STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 12, 2013

Jaji Mark Bomani aipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba


Jaji Mark Boman akizungumza mchana wa leo jijini Dar es Salaam
Na Suleima Msuya.
WAKATI Taifa  likiwa katika mjadala juu ya rasimu ya katiba ijayo Mwanasheria Mkuu Mstaafu wa Serikali, Jaji Mark Boman ameipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya Jaji Mstaafu Joseph Warioba kwa kuja na rasimu nzuri na kuitaka kutoharakisha uwepo wa katiba husika ili iweze kukidhi mahitaji ya wananchi.
Jaji Boman amesema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya habari maelezo Jijini hapa.
Alisema mchakato mzima wa kuandaa rasimu unahitaji umakini, uadilifu na kuhakikisha kuwa hakuna misukumo yoyote ya kufanikisha suala hilo hivyo ni vyema wakahakikisha kuwa mambo ya msingi yanayohusu jamii yanahusika.
Mwanasheria Mkuu huyo Mstaafu alisema jambo ambalo linaonekana kugusa jamii kwa asilimia kubwa ni kuhusu muungano, hivyo ni vyema tume ikafanya tathmini sahihi juu ya utekelezaji wake ili kuhakikisha kuwa inakidhi kiu ya Watanzania.
Alisema kutokana na rasimu hiyo ilivyochambuliwa na tume imejikita hasa kuhusu jinsi ya kuwa na muungano wa nchi lakini ikajisahau kuwa ilikuwa ni fursa muhimu kwa wananchi kuhusika moja kwa moja juu ya aina ya muungano wanaotaka na isiwe na maoni ya wajumbe wa tume.
"Mimi kama Mtanzania na pia mwanasheria mkongwe ambaye najua masuala ya nchi hii kwa upana naamini tume imejitahidi kwa kiwango chake ila naona haipo sababu ya kukimbilia kuwepo kwa katiba bila kuhakikisha kuwa mahitaji ya msingi hajatekelezwa hasa ambayo yanagusa jamii," alisema.
Jaji Boman alisema suala la muungano linahitaji mchango wa wadau hasa wananchi kwani ni jambo ambalo linaweza kuweka muafaka wa hatma ya nchi kwa miaka ijayo.
Alisema ni vema Tume ikatambua kuwa suala la muungano halihitaji maoni ya watu wachache kwani ni wazi kuwa suala hilo limekuwa likiibua migogoro mingi kwa muda mrefu hasa katika upande wa Zanzibar.
Alisisitiza kuwa katika harakati za kutafua ufumbuzi juu ya sauala hilo la muungano ni vema tume ikachukua maoni ya waliowengi ili kuhakikisha kuwa haja yao inatimia hata kama wachache wenye uelewa watakuwa wanapinga.
Boman alisema dhana kuhusu serikali tatu kuwa zitaongeza gharama za undeshaji wa Serikali ni mtazamo finyu kwani kuna mifano ya nchi nyingi ambazo zimeungana na kuendeshwa kwa mfumo huo na hakuna athari ya moja kwa moja ambayo imeonekana.
Alisema ni vyema tume ikajikita kwa wananchi na kuachana na mitazamo ya baadhi ya viongozi wa kisiasa ambao wengine wanaonekana kuwa yapo mambo ambayo wanataka yawepo kwa maslahi yao na sio ya Taifa
Kwa upande mwingine Jaji Boman ameiomba tume kuhakikisha kuwa rasimu hiyo ya katiba ya nchi inakuwa na muongozo juu ya dira ya nchi, maslahi ya kijamii kwa jamii na mahitaji muhimu yatajwe ili iwe ni muongozo sahihi kwa kiongozi yoyote ambaye atapata kuongoza nchi.
Pia alisema ni vyema rasimu hiyo ya katiba ianishe uwepo na uatambuzi wa rasilimali za nchi ambazo kwa kiasi fulani zimeonekana kutumiwa kinyume na taratibu hivyo kutowafaidisha wananchi kwa ujumla.
Alitolea mfano suala la mikataba mibovu ambayo imekuwa ikiingiwa na Serikali iwapo kutakuwepo na muungozo wa kikatiba juu ya suala la mikataba inaweza kuwa njia sahihi ya kuwabana wahusika.
Alisema iwapo mambo hayo ya msingi yakikosekana ni dhahiri kuwa kila kiongozi anaweza kufanya anachotaka kutokana na mahitaji yake jambo ambalo ni kinyume na utawala unavyotaka hasa katika ngazi ya nchi.

TNMC kuvishughulikia vyuo 'feki' vya uuguzi


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6m8bWbGudkyYCLSAr7cUMFUQr9SmTb9v62BhYhc-M3bgI-zC2B5sQAqm9gE8r1TQo15IS3oazEpq75Zw8ejIMXf-22BKbgC5Vg7G52lxFFWt9hSVk-KcCnab1HsUWThzJ6VCc5L4fP4FY/s1600/baraza+la+uuguzi1.JPG
Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Lena Mfalila akizungumza leo jijini Dar (picha:Audiface Jackson Blog)
BARAZA la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC) , limetangaza kuvisaka na kuvifungia vyuo vyote vinavyotoa mafunzo ya ngazi ya cheti na stashahada yasiyokidhi viwango vilivyowekwa na baraza hilo.
 
Aidha imeelezwa kuwa vyuo zaidi ya 200 nchini kote havina sifa ya kutoa mafunzo ya taaluma hiyo kwa kutokusajiliwa na TNMC.
 


Msajili wa vyuo vya uuguzi na ukunga nchini Lena Mfalila alisema hadi sasa Baraza linatambua uwepo wa vyuo 34 vinavyotoa mafunzo ya uuguzi nchini.
    
Mfalila alisema ili mafunzo ya chuo yaweze kutambulika ni lazima kiwe kimesajiliwa, kiwe na walimu wenye sifa pamoja kutumia mitaala inayotambuliwa na Baraza.
 
Aliwataka wazazi na wanafunzi wote wanaohitaji kupata elimu katika vyuo mbalimbali hapa nchini kuvichunguza kwanza kabla ya kujiunga navyo kwani wasipofanya hivyo watakuwa wanapoteza muda wao.
 
“Lazima wanaotaka kujiunga na chuo wanachotaka kusoma wahakikishe kama kimesajiliwa na baraza chini ya sheria ya ‘Nursing and Midwifery’ ya mwaka 2010 na kuangalia mitaala yao ya  kufundishia,” alisema Mfalila.
 
Kwa upande wa vyuo vinavyofundisha uuguzi, alisema Baraza limekumbana na changamoto nyingi ikiwa ya kuibuka kwa vyuo ambavyo havitambuliki kisheria lakini vinaendesha mafunzo kinyemela.
 
Aidha alisema kutoka na  malalamiko ya jamii kuhudumiwa huduma duni ya uuguzi na ukunga zinazotolewa na watumishi wa afya ambao wameajiriwa kutoka vyuo  visivyotambulika,baraza limetoa agizo kwa watumishi wa afya kutoa taarifa.

Ivory Coast kutua nchini kesho na nyota wote, ispokuwa Drogba

http://0.tqn.com/d/goafrica/1/0/Y/L/ivorycoastteam.jpg
Kikosi cha Ivory Coast, japo Didier Drogba hatakuja hiyo kesho

Na Boniface Wambura
MSAFARA wa timu ya Taifa ya Ivory Coast (The Elephants) wa watu 80 wakiwemo wachezaji 27 unatarajiwa kuwasili nchini kesho (Juni 13 mwaka huu) kwa ndege maalum kwa ajili ya mechi dhidi ya Taifa Stars.

