STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 5, 2013

Wafanyakazi TTCL wafanya usafi Muhimbili kuadhimisha siku ya Mazingira Duniani

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu nchini TTCL wakijumuika kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo wafanya kazi hawo walikuwa wakiungana na watu wote duniani kuadhimisha siku hiyo ambapo wamewaomba wananchi kuwa na moyo wa kufanya usafi katika maeneo yanayowazunguka na kuto tupa takataka ovyo TTCL ina azimisha siku hiyo kwa kaulimbiu yao ya 'TTCL  huleta watu karibu'


Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu nchini TTCL wakijumuika kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu nchini TTCL wakijumuika kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu nchini TTCL wakijumuika kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo

BAADHI YA MAOFISA WA TTCL WAKIWA NA MAFAGIO KWA AJILI YA KUSAFISHA MAZINGIRA YA MAENEO YA HOSPITALI YA TAIFA


BAADHI YA MAOFISA WA TTCL WAKIWA NA MAFAGIO

Maelfu wajitokeza kumuaga Ngwair

Sehemu ya umati uliojitokeza kumuaga Ngwair viwanja vbya leaders
Diamond Platnumz akipita mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Albert Mangwea kutoa heshima zake za mwisho.


Rais wa Chama cha Wanamuziki Nchini.

Mwili wa marhemu Albert Mangwea ukiwa kwenye jeneza tayari kwa watu kutoa heshima za mwisho



Umati wa watu wakiwa wamepanga mstari tayari kwa kwenda kuaga huku kikosi cha msalaba mwekundu na polisi kikiwa stand by.
Baadhi ya wasanii wa bongo wakiwa kwenye mstari tayari kwa kuaga.








Umati wa waliojitokeza kumuaga Ngwair leo(Picha zote Mpekuzi Huru)



    




Simba, Golden Bush kupimana ubavu Jumamosi

Kikosi cha Golden Bush
Kikosi cha Kikijifua uwanja wa Kinesi
TIMU isiyofungika ya Golden Bush Fc ya jijini Dar es Salaam inayoshiriki Ligi Daraja la Nne Wialaya ya Kinondoni, wikiendi hii itashuka dimbani kupimana ubavu na Simba inayojiandaa na michuano ya Kombe la Kagame itakayofanyika nchini Sudan.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mlezi wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' pambano hilo la kirafiki ya kujipima nguvu litafanyika siku ya Jumamosi saa 10:30 jioni kwenye uwanja wa Kinesi.
Ticotico alisema mechi hiyo ni muhimu mno kwa vijana wake, lakini pia amemwagia sifa kocha wa Simba, King Abdallah Kibadeni kwa kukubali ombi la timu hizo kupepetana.

Taarifa rasmi ya Golden Bush iliyotumwa na Ticotico kwa blogu hii ni kama ifuatavyo hapo chini;

Naomba nitoe taarifa kwamba siku ya jumamosi weekend hii pale uwanja wa Kinesi timu yetu ya vijana Golden bush itaumana uso kwa uso na Simba sports club kuanzia saa kumi na nusu jioni. ni game ambayo Simba watatumia kama maandalizi yao ya mwishomwisho kwa ajili mashindano ya Kagame Cup huku Golden bush tukitumia game hiyo kungalia vijana wetu wameiva kiasi gani ajili ya mzunguko wa pili wa ligi daraja la nne Kinondoni. tunawaomba mashabiki, wapenzi, wadau, wakereketwa tufike Kinesi jumamosi jioni ili tushuhudie mpambano wa kutaka na shoka.

Aidha nichukue nafasi hii kumpongeza King Kibadeni kwa kukubali game yetu bila mizengwe, ikumbukwe kwamba King ndiye alifanikisha game yetu na Kagera sugar wakati ule akiwa kocha wao. juzi tena Uongozi umeomba game na bila ajizi King kasema kipigwe siku ya jumamosi.

Najua veterans watakuwa na game weekend hii na kama itakuwa jumamosi basi mkae mkao wa kula maana Golden bush tutao burudani asubuhi na jioni, kwa kiswahili unapiga nyuma na mbele.

naomba kutoa hoja.

Monday, June 3, 2013

Mwili wa Ngwair waagwa rasmi, kutua nchini kesho mchana


Baadhi ya Watanzania waishio Afrika Kusini wakiuaga mwili wa Ngwair (Picha kwa hisani ya deejaydeo.blogspot.com)


Kinjekitile 'Kinje' Ngombale Mwiru (mbele) akiwa na watanzania wengine kufanya harakati za mwili wa Ngwair kurejeshwa nchini.

BAADA ya danadana ya siku kadhaa juu ya ratiba kamili ya kuwasili kwa mwili wa msanii Albert Mangwea 'Ngwair' aliyefariki Jumanne iliyopita nchini Afrika Kusini, sasa imethibitika kuwa atatua nchini kesho mchana kabla ya mwili huo kuagwa na watanzania kwenye viwanjavya Leaders, Kinondoni.
Taarifa zilizopatikana jioni hii zinasema kuwa mwili wa msanii huyo umeagwa rasmi na watanzania waliopo nchini humo na kwamba kila kitu kimekamilika kwa ajili ya kesho kurafirishwa kuletwa Tanzania tayari kwa mazishi yatakayofanyika Alhamis katika makaburi ya eneo la Kihonda, Morogoro.
Awali kulikuwa na sintofahamu juu ya siku halisi ya mwili wa mkali huyo wa (free Style) kutokana na taarifa ya kwanza kuelezwa angetua nchini Jumamosi, kisha kuelezwa Jumapili kabla ya ratiba hiyo kuutwa asubuhi ya siku hiyo na kuelezwa ingekuwa leo au kesho.
Hata hivyo uhakika kabisa ni kwamba mwili wa nyota huyo wa albamu ya a.k.a Mimi na Ng'e utatua kesho kabla ya kuagwa jijini na kusafirishwa kwenda kuzikwa mjini Morogoro ambapo matayarisho mengine yamekamilika kwa kuhifadhi mwili wa mkali huyo aliyeenda Afrika Kusini kufanya maonyesho ya muziki na msanii mwezake M to the P, anayeendelea vyema kiafya nchini humo baadaya awali kuwa mahututi.

