STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 29, 2014

Samuel Eto'oo afunguka 'Sina bifu na Mourinho'

MSHAMBULIAJI mpya wa Evetrion, Samuel Eto'o ametupilia mbali madai kuwa ana bifu na Jose Mourinho wakati timu yake ikijiandaa kuivaa Chelsea katika mechi ya Ligi Kuu tya England kesho Jumamosi.
Eto’o, Mchezaji wa Kimataifa wa Cameroon, na Meneja wa Chelsea Jose Mourinho walikuwa pamoja huko Inter Milan na kutwaa UEFA CHAMPIONS LIGI pamoja na akaja England Mwaka mmoja uliopita kuungana na Mourinho huko Chelsea.
Lakini uhusiano wa Eto’o na Mourinho ulipata msukosuko pale Mreno huyo aliponaswa kwenye Kamera bila kujijua akidhihaki Umri wa Eto’o na kudai ni Mzee kupita Miaka inayodaiwa anayo.
Mara baada ya tukio hilo Eto’o, mwenye Miaka 33, alifunga Bao akiichezea Chelsea na kwenda kushangilia mithili ya Mzee akishika Kibendera cha Kona kama Mkongojo huku akijishika Kiuno ili kumdhihaki Mourinho.
Akiongea na Wanahabari mara tu baada ya kutambulishwa kama Mchezaji mpya, Eto’o alipuuza madai hayo ya kuwa na bifu na Mourinho na badala yake kusema anamshukuru Mourinho kwa kumleta Ligi Kuu England.

Nae Meneja wa Everton Roberto Martinez amedokeza kuwa huenda Mkongwe huyo wa Cameroon akaivaa Chelsea Jumamosi wakati watakapopambana Goodison Park katika Mechi ya Ligi Kuu England.

Mashali kumvaa Mkenya Novemba 4

 Bondia Thomas Mashali katikati akisaini mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya Novemba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam. Wanaoshudia kushoto ni Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za kulipwa nchini TPBO, Yassini Abdallah 'Ustaadh' na promota wa mpambano huo Khamis Ally.
 Rais wa TPBO Yassin Abdallah akirekebisha mkataba wa bondia Thomas Mashali katikati atakayepambana na mkenya Henry Wandera Novemba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam kulia ni  promota wa mpambano huo Khamis Ally 
Bondia Thomas Mashali katikati akiwe Dole Gumba katika mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya Novemba 4.
****
BONDIA Thomas Mashali 'Simba Asiyefugika' anatarajia kupanda tena ulingoni Novemba 4 kumvaa Mkenya Henry Wandera katika pambano litakalofanyika katika ukumbi wa New Madiba zamani Korini.
Mashali anapigana akiwa na historia ya kupoteza mpambano wake wa mwisho zaidi ya bondia Mada Maugo ambapo walicheza katika uwanja wa taifa na kupoteza kwa pointi mpambano huo.
Akizungumzia mpambano huo Mashali amesema hatokubali kupoteza tena mchezo huo ukizingatia anachezea nyumbani mahali alipozaliwa na ndipo alipoanzia ngumi maeneo ya Tandale.
"Sintokubali niaibike mbele ya ndugu zangu hivyo nawaambia wapenzi waje kwa wingi kuangalia Mashali anavyofanya kazi yake ya mchezo wa masumbwi.
Naye promota wa mpambano huo Khamis Ally amewahakikishia kuwa sehemu ya kuegeshea magari ni kubwa na ulinzi ni wa kutosha kifupi katika ulinzi tumejipanga vizuri pia siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine mazuri ya utangulizi ambapo mabondia wengi wamejitokeza kucheza siku hiyo.
Siku hiyo pia kutakuwa na uuzwaji wa DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.
Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Pacquaio, Floyd Maywether, Amir Khan, Muhammed Ali, Mike 'Iron' Tyson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani.
Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi.

Kikwazo cha Tanzania kuandaa AFCON 2017 HIKI HAPA!

http://bigeye.ug/wp-content/uploads/2014/08/afcon-trophy.pngSHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeliandikia Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kutaka kipengele cha kutaka kwanza nchi iandae Fainali za Afrika kwa Vijana ndiyo iwe na sifa ya kuandaa Fainali za Afrika (AFCON) kiondolewe.
TFF ilishapeleka barua CAF kutaka kipengele hicho kiondolewe, na kutaka kijadiliwe katika Congress (Mkutano Mkuu) ijayo ya CAF.
Tanzania imeshaiandikia CAF barua kuomba uenyeji wa Fainali za AFCON za 2017 baada ya Libya iliyokuwa imepewe uenyeji huo kujitoa. Uamuzi wa Tanzania kuomba kuandaa fainali hizo ulifanywa na Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Agosti 24 mwaka huu.

