza labda hatutakuwa mabingwa.
"Kama [City] itashinda mechi zote 12 ilizo nazo, watakuwa mabingwa. Wana bahati mkononi mwao."

Wavuvi wawili wauwawa kwa risasi wakivua samaki mtoni

Na   Walter Mguluchuma, Katavi
WATU wawili  James  Mauto  21 Mkazi wa Kijiji  cha  Ugala Wilaya ya Mlele   na  January  Marekani  18 Mkazi wa Kijiji  cha Mtapenda  Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele  mkoa  wa Katavi wameuwawa  kwa kupigwa  risasi   na Askari wa Geme Reserve wakati  wakiwa wanavua  samaki  ndani ya   Hifadhi  ya Pori la akiba la Ugala na mwenzao mmoja kujeruhiwa  kwa Risasi sehemu ya mbavu zake
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa  wa Katavi Dhahiri Kidavashari   tukio hilolilitokea hapo  Februari  28 mwaka huu majira ya saa  tisa Alasiri  ndani ya Hifadhi ya pori  la akiba la Ugala Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi 

Alieleza siku hiyo ya tukio    James Mauti  na  Januari Marekani walikuwa wakivua samaki ndani ya mto Ugala uliko kwenye  Hifadhi  ya pori la akiba la ugala wakiwa na mwenzao mmoja  aitwaye  Seif Juma  40  Mkazi wa kijiji  cha Mtapenda  Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele
Kamanda Kidavashari alisema  wakati wakiwa wanaendelea kuvua samaki ndani ya mto huo  alitokea Askari  wa Geme Reserve  ambae alikuwa amevalia sare   huku akiwa na silaha  bunduki  ambayo haikuweza kufahamika aina yake
Alisema Askari huyo aliwaamuru  wavuvi  hao wajisalimishe kwake  hata hivyo wavuvi  hao waliokuwa wakiendelea na uvuvi  kufutia amri hiyo ya Askari  waliamua kutupa nyavu zao walizokuwa wakivulia samaki  na kukimbia mbio  kila mmoja sehemu yake
Ndipo Askari huyo  alipoanza  kuwarushia  risasi  wavuvi  hao  na kuwauwa  kwa risasi James Mauto   na Januari  Marekani  na kumjeruhi Seif  Juma sehemu za  mgongoni na kwenye mbavu
Majeruhi  ambae ni Seif  Juma  alifanikiwa  kufika katika kijiji  cha Ugala  na  kutoa taarifa kijijini hapo kwa uongozi wa Serikali ya Kijiji juu ya tukio hilo  na aliweza kupatiwa msaada wa kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa ajiri ya matibabu
Kamanda Kidashari  alieleza  kuwa mvuvi huyo  ambae ni majeruhi  kwa kuhofia kukamatwa na kuhojiwa  na polisi  baada ya kufikishwa  Hospitali alitoroka  na mpaka sasa  haijajulikana mahari alipo na anatibiwa wapi majeraha yake ya risasi
Alisema  kutokana na tukio hilo kuhusishwa  na Askari  wa Geme  Reserve  katika hifadhi  hiyo  jeshi la polisi Mkoa wa Katavi  linawasiliana  na mkuu wa  kikosi cha  wanyama pori  mkoa wa Tabora  ambako ndio  walikuwa wametoka Akari waliohusika na tukio la mauwaji hayo
Alifafanua  kuwa  tayari mkuu wa Kikosi hicho  cha wanyama pori  ametuma kikosi chake kwenye eneo hilo la tukio  ilikubaini  ni Askari  gani waliokuwa kwenye  doria  eneo hilo  ili kuwabaini  na kisha  sheria ichukuwe mkondo wake  kwa askari  aliyehusika au waliohusika  kwa tukio la mauwaji hayo ya kinyama kwa binadamu hao.
Pambana na Climate Change

