STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 12, 2016

Hakuna ujanja FDL yafikia mwisho nani kupanda Daraja?

Lyon na Ashanti katika mechi yao
PATAMU! Ligi Daraja la Kwanza Bara (FDL), imefikia patamu kwani wikiendi hii, lazima kieleweke wakati mechi za kufungia msimu zitakapopigwa.
Licha ya kufungia msimu, lakini mechi hizo zitakazochezwa katika muda mmoja bila kujali tofauti mazingira ya hali ya hewa, pia zitatoa timu mbili za mwisho za kupanda daraja kucheza Ligi Kuu Bara msimu ujao wa 2016-2017.
Kwa mujibu wa agizo la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) mechi zote zitachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni, huku makundi ya A na C yakimulikwa kwani ndio yanayoshikilia hatma ya timu mbili za mwisho za kuungana na Ruvu Shooting kucheza Ligi Kuu ijayo.
Kundi C keshoJumamosi itashuhudia michezo minne, ila miwili ndiyo mikali ikizihusisha JKT Kanembwa dhidi ya Geita Gold mjini Kigoma na ule wa Polisi Tabora itakayoialika Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora.
Geita na Polisi zote zina nafasi sawa ya kupanda daraja zikiwa na pointi 27 kileleni, huku zikitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa, japo pia viwanja vingine zitapigwamechi za Mbao dhidi ya Polisi Mara na Panone itakayomalizana na Rhino Rangers .
Katika kundi A African Lyon, Friends Rangers na Ashanti Utd zote zina nafasi ya kufuzu VPL na zote zitashuka uwanjani keshokutwa Jumapili.
Friends itaivaa Kiluvya United pale Chamazi, jijini Dar, Ashanti na Lyon zitamalizana Karume, Dar es Salaam, huku Polisi Dar na Polisi Dodoma zitacheza Uwanja wa Mabatini, Mlandizi na CDA itamalizana na KMC.
Lyon ina pointi 26 ikihitaji sare kurudi Ligi Kuu, wakati Friends na Ashanti kila moja ina pointi 23 zikihitaji kushinda na kuiombea Lyon iteleze ili mojawapo ipande daraja.
Mechi za kukamilishia ratiba ya kundi B zipo hivi; Kimondo itacheza na Kurugenzi, Njombe Mji dhidi ya Lipuli, Ruvu itaikaribisha Polisi Moro na Burkina Faso itavaana na JKT Mlale mjini Morogoro.
Timu mbili za kushuka daraja kuungana na Kanembwa zinatarajiwa kufahamika katika mechi hizo za kesho na keshokutwa.

Msimamo Kundi A
                                   P   W  D  L    F   A  Pts
Africans Lyon                13  8   2  2   17  9  26
Friends Rangers            13  6   5  2   21  10  23
Ashanti Utd                   13  6   5  2   18  11  23
KMC FC                         13  6   4  3   12  10 22
Kiluvya United               13  5   5  3   12   8   20 
Polisi Dar                       13  3   5  5    9  13  14
Polisi Dom                     13  2   1  10  10 23  7
CDA                              13  1   3   9   6   21  6

Msimamo Kundi B
                               P  W  D  L  F  A  Pts
Ruvu Shooting          13  10  2  1  26 7  32
Njombe Mji               13   7   1   5  14  12 22
JKT Mlale                  13   5   6  2  17 10 21
Kurugenzi                 13   6   3  4  16 13 21
Polisi Moro                13  5   2  6   12 17  17
Lipuli Fc                    13   3  5   5   12  15 14
Kimondo                   13   2   3  8   8  22 9
Burkina Faso             13   1   4   8  10 18 7

Msimamo Kundi C
                              P W  D  L  F   A  Pts
Polisi Tabora            13  8  3  2  20  5   27
Geita Gold               13  8  3  2  20  6   27
Oljoro JKT               13  6  4  3  12  14  22
Mbao FC                  13  5  4  4  14  18  19
Panone                    13   4  4  5  16 13  16
Polisi Mara               13   2  7  4  11  15  13
Rhino Rangers          13   2  6  5  8   13  12
JKT Kanembwa         13  0  3  10  7  24  3

Ratiba kamili ya wikiendi hii:
Kesho Jumamosi:
Kimondo FC      vs     Kurugenzi FC    
Njombe Mji       vs     Lipuli FC                      
Ruvu Shooting   vs     Polisi Morogoro    
Burkinafaso FC  vs     JKT Mlale    
Mbao FC            vs     Polisi Mara    
Polisi Tabora       vs     JKT Oljoro    
JKT Kanembwa   vs     Geita Gold FC    
Rhino Rangers    vs     Panone FC    

Jumapili:
Polisi Dar            vs     Polisi Dodoma    
Mji Mkuu             vs     KMC FC                      
African Lyon        vs     Ashanti United    
Friends Rangers   vs     Kiluvya United   
 

BASATA YAUPIGA STOP 'SHIKA ADABU YAKO'