Malinzi kuzuru Kanda ya Kaskazini, mechi za Electronic kupigwa TA, BK

http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2013/10/Jamal-Malinzi.jpgTIMU za Mgambo Shooting na African Sports za Tanga zitapambana Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) katika mechi ya majaribio ya matumizi ya tiketi za elektroniki itakayochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga kwa kiingilio cha sh. 1,000 tu.
Mechi nyingine ya tiketi za elektroniki siku hiyo itachezwa Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba kwa kuzikutanisha timu za Kagera Sugar na Geita Gold SC ya mkoani Geita. Geita Gold iko Daraja la Kwanza.
Kabla ya mechi hizo, Ijumaa (Agosti 29 mwaka huu) saa 3 asubuhi kwenye viwanja hivyo kutakuwa na mafunzo ya matumizi ya tiketi za elektroniki pamoja na jinsi mfumo huo unavyofanya kazi.
Washiriki wa mafunzo hayo ni wasimamizi wa vituo vya Tanga na Bukoba, viongozi wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Kagera (KRFA) na Tanga (TRFA), makatibu na maofisa habari wa klabu za Kagera Sugar, Mgambo Shooting, African Sports na Geita Gold, mameneja wa viwanja vya Kaitaba na Mkwakwani na wasaidizi wao, maofisa usalama wa TRFA na KRFA, wachanaji tiketi, wasimamizi wa milangoni, wasaidizi (stewards) na waandishi wa habari.
Wakati huo huo Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atatembelea mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara.
Katika ziara hiyo atakutana na viongozi na kuangalia hali hali ya mpira wa miguu katika mikoa hiyo na mahitaji yake. Pia atazungumzia maono (vision) ya TFF katika mpira wa miguu.
Rais Malinzi atawasili mkoani Manyara, Agosti 29 mwaka huu, na ataanza ziara rasmi katika mkoa huo Agosti 30 mwaka huu. Agosti 31 mwaka huu atakuwa Arusha, na kumalizia Septemba 1 mkoani Kilimanjaro.
Katika ziara hiyo, Rais Malinzi atafuatana na Mkurugenzi Msaidizi (Wanachama) wa TFF, Eliud Mvella. Pia Septemba 8 mwaka huu, Rais Malinzi ataanza ziara ya mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe.

Kenya, Rwanda, Uganda kuandaa pamoja Afcon 2017?

http://www.thepeople.co.ke/wp-content/uploads/2014/04/Screen-Shot-2014-04-12-at-8.13.22-AM.png
Sam Nyamweya
NAIROBI, Kenya
KENYA, Rwanda na Uganda zinajadili uwezekano kupeleka maombi Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kuandaa kwa pamoja fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2017.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka nchini Kenya (FKF), Sam Nyamweya Jumatano alithibitisha kuwa mipango iliyopo ni kwa nchi tatu kuungana kuomba kuwa mwenyeji wa michuano hiyo ya Afrika ili kupunguza gharama.
 "Ni mwenye furaha kwamba Uganda na Rwanda wamepokea kwa mikono miwili wazo la FKF la kuungana kuomba uenyeji wa Mataifa ya Afrika 2017 ambayo ipo wazi kutokana na Libya kujitoa kuwa mwenyeji," alisema Nyamweya.
Libya haitakuwa mwenyeji wa Afcon 2017 kutokana na mapigano ya kisiasa nchini humo ambayo yamesababisha kuchelewa kwa mipango ya ujenzi wa viwanja vitakavyotosha timu 16 zinazoshiriki michuano hiyo.
Nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika ilipanga kujenga viwanja 11 kwa gharama ya Dola za Kimarekani 314 ikiwa ni pamoja na unaochukua watazamaji 60,000 eneo la kambi ya jeshi jijini Tripoli.
CAF imekaribisha maombi kwa nchi zinazohitaji kuandaa michuano hiyo, na milango ipo wazi hadi Septemba 30. Uamuzi wa nchi itakayopewa nafasi hiyo ya Libya utatolewa mwakani.

Waamuzi, makamisaa kutahiniwa Sept 5

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgGe9znsbu8-SC-K7pcwh_X4R1keXlQEZ6eKkKsYFEcEiMd59lZ-pvZBtMypkT-3vsbM6KKk8-HTX-AtQvj4Qa97tZCeIIr-3noVEg8sxx5YnUqt3q9IZm6Ar3VB-IJWfyVSQQ5vhOcAT9D/s1600/DSC_8192.JPG
Waamuzi wanatakiwa kuwa fiti kama hivi wawapo uwanjani
MTIHANI wa utimamu wa mwili (physical fitness test) kwa waamuzi wanaotaka kuchezesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu utafanyika katika vituo viwili kuanzia Septemba 5-6 mwaka huu.
Waamuzi watakaoshiriki mtihani huo ni wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na wale wa class one. Pia kutakuwa na semina wa makamishna wanaotaka kusimamia mechi za VPL na FDL ambayo itafanyika Septemba 7 mwaka huu.
Vituo vya mtihani huo ni Dar es Salaam na Shinyanga. Kituo cha Dar es Salaam ni kwa waamuzi na makamishna kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Njombe, Pwani, Ruvuma na Tanga.
Kituo cha Shinyanga ni kwa waamuzi na makamishna kutoka mikoa ya Arusha, Geita, Kagera, Katavi, Kigoma, Manyara, Mara, Mwanza, Rukwa, Shinyanga, Simiyu, Singida na Tabora.
Waamuzi wote ambao wamechezesha VPL na FDL msimu wa 2013/2014 na kupata matatizo au kuondolewa kwenye ligi hawahusiki na mtihani huo.
Washiriki wanatakiwa kufika kituoni siku moja kabla.Wasimamizi ni Charles Ndagala, Israel Mujuni, Issarow Chacha, Joan Minja, Pascal Chiganga, Riziki Majala, Said Nassoro, Salum Chama, Soud Abdi, Victor Mwandike na Zahara Mohamed.

KOZI YA UKUFUNZI WA UTAWALA YA FIFA KUFANYIKA DESEMBA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-2-gEQjN-kUTDr5XYxr2xEbeHBZeqpiBVaxDBdXtEHTCTfXJMtFnrt4_lV5Gtu_cfAfZtDPsXoHZdVtbLhyphenhyphenBQsa9f8OgTtpmurttsK_XY2cD3KZVsKqVdjpzI97j-jLPVmU6Qy3ft4BE/s1600/mwesigwa.JPG
Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa aliyesimama
SHIRIKISHO la Soka Tanzania,TFF kwa kushirikiana na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wameandaa kozi ya ukufunzi wa utawala itakayofanyika Desemba mwaka huu.
Kozi hiyo itakayoendeshwa na wakufunzi kutoka FIFA itafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Desemba 1 hadi 5 mwaka huu, ambapo sifa ya chini ya elimu kwa wanaotaka kushiriki ni kidato cha nne.
Kwa wanaotaka kushiriki kozi hiyo wanatakiwa kutuma maombi yao kwa Katibu Mkuu wa TFF. 
Mwisho wa kupokea maombi hayo ni Septemba 5 mwaka huu ambapo wanatakiwa pia kuwasilisha nakala za vyeti vyao vya kitaaluma.

