STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 6, 2014

Ubaguzi! Mchezaji afungiwa kwa kubaguliwa Urusi

Kanga (kushoto) aliyefungiwa Russia kwa kutoa ishara za matusi baada ya kubaguliwa na mashabiki wa Spartak Moscow
KIUNGO wa kimataifa wa Gabon, Guelor Kanga amefungiwa mechi tatu na Shirikisho la Soka la Urusi, RFU baada ya kuonyeaha ishara ya matusi akikerwa na ubaguzi aliofanyiwa na mashabiki wa Spartak Moscow.
Kanga alionyesha ishara hiyo baada ya kuonyesha ishara ya matusi kwa mashabiki wa Spartak Moscow ambao walimfanyia vitendo vya ubaguzi wa rangi. 
Kiungo huyo wa klabu ya FC Rostov mwenye umri wa miaka 24 alikuwa akipigiwa kelele za nyani na mashabiki wa Spartak wakati wa mchezo wa Ligi Kuu nchini humo uliofanyika jijini Moscow.
Katika kujibu mapigo ya kejeli hizo nyota huyo alitoa ishara hizo hatua ambayo RFU ilibidi kuchukua hatua kwa kumtoza pia na faini ya paundi 600. 
Spartak nao walitozwa faini ya paundi 830 kutokana na mashabiki wao kuonyesha vitendo vya kibaguzi. 
Septemba mwaka huu beki wa Dynamo Moscow Christopher Samba alifungiwa mechi mbili kwa kufanya tukio kama hilo wakati mashabiki wa timu ya Torpedo Moscow walivyomfanyia vitendo vya kibaguzi.
KIUNGO wa kimataifa wa Gabon, Guelor Kanga amefungiwa mechi tatu na Shirikisho la Soka la Urusi-RFU kwa kuonyesha ishara ya matusi kwa mashabiki wa Spartak Moscow ambao walimfanyia vitendo vya ubaguzi wa rangi. Kiungo huyo wa klabu ya FC Rostov mwenye umri wa miaka 24 alikuwa akipigiwa kelele za nyani na mashabiki wa Spartak wakati wa mchezo wa Ligi Kuu nchini humo uliofanyika jijini Moscow jana. Nyota huyo naye alijibu mapigo hatua ambayo RFU ilibidi kuchukua hatua kwa kumtoza pia na faini ya paundi 600. Spartak nao walitozwa faini ya paundi 830 kutokana na mashabiki wao kuonyesha vitendo vya kibaguzi. Septemba mwaka huu beki wa Dynamo Moscow Christopher Samba alifungiwa mechi mbili kwa kufanya tukio kama hilo wakati mashabiki wa timu ya Torpedo Moscow walivyomfanyia vitendo vya kibaguzi.

Make Money

Arsenal yafa ugenini, Spurs, Liverpool zang'ang'aniwa

Stoke's Peter Crouch recreates the 'Cristiano Ronaldo' celebration for his goal
Crouch akishingalia bao lake la mapema dhidi ya Arsenal
Ryan Mason and Marouane Chamakh
Vita ya Spurs na Crystal ilikuwa hivi
Steven Gerrard
Nahodha Steven Gerrard akiipigiania LIverpool akitokea benchi bila ya mafanikio
Charlie Austin
QPR ilipotakata nyumbani
SAA chache baada ya vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea kunyukwa ugenini ikiwa ni kwa mara ya kwanza, Arsenal nayo imekumbana na aibu kama hiyo ugenini baada ya kulala mabao 3-2 kwa Stoke City.
Dalili mbaya kwa Arsenal zilianza mapema baada ya kufungwa bao la kushtukiza dakika moja tu tangu kuanza kwa pambano hilo wakati Peter Crouch alipoiandikia Stoke bao la kuongoza akimaliza kazi ya Mamme Diouf.
Dakika ya 35 Bojan aliiongezea wenyeji bao kabla ya kumegewa pande na Jonathan Walters, ambaye alifunga bao jingine la Stoke lililokuwa la tatu sekundu chache kabla ya mapumziko.
Vijana wa Arsene Wenger walirejea kwa kasi katika kipindi cha pili kwa kuanza kurejesha mabao hayo, baada ya Santi Cazorla kuandika bao dakika ya 68 kwa penati kabla ya Aaron Ramsey kuongeza dakika mbili baadaye akimalizia kazi ya Alexis Sanchez.
Arsenal ilijikuta ikimpoteza beki wake Calum Chembers baada ya kuonyesha kadi ya pili ya manjano iliyoambatana na nyekundu.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Liverpool ikiwa nyumbani iling'ang'aniwa na Sunderland na kutoka suluhu sawa na ilivyokuwa kwa Tottenham Hotspur iliyoshikiliwa na Crystal Palace na Hull City kushindwa kutoshana nguvu na Wes Bromwich Albion kwa kutoka pia suluhu huku QPR ikipata ushindi wake wa pili kati ya mechi zake tatu za karibuni.
Kwa hivi sasa mabaingwa watetezi Manchester City wapo dimbani kuumana na Everton katika pambano linalochezwa uwanja wa Etihad.
Jumatatu kutakuwa na pambano moja la kukata na shoka kati ya Southampton itakayoialika Manchester United ambayo inasaka kuingia kwenye Tatu Bora.