YAMETIMIA. Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) hatimaye limeufungia rasmi wimbo mpya wa nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nay wa Mitego uitwao 'Shika Adabu Yako'.
Basata ilitangaza hatua hiyo leo Ijumaa kupitia taarifa yake iliyosainiwa na Katibu Mtendaji wake, Godfrey Mngareza, ikiwa saa chache tangu kuzagaa kwa taarifa hizo baada ya wimbo huo kuwa gumzo kupitia mitandao ya kijamii.
Katika wimbo huo ulioachiwa mapema wiki hii, rapa huyo aliichana Basata katika moja ya mistari yake na taarifa hiyo ya Basata imesema imeufungia wimbo huo kwa mujibu wa mamlaka iliyonayo. Ikitumia kifungu cha 4 (1) (i) ya sheria  namba 23 ya mwaka 1984 na kifungu cha 4 (2) baraza hilo limetangaza kuupiga marufuku wimbo huo na kumpa onyo kali msanii huyo.
"Tunafahamu kuna wsanii wamekuwa wakifanya hivyo makusudi kutafuta umaarufu uchwara ambao wanadhani utakuja kutokana na kuzungumzwa sana. Tunapenda kusema wazi kuwa umaarufu hauji kwa upuuzi wa namna hiyo..."
Sehemu ya taarifa hiyo ya Basata ilisomeka hivyo, ikifafanua pia imechukua hatua hiyo dhidi ya wimbo huo kutokana na ukiukwaji mkubwa wa maadili, kashfa, uchochezi, kudhalilisha watu na kuhatarisha amani na utengani miongoni wa wasanii na jamii.
na kuzima tetesi zilizotapakaa tangu juzi kuwa wimbo huo uliorekodiwa na Mr T Touch umefungiwa kutokana na kuwa na mistari inayowananga wasanii mbalimbali akiwamo Wema, Ray, Ommy Dimpoz, Shetta, DJ Choka na hata Basata lenyewe.
"Ujumbe huu uwafikie Basata.....kazi kufungia nyimbo za wasanii, hivi mnajua tabu tunazopata, mmeshindwa kazi kama mngekuwa watoto tungeshawachapa..." 
Ni moja ya mstari uliopo kwenye wimbo huo ambao umelalamikiwa na wasanii waliombwa na kuwagawa mashabiki wengine wakiuponda na kuufagilia.
Basata imesisitiza pia kwa kumuonya msanii huyo kuwa makini katika kazi zake vinginevyo atachukuliwa hatua zaidi. Wa Mitego hakupatikana kusema lolote, lakini juzi alikakariwa kuwa hata kama wimbo utafungiwa basi wakubwa watakuwa wamechelewa kwa sababu kama ujumbe umeshafika kwa jamii na akitetea alichokiimba ni ukweli mtupu.

Hatimaye Yanga wapaa usiku huu kwenda Mauritius

Picha haihusiani na habari hii. Wachezaji wa Yanga wakiwa katika moja ya safari zao
KIKOSI cha Yanga kilichokwama kuondoka alfajiri ya leo kwenda Mauritius hatimaye kimepaa muda huu kuelekea nchini humo kwa ajili ya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Cercle de Joachim utakaochezwa kesho jioni.
Yanga ilikwama kuondoka na ndege ya ATCL kutokana na kuharibika kwa kifaa kilicholazimika kwenda kununuliwa Afrika Kusini na kufungwa, huku marubani wa ndege hiyo wakitishwa na hali ya hewa ya huko waendako.
Mpaka saa 12 jioni kulikuwa bado kuna hatihati ya safari hiyo baada ya rubani wa ndege kutaka kupimwa kwa watu wote wa msafara ili kuona kama uzito wao utaendana na safari yao wakiwa angani.
Hata hivyo mwishowe saa 1 msafara huo ulipaa kuelekea huko, licha ya kwamba Yanga kuonekana ilishavunja Kanuni ya 8 ya michuano ya CAf juu ya timu wageni kutakiwa kuwa nchi wanayoenda kucheza ndani ya saa 48. Kitu kizuri ni kwamba Mkuu wa msafara wa Yanga, Ayoub Nyenzi aliwasiliana mapema na CAF na wenyeji wao pamoja na kamisaa kuwajulisha juu ya tatizo lao.
Kwa taarifa hiyo, kikao cha mchezo huo (pre-match meeting) ambacho hufanywa siku moja kabla ya mchezo husika kimesogezwa mbele hadi kesho asubuhi na jioni mchezo utapigwa kama kawa, licha ya kwamba Yanga itaingia Mauritius usiku wa manane.
Mwendo wa kutoka jijini Dar es Salaam mpaka Curepipe mji utakaochezwa mchezo huo kwenye Uwanja wa George V ni kama saa nane, hivyo ni wazi Yanga huenda ikafika kati ya saa 9 alfajiri na jioni watashuka dimbani bila hata ya kupasha.
Kosa hilo la kuchelewa kwa Yanga ambayo awali ilikuwa ipae tangu Jumatano kabla ya kubadilishwa kwa ratiba yao, inaweza kuwa faida kwa wenyeji ambao kwa msimu wa pili sasa ndio mabingwa wa taifa hilo la kisiwani katika Bahati ya Hindi.

TASWA YALAANI UHUNI WA KAZIMOTO KUMPIGA MWANDISHI


Kazimoto anayetuhumiwa kumpiga mwanahabari, Mwanahiba Richard mjini Shinyanga

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini (TASWA) kimelaani vikali kitendo cha kiungo wa Simba, mwinyi Kazimoto kumpiga mwandishi wa gazeti la Mwanaspoti, Mwanahiba Richard akitekeleza majukumu yake mjini Shinyanga. taarifa rasmi ya Taswa inasomeka hivi:

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Chama Cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini (TASWA), kimestushwa na kitendo cha mchezaji wa Simba kudaiwa kumpiga mwandishi  kwa masikitiko makubwa kitendo cha wa  habari za michezo la gazeti la Mwananchi, Mwanahiba Richard.
Tumeongea na Mwandishi mwenyewe kujua ukweli, tumemtafuta kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Mika Nyange naye kutaka kufahamu hali ya upelelezi ilipofikia lakini kufanyika haraka kwa uchunguzi ili  haki ya kila mtu ipatikane.
Lakini tumeweza kuzungumza na upande wa pili, kwa viongozi wa Simba kujua kama nao wao wamebaini kosa la mchezaji huyo.Mwenyekiti wa Simba,Evans Aveva ameahidi kutoa ushirikiano na kuomba tusubiri uchunguzi wa Polisi ndipo upatikane ukweli wa jambo ili.
Sisi kama TASWA tunalaani tukio ili na tumekuwa tukikemea sana vitendo hivi kwa kupiga waandishi, lakini kumekuwa hakuna jitihada zozotew ambazo polisi inalichukua kwa wahusika na badala yake madai kama haya yanapotea.
Kwa kuwa jeshi la polisi limeahidi kutoa ufafanuzi wa upelelezi wa tukio ili haraka iwezekanavyo, naomba waandishi wenzangu pamoja na muathirika wa tukio ili, tuvute subira ili haki ichukue mkondo wake ili sheria ifanye kazi yake.
Taswa itaendelea kulinda heshma ya mwandishi wa habari za michezo na isingepeda kuona mwandishi anaonewa na kudhalilishwa wakati akifanya majukumu yake.
Kwa upande wetu napenda kutoa shukrani kwa nahodha wa Simba, Mussa Hassan Mgosi na kocha wa timu hiyo Jackson Mayanja kwa ushirikiano walioonesha katika tukio hilo na wamedhihilisha uwezo wa kuwaongoza wenzao.
TASWA itakuwa inafuatilia suala ili kwa karibu zaidi.Tupo katika kuhakikisha waandishi anafuata taratibu, sheria za taaluma ya habari.Jambo ambalo Mwanahiba amelifanya kwa kumlinda source wake hadi kupata kipigo .
Juma Pinto
Mwenyekiti TASWA
12.02.2016