Wenger akiri Giroud kuwa nje, akiwakana Falcao, Song Emirates

http://static.goal.com/310700/310713_heroa.jpg
Arsene Wenger
http://www.footmercato.net/images/a/falcao-cible-potentielle-des-gunners_101362.jpg
Falcao
http://www.standard.co.uk/incoming/article8026635.ece/alternates/w620/alex-song.jpg
Alex Song
MENEJA wa Arsenal , Arsene Wenger amethibitisha kuwa Olivier Giroud anatarajiwa kuwa nje ya uwanja hadi angalau Desemba kutokana na majeraha ya kifundo cha mguu lakini akasisitiza kuwa hana mpango wa kusaka mshambuliaji mwingine yeyeote akiwakana Radamel Falcao, Alex Song na Danny Welbeck.
Giroud (27), ambaye alikuwa mfungaji bora wa Arsenal msimu uliopita akitupia mabao 22 katika michuano yote, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa muda wa kufikia miezi minne kufuatia kufanyiwa upasuaji wa 'enka' aliyoumia katika mechi ya Jumamosi iliyomalizika kwa sare ya 2-2 ugenini dhidi ya Everton katika Ligi Kuu ya England.
Alipoulizwa kuhusu Falcao, Wenger alisema nyota huyo wa Napoli hayumo katika mipaka ya bei anayoweza kutoa na akabainisha kwamba pia hamhitaji Welbeck. Kuhusu uwezekano wa kumsajili Song, Mfaransa huyo alisema: "Alex Song hatarejea hapa."
Kocha huyo akasema kuhusu nyota wa Chile, aliyefunga goli la ushindi katika mechi ya "kapu" ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Besiktas: "(Alexis anaweza kucheza kama mshambuliaji wa kati) kwa miezi mitatu ama minne? Anaweza kucheza pale maisha yake yote.
"Nilimnunua acheze kama mshambuliaji wa kati, siyo kwenye wingi. Naamini huwezi kununua kila pale mchezaji anapoumia. Kama umepata majeruhi Septemba mosi bado utatakiwa kuishi nalo.
"Nilimnunua Sanchez awe mshambuliaji, Walcott anaweza kuwa mshambuliaji mzuri, (Lukas) Podolski anaweza kucheza pale, (Yaya) Sanogo ni mshambuliaji mzuri sana, (Joel) Campbell ukimuuliza yeye ni nani, atasema ni mshambuliaji. Wote ni wachezaji wa ubora wa juu.
"Kupata wachezaji bora zaidi ya tulionao itakuwa ngumu sana."

BRAD PITT NA ANGELINA JOLIE WAOANA!


Jolie na Pit walichumbiana mwaka 2012
NYOTA wa filamu duniani, Brad Pitt na Angelina Jolie ambao wameishi kwa muda mrefu kama mke na mume, wamefunga ndoa rasmi.
Pitt, mwenye umri wa miaka 50 na Jolie mwenye umri wa miaka 39, walifunga pingu za maisha nchini Ufaransa Jumamosi na kumaliza miaka mingi ya sintofahamu ikiwa watawahi kuoana.
Waigizaji hao inaarifiwa walioana katika sherehe iliyofanywa kimya kimya katika kanisa ndogo eneo la Chateau Miraval Ufaransa.
Sherehe hio ilifanyika kwa faragha na kuhudhuriwa tu na familia za wawili hao pamoja na marafiki zao.
Watoto wao pia walihusishwa katika sherehe hiyo.
Jolie aliambatana na wanawe wakubwa wa kiume, Maddox na Pax, wenye umri wa miaka 13 na 10 mtawalia.
Watoto wao wa kike Zahara na Vivienne, wote waliwarushia mauwa wazazi wao walipokuwa wanatembea kuelekea kanisani. Inaarifiwa sherehe hiyo haikufuata dini yoyote.
Wacheza filamu hao walianza uhusiano wao wa kimapenzi mwaka 2005 walipoigiza katika filamu ya 'Mr and Mrs Smith'. Walichumbiana Aprili mwaka 2012.
Kabla ya ndoa yake kwa Jolie, Pit alikuwa amemuoa muigizaji, Jennifer Aniston, wakati Jolie alikuwa ameolewa na Jonny Lee Miller na Billy Bob Thornton. Ndoa yake kwa wawili hao ilivunjika
BIG

Thursday, August 28, 2014

Ronaldo ndiye Mchezaji Bora Barani Ulaya

http://www.free-top10.com/Data/Sites/1/Free/Free%20Video/Free-Video-Ronaldo-European-Football-Player-Of-The-Year.jpg 
http://www.sokkaa.com/wp-content/uploads/Neuer-Christiano-and-Robben.jpg
Waliokuwa kwenye Tatu Bora Ulaya
MSHAMBULIAJI nyota wa Ureno anayeichezea klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa Mchezaji Bora wa Ulaya.
Mkali huyo alipata tuzo hiyo baada ya kuwaangusha wachezaji wenzake wawili wanaoichezea Bayern Munich ya Ujerumani.
Ronaldo alitangazwa jioni hii kushinda tuzo hiyo mbele ya Arjen Robben na kipa Manuel Neuer wa Bayern Munich.