Yanga yaidonyoa Express, Maximo amficha Emerson

Emerson (wa pili kulia) akiwa na Hussen Javu, Kiiza na Coutinho
IKICHEZA bila kiungo mkabaji mpya toka Brazil, Yanga imetuma salamu kwa watani zao Simba baada ya kuifunga Express ya Uganda kwa bao 1-0 katika pambano la kirafiki la kimataifa lililochezwa uwanja wa Taifa.
Bao pekee lililoizamisha Express ambao jana walilazimishwa suluhu na Simba katika pambano jingine la kirafiki la kimataifa liliwekwa kimiani na Mganda, Hamis Kiiza 'Diego' katika dakika za lala salama na kuzima ndoto za Waganda wenzake kuambulia suluhu katika mchezo huo.
Kiiza aliyeingia uwanjani toka benchi alifunga bao hilo kwa shuti baada ya kuunganisha krosi ya Simon Msuvah, na mashabiki waliofurika uwanjani walikosa uhondo kwa kushindwa kumuona Emerson Oliveira ambaye kocha Marcio Maximo aliamua kutompanga kabisa ili kuficha makali yake kabla ya kuvaana na Simba Jumamosi ijayo kwenye mechi ya Bonanza ya Nani Mtani Jembe.

Newcastle United yaiadabisha Chelsea, Cisse shujaa

Newcastle striker Papiss Cisse puts his side in front against Chelsea
Cisse akimtungua kipa wa Chelsea
Papiss Cisse scores for Newcastle against Chelsea
Cisse alikuwa na kazi ya kufunga tu St James Park
MABAO mawili ya mtokea benchi, Demba Cisse yameiwezesha Newcastle United kusitisha rekodi ya ushindi mfululizo wa Vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea baada ya timu hiyo kucharazwa mabao 2-1.
Cisse aliyeingizwa dimbani kipindi cha pili alidhihirisha umuhimu wake katika timu hiyo baada ya kufunga mabao hayo akiunganisha korsi pasi za Mousa Sissoko katika dakika za 57 na 78  kabla ya Didier Drogba kuipatia Chelsea bao kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu dakika ya 83.
Adabu hiyo ilitokana na Steven Taylor kucheza rafu iliyofanya aonyeshwe kadi ya pili ya njano na kuunganishiwa nyekundu dakika ya 81, hata hivyo pamoja na Chelsea kucharuka matokeo yalisalia kuwa 2-1.
Kipigo hicho ni cha kwanza kwa Chelsea kwa msimu huu na kuendeleza unyonge wake kwa Newcastle kwa mechi ya tatu mfululizo kila wanapoifuata nyumbani kwao St James Park.
Kabla ya klipigo hicho Chelsea ilikuwa imcheza mechi 23 bila kupoteza na 14 zikiwa za ligi na kukatisha ndoto za mashabiki wa klabu hiyo wakiifikia rekodi ya Arsenal iliyocheza mechi 49 katika msimu wa 2003-2005.

Friday, December 5, 2014

TFF yaionya Simba usajili wa Sserunkuma kwa Kiongera

Kiongera aliyetajwa kuachwa kinyemela

http://www.standardmedia.co.ke/images/wednesday/ssekum56768.jpg
Dan Sserunkuma
BAADA ya kumuondoa kiutata kikosini mshambuliaji Mkenya Paul Kiongera, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limeitaka Klabu ya Simba kuwa makini katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo.
Uongozi wa Simba juzi ulimsainisha mkataba wa miaka miwili mshambuliaji Mganda Danny Ssrerunkuma huku ukitangaza kusitisha kwa muda mkataba wa Kiongera hadi pale atakapofanyiwa upasuaji na kupona majeraha ya goti yanayomkabili.
Timu za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) zinapaswa kuwa na idadi isiyozidi wachezaji watano wa kigeni kwa mujibu wa Kanuni za Ligi za TFF Toleo la 2014. Ujio wa Sserunkuma umeifanya Simba kuwa na wachezaji sita wa kigeni; Waganda watatu (Emmanuel Okwi, Joseph Owino na Sserunkuma, Warundi wawili (Amissi Tambwe na Pierre Kwizera) na Mkenya mmoja (Kiongera).
Katika mahojiano maalum  kwenye ofisi za Makao Makuu ya TFF zilizopo Posta jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mashindano wa shirikisho hilo, Boniface Wambura, alisema Simba wanapaswa kusajili kwa kufuata Kanuni za Ligi za TFF na taratibu zinazoongoza soka.
"Kwa sasa (jana saa 6:37 mchana) hatujapokea kitu chochote kutoka Simba kuhusu usajili unaoendelea wa dirisha dogo, tunasikia tu wamemsajili Sserunkuma lakini hatujapata taarifa rasmi," Wambura alisema.
"Simba itaruhusiwa kusajili mchezaji mpya/wapya wa kigeni msimu huu endapo tu itavunja mkataba/mikataba na wachezaji wa kigeni ilio nao kwa sasa.
"Kuna mambo matatu yanayothibitisha kuvunjwa kwa mkataba wa mchezaji; mchezaji mwenyewe kuvunja mkataba, mchezaji kufariki au klabu kuamua kuvunja mkataba wa mchezaji husika. Hili la Kiongera na Sserunkuma hawajatueleza maamuzi yao."
Simba kupitia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hanspope imeeleza kuwa imesitisha mkataba wake na Kiongera na kumuondoa kwenye orodha ya wachezaji wake kwa ajili ya msimu huu na atakapopona, mkataba huo utaendelezwa, kauli ambayo inaonekana kama Kiongera bado ni mchezaji wa Simba. Dirisha dogo la usajili lilifunguliwa Novemba 15 na litafungwa Desemba 15.
NIPASHE