Maskini Yondani, TFF yamfungia mechi tatu alimwa faini kwa ubabe

KELVIN Yondani ndio basi tena, kwani Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kupitia kamati yake ya Kusimamia na Kuendesha ligi iliyokutana kwa saa 72 jana Jumatano kupitia taarifa na ripoti mbalimbali za michezo ya Ligi Kuu (VPL), na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zinazoendeea kutimua vumbi katika viwanja mbalimbali nchini imemkuta na hatia.
Taarifa rasmi ya TFF inasomeka hivi:
Ligi Kuu ya Vodacom
Mchezaji Kelvin Yondani wa Yanga amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kumpiga usoni kwa box la dawa Dk. Mganga Kitambi wa Coastal Union wakati akitoa huduma kwa kipa wake katika mechi namba 121 kati ya timu hizo iliyofanyika Januari 30, 2016 kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Yondani alitenda kosa hilo baada ya kumuomba maji Daktari huyo, lakini akamnyima. Adhabu huyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 37(3) ya Ligi Kuu Toleo la 2015 ambapo baada ya kutumia adhabu ya mechi hizo, hataruhusiwa kucheza hadi atakapokuwa amelipa faini hiyo.
Naye Dk. Kitambi anapelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu kwa kitendo chake cha kumrudishia Yondani kwa kumpiga ngumi. Kitendo cha Daktari huyo ni kinyume cha Kanuni ya 41(2), na pia Kanuni ya 36 kuhusu mchezo wa kiungwana.
Klabu ya Yanga imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) kutokana na washabiki wake kuwatupia chupa za maji wachezaji wa Coastal Union walipokuwa wakishangilia bao la pili.
Nayo klabu ya Coastal Union imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa washabiki wake kuvamia uwanja baada ya filimbi ya mwisho, kitendo ambacho ni kinyume cha Kanuni ya 14(11) inayohusu taratibu za mchezo.
Mgambo Shooting imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kutumia chumba cha waandishi wa habari badala ya kile cha timu wakati wa mechi kati yao na Simba iliyochezwa Februari 3, 2016 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Adhabu hiyo imetolewa kwa uzingativu wa Kanuni ya 14(13) ya Ligi Kuu kuhusu taratibu za mchezo.
Kocha Ally Jangalu wa Coastal Union ameripotiwa kutoa matamashi ya kuidhalilisha TFF kwenye vyombo vya habari kuwa Refa wa mechi kati yao na Ndanda SC iliyochezwa mjini Tanga alikwenda na maelekezo ya kuhakikisha wapinzani wao wanashinda. Coastal Union ilifungwa bao 1-0 katika mechi hiyo iliyochezwa Februari 4, 2016. Suala lake linapelekwa Kamati ya Nidhamu.
Mchezaji Daud Jumanne amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kumkanyaga vidole kwa makusudi mchezaji wa Simba aliyekuwa akisubiri kupatiwa matibabu kwenye mechi kati ya timu hizo iliyofanyika Februari 7, 2016 kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 37(3) ya Ligi Kuu Toleo la 2015. Pia kwa kuzingatia Kanuni ya 37(20), hauruhusiwi kucheza mechi inayofuata ya timu yake mpaka faini hiyo iwe imelipwa. Iwapo atacheza kabla ya kulipa faini hiyo, timu yake itapoteza mchezo husika.
Klabu ya Stand United imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kutoingia vyumbani wakati wa mapumziko katika mechi dhidi ya African Sports iliyochezwa Februari 6, 2016 kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. Kitendo hicho ni kinyume na Kanuni ya 14(13) kuhusu taratibu za mchezo.
Kamishna wa mechi hiyo namba 140, Idelfonce Magali amepewa karipio kwa kutoripoti vizuri tukio hilo, wakati Refa Elly Sasii amepewa karipio kali kwa kutoripoti kabisa tukio hilo.
Ligi ya StarTimes
Wachezaji Ismail Nkulo, Said Juma, Idd Seleman na Edward Amos wa Polisi Dodoma wanapelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu baada ya kumzonga, kumtolea lugha ya matusi ya nguoni na kutaka kumpiga Refa katika mechi ya Ligi ya StarTimes kati ya timu yao na African Lyon iliyofanyika Januari 30, 2016.
Kitendo hicho katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma ni kinyume cha Kanuni ya 37(7) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu udhibiti wa wachezaji.
Kiongozi wa Friends Rangers, Heri Mzozo anapelekwa Kamati ya Nidhamu kwa kutoa lugha chafu kwa viongozi na waamuzi muda wote wa mchezo dhidi ya Ashanti United uliofanyika Januari 31, 2016 kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. Vitendo vyake ni kiyume na Kanuni ya 41(2) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu udhibiti wa viongozi.
Mwamuzi Msaidizi namba 2 kwenye mechi kati ya Kimondo na Ruvu Shooting, Idd Mikongoti wa Dar es Salaam ameripotiwa na Kamishna kuondoka na timu ya Ruvu Shooting kwa kupanda basi lao mara baada ya mchezo, kitendo ambacho ni kinyume na maadili ya uamuzi. Suala lake limepelekwa kwenye Kamati ya Waamuzi kwa ajili ya hatua stahiki dhidi yake.
Klabu ya Geita Gold imepigwa faini ya sh. 1,000,000 (milioni moja) na onyo kali kwa kukataa kuingia kwenye chumba cha wachezaj, na badala yake kutumia chumba kingine ambacho pia walijisadia haja ndogo wakati wa mechi dhidi ya Polisi Tabora iliyofanyika Januari 31, 2016 kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Nayo Polisi Tabora imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na kitendo cha mshabiki wake kupita pembezoni ya uwanja (running track) kwa kasi wakati mechi hiyo dhidi ya Geita Gold ikiendelea.
Pia klabu ya Polisi Tabora imepewa onyo kali kutokana kipa wa timu yake kuvaa jezi ambayo haikuwa na nembo (logo) ya Mdhamini wa Ligi Daraja la Kwanza wakati wa mechi hiyo.
Geita Gold imepewa ushindi wa pointi tatu na mabao matatu baada ya JKT Oljoro kugomea mchezo kati ya timu hizo uliofanyika Februari 6, 2016 kwenye Uwanja wa Nyankumbu Girls mkoani Geita. Timu hiyo iligomea mechi hiyo dakika 70 baada ya kufungwa bao la pili. Kitendo hicho ni kinyume cha Kanuni ya 29(1) ya Ligi Daraja la Kwanza.
Pia JKT Oljoro imepigwa faini ya sh. 1,000,000 (milioni moja) kutokana na kitendo hicho kwa kuzingatia Kanuni ya 29(4), wakati wachezaji wake Kapteni Shaibu Nayopa na Sunday Paul waliomvamia na kumpiga Refa wanapelekwa Kamati ya Nidhamu kwa ajili ya kuchukuliwa hatua stahiki.
Naye Kocha Msaidizi wa JKT Oljoro, Bunu Abdallah  ambaye alitolewa kwenye benchi la timu yake kwa kosa la kumtolea lugha chafu Mwamuzi Msaidizi namba 1 anapelekwa Kamati ya Nidhamu kwa ajili ya hatua stahiki.

