STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 8, 2014

Wababe wa Azam wang'oka Kombe la Shirikisho


WABABE wa waliokuwa wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Azam timu ya Ferroviario de Beira imeondolewa kwenye michuano hiyo baada ya kunyukwa bao 1-0 na ZESCO ya Zambia katika mechi ya marudiano iliyochezwa leo jijini Lusaka.
Ferroviario iliiondosha Azam kwenye raudni ya awali kwa kuilaza jumla ya mabao 2-1 baada ya awali kulala 1-0 nyumbani Tanzania na kwenda kushinda kwao 2-0, ilishindwa kuhimili vishindo vya Wazambia ambao katika mechi ya awali ugenini ililazimisha sare.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo zilizochezwa leo, Etoile du Sahel imepata ushindi mnono nyumbani kwa kuicharaz a CARA Brazzaville kwa maba0 3-0 na kufuzu kwa jumla ya mabao 3-1 kwani mechi iliyopita walilala ugenini bao 1-0 mjini Brazzaville Congo.
Nayo timu ya ASEC Memosa ya Ivory Coast, imepenya raundi ya pili baada ya kulazimishwa sare nyumbani na COB ya Mali lakini ikifaidika na ushindi wa mabao 2-0 iliyopata ugenini wiki iliyopita, huku How Mine ya Zimbabwe ikiing'oa St Michel United ya Sychelles kwa jumla ya mabao 6-4 baada ya leo kulala ugenini mabao 3-1 kwa Washelisheli hao, ila katika mechi yao iliyoipita walishinda nyumbani mabao 5-1.
AS Kigali nayo ilipenya hatua ya pili baada ya kuingoa Al Ahly Shendi ya Sudan Kusini kwa mikwaju ya penati baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 ugenini wiki moja baada ya kushinda ushindi kama huo nyumbani.
Timu ya  Bayesla United ya Nigeria ilifuzu hatua inayofuata baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Kondzo ya Kongo ambao walitoka nao suluhu ya kutofunga katika mechi yao wiki iliyopita.
Katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika zilizochezwa leo mbali na mechi tuliyoripoti mapema kati ya KCCA na Nkana, timu ya Kaizer Chiefs ya Agfrioka Kusini ilifuzu raundi ya pili kwa kishindo baada ya kuibutua Liga Maculmana ya Msumbiji kwa kuilaza mabao 3-0 na kufuzu kwa jumla ya mabao 7-0 baada ya wiki iliyopita kushinda nyumbani kwa mabao 4-0.
Nayo timu ya Leopards de Dolisie ya  Kongo imeingoa 1st de Agosto ya Angola kwa jumla ya mabao 4-3 baada ya leo kukubali kipigop ugenini mjini Luanda cha mabao 2-00 lakini ikibebwa na ushindi mnono iliypata nyumbani kwao wiki iliyopita ilkipoifumua Waangola mabao 4-1.
Mabingwa wa zamani wa Afrika Enyimba ya Nigeria licha ya kushinda bao 1-0 ugenini dhidi ya Real Bamako imejikuta iking'oka mashindanoni baada ya mechi ya kwanza kulala nyumbani mabao 2-1 kwa wapinzani wao na kufanya matokeo kuwa 2-2 ila Bamako kunufaika na faida ya mabao ya ugenini.
Nao ES Setif ya Algeria kufuzu hatua ya pili baada ya kulazimisha suluhu ugenini dhidi ya ASFA-Yannenga ya Burkina Faso baada ya wiki iliyopita kupata ushindi mnono nyumbani wa mabao 5-0.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea kesho kwa michezio mingine kadhaa ya kuhitimisha mechi za marudiano na kufahamika timu zilizotinga hatua ya 16 Bora, ambapo moja ya mechi hizo itazikutanisha watetezi Al Ahly ya Misri dhidi ya Yanga ambayo ilishinda mechi ya kwanza nyumbani Tanzania kwa bao 1-0.
Mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu itachezwa kwenye jiji la Alexandria, baada ya wenyeji kuhofia mashabiki wao wakorofi jijini Cairo ambao walichukizwa na kipigo ilichopewa timu yao ugenini na Yanga.





Chelsea yaibutua Spurs 4-0 darajani

Et'oo akishangilia bao lake
Samuel Eto'o is congratulated by teammate Branoslav Ivanovic after putting Chelsea ahead
Eto'o akipongezwa baada ya kufunga bao la utangulizi
John Terry
Nahodha John Terry akimpongeza Eto'o
VINARA wa Ligi Kuu ya England ikiwa katika kiwango tishio imeitubua Tottenham Hotspur kwa mabao 4-0 katika mfululizo wa mechi za ligi hiyo, huku mtokea benchi Demba Ba akifunga mabao mawili dakika za jioni kwenye uwanja wa Stanford Bridge.
Samuel Ot'oo alikuwa wa kwanza kuifungia Chelsea bao dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kabla ya Edin Hazard kuongeza la pili kwa mkwaju wa penati dakika ya 65 baada ya Younes Kaboul kumchezea vibaya Et'oo kosa lililomfanya alimwe kadi nyekundu na kutolewa uwanjani.
Kocha Jose Mourinho alifanya mabadiliko ya haraka haraka akimtoa Etoo na nafasi yake kuchukuliwa na Demba Ba ambaye hakuwa na ajizi baada ya kufunga mabao mawili katika dakika ya 88 na 90 yaliyotosha kuihakikisha Chelsea kukaa kileleni ikiwa na pointi 66 saba zaidi ya iliyonayo Liverpool na Arsenal zenye 59 kila moja..
Katika mechi nyingine za mapema Cardiff City ikiwa nyumbani iliisasambua Fulham kwa kuicharaza mabao 3-1, Southampton ikiwa ugenini ilipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Crystal Palace, huku Norwich City na Stoke City ilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1.

