STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 16, 2013

Waliokufa Darfur waagwa, JWTZ lakana ongezeko la vifo



WAKATI miili ya wanajeshi saba wa Tanzania waliouwawa huko Darfur, Sudan wakiagwa kwa heshima nchini humo na kuanza mipango ya kurejeshwa nchini kwa ajili ya mazishji yake, Jeshi la Watanzania Tanzania, JWTZ, limekanusha taarifa za kuwepo kwa ongezeko la vifo vya askari wake.
Msemaji wa jeshi hilo. amenukuliwa hivi punde na Clouds FM kwamba hakuna askari mwingine aliyefariki japo alikiri mmoja wa majeruhi wa tukio hilo hali yake ni tete kiasi cha kuhamishwa hospitali aliyokuwa akipewa huduma na wenzake 9 na kupelekwa Khartoum kwa matibabu zaidi.
"Hatujui hizi taarifa zinazowekwa kwenye mitandao ya kijamii wanazipata wapi wakati sisi ndiyo wenye kuhusika na tukio, ila ukweli ni kwamba hakuna idadai iliyoongezeka ya vifo na jeshi halina sababu ya kuficha kitu," alisema Kanali Kapambala Mgawe Msemaji wa JWTZ.
Kanali Mgawe alisema hali za majeruhi wengine tisa zinaendelea vyema kiasi cha kuweza kutembea wenyewe japo mwenzao mmoja amehamishiwa Khartoum kwa matibabu zaidi na kuwataka watanzania wasiwe na hofu wala kuziamini taarifa hizo zinazoandikwa na kuwekwa kila muda katika mitandao hiyo.
"Watanzania hawana haja ya kuwa na hofu hali za askari wetu zinaendelea vyema japo mmoja hali yake siyo nzuri sana na kulazimika kuhamishiwa mjini Khartoum kwa matibabu zaidi na wenzake tisa tunashukuru kwani wanaendelea vyema," alisema.
Hapo chini ni baadhi ya picha za miili ya wanajeshi hao ikitolewa heshima na wanajeshi wenzao, sambamba na majeruhi waliolazwa baada ya tukio hilo la kushambuliwa na waasi wakati katika msafara wao wa kulinda amani katika jimbo hilo la Darfur.


The African Union – United Nations Mission in Darfur (UNAMID), held a memorial ceremony, in Nyala, the capital of South Darfur, to honor the seven fallen peacekeepers who lost their lives in the 13 July attack in South Darfur. The bodies are scheduled to be repatriated to Tanzania, the home country of the fallen peacekeepers. In addition to the seven killed, 17 military and police personnel were wounded, among them two female Police Advisors, all of whom are recovering from their injuries in UNAMID’s hospital in Nyala, South Darfur. Photo by Saidi Msonda, UNAMID.












 On 14 July 2013, following a 13 July attack in which seven military peacekeepers of the African Union - United Nations Mission in Darfur (UNAMID) were killed and 17 military and Police personnel wounded, among them two female Police Advisers, Joint Special Representative Mohamed Ibn Chambas visited the wounded peacekeepers at UNAMID’s hospital in Nyala to provide encouragement and support. Photos by Albert González Farran, UNAMID.


Casillas amkwamisha Kaseja kutua Mtibwa Sugar

http://api.ning.com/files/yP-BaUmjm1TVvubOvsoSqSDjHM5i*EFqxCiKIcJqP*Hp44nQRbrCsfGtyPFzTEVokJ7c7hN7dlExU4cM0Rphezsk191ETtnq/KASEJA.jpg?width=366
Juma Kaseja
http://www.ippmedia.com/media/picture/large/hussein%20sharrif%20%5C%27Casil.jpg
Hussein Sharrif 'Casillas'

KUKWAMA kwa kipa Hussein Sharrif 'Casillas' kujiunga na Fc Lupopo baada ya klabu yake ya Mtibwa kushindwa kuafikiana dau na timu hiyo ya DR Congo kumemfanya 'Tanzania One', Juma Kaseja kushindwa kutua Manungu kuichezea timu hiyo kwa msimu ujao wa Ligi Kuu.
Kaseja aliyetemwa na Simba baada ya kuitumikia miaka karibu 10, alikuwa akitajwa kuwa mbioni kusajili wa Mtibwa, lakini Mkurugenzi wa klabu hiyo, Jamal Bayser aliiambia MICHARAZO muda mchache uliopita kuwa, mpango huo umekufa baada ya Casillas kukwama kutua Lupopo.
Casillas alifuzu majaribio katika klabu hiyo ya Ligi Kuu ya DR Congo na alikuwa katika maandalizi ya kuondoka kwenda kujiunga na timu hiyo wakati klabu hizo mbili zikifanya mazungumzo ya mwisho kuhusu dau la uhamisho wake.
Hata hivyo Bayser alisema kuwa  mazungumzo hayo ya Casillas kuhamia Lupopo yamekwama baada ya Wakongo kushindwa  kuafiki dau walilokuwa wakilitaka na hivyo kipa huyo atasalia Mtibwa kwa msimu ujao na kwa maana hiyo hawana mpango na kipa mpya.
Bayser alisema walikuwa na dhamira ya kumnyakua Kaseja iwapo mazungumzo baina yao na Lupopo yangeenda vyema kwa Casillas kuondoka, lakini kw ahali ilivyo wamesitisha mipango ya kumsajili Kaseja ambaye alimtaja kama kipa bora ambaye kila timu inatamani iwe naye.
"Mazungumzo yetu na Fc Lupopo juu ya kuwapa Casillas yamekwama na hivyo kipa huyo atasalia Mtibwa na kwa maana hiyo hatuna haja ya kumuongeza kipa yeyote mpya kama ambavyo tulikuwa tumepanga tukimfikiria Kaseja," alisema Bayser.
Bayser aliongeza pia klabu yao haina mpango wowote wa kusajili mchezaji kutoka nje ya nchi na badala yake wataendelea kuwaamini vijana wazawa kama walivyofanya msimu uliopita na kumaliza ligi wakiwa katika nafasi ya tano.
Kwa wiki moja sasa kulikuwa na tetesi kwamba huenda Kaseja aliyetemwa Simba angetua Mtibwa Sugar au Coastal Union, kabla ya Coastal kuweka bayana kuwa haina mpango naye.