Mechi hiyo itachezwa Jumapili (Juni 16 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 9 kamili alasiri, na itachezeshwa na Charef Mehdi Abdi kutoka Algeria.

Kikosi hicho kitawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 2.50 usiku na kitafikia hoteli ya Bahari Beach iliyoko nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Timu hiyo inatarajia kuondoka saa chache baada ya mechi hiyo.

Wachezaji walioko katika kikosi hicho ni Abdoul Razak, Akpa Akpro Jean-Daniel Dave Lewis, Angoua Brou Benjamin, Arouna Kone, Aurier Serge Alain Stephane, Bamba Souleman, Barry Boubacar, Boka Etienne Arthur, Bolly Mathis Gazoa Kippersund, Bony Wilfried Guemiand, Cisse Abdoul Karim, Diarrassou Ousmane Viera na Dja Djedje Brice Florentin.

Doumbia Seydou, Gbohouo Guelassiognon Sylvain, Gosso Gosso Jean-Jacques, Kalou Salomon Armand Magloire, N’dri Koffi Christian Romaric, Sangare Badra, Serey Die Gnonzaroua Geoffroy, Sio Giovanni, Tiote Cheik Ismael, Toure Yaya Gnegneri, Traore Lacina, Ya Konan Didier, Yao Kouassi Gervais na Zokora Deguy Alain Didier.

Taifa Stars iko kambini hoteli ya Tansoma tangu iliporejea kutoka Marrakesh, Morocco ambapo leo na kesho itafanya mazoezi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 9 kamili alasiri. Ijumaa itapumzika, na itafanya mazoezi ya mwisho Jumamosi kwenye uwanja huo huo kuanzia saa 10 kamili.

Makocha wa timu zote mbili (Taifa Stars na The Elephants) watakutana na waandishi wa habari Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF kuzungumzia jinsi walivyojiandaa kwa mechi hiyo.

Kuziona Stars, Tembo wa Ivory Coast buku 5

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYAEJnMep386ng2e6L-Xp7ihgOGJ6Y1njuUmZTl3tWSLCFh0Aaet_MipiFJl65Wz1qUPMItFRmYeQybFVR7XwKmsCIBzzsYS1h-kpMJyhW6iERC_YNUPjIrqKnczOLYE4_0DWL42gZJfM/s1600/ltvSearch-Ivory-Coast-vs-Tanzania.jpg
Stars na Ivory Coast zilipochuana siku za nyuma

Na Boniface Wambura
KIINGILIO cha chini katika mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Ivory Coast (The Elephants) itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani.

Viti vya kijani katika uwanja huo wenye uwezo wa kumeza watazamaji 60,000 viko 19,648. Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu ambavyo viko 17,045 ni sh. 7,000. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 ni sh. 10,000.

Viingilio vya daraja la juu ni kama ifuatavyo; VIP C yenye watazamaji 4,060 ni sh. 15,000 wakati sh. 20,000 ni kwa VIP B yenye watazamaji 4,160. VIP A yenye watazamaji 748 kiingilio chake ni sh. 30,000.

Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo itakayoanza saa 9 kamili alasiri zitaanza kuuzwa siku mbili kabla ya mchezo (Ijumaa na Jumamosi) katika vituo vifuatavyo; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.

Katika vituo hivyo tiketi zitauzwa katika magari maalumu. Magari hayo pia yatafanya mauzo ya tiketi uwanjani siku ya mechi. Tunapenda kuwakumbusha watazamaji kutonunua tiketi mikononi mwa watu au katika maeneo yasiyohusika ili kuepuka kununua tiketi bandia, hivyo kukosa fursa ya kushuhudia mechi hiyo.

Utaratibu katika mechi hiyo utakuwa kama ilivyokuwa katika mchezo wa Simba na Yanga, ambapo hayataruhusiwa kuingia uwanjani isipokuwa kwa yale yatakayokuwa na sticker maalumu kutoka TFF.

Kitale, Montanabe wambeba Yosso

Yosso katika pozi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgjUX0UuRHZCjpum88LxYKRrQQH9fBvXBr0ag_0HocuumBL73z3ukSfyIUXEnGP0R-fe9rJ-i6FExclERL_nAl-9X_cknf204za2pnU8LPxlp8DDtHS8nXFG6YWbamC_rUGDjMHpekWpM3G/s1600/Kitale.jpg
Kitale katika pozi zake za 'kiteja'

MCHEKESHAJI ambaye kwa sasa ni mpiga picha wa filamu , Mussa Rashid 'Yosso' amejitosa kwenye muziki akijiandaa kuibuka na wimbo uitwao 'Mwanangu' alioimba akishirikiana na Mussa Yusuf 'Kitale' namuimbaji wa Extra Bongo, Michael Athanas 'Montanabe'.
Akizungumza na MICHARAZO, Yosso, aliyewahi kutamba na igizo la 'Sekeseke' lililorushwa na kituo cha ITV wakati akiwa na kundi la Kambarage, alisema wimbo huo umekamilika na kwa sasa anafanya mipango ya kuachia hewani ili mashabiki wake wapate uhondo.
Yosso, alisema wimbo huo upo katika miondoko mchanganyiko na ndani mwake Kitale na Montanabe wamefanya mambo makubwa katika kuunogesha ikizingatiwa hivyo ndiyo kazi yake ya kwanza na hivyo hakupenda kuanza vibaya ndiyo maana ameshirikisha wakali hao.
"Katika kukiendeleza kipaji changu cha muziki nilichokuwa nacho tangu mdogo kabla ya kujitosa kwenye uiogizaji, nimekamilisha wimbo wangu uitwao 'Mwanangu' ambao nimeimba pamoja na Montanabe wa Extra Bongo na Kitale, ni bonge la 'ngoma'," alisema.
Alisema wakati wimbo huo ukiandaliwa kuachiwa hewani, pia tayari ameshaanza kutayarisha nyimbo nyingine ili mara baada ya kufyatua video yake iwe rahisi kwake kurejea studio kuwapakulia mashabiki wake burudani zaidi.
Yosso, anayeandaa kipindi cha Vituko Show kama mpiga, alisema anaamini wimbo huo mpya utaonyesha ni jinsi gani alivyojipanga katika ulingo huo wa muziki baada ya kutamba kwenye uigizaji akipitia makundi ya Mtandao Arts, Dar Talent na Kambarage.

Miaka 13 ya Kikosi sasa kuanzishwa Juni 21


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghEkj6It8ASp1m0W0hdhVaUWKSvzQLRN6D7aJbqHj2Mrl5a5u2jTOTOhWw_yzmlCqCnwWH_fGuqhkDknHP6Wz9iPLA-X7klsuuOtve9KuPx-zOl5HAhpRxTcdRLalVIRNUuwxZEdo8Kl8/s1600/kalla+pina.jpg
Kalapina kiongozi wa Kikosi cha Mizinga