Barcelona yazamishwa tena Hispania

Fausto Rossi celebrates
Fausto Rossi akishangilia bao lake lililoizamisha Barcelona leo
Lionel Messi looks upsetBAO pekee lililofungwa na Fausto Rossi katika dakika 17 lilitosha kuizamisha Barcelona ikiwa ugenini wakati ikiumana na Real Valladolid katika mchezo wa Ligi Kuu ya Hispania na kuifanya watetezi hao kushindwa kuwaengua kileleni Real Madrid watakaoshuka dimbani kesho.
Barcelona licha ya kuchezesha kikosi chake cha hatari kikiwajumuisha nyota wake kama Lionel Messi, Neymar na wengine ilishindwa kabisa kufurukata mbele ya wenyeji wao na kuwafanya walale na kuwaacha Real wakipumua kileleni wakitofautiana pointi moja, Real wakiwa na 64 na Barca wakiwa na 63 wakitishiwa kuporomoshwa zaidi hadi nafasi ya tatu iwapo Atletico Madrid itakayoshuka dimbani baadaye kama itaibuka na ushindi ugenini dhidi ya Celta Vigo.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jioni hii timu ya Real Betis iliifunga Getafe kwa mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa nyumbani kwa washindi.

Mbeya City yaishusha Yanga, Ruvu yazinduka


Mbeya City iliyotakata nyumbani
Ruvu Shooting ilizinduka
WAKATI watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga wakiwa ugenini kujiandaa na mechi yao ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly, nyumbani wameenguliwa kutoka nafasi ya pili ya Ligi Kuu baada ya Mbeya City kupata ushindi wa 3-1 dhidi ya Rhino Rangers.
Mbeya City ikiwa uwanja wa nyumbani wa Sokoine, jijini Mbeya ilipata ushindi huo na kufikisha jumla ya pointi 39 na kuwa nyuma ya pointi moja dhidi ya Azam wanaoongoza msimamo ikiwa na pointi 40 licha ya kutofautiana michezo iliyocheza.
Mabao ya washindi hao waliwekwa kimiani na Saada Kipanga aliyefunga mabao mawili akiiangamiza timu yake ya zamani aliyoipandisha daraja ambayo inaendelea kukaa mkiani kwa msimamo wa ligi hiyo inayoelekea ukingoni kabla msimu haujamalizika.
Kabla ya Kipanga kufunga mabao hayo, beki wa Mbeya City Yohana Morris alijifunga katika dakika ya pili ya mchezo huo katika harakati za kuokoa shambulizi kali la Rhino Rangers.
Kipanga alisawazisha dakika ya 8 kabla ya kuongeza jingine dakika ya 24 na baadaye Deusi kaseke kufunga bao la tatu dakika ya 35.
Kipindi cha pili hakukuwa na jipya zaidi ya matukio ya kibabe yanayodaiwa kufanywa na wachezaji wa Rhino na kocha wao msaidizi, Tumaini Shija kupewa kadi nyekundu kwa kumtolea matusi mwamuzi Godfrey Tumaini.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo 'wazee wa wiki' Ruvu Shooting ikiwa uwanja wa nyumbani Mabatini-Mlandizi, ilipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya maafande wenzao wa Oljoro JKT na kuwafanya wakwee hadi nafasi ya saba ya msimamo ikiwa na pointi 28.
Bao lililoipa ushindi Ruvu ambayo katika mechi zake mbili zilizopita ilizipoteza kwa Simba na Yanga na kufungwa mabao 10-2, liliwekwa kimiani na Ayoub Kitala katika dakika ya 65.
Nao mabingwa wa zamani wa soka nchini Coastal Union ya Tanga ilishindwa kutamba baada ya kulazimishwa suluhu ya bila kufungana na Ashanti Utd kwenye uwanja wa Mkwakwani.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mechi kati ya Prisons-Mbeya itakayoikaribisha Simba kwenye uwanja wa Sokoine na jijini Dar kwenye uwanja wa Chamazi, JKT Ruvu iliyokea Kagera ilipoenda kukumbana na kipigo kwa Kagera Sugar itaumana na Mtibwa Sugar.

Timu ya Babi, UiTM yazidi kuzama Malaysia

Photo: Thamani.yangu na uwezo .wangu na nithamu yangu ndio inayonifanya .nipewe ukepten..ndani ya nchi na nje ya .nchi..nawatakia kila la heri YANGA..
Abdi Kassim (kushoto wa kwanza) akiwa na utepe wa unahodha katika timu yake uya UiTM
TIMU ya UiTM ya nchini Malaysia anayoichezea kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Abdi Kassim 'Babi' imeendelea kuwa urojo katika Ligi Kuu ya nchi hiyo baada ya jana kukubali kipigo cha tatu mfululizo kwa kufungwa na 'vibonde' wa ligi hiyo Perlis.
Babi aliyekuwa nahodha katika mchezo huo, aliishuhudia UiTM ikilambwa mabao 2-1 katika mechi hiyo iliyochezwa uwanja wa Darul Aman mjini Alor Setar.
Hicho kilikuwa ni kipigo cha tatu mfululizo kwa timu hiyo, kwani baada ya kushinda mechi yao ya kwanza dhidi ya Kuala Lumpur kisha kutoka droo na Johor, ilijikuita ikifungwa mechi mbili mfululizo kabla ya jana kuotewa tena na kuifanya timu hiyo isaliwe na pointi zake nne ikiwa nafasi ya 9 katia ya timu 12 za ligi hiyo.
Katika mechi nyingine zilizochezwa jana baada ya wiki kusimama kwa wiki mbili,timu ya PDRM ilizididi kujizatiti kileleni baada ya kushinda mechi yake ya tano mfululizo kwa kuizamua DRM -Hicom kwa mabao 2-1 ikiwa ugenini, Sabah ikishinda nyumbani kwa mabao 3-2, PBAPP ikilala nyumba 2-1 na Palau Pinang, Felda United ikitoshana nguvu ya kufunga 2-2 na Johor naNegeri Sembilan na Kuala Lumpur SPA zikitosa sare ya bila kufungana.











































KCCA yakwama kwa Nkana Ligi ya Mabingwa Afrika

The KCC FC team that started against Zambia's Nkana Red Devils in Kitwe
KCCA iliyong'olewa jioni hii kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kukubali kipigo nyumbani
MABINGWA wa Kombe la Mapinduzi, KCCA ya Uganda muda mfupi uliopita imejikuta ikiaga mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa mabao 2-1 na Nkana Red Devils ya Zambia katika mechi ya marudiano iliyochezwa jijini Kampala Uganda.
KCCA ilipata sare ya mabao 2-2 ugenini wiki iliyopita mjini Lusaka, ilijikuta ikienda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao 1-0 kabla ya kulirejesha na kuonekana kama ina nafasi ya kusonga mbele kabla ya kuruhusu bao la ushindi la wageni linalowafanya Waganda hao kung'oka kwa jumla ya mabao 4-3.
Washindi wa mchezo huo, Nkana sasa itavaana na Zamalek ya Misri katika mechi ya mkondo unaofuata baada ya jana Wamisri hao kulazimishwa sare ugenini ya bila kufungana na Kabuscorp ya Angola na kufuzu kwa jumla ya bao 1-0 kwa vile mechi iliyopita Zamalek ilishinda nyumbanio bao 1-0.