Petr Cech hakamatiki Tuzo ya Mchezaji Bora Czech

KIPA wa klabu ya Chelsea ya England, Petr Cech hashikiki katika Tuzo yta Mchezaji Bora wa Mwaka wa Jamhuri ya Czech baada ya kutangazwa tena kuwa mshindi wa mwaka 2013 ikiwa ni mara yake ya sita mfululizo kati ya saba aliyonyakua tuzo hiyo.
Cech (31) ameshinda tuzo hiyo kwa mara ya sita baada ya kupigiwa kura nyingi kutoka kwa wachezaji, makocha, viongozi wa shirikisho la soka na waandishi wa habari.
Kiungo wa Arsenal, Tomas Rosicky ameshika nafasi ya pili wakati mchezaji wa Freiburg, Vladimir Darida akishika ya tatu.
Kipa huyo ndiye tegemeo wa Chelsea inayopigana kunyakua ubingwa kwa msimu huu ikiwa chini na kocha aliyewahi kuipa mafanikio huko nyuma, Jose Mourinho.

Taifa Stars dimbani leo Namibia bila Samatta, Ulimwengu

Taifa Stars
Mbwana Samatta (kulia) atakayelikosa pambano la leo nchini Namibia

TIMU ya Taifa (Taifa Stars), itawakosa nyota wake wanaocheza soka nje ya nchi katika mechi ya kirafiki ya Kimataifa dhidi ya Namibia itakayochezwa leo kwenye Uwanja wa Sam Nujoma jijini Windhoek nchini humo.
Hatua hiyo inakuja baada ya Shirikisho la Soka nchini (TFF) kushindwa kupata usafiri wa uhakika wa kuwarejesha ndani saa 24 katika klabu yao, washambuliaji Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu wanaoichezea TP Mazembe ya DR Congo pamoja na Mwinyi Kazimoto anayeichezea Al-Makhiya ya Qatar.
Stars ya TFF (iliyoteuliwa na shirikisho hilo badala ya kocha), iliondoka nchini juzi alfajiri ikiwa chini ya Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi wa shirikisho hilo, Salum Madadi, aliyeshika kwa muda nafasi ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Mdenmark Kim Poulsen, ambaye alitimuliwa wiki iliyopita.
Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, aliliambia NIPASHE jijini Dar es Salaam jana kuwa, Stars itashuka dimbani bila ya wachezaji wake wanaosakata kabumbu la kulipwa nje ya nchi, Ulimwengu, Samata  na Kazimoto.
Alisema wachezaji hao wanakosekana baada ya TFF kukosa ndege ya kuwarudisha katika timu zao ndani ya saa 24 baada ya mechi hiyo kumalizika kama Kanuni za Fifa zinavyoelekeza.
"Ndege tulizopata zinapita Nairobi kwenda Lubumbashi Machi 8, wakati Samata na Ulimwengu wana mechi muhimu ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwishoni mwa wiki," alisema Wambura.
Aidha, Wambura alisema Stars itawakosa wachezaji Hassan Mwasapili na Edward Charles ambao wamekosa hati za kusafiria (passport).
Kutokana na kukwama kwa nyota hao, Stars sasa imebaki na wachezaji 15 wakiwamo makipa Mwadini Ally (Azam) na Shaban Kado (Coastal) aliyeitwa kuziba nafasi ya Ivo Mapunda (Simba) aliyefiwa na baba yake mzazi wiki iliyopita.
Mabeki ni Erasto Nyoni, Said Moradi na Aggrey Morris (Azam), Abdi Banda (Coastal) na Michael Aidan (Ruvu Shooting), wakati viungo ni Amri Kiemba (Simba), Jonas Mkude (Simba) na Himid Mao kutoka Azam FC.
Washambuliaji ni Athanas Mdamu (Alliance Mwanza), Haruna Chanongo (Simba), Khamis Mcha (Azam), Ramadhan Singano (Simba) na Juma Luizio kutoka Mtibwa Sugar.