Dereva wa Bodaboda afa, wengine wajeruhiwa katika ajali

e47f5cfc9fL 
Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi, Handeni.
DEREVA mmoja wa Bodaboda amefariki dunia papo hapo na wengine wanne kujeruhiwa kwenye ajali baada ya pikipiki mbili kugongana usukani kwa usukani huko kwenye eneo la Mzundu wilaya ya Handeni mkoani Tanga.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga ACP Constantine Massawe, amemtaja Dereva huyo wa Bodaboda kuwa ni Ismail Mhando(30), mkazi wa Kabuku wilayani Handeni. Amesema kuwa ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Mzundu wilayani Handeni mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo katika uchunguzi wa awali wa tukio hili Polisi walibaini kuwa imesababishwa na mwendo kasi kwa kila mmoja na kutokuwa makini barabarani.
 
Amesema marehemu Mhando akiendesha pikipiki yenye nambari za usajili T.256 AYM akitokea Kabuku kwenda Mzundu akiwa amempakia dada mmoja aitwaye Salama Bakari, aligongana na pikipiki nyingine iliyokuwa ikitokea Mzundu kwenda Kabuku yenye namba za usajili T.584 CCS. Alisema pikipiki hiyo ikiendeshwa na Sudi Nassoro ilikuwa imepakia abiria wawili maarufu kama mshikaki na ilikua ikitokea katika kijiji cha Mzundu kwenda Kabuku wilayani humo.
 
Kamanda Massawe amesema majeruhi wanne wa ajili hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni kwa matibabu zaidi na hali zao amesema zinaendelea vizuri.
 
Kamanda Massawe ametoa wito kwa Madareva wote wa Bodaboda kuwa makini wanapokuwa barabarani na kujiepusha na upakiaji abiria zaiidi ya mmoja ili kuepuka matukio ya ajali zinazowahusisha watu wengi kwa wakati mmoja.
 
Amewataka kila mmoja wao kuwa mlinzi wa mwingine na kutoa taarifa pale wanapomuona mwenzao mmoja anavunja sheria na kutotii sheria bila ya shuruti ili achukuliwe hatua ili kuwanusuri wengine wanaofanya kazi zao vizuri.


Kifo mkweli ahadi! Fundi anusurika kifo licha ya kuchomwa chuma kichwani

Liu Fenghe akiwa hospitali na chuma kichwani
Picha ya X-ray ikionyesha jinsi chuma hicho kilivyoingia kichwani mwa bwana Liu. (Picha: HAP/Quirky China News/Rex)

FUNDI majengo Liu Fenghe wa nchini China, amenusurika kifo baada ya kuchomwa na chuma kichwani na kuzama inchi 8 ambazo ni sawa na sentimita 20.

Liu alikuwa akiongea na rafiki yake na kwa bahati mbaya alidondokewa na chuma hicho kilichomchoma kichwani.

Rafiki yake Liu aitwaye Zhang anasema:
"Ilikuwa ghafla. Kabla sijafanya chochote Liu alikuwa katika dimbwi la damu."Inadhaniwa kuwa chuma hicho kilidondoka kutoka ghorofa ya 25 ya jengo walilokuwemo mafundi hao mpaka kusababisha maafa hayo.
Madaktari walimfanyia upasuaji wa haraka katika hospitali iliyopo jimbo la Shanghe nchini China na kueleza kuwa Liu hayupo tena katika hatari japo bado haijajulikana ni lini ataweza kurudi kazini.

Fabregas azikata maini Arsenal, Man United

2013 cesc fabregas barcelona
Cesc Fabregas

SIKU moja tu baada ya klabu ya Manchester United kutangaza kuongeza dau ili kumnasa nahodha wa zamani wa mahasimu wao Arsenal, Cesc Fabregas, kiungo huyo ameikata maini timu hiyo.
Kiungo huyo wa timu ya taifa ya Hispania anayeichezea Barcelona alikuwa chaguo la kwanza la David Moyes baada ya kumkosa Thiago Alcantara, pia alikuwa akiwindwa na klabu yake ya zamani. Hata hivyo  kocha wa Barcelona, Tito Vilanova amefichua kuwa,  aliongea na kiungo huyo na kumwambia kuwa kwamba anahitaji kuendelea kubaki Camp Nou.
Jana iliripotiwa kwamba United walituma ofa ya kwanza ya kiasi cha £25.9 million  kwa ajili ya kumsajili Fabregas, ambaye amefeli kupata nafasi katika kikosi cha kwanza tangu aliporudi akitokea Arsenal.
Lakini akiongea na waandishi wa habari leo mchana, Vilanova amesema wazi kwamba Fabregas bado anataka kubaki kwenye klabu yake hiyo ya utotoni, na hana mawazo ya kuondoka.
 "Ninafahamu kwamba tumepokea ofa kadhaa kutoka kwa vilabu tofauti. Niliongea na Cesc na ameniambia kwamba anataka kubaki.
"Cesc hana mawazo ya kuondoka kwenda klabu nyingine. Anajua ushindani ni mkubwa hapa na ana ndoto za kuendelea kuwa hapa na kufanikiwa.


MIUJIZA! Mtoto azaliwa na Tasibhi shingoni mwake

clip_image001KATIKA tukio la kustaajabisha, mtoto mmoja huko nchini Nigeria amezaliwa akiwa na tasbihi shingoni mwake na kuwashangaza wengi akiwemo wakunga waliomzalisha mama wa mtoto huyo.
Maelfu ya watu walifika hospitali binafsi ya uzazi kwenye jiji la Kotaworo eneo la Bida, iliyopo jimbo la Niger  Jumapili, kwa lengo la kwenda kumshuhudia mtoto wa kike aliyezaliwa akiwa amevaa Tasbihi inayotumika katika utajo wa Mwenyezi Mungu shingoni mwake.
Inaelezwa kwamba mama wa mtoto huyo ambaye ana miaka ya kati, Adijat, alikimbizwa hospitali karibu na nyumbani kwa  Mohammed Bello Masaba, mida wa saa 8 mchana na baada ya pilika za uzazi alifanikiwa kujifungua mtoto huyo.
Kwa mujibu wa mmiliki wa hospitali hiyo ya uzazi, Alhaji Abubakar Baiwa Shasha ambaye ndiye aliyesimamia zoezi hilo la kujifungua alisema; 
“Nilishtuka nilipoona mtoto anatoka akiwa na Tasbihi shingoni mwake, na wakati wa uzazi mtoto alizaliwa tasbihi hiyo ilikuwa nyeusi," alisema Shasha.
“Ila nilishangaa baada ya muda tasbihi hiyo ilibadilika na kuwa nyeupe huku kukiwa na watu wengine wamezunguka.”
“Mara baada ya habari hiyo kusambaa mjini, maelfu ya watu walifika kwenye hospitali hiyo ya uzazi huku wakisema “Allahu Akibar; Allahu Akibar (Mungu ni Mkubwa) huku wakifika na kumgusa mtoto huyo.”
Juhudi za kumpata Baba wa mtoto huyo aitwaye Isah, ambaye anatokea eneo la Loma ndani ya Jimbo la Kwara  zilishindikana baada ya kukataa kuongea na mtoa habari.
Mwanachuo mmoja wa Kiislamu, Malam Idiris Ndajiwo alisema, kuzaliwa kwa mtoto huyo akiwa na kitu kama hicho inaonyesha ukuu wa Allah (SW). Kuzaliwa kwa mtoto huyu leo, kwenye mji huu na eneo hili (Kutaworo) ni kitu kikubwa kwa Waislamu. Hii hakika inakuja kuonyesha kwamba Allah ndiye mwenye kupanga kwa lolote kutokea kwa yeyote kwenye ulimwengu huu.”