BAADA ya msiba wa Albert Magweha 'Ngwair' kusababisha kuahirishwa kwa onyesho maalum la maadhimisho ya miaka 13 ya kundi la Kikosi cha Mizinga, sasa onyesho hilo litafanyika Juni 21, huku idadi ya burudani ikiongezeka ikiwamo kuongezwa kwa Fid Q, Stereo na Hamidu.
Kiongozi wa Kikosi, Karama Masoud 'Kalapina' alisema baada ya kumpumzisha msanii mwenzao, sasa onyesho lao la miaka 13 ya Kikosi itafanyika Juni 21 kwenye ukumbi ule ule wa Msasani Club, kwa kila shabiki kujilipia Sh 5,000 ili kuhudhuria na kuburudishwa kwa tani yao na burudani zilizopangwa.
Kalapina alisema kati ya burudani zitakazosindikiza maadhimisho hayo mbali na wasanii mbalimbali kama Afande Sele, Nikki Mbishi, mshindi wa tuzo tatu za Kili Music 2013, Kala Jeremiah, Nash Mc wa LWP na Manzese Crew, pia mkalio Fid Q, Stereo na Dodo Hamidu 'Nyandu Tozi' watakuwepo.
"Pia tumepanga kufanya maonyesho ya uchoraji, kuimba Free Style, maonyesho ya mavazi na kutoa tuzo kwa wadau wote waliosaidia Kikosi cha Mizinga kufika hapa ilipo wakiwamo wanahabari, wadhamin, mashabiki an wengineo waliokuwa bega kwa bega na Kikosi tangu lianzishwe," alisema Kalapina.
Kalapina alisema ameona ni vyema kupeleka onyesho lake Juni 21 ili kutogongana na maonyesho ya wasanii wengine ambao yatafanyika wiki hii ambayo nayo yaliahirishwa kabla ya kifo cha Ngwair yakiwa yamepangwa kufanyika siku moja ya Mei 31 katika kumbi tatu tofauti.
Maonyesho hayo ni ya miaka 13 ya Lady Jaydee na lile la MwanaFA ambayo kama ilivyokuwa awali yote yafanyika siku moja Juni 14 yaani Ijumaa kwenye kumbi tofauti jijini Dar es Salaam.

Mwamuzi jela miezi 6 kwa kupanga matokeo ili apewe uroda


http://www.dutchreferee.com/wp-content/uploads/2013/03/ali-sabbagh-twitter-referee.jpg
Ali Sabbagh

REFA wa kimataifa na maarufu nchini Lebanon, Ali Sabbagh amehukumiwa kwenda jela baada ya kukutwa na hatia ya kupanga matokeo ya michezo uwanjani kwa malipo na ngono.
Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari za nchini Singapore, mwamuzi huyo ambaye amekuwa akicheza mechi mbalimbali za kimataifa zikiwamo za kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia amekutwa na hatia hiyo yeye na wasaidizi wake wawili na mahakama moja nchini Singapore.
Sabbagh, 34 inadaiwa amekuwa akipanga matokeo kwa minajili ya kulipwa ujira wa ngono na wanawake aliokubaliana nao, jambo lililomshangaza jaji aliyekuwa akiisikiliza kesi hiyo na kutoa hukumu hiyo Jumatatu wiki hii akihojikama kesi hiyo tu katutwa na hatua je ni michezo mingapi amekuwa akilipwa ujira huyo wa kubadilisha mechi kwa ngono?
Wasaidizi wake waliohukumiwa miezi mitatu kila moja kwa makosa hayo ni  Ali Eid, 33, na Abdallah Taleb, 37.
Inaelezwa waamuzi hao walikutwa na hatia ya kupanga matokeo katika pambano la Kombe la Shirikisho kwa nchi za Asia lililofanyika Aprili 3, kati ya klabu ya Singapore Tampines dhidi ya East Bengal ya India, iliyoshinda mabao 4-2 dhidi ya wenyeji wao.
Waamuzi hao wanadaiwa walifanya mipango hiyo wakishirikiana na mfanyabiashara anayesifika kwa dili za upangaji matokeo nchini Singapore, Ding Di Yang kwa kukubaliana na wanawake kupanga matokeo ya pambano kwa kulipwa mapenzi.
Wakili wa mwamuzi huyo, Gary Low, alisema haoni sababu ya mteja wake kuadhibiwa iwapo hakunufaika kifedha na mchongo huo anaoshutumiwa kuufanya ambao ni tuki jipya katika rushwa michezoni.

Simba yambakisha Kiemba, wamsubiri Ssenkoomi apone wampime

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiP0QuoB3LnN_dNgd3q1ieOi9oIREYb8lgwgkz80_MnS4-OLyCavzfGHUBYNeWWMtARhONNzwQmgVQl2PE66lM1wpAjdaqodESgwiQ3okTldAG890TZ1b5fQjWCR5TU69GJPgXettcRbxXM/s1600/KIEMBA+NA+MPIRA.jpg
Amri Kiemba

BAADA ya tetesi za muda mrefu kwamba kiungo mahiri nchini wa Simba, Amri Kiemba ametua kwa mahasimu wa Msimbazi, Yanga kwa kitita cha Sh. Mil 38, hatimaye ukweli umebainikwa kuwa uvushi huo haukuwa wa kweli baada ya uongozi wa Simba kumsainisha kiungo huyo kwa kitita cha Sh. Mil. 35.
Simba wamembakisha kiungo huyo kwa mkataba wa miaka miwili na kwamba umeondoa hofu ya mchezaji huyo kuhamia kwa Yanga akiwa amerejesha kiwango chake na kuonyesha soka la aina yake kiasi cha kurejea timu ya taifa, Taifa Stars.
Kwa mujibu wa wakala wa Kiemba, Ulimwengu Hamim, kiungo huyo alisaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kuichezea Simba jana mchana.

Habari za Kiemba ambaye pia anakipiga timu ya taifa ‘Taifa Stars’ kurejea Yanga alikowahi kuitumikia miaka ya nyuma, ziliibua mjadala na kuwaweka katika wakati mgumu mashabiki wa Simba, ambao bado wana kumbukumbu nyota mwingine, Mrisho Ngasa, ambaye alikipiga Msimbazi nusu msimu na hatimaye kurejea Jangwani.

Awali, Kiemba alidai kuwa soka ndiyo ajira yake hivyo kupitia kwa wakala wake, angeangalia pa kwenda patakapomridhisha.

Kiemba hivi sasa yuko kwenye midomo ya wapenzi na mashabiki wa soka, hasa baada ya mwishoni mwa wiki kuonyesha kiwango cha juu katika mechi ya kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia, kati ya Stars na Morocco, ambako bao lake liliacha gumzo. Katika mechi hiyo, Stars ililala 2-1 ugenini.

Katika hatua nyingine, kocha mkuu wa Simba, Abdallah Kibadeni, amesema licha ya kuumia kwa beki wao wa kimataifa, Samuel Senkoomi, raia wa Uganda, wanamsubiri aweze kupona ili aendelee kumchunguza ili kuona kama anawafaa katika kikosi chao.

Senkoomi beki aliyetua Msimbazi akitokea URA, aliumia kifundo cha mguu katika mazoezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Kinesi jijini Dar es Saalam.

Kibadeni, akizungumza mara baada ya kumaliza mazoezi kwenye uwanja huo, alisema, wanatarajia kumtumia mchezaji huyo, ila mpaka kiwango chake kimvutie ili aweze kusajiliwa.

“Nimemtazama, ila bado sijamtazama vizuri, kwa kuwa siku mbili tu za mazoezi akaumia, nasubiri aweze kupona halafu nimwangalie kama atatufaa,” alisema Kibadeni.

Aidha alisema anatarajia kupata kikosi cha kwanza wiki ijayo, baada ya nyota walioko timu ya taifa kuungana na wenzao.

“Ningeishapata kikosi, ila nawangoja vijana waliokuwa timu ya taifa, nina imani wakija nitapata kikosi cha kwanza,” alisema.

Kibadeni, nyota wa zamani wa Simba, Majimaji na Taifa Stars, amerejea Msimbazi kuchukua mikoba ya Mfaransa, Patric Liewig, ambaye katupiwa virago kutokana na matokeo mabovu, akitokea Kagera Sugar.

