STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 13, 2014

Ghana waanza vyema CHAN wainyuka Congo kimoja

CHAN 2014 : Group C Ghana and Congo collide
GHANA imeanza vyema michuano ya CHAN inayofanyika nchini Afrika Kusini baada ya jioni hii kuilaza Jamhuri ya Kongo kwa bao 1-0 katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Free State.
Bao pekee lililoihakikishia 'vigogo' hao kukusanya pointi tatu muhimu, lilitupiwa kambani na Theophilus Anobaah katika dakika ya 34 ya pambano hilo.
Muda mfupi ujao kundi hilo la C litashuhudia pambano jingine kali kati ya DR Congoi itakayoumana na Ethiopia kwenye uwanja huo huo katika mfululizo wa michuano hiyo.

Simba yashindwa kutamba kwa Waganda taji hilooo!


FUPA lililowashinda watetezi wa Kombe la Mapinduzi, Azam jioni ya leo umewashinda pia Simba, baada ya 'Mnyama' kuchezea kichapo cha bao 1-0 toka kwa vijana wa KCC ya Uganda ambao wamenyakua taji hilo na kuondoka nalo ikiwa ni kwa mara ya kwanza kwa timu ya nje ya Tanzania kutwaa kombe hilo.
Simba ambayo ilikuwa ikipewa nafasi kubwa ya kuficha aibu ya Tanzania kushuhusia timu zake zote zikikongotwa na wageni, ilishindwa kuhimili vishindo vya Waganda licha ya kucheza jihad hasa dakika za lala salama.
Bao pekee lililowanyong'onyesha Simba na watanzania kwa ujumla lilitumbukiwa na Herman Wasswa katika kipindi cha kwanza.
Kwa ushindi huo KCC imekuwa klabu ya kwanza nje ya Tanzania kunyakua taji hilo tangu lilipoanzishwa mwaka 2006, ikiwa haijapoteza mchezo wowote tangu kuanza kwa michuano hiyo Januari Mosi.
Timu hizo zote zilikuwa kundi B mpaka kufika fainali zilikuwa hazijapoteza mechi zao na katika mechi baina yao zilishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu.
Michuano hiyo ilishirikisha timu 12 nne kutoka nje na nyingine za Tanzania Bara na Zanzibar. klabu za nje ni URA na KCC za Uganda, Tusker na AFC Leopards za Kenya.
Kutwaa kwa taji hilo KCC imefuata nyayo za dada zao wa netiboli waliotwaa ubingwa wa mchezo huo kwa kuifunga Tanzania katika fainali siku mbili zilizopita.
Simba iliifunga URA ya Uganda katika mechi ya nusu fainali na KCC ikailamba Azam kwa mabao 3-2 na kuitemesha taji ililotwaa mwaka jana kwa kuichapa Tusker ya Kenya.

Yanga wampa kazi Mholanzi kuing'oa Al Ahly


Tayari Yanga imekubaliana na kuingia mkataba wa miaka miwili na Kocha Mholanzi, Johannes Franciscus ‘Hans’ van der Pluijm.

Kazi hiyo ilipangwa kumalizika leo asubuhi na kocha huyo ana mambo mengi sana ya kuburudisha.

Pamoja na kuwa na miaka 64, lakini ni mchapakazi na amekuwa gumzo alipokuwa na kikosi cha Berekum Chelsea ya Ghana.

Akiwa na timu hiyo msimu wa 2012-13, alizitoa jasho na kuzipa wakati mgumu pia timu vigogo kama Al Ahly, TP Mazembe na Zamalek.

Sasa ndiyo wakati wake na Yanga wamempa kazi ya kuhakikisha kikosi chao kinafanya kazi ya uhakika katika Ligi ya Mabingwa na mtihani mkubwa ni watakapokutana na Al Ahly kama watavuka kizingiti laini cha Wacomoro.

Gazeti la Championi lilikuwa chombo cha kwanza nchini cha habari kuandika kuhusu uamuzi wa Yanga kujitupia kwa van der Pluijm.

Sasa tayari yuko na leo alikuwa apelekwe Zanzibar, lakini huenda akapumzika kujiandaa na safari ya Uturuki.

Pamoja na mambo mengi lakini kocha huyo ana mambo mengi ya kujifunza kutoka kwake.

Utulivu:
Yanga imeamua kufanya kwa utulivu suala la kocha, awali lilikuwa likipelekwa mbio na kambi ya Uturuki, ikitaka kocha awahi kambi hiyo.
Lakini sasa uongozi wake umekubali hata kama kocha mpya hatakwenda Uturuki, lakini inataka ipate ‘mtu’ wa uhakika wa kuziba nafasi ya Brandts na ambaye atakuwa na uwezo kweli.

Mvuto:
Mvuto wa van der Pluijm kwa Yanga umetokana na mafanikio yake kwa Berekum Chelsea ambayo ilifanya vizuri katika Ligi ya Mabingwa msimu uliopita.
Ilikuwa Kundi B na timu za Al Ahly, TP Mazembe na Zamalek ambao ni vigogo waliowahi kuchukua ubingwa Afrika zaidi ya mara moja, lakini Berekum Chelsea ikaonyesha inaweza.
Hicho ndiyo kitu cha kwanza kilichoivutia Yanga kwa kuwa inahitaji kocha wa kuifikisha mbali kwenye Ligi ya Mabingwa ikizingatiwa katika mechi ya pili tu (kama itawang’oa Wacomoro), itakutana na Al Ahly ambao ndiyo mabingwa.
Kingine kinachoonyesha kuwavuta Yanga ni umri wa kocha huyo, miaka 64 ni sawa na mzazi hasa, lakini makocha wengi wenye umri huo wamekuwa wakali, wanajali zaidi kazi na wasiokuwa na mzaha hata kidogo.

Mazingira:
Kwa mazingira ya nchi za Kiafrika, van Pluijm hawezi kuwa na hofu hata kidogo kwa kuwa ameishi katika bara hili kwa zaidi ya miaka 10.
Miaka yote hiyo ameishi nchini Ghana ambako ameoa mrembo wa Kiafrika wa nchi hiyo.