Arsenal yatinga Semi Fainali ya FA, yaifumua Everton 4-1

Arteta kifungwa mkwaju wake wa penati

Arsenal v Everton
Lukaku akishangilia bao lake ambalo halikuisaidia Everton kwa Arsenal leo
Giroud scores
Mtokea benchi Oliver Giroud akiwatoka washindi na kufunga moja ya mabao yake mawili leo

KIUNGO Mesut Ozil amefunga bao boa na kusaidia jingine lililtumbulizwa kimiani na Oliver Giroud wakati Arsenal ikiifumua Everton kwa mabao 4-1 na kutinga hatua ya Nusu Fainali ya Kombe la FA kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2009.
Ozil ambaye amekuwa na wakati mgumu kwa mashabiki wa Arsenal tangu alipokosa mechi ya Arsenal dhidi ya Liverpool walipofungwa mabao 5-1 na kuja kukosa penati kwenye Ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern, alionyeha kiwango cha juu katika mchezo huo uliochezwa uwanja wa Emirates.
Kiungo huyo wa Ujerumani alifunga bao la kuongoza dakika ya 7 kwa pasi ya Santi Cazorla kabla ya Romelu Lukaku kuisawazishia Everton bao dakika ya 32 na kufanya timu hizo ziende mapumziko zikiwa sare ya 1-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa Arsenal kujiongezea bao la pili kwa amkwaju wa penati  dakika ya 68 iliyofungwa na Mikel Arteta kabla ya mtokea benchi Giroud kufunga mengine mawili dakika za saba za mwisho za mchezo huo.
Mchezaji huyo alifunga bao lake la kwanza na la tatu katika mchezo huo dakika ya 83 akimalizia kazi ya Bacary Sagna na dakika mbili baadaye kuongeza jingine baada ya kazi nzuri ya Ozil na kuiofanya Arsenal kuibuka kidedea kwa maba0 4-1 na kutina Nusu Fainali ya michuano ya Kombe hilo.

Michezo mingine ya Robo Fainali ya michuano hiyo itachezwa kesho kwa mechi itakayozikutanisha Sheffield United dhidi ya Charlton Athletic mechi itakayochezwa mapema kabla ya Hull City kuvaana na Sunderland na Manchester City usiku kuvaana na Wigan Athletic.

Manchester Utd yaifumua West Brom 3-0

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/73455000/jpg/_73455370_73455369.jpg
Wayne Rooney akifunga bao la pili la Manchester Utd leo
Man Utd defender Phil Jones heads his side into the lead at West Brom
Jones akifunga bao la kwanza la Mashetani Wekundu kwa kichwa

MASHETANI wekundu wakiwa ugenini muda mfupi uliopita imepata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya West Bromwich kiatika mechi ya Ligi Kuu ya England na kuifanya timu hiyo kuiengua Everton kwenye nafasi ya sita ikiifupumua Tottenham Hotspur inayoshuka dimbani baadaye dhidi ya Chelsea.
Mabao ya Phil Jones la dakika ya 34 kwa pasi ya Robin van Persie  lililidu kipindi cha kwanza na mengine ya kipindi cha pili kupitia wa Wayne Rooney dakika ya 65 na Danny Welbeck  kwa pasi ya Rooney dakika ya 82 ilitosha kuifanya Manchester United kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 na kufikisha pointi 48 sawa na Everton, lakini wakitangulia mbele kwa uwiano wa mabo ya kufunga na kufungwa.
Ushindi huo wa ugenini umekuwa afueni kwa kocha David Moyes kuelekea kwenye mbio za kupata nafasi ya ushiriki wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani baada ya mbio za ubingwa kuwa mbali kwao kwa sasa na kuelekea kutemeshwa taji lake.

Tambwe, Mgosi walimwa faini, kisa...!

Tambwe wa Simba
Mgosi
STRIKA nyota wa Simba, Amissi Tambwe amepigwa faini ya Sh 500,000 kwa kuonyesha ishara ya matusi wakati akishangilia bao lake.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema Tambwe alionyesha alama ya matusi kutumia kidole chake wakati anashangilia.

Tambwe alifanya hivyo baada ya kuifungia Simba bao wakati ilipoivaa Mbeya City mjini Mbeya.

Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya bao 1-1, Tambwe raia wa Burundi akiwa ni shujaa wa Simba.

Hadi sasa Mrundi huyo ana mabao 17 akiwa kileleni kwa upachikaji mabao.

Naye, mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Musa Mgosi amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kosa la kupiga uwanjani kwenye mechi dhidi ya Ashanti United ambapo vilevile atakosa mechi tatu za ligi. Coastal Union imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa washabiki wake kumrushia chupa za maji kipa wa Mbeya City.