Robbie Keane ang'ara Marekani

http://www.trbimg.com/img-547ffbde/turbine/la-sp-keane-mls-mvp-20141204-001/500/500x281MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya Los Angeles Galaxy Robbie Keane ametajwa kuwa mchezaji mwenye thamani zaidi maarufu kama MVP katika Ligi Kuu ya Soka nchini Marekani-MLS kwa mwaka huu. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Ireland amefunga mabao 19 katika mechi 29 hivyo kuwapita washambuliaji wengine akiwemo Lee Nguyen wa New England Revolution na Obafemi Martins wa Seattle Sounders. Akihojiwa Keane amesema hakwenda nchini Marekani kwa ajili ya likizo bali kufanya kazi hivyo anafurahi kunyakuwa tuzo hiyo. 
Keane mwenye umri wa miaka 34 ambaye ndiye mfungaji mwenye mabao mengi katika timu yake ya taifa aliendelea kudai kuwa bado anapenda kuendelea kucheza kwa kiwango cha juu.

Pellegrini amvulia kofia kun Aguero

KOCHA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amemmwagia sifa lukuki mshambuliaji wake Sergio kun Aguero akisema ni mmoja kati ya wachezaji watano bora duniani.
Meneja huyo aliyasema hayo baada ya mshambuliaji huyo wa Argentina, kuisaidia timu yake kupata ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Sunderland juzi. 
Katika mchezo huo City walitoka nyuma na kufanikiwa kushinda mchezo huo muhimu kwa kufunga mabao mawili na kumfanya Aguero kufikisha jumla ya mabao 14 msimu huu. 
Pellegrini amesema anadhani Aguero yuko katika orodha ya wachezaji watano bora duniani na kwa umri wa miaka 26 alionao bado ana nafasi ya kuimarika zaidi. 
Mbali na Aguero, kocha huyo pia aliwapongeza viungo wake Yaya Toure na Samir Nasri kwa juhudi zao kubwa kuhakikisha wanajiimarisha katika nafasi ya pili ya msimamo wa Ligi Kuu.

Chelsea kumpa kibarua cha kudumu Drogba

Mourinho akiwa na Drogba
MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amesema mshambuliaji wake Didier Drogba bado atakuwa na kazi Stamford Bridge wakati akiamua kustaafu rasmi kucheza soka. 
Drogba mwenye umri wa miaka 36 kwasasa anaichezea kwa mara ya pili klabu hiyo huku akifunga bao katika mchezo wa jana ambao Chelsea waliibugiza Tottenham Hotspurs kwa mabao 3-0. 
Akihojiwa Mourinho amesema jambo ni kwamba nyota huyo atamalizia soka lake akiwa na Chelsea na inavyoonekana anaweza kubakia akifanya mambo mengine pindi atakapostaafu. 
Drogba amefanikiwa kushinda mataji 10 akiwa na Chelsea mara ya kwanza kati ya mwaka 2004 mpaka 2012 huku akifunga mabao 157 katika mechi 341 alizocheza. 
Nyota huyo alijiunga tena na Chelsea katika kipindi cha majira ya kiangazi mwaka huu baada ya kuondoka klabu ya Galatasaray ya Uturuki.

Simba, Yanga kula shushu Mtani Jembe, viingilio vyatajwa

Vikosi vya Simba na Yanga
KLABU za Simba na Yanga watapata nafasi ya kubadili hadi wachezaji watano katika mechi ya kirafiki ya Bonanza, maarufu kama Mtani Jembe, ambayo viingilio vya mechi hiyo vimkitangazwa hadharani.

Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Boniface Wambura amesema wamefikia uamuzi huo kuwa wachezaji wanaoruhusiwa kuingia katika dakika 90 ni hadi watano kwa kila timu.
“Sub imeongezwa siku hiyo, badala ya wachezaji watatu, itakuwa hadi wachezaji watano.
“Kama mechi itaisha ndani ya dakika tisini bila ya kupata mshindi, basi zitapigwa penalti tano tano kwanza.
“Kikubwa katika mechi hiyo ni lazima siku hiyo mshindi apatikane,” alisema Wambura.
Wambura alisema pambano hilo litachezwa kwa dakika 90 tu na kama muda huo hatapatikana mshindi, mikwaju ya penalti itatumika na kwamba mshindi na marefa watakaolisimamia wanatarajiwa kutajwa leo na Kamati ya Waamuzi ya shirikisho.
Pia aliweka bayana viingilio vya mechi hiyo ya Jumamosi ijayo kuwa kiingilio cha chini kitakuwa Sh 7000 na cha juu Sh 30,000.

"Viingilio vya mechi hiyo ni Sh. 30,000 kwa VIP B, Sh. 20,000 kwa VIP C, 15,000/- kwa viti vya rangi ya chungwa na Sh. 7,000 kwa viti vya bluu na kijani. Tiketi zitakazotumika ni za kawaida na zitauzwa kwenye vituo ambavyo vitatangazwa baadaye," alisema Wambura.Mechi hiyo ya Bonanza inasubiriwa kwa hamu kubwa.

Tom Oloba apewa jukumu ya kunasa msaidizi wa Mombeki

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiYcQ4GKfL84y4L09fZetG_9-iVLkU_gy6fWn9b2LjkoG-I89l_VehzDBlZEEPOxfcGAfGdq90_0rMu0KqwI3yOU4rTJc6B2UkJ6pWcErF0K-kEibqKmTapUgHCgW67ki5XFunEQjgRTfQ/s1600/IMG_6927.JPG
Mombeki alipokuwa Simba
UONGOZI wa klabu ya Ruvu Shooting, umesema hatma ya mshambuliaji mpya wa pili anayehitajiwa na kikosi chao ipo mikononi mwa kocha wao Tom Olaba, kwani tayari wachezaji zaidi ya watatu wanaendelea kufanyiwa majaribio kwenye mazoezi ya timu hiyo.
Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire alisema baada ya kumsainisha mkataba wa mwaka mmoja mshambuliaji wa zamani wa Simba, Betram Mombeki kwa sasa wanasaka mchezaji wa mwisho na tayari chipukizi kadhaa wanafanyiwa majaribio kabla ya kocha Oloba kuamua.
Bwire alisema, Mkenya Olaba ndiye mwenye jukumu la kuamua nani anayemfaa katika kikosi chake kama alivyoamua kwa Mombeki ambaye alisainishwa mkataba wake mapema wiki hii.
"Tumefanikiwa kumnasa Mombeki na sasa kocha anaendelea kuwapima wachezaji waliojitokeza kwenye mazoezi, atakayemfaa ndiye atakayetueleza tumsainishe kwa ajili ya kukipa katika timu yetu, ila tunaamini tutafunika ligi ikiendelea kwa namna kikosi chetu kinavyoendelea kujifua," alisema.
Bwire alisema timu yao ipo kambi ya mazoezi tangu Novemba 24 na walianza mapema kwa ajili ya kutoa nafasi kwa kocha wao kurekebisha mapungufu yaliyoiangusha timu kwenye mechi za raundi saba zilizopita ambapo timu hiyo ilijikuta ikienda mapumziko wakiwa kwenye nafasi ya 11 kati ya timu 14 zinazoshiriki ligi hiyo kwa kukusanya pointi saba tu.
Ruvu inatarajiwa kuendelea na ligi Desemba 28 kwa kuvaana na ndugu zao wa JKT Ruvu wanaonolewa na kocha Fred Felix Minziro wanaokamata nafasi ya sita wakiwa na pointi 10.

Simba kuivaa Express bila Mkude, Sserunkuma ndani

Dan Sserunkuma anayeterajiwa kuonekana na uzi mwekundu leo
Kikosi cha Simba kitakachoshuka dimbani leo dhidi ya Express
MSHAMBULIAJI wa Simba Jonas Mkude anatarajia kuikosa mechi ya leo ya majaribio dhidi ya timu ya The Express  kutoka nchini Uganda kutokana na kuwa majeruhi, huku pia Dan Sserunkuma akitarajiwa kuonekana uwanjani na timu hiyo kwa mara ya kwanza.
Akizungumza jana Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri alisema, Mkude, Ivo Mapunda na Hussein Shariff 'Casilas' wote wataikosa mechi hiyo ambayo ni muhimu kwa timu kujipima uwezo kabla ya mchezo wa 'Nani Mtani Jembe 2' dhidi ya Yanga Desemba 13, mwaka huu.
"Mechi ya leo ni muhimu kwetu, kwa sababu itatuonesha kipimo cha wachezaji kabla ya mchezo wetu wa Nani Mtani Jembe dhidi ya watani wetu Yanga,"alisema Phiri.
Alisema lengo la mchezo huo ni pamoja na kujiweka sawa kabla ya mchezo huo na Yanga na ule wa mzunguko wa nane wa Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 26, mwaka huu katika viwanja tofauti hapa nchini.
Alisema mchezo huo pia utatumika kumpima mchezaji kutoka Gambia Omary Mboob ambaye anafanya majaribio kwa ajili ya kusajiliwa katika dirisha dogo la usajili linalofikia ukingoni Desemba 15, mwaka huu.
Akizungumzia mazoezi kwa ujumla alisema yanaendelea vizuri ambapo alisema wachezaji wameonyesha moyo wa kujituma pale wanapokuwa uwanjani kuendelea na mazoezi.