Tuesday, March 4, 2014

Young Hassanally kuzindua Nyongo Mkaa na Ini

* Uzinduzi kufanyika Ijumaa Travertine Hotel
* Khadija Kopa, Jokha Kassim,Mwanahawa Ally ndani
Muimbaji Hassani Ally 'Young Hassanally'
Mwanahawa Ally naye atakuwepo ukumbini kumsindikiza Young Hassanally
Khadija Kopa (kushoto) naye atakuwepo Travertine Hotel
MALKIA wa Mipasho nchini, Khadija Kopa, Mwanahawa Ally na Jokha Kassim wanatarajiwa kusindikiza uzinduzi wa albamu mpya binafsi ya muimbaji nyota wa muziki wa taarab nchini anayeliimbia kundi la King's Modern Taarab, Hassan Ally 'Young Hassanally'.
Uzinduzi huo wa albamu hiyo inayofahamika kwa jina la 'Nyongo Mkaa na Ini' utafanyika siku ya Ijumaa kwenye ukumbi wa hoteli maarufu iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO, Young Hassanally, alisema mbali na waimbaji hao mahiri nchini, pia uzinduzi huo utasindikizwa na kundi la King's Modern Taarab maarufu kama 'Wana Kijoka'.
Hassanally, alisema ameamua kuwashiriki wakali hao katika uzinduzi wake ili kuunogesha na kuwapa burudani mashabiki wa muziki wa mwambao.
"Siku ya Ijumaa natarajia kuzindua albamu yangu ya pili mpya iitwayo 'Nyongo Mkaa na Ini' ambapo nitasindikizwa na wakali wa muziki wa mwambao Afrika Mashariki na Kati, Al-hanisa Khadija Kopa, Mwanahawa Ally 'B52' na Jokha Kassim pia kundi langu la King's Modern litakuwapo ukumbini Magomeni kunisindikiza," alisema.
Hiyo ni albamu ya pili binafsi ya staa huyo baada ya awali kuzidnua albamu ya 'Aibu Yao Aibu Yetu' na  aliongeza kuwa maandalizi yote ya uzinduzi huo yamekamilika na kwa sasa kinachosubiriwa na siku ya uzinduzi huo ili mashabiki wapate burudani, huku akitaja viingilio ni Sh. 5000 tu kila kichwa.

Ridhiwani Kikwete kuitetea CCM-Chalinze, ambwaga Madega

Ridhiwani Kikwete (kulia)
Kuelekea uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani lililoachwa wazi baada ya mbunge wake SAID BWANAMDOGO kufariki hivi karibuni Chama cha Mapinduzi kimefanya kura ya maoni ili kumpata mrithi wa Jimbo hilo atakayechuana na wagombea kutoka vyama vingine.

Katika kura hiyo ya maoni wagombea watatu wamejitokeza kuwania nafasi ya ubunge wa Jimbo la Chalinze kupitia chama cha CCM akiwemo mbunge wa zamani wa Jimbo hilo RAMADHAN MANENO, mwenyekiti wa zamani wa Yanga IMANI MADEGA na mdau mkubwa wa soka hapa nchini na mwanachama wa Yanga RIDHIWANI KIKWETE.
Baada ya kura kupigwa RIDHIWANI KIKWETE ndiye amepata Baraka za wanaCCM kuingia kwenye kinyang’anyiro cha Ubunge kwa kumpa kura 758 huku IMANI MADEGA akishika nafasi ya pili kwa kupata kura 335 na RAMADHAN MANENO akishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 206.
SHAFFIH DAUDA

Steve Nyerere aja na Snake Kingdom

Hii ndiyo kazi mpya ya Steve Nyerere itakayosambazwa na Proin Promotions
MWENYEKITI wa Bongo Movie Unity (BMU), Steven Mengele 'Steve Nyerere' anajiandaa kuiachia hadharani filamu yake mpya kwa mwaka 2014 iitwayo 'Snake Kingdom'.
Akizungumza na MICHARAZO, Steve Nyerere alisema filamu hiyo ya kijamii ameigiza na wakali wenzake kama Chuchu Hans, Mayasa Mrisho, Cathy Rupia, Bi Terry 'Mama Nyamayao' na wengine.
Steve Nyerere alisema filamu hiyo ni ya aina yake na kuwataka mashabiki kujiandaa kupata uhondo mara itakapoachiwa mtaani hivi karibuni chini ya kampuni mpya na inayokuja kwa kasi katika kusambaza kazi za wasanii wa filamu nchini ya Proin Promotions.
Mchekeshaji huyo anayeigiza sauti za viongozi mashuhuri, alisema 'Snake Kingdom' ni filamu iliyozalishwa na kampuni yake iliyowahi kutoa filamu kama 'Mwalimu Nyerere', 'My President', 'My Son', 'Mke Mwema' na nyingine.