Uwanja:
Mholanzi huyo ni mtu wa misimamo sana, amewahi kususia mazoezi kutokana na ubovu wa uwanja. Kama Yanga itaingia mkataba naye, basi ina wakati mgumu kuhakikisha inamaliza tatizo hilo.
Kabla ya kuondoka kwa Brandts, kilio chake kilikuwa uwanja usiokuwa na kiwango na magoli madogo, maana yake van Pluijm lazima atalizungumzia, kama halitatekelezwa kama ilivyokuwa kwa Brandts, basi kuna tatizo linaweza kutokea.

Misimamo:
Van der Pluijm ni mtu mwenye misimamo kweli, kama akikubaliana na Yanga na kuanza kazi, maana yake wachezaji wajiandae.
Anatoa ushirikiano mkubwa kwa wachezaji, lakini ni mkali na asiyehofia jina la staa yeyote.
Vyombo vya habari vya Ghana vilimbandika jina la Kiboko ya Vigogo kwa sababu mbili, kwanza kuzipa wakati mgumu timu kongwe za Ghana kama Asante Kotoko lakini kuwaweka benchi wachezaji nyota walioonekana kuvimba vichwa na timu ya Berekum Chelsea ikaendelea ‘kukamua’.

Wachezaji wageni:
Amekuwa na msimamo wa kutaka wachezaji wa kigeni wanaoonyesha uwezo mkubwa kuthibitisha tofauti yao na wenyeji.
Hivyo, Emmanuel Okwi, Mbuyu Twite, Hamisi Kiiza na Didier Kavumbagu wanalazimika kufanya kazi kweli na si kubahatisha, la sivyo kibarua kitakuwa kigumu ikizingatiwa msimu ujao ni wachezaji watatu tu.

Mfumo:
Uchezaji wa timu anazozifundisha ni kasi sana, anataka washambulie pamoja na kurudi pamoja, lakini amekuwa akisisitiza kikosi chenye walinzi warefu au wenye uwezo mkubwa wa kupiga vichwa.
Mchezaji akiwa mvivu, huenda akawa na wakati mgumu wa kupata namba katika kikosi chake.
Ndiyo maana mazoezi yake ya mwanzo wa msimu kama timu ataanza nayo, yanakuwa makali sana kuhakikisha wachezaji wake wanakuwa fiti kweli.

Van Nistelrooy:
Alimuibua mshambuliaji nyota wa Uholanzi, Ruud van Nistelrooy akiwa na umri wa miaka 17 tu na kumpa nafasi ya kucheza katika kikosi cha FC Den Bosch cha nchini kwao Uholanzi.
Van Pluijm aliitumikia FC Den Bosch kwa miaka 28 akiwa mchezaji na baadaye kocha. Akiwa kipa alicheza mechi 338 kwa misimu 18 kabla ya maumivu ya goti kumlazimisha kupumzika soka.
Aprili 1995, aliingia mkataba wa miaka miwili kuinoa SBV Excelsior hadi Desemba kabla ya kumuachia nafasi hiyo msaidizi wake John Metgod.
Mwaka 1999 alitua nchini Ghana na kujiunga na Ashanti Gold SC na kusaini mkataba wa mwaka, baadaye alitua nchini Ethiopia na kuanza kuinoa Saint George.
Sasa amekuwa akifanya kazi ya kuinoa timu ya vijana ya Feyenoord Ghana inayopata msaada kutoka katika klabu ya Feyenoord ya Rotterdam nchini Uholanzi.

Ngumi mkononi:
Oktoba, mwaka jana, akiwa na kikosi cha mabingwa wa Ghana wakati huo cha Medeama Sporting Club, van Der Pluijm alisaini mkataba wa miaka miwili, lakini hakudumu hata robo ya mkataba huo.

Kwani siku chache baada ya Makamu wa Rais wa Madeama, Albert Commey, kumtangaza kuwa kocha mkuu, akiwa ameiongoza timu hiyo katika mechi saba tu, van Der Pluijm alitangaza kuachia ngazi.
Uongozi wa Madeama ulikubali na kuficha, lakini ukweli baadaye uligundulika kuwa kocha huyo Mholanzi alizozana na msaidizi wake akavurumisha ngumi.
Katika mahojiano yake na mtandao wa Caf na vyombo vingine vya habari, Mholanzi huyo amekuwa akisisitiza kutotaka kulizungumzia suala hilo kwa madai ni sawa na kuongeza maadui bila sababu za msingi.
Kutokana na hali hiyo, alionyesha kuchukizwa na mwenendo wa mambo kwa kuwa kila alichokuwa akieleza kibadilishwe hakikufanyika, pia msaidizi wake pamoja na kwamba alipendekeza kuchukuliwa kwa Mholanzi huyo kama bosi wake, alikuwa mbeya sana.
Pamoja na hivyo, kikosi chake cha Madeama hakikufanya vizuri kabisa, kwani alianza na mechi ya Kombe la Super Cup dhidi ya Asante Kotoko na kuchapwa  bao 3-0. Aliiongoza timu kwa jumla ya mechi saba, badala ya kubeba jumla ya pointi 21, timu yake ilipata pointi nane tu!
Katika mechi hizo saba, kikosi chake kilishinda mechi moja tu, sare tano na kupoteza mechi moja.
Wakati anaondoka alikiacha kikiwa katika nafasi ya tisa kwenye ligi hiyo kwa tofauti ya pointi 10 dhidi ya vinara wakati huo, Asante Kotoko.
 
Credit:SALEH ALLY BLOG

TFF yatoa ubani msiba wa Njohole, kuzikwa kesho Mngeta


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Reli Morogoro, Boniface Njohole kilichotokea jana (Januari 12 mwaka huu) mkoani Morogoro.
Njohole ambaye alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Ufundi na Mashindano ya Chama cha Soka Morogoro (MRFA) hadi umauti unamkuta anatarajia kuzikwa kesho (Januari 14 mwaka huu) kijijini kwao Mngeta wilayani Ifakara.
TFF imesema msiba huu ni mkubwa kwa jamii ya mpira wa miguu kwani alitoa mchango akiwa mchezaji, kocha na kiongozi kwa nyakati tofauti, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF imetoa pole kwa familia ya marehemu Njohole, klabu ya Reli na MRFA na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. 
Aidha, TFF itatoa ubani wa sh. 200,000 kwa familia ya marehemu kama rambirambi zake.
Wakati huo huo: Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania (TPLB) ya TFF, Hamad Yahya atakuwa mgeni rasmi katika ufungaji wa semina ya waamuzi na makamisha.
Semina hiyo ya siku mbili itafungwa kesho (Januari 14 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Waamuzi zaidi ya 100 na makamishna 50 wanashiriki katika semina hiyo. Makamishna hao ni baadhi ya wale wanaosimamia mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
Kwa upande wa waamuzi ni wale wa daraja la kwanza (class one) ambao ndiyo wanaochezesha mechi za VPL na FDL. TFF inatarajia kuandaa semina nyingine baadaye mwaka huu kwa makamishna wapya wanaotaka kusimamia mechi za VPL na zile za FDL.