Kijana mbaroni kwa kumchinja mfanyakazi mwenzake


Mwili wa Perpetua ulipotolewa katika shimo la taka na Polisi (Picha:Hisia za Mwananchi)

http://1.bp.blogspot.com/-MVUICKkwko4/UIFMQ3WHVbI/AAAAAAAB1uU/oRJvBq38NN8/s640/Kovakamanda.jpg
Kamanda Kova
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu wanane, akiwamo mfanyakazi wa ndani anayetuhumiwa kumuua mfanyakazi mwenzake waliyekuwa wakifanya kazi nyumbani kwa Jaji Kileo kwa kumchinja kama kuku.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari jana.

Alisema Philemon Laiza (27), mkazi wa Mikocheni B, anatuhumiwa kuhusika na mauaji ya Perptua Maina (30) kwa kumchinja na kisha kutelekeza mwili wake kwenye dampo la takataka.

Kova alisema mtuhumiwa anashikiliwa na Polisi na upelelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani.

Katika tukio la pili, alisema watu wawili; Isaya Mafuru (31) na Yusufu Machela (33), wanatuhumiwa kwa uporaji wa mali za raia wa Sweden, Gisela Bergstorm katika maeneo ya Coco Beach.

Katika tukio la lingine, alisema watu wanne, ambao ni Thenase Benjijimana (26), raia wa Burundi, Said Hassan (37), mkazi wa Mbande, Obadia Bukuku (25) na Benedict Mohamed (32) wakazi wa Tabata, wanatuhumiwa kwa kukutwa na gari ya wizi aina ya Noah T 157 BWC, pamoja na pikipiki aina ya Boxer T 568 CDL.

Wote kwa pamoja wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya upelelezi zaidi.

Hivi ndivyo alivyopumzishwa marehemu Kashi

 
 
 
 
 
 
 
Pichani juu ni mazishi ya msanii ya mwigizaji  Jaji Khamis 'Kashi' aliyefariki juzi mchana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar yaliyofanyika jana mchana majira ya saa nane kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Marehemu Kashi alikumbwa na umauti baada ya kuugua ghafla malaria na kifua. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Kashi mahali pema peponi. AMEN!

Tuesday, June 11, 2013

MABONDIA WA JIJI DAR, MORO KUPAMBANA JUMAPILI 

KING CLASS MAWE 

Patrick  Kavako'Baunsa'





 

 

 

 

 

 

 

Bondia  Patrick Anthony Kavako 'Baunsa' wa Morogoro  ametamba kumsambalatisha Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mpambano wao wa raundi nane utakaofanyika siku ya jumapili june 16 katika ukumbi wa panandi panandi uliopo Ilala Bungoni Dar es salaam

Akizungumzia mchezo huo Kocha wa Kimataifa ambaye ni mratibu  wa mpambano huo Rajabu Mhamila 'Super D' alisema kuwa mpambano huo ni wa kukata na shoka ambao si wa kukosa kwani kila mmoja amejitahalisha kivyake hivyo wasubili tu siku ya mpambano huo

Unajua morogoro na Dar es salaam ni mahasimu katika michezo yote ukiangalia na sasa wamekutanishwa vijana katika masumbwi hivyo kila mmoja anaitaji ushindi ili ajiongezee rekodi yake kwani 'King Class Mawe' ato kubali kupigwa na Kavako ato kubali kabisa kupoteza mpambano wake kiraisi kwani na yeye anaitaji ajulikane katika ulimwengu wa masumbwi na kuiperekea sifa morogoro kama ilivyo kwa mabondia wengine wanao tamba mkoani hapo 
Mpambano huo ulioratibiwa na Kinyogoli Fondition kwa kushlikiana na PST itakuwa chachu kwa vijana kuendelea kuupenda na kuucheza mchezo huo unaopendwa na wengi nchini
mbali ya mpambano uho kutakuwa na mapambano mengine ya kukata na shoka bondia Abuu Mtambwe ataoneshana umwamba na Kassim Gamboo na Bondia mkongwe kabisa Yohana Robart atamenyana na Mussa Sunga
 
Kocha huyo wa kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini,Rajabu Mhamila ‘Super D’ ametoa DVD mpya 3 kwa ajili ya mafunzo ya mchezo wa ngumi ndani yake kukiwa na clips za mabondia  wanaofanya vizuri Tanzania kama Thomas Mashali vs Fransic Cheka na mambondia wengine mbalimbali

CD hizo zilizotengenezwa kwa umakini wa ali ya juu ambazo zitakuwa chachu kwa ajili ya kuvutia wapenzi na mashabiki mbalimbali kujua mchezo wa masumbi wakiwa wanangalia live mana DVD hizo zina maelekezo ya sheria mbalimbali ambazo zinatumika katika masumbwi

DVD hizo kwa sasa zinapatikana katika makutano ya barabara ya Uhuru na Msimbazi au unaweza kuzipata jengo la Azam lililopo mtaa wa Msimbazi karibu na kituo cha Polisi Post Gelezani kwingine ni GYM ya Amana iliyopo Ilala au unaweza kuwasiliana na kocha kwa simu 0713406938 ili uweze kupata DVD hizo kwa ajili ya kujifunza zaidi mchezo huo

Mbali ya kupatikana katika maeneo hayo pia
 
katika mchezo mbalimbali ya masumbwi kutakuwa na CD na DVD za mafunzo wa mchezo
huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.
Aliongeza kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo katika CD na DVD
hizo ni ya Kalama Nyilawila ,Japhert Kaseba,Rashidi Matumla, Hassani Matumla,Thomas Mashali Dhidi ya Francis Cheka, Mbwana Matumla na
Francis  Miyeyusho,Japhert Kaseba na Maneno Oswald, Said Mundi na King Class Mawe. 
 
 mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali 
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

“Ninatarajia kuwepo kwa ajili ya kuwauzia DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika Mpambano  ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi”, alisema Super D .