Maokola, MP Minoma kumaliza ubishi Desemba 19

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2DnzKJGvRGtEhB1V2Y09n6CRWs1Qt2k8RO129VGkP8domwzd7Qm7S2j22fN_8byoAanbCE1dOXeQuGqyfZL8iyAHSvvq8FQcnkAuxOo_2eVfUR0EAtGwI2zAtLZxL8f51cHY02Lq5eXTB/s1600/IMG_0408.JPG
Maokola na Mkalakala watakaorudiana tena kuwania ubingwa wa TPBC
BINGWA wa ngumi za kulipwa wa uzito wa Light Middle anayetambuliwa na Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), Ibrahim Maokola anatarajiwa kupanda ulingoni Desemba 19, mwaka huu kwa ajili ya kutetea ubingwa wake huo dhidi ya Seleman Mkalakala 'MP Minoma'.
Rais wa TPBC, Chaurembo Palasa aliliambia MICHARAZO kuwa pambano hilo litakalokuwa la raundi 10 na litakalosindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi, litachezwa kwenye Ukumbi wa Vigae Pub, Mbagala Dar es Salaam.
Palasa alisema sababu ya kupeleka pambano hilo Mbagala ni kutaka kuhamasisha mchezo huo wa ngumi katika maeneo mengine badala ya kuendelea kuchezwa katika kumbi zile zile zilizozoeleka.
"Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), tumeidhinisha pambano la ngumi kati ya Ibrahim Maokola atakayekuwa akitetea taji lake dhidi ya Seleman Mkalakala, mchezo huo utasindikizwa na michezo mingine kadhaa ya utangulizi," alisema Palasa.
Palasa alitaja baadhi ya michezo ya utangulizi kuwa ni lile la wapinzani wa jadi, Abdallah Mohammed 'Prince Nassem' dhidi ya Salehe Mkalekwa.
"TPBC inataka kuleta mvuto kwa mchezo huo kwa kupelekwa katika maeneo mengine nje ya kumbi zilizozoeleka, ili kuwavutia wadhamini sambamba na kuhakikisha vipaji vipya vinaibuka ndani na nje ya jijini la Dar es Salaam ili kuendeleza ngumi," alisema Palasa.
Aidha, Palasa alitoa tahadhari kwa mabondia, waratibu na mapromota ambao watakiuka sheria na kanuni za mchezo kuwa watachukuliwa hatua kali za kinidhamu ili kuhakikisha ustaarabu unaendelea kuwepo katika mchezo huo.

Zahoro Pazi kumbadili Mrwanda Polisi Moro

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgeIFO6Ts0oOYH-zSbZQpHtdE3LBHVEuBeH3qRPbnGO4jkbsbTrXqiLajnsS3YTyKidqQxsd0gZR9d434iV_lBuB4lrqz1F_FDTjFIQMRqaHqCmd338YusINEHVosFi2MAeESOCzguCrgXd/s1600/pazi.JPG
Zahoro Pazi alipokuwa Simba
TIMU ya Polisi ya Morogoro inayoshiriki Ligi Kuu imemsajili mshambuliaji wa Simba, Zahor Pazi, mtoto wa kipa wa zamani wa wekundu hao, Idd Pazi 'Father' katika kipindi hiki cha dirisha dogo linalotarajiwa kufugwa Desemba 15, mwaka huu.
Zahor ambaye anacheza nafasi ya ushambuliaji, amesaini mkataba wa kuichezea timu ya Polisi ya Morogoro kwa kipindi cha mwaka mmoja katika ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoani hapa, ambaye pia ni mlezi wa timu hiyo.
Hatua ya Polisi kumsajili mchezaji huyo ni kujibu mapigo baada ya timu ya Simba kuwa mbioni kumsajili mshambualiaji wao tegemeo, Danny Mrwanda.
Akizungumza na waandishi wa habari, mwenyekiti wa timu hiyo ya Polisi, Issa Bushir alisema kuwa wameamua kumchukua mshambuliaji huyo kutokana na uwezo alionao na kwamba wanaamini kuwa ataisaidia timu hiyo katika ligi inayotarajiwa kuendelea wiki mbili zijazo.
Naye mlezi wa timu hiyo ya Polisi, ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonald Paul, alisema wanaamini mshambuliaji huyo ataweza kuziba pengo la Mrwanda anayehamia timu ya Simba.
Kwa upande wake Zahor alihaidi wanachama na wapenzi wa timu ya Polisi Morogoro kuwa atajituma kwa kushirikiana na wachezaji wenzake ili kuiletea ushindi timu hiyo ya 'maafande'.

