STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 15, 2015

Edin Dzeko atua AS Roma toka Etihad

www.bukobasports.com
MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Manchester City Edin Dzeko amejiunga na klabu ya ligi ya Seria A Roma kwa mkopo.
Roma imetoa kitita cha pauni milioni 2.9, na nyingine pauni 7.9 zikitarajiwa kulipwa iwapo uhamisho huo utabadilika na kuwa wa kudumu.
''Nimekuja hapa kushinda mataji'',alisema Dzeko.
''Ninaweza kuahidi kitu kimoja kwamba nitajitahidi vilivyo katika kilabu hii''.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na kilabu ya Etihad kutoka Wolfsburg mnamo mwaka 2011 kwa pauni milioni 27.
Alikuwa ameweka sahihi ya kandarasi ya miaka minne katika uwanja wa Etihad msimu uliopita.
Hatahivyo,meneja manuel Pelegrini hivi majuzi alikiri kwamba Dzeko alikuwa na uwezo mkubwa kuondoka katika Etihad kufutia usajili wa Raheem Sterling kutoka Liverpool kwa kitita cha pauni milioni 49.

Mtaipendaje Simba? Baada ya Agban kusaini sasa zamu ya Mzenji

Simba Day
Simba wakishangilia ushidni wa mechi yao na SC Villa ya Uganda siku ya Tamasha la Simba Day
KLABU ya Simba kwa hakika imepania msimu huu, kwani baada ya kumlambisha mkataba wa miaka miwili kiungo wake wa Kizimbabwe, Justice Majabvi, iliona haitoshi, ikamsainisha tena kipa Muivory Coast, Vincent Agban. Sasa kama  ulidhani walishamaliza kazi, umekosea kwa sasa klabu hiyo imemuita jijini kipa wa JKU-Zanzibar, Mohammed Abdulrahman ili kumalizana naye.
Kipa huyu ndiye waliyewahi kumtangaza mapema kwamba imemnasa kisha ikabainika kuwa bado ana mkataba mrefu na klabu yake kama ilivyokuwa pia kwa straika wa Vital'O, Laudit Mavugo.
Baada ya kutafakari kwa kina na hasa kutokana na kipa Ivo Mapunda kuwadengulia tangu wampe Sh. Milioni 10 za kusaini mkataba mpya, Simba ilipiga hesabu kumleta kipa Mbrazili, Ricardo Andrade, lakini ikamshtukia ana umri mkubwa mno, hivyo wakaachana naye.
Ndipo wakaamua kurudi kwa Abdulrahaman ambaye leo hii atatua jijini Dar es Salaam kumalizana na viongozi wa Simba tayari kuidakia timu hiyo katika michuano ya Ligi Kuu msimu wa 2015-2016.
Viongozi wa Simba wamekuwa wasiri katika suala la kipa huyo, lakini MICHARAZO inafahamu kuwa Abdulrahaman jana alikuwa Bububu na leo Jumamosi atapata boti kuitikia wito wa viongozi wa Simba ambao wiki sasa wamekuwa wakifanya mazungumzo naye na klabu yake ya JKU itakayoshiriki Kombe la Shirikisho Afrika mwakani,
Simba tayari imeshamshainisha kipa Agban aliyewahi kufanya majaribio timu ya vijana ya Chelsea na kuonekana kijeba na mwezi mmoja uliopita alikuwa akijifua na Azam kusaka nafasi ya kusajiliwa kabla ya kocha Stewart Hall kumpotezea kwa kuamini kazi nzuri ya Aisha Manula na Mwadini Ali.

Tuesday, August 11, 2015

Yaya Toure aibeba Man City, ikishinda ugenini

Yaya Toure akifunga moja ya mabao yake usiku wa jana kuisaidia Manchester City kushinda ugenini mabao 3-0
http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/003/494/423/hi-res-b27d356a2da129aaa8e144db5c571976_crop_north.jpg?w=630&h=420&q=75
Vincent Kompany akishangilia bao lake lililokuwa la tatu kwa Man City
Ivorian midfielder Toure wheels away in celebration as Fernandinho congratulates his team-mate for the early strike
Oyooo Oyoooo! Man City wakishangilia mabao yao jana usiku
MANCHESTER City imeanza vyema msimu mpya wa Ligi Kuu ya England baada ya kupata ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya West Bromwich.
City ilipata ushindi huo usiku wa kuamkia leo, huku Mwanasoka Bora wa Afrika, Yaya Toure akifunga mabao mawili na kuipeleka timu yake kileleni mwa msimamo baada ya raundi ya kwanza.

Kiungo huyo wa kimataifa wa Ivory Coast, Yaya Toure aliyefunga alianza kuifungia Manchester City dakika ya tisa baada ya shuti lake la umbali wa mita 20 lililombambatiza Boaz Myhill na kutinga nyavuni, kabla ya kufunga la pili dakika ya 24.