Huwezi kuamini! Kaole Sanaa Group 'lafufuka' na Kipusa

Issa Kipemba 'Kipemba' aliyepigana kuirejesha tena Kaole Sanaa
Mmoja wa waasisi wa Kaole Sanaa, Bi Chuma Suleiman 'Bi Hindu' aliyecheza igizo la 'Kipusa'
Unamkumbuka Mzee wa Mabreka? Swebe Santana naye ndani dah!
JANA niliwaacha na maswali mengi juu ya taarifa inayokuwa ikiuliza unalikumbuka kundi la Kaole Sanaa Group, kundi lililochangia kupatikana kwa asilimia kubwa ya mastaa wanaotamba kwenye Bongo Movie.
Kundi hilo lililoasisiwa na kuundwa na wasanii wakongwe wa maigizo waliotamba kupitia Radio Tanzania (RTD) na lililokuja kutamba na michezo yao ya kwenye runinga kupitia kituo cha ITV kabla ya kuhamisa TVT (sasa TBC1) lilikuwa kama 'limekufa' hasa baada ya mastaa wake kuhamia kwenye filamu.
Hata hivyo mmoja wa mastaa wake, Issa Kipemba na wenzake kadhaa walikaa chini na kutafakari ili kulirejesha tena kwa nguvu kundi hilo.
Vikao kadhaa vilivyowahusisha baadhi ya waasisi wake kama Chuma Suleiman 'Bi Hindu' na wengine hatimaye kundi hilo limeanza kurekodi igizo lao jipya kwa ajili ya kuwarejesha burudani mashabiki wake ambayo waliikosa kwa kipindi kirefu.
Igizo hilo ambalo hata hivyo bado halijafahamika litaonyeshwa katika kituo gani cha runinga kwa sasa nchini, utafahamika kwa jina la 'Kipusa' ambapo sehemu kubwa ya tamthilia hiyo imesharekodiwa sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO mmoja wa nyota wa kundi hilo Adam Malele 'Swebe Santana' alisema tamthilia hiyo imewashirikisha asilimia kubwa ya nyota za zamani wa kundi hilo.
Swebe aliwataja baadhi ya nyota hao akiwamo yeye ni pamoja na Rashid Mwinshehe 'Kingwendu', Issa Kipemba 'Kipemba', Abdallah Mkumbira 'Muhogo Mchungu' na Ndimbango Misayo 'Thea'.
"Pia igizo hilo limewashirikisha Khadija Yahya 'Davina', Bi. Star, Happiness Stancelaus ‘Nyamayao’, Mzee Chap Chapuo,Davina, Bi Star, Bi Hindu, Mama Nyamayao na wengine," alisema Swebe.
MICHARAZO ilikuwa wa kwanza kudokeza kuwepo kwa mipango ya kurejeshwa upya kwa kundi hilo baada ya kuwafumania Lango la Jiji wakifanya vikao na sasa imethibitika suala hilo ni kweli tupu.
Taarifa zaidi na wasifu wa washriki walioucheza mchezo huo MICHARAZO itaendelea kuwajuza kila mara.

TFF/TWFA kutoa mafunzo maalum Siku ya Wanawake


Mwenyekiti wa TWFA, Linnah Mhando
KATIKA kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani na kudhamini mchango wa wanawake katika michezo Shirikisho la Soka ya Wanawake Tanzania (TWFA) ikishirikiana na TFF itaendesha mafunzo maalum.
Mwenyekiti wa TWFA, Linnah Mhando amesema shirikisho lake kupitia Kamati ya Wanawake ya mpira wa miguu kwa wanawake, wanatambua umuhimu wa siku ya wanawake duniani.
“Mpira wa miguu kwa wanawake ni moja ya michezo inayokuwa kwa kasi katika bara la Afrika na hata hapa nyumbani. Idadi ya wasichana wanoshiriki katika mpira wa miguu imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.
Katika kusheherekea  siku ya wanawake duniani mwaka 2014. Sherehe rasmi zitafanyika katika mkoa wa Tanga
TFF /TWFA wanaamini kuwa ili kuwa na kiwango kizuri na maendeleo katika mpira wa miguu wanawake  ni lazima kuanza na vijana wadogo hivyo basi Shirikisho na chama cha mpira wa miguu Tanga limeandaa mafunzo kwa walimu wapatao 30 toka shule15 za mkoa wa Tanga.
Walimu hao watapatiwa mafunzo kwa siku mbili na tarehe 08/03/2014 kutakuwa na Tamasha la Grassroot litakalojumusha jumla ya wanafunzi wapatao 1000 toka shule husika.
Ni matumaini ya shirikisho kuwa mafunzo hayo na tamasha la grassroot litaleta mwamko wa mpira wa miguu katika mkoa wa Tanga na hamasa kwa watoto wa kike,wasichana na kina mama katika ushiriki wa mpira wa miguu wanawake.