Jamal Malizni kuzuru kituo cha soka Alliance cha Mwanza


Rais wa TFF, Jamal Malinzi
Na Boniface Wambura RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atafanya ziara ya siku moja kutembelea kituo cha mpira wa miguu wa vijana cha Alliance cha jijini Mwanza. Lengo la ziara hiyo ni kuangalia jinsi Alliance inayoendesha shughuli zake ili Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liweze kushirikiana na kituo hicho kwa karibu. Rais Malinzi katika ziara hiyo atakayoifanya keshokutwa (Januari 15 mwaka huu) atafuatana na Mwenyekiti wa Kamati ya ya Vijana ya TFF, Ayoub Nyenzi na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Ramadhani Nassib.
Alliance inatarajia kufanya mashindano yatakayoshirikisha vituo vyote vya kuendeleza soka kwa vijana (academy) wiki ya tatu ya Februari mwaka huu jijini Mwanza.
Mashindano hayo yatashirikisha timu za umri wa miaka 13, 15 na 17 ambapo Alliance itagharamia malazi, chakula na usafiri wakati timu hizo zikiwa jijini Mwanza.

AC Milan yazidi kudoda Seria A

Berrard Demonico
Sassuolo - AC milan
'Muuaji' Demonico Berardi (25) akishangilia bao na wachezaji wenzake walipoiangamiza AC MIlan

KLABU ya AC Milan imeendelea kuteseka kwenye Ligi Kuu ya Italia Seria A baada ya usiku wa jana kunyukwa mabao 4-3 na 'vibonde' Sassuolo iliyokuwa uwanja wake wa nyumbani.
Shujaa wa wenyeji alikuwa ni Domenico Berardi aliyefunga mabao yote manne ya Sassuola katika dakika za 15, 28, 41 na 47 na kinda huyo mwenye miaka 19 kuweka rekodi ya kuwa mchezaji mdogo kufunga idadi hiyo ya mabao manne katika Seria A ikiwa ni baada ya zaidi ya miaka 80 na kumweka pabaya kocha wa AC Massimiliano Allegri.
Wageni walianza kuwaduwaza wenyeji kwa kupata mabao mawili ya chapchap kupitia nyota wake, Robinho na Mario Balotelli waliofunga dakika ya 9 na 13 kabla ya Berardi kuyarejesha na kuongeza jingine na kufanya timu ziende mapumziko zikiwa 3-2.
Kipindi cha pili Berardi aliendelea kuinyanyasa ngome ya AC Milan kwa kuongeza bao jingine kabla ya wageni kujipatia bao jingine la kujifutia machozi lililofungwa na Montolivo dakika nne kabla ya kumalizika kwa mchezo huo na kuicha Milan ikisaliwa na pointi zake 22 ikiwa nafasi ya 11.
Kwa ushindi huo Sassuolo iliyokuwa nafasi ya 18 imepanda hadi kwenye nafasi ya 16 ikifikisha pointi 17.



















Uganda The Cranes waanza vyema CHAN 2014


Man of the match Yunus Ssentamu celebrates his second goal against Burkina Faso
Sentamu akishangilia bao lake la pili

VINARA wa kandanda Kanda ya Afrika Mashariki, Uganda The Cranes imeanza vyema kampeni zake za kuwania ubingwa wa fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) baada ya kuisambaratisha Burkina Faso kwa mabao 2-1 katika pambano la kundi B lililochezwa usiku wa jana.
Mabao mawili kutoka kwa aliyekuwa nyota wa mchezo huo, Yunus Sentamu moja kila kipindi yalitosha kuiweka Uganda kileleni mwa kundi hilo ikifikisha pointi tatu na mabao mawili, huku Burkina Faso wakienda mpaka mkiani ikiwa haina pointi yoyote.
Sentamu alifunga bao la kwanza kwenye dakika ya 15 kabla ya kuongeza jingine dakika ya 73 na wapinzani wao kupata bao la kufutia machozi dakika mbili kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kupitia kwa Cyrille Bayala.
Michuano hiyo itaendelea tena jioni ya leo kwa mechi za kundi C, Ghana kuvaana na Jamhuri ya Congo na Libya kukabiliana na wawakilishi wengine wa ukanda wa CECAFA, Ethiopia.