Sunday, January 10, 2016

Yanga yawafuata Simba Dar, watolewa na URA

YANGA imeifuata Simba baada ya kutolewa na URA kwa penalti 4-3 baada ya kumaliza dakika 90 matokeo yakiwa 1-1.

Pambano limeisha Yanga, URA kwenye penalti

PAMBANO la nusu fainali ya pili ya Kombe la Mapinduzi, kati ya Yanga na URA limemalizika baada ya dakika 90 kuisha matokeo yakiwa bao 1-1.
Kwa sasa timu zinajiandaa kupigiana penalti. Ngoja tuone mambo yatakuwaje kwa wababe hao wa Tanzania na Uganda.

SAMATTA NAHIODHA MPYA WA TAIFA STARS

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa, amemtangaza mshambuliaji Mbwana Ally Samatta kuwa Nahodha mpya wa timu hiyo, akichukua nafasi ya Nadir Haroub Ali ‘Cannavaro’. Akizungumza na leo, Mkwasa amesema kwamba uamuzi huo umetokana na kazi nzuri ya Samatta kuitangaza Tanzania na Taifa Stars kimataifa. “Anastahili kuwa Nahodha wa Taifa Stars kuanzia sasa, na ingawa tumekuwa na Nahodha ambaye anastahili kuendelea, lakini tumeona kitu pekee cha kumlipa Samatta kwa sasa ni beji ya Unahodha,”amesema Mkwasa.

Mkwasa amesema kuanzia sasa Cannavaro atakuwa Nahodha wa kikosi cha wachezaji wanaocheza nyumbani kwa ajili ya michuano ya CHAN, wakati John Bocco atakuwa Nahodha Msaidizi wa Taifa Stars chini ya Samatta.
Samatta ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora Anayecheza Afrika katika sherehe zilizofanyika usiku wa Alhamisi ukumbi wa mikutano wa Kimataifa mjini Abuja.
Samatta alipata pointi 127, mbele ya mchezaji mwenzake wa TP Mazembe, kipa Robert Muteba Kidiaba wa DRC, aliyepata pointi 88, wakati mshambuliaji wa Etoile du Sahel ya Tunisia na timu ya taifa ya Algeria, Baghdad Bounedjah amepata pointi 63.
Mafanikio ya Samatta anayeweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa ukanda w Afrika Mashariki na Kati kushinda tuzo kubwa ya Afrika, yanakuja baada ya kuiwezesha Mazembe kutwaa taji la tano la Ligi ya Mabingwa Afrika, huku akiibuka mfungaji bora kwa mabao yake nane.
Aidha, Samatta sasa ndiye anaweza kuitwa Mchezaji Bora zaidi kuwahi kutokea Tanzania – bada ya miaka mingi ya kutokuwa na uhakika wa nani apewe sifa hiyo.
Samatta alijiunga na Mazembe mwaka 2011 akitokea Simba SC aliyoichezea kwa msimu mmoja akitokea African Lyon iliyomtoa Mbagala Market, ambayo ilimuibua Kumbagulile FC ya kwao, Mbagala.
Chanzo-Bin Zubeiry

URA wanachomoa bao URA 1, Yanga 1

http://urafc.co.ug/wp-content/uploads/2015/02/URA-Peter-Lwasa-300.jpg
PETER Lwasa aliyeingia kipindi cha pili, anaisawazishia bao URA kutokana na wachezaji wa Yanga kucheza Offside-trick ambapo mabeki walidhani mfungaji ameotea, lakini bado ndivyo tena. Yanga 1 URA 1