Pigo! Jaji Chipeta afariki dunia




Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Buxton Chipeta enzi za uhai wake
HABARI zilizopatikana hivi punde zinasema kuwa aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu Tanzania,Buxton Chipeta amefariki dunia muda mfupi uliopita.

Kwa mujibu wa mmoja wa wanafamilia, Jaji Chipeta alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kisukari ambapo ilifikia wakati akalazimika kukatwa vidole kadhaa vya miguuni.

Enzi za uhai wake, Jaji Chipeta aliweza kujijengea heshima katika kazi yake na kufikia kuwa mmoja wa majaji wanaoheshimika mno hapa nchini.
 

Pia Jaji Chipeta aliwahi kuwa miongoni mwa majaji wa Tume ya kurekebisha Sheria yeye akiongoza kanda ya Dar es Salaam.
 

MICHARAZO  inaungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki cha majonzi ya kuondokewa na mpendwa wao na kuwaombea kwa Allah Subhana Wataala kuwa na subira na uvumilivu kwa kuamini kuwa kila nafsi itaonja mauti na kurejea kwa aliyetuumba. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema.

Walimu Shule ya Msingi King'ongo wawalia wazazi, kisa utoro wa wanafunzi



UONGOZI wa Shule ya Msingi King'ongo, iliyopo Kata ya Saranga, wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam, umelia na vitendo vya utoro uliokithiri kwa wanafunzi wanaosoma shule hiyo hasa wale wa darasa la saba na kuwaomba wazazi wa wanafunzi hao kuingilia kati kuwasaidia.
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Flora Salila alitoa kilio hicho katika mkutano wa pamoja kati yao na wazazi wa wanafunzi wa darasa la saba uliofanyika juzi shuleni hapo.
Mwalimu Salila, alisema uongozi wao umekuwa katika wakati mgumu kutokana na vitendo vya utoro kwa wanafunzi na hasa wa darasa la saba, ambapo kuna wakati hufikia mpaka wanafunzi 58 kati ya 268 wa darasa hilo la saba kutoonekana shuleni.
Mwalimu huyo alisema vitendo hivyo huenda vinachangiwa na wazazi kutojenga utamaduni wa kufuatilia maendeleo ya watoto shuleni na kuwapa wakati mgumu walimu ambao hujaribu kutatua tatizo hilo la utoro bila mafanikio kwa kukosa ushirikiano na wazazi.
"Lazima niwaeleze ukweli kuwa, utoro ni tatizo sugu shuleni kwetu hasa hawa wa darasa la saba kwa mfano karibu wanafunzi 58 miongoni mwa 268 wa darasa hilo hawakuwepo shuleni wakati wa upigaji wa picha za maandalizi ya mitihani, hii siyo jambo zuri, wazazi tusaidieni," alisema.
Aliongeza kwa jumla ya wanafunzi 1762 waliopo shuleni hapo kwa siku watoto kati ya 100-200 huwa hawafiki shuleni na kuhoji wazazi wenye watoto hao wanafanya nini katika kuwasaidia walimu kuwaondoa watoto katika vitendo hivyo vinavyochangia kudumaza taaluma.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Shule hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa King'ongo,  Demetrius Mapesi alisema ni lazima wazazi washirikiane na walimu kutatua utoro shuleni hapo iwapio wanataka shule yao iendelee kushika nafasi ya pili katika Kata ya Saranga.
Mapesi alisema wazazi wamekuwa wakishindwa kufuatilia nyendo za watoto wao na kuishia kuwatumia lawama walimu pale watoto wao wanapofanya vibaya kwenye mitihani wakati jukumu hilo ni la lazima kwao kabla ya walimu kufuatia hasa wanapokuwa shuleni.
"Wazazi badilikeni, kutofuatilia nyendo za watoto wenu ndiyo chanzo cha kuharibika kwa vijana, dunia ya sasa imeharibika na haiaminiki, ukijifanya upe bize na kazi ujue unazalisha watoto machangudoa, vibaka na hata mashoga, mtakuja kumlaumu nani," alihoji Mapesi.

Mwisho

Polisi Dar wawanasa watuhumiwa wa ujambazi, mbakaji

wanachuo walipoandama baada ya tukio la kuvamiwa na kupigwa risasi kwa wenzao na majambazi waliokamtwa na jeshi l polisi