APPT Maendeleo yaifagilia Rasimu ya Katiba



http://www.thisday.co.tz/media/picture/large/Peter%20Kuga%20Mziray-%20%20APPT%20Maendeleo.jpg
Rais wa APPT Maendeleo, Peter Kuga Mziray
WAKATI Watanzania wa kada mbalimbali wakiendelea kuchambua na kutafakari juu ya Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyozinduliwa hivi karibuni Chama cha African Progressive Party of Tanzania (APPT Maendeleo) kimeibuaka na kuwataka waipokee kwa mikono miwili kwani rasimu hiyo imekuja kutatua kero zao.
Kauli hiyo imetolewa na Rais Mtendaji wa APPT Maendeleo Peter Kuga Mziray wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
Mziray alisema tangu rasimu hiyo izinduliwe rasmi 3/6/2013 kumekuwepo na mitazamo mbalimbali ya kuipongeza na kuipinga kwa baadhi ya watu ambao kimantiki wanaipinga  ni watu wenye  malengo yao ya kuwa Marais wa Tanzania jambo ambalo linaelekea kufa.
Alisema Watanzania hasa wale wa Bara wamekuwa na kilio cha miaka mingi cha kuhitaji uwepo wa Tanganyika kama ilivyo Zanzibar lakini hawakusika jambo ambalo kwa sasa limepatiwa muafaka na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Rais Mtendaji alisema mapendekezo ya Tume ni mazuri kwa asilimia kubwa kwani yamezingatia maoni ya watu wengi ambao walikuwa wakihitaji rasimu ya katiba iwe hivyo bila kuogopa vivuli vya baadhi ya watu ambao wamejionyesha dhahiri kutokubaliana nayo.
“Kimsingi naunga mkono mapendekezo ya Tume kwani yamezingatia mahitaji ya Watanzania wote wa Bara na Visiwani na pia yana nia ya kuhakikisha kuwa Tanzania inaendelea kudumu bila mitafaruku,” alisema.
Alisema wapo watu wameibuka na kusema Serikali tatu zitakuwa ni kuongeza gharama kubwa kuziendesha jambo ambalo sio kweli kutokana na ukweli kuwa kila nchi itakuwa ikitumia rasilimali zilizopo katika upande wake na kuchangia Serikali ya Muungano ambayo haitakuwa kubwa.
Mziray alisema mapendekezo ya Tume yameaanisha mambo muhimu katika muungano ambayo yapo saba jambo ambalo ni ishara tosha kuwa hakukuwa na serikali kubwa kama inavyofikiriwa.
Mambo ayalitajwa kuhusika na muungano ni pamoja na katiba na mamlaka ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, ulinzi na usalama wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, uraia na uahamiaji, sarafu na benki kuu, mambo ya nje, usajili wa vyama vya siasa na ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo na kodi yatokanayo na mambo ya muungano.
Aidha alisema rasimu hiyo imeenda mbali pale ilipoweka wazi kuwa ili mgombea wa Urais atangazwe anapaswa kushinda kura ambazo zitampatia 50 ya kura zote, pamoja na wagombea wa Urais kupata haki ya kuenda mahakamani kupinga matokeo.
Rais Mtendaji huyo pia alisema kupunguzwa kwa madaraka na kuwajibishwa kwa wabunge ambao hawafanyi kazi katika majimbo yao ni jambo muhimu ambalo Tume inapaswa kupongezwa kutokana na umuhimu wake hasa ukizingatia kuwa baadhi ya wawakilishi wa wananchi wamekuwa wakiishi mijini zaidi.
Maziray alisema pamoja na mapendekezo hayo ya tume ni vema mabaraza ya katiba yakapendekeza adhabu ambazo zinaweza kutolewa kwa utoro unaofanywa na wabunge jambo ambalo linaweza kurejesha hadhi ya Bunge ambalo kila siku linaonekana lipo wazi.
Kwa upande mwingine Mziray ameiomba Serikali kuanza mchakato wa uwepo wa Katiba ya Tanganyika ili iweze kuendana na mchakato wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jambo ambalo litarahisisha uwepo kwa serikali hiyo.
Alisema bila kuwepo kwa Katiba ya Tanganyika itakuwa ngumu kutekeleza mapendekezo ya Tume ambayo yanahitaji kuwepo kwa Serikali tatu ambazo ni Tanganyika, Zanzibar na Tanzania.
Rais Mtendaji alisema mchakato huo hautakuwa na kazi ngumu kwani ukweli unaonyesha kuwa maoni mengi ambayo yapo katika rasimu na yalioachwa yalikuwa yanahusu serikali ya Tanganyika.

Vita ya Ally Choki, Asha Baraka yafika pabaya


MKURUGENZI wa Extra Bongo Ally Chocky ametoa kauli nzito kuhusu waajiri wake wa zamani, Asha Baraka na Baraka Msilwa.

Katika maongezi yake  Chocky alisema katika watu asiowapenda duniani ni Asha Baraka (Mkurugenzi wa ASET) na Baraka Msilwa (Mwenyekiti wa ASET). Asha Baraka na Baraka Msilwa ni mtu na kaka yake.

Kiongozi huyo wa Extra Bongo akaenda mbali zaidi kwa kusema: “Nikifa leo hii Asha Baraka na Baraka Msilwa wasije kwenye mazishi yangu, na kama watanitangulia wao na mimi sitakwenda kwenye mazishi yao.

“Nina uhakika leo hii nikipata matatizo au nikifa Asha na Msilwa watafurahi, sasa kuna haja gani ya watu kama hao kuja kwenye mazishi yangu.

“ASET ni kama simba wako tayari kukutafuna hadi macho, nimetafakari kwa muda mrefu sana nimevumilia mengi sana lakini nimeshindwa na sasa natamka rasmi, Nikifa wasinizike.”

Chocky ameorodhesha sababu nyingi sana za kufikia hatua hiyo lakini miongoni mwa sababu zake ni hizi tatu:

Kwanza kitendo cha Aset kumpeleka mahakamani kumdai gari, pili Aset kukataa kurudisha pesa za Miraji Shakashia na tatu ni ASET kutothamini michango ya wasanii walioizalishia pesa nyingi.

Chocky ansema kitendo cha Aset kumpeleka mahakamani kumdai gari ambalo walimpa mwenyewe kilimkera sana.

“Mtu anapokupeleka mahakamani maana yake ni kwamba yupo tayari hata ufungwe, ukifungwa maana yake ni kila kitu kwenye maisha yako kinaharibika.

“Gari walinipa wenyewe na maandishi yapo kwamba nikimaliza mkataba wangu gari litakuwa la kwangu.

Lakini badala yake wakanigeuzia kibao na kwenda kunidai mahakamani kwamba nimeiba gari.

Kuhusu Shakashia, Chocky amesema mwanamuziki huyo alichukua shilingi milioni tano za Extra Bongo ili ajiunge nayo na akasaini mkataba wake.

“Lakini badala yake Shakashia akaingia mitini na pesa zetu, Aset wakasema watazirudisha wao na sasa wanakuja na hadithi mpya.

“Wanasema hawawezi kurudisha hizo pesa eti kwa vile wananidai, wanasahau kuwa mkataba wa Shakashia ni kati yeke na Extra Bongo na sio Ally Chocky.

“Hata kama kipo wanachonidai hiyo ni kati ya Chocky na Aset na haiingii akilini kuliingiza suala la Shakashia ndani yake.

“Huu ni utapeli na inatoa picha kuwa Aset walimtumia Shakashia kufanya utapeli huu, lakini wajue kuwa mwisho wa siku atakayeathirika ni Shakashia mwenyewe,” alisema Chocky.

Kuhusu kutothamini wasanii waliozalishia pesa nyingi kampuni, Chocky anasema wasanii walipota ASET na kuizalishia pesa hawana chochote walichopewa kulingana na thamani ya kile walichokizalisha. “Sio pesa tu bali hata heshima pia hakuna,” alifafanua Chocky.

Chocky akazama zaidi na kuwataja wakongwe kama Shem Karenga na Kasongo Mpinda ambao waliwahi kufanya kazi katika familia ya kina Asha Baraka kupitia bendi za MK Group na MK Beats.

“Wako wapi Kasongo Mpinda na Shem Karenga, Kasongo aliwatengenezea pesa nyingi kupitia MK Group “Ngoma za Magorofani” huku Shem Karenga  akiwatengenezea utajiri katika MK Beats “Tukunyema”.

“Lakini hebu tujiulize wako wapi hawa wazee na wana kipi cha kujivunia?” alihoji Chocky.
 
 Haikuishia hapo, tuliamua kumpigia Asha Baraka ambaye naye alikuwa na yake ya kujibu kuhusu  mapigo ya Chocky.

Asha Baraka amesema hayo ni mambo ya kike na kwamba kuzikana si tija.

Asha Baraka akasema: “Hata mimi sina mpango wa kwenda kwenye mazishi yake na yeye pia asije kwenye mazishi yangu.