Tetesi za usajili majuu zipo hivi

http://i2.walesonline.co.uk/incoming/article6494703.ece/ALTERNATES/s615/1Gareth-Bale.jpgDIRISHA la usajili kwa mwezi Januari lipo wazi na klabu kadhaa zimeanza kuchangamkia kwa kunyakua nyota mbalimbali, huku tetesi nyingine zikizidi kuenea kila uchao.
Straika wa Real Madrid, Gareth Bale anatarajiwa kukataa maombi ya kutoka Manchester United na Chelsea kufuatia nyota huyo wa kimataifa wa Wales kutaka kuendelea kubakia Santiago Bernabeu. Pia inaelezwa kuwa Klabu ya Manchester United inaripotiwa kujipanga kumchukua meneja wa Tottenham Hotspurs Mauricio Pochettino kama mbadala wa Louis van Gaal, huku meneja wa Paris Saint-Germain Laurent Blanc naye akitajwa kufikiriwa katika nafasi hiyo. Hii ni kwa mujibu wa Sunday Mirror. 
Kwingineko klabu ya Tottenham Hotspurs inajipanga kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Loic Remy kwa mkopo majira haya ya kiangazi, huku Manchester United inataka kitita cha paundi milioni 24 kwa ajili ya Marouane Fellaini lakini hawatakubali kiungo huyo kuondoka kwa mkopo. Pia klabu hiyo ya Manchester United inakaribia kumsajili mshambuliaji wa Mainz Yoshinori Muto kwa kitita cha paundi milioni 12 hii ni kwa mujibu wa Sunday Mirror.
The Suna lenyewe limeeleza kuwa Klabu ya Manchester City imeingia katika kinyang’anyiro cha paundi milioni 80 na Real Madrid na Paris Saint-Germain kama Eden Hazard ataamua kuondoka Chelsea kipindi hiki cha majira ya kiangazi, huku Chelsea nayo ikidaiwa kuwa inamuwinda meneja wa Atletico Madrid Diego Simeone ili aweze kuwa mbadala wa Guus Hiddink pindi atakapomaliza muda wake mwishoni mwa msimu huu.

Tambwe aifungia Yanga bao

AMISSI Tambwe ameifungia Yanga bao la mapema na kuifanya iende mapumziko ikiwa mbele dhidi ya URA ya Uganda. Kipindi cha pili kimeanza matokeo yakiwa bado ni 1-0, Yanga wakiwa mbele.
Matokeo yakibaki hivi Yanga itakutana na Mtibwa katikam fainali za Kombe la Mapinduzi kama ilivyokuwa mwaka 2007.

Spurs chupuchupu, Chelsea yapeta Kombe la FA

Harry Kane akishangilia penalti yake iliyoiokoa Spurs kulala nyumbani
WAKATI Chelsea ikivuka hadi raundi ya nne baada ya kuifunga timu ya Scunthorpe kwa mabao 2-0 katika mechi ya mfululizo wa michuano ya Kombe la FA, Tottenham hotspur ikiwa nyumbani ilinusurika kulala baada ya kutoka sare ya mabao 2-2.
Penalti ya Harry Kane katika dakika za lala salama iliiokoa Spurs kulala kwa Leichester City, huku Swansea City iking'olewa na Oxford United kwa mabao 3-2.
Chelsea wenyewe wakiwa nyumbani kwao Stamford Bridge ilipata ushindi wa mabao 2-0 na kuungana na vigogo wengine wa Ligi Kuu kufuzu raundi nyingine ya michuano hiyo ambayo bingwa mtetezi ni Arsenal iliifumua Sunderland jana Jumamosi kwa mabao 3-1.



Simba yatemeshwa taji, Mtibwa hiyoo fainali za Mapinduzi

Ibrahim Rajab 'Jeba', akichuana na Mohammed Tshabalala wa Simba jioni ya leo na Simba kulala bao 1-0
NDIVYO hivyo tena. Simba imetemeshwa taji lake la Kombe la Mapinduzi baada ya kulala bao 1-0 kwa Mtibwa Sugar.
Bao pekee la sekunde chache kabla ya mapumziko lililofungwa na Ibraihm Rajab 'Jeba' lilitosha kuirudisha Simba jijini dar es Salaam na kuiacha Mtibwa ikitangulia fainali yao ya tano.
temesha Simba ubingwa wa Kombe la Mapinduzi na kuifungasha virago kurudi jijini Dar es Salaam.
Katika pambano hilo la kwanza la nusu fainali lililochezwa jioni kwenye Uwanja wa Amaan, visiwani humu, Simba itabidi ijilaumu kwa kutemeshwa taji.
Na kama kuna mtu ambaye atajuta kwa kung'oka kwa Simba ni kipa Peter Manyika aliyeizawadia Mtibwa bao baada ya kushindwa kudaka mpira uliiopigwa na Shiza Kichuya na kumfanya Jeba kumpoka na kufunga bao hilo.

Mtibwa sasa inasubiri kujua itacheza na nani kati ya Yanga na URA ambazo zinaendelea kuumana muda huu.
Hizo ni fainali za tano kwa Mtibwa tangu michuano hiyo ilipoasisiwa mwaka 2007 ikikutana na Yanga kwa mara ya kwanza mwaka huo na kufungwa.
Pia hii itakuwa fainali ya pili mfululizo ya Mtibwa baada ya mwaka jana kucheza fainali dhidi ya Simba na kufungwa kwa mikwaju ya penalti.
Pamoja na Simba kufanya mashambulizi mengi langoni mwa Mtibwa na hasa katika kipindi cha pili baada ya kufanya mabadiliko, lakini umakini mdogo wa washambuliaji wa Msimbazi wakiongozwa na Danny Lyanga, Mussa Mgosi na Ibrahim Ajib.

Friday, January 8, 2016

Simba yaikwepa Yanga kiaina, kuvaana na Mtibwa

Mashabiki wa Simba wanaosubiri kuipa sapoti timu yao Jumapili jioni dhidi ya Mtibwa Sugar
BAO pekee la Jonas Mkude la dakika ya 65 limeiwezesha Simba kutinga nusu fainali na sasa itaavana na Mtibwa Sugar jioni ya Jumapili, ikikwepana kuvaana na Yanga iliyotangulia mapema tangu jana.
Kulikuwa na dalili za Simba kuvaana na Yanga kama matokeo yangeisha kwa sare ya 0-0, lakini bao la Mkude liliweka mambo sawa na sasa vijana wa Msimbazi watakuwa wakinoa makucha yao ili kuvaana na Mtibwa waliocheza nao fainali za mwaka jana na kuichapa kwa mikwaju ya penalti.
Yanga wenyewe itakuwa na kibarua dhidi ya URA ambayo mapema jioni ya leo ilipata ushindi wa baoa 1-0 dhidi ya Jamhuri.
Kama Yanga na Simba zitavuka hatua hiyo zitaumana Jumatano usiku kwenye fainali ikirejea fainali za mwaka 2011, ambazo Simba ilitwaa taji lake la pili kwa kuizabua Yanga mabao 2-0.