Nahodha wa Man City, Vincent Kompany akakamilisha ushindi mnono katika mchezo wa kwanza wa timu yake kwa kufunga bao la tatu dakika ya kwa kichwa 59.  

Mchezaji mpya, Raheem Sterling aliyesajiliwa kutoka Liverpool, alicheza vizuri katika kikosi cha City jana, lakini akapoteza nafasi nzuri na ya wazi ya kufunga.

Arsene Wenger awashushua wapambe nuksi

http://xmedia-nguoiduatin.cdn.vccloud.vn/149/2014/8/12/Arsene%20Wenger.jpg
BAADA ya kuanza Ligi Kuu ya England kwa kipigo cha nyumbani cha mabao 2-0 kutoka kwa West Ham United, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amewashushua wanaolazimisha afanye usajili ili kuimarisha kikosi chake kwa kusema huwa hakurupuki.
Wenger amesema kuwa hatakurupuka kukimbilia sokoni kutafuta wachezaji wapya kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kiangazi baada ya kipigo cha kushtusha walichopewa.
Kipa Petr Cech ndio sura mpya pekee iliyotua Emirates katika kipindi hiki cha usajili na ameonekana kuanza vibaya kibarua chake hicho toka atoke Chelsea.
Kuna tetesi kuwa Wenger ameshatenga fungu kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzema.
Lakini meneja huyo amesema hatakurupuka kusajili kwasababu ya kupoteza mchezo wao kwanza katika ligi kwani jambo la msingi ni kuangalia walipokosea na kurekebisha.

Depay ajiapiza kuhusu jezi No. 7

http://images.thepeoplesperson.com.s3-eu-west-1.amazonaws.com/wp-content/uploads/2015/06/12150615/memphis.jpg
Depay
UKISIKIA kujishtukia ndiko huku, Mshambuliaji Mpya wa Manchester United, Memphis Depay amesem ana uhakika kuwa ataweza kuitendea haki jezi namba namba aliyopewa na klabu hiyo kama nyota wengine waliowahi kuivaa.
Depay alipewa namba hiyo mashuhuri baada ya Angel Di Maria kuondoka kwenda PSG na kufuatia nyayo za nyota wengine waliowahi kuvaa jezi kama Cristiano Ronaldo, David Beckham, Eric Cantona na George Best.
Nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi amesema yuko tayari kuitendea haki jezi hiyo kama ilivyokuwa kwa nyota wengine na kutamba kuwa atafanikiwa akiwa Old Trafford.
Depay aliendelea kudai kuwa anafahamu changamoto yake na historia lakini ana uhakika ataendelea kuimarika zaidi na kupata mafanikio kama ilivyokuwa kwa wengine.
Manchester ilianza Ligi Kuu ya England kwa kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Tottenham Hotspur kwa bao la kujifunga la beki wa Spurs Kyer Walker.

Monday, August 3, 2015

Uchafu waikwaza Rio de Jeneiro Olimpiki 2016

Maeneo ya Fukwe za Rio De Jeneiro yatakayofanyika mashindano ya Olimpiki ya mwakani

Rais wa Kamati Kuu ya Kimataifa ya Olimpiki (OIC), Thomas Bach, amesema kuwa uchafuzi wa bahari ni moja ya kikwazo kwa jiji la Rio de Janeiro, Brazili katika maandalizi ya michuano ya hapo mwakani.
Hata hivyo kutokana na hali hiyo waandaji wa mashindano hayo ya riadha wamesema kuwa watafanya kila linalowezekana kwa afya ya wanariadha wakati wa Olympiki.
Takribani asilimia 70 ya maji taka yanamwagika Rio de Janeiro katika fukwe za Guanabara,eneo ambalo wapiga mbizi watafanyia mashindano yao.
Katika hali inayoonyesha ni hatari kwa afya wanariadha walioko kwenye mafunzo katika pwani hiyo wameona mizoga ya wanyama na uchafu ukiwa ukingoni mwa eneo hilo ambalo mashindano hayo yatafanyika.