“Hivi kuzikana ni nini? Wazazi wangu walifariki na Chocky hakuja kuzika, kilipungua nini? Halafu mi nikifa sitaona na yeye akifa sitaona kwahiyo hiyo siyo ishu, wamanyema wenzangu watatosha kunizika hata wasanii wote wasipokuja achilia mbali huyo Chocky.

“Nilimzikia wazazi wake na hakuliona hilo kwahiyo hata tusipozikana hakipungui kitu.

“Chokcy tunamdai gari na pesa shilingi milioni 13, kwenda mahakamani ni sehemu ya kudai haki na yeye kama anaona amedhulumiwa kuhusu pesa za Shakashia basi aende mahakamani.”

Asha Baraka alimtaka Chocky aelewe kuwa baadhi ya wasanii wa Twanga ni virusi na watammalizia pesa zake bure.

“Wako wasanii wamelelewa vizuri, wamefanyiwa mengi na Twanga na wanaelewa utu kwahiyo akijipendekeza kwao atapoteza pesa zake bure.

“Hao ni virusi wetu, wanatuletea taarifa zote za kila mtu anapotaka kuwachukua.


Asha Baraka amesema kama ni roho mbaya Chocky ndio anaoongoza kwa roho mbaya.

“Alikaa yeye na kamati yake yenye wakiwemo mpaka wafanyakazi wa umma na kuzoa wanamuziki wa Twanga”

Anawataja wasanii wa Twanga waliowahi kuchukuliwa na Extra Bongo ni pamoja na Ferguson, Rogart Hegga, Hosea, Otilya, Nyamwela, Danger Boy, Aisha Madinda, Maria Soloma, Subrina pamoja na Kanuti ambaye baadae alirudisha pesa zao na kubakia Twanga.

Asha Baraka anawataja wasanii wengine wenye damu ya Aset ambao wako Extra Bongo ni Ephraim Joshua, Martin Kibosho, Athanas, Banza Stone na yeye mwenyewe Chocky.

“Kwa mfumo huo utaona wazi kuwa Extra Bongo inapumua kwa nguvu ya Aset lakini sisi hatujasema kitu, kama ni kutoa kauli ya kutozikana basi sisi ndio tulipaswa kuwa wa kwanza,” alifafanua Asha.

“Tunajua pia kuwa Chocky alihusika kushawishi usajili wa Chaz Baba Mashujaa Band akiamini kuwa kwa kuondoka Chaz Twanga itakufa,” aliongeza

Asha Baraka amemtaka Chocky aonyeshe mfano wa namna ya kulea wasanii kwa kuwapa maisha mazuri wanamuziki waandamizi kama Banza na Rogart.

“Asiangalie mambo ya Aset, ajitazame yeye anaishi vipi na Banza anaishi vipi, badala ya kutoa milioni tano kumnunua Shakashia, angemnunulia japo Corola Banza au Rogart.

“Chocky aitishe mkutano wa waandishi wa habari halafu mimi na yeye twende na mikataba ya wasanii inayoonyesha mishahara na marupurupu tuone nani analea vizuri wasanii.

“Mimi nilifanya kazi Bima na sijajengewa nyumba wala kununuliwa gari, silalamiki kwa kuwa haikuwa sehemu ya makubaliano yetu.

“Kama Chocky anadhani muziki unalipa kiasi cha kumnunulia kila mtu gari na nyumba basi atuonyeshe mfano kupitia Extra Bongo.

“Kila baya linalomfika basi mchawi ni Aset, mbona mimi naumwa mguu na sijawahi kusema ni Chocky?

“Chocky akapime afya yake apate ukweli, tunajua rekodi ya sehemu alizopita, sasa asije akadondoka akasema ni Aset …akapime kwanza” alimaliza Asha Baraka.
 
MPEKUZI HURU

Bosi Masinde 'kulifufua' kundi la Shirikisho Msanii Afrika


Bosi Masinde katika pozi
MUIGIZAJI mkongwe aliyewahi kutamba na michezo ya kwenye runinga kupitia kituo cha ITV anayekimbiza kwa sasa kwenye filamu, Richard Mshanga 'Bosi Masinde' amesema anafikiria kulifufua upya kundi la Shirikisho Msanii Afrika baada yha kundi hilo kusambaratika kitambo.
Masinde, alisema wazo la kulirejesha upya kundi hilo katika 'uhai' baada ya kuzimika miaka kadhaa iliyopita inatokana na ushawishi anaopata kwa baadhi ya wasanii wenzake wa zamani pamoja na mashabiki ambao walikunwa na maigizo ya kundi hilo wakati likiwa kileleni.
Akizungumza na MICHARAZO, Masinde alisema Shirikisho Msanii Afrika halijafa kimoja, ila liligawanyika pande mbili mara baada ya yeye kujiweka kando na kulifanya kundi hilo lizimike tofauti na iliovyotamba enzi zake likitesa kituo cha ITV.
"Nimekuwa nikiombwa na baadhi ya wasanii nami nafikiria kama nirejeshe majeshi na kulifufua upya kundi hilo ambalo lifukuzana sambamba na Kaole Sanaa kama fitina hazijaingia na kuilisambaratisha," alisema Masinde.
Mshindi huyo wa tuzo ya Muigizaji Bora wa Mwaka wa ZIFF-2012, alisema anajihisi ana wajibu wa kuwarejeshea mashabiki wao burudani kama walivyoipata kupitia michezo kadhaa ilizotamba enzi zao kiasi cha kundi hilo kuwa 'gumzo' la jiji mbali na kuibua nyota kibao.
Enzi za kundi hilo lilitamba na michezo kama 'Tamu Chungu', 'Gumbizi', 'Hatia', 'Dumaza' na mingine huku likiwaibua mastaa wa sasa wa filamu nchini kama akina Amanda, Mama Kawele, Bakar Makuka, Aunty Ezekiel, Nyatawe na wengineo.

Machava yapeta RCL, kipute cha raundi ya 3 wikiendi hii


Na Boniface Wambura
MICHEZO ya kwanza za hatua ya tatu ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) kuwania nafasi tatu za kupanda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao zitachezwa Jumamosi (Juni 15 mwaka huu) wakati za marudiano zitachezwa Jumatano ya Juni 19 mwaka huu.

Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana leo (Juni 11 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za michezo iliyopita na kufanya uamuzi mbalimbali ikiwemo mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars na Machava FC ambayo haikuchezwa.

Machava FC ambayo ilishinda mechi ya kwanza iliyochezwa mjini Moshi kwa mabao 2-0 inaendelea katika hatua ya tatu kwa vile haikuhusika katika kukwamisha mchezo wa marudiano uliopangwa kuchezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma (DOREFA) kiliuhamishia mchezo huo kwenye Uwanja wa Mgambo mjini Mpwapwa kinyume na maelekezo ya Kamati ya Mashindano ya TFF. Kamati katika kikao chake cha awali iliekeleza kuwa mechi zote za RCL zitachezwa makao makuu ya mikoa isipokuwa kwa Morogoro ambapo timu ya Techfort FC iliruhusiwa kutumia Uwanja wa CCM Mkamba mjini Ifakara.

Hivyo timu nane zilizofuzu kucheza raundi hiyo ni Friends Rangers ya Dar es Salaam, Kariakoo ya Lindi, Katavi Warriors ya Katavi, Kimondo SC ya Mbeya, Machava ya Kilimanjaro, Njombe Mji ya Njombe, Polisi Jamii ya Mara na Stand United FC ya Shinyanga.

