STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 27, 2014

Zitto Kabwe ajitosa 'bifu' la Diamond, Ali Kiba

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2012/07/Zitto-Queen-Darlin-Mwasiti-na-wengine.jpg
Zitto Kabwe kati kati na wasanii wa Leka Dutigite
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiGj0GmR29OLVja_Ne6iqPPepXro0cl0KYsdtlk0FnXs6HVn77yq9d3I-IkfJuMIB_yYqsh__7Nqd03BCZ773OICts1TrjLHk2mjAm4GaZROS6hm6eaePjgcm5SF_3H52QfaMCsRsld1LCD/s1600/Ali+K+na+Diamond.jpg
Ali Kiba na Diamond ambao wanadaiwa hawaivi, japo Kiba amekanusha taarifa hizo akidai hana 'bifu' na Diamond
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, amejitosa kusuluhisha ugomvi wa muda mrefu wa wasanii wawili wa muziku wa kizazi kipya nchini, Ali Kiba na Nasibu Abdul 'Diamond'.
Zitto alitoa kauli hiyo juzi wakati akihojiwa katika Kipindi cha Mkasi kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha EATV baada ya kuulizwa kuwa ni jitihada gani amezifanya kusuluhisha ugomvi wa wasanii hao akiwa kama mlezi wa wasanii wanaotoka mkoani Kigoma.
Alisema anafahamu kuwapo kwa ugomvi wa kutoelewana kati ya wasanii Ali Kiba na Diamond na kwamba alishawahi kufanya jitihada za kuwaita kila mmoja kwa nyakati tofauti.
Alifafanua kuwa katika kuhakikisha anawasuluhisha wasanii hao, anaifanya kazi hiyo kwa umakini kwa sababu hataki kuonekana anaingilia maisha ya watu na kwamba ana imani atafanikiwa kuwapatanisha.
Kuhusu madai kwamba ana uhusiano wa kimapenzi na msanii Mwasiti Almas, alisema ni kweli kumekuwapo na uvumi huo lakini kimsingi hana uhusiano wowote wa kimapenzi na msanii huyo.
"Nasikitishwa na madai hayo yanayotolewa na baadhi ya watu, Mwasiti ni kama dada yangu ambaye nimekuwa nikimsaidia katika kazi zake, kuhusishwa naye kimapenzi ni jambo linalonisononesha,"alisema.
Zitto alisema wanaomhusisha katika suala la mapenzi na msanii huyo ni kwa sababu Mwasiti ameimba wimbo ambao amemtaja yeye (Zitto) lakini kiukweli hana uhusiani naye wa kimapenzi.
Alipoulizwa ni lini ataoa, alisema bado 'yupo yupo' na kwamba kuna mwanamke aliyemtaja kwa jina la Jack ambaye amezaa naye mtoto ambaye kwa sasa miaka nane na anasoma darasa la pili nchini Uganda.
Zitto alizungumzia pia kampuni ya Leka Dutigite inayounganisha wasanii wa Kigoma All Stars, na kusea kuwa ni kampuni ambayo kila msanii anayetoka mkoani Kigoma ana hisa na ikipata faida wanagawana.
Zitto alisema Leka Dutigite pia inamiliki kampuni nyingine ambayo imekuwa ikipata kazi mfano katika Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) na yeye kama mlezi amekuwa akitoa fedha zake kusaidia.

Hatimaye Di Maria rasmi Man Utd




HATIMAYE Muargentina, Angel Di Maria ametua na kusaini mkataba wa miaka mitano kuichezea Manchester United.
Mkataba huo ndiyo rekodi mpya ya usajili baada ya Man United kukubali kutoa pauni milioni 59.7 ambazo ni pauni milioni 60 ili kumpata.
Atakuwa akilamba mshahara wa pauni 200,000 kwa wiki, anachukua nafasi ya pili kwa mshahara mkubwa baada ya nahodha wake, Wayne Rooney.
Mchezaji huyo hata hivyo aliingia Old Trafford na mguu mbaya baada ya klabu yake hiyo kulambwa mabao 4-0 na timu ya Daraja la Kwanza katika mechi ya Kombe la Ligi na anategemea kuwemo katika kikosi cha Mashetani hao Wekundu katika mechi ya Ligi Kuu siku ya Jumamosi dhidiya Banley.

Giroud awapa presha Arsenal

HUENDA Olivier Giroud akakaa nje ya dimba kwa miezi mitatu ijayo baada ya vipimo kuonyesha kuwa amevunjika mfupa katika unyayo wakati wa mechi dhidi ya Everton Jumapili kwenye Uwanja wa Goodison Park, kwa mujibu taarifa kutoka Ufaransa.
Jarida la Ufaransa la L'Equipe limeripoti matokeo hayo ya majeraha ya Giroud yamezua hofu kwa Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger na kwamba sasa atalazimika kurudi sokoni kwa kasi kununua mshambuliaji.
Wenger alikuwa amesisitiza kwamba hana mpango wa kusajili mshambuliaji katika dirisha hili la usajili wa majira ya joto, akiamini kuwa usajili mpya wa Alexis Sanchez, huku hivi karibuni Theo Walcott akitarajiwa kurejea pamoja na uwapo wa Yaya Sanogo kungemwezesha kuwa na safu bora ya ushambuliaji.
Hata hivyo, kitendo cha Giroud kutokea benchi katika Uwanja wa Goodison Park Jumamosi na kusawazisha kulimpa matumaini kocha huyo, hatua iliyomfanya kumtabiria kuwa atamaliza Ligi Kuu England akiwa na mabao 25.
Kama taarifa hizo zitathibitishwa, mipango yake hiyo itafanyiwa mabadiliko, wakati huu ambao chumba cha majeruhi cha  Arsenal kikianza kusheheni wagonjwa ndani ya wiki mbili hizi za mwanzo wa msimu mpya.
Kuwa majeruhi kwa Giroud, kutamlazimisha Wenger kusaka huduma ya mshambuliaji wa Queens Park Rangers, Loic Remy, licha ya mapema majira haya ya joto kutupilia mbali uwezekano wa kumsajili Mfaransa huyo.