Sunday, January 12, 2014

Simba, KCC hapatoshi kesho Fainali Kombe la Mapinduzi

kikosi cha Simba
KCC ya Uganda
 KIVUMBI cha michuano ya Kombe la Mapinduzi kinatarajiwa kumalizika kesho kwa pambano la Fainali kati ya Simba dhidi ya KCC ya Uganda litakalochezwa jioni kwenye uwanja wa Amaan, visiwani Zanzibar.
Simba inaivaa KCC baada ya kuitoa nishai URA pia ya Uganda kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na Mganda Joseph Owino, aliyekuwa akiichezea timu hiyo kabla ya kurejea Msimbazi na lile la Amri Kiemba.
KCC wenyewe waliwavua ubingwa Azam kwa kuwakandika mabao 3-2, licha ya kutanguliwa kufungwa 2-1 hadi wakati wa mapumziko.
Simba iliyowahi kunyakua taji hilo miaka miwili iliyopita, itakuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha Kombe hilo halichukuliwi na wageni kwani tangu ilipoanzishwa michuano hiyo taji hilo halijawahi kutoka nje ya Tanzania.
Ikiwa chini ya kocha Zdrakov Lugarosic, Simba itaendelea kuwategemea wachezaji wake nyota Ramadhani Singano, Harun Chanongo, Amri Kiemba na golini atakuwa Ivo Mapunda kuhakikisha KCC hawafuruki katika mchezo huo wa fainali unaotarajiwa kuhudhuriw ana viongozi wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na wale wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikizingatiwa kesho ni mapumziko kitaifa.
KCC ambayo haikuwa ikipewa nafasi kubwa, kabla ya kuja kuongoza kundi A walilokuwa na Simba katika mechi za awali siyo timu ya kubeza kwani imetoa upinzani mkubwa ikiwa haijafungwa mchezo wowote kama wapinzani wao ambao wana nyongeza ya rekodi ya kutoruhusu bao lolote langoni mwao mpaka sasa.
Timu huyo ya Jiji la Kampala inawategemea wachezaji wake kadaa nyota kama Ibrahim Kiiza na wengine ambao waliisimamisha Azam na kuwavua taji katika mechi ya Nusu Fainali ya kwanza juzi.
Uongozi wa Simba umenukuliwa jioni hii toka Zanzibar wakisema kikosi chao kipo imara tayari kuwapa raha Wazanzibar wanaosherehekea miaka 50 ya Mapinduzi na watanzania kwa ujumla ili kulibakisha taji hilo katika ardhi ya Tanzania kwa kuwazuia KCC wasiondoke nalo kama walivyofanya dada zao wa netiboli walioifunga timu ya taifa ya Tanzania kwenye fainali pia juzi.

Liverpool yatakata, Suarez nouma!

Liverpool's Steve Gerrard scores from the spot
Gerrard akitupia kambani bao la penati la Liverpool

LUIS Suarez ameendelea kuonyesha dhamira yake ya kunyakua kiatu cha dhahabu cha Ufungaji Bora wa Ligi Kuu ya England baada ya muda mfupi uliopita kufunga mabao mawili na kufikisha mabao 22 wakati akisaidia Liverpool kupata ushindi mnono ugenini wa mabao 5-3 dhidi ya Stoke City.
Suarez alifunga mabao hayo katika dakika za 32 na 71, huku wachezaji waliokuwa majeruhi nahodha Steven Gerrard na Daniel Sturridge wakifunga bao moja moja, Gerrard akifunga kwa mkwaju wa penati, huku bao la kuongoza la Liverpool likifungwa na beki wa Stoke City, Ryan Shawcross dakika ya 5 tu ya mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa Britannia.
Sturridge alifunga bao la tano dakika tatu kabla ya kumalizika kwa pambano hilo akitokea benchi, huku wenyeji wakipata mabao yao ya kufutia machozi kupitia kwa  Peter Crouch, Charlie Adam na Jonathan Walters.
Kwa ushindi huo Liverpool imefikisha jumla ya pointi 42 na kurejea kwenye nafasi ya nne ikiishusha Everton na Tottenham ambazo jana zilitakata na ushindi wa mabao mawili kila moja.

Zimbabwe yaibana Morocco CHAN 2014

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/en/8/8d/2014_African_Nations_Championship.png
TIMU ya soka ya taifa ya Zimbabwe imefanikiwa kuvuna pointi moja mbele ya Morocco baada ya kutoka nayo suluhu ya kutofungana katika pambano la kundi B la Michuano ya Fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani iliyoanza jana nchini Afrika Kusini.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Athlone, mjini Cape Town lilikuwa la vuta nikuvute kwa muda wote wa dakika 90 na kushuhudiwa timu hizo zikikosa mabao ya wazi na kufanya matokeo kuwa 0-0.
Mechi nyingine ya kundi hilo inatarajiwa kuanza hivi punde kati ya Uganda The Cranes itakayoumana na Burkina Faso kwenye uwanja huo huo wa Athlone.
Kesho katika mfululizo wa michuano hiyo iliyoasisiwa mwaka 2008,  Ghana itaumana mapema na Congo kabla ya Libya kuvaana na Ethiopia katika mechi za Kundi C na mechi za raundi ya kwanza zitamalizika Jumanne kwa mechi za kundi D kati ya DR Congo dhidi ya Mauritania na Gabon kuumana na Burundi.

Juventus haikamatiki Seria A, Roma, Napoli nazo zaua Italia

TIMU ya Juventus imeendelea kujikita kileleni baada ya kupata ushindi ugenini dhidi ya Cagliari, huku Roma na Napoli nazo zikipata ushindi wa kishindo katika mechi zao za Seria A jioni ya leo.
Juventus kwa ushindi huo wa mabao 4-1 dhidi ya wenyeji wao imeifanya ifikishe pointi 52 na kufuatiwa na Roma  yenye 44 baada ya kushinda nyumbani mabao 4-0 dhidi ya Genoa na Napoli kushinda mabao 3-0 na kujikita nafasi ya tatu ikiwa na pointi 42.
Mechi nyingine za leo katika Seria A imeshuhudia Fiorentina ikipata sare ya 0-0 ugenini dhidi ya Torino na  Atalanta ikishinda nyumbani 2-1 dhidi ya Catania.

Manchester City yaiua Newcastle kwao, na kuing'oa Chelsea kileleni

Edin Dzeko akishangilia bao lake dhidi ya Newcastle



BAO la mapema lililofungwa na Edin Dzeko katika dakika ya nane na jingine la dakika za lala salama kupitia kwa Alvaro Negredo yametosha kuipaisha Manchester City hadi kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England wakiiporomosha Chelsea iliyokwea nafasi hiyo jana.
City wakiwa ugenini kuifuata Newcastle United iliweza kupata mabao hayo na kuifanya ifikishe pointi 47, moja zaidi ya ilizonazo Chelsea iliyoibamiza Hull City nyumbani kwao kwa mabao 2-0.
Dzeko alifunga bao la kwanza akimalizia kazi nzuri ya beki wa pembeni wa City, Aleksandar Kalarov kabla ya Negredo kuwaduwaza wenyeji dakika za nyongeza kwa kufunga bao la pili na kuifanya City imalize mechi hiyo ikiwa vidume, ikiwa ni mechi yao ya sita mfululizo kushinda katika Ligi.
Hata hivyo vijana hao na Manuel Pelligrini wanaweza kusalia kwa muda tu kileleni hapo kama Arsena ambayo kesho itashuka dimbani itapata ushindi ugenini dhidi ya Aston Villa katika mechi pekee ya ligi hiyo.
Hivi punde pambano la Stoke City dhidi ya Liverpool litaanza kuchezwa katika mfululizo wa ligi hiyo.