Shule ya Joyland wahimiza amani Uchaguzi Mkuu 2015

Wahitimu wa masomo ya awali shule ya Kimataifa ya Joyland, wakiimba wimbo wa Shule wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam
Wanafunzi  shule Darasa la nne Shule ya Kimataifa ya Joyland, wakiimba wimbo wa Shule wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam

Wahitimu wa masomo ya awali shule ya Kimataifa ya Joyland, wakiimba wimbo wa Shule wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam

Wanafunzi  wa Darasa la awali  Shule ya Kimataifa ya Joyland, wakiimba wimbo  wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam
Capt 5
Wanafunzi waDarasa pili Shule ya Kimataifa ya Joyland, wakicheza ngoma ya utamaduni (Ndolela) wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Shule ya Kimataifa ya Joyland, Fedrick Otieno akiwasaidia watoto wa darasa la awali kupanda juu ya jukwaa kuimba wimbo maalum wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam

Skauti wa Shule ya Kimataifa ya Joyland, wakiruka sarakasi  wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam
Mhitimu wa masomo ya awali shule ya Kimataifa ya Joyland, Colin Christopher akisoma hotuba wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam

Mkaguzi Mkuu wa Elimu Kanda, Shani Kanungira akitoa hotupa ya awali kabla ya mgeni rasmi wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam

Mwakilishi wa Afisa Elimu ya Msingi Manispaa ya Temeke, Frank Makingi akizungumza Tuangoma Kigamboni Dar es Salaam wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo
Na Tariq Badru
UONGOZI wa Shule ya Kimataifa ya Joyland, umewaomba kuwa kuwakumbusha watanzania na hasa viongozi na wanasiasa kuhakikisha Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu unakuwa wa amani na utulivu.
Mkurugenzi wa shule hiyo, Fredrick Otieno alisema vurugu za aina yoyote kutokana na ushindani wa kisiasa unaweza kuiweka Tanzania pabaya na kuvuruga kila kitu na kuwapa wakati mgumu watoto na watu wengine wasiojiweka ambao wanahitaji utulivu na amani kufanya mambo yao.
Otieno aliyasema hayo wakati wa hotuba yake katika mafahari ya wanafunzi wa masomo ya awali wa shule hiyo ya Joyland yaliyonyika mwishoni mwa wiki Tuangoma Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
"Leo wanafunzi na watoto wanafurahi na sisi wazazi na walezi tunajumuika pamoja shuleni kuwapongeza wahitimu wetu, kama kunakuwa na vurugu hili haliwezi kufanyika na watoto hawatapata haki yao ya kusoma au kufurahia maisha yao duniani," alisema Otieno.
Aliongeza ni vema wanasiasa, viongozi na wananchi kwa ujumla kushiriki uchaguzi uliopo mbele yetu kwa amani na utulivu kwa hizo ni neema ambazo kwa mataifa mengine wanatafuta kwa vile nchi zao zimevurugwa kwa sababu na mambo hayo na mengine yaliyokimiza amani na utulivu.
Aidha aliwakumbusha wazazi nchini kote kujenga utamaduni wa kuwalipa ada watoto wao na kufuatilia nyendo za watoto wao wanapokuwa likizo na hata shuleni ili kurahisisha kazi kwa walimu katika kuwapa elimu itakayojenga misingi imara ya maisha yao ya baadaye. Alisema kwa mfano shuleni kwake wazazi na walezi wamekuwa wazito wa kulipa ada kiasi kwamba shule inadai zaidi ya Sh milioni 100, lakini wanashindwa kuwafukuza watoto kwa vile wanaamini hawana makosa yoyote na ndiyo maana wanataka wazazi na walezi kutimiza wajibu wao katika suala la elimu za watoto wao.
Mkurugenzi huyo alisisitiza kuwa hakuna hazina bora kama mtoto kupewa elimu ambayo huja kumsaidia ukubwani kwa kuzingatia kuwa dunia ya sasa inaendeshwa kisasa na bila elimu bora na ya kutosha ni vigumu kijana kusimama na kukabiliana na changamoto hizo.
Naye Mkaguzi Mkuu wa Elimu Kanda, Shani Kanungira aliwasisitiza wazazi kutumia kujitolea na kutimiza wajibu wao kuwasomesha watoto badala ya kutumia fedha nyingi kwa mambo yasiyo na tija kwa watoto na familia zao kwa ujumla.
Shani alitoa nasaha yake kabla ya kumpisha Mwakilishi wa Afisa Elimu ya Msingi Manispaa ya Temeke, Frank Makingi aliyesisitiza umuhimu wa wazazi na walezi kujenga utamaduni wa ushirikiano dhidi ya walimu wa shule wanazosoma watoto wao.
Makingi alisema siyo kila jambo la wanafunzi kuachwa mikononi mwa walimu tu, kadhalika alikumbusha kuwasaidia watoto katika kuwalea katika maadili mema ili kulifanya taifa kuwa na raia wema na viongozi wazuri na waadilifu wa baadaye.