Arsenal katika mtihani mzito leo Ulaya

WAKATI kiungo wake mahiri, Jack Wilshere akiamini kuwa sare ya 2-2 waliyopata na Everton mwishoni mwa wiki itawasaidia kuwapoa morali wa kufanya vyema katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, Arsenal ina mtihani mgumu leo.
Klabu hiyo ya meneja Arsene Wenger inaikaribisha Besiktas ya Uturuki katika mechi ya marudiano ya mtoano wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Ze Gunnerz wakihitaji ushindi ili kuingia kwenye makundi.
Katika mechi ya mkondo wa kwanza timu hizo zilipokutana mjini Instabul, zilishindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya bila magoli, huku Arsenal ikimpoteza nyota wake kwa kupewa kadi mbili za njano na kufuatia nyekundu.
Walshere anaamini Arsenal wapo poa baada ya kufanikiwa kutoka nyuma kwa kufungwa mabao 2-0 na kufanikiwa kutoa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Everton Jumamosi iliyopita. 
Akihojiwa Wilshere amesema alama waliyopata dhidi ya everton ilikuwa ni muhimu kwani inawapa nguvu kwa ajili ya mchezo wao wa leo ambapo sare ya aina yoyote inaweza kuwaondoa mashindano ikiwa ni mara ya kwanza baada ya miaka mingi kwa vijana hao wa Emirates.

Kocha amuonya Balotelli, amwambie akiharibu inakula kwake

http://assets2.sportsnet.ca/wp-content/uploads/2013/05/balotelli_mario640.jpgMARIO Balotelli yuko katika "nafasi yake ya mwisho" baada ya kujiunga na Liverpool kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 16, alisema kocha Brendan Rodgers.
Mshambuliaji huyo wa Italia mwenye umri wa miaka 24 aliishuhudia kutokea jukwaani Liverpool ililala 3-1 ugenini dhidi ya klabu yake ta zamani ya Manchester City juzi baada ya kujiunga akitokea AC Milan kwa mkataba wa miaka mitatu.
Balotelli alikuwa maarufu kwa matukio ya utata wakati akichezea Man City lakini Rodgers anakubali kuwa kumsajili nyota ni "kama kucheza kamari" lakini anasema anaweza kujirekebisha.
"Tunaweza kumfanya awe bora kama mchezaji na ajutambue kama mtu mzima," alisema.
"Ni kijana mzuri. Alikuwa mwerevu sana. Anatambua mahala alipo ni wapi, katika wakati wake huu, na anatambua kwamba pengine hii ni fursa yake ya mwisho.
"Muda utaongea. Hakika ni kama kamari. Sitasema kwamba hafiti, ila anatambua anapaswa kufiti katika utamaduni wetu."

Mbunge Viti Maalum ataka viti maalum vifutwe Katiba Mpya

Ritta Kabati alipokuwa kitoa mtazamo wake kuhusu viti maalumu vya ubunge


MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Ritta Kabati (CCM) amesema moja ya mambo anayounga mkono katika mchakato wa Katiba Mpya ni kufutwa kwa viti maalumu vya ubunge.
Akizungumza hivi karibuni nje ya jengo la CCM Mkoa wa Iringa, Kabati alisema Viti Maalumu vina faida zake katika mchakato wa maendeleo lakini vinawadhalilisha sana wanawake.
“Siku hizi wabunge wanawake wa viti maalumu tunaitwa wabunge wa vitanda maalumu, huu ni udhalilishaji kwa sababu wengi wanahisi upatikanaji wake una mahusiano yasiofaa,” alisema.
Alisema utaratibu unaotumiwa na nchi kama Uganda na Rwanda kupata wawakilishi wanawake katika mabunge yao ndio unaopaswa kutumiwa na Tanzania na kama ikishindikana basi wanawake nao wapewe nafasi sawa na wanaume ya kugombea moja kwa moja kwenye majimbo ya Uchaguzi.
“Tumetembelea Uganda na Rwanda, kule hawaiti viti maalumu vya wanawake, wanaita viti vya wilaya vinavyoshindanisha wanawake wa vyama mbalimbali katika wilaya hizo,” alisema.
Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwakani, Kabati alisema endapo viti maalumu vitafutwa ataamua wapi atupe karata yake kati ya jimbo la Iringa Mjini au Kilolo.

“Kilolo ni kwetu na Iringa Mjini ni kwetu, kwahiyo kama Katiba Mpya itaondoa viti maalumu basi nitaamua wapi niende kati ya majimbo hayo,” alisema.

Mkubwa na Wanae kutambulisha chipukizi wapya

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6Kc_Ur8Lec9lYrBOF-IQAUaRSFQDK8Cdxz_8hhYUt4XGOWTORG7E7OH7FEYP_r6op9UjS_24xidUE0xrJVx_XNzUQTPr_8iyprsuw_DKzExTICOG6MOUOobngot5tCcegYMZg5V4AfR0/s1600/ya+moto+band.jpg
Said Fella akiwa nna wasanii wa Moto Band ambayo ni chimbuko lililoibuliwa na kito cha Mkubwa na Wanae
KITUO cha kukuzia na kuendeleza vipaji vya wasanii cha Mkubwa na Wanae kinatarajiwa kuwatambulisha rasmi wasanii chipukizi pamoja na nyimbo zao mpya siku ya Jumapili jijini Dar es Salaam.
Onyesho hilo litafanyika kwenye ukumbi wa Maisha Club na wasanii hao watasindikizwa na 'kaka' zao wa TMK Wanaume Family na Moto Band.
Akizungumza na MICHARAZO mmoja wa wakurugenzi wa kituo hicho, Said Fella 'Mkubwa Fella' alisema wasanii watakaotambulishwa katika onyesho hilo la Agosti 31 ni Dogo Muu, Getu, Dulla Yeyo, Mugogo na chipukizi wengine ambao wamekamilisha nyimbo zao mpya hivi karibuni chini ya kituo hicho.
"Tunatarajia kuwatambulisha rasmi wasanii wetu wapya ambao wamekamilisha nyimbo mpya. Onyesho hilo litafanyika Agosti 31 Masaki," alisema Fella.