Afrika Kusini, Mali waanza vyema CHAN 2014

Wachezaji wa Bafana Bafana wakishangilia ushindi wao jana dhidi ya Msumbiji

TIMU ya taifa ya Nigeria jana ilianza vibaya michuano ya CHAN baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 toka kwa Mali huku wenyeji wa michuano hiyo inayohusisha wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika, ikipata ushindi mnono wa mabao 3-1 dhidi ya Msumbiji.
Katika mechi ya wenyeji iliyochezwa uwanja wa Cape Town, jijini Cape Town, Msumbiji iliwashtua wenyeji wao kwa kupata bao la kuongoza lililofungwa kwenye dakika ya 11 kupitia Diogo.
Bao hilo lilikuja kurejeshwa na Bernard Parker katika dakika ya 30 kwa mkwaju wa penati na kufanya hadi mapumziko timu hizo kuwa nguvu sawa  kwa bao 1-1.
Kipindi cha pili kilikuwa cha wenyeji baada ya kujipatia mabao mawili kupitia kwa Hlompho Kekana na Parker kwa mara nyingine tena na kufanya Afrika Kusini kuzoa pointi tatu na kuongoza kwenye kundi lake la A ikifuatiwa na Mali waliowazabua majirani zao Nigeria kwa mabao 2-1.
Mabao ya washindi yalifungwa na Abdoulaye Sissoko katika dakika ya 11 na Adama Troure la dakika ya 54 kabla ya Nigeria kupata bao la kufutia machozi lililofungwa na Fuad Salami.
Jioni hii kuna mechi nyingine mbili zinazoendelea ambako Zimbabwe na Morocco mpaka sasa hazijafunga zikikaribia kwenda mapumziko na mechi ya Uganda The Cranes na Burkina Faso itafanyika usiku na MICHARAZO itawaletea matokeo yake.

Tanzia! Nyota wa zamani wa Reli, Taifa Stars afariki


Boniface Njohole enzi za uhai wake (Picha: Mtanda Blogu)
MCHEZAJI wa zamani wa klabu ya Reli ya Morogoro na Taifa Stars, Boniface Njohole amefariki dunia katika kijiji cha Mngeta tarafa ya Ifakara wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro. 
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mkoani Morogoro Karibu Mtendaji wa chama cha soka mkoa wa Morogoro (MRFA) Hamis Semka alisema Njohole amefariki dunia katika kijiji cha Mngeta majira ya saa 5:30 asubuhi baada ya kuumwa kwa muda mrefu.
Hata hivyo taarifa zaidi zinasema kuwa Njohole aliyekuwa akifahamika kama Boni, alikuwa akisumbuliwa na matataizo ya Figo na alikuwa akitibiwa Moshi, kabla ya kurejeshwa nyumbani kwake Ifakara na kukutwa na mauti. 
Taarifa zaidi zinaendelea kufuatiliwa kujua mazishi na taratibu nyingine juu ya msiba wa mwanandinga huyo
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na wadau wote wa soka kwa msiba wa Boniface Njohole na kutakia moyo wa subira kwa kutambua kuwa Kila Nafsi Itaonja Mauti. Mungu Aiweke Roho ya Marehemu Mahali Pema. Ameen

TFF yamlilia Sultan Sikilo

Jeneza la Mwili wa Sultan Sikilo likiswaliwa kabla ya kwenda kuzikwa jana, jijini Dar es Salaam..
Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mtangazaji wa michezo wa Radio Abood, Sultan Sikilo kilichotokea jana alfajiri (Januari 11) jijini Dar es Salaam.

Sikilo ambaye pia aliwahi kufanyia kazi Radio Times na Radio Kheri na hadi umauti unamkuta alikuwa Mweka Hazina Msaidizi wa Chama cha Waandishi wa habari za Michezo Tanzania (TASWA) amezikwa jana jioni katika makaburi ya Kibada, Kigamboni.

Msiba huo ni mkubwa katika sekta ya habari na mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Sikilo alifanya kazi na TFF kwa kuripoti shughuli zetu nyingi za mpira wa miguu, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Sikilo, Radio Abood na TASWA na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Pia TFF imetoa ubani wa sh. 100,000 kwa familia ya marehemu kama rambirambi zake.

Jamal Malinzi aanza vita dhidi ya dawa za kulevya katika soka

Rais wa TFF, Jamal Malinzi akizungumza kwenye uzinduzi wa programu ya Ishi Huru
Na Boniface Wambura
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amezindua programu ya kutoa elimu ya kupambana na matumizi ya dawa za kulevya kwa vijana iitwayo Ishi Huru.
Programu hiyo iliyozimduliwa jana (Januari 10 mwaka huu) jijini Dar es Salaam iko chini ya taasisi ya Africa Inside Out inayoongozwa na Rebecca Young wakati washirika (partners) ni TFF na kampuni ya Rhino Resources ya Marekani.
Rais Malinzi amesema matumizi ya dawa za kulevya nchini yamekuwa yakiongezeka, hivyo kuwa kikwazo kwa maendeleo ya vijana ambapo ameipongeza Africa Inside Out kwa programu hiyo kwa vile itazuia vijana
wengi kujiingiza katika matumizi ya dawa hizo.
“Moja athari kubwa za matumizi ya dawa za kulevya ni kupata maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutokana na kuchangia sindano za kujidunga dawa hizo.
“TFF tutatoa ushirikiano wa kutosha katika programu hii. Lakini pia tutaingiza Ishi Huru katika programu zetu za mpira wa miguu kwa vijana. Tutahamasisha jamii katika kupambana na dawa za kulevya,” amesema.
Katika uzinduzi huo, pia Rais Malinzi alizundua semina ya waelimishaji na kuwaeleza kuwa wamepata fursa hiyo kwa vile ni vijana wanaojituma, hivyo watafikisha vizuri ujumbe wa Ishi Huru katika shule na vituo vya vijana.