Azam yaanika silaha zake kwa msimu wa 2013-2014

Kocha Stewart John Hall akionyesha makeke yake kwenye mazoezi

Wakali wa klabu ya Azam ambapo baadhi wa hawatakuwa kwenye kikosi cha msimu ujao akiwemo Gaucho (24)
 
KLABU ya soka ya Azama imeweka bayana kwamba haitaacha mchezaji iliyo na mkataba naye na wala haitaongeza mchezaji mwingine katika kikosi ilichonacho sasa. 
Kwa mujibu wa taarifa yake, Azam imesema kama ilivyokuwa wakati wa dirisha kubwa la usajili 2012/13 ambapo Azam  ilimuongeza George Odhiambo 'Blackberry' pekee, safari hii imepandisha twachezaji wawili wa U20, Mudathir Yahaya na golikipa Hamadi Juma Yahya Kadedi na kufunga zoezi la usajili.
Taarifa hiyo inanukuu ripoti toka kwa Kocha mkuu wa Azam Stewart Hall, kuwa hakuna sababu ya klabu kwenda nje kusajili wachezaji ambao viwango vyao havipishani na waliopo klabuni.
Mchezaji Abdulhalim Humoud amepata timu nchini Afrika ya Kusini, Abdi Kassim 'Babi' mkataba wake umekwisha kama ilivyo kwa Deogratius Munishi Dida huku Uhuru Selemani akirejeshwa Simba SC baada ya kumaliza msimu wa mkopo na Azam FC.
Wachezaji wengine wote waliosalia wanabaki klabuni na kocha mkuu amependekeza baadhi ya makinda wa Under 20 walioonesha viwango vya juu wapandishwe timu kubwa, wapewe mikataba na kisha wapelekwe kwa mkopo ili wakapate nafasi ya kucheza. Wachezaji hao ni Omary Mtaki na Kevin Friday.
Azam ambayo imemaliza ligi ikishika nafasi ya pili kwa msimu wa pili mfululizo itaanza kambi ya kujiandaa na msimu mpya hapo June 24 kwa mujibu wa ratiba ya mwalimu na baada ya kumaliza kipindi cha pre season, kikosi cha Azam kitasafiri nje ya nchi kucheza mechi za majaribio kama ilivyo kawaida yake.

Wachezaji wanaounda kikosi cha Azam FC ni;

Magolikipa; Mwadili Ally, Aishi Salum na Hamad Juma Yahya

Mabeki; Himid Mao, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Samih Nuhu, Luckson Kakolaki, Aggrey Morris, Said Moradi, David Mwantika na Jockins Atudo

Viungo; Kipre Bolou, Salum Abubakar, Jabir Aziz, Ibrahim Mwaipopo, Humphrey Mieno na Mudathir Yahya

Washambuliaji; John Bocco, Gaudence Mwaikimba, Khamis Mcha, Kipre Tchetche, Brian Umony na Abdallah Seif Karihe

Sh Mil 32 zachangwa msiba wa Ngwair, mwili kutua kesho

Ngwair enzi za uhai wake


KAMATI ya Mazishi ya aliyekuwa Msanii wa Bongo Fleva, Albert Mangwea ‘Ngwea’, mpaka jana mchana ilikuwa imekusanya jumla ya Sh milioni 32 kutoka kwa wadau mbalimbali.

Kamati hiyo inahitaji Sh milioni 50 kwa ajili ya kusaidia kusafirisha mwili wa marehemu kutoka Afrika Kusini mpaka Morogoro kwa ajili ya mazishi. Fedha hizo pia zinahitajika kwa ajili ya kuratibu shughuli nzima ya mazishi.

Mangwea alifariki dunia Jumanne iliyopita nchini Afrika Kusini akiwa usingizini kwa madai ya kuzidisha matumizi ya madawa ya kulevya. 

Alitarajiwa kuwasili nchini jana lakini kushindwa kutoka kwa ripoti ya uchunguzi wa madaktari kwa wakati, kumesababisha isijulikane atatua lini, licha ya kudaiwa kuwa anaweza kutua leo.

Kamati ya Mazishi bado inaendelea na mchakato wa kuratibu shughuli hiyo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mwandishi wetu akiwa Mbezi Goig jijini Dar ambako ndiko kwenye msiba huo, mmoja wa waweka hazina wa kamati hiyo, Paul Matthysse ‘P-Funk’, alisema mpaka sasa kamati yake imefikisha Sh 32,259,000 ingawa wanatarajia kuendelea kupokea michango mbalimbali kutoka kwa wadau.

Miongoni mwa watu wa kwanza kutoa michango yao katika msiba huo ni P-Funk aliyetoa Sh milioni tano, Clouds Media Group (Sh milioni tano) na Push Mobile (Sh milioni tano). 

Juzi Kampuni ya Global Publishers ilitoa Sh milioni moja.
“Nawasisitiza Watanzania waendelee kutoa michango yao kwa ndugu yao ili kuonyesha umoja tulionao. Fedha zikiwa nyingi tunataka kumfanyia kitu mama yake ili kuendelea kumfariji kwani kipindi hiki ni kigumu kwake,” alisema P-Funk.
 