Monday, July 20, 2015

Michael Olunga aipeleka Gor Mahia robo fainali Kagame Cup

http://www.standardmedia.co.ke/images/saturday/stdrclwhqpq.jpg
Michael Olunga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgKxRDIwrjKq6PNP8GUEXC5s6MqT9DpyWecXpY324qzrHOoXoIVRN1JTFo2JKNATy2Jsgaq2axLJ8TZAjWy9G7sdYv_QZSQK4XJBmlJA8gqO93Qfu2HMbmhFDE2Tvc2HSUBSkRfgJDIcrg/s1600/IMG_3285.JPG
Olunga (kulia) alipoikimbiza Yanga katika mechi yao ya kwanza ya Kombe la Kagame ambapo alifunga moja kuisaidia Gor Mahia kushinda 2-1
MSHAMBULIAJI nyota wa Gor Mahia, Michael Olunga ameendelea kuonyesha dhamira yake ya kunyakua kiatu cha dhahabu katika michuano ya Kombe la Kagame baada ya jioni hii kutupia mabao mawili kambani wakati timu yake ikiizamisha KMKM kwa mabao 3-1.
Olunga alifunga mabao hayo katika kipindi cha pili na kuiwezesha Gor Mahia kuwa timu ya kwanza kukata tiketi ya kucheza robo fainali ikitokea Kundi A kwa kukusanya pointi sita na mabao matano baada ya mechi yao ya awali kuitoa nishai Yanga kwa mabao 2-1.
Katika mechi huo wa kwanaa Olunga anayewindwa na Simba, ingawa ni ngumu kumpata kwani ana mkataba wa miaka miwili, alifunga bao moja.
Kwa kufunga mabao hayo mawili jana, imemfanya kuongoza orodha ya wafungaji wa michuano hiyo akiwa na magoli matatu akimzidi kete Sallah Bilal wa Al Khartoum ambaye alikuwa akiongoza kwa mabao mawili baada ya mchana wa leo kuingoza timu yake kuilaza Telecom kwa mabao 5-0.
Mara baada ya mechi yake ya Yanga, Olunga alinukuliwa akisema kuwa amekuja Tanzania akiwa na nia moja ya kuwa Mfungaji Bora wa michuano hiyo, kitu kinachoonyesha ni kweli baada ya kufanikiwa kufunga mabao hayo mawili.
Kabla ya Olonga kufunga mabao hayo, Meddie Kagere mkali mwingine wa Gor Mahia aliifungia timu hiyo bao la mapema akimalizia pande la Olunga kabla ya KMKM kusawazisha na kwenda mapumziki timu zikiwa sare ya 1-1 mpaka kwenye dakika ya 65 Olunga alipoanza kufanya yake na kuwazamisha Wazanzibar.

FIFA yatangaza tarehe ya uchaguzi wake mpya

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/04/Sepp-Blatter.jpg
Rais wa Fifa, Sep Blatter aliyetangaza kujiuzulu mrithi wake atapatika February
SHIRIKISHO  la Soka Duniani, FIFA limetangaza kwamba uchaguzi mkuu wa Rais utafanyika Februari 26 mwakani.
Maamuzi haya yamefanyika leo katika kikao cha kamati ya utendaji ya Shirikisho hilo kilichofanyika mjini Zurich, Uswisi.
Sepp Blatter aliyejiuzulu siku nne baada ya kuchaguliwa amethibitisha kuwa ataendelea kukaa madarakani mpaka uchaguzi mkuu utapofanyika kupata mrithi wake.
Wakati huo, kundi la watu wanaoshinikiza  kufanyika kwa mageuzi wamekutana leo mjini humo wakimuomba katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan kuongoza mapinduzi hayo.
Kundi hilo limesema Annan ni mtu makini ambaye anapaswa kuongoza tume ya mageuzi wakati  huu Dunia ikielekea kupata mrithi wa Sepp Blatter aliyejiuzulu Urais kutokana na kashfa nzito ya rushwa iliyokumba FIFA.
Shirika la Ujasusi la Marekani, FBI liliwatia mbaroni Maafisa saba wa ngazi za juu wa FIFA kwa tuhuma za rushwa.

Stewart afungka mbinu walizoizamisha KCCA

Stewart Hall akiteta na Migi
KOCHA Stewart Hall ni mjanja sana, baada ya kufichua siri ya kuwaanzisha viungo wengi na kucheza soka la kujihami na kushambulia kwa kutumia mipira mirefu. Akizungumzia mbinu zake, Hall alisema alilazimika kutumia mbinu hiyo kwa sababu wachezaji wake wengi bado hawapo fiti. “Tupo katika kipindi cha maandalizi ya mwanzo wa msimu, wachezaji wangu Kipre Tchetche, Didier Kavumbagu na Ramadhani Singano bado hawajawa fiti kwa asilimia mia, lakini naamini tutafika fainali.” alisema Hall Hall aliongeza kuwa timu inayomtisha zaidi ni Gor Mahia kwa sababu wamekuja wakati ligi ya Kenya inaendelea hivyo wachezaji wao wapo fiti.