WATU wanne wanaodaiwa kuwa majambazi wamenaswa na Jeshi la Polisi  Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za kuhusika na tukio la ujambazi lililotokea Juni 21, mwaka huu, katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), katika eneo la bweni la Yombo One.
Aidha mtu mwingine anayedaiwa kumlewesha kwa dawa za kulevya kisha kumbaka kabla ya kumpora mfanyabiashara nyumbani kwake naye katiwa mbaroni na jeshi hilo baada ya kuendesha msako dhidi yake.
Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda hiyo, Ally Mlege, alisema watuhumiwa wanne waliohusika na tukio la Chuo Kikuu,  walikamatwa na jeshi hilo Julai 8, mwaka huu, kwenye kituo cha Daladala Ubungo.
Kamanda Mlege, alisema jeshi hilo lilifanikiwa kuwakamata watu hao wakiwa na silaha aina ya SMG ikiwa na risasi moja, laptop mbili aina ya Toshiba, simu aina ya Samsung, panga moja na nyundo.
Alisema baada ya mahojiano, majambazi hayo yalikiri kuhusika katika tukio la unyang’anyi lililotokea UDSM.
Afande Mlege, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Dolisera Gerald (22), Leonard Mathias (21), Leonard Leopard (32), Gerald Moses (23), ambao licha ya kukiri kuhusika katika tukio hilo pia  walikiri kuhusika katika matukio mbalimbali ya kihalifu sehemu tofauti jijini.
Wakati huo huo Kamanda Mlege alisema jeshi hilo limemtia mbaroni mkazi wa Kimara, jijini Dar es Salaam, Ezekiel Matiti (35), kwa tuhuma za kumlewesha dawa za kulevya mkazi wa Makongo Juu, jijini humo, Aida Kiangi.
Kwa mujibu wa Mlege baada ya mtuhumiwa kumlewesha Aida, alimpeleka nyumbani kwake (Makongo Juu) na kumuingiza ndani na kumbaka na kisha kumuibia runinga, pamoja na vitu mbalimbali vyenye thamani ya Sh. milioni nane.
Aidha aliongeza kuwa, katika tukio lingine, polisi inawashikilia Michael Pascal (35), Donald Joseph (43), Kulwa Adamson (43), na Ally Akiri (41),  na watuhumiwa wengine watano, kwa tuhuma za kuhusika katika tukio la kurushiana risasi na askari polisi eneo la Kunduchi Mtongani.

Hussein Javu atamani soka la kulipwa

Hussein Javu (kulia) akikabana na Aggrey Morris wa Azam katika moja ya mechi za igi Kuu

MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya Mtibwa Sugar, Hussein Javu amesema anatamani kupata nafasi ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchini bila kujali kama ni Afrika au barani Ulaya, ili kutimiza ndoto zake za tangu utotoni.
Javu, aliye katika kikosi cha pili cha taifa 'Young Taifa Stars' alisema ipo mipango anaiweka sawa ili kutimiza ndoto hizo za kucheza soka la kulipwa akiwa tayari kutua kokote hata kama ni nchi jirani za Kenya, DR Congo au Msumbiji.
Alisema kwa sasa anamsikilizia wakala wake kuona mipango hiyo inakwendaje, ingawa alisisitiza kuwa bado ana mkataba wa kuitumikia timu yake ya Mtibwa hadi mwakani.
Mshambuliaji huyo ambaye amekuwa wakitajwa kama miongoni mwa wachezaji wapya wa Yanga, ingawa mwenyewe anakanusha kuwa hajasaini kokote zaidi na kujitambua kama mchezaji wa Mtibwa kulingana na mkataba aliokuwa nao na klabu hiyo aliyojiunga nayo tangu mwaka 2007 katika kikosi cha vijana, alisema kiu ya kucheza soka la kulipwa ni kubwa kiasi cha kutoelezeka.
"Hakuna kitu ninachokitamani na kulilia kama kwenda kucheza soka la kulipwa nje ya nchi, kuna mipango inafanywa lakini siwezi kuiweka wazi kwa sasa kwa vile ni mapema, ila nitafarijika sana kama nitaenda hata Kenya tu," alisema.
Javu anayemhofia dimbani beki wa zamani wa Simba aliyehamia Coastal Union Juma Nyosso, alisema kiu yake ya kucheza nje ya nchi imeongezeka baada ya kuona mafanikio ya wachezaji wenzake wa timu ya taifa, Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu na watanzania wengine wanaocheza soka hilo barani Afrika katika nchi za DR Congo, Kenya, Msumbiji na Angola.
Pia aliweka bayana kwamba mbali na kiu ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi, pia angependa kuichezea timu mojawapo kubwa nchini kati ya Simba na Yanga ambazo zimekuwa zikimuwinda ili kumsajili.

Maugo, Mwakyembe kutimka J4 ijayo kwenda Urusi

Mada Maugo
MABONDIA machachari wa Ngumi za Kulipwa nchini, Mada Maugo na Benson Mwakyembe wanatarajia kuondoka nchini wiki ijayo kwenda Russia kwa ajili mapambano yao ya kimataifa dhiddi ya wenyeji wao itakayochezwa mwishoni mwa mwezi huu.
Rais wa TPBO-Limited, Yasin Abdallah 'Ustaadh', aliiambia MICHARAZO mabondia hao wataondoka Julai 23, ambapo Maugo ataenda kupigana na Movsur Yusupov na Mwakyembe ataonyeshana kazi na Apti Ustarkhanov kwenye michezo itakayochezwa kwenye ukumbi wa Trade &Intertainment uliopo mji wa Kasiysk, nchini Russia.
Ustaadh alisema watanzania hao watapigana na Warusi hao katika michezo ya kilo 75 (Super Middle Weight) itakayokuwa na raundi nane kila mmoja.
Rais huyo wa TPBO alisema mpinzani wa Maugo rekodi yake inaonyesha kuwa amecheza mapambano matatu na yote ameshindwa moja likiwa kwa KO wakati mpinzani wa Mwakyemba amecheza mechi mbili na kushinda moja na mwingine kupigwa.
"Pamoja na rekodi ndogo za wapinzani wao, lakini ikumbukwe kuwa mabondia wa Russia na kwingineko Ulaya huwa hawachezi ngumi za kulipwa bila kucheza ngumi za ridhaa na kufikia hatua ya kushiriki michuano ya Olimpiki kwa maana hiyo Maugo na Mwakyembe wakitarajiwe wepesi Russia," alisema Ustaadh.
Ustaadh aliongeza kuwa tayari mabondia hao wa Tanzania wameshaombewa visa za kwenda nchini humo gharama zote zikilipwa na TPBO-Limited na wataondoka nchini wakiongoza na wakala wao kutoka Kenya, Thomas Mutua atakayeondokea Kenya na kukutana na mabondia hao Dubai.