Wakati huohuo jana  taarifa zilisema mama mzazi wa Mangwea aishie Morogoro, Denisia Mangwea, alipandwa na presha baada ya jana kupata taarifa kuwa mwili wa mwanaye umezuiwa Afrika Kusini kutokana na uchunguzi wa madawa ya kulevya. Alikimbizwa hospitali na inadaiwa anaendelea vizuri.

Mangwea aliwahi kutamba na nyimbo kadhaa kali zikiwemo Gheto Langu, She Got a Gwan, Mikasi na Tupo Juu.

Chelsea yathibitisha Mourinho kutua darajani


Back in town: Jose Mourinho holds his Chelsea shirt after being confirmed as the new Chelsea manager
Kocha Jose Mourinho akiwa na uzi wa Chelsea baada ya kutambulishwa jioni hii

KLABU ya Chelsea imethibitisha  kumjeresha kikosi aliyekuwa kocha wao, Jose Mourinho kwa mkataba wa miaka minne akitokea klabu ya Real Madrid ya Hispania.
Kwa mujibu taarifa zilizotolewa na klabu hiyo jioni hii inasema kuwa wamemalizana na kocha huyo kutoka Ureno na kwamba Mourinho ataanza kazi wiki hii.
Klabu hiyo imemtambulisha rasmi kocha huyo na kukabidhiwa jezi ya klabu hiyo kuthibitisha kuwa sasa ni rasmi karejea nyumbani baada ya kuondoka kwa kuipa mafanikio makubwa ikiwamo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England mara mbili na lile la Carling Cup mara mbili na Kombe la FA alipotua hapo kwa mara ya kwanza mwaka 2004 hadi 2007 alipoondoka kwenda Inter Milan kabla ya kuchukuliwa Real Madrid.
Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Mourinho kuinoa Chelsea ambao wanashikilia taji la Ligi ndogo ya Ulaya baada ya kuinyoa Benfica katika pambano la Fainali lililofanyika Mei 15 mwaka huu, ikiwa ni miezi kadhaa tangu walipolitema taji la Ligi ya Ulaya walilotwaa mwaka jana kwa kuilaza Bayern Munich.

SITA WAPOTEZA MAISHA KTK AJALI MBEYA KADHAA WAJERUHIWA

 HIVI NDIVYO DALADALA HII ILIVYO HARIBIKA BAADA YA AJALI HIYO KUTOKEA 
 
 GARI LA ABIRIA AINA YA HIACE IKIWA IMEGONGANA USO KWA USO NA GARI AINA YA LAND CRUISER
HIZI NI BAADHI YA MAITI ZILIZO OKOLEWA PUNDE BAADA YA AJALI KUTOKEA  
MWILI WA DEREVA WA DALADALA ALIYE FARIKI PAPO HAPO UKIPELEKWA CHUMBA CHA KUHIFADHIA MAITI RUFAA
******************************

Watu sita wamefariki Dunia na wengine Sita kujeruhiwa katika ajali ya Barabarani iliyo tokea Nanenane Darajani eneo la Uyole Mbeya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mbeya Barakael Masaki amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuwataja marehemu hao kuwa ni pamoja na madereva wote wa magari hayo. 

Masaki amesema dereva wa Hiace amefahamika kwa jina la Meshack Hosea aliye kuwa anaendesha Gari nambali T178 AAV aina ya Toyota Hiace inayofanya kazi Sokomatola na Uyole ambapo muda huo ilikuwa ikitokea Sokomatola kuelekea uyole. Dereva wa pili aliyekuwa anaendesha Gari aina ya Toyota Land Cruiser iliyokuwa inatokea Uyole kwenda mjini yenye namba za usajili T 181 BHT iliyokuwa inaendeshwa na Dereva Abdalah Ndabagi .

Maiti nne hazijatambuliwa hadi sasa wakiwemo wanawake wanne waliokuwa abiria katika Daladala hiyo na miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa jijini Mbeya.

Aidha amesema majeruhi sita wamelazwa katika hospitali ya Rufaa wakiwemo wanawake watano na Mwanamke mmoja . Ambao mpaka sasa majina yao hayatambuliwa kutokana na kujeruhiwaa vibaya.

Chanzo cha ajali hiyo kimetajwa kuwa ni  mwendo kasi wa Magari hayo na wito ameutoa kwa Madereva kuwa makini na kufuata sheria za Barabarani ili kuepusha ajali ambazo zingeweza kutokea. Ikizingatiwa hilo ni eneo la Jiji.

Picha na Mbeya yetu Blog

JB, Irene Uwoya waja na Zawadi

Jacob Stephen 'JB'

MUIGIZAJI na mtayarishji hodari wa filamu nchini, Jacob Stephen 'JB' anatarajiwa kuibuka na filamu mpya iitwayo 'Zawadi Yangu'.

Filamu hiyo ambayo imekamilika hivi karibuni ikiwa kwenye foleni kabla ya kuachiwa mtaani ameicheza msanii huyo akiwashirikisha wakali wengine akiwamo mwanadada Irene Uwoya 'Mama Krish', Chuma Suleiman 'Bi Hindu' na Shamsa Ford.

JB anayefahamika pia kwa jina la 'Bonge la Bwana' alisema filamu hiyo ya kijamii inayoonyesha jinsi kinamama wanavyoweza kutawala sehemu kubwa ya ndoa za watoto zao na kudai ni moja ya kazi murua kutoka Jerusalem Films Production kwa namna simulizi lake lilivyo.