Ndanda kuanza kuiwinda Mbeya City Jumatatu Dar

Kikosi cha Ndanda Fc
TIMU ya Ndanda ya Mtwara inayoshiriki Ligi Kuu kwa mara ya kwanza msimu huu inatarajiwa kuanza kambi ya mazoezi keshokutwa jijini Dar es Salaam, huku uongozi wake ukiendelea kuficha majina ya wachezaji wapya iliyowasajili kwenye dirisha dogo.
Mkurugenzi na Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Edmund Njowoka aliliambia MICHARAZO mapema leo kuwa, kambi yao ya mazoezi kwa ajili ya kujiwinda na mzunguko wa nane wa ligi hiyo itaanza siku ya Jumatatu badala ya Desemba 4 kama walivyokuwa wametangaza awali na itakuwa jijini Dar es Salaam.
Njowoka alisema uongozi wao umeamua kuiweka kambi hiyo jijini Dar es Salaam ili kutoa nafasi nzuri kwa kocha wao Meja Abdul MIngange kuwanoa vizuri wachezaji wapya ambao wamenyakuliwa na klabu hiyo katika dirisha dogo.
Hata hivyo alipoulizwa juu ya wachezaji wapya iliowaongeza, Njowoka alisema hawezi kuwataka kwa madai ni mapema mno kwa sasa na atafanya hivyo baada ya kufungwa kwa dirisha hilo Jumatatu ijayo.
"Hatuwezi kuzungumza vitu nusu nusu, wapo tuliofanikiwa kuwanyakua na wengine tunamalizana nao, hivyo subirini tumalize usajili wote kisha tuutangaze umma kitu kilichokamilika," alisema Njowoka.
Hata hivyo tayari timu hiyo ilishamtangaza kumsajili kiungo mshambuliaji wa Mtibwa, Masoud Chile na ilikuwa mbioni kuwanyemelea nyota wengine toka Yanga akiwamo kipa Ally Mustafa 'Barthez'.
Timu hiyo iliyopanda msimu huu sambamba na timu za Stand United na Polisi-Moro inatarajiwa kuvaana na Mbeya City katika mechi yao ijayo na mpaka ligi inasimama waliwakuwa katika nafasi ya pili toka mkiani ikiwa na pointi 6, moja zaidi ya wanaoshika mkia Mbeya City.

Thursday, December 4, 2014

Mgendi aachia Wema ni Akiba, 'audio' albamu kabla ya X-mass


MUIMBAJI nyota wa muziki wa Injili ambaye pia ni muigizaji wa filamu, Jennifer Mgendi ameachia wimbo mpya uitwao 'Wema ni Akiba' ikiwa ni utambulisho wa albamu yake mpya ijayo.
Tayari wimbo huo wa Mgendi umeanza kutamba kwenye vituo vya redio na katika mitandao ya kijamii baada ya kuuachia mapema wiki hii.
Akizungumza na MICHARAZO Mgendi alisema kuwa albamu yake ijayo itakuwa na nyimbo saba na ameutanguliza uliobeba jina kwa nia ya kuitambulisha kabla ya kuja kuiachia rasmi baadaye.
"Nimeachia wimbo wangu mpya ambao ni utambulisho wa albamu ijayo itakayofahamika kwa jina la 'Wema ni Akiba' itakayokuwa na nyimbo saba," alisema Mgendi.
Muimbaji huyo alizitaja baadahi ya nyimbo za albamu hiyo kuwa ni 'Wema ni Akiba', 'Usiniache Njiani', 'Nimempata Yesu', 'Nani Kama Mungu' na 'Kimbilia Msalabani'.
Albamu hiyo mpya imekuja wakati albamu ya msanii huyo iitwayo 'Hongera Yesu' ikiwa bado haijachuja sokoni ambayo aliiachia mapema mwaka huu.
Kuhusu video ya albamu hiyo, Mgendi, amesema ataanza zoezi la upigwaji picha za video Januari mwakani kabla ya albamu hiyo kuachiwa sokoni Juni, 2015.
Alisema uchukuaji wa video utahusisha nyimbo zote saba zitakazokuwa katika albamu hiyo inayokuja baada ya kutamba na 'Hongera Yesu'.
Jennifer alisema ataanza kurekodi video ya wimbo wa 'Wema ni Akiba' ambao tayari ameshauachia hewani ili kuitambulisha albamu hiyo ambayo ni ya nane kwake.
"Mchakato wa kurekodi video ya albamu yangu ijayo utaanza mapema Januari na nitaitoa rasmi Juni 2015, ila kwa sasa nimeachia 'audio' ili kuwapa ladha mpya ya Jennifer Mgendi," alisema muimbaji huyo ambaye pi ni muigizaji, mtayarishaji na muongozaji filamu.
jennifer alifafanua kuwa 'audio' albamu ya Wema ni Akiba itaachiwa ndani ya mwezi huu kabla ya Sikukuu ya Xmass.
"Audio albamu ya Wema ni Akiba nitaiachia sokoni kabla uya Krismasi ila video yake ndiyo itatoka Juni baada ya kuanza kurekodi mwezi ujao," alisema Jennifer.
Jennifer ambaye kitaaluma ni mwalimu, alianza kutamba kwenye muziki wa Injili mwaka 1995 akitoa albamu saba sambamba na filamu zilizomjengea jina kubwa miongoni mwa wasanii wa kike nchini.