TFF kuwaadhibu wawili Twiga Stars

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) linatafakari hatua zaidi za kinidhamu dhidi ya wachezaji wawili wa kikosi cha Twiga Stars walioondolewa kwenye timu hiyo na Kocha Rogasian Kaijage. Kocha Kaijage aliwatimua kambini wachezaji Mwapewa Mtumwa na Flora Kayanda kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu wakati Twiga Stars ikijiandaa kwa mechi ya marudiano ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Zambia.
Twiga Stars ilipoteza mechi ya kwanza ugenini mabao 2-1 na kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya marudiano iliyochezwa Februari 28 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex, hivyo kutolewa katika mashindano hayo kwa jumla ya mabao 3-2.
“TFF tunaunga mkono hatua iliyochukuliwa na Kocha Kaijage dhidi ya wachezaji hao wakongwe wa Twiga Stars, kwani katika shughuli yoyote ile inayohitaji ufanisi nidhamu ni kitu cha kwanza,” imesema taarifa ya TFF.
Twiga Stars itacheza mechi za mchujo za michezo ya 11 ya Afrika (All Africa Games) ambayo itafanyika mwakani nchini Congo Brazzaville.

Sikia hii! Mchungaji akataza waumini wake wasivae Ch**pi


UKISIKIA Mwisho wa Dunia haupo mbali ndiko huku, Mchungaji mmoja nchini Kenya amewapiga marufuku waumini wake wa kike kuvaa nguo za ndani waendapo kufnya ibada ndani ya kanisa analoliongoza ili wampokee YESU wakiwa huru.
Mchungaji huyo Mkenya amenukuliwa nchini mwake kuwa waumini wanapaswa kuwa huru kimwili na kiroho wakati a kumpokea Bwana hivyo wanapaswa kutovaa nguo za ndani.
Ebu soma taarifa hiyo hapo nchini uone maajabu ya mwisho wa dunia na wanaojifanya wachungaji wa Kondoo za BWANA.
KENYAN Pastor Orders Female Congregants To Attend Church Without Putting On Bras & Panties For Christ To Enter Their Lives 'Freely'

A Kenyan pastor has ordered his female congregants to go to the church 'free' - That
is without bras and panties for Christ to enter their
lives.

According to kenyan-post.com, Reverend Njohi of the Lord's Propeller Redemption Church in Nairobi reportedly advised female worshippers against
wearing any undergarments to the church, calling them ungodly.

In a meeting chaired by him, a law was passed banning the wearing of inner wears.

Njohi claims that when going to church, people need to be free in 'body' and 'spirit' to receive Christ.

He went ahead to warn members of dire consequences if they secretly put on their inner wears.

Mothers were also advised to do same and check their daughters when coming to church on Sundays so as to receive Christ too.