Wanawake, viongozi wa kitaifa, waalikwa Maulid Dar

MWENYEKITI Kamati ya Maandalizi ya Sherehe za Maulid kwa wanawake wa    mkoa wa Dar es Salaam, kuadhimishwa kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W),  Aisha Sururu (wa kwanza kulia), akiwaongoza wanawake wengine kuomba dua, baada ya kumaliza kikao cha maandalizi ya sherehe hizo
zitakazofanyika kesho, katika Ukumbi wa Diamond Jubilee.
***
WANAWAKE viongozi wa kitaifa na mkoa wa Dar es salaam, wameombwa
kujitokeza ili kuungana na wanawake wengine wa kiislam, katika
sherehe ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W).

Wito huo ulitolewa na Kamati ya Maandalizi ya sherehe hizo kwa upande
wa wanawake, na kubainisha kuwa hawataalika mgeni rasmi, badala yake ,
viongozi na wanawake wengine wawe kitu kimoja kuadhimisha siku hiyo.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Aisha Sururu, alisema, sherehe itafanyika
Januari 14, katika ukumbi wa Diamond Jubilee, na kwamba
itawakutanisha wanawake waislam wa mkoa wa Dar es Salaam na mkoa
jirani wa Pwani.

"Wanawake wa hali ya chini, wamefikiria kwanini sherehe za kidini
ambazo hazina harambee, michango wala kitu chochote, tualike mgeni
rasmi? Wakaona ni vyema kutangaza ili nao kama wananchi wajumuike na
wanawake wa hali ya chini, ambao watafarijika zaidi, kuona wamekaa
mkekani pamoja na viongozi wakubwa,"alisema
Aisha.

Mwenyekiti huyo, ambaye pia ni diwani viti maalum Ilala, alisema, kwa
wale ambao hawatafikiwa kwa mualiko wa mmoja mmoja, wanaruhusiwa
kujumuika na wenzao siku hiyo ya maadhimisho.

Maulid ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W), huadhimishwa duniani  kote kila ifikapo mfungo wa sita kwa kalenda ya kiislam. ikiwa ni

kumbukumbu tangu kuzaliwa kwa kiongozi huyo wa wafuasi wa dini ya
kiislam.

Maandalizi ya sherehe hiyo kitaifa, mwaka huu yatafanyika mkoani
Kigoma, ambapo Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA), limesema
mgeni rasmi atakuwa Rais Jakaya Kikwete.

Kesho, Keshokutwa Wabongo kula shushu!

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com press@ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
       P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
                                         
TAARIFA KWA  UMMA.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza kuwa kesho, Jumatatu, Januari 13, 2014, itakuwa ni Siku ya Mapumziko (Public Holiday) kwa Watanzania wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Rais Kikwete ameutangaza uamuzi huo mjini Zanzibar ambako leo ameungana na Watanzania na Wazanzibari wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, mwaka 1964.

Mapinduzi hayo yaliyoongozwa na mwasisi wa Zanzibar na Taifa la Tanzania, Hayati Abeid Amaan Karume yalifanikiwa kuung’oa madarakani utawala dhalimu wa Sultan na kuwawezesha kwa mara ya kwanza katika historia Waafrika walio wengine kujitawala ndani ya nchi yao wenyewe.

Yalikuwa ni Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofungua njia ya kuzaliwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar – miezi mitatu baada ya Mapinduzi hayo – Aprili 26, 1964.               
Naye Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein ametangaza kuwa kesho itakuwa Siku ya Mapumziko Tanzania Visiwani kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Rais Shein alitangaza mapumziko hayo wakati alipohutubia wananchi kwenye Uwanja wa Michezo wa Amaan mjini Zanzibar katika kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi.

Rais Shein alitangaza mapumziko hayo wakati alipohutubia wananchi kwenye Uwanja wa Michezo wa Amaan mjini Zanzibar katika kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi.

Mwisho.
Imetolewa na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS
Ikulu,
es Salaam.
12 January, 2014

Manchester City kuiengua Chelsea kileleni itaivaa Newcastle Utd

KLABU tishio kwa sasa nchini England, Manchester City chini ya kocha Manuel Pellegrini leo ina nafasi ya kukalia kiti cha uongozi wa Ligi Kuu ya Engalnd iwapo itaishinda ugenini dhidi ya Newcastle United na kuinegua Chelsea iliyoing'oa Arsenal jana kwa kuicharaza Hull City.
City itakuwa ugenini kuvaana na Newcastle ina pointi 44 na iwapo itashinda mechi hiyo ya jioni ya leo itafikisha pointi 47, moja zaidi ya zile ilizonazo Chelsea iliyokaa kileleni na pointi 46, moja zaidi ya waliokuwa vinara Arsenal ambayo yenyewe itashuka dimbani kesho kuvaana na Aston Villa ugenini.
Kikosi cha Pellegrini ambayo kimecheza mechi 12 kuanzia Desemba Mosi na kufunga mabao 36 katika michuano yote inayoshiriki msimu huu, huku ikiwa na rekodi ya kushinda nyumbani hata hivyo hawatakuwa na kazi nyepesi kwa Newcastle watakaokuwa uwanja wao wa nyumbani wa St James Park kutokana na timu kupoteza mechi mbili mfululizo kutoka kwenye lindi la ushindi wiki chache zilizopita.
Manchester City wanapewa nafasi kubwa ya kushinda pambano hilo kutokana na kuwa na safu kali ya ushambuliaji ikiongozwa na Alvaro Negredo, Edin Dzeko na kiungo Yaya Toure Mchezaji Bora wa Afrika kwa mara ya tatu mfululizo.
Mbali na mechi hiyo inayofuatiliwa kwa ukaribu na mashabiki wa kandanda pia leo kuna mechi nyingine nzuri ya Stoke City itakayopikaribisha Liverpool kabla ya kesho kuhsuhudiwa Aston Villa kuialika Arsenal katika pambano ambalo kama The Gunners watashinda itadhihirisha dhamira yake ya kunyakua taji la Ligi msimu huu baada ya miaka mingi ya kulikisikia kwenye bomba tu.