IDFA yaitakia kila la heri Yanga kesho Misri

Yanga yenye kibarua kizito kesho mjini Alexandria
UONGOZI wa Chama cha Sokla Wilaya ya Ilala (IDFA) umeitakia kila la heri na kuwaomba watanzania kuiombea dua njema wawakilishi pekee wa michuano ya kimataifa, Yanga katika mchezo wao wa kesho dhidi ya Al Ahly ya Misri.
Yanga wataumana na wenyeji wao katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo Al Ahly ndiyo watetezi wake, ili kuamua hatma ya  kuvuka hatua ya 32 Bora kutinga 16 Bora ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika kwa ngazi ya klabu, mechi ikichezwa mji wa Alexandria badala ya Cairo.
Kwa kutambua Yanga ina kibarua kizito mbele ya Ahly hiyo kesho, uongozi wa IDFA ambao ni walezi wa klabu za Ilala ikiwamo Simba na Yanga, wamewaomba watanzania kuiombea dua njema timu hiyo na wao wenyewe (IDFA)  wakisema wanaitakia kila la heri kuweza kuwang'oa Wamisri.
Katibu Mkuu wa chama hicho, Daud Kanuti aliiambia MICHARAZO kuwa, IDFA ipo katika maombi kuiombea Yanga ifanye vyema na kuendelea kupeperusha bendera ya taifa na kuwaomba wadau wengine wa soka bila kujali itikadi zao kuwaombea dua njema wawakilishi hao wavuke hatua hiyo.
Kanuti alisema kufanya vyema kwa Yanga katika mechi hiyo na michuano hiyo ya Mabingwa, ni sifa kwa Tanzania na kuongeza, anaamini wachezaji wa Yanga wakicheza 'jihad' na tahadhari kubwa dhidi ya wapinzani wao wanaweza kurejea kilichofanywa na Simba.
Kanuti alisema anaamini wachezaji  wameandaliwa kisaikolojia ili kuhimili vitimbi wanavyoweza kukutana navyo Misri kama ilivyo kawaida ya mechi za timu za kiarabu wanapokuwa uwanja wa nyumbani.
"IDFA tunaitakia kila la heri na kuiombea dua njema ili ifanye vyema kwenye mechi yake ya Jumapili, chama tumefurahishwa na ilichokifanya katika mchezo wa kwanza na tunaamini watarejea tena ugenini," alisema.
"Wana nafasi ya kurejea ilichofanywa na watani zao walipoing'oa Zamalek katika ardhi yao mwaka 2003, ila ni muhimu wachezaji wakaandaliwa kupambana na kuweka akili zao katika pambano hilo ili kuivusha Yanga katika hatua hiyo," aliongeza Kanuni.
Kanuti alisema IDFA inatambua mchezo huo wa kesho utakuwa mgumu kwa vile Al Ahly itakuwa nyumbani na rekodi zinaonyesha timu za kiarabu huwa wagumu kufungwa kwao, lakini Yanga ikipambana itawaondosha watetezi hao kama ilivyofanya Simba kwa Zamalek mwaka 2003.
Katika mwaka huo Simba ilishinda nyumbani bao 1-0 dhidi ya Zamalek pia ya Misri waliokuwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa mwaka huo kisha kwenda kukubali kipigo kama hicho ugenini mjini Cairo na kupigiana penati na Simba kuibuka kidedea kuingia hatua ya makundi.
Iwapo Yanga itafanikiwa kuing'oa Ahly huenda ikakutana kwenye raundi inayofuata kati ya timu ya Berekum Chelsea ya Ghana au Ahly Benghazi ya Libya ambazo zilitoka sare ya 1-1 katika mechi yao ya awali na zinatarajiwa kurudiana leo.

Ushirikina waiponza Simba, TFF yakunjua kucha

Kikosi cha Simba na kocha wao, Logarusic (kulia waliosimama)
BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeipiga faini ya jumla ya sh. milioni moja klabu ya Simba kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo vitendo vinavyoashiria ushirikina uwanjani.

Simba ilifanya vitendo hivyo katika mechi yake dhidi ya Mbeya City ambapo imepigwa faini ya sh. 500,000. Pia imepigwa faini nyingine ya sh. 500,000 kwa makocha wake Loga, Selemani Matola na Idd Pazi kuingia uwanjani na kumzonga mwamuzi kwenye mechi hiyo.

Mbeya City imepigwa faini ya sh. 300,000 kwa washabiki wake kuingia uwanjani kwenye mechi dhidi ya Kagera Sugar iliyochezwa mjini Bukoba. Klabu za Yanga na Coastal Union zimepigwa faini ya sh. 500,000 kila moja kwa washabiki wao kurusha chupa za maji uwanjani wakati timu hizo zilipopambana jijini Tanga.

Kiungo wa Mtibwa Sugar, Shabani Nditi amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kumpiga mchezaji wa Simba, wakati Salvatory Ntebe pia wa Mtibwa Sugar amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kumtukana refa kwenye mechi dhidi ya Mbeya City.

Nayo JKT Ruvu imepigwa faini ya sh. 300,000 kwa kuchelewa kufika uwanjani kwenye mechi dhidi ya Simba iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Vilevile wamiliki wa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wameandikiwa barua ya kufanya marekebisho ya vyumba vya wachezaji, kwa vile havina hewa ya kutosha.

Kwa upande wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) klabu zilizopigwa faini kutokana na makosa mbalimbali ni Friends Rangers (sh. 200,000), Lipuli (sh. 200,000), Majimaji (sh. 400,000), Polisi Morogoro (sh. 400,000) na Transit Camp (sh. 200,000).

Kocha Msaidizi wa Polisi Morogoro, John Tamba atapelekwa kwenye Kamati ya Maadili kutokana na vitendo visivyo vya kimaadili katika mechi dhidi ya Burkina Faso.

Kiongozi wa Lipuli, Hamis Kiemba na wachezaji Boniface Sawaka, George Enock na Green Paul watapelekwa katika Kamati ya Nidhamu kutokana na utovu wa nidhamu waliofanya kwenye mechi dhidi ya Kimondo.

Naye mchezaji Sangalau Nyamoka wa JKT Kanembwa aliyelalamikiwa uhalali wake na Polisi Tabora suala lake linapelekwa Kamati ya Nidhamu.