"Sijisifu, ila filamu hii mpya ya 'Zawadi Yangu' ni kati ya filamu ambazo nimeiandaa kwa umakini mkubwa na yenye ujumbe maridhawa kwa jamii," alisema JB.

Alisema filamu hiyo itatoka mapema mwezi huu akiwa tayari ameshaanza maandalizi ya 'kupika' kazi nyingine ambayo hata hivyo hakupenda kutaja jina kwa sasa akidai ni mapema mno.

JB aliyewahi kutamba na maigizo kupitia kituo cha ITV akiwa na makundi ya Mambo Hayo na Nyota Ensemble alisema kama ilivyo kwa 'Zawadi Yangu' hata kazi ijayo itakuwa kali na ikishirikisha nyota nchini.

Msondo Ngoma yajiandaa kuingioa studio kupakua albamu

 
Baadhi ya wanamuziki wa Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki'
BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Msondo Ngoma inatarajiwa kuingia studio wiki chache zijazo kurekodi albamu ya kwanza tangu mwaka 2010.

Kwa muda mrefu mashabiki wa Msondo wamekuwa wakiililia albamu mpya tangu ilipotolewa 'Huna Shukrani' miaka mitatu iliyopita na kilio chao kimesikika kwa uongozi wa bendi kwa kuiingiza Msondo studio.

Mmoja wa watunzi wa bendi hiyo, Juma Katundu aliiambia MICHARAZO kuwa wataingia  studio Juni 12.

Katundu ambaye katika albamu hiyo ana wimbo uitwao 'Nadhiri ya Mapenzi', alisema kila kitu kimekaa vyema kwa ajili ya kuanza kazi hiyo ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa hamu ya Wanamsondo kwa ujumla kuanzia wanamuziki hadi mashabiki wao.

"Tunatarajiwa kuingia studio Juni 12 kuanza kurekodi nyimbo za albamu yetu ambayo itakuwa na nyimbo sita, mmojawapo ikiwa ni utunzi wangu," alisema.

Alizitaja nyimbo nyingine zitakazorekidiwa kuwa ni 'Baba Kibene' na 'Lipi Jema' za Eddo Sanga, 'Kwa Mjomba Hakuna Mirathi' wa Huruka Uvuruge, 'Dawa ya Deni' na 'Suluhu' wa Shaaban Dede.

Msondo ilitoa albamu ya mwisho mwaka 2010 ambayo ni 'Huna Shukrani' baada ya kuzindua kwa kishindo mwaka mmoja uliotangulia albamu ya 'Kicheko kwa Jirani' iliyokuwa albamu ya kwanza tangu bendi hiyo iondokewe na nyota wake mkubwa, Tx Moshi William.

Vipimo halisi vya kifo cha Ngwair vyatoka



https://fbcdn-sphotos-e-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash3/p480x480/579293_526768957387103_1440212486_n.jpg
Albert Mangwea 'Ngwair' enzi za uhai wake

RIPOTI ya vipimo halisi vya kifo cha msanii wa Bongofleva, Albert Mangweha a.k.a Ngwair, imetolewa baada ya mwili wake kufanyiwa uchunguzi na madaktari wa hospitali ya St. Hellen Joseph mjini Johannesburg, Afrika Kusini.

Akizungumza na NIPASHE jana saa 9:50 jioni maeneo ya Mbezi Goig jijini Dar es Salaam ambako msiba wa msanii huyo upo, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Radhia Msuya, ambaye alitembelea familia ya marehemu, alisema kuwa tayari madaktari wameshabaini chanzo cha kifo cha Ngwair na kwamba vipimo vitakabidhiwa kwa familia ya marehemu.

Msuya alisema kuwa ndugu wa marehemu ndiyo wenye mamlaka ya kuviweka wazi ama kutoiambia jamii kilichomo kwenye ripoti hiyo ya madaktari.

"Serikali imeshtushwa na kifo cha msanii huyu kwa sababu ni kijana. Tumepoteza mtu muhimu kwa sababu alikuwa balozi mzuri wa Tanzania anapokuwa nje ya nchi," alisema Msuya.

Alisema kuwa mwili wa marehemu umechelewa kuwasili nchini kwa sababu ya taratibu za vifo na mazishi nchini Afrika Kusini ambazo zinatofautina kwa kiasi kikubwa na taratibu za Tanzania.

"Mwili wa marehemu ungesafirishwa mapema lakini kilichochelewesha ni 'death certificate' (cheti cha kifo). Afrika Kusini mazishi hufanyika kwa siku za Jumamosi na Jumapili tu na sheria zao za vifo ni tofauti kabisa na za kwetu," alisema.

"Kinachoendelea kwa sasa ni 'booking' ya ndege. Kufikia kesho asubuhi zoezi hilo litakuwa limekamilika na mwili utawasili nchini kesho (leo) ama keshokutwa (kesho)," aliongeza balozi huyo.

Msuya alisema kuwa endapo mwili wa marehemu utasafirishwa kwa ndege ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini, utafika jijini Dar es Salaam leo saa moja jioni, lakini utafika kesho saa mbili asubuhi kama ukisafirishwa kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya.

Aidha, balozi huyo aliwapa pole ndugu, jamaa, marafiki na wasanii waliokuwa kwenye msiba wa marehemu kisha akazungumza na kamati ya mazishi inayoongozwa na Adam Juma.

Ngwair, aliyepata umaarufu mkubwa nchini kupitia tungo zake kali zikiwamo za 'Ghetto Langu' na 'Mikasi' alifariki Jumanne iliyopita nchini Afrika Kusini ambako alienda kwa ajili ya maonyesho ya muziki.