RATIBA
Jumapili Januari 12 
17:05 Newcastle V Man City
19:10 Stoke V Liverpool
Jumatatu Januari 13 

23:00 Aston Villa V Arsenal

Ni Bobby Williamson au Adel Amrouche kuinoa Yanga

Bobby Williamson




Adel Amrouche


Na Sanula Athanas, Zanzibar
MAKAMU Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Clement Sanga ameweka wazi kuwa pamoja na kupokea majina ya makocha 60 walioomba kazi ya kuifundisha timu hiyo, ni makocha wawili tu ambapo Yanga wameona wanauwezo wa kuifundisha timu hiyo.
Akizungumza mjini Zanzibar juzi usiku, Sanga alisema Kocha wa Gor Mahia, Bobby Williams raia wa Scotland na Kocha wa timu ya taifa ya Kenya (Harambee Stars), Mbelgiji Adel Amrouche, ndiyo makocha pekee wenye sifa za kuinoa timu yao inayokabiliwa na mashindano ya Klabu Bingwa Afrika mapema mwezi ujao.
Sanga, aliyekuwa kisiwani hapa tangu juzi kwa ajili ya kuiomba radhi serikali ya Zanzibar kwa kutoleta timu yao kushiriki mashindano ya Kombe la Mapinduzi, alisema baada ya kufanya mchujo wa majina zaidi ya 60  waliyokuwa nayo makocha hao ndio wawili ndiyo wamekidhi vigezo vinavyotakiwa na klabu hiyo ya Jangwani.
 “Unajua yanazungumzwa mengi kuhusu kocha wetu ajaye, lakini ukweli ni kwamba mpaka sasa hatujapata kocha mkuu na timu itaendelea kuwa chini ya Mkwasa (Boniface) hadi pale tutakapopata,” alisema kiongozi huyo.
“Tulipata zaidi ya maombi ya makocha 60, wanaotufaa ni Bobby na kocha wa Harambee Stars (Amrouche). Tumefanya mazungumzo nao lakini kuna masharti magumu yanayotuchelewesha kwa sababu wana mikataba na timu zao,” aliongeza Sanga.
Alisema kuwa bado wapo kwenye mazungumzo kuona ni kwa namna gani wanaweza kumpata kocha mmoja wapo kati ya hao kwa ajili ya kuchukua nafasi ya kocha aliyetimuliwa, Ernest Brandts raia wa Uholanzi.
Kocha huyo alitimuliwa siku mbili baada ya kufungwa na Simba magoli 3-1 kwenye mchezo maalum wa kirafiki wa 'Nani Mtani Jembe' uliochezwa Desemba 21 mwaka jana.
Kikosi cha Yanga kwa sisi kipo chini ya Kocha Charles Mkwasa ambaye amchukuliwa pamojana Juma Pondamali kuchukua nafasi za Fred Felix 'Minziro' na Mkenya Razaq siwa ambao pia walitupiwa virago pamoja na Brandts.

Yanga ipo nchini Uturuki ilipokwenda kuweka kambi ya wiki mbili kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu pamoja na ligi ya klabu bingwa Afrika.NIPASHE JUMAPILI

Waziri Miuu wa zamani wa Israel, Ariel Sharon afariki

BDEA70B3-44DF-4D1E-BDDB-A5DCEBA4F87F_w640_r1_sWaziri mkuu wa zamani wa Israel, Ariel Sharon, amefariki dunia Jumamosi akiwa na umri wa miaka 85.
Alikuwa waziri mkuu wa Israel mwaka 2001.
Amekuwa mahututi tangu mwaka 2006 kufuatia mfululizo wa matatizo ya kiharusi. 
Ariel Sharon alikuwa askari wa vita na baadae kuwa kiongozi wa nchi.
Alipokuwa mwanajeshi, alijulikana kwa ushujaa wake katika uwanja wa mapambano kwa miongo kadhaa kufuatia kuundwa kwa taifa la Israel, akijulikana hasa wakati wa vita vya jom kippur vya mwaka 1973. Katika mbinu za hali ya juu alizozionyesha, aliwaongoza wanajeshi wa Israel kuvuka mfereji wa suez, na kulikabili jeshi la misri.
Pia alijulikana na wengi kwa kuwa jabari na mbabe. Mwaka 1982, aliongoza uvamizi wa Lebanon ambao ulipelekea mauaji yaliyofanywa na wanamgambo wa Lebanon kwa mamia ya wapalestina katika kambi za wakimbizi za sabra na shatilla huko Beirut.
Kama mwanasiasa, Ariel Sharon pia alikuwa na utatanishi. Akiwa waziri, alihamasisha kuundwa kwa makazi ya walowezi wa kiyahudi kote katika maeneo ya wapalestina.
Serikali yake ilizikandamiza vurugu katika muda wa miaka michache, na kuanza kazi ya kuweka vizuizi vya usalama ambavyo hivi sasa vinawatenga waisraeli na wapalestina.
Mwaka 2006, bwana Sharon alipata mfululizo wa matatizo ya kiharusi na kuingia katika hali ya kupoteza fahamu. Nafasi yake ya waziri mkuu ilichukuliwa na Ehud Olmert.
Chanzo:VOASWAHILI.COM

Saturday, January 11, 2014

SUAREZ, PELLEGRINI WASHINDA TUZO ZA MWEZI.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Liverpool, Luis Suarez ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Desemba wa Ligi Kuu nchini Uingereza huku meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini akitajwa kama kocha bora wa mwezi. Suarez ambaye anakipiga katika klabu ya Liverpool alianza mwezi vibaya baada ya timu hiyo kukubali vipigo kutoka kwa Hull City, Manchester City na Chelsea lakini alionyesha kiwango cha juu baadae kwa kufunga mabao 10 katika mechi nne pekee. 


Mabao hayo alifunga katika mechi dhidi ya Norwich City ambapo alifunga manne, West Ham United mabao mawili, Totehham Hotaspurs mabao mawili na mengine mawili katika mchezo dhidi ya Cardiff City. Mabao hayo yaliisaidia Liverpool kushika usukani wa ligi katika kipindi cha Christmas iangwa baadae waliteleza mpaka nafasi ya tano katika kipindi cha mwaka mpya. Naye Pellegrini mwezi Desemba ulikuwa mzuri kwake baada ya kushinda mechi zote sita kati ya saba walizocheza huku mmoja wakitoka sare ya kufungana bao 1-1 na Southampton.