Huyu ndiye kocha mpya wa Taifa Stars


Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
KOCHA mpya wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ni Martinus Ignatius ‘Mart’ Nooij ambaye anatarajiwa kutambulishwa rasmi Machi 24 mwaka huu na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi.
Tangu TFF kusema inatafuta kocha mpya atakayerithi mikoba ya Mdenmark, Kim Poulsen, BIN ZUBEIRY imekuwa ikifuatilia kwa undani mwalimu mpya wa Stars atakuwa nani na sasa inaibuka na jibu ni Mart Nooij.
Tayari Nooij ambaye kwa sasa ni kocha wa St George ya Ethiopia amekwishasaini Mkataba wa miaka miwili na TFF na atakuja nchini mwishoni mwa mwezi huu.
Atatutoa?; Kocha mpya wa Taifa Stars Mart Nooij anatarajiwa kutua nchini mwishoni mwa mwezi huu

Ulikuwa mchakato makini, uliohusisha wataalamu na washauri wa kimataifa juu ya masuala ya ufundi ya soka ambao umefanikisha kupatikana mwalimu huyo wa Kiholanzi aliyezaliwa Julai 3, mwaka 1954 mjini Beverwijk, Uholanzi.
Nooij amewahi kuwa mwalimu maalum katika programu za maendeleo ya soka katika Chama cha Soka Uholanzi (DFA) na pia amewahi kufundisha timu ya EVC 1913 ya Marekani na baadaye Kazakhstan.
Alikuwa kocha wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Burkina Faso katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2003 na mwaka 2004 alikuwa kocha wa muda wa klabu ya FC Volendam ya Uholanzi.
Mwaka 2007 aliteuliwa kuwa kocha wa Msumbiji na akaiwezesha kufuzu kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2010, hiyo ikiwa ni mara ya kwanza Mambas wanashiriki AFCON baada ya msoto wa miaka 12.
Hata hivyo, katika fainali hizo, Msumbiji ilishika mkia katika kundi lake baada ya kuambulia sare moja na kufungwa mechi mbili. Baada ya kukosa tiketi ya  AFCON 2012, Nooij akajiuzulu Septemba mwaka 2011 na nafasi yake kuchukuliwa na Mjerumani, Gert Engels.
Aprili 19 mwaka 2012, aliajiriwa na klabu ya Santos ya Afrika Kusini, ambako hata hivyo alifukuzwa Desemba 18, mwaka 2012 na kunyakuliwa na St George ya Ethiopia anakoendelea na kazi hadi sasa.
Baada ya kusaini Mkataba wa miaka miwili na TFF kuja kuifundisha Stars, Nooij anasubiri barua maalum ya kuruhusiwa kuondoka baada ya kukamilisha taratibu za kuvunja Mkataba uliokuwa unaelekea ukingoni na klabu hiyo ya Addis Ababa.
Yanga SC pia inafundishwa na kocha Mholanzi, Hans van der Pluijm.
Chanzo: Bin Zubeiry

Friday, March 7, 2014

Jack Wilshere awatuliza mashabiki wa Arsenal

JACK Wilshere amewapoza mashabiki wake baada ya vipimo kwenye mguu wake kuonyesha kwamba hana tatizo kufuatia mechi ya kirafiki ya England waliyoshinda 1-0 dhidi ya Denmark juzi.
Kiungo huyo wa Arsenal, aliachwa amelala chini kwenye uwanja wa Wembley kufuatia kuchezewa vibaya na Daniel Agger tukio lililolazimisgha mchezo kusimama wakati akihitaji matibabu.
Wilshere aliendelea kucheza baadaye kabla ya kutoka na nafasi yake kuchukuliwa na Adam Lallana muda mfupi kabla ya dakika ya 60. Kiungo huyo (22) haraka aliwapoza mashabiki wake waliohofu kwamba huenda ameumizwa vibaya kufuatia kuvaana na beki huyo wa Liverpool.
"Niko poa," alisisitiza kwa Sky Sports. "Panauma kidogo lakini ni mchubuko tu. Nimefanyiwa vipimo na tayari imeonyesha ni mchubuko tu hivyo itakuwa poa."

Dihile: Bado niponipo sana langoni

Dihile (chini)
KIPA mkongwe na nyota wa zamani wa Taifa Stars, Shaaban Dihile anayeidakia JKT Ruvu ameweka bayana kwamba hana mpango wa kustaafu soka kwa sasa kama alivyotangaza nahodha wake, Husseni Bunu waliojiunga wote katika timu hiyo mwaka 2005.
Akizungumza na MICHARAZO, Dihile alisema bado yupo sana dimbani katika kuendelea kucheza soka akiamini uwezo na umri unamruhusu kufanya hivyo kwa muda mrefu.
Dihile, alisema kwa nafasi ya kipa kadiri umri unavyosonga mbele ndivyo uimara wa makipa unavyoimarika na kwamba hadhani kama atatundika 'glovu' zake mapema katika misimu ya karibuni.
"Sijafikiria kustaafu kwa sasa, bado najiona nina uwezo na umri wa kuendelea kucheza kwa muda mrefu, japo kustaafu kunategemea mambo mengi ukiacha suala la umri," alisema.
Alisema kupata majeraha makubwa ni sababu inayowaondoa wachezaji uwanjani na kwa bahati nzuri yeye hajawahi kupatwa na kitu hicho hivyo haoni sababu ya kutundika glovu zake kwa sasa, labda kama ataamua mwenyewe kwa masuala mengine ikiwamo kutaka kuzisimamia miradi yake ya biashara anayoiendesha kwa sasa.
"Ya Mungu mengi, naweza kufanya maamuzi hayo labda kutaka kusimamia biashara zangu, lakini kwa sasa zinaendelea vyema ndiyo maana sina mpango wa kustaafu kwani najiona bado sana kisoka," alisema Dihile aliyewahi kuichezea Pan Africans ya jijini Dar.
Nahodha wa JKT Ruvu, Hussein Bunu alinukuliwa na MICHARAZO katika mahojiano yake maalumu wiki iliyopita akidai huu ni msimu wake wa mwisho kucheza kwa vile atatundika 'daluga' zake na kujikita kwenye ukocha aliouanza kwa sasa.