Haya ndiyo makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya 2014

MAKUNDI ya Ligi ya Mabingwa Ulaya yametangazwa jioni hii ambapo Mabingwa wa Engand, Manchester City wamejikuta wakiangukia kundi moja na Bayern Munich huku Liverpool ikiangukia kundi B lenye vigogo Real Madrid.
Kwa mara nyingine Arsenal wameangukia kundi gumu, safari hii wakiwa D lenye timu za Arsenal, 
Borussia Dortmund, 
Galatasaray na Anderlecht.
Chelsea wao wako kundi G lenye timu za 
Schalke, 
Sporting
 na Maribor.
Yacheki makundi yote hapo chini:
Kundi A


Atletico Madrid, Juventus,
 Olympiacos na 
Malmo
Kundi B
Real Madrid, 
Basle, 
Liverpool,
 Ludogorets
Kundi C
Benfica, 
Zenit St. Petersburg,
 Bayer Leverkusen na Monaco
Kundi D
Arsenal, 
Borussia Dortmund,
 Galatasaray na Anderlecht
Kundi E
Bayern Munich,
 Man City, 
CSKA Moscow na 
Roma
Kundi F
Barcelona, 
PSG, 
Ajax, 
Apoel Nicosia
Kundi G
Chelsea,
Schalke, 
Sporting
 na Maribor
Kundi H
FC Porto,
 Shakhtar Donetsk,
 Athletic Bilbao 
na BATE

Michel Platin achomoa kuwania Urais FIFA

KATIKA kinachoonekana kama kumgwaya Rais wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, Sepp Blatter, Rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya,UEFA, Michel Platini amesema hatagomea nafasi hiyo ya dunia kama ilivyokuwa ikivumishwa.
Platin amesea ni vyema kutilia mkazo kibarua chake cha sasa kuliko UEFA badala ya kushiriki uchaguzi huo wa FIFA.
http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2011/5/31/1306848649705/Michel-Platini-and-Sepp-B-007.jpg
Platin (kushoto) na Blatter
Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa alikuwa akiaminika kuwa anafikiria kugombea nafasi nhiyo lakini alifafanua katika mkutano wa vyama 54 vya soka barani Ulaya uliofanyika huko Monte Carlo kuwa atabakia katika nafasi yake hiyo.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya FIFA, Michel D’Hooge alikaririwa akidai kuwa ni ujumbe chanya uliotolewa na Platini na amefurahi kwani inamaanisha kuwa safari hii hakutakuwa na ushindani kati FIFA na UEFA. 
Platini amekuwa akimkosoa vikali Blatter kwa zaidi ya mara moja na mapema mwaka huu alieleza kuwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 78 amekwisha kama mtu sahihi wa kuiongoza FIFA. 
Blatter aliwahi kudai kuwa ataachia ngazi mwishoni mwa muhula wake huu wa nne lakini alibadili mawazo na uamuzi wake baadae na kuweka wazi kuwa atatetea tena kiti chake katika uchaguzi ujao. 
Blatter amekuwa akifanya kazi FIFA toka mwaka 1975 na alichaguliwa kwa mara ya kwanza kushika nafasi ya urais mwaka 1998.

Alexis Sanchez amkuna Wenger Arsenal

http://pbs.twimg.com/media/BuDK8W3IIAAy0Qv.jpgKIWANGO alichokionyesha mshambuliaji Alexis Sanchez kimemkuna Kocha wa timu ya Arsenal, Arsene Wenger.
Meneja huyo wa Ze Gunners amesema kiwango cha Alexis Sanchez alichoonyesha katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Besiktas imeinyesha kuwa ana ubora wa kumfanya afanikiwe katika Ligi Kuu nchini Uingereza.
Nyota huo aliyesajiliwa kwa paundi milioni 35 akitokea Barcelona alifunga bao pekee katika mchezo huo na kuipa Arsenal ushindi mwembamba wa 1-0 katika Uwanja wa Emirates na kuwafanya kufuzu hatua ya makundi ya michuano hiyo.
Akihojiwa Wenger amesema Sanchez alionyesha mchezo mzuri kwani alikuwa akielewana vyema na wenzake na alikuwa akionyesha ari ya kupambana huku akiwa hatari anapokuwa katika lango la adui. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa ubora huo ndio unaotakiwa katika ligi. Bao hilo la kwanza kwa mchezaji huyo toka ajiunge na timu hiyo alilifunga muda mchache kabla ya mapumziko na kuingiza Arsenal katika ratiba ya makundi yaliyopangwa leo.
Hata hivyo Wenger amekiri kuwa aliingiwa na woga kidogo wakati beki wake Mathieu Debuchy alipotolewa nje kwa baada ya kupewa kadi ya pili ya njano zikiwa zimebaki dakika 14 mpira kumalizika.

Kocha Mexime awakuna wachezaji Mtibwa Sugar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjVzufGN29F3EQO9M7DaKGF8TdIspdiztoQgVTGD8zWO2W1YB8ab9wJMCTc5-pqvYnHKlB2JLmq-wB7XAxld2-4Kh7Xb9sz0CVRFZKAKfjnWABu_wB-VYdQ1hq18g8-TqWULxVQIjQbjic/s1600/IMG_0621.JPG
Benchi la ufundi la Mtibwa Sugar
MSHAMBULIAJI nyota wa Mtibwa Sugar, Abdallah Juma amemwagia sifa kocha wake, Mecky Mexime huku akiitabiria Mtibwa kufanya vema kwenye msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Abdallah maarufu kama 'AJ' aliyeifungia Mtibwa mabao manne msimu uliopita ikiwamo hat trick wakati wakiizamisha JKT Oljoro, alisema tangu kocha wao amerejee toka masomoni amekuwa akiwapa mbinu ambazo zinawafanya kuzidi kuwa wakali na kufufua ari zao.
Nyota huyo wa zamani wa AFC Arusha, Kagera Sugar na Simba, alisema kwa namna kocha wao anavyowapa mbinu za kinazohusu mikasa aliyokutana nayo katika maisha yake.
"Kocha wetu ni kama 'amezaliwa' upya, yupo tofauti na msimu uliopita kwa jinsi anavyotupa mbinu mpya ambazo tunaamini zitaifanya Mtibwa Sugar itishe kwenye ligi ya msimu huu," alisema.
Abdallah alisema mpaka Septemba 20 ligi itakapoanza kwa wao kuwakaribisha Yanga kwenye uwanja wa Jamhuri watakuwa wameiva na kuanza mbio zao za kurejesha heshima yao baada ya kushindwa kufanya vema ligi iliyopita.
Mshambuliaji huyo alisema anaamini msimu wa 2014-2015 utakuwa wa Mtibwa Sugar licha ya kwamba wadau wa soka wanaziangalia Simba, Yanga, Azam na pengine Mbeya City baada ya msimu uliopita kupanda Ligi Kuu na kuonyesha kiwango cha hali ya juu.