Mitandao ya kijamii na magazeti mbalimbali nchini (siyo NIPASHE) vilikurupuka kuchapisha ripoti 'feki' iliyozagaa kwenye internet ikidaiwa kuwa ndiyo chanzo cha kifo cha msanii huyo nyota ilhali hata vipimo vilikuwa havijafanyika.

Hadi kufikia jana hali ya msanii mwenzake Ngwair, M 2 The P ambaye naye amelazwa baada ya kuzidiwa pamoja na rapa huyo, ilikuwa ikiendelea vyema nchini Afrika Kusini.

Chanzo:NIPASHE

Sunday, June 2, 2013

Makocha Ilala wainyuka Kinyerezi Veterani


TIMU ya makocha wa soka wilayani Ilala, Ilala Coaches Fc, imeinyuka Kinyerezi Veterani kwa bao 1-0 katika mfululizo wa mechi zao za kila mwezi, mchezo uliochezwa uwanja wa Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa, Ilala Dar es Salaam.
Bao pekee la makocha hao, lilitumbukizwa kimiani na Hashim Gadiola na kuendeleza ubabe wa kikosi chao kinachojumuisha makocha mbalimbali wa Ilala.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chama cha Makocha Ilala, TAFCA-Ilala, Hugho Sseseme Makocha Ilala walionyesha uwezo wa hali ya juu licha ya wapinzani wao kuonyesha upinzani na kusababisha ushindi katika mechi hiyo ya leo kuwa kiduchu.

Taifa Stars, Sudan zashindwa kutambiana Ethiopia


TIMU ya soka ya taifa, Taifa Stars jioni hii imetoshana nguvu na Sudan katika pambano la kimataifa la kirafiki lililochezwa mjini Addis Ababa, nchini Ethiopia ilipoweka kambi yake ya kujiandaa na michuano ya kufuzu Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika nchini Brazili.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Boniface Wambura Stars ilionyesha uwezo mkubwa licha ya kuchezesha vijana katika pambano hilo kwa nia ya kuwapa uzoefu zaidi katika kikosi hicho ambacho kwa sasa wapo kwenye hafla nyumbani kwa Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Kikosi hicho kitaondoka kesho nchini Ethiopia kwa ajili ya kuanza safari ya kwenda Morocco kwa kupitia Misri ili kukwaruzana na wenyeji wao katika pambano la marudiano la kundi C kwa nia ya kuwania kucheza fainali hizo za Brazili.
Katika mechi ya kwanza  Stars iliinyuka Morocco mabao 3-1 na ushindi huo iliifanya Stars kuendelea kusalia nafasi ya pili ikijikusanyia pointi 6, moja nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba ambayo nayo wikiendi ijayo itakuwa dimbani klupambana na Gambia.

Abajalo yang'oka RCL, yalala 1-0 Ilulu

TIMU ya soka ya Abajalo imeng'olewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) baada ya kulazwa bao 1-0 na Kariakoo Lindi katrika mechi ya marudiano lililochezwa uwanja wa Ilulu.
Katika pambano lililochezwa wiki iliyopita timu hizo zilishindwa kutambiana baada ya kufungana mabao 2-2 na hivyo,  Abajalo iomeng'olewa kwenye hatua hiyo ya pili kwa jumla ya mabao 3-2.

Borussia Dortmund yamtolea macho Podolski

http://img.thesun.co.uk/multimedia/archive/01595/PODOLSKI_1595719a.jpg
Lucas Podolski



KLABU ya Arsenal inakabiliwa na changamoto kubwa ya kumbakisha mshambuliaji wake nyota Lucas Podolski, baada ya mchezaji huyo aliyesaidia timu yake kupata ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Ecuador kunyemelewa na wana fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya, Borussia Dortmund.
Podolski, aliyewahi kuripotiwa na gazeti la The Sun mwezi Aprili kuhitajiwa na Atletico Madrid, alitua Emirates mwaka jana kwa kitita cha Pauni Mil. 11, lakini kwa sasa atupiwa macho na Dortmund iwap[o Arsenal inaridhia kumuachia.
Klabu hiyo ya Ujerumani imepata jeuri ya kumtaka Podolski aliyesajiliwa na Arsenal akitokea timu nyingine ya Bundesliga ya Cologne kutokana na kuvuna mamilioni ya fedha kwa kumuuza Mario Gotze kwa kitita cha Pauni Mil. 31.5 na nyota wake mwingine Robert Lewandowski akiwa njiani kumfuata mwenzake kwa mabingwa hao walioweka rekodi msimu huu kutwaa taji la Ligi ya Ulaya, Bundesliga na Kombe la Ujerumani.
Hata hivyo Dortmund itabidi ifanye kazi ya ziada kumshawishi Arsene Wenger kumtoa mchezaji huyo wakati akiwa ameaminiwa na mabosi wake kuendelea kukisuka upya kikosi hicho ili angalau kufuta 'ukame' wa mataji katika klabu hiyo uliodumu kwa miaka kadhaa sasa.
Mshambuliaji huyo mwenye asili ya Poland na aliyeichezea timu ya taifa ya Ujerumani mara 109 na kuifungia mabao 46, tangu alipotua Arsena; ameichezea mechi 33 za Ligi na kuifungia mabao 11 na amekuwa akinukuliwa akifurahia maisha Emirates.