Thursday, March 6, 2014

Ajali nyingine basi la AM Coach lagongana na lori Tabora


Ajali mbaya ya basi la kampuni ya AM Coach lenya namba T 763 AYN imetokea leo asubuhi mkoani Tabora baada ya basi hilo kugongana na lori mali ya kampuni ya soda ya Coca Cola lenye namba za usajili T 256 BPP

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Tabora ajali hiyo ilitokana lori hilo kutaka kulipita basi bila kuwa makini na kisha kwa ufinyu wa barabara hiyo ndipo ikatokea 'mzinga' huo.
Mmoja wa abiria aliyenusurika alinukuliwa akisema kuwa;

"Dereva wa lori kajaribu kutukwepa lakini ufinyu wa barabara, mbele kuna lori scania linakuja,kwa hiyo akajikuta kagonga kushoto kwake na kulia kwake ila lori la kushoto kwetu halikusimama

Dereva wetu akashindwa kurudi upande wa kushoto kwa sababu kulikuwa na lori ambalo alikuwa anataka kulipita, basi letu lilikuwa 'linaovertake'(linataka kupita), basi nia AM Coach na lori ni la Coca Cola"

Bado haijafahamika madhara makubwa ya ajali hiyo ila taarifa zinafuatiliwa.
Ajali hiyo imekuja siku chache baada ya watu saba kupoteza maisha yao katika ajali mbaya iliyotokea eneo la Chalinze mkoani Pwani ikihusisha magari mawili ikiwamo Coaster iliyokuwa imebeba abiria.
EDDY

Neymar ampagawisha 'dogo' Sauzi

Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi, mtoto mdogo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka mitano jana usiku alivamia ndani ya uwanja wakati Brazil ilipokuwa ikimenyana na Afrika Kusini na kwenda moja kwa moja kwa mshambuliaji Neymar wa Brazil. 
Katika kuonyesha furaha ya kufuatwa na mchezaji huyo, Neymar aliamua kumkumbatia na kisha wachezaji wote wa Brazil waliamua kumbeba juu. Katika mechi hiyo, Brazil iliinyuka Afrika Kusini mabao 5-0, huku Neymar akifunga mabao matatu (hat trick).

Party maalum Siku ya Wanawake kufanyika Mango Garden




KATIKA kusherehekea siku ya Wanawake Jumamosi hii tarehe 08-03-2014 Bendi yako PENDWA ya Twanga Pepeta ikishirikiana na Mdau wake mkubwa Christer Bella Mwingira na Rukia Saloon, kwa pamoja wameandaa bonge la Pati kwa ajili ya kusherehekea sikukuu hii.
Pati linataraji kufanyika ndani ya Twanga City Mango Garden ambapo muonekano wake utakuwa tofauti na siku za kawaida kwa kuwa ukumbi utapambwa vilivyo.
Mavazi rasmi yatakuwa ni ya ya rangi NYEKUNDU, NYEUPE na NYEUSI.
Zawadi kedekede zitatolewa na Rukia Saloon na Christer Bella Mwingira kama vitenge na Khanga ambayo ni mavazi rasmi ya mwanamke.
Kutakuwa na ofa maalum kwa ajili ya akina mama toka kwa Mkurugenzi wetu Asha Baraka kwa kila atakayefika katika onyesho atalipia Tshs 5,000. kuanzia saa mbili mpaka saa nne usiku.
Kiingilio kitakuwa ni Tshs 10,000. kwa VIP pamoja na kinywaji na kawaida ni Tshs 7,000/=

Shigongo afafanua madhara ya Ugonjwa wa Ini


Shigongo akizungumza kwa masikitiko jinsi watu wengi walivyo kwenye hatari ya kufa kwa ugonjwa wa ini.

…Akiwa na jopo la madaktari. Kushoto ni Dk. Mtebe Majigo, Mganga Mkuu wa Amana, Meshack Shing'wela (wa pili kulia) na Daktari Kiongozi Andrew Method.

Ndeonasio Towo kutoka Damu Salama akielezea umuhimu wa wananchi kupima damu kubaini maradhi mbalimbali bila kusahau virusi vya homa ya ini.
Mwakilishi kutoka SD Tanzania ambao ni wadau wa ugonjwa huo, Phillip Sawe, akielezea umuhimu wa kupima mapema ugonjwa huo kabla mwili haujashambuliwa.
Daktari Kiongozi wa Hospitali ya Amana, Andrew Method (kulia) akisistiza jambo.
Mapaparazi kazini.
Shigongo akimueleza jambo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana.
Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdalah Mrisho (kushoto) na Mwakilishi kutoka Sanofa, Edwin Kisimbo, wakifuatilia kwa makini kilichokuwa kikiendelea.
Dk. Majigo (wa pili kulia) akielezea ugonjwa huo unavyoambukiza kwa njia ambazo huambukiza Ukimwi.
Meshack Shing'wela akifafanua jambo.
…Akimshukuru Shigongo kwa kuanzisha kampeni za kutokomeza ugonjwa huo.
MKURUGENZI wa Kampuni ya Global Publishers Ltd, Eric Shigongo, na wadau mbalimbali wa afya leo walizungumzia madhara ya ugonjwa hatari wa homa ya ini kwenye mkutano na wanahabari uliofanyika Hospitali ya Mkoa wa Ilala, Amana Jijini Dar.
Miongoni mwa wadau waliokuwa kwenye mkutano huyo ni madaktari mbalimbali, Sanofa ambao huhusika na vipimo vya ugonjwa huo, Damu Salama ambao huhusika na upimaji wa damu na SD Tanzania.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL)

Ujerumani, England, Ureno zaua kirafiki Ulaya


article-2574068-1C10556200000578-473_634x396
Ujerumani wakishangilia goli lao dhidi ya Chile
Ronaldo akipambana na kuweka rekodi ya mabao dhidi ya Cameroon walioizabua 5-1

Messi alishindwa kuibeba Argentina dhidi ya Romania
Italia walitepeta kwa Hispania 1-0, Diego Costa akiichezea timu yake hiyo kwa mara ya kwanza

Sturridge akishangilia bao liliuloibeba England jana
UJERUMANI usiku wa jana imefanikiwa kuizabua Chile kwa kuwalaza bao 1-0, huku England nayo ikipata ushindi kama huo kwa Denmark, na Brazili ikiifanyizia Afrika Kusini kwa kuifunga kwao mabao 5-0.
Bao la Ujerumani katika mechi yake na Chile lilifungwa na Mario Gotze aliyeshirikiana vyema na Mesut Ozil.
Matokeo mengine ya michezo ya kirafiki ya kimataifa inayotambuliwa na FIFA iliyochezwa jana na alfajiri ya leo Hispania iliilaza Italia baop 1-0 na kudhihirisha haikuiotea kwenye Fainali za Ulaya walipoisasambua mabao 4-0 mpaka kumfanya Mario Balotelli kumwaga chozi.
Mexixo na Nigeria zenyewe zilishindwa kufungana, Ivory Coast ikitoka sare ya mabao 2-2  na Belgiaum, huku Ureno ikiifumua Cameroon kwa mabao 5-1 Cristiano Ronaldo akifunga mawili na kuweka rekodi ya kuwa mfungaji wenye mabao mengi kwa timu ya taifa lake akimzidi Pauleta.
amabaoUshirikiano wa kiungo wa Bayern Munich Mario Gotze na kiungo wa Arsenal Mesut Ozil ulizaa matunda jana usiku katika mchezo wa kirafiki baina ya Ujerumani dhidi ya Chile.
Wachezaji wawili walishirikiana vizuri katika goli la ushindi lilofungwa na Gotze kutoka na pasi nzuri ya mwisho ya Ozil. Mchezo ulimalizika kwa matokeo ya 1-0.