Manchester Utd majanga matupu, yanyukwa 4-0

Finish: Arsenal loanee Benik Afoba (left) losts home under pressure from Keane for 3-0 with 20 minutes remaining in the game
Efoba akiwatungua Mashetani Wekundu bao la tatu
Unbelievable: United players stand shocked after MK Dons scored to make it 2-0, but worse was to come for Louis van Gaal's menJINAMIZI baya limeendelea kuiandama Manchester United baada ya usiku wa kuamkia leo kubamizwa mabao 4-0 na timu ya MK Dons.
Pambano hilo lililokuwa la michuano ya Kombe la Ligi (Capital One) limemuacha katika sintofahamu Kocha
Louis van Gaal ambaye ni kipigo cha pili kwa vijana wake tangu msimu mpya wa soka England uanze.
Mashetani Wekundu hao walikumbana na kipigo hicho kutokana na magoli ya Will Grigg dakika ya 25 na 63 na Benik Afobe anayecheza kwa mkopo MK Dons akitokea Arsenal aliyefunga pia mawili dakika ya 70 na 83.
Kipigo hicho kilimuacha kocha msaidizi wa Manchester United, Ryan Giggs kutokwa na machozi, huku LVG akishindwa kuamini kama timu ya 'mchangani' imewanyoa.

Serikali kufuta ada za shule hadi 'O Level'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhrXO0r3kx_dcsso6MygK29qiL6SqNgulI6NYBe6WNU4JSxVorninEgC8Jb5DESiJR9honvccMTJLLnYzpag6L0krQJgEKmhXaqk7S8R4a-XBtNL4hqkrcXjLcy4Qjk8K0vJ3sUEvwzdlHJ/s400/GO9G4311.JPG
Rais Kikwete akisamiliana na wanafunzi wa Shule ya Sekondari.
SERIKALI inajipanga kufuta ada za sekondari, ili elimu kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne, itolewe bure. 
Rais Jakaya Kikwete, alisema hayo juzi katika mkutano wake na wanajumuiya ya Chuo Kikuu cha Mzumbe cha Morogoro, na wakazi wa vijiji vya jirani na chuo hicho, katika ziara yake inayoendelea katika Mkoa wa Morogoro iliyoanza Agosti 20.
“Sasa hivi tunaangalia jinsi ya kufuta karo katika shule zetu zote za sekondari za Serikali, ili kuhakikisha kila mtoto anayeanza darasa la kwanza, awe na nafasi ya kumaliza sekondari kwa maana ya kidato cha nne, bila kulazimika kuacha shule kwa sababu ya ada.
“Tunaangalia kuondoa ada hii, ambayo wazazi wanalipa Sh 20,000 kwa shule za kutwa na Sh 70,000 kwa shule za bweni, ili watoto wetu waingie darasa la kwanza, na kwenda moja kwa moja hadi kidato cha nne bila wasiwasi wa kukwamishwa na ada,” alisema Rais Kikwete.
Kwa hatua hiyo, Rais Kikwete alisema mbali na kulenga kuinua elimu, pia itawapunguzia mzigo wazazi na walezi wa watoto wanaosoma katika shule hizo za sekondari za Serikali.
Alisema zipo sababu za msingi zinazokwamisha wanafunzi wengi wa shule za sekondari, kuendelea na masomo yao kutokana na wazazi wao kushindwa kulipia karo ya shule, kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo za umasikini.
Rais Kikwete alisema pamoja na kejeli nyingi zilizoelekezwa kwa shule za sekondari za kata, kiasi cha kuitwa Yeboyebo katika miaka ya mwanzoni ya shule hizo, bado zimekuwa na mafanikio makubwa, ambayo ni sehemu ya mafanikio ya Sekta ya Elimu katika miaka karibu tisa ya uongozi wake.
Akielezea historia ya kuanzishwa kwa shule za sekondari za kata, Rais Kikwete alisema wakati alipokuwa akiingia madarakani, hali ya watoto kuingia sekondari kutoka shule za msingi ilikuwa mbaya.Kwa mujibu wa Rais Kikwete, hali hiyo ilisababisha asilimia kati ya sita na kumi tu ya wanafunzi waliomaliza darasa la saba, kusonga mbele kwa sababu shule za sekondari zilikuwa chache.
“Kwa miaka mingi, hatukujenga shule mpya za sekondari na kama mnavyojua, Wakoloni wa Kiingereza ndio kabisa hawakujenga shule. Kazi hiyo waliwaachia Wamisionari. Kwa hiyo wakati tunaingia madarakani, hali ilikuwa mbaya ndiyo maana tukaja na Sera ya Shule za Kata,” alisema Rais Kikwete.
Alisema takwimu rasmi zinaonesha kwamba, kulikuwa na  shule za sekondari 1,745 mwaka 2005, zikiwemo shule 1,202 za Serikali na sasa ziko shule za sekondari 4,576, zikiwemo shule 3,528 za Serikali.
Mafanikio hayo ya kupanuka kwa sekta ya elimu, kwa mujibu wa Rais Kikwete, yalileta changamoto hasa ya ukosefu wa walimu wa masomo ya sayansi. Alisema Serikali imepambana na changamoto hiyo na zingine zilizojitokeza, ambapo sasa wapo walimu karibu wa kutosha wa masomo hayo kwa shule za sekondari zote nchini.
Mbali na kusudio la kufuta ada, Rais pia alisema Serikali  inaandaa utaratibu maalumu utakaowezesha kujenga mabweni katika  shule za msingi na sekondari zilizopo maeneo ya jamii ya wafugaji.
Alisema lengo ni kuwawezesha watoto wa jamii hiyo, waendelee kusoma hata pale wazazi na walezi wao wanapohama kutoka eneo moja kwenda jingine  kufuata malisho ya mifugo yao.
“Tuna tatizo kubwa katika eneo hili...watoto wengi wa wafugaji wanakatishwa masomo kutokana na wazazi ama walezi kuhama kutoka eneo moja kwenda jingine kufuata malisho...wanaohama wanaondoka na watoto wao wote na kuwakosesha fursa ya kusoma,” alisema Rais.
Kuhusu elimu ya juu, Rais Kikwete alisema  kwa sasa kuna vyuo vikuu 51, vikiwemo 15 vya umma na pia kuna ongezeko la fedha za mikopo ya elimu kutoka Sh bilioni 16 mwaka 2005 na kufikia Sh bilioni 345 kwa sasa.
Mbali na ongezeko la fedha za mikopo ya elimu ya juu, Rais Kikwete alisema wanafunzi wanaonufaika na mikopo ya elimu ya juu waliongezeka kutoka wanafunzi 16,000 mwaka 2005 hadi kufikia 95,000 kwa sasa.
Awali Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Profesa Joseph Kuzilwa, alipongeza Serikali kwa kukuza mitaala ya wanafunzi wa vyuo vikuu na kushauri kuwa ili wanafunzi washindane katika soko la ajira, upo umihimu wa mitaala  kuendelea kuboreshwa.
Alimwomba Rais Kikwete kusaidia kuboresha miundombinu mbalimbali ya chuo hicho kutokana na uchakavu wa majengo yake.
Naye Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo hicho, Boniface Maiga, alitaja changamoto kubwa zinazowakabili  kuwa ni pamoja na uhaba wa sehemu za malazi uliosababishwa na idadi kubwa ya wanafunzi wanaodahiliwa  na uchakavu wa miundombinu.
Alisema licha ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB),  kutoa mikopo hiyo kwa wakati, bado kuna malalamiko mengi kuhusu watoto wa matajiri na wenye uwezo, ambao wameendelea kupewa mikopo.
Aliiomba serikali kufanyia utafiti suala hilo na ikibaini hali hiyo, fedha hizo zitolewe kwa watoto wengi masikini.