Monday, July 15, 2013

CHADEMA KUFUTWA? TENDWA ALIPUKA




Msajili wa vyama vya siasa nchini, John Tendwa.
MSAJILI wa Vyama vya Siasa Tanzania, John Tendwa ameibuka na kusema sasa anaandaa kalamu yake kukifuta Chama kikuu cha upinzani nchini CHADEMA.
Katika Taarifa yake kwa vyombo vya habari muda mfupi uliopita Tendwa amesema CHADEMA wanataka kuanzisha kikundi cha mgambo ambacho ni kinyume na sheria, katiba ya nchi na sheria za usajili wa vyama.
Msajili huyo amesema kwamba kama madai ya CHADEMA ni kuanzisha kikundi cha kujilinda dhidi ya Green Guard wa CCM madai hayo hayana msingi wowote kwani kama CHADEMA wana taarifa kwamba Green Guard wanahatarisha amani basi wanapaswa kuripoti suala hilo polisi ili lifanyiwe kazi kwa mujibu wa sheria.
Tendwa amezidi kuonya kwamba uamuzi wake ni wa mwisho na atakapoifuta CHADEMA maamuzi yake hayapingwi popote kisheria.
Source: JF

Manchester United sasa yamgeukia Fabregas

Cesc Fabregas
 BAADA ya kumkosa kiungo Thiago Alcantara aliyetimkia kwa Mabingwa wa Ulaya, Bayern Munich, klabu ya Manchester United imeelekeza shabaha yake kwa kiungo wa zamani wa Arsenal anayeichezea Barcelona, Cesc Fabregas.
Mashetani Wekundu hao, wameamua kuweka mezani kitita cha pauni 26 ili kumnasa nyota huyo wa Hispania ili atue Old Trafford.
United imepania kumnasa mkali huyo ikichuana na Arsenal ambao pia wameonyesha nia ya kumrejesha kiungo huyo Emirates baada ya kumuuza miaka miwili iliyopita kwa dau la pauni milioni 31.
Ofa iliyotangazwa na United kwa Fabregas ni pungufu ya kiasi cha Pauni Milioni 5 kufika dau la Pauni Mil 30.75 inayoendelea kushikilia rekodi ya mchezaji wa bei ghali kusajiliwa OT ilipomnunua mshambuliaji wa Tottenham, Dimitar Berbatov mwaka 2008. 
Duru za soka zimekuwa zikisema kuwa kuna uwwezekano mkubwa kwa Cesc kurejea Arsenal licha yha kwamba mwenyewe alishanukuliwa kwamba angependa kuendelea kuichezea Barcelona kwa vile anafurahia kuwepo hapo ili kupigania nafasi katika kikosi cha kwanza cha timu.
Kama atatua kwa United, kutamfanya nahodha huyo wa zamani wa Arsenal kuungana tena na mchezaji wenzake wa zamani wa Emirates Robin van Persie ambaye alihama klabu hiyo na Arsena msimu uliopita na kufanikiwa kutwaa nao taji la ubingwa wa EPL.

Rais Kikwete ateta na uongozi wa Benki ya TIB

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo toka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Maendeleo ya TIB, Bw Peter Noni, Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 13, 2013. Bw. Noni na ujumbe wake walifika Ikulu kumwelezea Rais Kikwete mipango na mikakati kabambe ya kuijenga upya benki hiyo iliyokuwa ikijulikana kama Tanzania Investment Bank (Benki ya Rasilimali Tanzania) ikiwa ni pamoja na miundo mbinu na upanuzi wa wigo wa biashara. PICHA NA IKULU
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Maendeleo ya TIB, Bw Peter Noni, Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 13, 2013. Bw. Noni na ujumbe wake walifika Ikulu kumwelezea Rais Kikwete mipango na mikakati kabambe ya kuijenga upya benki hiyo iliyokuwa ikijulikana kama Tanzania Investment Bank (Benki ya Rasilimali Tanzania) ikiwa ni pamoja na miundo mbinu na upanuzi wa wigo wa biashara.

'Mesut Ozil aondoki Santiago Bernabeu'

Mesut Ozil

BABA wa kiungo wa Real Madrid, Mesut Ozil, amesema mwanae hana mpango wa kuondoka Santiago Bernabeu.
Ozil amekuwa akitajwa kutaka kwenda kucheza Ligi Kuu ya England, lakini baba wa mchezaji huyo,  Mustafa amefichua kuwa mwanae hana mpoango huo badala yake anahitaji mkataba mpya wa kuendelea kuitumia timu yake.
Ozil mkubwa alisema mwanae mwenye umri wa miaka 24 ndiyo kwanza amefungua meza ya mazungumzo ya kusalia klabu hapo tofauti na hisia kwamba angependa kumtikia Engaland.
Ozil, nyota wa Kijerumani anatajwa thamani yake ni Pauni Mili 30 na alikuwa akiwindwa na klabu kubwa za Engand, lakini baba yake alisisitiza kuwa; "Mesut anafuraha kubwa ndani ya Madrid," alisema Mustafa na kuongeza imani yao dili mpya kati ya mwanae na klabu yake itambakisha mkali huyo mpaka 2019.

Arsenal bado yamng'ang'ania Suarez sasa yaongeza dau la kumng'oa Liverpool

Luis Suarez

KLABU ya Arsenal bado haijakata tamaa na nia yake ya kumng'oa mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay, Luis Suarez kutoka Liverpool kwa kudaiwa ipo tayari kuongeza dau hadi kufikia pauni Mil. 35 mradi iimnyakue mkali huyo wa mabao.
Suarez amekuwa chaguo la kwanza la kocha Arsene Wenger katika usajili wa majira ya joto na iko tayari kutoa dau zaidi ya ile ya awali ya pauni Mil.30 iliyokataliwa na Liverpool wanaotaka angalau pauni Mil 40.
Klabu hiyo ya London ya Kaskazini inachuana na Manchester City na Real Madrid zinazomfukizia pia 'mtukutu' ambaye amekuwa na wakati mgumu nchini England kutokana na kuandamwa na vyombo vya habari hasa kwa kadhia zake tata za hivi karibuni katika EPL.
Wenger amekuwa akimhitaji mshambuliaji huyo huku pia akimwinda Higuian Gonzalo ambaye bado haijafahamika kama itakuwa naye katika msimu ujao baada ya kuelezwa amejiunga na timu yake ya Real Madrid kuanza mazoezi.
Hata hivyo kuna kila dalili Arsenal kumnasa mshambuliaji huyo wa Argentina na iwapo itafanikiwa kuishawishi Liverpool kumuachia Suarez itakuwa imelamba dume baada ya kuwa misimu karibu nane isiyo na tija yoyote England na kimataifa.