Duh, Vibaka Nouma kweli wamliza Ally Choki

Ally Choki 'Mzee wa Ambulance' aliyelizwa na vibaka
AMA kweli kwenye msafara wa mamba kenge hawakosekani. Mkurugenzi wa bendi ya muziki wa dansi Extra Bongo Next Level 'Kamarade' 'wazee wa Kimbembe' Ally Choki alijikuta akimwaga machozi baada ya watu wanaodhaniwa kuwa vibaka kujipenyeza wakati wa uzinduzi wa albamu ya 'Mtenda Akitendewa' Februari 22 mwaka huu na kumuibia saa ya silva yenye thamani ya dola 300 sawa na sh.500,000.
Extra Bongo ilizindua albamu hiyo ndani ya Ukumbi wa Dar Live Mbagala jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mamia ya mashabiki na wadau wa muziki wa dansi ambapo Choki aliingia ukumbini akiwa ndani ya gari la kubeba wagonjwa 'Ambulance' na kulakiwa juu kwa juu.
Choki, alieleza, tukio la kuibiwa lilimkuta wakati akishuka kwenye ambulance ambapo ndani ya kundi la mashabiki waliompokea kulikuwepo na vibaka waliofanikwa kumvua saa hiyo pasipo yeye kujitambua.
"Kwa kweli saa yangu inaniuma sana nililetewa zawadi na rafiki yangu kutoka Qatar lakini ndo hivyo vibaka wameniingiza mjini alisema Choki kwa masikitiko na kuongeza.
"Wakati nimepanda jukwaani ndiyo nikashtukia nimelambwa saa, bahati nzuri simu na vitu vyangu vingine vya thamani nilikuwa nimeviacha kwa mlinzi wangu vinginevyo hali maumivu yangekuwa makali zaidi ya hivi.
Tukio la Choki kuibiwa linakumbusha tukio jingine lililowahi kutokea miaka kadhaa nyuma kwa aliyekuwa rapa wa bendi ya Tanzania One Theatre (TOT) Papii Kocha 'Mtoto wa Mfalme' kuporwa cheni na vibaka akiwa jukwaani wakati wa uzinduzi wa moja ya albamu za bendi hiyo katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.
Aidha Choki alisema atatoa zawadi ya sh.300,000 kwa mtu yoyote atakayeweza kufanikisha kupatikana kwa saa hiyo huku akitaka aliyeiba kumrejeshea kiroho safi na atampatia kiasi hicho cha fedha pasipo kufikishwa kwenye vyombo vya dola.
"Nimeamua kutoa zawadi kwa atakayewezesha niipate saa yangu au kwa aliyechukua kuirudisha kwangu, hii ni sababu nilikuwa naipenda sana alieleza.

Samuel Sitta ndiye Mwenyekiti wa Bunge la Katiba

  CCM waridhia awanie uenyekiti Bunge la Katiba
  Samia Hassan Suluhu kuwania umakamu
Mhe Samuel Sitta
WAJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamemaliza ‘mnyukano’ wa muda mrefu wa vigogo wa kuwania uenyekiti wa kudumu wa Bunge hilo, baada ya kutoa baraka zote kwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kugombea nafasi hiyo.

Wakati Waziri Sitta akipewa baraka hizo na wajumbe hao kupitia Kamati ya Uongozi ya Wabunge wa CCM, Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge, ameripotiwa kuamua kutogombea nafasi hiyo.

Pia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Hassan Suluhu, amepitishwa na kamati hiyo kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Kudumu wa Bunge hilo kutokea Zanzibar.

NIPASHE lilimtafuta Sitta jana kueleza kupitishwa na chama chake, lakini alisema kuwa hakuwa kwenye mkutano huo hadi mwisho. “Niliingia kwenye kikao na kutoka mapema, sijui kama uamuzi huo umefikiwa,” alisema.

Vyanzo mbalimbali vya NIPASHE kutoka ndani ya kikao hicho vinaeleza kuwa, uamuzi wa kamati hiyo ulifikiwa baada ya kuwaita viongozi hao na kuwahoji kwa nyakati tofauti iwapo wana nia ya kugombea nafasi hizo au la.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, Waziri Sitta na Waziri Suluhu, walipitishwa kwa kauli moja kuwania nafasi hizo, baada ya kamati hiyo kujiridhisha kwamba, wamekidhi sifa.

Mbali na Sitta, Suluhu na Chenge, chanzo hicho kilieleza kuwa mwingine, ambaye aliitwa na kuhojiwa na kamati hiyo ni Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, aliyefahamika kwa majina la Mwajuma Mgeni, ambaye hata hivyo, naye kama Chenge aliamua kutogombea nafasi hiyo.

Kabla ya kamati hiyo kutoa baraka hizo, kiongozi pekee aliyejitokeza hadharani na kutangaza azma ya kuwania nafasi hiyo ni Sitta pekee.

Sitta alisema anataka kuwania nafasi hiyo ili apate fursa ya kutimiza kwa vitendo ndoto ya Rais Jakaya Kikwete ya kuhakikisha Tanzania inapata katiba bora.