Simba inaoongoza kwa bao 1-0 dhidi ya JKU

SIMBA inaongoza bao 1-0 baada ya Jonas Mkude kuipatia bao la kichwa katika dakika ya 65. Pambano bado ni kali na kuna dalili za wapinzani wajadi Simba na Yanga kutokutana katika hatua ya nusu fainali.

Claudio Makelele apewa shavu Monaco


http://img1.cfstatic.com/psg/claude-makelele_35549_wide.jpg
Claudio Makelele
KLABU ya Monaco ya Ufaransa, imemteua kiungo wa zamani wa Chelsea na Real Madrid, Claudio Makelele kuwa Mkurugenzi Mpya wa Ufundi. 
Klabu hiyo ilitangaza jana Alhamisi uteuzi wa nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa, ikielezea kuwa, kibarua chake kikubwa kitakuwa ni kumsaidia Makamu wa Rais Vadim Vasilyev kuongoza upande wa michezo wa timu hiyo. 
Makelele alitimuliwa kibarua cha kuinoa Bastia Novemba 24, 2014 baada ya kufanya kazi kama Kocha Msaidizi katika klabu ya Paris Saint-Germain. Akihojiwa na mtandao wa klabu hiyo, Makelele amesema amefurahi kujiunga na klabu hiyo muhimu katika soka la Ufaransa na kuahidi kufanya bidii na kuisaidia timu hiyo.
Enzi za uchezaji wake, mkali huyo alikuwa akitawala dimba la kati kiasi cha kuwapa wakati mgumu wapinzani wake.
 

Simba yaisaka Yanga kimtindo

DAKIKA 45 za kwanza za pambano la kukamilisha ratiba kati ya Simba na JKU zimemalizika matokeo yakiwa bao 0-0.
Pambano ni kali na Simba itajilaumu kwa kukosa angalau bao hata moja katika dakika hizo kutokana na kukosa mabao ya wazi.
Kama matokeo yataendelea hivi Simba itakuwa imeangukia mikononi mwa Yanga waliomaliza nafasi ya kwanza kwenye kundi B. URA wanaoongoza kundi A tayari imeshatinga nusu fainali, kama ilivyo kwa Mtibwa Sugar, lakini hakuna anayejua atacheza na nani Jumapili ijayo mechi za nusu fainali zitakazpochezwa jioni na usiku.

Sunderland wanasa kifaa toka Bayern Munich

https://i.guim.co.uk/img/media/714c8f8cc7ab15b56bb5fb6c9eb01c24b719ae6c/0_149_5128_3080/master/5128.jpg?w=620&q=85&auto=format&sharp=10&s=daec3160be3fec2cb53a6ae0d3112b65IKIWA na kibarua kigumu wikiendi hii dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Sunderland imetangaza kumsajili beki wa Bayern Munich, Jan Kirchhoff kwa ada ambayo haikuwekwa wazi.
Beki huyo wa kati mwenye umri wa miaka 25, alianza soka lake katika timu ya Mainz kabla ya kujiunga na Bayern mwaka 2013, akiwa pia amecheza kwa mkopo Schalke ametua kwa Paka Weusi hao kabla ya kuvaana na Arsenal kwenye mechi ya mzunguko wa tatu wa michuano ya Kombe la FA.
Meneja wa Sunderland, Sam Allardyce aliuambia mtandao wa klabu hiyo kuwa Jan ni mchezaji mzuri na mwenye uzoefu pamoja na umri mdogo alionao hivi sasa. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa anaamini beki huyo atazoea haraka mazingira katika klabu hiyo na kuwasaidia kufikia malengo yao waliyojiwekea msimu huu.
Sunderland iko katika mapambano ya kutoshuka daraja wakishika nafasi ya 19 katika msimamo wakiwa na alama 15 katika michezo 20 waliyocheza.

Sanchez bado hakijaeleweka Emirates

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2015/01/11/14/Alexis-Sanchez.jpgBADO hakijaeleweka tu. Kocha wa  Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuwa straika wake matata, Alexis Sanchez ataukosa mchezo wa mzunguko wa tatu wa Kombe la FA dhidi ya Sunderland ikiwa kama tahadhari.
Nyota huyo wa kimataifa wa Chile amekuwa nje ya Uwanja kwa zaidi ya mwezi mmoja baada ya kupata majeruhi ya misuli katika mchezo dhidi ya Norwich City, Novemba 29 mwaka jana.
Sanchez alikuwa akitegemewa kurejea uwanjani kabla ya Krismasi, lakini alichelewa kupona na Wenger hayuko tayari kumwahisha kutokana na kukabiliwa na mechi ngumu za za Ligi Kuu dhidi ya Liverpool na Stoke City wiki ijayo.
Akizungumza katika mtandao wa klabu hiyo, Kocha Wenger amesema taarifa mbaya aliyonayo wiki hii ni kukosekana kwa Sanchez ambaye pamoja na kupona, lakini ameamua kumpa muda zaidi kama tahadhari.
Wenger ameendelea kudai kuwa kiungo Mikel Arteta atakuwepo katika kikosi cha kwanza kwa mara ya kwanza toka Novemba 21 wakati Tomas Rosicky naye ataanza mazoezi rasmi wiki ijayo baada ya kupona majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua.
Arsenal ndio wanaoongoza kwa sasa msimamo wa Ligi Kuu ya England  ikiwa na pointi 42, mbili zaidi na ilizonazo Manchester City wanaofuata nyuma yao.