Stars kujipima nguvu na Sudan kabla ya kesho kwenda Morocco


KIKOSI cha timu ya taifa, Taifa Stars kilichopo kambini mjini Addis Ababa, Ethiopia kujiandaa na mechi ya kuwania tiketi ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco Juni 8, leo itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan.
Stars chini ya Kocha wake, Kim Poulsen, iliyopiga kambi katika Hoteli ya Hilton kujiandaa na mechi hiyo, ipo nafasi ya pili kwenye kundi la C; nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura aliyehojiwa na kituo kimoja cha redio nchini alisema kuwa pambano hilo litatumiwa na kocha Poulsen kukiangalia kikosi chake kabla ya kesho kuondoka kueleka Morocco.
Wambura alisema mara baada ya mechi hiyo wachezaji na viongozi wa Stars watakwenda Ubalozi wa Tanzania nchini humo walikoalikwa na Balozi Joram Biswaro, ambapo watapata fursa ya kukutana na baadhi ya Watanzania wengine waishio nchini huo kwa ajili ya kuwaaga.
Kikosi cha nyota 22 kitaondoka Ethiopia alfajiri ya kesho kwenda Marrakech, Morocco kupitia Cairo, Misri ambao ni Juma Kaseja, Aggrey Morris, Mwadini Ally, Ally Mustafa, Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Erasto Nyoni, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vincent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd, Haruni Chanongo na Zahoro Pazi.


Ruvu Shooting waanza kuimarisha kikosi chake

Kikosi cha Ruvu Shooting Stars

KLABU ya soka ya Ruvu Shooting ya Pwani imemsajili mchezaji Cosmas Ader Lewis kwa mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia klabu hiyo katika Ligi Kuu Tanzania Bara.
Cosmas aliyeichezea kwa mkopo African Lyon msimu uliopita akitokea Azam, alisaini mkataba huo mwishoni mwa wiki kwenye ofisi za klabu hiyo ya jeshi zilizopo Kikosi cha Jeshi 832 Ruvu JKT Mlandizi, Kibaha-Pwani.
Mchezaji huyo alikuwa na mkataba wa mwaka mmoja na klabu ya Azam ambao umeisha na kuifanya Ruvu kufanikiwa kumnyakua na kuzizidi kete timu nyingine zilizokuwa zikimnyemelea ikiwamo Simba.
Msemaji wa timu hiyo Masau Bwire aliiambia MICHARAZO kuwa usajili wa mchezaji huyo ambaye ni mshambuliaji kinda aliyezaliwa Novemba 1995, una lengo la kuifanya Ruvu Shooting ifanye vyema kwa msimu ujao baada ya msimu uliosha hivi karibuni kushindwa kutimiza malengo yao ya kumaliza kwenye 5 Bora.
Bwire alisema kunyakuliwa kwa mchezaji huyoa ni mwanzo wa timu yao kujiimarisha kwa msimu ujao ambao huenda ukaanzxa kati ya Agosti na Septemba mwaka huu.
"Tunaamini kutua kwa Lewis Ruvu Shooting kutakuwa na tija na ufanisi mkubwa kwa msimu ujao kwani ni mmoja wa wachezaji mahiri na ndiyo maana tumeamua kumnyakua, "alisema Bwire.
Bwire alisema usajili wao kwa kikosi cha msimu ujao ufanywa kwa umakini mkubwa ili kuondoa dhana kwamba timu za majeshi ni wasindikizaji tu katika Ligi Kuu Tanzania Bara, ambayo kwa sasa bingwa wake ni Yanga ambao walinyakua nafasi ya kwanza na kufuatiwa na Azam kisha Simba.

Simba, Yanga kutoshiriki Kagame, kisa....!

 
Simba

Mabingwa watetezi wa Kagame, Yanga
VIONGOZI wa klabu ya soka ya Simba na Yanga wanatarajiwa kukutana haraka iwezekanavyo kwa nia ya kutoa msimamo wao juu ya kwenda Sudan kushiriki michuano ya Kombe la Kagame ambayo inatarajiwa kuanza katikati ya mwezi huu.
Michuano hiyo ilitangazwa na Baraza la Vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati - CECAFA kuwa ingefanyika mjini Darfur -Sudan, lakini serikali ya Tanzania imetoa tamko kuhusu timu za Simba na Yanga kwenda kushiriki michuano hiyo huko Sudan kwenye eneo ambalo limekuwa likiandamwa na vurugu kwa miaka kadhaa sasa.
 Kwa mujibu wa msemaji wa klabu ya Simba Ezekiel Kamwaga ni kwamba serikali haidhani ni busara kwa vilabu vya Simba na Yanga kwenda kwenye eneo hilo kushiriki Kagame Cup kutokana hali mbaya ya usalama iliyopo Darfur.
Kamwaga aliadnika hivi katika ukurusa wake wa Facebook;
Breaking News...... Serikali imesema haioni busara ya Kagame Cup kupigwa Darfur.... Hakuna hoteli ya maana na watu wanashauriwa kutembea na fulana zinazozuia risasi kupenya... Nadhani hii ndiyo stori kubwa ya kimichezo kwa leo.... Je, mnadhani itakuwa busara kwa Simba na Yanga kushiriki?
Hata hivyo taarifa zilizopatikana mchana huu ni kwamba viongozi wa Simba na Yanga kwa nafasi zao wanatarajiwa kukutana kujadili tamko hilo na kutoa msimamo wao kama wataenda Sudan au la, kwa hofu ya machafuko yanayoendelea huko.
Kagame ili[elekwa huko kwa nia ya kuhamasisha amani katika mji huo, lakini hali haionyeshi matumaini na wadau wengi wanadhani si busara timu za Tanzania kwenda kwa kuhofia kutokea maafa ywa wachezaji wa timu hizo. TUSUBIRI Tuone