Imeelezwa kuwa wajumbe kadhaa walipendekeza jina la Sitta lipitishwe pasipo kuwapo mgombea mwingine, kwa maelezo kuwa wana-CCM wengine waliokuwa wanatajwa, wanaonekana kutokuwa na uwezo wa kulimudu Bunge hilo.

“Tumetoka kwenye kikao cha wajumbe wa CCM na kwa namna ya pekee, imekubalika kwamba Sitta ndiye anayefaa kwa uenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,” kilieleza chanzo kimojawapo kwa sharti la kutokutajwa jina lake gazetini.

“Kama chama kimeonyesha imani yake kwa Sitta, na kwa mujibu wa Sheria, Makamu wake anatakiwa kutoka Zanzibar ambapo jina la Samia Suluhu limepitishwa ndani kwa wajumbe wa CCM,” kilieleza chanzo hicho.

Sitta amekuwa akitajwa ndani na nje ya Bunge Maalum la Katiba, kwamba anafaa kuchukua nafasi hiyo kutokana na rekodi nzuri aliyoiacha alipokuwa Spika wa Bunge la Tisa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

ZENGWE LA SERIKALI TATU
Hata hivyo, waliokuwa wanampinga Sitta waliibua hoja kwamba mwanasiasa huyo mkongwe, amekuwa na mwelekeo wa kutaka kuwapo kwa serikali tatu, hoja aliyoipinga mara kadhaa akisema uamuzi wowote kuhusu hatima ya Katiba Mpya na hususani mfumo wa utawala utakavyokuwa, vitaamriwa na Watanzania.

HAKUNA MARIDHIANO
Katika hatua nyingine, matumaini ya kufikia maridhiano yatakayowezesha kupatikana kwa katiba mpya, yamezidi kufifia.

Hiyo ni baada ya wajumbe wa Bunge hilo kutoka vyama vya upinzani na makundi ya kijamii na wale wanaotoka CCM kuendelea kuvutana kuhusu utaratibu utakaotumiwa kupata uamuzi katika vikao vya Bunge hilo.

Katika mvutano huo, wajumbe wa CCM wanataka utaratibu utakaotumiwa kupata uamuzi katika vikao vya Bunge hilo uwe wa kura ya wazi, huku wale wanaotoka katika vyama vya upinzani na wa baadhi wanaotoka katika makundi ya kijamii wakitaka utumike wa kura ya siri.

Msimamo wa wajumbe kutoka vyama vya upinzani na makundi ya kijamii, ulifikiwa kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika kikao chake kilichofanyika juzi.

Chanzo chetu kutoka ndani ya kikao cha wajumbe wa CCM zinaeleza kuwa baadhi ya wajumbe walilalamikia kile walichokiita mjadala wa Rasimu ya Kanuni za Bunge Maalumu kuachwa kuhodhiwa na wapinzani bungeni.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, baadhi ya wajumbe katika kikao hicho walitoa mfano wakisema uundwaji wa Kamati ya Kanuni za Bunge Maalumu, ambao walidai kuwa imeachiwa kuhodhiwa na wapinzani.

Mbunge huyo alieleza pia kuwa wajumbe wengine katika kikao hicho walidai kwamba hata Rasimu ya Kanuni ya Bunge Maalumu ya Mwaka 2014 zimetungwa kwa kuwabeba wapinzani.

Alieleza kuwa kuwa baadhi ya wajumbe katika mjadala huo, walitaka kumjua waliyemuita “mchawi” aliyesababisha hali hiyo.

MKAKATI WA KUTEKA BUNGE
Mtoa taarifa wetu alieleza kuwa baada ya majadiliano yaliyochukua takriban saa sita, hatimaye kikao kilifikia maamuzi mbalimbali, ikiwamo namna wajumbe watahakikisha utaratibu wa kupata uamuzi katika Bunge hilo kwa kura ya siri unadhibitiwa.

Alieleza kuwa jambo lingine, ambalo lilitolewa uamuzi na kikao hicho, linahusu namna ya kumdhibiti mwenyekiti wa muda wa Bunge hilo, Pandu Ameir Kificho.

Chanzo hicho kilisema udhibiti huo utalenga zaidi katika maelekezo yoyote yatakayotolewa na mwenyekiti huyo wakati wa kusimamia mjadala wa rasimu ya kanuni hizo hadi azimio la kuzipitisha litakapotolewa na Bunge hilo.