Wakati timu nyingine zimefuzu kwa kushinda mechi zao za raundi ya mbili, Njombe Mji imeingia hatua hiyo kwa kuwa timu yenye uwiano mdogo wa kufungwa (best looser) katika hatua ya pili.

Katika hatua hiyo mechi ni ifuatavyo; Kariakoo vs Friends Rangers, Machava FC vs Stand United FC, Polisi Jamii vs Katavi Warriors, na Kimondo SC vs Njombe Mji. Timu zilizoanza kutajwa ndizo zinazoanzia nyumbani.

Vilevile Kamati ya Mashindano imeagiza Kamishna wa mechi ya marudiano kati ya Mpwapwa Stars vs Machava FC, Mwijage Rugakingira wa Tanga ambaye alikwenda Uwanja wa Mgambo badala ya Uwanja wa Jamhuri kinyume na maelekezo ya TFF aondolewe kwenye orodha ya makamishna.

Pia waamuzi wa mechi hiyo ambao nao walikwenda Mpwapwa badala ya Dodoma Mjini wamepelekwa Kamati ya Waamuzi ya TFF kwa ajili ya kuchukuliwa hatua kutokana na tukio hilo.

Kamati ya Mashindano imekumbusha kuwa RCL ni mashindano yanayosimamiwa na TFF, hivyo maelekezo yoyote kuhusiana na mashindano hayo pia yatatoka TFF na si mahali pengine popote. Hivyo, msimamizi wa kituoa hana mamlaka ya kubadili uwanja.

Hatua ya nne ya RCL itachezwa kati ya Juni 23 na 23 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 29 na 30 mwaka huu.

PARTY YA LADY JAYDEE 'ANACONDA' IJUMAA HII SI YA KUKOSA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjzSsnvfgzuiBzhvHAdJtj8JnKhjDIlp_mjeidbuAC2oLPoUAJsBO5WWkH2NAAC3LvI41jBB_cOBUuoOWCo1PVHKxiIIEQLtxWNwtFt9M5W7bZ9jxlLzb9NAErM32e1Z_DaPD-Jn3upqoE/s1600/Jaydee+Balance.jpg

Waaljeria kuzihukumu Stars, Ivory Coast

Kocha Kim Poulsen akiwoanyesha kwa vitendo wachezaji wa Stars

Na Boniface Wambura

SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limeteua waamuzi kutoka Algeria kuchezesha mechi kati ya Taifa Stars na Ivory Coast itakayofanyika Jumapili saa 9 alasiri kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Waamuzi hao watakaochezesha mechi hiyo ya kundi C kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil wataongozwa na Charef Mehdi Abid atakayepuliza filimbi. Atasaidiwa na Hamza Hammou na Bouabdallah Omari wakati mezani atakuwa Sofiane Bousseter.

Abdi na wezake wanatarajiwa kutua nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 12 asubuhi kwa ndege ya EgyptAir. Mtathmini wa waamuzi ni Athanase Nkubito kutoka Rwanda ambaye atatua nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 12 jioni kwa ndege ya RwandAir.

Kamishna wa mechi hiyo ni Bernard Mfubusa kutoka nchini Burundi ambapo atawasili nchini Ijumaa (Juni 14 mwaka huu) saa 3.35 asubuhi kwa ndege ya Kenya Airways. Maofisa wote hao wa mechi hiyo watarejea makwao Jumatatu (Juni 17 mwaka huu).


Monday, June 10, 2013

Breaking Newzzz: Muigizaji nyota Kash afariki dunia



Jaji Khamis 'Kashi' enzi za uhai wake

 
Kash enzi za uhai wake
MUIGIZAJI nyota wa zamani wa kundi la Shirikisho Msanii Afrika, Jaji Khamis 'Kashi' amefariki dunia akiwa kalazwa hospitali ya Muhimbili.
Habari iliyotufikia jioni hii  zinasema kuwa Kash alifariki mchana wa leo hospitalini hapo alipokuwa amelazwa .
 Baadhi ya wasanii wenzake wa zamani wa kundi hilo lililotamba na maigizo yake kwenye kituo cha ITV, wamethibitisha kufariki kwa muigizaji huyo ambaye pia alikuwa akicheza filamu.
Kashi alitamba na wasanii wenzake kupitia michezo kama Tamu Chungu, Dumaza, Hatia, Gumbizi na mengine.
Wasanii waliokuwa akiigiza nao kabla ya kundi hilo kuzimika ni pamoja na Bakar Makuka 'Beka', Richard Mshanga 'Bosi Masinde', Samson, Vailet, Grace Mapunda 'Mama Kawele' na wengine.
Mwili wa muigizaji huyo unatarajiwa kuzikwa kesho Jumanne na msiba upo Kinondoni-Mkwajuni jijini Dar es Salaam.
Mungu ailaze roho ya marehemu Kashi mahali Pema Peponi Ameen.

Man City yamtolea macho Al ShaarawySp

Stephan Al Shaarawy
KLABU ya Manchester City inamtolea macho mshambuliaji kinda wa Italia anayeichezea AC Milan, Stephan El Shaarawy, japo mchezaji huyo kuitaka klabu hiyo kufanya kweli kama kweli inamtaka amesisitiza kuwa hafikirii kung'oka katika klabu yake ya sasa.
Habari zilizoripotiwa na gazeti la The Sun linasema kuwa kinda hilo linatakiwa Etihad kwa kitita cha paundi Mil. 30, lakini mwenyewe amenukuliwa akisema hafikirii kuondoka San Sirro.
"Sifikirii kuondoka Milan, iwapo City ni kweli inanihitaji mimi, ifanye hivyo, lakini nataka kubaki AC Milan, Mara zote najihisi kujiamini kwa sapoti ninayopewa na klabu, kocha Massimiliano Allegri na timu nzima," alisema.
"Pia nawashukuru wote kwa kunisaidia kuwepo kwenye timu ya taifa ya Italia," alisema mkali huyo wa mabao.

TCRA yaichimba mkwara Star Tv, kisa kujitoa Startimes




Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Prof. John Nkoma akitoa maamuzi kuhusu kujitoa kwa kituo cha Star Tv katikka king'muzi cha Star Times.

MAMLAKA ya Mawasiliano nchini, TCRA imeagiza kituo cha runinga cha Star tv kurejesha channel yake mara katika  Star Times kabla ya saa kumi jioni leo.

Aidha Star Times na Star TV wameelezwa kuwa wote wamevunja sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya 2010 na Kanuni zake na kutakuwa kujitetea tarehe 17 Juni 2013.

Agizo la kurudishwa kwa Chaneli ya Star TV linatakiwa kutekelezwa ili kuhakikisha kuwa wananchi hawanyimwi haki ya kupata habari.

Vile vile wote wametakiwa kufuata Sheria inapotokea kutokuafikiana badala ya kutoa maamuzi bila kumshirikisha Mdhibiti (TCRA

Lwakatare akwama tena kupata dhamana

Lwakatare (kulia) na mtuhumiwa mwenzake Ludovick wakiwa mahakamani leo.
 Baadhi ya wanachadema waliofika mahakamani leo.
Lwakatare akifunguliwa pingu.

Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Muganyizi Lwakatare, kwa mara nyingine ameshindwa kuwekewa dhamana leo katika kesi inayomkabili ya kujaribu kumwekea sumu Dennis Msaki iliyosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisuru jijini Dar es Salaam. 

Sababu za kuahirishwa kesi hiyo ni madai ya hakimu kuwa hakuweza kupata muda wa kupitia mafaili ya kesi hiyo maana alikuwa likizo. Lwakatare amerudishwa Segerea na kesi yake imetajwa kurudishwa mahakamani kesho asubuhi (Juni 11 mwaka huu).