Misri yaongeza idadi inayowania AFCON 2017

CHAMA cha Soka nchini Misri kiomeongeza idadi ya nchi zinazowania uaandaaji wa Fainali za Afrika 2017 baada ya kujitosa kwenye kinyang'anyiro hicho ambacho Tanzania nacho imeingia tangu juzi.
Misiri ilianda mara ya mwisho fainali hizo mwaka 2006 na inawania nafasi hiyo na nchi nyingine baada ya waliokuwa wawe wenyeji, Libya kutangaza kujitoa.
Vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini Libya viwalazimisha kujitoa kwa mara ya pili baada ya mwaka jana kushindwa na kuiachia Afrika Kusini kuandaa.
Kutokana na hali hiyo ambayo imeikwaza nchi hiyo kutekeleza mikakati ya ujenzi wa viwanja na kuifanya Shirikisho la Soka Barani Afrika-CAF kutafuta mwenyeji mwingine wa michuano hiyo. 
Chanzo kimoja cha habari kutoka ndani ya EFA kimebainisha nia ya kutaka kuwa mwenyeji wa michuano hiyo lakini bado hawajafanya uamuzi wa mwisho kuhusiana na suala hilo. 
Makamu wa rais wa EFA Hassan Farid naye alithibitisha nia yao hiyo lakini amesema bado wanataka kuzungumza na baadhi ya wizara serikalini ili kupata ushirikiano wao. 
Misri ni mojawpao ya nchi chake barani Afrika zenye miundo mbinu mizuri ya kuandaa michuano mikubwa kama Afcon.

Rooney nahodha mpya England Hodgson atangaza kikosi

http://static.guim.co.uk/sys-images/SPORT/Pix/pictures/2012/6/27/1340795627494/Roy-Hodgson-008.jpg
Sasa wewe ni nahodha wa kikosi usiniangushe, Kocha Hodgson akifurahia jambo na Rooney
NYOTA wa klabu ya Manchester United, Wayne Rooney ametajwa kuwa nahodha mpya wa timu ya taifa ya Uingereza Three Stars na kocha Roy Hodgson. 
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 amechukua kitambaa hicho akimrithi kiungo wa Liverpool Steven Gerrard aliyestaafu rasmi soka la kimataifa baada ya nchi hiyo kutolewa katika michuano ya Kombe la Dunia. 
Mshambuliaji huyo nyota amefunga mabao 40 katika mechi 95 za kimataifa na alitajwa kuwa nahodha wa United na kocha Louis van Gaal mapema mwezi huu. 
Rooney alithibitisha uteuzi huo katika mtandao wake na kudai kuwa ataitumikia nafasi hiyo kwa bidii na kujivunia huku akidai kuwa zilikuwa ndoto zake za muda mrefu. 
Rooney ataanza kuvaa beji rasmi akiwa na timu ya taifa Septemba 3 mwaka huu wakati Uingereza watakapoikaribisha Norway katika Uwanja wa Wembley kwa ajili ya mchezao wa kirafiki wa kimataifa.
Kocha huyo amekitangaza kikosi cha wachezaji wake watakaocheza mechi hiyo na ile ya kuwania kufuzu EURO 2016 dhidi ya Uswisi akiwajumuisha wachezaji wanne ambao hawajawahi kabisa kuichezea timu hiyo.
Makinda hao waliotwa katika timu hiyo ni Jack Colback, Calum Chambers, Danny Rose na Fabian Delph, huku Andros Townsend akirejeshwa kikosini tena.
 
Kikosi kamili ni kama ifuatavyo; MAKIPA: Fraser Forster (Southampton), Ben Foster (West Bromwich Albion), Joe Hart (Manchester City)
MABEKI: Leighton Baines (Everton), Gary Cahill (Chelsea), Calum Chambers (Arsenal), Phil Jagielka (Everton), Phil Jones (Manchester United), Danny Rose (Tottenham Hotspur), John Stones (Everton)
VIUNGO: Jack Colback (Newcastle United), Fabian Delph (Aston Villa), Jordan Henderson (Liverpool), James Milner (Manchester City), Alex Oxlade-Chamberlain (Arsenal), Raheem Sterling (Liverpool), Andros Townsend (Tottenham Hotspur), Jack Wilshere (Arsenal)
WASHAMBULIAJI: Rickie Lambert (Liverpool), Wayne Rooney (Manchester United), Daniel Sturridge (Liverpool), Danny Welbeck (Manchester United).

Eto'o, Xabi Alonso kama Lampard soka la kimataifa

http://www.tiemporeal.mx/files/image/0/416/5117b02d5f66c.jpg
Samuel Eto'o
frank-lampard-volley
Lampard
http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Xabi+Alonso+Portugal+v+Spain+UEFA+EURO+2012+3JngxodQREjl.jpg
Xabi Alonso

SIKU chache baada ya Frank Lampard kutangaza kustaafu soka la kimataifa – jana ilikuwa siku nyingine kwa wanasoka wawili wa kimataifa barani nao walitangaza uamuzi wa kuachana na soka la kimataifa.