Tuesday, August 26, 2014

TFF yaja na sheria kali kwa wauza, wanunua mechi

http://tff.or.tz/wp-content/uploads/2014/08/TFF-voda-Logo.jpg 
KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imeamua kuanzia sasa adhabu kwa watu wanaotoa rushwa au kupanga matokeo katika mchezo huo itakuwa ni kufungiwa maisha kujishughulisha na mchezo huo. Taarifa katika tovuti ya TFF imesema kwamba hayo yamefikiwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya shirikisho hilo juzi. Kwa muda sasa, kumekuwa na tuhuma nyingi za wachezaji na marefa kuhongwa ili kupanga matokeo- lakini hakukuwa na sheria madhubuti ya kupambana na hali hiyo- lakini kwa hatua hii mpya ya TFF dhahiri itasaidia kupunguza mchezo huo mchafu.  
  Aidha, baada ya Libya kujitoa kuwa mwenyeji wa Fainali za Afrika (AFCON) za 2017, Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limealika nchi wanachama kuomba uenyeji wa fainali hizo.
Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Agosti 24, mwaka huu imeamua Tanzania kuomba uenyeji wa fainali hizo.
“Tunatambua kuwa moja ya masharti ya kuandaa fainali hizo ni pamoja na nchi kuwa imeandaa moja ya mashindano ya vijana. Lakini kwa kuwa suala hili liko katika mazingira maalumu (exceptional circumstances) tunaamini CAF watafikiria ombi letu kwa msingi huo,”.
Awali Libya ilipewa uenyeji wa fainali hizo 2015, lakini zikahamishiwa Afrika Kusini kutokana na sababu za kiusalama. Hivyo, Libya ikapewa fainali za 2017 ambapo sasa imejitoa yenyewe kuandaa fainali hizo.
Wakati huo huo: Kamati ya Utendaji ya TFF imemteua Boniface Wambura kuwa Mkurugenzi mpya wa Mashindano kuanzia Septemba 1 mwaka huu.
Kabla ya uteuzi huo, Wambura alikuwa Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF kuanzia Januari 1, 2011. Nafasi hiyo sasa iko wazi na itajazwa baadaye na Kamati ya Utendaji.

26 waitwa Stars kuivaa Morocco



KOCHA mkuu wa timu ya soka ya Taifa, Mart Nooirj ametangaza kikosi cha wachezaji 26 kitakachocheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Morocco.
Mechi hiyo, ambayo imo kwenye kalenda ya Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA), imepangwa kuchezwa Septemba 5 mwaka huu nchini Morocco.
Wachezaji wapya waliomo kwenye kikosi hicho ni kiungo Said Ndemla wa Simba SC na washambuliaji Mwagane Yeya wa Mbeya City na Juma Luizio wa ZESCO United ya Zambia.
Kikosi kamili ni makipa; Deogratias Munishi (Yanga) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni Said Morad (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Shomari Kapombe (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Azam), Aggrey Morris (Azam), Joram Mgeveke (Simba) na Charles Edward (Yanga).
Viungo; Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba), Said Juma (Yanga) na Haruna Chanongo (Simba).
Washambuliaji; John Bocco (Azam), Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City) na Juma Liuzio ZESCO, Zambia).
Kikosi hicho kinatarajiwa kuingia kambini Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) mchana katika hoteli ya Accomondia mjini Dar es Salaam na kitakuwa kikifanya mazoezi Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

BASI LA HOOD LAGONGANA NA LORI ARUSHA

Basi la Hood lililopata ajali asubuhi ya leo eneo la Kikatiti, Arusha.
Raia wakishuhudia ajali ya basi la Hood ilivyotokea.
BASI la kampuni ya Hood lililokuwa likitoka Arusha kwenda Iringa llimepata ajali asubuhi ya leo eneo la Kikatiti, Arusha. Basi hilo lilitaka kugongana uso kwa uso na lori la mizigo, ndipo katika kukwepana ikatokea ajali hiyo. Abiria wa basi wamenusurika , ila lori lilidumbukia darajani na hakukuwa na mtu aliyepoteza maisha.