Dorice Mollel ndiye Miss Tabata 2013

Miss Tabata Dorice akipozi na Mshindi wa pili Upendo Lema (kulia) na mshindi wa tatu Recho Mushi (kushoto).
MWANAFUNZI wa mwaka wa pili katika chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Dorice Mollel (22) usiku wa kuamkia jana alishinda taji la Miss Tabata kwenye shindano lililofanyika katika ukumbi wa Dar West Park, Tabata.
Dorice aliwabwaga  warembo wengine 14 kumrithi Noela Michael aliyekuwa anashikilia taji hilo. Noela ndiye anayeshikilia taji la Miss Ilala kwa sasa.
Mshindi huyo alizawadiwa Sh 600,000 na king’amuzi kutoka Multichoice pamoja na warembo waliyoshika tano za juu watawakilisha Tabata katika shindano la Miss Ilala baadaye mwaka huu.
Warembo hao ni Upendo Lema (22) aliyezawadiwa sh 400,000 baada ya kushika nafasi ya pili na Recho Mushi (20) alipata Sh 300,000 baada ya kushika nafasi ya tatu.  Wengine ni Kazunde Kitereja (19) alishinda nafasi ya nne na kuzawadiwa Sh 200,000 na Kabula Juma Kibogoti (20) alipataSh 150, 000 kwa kushika nafasi ya tano.
Warembo wengine waliyoingia kumi bora kila moja alipata shilingi laki moja. Nao ni Madgalena Bhoke (21), Eunice Nkoha (19), Rehema Kihinja (20), Brath Chambia (23) na Joaniter Kabunga (21). Warembo waliyosalia walipata kifuta The rest got consolation prize of Sh 50,000 each.
Miss Tabata iliandaliwa na Bob Entertainments na Keen Arts chini ya udhamini wa Dodoma Wine, Redd’s Original, Nipashe, Vayle Springs, Multichoice, Fredito Entertainment, Integrated Communications Limited, CXC Africa, Brake Point na Saluti5.

Mwili wa Ngwair wakwama tena, sasa kutua Jumanne

https://fbcdn-sphotos-e-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash3/p480x480/579293_526768957387103_1440212486_n.jpg
Ngwair

MWILI wa aliyekuwa nyota wa muziki wa Hip hop nchini, Albert Mangwea 'Ngwair' uliokuwa uwasili nchini huu umeshindikana na sasa utawasili nchini Jumanne ukitokea Afrika Kusini ambapo ndipo msanii huyo alipopatwa na mauti.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Mazishi ya msiba wa msanii huyo, umewaomba radhi Watanzania ambao wamekuwa na shauku ya kuupokea mwili wa kipenzi chao huyo, aliyekuwa ametangazwa awali angetua jana mchana kabla ya kubadilishwa na kuelezwa ungetua leo saa 8 mchana.
Taarifa rasmi ya kamati hiyo inasomeka hapo chini, ingawa taarifa zaidi kutoka Afrika Kusini zinasema kuwa mwili wa Ngwair utawasili nchini Jumanne mchana na kuagwa siku inayofuata kabla ya kwenda kuzikwa Morogoro Alhamisi.
Kwa mujibu wa ujumbe wa mtangazaji wa Clouds Millard Ayo aliyepo Johannesburg, Afrika Kusini aliotwitte kwenye akaunti yake ni kwamba mwili wa Ngwair utawasilia Jumanne mchana.

                  TAARIFA YA KAMATI NDIYO HII HAPA:
Kamati ya msiba tunaomba kutoa ya taarifa kwamba mwili wa Ndugu yetu Albert Mangwea hautoweza kufika siku ya jumapili ya tarehe 2/06/2013 kama ilivyo taarifa hapo awali, hii ni kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu.Kwa sasa tunasubiri taarifa kamili kutoka kwa wenzetu/wawakilishi wetu waliopo nchini Afrika Kusini, mara tutakapopata taarifa hizo tutawafahamisha zaidi.Tunaomba radhi watanzania wote kwa usumbufu wote uliojitokeza tushirikiane na uvumilivu kwa hili.
Asante
Mwenyekiti wa Kamati
Kenneth Mangweha
…………………………………
Msemaji wa Kamati
Adam Juma
……………………….

Mwanamke aishi kama mkimbizi baada ya kunusurika kuchinjwa


Mary Mbosa aliyenusurukia kuchinjwa na mtalaka wake na kulzaimika kuishi porini kama mkimbizi.

Na Gustav Chahe, Iringa



MAMA mmoja mkazi wa Itunundu – Pawaga katika Mkoa wa Iringa Mery Mbosa anaishi kama digidigi baada ya kunusurika mara kadhaa kuchinjwa na mtalaka wake na kulazimika kuhama kijiji kwa ajili ya kunusuru maisha.



Akiongea na mtandao huu jana, Bi Mbosa alisema maisha yake yapo hatarini kutokana na kuvamiwa na mtalaka wake mara kadhaa akiwa nyumbani na kumuumiza.



Alisema alilazimika kutalakiana baada ya mwanamume huyo kuwa mkorofi kiasi cha kupigwa, kutokuwa huru kutumia mazao ambayo walilima wote na hata kutokuwa huru kuongea na watu hata kama ni ndugu zake kwa madai kuwa ni wivu wa kimapenzi.



Alisema mtalaka wake amegeuka kuwa mnyama na kufika nyumbani kwake usiku wa manane na pindi anapokuta mlango umefungwa huanza kurusha mawe madirishani huku akitaka kuvunja mlango ili kuingia kumdhuru.



Amemtaja mtalaka wake kuwa ni Phabiani Msilamgunda ambaye miezi ya hivi karibuni alikutana na ye njiani akielekea shambani akamvamia akiwa na kisu kwa kutaka kumchinja na kuokolewa na watu ambao walikuwa jirani.