Dortmund na sizitaki mbichi kwa Januzaj

http://cdn.images.express.co.uk/img/dynamic/67/590x/Adananjjjj-604533.jpgKLABU ya Borussia Dortmund imedai ulikuwa ni uamuzi wa Adnan Januzaj mwenyewe kurejea Manchester United na kukiri dili lake halikuwa na manufaa kwa klabu yoyote. 
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 alijiunga na Dortmund kwa mkopo wa msimu mzima mwishoni wa Agosti mwaka jana, lakini amefanikiwa kuichezea timu hiyo mechi 12 pekee. 
Kurejea kwa Januzaj Old Trafford kulifanywa rasmi jana na mkurugenzi wa michezo wa Dortmund amekiri kuwa kusitisha mkataba wa nyota huyo ni jambo bora kwa pande zote husika. 
Mkurugenzi huyo amesema yalikuwa ni mapendekezo ya Januzaj mwenyewe kurejea United na uwepo wake Dortmund haukuwa na faida yeyote kwa klabu hiyo.
Man imemrejesha winga huyo kwa ajili ya kuimatrisha kikosi chake baada ya Kocha Louis Van Gaal kuuza wachezaji wake kadhaa nyota akiwamo Nani, Chicharito na Angel di Maria

Samatta sasa kina kona, anukia Nantes

KLABU ya Ligi Kuu ya Ufaransa, Ligue 1 ya Nantes inaripotiwa kuanza mazungumzo rasmi na wawakilishi wa Mbwana Samatta pamoja na klabu ya TP Mazembe. 
Klabu hiyo imedaiwa kuwa ina nia ya kupata saini ya Samatta katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili ili iweze kumtumia kwa msimu uliobakia. 
Kwa mujibu wa mwakilishi wa Samatta, Nantes inataka kila kitu kimalizike kabla ya Januari 20. Nantes inamtaka Samatta ili kuimarisha safu yake ya ushambuliaji ambayo msimu huu inaonekana kuwa butu kwa kufunga mabao 14 pekee. 
Nantes inashikilia nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi hiyo baada ya kucheza michezo 19 ikikusanya jumla ya pointi 24.
Timu hiyo Jumapili itashuka uwanjani kuvaana na St Entienne katika mfululizo wa ligi hiyo.

HIKI NDIKO KIKOSI AMBACHO SAMATTA NAYE NDANI

MBWANA Samatta jana alirejea tukio lililowahi kufanywa na straika wa kimataifa nchini, Haji Dilunga alipoteuliwa timu ya Afrika sambamba na kipa Omary Mahadhi mwaka 1973 baada ya kuingia kwenye kikosi cha kwanza cha Afrika 2015 sambamba na nyota wengine.
Kikosi kamili kipo hivi;


NI SIMBA VS YANGA MAPINDUZI AU YANGA V JKU?

http://24tanzania.com/wp-content/uploads/2013/09/9072Simba-Yanga.jpgKLABU ya Yanga inasubiri kujua itacheza na nani kati yake na watani zao Simba au URA ya Uganda katika mechi za nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar.
URA imekuwa timu ya tatu kutinga hatua hiyo baada ya jioni ya leo kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Pemba na kuiacha nafasi moja kwa 'Mnyama' ili kujua itaangukia kileleni au nafasi ya pili.
Kama Simba ambayo usiku huu itavaana na JKU ya Unguja, itashinda mchezo huo, itaikwepa Yanga na hivyo kusubiri kuona kama zitakutana fainali Jumatano ijayo.
Iwapo Simba itatokla sare au kupoteza itaangukia nafasi ya pili na kuingia 18 za vijana wa Jangwani ambao usiku wa jana ilipasta ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mtibwa.
Simba ambao ni mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo ya Mapinduzi iliyoasisiwa mwaka 2007 ina pointi nne mpaka sasa ikiwa nafasi ya pili, nyuma ya URA ilitimiza pointi 6 baada  ya ushindi wake wa jioni huu kwa bao la Saio Kyayune  la dakika za lala salama.
Kama timu hizo kongwe nchini zitakwepana hatua hiyo ya nusu fainali kulingana na matokeo ya usiku wa leo, basi zinaweza kukutana fainali na kurejea fainali za mwaka 2011 ambapo Yanga ilikubali kichapo cha mabao 2-0 mbele ya Simba kwa mabao ya Mussa Hassan Mgosi na Shija Mkina.

Nusu fainali:
J'Pili Jan 10
Samba/JKU v Mtibwa Sugar Saa 10:15 jioni
Yanga v Simba/JKU Saa2:15 usiku

Msimamo
Kundi A

                P  W D  L  F A Pts
URA          3   2  0  1 4 2  6*
Simba       2   1  1  0 3 2  4
JKU           2   1  0  1 4 3  3
Jamhuri     3   0  1  2 2 6  1

Kundi B

               P  W D  L  F  A Pts
Yanga      3   2  1  0  6  2  7*
Mtibwa     3   1  1  1  3  3  4*
Mafunzo   3   1  0  2  2  5  3
Azam       3   0  2  1  3  4  2
* Zimefuzu nusu fainali

Wafungaji:

2-Donald Ngoma (Yanga)
   Awadh Juma (Simba)
   Villa Oromuchan (URA)
   Mohammed Abdallah (JKU)
  Kipre Tchetche (Azam)
1-Paul Nonga (Yanga)
  Hussein Javu (Mtibwa)
  John Bocco (Azam)
  Oscar Aggaba (URA)
  Emmanuel Martin (JKU)
  Said Bahanuzi (Mtibwa)
  Vincent Bossou (Yanga)
  Mwalimu Khalfan (Jamhuri)
  Ammy Bangaseka (Jamhuri)
  Nassor Juma      (JKU)
  Ibrahim Ajib      (Simba)
  Rashid Abdalla (Mafunzo)
  Sadick Rajab   (Mafunzo)
  Saio Kyayune   (URA)
  Shiza Kichuya  (Mtibwa)
  Issofou Boubacar (Yanga)
  Malimi Busungu  (Yanga)

Orodha ya Mabingwa

2007  Yanga SC
2008  Simba SC
2009  Miembeni
2010  Mtibwa Sugar
2011  Simba SC
2012  Azam FC 
2013   Azam FC
2014  KCCA      
2015  Simba SC
NB:Simba imeingia fainali nyingi za Mapinduzi (5) ikifuatiwa na Mtibwa (4)