Kilisema kuwa maamuzi hayo pia yalipinga ushauri uliotolewa na Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela, wakati akichangia mjadala wa rasimu ya kanuni hizo wiki iliyopita, kwamba ushauri huo hauna maslahi na chama.

Chanzo hicho kilieleza kuwa kikao hicho pia kilipitisha maamuzi ya kujengwa mazingira ya kuahirishwa makusudi kikao cha Bunge cha jana asubuhi, kama ilivyotokea.

Kilieleza kuwa uamuzi huo ulipitishwa ili kuwapa fursa wajumbe wa CCM kuifanya marekebisho rasimu ya kanuni hizo kama wanavyotaka.

NDIYO DHIDI YA SIRI

Chanzo hicho kilieleza pia kuwa uamuzi mwingine uliofikiwa na kikao hicho ulitaka lazima mwenyekiti wa muda wa Bunge hilo ahakikishe upitishaji wa vifungu vya rasimu ya kanuni hizo unafanyika kwa kura za wajumbe kupaza sauti za ndiyo au hapana.
 

Katibu wa wajumbe wa CCM, Jenista Mhagama, hakupatikana jana kuzungumzia yaliyojiri katika kikao chao cha juzi na hata alipopigiwa, simu yake ilikuwa inaita bila majibu.
 
CHANZO: NIPASHE

Inatisha jamaa afukua kaburi na mwanamke akiwa uchi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjzMYECCwkRKCFGbps0HoMYnLTH_Qnj1FT7Lc8nRmd6SQUU_iopPLSDtZrhMxlJqwdEv1hBiLOV3Fs1G4dPx8oHT59kcCtTbMznrMoHiZBiLDy-JI7LOQzK-Fx1WsVNz5jA8b1Zw9jA7npz/s1600/4680222.jpg
MKAZI wa kijiji cha Ikola  Wilaya ya Mpanda Mkoa  wa Katavi  Richard  Clavery  34 amefikishwa  Mahakamani  katika mahakama ya Wilaya ya Mpanda kujituhuma za kufanya vitendo vya ushirikina  wa kufukua kaburi la mwanamke aliyekufa.
Mtuhumiwa  alifikishwa kizimbani hapo Februari   25 mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa   na kusomewa mashitaka na mwendesha mashitaka  Godfrey  Luzabila
Mwendesha mashitaka alidai  Mahakamani hapo kuwa  mtuhumiwa  alitenda kosa hilo hapo Februali   18 mwaka huu majira ya saa nne usiku nyumbani kwa  Lenada  Sakafu
Mwendesha mashitaka   Luzabila  aliiambia mahakama kuwa siku  hiyo ya tukio  mtuhumiwa alifika nyumbani kwa Lenana  Sakafu  na kufukua  maiti ya mdogo wake na Lenada  aitwaye Tabu Omera  ambae alikuwa amefarii  siku tatu kabla ya tukio  hili
Aliendelea kuieleza Mahakama   siku hiyo  Lenada  alikuwa nyumbani  kwake pamoja na   majirani na ndugu  zake wakiendelea kuomboleza msiba  ghafla alitokea  mtoto wake aitwaye  Brandina  na kuwaeleza  kuwa ameona mtu nje akifukua kaburi la marehemu   ambae alikuwa amezikiwa  kwenye eneo la nyumba yao
Alieleza ndipo watu hao walipoamua kutoka nje   na kumkuta  mtuhumiwa  Richard  Clavery   akifukua kaburi  hilo huku akiwa  amevua nguo zake zote  ambazo alikuwa amezitundika kwenye msalaba  wa kaburi  hilo  na walipomsemesha mtuhumiwa  alijifanya kupandisha majini
Mtuhumiwa  baada ya kusomewa mashitaka  alikana   na Hakimu Mkazi Mfawidhi  Chiganga Ntengwa aliharisha kesi hiyo hadi hapo machi 6 na mtehumiwa alipelekwa rumande  baada ya kushindwa kutimiza masharti ya mdhamana ambapo alitakiwa adhaminiwe na mtu mmoja kwa  dhamana ya shilingi milioni  moja