UTAMU WA KOMBE LA KAGAME WAZIDI KUNOGA DAR

https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AKh2imIAABZpVaY5ZwsQCBMD2%2BU&midoffset=2_0_0_1_4350124&partid=2&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000http://rushyashya.net/IMG/jpg/apr_fc_team_-_rwanda_-_kigalitoday-2-2.jpg
APR Rwanda
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/07/Yanga-leo-14.jpg
Yanga na Gor Mahia
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgU-pwUoReK1Inoqwa-tv9F7B4FsQQHzQW9GaG7wzubvb9SCAbF6zgGuLW0T-HTTo2ede7ls9zqJuGTrYNNSoghMV8GO4-5kfnAbuNX1yjWmHghK_qRzBu2MQ1YkUVYSo-N7z6p23PgLzs/s640/426464_358635040821389_1508036080_n.jpg
Al Shend
http://kabumbu.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/kikosi-azam-fc.jpg
Azam ya Tanznaia Bara
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiYr-ePKerYIvN49hCZ9IJI-ICEdPieA86ey85RJHvQ131iGA6GEbCXWWbDogjLkjX3y6u7CQrhi07Wnmkj3cDy2Drr-O8hj23no_e0NxN6qDxt_0KSgzSb0084QpabXSEI7dIMJoRXD4bc/s1600/1385637_526389100785782_1638137288_n.jpg
Telecom ya Djibout
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg3v7qvqTyHyaPiHb4iJPQ2UjF7MIw0nVpNbqWGraZLfn3zrJ6t9J4bGJ0Ok268cn_goKj9RqzWVvhzIbNvWOTsBfGmrrJGfaTXfZfAcFez2kVA97hfblC6PDlqUiHoUIKjm5SeoML2U9q_/s1600/IMG_9898.JPG
KMKM ya Zanzibar
http://entebbenews.com/wp-content/uploads/2014/09/KCCA-Mulindwa-9.jpg
KCCA ya Uganda
Kikosi cha Yanga

Kikosi cha Gor-Mahia

Mchezaji wa Yanga, Amis Tambwe akiwa chini huku wachezaji Collins Okoth (kulia) na Harun Shakava (kushoto) wa Gor Mahia ya Kenya wakiwania mpira wakati wa mchezo wa ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Kagame uliochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Yanga imefungwa mabao 2-1.
Mashabiki wa Yanga

MICHUANO ya Kombe la Kagame imezidi kushika kasi ikiwa inaingia siku yake ya tatu leo tangu yalipofunguliwa rasmi siku ya Jumamosi, huku Al Khartoum ya Sudan ikitoa onyo kwa kuopata ushindi wa kishindi mchana huu dhidi ya Telecom ya Djibout.
Wawakilishi hao wa Sudan waliokuwa sambamba na Al Shandy kuchukua nafasi za mabingwa watetezi Al Merreikh na Al Hilal waliitandika bila huruma Telecom kwa mabao 5-0 na kukwea kileleni mwa Kundi A, ingawa kwa sasa Gor Mahia inayokamata nafasi ya pili na KMKM waliopo nafasi ya tatu wakiendelea kutifuana kwenye Uwanja wa Taifa.
KMKM ambayo ilichukuliwa poa katika kundi hilo, inaendelea kuonyesha kuwa haisindikizi mtu kwani ilitanguliwa kufungwa bao la kwanza na Gor Mahia iliyowazamisha Yanga kwa mabao 2-1 katika pambano la ufunguzi juzi, lakini ikakomaa na kulirejesha dakika tisa baadaye.
Wakenya walipata bao la mapema dakika ya tatu kupitia Meddie Kagere aliyemaliza pande tamu la Michael Olunga ambao ulimbabatiza beki mmoja wa KMKM na kumpoteza kipa wao, lakini Simon Mateo alifunga bao dakika ya 12 tu ya mchezo na muda huu wametoka kukosa bao la wazi.
Mpaka sasa wakati karibu timu zote zikiwa zimeshacheza mechi moja moja, Yanga na Telecom ndio wanaoburuza mkia katika kundi A zikiwa hazina pointi, ingawa Yanga wanakamata nafasi ya nne.
Katika Kundi B, APR ya Rwanda inaongoza msimamo baada ya kuishinda Al Shandy kwa bao 1-0 katioka mchezo wa kwanza, huku timu za Heggan ya Somalia na LLB AFC ya Burundi zinafuatia baada ya jana kutoka suluhu ya kutofungana.
Malakia ya Sudan Kusini inaongoza kundi C ikiwa na pointi tatu sawa na Azam iliyoitambia KCCA ya Uganda jana, lakini wanatofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa. Malakia iliitambia Adama City ya Ethiopia kwa bao 2-1, wakati Azam yenyewe iliishinda KCCA bao 1-0.
Mpaka muda huu unaosoma blogu hii jumla ya mabao 18 yameshatinga wavuni kwa mechi 8 zilizokwisha kucheza mpaka sasa baada ya jioni hii Gor Mahia kuitambia KMKM kwa mabao 3-1.