TBL yakabidhi Simba fedha za mkutano wao



KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia yake maridadi ya Kilimanjaro Premium Lager, leo imekabidhi hundi ya Sh. Milioni 20 kwa klabu ya Simba kwa ajili ya mkutano mkuu wa klabu hiyo utakaofanyika Julai 20, 2013 jijini Dar es Salaam.
Akikabidhi hundi hiyo, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema: “Tunakabidhi fedha hizi ikiwa ni mwendelezo kutekeleza majukumu yetu kama mdhamini mkuu wa Simba SC. Kwa kuzingatia hilo tungependa kuona maendeleo ya klabu ya Simba uwanjani na nje ya uwanja,”.
“Tunaiunga mkono klabu hii katika mkutano wake mkuu tukiamini kuwa mkutano huu utaimarisha uhusiano uliopo kati ya klabu na wanachama wake kwa kuwapa fursa ya kuhakiki mwelekeo wa klabu yao waipendayo,”alisema.
“Ikiwa na mamilioni ya mashabiki nchini, klabu hii imejengeka kutokana na rekodi nzuri ya mafanikio kwa muda mrefu – na Kilimanjaro Premium Lager inajivunia kuwa sehemu ya klabu hii,”.
“Tunaamini kwamba mbali na wanachama, wapenzi na mashabiki wa Simba kuona timu yao ikishinda lakini pia tunatambua kwamba ni haki yao ya msingi kuwasiliana na klabu na kupata taarifa mbalimbali za mwenendo wa klabu,”.
“Kutokana na sababu hizi, sisi kama wadhamini wakuu wa klabu hii tunatoa mchango wa shilingi milioni ishirini ili kuunga mkono jitihada za klabu kuendelea kuwajibika kwa wanachama wake,”.
“Tunatambua wajibu wetu kama wadhamini wakuu wa Simba katika kutekeleza mkataba wetu, tutaendelea kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha tunalipeleka soka la Tanzania kwenye kilele cha mafanikio huku tukiwaburudisha na bia yenu muipendayo Kilimanjaro Premium Lager – Bonge la Kiburudisho”.

Rais JK awalilia wanajeshi waliokufa Darfur


Amir Jeshi Mkuu wa Tanzania, Rais Jakaya Kikwete
  Rais Jakaya Kikwete, ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ameeleza kushtushwa na kuhuzunishwa na mauaji ya wanajeshi saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliokuwa wanalinda amani Darfur, Sudan baada ya kushambuliwa na waasi wa Sudan.
Katika shambulizi hilo ambalo pia wanajeshi wengine 14 walijeruhiwa, pia ametuma salamu za rambirambi kwa JWTZ na kwa familia za wafiwa wote.
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais iliyotolewa jijini Dar es Salaam jana ilisema kuwa Rais Kikwete anaungana na Watanzania wote na hasa maofisa na wapiganaji wa JWTZ na familia za wafiwa kuomboleza vifo vya askari hao na anawaombea walioumia katika tukio hilo wapone haraka na kuendelea na majukumu yao ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa.
Katika salamu zake za rambirambi kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange na familia za wafiwa, Rais Kikwete na Amiri Jeshi Mkuu amesema:
“Sina maneno ya kutosha ya kuelezea mshtuko, huzuni na masikitiko yangu makubwa kufuatia vifo vya vijana wetu hao ambao wamepoteza maisha yao katika shughuli muhimu sana ya utekelezaji wa majukumu ya Umoja wa Mataifa ya kulinda na kuleta amani katika eneo la dunia ambako maelfu kwa maelfu ya watu wamepoteza maisha yao kwa kushambuliwa na waasi.”

“Napenda kwa niaba ya Watanzania wenzangu niwahakikishieni kwamba hakuna shaka kuwa vijana wetu hao tokea walipokwenda  Darfur Februari mwaka huu, na kwa hakika tokea Tanzania ilipoanza kuchangia walinzi katika eneo hilo mwaka 2007, wamefanya kazi nzuri sana, kazi iliyoongozwa na weledi wa hali ya juu na kazi ambayo imeiletea nchi yetu heshima kubwa.
Tutaendelea kuwaenzi kwa kujivunia kazi yao,” amesisitiza katika salamu hizo. Kupitia kwa Jenerali Mwamunyange, ametuma salamu za rambirambi kwa maofisa wakuu na maofisa wadogo pamoja na wapigaji wote wa JWTZ kwa kupotelewa na wenzao.
“Aidha, kupitia kwako, nawatumia salamu zangu kwa wanafamilia za waliopotelewa na wapenzi wao na ndugu zao katika tukio hilo.
Wajulishe kuwa naungana nao katika kuomboleza. Wajue kuwa uchungu wao ni uchungu wangu pia na wa Watanzania wote na kuwa kwa pamoja tunamwomba Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu.
Vile vile kwa pamoja tunamwomba Mwenyezi Mungu azilaze peponi roho za marehemu,” alisema.
Wanajeshi waliouawa na kujeruhiwa walikuwa sehemu ya askari 37 na ofisa mmoja ambao walikuwa wanasindikiza msafara wa waangalizi wa kijeshi huko Darfur kutoka eneo la Khorabeche kwenda Nyara waliposhambuliwa na waasi kiasi cha kilomita 20 kutoka Khorabeche saa tatu asubuhi Jumamosi iliyopita.
JWTZ YAPELEKA KIKOSI KUCHUNGUZA
Wakati guo huo, JWTZ  limetuma kikosi maalum kwenda  nchini Sudan  kufanya uchunguzi kuhusu mazingira ya kuuawa kwa wanajeshi saba wa Tanzania huko  Darfur.

Vile vile, Jeshi hilo limesema linaendelea kufanya mawasiliano na Umoja wa Mataifa (UN),  kuangalia namna ya kuongeza uwezo wa kujilinda na mashambulizi pindi kikosi cha Tanzania cha kulinda amani kinapokabiliana na mashambulizi ya aina hiyo.

Akitoa taarifa ya awali kwa waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaama, Msemaji wa Jeshi hilo ambaye ni Mkurugenzi  wa Habari na Uhusiano,  Kanali Kapambala Mgawe, alisema tukio hilo lilitokea juzi asubuhi baada ya kikundi cha askari 36 kutoka Tanzania akiwamo ofisa wao mmoja kushambuliwa na kikundi cha waasi wa Sudan.

Mgawe alisema  msafara huo uliojumuisha maafisa na askari kutoka mataifa mengine ambao pia walijeruhiwa,  ulishambuliwa  umbali wa kilomita  20 kutoka  Makao Makuu ya Kikosi hicho.