MAP kutumia michoro kutoa elimu dhidi ya Sickle Cell

Mchoro unaonyesha Red cell na tatizo la Sickle Cell
Na Suleiman Msuya
TAASISI ya Motion Art Production (MAP) inatarajia kufanya onyesho la michoro mbalimbali Juni 17 mwaka huu katika Jumba la Makumbusho ya Taifa lengo likiwa ni  kutoa elimu na ufahamu dhidi ya ugonjwa wa maumbile mabaya ya damu (sickle cell).
Hayo yamebainishwa na Mwasisi wa taasisi hiyo Honeymoon Aljabri wakati akizungumza na mwandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Alisema watatumia maonyesho hayo kujadiliana na watu mbalimbali ambao watatembelea kuona michoro yao ambayo itakuwa inahusu rasilimali mbalimbali zilizopo hapa nchini kwa kutambua kuwa upo uwezekano wa kutokomeza ugonjwa huo ambao unau watu wengi.
Aljabri alisema ugonjwa huo wa sickle cell umesahaulika lakini takwimu zinaonyesha kuwa unamadhara makubwa kwa jamii hasa katika nchi zinazoendelea Tanzania ikiwa moja wapo.
“Sisi tunajihusisha na mambo ya sanaa lakini nimekaa na kufikiri kuwa nina wajibu wa kutoa mchango wangu katika jamii kwa njia nyingine hivyo nitatumia michoro mbalimbali ambayo ninachora kutoa elimu na kujadiliana jinsi ya kutokomeza ugonjwa huu,” alisema.
Mwasisi huyo wa taasisi ya MAP alisema pamoja na kutumia maonyesho hayo pia wanatarajia kufanyua matembezi ya kilometa tano mwezi Septemba ambapo ni maadhimisho ya ugojwa huo.
Alisema katika matembezi hayo wanatarajia kuchangia damu pamoja vitu mbalimbali ili kuweza kuwasaidia waathirika wa ugonjwa huo hapa nchi.
Aljabri ametoa rai kwa Watanzania kuunga mkono juhudi hizo kwani madhara ya ugonjwa huo ni makubwa hivyo ni wajibu kwa kila mtu mwenye uwezo kuweza kusaidia ili kuweza kufikia malengo waliojiwekea.
Aidha Mwasisi huyo wa MAP alisema pamoja na juhudi zao hizo malengo yao ya kudumu ni kufungua kituo cha taarifa ambacho kitasaidia watu wenye sickle cell kupata taarifa wapi wanaweza kupata huduma kwa urahisi.
Pia alisema kwa mwaka huu wataendesha kampeni hiyo katika mkoa wa Dar es Salaam  pekee lakini matarajio yao ni kuhakikisha kuwa kwa miaka ijayo wanafanya kazi katika maeneo yote ya nchi.

Salvatory Mtebe aitamani Simba

Mtebe (kushoto) akimdhibiti Jerry Santo
BEKI mahiri wa klabu ya soka ya Mtibwa Sugar, Salvatory Mtebe aliyebakisha mwaka mmoja kabla
ya mkataba wake na klabu yake ya sasa kuisha amesema anatamani kutua Msimbazi, kuichezea Simba.
Aidha beki huyo wa zamani wa Kagera Sugar na Athletico ya Burundi, amejipigia debe akidai anaweza kuwa suluhu ya ukuta wa Simba ambao tangu umpoteze Kelvin Yondani na Joseph Owino 'haujatulia'.
Akizungumza na MICHARAZO mapema leo beki huyo wa zamani wa Taifa Stars, alisema pamoja na kwamba amebakisha mwaka mmoja wa mkataba wake na Mtibwa, angependa kutua Msimbazi moja ya
klabu kubwa na zenye mafanikio makubwa kisoka.
Mtebe alisema anadhani kutua kwake Msimbazi kuitaweza kutengulia kitendawili cha tatizo la beki
wa kati iliyonayo klabu kwa kipindi kirefu sasa kwa kujiaminia uwezo alionao.
"Mimi bado nina mkataba wa mwaka mmoja Mtibwa, lakini kama nitapata klabu ya kuichezea sintakuwa na tatizo, kuna wakati Simba walikuwa wakinifuatilia lakini wakasitisha mipango pengine kwa kukwepa gharama za uhamisho, lakini nadhani mie nitawafaa sana pale kati, alisema.
Mtebe alisema kama Simba itashindwa kumnyakua bado milango i wazi kwa klabu nyingine yoyote
itakayokuwa inamhitaji mradi imalizane na uongozi wa klabu yake kwa ajili ya uhamisho wake na kuahidi kuifanyia makubwa kama anavyofanya akiwa na kikosi chake cha sasa akiwa na uwezo pia wa kupachika mabao kama alivyofanya kwa msimu wa ligi ilioisha hivi karibuni.

Hali ya kiafya ya Mzee Mandela sivyo nzuri tumuombeeni

Nelson Mandela, Winnie, Jacob ZumaRais mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela akisaidiwa kutembea na Rais wa Jacob Zuma kushoto na mke wake wa zamani, Winnie Mandela kulia katika picha ya hivi karibuni nchini Afrika ya Kusini.
RAIS mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela, angali katika hali mbaya ingawa imeweza kudhibitiwa huku akiwa amelazwa katika hospitali moja mjini Pretoria.
"mzee Mandela yuko hospitalini na hali yake bado haijabadilika.''
Maombi yakekuwa yakifanywa makanisani kote nchini Afrika Kusini kumuombea Mandela amb
aye anatibiwa kwa ugonjwa wa mapafu.

Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 94, alipelekwa hospitalini mapema Jumamosi , ikiwa ni mara ya tatu kulazwa hospitalini mwaka huu.Nelson MandelaMzee Mandela akifurahia jambo na watoto nyumbani kwake hivi karibuni.
Kwa mujibu wa duru za urais, Mandela amekuwa akiugua kwa muda mjini Johannesburg baada ya kukumbwa tena na ugonjwa wa mapafu.

Alilazwa hospitalini baada ya hali yake kuwa mbaya zaidi mnamo Jumamosi.

Kwa mujibu wa taarifa za urais, Rais President Jacob Zuma, amerejelea wito wake kwa watu nchini Afrika Kusini kumuombea Madiba wakati huu anapougua.

Lakini mwandishi wa BBC mjini Pretoria, Karen Allen, anasema kuwa kuna matumaini amdogo kuwa Mandela aliyeongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, huenda kupona.

Anasema kuwa wengi walipata matumani baada ya bintiye Mandela Zindzi, kusema kuwa babake yuko salama na kuwa anaendelea kupata nafuu.

Mkewe Mandela Graca Machel, alifutilia mbali, ziara yake mjini London Jumamosi ili kuwa kando ya mumewe.

Mandela alikuwa Rais wa Afrika Kusini kati ya mwaka 1994 hadi 1999.

Alifungwa jela miaka 27 na anaaminika kuwahi kuugua ugonjwa wa mapafu alipokuwa akifanyishwa kazi ngumu katika machimbo ya mawe akiwa jela. 
 
BBC

KIBANDA USO KWA USO NA DK BILAL JIJINI DAR ES SALAAM


2 7b5b3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mhariri wa Jukwaa la Wahariri na Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006) Ltd, AbsalomKibanda, wakati alipofika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Juni 10, 2013 kwa mazungumzo. Kibanda alimtembelea Mhe. Makamu ili kumwelezea hali yake kiafya inavyoendelea baada ya matibabu. Picha na OMR