“Ilikuwa 23 Machi mwaka huu nilikuwa nikielekea shambani nikakutana na mtalaka wangu akiwa na kisu mkononi akanivamia huku akisema nakuchinja laeo lakini kwa bahati nzuri kulikuwa na watu jirani wakaniokoa vinginevyo ningekuwa marehemu.



“Lakini hata hivyo amekuwa akimtukana hata mama yangu mzazi (mama mkwe) akitaka kupiga pia na kila wakati nimekuwa nikishtaki hadi ofisi zinanichoka pamoja na kuwa ninapokelewa na akiitwa haendi kwa sababu amekuwa mbabe” alisema bi Mbosa.



Hata hivyo Mbosa alisema kuwa aliwahi kupigwa na kuumizwa vibaya na kulazimika kushtaki mahakamani japo kuwa hukumu ilivyotolewa haikuwa ya haki na kuhatarisha zaidi maisha yake.



“Nilipigwa na kuumizwa vibaya kesi ikapelekwa mahakamani lakini hukumu ilivyotolewa haikuwa ya haki kwangu na baada ya hukumu maisha yangu yamekuwa ni ya hatari zaidi” alisema.



Kwa mujibu wa maelezo ya wananchi wa kijiji hicho ambao wameeleza kushuhudia mama huyo akinusurika kuuawa na jinsi maisha yake yanavyozidi kuwa mabaya, walisema kiburi cha Msilamgunda kinatokana na dada yake ambaye ni diwani wa viti maalum (CCM).



Gazeti hili limebaini kesi ambayo mama huyo hajaridhika na hukumu ni Jinai No. 22/2013, mshitakiwa Phabiani Msilamgunda ambayo ilitolewa hukumu Mei 21 Mwaka huu.



Imeelezwa kuwa katika utoaji huku hiyo hakimu aliyetajwa kwa jina moja la Masuwe alimtaka mtuhumiwa alipoe faini ya shilingi laki mbili pamoja na gharama ya kesi shilingi 45 elfu jambo ambalo lilifanyika hivyo na mtuhuhumiwa kuwa huru kwa vitisho kuwa lazima ammalize mwanamke huyo.



Pamoja na kutokuridhika na hukumu iliyotolewa, Mkuu wa kituo cha Polisi cha Pawaga Fedrick Nyavilwe anatuhumiwa kumdhurumu mama huyo na kuiomba serikali kumsaidia ili aishi kama wanavyoishi wananchi wengine.



Nyavilwe anatuhumiwa kumdhurumu mwanamke huyo mbegu ya mpunga na kumfanya kuwa mtumwa kwa kukosa chakula bila kujua hatima ya maisha yake.



“Baada ya hukumu nilikwenda shambani nilikokuwa ninaanda mbegu ya mpunga kwa ajili ya kupanda nikakuta watu wananing’oa, nilipouliza walisema wametumwa na Mkuu wa kituo cha polisi. Hivi sasa naishi kama ndege jamani sijui nitakula nini kwa sababu hata mashamba niliyokuwa nalima nilinyang’anywa na mbegu niliyokuwa nimeandaa kwa ajili ya kupanda polisi wameninyang’anya” alisema.



Alipotafutwa kwa njia ya simu kwa ajili ya kutolea maelezo, Veronica Msilamgunda ambaye ni ndugu na Phabian Msilamgunda alisema hawezi kuzungumza chochote kwa kuwa yupo kwenye mkutano.



Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho Joseph Malinga alipotafutwa kwa ajili ya ufafanuzi Alikiri kuwa mama huyo ni mhanga mkubwa na anaishi kama mkimbizi kwa hofu ya kuuawa.



“Nalijua sana hilo na ninashukuru kwa kuwa umenitafuta ili nikueleze. Maisha ya huyo mama hatuji yataishia wapi kwa sababu hali ilivyo kwa sasa ni ngumu na anaishi kama mkimbizi.




“Hata akiwa sehemu yenye ulinzi anaona kama hakuna ulinzi kwa sababu ya kile anchofanyiwa. Kiujumla hata sisi viongozi wa kijiji tunaishi kwa mashaka kwa sababu tunatishiwa kuuawa tunapotaka kutafutas suluhu ya huyo mama. Huyu mwanaume tunashindwea kuelewa kama ni mtu wa kawaida maana amegeuka kuwa kamas samba” alismea Malinga.



Hata hivyo alisema anaomba kwa watu wanaoweza kumsaidia mama huyo kupata hifadhi ili aondokane na maisha ya kuishi kama digidigi kule kijijini.

Saturday, June 1, 2013

BASATA NALO LAMLILIA NGWAIR


Ngwair enzi za uhai wake
BARAZA la Sanaa la Taifa limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba wa msanii wa tasnia ya Muziki nchini Albert Mangwea a.k.a Ngwair.
“ Baraza limestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa ya kifo hiki cha Ngwair ambaye mchango wake unahitajika sana katika tasnia ya sanaa, pengo aliloliacha ni kubwa kwani ubunifu wao bado unahitajika katika tasnia hii.” Baraza linatoa pole kwa familia ya marehemu na wasanii wote nchini, aidha linawatakia moyo wa subira katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na mpendwa wetu.
Tunaomba mwenyezi Mungu aipumzishe mahala pema peponi roho ya marehemu. Baraza liko pamoja na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, tutambue kuwa haya ni mapenzi ya Mungu.
Imetolewa na
Ghonche materego
Katibu Mtendaji
Baraza la Sanaa la taifa.