Mgawe alisema tukio hilo lilitokea katika eneo la sheria ya ulinzi wa amani (chapter 6) ambayo hairuhusu mashambulizi ya silaha.

“Kwa kuwa mazingira ya sasa  Darfur hayapo katika sheria inayoruhusu mashambulizi, hivyo tunaendelea kuwasiliana na UN  na kuwaomba kubadili sheria hiyo ili kuruhusu kutumika ile ya chapter 7 kwa ajili ya kukiwezesha kikundi chetu kujilinda pindi kinapokabiliwa na  mashambulizi ya aina hiyo,” alisema Mgawe

Kadhalika,  Mgawe alisema mpaka sasa taratibu zilizokwishafanyika ni kuhamisha miili ya marehemu kutoka eneo la tukio na kupelekwa Nyara ambako kuna  Hospitali kuu ya eneo la Operesheni kwa ajili ya kuhifadhiwa na majeruhi kupatiwa matibabu.

Pia alisema wanawasiliana na familia za marehemu hao,  na kwamba utaratibu huo ukikamilika majina ya askari hao yatatangazwa.

“Wanajeshi wetu wamepatwa na mkasa huo wakiwa katika utekelezaji wa jukumu lao la Umoja wa Mataifa la kulinda amani nchini Sudan eneo la Darfur,  kwa utaratibu wa Kijeshi hatuwezi kutangaza majina yao mpaka tuwasiliane na familia zao kwanza,” alisema.

Mgawe alisema taarifa hiyo ni ya awali na kwamba taarifa zaidi juu ya tukio hilo  zitaendelea kutolewa.

Hii ni mara ya pili kwa wanajeshi wa Tanzania kuuawa katika Jimbo la Darfur, ambapo Agosti mwaka jana , Kanali Mgawe alinukuliwa na vyombo vya habari akithibitisha kutokea kwa vifo vya askari watatu ambao gari lao lilizolewa na maji walipokuwa wa kivuka mto uliokuwa umefurika maji, huku wakiwa katika utekelezaji wa jukumu lao la Umoja wa Mataifa la kulinda Amani nchini humo.

CHANZO: NIPASHE

Mugabe atoa mpya, ataka mashoga, wasagaji wapeane mimba la sivyo...!

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe
 RAIS wa Zimbabwe, Robert Mugabe ametoa kali ya mwaka kwa kuwachimba mkwara Mashoga na Wasagaji kwamba wasipotiana mimba ni lazima atawafunga jela.
Mubabe ametoa kali hiyo Ijumaa  wakati akizindua kampeni za chama chake cha kwa ajili ya uchaguzi utakaofanyika mwezi.
Isome taarifa nzima ya rais huyo mwenye umri mkubwa aliye madarakani duniani na ambaye wazungu wanambloo kwa misimamo yake isiyoyumba.
 President Robert Mugabe on Friday threatened to jail gay and lesbian couples who fail to conceive any offspring as he launched his party’s campaign for this month’s general election.

The Zanu PF leader also attacked bitter rival and coalition partner Morgan Tsvangirai for his bed-hopping habits saying it was inconceivable that such a character could want to lead the country.

Mugabe, a rabid critic of homosexuality returned to the theme as he addressed thousands of supporters in Harare’s Highfield township.

He said he was shocked to learn that US President Barack Obama had called on African countries to embrace the practice.

The Zanu PF leader said in Shona: “Ndakanzva Obama achiti ah, dai muno muAfrica mabvuma kuti murume nemurume vachate, mukadzi nemukadzi vachate, ndikati nhai nhai, taitoti baba vako zvaari mutema, iwe uneruva neruzivo netsika dzevatema waakunotora zvevarungu futi!

Apparently joking Mugabe added: “So how would they (gay couples) have children?

“I should like to shut them-up in some room and see if they get pregnant; if they don’t then its jail because they have claimed they can have children. So, to that kind of rot, we say no, no, no, no!”

Continuously breaking into laughter as he warmed up to his gay bashing, Mugabe further criticised the Anglican Church for blessing homosexual marriages which he said was taboo among Africans.

He dared lesbians who assume the role of the husband in their relationships to prove that they were indeed ‘men’.

“Women are also engaged in this vile activity. We have some claiming to be men but what is it that makes you a man?

“Show us your manhood; you want to make other women your wives and you the husband? Well, that is madness; we refuse to accept that,” he said.

Polisi Tanga wanasa kete za dawa za kulevya

Baadhi ya dawa za kulevya vinazonaswa nchini
WIMBI la biashara ya dawa za kulevya linazidi kushika kasi baada ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga limefanikiwa kukamata kete 46 za dawa za kulevya aina ya Cocaine baada ya kufanya msako kwenye maeneo yanayosadikiwa wanakaa watumiaji wa dawa hizo wilayani Pangani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constatine Massawe, alisema jana kuwa dawa hizo zilikamatwa Jumatano iliyopita baada ya polisi kuvamia eneo hilo na kuwakamata watumiaji wanne.
Alisema polisi walifanikiwa kukamata dawa hizo kutokana na taarifa walizopata kutoka kwa raia wema.
Aliwataja waliokamatwa katika tukio hilo ambao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kuwa ni Shaban Ramadhan (20), mvuvi na mkazi wa Malindi wilayani Pangani, Mohamed Kijiba, mkazi wa Fungoni na Iddi Hamdan (21), mkazi wa Fungoni mjini Pangani ambao wote ni wavuvi.
Kwa siku za karibu janga la dawa za kulevya limezidi kushika kasi na kuonyesha wazi 'vita' dhidi ya dawa hizo ni kama hazizai matunda kutokana na kila uchao kunaswa 'unga' ambao huingizwa nchini toka ng'ambo.