Utamu wa michuano hiyo upo hivi kwa mwaka huu wa 2015
MAKUNDI:

KundiA: Yanga-Tanzania, Gor Mahia-Kenya, Khartoum-Sudan, Telecom-Djibout, KMKM-Zanzibar
Kundi B: APR-Rwanda, Al Shandy-Sudan, LLB-Burundi, Heegan-Somalia,
Kundi C: Azam-Tanzania, Malakia-Sudan Kusini,  KCCA- Uganda, Adama City- Ethiopia.

Viwanja:
Taifa- Temeke
Karume-Ilala


MATOKEO:

APR              1-0  Al Shandy
KMKM           1-0  Telecom
Yanga           1-2  Gor Mahia
Adama City   1-2  Al Malakia
LLB              0-0   Heegan
Azam           1-0   KCCA
Telecom        0-5  Al Khartoum
Gor Mahia     3-1  KMKM
 

MSIMAMO:
Kundi A:
                      P  W  D  L   F  A PtsGor Mahia       2   2   0  0   5  2  6Al Khartoum    1   1   0  0   5  0  3
KMKM             2   1   0  1   2  3  3
Yanga             1   0   0  1   1  2  0
Telecom          2   0   0  2   0  6  0

Kundi B:
                     P  W D  L  F  A Pts
APR               1   1  0  0  1  0  3
LLB AFC         1   0  1  0  0  0  1
Heegan          1   0  1  0  0  0  1
Al Shandy      1   0  0  1   0  1  0

Kundi C:

                     P  W D  L  F  A  Pts
Al Malakia       1  1 0  0  2  1   3
Azam              1  1 0  0  1  0   3
Adama City     1  0  0  1  1  2  0
KCCA              1  0  0  1  0  1  0

Wafungaji:

3-Michael Olunga         (Gor Mahia)

2- Salah Bilal               (Al Kahrtoum)
1- Ousmaila Baba         (Al Khartoum)
    Haruna Shakava       (Gor Mahia)
    Michael Olunga         (Gor Mahia)
    Kirkir Glay (og)         (Gor Mahia)
    John Bocco               (Azam)
    Bizimana Djihad        (APR)
    Takele Elemayehu     (Malakia)
    Samuel Ssekamatte  (Malakia)
    Jafar Delil                 (Adama City)
    Juma Mbwana           (KMKM)
    Wagdi Abdallah         (Al Khartoum)
    Murwan Abdallah      (Al Khartoum)
    Meddie Kagere          (Gor Mahia)
    Simon Mateo            (KMKM)
    Meddie Kagere          (Gor Mahia)
RATIBA
KESHO Jumanne

Saa 8 Mchana  Al Shandy vs LLB-Karume
Saa 10 Jioni     Heggan vs APR-Karume
Saa 10 Jioni     Malakia vs Azam-Taifa

Jumatano

Saa 10 Jioni     Khartoum vs KMKM-Karume
Saa 8 Mchana  KCCA vs Adama City-Taifa
Saa 10 Jioni     Telecom vs Yanga-Taifa

Julai 23

Saa 8 Mchana  Hegaan vs Al Shandy-Taifa
Saa 10 Jioni     APR vs LLB-Taifa

Julai 24

Saa 8 Mchana  Khartoum vs Gor Mahia-Taifa
Saa 10 Jioni     KMKM vs Yanga-Taifa

Julai 25

Saa 8 Mchana  KCCA vs Malakia-Taifa
Saa 10 Jioni     Adama City vs Azam-Taifa

Julai 26

Saa 8 Mchana  Gor mahia vs Telecom-Taifa
Saa 10 Jioni     Yanga vs Khartoum-Taifa

Julai 27 Mapumziko
Julai 28-Robo fainali
B1 vs A3
A1 vs Best Looser

Julai 29
B2 vs C2
Ca vs A2

Julai 30-Mapumziko

Julai 31-Nusu Fainali
Winner B2/C2 vs C1/A2
    ""      B1/A3 vs A1/Best Looser
Agosti 01-Mapumziko

Agosti 02-Fainali

Saturday, July 11, 2015

DK SLAA NDIYE MGOMBEA URAIS WA UKAWA

WAKATI CCM ikiendelea na mchakato wake wa kumteua mgombea mmoja wa Urais miongoni mwa wagombea watano waliopitishwa na Kamati Kuu ya chama hicho, Umoja wa Katiba ya Watanzania (UKAWA) wamemaliza udhia kwa kumteua Mgombea wao wa Urais kwa Uchaguzi wa 2015.
.

Baada ya jina la katibu Mkuu wa Chadema Dk Wibroad Slaa likiwa limeteuliwa na UKAWA kuwa mgombea wake wa nafasi ya Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba.
Dakika chache zilizopita kwenye ukurasa  wa @twitter wa Dr Slaa kathibitisha kuteuliwa na UKAWA.
.