Sami Khadira atolewa hospitalini, majaliwa yake bado...!

http://completesportsnigeria.com/wp-content/uploads/2014/08/Sami-Khedira.jpgKIUNGO nyota wa klabu ya Real Madrid, Sami Khedira ameruhusiwa kutoka hospitali baada ya kulazwa kwa siku moja kwa uangalizi kutokana na mtikisiko katika ubongo wakati wa mchezo wa Kombe la Mfalme dhidi ya Cornella. 
Khedira aligongana na kiungo wa Cornella David Garcia muda mfupi baada ya mapumziko katika mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Santiago Bernabeu kabla ya kucheza kwa dakika chache na baadae kutolewa nje na nafasi yake kuchukuliwa na Jese. 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo, Khedira alifanyiwa vipimo zaidi jana na kuruhusiwa lakini haijajulikana na muda gani atakaa nje ya uwanja. 
Madrid ambao ndio mabingwa watetezi wa michuano hiyo walitinga hatua ya timu 32 bora bada ya kushinda mchezo wao wa mkondo wa pili kwa mabao 5-1 dhidi ya timu hiyo ya daraja la tatu hivyo kuwafanya kusonga mbele kwa jumla ya mabao 9-1. 
Madrid sasa inakabiliwa na mchezo mwingine wa La Liga Jumamosi hii dhidi ya Celta Vigo huku wakiwa na matumaini ya kushinda na kuendelea pengo lao la alama mbili dhidi ya mahasimu wao Barcelona.

Make Money at : http://bi

Dokii Hakuna Kama Mwanamke videoni


MSANII Ummy Wenceslaus 'Dokii' ameachia video ya wimbo wake mpya wa 'Hakuna Kama Mwanamke' huku akianza mchakato wa kutengenezea video ya wimbo wake mwingine uitwao 'Nampenda Dereva wa Bodaboda'.
Akizungumza na MICHARAZO, Dokii alisema video yake mpya imetengenezwa na Pablo ambaye pia ndiye aliyepewa jukumu la kuitengeneza video ya wimbo wa 'Nampenda Dereva wa Bodaboda'.
"Tayari nimeshaiachia video ya wimbo wangu wa 'Hakuna Kama Mwanamke' ambao 'audio' yake imetengenezwa studuio za Recho Records chini ya mtayarishaji aitwaye Shivo," alisema Dokii.
Alisema wimbo wake wa Nampenda Dereva wa Boda Boda' uliotengenezwa Akhenato Records chini ya Lil Ghetto, utaanza kurekodiwa video yake wiki ijayo kabla ya kuachiwa hewani.
"Video hiyo nayo itatengenezwa na Pablo, hivyo mashabiki wangu wajiandae kushuhudia kazi hiyo mapema kabla ya kumalizika kwa mwezi huu," alisema Dokii.
Muigizaji na mwanamitindo huyo alisema, ameamua kutoa kazi hizo mfululizo kuthibitisha alivyoelekeza nguvu zake katika fani ya muziki akiipa kisogo kwa muda kazi ya uigizaji filamu.

Hatari! Cameroon, Ivory Coast kundi moja AFCON 2015

Results of the Orange AFCON 2015 draw
SHIRIKISHO la Soka Afrika, CAF, imetangaza droo ya makundi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) itakayofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea kwa kuziweka kundi moja timu za Ghana, Algeria, Afrika Kusini na Senegal.
Kwa mujibu wa droo iliyofanywa usiku wa jana, timu hizo zimewekwa kundi moja la C ambalo ni la kifo kama lilivyo kundi D lenye timu za Ivory Coast, majirani za Cameroon, Guinea na Mali.
Makundi mengine mawili ya A na B yanaonekana siyo ya kutisha ingawa timu zote 16 zitakazochuana kwenye fainali hizo za mwakani zinapewa nafasi sawa ya kutwaa ubingwa huo ambao hauna mwenyewe baada ya Nigeria kuvuliwa hatua ya makundi.
Katika Kundi A zimepangwa timu wenyeji Equatorial Guinea sambamba na Burkina Faso, Gabon na Congo, huku Kundi B likiwa na timu za zambia, Tunias, Cape Verde na DR Congo.
Fainali hizo zinatarajiwa kuanza kuchezwa Januari 17 na kufikia tamati kwa bingwa kufahamika Februari 8.