Samatta aanza kupokea pongezi za tuzo yake

HONGERA. Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi amempongeza mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania na klabu ya TP Mazembe ya Congo DR kwa kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ndani.
Samatta ameshinda tuzo ya mchezaji bora kwa wachezaji wanaocheza Afrika baada ya kwashinda Robert Kidiaba (Congo DR) alieshika nafasi ya pili na Bounedjah Baghdad (Algeria) aliyeshika nafasi ya tatu.
Kwa kushinda tuzo hiyo, Samatta amekua mchezaji wa kwanza kwa ukanda wa Afrika Mashariki kushinda tuzo kubwa barani Afrika.
Pamoja na kushinda tuzo hiyo, Samatta pia amejumuishwa katika kikosi bora cha wachezaji wa Afrika kwa mwaka 2015 sambamba na Robert Kidiaba (Congo DR), Sergie Aurier (Ivory Coast), Aymen Abdenmor (Tunisia), Mohamed Meftah (Algeria), Sadio Mane (Senegal), Yaya Toure (Ivory Coast), Yacine Ibrahim (Algeria), Andrew Ayew (Ghana), Mbwana Samatta (Tanzania), Pierre-Emercik Aubameyang (Gabon) na Baghdad Bounedjah (Algeria).
Mshambuliaji Mbwana Samatta alieyambatana na Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine wanatarajia kuwasili nchini leo saa 8 usiku kwa shirika la ndege la Ethiopia.
Wakati Huo huo Shirikisho la Soka Tanzania, TFF limetuma salamu za rambirambi kwa kocha msaidizi wa Taifa Stars Hemed Suleiman “Morocco” kufutia kifo cha baba yake mzazi Suleiman Ally Hemed kilichotokea juzi kisiwani Zanzibar.
Katika salamu hizo za rambirambi, TFF imewapa pole wafiwa, ndugu jamaa na marafiki na kusema wapo pamoja na familia ya marheemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Aidha pia TFF imetuma rambirambi (ubani) wa shilingi laki mbili (200,000) kwa familia ya kocha Hemed Moroco kufuatia kifo cha baba yake Suleiman Ally.
Mazishi ya marehemu Suleiman Ally Hemed yamefanyika jana Alhamisi jioni mjini Zanzibar.

MWANAUMEEEEEEEEEEEEEEEE NI MBWANA SAMATTA

 
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/samatta-1.jpg
Add caption
MWANASOKA Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani ni Mbwana Samatta, huku Yaya Toure MBWANA Samatta kila kona. Mwanasoka wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta usiku wa kuamkia leo ameweka rekodi ya kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani. Samatta amekuwa Mtanzania wa kwanza kunyakua tuzo hiyo baada ya kuwashinda Robert Kidiaba na Baghdad Bounedjah.
Hiyo ni tuzo ya pili kwa Samatta baada ya ile ya Mfungaji Bora wa Afrika akiwa ameisaidia klabu yake ya TP Mazembe kutwaa ubingwa wa Afrika mwaka 2015.
Klabu hiyo ya Mazembe ilishinda tuzo ya Klabu Bora Afrika, huku timu ya taifa ya Ivory Coast ikishinda tuzo Timu bora ya Afrika kwa wanaume na Cameroon ikishinda kwa upande wa wanawake.
Mfaransa Herve Renard, Kocha wa Ivory Coast alitwaa tuzo ya Kocha Bora wa Mwaka kwa mara ya pili baada ya mwaka 2012 kunyakua pia tuzo kama hiyo alipoisaidia Zambia kutwaa ubingwa wa Afrika na  kufikia rekodi ya  Bruno Metsu aliyenyakua mwaka 2001-2002
Mwanasoka Bora wa Afrika kwa mwaka 2015 ni Pierre-Emerick Aubameyang, akimpikua Yaya Toure wa Ivory Coast na Andre Ayew wa Ghana.

ORODHA KAMILI YA WASHINDI
MCHEZAJI BORA WA AFRIKA - Pierre-Emerick AUBAMEYANG (Gabon)
MCHEZAJI BORA ANAYECHEZA AFRIKA – Mbwana Aly SAMATTA
MCHEZAJI BORA WA KIKE - Gaelle ENGANAMOUIT (Cameroon)
MCHEZAJI BORA KIJANA - Victor OSIMHEN (Nigeria)
MCHEZAJI BORA ANAYECHIPUKIA VIZURI - Etebo Peter OGHENEKARO (Nigeria)
KOCHA BORA WA MWAKA- Herve RENARD (Ufaransa) – Kocha wa zamani wa Ivory Coast
REFA BORA WA MWAKA - Bakary Papa GASSAMA (Gambia)
TIMU BORA YA TAIFA – Ivory Coast
TIMU BORA YA TAIFA YA WANAWAKE- Cameroon
KLABU BORA YA MWAKA - TP Mazembe (DRC)
GWIJI WA AFRIKA - Charles Kumi GYAMFI (Ghana)
Samuel MBAPPE LEPPE (Cameroon)

KIKOSI BORA AFRIKA

Kipa: Robert Muteba KIDIABA (DRC)
Mabeki: Serge AURIER (Ivory Coast), Aymen ABDENNOUR (Tunisia), Mohamed MEFTAH (Algeria)
Viungo: Andre AYEW (Ghana), Yaya TOURE (Ivory Coast), Sadio MANE (Senegal), Yacine BRAHIMI (Algeria),    
Washambuliaji: Mbwana Aly SAMATTA (Tanzania), Pierre-Emerrick AUBAMEYANG (Gabon), Baghdad BOUNEDJAH (Algeria) 

WACHEZAJI WA AKIBA;

Djigui DIARRA (Mali)
Azubuike OKECHUKWU (Nigeria)
Kelechi NWAKALI (Nigeria)
Zinedine FERHAT (Algeria)
Adama TRAORE (Mali)
Victor OSIMHEN (Nigeria)

Kermit ERASMUS (Afrika Kusini)