Samuel Eto’o na Xabi Alonso kwa wakati tofauti jana walitumia mitandao ya kijamii kutangaza uamuzi wao wa kuachana na soka la kimataifa.
Alianza Xabi Alonso kupitia mtandao wa Twitter kutangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Spain.
Kiungo huyo wa Real Madrid ameshaitumikia Spain kwa muda wa miaka 11 na ameifungia nchi hiyo magoli 16 katika mechi 114.
Wakati huo huo mfungaji mabao mengi zaidi wa timu ya taifa ya Cameroon Samuel Eto’o ametangaza kustaafu soka la kimataifa.
Mshambuliaji huyo ambaye ameifungia Cameroon mabao 56 amejiunga na Everton ya Uingereza juzi .
Kufuatia kauli hiyo mshambuliaji huyo sasa hatakuwepo katika kipindi chote cha cha kombe la mataifa bingwa barani Afrika mwezi Januari mwakani.
“Nataka kuwajuza kuwa nimestaafu mashindano yote ya kimataifa ”aliandika Etoo katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram .

Bosi wa zamani wa TBS atupwa jela miaka mitatu

Charles Ekelege akiwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam leo ambapo alihukumiwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja baada ya kupatikana na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka na kulipa faini ya sh.milioni 68.
Ekelege akiteta jambo na kijana aliyedaiwa kuwa ni mtoto wake.


 Ekelege akiteta jambo na familia yake akiwa Mahakamani hapo.

Hapa Ekelege akiwa amekaa nje ya Mahakama hiyo na familia yake  kabla ya kuhukumiwa.

 Askari polisi akiwa na familia ya Ekelege (wa pili kulia), wakati akitoka kwenye mahakama hiyo ----
Aaliye kuwa Mkurugenzi wa Shirika la viwango Tanzania TBS Bw Charles Hekelege, ametiwa hatiani na kufungwa miaka mitatu jela baada ya kukutwa na kosa la kuhujumu uchumi. Hekelege amefungwa jumla ya miaka mitatu jela kwa makosa matatu kila kosa moja mwaka mmoja kwa maana hiyo atatumikia mwaka moja gerezani.
www.habariza jamii.com

Afande Bright aachia mpya za Injili

Kava la albamu ya Afande Bright linavyoonekana kwa wanayoitaka wanaweza kuwasiliana kwa namba zinazoonekana chini kushoto kwenye kava hilo
Afande Bright katika pozi
MSANII aliyekuwa anakuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya aliyejitosa kwenye muziki wa Injili baada ya kuponea chupuchupu kufa ajalini, Bright Mbwilo 'Afande Bright' ameachia albamu yake ya kwanza ya miondoko hiyo mipya iitwayo 'Ahsante Bwana'.
Akizungumza na MICHARAZO, Bright alisema albamu hiyo ambayo kwa sasa ipo sokoni wakati akijipanga kuitengenezea video yake, ina nyimbo nane.
Bright alizitaja nyimbo hizo ni 'Ahsante Bwana', 'Upendo', 'Vita', 'Hamjui', 'Itakuwaje', 'Twakuheshimu', 'Jinsi Gani' na 'Vita Remix', huku akisema karibu nyimbo zote ni simulizi la kweli zilizowahi kumpata au kuwapata watu wake wa karibu.
"Baada ya kunusurika katika ajali mjini Morogoro, nimeamua kumgeukia Mungu na sasa naimba muziki wa Injili nikiwa nimeachia albamu inayofanya vyema sokoni na kwenye vituo vya redio iitwayo 'Ahsante Bwana' yenye nyimbo nane," alisem Bright.
Aliongeza kabla ya kutumbukia kwenye muziki huo wa kumtukuza MUNGU alikuwa kiimba muziki wa kizazi kipya na aliwahi kutoa albamu moja iliyofanya vyema sokoni iitwayo 'Tanzania' iliyokuwa na nyimbo nane.
Baadhi ya nyimbo hizo ni 'Tanzania', 'Ndani ya Dancehall', 'Zako Style', 'Kiza Kinene', 'Jakaya', 'Nimedata', 'Hawapendi', 'Watanzania', 'Nikiachwa leo' na 'Leave Me Alone'.

TFF yaongeza usajili kwa saa 48

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiNvkecPaytXUwsqfpHaifVRHqmPmJ_u0TP-5BxX76mv8bd84h44qP-FTYcfR-aTLu6MK4XJBsNnW1KVuBppUBi8WNFTZvzyTzC278WST8a4X69WDeqN5-BrLV3HnOv5-7VjeVRKHwumMds/s1600/DSC_0428.JPG
Viongozi wakuu wa TFF
DIRISHA la usajili la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa wachezaji wazalendo limesogezwa mbele kwa Saa 48 kuanzia jana, kutokana na timu kushindwa kukamilisha usajili katika muda husika jana.
Akizungumza leo jijini Dar Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa alisema sababu za kusogeza mbele ni klabu zote za Ligi Kuu kushindwa kukamilisha usajili jana.
“Nadhani wameshindwa kuutumia huu mfumo wetu mpya wa elektroniki, sasa tumewapa Saa 48 zaidi warekebishe, zikiisha hizo, hapo hakuna nafasi tena, tunasonga mbele,” amesema Mwesigwa. 

Amesema kwamba hadi muda wa kufunga usajili jana Saa 6:00 usiku, ni timu moja tu, Kimondo FC ya Daraja la Kwanza ndiyo iliyokuwa imefanikiwa kukamilisha usajili wake katika mfumo huo. 
“Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza Kimondo kwa kumudu kuutumia mfumo huu na kuwasilisha usajili wao ndani ya muda,” amesema. 
Aidha, Mwesigwa amesema kwamba dirisha la usajili kwa wachezaji wa kigeni litafungwa Septemba 6, mwaka huu. 
“Hili dirisha la wachezaji wa kigeni likifungwa, hakuna nyongeza ya muda tena, kwa kuwa hili lipo katika mfumo wa kimataifa chini ya FIFA, likifungwa, limefungwa dunia nzima, hivyo nawasihi viongozi wa klabu wahakikishe hawafanyi makoasa,”amesema.  