Wednesday, December 3, 2014

Liverpool, Man Utd zaua, Arsenal, Chelsea kazi kwao leo

Liverpool captain Gerrard (right) wheels away after giving Liverpool the lead with his 177th goal for the club
Steven Gerrard akishangilia bao lake usiku wa jana
Gerrard (right) orchestrates play from central midfield as Liverpool chase the game in the opening half
Nahodha akionyesha maujuzi yake
Fellaini takes an early touch at Old Trafford with Stoke defender Erik Pieters in attendance
Fellaini akichuana na mchezaji wa Stoke City
Jordan Henderson (left) and Lallana (right) scream towards the away fans after Gerrard's goalUnited midfielder Juan Mata tries to shake off Stoke's Geoff Cameron in the opening exchangesKIUNGO wa kimataifa mkongwe, Steven Gerrard juzi alidhihirisha kuwa 'bado wamo' baada ya kuisaidia Liverpool kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Leicester City katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England (EPL).
Nahodha huyo ambaye aliwekwa benchi katika mechi iliyopita dhidi ya Stoke City, alianzishwa katika pambano hilo la ugenini lililochezwa kwenye uwanja wa King Power dhidi ya 'vibonde' Leicester City na kufunga bao moja kati ya mabao matatu yaliyozidi kuifufua Liverpool katika ligi hiyo.
Wenyeji ambao walimaliza pambano hilo wakiwa pungufu ya mchezaji mmoja kutokana na Wes Morgan kulimwa kadi nyekundu katika dakika ya 63, ndiyo wlaikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 22 baada ya kipa Simon Mignolet kujifunga kufuatia shuti la Leonardo Ulloa kugonga mwamba na katika harakati za kuokoa akajikuta akijifunga.
Hata hivyo dakika nne baadaye Adam Lalana aliisawazishia Liverpool bao hilo dakika nne baadaye kutokana na kushirikiana vyema na Ricky Lambert na kufanya hadi mapumziko matokeo yawe sare ya 1-1.
Gerrard aliiandikia Liverpool bao la pili dakika ya 54 kabla ya Jordan Henderson kuongeza la tatu dakika ya 83 na kumfanya Kocha Branden Rodgers kupumua baada ya Liverpool kuchupa kutoka nafasi ya 11 hadi ya 8 ikiwa na pointi 20.
Katika mapambano mengine ya ligi hiyo yaliyochezwa juzi, Manchester United ikiwa uwanja wa Old Trafford walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Stoke City, huku West Ham United ilitokana nyuma ugenini na kuichapa West Bromwich Albion mabao 2-1 katika pambano jingine.
Vijana wa Luis Van Gaal walipata mabao yao kupitia kwa Marouane Fellaine aliyemaliza pasi safi ya Ander Herrera katika dakika ya 21 na Juan Mata aliyefunga kwa mkwaju wa adhabu ndogo katika dakika ya 59, huku bao la wageni lilifungwa na Stephen N'Zonzi katika dakika ya 39.
Nao West Ham walipata ushindi wa mabao 2-1 ugenini baada ya kutanguliwa kufungwa, huku Burnley na Newcastle United zilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1, Swansea City ikiwa nyumbani ilitakata kwa kuichapa QPR kwa mabao 2-1 na Aston Villa kuiduwaza nyumbani Crystal Palace kwa kuinyuka bao 1-0.
Ligi hiyo ilitarajiwa kuendelea tena usiku wa leo kwa michezo minne Arsenal itakuwa nyumbani kuwakabili
Southampton, vinara Chelsea wataialika Tottenham Hotspur, huku Everton na Hull City zikionyeshana umwamba na Sunderland kuwakabili Mabingwa watetezi Manchester City.

Vumbi jingine litaendelea Jumamosi kama hivi;
Newcastle United vs Chelsea
Hull City vs West Bromwich Albion
Liverpool vs Sunderland 
QPR vs  Burnley
Stoke City vs Arsenal
Tottenham Hotspur vs Crystal Palace
Manchester City  vs Everton

Arsene Wenger awaonya wachezaji kuhusu Mitandao ya Kijamii

http://www.whoateallthepies.tv/EMP-6272392.jpg
Arsene Wenger
MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger anaamini ni juu ya wachezaji kuchambua kile wanachoandika wakati wakituma ujumbe wao katika mitandao ya kijamii.
Kauli hiyo ya Wenger imekuja baada ya mshambuliaji wa Liverpool Mario Balotelli kuomba radhi kwa ujumbe aliochapisha ambao ulionekana kama wa kibaguzi.
Akihojiwa Wenger amesema jambo kubwa wanalofanya ni kuwaonya athari zake lakini hakuna anaweza kuwalinda saa 24 kwa siku. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wachezaji wenyewe wanapaswa kuwajibika na kuelimika jinsi ya kudhibiti wanachokiongea.