Mario Balotelli akabidhiwa namba ile ile 45

MSHAMBULIAJI nyota wa Italia, Super Mario Balotelli amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Liverpool kwa pauni milioni £16 akitokea AC Milan kwa mkataba wa miaka mitatu na kukabidhiwa jezi namba 45.
Balotelli, 25 alitua mchana wa jana Melwood na kumalizana na uongozi wa Liverpool kabla ya kusaini mkataba huo na kukabidhiwa jezi yenye namba hiyo ambayo amekuwa akitumia kuanzia Manchester City na AC Milan alikotokea kwa sasa.
Alifanyiwa ukaguzi wa afya na mtaalamu wa mambo ya utabibu wa Liverpool Ryland Morgans.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester City atakuwa akilipwa kwa wiki kiasi cha pauni £125,000 ndani ya uga wa Anfield, alihudhuria pambano la usiku wa jana dhidi ya Manchester City, ambapo klabu yake mpoya ilinyukwa na ile aliyoichezea kabla ya kwenda Milan.
History makers: Italian striker Balotelli poses with the European Cup, which Liverpool have won five times, most recently in 2005
Mshambuliaji wa kimataifa wa Italia Balotelli akiweka pozi mbele ya kikombe cha Ulaya ambacho Liverpool imetwaa mara tano huku mara ya mwisho ikiwa ni 2005
Ready for business: The 24-year-old arrived at Melwood on Monday afternoon to put the finishing touches to the transfer
Balotelli  akiwa amepozi pembeni ya nembo ya klabu yake mpya ya Liverpool.
Signing up: Balotelli returns to England after an 18-month absence having scored 30 goals with AC Milan
Balotelli akisaini mkataba wa kuichezea Liverpool akiwa anarejea England baada ya miezi 18 kupita tangu aondoke Manchester City kwenda AC Milan na kuifungia mabao 30.
Raring to go: Balotelli poses in the boot room at Melwood, and will be in attendance for Liverpool's clash with Manchester City on Monday
'A great team with young players': Balotelli, who left Manchester City in 2013, said Liverpool are one of the best teams in England

Hivi ndivyo Di Maria alipotua Manchester United

On the look out: Di Maria peers out of his United car as he arrives for the completion of his trasferKIUNGO Angel di Maria amewasili viwanja vya mazoezi vya Manchester United, Carrington kwa ajili ya kukamilisha uhamisho wa Pauni 60 kutoka Real Madrid ya Hispania.
Nyota huyo wa Argentina aliyeng'ara kwenye Kombe a Dunia amewasili England huku viongozi wa Old Trafford wakiendelea na mazungumzo na Real Madrid juu ya kukamilisha uhamisho wa dau la rekodi Uingereza.
Di Maria, mwenye umri wa miaka 26, anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake usiku huu ambao utamfanya alipwe Pauni 200,000 kwa wiki kwa zaidi ya miaka mitano, mshahara ambao pia utamfanya awe mchezaji wa pili kulipwa zaidi katika klabu hiyo baada ya Nahodha, Wayne Rooney. 
Uhamisho wote utaigharimu United zaidi ya Pauni Milioni 90 na mchezaji huyo ataingia moja kwa moja katika kikosi kilichojeruhiwa cha Louis van Gaal kwa ajili ya mchezo dhidi ya timu iliyopanda Ligi Kuu, Burnley.

Liverpool yamkaribisha Balotelli kwa kichapo


Balotelli akiishuhudia Liverpool ikilala Etihad kwa mabao 3-1
http://img.theepochtimes.com/n3/eet-content/uploads/2014/08/22/453741350-676x450.jpg
Kun Aguerro akishangilia bao lake walipoifumua Liverpool mabao 3-1
VIJANA wa Brendan Rogers, Liverpool wamemtambulisha mshambuliaji wao nyota kutoka AC Milan , mario Balotelli, wamejikuta wakipata kipigo cha mabao 3-1 ugenini mbele ya mabingwa watetezi Manchester City katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Machester City ni kama ilimkaribisha tena Balotelli kwenye dimba la Etihad kwa kuwaonyesha kuwa wao ni zaidi kwa ushindi huo ambao umeifanya timu hiyo kujogea kwenye nafasi za juu za msimamo wa ligi hiyo iliyomaliza raunid mbili za awali.
Mabao mawili ya Stevan Jovetic na jingine la Sergio 'Kun' Aguerro yalitosha kuwazima vijogoo vya Anfield ambao wanahaha kusaka mbadala wa mshambuliaji wao nyota waliyemuuza Barcelona, Luis Suarez.
Liverpool ingeondoka patupu Etihad kama siyo beki wa City Zabaleta kujifunga na kuwaoa bao la kufutia machozi na kuwapa wakati mgumu kujiandaa kuwakabili Tottenham Hotspur ambao wanaoongoza msimamo kwa sasa japo wanalinda pointi na Chelsea na City walioruhusu nyavu zao kufungwa bao moja tofauti na Spurs ingawa zote zina pointi 6 na mabao matano ya kufunga.