Twiga Stars kwenda Bondeni kirafiki

http://api.ning.com/files/STHDuz-8NrUpchIxJtAG7Yhc*bs7v9f6guq0lMwxNXrwwbY8mQyceglvUwtFfk9Y9Lg8A7-*-yAlwpgOnTx01kmvHI749vQs/TWIGA.JPGKIKOSI cha timu ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars) inatarajia kuondoka nchini Ijumaa (Agosti 29 mwaka huu) kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya mechi ya kirafiki na timu ya Taifa ya nchi hiyo (Banyana Banyana). Twiga Stars inakwenda huko kwa mwaliko wa Chama cha Mpira wa Miguu Afrika Kusini (SAFA) kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) katika mji wa Polokwane.
Msafara wa timu hiyo utaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Saloum ambapo utajumuisha wachezaji 18 na benchi la ufundi lenye watu watano.
Wachezaji kwenye msafara huo ni Amina Bilali, Anastaz Katunzi, Asha Rashid, Donisia Minja, Esther Chabruma, Etoe Mlenzi, Fatuma Jawadu, Fatuma Makusanya, Fatuma Maonya, Fatuma Swaleh, Happiness Mwaipaja, Maimuna Said, Mwajuma Abdillahi, Mwanahamis Shurua, Shelda Mafuru, Sophia Mwasikili, Therese Yona na Zena Rashid.
Benchi la Ufundi linaongozwa na Kocha Rogasian Kaijage, na msaidizi wake Nasra Mohamed. Wengine ni Christine Luambano (daktari), Furaha Mnele (Meneja) na Mwanahamisi Nyomi (mtunza vifaa). Timu hiyo inatarajia kurejea nchini Septemba 2 mwaka huu kwa ndege ya Fastjet.

Breaking News: Okwii arejea Simba kama utani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi30ecePnhZEckX89NHVLlKiHlv20Jo1JaBMTfcadNELgBqw6SY-HjetDd8JGlpJezz8znqtCdwiBagxQUz85BaW2fhh9X271wkFUhuDo05NLnVd2-N6uMfJ9eE6k8-5Iz-5Jt9REAwWNI/s1600/EMMANUEL+OKWI.JPG
Emmanuel Okwi karudi nyumbani Msimbazi
WAKATI Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) likiongeza muda wa usajili kwa saa 48, klabu ya Simba imemrudisha kundini kiungo wao mshambuliaji, Mganda Emmanuel Okwi.
Okwi aliyekuwa akiichezea Yanga imedaiwa amekamilisha usajili wake wa kukipiga Simba na tayari jina lake ni miongoni mwa majina 29 yaliyopelekwa TFF kwa ajili ya kuombewa usajili kwa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Septemba 20.
Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya Simba, Zakaria Hanspope amethibitisha kumsainisha miaka miwili mshambuliaji huyo anayeichezea pia timu ya taifa ya Uganda The Cranes.
Kurejea kwa Okwi ndani ya Msimbazi ni kama imeirahisishia kazi Yanga iliyokuwa njia panda kuamua nani ikate jina lake kati ya nyota wake wa kigeni sita waliokuwa wapo kwenyue kikosi chao.
"Ni kweli Okwi tumemsajili kwa miaka miwili na atakuwa kwenye kikosi cha Simba kwa msimu ujao," Hanspope amenukulia akisema kwa kujiamini.
Yanga ilikuwa katika sintofahamu ya kuamua imuache nani kati ya Okwi na Jaja Brazil aliyepigiwa debe na kocha Marcio Maximo, ambaye hata hivyo uongozi ya Jangwani ulikuwa haujaridhika naye.
Hayo yakijiri TFF imeongeza siku mbili zaidi za usajili wa wachezaji wa ndani ingawa zoezi hilo lililikuwa limekamilika usiku wa jana.
Kwa usajili wa Mapro zoezi litaendelea hadi Jumamosi ijayo yaani Septemba 6.

Wednesday, August 27, 2014

Sanchez aibeba Arsenal, Napoli hoi Ulaya

Alexis Sanchez
Cazorla akishangilia nao la sanchez. Yeye alikosa penati usiku huu
Alexis Sanchez
Sanchez akishangilia bao lake
Jack Wilshere
Welshere akisikitika baada ya kukosa bao
Nenda nje bwana we si uonyeki mara moja'

Alexis Sanchez
Sanchez akifunga bao la Arsenal
Mathieu Debuchy
Mathieu Debuchy akisikitika baada ya kulimwa kadi ya pili ya njano iliyoambana na nyekudnu na kutolewa uwanjani usiku huu.
Alexis Sanchez pays off his transfer fee in one swoop.
Oyooooooooooooo!
STRIKA mpya wa Arsenal kutoka Chile, Alexis Sanchez  usiku huu ameibuka shujaa baada ya kuivusha timu yake hiyo kwenye hatua ya makundi kwa mwaka wa 17 mfululizo baada ya kufunga bao pekee dhidi ya Besiktas ya Uturuki.
Katika mchezo huo Arsenal ilijikuta wakicheza pungufu baada ya Methieu Debuchy kulimwa kadi nyekundu baada ya kupewa kadi mbili za njano, moja kila kipindi katika pambano hilo lililochezwa uwanja wa Emirates, mjini London.
Sanchez aliyesajiliw ana Arsenal hivi karibuni akitokea Barcelona alifunga bao hilo pekee katika dakika ya 45 za kipindi cha kwanza akimalizia kazi nzuri ya Jack Wilshere na kuifanya Ze Gunnerz kufuzu kwa ushindi wa jumla wa bao 1-0.
Katika mechi ya kwanza baina ya timu hiyo wiki iliyopita zilishindwa kutambiana kwa kutofungana mjini Instabul.
Katika mechi nyingine za Ligi hiyo ya mabingwa Ulaya,  Malmo ya Sweden iliitambia Salzburg ya Uswisi kwa kuichapa mabao 3-0 na kufuzu kwa jumla ya mabao 4-2 kwani katika mechi ya kwanza Malmo walifungwa mabao 2-1 ugenini.
Bayer Leverkusen wakiwa nyumbani nchini Ujerumani walipata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya  Copenhagen na kufuzu kwa mabao 7-2 kwani mechi ya awali walishinda ugenini mabao 3-2, huku Athletico Bilbao ikiizima napoli kwa mabao 3-1 baada ya wiki iliyopita kutoshana nguvu ya kufungana bao 1-1.