Nashukuru UKAWA kwa imani kubwa. Kazi ya mabadiliko iliyoanza 1992 kwa vyama vingi imebakiza miezi michache kushinda. Kura yako ni ukombozi –  @willibrordslaa
Nashukuru UKAWA kwa imani kubwa. Kazi ya mabadiliko iliyoanza 1992 kwa vyama vingi imebakiza miezi michache kushinda. Kura yako ni ukombozi.

Man United yamtambulisha rasmi Memphis Depay

Meneja wa Manchester United Louis van Gaal Leo huko Old Trafford Jijini Manchester alimtambulisha rasmi Mchezaji mpya Memphis Depay mbele ya Wanahabari katika Mkutano maalum na pia kuthibitisha Mchezaji wa Kimataifa wa Italy Matteo Darmian anaelekea England kukamilisha Uhamisho wake kutoka Torino.
Hata hivyo, Van Gaal alikataa kuzungumza lolote kuhusu habari za kuuzwa kwa Mholanzi mwenzake Robin van Persie kwa Klabu ya Uturuki Fenerbahce.
Akijibu swali kuhusu kuuzwa kwa Van Persie, Van Gaal alisema: "Tukihisi anapaswa kwenda, utasikia toka Manchester United. Kwa sasa bado."
Alipohojiwa kuhusu mipango yao ya Uhamisho na kama inakwenda kama walivyotarajia, Van Gaal alikataa kusema kwa undani na badala yake kueleza: "Huwezi kujibu hilo kwani kununua na kuuza ni kitu kinachoendelea na hatujafika mwisho wake. Mwisho ni Agosti 31. Hatuwezi kusema lolote kuhusu Uhamisho wetu, mikakati yetu kwani nyie mtaandika kila kitu."
Aliongeza: " Manchester United haiwezi kununua kwa sababu ya kununua tu. Ukinunua lazima iwe ni kitu bora kuliko ulichonacho."
Nae Memphis Depay, mwenye Miaka 21 na alienunuliwa Mwezi uliopita kutoka PSV Eindhoven ya Holland Klabu aliyoisaidia kuwa Mabingwa Msimu uliopita huku yeye akiwa ndie Mfungaji Bora wa Ligi, alisisitiza amejiunga na Manchester United ili kutwaa Vikombe vyote vinavyowezekana na yeye atajituma hadi mwisho.
Depay aliongea: "Hii ni Klabu kubwa Duniani na hivyo ni lazima nicheze kwa ajili ya Vikombe. Nimekuja kushinda Vikombe."
Alipoulizwa kuhusu kufanana na Cristiano Ronaldo aliejiunga Man United akiwa na Miaka 18, Depay alieleza: "Sitaki kujifananisha na Mtu kama yeye. Cristiano Ronaldo ni mmoja wa Wachezaji bora Duniani na sitaki kusema sana, nitaachia Miguu yangu iongee!"

Friday, July 10, 2015

Turan ajifunga miaka mitano Barcelona

http://static.sportskeeda.com/wp-content/uploads/2014/02/arda_turan-2116949.jpgKIUNGO wa kimataifa wa Uturuki, Arda Turan amekamilisha usajili wake katika klabu ya Barcelona baada ya kutia saini katika mkataba wa miaka mitano leo. 
Barcelona walikubali kutoa kitita cha Euro Milioni 41 kwa Atletico Madrid kw ajili ya nyota huyo wiki iliyopita. 
Hata hivyo, Turan amesisitiza hana shaka kuhusu uwezekano wa kurejea Atletico kwa muda mpaka Januari pindi Barcelona watakaporuhusiwa kumtumia. Kwa sasa Barcelona wanatumikia adhabu ya kutosajili kwa msimu miwili baada ya kukutwa na hatia ya kukiuka Sheria za Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kwa kusajili wachezaji walio chini ya umri wa miaka 18 kinyume cha sheria, adhabu ambayo inaishia Januari mwakani. Mkali huyo ametua akitegemewa kuziba pengo lililoachwa na Xavi aliyekimbilia Umangani.