Monday, August 25, 2014

Samuel Eto'o ajiandaa kutua Everton

http://www.foci-live.hu/files/2014/05/samuel-etoo-chelsea1.jpgBAADA ya Liverpool kumpotezea na kuamua kumsajili Mshambuliaji mtukutu kutoka AC Milan, Mario Balotelli, Mcameroon, Samuel Eto'o anajiandaa kutua kwa mahasimu wa Liverpool, Everton imethibitika.
Eto'o aliye huru baada ya kumaliza mkataba wake wa mwaka mmoja na Chelsea, inaelezwa yupo hatua ya mwisho kutua kwa kikosi cha kocha Roberto Martinez.
Nyota huyo wa zamani wa klabu za Real Madrid, Barcelona, Inter Milan na Chelsea, alikuwan akitajwa kuelekea Anfield baada ya Jose Mourinho kumchunia Stamford Bridge.
Mshindi huyo wa tuzo ya klabu bingwa Ulaya, Eto’o amekuwa akihusishwa na vilabu kadhaa kiangazi hii lakini taarifa za hivi punde zinaonekana wazi kuwa Everton maarufu kama Toffees wameshindwa mbio za kupata huduma yake.
Eto'o 33 amehifadhi rekodi nzuri ya kufunga zaidi ya magoli 300 na Martinez anataka mtu wa kutumainiwa nyuma ya mshambuliaji wake Romelu Lukaku.
Arouna Kone amekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na kuwa majeruhi na bado ataendelea kukosekana ilhali Steven Naismith akiwa ndio mshambuliaji namba mbili.
Eto’o atalazimika kupunguza kiasi cha malipo anayotaka cha pauni £130,000 kwa wiki endapo atakabidhiwa mkataba wa miaka miwili ambao inaonekana ni kama Everton imefanya usajili kwa fedha fedha nyingi msimu huu wa uhamisho.

Mshindi wa Mwanamakuka 2013 kuzikwa kesho Dar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiL5zHRfDLq1GCnpOrurq-fFbkQa4bBB05ILyLnvaZizKwGBUSjk2dDSjaI5R7R6k_7Lqv1H1dGiVoXsgsoxON0J4v0oEtOvMYDpcPFXkzrwjk-9wwY7QKJpardBHV8n8tGn2aDT8HlVLpO/s1600/Mwanamakuka.jpg
Aziza Mbogolume enzi za uhi wake akiwa na washindi wenzake wa Tuzo za Mwanamakuka 2013, Leila Mwambungu Kushoto na Theo aliyekuwa mshindi wa tatu.
MWILI wa aliyekuwa Mwanamakuka 2013, Aziza Mbogolume unatarajiwa kuzikwa kesho majira ya mchana.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopenyezwa na chanzo chetu ni kwamba msiba wa marehemu upo Magomeni Mwembechai na kwamba tayari wanandugu na marafiki wa marehemu wamekusanyana na kupanga kumhifadhi mwenzao kesho mchana maeneo ya Magomeni Kagera.
"Marehemu Aziza Mbogolume anatarajiwa kuzikwa kesho saa 9 mchana Magomeni, na hapa tulipo tunajipanga kwa ajili ya shughuli hiyo ili kumsindikiza mwenzetu," chanzo hicho kilisema.

Tanzania kuandaa AFCON 2017?

Rais wa TFF, Jamal Malinzi anayeipigania Tanzania kuandaa Fainali za Afrika 2017
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetuma maombi kwa Shirikisho la Soka Africa (CAF) kwa ajili ya kuwa wenyeji wa michuano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) za mwaka 2017, kufuatia Libya kujitoa.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa, tayari barua ya ombi hilo imetumwa CAF na Rais Jamal Malinzi.

Malinzi amenukuliwa mapema leo akisema kuwa wana uwezo na wako tayari kuwa wenyeji wa fainali hizo- hivyo wataomba. “Tutaomba kuwa wenyeji wa AFCON ya 2017 kuziba pengo la Libya, tuko tayari na tuna uwezo, tunatarajia sapoti kubwa ya Serikali na wadau wengine wa Tanzania katika hili,”amesema Malinzi. Libya imeamua kujitoa kutokana na vurugu za kisiasa zinazoendelea nchini humo- hivyo kuhofia mazingira ya kiusalama. Awali, Libya ilipewa uenyeji wa fainali za mwaka 2013, lakini ikajitoa kwa sababu kama hizo na Afrika Kusini ikapewa nafasi hiyo- huku makubaliano yakifikiwa wao wataandaa AFCON ya mwaka 2017.
Jumamosi ikatangazwa tena, Libya imejitoa baada ya viongozi wa nchi hiyo kukutana na Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Issa Hayatou.
CAF ikasema jitihada za kumsaka mbadala wa Libya zinaanza mara moja- maana yake kujitokeza kwa Tanzania ni ahueni kwao.
Kwa sasa, Tanzania inaweza kabisa kuwa mwenyeji wa fainali hizo kwa kuwa ina viwanja visivyopugua vitatu vyenye sifa, ingawa vingine vitahitaji marekebisho madogo.
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam hakuna shaka una sifa zote, wakati CCM Kirumba mjini Mwanza na Sheikh Amri Abeid Arusha vitahitaji marakebisho kidogo.   
Iwapo Tanzania itafanikiwa kupata uenyeji wa fainali za mwaka 2017, itakuwa imefuzu moja kwa moja kucheza michuano hiyo bila kupitia kwenye hatua ya mchujo.
Na hiyo itakuwa mara ya pili kihistoria kushiriki AFCON baada ya 1980 mjini Lagos, Nigeria wakati huo bado michuano hiyo ikiitwa Kombe la Mataifa ya huru ya Afrika.
Tanzania ilipangwa Kundi A pamoja na wenyeji Nigeria, Ivory Coast na Misri na ikashika mkia. Ilifungwa 3-0 na Ngeria, 2-1 na Misri na kutoka sare ya 1-1 na Ivory Coast.  
Yapo matumaini makubwa Tanzania ikafanikiwa kupewa yenyeji wa michuano hiyo mwaka 2017, kutokana na uhusiano mzuri baina ya Hayatou na rais wa sasa wa TFF, Malinzi. Kwa ujumla, FIFA na CAF zina imani kubwa na utawala wa Malinzi.