Matokeo Mengine ni kama ifuatavyo
Japan     4 - 2     New Zealand    
Iran     1 - 2     Guinea    
Russia     2 - 0     Armenia    
Bulgaria     2 - 1     Belarus    
South Africa     0 - 5     Brazil    
Algeria     2 - 0     Slovenia    
Namibia 1-1 Tanzania
Greece     0 - 2     Korea Republic    
Hungary     1 - 2     Finland    
Montenegro     1 - 0     Ghana    
Czech Republic     2 - 2     Norway    
Israel     1 - 3     Slovakia    
Bosnia-Herzegovina     0 - 2     Egypt    
Cyprus     0 - 0     Northern Ireland    
Colombia     1 - 1     Tunisia    
Turkey     2 - 1     Sweden    
Romania     0 - 0     Argentina        
Ukraine     2 - 0     United States    
Austria     1 - 1     Uruguay    
Switzerland     2 - 2     Croatia    
Germany     1 - 0     Chile    
Republic of Ireland   1 - 2     Serbia    
Belgium     2 - 2     Côte d'Ivoire    
Poland     0 - 1     Scotland    
Wales     3 - 1     Iceland    
France     2 - 0     Netherlands    
England     1 - 0     Denmark    
Australia     3 - 4     Ecuador    
Portugal     5 - 1     Cameroon    
Spain     1 - 0     Italy    
Honduras     2 - 1     Venezuela    
Mexico     0 - 0     Nigeria        
Costa Rica     2 - 1     Paraguay

Yanga wapaa kuifuata Al Ahly ikijiamini

KIKOSI cha wachezaji 18 na viongozi wa klabu ya Yanga wameodnoka nchini usiku wa kuamkia leo kuelekea Misri kwa ajili ya pambano lao la marudiano dhidi ya Al Ahly wakijiamini wanaenda kumaliza kazi.

Msafara huo umeondoka bila nyota wake kutoka Uganda,Hamis Kiiza na Emmanuel Okwi waliokuwa nchini Zambia kuichezea timu yao ya taifa Uganda The Cranes ambao walilala 2-1 kwa wenyeji wao Chipolopolo.
Hata hivyo wachezaji hao wanatarajiwa kuungana nao wenzao nchini Misri baadaye leo mchana wakitokea Zambia tayari kuivusha Yanga kwenye hatua ya 32 na kuipeleka katika 16 Bora mbele ya mabingwa wateteziu hao wa Ligi ya Mabingwa Afrika na mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo.
Wachezaji waliondoka kwenda kuiua Al Ahly ni  Ally Mustapha ‘Barthez’, Juma Kaseja, Deogratius Munishi ‘Dida’, Nadir Haroub ‘Cannavaro, Juma Abdul, Kelvin Yondani, Mbuyu Twite, Oscar Jushua, Nizar Alfan, Franck Domayo, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Mrisho Ngasa, Said Bahanuzi, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, David Luhende na Jerry Tegete.
Kwa mujibu wa uongozi wa Yanga mpaka sasa hawajajua mechi yao itakayochezwa Jumapili usiku itafanyika kwenye uwanja gani baada ya uongozi wa Al Ahly kuficha taarifa hizo mpaka jana mchana.
Hata hivyo, Afisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto aliyetangulia Cairo alsema huenda  mchezo huo ukachezwa kwenye Uwanja wa Arab Contractors uliopo jijini Cairo. na kwamba maandalizi ya kuipokea timu yao inaendelea vyema kujipanga kuivaa wenyeji wao ambao hawaamini mpaka sasa kama walefungwa na timu ya Afrika Mashariki .

Cannavaro atamba Yanga itafanya maajabu Cairo

 
NAHODHA wa klabu ya Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' amesema kwamba kikosi chao kitafanya maajabu kwenye mechi yao ya marudiano dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi ya Klabu Bingwa Afrika, Al Ahly ya Misri siku ya Jumapili.
Yanga itaumana na Al Ahly katika mechi yao ya marudiano ya hatua ya kwanza itakayochezwa usiku wakiwa na ushindi wa 1-0 waliopata katika pambano lao la awali jijini Dar es Salaam kupitia goli lililofungwa kwa kichwa katika dakika ya 82 na nahodha huyo.
Akizungumza na MICHARAZO, Cannavaro alisema wanajua wa mchezo huo utakuwa ni mgumu, lakini wanaenda Cairo kuhakikisha wanatimiza ndoto zao za kuivusha Yanga kwenye 16 Bora.
"Tutaenda kupambana japo tunatarajia ushindani mkubwa baada ya kuwafunga hapa nyumbani," alisema beki huyo wa kati.
Cannavaro alisema wachezaji karibu wote watakaokuwa kwenye msafara wao uliotarajiwa kuondoka usiku wa jana, wamepania kuhakikisha Yanga inaing'oa Al Ahly na kurejea kilichowahi kufanywa na watani zao Simba mwaka 2003.
Katika mwaka huo Simba iliwafunga waliokuwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa, Zamalek pia ya Misri kisha kwenda kukubali kipigo cha 1-0 ugenini na kufanya timu hizo zikipigiane penalti na Simba kushinda kwa mikwaju 3-2.
"Tupo tayari kwa vita na Inshallah tutapambana mpaka kieleweke mjini Cairo kwa sababu tumepania kuifikisha mbali timu yetu, " alisema Cannavaro.
Bao la Cannavaro alililofungwa kwa kichwa cha kuchupia liliiwezesha Yanga kuvunja uteja kwa timu za Afrika Kaskazini zikiwamo kutoka Misri uliodumu kwa miaka zaidi ya 30 na watalazimika kupata japo sare ugenini ili kusonga mbele.