Man United yamtengea kitita Thomas Muller

http://leadership.ng/wp-content/uploads/2015/07/thomas-muller.jpgBAADA ya kuelekea kumpoteza mshambuliaji wake matata, Robin van Persie, klabu ya Manchester United imepanga kutoa kitika cha pauni Milioni 60 ili kumnasa mshambuliaji wa Kijerumani Thomas Muller.
Muller mwenye umri wa miaka 25 anaichezea klabu ya Bayern Munich na United itamsajili Mjerumani huyo kama mbadala wa RVP ambaye anatarajiwa kuuzwa klabu ya Fenerbahce ya Uturuki. Klabu hiyo ya Uturuki imekubaliana na Mashetani Wekundu kulipa dau la Pauni Milioni 4.7 kama ada ya uhamisho wa RVP ambaye atafanyiwa vipimo vya afya wikiendi hii na kusaini mkataba wa miaka minne ambao utamuwezesha kulipwa mshahara wa Pauni 200,000 kwa wiki. 
Nyota huyo alijiunga na United akitokea Arsenal kwa kitita cha Pauni Milioni 24 Agosti mwaka 2012 na alianza vyema msimu wake wa kwanza akimaliza kama Mfungaji Bora wa EPL wakati taji likienda Old Trafford. 
Lakini Van Persie sasa amepungua makali kutokana na kuwa chini ya kiwango kutokana na majeruhi yaliyomuandama chini ya kocha Louis van Gaal.

Azam yaenda Tanga kutambulisha nyota wake

https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=11&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Wachezaji wakijiandaa na safari kuelekea Tanga
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=4&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Usiniangushe Migi
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=5&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Muingereza mwenyewe huyu hapa
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=7&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Migi akipasha na wenzake mapema leo

KLABU ya Azam ikiwa na nyota kadhaa wa kimataifa akiwamo Jean Baptiste Mugiraneza 'Migi'na Muingereza Ryan Burge imeondoka jijini kuelekea Tanga tayari kwa mechi mbili za kujipima nguvu kujiandaa na Kombe la Kagame litakaloanza wiki ijayo jijini Dar es Salaam.
Azam iliyofanya mazoezi mapema leo asubuhi itashuka dimba la Mkwakwani, Tanga kesho kuumana na Africans Sports kabla ya Jumapili kupepetana na Wagosi wa Kaya kwa mechi ya pili, kisha kurudi Dar kusubiri mechi zake za kundi C katika michuano hiyo ya Kagame itakayomaliza Agosti 2.
Mabingwa wa zamani wa Tanzania wanaenda kunoa makali kabla ya kuja kufanya kweli Dar katika Kagame ambayo inashirikisha timu 13 na Azam imepangwa kundi moja na KCCA ya Uganda, Al Malakia ya Sudan Kusini na Adama City ya Ethiopia.
Katika mechi hizo za wikiendi, Azam itatambulisha nyota wake wapya akiwamo Migi na Burge ambao wapo hatua ya mwisho kutua kwa Matajiri hao wa Tanzania.

Yohan Cabaye arejea England, aitosa PSG

http://e2.365dm.com/14/02/768x432/Yohan-Cabaye-Paris-St-Germain_3076500.jpg?20140201152736
Yohan Cabaye
KIUNGO fundi wa zamani wa Newcastle United, Yohan Cabaye amerejea Ligi Kuu ya England kutoka Ligue 1 ya Ufaransa.
Kiungo huyo amemwaga wino wa kukipiga klabu ya Crystal Palace akitokea PSG ya Ufaransa na kumfanya aungane tena na kocha wake, Alan Pardew. 
Klabu ya Crystal Palace imethibitisha kumsajili kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa kwa mkataba wa miaka mitatu. 
Inaaminika kuwa Palace imelipa ada ya Pauni milioni 10 kwa ajili ya kumnasa kiungo huyo aliyefanya kazi na Pardew kwa miaka mitatu wakati kocha na yeye wakiwa katika klabu ya Newcastle United. Kipindi akiichezea timu hiyo, Cabaye alikuwa akihesabiwa kama mmoja wa viungo bora katika Ligi Kuu. Kiwango chake hicho ndio kilichangia kwa kiasi kikubwa kuwafanya PSG kutoa karibu pauni milioni 20 kumsajili mapema mwaka jana.

Jordan Henderson rasmi nahodha wa Liverpool, amrithi Gerrard

http://i1.liverpoolecho.co.uk/incoming/article8381445.ece/ALTERNATES/s1227b/Gerrard-Henderson.jpg
Nakukabidhi mikoba, usiniangushe!
WAKATI ikiendelea kumbembeleza nyota wake Raheem Sterling asalie klabuni, Liverpool, imethibitisha Jordan Henderson kuwa nahodha mpya wa timu hiyo akichukua nafasi ya Steven Gerrard aliyeondoka mwishoni mwa msimu uliopita. 
Henderson ambaye amesaini mkataba mpya Aprili mwaka huu, ndio aliyekuwa akipewa nafasi kubwa ya kupewa beji hiyo baada ya Gerrard kuhamia katika klabu ya Los Angeles Galaxy ya Marekani. 
Akihojiwa Henderson amesema siku zote amekuwa akitaka majukumu zaidi hususani katika kipindi hiki cha soka lake. 
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa anajiona amekuwa kwasasa na yuko tayari kwa majukumu hayo kwani amejifunza mengi kutoka Gerrard katika kipindi chote ambacho chini yake.