Diamond azidi kutusua kimataifa, Mdogomdogo wambeba

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nasib Abdul 'Diamond' amezidi kuangukiwa na neema ibaada ya kuteuliwa kuwania tuzo za muziki za kimataifa za IRAWMA kupitia wimbo wake mpya wa Mdogo Mdogo.
Nyimbo nyingine zilizopo katika kinyang'anyiro hicho katika category ya 'Best African Song/Entertainer' ni pamoja na Aye wa Davido toka Nigeria, Bundeke wa Awilo Longomba toka Congo, Tam Tam wa Willy Paul Msafi toka Kenya, Sitya Loss wa Eddy Kenzo toka Uganda na Mama Africa wa Brakets toka Nigeria
Hii ni mara ya nne kwa Diamond kupenya kwenye tuzo za kimataifa baada ya mwaka huu kuteuliwa kuwania tuzo za MTV za Afrika Kusini, BET za Marekani na AFRIMMA ambapo ndipo pekee alipoibuka kidedea.
Kuteuliwa kuwania tuzo hizo za sasa zinazidi kumpa nafasi msanii huyo kuzidi kutamba anga la kimataifa.

Sijadungwa Mimba na Mchungaji Gwajima-Flora Mbasha




NYOTA wa muziki wa Injili nchini, ambaye pia ni Mke wa Emmanuel Mbasha amefunguka na kusema kuwa hana mahusiano yoyote ya kimapenzi na na Mchungaji wa Kanisa la kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima,


Flora Mbasha akichat Live katika ukurasa wa Facebook wa EATV, amefunguka na kusema kuwa hata mimba aliyonayo siyo ya mchungaji Gwajima kama inavyopakaziwa na baadhi ya vyombo vya habari.
Flora amesema hayo leo alipokuwa akichat Live kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live kinachofanyika kila siku ya Jumatano kuanzia saa Sita kamili.
Flora amesema kuwa hawezi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu ambae ni ndugu yake hivyo
Mchungaji Gwajima ni mjomba wake na si mpenzi wake kama ambavyo watu wamekuwa wakizusha kwa lengo la kumchafua na kumshushia hadhi.

"Hayo ni maneno tu ya watu mtaani ila Mchungaji
Gwajima ni mtumishi wa Mungu na ni uncle wangu ninawezaje kuwa na mahusiano na uncle wangu..? " Alisema Flora, wakati akijibu ya maswali ya mashabiki ambayo mengi yao yalikuwa yakimtuhumu na huku watu wengi wakitaka kujua ukweli juu ya ugomvi uliopo kati yake na Mumeo kama ni kweli au ni skendo tu za magazeti.

Flora aliweka wazi kuwa kuna vyombo vya habari ambavyo vimekuwa na lengo la kumchafua na kumualibia sifa ndio maana walitumia gharama kubwa kufanya wanavyoweza ili kutimiza malengo yao.
Muimbaji huyo amedai kuwa alimua kukaa kimya kwa kuwa hakukuwa na ukweli wowote.
"Hizo stori mnazosikia hazina ukweli wowote na ndio maana niliamua kukaa kimya sikutaka kujibizana kwenye vyombo vya habari kwa uongo wa
baadhi ya magazeti ya udaku ila ninasikitika sana kwani kuna watu wamekaa na kujipanga kisawa sawa kwa ajili ya kuhakikisha wanaharibu huduma yangu kwa gharama zozote, lakini bado ninasonga mbele kwani mwanzilishi wa huduma yangu ni Mungu na huyo ndiye atakayeimaliza na sio mwanadamu. 

"Hata hivyo ninawashukuru kwa kuwa wamenitabilia nkuja kumiliki jumba na magari ya kifahari ingawa yote ni ubatili"
 

HAJAACHANA NA MBASHA KWA AJILI YA GWAJIMA
Flora Mbasha amesema kuwa watu wengi wanasema kuwa ameachana na Mumewe kisa Gwajima hilo swala halina ukweli wowote hajaachana na Mbasha sababu ya Gwajima na amedai kuwa bado anampenda sana ila anampenda Mungu zaidi.

Ila amekuwa na matatizo katika ndoa yake kati yake na mumewe na ni matatizo yao ya ndani ambayo asingependa kuyaweka wazi katika vyombo vya habari maana kufanya hivyo ni sawa na kumvunjia heshima mumewe, maana mambo ya chumbani ni siri yao wenyewe asingependa kuwa wazi sababu wanamtoto mkubwa sasa.
"Sijamwacha mume wangu sababu ya Gwajima na kweli bado napenda sana Mbasha lakini nampenda zaidi Mungu"
Wakati anazungumzia suala hili Flora ameweka wazi kuwa kwa sasa ni mjamzito na ujauzito huo ni wa Mume wake ambae ni Emmanuel Mbasha maana ameishi nae katika ndoa zaidi ya miaka kumi na katika kipindi chote hicho hajawahi hata siku moja kumsaliti Mumewe na kwenda kwenye michepuko hivyo huo ujauzito ni wa Mume wake Emmanuel Mbasha na siyo Gwajima.