Rais Kikwete amtunuku Luis Figo Tuzo Ikulu


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa zawadi ya kinyago mchezaji veterani wa timu Real Madrid Luis Figo wakati wa hafla ya chakula cha jioni aliyowaandalia wachezaji wa timu hiyo na timu ya maveterani ya Taifa Stars ikulu jijini Dar es Salaam jana usiku baada ya mechi ya kirafiki ambapo Real Madrid illifungaTaifa Stars 3-1 katika uwanja wa Taifa. Picha na Freddy Maro

Boniface Wambura azidi kuula TFF

Mkurugenzi Mpya wa Mashindano wa TFF, Boniface Wambura
AFISA Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Boniface Wambura Mgoyo ameula baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mashindano wa shirikisho hilo.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa, Wambura amepandishwa cheo na hivyo ataachana na kiti chake cha sasa cha usemaji wa shirikisho hilo.
Wambura amekuwa kipenzi cha wanahabari kutokana na ushirikiano wake kwa vyomo vya habari na alikuwa katika uongozi uliopita wa rais Leodger Tenga.
Mkurugenzi huyo mpya wa Mashindano wa TFF anatajwa kama Afisa Habari Bora aliyewahi kutokea ndani ya TFF tangu shirikisho hilo lilipobadilisha mfumo wake wa uongozi kwa kuajiri baadhi ya watendaji wake.

Stars kukipiga na Morocco kirafiki tarehe ya FIFA

http://tff.or.tz/wp-content/uploads/2014/05/taifa-stars-2014.jpgTIMU ya soka ya taifa, Taifa Stars kitasafiri mpaka Morocco kwenda kucheza na wenyeji wake katika mechi ya kirafiki ndani ya tarehe za Fifa.
Mechi hiyo imepangwa kuchezwa Septemba 5 nchini Morocco. Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Mwesigwa Celestine amesema wamepokea mwaliko na tayari Kocha Mart Nooij ameishatangaza kikosi chake.
"Ni tarehe ambayo iko ndani ya tarehe za Fifa, hivyo maandalizi yanaanza na kocha ameishaita kikosi," alisema Mwesigwa ambaye pia ni katibu mkuu wa zamani wa Yanga.
Katika mechi yake ya mwisho, Stars ilichapwa kwa mabao 2-1 ikiwa ugenini nchini Msumbuji na kutolewa katika mbio za kuwania kucheza michuano ya Mataifa Afrika.

Mashetani Wekundu kuweka rekodi mpya England

http://www3.pictures.gi.zimbio.com/Angel+Di+Maria+Hertha+Berlin+v+Benfica+UEFA+At4PKx7NL51l.jpgKLABU ya Manchester United inajiandaa kuvunja rekodi ya usajili nchini Uingereza kwa kutaka kumsajili winga mahiri wa timu ya Real Madrid ya Hispania, Angel Di Maria. 
Meneja wa Madrid Carlo Ancelotti amebainisha kuwa Di Maria, 26 tayari ameshawaaga wachezaji wenzake kuelekea katika uhamisho wake huo. 
Inakadiriwa kuwa United italazimika kuilipa Madrid kitita cha paundi milioni 75 kama wanahitaji saini ya winga huyo. 
Iwapo United itafanikiwa kutoa kitita hicho watakuwa wamevunja rekodi ya usajili iliyowekwa na Chelsea wakati walipomsajili Fernando Torres kwa paundi milioni 50 kutoka Liverpool mwaka 2011. 
Usajili mkubwa uliowahi kuweka rekodi na kufanywa na United ulikuwa ni wa Rio Ferdinand ambaye alitua Old Trafford kwa paundi milioni 29.1 akitokea Leeds mwaka 2002. 
Muargentina huyo alitua Madrid akitokea Benfica kwa ada ya paundi milioni 36 mwaka 2010 na kufanikiwa kushinda taji la La Liga mwaka 2012 na Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita.
United iliyoanza Ligi Kuu ya England kwa kuchechemea ikivuna pointi moja tu katika mechi zake mbili za awali inahitaji kuimarisha kikosi ili kuepuka aibua ya msimu uliopita ilipoambulia patupu na kushika nafasi ya saba katika msimamo.