Mbishi Real ataka watanzania kuutakaa udini

Mbishi Real katika pozi
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Fred Kaguo 'Mbishi Real' ameibuka na kampeni mpya ya kuwahamasisha watanzania kuepuka vitendo vya kibaguzi vya udini na ukabila iitwayo 'Tanzania Tuukatae Udini'.
Akizungumza na MICHARAZO, Mbishi anayetamba na nyimbo kadhaa ikiwamo 'Tozi wa Mbagala' alisema kampeni hiyo ni maalum kwa kutaka kuwakumbusha Watanzania kuwa wote ni wa moja na hakuna aliye bora zaidi ya wengine.
"Hakuna asiyejua hali inayoendelea nchini kwa sasa japo ni kwa chinichini, hivyo kama msanii nimeona nitumia kipaji changu kuwahamasisha watanzania wenzangu kuukata udini ili kutovunja umoja wetu tuliokuwa nao kwa muda mrefu," alisema.
Mbishi alisema kampeni hiyop ambayo kwa sasa inatafutiwa wadhamini ili kuanza rasmi baada ya kumalizika kwa mfungo wa Ramadhani utafanyika nchini nzima kwa kushirikisha maonyesho mbalimbali ya sanaa ikiwamo nyimbo toka wa wasanii na makundi tofauti.
"Ni kampeni niliyopanga kuifanya nchi nzima kuwahamasisha wenzangu na itaambatana na burudani mbalimbali, kwa sasa najiandaa kupeleka maombi serikalini na kwa wafadhili ili kufanikisha vyema kilichjokusudiwa kwenye kampeni hiyo," alisema Mbishi.
Mbishi alisema matrukio machache yaliyotokea katika baadhi ya maeneo ya nchi yenye kuhusiana na masuala ya kidini kama yale ya kugombea kuchinja na milipuko ya mabomu kanisani na kukojolewa na kuchanwa kwa Qur'an ni dalili mbaya kwa Tanzania yenye amani.


CHADEMA noma yaigaragaza CCM udiwani Arusha



 Polisi wakimsihi Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  aondoke nje ya kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu, pamoja na makada wa CCM hawako pichani ambapo walitakiwa kukaa mita 200 badala ya mita 100. Katika uchaguzi huo Chadema imeshinda katika kata zote nne. (Picha zote na Ferdinand Shayo)
 Polisi wakimsihi Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  aondoke nje ya kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu, pamoja na makada wa CCM hawako pichani ambapo walitakiwa kukaa mita 200 badala ya mita 100.
 Makarani wa uchaguzi wakiingiza masanduku ya kura katika ofisi ya kata ya Kimandolu kutoka  kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi kimandolu. 
Makarani wa uchaguzi wakiingiza masanduku ya kura katika ofisi ya kata ya Kimandolu kutoka  kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi kimandolu. 
 Polisi wakiimarisha ulinzi katika lango kuu la kuingilia  kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu katika uchaguzi ulifanyika leo mjini Arusha. 
 Mkazi wa kata ya kimandolu akichomvya wino mara baada ya kukamilisha zoezi  la kumchagua diwani wa kata hiyo liliofanyika Julai 14 katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata.
 Mkazi wa Kata ya Kimandolu akitumbukiza kura yake wakati wa uchaguzi wa madiwani uliofanyika mjini Arusha.
 Mkazi wa kimandolu,Juliana Mosha akitumbukiza kura yake katika sanduku la kura katika uchaguzi wa madiwani uliofanyika jana kuziba nafasi  ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo,zoezi hili lilifanyika katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata
 Dina Naftal Mkazi wa kata ya kimandolu akitumbukiza kura yake katika sanduku la kura katika uchaguzi wa madiwani kuziba nafasi  ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo, zoezi hili lilifanyika katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata.
 Wakala wa chama cha siasa akihakiki kitambulisho cha mpiga kura kabla ya kuruhusiwa kupiga kura ya kumchagua diwani wa kata hiyo ya Kimandolu, zoezi hili lilifanyika katika kituo cha kupigia kura cha ofisi ya kata
 Wakazi wa kimandolu wakifuatilia majina yao kwa makini ili kufahamu vyumba husika vya kupigia kura.
 Wakazi wa kimandolu wakifuatilia majina yao kwa makini ili kufahamu vyumba husika vya kupigia kura.
Wakazi wa kimandolu wakifuatilia majina yao kwa makini.
 Wakazi wa kimandolu wakifuatilia majina yao.
Polisi akiwasogeza wananchi waliokuwa karibu na kituo cha kupigia kura cha Shule ya msingi Kimandolu ambapo walitakiwa kukaa umbali wa mita 200 na sio mia 100 kama ilivyozoeleka.

Benki ya CRDB yafuturisha wateja Znz


Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa CRDB ya Benki, TullyEsther Mwambapa akizungumza katika hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake.
 Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum Zanzibar Machano Othman Said akizungumza wakati wa hafla ya kufuturisha wateja wa benki ya CRDB iliyofanyika mjini Zanzibar.
 Wadau mbalimbali wakipata futari.
 Wafanyakazi wa benki ya CRDB wakijumuika pamoja.
Baadhi ya wateja wa benki ya CRDB katika hafla ya kufuturisha.
Baadhi ya wateja wa benki ya CRDB wakiwa katika hafla hiyo.
Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum Zanzibar Machano Othman Said akizungumza katika hafla hiyo.
Meneja wa benki ya CRDB tawi la zanzibar, Nassor Uzigo akipata Chai.
 Wafanyakazi wa benki ya CRDB wakishiriki katika hafla ya kufuturisha iliyofanyika mjini Zanzibar.
 Wafanyakazi wa benki ya CRDB pamoja na wateja wakipata futari.
 Baadhi ya wateja wa benki ya CRDBwakipata futari.
Wadau wakipata futari.
 Meneja Mahusiano wa Benki  ya CRDB, Godwin Semunyu akigawa futari kwa wateja wa benki hiyo katika hafla ya kufuturisha iliyofanyika katika hoteli ya Zanzibar Beach Resort
Wateja wa benki ya CRDB wakipata futari.
 Wadau mbalimbali wakipata futari.
 Meneja wa benki ya CRDB tawi la Zanzibar, Nassor Uzigo lililopo eneo la Mkunazini mjni Zanzibar akipata chai wakati wa hafla ya kufuturisha  iliyoa andaliwa na ben
Sheikh akiomba duah.
Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum Zanzibar Machano Othman Said akishiriki katika uomba dua wakati wa hafla hiyo.
Picha ya pamoja.
Wafanyakazi wa benki ya CRDB pamoja na wadau wa benki hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa kwaza wa Rais Fatma Abdull Habib Fereji (wa tatu kulia) 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa kwaza wa Rais Fatma Abdull Habib Fereji (kulia) akizungumza mara baada ya hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na benki ya CRDB mjini Zanzibar.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa CRDB ya Benki, TullyEsther Mwambapa (wa pili kushoto) akimsikiliza kwa makini Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa kwaza wa Rais Fatma Abdull Habib Fereji wakati wa hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na benki ya CRDB kwa ajili ya wateja wake.