'Simba hatuhusiki uvunjwaji wa viti Taifa'

UONGOZI wa Klabu ya Soka ya Simba umesema kuwa hauhusiki na vurugu za kuvunja viti zilizotokea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati Yanga inacheza mechi yake ya mabingwa wa Ligi ya Klabu Bingwa Afrika, Al Ahly ya Misri.
Simba ilisema jana kuwa imeamua kutoa taarifa hiyo kutokana na kuwapo kwa 'uvumi' kwamba klabu hiyo huenda ikapigwa faini kufuatia baadhi ya mashabiki wake kudaiwa kuvunja viti siku ya mchezo huo.
Baadhi ya picha zilizoonekana kwenye vyombo vya habari zilionyesha mashabiki waliovaa jezi nyekundu na wengine njano wakirushiana viti na kuacha kushangilia.
Afisa Habari wa klabu hiyo, Asha Muhaji, alisema kuwa mashabiki wa Simba hawawezi kuvunja viti kwa sababu mechi hiyo ilikuwa inawahusu wapinzani wao, Yanga na Al Ahly.
Muhaji alisema kuwa si kila shabiki aliyevaa jezi nyekundu ni wa Simba kwa sababu rangi hiyo inavaliwa na klabu mbalimbali za hapa nchini kama Coastal Union, Small Simba na Al Ahly iliyokuwa inashiriki mchezo huo.
"Sisi tunaamini waliofanya vurugu ni mashabiki wa Al Ahly ambao ndio walikuwa na wapinzani wa Yanga, inashangaza Simba tunatajwa kuhusika na vurugu hizo katika mechi tusiyokuwa na maslahi nayo," alisema Muhaji.
Aliongeza kwamba Simba inataka kuweka wazi kuwa vurugu zilizofanyika katika mchezo huo haziwezi kuhusishwa na klabu yao kwa namna yoyote.
Mara kadhaa mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, amekuwa akisisitiza mashabiki wa soka kuwa wazalendo pale timu mojawapo inapokuwa inapeperusha bendera ya nchi kushangilia na kuacha mazoea ya kuzomea.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesema linaendelea kufanya uchunguiz juu ya tukio hilo kabla ya kutoa tamko, japo imelaani vurugu hizo na kuwaonya mashabiki kuwa wastaarabu kwa kuwa uwanja wa Taifa siyo wa klabu chache bali ni wa Watanzania wote.

Taifa Stars angalau, yatoka sare ya 1-1 ugenini Namibia

Na Prince Akbar, Windhoek, Namibia
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania Taifa Stars imetoka sare ya kufungana bao 1-1 na Namibia katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki unaotambuliwa na Fifa uliochezwa Jumatano usiku kwenye uwanja wa Sam Nujoma nchini Namibia.
Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika,timu hizo zilikuwa bado hazijafungana na kocha Salum Madadi akafanya mabadiliko katika kipindi cha pili kwa kuwatoa Erasto Nyoni, Ramadhani Singano ‘Messi’ na juma Luizio na nafasi zao kuchukuliwa na Michael Aidan, Athanas Mdam na khamisi Mcha ‘Vialli’.
Kikosi cha kwanza cha Timu ya Taifa, Taifa Stars kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo dhidi ya Timu ya Taifa ya Namibia, Brave Warriors na kutoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mchezaji wa Taifa Stars, Jonas Mkude  (katikati) akijaribu kupiga mpira katikati ya wachezaji wa timu ya taifa ya Namibia ‘Brave Warriors’ wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu hizo mbili katika uwanja wa Sam Nujoma  jana usiku. Tumu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mlinzi wa Taifa Stars, Saidi Morad  (kulia) akiwania mpira na mchezaji wa timu ya taifa ya Namibia ‘Brave Warriors’ Lous Jereme  wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu hizo mbili katika uwanja wa Sam Nujoma jana usiku. Tumu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mlinzi wa Taifa Stars, Erasto Nyoni (kulia) akijaribu kuudhibiti mpira mbele ya mchezaji wa timu ya taifa ya Namibia ‘Brave Warriors’ Puriza Hosea wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu hizo mbili katika uwanja wa Sam Nujoma  jana usiku. Tumu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Stars, inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager ndio walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 86 baada ya kona  iliyopigwa na Khamisi Mcha ‘Vialli’ aliyetokea benchi na kuingia moja kwa moja nyavuni bila kuguswa.
Namibia walisawazisha bao hilo katika dakika ya tano ya muda wa nyongeza baada ya kutimu dakika 90 za kawaida, lililofungwa na Nekundi Haleluya Panduleni kwa adhabu.
Refa wa mechi hiyo aliingia lawamani kwa kuzidisha muda kupita kiasi, kwani mwamuzi wa mezani alionyesha dakika tano za nyongeza lakini muamuzi alichezesha dakika tano nyingine hivi kuwawezesha Namibia kupata bao.
Lakini katika hali ya kushangaza waamuzi toka nchini Zambia na msimamizi wa mechi toka nchini Afrika Kusini waliopangiwa kuchezesha mchezo huo hawakutokea, na badala yake shirikisho la soka Namibia NFA, wakaamuru mchezo huo uchezeshwe na waamuzi wa Namibia kwa makubaliano ya pande zote mbili.
Mwalimu Salum Madadi alisema licha ya kuwakosa wachezaji wengi nyota, kikosi hiki kilipigana hadi dakika ya mwisho na ameridhishwa na matokeo yaliyopatikana.
Wachezaji walioshindwa kujiunga na kikosi cha Stars ni Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu na Mwinyi Kazimoto ambao hawakuruhusiwa na vilabu vyao kutokana na kukosekana na usafiri wa kuwarudisha vilabuni kwa muda unaotakiwa.
Wengine walioshindwa kufika ni Edward Charles na Hassan Masapili ambao hati zao za kusafiri hazikuwa zimekamilika. Viwango
Matokeo haya huenda yakaiweka Stars kwenye nafasi nzuri ya viwango vya Fifa kwa kupata sare ugenini.
BIN ZUBEIRY