YANGA YAANZA KAMBI VEMA KWA KUICHAPA 3-0 ANKARA SEKERSPOR

Kikosi cha Young Africans kilichoanza leo dhidi ya Ankara Sekerspor
Young Africans imeanza vizuri katika kambi yake ya mafunzo nchini Uturuki baada ya kuifunga timu ya Ankara Sekerspor kwa mabao 3-0 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika pembeni kidogo ya eneo ililofikia katika mji wa Manavgat Antalya.

Kocha wa Young Africans aliwatumia wachezaji 18 jumla katika mchezo huo ambao wenyeji mara baada ya mchezo walimpongeza kwa timu yake kwa kucheza vizuri katika mchezo huo wa kirafiki.
Dakika ya 10 ya mchezo shuti lililopigwa na mganda Emmanuel Okwi lilishinda mlinda mlango wa Ankara Sekerspor ambapo aliutema mpira huo na kumkuta Didier Kavumbagu aliyeukwamisha mpira huo wavuni na kuhesabu bao la kwanza.

Timu zote ziliendelea kushambuliana kwa zamu na mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Ankara Sekerspor i0 - 1 Young Africans .
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na iliwachukua dakika moja Young Africans kujipatia bao la pili la mchezo kupitia kwa Emmanuel Okwi aliyeitumia vyema pasi ya mwisho ya kiungo Mrisho Ngasa aliywatoka walinzi wa Ankara Sekaspor na kumpasia mfungaji ambaye hakufanya makosa na kuukwamisha mpira wavuni.
Dakika ya 58 kocha Mkwasa alifanya mabadiliko, ambapo waliingia Hamis Kizza na Nizar Khalfani kuchukua nafasi za Didier Kavumbagu na kiungo Hassan Dilunga.

Hamis Kizza aliipatia Young Africans bao tatu la mchezo na la ushindi dakika ya 61 ya mchezo baada mpira aliogongewa na Domayo kuwapita walinzi wa Ankara Sekerspor na kumkuta Kizza ambaye alipiga shuti liliomgonga mlinzi wa Ankara Sekerspor wakati akiokoa na kujaa wavuni.

Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Ankara Sekerspor 0 -3 Young Africans.
Mara baada ya mchezo kaimu kocha mkuu wa Young Africans Charles Boniface Mkwasa alisema anashukuru vijana wake walicheza vizuri kwa kufuata malekezo na ndio maana wakaweza kupata ushindi huo,makosa yapo machache yaliyojitokeza na ataendelea kuyafanyia kazi.

"Mechi ilikua ni nzuri ukizingatia ndo mchezo wetu wa kwanza wa kirafiki tukiwa na siku ya tatu tangu tufike hapa Uturuki, kwa mazoezi ya jana vijana wameosha mabadiliko na leo wameweza kucheza vizuri na kuweza kupata ushindi, kikubwa naamini kwa siku zilizobakia nitaendelea kufanya marekebisho na kukifanya kikosi kuendelea kuwa bora pindi kitaporejea nchini tayari kwa mzunguko wa pili wa Lig Kuu ya Vodacom" alisema Mkwasa 

Kikosi cha Young Africans kilichocheza leo ni:
1.Juma Kaseja/Ally Mustafa "Barthez" (dk65), 2.Juma Abdul, 3.Oscar Joshua/David Luhende(dk 82), 4.Mbuyu Twite (C), 5.Kelvin Yondani, 6.Frank Domayo/Ibrahim Job(dkk 80), 7.Haruna Niyonzima/Saimon Msuva (dk72), 8.Hassan Dilunga/Nizar Khalfan (dk58), 9.Didier Kavumbagu/Hamis Kizza (dk58), 10.Mrisho Ngasa/Jerson Tegete (dk 68), 11. Emmanuel Okwi/Said Bahanuzi (dk 85)

Chelsea yaiengua Arsenal kileleni

 Eden Hazard scores for Chelsea
MABAO mawili moja kutoka kwa Ezen Hazard na jingine la Fernando Torres 'El Nino' yameiwezesha Chelsea kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 ugenini na kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England kwa muda.
Chelsea ilipata ushindi huo dhidi ya Hull City kwenye pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Kingstons Communication na kuifanya kufikisha pointi 46, moja zaidi ya Arsenal ambao watashuka dimbani keshokutwa.
Hazard alifunga bao la kwanza dakika ya 56 akimalizia kazi nzuri ya Ashley Cole kabla ya Torres kuongeza la pili dakika ya 87 na kuwakatisha tamaa wenyeji.
Jioni hii kuna mechi nyingine zinazoendelea katika ligi hiyo na baadaye Manchester United itaikaribisha Swansea City waliowatoa nishai kwenye michuano ya Kombe la FA katika dimba hilo hilo.

Simba yavunja mwiko, Kiemba we acha tu

 
AMRI Kiemba amezidi kudhihirisha kuwa yupo kikazi zaidi kama alivyopwahi kunukuliwa na Blogu hii baada ya usiku wa jana kuhusika na mabao mawili yaliyotosha kuvunja mwiko wa URA wa kutofungwa na Simba kwenye mechi ya Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi.
Kiemba, alitengeneza bao la kwanza lililofungwa na beki Joseph Owino kabla ya kuongeza jingine na kuipa Simba ushindi wa mabao 2-0 na kuivusha hadi Fainali ya michuano hiyo.
Mabao yote mawili yalifungwa kwenye kipi8ndi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kuisha timu zikiwa hazijafungana na URA wakicheza punguyfu baada ya nyota wao Oweni Kasule kutolewa kwa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu Ramadhani Singano 'Messi'.
Kwa ushindi huo asmbao umeifanya Simba kuweka rekodi kwa kuondoa uteja kwa URAnma kutinga Fainali bila kupoteza mchezo zozote wala kufungwa bao lolote katika lango lao, limeifanya Simba sasa kukutana na KCC ya Uganda iliwatemesha taji waliokuwa watetezi, Azam.
Azam walikumbana na lkipindi cha mabao 3-2 katika mechi ya kwanza iliyochezwa jioni kwenye dimba la Amaan licha ya kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-1, mabaoi yake yakiwekwa kimiani na kinda, Joseph Kimwaga.
Fainali ya michuano hiyo itachezwa Jumatatu kwenye uwanja huo wa Amaan.