Msiba! Mshindi wa Mwanamakuka 2013 afariki ghafla Dar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhyYwoD36yvdGlaOL3ORieTYDqvxgwsMZIsGstevHX_YaoQUruSXJkbqlOgESxvUAZ0mKG4ppueLUIfB4QR6Ju9zwPnP1y4u6UA3VVUKvEzFRx23Hz2_GQGJgQ4iTx0l26MHCnbPjmDgrE/s1600/03.jpg
Aziza Mbogolume (wa pili kulia) enzi za uhai wake wakati akipokea mfano wa hundi baada ya kushinda tuzo ya Mwanamakuka 2013 kutoka kwa Mke wa Makamu wa Rais, Aisha Bilal.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjEhuHL63Ig6gjF5Xc1JpxqSt6vf2aLhmZacDjbwGHioBlL2Kz-ulsLv7cr0u9yRc1cBCRQN1BcSvJEpTwV9AEuu7SLra67sfOijJkTAcp25ZG4F7Ab78fk7TabOZ4lz7AWJ0pGrAn-iLku/s640/DSC_3104.JPG
Baadhi ya viongozi waratibu wa shindano la Tuzo za Mwanakuka wakistaajabia kazi za mikono ya Aziza Mbogolume (wa pili toka kushoto) enzi za uhai wao katika maonyesho ya mwaka huu yaliyofanyika Escape 1 Mikocheni
HABARI zilizotufikia muda mfupi uliopita zinasema kuwa, aliyekuwa mshindi wa Shindano la Wajasiriamali Tanzania maarufu kama Tuzo za Mwanamakuka zilizoasisiwa mwaka 2012 Aziza Mbogolume amefariki dunia ghafla mchana huu jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo MICHARAZO imepenyezewa na wasomaji wake na kuthibitishwa na Mshindi wa mwaka huu, aliyekuwa wa pili wakati marehemu Aziza akiibuka kidedea, Leila Mwambungu ni kwamba marehemu alikumbwa na mauti mchana wa saa 9 kutokana na tatizo la shinikizo la Moyo.
Inaelezwa kuwa kabla ya kukumbwa na mauti, Aziza aliyenyakua tuzo hiyo na kuzoa kitita cha Sh. Mil 6 toka kwa waandaji wa shindano hilo Marafiki Wanawake wa Tanzania UWF na kudhaminiwa na benki ya Wanawake Tanzania (TWB) kwa kipaji chake cha kuchora picha mbalimbali za mapambo alikuwa akisumbuliwa na tatizo hilo.
"Ni kweli hata mwenzetu amefariki. Nilipigiwa simu na Mwenyekiti wa UWF, Mariam Shamo na kunijulisha na nimempigia mtoto wa marehemu naye amenithibitishia. Kwa kweli inasikitisha kwa sababu ni wiki iliyopita nimetoka kjuwasiliana naye na kuahidi kuja kuniona," alisema Leila kwa sauti na huzuni.
Leila alisema, yeye ametoka kujifungua na hivyo alimjulisha mshiriki mwenzake wa tuzo hizo na shoga wake juu ya kujifungua kwake salama na kumjulisha angeenda kumjulia hali na ghafla leo mchana napigiwa simu juu ya msiba wa Aziza.
Mipango ya mazishi ya marehemu Mwanamakuka huyo wa 2013 zinaendelea na MICHARAZO itawajulisha mara itakapopatra taarifa kamili.
Marehemu Aziza aliyezaliwa miaka zaidi ya 40 mjini Tabora na ameacha mtoto mmoja wa kike aliyekuwa akiishi naye Magomeni Mwembechai na kufanya shughuli zake za uchoraji na uuzaji wa bidhaa za mapambo eneo la Mwenge Vinyago. Mwenyezi Mungu Aiweke Roho ya marehemu Mahali Pepa Peponi. Innalillah Waina Illah Rajiun.
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, familia na jamaa wa marehemu Aziza Mbogulume na kuwatakiwa kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Kinyambe aamua kuanzisha kampuni Mbeya

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi5-pbZqCmcNeiYqrVHRY3y_sfqCVb4UIpeChgSXdfJrz3hNMke98YqCfzCkGaH1Y63h7esADXTOSwKFTDD4NMAsQWlUV49YDxA9oMxEWSPWmz_SeHnc7E7D47-Dzd5qppBKntAyhY9rYLb/s1600/1521701_579327915475733_414873147_n.jpg
Kinyambe kushoto, alipokuwa Vituko Show akiwa na mpiga picha Yosso Komando
MCHEKESHAJI maarufu nchini James Mohammed 'Kinyambe' ameanzisha kampuni yake ya kutengeneza filamu iitwayo Kinyambe Video Production ambayo ipo njiani kuachia kazi ya kwanza iitwayo 'Fumbafu Thana', huku akimaliza nyingine jijini Mbeya.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka kambini Mbeya, Kinyambe alisema kampuni hiyo ambayo inadili na kutengeneza filamu na video za muziki, itakuwa ikisaidia wasanii chipukizi wa mkoani humo na kwingineko ambao watakuwa wakihitaji kuendeleza vipaji vyao.
Kinyambe aliyejipatia umaarufu mkubwa kwa staili yake ya kuigiza kama zezeta na kuyabadilisha macho yake kama kinyonga, alisema filamu ya 'Fumbafu Thana' ilitengenezwa mapema, lakini ilikwama kutokana ambapo sasa itaachiwa mapema mwezi ujao.
Alisema wakati filamu hiyo ikiwa njiani kutoka, pia ameshaanza kutengeneza filamu nyingine aliyoigiza na wasanii chipukizi wa jijini Mbeya akiwamo Deus Luis aliyewahi kuuza sura na marehemu Steven Kanumba katika filamu ya 'Poison Leather'.

Juma Luizio 'Ndanda' achekelea maisha mapya Zesco

http://images.uncova.com.s3.amazonaws.com/fad774132f9c41bc2ebfb8ec3a7a75a625cd45e6.jpg
Juma Luizio akiwa kwenye mazoezi ya timu ya Zesco nchini Zambia
MSHAMBULIAJI chipukizi wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa katika klabu ya ZESCO ya Zambia, Juma Luizio 'Ndanda', amesema hakuna kitu kinachomstaajabisha ugenini kama viwanja vya mazoezi vya timu.
Ndanda anayeichezea pia timu ya taifa aliyetua Zesco akitokea Mtibwa Sugar alisema klabu za Zambia zinajitahidi mno kuwa na viwanja vya mazoezi tofauti na ilivyo nyumbani Tanzania.
Akizungumza na MICHARAZO kwa njia ya mtandao mapema leo asubuhi, mchezaji huyo alisema mazingira mazuri aliyokutana nayo Zambia yamemfanya kujisikia faraja.
"Dah mazingira ya huku fresh sana kaka wametuzidi sana kwa sababu kwamba ni waelewa wanaojua nini maana ya mpira, pili wanawalipa vizuri wachezaji pia kuhusu viwanja dah! Aisee kila timu wamejitahidi kuwa na uwanja wa mazoezi na mechi tena vizuri tofauti na huko," alisema.
Luizio aliyemaliza msimu uliopita akiwa mmoja wa wafungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara, alisema kwa kipindi kifupi tangu atue Zesco aliyoingia mkataba wa miaka mitatu ameyazoea mazingira ya soka la nchini hiyo.
"Nashukuru sana nimeshazoea maisha ya huku na naahidi kuitangaza vyema nchi yangu nikiwa na ndoto za kupata nafasi ya kucheza soka Ulaya," alisema.